Alhamisi, 13 Agosti 2020

Imba wewe uliye tasa!

Isaya 54:1-4Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema Bwana. Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu. Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena”.


Utangulizi.

Katika changamoto mbaya sana duniani, tunazoweza kuorodhesha na zinazotesa sana watu utasa inaweza kuwa mojawapo, Utasa ni moja ya tatizo baya sana katika historia ya mwanadamu, utasa ni hali ya mwanamke au mwanaume kushiriki tendo la ndoa bila kinga yoyote kwa zaidi ya miezi kumi na mbili bila kupata matokeo!, Tatizo la utasa ni tatizo gumu sana na linaweza kusababishwa na kutokuwa sawa kwa homoni za mwanamke au mwanaume kunakopolekea kuleta shida katika mfumo wa uzazi. Tatizo kubwa linalozaliwa ni uwezo mdogo wa kubeba ujauzito na kunaweza kusiwepo ugonjwa mwingine. Kwa kuwa utasa sio ugonjwa lakini ni tatizo na lina uwezo wa kuathiri eneo kubwa sana la maisha ya mwanadamu, linasababisha kuweko kwa Mauvimbe ya ajabu kuzalishwa tumboni, fadhaa kubwa kwa mtu anayehitaji matokeo, matatizo ya kisaikolojia, wasiwasi, kupoteza matumaini, msongo wa mawazo, hatia, na kujihisi kama mtu usiyefaa kitu na hata kujisikia kufa, licha ya matatizo ya ndani anayoyapitia mtu aliye tasa pia kuna shutuma kutoka nje wanazopitia watu wasio na uwezo wa kuzaa

Wataalamu wa maswala ya uzazi wanaeleza kuwa katika utafiti walioufanya kwa wagonjwa 200 wanandoa wanaohudhuria clinic kwaajili ya kutaia uzao asilimia 50% ya wanawake na asilimia 15% ya wanaume walibainika kuwa na matatizo ya kiakili yaani kisaikolojia, aidha walipitia aina fulaninya mateso na manyanyaso na hayo yaliwapotezea furaha na kusababisha utasa, aidha katika utafiti mwingine wanawake 488 waliokuwa na tatizo la utasa walipoulizwa maswali walibainika kuwa na tatizo la msongo wa mawazo linalopelekea wao kuwa tasa.

Kwa ufupi utasa ni tatizo baya sana  ambalo wakati mwingine matabibu hawana uwezo nalo, na wakati mwingine ni Mpaka Mungu mwenyewe aingilie kati, Katika jamii ya Israel Mtu alipokuwa tasa alinyanyaswa sana na alijiona duni na mtu asiyefaa katika Israel utasa lilikuwa ni kama jambo la aibu kubwa na fedhea na watu waliokuwa tasa walinyanyapaliwa hata na wanawake wenzao kwa hiyo maumivu ya wanawake tasa katika jamii yalikuwa makubwa na yenye uchungu mno

a.       Sara alinyanyaswa na kijakazi wake ambaye alishika mimba ilihali bibi yake akiwa hana kitu mara baada ya hajiri kupokea ujauzito alimdharau sana Sara na kumdhihaki huku akijiona yeye kuwa ni bora zaidi ona Mwanzo 16:1-5Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake. Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. BWANA na ahukumu kati ya mimi na wewe.”

b.      Rebbeca alikuwa ni mwanamke mwingine anayetajwa katika Biblia kuwa alikuwa tasa mwanamke huyu kutokana na manyanyaso katika jamii alimsumbua mumewe akimwambia nipe watoto, alilewa Isaka akiwa na miaka 40 na alipata mtoto akiwa na mika 60 ona Mwanzo 25:20-26Isaka akawa mwenye miaka arobaini alipomtwaa Rebeka binti Bethueli, Mshami, wa Padan-aramu, ndugu wa Labani, Mshami, kuwa mke wake. Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA akamwambia, Mataifa mawili yamo tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo. Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake. Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau. Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.”

