Jumatano, 30 Oktoba 2019

Sisi je! Tutapataje kupona, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII?


Andiko la Msingi: Waebrania 2:1-3Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.  Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;”




Utangulizi:

Yesu Kristo alikuja Duniani kwa makusudi makubwa mengi, lakini kusudi kubwa ni ili apate kutuokoka! Luka 10:19Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.” 

Na ndio maana Yesu pia anaitwa mwokozi, ametukomboa katika mambo mengi lakini kubwa zaidi ametuokoa na adabu ya dhambi  

Mathayo 1:21Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.” Kwa hiyo unaweza kuona kuwa kusudi kubwa la Yesu ni kutuokoa na ametuokoa na mambo mengi lakini zaidi sana ametuokoa na Dhambi zetu, kwa nini kuokolewa nadhambi ni kwa muhimu sana kwa sababu kila aina moja ya dhambi tuifanyayo msahara wake ni mauti ona 

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” kwa hiyo kutokana na kuweko kwa dhambi katika nasfi zetu adhabu yake ilikuwa ni kifo, kifo cha mwili huu na kifo cha kiroho ambacho ni kutengwa na Mungu milele lakini Yesu akaja Duniani akatuelekeza njia kwa mafundisho yake akaandaa watu watakaotufundisha neno lake kisha Yeye mwenyewe alikufa kwaajili yetu yaani kwa niaba yetu, ili damu yake itakayomwagika iwe malipo kwa niaba ya damu zetu na hivyo tukimuamini hukumu hii haina nguvu na tunasamehewa na huu ndio wokovu mkuu, kwa hiyo sasa kazi yetu ni kumuamini yeye na kukubali kazi yake aliyoifanya pale msalabani ili tuweze kuwa na uzima wa milele  

Yohana 3:16Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Kwa hiyo wajibu wako mkubwa ni kumuamini yetu, yaani kutambua na kukubali kuwa alikufa msalabani kwaajili yako na yangu na ukifanya hivyo wewe una uzima wa milele.


Kwa nini wokovu ni mkuu?

Hakuna tukio baya duniani au laana mbaya kama kutengwa na uso wa Mungu! Mwanzo 4:13-14. Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.”

 Mara moja mtu anapokuwa dhambini anatengwa na uso wa Mungu anakuwa mtoro duniani na kila kitu kinakuwa adui yake na hata mbu au bacteria wanaweza kukuua ni jambo bay asana kupungukiwa na utukufu wa Mungu ni hasara ya hali ya juu hata kama una heshima kiasi gani kwaajili ya hayo basi Neno la Mungu linatuonya kutokuuchezea wokovu, wokovu ni neema tu sio wote wanaojaliwa kuukubali, sio watu wote watajaliwa kuupata wokovu au hata kuufahamu, ikiwa wewe umepata neema ya kuufahamu basi usiuchezee wokovu ni mkuu mno, msamaha wa dhambi ni baraka kubwa mno kuliko kutolewa gerezani, ndio maana mwandishi wa kitabu cha waebrania ametuonya kwamba tunapaswa kuuangalia sana kuutunza sana wokovu na tusiuchezee 

 Waebrania 2:1-3Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;Kwa nini mwandishi anauona 

wokovu kuwa ni mkuu kwa sababu muhimu zifuatazo;-

Ulinenwa na Bwana mwenyewe, yaani ni zawadi ni mpango  wa Mungu mwenyewe tusingeweza kujisamehesha mbele zake ni yeye mwenyewe kwa hiyari yake aliamua kutusamehe
Umethibitishwa ndani yetu, yaani unapoukubali kwa imani unapewa furaha ya dhati moyoni inayokushuhudia kuwa wewe ni wa Mungu tofauti na jinsi watu wanavyokujua na kukufahamu au kukuangalia

Umethibitishwa kwa ishara na miujiza na Roho Myakatifu, yaani Mungu roho Mtakatifu amewaponya wengi na kufanya miujiza mingi kwa kusudi la kututhiboitishia kuwa kama anaweza kutufanyia ukarimu huumkubwa wa kuiponya miili yetu anashindwaje kutusamehe dhambi zetu miujiza iko ili tupate kuamini kuwa Yesu ni mwokozi, kama watu watafurahia miujiza kuliko kuufurahia wokovu na msamaha wa dhambi watakuwa hawajui thamani ya wokovu Zaburi 103:3Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,” Ni msamaha wa dhambi unaoweza kutuletea pia uponyaji wa mwili na nafsi zetu.

Umegharimu maisha ya mwana wa Mungu, ni kwaajili ya kutuokoa ilimpasa Yesu kufa msalabani kwa kifo cha aibu ili mimi na wewe tuweze kuokolewa kuupuuzia wokovu ni kuidharai kazi ya Yesu aliyoifanya pale msalabani, kurudi nyuma na kuacha wokovu ni kudharau msalaba  Waebrania 6:4-6 Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.” Tabia ya kuendelea kuukataa na kuupinga wokovu na kuidharau kazi iliyofanywa na Yesu msalabani inaweza kutufikisha mahali pabaya sana na huu ndio unaitwa ukengeufu, hii ni dhambi ya mauti, huku ni kushindana na Roho Mtakatifu, hatujui ni lini na wapi mtu anaweza kufikia dhambi hii ngumu lakini jnaanza na kudharau wema wa Mungu hivyo kama hujui wokovu uligharimu nini usiutukane!


Unatupa Uzima wa milele unatuokoa na dhambi mauti na kuzimu , kama tukiukubali wokovu na kuupokea licha ya kusamehewa dhambi zetu kila wakati pia tunakuwa na uzima wa milele lakini Mungu anatulinda na dhambi ya mauti yaani ya kukataa kazi za Roho Mtakatifu na kuipinga zawadi ya wokovu

Tumeokolewa kwa neema !

Kule kuwa mbali na Mungu ni kifo, lakini kupitia wokovu kama tumeuamini ni zawadi kubwa sana kutoka kwa Mungu hivyo hatupaswi kuichezea neema ya Mungu Waefeso 2:1-5Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;  ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.  Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.”


Nimalizie ujumbe huu kwa stori hii 

Mfanya biashara mmoja alikuwa akifanya biashara ya kuuza chumvi, alisambaza chumvi yeke sehemu mbalimbali akitumia punda, kila alipoelekea sokoni ilimlazimu kuvuka  mto ili aweze kuelekea sehemu mbalimbali kwaajili ya kuuza chumvi yake, siku moja punda wake kwa bahati aliangusha mzigo wa gunia la chumvi kwenye mto, na hivyo chumvi iliyeyuka na kwenda na maji kutokana na hali hiyo gunia la chumvi likawa Jepesi, hali hii ilimpa punda yule furaha kubwa mno.

Kwa hiyo punda yule alianza kuwa na mchezo mbaya ilikuwa kila siku akibeba chumvi akifika eneo lenye mto aliliangusha gunia kwa makududi yaleyale, Muza chumvi alijiuliza ni kwanini hali ile inatokea mwisho aliweza kugundua tabia ya punda wake na akakusudia kumfundisha somo, safari moja alimbebesha gunia la Pamba na punda bila kujalia amebeba nini alipofika pale aliliangusha tena gunia la Pamba, akijua kuwa litakuwa jepesi vilevile kama ilivyokua kwa chumvi, lakini mambo yalikuwa tofauti safari hii, gunia la pamba lilikuwa zito mno kuliko maelezo na hivyo punda alipata taabu sana na akaacha tabia yake ya mchezomchezo na mfanya biashara yule akawa na furaha.

Usichezee neema ya wokovu kwa sababu bahati haiji mara mbili, iko siku unaweza kupoteza kila ulichojaaliwa na Mungu na ukajikuta unapata tabu , shika sana ulicho nacho.
Bwana ampe neema kila mmoja wetu asiuchezee wokovu katika jina la Yesu Kristo amen!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye hekima.

0718990796

Jumamosi, 19 Oktoba 2019

Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?





Zaburi 119:9Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.



Ni muhimu kufahamu kuwa mojamya maswali muhimu sana ya kujiuliza au yaliyopatwa kuulizwa katika maandiko ni pamoja na swali hili Jinsi gani kijana aisafishe njia yeke! Swala hili ni nyeti na muhimu mno ni swali la kifalasafa, Katika zaburi hii ya Hekima mwandishi anataka kutuonyesha wazi kuwa mwanadamu anapaswa kuishi maisha yanayompendeza Mungu katika maisha yake yote,lakini katika wakati wote wa maisha ya mwanadamu hakuna kipindi hatari kama kipindi cha ujana kwa hiyo mwandishi ni kama anaziona changamoto za vijana na kisha anahoji akiangalia wakati tulio nao na changamoto walizo nazo vijana Mwandishi wa zaburi hii ni kama anauliza, Je kijana anawezaje kuishi maisha matakatifu kivitendo katika wakati huu wa sasa? Ni kijana moyo wa wakati wa ujana unawaka sana , Shauku ya vijana iko juu lakini wakati huohuo maarifa yao bado ni machanga na pia hawana ujuzi au uzoefu sasa anawezaje kwenda sawasawa ni wakati gani wa kujiuliza swali hili la muhimu? Je ni wakati ambapo tumezeeka au wakati ambapo tumeshakosea sana? Wakati wa ujana ndio wakati muhimu sana wa kujiuliza swali hili ndio wakati wa kuchagua njia itakayokufaana kuiendea , ili kijana asifanye makosa kama makosa yaliyofanywa na wengi waliotutangulia, njia ya kijana ndio inayowindwa zaidi ili iharibike, ni vijana ndio ambao wana muda mrefu zaidi wa kukabiliana na magumu, vikwazo na changamoto, watakuaje na furaha je ni kwa kusubiri waharibu katika ujana wao kisha waje wajute katika uzee wao, wanawezaje kutembea katika njia ya haki? Je mwanzoni mwa maisha yao, au siku zote za maisha yao au mpaka wakati wakiwa wazee?  Wanakabiliwa na magumu sasa ili njia yao iweze kuwa njema tangu awali wanapaswa kutii na kulifuata neno la Bwana!



