Jumanne, 26 Julai 2016

Ujumbe: Kikombe Changu Cha Uaguzi!


Mwanzo 44:1-5 Biblia inasema Hivi “1. Akamwamuru yule msimamizi wa nyumba yake akisema, Jaza magunia ya watu hawa chakula kwa kadiri wawezavyo kuchukua, utie na fedha ya kila mtu kinywani mwa gunia lake. 2. Na kikombe changu, kikombe kile cha fedha, ukitie kinywani mwa gunia la yule mdogo pamoja na fedha ya nafaka yake. Akafanya kama vile alivyomwambia Yusufu. 3. Asubuhi kulipopambazuka, hao watu wakapewa ruhusa, wao na punda zao. 4. Na walipotoka mjini, wala hawajaendelea sana, Yusufu akamwambia yule msimamizi wa nyumba yake, Ondoka, uwafuate watu hawa, nawe utakapowapata, waambie, Kwa nini mmelipa mabaya kwa mema? 5. Je! Kikombe hiki, sicho anyweacho bwana wangu? Naye hufanya uaguzi kwa hicho. Mmefanya vibaya kwa kufanya hivi.” 

 kikombe cha uaguzi hakikuhusu maswala ya uchawi bali kilihusu upambanuzi wa Kimungu kuhusu badiliko la Ndugu zake yaani wana wa Israel


Leo tunataka kuchukua Muda kujifunza kwa undani kutoka katika kifungu hicho hapo juu cha maandiko, Ni muhimu kufahamu kuwa watu wengi sana wanapenda sana Mungu awabariki na kuwafanyia mambo mazuri, huku wanasahau kuwa Mungu naye anahitaji mambo Fulani ya muhimu kutoka kwetu ili atubariki na kutimiza ahadi zake na makusudi yake kwetu. “Kama tukimpa Mungu yale anayoyahitaji kwetu, Mungu atatupa lolote tulitakalo kwake” alisema Muhubiri Mkubwa mwenye asili ya Afrika TD Jakes.

Katika kifungu hiki cha maandiko wote tunakumbuka Vizuri Habari ya Yusufu, tunakumbuka wazi jinsi Yakobo alivyompenda sana Yusufu, tunakumbuka jinsi ndugu zake walivyomchukia na kumtendea mabaya, tunakumbuka uchungu aliokuwa nao Yakobo kwa kumpoteza Yusufu, aliomboleza maombolezo makubwa sana kumpoteza Yusufu, na sasa upendo wake mkubwa umeelekezwa kwa Benjamin, ambaye Yakobo alimtoa kwa shida sana akihofia kuumia moyo kama alivyompoteza Yusufu aliogopa sasa asimpoteze Benjamin.Wakati umefika sasa Yusufu aliyetunzwa na Mungu huko Misri kwa muujiza mkubwa sasa anataka kujifunua kwa ndugu zake amekwisha kuwahoji mengi na kuwajaribu kwa namna nyingi sasa anataka kujifunua kwao, lakini anataka kujua Je Ndugu zake wamebadilika? Atajuaje sasa anatumia Kikombe cha Fedha kupambanua mabadiliko yao huu ndio mpango wake kupitia kikombe hiki je kikombe hiki kilihusu nini?

1.      Mpango wa siri wa kutafuta uhakika  
·        Yusufu na Ndugu zake walikuwa na wakati mzuri wa kufurahi pamoja Mwanzo 43:31-34 Ndugu zake bado hawajamfahamu kuwa ni Yusufu, lakini yeye amekwisha kuwajua na kupata uhakika, anawajua vilivyo kuliko wao wanavyo mjua, Mfano walipokuwa wakila aliwapanga kwa kufuata umri wao kuanzia mkubwa hata mdogo, Mwanzo 43:33, Benjamini alikuwa amependelewa kwa chakula kingi mara tano zaidi ya nduguze Mwanzo 43:34.