c.       Hanna aliteseka na hali ya utasa inaonekana mumewe pamoja na upendo mkubwa sana alishauriwa aoe mke mwingine na kama haitoshi mwanamke huyo alizaam, Hana hakuwa na mtoto hivyo alichokozwa na kutendewa vibaya na mke mwenza hali hii ilisababisha maumivu makubwa sana        kiasi cha kumfanya mwanamke huyu kushinda hekaluni akilia na kumuomba Mungu ona 1Samuel 1:1-10Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu naye alikuwa na wake wawili; jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina; naye huyo Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto. Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea Bwana wa majeshi dhabihu katika Shilo. Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa Bwana, walikuwako huko. Hata siku ile ilipofika Elkana alipotoa dhabihu, kumpa mkewe Penina sehemu, akawapa na watoto wake wote, waume kwa wake, sehemu zao; lakini Hana humpa sehemu mara mbili; maana alimpenda Hana, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo. Ila mwenzake humchokoza sana, hata kumsikitisha, kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo. Tena mumewe akafanya hivyo mwaka kwa mwaka, hapo yule mwanamke alipokwea kwenda nyumbani kwa Bwana, ndivyo yule alivyomchokoza; basi, kwa hiyo, yeye akalia, asile chakula. Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo wako una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi? Ndipo Hana akainuka, walipokwisha kula na kunywa huko Shilo. Naye Eli, kuhani, alikuwa akiketi kitini pake penye mwimo wa hekalu la Bwana.Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba Bwana akalia sana.”

Unaona wanawake hao na wengine wengi wanatajwa katika maandiko kuwa walipitia changamoto ngumu sana ya utasa, utasa ni tatizo bay asana kila mwanadamu na mwanamke mwenye akili timamu anatamani kuzaa, tena anatamani kuzaa kwa kiwango cha kutosha uzao ni Baraka kubwa nay a kwanza ya mwanadamu Mwanzo 1:28 “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” ili mwanadamu aendelee kuwepo juu ya uso wan chi anapaswa kuwa na uzao, uzao ndio unaoendeleza ukoo, mali na shughuli zote ntunazozifanya zitakosa warithi kama hatuna uzao, Mungu akikupa uzao amekupa urithi juu ya nchi  amekupa silaha tena hasa watotowanaozaliwa ujanani Zaburi 127:3-4” Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu. Kama mishale mkononi mwa shujaa, Ndivyo walivyo wana wa ujanani.” Kukosa watoto ilihesabika kama adhabu kubwa sana duniani ilikuwa kama laana, utasa ni kitu kibaya sana aidha pia kuharibika kwa mimba ni tukio bay asana Mungu aliwaahidi watu wake kama watamtumikia ataondoa kabisa utasa kabisa na kuwa hatakuwako aliye tasa wala mwenye kuharibu mimba ona Kutoka 23:25-26 “Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.   Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.

