Jumapili, 26 Julai 2026

UMUHIMU WA SHULE YA HUDUMA.


 

Waefeso 4:11-12 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa kusudi kubwa la shule ya huduma ndani ya kanisa ni kwaajili ya kukumbushana wajibu wetu wa kulijenga kanisa la Mungu, Mungu alitoa wengine kuwa Mitume, wengine kuwa Manabii, wengine kuwa Wainjilisti, wengine kuwa Wachungaji na Walimu kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, na kuhakikisha kazi ya huduma inatendeka na mwili wa Kristo unajengwa kwa hiyo kila mtenda kazi ni mjenzi katika nyumba ya Mungu Kanisa la Mungu linafananishwa na shamba, linafananishwa na jengo na sisi ndio wafanyakazi pamoja na Mungu kwa hiyo kila mtenda kazi ni mjenzi katika nyumba ya Mungu na tunapaswa kuifanya kazi yetu vema na kwa usahihi kwa sababu Mungu ataipima kazi ya kila mtu kwa hiyo kila mjenzi anapaswa kuwa makini namna anavyojenga katika jengo la Mungu.

1Wakorintho 3:6-15 “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu. Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.”

Katika nyumba ya Mungu kuna maeneo mbalimbali ambayo yanatutaka sisi kama watenda kazi kuwa makini, kuwa macho na kuyasimamia endapo tunataka kanisa letu likue kiroho na liwe kubwa lenye maelfu ya watu, ikumbukwe kuwa kadiri kanisa linavyokuwa kubwa linahitaji wahudumu wengi zaidi watakaotoa macho na kuhudumia maeneo mbalimbali na kumbuka kila tunapohudumu tunahudumia pamoja na Mungu kwa hiyo Baraka za Mungu huwa kubwa kwa kila mtenda kazi anayeifanya kazi yake kwa uaminifu, watenda kazi wengi wanapotupia macho maeneo mbalimbali ya kihuduma tunawapa watumishi wa Mungu nafasi kubwa ya kuomba na kulihudumia neno badala ya kushughulika na maswala ambayo yangeliweza kuangaliwa na watu wengine, aidha kanisa linapokua linatakiwa kuwa na wahudumu wengi zaidi ili kuzuia manung’unuiko miongoni mwa jumuiya ya  washirika katika kanisa la Mungu.

Matendo 6:1-4 “Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.”

Kwa msingi huo basi tutachukua muda kujifunza somo hili UMUHIMU WA SHULE YA HUDUMA kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo;-


  • Sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu
  • Jinsi tunavyoweza kujenga pamoja na Mungu
  • Vema mtumwa mwema na mwaminifu

 

Sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu.

Paulo mtume anaelezea wazi kuwa sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu, anasema hayo kwa kusudi la kuweka mkazo kuwa kazi ya Mungu haiwezi kwenda mbele bila wanadamu, Mungu alimuumba mwanadamu kwa kusudi la kuwa na ushirika na yeye na kwa sababu hiyo sisi tunabeba kusudi lote la Mungu hapa duniani, jukumu hili kamwe Mungu hajawahi kuwapa malaika lakini ametupa sisi, kwa hiyo ni jukumu la kila mtu aliyeokolewa kulijemga kanisa la Mungu na kuifanya kazi ya Mungu kazi hii iliyo njema.

1Wakorintho 3:9 “Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.”

2Wakorintho 6:1-2 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure. (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Mungu amempa mwanadamu jukumu zima la kuihubiri injili na kuieneza na kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi, hii ni heshima kubwa sana kwani tunapoifanya kazi hiii Mungu huwa hakuachi anakuwa pamoja nawe kwa sababu kazi hii sio yetu ni ya kwake kwa hiyo wewe kama mtoto wake unashirikiana naye katika kuikamilisha hakuna mahali popote ambapo Mungu alimuagiza mtu kazi kisha akamuacha, wakati wote mtu anapoifanya kazi ya Mungu neno la Mungu linaonyesha kuwa Bwana akawa pamoja naye

Marko 16:19-20. “Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]

Paulo anatumia mfano wa shughuli za kilimo kama kupanda na kumwagilia na hata maswala ya ujenzi kuonyesha kuwa katika mwili wa Kristo kila mmoja wetu ana majukumu mbalimbali, kutokana na vipawa mbalimbali na karama mbalimbali  lakini wote sisi tunaifanya kazi moja, kwa hiyo katika shule hii ya watenda kazi tunaainisha maeneo mbalimbali ya kiutendaji , hata kama wote tunajifunza hizi ili kumtumikia Mungu kwa pamoja baadae utaweza kuona kuwa tutamtumikia Mungu sehemu mbalimbali na kufanya huduma mbalimbali lakini katika mwili huu huu mmoja.

1Wakorintho 12:12-27 “Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi. Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo? Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa? Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.”

Kwa hiyo tutafanya kazi katika maeneo tofauti tofauti wakati mwingine kwa kupangiwa au wakati mwingine kutokana na kile kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yako lakini sisi sote tu watenda kazi na tufahamu kuwa tunaifanya kazi moja, asitokee mtenda kazi akafikiri kuwa hajaheshimiwa kwa kupangiwa eneo fulani, kokote tutakakoenda kumbuka Bwana yuko pamoja nawe na anajua kuwa unaujenga mwili wa Kristo, aidha tunafanya huduma hizi kwa neema ya Mungu kwa hiyo neema zinatofautiana kinachotakiwa kwetu ni uaminifu, usitake kuwa na huduma kama ya fulani kwa sababu kila mmoja ana neema tofauti na hivyo tutatumia neema hizo kwa kufaidiana

Waefeso 4:7-8 “Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.”