Neno la Mungu lina ushauri mwingi na wa kutosha namna na jinsi vijana wanavyopaswa kuenenda, Biblia inamtarajia mtu mzee kuwa mwenye hekima kubwa kutokana nay ale aliyojifunza wakati wote wa maisha ya ujana wake, Mzee anapaswa kuwa mwalimu wa vijana Mithali 20:29 “Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.” Biblia inapotaja mvi inamaanisha ukomavu katika ujuzi na uzoefu unaoweza kuwafaa wengine  na nguvu ni wakati wa kutenda vijana wanapaswa kuyatendea kazi maneno ya Mungu na ushauri wake katika neno la Mungu ambao utawapa mwelekeo utakawaosaidia katika maisha yao yote.


Mstari wa msingi una mambo makuu mawili hapa;-
·         Jnsi gani kijana aishafishe njia yake ni swali linaloulizwa toka kwa vijana
·         Kwa kutii, akilifuata neno lako anajibu mtu mwenye hekima
Msingi wa kwanza na ambao ni wa muhimu kwanza ni lifuata neno la Mungu:

a.       Neno la Mungu lina utoshelevu wa ajabu sana wa kuifanya njia ya kijana na mtu yeyote yule kuwa njema, Neno la Mungu lina nguvu ya kutosha katika kuyaongoza maisha yetu na kutuondolea vikwazo, lina uwezo wa kututia nguvu na kutufariji na kutupa msaada wa namna na jinsi inavyotupasa kuenenda hata tukahitimisha maisha haya tukiwa wenye furaha ya ajabu na kuwa walimu wenye busara wakati wa uzee wetu.

1.       Kumcha Bwana ndio chanzo cha maarifa 

Mithali 1:7, “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.” Mithali 9:10-11, ”Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima; Mfundishe mwenye haki, naye atazidi kuwa na elimu; Kumcha Bwana ni mwanzo wa hekima; Na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.” Mithali 15:33 ” Kumcha Bwana ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.” Kumbe basi mtu awaye yote anayetaka kufanikiwa katika njia yake ni lazima kwanza awe anamcha Mungu, awe mtu wa ibada anayemuabudu Mungu, awe mtu anayeishi kwa hofu ya Mungu, Mungu hapaswi kuwa kichaka cha kujichimbia na kuishi kama tunavyotaka Mungu ni lazima apewe kipaumbele cha kwanza katika maisha ya mtu awaye yote na katika ujana wetu hii ndio msingi wa maarifa mema yatakayotusaidia katika maisha yetu ili baadaye tusijute tusiyadharau  maonyo na hekima na adamu tukawa wapumbavu.

2.       Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako

Muhubiri 12:1-7 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;  Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;  Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa; Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani. Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani; Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.” 

 Neno la Mungu linatuasa kwamba wakati wa kumchua Mungi ni sasa, hatuwezi kusubiria mawazo ya kijinga sana kufikiri kuwa tuna muda wa kutosha duniani, ni mawazo ya kijinga kusubiri umche Mungu utakapokuwa mzee, ni uzembe kusubiri wakati ambapo hata biblia itakuwa taabu kuisoma, ni ujinga kusubiri wakati ambapo hata kuhudhuria mikesha itakuwa tabu kwako, ni ujinga kusubiri meno memomonyoka ndio umkumbuke Mungu, lakini neno la Mungu pia linatuonya kuwa mtungi unaweza kuvunjikia kisimani, yaani ule wakati wa muhimu tunaoufikiri lolote laweza kutokea na ukashindwa kutii kiu ya kumcha Mungu ambayo uneiamua leo lakini ikaishia njiani Neno la Mungu linazidi kutuonye kuwa tunaweza kufikiri kuwa wakati wa ujana ndio wakati wa kujipa raha na kujifanyia lolote tunalopenda kulifanya ni wakati wa kuupa moyo wako lolote unalopenda kuupa ni kweli lakini lazima ukumbuke yuko Mungu atakayekuhukumu kwa kila utakalolifanya na ndipo utakapokumbuka kuwa ujana nao ni ubatili na utu uzima pia heri usingepoteza muda wako 

Muhubiri 11:9-10 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni. Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.

3.       Fuata njia ya Mungu

Maandiko bado yanawaasa vijana kufuata njia ya Mungu kwamba nnia ya Mungu itakupa kibali mbele za Mungu na mbele za wanadamu na italeta mafanikio makubwa sio hivyo tu itakupa maisha marefu na yenye furaha  Mithali 3:1-4 “Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani. Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako. Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamuVijana wanaonywa na wenye hekima kwamba wafuate njia za Mungu katika wakati huu wa sasa inaweza kuonekana kuwa ni jambo la kipuuzi na la kijinga na ushamba kuishi katika njia ya Mungu lakini neno lake linatuasa tumfuate nah ii itatupa kupendwa na Mungu na wanadamu na kufanikiwa ni lazima tuliweke neno la Mungu ndani yetu na kuhakikisha kuwa limekaa kwa wingi na kuwa ndilo linalotuongoza akijibu swali alilojiuliza mwandishi wa mashairi yanzaburi ya 119 ana jijibu kuwa ili kija a afanikiwe ni muhimu na lazima afanye yafuatayo Zaburi 119:10-12 “Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi. Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zakoNi vijana wangapi leo wanaweza kuweka nadhiri kama hii? Wanaweza kuamua kwa moyo wao wote kumfuata Mungu? Wanaweza kukubali kunyenyekea chini ya mkono wa Mungu na kukubali kujifunza maagizo yake na kulitunza neno ma Mungu moyoni mwao na kuiogopa dhambi? Nani anaweza kukubali leo kufundishwa amri za Mungu, watu wanaweza kuwa na bidii kujifunza mambo mengine mpaka wanayaweza lakini ni wachache wanaweza kuwa na bidii ya kujifunza neno la Mungu na mari zake.

4.       Mtumaini Mungu katika njia zako zote.

Moja ya tatizo kubwa sana kwa jamii ya vijana ni pamoja na kumuamini Mungu kumtegemea yeye katika njia zetu zote hii nayo ni habari nyingine usifikiri ni rahisi kumtegemea Mungu katika njia zetu zote usidhani ni rahisi Lakini ili tuweze kufanikiwa ni lazima tumtegemee Mungu Mithali 3:5-6 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;  Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.” Mtumaini Bwana lugha njyingine ya kibiblia ni mtegemee Bwana trust him, ushindi wa mwanadamu yeyote yule ahata ka ahayuko sahihi uko katika kumtegemea Mungum bilia inaonyesha kuwa kuna baraka kubwa sana kwa mtu anayemtegemea Mungu na kuna laana kwa mtu anayemteemea mwanadamu, kumtegemea mwanadamu ni pamoja na kujitegemea wewe mwenyewe badala ya Mungu Kumtegemea Mungu kuna baraka kubwa sana Yeremia 17:5-7 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda.Kumtumaini Bwana kunalipa hususani wakati wa ujana Biblia imejaa mifano kibaoya vijana waliomtumaini bwana na Mungu hakuwaacha labda walikuwa wamejifunza Zaburi 125:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.” Shadrak, na Meshack na Aberdnego walikuwa ni mifano ya vijana waliomtegemea Mungu na kamwe hawakuwahi kuytikisika katika imani yao kwa Mungu je ni wakati gani siisi nasi tunaweza kuiga mfano wao je tutasubiri tukiwa wazee? Tutasubiri tukiwa tumechoka? Lazima tuithibitishie Dunia kuwa sisi ni watu wa tofauti na kuwa tumemtegemea yeye tangu utoto wetu. Kila jambo gumu lilipotokea wao pamoja na Daniel waliutafuta uso wa Mungu walifunga na kuomba waliyatafuta mapenzi ya Mungu walkionyesha wazi kuwa wao hawakuwa na tegemeo lingine lolote isipokuwa Yehova tu  Nguvu yao ya ujana waliyoiwekeza katika kumtegemea Mungu ilifanya watu wote wamuamini Mungu wao Daniel 3:1-30 “Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli. Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha. Ndipo maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, wakakusanyika ili kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha; wakasimama mbele ya ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha. Ndipo mpiga mbiu akapiga kelele akisema, Enyi watu wa kabila zote, na taifa, na lugha, mmeamriwa hivi, wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha. Na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa saa iyo hiyo katika tanuru ya moto uwakao. Basi wakati huo, watu wa kabila zote walipoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, watu wote na mataifa na lugha wakaanguka, wakaiabudu ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha. Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi. Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadreza, Ee mfalme, uishi milele. Wewe, Ee mfalme, ulitoa amri ya kwamba kila mtu atakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, ni lazima aanguke na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu; na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa katika tanuru ya moto uwakao.  Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha. Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme. Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha? Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?
       
Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha. Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto. Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto. Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto. Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme. Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu. Kisha Nebukadreza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Akanena, akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye juu, tokeni, mje huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakatoka katika ule moto. Na maamiri, na manaibu, na maliwali, na mawaziri, waliokuwa wamekusanyika pamoja, wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo. Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe. Basi mimi naweka amri ya kuwa kila kabila ya watu, na kila taifa, na kila lugha, watakaonena neno lo lote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watakatwa vipande vipande, na nyumba zao zitafanywa jaa; kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.Kisha mfalme akawakuza Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli.”

