Jumatano, 19 Septemba 2018

Tena mmeyasahau yale maonyo!



Waebrania 12:5-11tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake. Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.


 

“Kila mmoja anapaswa kuchagua njia mojawapo kati ya mbili, maumivu ya Nidhamu au maumivu ya Majuto” – John Rohn

Utangulizi.

Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kufahamu kwamba maisha yetu hayawezi kuwa na wingi wa furaha na amani  na hata mafanikio kama tutasahau kuishi kwa Nidhamu, ni ukweli ulio wazi kwamba Nidhamu ndio njia sahihi ya maisha, Nidhamu haina mipaka kila mtu anapaswa kuishi kwa nidhamu, Nidhamu haina mwenye pesa, au asiye na pesa, mwenye utajiri au asiye tajiri, swala la nidhamu linategemeana na jinsi mtu alivyofunzwa na anavyokubali kujifunza, Nidhamu ni tabia na haipatikani kwa kurithi, kwa msingi huo kila mmoja anaweza kujifunza kuishi kwa nidhamu na akafanikiwa katika maisha, wengi wa watu wenye mafanikio ya kiroho na kimwili, na maswala mengineyo yote ni wale waliofanikiwa kuishi na kuenenda kwa Nidhamu. Tunahitaji Nidhamu ili kuyafikia maono, tunahitaji nidhamu ili kutunza utajiri, tunahitaji nidhamu ili kuepuka matatizo,mtu akiwa na nidhamu ni kama ana stadi ya maisha iliyo ya juu zaidi, watu wanaofanya kazi kwa bidii na wenye vipawa vikubwa hawawezi kuwa na mafanikio makubwa kama hawatakuwa na nidhamu, yaani huwezi kuzungumzia huduma, maisha, kazi, kusoma, mtindo wa maisha, ubora wa shule au taasisi au chuo, au taifa, au michezo, au jeshi kama katika kila secta watu hawatakuwa wamejifunza kuishi kwa nidhamu.

“We don’t have to be smarter than the rest, we have to be more Displined than the rest” warren Buffet 
“Hatuhitaji kuwa bora kuliko wengine, tunahitaji kuwa na Nidhamu kuliko wote” Warren Buffet
“Everyone must choose one of two pain, the pain of Displine or the pain of regret” John Rohn
“Kila mmoja anapaswa kuchagua njia mojawapo kati ya mbili, maumivu ya Nidhamu au maumivu ya Majuto” – John Rohn
“He who lives without discipline dies without HONOR”
“Wanaoishi bila Nidhamu huwa wanakufa bila heshima”

Nidhamu inahitajika katika kila Nyanja, huwezi kuwa mwalimu Mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa Dereva mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa Mchungaji Mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa daktari mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa mwana siasa mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa bondia mzuri kama huna nidhamu, huwezi kuwa mchezaji mpira mzuri kama huna nidhamu, nidhamu ni maisha kula, kuvaa, na hata kuishi ni nidhamu nidhamu ndio kila kitu, kuomba ni nidhamu, kufunga ni nidhamu kila kitu kinahitaji nidhamu
“Kama kuna somo kubwa ambalo ningependa Dunia nzima ijifunze jibu langu lingekuwa ni rahisi Nidhamu tu” – Rev. Kamote
“If there is a great subject that I would like the world to learn my answer could be simple Discipline”
Nidhamu ndio somo kuu na la kwanza ambalo wazazi walitufundisha Nyumbani, na walimu wanalikazia shuleni, na wakristo wameagizwa kulihubiri, Jamii yoyote ile ambayo unaweza kusema kuwa haijaelimika basi ni jamii wa watu wasio na nidhamu – Rev. Innocent Kamote

Maana ya neno Nidhamu.

