Jumanne, 28 Juni 2016

Birthday iliyonifanya nitumbuliwe na mke wangu!


Week iliyopita nilikuwa na birthday yangu lakini mke wangu, watoto wangu hata wazazi wangu wote hawakunitakia heri ya kuzaliwa.

 Mke wangu mara baada ya kunikuta nimechizika kwenye sofa!
 
Nilienda kazini lakini hakuna hata mfanyakazi hata mmoja aliyenitakia heri ya kuzaliwa, nilipokuwa naingia ktk ofisi yangu katibu muhtasi wangu (secretary) akaniambia "Happy birthday bosi wangu" hapo ndipo nilijihisi wa maalumu (special) mnoo.
 
Akaniomba mchana twende tukapate lunch pamoja! Nilimkubalia na kuona kuwa hakuna maana hata ya kuwaza nyumbani tena, Tulienda na baada ya lunch akanialika nyumbani kwake anakoishi nalo niliona halina shida hata nikikawia kurudi nyumbani haijalishi.
 
Tulienda kwake na tulipoingia kwake akaniambia kwa sauti ya mahaba "Naomba niende chumbani kwa dakika moja narudi sasa hivi"  alisikika akibembeleza kimahaba nilijibu sawa huku nikiwa na mchecheto mno na kiroho kilianza kwenda kwa kasi.

Nilijua wazi kuwa huyu demu atakuwa ameni mind na huenda anakwenda kujiandaa kwa sex na mimi, na nilihisi atarejea akiwa ameondoa suti yake nzuri aliyokuwa amevaa siku hiyo na kwa vyovyote atarejea akiwa katika hali ya kunipa mahaba mazito

Sasa, kutokana na kujawa na mawazo ya kingono nilikuwa tayari nimejiandaa kumpokea kwa mahaba mazito na tayari kujibu shambulizi lolote la kimapenzi mara mara atakaporudi!
 
Alitoka baada ya dakika tano hivi alirejea akiwa amebeba keki ya birthday  Lakini kama haitoshi huku alikuwa ameambatana  na mke wangu, watoto wangu, mama yangu,Msichana wetu wa kazi na baadhi ya rafiki zangu wote wakisema  kwa nguvu sana SUPRISEEE!!!
 
Na nilikuwa nikisubiri katika sofa pale sebuleni NIKIWA NSHAVUA SURUALI NA PEPO LA NGONO LISHENIPANDA!
 
Masikini mie! Mawazo ya Ngono yameniponza! 

Kwa akili zako finyu unadhani nitakuwa nimejitumbua au nimetumbuliwa?
 
Hapa ninapozungumza mwenzenu Sina mke hivi sasa na heshima yangu iko jalalani!.

"Heri wenye Moyo safi maana hao watamuona Mungu" Mathayo 5:8 

Na Kirima Gs Baba God!
Edited by Rev. Kamote Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima!

Jumapili, 26 Juni 2016

Bwana Ndiye Mchungaji wangu!


Zaburi 23:1-6 Biblia inasema
 1. Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 2. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 5.Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. 6. Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.”

 Bonde la Wadi Quelt linalotajwa na daudi kama Bonde la Uvuli wa Mauti katika Zaburi 23.

Zaburi hii ni moja ya zaburi muhimu sana na Yenye maneno ya maana sana yenye usalama, Ingawa maandiko yake ni machache lakini yamebeba maana pan asana na nzito mno isiyoweza kupimika kuhusu Upendo wa Mungu kwa watu/mtu wake, Ni zaburi ambayo inaweza kutufunulia kwa kina upana na urefu wa Hali halisi ya uhusiano wa Mfalme Daudi na Mungu. Tutajifunza Zaburi hii kwa kutafakari vipengele vitatu vifuatavyo:-

·         Historia ya Zaburi hii
·         Bwana ni Mchungaji wa Ajabu
·         Sitaogopa Mabaya

Historia ya Zaburi hii:-

Zaburi ziko za Aina mbalimbali, lakini zaburi hii inaangukia katika Kundi la Zaburi za kujitia moyo, Katika moja ya chanzo yaani Commentary ambayo niliiisoma, inatuhakikishia wazi kuwa zaburi hii ni ya Daudi aliyekuwa mfalme wa Israel, Lakini sababu ambazo zilipelekea Daudi kuandika zaburi hiii ambayo inaonekana aliiandika kabla ya kuwa mfalme inazungumzia mazingira ya Bonde liitwalo kwa Kiarabu Wadi Quelt unaweza kugoogle jina hilo katika wikipidia, Bonde hili liko katika ukanda wa Magharibi yaani West Bank wa Mto Jordani Karibu na Yerusalem njia ya kuelekea Yeriko karibu na bahari ya Chumvi, Eneo hilo lilikuwa ni eneo hatari sana na lenye majabali ambapo kama mtu angeangukia huko kifo tu ndio kingekuwa zawadi yake, ni Bonde la Kutisha sana na njia yake pia ilikuwa na vibaka na majambazi na huenda ilikuwa ni simulizi na maonyo kutokupita eneo hilo hatari lililoogopewa sana, Bonde hilo lenye kutisha lilikuwa ni halisi na ni halisi hata sasa kwa vile liko hata leo, Kwa vile lilikuwa ni Bonde lenye kuogopesha wengine waliliita Pango la Jabali au Bonde la Mauti, kuna uwezekano kuwa watu wengi walipoteza Maisha katika eneo hilo na hata wachungaji walipoteza mifugo yao huko na walishindwa kuiokoa.

Bwana Ni Mchungaji wa Ajabu:-

Daudi anataka kumfunua Mungu anayemjua Yeye na mwenye uhusiano naye Jinsi alivyomkuu na alivyo na ujasiri kumtegemea, anataka kuionyesha jamii kuwa yeye anaweza kupita katika Bonde hilo lenye harufu ya kifo na akatoka salama, kule ambako jamii nzima inaogopa yeye angeliweza kupita tu kwa  sababu hakuna jambo lolote lenye kuogopesha linaweza kulinganishwa na Mungu wa Daudi na Mchungaji mwema, Kuweza kufahamu kila Daudi anakizungumzia ni lazima tufanye uchambuzi wa Maneno mazito yaliyomo katika zaburi hii.

1.       Bwana ni Mchungaji wangu – Kwa ufupi sana Daudi anatumia Mfano huu (Metaphor) ambao mara nyingi umetumiwa sana na waandishi wa Biblia hususani katika Agano la kela kuonyesha jinsi Mungu anavyojali na kujihusisha na watu wake (Zaburi 28:9, 79:13, 80:1, 95:7 Isaya 40:11Yeremia 31:10 na Ezekiel 34:6-19) Yesu mwenyewe alikuja kuuweka wazi kabisa kuwa Yeye ndiye huyu Mchungaji mwema anayetajwa katika zaburi hii na maandiko mengine  Yohana 10:11-16, Ukweli unaofunuliwa hapa ni sisi ni watoto wa Mungu Mungu ni Baba na ni mwangalizi mkuu wa Maisha yetu, Yeye hutujali na kutuangalia kwa upendo mkubwa sana kuliko wachungaji wanavyoangalia mifugo, Jambo kubwa la Msingi ili kunufaika na Bwana kama ilivyokuwa kwa Daudi ni lazima uwe na uhusiano wa kudumu na Mungu wetu.