Katika mstari wa msingi Mungu analiona taifa la Israel na mataifa mengine na kumtumia Isaya nabii kuwaletea habari njema Israel walikwenda utumwani, katika hali ngumu sana wakidharauliwa na watu kama ilivyo kwa mwanamke aliye tasa, Na mataifa mengine wakiwa kama mwanamke asiyeolewa kila mmoja kwa jinsi yake anapitia hali Fulani katika maisha ambayo haizai, inaweza kuwa taifa, inaweza kuwa mtu, unapokuwa na hali ya umasikini, kile unachotaka kukitimiza au kukifanya hakifanikiwi, uko katika hali ya kushindwa kuzalisha au mipango isiyofanikiwa ni kama unataka mpenyo na hupati mpenyo unaokusudiwa hiyo ni hali ya utasa, huna furaha huna amani ni hali ya utasa, huna unalilifanya likafanikiwa ni hali ya utasa Nabii Isaya anawataka wote wanaopitia hali kama hiyo waimbe kwa maana Mungu anaahidi kuuondoa utasa, utasa ni tatizo ambalo linaweza kukabiliwa na Mungu pekee, yeye ndiye anayeweza khbadili hali ya mambo katika maisha yako, huduma yako, ukoo wako kijiji chako, taifa lako, familia yako, kushindwa kuzalisha kumekuletea fadhaa kubwa Isaya anasimama leo kutoa habari njema anasema imba wewe uliye tasa kwa maana watoto wako ni wengi mno watoto wako wanakuja , hakuna sababu ya kufadhaika yeye aliyebadili maisha ya Sara, akabadili maisha ya Rebbeka, akabadili maisha ya Hanna akabadili masiha ya Manoa akabadili maisha ya Elizabeth ana uwezo wa kubadili maisha yako leo na kuyafuta machozi yako na kukufanya uwe productive uwe mwenye faida mahali ambako umeonekana huna faida yoyote Mungu anajua fadhaa zako anajua uchungu wako anajua unayoyapitia na yuko tayari kutoa msaada unaolinga na na mahitaji yako! Kwa kawaida mambo yanapokuwa magumu mwanadamu hulia na hawezi kuimba lakini Isaya anatangaza mtu aimbe mtu achangamke kwa kuwa bwana anaahidi kubadilisha mambo katika maisha yako! Ni maombi yangu kuwa unapomaliza kusoma ujumbe huuu Mungu abadilishe mtazamo wako na kukupa uzao, uwe ni uzao wa tumbo lako, huduma yako, kanisa lako, biashara yako, kazini kwako shambani kwako na amani yako Mungu na akufanie muujiza akupobnye na kuondoa fedhea katika kila eneo la maisha yako akupe nguvu kwa upya ili uwe na uzalishaji katika maisha yako amen!

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

Jumanne, 4 Agosti 2020

Haki yenu isipozidi hiyo haki ya Waandishi na Mafarisayo



Mathayo 5:20 “*Maana nawaambia haki yenu isipozidi Hiyo haki ya waandishi na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa Mbinguni*



Utangulizi:

Waandishi na Mafarisayo ni akina nani ?

Ni muhimu kufahamu kuwa  nyakati za ulimwengu wa agano jipya yaani wakati wa Yesu Kristo katika Dini ya kiyahudi kulikuwa na Makundi (Madhehebu) mbalimbali ya watu mbalimbali wenye misimamo kadhaa ya kidini lakini makundi makubwa yaliyojulikana zaidi walikuwa Mafarisayo na Masadukayo, lakini kulikuwa na kundi lingine maarufu lililojulikana kama waandishi au wanasheria, na mengineyo yenye misimamo ya kisiasa na kidini lakini hapa nitawazungumzia Waandishi na mafarisayo tu kwa sababu ndio ambao wametajwa katika mstari wa Msingi kwamba “Haki yetu (Wakristo au wanafunzi wa Yesu) isipozidi hiyo haki ya Waandishi na mafarisayo Hatutaingia kamwe katika ufalme wa Mungu” kwanza tuwajue hao ni kina nani:-

Waandishi

Waandishi ni kundi la jamii katika dini ya kiyahudi waliokuwepo wakati wa Agano jipya ambao walikuwa ni walimu na watafasiri wa Sheria ya Musa Yesu alilitaja kundi hili kwa sababu walikuwa wasomi na watu waliobobea katika ujuzi wa torati, kazi yao kubwa pia ilikuwa kunakili sheria kutoka katika magombo ya chuo yanayochakaa au ya zamani na kuyanakili katika magombo mapya aidha watu hawa pia walijikita katika kusoma na kuielewa sheria ili kuwafundisha au kuwafafanulia watu.

                      Walijulikana pia kama wanasheria
                      Ni kundi la uamsho wa kimaandiko lililoanza wakati wa Ezra mwandishi baada ya watu kurejea kutoka uhamishoni Babeli
                      Waliitwa “SOFERIM” Kwa Kiebrania, maana yake watu wanaojua maandiko lakini pia waliitwa wenye hekima.

Ezara 7:10 “Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake kuitafuta sheria ya Bwana, na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli”.

Mafarisayo.