5.       Kubali maonyo.

Ndugu hekima ujuzi na maarifa haviji hivi hivi wakati mwingine ni lazima ukubali kuonywa lazima ujue kuwa katika maisha kuna maonyo, hatupaswi kupuuzia maonyo, tukipuuzia maonyo tutakuwa wapumbavu, neno la Mungu linatutaka tuwe watu wenye kupenda maonyo na tusiyadharau yanapokuja kwetu Mithali 1:7 “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.” Biblia inaonyesha kuwa wapumbavu hudharau maonyo kuonywa ni sehemu ya maisha yanayotufanya tukae katika njia iliyonyooka, tuwapo duniani tutapokeamaonyo kutoka katika maeneo na mazingira mbalimbali tutaonywa na wazazi wetu  Mitahli 1:8-9 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwakounaweza kuona pia katika Mithali 4:1-5 “Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu. Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu. Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu, Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu. Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi. Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu” unaweza nkuona npia katika Waebrania 12:5-11 “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake. Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.” Jamii yoyote au mtu nawaye yote aliyedekezwa au kukulia katika familia yenye kudekeza watoto anaweza kujikuta anaharibikiwa na awaye yote ambaye amekulia katika jamii ya watu wenye kupokea maonyo unatewe kuona kuwa maisha nyanaweza yasimsumbue , ndio maana neno la Mungu linatutaka tusiyaouuzie maonyo ni lazima tukubali kuonywa ndani ya maonyo kuna uzima, maonyo ni muongozo, maonyo ni ulinzi maonyo ni unabii, maonyo ni nuru wakati wa giza, yatakuepusha na majanga mengi ya kutisha Kama mtu anakupenda kweli upendo wa kweli utadhihirika vilevile kupitia maonyo Mithali 13:24 “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.”

6.       Usifungiwe nira na wasioamini

2 Wakoritho 6:14-18 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike”, Namna nyingine ya kuishafisha njia yako kama kijana ni kuhakikisha kuwa haufungiwi nira na asiyeamini, yaani lazima uangalie wale wanaokuzunguka na unaowafanya kuwa washirika wako wa karibu kuwa ni watu wa namna gani, biblia inaonyesha kuwa wawili hawawezi kuambatana pamoja wasipopatana Amosi 3:3 “Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?” ni lazima uhakikishe kuwa unavunja mapatano na watu wasiofaa, kama mtu sio wa imani yako ni muhimu kuhakikisha kuwa unavunja naye urafiki biblia inakataza hata kuoa mtu asiye wa imani yako Kumbukumbu la Torati 7:1-4 “Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang'oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe; wakati Bwana, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao; binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake. Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi.Mungu aliweka wazi wazi kabisa sababu ya kutokuwaona au kuwaoza vijana kwa watu wasio wa imani yako kwa sababu watakuongoza katika kuiabudu miungu mingine, sio hivyo tu watu waliokaidi amri hii Mungu alihakikisha kuwa wanapata taabu maisha yao yote kwa wanawake hao au wanaume hao kuwa miiba mbavuni mwao Yoshua 23:12-13 “Lakini mkirudi nyuma kwa njia yo yote na kushikamana na mabaki ya mataifa, yaani, mataifa haya yaliyobaki kati yenu, na kuoana nao, na kuingia kwao, nao kuingia kwenu; jueni hakika ya kuwa Bwana, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hata mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo Bwana, Mungu wenu, amewapa ninyi.” unaweza kuona pia katika Waamuzi 2:1-3 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi; nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani? Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.” Biblia sio tu imetukataza kufungiwa nira na wasioamini lakini pia inahoji kuna urafiki gani kati ya Haki na nuasi? Tena Pana shirika gani kato ya nuru na giza,  tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na beliari na tena aaminiye ana ehemu  gani na yeye asiyeamini na tena pana patano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Watu wengi sana wameingia katika migogoro na matatizo yasiyokwisha hata kwa maombi kwa sababu ya kufungiwa nira na wasioamini, kimsingi biblia imeonya vikali kuwa asiyeamini hana nafasi kwa aaminiye, jambo hili limepuuziwa na kanuni hii imekiukwa kimsingi wanapochanganyika watu wasiomcha Mungu na wanaomcha Mungu wasiomcha Mungu ndio watakaonyonywa kiroho na kuisha kabisa, hata uwe na hekima kiasi gani utageuzwa moyo, watu watakupima na jinsi ulivyokuwa mwanzo na ulivyo sasa baada bya kufungiwa nira na mtu asiyeamini na itabainika wazi kuwa umekwisha kwa sababu ya kufungiwa nira na wasioamini 1Wafalme 11:1-6Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti, na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda. Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo. Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. weweKwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni.Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.” Vijana wengi leo ukiwaambia usiolewe na huyo au usioe huyo sio wa imani yako hawataki hata kusikia, huyu n hajaokka wewe umeokoka achana naye hawataki kusikia wanafikiri kuwa watawaweza Sulemani na hekimayake yote aligeuzwa maoyo na dhambi yake ikawa tatizo la Israel kwa muda mrefu sana, Wako wengine wana madai ya kimaandiko kwamba Mbona Rahabu alikuwa kahaba lakini aliolewa na Muislaeli au mbona Ruth alikuwa mmoabu lakini aliolewa na Boazi? Ilivyo ni kuwa wanawake hao waliingia katika mkutano wa watu wa Mungu kwa sababu walimuamini Mungu wa Israel angalia Yoshua 6:25Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu, yule kahaba, na watu wa nyumba ya baba yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo; naye akakaa kati ya Israeli hata leo; kwa sababu aliwaficha wale wajumbe aliowatuma Yoshua ili kuupeleleza mji wa Yeriko.“ Kwa nini Yoshua alimuhifadhi hai kahaba Rahabu ambaye baadaye anatajwa kuolewa na watu wa Yuda na kuja kuwa Bibi za Yesu Kristo sababu kubwa ni kuwa alimuamini Mungu wa Israel alifanya maamuzi magumu kwa imani Yoshua 2:9-13akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu. Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng'ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa. Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini. Basi sasa, nawasihi, niapieni kwa Bwana, kwa kuwa nimewatendea ihisani, ya kwamba ninyi nanyi mtaitendea ihisani nyumba ya baba yangu; tena nipeni alama ya uaminifu;  ya kwamba mtawaponya hai baba yangu na mama yangu, na ndugu zangu wanaume na wanawake, na vitu vyote walivyo navyo, na kutuokoa roho zetu na kufa.’’  Ni katika hali kama hii ambapo Rahabu alionyesha imani na badiliko gumu la kiimani aliweza kukubalika katika jamii ya Israel na ndivyo ilivyokuwa kwa Ruthu, angalia maneno ya Ruthu utaweza kuna kuwa aliamini na kuongoka na kuwa miongoni mwa hao waaminio kutokana na imani yake kwa Mungu wa Israel aifanya maamuzi magumu  Ruthu 1:16-18 “Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami. Basi alipomwona kuwa amekaza nia yake kufuatana naye, aliacha kusema naye.Unaona kwa msingi huo basi haiwezekani kuwa na ushirika wa ndani na mtu asiyeamini, tunapozungumzia ushirika wa ndani maana yake ni kama kuungwa kwa agano mfano wake halisi ni ndoa, au maagano au mikataba na hususani ile inayowafungamanisha kwa nafsi na imani , ili kijana aishafishe njia yake isijekuwa ya majuto hana budi kulizingatia hilo.
Hivyo basi :-
a.       Mithali 1:10 Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usikubali.
b.      Mithali 1:15 Usiambatane nao Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.
c.       Mithali 4:14-15 usiifuate njia yao “Usiingie katika njia ya waovu, Wala usitembee katika njia ya wabaya. Jiepushe nayo, usipite karibu nayo, Igeukie mbali, ukaende zako
d.      Kwa nini Mungu hakutaka mchangamano na mataifa? Wasioamini
i.        Kwa nini tusifungiwe nira na wasioamini? Hii maana yake ni nini? Neno la Mungu halimaanishi kuwa tujitenge na watu wa dunia hii kwani hapo ingetulazimu kuhama duniani, Lakini Mungu anamaanisha kuwa  watu waliamini ni jamii tofauti kabisa na wasioamini na kwa jinsi hiyo hatupaswi kufanya au kuishi kwa mfano wao Zaburi 1:1 “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
ii.  Hatupaswi kutenda sawa sawa na watu wasioamini Kumbukumbu 22:10 “Usilime kwa ng'ombe na punda wakikokota jembe pamoja.
iii. waamini ni taifa takatifu, ukuhani mteule na watu wa miliki ya Mungu 1Petro 2:9-12 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema. Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa
kwa msingi huo huwezi kuwa sawasawa na mtu asiyeamini,lazima uwe tofauti
a.       Wewe ni mwenye haki wao ni waasi
b.      Wewe ni nuru wao ni  giza
c.       Wewe ni wa Kristo wao ni wa Beliari (Shetani) wa yule muovu
d.      Wewe ni muamini yeye ni asiyeamini
e.      Wewe ni Hekalu wao ni sanamu
Kwa hiyo hatuwezi kufungamana katika agano (Covenant) na moja ya maagano yaliyo wazi ni kuoana nao.
Waefeso 5:11 “Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee
Usikubaliane na uovu au waovu Warumi 1:32 “ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao
Wala usiifuatishe namna ya dunia hii Warumi 12:2 “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”

7.       Jaa neno la Mungu!

Zaburi 119:11Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.  Mwandishi wa Zaburi hii anaonyesha kuwa namna nyingine ya kijana kuisafisha njia yake ni kuliweka neno la Mungu Moyoni, kuyakumbuka maagizo ya bwana Neno la Mungu likijaa moyoni mwetu ni vigumu kukengeuka na kumtenda Mungu dhambi, Neno la Mungu litatupa ufahamu wa jambo lipi ni jema na jambo lipi ni baya na kama ni baya ni baya kwa kiwango gani, Ushindi mkuwa katika maisha yetu ya ujana utategemea kujaa kwetu neno, Maisha yetu na mafanikio yetu yamefungwa katika maagizo ya Mungu wetu Yoshua 1:5-8 “Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha. Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa. Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.” Unaweza kuona pia 1Wafalme 2:1-3  Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema, Mimi naenda njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari, ujionyeshe kuwa mwanamume; uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako; Lazima vijana tuhakikishe kuwa tunajaa neno la Mungu, maisha yetu yafurike neno la Mungu, mwenendo wetu uwe unaongozwa na neno la Mungu, kula neno jaaa neno mpa aucheue neno la Mungu, ushindi wetu na mafanikio yetu ujae katika neno la Mungu katika agano jipya tunaelezwa kuwa neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.Usisubiri uwe mzee ndipo ujae neno la Mungu utalihubiria wapi lazima ukubali kujaa neno la Mungu sasa ili uisafidhe njia yako.