Neno nidhamu maana yake ni mfumo wa kuwafunza watu, ili wawe watii, au wawe wenye tabia njema na mwenendo Mzuri, Ni malezi au makuzi yenye kuzingatia,  Maonyo, Sheria, Taratibu,mamlaka, uthabiti, weledi, uthibiti, Heshima, mwelekeo, wajibu, utii, kiasi na kujiongoza na kushikisha adabu kwa ujumla wake kuwa na Nidhamu.
Neno nidhamu pia linaweza kutumika kuelezea mafunzo maalumu yenye kumfanya mtu awe mtii kwa sheria tabia na mwenendo na kurekebishika pale inapohitajika, ni mafunzo, Mafundisho, Shule, kocha, elimisha, na hekimisha, na kumfanya mtu awe na uwezo wa kujidhibiti yaani “self control” au Marudia au nidhamu kwa kiingereza Displine. Kushikisha adabu au kunadhimisha na kutoa maonyo au adhabu ili kumrekebisha mtu kwa lengo la kumfanya awe thabiti. Kwa kiibrania kuna maneno mawili yanayotumika kumaanisha Nidhamu 1 ni “YASAR” (NIDHAMU AU KUADHIBIWA) NA “YAKACH” (MAONYO) yametumika maneno hayo katika Mithali 3:11 “Mwanangu usidharau Kuadhibiwa na Bwana wala usione taabu kurudiwa naye
Biblia katika Waebrania 12:5-11 inatuasa kwamba tumeyasahau yale maonyo ni maonyo gani haya ambayo Biblia inatuasa kutokuacha kuyasahahu? Ni swala la Nidhamu au Marudia Biblia ya kiingereza inasema hivi katika fungu hilo la maandiko
And have you completely forgotten this word of encouragement that addresses you as a father addresses his son? It says,
“My son, do not make light of the Lord’s discipline,
    and do not lose heart when he rebukes you,
because the Lord
disciplines the one he loves,
    and he chastens everyone he accepts as his son.”[
a]
Endure hardship as discipline; God is treating you as his children. For what children are not disciplined by their father? If you are not disciplined—and everyone undergoes discipline—then you are not legitimate, not true sons and daughters at all. Moreover, we have all had human fathers who disciplined us and we respected them for it. How much more should we submit to the Father of spirits and live! 10 They disciplined us for a little while as they thought best; but God disciplines us for our good, in order that we may share in his holiness. 11 No discipline seems pleasant at the time, but painful. Later on, however, it produces a harvest of righteousness and peace for those who have been trained by it.

Katika kifungu hiki utaweza kuona neno Marudia yaani Nidhamu katika Biblia ya Kiswahili SUV limetajwa mara saba (7) na katika Biblia ya kiingereza limetajwa mara kumi (10), Kama katika kifungu hiki tungeambiwa tutafute neno kuu yaani “key word” basi ni wazi kuwa neno kuu ni “Descipline” na “Marudia” isipokuwa mimi ningependa zaidi kutumia neno Nidhamu, au Maonyo Neno hili ni neno la Muhimu sana sana na ni neno la kutia moyo ambalo kanisa halipaswi kulisahau kamwe Nidhamu, Nidhamu Nidhamu.

Umuhimu wa kutokuyasahau yale Maonyo (Nidhamu).

Biblia inahitimisha katika kifungu hiki kwamba wakati tunafundishwa nidhamu au tunazoezwa nidhamu haionekani kuwa ni jambo lenye kufurahisha sana lakini ukiisha kuzoezwa nayo inaleta faida yaani matunda ya haki na amani, Ni kama maandiko yanataka kutuambia kuwa kuna faida kubwa sana kwa mtu aliyejifunza kukaa katika nidhamu, kuzingatia yale maonyo, ziko faida nyingi sana za kujitia nidhamu ambazo zinajibu swali kwa nini nidhamu ni Muhimu Waebrania 12:11Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”

1.       Nidhamu itakupa kufikia malengo :- 

Kama mtu awaye yote ana ndoto ya aina yoyote na anakusudia kuifikia ni lazima awe na nidhamu, Ushuhuda wa kidunia unaonyesha kuwa watu wote waliofanikiwa katika kila Nyanja na hata kutimiza malengo yao katika maisha na kupata mafanikio makubwa walikuwa ni watu waliojifunza kukaa katika nidhamu, Nidhamu inatusaidia kufaulu masomo, kumaliza shule salama, kumaliza jeshi salama, kukaa katika kazi zetu salama, kufanya kazi zetu vema na kufikia malengo vizuri, Mtu awaye yote mwenye makusudi na mpango mwema atatulia na kufanya kazi kwa bidii kila siku ili kuyafikia malengo, ni nidhamu pekee inayoweza kumfikisha mtu kule anakokusudia, kinyume na nidhamu ni vigumu sana kwa mtu kuyafikia malengo, Biblia inaonyesha kuwa wana michezo wote huwa na tabia ya kujitia nidhamu ili kwamba waweze kushinda na kupata taji ya kile wanachokikusudia, mwanamichezo yoyote ambaye hana nidhamu au mwanjeshi yeyote ambaye hana nidhamu atapoteza malengo, Ubora wa mwanamichezo yoyote bila kujali kipawa alichonacho kama hana nidhamu, kuna uwezekano mkubwa sana wa kupoteza malengo au kutokuyafikia malengo

 1Wakoritho 9:25-27Na kila ashindanaye katika michezo HUJIZUIA KATIKA YOTE; (Maana yake hujitia nidhamu). basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika. Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.”