Kundi lingine la kidini katika dini ya kiyahudi waliokuwepo pia wakati wa agano jipya na wakati wa Yesu walijulikana kama Mafarisayo hawa walikuwa watu walijitahidi sana kuishi kwa haki na kuitii sheria ya Mungu kivitendo na kwa kujiamini na kujivunia Yesu alilitaja kundi hili kwa sababu lilikuwa na bidii katika utii wa torati lakini sio kwa moyo mweupe na hata wale waliokuwa na moyo mweupe waliishika sheria katika misingi ya kujipatia haki nje ya neema ya Mungu  Matendo 26:4-5Kwa maana Wayahudi wote wanajua maisha yangu tangu ujana, yaliyokuwa tangu mwanzo katika taifa langu huko Yerusalemu, wakinijua sana tangu mwanzo, kama wakipenda kushuhudia, ya kwamba nalikuwa Farisayo kwa kuifuata madhehebu ya dini yetu iliyo sahihi kabisa
               
                      Pamoja na Torati ya Musa pia waliamini maandiko mengine ya manabii na masimulizi ya kale ya kiyahudi kuwa ni neno kamili la Mungu
                      Walikazia sana maswala ya uadilifu kuliko Theolojia
                      Waliamini kuwa kuna maisha baada ya kufa, na pia wafu watafufuliwa
                      Wakliamini uwepo wa malaika, maono, na kuwepo kwa pepo wabaya

Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na mafarisayo!

Moja ya maandiko ambayo hutumiwa vibaya na wahubiri wengi wa injili ni na walimu wa Biblia  ni pamoja na andiko hili  *Mathayo 5;20* Maana nawaambia haki yenu isipozidi Hiyo haki ya waandishi na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa Mbinguni*” kimsingi kutokana na maandiko haya wakristo waliookoka na hata wale wasiookoka wametengenezewa makongwa mengi  na mazito sana  siku zote watafasiri wa neon la Mungu au maandiko wakikosea hata kidogo tu katika kuitafasiri maandiko wanaweza kusababisha tatizo kubwa sana sawa na Daktari kuzidisha dozi au kutoa dozi iliyo chini ya kiwango na ndivyo ilivyotokea kwa miaka mingi katika tafasiri ya mstari huu hebu sasa tuuangalie tena mstari huu kwa kina kwa kawaida mstari huo unasomeka hivi “*Maana nawaambia haki yenu isipozidi Hiyo haki ya waandishi na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa Mbinguni*” ndugu msomaji wakristo wengi  narudia tena wamefanywa kuwa watumwa na kubeba mizigo isiyowahusu kupitia andiko hili jinsi andiko hili lilivyo na kile kinachotafasiriwa au kukaziwa na wahubiri  na badhi ya walimu wa maandiko ni tofauti sana na hata na jinsi Kristo alivyokusudia  andiko hili kutumika.

Kwa ujumla kile ambacho wahubiri  na waalimu wengi wa neon la Mungu wengi wanakimaanisha katika maandiko haya ni kama maandiko haya yanasomeka hivi “*Maana nawaambia Matendo yenu yasipozidi Hayo Matendo ya waandishi na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa Mbinguni*” nimewahi kuwasikia wahubiri wakikazia wakristo kuwa na matendo yanayowazidi mafarisayo na waandishi yaani waalimu wa sheria tunapounganisha na swala zima la wokovu mafundisho ya aina hiyo sio injili sahihi tuliyoipokea toka kwa Bwana,