8.       Waheshimu baba yako na mama yako!

 Zaburi 119:11-19 “Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako. Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako. Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi. Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako. Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako. Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako. Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako. Mimi ni mgeni katika nchi, Usinifiche maagizo yako  Mwandishi anaonyesha kuwa yuko tayari kujifunza neno la Mungu, yuko tayari kutangaza lakini vilevile anatamani mafanikio na kuishi maishga marefu, hii haiwezekani hivi hivi Biblia inaonyesha kuwa ili mtu afanikiwe kuwa na maisha marefu na kuwa na heri duniani moja ya maagizo muhimu ya Mungu yenye ahadhi hii ni kuwatii wazazi Kutoka 20:12 “. Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.” Na katika agano jipya bado neno hili limerudiwa na kukaziwa tena Waefeso 6:1-3 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia. Ni jambo la kushangaza katika nyakati za leo vijana wengi hawawaheshimu wazazi, wanawadanganya, hawataki maonyo hawataki kuongozwa wanawaongoza wazazi wao, wanasema uongo wanawaibia na wengine wamelala na mama zao au baba zao, hii maana yake ni nini huwezi kufanikiwa, huwezi kuifanya njia yako kuwa safi kama huwatii wazazi nah ii inaweza kuwa pana zaidi ya wazazi waliotuzaa mtu awaye yote aliyekuzidi umri ni mzazi, awaye yote ambaye anakulea ni mzazi awaye, walimu ni wazazi ili tubarikiwe ili tuwe na uheri duniani huitaji kutambika huitaji kwenda kutambikia Mizimu iliyokwisha kufa baba yako na mama yako wazazi wako ni mzimu tosha wahehimu Kumbu kumbu la Torati 5:16 “Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.”kumbe ukitaka kuzidisha siku zako hapa duniani basi wahehimu wazazi, watii tena biblia inasema watii katika kila jambo na kuwa jambo hili linampendeza Mungu Wakolosai 3:20 “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.Biblia inatuambia kuwa Yesu ingawa alikuwa na uweza mkubwa wa uungu ndani yake aliwatii wazazi wake Luka 2:51-52 “Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake. Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.” Wewe bado hujawa maarufu kama Yesu, huna lolote lakini hutaki kuwaheshimu wazazi wako, Mungu ampe neema kila mmoja wetu kuwa na heshima kwa wazazi wetu ili tupate miaka mingi na heri duniani, tusiwaache wazazi wetu wakaaibika, tuwatunze, tuwafunike aibu zao tusiufunue utupu wao.

9.       Jilinde na kiburi

Zaburi 119:20-22 “Roho yangu imepondeka kwa kutamani Hukumu zako kila wakati. Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako. Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.Mwandishi anataka kutuonyesha kuwa ili kijana aishafishe njia yake hana budi kuwa mtu aliyepondeka, mtu aliyepondeka ni mtu mnyenyekevu, na huku akisema uwakemee wenye kiburi, na uniondolee dharau, kwa nini ?, moja ya tatizo kubwa sana linaloweza kuondoa kibali kwa Mungu na kutuharibia nji yetu ni tatizo la kiburi, Mungu anapoona kuwa tuna kiburi ni rahisi sana kutushughulikia kwa haraka, kiburi kinaondoa kabisa neema ya Mungu juu yetu. Na kinaondoa kabisa uwepo wa Mungu kati yetu na kinaweza kutuletea aibu Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu” Kwa nini ujitie aibu duniani Biblia imeonyesha njia iliyo njema na njia hii ni unyenyekevu, na una faida nyingi. Kiburi ni nini? Kiburi ni hali ya kujiona kuwa uko daraja la juu katika ubora kuliko watu wengine, ni hali ya kufikiri kuwa unajitosheleza wewe mwenyewe kutokana na mafanikio fulani, au ngazi ya daraja fulani unalotokea ni kujiamini na kujiweka katika viwango flani vya kutokuhisi kuwa una mapungufu. Sio rahisi sana kukielezea kiburi, unaweza kuwa tjiri na mwenye mali nyingi sana na ukawa mnyenyekevu na unaweza kuwa masikini sana na ukawa na kiburi, lakini hata hivyo kiburi kinaweza kuletwa na aina fulani ya mafanikio tuliyonayo, kiujuzi, kielimu, kibiashara na hata katika maisha ya utauwa tunaweza kujihesabia haki. Mwandishi anajua madhara ya kiburi hivyo anakubali kupondeka na kujinyenyekeza kwa Mungu Isaya 66:2 “Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.Habari njema ya ufalme wa Mungu ni rahisi kupokelewa kwa wanyenyekevu, kwaasili mtu mwenye kiburi hawezi kuipokea injili, habari ya maneno ya Mungu kwa mtu mwenye kiburi ni upuuzi tu  ni watu wanyenyekevu pekee wanaoweza kupokea habari hii na ninaweza kusema katika njia iliyo wazi kabisa kuwa Maswala ya Mungu yamedizainiwa maalumu kwa watu wanyenyekevu Isaya 61:1-2 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;” so mwandishi anakiona kiburi kuwa ni chenye madhara na kwa bahati mbaya vijana wengi ndio wanaokubwa na hali ya kuwa na kiburi na hivyo hatuna budi kujifunza unyenyekevu, Unyenyekevu ni swala la maamuzi ni swala la kujivika sisi wenyewe Wakolosai 3:12-14 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.” Katika maswala ambayo watu wanapaswa kujivika ni pamoja na unyenyekevu, si vema kumuomba Mungu akupe unyenyekevu shule yake itakuwa ngumu mno lakini ni vema kuamua kujivika unyenyekevu, tusipofanya hivyo tutapoteza neema na Mungu atatupinga na njia yetu haitakuwa njia iliyonyooka 1Petro 5:5-6 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.  Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;Kwa msingi huo basi iwapo kjana anataka kufanikiwa basi hana budi kumsihi Mungu ampe neena ili asijivune na akubali kuwahesabu wengine kuwa bora kuliko nafsi yake na kuweza kufanikiwa katika njia zake, kutii neno la Mungu kunategemeana na namna na jinsi anavyopaswa kuwa na moyo wa unyenyekevu bwana atupe neena kuwa mbali na kiburi katika jina la Yesu.  Njia ya Mungu ya kupelekwa juu zaidi ni unyenyekevu, na njia ya kupelekwa chini zaidi ni kiburi Wafilipi 2:3-11”Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.  Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;  ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;  na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”
Maandiko yanaonyesha wazi kuwa mtu akijinyenyekeza Mungu humuinua na mtu akijiinua mUngu humdhili Luka 18:10-14Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.” Biblia inatuonya kuwa hatupaswi kujivunia chochote hapa duniani majivuno ni sehemu ya kiburi, wala hatupaswi kujivunia akili bali tukubali kushughulishwa na mambo manyonge kukubali kufanya mambo ya nchini  Warumi 12:16  Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.”