·        Siku ya pili baada ya karamu kila mmoja akiwa na furaha na uhakika kuwa wamemthibitishia waziri mkuu wa Misri kuwa wao sio wapelelezi, na kuwa wamefanikiwa kumuokoa Ndugu yao Simeon ambaye alikuwa amefungwa kwa muda na kuwa wanarudi nyumbani wakiwa na Benjamin ambaye Yuda alimuapia baba yake kuwa atahakikisha anamrudisha mtoto Mwanzo 43:3-10.

·        Sasa wanarejea nyumbani asubuhi mizigo ikiwa juu ya punda zao na mbegu na chakula, hawana mashaka wamejawa na furaha  wanafikiri kufika nyumbani na kuungana na familia zao na watoto wao, wanafurahia mafanikio yao nay a safari yao, Lakini hawakuwa wanajua kuwa Mungu yuko nyumba ya mambo anataka kuwakutanisha na dhambi yao waliyoifanya miaka 22 takribani iliyopita

·        Wakati wanajiandaa kuondoka Yusufu anamtuma mtumishi wake kuwaandalia nafaka na kuwapatia kadiri wawezavyo kubeba, alimwambia pia awarudishie na fedha zao walizolipa kwa nafaka, lakini Yusufu alimwambia Mtumishi wake afanye jambo geni zaidi, kuweka kikombe chake cha fedha katika mzigo wa Benjamin mdogo wake wa kunyonya hayo yalifanyika wakiwa bado hawajaondoka

·        Baada ya kuwa wamefika mbali Yusufu anamtuma mtumishi wake kuwakabili na kuwahoji kwa nini wamelipa Mabaya kwa mema? Wao walikuwa na uhakika kuhusu haki yao, walikuwa na uhakika kuwa hawakuwa wezi kwa vile walirejesha fedha zote ambazo waliwekewa mwanzoni na hivyo hawakuwa na sababu ya kuiba kikombe cha Yusufu cha fedha na hatimaye kwa kujiamini waliapa kuwa  swa atakayekutwa na kikombe chako cha fedha na afe! Na sisi tutakuwa watumwa wa wamisiri

·        Hili lilikuwa jambo geni sana kufanywa na Yusufu Mungu alikuwa anamtumia Yusufu kuwarejesha ndugu zake katika toba ya kweli, wao walikuwa wamemtenda mabaya Yusufu lakini Yusufu alikuwa anawalipa Mema, Ni lazima tukumbuke kuwa katika maisha haya hakuna jambo linalotokea kwa bahati mbaya kila jambo linalotokea katika maisha yetu ni mpango kamili wa Mungu nyuma yake Warumi 8:28Nasi twajua yakuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema wale walioitwa kwa kusudi lake” Mungu hufanya kazi kwa kusudi la kutuleta katika mapenzi yake njia zake ziko juu sana Isaya 55:8-9Maana mawazo yangu si mawazo yenu wala njia zenu si njia zangu asema Bwana kwa maana kama vile mbigu zilivyo juu sana kuliko nchi kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu na mawazo yangu kuliko mawazo yenu” Jambo hili Mungu hulifanya pia anapojihusisha na tabia zetu mbaya anapotaka kutubadilisha na kutuleta katika toba

·        Uko wakati ambapo tunaweza kujisahau katika maisha yetu na tukaendelea kuishi maisha ya dhambi na tukaona Mungu yuko kimya kama hashughuliki namaisha yetu wala hajatughadhabikia wala kutuonya tukaendeleza tabia Fulani kama kawaida na tukaona Baraka zake huku akitufanikisha na kukutana na mahitaji yetu, akitutumia na watu wakibarikiwa na kila huduma tuifanyayo, Ukweli unabaki kuwa Mungu anajua ni namna gani atatuagua atatutibu tatizo letu anajua namna anavyoweza kukutana na kuzungumza na mioyo yetu, na hapo ndipo hufikia wakati nanabana kifungi Fulani maalumu kutunyenyekesha na kutuleta katika toba