Wakati Fulani kwa sababu ya mafundisho ya aina hiyo nilikuwa nimejipangia kuwa ni lazima niamke kuomba Alfajiri kama vile waislam wafanyavyo na kwakuwa niliamini kuwa wao hawana Mungu wa kweli na aliye hai  kama niliye naye, Na kutokana na msisitizo wa mahubiri ya wachungaji wengi nilijifunza kuwa ninalazimika kuamka kabla ya Waislamu  hawajaamka na kumuomba Mungu ili matendo yangu yazidi hayo matendo ya mafarisayao na kwakuwa maisha yangu ya mwanzo kabla ya kumjua Mungu nilikuwa nikilala na kuamka kwa saa nilizotaka uamkaji wa Alfajiri lilikuwa jambo jipya katika maisha yangu na halikuwa jambo jepesi kusema ukweli. niliambiwa kuwa huko Korea ya kusini wakristo huamka alifajiri na kumuomba Mungu na wamepata mafaniko makubwa sana lakini sisi Afrika Mashariki wamishionari wetu  waliokuja mapema na kuleta Ukristo hawakuwa wametufunza kuamka alfajiri kwa  Msingi huo mwanzoni nilichapa usingizi lakini nilipomjua Mungu na kujifunza kuhusu kuamka alifajiri niligundua kuwa ninapaswa kuwawahi waislamu na siku kama ikitokea nimechelewa kuamka na wakanitangulia nilijihisi vibaya na kuonakama  kuwa siku hiyo ni chungu na sio siku nzuri  na labda imeharibika na nilihisi au niliiishi kwa maumivu ambayo sikuwa nayo kabla ya kuokoka kwa nini nilijifunza kuwa matendo yangu lazima yazidi yale ya Mafarisayo.

Kumbe nilikuja kugundua siri kutoka kwa Roho wa Mungu kuwa Mungu hakumaanisha kile nilichokifanya kimsingi Yesu alikuwa akizungumzia “*HAKI*” na sio “*MATENDO*” nililazimika kujifunza kuhusu haki kama mstari halisi unavyosema na niligundua kuwa kwanza hakuna mwanadamu mwenye haki hata mmoja *Warumi 3:10-12, Biblia inasema hivi “Kama ilivoandikwa ya kwamba hakuna mwenye haki hata mmoja hakuna afahamuye, Hakuna amtafutaye Mungu Wote wamepotoka wameoza wote pia hakuna mtenda mema la! Hata mmoja”* nilijiuliza kama hakuna mwenye haki hata mmoja inakuwaje Yesu aseme haki yetu isipozidi haki ya mafarisayo hatutauona ufalme wa Mbinguni?

Nikagundua kuwa kumbe Mafarisayo hawakuwa na haki hawakuwa na haki ya kweli haki waliyokuwa nayo ilikuwa haki ya nje tu, Yesu aliwataja waandishi kwa sababu walikuwa wasomi waliobobea katika maandiko na aliwataja mafarisayo kwa kuwa walikuwa na juhudi ya kutafuta haki kwa nguvu zao, Makundi haya yalikuwa na haki ya nje ya kidini tu na haikuwa haki yenye faida yoyote kwa ufalme wa Mungu haki yao iliwekwa katika misingi ya matendo ya nje yasiyotoka moyoni na yenye kubeba utukufu wa kibinadamu tu na zaidi sana waliwadharau watu wengine wakifikiri kuwa watu hao ni wenye dhambi na wasiofaa au ambao hawawezi kukubaliwa na Mungu kwa sababu ya kujifikiri kuwa waio ni bora zaidi  ona kwa mfano Luka 18:10-14  Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.” Unaweza kuona kwa hiyo kwa mtazamo wa nje na wa kibinadamu waandishi na Mafarisayo waliokuwa wenye haki iliyochanganyika na kiburi, wakijidhani kuwa wao ni watakatifu na wenye kibali kwa Mungu kuliko wengine walikuwa hawana ujuzi kuwa Mungu ndiye mwenye kutuhesabia haki na kuwa ni Mungu ndiye anayeujua moyo wa Binadamu.      

 “*Mathayo 23;25-28* “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia. Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang'anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi. Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote.Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi”.

