Jumapili, 27 Septemba 2020

Bwana ni Mtu wa Vita!

Kutoka 15:2-3 BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza. BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake.


 

Bwana ni Mtu wa Vita.

Ni muhimu kufahamu kuwa moja ya ufunuo mkubwa zaidi wa Mungu kwa wana wa Israel ukiacha kujitambulisha kama NIKO AMBAYE NIKO Mungu vilevile alijifunua kama Bwana wa vita au Mtu wa vita! Katika Biblia ya Kiebrania mara zote jina Yahweh, na jina Elohim wakati wote huambatana na neno tzevaotao Sabaothambayo maana yake ni Majeshi kwa hiyo jina la Mungu katika israel husomeka YHWH Elohe Tzevaot kwa kiingereza Jehova Lord of Host kwa kiswahili Bwana Mungu wa majeshiNeno hili Bwana wa Majeshi limejitokeza mara 300 katika biblia, Ufunuo huu kuhusu Mungu ulikuwa dhahiri hasa pale wana wa Israel  walipokuwa wamekwama katika eneo ambalo kushoto kulikuwa na mwamba mkubwa sana na kulia kulikuwa na mwamba mkubwa sana na mbele yao ilikuweko bahari ya shamu, wakati huu wakiwa katika kona hii, Farao aliwaamuru majeshi yake kuwafuatia wana wa israel na kuwaangamiza kabisa majeshi yake yalitii na kuwafuatia wana wa Israel ambao wakati huu walikuwa hawajajifunza vita na hawana wa kuwapigania

Kutoka 14:9-10
Wamisri wakafuata nyuma yao, farasi zote na magari yote ya Farao, na askari zake wenye kupanda farasi, na jeshi lake, nao wakawapata hali wamepanga pale karibu na bahari, karibu na Pi-hahirothi, kukabili Baal-sefoni. Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia BWANA.

  
Kwa Mujibu wa mwana historia wa kiyahudi wa nyakati ya karne ya kwanza Flavious Josephus anasema kwamba Majeshi yaliyokuwa yakiwafuatia Israel yalikuwa ni majeshi katili ya makomandoo hodari waliokuwa na Magari ya farasi 600, wapiganaji wa juu ya farasi 50,000 na askari wa miguu 200,000. kwa hiyo unaweza kupata picha kwa taifa hili changa ilikuwa ni haki yao kupiga kelele na kuhitaji msaada wa Mungu, Musa kama Nabii wa Bwana alisema kwa niaba ya Mungu kuwa Israel hawapaswi kuogopa badala yake wanatakiwa kusimama na kuuona wokovu wa Bwana!  Na kuwa hawa wamisri wanaowaona leo hawatawaona tena milele! Bwana atawapigania nao watanyamaza kimya 

Kutoka 14:13-14
Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Ni ukweli usiopingika kwamba Jeshi hili kali lingewamaliza Vibaya Israel bila huruma, lakini hata hivyo Bwana aliwapigania kwa jinsi ya ajabu mno, Kumbuka ya kuwa unaposikia Bwana anampigania mtu ni muhimu kufahamu kuwa huwa hapigani yeye, Yeye hutumia malaika wake

Mathayo 26:52-56
Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga. Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?  wanauwezo mkubwa sana na wanapiga vibaya mno, Jambo kubwa ambalo Mungu alilifanya kwanza ni kumtuma malaika aliyesimama kuwatenga Israel na Majeshi ya wamisri

Malaika wa Bwana ndio hufabya kazi ya kupigania watu wa Mungu, Mungu hawezi kupigana na yoyote wala hawezi kupigana na kiumbe chake Yeye ni mwenye nguvu sana uwezo wake ni mzito mno ukimuona tu unakufa mwenyewe hata kabla ya lolote kwa hivyo yeye hutumia malaika ni malaika wa Bwana aliyekwenda kusimama katikati ya wana wa Israel na wamisri ona
 

Kutoka 14:19
Kisha malaika wa Mungu, aliyetangulia mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akaenda nyuma yao; na ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao, ikasimama nyuma yao;

Hapa Malaika wa Bwana alikuwa anatenganisha kwanza kwa ulinzi wake kwa kawaida Mungu anapotulinda hutumia malaika lakini pia hutumia ukuta wa moto ona
 

Zekaria 2:5
Kwa maana mimi, asema Bwana, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake.”  