1Petro 10-11 “kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.”

Warumi 12:3-5 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani. Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.”               

Kwa hiyo utaweza kuona Mungu ametuita kutenda kazi pamoja naye kwa neema na vipawa na karama tofauti tofauti, tutumie kila alichotupa Mungu kumtumikia bila kuumiza mwili wa Kristo kwa migawanyiko na manung’uniko mbalimbali kwani wote tutaifanya kazi hii kwa kufikia lengo moja kuufikia ulimwengu na kuwaleta watu kwa Yesu na kulijenga kanisa lake ili baada ya utumishi wetu duniani tukakae naye kule mbinguni

Jinsi tunavyoweza kujenga pamoja na Mungu

Katika kanisa la Mungu kuna namna mbalimbali za utumishi ambazo kwazo tunaweza kuzitumia katika kumtumikia Mungu, Ni muhimu kwetu kufahamu kuwa tukiifanya kazi hii ya Mungu kwa hiyari, kwa moyo na kwa uaminifu Mungu mwenyewe atakupa thawabu na kukupongeza na kukufuta machozi kwa kazi hii ambayo ina upinzani kutoka kwa adui shetani lakini simama kwa uaminifu kwaajili ya Bwana kama alivyofanya mtume Paulo ambaye alivumilia

Mathayo 25:21-23. “Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.”

Washirika wanapohudumiwa vema na kufikiwa katika mazingira yote hasa katika makanisa makubwa wanaona kuwa wanajaliwa hata kama hawamuoni mchungaji kiongozi kutokana na majukumu yake umoja wa kanisa utaimarika, kanisa letu litakuwa kwa kasi kwa ukuaji wa aina zote nazungumzia ukuaji wa kiroho, ukomavu na wa kiidadi na kuwa kanisa la maelfu, umoja utaimarika hata pamoja na ukubwa wa kanisa, na wingi wetu utageuka utajiri na afya ya kila mmoja wetu na miujiza haitakoma umati utavuta umati na Mungu atataka kujidhihirisha kwenye kusanyiko la watu wengi, sasa haya ndio maeneo na mazingira tunayoweza kumtumikia Mungu wetu:-

  1. Kuwahudumiwa waamini wapya – Mojawapo ya eneo Muhimu sana ambalo watenda kazi wote, wanafunzi wote na wenye hekima wote tunapaswa kulipa uzito mkubwa sana sana ili tupate kanisa lililobora ni kuwahudumia waamini wapya, au kuwahudumia watoto wachanga kiroho, kuwafuatilia, kuwalisha kwa neno la Mungu na kufanya malezi, Kama tunampenda sana Yesu upendo wetu utaonekana kwa jinsi tunavyowalisha kondoo zake

 

Yohana 21:15-17 “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.”

 

Agizo hili ni pana kwani linahusu ulishaji mzima wa kondoo, watumishi wa Mungu walioitwa katika wito maalumu wataifanya kazi ya kuwalisha kondoo katika ibada, tulizojipangia na katika semina zitakazojitokeza na kadhalika, lakini watenda kazi, wanafunzi na wenye hekima (Wiseman) wao watapaswa kuhakikisha kuwa wanawahudumia na kuwalisha watoto wachanga kiroho kwa kuwafundisha masomo ya mwanzo ya wokovu, ukiwaimarisha waamini wapya katika wokovu, kwa kuwaombea, kwa kuwafundisha kuisoma Biblia, na kuwaelekeza kuhusu maisha  tamaduni na Misingi  ya imani ya kanisa letu

 

  1. Kuwahudumia waamini wote ibadani    - Eneo lingine la huduma zetu kama watendakazi, wanafunzi na wenye hekima ni kuwahudumia watu wote wanaohudhuria ibada katika kanisa letu, watu waliopitia shule hii ya huduma watawahudumia watu kwa kuwapokea vizuri na kwa heshima, kuwapokelea vitu vyao, watoto na kuwaongoza mahali sahihi pa kuketi, sio hivyo tu kama ni mgeni utafanya kila jitihada kutambua anaitwa nani namba zake za simu na atakuwa pamoja nasi kwa muda gani, kama ni wadhaifu tutawatia nguvu, na tutaanza kuwapandisha imani kuwa umefanya uamuzi wa busara kuja kuabudu katika kanisa letu hili zuri, hakikisha kuwa kila mtu ana mazingira salama ya kuabudu, atajua vyoo viko wapi, wasaidie kujua mambo muhimu wanayopaswa kuyajua, tutakuwa tayari kuhudumu pamoja na Muhubiri katika ibada kuu na maombezi na kusawaidia watu wanaoanguka kwa mapepo au nguvu za Mungu na wale wanaofunguliwa na kuhakikisha kuwa tunawahifadhi kwa nguo maalumu safi na kuwafunika, Pia kuwapeleka mahali salama na sahihi zaidi na katika ibada nyingine maalumu kama ubatizo, meza ya Bwana, kubariki watoto, na kadhalika

 

Yohana 10:14 “Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi

 

1Wathesalonike 5:14 “Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.”

 

Waefeso 4:1-3 “Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.”