2.       Sitapungukiwa kitu – Mungu kama Mchungaji mwema yuko tayari kurupatia malisho, huu ndio ulikuwa wajibu mkuu wa wachungaji wa wanyama walipaswa kuhakikisha kuwa Konndoo wanashiba ipaswavyo, ni wazi kuwa Mungu hushughulkika na mahitaji yetu kiasi ambacho hatutapungukiwa na kitu

3.       Kando ya malisho ya majani mabichi hunilaza – Ulikuwa ni wajibu mwingine wa Mchungaji kuhakikisha kuwa anawapa raha mifugo yake, ikiwa Mungu ni Mchungaji mwema na sisi tu Kodnoo zake yeye hutupa kustarehe pia Yesu alisema Njooni kwangu ninyi nyote wenye kuelemewa na Mizigo nami nitawapumzisha “Mathayo 11:28” haingekuwa hekima ya kawaida common wisdom kwa Mchungaji kuwazungusha mifugo kutwa nzima bila kuwapa pumziko, Mungu anajua kuwa tunahitaji pumziko, ingawa tunapitia changamoto za aina mbalimbali katika ulimwengu huu, Mungu atatupa nyakati za Kuburudika, Acha kusema kuwa utapumzika Kaburini, au au Heri wafu wafao katika Bwana, hayo maneno Daudi hakuyatamka hata kidogo yeye alljua kuwa Mungu atampa pumziko sawa kuna hilo la baadaya lakini hapahapa duniani pia tutafaidika na kazi za Mchungaji mwema, Mungu atalitumia neno lake kama chakula kutulisha na kututia nguvu,Yohana 6:32

4.       Kando ya maji ya utulivu huniongoza. – Ni wazi kuwa Maji yanawakilisha uwepo na faraja ya Roho Mtakatifu, kwa wale wakristo amabao wamejazwa Roho mtakatifu wanafahamu jinsi anavyoburudisha na kuleta utulivu mioyoni mwetu hata kama twapitia majaribu ya aina mbalimbali, Yeye ndio Chemichemi ya uzima acha kujichimbia visima vyako Yeremia 2:13 Roho wa Mungu yuko kutupa faraja ya kweli, ambayo haipatikani kwa Pombe au zinaa au uvutaji wa Bangi kila aina ya burudiko na bubujiko lililo bora utalipata kwa Roho wa Mungu

5.       Hunihuisha nafsi yangu – katika ulimwengu huu tulio nao yako mambo mengi ya kukatisha tamaa na kuvunja Moyo na kuifanya nafsi kuinama, Mungu wa Daudi aliweza kumtia nguvu alimtia Moyo, Zaburi 42:11, Tunapokutana na wakati mgumu wa kukabiliana na changamoto mbalimbali kama tumemfanya Yehova kuwa Mchungaji wetu atatufariji na kuzihuisha nafsi zetu, Daudi alilifahamu hilo vema aliona wema wa Mungu ukifanya hayo katika maisha yake

6.       Huniongoza Katika njia za Haki – Ni muhimu kufahamu kuwa ni Mungu kupitia Roho wake mtakatifu ndiye anayetuongoza katikia njia ya haki Warumi 8;14, Kwaasili mwanadamu havutiwi sana na kutembea katika haki, moyo na nia ya kuhakikisha kuwa tunatembea katika haki hupatikana kwa msaada wa Roho Mtakatifu, na ndio maana ni muhimu ikaeleweka wazi kuwa haki tuliyo nayo haitokanani na uweza wetu na uamuzi wetu ni haki ya Yesu Kristo na tunatembea katika hiyo kwa neema na uongozi wake Daudi alilijua hili wazi,Warumi 8:5-14, alitambua nia ya mwili siku zote inafanya uadui dhidi ya Mungu na kuwa kama anatembea katika haki ni kwa sababu ya utii wake wa kukubali kumsikiliza Mchungaji mwema na so sauti ya Mgeni Yohana 10:3-4, 5.

7.       Kwaajili ya Jina lake:-  Mungu hutufanyia miujiza mikubwa na kutisha na kushangaza kwaajili ya jina lake, wema wote anaotutendea Mungu hufanya ili apate utukufu Zekaria 2:8Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake” Mungu hututetea kwaajili ya Utukufu wake Daudi alijua wazi kuwa kuna kitu cha ziada ndani yake jina la bwana linatukuzwa na hivyo kamwe Mungu hataacha kumuongoza katika njia za haki kwa sababu ya Jina lake takatifu aliloliweka ndani ya Daudi, Mungu akiweka kitu ndani yetu atatuongoza kwaajili yake

8.       Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami:- Daudi sasa analitaja lie Bonde la Wadi Quelt Bonde lenye kutisha sana, ni wazi kuwa Daudi analitumia Bonde hilo kuonyesha kuwa kuna magumu katika ulimwengu huu kuna mambo ya kutisha katika ulimwengu huu, Mungu hatatuacha tusipitie katika magumu, na majaribu, kwamba iwe ni nyakati za hatari, Magumu au hata hatari za kifo Yeye hataogopa mabaya kwa sababu Mungu atakuwa npamoja nayeYeye ni Mlinzi wetu,na ni Mwaminifu kamwe hawezi kutuacha Mathayo  28:20 Nami nitakuwa pamoja nayi hata ukamilifu wa Dahari Mungu ataendelea kuwa pamoja nasi

9.       Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.:-  Fimbo na gongo vinawakilisha Mamlaka na silaha za Mungu pia humaanisha kutia nidhamu, au kurudi, kuadhibu, pia inawakilisha nguvu na utendaji wa Mungu Kutoka 21:20, Ayubu 9:34 fimbo ilitumika katika kumrudisha kondoo katika njia au kundi sahihi na iliwaadhibu pale walipokuwa kinyuma na matakwa ya Mchungaji, Mungu huwadhibu wale wampendao ili kuwapa nidhamu yeye mwenyewe lakini pia huwalinda na kuwatetea Gongo liko kwaajili yanulinzi na Usalama wa Kondoo.