·        Kikombe cha uaguzi cha Yusufu kilikuwa ni kibano cha dakika za mwisho cha kuwapima wana wa Israel kama wametubu, wamebadilika, wanampenda baba yao ambaye walikuwa wamemdanganya kuhusu Yusufu, walikuwa wanampenda Benjamin ambaye sasa anapendwa na baba yao zaidi baada ya Yusufu, wanampenda Benjamini ambaye ni mtoto wa raheli kama Yusufu, wanawajibika kiasi gani kwa familia zao, ndugu na baba yao.

·        Mungu anajua namna ya kutuleta katika ukamilifu, anajua namna ya kupima mioyo yetu kujua tumekuwa kiasi gani na kubadilika kiasi gani, na ili atupate anajua ni wapi akuweke katika kibano ambacho kitakuleta katika toba na badiliko la kweli, ni Mungu anayejua namna ya kuweka kikombe chake cha uaguzi katika gunia lako.

·        Hatuwezi kumficha Mungu maisha yetu kwa muamini au mkristo anayejua wajibu wake na mwenye kufikiri sawa sawa ni lazima akubali kutubu haraka Mithali 28:13 afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali aziungamayena kuziacha atapata rehema, Tukiziungama dhambi zetu yeye ni mwaminifu na wa haki anatusamehe 1Yohana 1:9, tukikataa toba na kubadilika gharama itakuwa kubwa kuliko tunavyoweza kufikiri, Waebrania 12:6-11 Mithali 13:15

·        Mungu alikuwa anatafuta uhakika wa mabadiliko katika maisha ya wana wa Israel, alitaka waonyeshe kuwa wamebadilika toba sio maneno ni vitendo ni mabadiliko makubwa katika maisha yetu, kama hatubadiliki kila wakati tutajikuta katika marudio ya mitihani ileile katika nmaisha yetu.

2.      Mpango wa Mungu wa kuwakabili
·        Magunia yalifunguliwa wana wa Israel walikuwa na uhakika hawana hatia wanasimama wakijiamini na wakiwa na nyuso za furaha kila mmoja anasaidia kufungua gunia lake  kwa ujasiri na sasa wanafika gunia la Benjamin hali inabadilika wanakuta kikombe cha fedha cha Yusufu katika namna isiyoweza kuaminika walipigwa na Butwaa!!!

·        Huu ni wakati wa majuto na ukweli sasa ni kipimo cha mwisho cha Yusufu kwa ndugu zake wakati woote Yusufu alikuwa anawajaribu ili kuona je kuna mabadiliko?
-         Walimleta Benjamin kama alivyowaagiza Mwanzo 43:15-16
-         Walirejea kwaajili ya kaka yao Simeon Mwanzo 43:23
-    Walirejesha Fedha yoote waliyokuwa wamezidishiwa na kurejeshewa katika magunia yao Mwazno 43:20-22

·        Haya yote yalikuwa ni majaribio, ni mkiaka karibu 22 imepita walimchukia Yusufu sana walimshambulia walimtupa katika shimo, walimuuza utumwani, walimuhuzunisha baba yao walimvinja moyo, walimuambia uongo kuhusu kilichomtokea Yusufu, walifanya msiba pamoja naye kama kwamba amekufa walipatana kwa nia moja kunyamaza kimya siku zote, walikaa na uongo huo kwa muda wote huo, sasa wangekuwa na nafasi nyingine ya kufurahia kifo cha mwana mwingine wa Raheli, Kwa vile sasa ni wazi kuwa Benjamin anapendwa sana na baba yao kama alivyopendwa Yusufu Mwanzo 42:36, 43:13-14, labda wakati huu wangeruhusu Benjamin kupatwa na mabaya kama ilivyokuwa kwa Yusufu, wangejirudia tu nyumbani, wangeuumiza tena moyo wa baba yao ambaye amevumilia maumivu ya kupotelewa na mwanae kwa miaka yote hiyo bila kujielewa Yusufu alikuwa anapata picha kuwa Ndugu zake wamebadilika sana wamekuwa watu wengine sasa wako tayari hata kufa hata kuwa watumwa ndugu zao na baba yao awe na furaha 