 

  1. Kusaidia huduma ya kichungaji – Watendakazi wote, wanafunzi na wenye hekima wanapaswa pia kufanya kazi ya kutoa msaada wa huduma ya kichungaji, ikumbukwe kuwa Mchungaji hawezi kufanya kila kitu peke yake, na akilazimika kufanya yote muda wa kukaa katika neno la Mungu na maombi utafilisiwa na kuathiri huduma za kiroho za jumla  na ndio maana mitume waliona vema kuwa na mashemasi kwaajili ya majukumu

 

Matendo 6:1-7 “Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno. Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia; ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao. Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.”

 

Warumi 16:3-4. “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

 

Kutoka 18:17-22 “Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako. Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao; nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.”

 

Wasaidizi wa huduma ya kichungaji watafanya majukumu ambayo yangewezwa kufanywa na mchungaji katika kanisa, majukumu hayo ni pamoja na kuwatembelea washirika, kuwasaidia katika maombi, kufanya ufuatiliaji, na kufanya uashauri wa kichungaji, huduma hizi zote zinafanyika chini ya utumishi wa mchungaji kiongozi katika kanisa

 

  1. Kuwahudumia wale wanaotokwa na pepo – watenda kazi, wanafunzi na wenye hekima ni wajibu wao kuhakikisha kuwa mambo yote katika nyumba ya Bwana yanafanyika kwa kufuata utaratibu, Mungu ni Mungu wa utaratibu na anataka mambo yote yafanyike kwa utaratibu, kwa msingi huo, moja ya huduma wanayotakiwa kuifanya ni kuwahudumia wenye kuteswa na mapepo hasa katika ibada za maombezi, wanaousumbuliwa na pepo kama ni wakati ibada inaendelea ni lazima wahamishiwe kwenye vyumba maalumu vya maombezi, lakini kama machungaji yuko katika kuwashughulikia na wanaangushwa au kusumbua miongoni mwa watu watolewe na kupelekwa mbele au sehemu maalumu wanakoweza kuwa na nafasi ya kuhudumiwa na kufunguliwa kanisa linapokuwa tayari na watendakazi wanapokuwa tayari kuhudumu pamoja na Mchungaji na kuhudumu pamoja na Roho wa Mungu kwa utaratibu maalumu, Mungu Roho Mtakatifu atafanya miujiza mikubwa zaidi, kama pepo watasumbua wakati neno la Mungu linaendelea, wenye pepo wapelekwe sehemu nyingine ili neno la Mungu lihubiriwe kwanza, na wasipoteze usikivu!

 

1Wakorintho 14:39-40 “Kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha. Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”

 

Waefeso 6:11-12 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”

 

Mapepo yanaweza kuwaathiri watu lakini kumbuka kuwa watu sio pepo, kwa hiyo utu wa aliyeathiriwa uthaminiwe na atunzwe kwa heshima zote, tusiwakasirikie wala tusiwe na msisimko ni lazima tuwe wapole na waungwana tuwahifadhi tuwasaidie kufunguka, tuwapeleke sehemu maalumu zilizoainishwa, tuwafute vizuri na tuchukue taarifa zao kwaajili ya ufuatiliaji na kwaajili ya kutunza muujiza na ushuhuda wa baadae

 

Mwondoe mwemye pepo katikati ya umati wa watu, kama ikiwezekana, tumia mamlaka kwa ustaarabu kuyakemea na sio kelele, usitumie nguvu kumbuka pepo wanatoka kwa jina la Yesu na kwa nguvu za Roho Mtakatifu wewe na mimi sio tunaotoa pepo, Pepo wanatolewa na Roho, sisi wajibu wetu ni kuwapa imani na kuwasaidia wao kupokea muujiza wao, msikemee watu wengi pepo mmoja mamlaka moja inatosha.

 

Mathayo 12:28-29 “Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.”         

 

2Timotheo 2:24 “Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;”

 

  1. Kuwahudumia watu wanaoangushwa chini – uwe na uwezo wa kutambua ni aina gani ya sababu imempeleka mtu chini, sio kila anayeanguka chini ni kwa sababu ya pepo, wengine wanaweza kuigiza tu, na wengine wanaweza kuwa wamehemewa na hisia kali, na wengine ni kwa sababu ya nguvu za Mungu anaangushwa chini lakini anaweza asiwe na pepo, kwa hiyo usikimbilie kukemea pepo, kwa sababu wengine huangushwa tu na nguvu za Mungu na anaweza kujisikia vibaya kudhaniwa kuwa ana pepo.

 

Luka 5:16-17 “Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba.Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.”

 

Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”

 

Wahudumu, watendakazi, wanafunzi na wenye hekima kumbuka ya kuwa lolote linaweza kutokea wakati wa maombezi, na wakati wa ibada jiandae kusimama nyuma kwa huduma, kwa wale wanaohudumiwa,  jiepushe kusukuma watu, tunza heshima ya watu hususani wanawake, wafunike wanapokuwa wamekaa vibaya, hakikisha kunakuwa na utulivu na amani tengeneza mazingira ya Amani, wasaidie kwa upole, omba kimya kimya, na usiwakasirikie wala kuwaudhi wao ni kama wagonjwa wetu na sisi ndio wahudumu wao, jua ya kuwa Mungu ndiye anayewahudumia pamoja nawe kwa sababu hiyo tuwahudumie kwa huruma na upendo

 