10.   Muombe Mungu “Omba”

Zaburi 119:25-29 “Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako. Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako. Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako. Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, Unitie nguvu sawasawa na neno lako. Uniondolee njia ya uongo, Unineemeshe kwa sheria yako.” Wote tunafahamu umuhimu wa Maombi na wote tunajua namna na jinsi Biblia inavyotuaguza kuomba bila kukoma na kwama haja zetu zote na zijulikane na Mungu Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu
Unaweza kuona sasa mwenye Hekima katika Zaburi hii anaomba, anajua umuhimu wa kuomba anamjulisha Mungu haja zake
a.       Nafsi yake imeambatana na mavumbi maana yake anaelemewa na huzuni kiasi cha kufa, nafsi imeinama hana furaha na amani ni kama yuko kwenye maombolezo, kwa hiyo anamuomba Mungu na Mungu alimjibu, alimpa amani alimuinua alifurahia.
b.      Anaomba Mungu amfundishe amri zake anataka kujua wazo lote la Mungu anatamani kujuujua moyo wa Mungu yaani kujua mapenzi yake ili aendelee kumtafakari Mungu. Amfahamishe njia zake na mausia yake ni muhimu kufahamu kuwa neno amri za Mungu, neno njia na neno sheria na neno hukumu na neno shuhuda limetajwa katika nzaburi hii mara kadhaa kwa mitindo tofauti
·         Law (Sheria) The Torah limetajwa mara 25 Katika zaburi hii mwandishi alikuwa anataka awe na ufahamu wa kutosha kuhusu Torati ya Mungu anaomba apate neema na ufunuo wa kujua sheria za Mungu kwa sababu zingemfanikisha
·         Word (Neno) Dabar limetajwa mara 24 Mwansihi akiwa anaomba Mungu amjulishe kila analolisema akijua kuwa akiyashika maneno ya Mungu atafanikiwa
·         Judgement (hukumu) Mispatim limetajwa mata 23 akimaanisha kuwa anataka awe na uwezo wa kuzijua sheria na Mungu na kuzitafakari ili awe na uwezo wa kupambanua mema na mabaya anakjua kuwa akiwa na uwezo huo atafanikiwa
·         Testimonies (Shuhuda) Edut/Edot  limetajwa mara 23 Matendo makuu ambayo Mungu aliyafanya kati yake na Israel mwenye hekima anajua kuwa akizitunza shuhuda za Mungu na kuyakumbuka matendo yake makuu atafanikiwa
·         Commandement (Amri) Miswah/Miswot limetumika mara 22 hiiinawakilisha kufuata utaratibu wote wa kiadilifu ambao Mungu ameamuru Mwandihi anajua kuwa kuwa akizishika amri za Mungu atafanikiwa
·         Stutus (Maandiko) Huqqim limetumika mara 21 likimaanisha imeandikwa au maandiko Mwandishi alikuwa anataka ayajue maandiko na hivyo akiyajua atafanikiwa
·         Tunapomuomba Mungu kuonyesha kuwa tuna moyo wa dhati ni muhimu kumuomba Mungu pia kuhusukujizua njia zake sio tu kwaajili ya kuvunjika kwetu moyo.
c.       Pia anaomba Mungu amtie nguvu, amuondolee njia ya uongo na amneemeshe kwa sheria yake
Wakati wowote tunapokuwa na uhitaji wa aina yoyote hatuna budi kuhakikisha kuwa tunamuomba Mungu, Nafsi zetu zinapolemewa na huzuni kiasi cha kufa  ni muhimu kumuomba Mungu, Nafsi zetu zinapozimia hatuna budi kumuomba Mungu, mwandishi anataka Mungu amrejeshee hali yake ya kuwa na furaha, Mwandishi anaonyesha kuwa anatubu kwa kumuomba Mungu amuondolee njia ya uongo. Ni ajabu kuwa mwenye hekima hapa anaonekana kuomba zaidi mahitaji ya kiroho kuliko ya kimwili, swala hili linaweza kuwa sawa kabisa na Jinsi Bwana alivyotufundisha kuwa tutafute kwanza ufalme wa Munguna haki yake yote na mengine yote tutazidishiwa Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.” Mwenye hekima anaonyesha hali ya juu sana ya ukomavu wa kiroho, ni rahisi sana kumuomba Mungumahitaji yetu ya mwilini kuliko mahitaji yetu ya Rohoni, lakini yeye anatamani sana kuzijua njia za Mungu, Sheria, shuhuda, amri, maagizo, mausia, na hukumu zake.
11.   Chagua njia ya kweli

(choosing the way of truth) Zaburi 119:29-30 “Uniondolee njia ya uongo, Unineemeshe kwa sheria yako. Nimeichagua njia ya uaminifu, Na kuziweka hukumu zako mbele yangu.” Moja ya swala gumu sana Duniani kulikwepa ni kusema uongo, au kutokufuata njia ya uongo, Mashujaa wengi wa Imani katika Biblia waliweza kusema uongo mara kadhaa sio rahisi kucha au kuushinda uongo kwa nguvu zetu, mwandishi anamuomba Mungu amuondolee njia ya uongo, amneemeshe kwa sheria yake na pia amfanye kuwa mwaminifu ili aweze kujua mema na mabaya, Vijana wengi sana wanakabiliwa na tatizo hili la kufuata njia ya uongo, uongo unaweza kutugharimu katika maisha yetu unaweza kuzuia mema katika maisha yetu 1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.  Neno hila hapo linamaanisha uongo kwa mujibu wa asili ya maandiko ambayo  Petro alinukuu kutoka katika  Zaburi 34:13 “
Mara kadhaa  Biblia inaonyesha Mashujaa wa imani walisema uongo kwa sababu fulani fulani
a.       Ibrahimu alimnena Sara kuwa ni Dada yake Mwanzo 20:1-5 “Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu. Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee Bwana, Je! Utaua hata taifa lenye haki? Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi
b.      Isaka alimnena Rebbecca kuwa ni Dada yake Mwanzo 26: 6-9Isaka akakaa katika Gerari.  Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso. Ikawa alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia dirishani, akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe.  Abimeleki akamwita Isaka, akasema, Yakini huyu ni mkeo, mbona ulisema, Ni ndugu yangu huyu? Isaka akamwambia, Kwa sababu nalisema, Nisife kwa ajili yake.”
 Isamuel 21:2, 8 na 1Samuel 27;8-10 “Naye Daudi na watu wake walikuwa wakikwea na kuwashambulia Wageshuri, na Wagirizi, na Waamaleki waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo, tangu Telemu, hapo uendapo Shuri, hata mpaka nchi ya Misri., Tena Daudi akaipiga nchi hiyo, asimhifadhi hai mume wala mke, akateka nyara kondoo, na ng'ombe, na punda, na ngamia na mavazi; kisha akarejea na kufika kwa Akishi.                Naye Akishi humwuliza, Je! Mmeshambulia upande gani leo? Na Daudi husema, Juu ya Negebu ya Yuda, au, juu ya Negebu ya Wayerameeli, au, juu ya Negebu ya Wakeni.”   Maandiko yanatutaka tuuvue uongo tuwe waaminifu tunaweza kabisa kuuondoa uongo kama vile tunavyoweza kubadilisha nguo Wakolosai 3:5-10” “Basi vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati,uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu: kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu. Katika hayo ninyi nanyi mlitembea zamani, mlipoishi katika hayo. Lakini sasa yawekeni mbali nanyi hayo yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano na matusi vinywani mwenu. Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu upya, unaofanywa upya upate ufahamu sawa sawa na mfano wake yeye aliyeuumba” Kwa hiyo Kuna umuhimu wa kumuomba Mungu atuondolee njia ya uongo kwa vile ni vigumu sana kukwepa kusema uongo au kufuata njia za uongo.

12.   Chagua njia ya haki

Zaburi 119:33-40 “Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hata mwisho. Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote. Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, Kwa maana nimependezwa nayo. Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa. Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako. Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, Inayohusu kicho chako. Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema. Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.Aina kama hii ya maombi haiwezi kufanywa na mtu wa kawaida asiyempenda Mungu tunaona mwandishi hapa anakazia kuwa anataka au ana kiu ya kujua au kufundishwa njia za Mungu na kuwa yaya atazishika hata mwisho yeye anajua kuwa ni Mungu pakee anayeweza kubadili mioyo yetu ikamuelekea yeye kwa uwezo wetu sisi hatuwezi kuzijua sheria za Mungu lakini kama mioyo yetu ikitaka na tukamuomba Mungu basi Mungu atafanya kazi ile tuitakayo ndani yetu kutaka kwetu na kutenda kwetu Wafilipi 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