10.   Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.:- Ukweli ni kuwa wanadamu hawafurahii mafanikio ya wanadamu wengine hata siku moja, kutokana na ubinadamu wao ndani yao kuna wivu na hivyo ni rahisi kuwa na maadui unapobarikiwa na Mungu, Lakini sio hivyo tu Mashetani majini na mapepo hayafurahii uhusiano wetu na Mungu, Daudi alifahamu wazi swala hilo lakini kutokana na ukuu na wema wa Mungu Daudi anamuona mungu kuwa ni mwenye kujali sana , ni mwenye kujali na kulata usalama kiasi ambacho pamoja na hatari ya mashetani na majini na mapepo na madui wa kibinadamu, Bado Mungu anatoa neema na Baraka za Kutosha anakubariki na kukufanikisha mbele ya wanaokuchukia, na hata wale waliokubali kutumiwa na shetani kututesa, Licha ya Baraka zake dhidi ya wanaotuchukio Mungu aliendelea kuonyesha kuwa Daudi ni Mtumishi wake tu ni mtumishi maalumu aliyemchagua amempaka mafuta! Hii ilikuwa ni Dalili ya wazi kuwa yeye amechaguliwa na Mungu na ana upendeleo maalumu na wa kipekee ana uhusiano na Roho Mtakatifu ulio wa Pekee  na kwa sababu hiyo hapungukiwi na kitu, Kikombe kilichofurika kinazungumzia mabalasi yenye uwezo wa kuchukua Galoni 40 za maji, Daudi alimaanisha kuwa kombe lake linafurika ukiwa na Mungu huna shaka maana Balasi lako halipungui, Ukimtegemea Mungu hutapungukiwa na kitu neema na rehema na kufurika roho wa Bwana kutaendelea kububujika siku zote za maisha yetu.

11.   Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele:- Mchungaji siku zote aliandamana na kondoo kila walikokwenda uhusiano ulistawi waliwapenda na kuwa kitu kimoja, Daudi amabaye ana ujuzi mkubwa wa Kuchunga anaelewa wazi kuwa Mungu yuko pamona naye anafuatana naye akiwa na uso wa wema akiwa yuko tayari kufadhili,alijua kuwa Mungu akiambatana nawe siku zote atatoa msaada wenye kudumu, wema na fadhili bila kujali nini kitatokea mbele yako, Mchungaji hufanya shughuli zake zote kwaajili ya kondoo wake, daudi anamalizia kwa kuonyesha kuwa Lengo lake kuu la kuambatana na mchungaji huyu mwema ni ili siku moja autazame uso wake amtumikie na kumuabudu yeye milele.

Sitaogopa Mabaya:-



Nataka kuhitimisha ujumbe huu kwa kukazia kuwa ukimjua Mungu katika viwango ambayo Daudi alimfahamu Mungu, Hutaogopa chochote katika maisha yako, Mungu ndio zindiko letu, yeye ndie Mwamba ngao na kimbilio hatupaswi kuogopa lolote unapotamka Neno hilo Bwana ndiyo Mchungaji wangu! Kifurushi hicho cha Bwana ndiye Mchungaji wangu kinabeba maswala kadhaa  Nina uhusiano wa kipekee na Mungu, Yeye ndio anayenitunza, yeye ndiye starehe yangu na faraja yangu, Yeye ni faraja yangu, yeye ndiye mlinzi wangu, yeye ni mwaminifu, atanishindia majaribu, nimewekwa wakfu kwake, amanibariki, amanipa upako, ananitosheleza, niko naye milele mpango wangu ni kutokumuacha haya yote yatakufanya usiogope kitu chochote katika maisha yako na yeyote atakayejifanya kuwa ni adui yako atashangaa ukiandaliwa Meza machoni pake, kwaajili ya utukufu wake.
 


Ujumbe na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote!

Alhamisi, 23 Juni 2016

Watu wa Kizazi Hiki!



Mstari wa Msingi: Luka 7: 29 – 35.
 
Biblia inasema :-  29. Na watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, waliikiri haki ya Mungu, kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohana. 30. Lakini, Mafarisayo na wana-sheria walilipinga shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye. 31. Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini? 32. Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia. 33. Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo. 34. Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi. 35. Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote”.
 
Katika kifungu hiki cha maandiko kuna maswala ya msingi sana ya kujifunza, kuhusiana na watu wa kizazi cha leo ambao hawatofautiani sana na Kizazi cha wakati wa Yesu na Yohana Mbatizaji walipokuwa Duniani.

Kifungu kinaonyesha kuwa:-

·         Watu wote walilisikia neno la Mungu yaani Shauri la Mungu na kusudi lake, waliosikia shauri la Mungu walikuwa watu wabaya, wenye dhambi,  watoza ushuru nk, lakini pia Mafarisayo na waandishi (waandishi wanaitwa Lawyers au an Expertise of the law of Moses) yaani wataalamu wa Sheria na Torati ya Musa wote walisikia ujumbe wa Mungu kupitia Yohana na baadaye Yesu

·         Wote walisikia Unabii na walifahamu sana habari za Zakaria aliyemzaa Yohana na Yohana mwenyewe walitambua kuwa walikuwa watu wa namna gani

·         Lakini jambo la kushangaza ni kuwa  Mafarisayo na waandishi walikataa ujumbe wa Yohana mbatizaji na zaidi ya yote walikataa pia ujumbe wa Yesu Kristo, hawakukubali kutii Ushauri wa Mungu, Hata pamoja na Mungu kutumia njia mbalimbali na mitindo mbalimbali ili waelewe kusudi lake

·         Kilikuwa ni kizazi ambacho huwezi kukifurahisha kwa namna yoyote, ukiwajia kwa shangwe na filimbi HAWACHEZI, sawa Ukiwajia kwa Maombolezo HAWALII, Yesu alikuwa anaonyesha ni Jinsi gani anawathamini sana na wanadamu na anataka kwa namna yoyote ile wamgeukie yeye na kufuata njia zake Lakini Yesu anaonyesha wazi kuwa ni vigumu sana Kumpendeza Mwanadamu kwa sababu Mungu mwenyewe walimkataa hata pamoja na kuwajia kwa njia mbalimbali.

Katika Nchi Yetu pia tunaweza kushuhudia maswala yanayofanana na hayo, Rais aliyepita alikuwa mpole, na alikuwa anasafiri sana kwenda nje, na hakuweza kuwashughulikia wabadhirifu, watu walipiga kelele sana , akaja rais ambaye ni mkali na ameanza kuwashughulikia mafisadi waziwazi, wakasema he is self appointed Judge, Hasafiri wakasema rais gani hasafiri, wekea wanafunzi Pilau kila siku na nyama kila siku watasema tumechoshwana nyaka kila siku, weka Pelege watasema zina minyoo, wapige maharage watasema kila siku maharage, weka Kade watasema makande tu, ondoa watasema tumeyamisi makande, Ni kawaida ya wanadamu kutokucheza mziki wowote ule iwe “Ragge”r au “Blues”

Maandiko yanatushauri kuwa tusikatae mashauri ya Mungu ziko sababu za msingi kwanini tuukubali Ushauri wa Mungu.