  1. Kuwahudumia wageni ambao ni mara yao ya kwanza – Wakristo wanahimizwa kuwa wakarimu, unapowapokea watu vizuri kwa tabasamu la upendo na kuwapa muongozo mzuri, bila papara na kwa kuwaonyesha upendo wao watajua kuwa kweli hapa ni kanisani, kanisani ni mahali ambapo watu wanapaswa kupokelewa kwa upendo kuliko mahali kokote kule, kanisani ni zaidi ya dukani, hotelini, gengeni  na kadhalika waonyeshe watu uungwana mkubwa, msalimie vizuri, mpe ratiba na muelekeo wa ibada,  usimuache akajitenga, zungumza kwa lugha za kawaida, waonyeshe shukurani waonyeshe kuwafuatailia baada ya ibada, wageni wangependa kuagana na mtu yule yule aliyempokea mwanzoni hasa kama ulimpokea vizuri, kwa hiyo yule utakayempokea mwanzoni ni mteja wako mpaka mwisho usimpoteze

 

Waebrania 13:1-2 “Upendano wa ndugu na udumu. Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.”

 

Yohana 13:34-35 “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”

 

1Wakorintho 9:19-23 “Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi. Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria. Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu. Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.”          

 

  1. Kuwahudumia viongozi wa serikali – Viongozi wa serikali na viongozi wakubwa wa kitaifa wanaweza kuwa wakristo wenzetu katika kanisa la Mungu lakini pia wanaweza kuwa rafiki zetu na wanaweza kutembelea kanisa letu kwa taarifa au ghafla watendakazi katika kanisa tunapaswa kuwahudumia kwa heshima na ustaarabu pia, heshimu nafasi waliyo nayo lakini usiwaabudu, usilichuje neno la Mungu kwaajili yao, weka heshima sawa na maelekezo ya injili, Mungu hana upendeleo, lakini anayestahili heshima heshima, viongozi wahudumiwe vizuri na kukaribishwa na kama iko sehemu maalumu ya wageni maalumu wanaweza kuelekezwa hapo, kama ni kiongozi mwenye itifaki (Protocol) kadhaa wasikilize viongozi wa itifaki walioambatana naye na shirikiana nao katika utaratibu mzuri, mawasiliano mazuri na kadhalika, kauli za kisiasa kanisani haziruhusiwi, unabii unaohusu wanasiasa, haufai, isipokuwa kama Mungu amesema hivyo, na hakuna sababu za kulazimisha maombi ya kitaifa kama hakukuwa na programu hiyo msibadili gea angani, jiamini, tunza heshima jiepushe na mizaha inayoweza kutafasiriwa vibaya maneno yako yajae neema.

 

Warumi 13:7-8 “Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima. Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.”

 

1Petro 2:17 “Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme

 

Wakolosai 4:5-6. “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.”  

 

  1. Kuwahudumia watumishi wa Mungu – Watenda kazi, wahudumu, wanafunzi pamoja na wenye hekima katika kanisa wanawajibu pia wa kumuhudumia mchungaji, wakati wote huduma inapoendelea pamoja na shughuli nyingine tutakuwa katika maombi ya kimya kimya tukiendelea kuhudumu pamoja na mtumishi wa Mungu, wafunikwe kwa kuwaombea, uwe na karama ya kupambanua roho na kung’amua kwa haraka watu wanaotaka kuwashambulia watumishi wa Mungu, angalia kama amechoka, angalia kama amekata tamaa, angalia kama anapingwa, angalia kama anahitaji kitambaa cha jasho, maji ya kunywa ama kama analetewa kitu kibaya, wekeni utaratibu wa ulinzi na usalama kwaajili ya kanisa zima na kwaajili ya mtumishi wa Mungu, dhibiti watu kumfikia kwa haraka bila utaratibu, au wale wanaotaka kumshambulia, wekeni timu ya itifaki ya namna ya kumfikia mtumishi wa Mungu, kataza wanaomsengenya, wasahihishe wasiomuelewa, mlinde bila kupigana, muheshimu bila kumuabudu, heshimu mipaka, wajibika kwake, lindeni kile Mungu ameweka ndani yake,  Mke wake na familia yake na kadhalika, tunapowahudumia watumishi wa Mungu tunamuhudumia Mungu pia.

 

Yohana 12:20-21. “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu. Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu. Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.”

 

Zaburi 105:14-15”Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.”

 

1Timotheo 5:17 “Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha

                 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima       

Jumapili, 19 Julai 2026

SHULE YA HUDUMA!


Waefeso 4:11-12 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;”



Utangulizi

Shule ya huduma ni mafundisho maalumu ya kibiblia  yaliyoandaliwa  na Rev. Innocent Samuel Kamote kwa kusudi la kuwaadaa watu wa Mungu kuwa tayari kwaajili ya huduma za kichungaji ndani ya kanisa, huduma za kikanisa, na huduma zote za kiroho kupita mafundisho ya Biblia, mafundisho haya huandaliwa kwa programu maalumu zinazolingana na maono ya kanisa letu na mtindo ambao sisi tumechagua kumtumikia Mungu kwa huo, Ni muhimu kujikumbusha kuwa kusudi kubwa la Mungu kutuokoa sio kwaajili ya kuhudhuria ibada makanisani pekee bali kwaajili ya kumtumikia yeye, Mungu anachukizwa sana na wakristo waliodumaa kiroho ambao anawatarajia labda wangelikuwa walimu wa wengine lakini kwa kutokufahamu wao wamebaki kuwa wachanga kwa miaka mingi sasa.