Yesu anawaonya mafarisayo “*Ole wenu waandishi na Mafarisao wanafiki …..*” kumbe mafarisayo walikuwa wanafiki hawakuwa na haki ya kweli, Haki yao ilikuwa haki ya nje walifanya mambo ili waonekane na watu *Mathayo 23;5a* “*Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu*;” kumbe mafarisayo haki yao ilikuwa ni haki ya nje haki ya kujionyesha tu walionekana na watu kuwa ni wenye haki lakini kwa kweli hawakuwa na haki ya kweli na ndio maana na sio hivyo tu walikuwa na dhambi ya dharau au walikuwa na kiburi wakijifikiri kuwa waoa ni watakatifu au wana kibali kwa Mungu kuliko watu wengine waliowadhani kwa akili zao na mawazo yao kuwa ni wenye dhambi ona maneno haya Luka 18:9 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.   Ni kwaajili ya haya utaweza kuona kuwa Yesu alisisitiza kuwa ni lazima iwepo haki mbadala, haki ambayo ni tofauti na haki na ile ya  waandishi na mafarisayo  ambayo kimsingi ni haki ya nje.  Sasa ili mtu aweze kuingia katika ufalme wa mbinguni hawezi kuingia kwa haki kama ile ya waandihi na mafarisayo ambayo ilikuwa ya nje ni kweli walionekana wanashika sheria walionekana wanaomba, walisifu na kufunga walisoma neno la Mungu  na hata kuhudhuria ibada  hata hivyo walifanya hayo ili waonekane na watu wasifiwe waonekane kuwa wao ni wa kiroho na washika dini wakubwa huu haukuwa mtazamo sahii, haki mbadala ni haki ambayo haitokani na matendo ya sheria  ni haki kutoka moyoni ni haki itokanayo na imani  ni neema ya kukubali kazi aliyoifanya Yesu Kristo kwaajili yetu Msalabani ni haki itokanayo na Kristo *Warumi 3;21-26*Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;  kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa.apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.*

Angalia pia Waefeso 2;1-9 *Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine. Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu

hii ndio haki mbadala aliyoizungumzia Bwana Yesu kwa hiyo Kristo hajatuita katika mashindano ya kuwazidi wale tunaowaita mafarisayo kwa matendo kama ukifanya hivyo wakikushinda unakuwa chini ya kongwa ambalo hata kabla ya kuokoka hukuwa nalo, Mtu anapomuamini Yesu mara moja Yesu anafanyika kuwa haki yetu ipatikanayo kwa neema na  wala sio kwa matendo  neema ya Kristo ndani yetu inatugeuza na kutufanya kuwa wema yenyewe na hivyo kutupelekea katika Tito 2:11-12 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na HAKI, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;  Kwa hiyo Yesu hakumaanisha kuwa matendo mema ni mabaya la hasha matendo mema yanakubalika kwake ykihusisha imani na rehema kutoka kwake Yesu yeye ndiye anakuwa haki yetu ambayo ni zawadi kutoka kwake ni neema kutoka kwake  Biblia inasema hivi

1Wakoritho 1:30 -31 “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na HAKI, na utakatifu, na ukombozi; kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.

2Wakoritho 5:21 “Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa HAKI ya Mungu katika Yeye.”

Kumbe unaweza kuona haki halisi haitokani na nafsi zetu haki halisi ni ile tunayopewa kwa imani kwa kumuamini Yesu na kukubali kazi yake aliyoifanya pale msalabani, ni aina hii ya haki ndiyo ambayo Yesu alikuwa anaizungumzia na manabii walitabiri kwa kumuamini Mungu yeye sasa anafanyika kuwa haki yetu

Yeremia 23:5-6 “Tazama siku zinakuja, asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi. Katika siku zake Yuda ataokolewa, Na Israeli atakaa salama, Na jina lake atakaloitwa Ni hili, Bwana ni haki yetu.”   

Kujaribu kwa njia za kibinadamu kuishi maisha ya kujitafutia haki bila imani kwa Yesu Kristo kutatufabya tuishi katika Kongwa kubwa sana la matendo yatakayotufanya tuuone wokovu kuwa ni kitu kigumu sana na kumbe wokovu ni mwepesi na raha nafsini mwetu

Ukiyajua hayo heri wewe ukiyatenda

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!