kuna hatua kadhaa hapa ambazo Mungu alizifanya na hatimaye Bwana akawapigania Israel ona
 Kutoka 14:19-28 Kisha malaika wa Mungu, aliyetangulia mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akaenda nyuma yao; na ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao, ikasimama nyuma yao; ikafika kati ya jeshi la Misri na jeshi la Israeli; napo palikuwa na lile wingu na lile giza, lakini lilitoa nuru wakati wa usiku; na hawa hawakuwakaribia hawa usiku kucha. Musa; akanyosha mkono wake juu ya bahari; BWANA akaifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wa nguvu utokao mashariki, usiku kucha, akaifanya bahari kuwa nchi kavu, maji yakagawanyika. Wana wa Israeli wakaenda ndani kati ya bahari katika nchi kavu; nayo maji yalikuwa ukuta kwao mkono wa kuume, na mkono wa kushoto.  Na wale Wamisri wakawafuatia, wakaingia ndani kati ya bahari, farasi zote za Farao, na magari yake, na wapanda farasi wake. Ikawa katika zamu ya alfajiri, BWANA akalichungulia jeshi la Wamisri katika ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha jeshi la Wamisri. Akayaondoa magurudumu ya magari yao, hata yakaenda kwa uzito; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa BWANA anawapigania, kinyume cha Wamisri. BWANA akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao. Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na BWANA akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari. Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.

ni baada ya israel kushuhudia tukio hili kubwa la kushangaza na utaratibu ambao Mungu aliutumia kuwapigania israel, Waliimba nyimbo za furaha na sasa walianza kumtambua Mungu kama Mtu wa vita , watu wengi wanamjua Mungu kama Mwingi wa rehema na fadhila, wanamjua kama Mungu wa upendo lakini hawajui pia kuwa Bwana ni Mtu wa vita  A man of war” “warriorsasa basi kwanini linatumika jina Mtu kwa kawaida Mungu sio mtu lakini kwanini hapa linatumika neno Mtu? Biblia ya kiebrania inatumia neno Iyshlinasomeka ishi ambalo maana yake ni Mwanaume, kwa hiyo kiebrania Mwanaume wa Vitalakini vilevile mwanaume ni mtu na neno Mtu linapotumika kwa Mungu linamaanisha Yesu Kristo ambaye yeye ni jemadari wa vita ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Mbinguni, Yesu ana nguvu dhidi ya taifa lolote linalompinga yeye, anauwezo dhidi ya yeyote anayesimama kinyume na kusudi lake anauweza na nguvu za kupigana kinyume na yeyote anayeshindana kinyume na agano lake, hakuna mtu, wala mfalme wala rais, wala taifa, wala mamlaka wala wakuu wa giza wala majeshi ya pepo wabaya yanayoweza kupambana naye yeye ni Mtu wa vita israel waliona hili alipowapigania

Farao alifanya ujinga kuamuru majeshi yake kusonga mbele alipaswa kuwaonya mapema warejee nyumbani lakini kwaajili ya kiburi na ubishi aliendelea kupambana na kuwafuatia israel Mungu alimuonyesha uwezo wake wa ajabu wa kupambana Mungu alimtia fadhaa, mungu alichomoa magurudumu yao Mungu alirejesha maji ya bahari mungu aliwafutilia mbali

Jinsi Bwana anavyopigana vita

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu hapigani au hapiganii mtu au watu hovyo hovyo tu, kama watu wengi wanavyofikiri Mungu hupigania watu wake katika medani ya uadilifu na haki kwa njia ya  juu sana  Kumbukumbu 32:4 Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; Maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, Yeye ndiye mwenye haki na adili.kwa msingi huo ili Mungu akupiganie kwanza ni lazima uzingatie maswala kadhaa yafuatayo;-