·        Hawakutaka hata kumuuliza Benjamin kikombe kimefikaje kwako, hawakutaka hayt kumkemea kwanini umechukua kikombe cha watu, walikuwa tayari kubeba mzigo wa Benjamin hata ikiwezekana kufa ili kuokoa maisha yake na baba yao, wako tayari kubeba hukumu bila kujali Benjamin alifanya nini, wameacha ubinafsi, wameacha uongo, wameacha kupenda fedha, wanalia kwa huzuni, hawamlaumu yoyote wakati huu

·        Huu ndio wakati ambao Mungu anausubiri kwa kila mmoja wetu, kuwa tayari kufanya mambo sahihi na kwa njia sahii, wana wa Israel wamekomaa sasa hawahukumu wengine, hawahukumiani tena, hawachekani, wako tayari kubeba tatizo lao kama la mtu mmoja, wako tayari kuwa wakeli hata kama ukweli utawagharimu

·        Ndugu yangu mpendwa Mungu anakusubiri ufikie wakati ambapo huwezi kumtupia mwingine lawama, wala kumsingizia mwingine tatizo kwa kushindwa kwetu kuwajibika, anataka tufikie wakati ambapo tutakuwa tayari kukabiliana na dhambi zetu wenyewe na kuzikiri na kuzitubu na kuziacha na kubadilika.

·        Mungu anatutaka tufikie wakati ambapo hatutanyoosha vidole kwa wengine, dhambi zetu sio za wazazi wetu, wala wake zetu, wala waume zetu, hakuna wa kulaumiwa Mungu anatusubiri tufikie ngazi hii ya kujitambua ndipo anapoweza kujifunua kwetu, Mungu anataka tufikie ngazi ya kuweza kuwa wakweli hata kama kweli hiyo itatugharimu

·        Mungu haogopi kuifunua dhambi yetu wazi kwetu ili kwamba tuweze kufikia toba, Mungu anapotutaka tumgeukie atatumia kila analoliweza kuhakikisha kuwa anarudisha uhusiano wetu nayeye, Ndugu zanhgu Dhambi si ya kucheza nayo, sio ya kuirudiarudia ni lazima itubiwe mara moja, kwa ukamilifu na uaminifu, hapo ndipo Mungu anapoweza kutusamehe, kutubariki, kujifunua kwetu na kuonyesha nguvu zake

3.      Mpango wa Mungu kuwarejesha katika toba
·        Sasa wana wa Israel wanarejea ikulu kwa Yusufu hapo hajajifunua kwao bado, Yusufu alikuwa anasubiri sasa kujifunua kwao, anataka kuona mabadiliko, je atamuona Benjamin peke yake? Maana ndiye aliyewekewa kikombe cha uaguzi, njia hii ilikuwa ni ya kumlinda Benjamin kutoka kwa ndugu zake kama wanekuwa hawana mabadiliko.

·        Walipotokea wote walimsujudia hata chini wakiitimiza ile ndoto ya Yusufu alipokuwa kijana Mwanzo 37:5-11, Yusufu anawauliza kuhusu kikombe chake cha fedha, na anawaambie hamkujua ya kuwa naweza kufanya Uaguzi?