1.       Mwanadamu hawezi kujiongoza Mwenyewe Yeremia 10:23
2.       Mwanadamu akijiongoza mwenyewe mwisho wake ni mauti Mithali 14:12
3.       Nje ya Mungu Hakuna njia Nyingine Yohana 6:68
4.       Watu wakimkataa Mungu Mungu huwacha wafuate njia zao zilizopotoka na hatimaye ataleta hukumu  Warumi 1:28.

 Watu wa Kizazi Hiki
5.       Mwisho ni hekima ya Mungu tu ndiyo itakayoshinda na shauri la Mungu litadumu na kujulikana kuwa la haki. Luka 7:35

Mwisho ni muhimu kufuata Mashauri ya Mungu na kusimama nayo kabla hatujachelewa
Rais wa Marekani John F Kennedy alisem:-

~“The time to repair the roof is when the sun is shining.”~

Tafasiri yangu isiyo rasmi
 
~“Muda wa kukarabati paa ni wakati jua linawaka”~
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote

Jumanne, 21 Juni 2016

Mti wenye kuleta Heshima kwa Mungu na wanadamu!



Waamuzi 9:8 – 13. Biblia inasema hivi:- 

“8. Siku moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti mzeituni, Tawala wewe juu yetu. 9. Lakini huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? 10. Kisha miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu. 11. Lakini huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende nikayonge-yonge juu ya miti? 12. Kisha miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu. 13. Huo mzabibu nao ukaiambia, Je! Niiache divai yangu, ambayo humfurahisha Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti?” 

Leo tutachukua muda kutafakari kwa kina na upana na marefu kuhusu mti wenye kuleta Heshima kwa Mungu na wanadamu, Ninazungumza jambo muhimu sana litakaloifaa jamii ya leo ambayo imejaa watu wanaoteseka kwa kukosa maarifa, kama utafuatilia somo hili kwa moyo maisha yako yatabadilika na utakuwa na furaha maishani mwako, Leo nataka kuzungumzia kuhuzu mti wa Mzeituni (Olive Tree) lakini kwanza nataka ufahamu jambo hili

Mwanzo kabisa Mungu alipouumba ulimwengu alitoa zawadi ya mimea na miche pamoja na miti kwa wanadamu kama chakula na zawadi soma Mwanzo 1:29 “ biblia inasema 

29. Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; 30. na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo. 
  
Miche na miti katika biblia ya kiingereza huitwa Herbs tuangalie Biblia ya Kiingereza tafasiri ya King James Bible inasema:-

"And God said, Behold, I have given you every herb bearing seed, which is upon the face of all the earth, and every tree, in the which is the fruit of a tree yielding seed; to you it shall be foe meal"

Ni wazi kuwa miti na mimea ndio chakula cha kwanza walichopewa wanadamu kabla ya kuongezewa nyama katika Mwanzo 9:3 baada ya gharika wakati wa Nuhu, Moja ya mti muhimu sana unaotajwa katika Biblia ni mti wa Mzeituni na tunda la zeituni na mafuta ya mzeituni huu ni moja ya mti muhimu sana katika uumbaji wa Mungu, Wayahudi na waarabu na wakristo wa zamani sana walifahamu sana umuhimu wa mmea wa mzeituni ukilinganisha na nyakati tulizonazo katika kizazi hiki, ni kwasababu hiyo leo Mkuu wa wajenzi ninataka kuchukua muda kueleza maswala kadhaa muhimu kuhusu mti huu wenye kuleta Heshima kwa Mungu na wanadamu.

Mmea wa Mzeituni ni mmea unaomea kwa wingi sana katika nchi ya Israel, Hata leo, mashamba ya mizeituni yametapakaa kutoka sehemu za chini ya Mlima Hermoni upande wa kaskazini hadi viunga vya Beersheba upande wa kusini. Mizeituni bado inapatikana kwenye pwani ya Uwanda wa Sharoni, vilima vyenye mawemawe vya Samaria, na mabonde yenye rutuba ya Galilaya lakini pia ni mmea unaostawi na kuzalishwa kwa wingi katika inchi ya Hispania (Spain) Nchi hii kwa sasa ndio inayoongoza kwa uzalishaji wa Mafuta ya Mzeituni na sehemu nyingine nyingi duniani, Mungu ameupa mmea huu uwezo wa ajabu sana kama tutakavyoweza kuona mbeleni lakini pia mmea huu kwa tabia zake ni mmea ambao hauwezi kuharibiwa,Unapoukata mzeituni unauwezo wa kutoa machipukizi mapya na ukaendelea kuwepo mara moja, Matunda yake yanauwezo wa kutoa au kuzalisha mafuta mengi ambayo hutumika kwa shughuli mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kupikia, kujipaka, kuwashia taa, na kutibu wanadamu, katika shughuli za Ibada mmea huu ni mmea wa kikuhani kwa vile unatumika kutangaza rehema za Mungu na unatumiwa katika ishara ya amani, kuweka wakfu viongozi wa kisiasa, kijamii na kidini yaani Wafalme, Makuhani na manabii. Aidha mti huu mafuta yake na matawi yake hutumika katika kufukuza Mapepo (Mashetani na Majini) kwa jina la Yesu.

Katika kuwatia Moyo Israel katika safari yao ya kwenda Kanaani moja ya vitu vyenye mvuto sana kwa wana wa Israel ambavyo Mungu alimtumia Musa kuvitaja ilikuwa ni pamoja na Mizeituni yenye mafuta.  Kumbukumbu 8:7-8 biblia inasema 

7. Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima; 8. nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;

·         Sifa za Mzeituni
·         Historia ya Kibiblia kuhusu Mzeituni
·         Matumizi ya Mzeituni

Sifa za Mzeituni.

Kwa kawaida Mzeituni ni mti usio na Mvuto ukiuona kwa mara ya kwanza. Si mrefu kama mierezi fulani yenye kuvutia ya Lebanoni. Mbao zake hazina thamani kama mbao za mberoshi, na maua yake hayavutii kama maua ya mlozi ambayo ilitumika kujengea Nyumba katika Israel kama maandiko yasemavyo katika wimbo ulio bora 

Wimbo Ulio bora 1:17 Biblia inasema hivi:- “Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi”. Na Amosi 2:9 9. “Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini”.

Sehemu muhimu zaidi ya mzeituni haionekani—iko chini ya ardhi. Mizizi yake mingi, ambayo hufikia kina cha meta sita chini ya ardhi na kwenda hata mbali zaidi kuelekea upande-upande, ndiyo hasa hufanya mti huo uzae sana na kustahimili hali ngumu.