Waebrania 5:11-14 “Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia. Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.”

Mungu anapotuokoa anataka tuimarike kwanza kiroho na kisha baada ya kuimarika atutumie sisi kuimarisha wengine, kwa hiyo Mungu hutukuza na kutukomaza kiroho, ili tuje tumtumikie na kuhakikisha kuwa kazi ya huduma inatendeka, kwa hiyo kila mtu aliyeokoka anapaswa kukua na kufikia ngazi ya kuwa mtenda kazi yaani watu wanaowahudumia wengine katika mwili wa Kristo, sio mpango wa Mungu wewe ubaki kama ulivyo kila mwaka!

Luka 22:31-32 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano; lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.”

Leo tunapochukua muda kuzama kwa kina na mapana na marefu katika kujifunza shule hii maalumu ya huduma, Mungu anataka kukuimarisha na kuleta ufahamu na ukomavu kwako ili wewe uweze kuwa msimamizi wa roho za watu ndani ya kanisa letu na kuwasaidia wengine, tutajifunza somo hili  shule ya huduma kwa kuzingatia vipengele vikuu muhimu vitatu vifuatayo:-


  • Sifa za mwanafunzi wa shule ya huduma.
  • Umuhimu wa kuwa na uzoefu katika huduma.
  • Mambo yatupasayo kufanya kama wahudumu katika kanisa.

 

Sifa za mwanafunzi wa shule ya huduma.

Nyakati za kanisa la kwanza walipochagua watenda kazi walikuwa makini sana kuzingatia sifa  za wale  waliowachagua walijua kuwa wale watakaochaguliwa au kuteuliwa kusaidia kazi mbalimbali wana sifa na vigezo vyenye kuwafaa sana na kuwa wanaaminika na ni wanyenyekevu na watii ambao kupitia wao wataisaidia kazi ya Mungu, na kuwasaidia watu wote walioamini kusimama imara katika Bwana na kuwafundisha wengine kuishika imani vile vile kama wao walivyofundishwa, tunaona kwa mfano Paulo Mtume alimchagua Timotheo mtu ambaye alikuwa anaheshimika sana katika Kanisa  kutokana na usafi wa Imani yake na sifa zake zilijulikana na watu wote wa makanisa yaliyokuwako Listra na Ikonio na baada ya kuongezeka kwake makanisa yakatiwa nguvu katika imani ona:-

Matendo 16:1-5 “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio.Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani. Basi walipokuwa wakipita kati ya miji ile, wakawapa zile amri zilizoamriwa na mitume na wazee walioko Yerusalemu, ili wazishike. Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.”

Ni imani yangu kuwa kila aliyechaguliwa/atakayechaguliwa kuingia katika shule hii ya huduma atakuwa mtii, atakuwa mnyenyekevu, atafuatilia kwa makini mafundisho yetu, na kujitahidi sana kuwa na sifa zinazohitajika sawa na maandiko ili aweze kutumika kwa uaminifu na kupitia wewe makanisa yetu yakatiwe nguvu na kuimarika lakini sio hivyo tu hesabu  ya watu wa makanisa yetu ikaongezeke kila iitwapo leo. Sasa basi mwanafunzi wa shule ya huduma anapaswa kuwa na sifa hizi kama neno la Mungu lisemavyo:-

  1. Kulishika neno la Mungu kama ulivyofundishwa – Mwanafunzi wa shule ya huduma anapaswa kuwa mtu anayeyaamini mafundisho yetu kuyakubali, kuyashahika na kuyafuata vile vile kama alivyofundishwa, mtu hawezi kuwa mwanafunzi wa mtu ambaye hayashiki mafundsho yake, mwanafunzi wetu ni lazima atusome, asome nia ya mitume wa kanisa kuwa wanataka nini wana maono gani na wanaelekea wapi, wanaamini nini, Misingi ya imani yetu ni ipi, kisha aanze kuishi sawa na kile alichojifunza kutoka kwetu na kukisimamia/tetea

 

Yohana 8:31-32 “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.”

 

Yohana 14:23-24 “Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka.”                                

 

Tito 1:7-9 “Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa MUNGU; asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu. Bali awe mkaribishaji, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake; akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.”

 

2Yohana 1:9-10 “Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia. Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.”

 

Mwanafunzi wetu ni lazima awe yule anayeyashika mafundisho ya Kristo, awe mtu aliyeiva katika neno la Mungu, amejaa neno, analijua neno analipenda anamoyo wa kujifunza na mwenye sifa za kumpenda Yesu huyu anaweza kwenda na kile ambacho Kristo amekikusudia akilishika neno la imani vilevile kama alivyofundishwa!.

 

  1. Awe mwaminifu – Kila mwanafunzi ambaye amechaguliwa au kuteuliwa katika shule ya huduma anapaswa kujifunza kuwa mwaminifu, Imani yangu ni kuwa kila ambaye yuko katika darasa hili atakuwa mwaminifu, na kama hauna uaminifu utaomba Mungu sasa akupe kuwa mwaminifu, Mungu anakuleta katika darasa hili ili akukabidhi injili, na injili inapaswa kukabidhiwa kwa watu waaminifu ambao wana sifa ya kuikabidhi kwa wengine, uaminifu huu unaanzia katika kuhudhuria ibada, zote kufika katika mafundisho ya neno la Mungu, kuandika na kukua kiroho, na kuwa tayari  kuyapeleka hayo katika makanisa yetu yote na nje ya makanisa yetu ili kujenga umoja na afya ya  kiroho inayofanana vile vile sawa na ile aliyotuachia Kristo  na mitume wa Bwana

 

Matendo 2:41-42 “Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.”