·        Ni muhimu kufahamu kuwa Yusufu hakuwa muaguzi wala hakufanya uaguzi kabisa, lakini uaguzi na ramli lilikuwa ni jambo la kawaida la wamisri na waaguzi walitumia kikombe cha Fedha na kukiweka divai na shanga za thamani na walitumia kusoma maisha ya watu, Yusufu hakufanya uaguzi huo lakini hapa alikuwa anawajua ndugu zake vilivyo, alifahamu sana matendo yao mabaya na tabia zao zilizokuwa za kutomkumjali Mungu, alitaka kujua kuwa Baba yake sasa amewafunza neno la Mungu na kuwa huenda je sasa wamebadilika au bado baba hana watu hapo ? Kitendo cha Yusufu kutambua kila kilichokuwa kinaendelea na wao kutokutambua, kitendo cha wao kuonyesha badiliko kubwa hata wakiwa mbali ambako watu hawawaoni kilionyesha uaminifu ulio wazi kuwa ni kweli wamebadilika je ni wangapi wanaweza kufanya uovu hata wakiwa katika miji au nchi ngeni ambako huko hakuna anayewajua? Yusufu alikuwa akifanya kile ambacho Mungu alikuwa anamuongoza kuwaleta nduguze katika ukamilifu wake

·        Yuda alikuwa wakwanza kujitokeza mbele na kuzungumza maneno ya muhimu sana katika neno la Mungu ni maneno yanayoonyesha kuwa ni moja ya watu waliobadilika sana
·        Alikiri wazi kuwa wamefanya dhambi alisema Mungu ameona uovu wao, alisema sisi sote nay eye aliyekutwa na kikombe chako ni watumwa wako, alitambua kuwa Mungu alikuwa akiwahukumu kwaajili ya dhambi, kitendo cha kuwa Mwenye kikombe anataka aliyekutwa na kikombe awe mtumwa wake, kilimkumbusha wazi kuwa ni ile dhambi ya kumuuza ndugu yao utumwani Misri sasa kimewageukia, alikubali kuwa yeye na ndugu zake wote ni watumwa tu Mwanzo 45:16
·        Yusufu alikataa wao kuwa watumwa wake aliwataka wote kuendelea na safari isipokuwa yeye aliyekutwa na kikombe chake cha uaguzi tu Mwanzo 45:17
·        Mwanzo 45”18-34 Ni maandiko yenye maneno mazito ya Yuda, alimkubusha Yusufu kuwa sababu ya kuja na Benjamin ilikuwa ni kwa vile yeye alikuwa amewaagiza 19-23 Yuda alimueleza Yusufu kuwa Baba yao Yakobo angekufa tu kama Benjamin atapatwa na mabaya ndiye mwanaye mdogo naye anampenda 24-31, kisha Yuda alisema yeye yuko tayari kuchukua nafasi ya Benjamin, alikuwa tayari kubaki Misri kama Mtumwa ili kwamba Benjamin aweze kurudi kanaani na ndugu zake 32-34, Moyo wa Yuda unakuwa kama wa yesu Kristo yuko tayari sasa kubeba adhabu ili ndugu zake na baba yake wawe na amani na furaha
·        Huu ulikuwa ni kama wakati muafaka ambao Yusufu alikuwa akiutazamia alithibitisha wazi kuwa wamebadilika sana
·        Wako na umoja kama mtu mmoja, wako tayari wameiva Yuda yuko tayari kuchukua nafasi ya Benjamin na kumpendezesha baba yake, hapa ndipo mambo yalipobadilika Ukiri wa Yuda ulionyesha wazi kuwa amebeba majukumu makubwa ya kuwajibika kwaajili ya familia yake hakuna ubinafsi ndani yake yuko tayari kupoteza kila kitu, kumbuka alikuwa na watoto na mke na mali zake lakini alikubali kubaki Misri kama mtumwa ndugu yake awe huru, aidha amefanya dhambi au hakufanya, na aliweza kuwaza moyo wa baba yake, kutokana na hali hii Yusufu alishindwa kujizuia na alijifunua kwa Ndugu zake Mwanzo 45:1-4