13.   Mungu atuepushe na tamaa

Zaburi 119:36-37 “Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa. Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako” Ni kama mwenye hekina anajua wazi kuwa Tamaa inaweza kuharibu njia zake na maisha yake na hivyo anajiombea kwa Mungu kwamba amsaidie moyo wake usiielekee tamaa  neno linalotumika hapa kwa tamaa katika kiibrania ni “BOICE”  maana yake kwa kiingereza “Selfish gain”  Ubinafsi Biblia imejaa mifano mingi ya watu walioahribiwa na tamaa
a.       Balaamu aliwakosesha watu wa Mungu na nasfi yake kwajili ya tamaa Hesabu 22:2, 2Petro 2:14-16 “wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana; wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu; lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.”
b.      Ahabu 1Wafalme 21:1-13 “Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria. Ahabu akasema na Nabothi, akamwambia, Nipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, maana ni karibu na nyumba yangu; nami nitakupa badala yake shamba la mizabibu lililo zuri zaidi; au ukipenda, nitakupa fedha sawasawa na thamani yake. Nabothi akamwambia Ahabu, Bwana apishe mbali nikupe wewe urithi wa baba zangu. Basi Ahabu akaenda nyumbani kwake, ana moyo mzito, tena amekasirika, kwa sababu ya neno lile aliloambiwa na Nabothi Myezreeli, akisema, Sitakupa urithi wa baba zangu. Akajilaza kitandani pake, akageuza uso wake, akakataa kula. Lakini Yezebeli mkewe akamwendea, akamwambia, Kwa nini roho yako ina huzuni hata usile chakula? Akamwambia, Kwa sababu nimesema na Nabothi Myezreeli, nikamwambia, Unipe shamba lako la mizabibu kwa fedha, au, ukipenda, nitakupa shamba la mizabibu lingine badala yake. Akajibu, Sitakupa shamba langu la mizabibu. Yezebeli mkewe akamwambia, Je! Sasa wewe unaumiliki ufalme wa Israeli? Ondoka, ule chakula, moyo wako ufurahi; mimi nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.  Basi, akaandika nyaraka kwa jina la Ahabu, akazitia muhuri yake, akazipeleka zile nyaraka kwa wazee, na kwa watu wenye nguvu waliokuwa katika mji wake, waliokaa pamoja na Nabothi. Akaandika katika zile nyaraka, akasema, Pigeni mbiu ya watu kufunga, mkamweke Nabothi juu mbele ya watu, mkainue watu wawili, watu wasiofaa, ili wamshitaki, na kumshuhudia, kunena, Umemtukana Mungu na mfalme. Kisha mchukueni nje, mkampige kwa mawe, ili afe. Wale wazee wa mji wake, na walio wenye nguvu waliokaa mjini mwake, wakafanya kama Yezebeli alivyowaagiza, kama ilivyoandikwa katika nyaraka alizowapelekea. Wakapiga mbiu ya watu kufunga, wakamweka Nabothi juu mbele ya watu. Na hao watu wawili, watu wasiofaa, wakaingia, wakaketi mbele yake; wale watu wasiofaa wakamshuhudia Nabothi mbele ya watu, wakasema, Nabothi amemtukana Mungu na mfalme. Ndipo wakamchukua nje ya mji, wakampiga kwa mawe hata akafa.”
c.       Achan Yoshua 7:21 “Nilipoona katika nyara joho nzuri ya Babeli, na shekeli mia mbili za fedha, na kabari ya dhahabu, uzani wake shekeli hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama, vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake.”
d.      Yuda Yohana 12:6 na Mathayo 26:14-16 Yohana 12:6 “Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini; bali kwa kuwa ni mwivi, naye ndiye aliyeshika mfuko, akavichukua vilivyotiwa humo.”
e.      Gehaz 2Wafalme 5:20-26 “Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; kama Bwana aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake. Basi Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani?                  Akasema, Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta ya fedha, na mavazi mawili. Naamani akasema, Uwe radhi, ukatwae talanta mbili. Akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi wake wawili; nao wakayachukua mbele yake. Naye alipofika kilimani, alivitwaa mikononi mwao, akaviweka nyumbani; akawaacha wale watu kuondoka, nao wakaenda zao. Lakini yeye akaingia, akasimama mbele ya bwana wake. Elisha akamwambia, Watoka wapi, Gehazi? Akanena, Mtumwa wako hakuenda mahali. Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng'ombe, na watumwa, na wajakazi?” Anania na Safira Matendo 5:1-8
Watu wote hapo juu waliharibikiwa kwa sababu ya tamaa, Mwenye hekina anaiona tamaa kama tatizo kubwa na kuwa bila msaada wa Mungu kwa vile yeye naye ni binadamu anaweza kujikuta akiingia katika kuyatendea kazi hayo, Tamaa ni kama mbegu ya dhambi na kwa sababu hiyo tusikubali ikakomaa, hatuna budi kuishughulikia mapema katika maisha yetu ili isiweze kuzaa Yakobo 1:13-15 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.Tamaa inaweza kuifanya njia yako kutokuwa safi na kuharibumaisha hivyo ni vema kuomba iwe mbali nasi kama mwenye hekima alivyojiombea.
14.   Penda neno la Mungu

Zaburi 119:41-48 “Ee Bwana, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako. Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako.  Nami nitaitii sheria yako daima, Naam, milele na milele. Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako. Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.  Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda. Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako. Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, Kwa sababu umenitumainisha.”
Mwenye hekima anaonyesha kuwa analitumainia neno na kuwa hataki neno la Mungu liondolewe kinywani mwake anaonyesha kuwa neno la Mungu ni kila kitu katika maisha yake atalitii kwa vile litampa uhuru kamili autakao, anadai hatalionea haya neno, atajifurahisha kwa hilo, huku ni kujitoa kuliko kukubwa sana katika neno la Mungu, kwa nini mwenye hekima anaonyesha kulitumainia neno la Mungu?
a.        anasema linauhisha (Preserve, nourish) Zaburi 119:25,37, 107
b.      Linaleta tumaini (gives hope) Zaburi 119:49, 147
c.       Ukilijua hutakwazika ( you will never Stumble)  Zaburi 119:165
d.      Ni tamu Zaburi 1119:103
e.      Linahekimisha kuliko hata umri wako Zaburi 119:100
f.        Linafikuza waovu Zaburi 119:29, 115
g.       Neno la Mungu ni faraja wakati wa taabu 119:50
h.      Neno la Mungu ni fimbo ya Mchungaji Zaburi 119:176

15.    Mkumbushe Mungu ahadi zake “Remind God on his Promises”

Zaburi 119:49-50 “Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, Kwa sababu umenitumainisha. Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha.”  Mwenye hekima hapa anamkumbusha Mungu neno lake au ahadi zake, ambayo anaeleza kuwa imempa matumaini Makubwa, mateso yake yote anayoyapata anafarijika kwa sababu ya ahadi ya Mungu, Kuna mambo yanafunuliwa hapa katika mstari huu, kwanza kabisa katika zaburi hii ilikuwa ngumu sana kufahamu kuwa imeandikwa na nani, lakini kupitia mstari huu wengi wanafikiri kuwa sasa moyo wa Mwandishi kujificha imeshindikana kwani ni wazi huyu ni Daudi na ni wazi kuwa alikuwa akitamani ahadi hii itimie 2Samuel 2:16-19 “Na nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele. Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.Ndipo Daudi, mfalme, akaingia, akaketi mbele za Bwana, akasema, Mimi ni nani, Bwana MUNGU, na nyumba yangu ni nini, hata umenileta hata hapa? Tena jambo hili lilikuwa dogo machoni pako, Ee Bwana MUNGU; hata umeleta habari ya nyumba yangu mimi, mtumwa wako, kwa miaka mingi inayokuja baadaye; na hayo kwa namna ya kibinadamu, Ee Bwana MUNGU.”  Hii ilikuwa ni ahadi ya kuja kwa Masihi kupitia uzao wa Daudi, kwa hiyo licha ya kuwa Mungu aliahidi lakini Daudi aliendelea kumkumbusha Mungu ahadi yake, alikuwa anatamani kuiona kwa macho yake ikitimia, Mwenye hekima anatukumbusha umuhimu wa kumkumbusha Mungu ahadi zake kwa njia ya maombi, hii haimaanishi kuwa Mungu hakumbuki hapana au hajui hapana lakini Mungu katika hekima yake anataka tulisome neno lake na kuzijua haki zetu na kuzidai kwa jinsi ya maombi angalia Isaya 43:26 “Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.
Mungu aliitimiza ahadi hii kimwili kupitia Solomon “ in a narrow cense” na kiroho ni Kwa Yesu Kristo “in a broad cense” 2Nyakati 7:17-18 “Nawe, ukienda mbele yangu kama alivyokwenda Daudi baba yako, ufanye sawasawa na yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu; ndipo nitakithibitisha kiti cha enzi cha ufalme wako, kama nilivyoagana na Daudi baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kutawala katika IsraeliLakini pia agano au ahadi hii ilikuwa inamuhusu Yesu Kristo angalia Luka 1:68-69 “Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa. Ametusimamishia pembe ya wokovu Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake.Ni vema sana kuendelea kumuomba Mungu ili aweze kukumbuka na kulitimiza agano lake na kuliangalia neno lake ambalo alisema nasi, ikiwemo ahadi ya Yesu Kristo kuja tena.

16.   Simama imara  Zaburi 119:51-54

Mungu huwatumia watu wenye msimamo watu imara watu wasiotikisika, baada ya kuwa umemjua Mungu na njia zake hupaswi kuyumbishwa hupawi kuwa mtu wa nia mbili hupaswi kuwa unyasi unaotikiswa na upepo ni lazima uwe imara 1Wakoritho 15:58Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.” Ndugu zangu wapendwa muimarike napenda sana mstari huu unavyosomeka katika biblia ya kiingereza Stand firm, do not be moved! Mungu anataka tuwe imara katika kumuamini yeye unaweza kuona Waefeso 6;10-11 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.” Kusimama imara ni pamoja na kuisimamia imani kwa gharama yoyote, kuhakikisha kuwa tunasimama katika haki na maelekezo ya Mungu, hatupaswi kuwa wenye kuyumba linapokuja swala la imani, Shadrack Meshak na Abednego waliweza kuisimamia imani kwa gharama ya maisha yao hata walipojua wazi kuwa wanaweza kutupwa katika tanuru ya moto wao walisimama upande wa Mungu Daniel 3:16-18 “ Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili. Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha”. Mungu anatarajia kuwa na vijana wenye msimamo mkali katika imani, vijana ambao watafanya kazi yake katika nyakati za mwisho wakiisimamia imani bila woga, Nyakati za leo vijana wengi hawana msimamo wanayumbishwa, kijana wa kiume anafanywa kuwa KIBENTENI anawekwa ndani anafugwa na sugar momy, wasichana wanauza miili yao, wasichana wa leo hawakatai, kila unayemtongoza anaingia laini, leo hakuna umri maalumu wa kutembea na mtu kijana mdogo akikaza anachukua mtu wa umri kama mama yake tu na mtu mzima akikaza anachukua bnti kama mjukuu wake tu, hakuna heshima, hakuna adabu nani ataifundisha dunia kuwa wako watu wamefunzwa na wanaitwa wakristo, watu wenye uadilifu watu wasioyumbishwa, watu walio majasiri, watu waio wepesi watu wasio unyasi unaotikiswa na upepo, watu wenye msimamo, watu waliojenga nyumba zao juu ya Mwamba ambao hawayumbishi na mvua, wala pepo wala mafuriko Mungu anataka watu wa aina hii wenye msimamo.,tafadhali simama imara.

17.   Kumbuka jina la Bwana Mungu wako!

Zaburi 119:55-60 “Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee Bwana, nikaitii sheria yako. Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako. Bwana ndiye aliye fungu langu, Nimesema kwamba nitayatii maneno yake. Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, Unifadhili sawasawa na ahadi yako. Nalizitafakari njia zangu, Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako.       Nalifanya haraka wala sikukawia, Kuyatii maagizo yako.”