Mizizi hiyo huiwezesha mizeituni kwenye vilima vyenye mawemawe istahimili ukame wakati ambapo miti iliyo kwenye bonde imekwisha kauka kwa kukosa maji. Mizizi huiwezesha kuendelea kuzaa zeituni kwa karne nyingi, ingawa huenda shina lisilovutia likaonekana kuwa lafaa tu kwa kuni. Mti huo usiovutia huhitaji tu nafasi ya kukua na udongo wenye hewa, bila magugu au mimea mingine inayoweza kuwa na wadudu waharibifu. Mahitaji hayo sahili yakitimizwa, mti mmoja utatoa lita 57 za mafuta kila mwaka.

Historia ya Kibiblia kuhusu Mzeituni.

Kibiblia Mzeituni unatajwa kwa mara ya kwanza katika Kitabu cha Mwanzo 8:6-12 “6. Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya; 7. akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi. 8. Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi; 9. bali yule njiwa hakuona mahali pa kutua kwa wayo wa mguu wake, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani. 10. Akangoja na siku saba tena; kisha akamtoa yule njiwa katika safina mara ya pili, 11. njiwa akamjia jioni, na tazama, alikuwa na jani bichi la mzeituni kinywani mwake, ambalo amelitunda, basi Nuhu akajua ya kwamba maji yamepunguka juu ya nchi. 12. Akangoja na siku saba tena, akamtoa yule njiwa; naye asimrudie tena kamwe.”

Mzeituni unatajwa kama mti ulioashiria amani baada ya Hasira za Mungu alipoangamiza dunia kwa maji, Nuhu alituma ndege Kunguru ambaye alizurura bila kutoa ripoti na njiwa ambaye alirejea na kijitawi cha jani la mzeituni Tangu wakati huu mzeituni ulipata umaarufu mkubwa sana na kitendo cha njiwa kurudi na Jani bichi la Mzeituni kinywani mwake kuliashiria taarifa ya amani kwa Nuhu na familia yake.

Alama ya “V” ya vidole inayotumika sehemu nyingi sana Duniani ni matokeo ya njiwa huyu aliyekuja na jani la mzeituni katika safina, aidha matumizi ya tawi la mzeituni kama alama ya AMANI/shalom/salaam, yalitumika sana na watu wa Magharibi Karne tano hivi kabla ya Kristo, Wayunani wa kale waliutumia mti huu, kama alama ya uzao na masimulizi na historia zinaonyesha pia waliutumia kufukuzia pepo wachafu, kwa jina la mungu aliyejulikana kama Eirene au Irene ambayo maana yake ni Shalom/Salaam au amani, wapagani wa Kirumi pia walitumia matawi ya Mzeituni kumaanisha mungu mke wa amani ambaye alijulikana kama PAX na katika Coins za zamani za Kirumi iliwekwa nyuma ya fedha maana hizi hazitofautiani sana na maana ya asili iliyotumiwa na waandishi wa Biblia.


Fedha ya zamani sana (Coin) ya Kirumi ikiwa na tawi la Mzeituni

Mara nyingi waandishi wa Biblia walitumia mzeituni kama mfano. Sehemu mbalimbali za mzeituni zilitumika kufananisha rehema ya Mungu, ahadi ya ufufuo, na maisha ya familia yenye furaha. Kuuchunguza mzeituni kwa makini kutatusaidia kuelewa marejeo hayo ya Kimaandiko na kutafanya tuuthamini sana mti huu wa pekee ambao pamoja na uumbaji mwingine wote, ni moja ya mti wenye matunda unaofanya kazi ya kumsifu Mungu Zaburi 148:7,9.

Matumizi ya Mzeituni na Mafuta ya Mzeituni.

Bila shaka, zeituni zilipendwa sana na Waisraeli kwa sababu ya mafuta yake yenye thamani. Walitumia katika nyumba zao taa zenye tambi zilizotumia mafuta ya zeituni. Pia Mungu aliagiza wana wa Israel kuleta mafuta ya mzeituni kwaajili ya Taa yenye vinara saba iliyopaswa kuwaka Daima katika nyumba ya Mungu.


Taa yenye vinara Saba iliwaka katika nyumba ya Bwana Daima ikitumia Mafuta ya Mzeituni

Mambo ya walawi 24:2 “1. Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia, 2. Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima. 3. Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele za BWANA daima; ni amri ya milele katika vizazi vyenu.”

Mafuta ya zeituni yalikuwa muhimu katika upishi. Yalikinga ngozi dhidi ya miali ya jua, na Waisraeli waliyatumia kutengenezea sabuni. Mazao muhimu ya nchi yalikuwa nafaka, divai, na zeituni. Hivyo, ungekuwa msiba mkubwa kwa familia ya Waisraeli mizeituni ikikosa kuzaa.

Kumbukumbu la Torati 7:13 Biblia inasema. “naye atakupenda na kukubarikia na kukuongeza tena ataubarikia uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, nafaka zako na divai yako, na mafuta yako, maongeo ya ng'ombe zako, na wadogo wa kondoo zako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwa atakupa.” Kubarikiwa kwa Divai na Mafuta yanayotajwa hapo ni Mafuta ya Mzeituni Habakuki 3:17 Ilikuwa ni laana nzito ni adhabu kama Bwana ataipiga nchi kiasi cha kufikia Mzeituni kuzaa kwa shida “Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula; Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe;”
 
Hata hivyo, kwa kawaida mafuta ya zeituni yalikuwa mengi. Yaelekea kwamba Musa aliliita Bara Lililoahidiwa ‘nchi ya zeituni’ kwa sababu mizeituni ilipandwa kwa wingi sana katika eneo hilo. Mtaalamu wa mambo ya asili, H. B. Tristram, wa karne ya 19 aliutaja mzeituni kuwa “mti wa kawaida wa nchi ya Kanaani yaani Israel.” Kwa sababu ya thamani yake na wingi wake, mafuta ya zeituni yalitumika katika eneo lote la Mediterania yakiwa kama fedha ya kimataifa. Yesu Kristo mwenyewe alitaja deni ambalo lilikadiriwa kuwa “vipimo mia vya bathi vya mafuta ya mzeituni.” Luka 16:5-6 “5.Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu? 6. Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini”.

“Baraka kuu zililinganishwa Kama Miche ya Mizeituni”

Mzeituni wenye mafaa ni mfano ufaao wa baraka za Mungu. Mtu anayemcha Mungu angethawabishwaje? “Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, vyumbani mwa nyumba yako,” mtunga-zaburi akaimba. “Wanao kama miche ya mizeituni wakiizunguka meza yako.” Zaburi128:3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako”.“Miche ya mizeituni” ni nini, na kwa nini mtunga-zaburi anailinganisha na wana?