·        Kwa ujumla kuna jambo la kujifunza kutoka kwa Yuda ni wazi kuwa dhambi yoyote ile ni matokeo ya ubinafsi na choyo na umimi, kadiri mtu anavyokuwa mbinafsi ndivyo na dhambi yake ilivyo, dhambi yoyote inayotendwa na wanadamu ni matokeo ya ubinafsi na kujihurumia, toba halisi inaonekana pale tunapoanza kujali wengine na kuweza kukubali kuwa tayari hata kujidhabihu kwaajili yaw engine kumbuka siku zote asili ya dhambi zote ni ubinafsi Isaya 14:12-15, 1Yohana 2:16

·        Tunapofanya dhambi huwa hatuko tayari kujali madhara yake tunajitoa kikamilifu kuasi kwa sababu ya ubinafsi, tunaweza wakati mwingine kutubu au kuogopa dhambi au kunyenyekea kwa sababu ya kuogopa aibu au kushikwa tu, Mkristo aliyekomaa anaiangalia dhambi kwa mtazamo zaidi ya huo, kuwa ina madhara kwa jamii, kanisa na familia nay eye mwenyewe na kazi ya mungu pia njia pekee ya kuikabili dhambi na kukubali kulipa gharama na kuwa wakweli kwa Mungu na nafsi zetu hata kama itatugharimu hivi ndivyo Yuda alivyofanya

·        Watu wengi wanataka Baraka za Mungu na Mungu amekuwa mvumilivu kwetu kwa miaka mingi, inawezekana unawacheka hata wale waliotengwa makanisani kwa kubainika kuwa ni wenye dhambi lakini wewe una za kwako haijawahi kuonekana lakini kiko kikombe cha uuguzi cha bwana kiko katika gunia lako atakubana tu ni vema sasa ukabadilika na kuacha dhambi na kuwa tayari kwa gharama yoyoye kuwa mbali na Ubinafsi na Yesu atajifunua kwako na kukupa memma ya nchi na kukuhifahdi na kukualika katika furaha yake, Yuda alitambua kuwa hawakuwa wamemfanyi Yusufu mabaya walijua kuwa wamemkosea Mungu, ni muhimu kwako kujitathimini yale unayowafanyia wengine kuwa unamkosea Mungu.
·        Je unakua kiriho?
·        Je una dhambi unapaswa kuitubu?
·     Je unaogopa hukumu ya Mungu (kikombe cha Fedha cha uaguzi) Badilika leo na Bwana takaubariki sana na kukustawisha sana.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev Innocent Kamote.

Alhamisi, 21 Julai 2016

Ujumbe: Kustahimili Mapingamizi makuu


Waebrania 12:3
Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.

Ulimwengu huu ni ulimwengu wa mapingamizi, ni ulimwengu ambao kadiri kunavyokucha vipingamizi vya aina mbalimbali, Yesu aliweza kuyashinda mapingamizi nyote na ndio maana mwandishi wa kitabu cha Waebrania anataka tumtafakari sana Yesu ambaye alishinda mapingamizi makuu sana 

 "Dhoruba Katika Maisha zisikubabaishe na kukusumbua Yesu alizishinda mtafakari yeye"

Ulimwengu huu tulionao ni ulimwengu ambao unazidi kuwa wenye kutisha siku hadi siku na watu wanapoteza matumaini kabisa  Jonathan Park alitunga shairi hili kuuzungumzia ulimwengu huu na kusema 