 

2Timotheo 2:2 “Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.”

 

1Wakorintho 4:1-2 “Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.”

 

Mathayo 24:45-47 “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.  Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”         

 

  1. Awe na unyenyekevu – Tunapoingia katika shule ya huduma kama hivi, tunaandaliwa kwa lengo, nia na makusudi ya kuwatumikia watu, watu ndio mtaji wetu mkubwa na sio vinginevyo, tunataka roho zao tuzipeleke kwa Kristo kwa ibada na  utumishi wake,  kwa hiyo ni lazima tujifunze unyenyekevu, hatuendi kuwa mabwana wakubwa tunakwenda kuwahudumia watu, Unyeyekevu unapaswa kuwa kama vazi letu iwe ni tabia yetu inayotutambulisha kila mahali, mavazi humtambulisha mtu, watumishi wa Kristo wanapaswa kutambulika kwa unyenyekevu wao kwa sababu ndivyo Bwana wetu Yesu alivyokua na sisi tu mawakili wake

 

Wakolosai 3:12-14 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.”

 

Wafilipi 2:5-8 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.”

 

1Petro 5:2-5 “lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka. Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

 

  1. Awe kielelezo – Katika shule ya huduma kila mwanafunzi anapaswa kudhamiria kuwa kielelezo chema katika Imani yetu na mafundisho yetu, Mungu anapoona kuwa sote tumedhamiria kuwa kielelezo kwa wale watakaoamini ataendelea kutuamini na kutuletea watu wengi zaidi, kwa sababu wanafunzi huigiza kila kitu kinachofanywa na walimu wao, wale tunaowahudumia wataigiza kila kitu kutoka kwetu hivyo neno la Mungu linasiistiza tuwe kielelezo yaani mfano wa kuigwa, wakristo wote watuigize sisi watuone ndio wa kuigizwa na sio wakrito pekee bali kila mahali katika jamii tuwe mfano bora wa kuigwa kwa tabia na mwenendo.

 

Neno kuwa kielelezo katika maandiko ya Kiyunani linatajwa kama neno “tupos” ambalo kwa kiingereza ni “a model for imitation” sawa na mfano wa kuigwa au kielelezo katika Imani, kila muhudumu anapaswa kuwa kielelezo katika usemi, mwenendo imani na usafi hakuna namna ya kukwepa jambo hili.

 

Tito 2:7-8 “katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.”

 

1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.”

 

1Wathesalonike 1:4-7 “Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu; ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu. Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu. Hata mkawa kielelezo kwa watu wote waaminio katika Makedonia, na katika Akaya.”

 

  1. Nidhamu – Ni muhimu kufahamu kuwa kamwe huwezi kumtenganisha mwanafunzi na maswala ya nidhamu, wanafunzi wa Yesu ni lazima wawe na nidhamu, hii ni sawa na kujitia nidhamu, kuwa na kiasi, kujidhibiti, Neno nidhamu katika kiingereza linatamkwa “Discipline” ambalo kwaa asili linatokana na neno la Kilatini “Discipulus” ambalo maana yake ni “leaner” au “Student”  hii ndio maana ya mzizi wa neno “Disciples” yaani wanafunzi,  kwa msingi huo wanafunzi ni watu wanaojitawala, wanaojitia nidhamu, kama tunataka kumtumikia Mungu kwa kiwango kikubwa na kumpa Mungu nafasi ya kututumia lazima tujitie nidhamu, maisha matakatifu  yanahitaji nidhamu, maombi yanahitaji nidhamu, kujisomea neno kunahitaji nidhamu, kutunza upako kunahitaji nidhamu, kufunga kunahitaji nidhamu, kuabudu kunahitaji nidhamu.

 

1Wakorintho 9:24-27. “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate. Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika. Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.”

               

  1. Upendo kwa watu – Kuna uhusino mkubwa sana kati ya kuhudumia watu na upendo, huduma zote zinazohusisha kuwahudumia watu zinahitaji uwe na upendo, na wala usiwe na ubinafsi, na unapaswa kuwa na huruma kwa watu, upendo huu sio wa hisia  wala wa kinafiki ni utendaji wa kivitendo unaohusisha kukutana na mahitaji ya wengine, kwa hiyo muda wetu, vipawa vyetu tunawekeza katika kuhakikisha tunawahudumia watu kwa huruma na upendo

 

Mathayo 9:35-38 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”

                               

Umuhimu wa kuwa na uzoefu katika huduma

Ni muhimu kufahamu kuwa nyakati za kanisa la kwanza walipotaka kuchagua mtu katika huduma mojawapo ya msingi waliouzingatia ulikuwa ni uzoefu katika huduma, jambo hili lilikubalika na jamii yote ya wanafunzi, kumtumikia Mungu na kutumikia watu linahesabiwa kama jambo la furaha katika Kristo na sio mzigo kwa sababu iliaminika kama njia ya kujiweka karibu na Mungu huku ukitimiza kazi hii njema ya kiungu

Matendo 1:21-26 “Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi. Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.”