Mzeituni ni wa pekee kwa kuwa machipukizi mapya huchipuka daima kutoka kwenye shina lake. Wakati shina kuu liachapo kuzaa kama zamani kwa sababu ya uzee, wakulima wanaweza kuacha miche au machipukizi mapya yakue na kuwa sehemu muhimu ya mti huo. Baada ya muda, mti wa awali utazungukwa na mashina machanga matatu au manne yenye nguvu, kama wana wanaoizunguka meza. Miche hiyo inatumia mzizi uleule, nayo hutoa mazao mazuri ya zeituni.
Hali hiyo ya mzeituni ni mfano ufaao wa jinsi imani ya wana na binti iwezavyo kuwa thabiti kwa sababu ya mizizi ya kiroho yenye nguvu ya wazazi wao. Watoto wakuapo, wao vilevile huzaa matunda na kuwategemeza wazazi wao, ambao hufurahi kuona watoto wao wakimtumikia Mungu pamoja nao. Mithali 15:20
 
“Mzeituni Unafundisha kuwa Yako Matumaini ”

Baba mzee-mzee anayemtumikia Mungu hupendezwa na watoto wake wenye kumcha Mungu. Lakini watoto haohao huomboleza wakati hatimaye baba yao ‘anapoenda njia ya ulimwengu wote.’ (1Wafalme 2:2). Ili kutusaidia kuvumilia msiba kama huo wa familia, Biblia hutuhakikishia kwamba kutakuwa na ufufuo. Yohana 5:28-29, 11:25

Aubu, aliyekuwa baba ya watoto wengi, alifahamu vizuri kwamba maisha ya mwanadamu ni mafupi. Aliyalinganisha na maua ambayo hunyauka upesi.  (Ayubu 1:2, 14:1,2). Ayubu alitamani sana kufa ili aepuke maumivu, akiliona kaburi kuwa mahali pa kujificha ambapo angeweza kutoka. “Mtu akifa, je! atakuwa hai tena?” Ayubu akauliza. Kisha kwa uhakika akajibu: “Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, hata kufunguliwa kwangu kunifikilie. Wewe ungeita, nami ningekujibu; ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.”Ayubu 14:13-15

Ayubu alionyeshaje imani kwamba Mungu angemwita kutoka kaburini? Kwa kutumia mti ambao kutokana na jinsi anavyoufafanua, yaelekea ni mzeituni. “Yako matumaini ya mti,” Yobu akasema. “Ya kuwa ukikatwa utachipuka tena.” Ayubu 14:7 Mzeituni unaweza kukatwa, lakini kufanya hivyo hakutauharibu. Utakufa tu uking’olewa. Mizizi isipong’olewa, huo mti utachipuka tena ukiwa na nguvu mpya.

Hata ikiwa ukame wa muda mrefu unanyaukisha mzeituni wa zamani, shina lililonyauka laweza kuchipuka tena. “Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, na shina lake kufa katika udongo; lakini kwa harufu ya maji utachipuka, na kutoa matawi kama mche.” Ayubu 14:8-9 Ayubu aliishi katika nchi kavu na yenye vumbi ambako yaelekea aliona mashina mengi ya mizeituni iliyozeeka ambayo yalionekana yamenyauka na bila uhai. Hata hivyo, mvua iliponyesha mti huo “mfu” ulichipuka tena na mizizi yake kutoa shina jipya kana kwamba ni “mche.” Uwezo huo wa kipekee wa kuchipuka tena ulifanya mkulima mmoja wa bustani wa Tunisia aseme: “Kwa kweli mizeituni haiwezi kufa.”

Kama vile mkulima anavyotamani kuona mizeituni yake iliyonyauka ikichipuka tena, ndivyo Mungu anavyotamani kufufua watumishi wake waaminifu. Anangojea kwa hamu wakati ambapo watu waaminifu kama Abrahamu na Sara, Isaka na Rebeka, na wengine wengi watafufuliwa. Mathayo 22:31-32 Itakuwa ajabu kama nini kuwakaribisha wafu na kuwaona wakiishi tena maisha kamili yenye manufaa!

Mzeituni wa Mfano
Sifa ya Mungu ya kutobagua na pia uandalizi wake wa ufufuo hudhihirisha rehema yake. Mtume Paulo alitumia mzeituni kuonyesha jinsi ambavyo Yehova huwarehemu watu bila kujali rangi au malezi yao. Kwa karne nyingi Wayahudi walijivunia kuwa wachaguliwa wa Mungu, “uzao wa Abrahamu.” Yohana 8:33, Luka 3:8
 
Haikuwa lazima uwe mzaliwa wa taifa la Kiyahudi ili kupata kibali cha Mungu. Hata hivyo, wanafunzi wote wa kwanza wa Yesu walikuwa Wayahudi, na walikuwa na pendeleo la kuwa wanadamu wa kwanza kuteuliwa na Mungu kufanyiza mbegu ya Abrahamu iliyoahidiwa Mwanzo 22:18 Wagalatia 3:29. Paulo aliwalinganisha wanafunzi hao Wayahudi na matawi ya mzeituni wa mfano.



Wengi wa Wayahudi wa asili walimkataa Yesu, wakijinyima pendeleo la kuwa washiriki wa “kundi dogo,” au “Israeli wa Mungu.” Luka 12:32: Wagalatia 6:16 Hivyo wakawa kama matawi ya mzeituni wa mfano yaliyokatwa. Ni nani wangechukua mahali pao? Mwaka wa 36 Baada ya Kristo., wasio Wayahudi walichaguliwa kuwa sehemu ya mbegu ya Abrahamu. Ilikuwa kana kwamba Yehova alipandikiza matawi ya mzeituni-mwitu kwenye mzeituni wa bustani. Wale ambao wangefanyiza mbegu ya Abrahamu iliyoahidiwa wangetia ndani watu wa mataifa. Wakristo wasio Wayahudi sasa wangeweza kuwa ‘washiriki wa mzizi wa unono wa mzeituni.’Warumi 11:17

Lingekuwa jambo lisilowazika na lililo “kinyume cha asili” kwa mkulima kupandikiza tawi la mzeituni-mwitu kwenye mzeituni wa bustani.  Warumi 11:24 “Pandikiza mti mzuri kwenye mti wa mwituni, na, kama vile Waarabu wasemavyo, ule mzuri utashinda ule wa mwituni,” chaeleza kitabu The Land and the Book, “lakini huwezi kupandikiza mti wa mwituni kwa mti mzuri ukafanikiwe.” Wakristo Wayahudi hali kadhalika walishangaa wakati ambapo Yehova ‘kwa mara ya kwanza alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwayo watu kwa ajili ya jina lake.’ Matendo 10:44-48, 15:14 Hata hivyo, hiyo ilikuwa ishara ya wazi kwamba kutimizwa kwa kusudi la Mungu hakukutegemea taifa moja tu. La, kwa kuwa “katika kila taifa mtu ambaye humhofu na kutenda uadilifu akubalika kwake.” Matendo 10:35

Paulo alionyesha kwamba kwa kuwa “matawi” ya mzeituni ya Wayahudi wasio waaminifu yalikatwa, mtu yeyote aweza kukatwa vivyo hivyo akikosa upendeleo wa Yehova kwa sababu ya kiburi na kutotii. Warumi 11:19,20 Kwa kweli jambo hilo laonyesha kwamba hatupaswi kupuuza fadhili isiyostahiliwa ya Mungu 2Wakoritho 6:1.