·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali Fulani amepoteza tumaini
·         Ni ulimwengu ambao mtu fulani mahali Fulani Ndugu kwa ndigu wanauana
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali Fulani anauawa kwaajili ya ngozi ya ragi yake
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali fulanmi anaona Fedha ni za muhimu kuliko imani, familia na marafiki
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani serikali inatumia nguvu zake kuwatendea mabaya raia wake
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani hawaruhusiwi hawaruhusiwi kuabudu Mungu au imani uitakayo
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anamuua mwingine kwa jina la Allah
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anamuua mwingine kwa jila la Mungu
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani sehemu Fulani huwezi kutembea bila milio ya risasi kusikika
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anakimbia nchi yake kutafuta maisha
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anakimbia nchi yake na anakumbana na kifo
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani baba anamtandika mtoto wake mpaka hawezi kutembea
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mama anamtupa mtoto wake wa kuzaa kwa vile eti hawezi kumtunza
·         Ni ulimwengu ambao maneno ya mtu au ahadi za mtu zimekuwa sio za muhimu tena
·         Ni ulimwengu ambao mwalimu anamwambia mwanafunzi huwezi kitu kabisa
·         Ni ulimwengu ambao watu wanasalitiana na marafiki wanakuwa maadui
·         Ni ulimwengu ambao vijana wanakata tamaa na kujiua
·         Ni ulimwengu ambao unakimbilia polisi au mahakamani upate haki unaishia kudhulumiwa
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani anapatwa na mabaya wengine wanafurahi
·         Ni ulimwengu ambao unamwahisha mgonjwa hospitali ili kuokoa maisha yake anakufa kwa kukosa huduma za wahudumu wasio na haraka
·         Ni ulimwengu ambao mjomba anamuharibu mtoto wa dada yake mwenyewe kwa ulawiti
·         Ni ulimwengu ambao wanaume kwa wanaume wanaoana na wana wake kwa wanawake
·         Ni ulimwengu ambao watu hawaaminiani tena 

Hi jinsi gani tunaweza kustahimili hali hizi zote zenye kukatisha tamaa? 2 Timotheo 2:3, 8 Biblia inasema hivi “Ushiriki taabu pamoja name kama aksari mwema wa Kristo Yesu; Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu”

Kwa nini maandiko yanatutaka tumtafakari Yesu tunapopitia mambo magumu  ni kwa sababu sehemu Fulani hapa ulimwenguni kuna tumaini tumaini hilo linapatikana kwa Yesu, kama sehemu moja ya ulimwengu ni Gisa sehemu ya pili kuna Nuru Yesu ni Nuru ya Ulimwengu  Yohana 1:5 “ Nayo Nuru yang’aa Gizani, wala giza halikuiweza, Yohana 12:46 “ Mimi nimekuja ili niwe Nuru ya ulimwengu, ili kila aniaminiye mimi asikae gizani”

Tukiyafikiria haya tunaweza kuzimia mioyoni mwetu, yaani tunaweza kukata tamaa na kuona kuwa ulimwengu umekuwa sio mahali salama tena pa kukalika lakini tukimtafakari sana Yesu ambaye alishindamap[ingamizi makuu namna hii, Hatutachoka wala kukata tamaa wala kuzimia moyo.

Jumatatu, 18 Julai 2016

Ujumbe: “Si kwa Uwezo, wala si kwa nguvu bali ni kwa Roho yangu”


Kiini: Umuhimu wa Kumuachia Roho wa Mungu atawale

Andiko la Msingi: Zekaria 4:6-10

.6. Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. 7.Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie. 8. Tena neno la Bwana likanijia, kusema, 9. Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu. 10. Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote. ”


Utangulizi:

Zerubabel alikuwa ni Liwali wa Jiji la Yerusalem baada ya Wayahudi kurudi kutoka Uhamishoni, Jina Zerubabel ni muungano wa Maneno mawili ya Kiibrania Zeri na Babilon ambalo maana yake ni Mzizi au Chipukizi kutoka Babeli, aliteuliwa kuwa liwali wa Yuda na Mfalme Artashasta, liwali huyu alikuwa anakabiliwa na kazi ngumu ya Ujenzi wa Hekalu, Kazi hii ilikuwa ni Mapenzi ya Mungu kabisa na Mungu alikuwa ameweka moyoni mwake  Mzigo wa kulijenga Hekalu, wakati huu kazi ya Ujenzi ilikuwa ngumu sana kuliko wakati wa Suleimani ni muhimu kufahamu kuwa ni kazi rahisi sana kujenga kitu mara moja lakini ni kazi ngumu sana kukirudia, Kazi ilikuwa ngumu na yenye upinzani mwingi sana, Kama ilivyokuwa kwa Nehemia Mungu alipoweka Moyoni mwake kuujenga ukuta wa Yerusalem kulikuwa na upinzani mkubwa sana, Zerubabel hali kadhalika alikutana na upinzani mkali wakati wa kulijenga Hekalu.