Tunapozungumzia uzoefu hapa tunamaanisha mtu aliyekaa katika mafundisho ya Bwana Yesu kwa muda wa kutosha au aliyepitia shule zote muhimu zinazohusiana na utumishi huu tulioitiwa, kwa maana nyingine hapaswi kuwa mtu aliyeokoka hivi karibuni au aliyepandishwa kwa haraka haraka, kanisa la sasa lina watu wengi walioibuka kama uyoga, mtu alikuwa mganga wa kienyeji, mchawi, sheikh hata hajakaa sawa tayari kesho unasikia ni mhudumu

1Timotheo 3:6-7 “Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”

Kanisa linalotaka uamsho mzito  na wa kudumu halina budi kwenda na msingi huu, ambapo neno la Mungu linaonya kuwa hatupaswi kumchagua mtu katika huduma ambaye bado ni mchanga, kumpaisha mtu kwa haraka kunaweza kutuletea madhara makubwa kutokana na kuwa mtu huyo anaweza asiwe na uzoefu wa ukomavu wa kiroho, kwa hiyo kumuinua mtu kwa haraka kunaweza kumletea kiburi na majivuno na anguko la haraka pia kama Shetani alivyoanguka kwa majivuno, kwa hiyo mwanafunzi anayeandaliwa kuwa mhudumu wa injili anapawa kuwa mtu mzima kiroho mtu aliyepitishwa na Mungu katika shule mbalimbali na sio kwa sababu ya kipawa chake  kuepusha hatari ya kuwa na majivuno kwa hiyo asiwe mtu mchanga au aliyeinuka haraka “Novice”  kwa Kiyunani “neophutos” maana yake kwa kingereza ni “Newly planted” yaani pandikizi jipya mtu ambaye hana ukomavu katika imani, kwa hiyo anaweza kuwa ameokoka hivi karibuni, au akawa mtu ambaye amedumaa kiroho, ndio maana siku hizi unaweza kuona mtu ni Askofu lakini ana bifu na mtu fulani, anabagua ana mtu ana uadui naye, ana uchungu, na ugomvi na kupoozesha kabisa sifa zinazomuonyesha kuwa ni mwanafunzi wa Yesu, makanisa mengi yamepoteza mwelekeo pale yalipowababaikia watu kwa sababu walikuwa Masheihk, au Wasomi, au wenye vyeo vikubwa na bila kupitia michakato kadhaa ya kiimani wakapaishwa kuwa viongozi wa kanisa na hii imechangia kuilifanya kanisa kupoa na kuwa na watu wenye kutumia akili zao zaidi kuliko hata kumsikiliza Mungu Roho Mtakatifu japo tunahitaji uwiano.

Onyo la kutokuweka viongozi wachanga katika kanisa linatolewa katika misingi mikuu minne ya tahadhari:-

  1. Kuanguka katika mtego wa ibilisi kuwa na kiburi
  2. Kuitia aibu kanisa kutokana na kukosa ukomavu na mizizi ya kiimani
  3. Kukosekana kwa msimamo katika mafundisho na kushindwa kuisimamia imani au kuitetea
  4. Kwamba bado anahitaji ukomavu katika wokovu,mafundisho na tabia, ukomavu wa hekima na busara

 

Matendo 6:3-4 “Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.”

Ukomavu wa kiroho ni mchakato unachukua muda, wokovu ni mara moja lakini kujengeka kiroho ni safari inayohitaji mchakato wa muda mpaka mtu akue afikie hatua ya kuweza kula chakula kigumu, wakati mtoto mchanga kiroho anahitaji maziwa na huduma ya kichungaji, mtoto mdogo anahitaji malezi na sio kubebeshwa mzigo, kuwabebesha watoto wachanga kiroho mzigo wa uongozi ni kutafuta kuwadhuru na kuwaharibu na pia kuliharibu kanisa, unaweza kuwafanya wawe na kiburi na majivuno, unaweza kusababisha imani yao ikaharibika, unaweza kuwafanya wakakata tamaa,angalau mtu awe amedumu katika Imani na mafundisho kwa muda usiopungua miaka mitatu kama alikuwa mwaminifu kuhuduhria ibada na mafundisho ya kanisa letu, anaijua imani yetu na anauwezo wa kuitetea.

Waebrania 5:14 “Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.”

1Wakorintho 3:1-2 “Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,”

1Timotheo 3:8-10 “Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu. Wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi.Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.”

Mambo yatupasayo kufanya kama wahudumu katika kanisa.

Kila mwanafunzi wa shule ya huduma anapaswa kufahamu kuwa ameitwa kuutumikia mwili wa Kristo huu ni utu mishi mwema sana na wa hali ya juu na kama kila mmoja atakuwa mwaminifu Mungu atampa thawabu, kwa hiyo huduma hii iko kwaajili ya kufaidiana yaani kuujenga mwili wa Kristo na sio kushindana na uongozi, bali kusaidia.

1Wakorintho 12:4-7 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.”

Neno kufaidiana katika maandiko ya kiyunani linatumika neno “Sumpherōambalo kwa kiingereza linatumika neno “Contribute” sawa na kuchangia kwa faida kama vile Paulo alivyosema mahali Fulani mmoja alipanda mwingine akatia maji bali mwenye kukuza ni Mungu, Mungu ametupa huduma na akili na vipawa mbalimbali ili viweze kuchangia katika kuujenga mwili wa Kristo ambao kimsingi hauwezi kujengwa na mtu mmoja kwa sababu hiyo tuhudumiane kwa Upendo.