Napenda Biblia ya Kiingereza inavyosema hapaEveryone who competes in the games goes into strict training” unaweza kuona neno “STRICT TRAINING”

Ni wazi kuwa Paulo mtume hapo anazungumzia uhusiano wa kujitia nidhamu kwa wana michezo ili waweze kuwa washindi, na kwamba hata wale wanaotaka kwenda mbinguni hawana budi kujitiisha kujifunza kuishi kwa nidhamu ni nidhamu pekee itakayoweza kutusaidia kutoka na kufanikiwa. Ni watu wenye kujitia nidhamu tu watakaoweza kufika Mbinguni, ni wahubiri wanaojitia nidhamu ambao hawataweza kukataliwa baada ya kuwahubiri wengine.

2.       Nidhamu inaleta Heshima:-

Ni muhimu kufahamu kuwa tukiishi kwa nidhamu watu watatuheshimu, watu wengi sana wanapenda kuheshimika kutoka kwa wengine lakini njia nyepesi ya mtu kuheshimika ni kuishi kwa nidhamu, watu wengi au wote duniani humkubali na kumuheshimu mtu mwenye nidhamu, sababu kubwa ni kwamba ni kazi ngumu kuwa na nidhamu na kwa sababu hiyo ukiwa nayo watu watakuheshimu, ukifanya kazi kwa nidhamu, ukatimiza kazi zako kwa wakati, ukawepo unapotakiwa kuwepo kwa wakati, ni lazima utaheshimika, Mwanafunzi mwenye nidhamu anajiandaa vizuri, anafanya kazi alizozipewa kwa wakati na kwa sababu hiyo ni rahisi kwake kuyafikia malengo. Kwa ujumla utakuwa kielelezo na mfano wa kuigwa

1Timotheo 4:12Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.”

Paulo mtume ni kama anamweleza Timotheo kuwa mtu asikudharau kwa sababu u kijana, lakini ni namna gani watu watakuheshimu? Ni kama utakuwa mfano yaani kielelezo, kwatika usemi, mwenendo, upendo imani na usafi, ni kama Paulo anamwambia Timotheo kuwa watu watakuheshimu bila kujali umri wako hata kama ni mdogo endapo tu utaishi kwa nidhamu. Binti au mwanamke, kijana au mwanaume anayejitia nidhamu anaheshimika katika jamii,

3.       Nidhamu itakupa Afya njema.

Jinsi na namna ya kutunza afya zetu pia ni swala linalohitaji nidhamu, namna tunavyokula, tunavyotumia chumvi, sukari au mafuta mengi sana na namna tunavyotumia dawa bila nidhamu au kwa nidhamu vina mchango mkubwa sana katika kuamua tuwe na afya ya namna gani, Lazima na ni muhimu kuoga vizuri, kufanya mazoezi, kutembea na kulala kwa wakati kwa ujumla mtindo wa maisha wenye kujitia nidhamu utaufanya mwili wetu na akili zetu kuwa njema na zenye afya nzuri wakati wote, magonjwa sugu hayatakuwa sehemu ya maisha yetu, kula kwa wakati funga kwa mpangilio mwema bila kuharibu mwili wetu kwa vile miili hii sio mali yetu wenyewe ni mali ya Mungu.