Hali halisi ya upinzani ilikuwa Hivi:-

1.      Watu waliokuwa wakiuzunguka mji walijaribu kuwakatisha tamaa, waliwatisha, waliiba baadhi ya vifaa vya ujenzi,
2.      Kila mara tunapojihusisha na kazi yoyote ya Mungu ni lazima shetani atatumia kila mbinu na hila kuharibu kabisa mikakati na mipango ya kimungu na kutukatisha tamaa.
3.      Shetani anaelewa wazi nini kinatokea watu wanapokuwa wamekata tamaa na kujichokea
4.      Watu wanapokata tamaa kumuamini Mungu kunapungua, Mambo yoyote yale yakifanyika katika hali ya hofu na kutokumcha Mungu mafanikio huwa ni madogo sana, Biblia inasema Mungu hakutupa Roho ya woga “2Timoth 1:7” watu waliokata tamaa hudumaa, hawawezi kufanya jambo lolote lile Duniani, ukiwa na jeshi la wanajeshi waliokata tamaa hata uwe na vifaa vya kisasa vya aina yoyoteile ushindi unaweza kuwa ni hadithi ya kusikiliza tu

5.      Shetani licha ya kututishia bali pia atashambulia na kuiba furaha tuliyonayo
6.      Watu walimuacha Zerubabeli peke yake na kila mtu akaanza kuangalia mambo yake na kujenga nyumba yeke mwenyewe na unjezi wa hekalu ukawa umesimama watu walikufa moyo “Mathayo 6:33” Kumbuka jinsi Israel walivyokufa moyo baada ya wapelelezi kuleta habari mbaya ya kuvunja Moyo, walisahahu kabisa kuwa Mungu yuko Pamoja nao, walianza kutumia akili
7.      Zerubabel alikata tamaa kwa sababu alikuwa haoni njia tena maono yake yalianza kufifia na moyo wake ulianza kupoteza matumaini jaribu lilionekana ni kubwa na tayari ujenzi wa Hekalu ulionekana kuwa mzigo na mlima mkubwa ambao sio rahisi kuusawazisha

Ndipo Mungu alipomuinua Nabii Zekaria kwaajili ya kumtia moyo Zerubabel  Na nabii Hagai kwaajili ya kuwatia Moyo wayahudi, Nabii Zekaria alimueleza wazi Zerubabel ujumbe kutoka kwa Mungu kwamba si kwa nguvu si kwa uweza Bali kwa Roho yangu asema Bwana, Mungu aliukemea mlima uliokuwa unamkabili Zerubabel na kuutabiria kuwa utakuwa Tambarare Mungu alimuahidi kuwa macho yake yanazunguka kuangalia duniani kote ni nani anamtumaini yeye na kila anayemtumaini yeye hatata tahayarika

Inawezekana hali kama ya Zerubabel inajitokeza katika Maisha yako, umeanza kukata tamaa,umeshambuliwa na kukosa msaada umeanza kutumia akili zako katikakutatua majaribio yako lakini wiki hii ninazo habari njema kwako kuwa Bwana amenituma nikuambie umtegemee yeye Machjo yake yanaangalia ni nani anamtegemea naye atamruhusu Roho wake mtakatifu kukutia nguvu na kukuwezesha atalikemea kila tatizo linaloonekana kuwa gumu katika maisha yako na litakuwa tambarare, Bwana akubariki na kukuongeza kwa utukufu wake katika Jina la Yesu amen

Ujumbe Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.