Mwandishi anaeleza kuwa wakati wa usiku amelikumbuka jina la Mungu, wakati wa usiku hapa sio lazima uwe ni wakati wa usiku kweli, hii inawezekana ni wakati ambapo giza la maisha limetanda, ni wakati wa vita vyake katika maisha ni jinsi gani anaweza kuishafisha njia yake  ni pamoja na kulikumbuka jina la Mungu wake wakati wa changamoto Za aina mbalimbali

Ni muhimu sana kufahamu kuwa nyakati za biblia mara kadhaa Jina limekuwa na maana kubwa na pana sana kuliko tunavyo fikiri katika wakati wa leo, Majina hayakutolewa tu bila sababu kwa sababu majina yalibeba maana kubwa sana kaytika maisha hivyo kuna wakati hata Mungu mwenyewe aliweza kuwabadili watu majina ili kuakisi kusudi la Mungu dhidi ya mtu huyo, mfano Abramu maana yake “Baba aliyetukuzwa” au “mwana wa kifalme” Mungu alimbadilisha jina lake kuwa Abrahamu maana yake baba wa wengi au “Mfalme wa wafalme wengiYakobo ambaye jina lake lilikuwa mwenye hila alibadilishwa na kutoka jina mfalme mwenye hila kuwa Mfalme pamoja na Mungu Israel, Sarai kutoka kuwa Malikia kuwa Mama wa wafalme wengi,  Tabia hii ya Mungu iliweza pia kuonekana katika agano jipya ambapo Yesu alibadili jila la Simeon kuwa Petro au Kefa Yohana 1:42 “Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).”
Katika maandiko jina linafunua sifa, uweza na mamlaka, Yesu alipokuja Duniani yeye alikuwa ni jina kamili la Mungu vile alivyojifunua alikuwa akiifunua siri ya Mungu Yohana 17;26 “Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.”               
Jina la Mungu ni msaada kamili wa kuwatosheleza wanadamu wakati wa mahitaji yao, Mwandishi anasema wakati wa usiku alilikumbuka jina la Mungu, ni wazi kuwa jila la Mungu lina utoshelevu wote katika maisha yetu ni jina la thamani kubwa sana Israel hawakupenda kulitaja hovyo lakini walijua kuwa jina la Mungu  Ni jina lenye utoshelevu wa mahitaji yao yote hivyo walimuita Munhgu majina mbalimbali kutokana na namna na jinsi alivyoukua akijifunua na kujidhihirisha katika mazingira mbalimbali.

·         Mfano Elohimu alipojifunua kama Mungu mwenyezi muumba wa mbingu na ardhi na vyote vijuzavyo ulimwengu
·         Yehova Nisi alipojifunua kutoa ushindi dhidi ya adui zao
·         Yehova Rapha alipojidhihirisha kama Mponyaji
·         Yehova Yire  alipojidhihirisha kuwa ni mtoaji
Mungu ana jina kwa kila hali ya mahitaji yetu katika maisha ana jina kwaajili ya kila changamoto tunayokutana nayo, jina lake linadhihirisha uwezo wake na sifa zake na tabia yakena mamlaka yake na nguvu zake ni jina linaloweza kukimbiliwa na likatupa amani ''Mithali 18:10- Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia akawa salama.'' Ni jina ambalo mtu awaye yote akiliitia katika shida aliyo nayo ataokolewa Matendo 2:21 “Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. “ Warumi 10:13 “kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.“ Jina hili lilikuwa jina adimu sana katika agano la kale, wayahudi walikatazwa wasilitaje bure jina la Bwana Mungu, jina hili waliliogopa sana hata kulitaja au kuliandika lakini sisi nyakati za agano jipya jina hili tumepewa na jina hili liko wazi tunawezxa kuliitia na kulitegemea na kulitumainia Wafilipi 2:9-11 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;  ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba. So Yesu aliagiza tuombe kwa jina hili nay a kuwa tukiomba lolote kwa jina lake baba wa mbinguni atalifanya  Yohana 14:13-14 “Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.  Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.” Na ndio maana sasa mwandishi wa zaburi anasema amelikumbuka jina la Mungu wakati wa usiku yaani analitegemea analiitia anaomba kupitia hilo wakati aonapo giza katika njia zake so jnsi gani kijana aishafishe njia yke ni pamoja na kulikumbuka jina la Bwana mungu wetu na kulitegemea na kulikimbilia
18.   Kumbuka Kumshukuru Mungu!

Zaburin 119: 61-68 “Kamba za wasio haki zimenifunga, Sikuisahau sheria yako. Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru, Kwa sababu ya hukumu zako za haki. Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako. Bwana, dunia imejaa fadhili zako, Unifundishe amri zako. Umemtendea mema mtumishi wako, Ee Bwana, sawasawa na neno lako. Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako. Kabla sijateswa mimi nalipotea, Lakini sasa nimelitii neno lako. Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.

Hakuna jambo muhimu Duniani kama kumshukuru Mungu na kuwashukuru wanadamu, au wote wanaotuzunguka kwa kuwa kila mmoja anachangia mafanikio yetu kwa namna moja ama nyingine, Kama hatutakuwa na shukurani kinyume chake tutakuwa na manung’uniko na lawama jambo ambalo halimpendezi Mungu na linaondoa baraka za Mungu, Hesabu 11:1 “Kisha hao watu walikuwa kama wanung'unikao, wakinena maovu masikioni mwa Bwana; Bwana aliposikia hayo, hasira zake zikawaka; na moto wa Bwana ukawaka kati yao, ukateketeza katika mipaka ya mwisho wa marago.” Wote tunakumbuka namna na jinsi wana wa Israel walivyoteseka huko Misri na Mungu alivyowapigania na kuwaokoa na kuwasaidia hata hivyo walipopata taabu hawakukumbuka mema ya Mungu bali walinung’unika na kunena maovu hawakuwawatu wa shukurani, licha ya kulishwa mana na kunyweshwa maji lakini hawakupokea mambo kwa shukurani, tunapokuwa vijana hata tutakapokuja kuwa watu wazima katika safari yetu ya maisha wako watu watatumiwa na Mungu kututoa katika hatua moja mpaka kutupeleka katika hatua nyingine hatuna budi kuwa watu wa shukurani, kuwashukuru lakini vilevile kumshukuru Mungu, Mwandishi wa zaburi hii anasema katikati ya usiku ataamka amshukuru Mungu, maana yake anataka kumuinyesha Mungu jinsi anavyokumbuka matedno yake mitego ya wasio haki ilimfunga lakini Bwana alimuokoa kwanini asishukuru? Je unakumbuka kuwa na Muda wa shukurani? Je umemshukuru Mungu leo asubuhi? 1Wathesalonike 5:18 Biblia inasema “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.”

Kumshukuru Mungu ni amri, hatuna budi kujifunza kushukuru kila siku katika maisha yetu, tuache kulalamika, tujifunze kumshukuru Mungu siku zote za maisha yetu, Kumpa Mungu shukurani huiweka mioyo yetu katika uhusiano sahihi na Mungu, naye atatuokoa hata katika hali yetu ya nhisia mbaya jambo ambalo litatuletea amani Waebrania 13:15 “Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.Dabihu ya sifa humaanisha kushukuru wakati wa mambo magumu Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.              

19.   Kubali Kujaribiwa
Zaburi 119:69-75 “Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako. Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Mimi nimeifurahia sheria yako.  Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, Nipate kujifunza amri zako.  Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha. Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, Unifahamishe nikajifunze maagizo yako.  Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelingojea neno lako. Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa.
Ilikuwa vema kwamba naliteswa Nipate kujifunza Amri zako” vinaja wanapaswa kujua kuwa wakati mwingine Mungu ataruhusu njia ya mateso kusudi aweze kutufundisha njia zake au amri zake Wafilipi 1;29 “ Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo si kumwamini tu ila na kuteswa kwaajili yake “ Mungu anazo njia zake ambazo ni njema katika maisha yetu, wakati mwingine itatuchukua muda mrefu sana kuona ndoto zetu zikitimia  kutokana na mpango wake na hekima yake yeye aliamua na kukusudia kabisa Israel wapiti Jangwani kusudi =awafundishe amri zake Umbali kutoka Misri kwenda Israel ni kilomita 623 tu. Lakini Musa na kundi lake (wana wa Israel) walitumia miaka 40 kutembea hadi kufika nchi ya ahadi. Huu ni wastani wa kilomita 15 kwa mwaka, sawa na kilomita 1.25 kwa mwezi. Hii ni sawa na mita 42 tu kwa siku, yani umbali nusu ya uwanja wa mpira. Kwa nini Mungu aliliruhusu ili ni kwa kusdi la kuwafundisha njia zake Kutoka 13:17-18Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri; lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha.”             Kwa nini Mungu aliwapitisha njia ile ngumu ya mateso kwa muda mrefu kuliko walivyofikiri ni ili aone je watashika amri zake? Kumbukumbu la Torati 8:1-18Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki. Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako, akurudivyo. Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.  Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima; nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali; nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake yafukuka shaba. Nawe utakula ushibe, utamshukuru Bwana, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa. Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo.  Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake; na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka; basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.  Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo. Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.” Mungu ana mafunzo mengi sana kwetu anapoamua kutupitisha katikia njia ndefu, anapoamua kutuacha tuingie katika majaribu, anapotuacha tuteseka anataka tujifunze amri zake jambo hili lilikuwa wazi kwa mwandishi wa zaburi hii mwenye hekima alizielewa nia za Mungu so ni jinsi gani kijana ataishafisha njia yake ni kwa kukubalimnjia za Mungu kwa kukubali kujaribiwa.