 1Wakoritho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;”

4.       Nidhamu inaleta uthabiti na uwezo wa kujitawala.

Kwa ujumla nidhamu ina faida kubwa sana katika ujumla wa mtazamo wa maisha, inakuumbia uthabiti na kujitawala au kujiamini na inakuepusha na hali zote za uvivu, kila mtu mwenye nidhamu utaweza kuona hawezi kuwa mzembe wala kuzembea au kutegea kazi, inaleta ufanisi kujitawala na kuwa na kiasi, Mtu mwenye nidhamu anauwezo mkubwa sana wa kujizuia au kujitawala atakuwa makini katika kujua kile kinatakiwa kuzungungumzwa na wakati kinapaswa kuzungumzwa, anajua nini cha kuvaaa na wapi pa kuvaa, anajua namna anavyotakiwa kuenenda na kwa sababu hiyo hujiepusha sana na matatizo na hivyo kuwa na uhusiano mzuri na watu, Nidhamu na kujitawala ni mfano wa mji wenye boma kama mtu akikosa kujitawala anakuwa kama mji usio na boma usio na ukuta ni rahisi kuvamiwa na kubomlewa kwa maangamizi makubwa Mithali 25:28 “Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.”  Kumbe kujitawala yaani nidhamu ni ulinzi wa hali ya juu, huwezi kupatwa na majanga na mashambulizi ya aina mbalimbali kama utajiyiisha katika nidhamu.

5.       Nidhamu inakwenda pamoja na ubora wa Elimu.

Elimu haiwezi kuwa bora kama hakuna swala la kukazia nidhamu, Lazima kila mwanafunzi ajifunze nidhamu, Nidhamu itamsaidia mwanafunzi kujifunza vema na kwa ufasaha darasani na kukamilisha silabasi nzima vema, Mwanafunzi hawezi kuwa mwanafunzi mzuri kama haamki kwa wakati, haogi, hanywi chai au kula kwa wakati na anayetoka toka hovyo bila sababu ya msingi, kwenda kujisaidia au kurejea nyumbani, ni nidhamu ndiyo itakayokufanya uwe na afya njema utulivu, heshima na adabu na kukua vema na kukuwezesha kujifunza, Hata kanisani haipendezi kuona watu wanatokatoka saa ya kujifunza neno la Mungu kisha eti wanaenda kujisaidia, au kusikiliza simu, iliyowekwa katika mtindo wa kimya eti kwamba una maswala Muhimu, Mungu anataka sikio lako na moyo wako ili akuonye na kukupeleka katika njia iliyonyooka Mithali 12: 1Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama”. Napenda zaidi Biblia ya kiingereza inavyoweka Msatari huu katika namna njema zaidi angalia “Whoever loves discipline loves knowledge, but he who hates reproof is stupid” hii ni kwa mujibu wa ESV, “Whoever loves discipline loves knowledge, but whoever hates correction is stupid”NIV, unaweza kuona so kwa lugha nyepesi inayokubaliana na somo langu ningeweza kusema Kila apendaye Maonyo, au (Nidhamu) anapenda maarifa (Elimu), lakini kila achukiaye maonyo ni mpumbavu, Kwa hiyo utaweza kuona kuwa hekima na maaruifa na elimu vinapatikana sambamba na Nidhamu au maonyo au marudia.

6.       Nidhamu inaleta furaha na amani.

Kuishi kwa nidhamu kunasaidia kufanya mambo yafanyike vema na kwa wakati, ingawa mambo mengine yanaweza kujitokeza na kuzuia lakini bado nidhamu inaweza kufanya mambo kufanyika kwa haraka na ufasaha  na hivyo kusababisha furaha na amani. Aidha biblia inaeleza kuwa kama mtoto amefunzwa vema atakustarehesha na kuifurahisha nafsi yako, lakini kama ameachiliwa atakuwa ni aibu kwa mama yake Mithali 29:15, 17 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye., Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”.

Makusudi ya Nidhamu katika mpango wa Mungu.

Ingawa neno nidhamu lina maana pana sana katika tafasiri yake kwa vila inahusu mambo mengi sana hata hivyo ni muhimu tukaangalia pia kwa kina makusudi ya nidhamu hasa katika mpango nwa Mungu, Maandiko ya Msingi yana mengi ya kutufunza kuhusu makusudi ya nidhamu katika mpango wa Mungu tunapoyaangalia maandiko ya msingi utaweza kuona kuna sababu kadhaa kama tano hivi ya makusudi ya Nidhamu katikia mpango wa Mungu

Waebrania 12:5-11tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake. Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.

a.       Kwa kusudi la kurekebisha mwenendo usiofaa.