Kupaka Mafuta kwa Maombezi ya Mgonjwa

Maandiko yanarejezea kihalisi na kwa mfano matumizi ya mafuta ya zeituni. Zamani, majeraha na machubuko ‘yalilainishwa kwa mafuta’ ili yapone haraka. Isaya 1:6 Kulingana na mojawapo ya mifano ya Yesu, Msamaria aliyekuwa jirani mwema alipaka mafuta ya zeituni na divai kwenye majeraha ya mtu aliyemkuta kwenye barabara ya kwenda Yeriko Luka 10:34.

Mtu huburudika na kupata kitulizo apakapo mafuta ya zeituni kichwani. Zaburi 141:5  Wazee Wakristo wanaweza ‘kumpaka mafuta mtu ambaye hawezi wanaposhughulika na ugonjwa wa mwili na kiroho.na Kuomba kwa Jina la Yesu Yakobo 5:14 Ushauri wenye upendo wa wazee unaotokana na Maandiko na sala zao za kutoka moyoni kwa niaba ya mwamini mwenzao aliye mgonjwa kiroho zinalinganishwa na mafuta ya zeituni yenye kutuliza. Yapendeza kwamba kuna usemi wa Kiebrania ambao wakati mwingine humwita mtu mzuri “mafuta safi ya zeituni.”



‘Mzeituni Unaostawi Katika Nyumba ya Mungu’

Kwa kuzingatia mambo ambayo yametajwa, si ajabu kwamba watumishi wa Mungu wanaweza kulinganishwa na mizeituni. Daudi alitamani kuwa kama “mzeituni mbichi, unaostawi katika nyumba ya Mungu.”  Zaburi 52:8Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.” Kama vile mara nyingi familia za Waisraeli zilivyokuwa na mizeituni iliyozingira nyumba zao, vivyo hivyo Daudi alitaka kuwa karibu na Mungu na kuzaa matunda kwa sifa ya Mungu.

Ufalme wa Yuda wa makabila mawili ulikuwa kama “mzeituni wenye majani mabichi, mzuri, wenye matunda mema” wakati walipokuwa waminifu kwa Mungu. Yeremia 11:15-1815. Mpenzi wangu afanya nini nyumbani mwangu, ikiwa amefanya uasherati? Je! Nadhiri zako na nyama takatifu zitakuondolea hatia? Ufanyapo maovu, ndipo uonapo furaha. 16. Bwana alikuita jina lako, Mzeituni wenye majani mabichi, mzuri, wenye matunda mema; kwa kelele za mshindo mkuu amewasha moto juu yake, na matawi yake yamevunjika. 17. Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekupanda, ametamka mabaya juu yako, kwa sababu ya maovu ya nyumba ya Israeli, na ya nyumba ya Yuda, waliyoyatenda juu ya nafsi zao wenyewe kwa kunikasirisha, wakimfukizia Baali uvumba. 18. Tena Bwana akanijulisha haya, nami nikayajua; ndipo uliponionyesha matendo yao.” Lakini watu wa Yuda na Israel walipoteza hali hiyo ya kupendelewa ‘walipokataa kusikia maneno ya Mungu; wakafuata miungu mingine. Yeremia 11:10 “Wameyarudia maovu ya baba zao, waliokataa kusikia maneno yangu; wamewafuata miungu mingine na kuwatumikia; nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, wameyavunja maagano yangu niliyoyafanya na baba zao.”

Ili kuwa mzeituni unaostawi katika nyumba ya Mungu, ni lazima tumtii Mungu na kuwa tayari kukubali nidhamu ambayo yeye hutumia “kutupogoa” ili tuweze kuzaa matunda zaidi ya Kikristo.Waebrania 12:5-6 Isitoshe, kama vile mzeituni wa kawaida huhitaji mizizi mingi ili kustahimili ukame, twahitaji kuimarisha mizizi yetu ya kiroho kusudi tuvumilie majaribu na mnyanyaso Mathayo 13:21, Wakolosai 2:6-7.

Mzeituni unafananisha vizuri na Mkristo mwaminifu, ambaye huenda asijulikane katika ulimwengu bali anatambuliwa na Mungu. Mtu kama huyo akifa katika mfumo huu, ataishi tena katika ulimwengu mpya unaokuja. 2Wakoritho 6:9, 2Petro 3:13.

Mzeituni ambao ni kama hauwezi kuharibiwa, ambao huendelea kuzaa matunda mwaka baada ya mwaka watukumbusha ahadi hii ya Mungu: “Kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” Isaya 65:22 Ahadi hiyo ya kiunabii itatimizwa katika ulimwengu mpya wa Mungu 2Petro 3:13.

Jinsi ya Kutumia Mafuta ya Mzeituni kwa shughuli (Mahitaji) Mbalimbali.

1.      Kuweka wakfu Kiongozi Mafuta ya mzeituni hutumika wakati wa kumuweka wakfu Kiongozi wa Kisiasa, Kidini na kijamii, Katika Israel Nabii, Mfalme na Kuhani waliwekwa wakfu kwa ibada maalumu na kupakwa mafuta unapompaka mtu mafuta kwa mujibu wa nafasi aliyo nayo utatangaza kupitia neno la Mungu Je Bwana Hakukupaka Mafuta Ili………………..(Unaeleza Kusudi la kumpaka mafuta hayo) kisha unamiminia na kumuombea neema kwaajili ya kazi hiyo kupitia Jina la Yesu Mfano 1Samuel 10:1 Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta akayamimina kichwani pake akambusu akasema Je Bwana hakukutia mafuta [Uwe mkuu juu ya watu wake Israel? Nawe utawamiliki watu wa Bwana na kuwaokoa na mikono ya adui zao kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia Mafuta ] uwe mkuu juu ya urithi wake” Unapompaka mafuta kiongozi lazima utangaze kusudi la kupakwa kwake mafuta nay ale yatakayonenwa yatampata.Kama anayepakwa Mafuta ni Mchungaji , Kuhani padre au nabii utasoma Kutoka 29:7 na kumuombea nneema ya majukumu yake na kumpaka mafuta,