1. Lazima ujue Bwana yuko upande wa nani!

Maandiko yanasema Bwan akiwa upande wetu Ni nani aliyejuu yetu? Warumi 8:31 Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?kwa hiyo swali kubwa unapohitaji msaada wa Bwana kwanza ni lazima ujue uko upande gani na Bwana yuko na nani Joshua 5:13-15 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake? Huyo amiri wa jeshi la Bwana akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo.”  Hapa Yoshua anatokewa na yule mtu mume yule mtu wa vita amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Bwana na Yoshua anauliza swali la Muhimu sana uko upande gani, kwanini swali hili ni la Muhimu kwa sababu watu wote ni mali ya Mungu Mungu ni Mungu wa wote wenye mwili, kwa hiyo unaweza kudhani yuko na wewe kumbe hayuko nawe, ni hatari kupigana upande ambao Bwana yuko kisha wewe ukawa kinyume naye kwa hiyo ili uweze kushinda ni lazima uwe upande wake na Bwana awe pamoja nawe hii ni kanuni muhimu sana Kumbukumbu 1:42-45 Bwana akaniambia, Uwaambie, Msiende, wala msipigane; kwani mimi si kati yenu; msije mkapigwa mbele ya adui zenu. Basi niliwaambia, msinisikize, bali mliasi amri ya Bwana, mkajikinai, na kukwea mlimani. Na Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo, waliwatokea juu yenu, wakawafukuza, kama wafukuzwao na nyuki,

wakawapomoshea Seiri mpaka Horma. Mkarudi mkalia mbele za Bwana; Bwana asiisikize sauti yenu, wala hakuelekeza masikio yake kwenu.

 unaweza kuona unapomtaka Bwana akupiganie kanuni ya kwanza Lazima Bwana awe upande wako na ndio maana watu wengi waliokuwa hodari wa vita kama Daudi mara kadhaa kabla ya kupigana vita ya aina yoyote waliuliza kwa Bwana kutaka kujua kuwa yuko na nani ona 2Samuel 2:1 Ikawa baada ya hayo, Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Niupandie mji wo wote wa Yuda? Bwana akamwambia, Haya! Panda. Daudi akasema, Niupandie mji upi? Akasema, Hebroni.

 na 2Samuel 5:19 Basi Daudi akauliza kwa Bwana, akisema, Je! Nipande juu ya Wafilisti? Utawatia mkononi mwangu? Naye Bwana akamwambia Daudi, Panda; kwa kuwa hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.

unaweza kuona kwa msingi huo kila mtu ambaye anataka Mungu ampiganie ni lazimaahakikishe kuwa Mungu yuko upande wake na ili Mungu awe upande wako ni lazima uishi maisha matakatifu, na yanayompendeza yeye nhuku ndiko kupigana katika mapenzi yake vinginevyo kichapo kitakuhusu.

2. Mungu hupigania mtu mwenye kusudi lake

Wako watu ambao wanabeba kusudi la Mungu, na umuhimu wao unakuwa ni mkubwasana katika macho ya Mungu kutokana na lile kusudi wanalolibeba, kama utapigana na mtu mwenye kusudi la Mungu, haraka sana Mungu atakuondoa wewe na atamuacha mtu mwenye kusudi lake aendelee kuwepo Matendo 5: 38-39 Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.unaona Mungu hupigania mtu au watu ambao ana kusudi nao na kama utapambana na mtu mwenye kusudi la Mungu Mungu haoni vibaya kukushughulikia vikali yeye makusudi yake hayawezi kuzuilika hata kidogo ona Ayubu 42:2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.kwa msingi huo kama mtu anapigana na Kanisa au israel au mtu mwenye kusudi la Mungu ni wazi kuwa unaweza kujikuta unapamba ana Mungu na ukasambaratika vibaya watu kama Ibrahimu, Isaka, Yakobo, Daudi na kadhalika ambao walikuwa wanabeba kusudi la Mungu ndani mwao, Mungu huingilia kati na kuwatetea sio kwa sababu wao ni wema sana bali kwa sababu wanakusudi lake ndani yao.