Biblia katika kitabu cha waebrania imeonya kuwa ni jambo la kutisha sana kuanguka katika mikono ya Mungu, yaani kuachana na neema na katika sura ya kumi na moja imekazia sana swala zima la mashujaa wa imani na kututaka tujifunze kupitia wao na kisha sura ya 12 inatutia moyo namna ya kufanya ili tuweze kufanikiwa kama wao kwa ufupi mashujaa wote wa imani walikuwa watu wenye nidhamu, na kutokana na kujitia nidhamu waliweza kufanikiwa na kuzirithi ahadi za Mungu
Kizazi cha ma hausegirl tulicho nacho leo, watoto wanalelewa boarding tangu wakiwa wachanga kwenye vituo vya day care, waliokosa malezi sahihi ya baba, wajomba mashangazi na wazazi wenye nidhamu nikizazi kilichopoteza muelekeo, kama kanisa halitakuwa  makini (Sirius) katika swala zima la nidhamu tutakuwa tumepoteza mwelekeo, ili tuweze kufanikiwa lazima turudi katika mpango wa Mungu wa kutoa maonyo kwa maneno na matendo YASAR (MARUDIA) YAKASH (MAKEMEO) Waebrania 12:5 “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye” hapa maneno yanayotumika Marudia au Makemeo yanakaziwa, haya maonyo yanataka wote wazazi na watoto kwa ujumla wasisahau wasichukulie kirahisi maonyo na makemeo ya Bwana yaani kutia nidhamu na kurekebisha tabia mbaya.

b.      Kwa kusudi la kuonyesha kujali na upendo.

Waebrania 12:6-9Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?” Moja ya njia iliyo njema zaidi ya kuonyesha kuwa unamjali mtoto wako na kumpenda ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na nidhamu, namna yoyote ile ya kumfanya mtoto ajisikie kuwa yuko salama kufanya na kuishi vyovyote atakavyo ni makosa makubwa sana ambayo yatatuletea huzuni kubwa lakini kama tutakubali kuumia wakati wa kuwatiisha na kuwafunza nidhamu basi ni wazi kuwa tutapata raha Mithali 29: 15, 17 “Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye, Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.” Hatuwezi kuwa na hekima kuliko maandiko wala hatuwezi kuwa na ufahamu kuliko Mungu, kama Mungu katika neno lake anataka tuchukue hatua stahiki dhidi ya watoto wetu ni wazi kuwa lazima kufanya kitu kwaajili ya watoto wote wa Mungu kwa upendo wenye kuonyesha kuwa tunajali badala ya kusubiri majuto ndio maana mwanafalsafa - John Rohn akasema   “Kila mmoja anapaswa kuchagua njia mojawapo kati ya mbili, maumivu ya Nidhamu au maumivu ya Majuto”  Tusipochukua hatua za kuishi kwa nidhamu maana yake tutajuata baadaye, na ndio maana Mungu katika mpango wake anatuonyesha upendo kupitia maonyo, Kama hatuna kuonywa ni dhahiri sisi tumekuwa wana wa haramu na maisha yetu yatajaa taabu na majuto mengi.

c.       Kwa kusudi la kufundisha utii

Tunapojifunza Nidhamu katika maisha yetu maana yake tunajifunza utii, tunajiweka katika neema ya Mungu, tunajifunza kutii kwa upendo, japo wakati wa mafunzo linaweza kuwa jambo lenye kuuma sana lakini linatupa matunda ya milele, mwanzoni itakuwa ni swala lenye kuumiza kwa nje lakini likihamia ndani linaleta ustaarabu wa kudumu, Biblia inasema katika Waebrania 12:11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.” Unaweza kuona kuwa kila adhabu, yaani nidhamu wakati wa kuijifunza haionekani kuwa ni furaha ni kama maumivu lakini ina faida kubwa baadaye.

d.  Nidhamu inatupa kuwa na Hekima 



Mungu ndiye chanzo cha Hekima na ni mkarimu kwa kila mmoja anasema katika Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.” Mojawapo ya njia ya kupokea hekima kutoka kwa Mungu ni pamoja na na kukubali maonyo, na hekima atakayotupa itatuongoza na kutusaidia kuwa waadilifu, watakatifu na kutuepusha na madhara ya kiroho Mithali 2:10-12 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako; Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi., Ili kukuokoa na njia ya uovu, Na watu wanenao yaliyopotoka;”, unaweza kuona hatimaye tutakuwa ytayari kumpenda Mungu na kumwabudu pasipo hofu, hatimaye kuingia katika uzima wa milele , Mungu anataka tuwe watakatifu na hivyo hututia nidhamu Waebrania 12:10Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake”. Yuda 1;21jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele.” 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

0718990796