 Ibada ya kumpaka mtu mafuta yaweza kufanyika hata Faragha
2.      Ikiwa unahitaji Mafuta haya kwaajili ya kumpokea Roho Mtakatifu utasoma Luka 4:18-19 pia 1Samuel 16:13 kisha ingia katika maombi ya kuhitaji kujazwa Roho mtakatifu na utashangaa nguzu za Mungu zitakushukia na utaanza kusema kwa lugha nyingine
3.      Ikiwa unatumia mafuta kwaajili ya kuondoa msongo wa mawazo, kujilinda na maadui wa kibinadamu na mashetani utachukua mafuta ya mzeituni utasoma Zaburi ya 23 yote na kisha utajipaka au utampaka mtu mwenye stresses Msongo wa mawazo na kisha utaomba neema na rehema huku ukiyasambaza mafuta hayo katika upaji wa uso kwa kutumia jina la Yesu na mtu huyo atapokea amani na furaha tangu wakati huo
4.      Ikiwa ni kwaajili ya kuombea Mgonjwa ambaye hawezi utachukua kichupa cha mafuta ya mzeituni, utaongena na mgonjwa na kumtia moyo na kumfariji kisha utasoma pamoja naye Yakobo 5:14-15 na Marko 16:17-18
5.      Ikiwa ni kwaajili ya kukemea vifungo vya shetani ba kutoa pepo chukua mafuta ya mzeituni kisha soma maandiko yafuatayo na weka mkono wako juu ya mtu mwenye pepo omba rehema kwaajili yake na kukemea kwa jina la Yesu Luka 4:18-19, na Marko 16:17-18
6.      Ikiwa ni kwaajili ya kujilinda na maadui wa aina yoyote yaani wakimwili na kiroho jipake mafuta ya mzeituni na kabla ya kujipaka utasoma maandiko haya kisha utajipaka na kujiombea au kumuombea mwenye uhitaji huo Zaburi 27:1-6, 1Samuel 2:10
7.      Ikiwa ni kwaajili ya nguvu za kiume au za kike utajipaka mafuta hayo ya mzeituni wakati unapokuwa unakwenda kulala katika sehemu ya via vya uzazi kisha utaomba kisha utaisema Zaburi ya 103:1-5 utasubiri kwa dakika tano nguvu zitakushukia kufurahia uumbaji wa Mungu
8.      Kwaajili ya kujitibu Mafua utajipaka katika eneo la pua na tundu zake mara tatu kwa siku ukitumia Marko 16:17
9.      Kwaajili ya kuua wadudu wabaya walioko tumboni utayaombea mafuta hayo na kunywa kijiko cha chai 1X2 kwa siku kwa mfululizo siku saba Marko 16:17-18
10.  Kwaajili ya kutunza kumbukumbu na kuponya ugonjwa wa kusahau chukua mafuta ya zeituni jipake katika paji la uso soma Zaburi ya 103:1-5 kisha muombe Mungu kwa jina la Yesu na utakuwa wa ajabu
11.  Kwa mtu alitepooza atachua eneo lililopooza mara mbili kila siku, mwenye pepo la Degedege atapaka mwili mzima kwa siku mara mbili maombi yatatangulia na Marko 16:17-18 itasomwana kuomba katika jina la Yesu
12.  Kwaajili ya kutunza Ngozi isizeeke kuondoia mikunjo, kuondoa alama za kuungua na jua, kukinga mionzi ya jua kulainisha mishipa, kukinga na saratani ya ngozi, kupambana na sumu kwenye ngozikilinda ngozi kupatwa na sumu,kuondoa mabaka kuondoa ukavu kwenye ngozi soma Zaburi 103:1-5 kisha omba nap aka mafuta haya mwili mzima kama mafuta ya kawaida hutazeeka haraka
13.  Ikiwa una kesi na hoja ngumu zinakukabili Mahakamani soma Isaya 54:17 kisha fanya maombi ya ushindi na ujasiri jipake mafuta ya mzeituni Bwana atakupigania nawe utanyamaza kimya 

14.  Mafuta ya Mzeituni yanaweza kutumika hata kwa kuukanda mwili Massaging na kusababisha mwili ku- relax kupata ahueni nakuondoa uchovu. Pia mizeituni huleta usingizi mzuri  
15. Mafuta ya mzeituni yanaweza pia kutumika kwa kuvunjia mikataba ya aina mbalimbali yaani nira na maagano ambayo ulijiingiza na kama unataka kujikomboa 
Mafuta ya Mizeituni hupatikana katika maduka mbalimbali supermarket, na sehemu nyinginezo kumbuka ni muhimu kupata mafuta Original na sio yaliyochanganyika na kitu kwa vila mengine utaweza kula, kujipaka na kadhalika huitaji msaada wa Mchungaji au kiongozi wa dini kuona matokeo ya mizeituni zaidi ya kujifunza, kuamini na kutendea kazi.


Matumizi ya neno la Mungu na mafuta yanaweza kutumika katika maeneo mengi zaidi ya haya itategemea na ufunuo wako na maandiko utakayoweza kuyatumia utayatumia kulingana nauhitaji wako, Hakuna utata wa kimaandiko kuhusu matumizi ya mafuta,sio lazima upewe na manabii au Mchungaji kanunue mwenyewe hata ndoo nzima kwa matumizi yako ingawa mafuta haya ni ghali, kwa muda mrefu sana nilimtumikia Mungu na kuombea watu bila ya matumizi ya mafuta, sikupanda kabisa kutaka kuyatumia, kwa zaidi ya miaka 20 ya kumtumikia Mungu sikutaka kuamini katika swala hili, nilisubiri kupata ufunuo kamili wa swala hili na dhamiri yangu kuhusu matumizi ya mafuta na Mungu aliponithibitishia kuwa Inatenda kazi naliona vema kama mkuu wa wajenzi kuweka fundisho hili wazi, Jambo kubwa la msingi usiyatumia mafuta kama Biashara, wala usiyatumie kama uganga bali yatumia kwa imani na maombi na neno la Mungu na utaweza kuona Mafanikio, Kwa maandiko zaidi kuhusu Mafuta katika Biblia soma mistari kadhaa ifuatayo:-

Kutoka 25:6, 29:7, 29:2, 29:29,30:3,22-26,40:9, 40:15,  Walawi.8:10,8:12,4:3,5,16,6:20, 
Zaburi.132:10,1Sam.16:13,2Sam.24:4,1Nyakati.16:22;Zab.105:15,1Wafalme-19:16 1Nyakati.16:22Zab.105:15, Isa. 21:5,Luke 7:38-40, Kumb. 28:40, Ruth 3:3,2Samuel 14:2,
Zab.104:15, 109:18, Isaiah 1:6,Mark 6:13, Yakobo. 5:14, Mark 14:8,Luka. 23:56, Zab. 2:2; 
Dan. 9:25, 26, 
Isa. 61:1, Zab. 45:7; Heb. 1:9, John 1:41; Mdo. 9:22; 17:2, 3; 18:5, 28, 1 Yoh. 2:20, Matt. 25:1-13