3. Mungu hupigania watu wanyonge wasioweza kujitetea

Mtu awaye yote ambaye ni masikini, mjane au yatima Zaburi 140:12 Najua ya kuwa Bwana atamfanyia mnyonge hukumu, Na wahitaji haki yao.Wanyonge masikini na wajane na yatima hutetewa na Mungu kwa msingi huo neno la Mungu linaahidi kuwa awaye yote atakayewadhulumu atapata hasara kubwa sana Mithali 22:16 Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara. Mungu anachukizwa sana na dhuluma na uonevu hususani dhidi ya masikini unapoingia katika vita na watu wa namna hii ambao hawana uwezo wa kujitetea kutokana na unyonge wao basi ujue unapambana na Bwana ! Mithali 22:22-23 Usimnyang'anye maskini, kwa kuwa ni maskini; Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni; Kwa sababu Bwana atawatetea; Naye atawateka uhai wao waliowateka.Mungu hawezi kuvumilia uonevu wa mtu mnyonge hata kama Mtu huyo yuko mikononi mwa mtu wa Mungu, Kuna wakati Sara alimtesa hajiri sana mpaka hajiri akakimbia jangwani, Sara alikuwa tajiri na hajiri alikuwa mtumwa wake kwa msingi huo sara alifikiri ya kuwa ana hati miliki ya Mungu, Kumbe Mungu huweza kujali na kutetea yoyote amtakaye ona Mwanzo 16:1-10 Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake. Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. BWANA na ahukumu kati ya mimi na wewe. Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake. Malaika wa BWANA akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri. Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai. Malaika wa BWANA akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake. Malaika wa BWANA akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.

4. Mungu hupigania watu wanyenyekevu /wapole.

Ogopa sana Mtu anayejishusha au mtu mpole ambaye yeye anamuachia Mungu tu kila kitu ili Mungu aingilie kati na kumtetea, Katika neno lake Mungu ameahidi kumwangalia mtu mnyonge ona Isaya 66:2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.Mungu hana muda na mtu mwenye kiburi, unapokuwa na kiburi haraka sana unanyimwa neema na kupingana na Mungu ona Yakobo 4:6 Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. mtu mnyenyekevu au mpole sana unapoingilia kati na kumsumbua Mungu ndiye atakayejibu kwa niaba yake ona Hesabu 12:1-10 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi. Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao. Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi. Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje. Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, Bwana, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake. Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.

5. Mungu hupigana kwaajili ya Jina lake takatifu

Kuna mambo Mungu anaweza kuyafanya katika maisha yetu kwa sababu tu tunabebajina lake Zaburi 23:1-3 Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.”  Kama ikitokea kuwa Mungu anaona jina lake linachafuliwa, Yeye amejikuza sana Duniani na jina lake amelitukuza mno Walawi 22:32 Wala msilinajisi jina langu takatifu; lakini nitatakaswa mimi katika wana wa Israeli; mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi,Inapotokea mtu anafanya mambo ya ajabu ajabu kisha anajivunia upuuzi wake kuliko jina la Mungu aliyehai Mungu husimama na mtu amabaye anajua kupitia yeye jina lake litatukuzwa ona 1Samuel 17:45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.

6. Mungu hupigana kwaajili ya masihi wake.

Watu waliotengwa kwa kusudi la kumtumikia Mungu huwa wanapakwa mafuta kwa kazi hiyo na maandiko huwa yanasema mtu akimtumikia Mungungu atamuheshimu ona Yohana 12:26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.wote wanaomtumikia Yesu, baba huwaheshimu sana Mungu hataacha heshima ya watumishi wake ivunjwe kwani kuvunjwa heshima ya watumishi wake ni kuvunjiwa hehsima yeye  ona Zaburi 105:14-15 Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.unapopambana na mtu wa Mungu na hasa aliyepakwa mafuta mwisho wa siku wewe ndiye utakayepondwa na kupigwa radi kisha Mungu ataitukuza pembe ya masihi wake 1Samuel 2:10 Washindanao na Bwana watapondwa kabisa; Toka mbinguni yeye atawapigia radi; Bwana ataihukumu miisho ya dunia; Naye atampa mfalme wake nguvu, Na kuitukuza pembe ya masihi wake.

Muhimu.
Mungu anaupendo mwingi na mkubwa sana na wala hapigani pasipo sababu, awaye yote akipigana na Mungu atakufa haraka sana, Na ndio maana Mungu sio mwepesi wa hasira wala hahesabu maovu yaya anatoa mwaliko kwa kila mtu kumjia kwa dhati na kumtegemea na kumtumainia kwa moyo wa dhati na yeye atakuwa pamoja nasi wakati wote tutakapomuomba Mungu atatusikia kama tutakuwa pamoja naye na kuishi kwa mujibu wa kanuni zake, Yeye ni Mtu wa vita lakini hapendi vita lakini uko wakati Mungu hupigana au hupigania watu wake kwa sababu kadhaa wa kadhaa zaidi ya zile zilizotajwa hapo juu hivyo kaa katika kusudi la Mungu uweze kutetewa na Mungu!

Na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Samuel Kamote

0718990796.