20.   Wape watu wazuri Nafasi ya pili.

Zaburi 119:76-79Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu, Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako. Rehema zako zinijie nipate kuishi, Maana sheria yako ni furaha yangu. Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako. Wakuchao na wanirudie, Nao watazijua shuhuda zako.” Ni muhimu kufahamu kuwa wakati wa majaribu ya aina mbalimbali wako watu wengine watakukimbia na hawatasimama na wewe  , wanaweza kufikiri kuwa Mungu hayuko na wewe japo nao wanampenda Mungu, hili ni jambo la kawaida katika maisha kwa sababu wakati unapitia majaribu sio kila mtu anaweza kuelewa kwa nini unapitia majaribu  Mwenye Hekima anasema yeye ni mwenzao kabisa watu wanaomcha Mungu Zaburi 119:63 “Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yakoHata hivyo wakati wa mambo magumu walimkimbia wakidhani kuwa labda Mungu amemuacha, wakati mwingine sio rahisi kuelewa namna na jinsi Mungu anavyoshughulika na mtu,  na hata tunapokosea watu hawajui ni saa ngapo tumetubu kwa hiyo hata watu wema wanaweza kudhani kuwa hauko sawa na Mungu na wakajitenga nawe, Hiki kilimtokea mwenye hekima alipokuwa katika mapito yake kuna wakati hata watu walio karibu wanaweza wasisimame nawe wakati huu unaweza kusikia maumivu kuachwa na watu wa karibu Zaburi 27:10 “Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake.”  Wakati watu wa karibu wanatukimbia na kutuacha ni muhimu kuendelea kuweka tumaini letu kwa Bwana Mungu wetu yeye hatatuacha, lakini ni lazima tukumbuke kuwa kuna wakati wa kuwa wenyewe kuna wakati wa nkuwa peke yetu huu ni wakati wa kumuita Bwana na kumkimbilia yeye Zaburi 142:5-6 “Utazame mkono wa kuume ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho. Bwana, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.” Jambo hili sio tu kuwa lilimtokea Daudi lakini hata Paulo mtume wakati wa kufungwa kwakwe kwa sababu ya injli,  lakini hatuna budi kusamehe wale wote wanaotuacha kwa sababu hawajua ni nini mapenzi ya Mungu 2Timotheo 4:16 “Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.Ni muhimu kuwapa nafasi ya pili watu wanaomcha Mungu, watu wema ambao wanatuacha kwaajili ya kutokuelewa mapenzi ya Mungu wakati nwa mapito yetu, Ayubu 42:10-11 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza. Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja.
       
21.   Uwe hodari kuliko walimu wako

Zaburi 119:80-100 “Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, Nisije mimi nikaaibika. Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelingojea neno lako. Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nisemapo, Lini utakaponifariji? Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, Sikuzisahau amri zako. Siku za mtumishi wako ni ngapi, Lini utakapowahukumu wale wanaonifuatia? Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, Ambao hawaifuati sheria yako. Maagizo yako yote ni amini, Wananifuatia bure, unisaidie. Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, Lakini sikuyaacha mausia yako. Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako. Ee Bwana, neno lako lasimama Imara mbinguni hata milele. Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa. Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, Maana vitu vyote ni watumishi wako. Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, Hapo ningalipotea katika taabu zangu. Hata milele sitayasahau maagizo yako, Maana kwa hayo umenihuisha. Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako. Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, Nitazitafakari shuhuda zako. Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali agizo lako ni pana mno. Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa. Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote. Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.

Mwandishi amezungumzia kwa kirefu sana namna na jinsi anavyoipenda sheria ya Mungu na kuishika amri zake na maagizo yake na mausia yake, na kuwa atayatafakari mausia ya Mungu, na vile vile alionyesha namna alivyoayashika mausia ya Mungu na kujionyesha namna na jinsi alivyojitoa kwa Mungu na neno lake na jinsi ambavyo neneo la Mungu limekuwa faraja yake kubwa sana hata hivyo, mwenye hekima hapa pia anajisifu kuwa amekuwa na ujuzi hata kuliko walimu wake, Jambo hili ni la msingi na la muhimu sana kila mtu anapaswa kuwa Hodari, na biblia inatutaka tuwe hodari, ikiwezekana tuwe na ujuzi kuliko walimu wetu, Katika mafunzo ya kijeshi cheo cha juu na cha mwisho kijeshi Duniani ni Gereral – Lakini Mwanajeshi huyo anapokuwa na uwezo mkubwa zaidi ya ule aliojifuza huwa anaitwa “Field -marshal” hiki ndio cheo cha juu zaidi cha kijeshi zaidi ya general Marshal kwa kiibraniamaana yake ni mtu aliye hodari hili neno linatumika katika Waebrania 11:32-34 “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni” neno kuwa Hodari maana yake ni kufanya zaidi ya jinsi ya ulivyofundishwa, kuwazidi walimu wako, uko usemi unaosema au uliosemwa na Yesu kuwa mwanafunzi hawezi kumpita mwalimu wake Matthew 10:24Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake.” Lakini ni ukweli usiopingika kuwa kuna wakati wasomi huwazidi walimu wao kwa uhodari kwa ujuzi na maarifa Apollo alikuwa mwanafunzi hodari wa neno la Mungu aliyewazidi hata walimu wake Prisilla na Akila Matendo 18:24-28 “Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko. Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu. Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi. Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu. Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo.” , na Paulo mtume alimzidi anania aliyemuwekea mikono kupokea Roho Mtakatifu na Mchungaji wake barnaba aliyempelekea Antiokia, Daudi naye anaonyesha kuwa unaweza kujifunza neno la Mungu na kulipenda na ukawa hodaroi kuliko walimu wako Zaburi 1119:98, Hiki ndicho Daudi alichokuwa akijisifia katika kifungu hiki cha maandiko kuwa amekuwa na ujuzi na hekima kuliko walimu wake jitengenezee mazingira ya kuwa na Ujuzi na elimu pana zaidi kuliko wengine, Daudi nsio tu alikuwa na hekina kuliko walimu wake bali pia wale watu wa zamani waliokuwa na hekima kabla yake  Ayubu 8:8-10 “Basi, uwaulize, tafadhali, vizazi vya zamani, Ujitie kuyaangalia yale baba zao waliyoyatafuta; (Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;) Je! Hawatakufunza wao, na kukueleza, Na kutamka maneno yatokayo mioyoni mwao?”
Mwandishi anaonyesha kuwa alikuwa Hodari kuliko mtu awaye yote katika kizazi chake alikuwa na hekina kuliko adui zake na ufahamu kuliko wazee, kimsingi Daudi anazungumzia ishu za kijeshi
1v – Lansi koplo
2v – koplo
3v- Sajent
Sir Maojr

Luteni usu
Luteni
Captain
Major
Luteni kanali
Kanali
Brigediaer
Brigedirer General
Luteni General
Genearal
Field Marshal
Katika vyeo vya Kijeshi general ndio cheo cha mwisho Duniani, lakini unapokuwa field Marshal maana yake wewe ni zaidi ya kawaida, Daudi alikuwa ni zaidi ya wakuu wa majeshi, aliweza kuwashinda, kina Sauli nakaka zake na kuwa na ujasiri wa kumpiga Giliath bila kupitia mafunzo ya kieshi, uhodari wake hapa ndio anaoutaka kuwa ni hekima na ufahamu na ujuzi mkubwa kuliko waliku wake.

22.   Lifanye neno la Mungu kuwa Taa ya Miguu yako!

Zaburi 119:101-105 “Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, Ili nilitii neno lako. Sikujiepusha na hukumu zako, Maana Wewe mwenyewe umenifundisha. Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu. Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo. Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Mwandishi anatukumbusha na kukazia umuhimu wa neno la Mungu, na mwenyewe akijua kuwa duniani sisi ni wapitaji na wasafiri, na kuwa hatuwezi kuwa na ugfahamu na ujuzi wa kilakitu duniani kwa vile sisis ni wageni basi ni neno la Mungu tu ndilo linaloweza kutuongoza na kutupelekea kule aliko kusudia Mungu 1Petro 2:11a “. Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.” Paulo mtume anasema kwa maana sisi wenyeji wetu uko mbinguni Wafilipi 3:20 “Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;” Dunia inatawaliwa na matendo ya giza, kuishi duniani kama wageni na wapitaji kunahitaji tuwe na dira na ramani taa na mwanga ili migu yetu iweze kupita kwa salama na  amani na ni neno la Mungu pekee linaloweza kufanya hivyo katika kile eneo la maisha yetu

Neno la Mungu ni taa Zaburi 119: 105, Nimeapa nami nitaifikiliza, Kuzishika hukumu za haki yako Litatusaidia wakati wa kufanya maamuzi Zaburi 119:106 Nimeteswa mno; Ee Bwana, unihuishe sawasawa na neno lako. litatuongoza wakati wa Mateso Zaburi 119:107, Litatulinda na mitego ya adui, litatuongoza kujitoa kwa Mungu  Litatuelimisha Zaburi 119:108-109, Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako. Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, Lakini sheria yako sikuisahau.Litatulinda na mitegi ya adui Zaburi 1119:109-110, “Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako” litatupa furaha na amani Heri kuuelekeza moyo wetu kwenye neno la Mungu daima Zaburi 119:111-112 “Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu. Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako, Daima, naam, hata milele

Kwa hiyo jumla ya majibu yote jinsi gani kijana aishafishe njia yake ni kwa kutii akilifuata neno la Bwana

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!