Wagalatia 5:13 “Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.”

Kila mwanafunzi wa shule ya huduma anapaswa kufahamu kuwa ameitwa kwaajili ya kuwatia nguvu wengine, kufarijiana, kujengana na kunoana, kumbuka kuwa chuma hunoa chuma!

1Wathesalonike 5:9-11. “Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala. Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.”

Kila mwanafunzi wa shule ya huduma anapaswa kufahamu kuwa anapaswa kusaidia huduma ya kichungaji, karama za huduma tulizo nazo ni huduma za masaidiano kwa hiyo katika kanisa tunawasaidia viongozi wetu katika kubeba maono, kulinda umoja na kusaidia kazi za kichungaji        

Warumi 12:4-8 “Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake. Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.”

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

 

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumanne, 14 Julai 2026

Nafsi yangu kwa nini kuinama?


Zaburi 42:5-6 “Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu. Nafsi yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo nitakukumbuka, Toka nchi ya Yordani, na Mahermoni, na toka kilima cha Mizari.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa ziko nyakati katika maisha ya mwanadamu na hata watu wa Mungu ambapo tunapitia vipindi ambavyo nasfi zetu zinainama kwa sababu ya kuzidiwa na maumivu ya  kihisia na kiroho, kunakosababishwa na huzuni, kukata tamaa, kukosa utulivu, kuwa na mashaka kusongwa na mawazo, hofu, kutokujitosheleza. Misiba na kuwa mbali na nyumbani au kuwa  ugenini au uhamishoni, Watakatifu waliotutangulia wanaonyesha kuwa nao pia katika nyakati tofauti tofauti walipitia hali hizi za kuzidiwa na mgandamizo wa mawazo, kukosa tumaini, kuhisi kama Mungu yuko mbali nao na kuelemewa na changamoto za maisha na upweke na hivyo kusababisha nafsi zao kuinama. Kutokana na hali hizo wakati mwingine waliziuliza nafsi zao maswali makali kwanini nafsi yangu unainama ilihali Mungu yupo? Kwa nini kufadhaika? Wakati Mungu ni tumaini lako?  Ona;-

Zaburi 43:3-5 “Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako. Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu. Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.”

Nafsi zetu zinaweza kuinama sio kwa sababu ya changamoto za maisha pekee lakini pia wakati mwingine ile hali ya maumivu ya kihisia, kiu ya kuhitaji uwepo wa Mungu, ukavu wa kiroho na ile tamaa ya kutaka uwepo wa Mungu uwe ndani yetu kwa wingi ili tuweze kuzishinda changamoto za nje kwa hiyo tunajifunza hapo kuwa tunaweza kuzihubiri nafsi zetu kuzikemea, kusema nazo na kuzitaka nafsi zetu zisivunjike moyo wala zisifadhaike na badala yake zimtegemee Mungu. tutajifunza somo hili Nafsi yangu kwa nini kuinama kwa kuzingatia vipengele vitatu muhimu vifuatavyo:-

·         Maana ya nafsi kuinama.

·         Sababu zinazopelekea nafsi zetu kuinama.

·         Nafsi yangu kwa nini kuinama?


Maana ya nafsi kuinama

Zaburi 42:5-6 “Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu. Nafsi yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo nitakukumbuka, Toka nchi ya Yordani, na Mahermoni, na toka kilima cha Mizari.”

Ni muhimu kufahamu kuwa neno nafsi iliyoinama katika lugha ya Kiebrania inasomeka kama “Shachach Nephesh” misamiati ambayo kwa Kiingereza inasomeka kama “downcast soul”, “discouraged soul”, “Depressed within me” au “overwhelmed soul” maana zake kwa Kiswahili ni nasfi iliyovunjika, nafsi iliyokata tamaa, au nafsi iliyolemewa na mawazo, nafsi iliyopoteza tumaini au nafsi iliyozidiwa na kuelemewa au nafsi inayopoteza nguvu na ujasiri, nasfi ya mtu ikiinama ni ukweli ulio wazi kuwa nguvu zote zinaisha na unapoteza kiu na shauku ya kufanya lolote, mtu mwenye nasfi iliyoinama anakuwa na changamoto ya kihisia kimwili na kiroho na wakati mwingine inachangiwa na kutoweka au kupotea kwa matarajio, kutokujibiwa maombi, mambo kutokuenda sawa na kuwa na hisia kana kwamba Mungu yuko mbali, upweke wa kiroho, na kadhalika, kwa ujumla mwandishi anaonyesha kuwa nafsi yake  imeinama kwa sababu ya kuwa mbali na uwepo wa Mungu, Yeye anaonekana kuwa mbali na nyumbani, na tena mbali na Nyumba ya Mungu iliyokuwako Yerusalem, Yeye yu katika chanzo cha mto Jordani katikati ya mlima Hermoni, mahali paitwapo Mizari mbali na Hekalu la Mungu wa Israel au ukuta ule wa kulia machozi mahali pa ibada.

Sababu zinazopelekea nafsi zetu kuinama.

Kiu na hisia za kuwa mbali na Mungu – Mwanadamu mwenye akili timamu anayempenda Mungu anapokuwa na hisia za kuwa mbali na Mungu au kukosa utoshelevu wa kiibada kwa kweli anakosa amani na kuhisi kupungukiwa, Mwandishi wa Zaburi hii nyakati za agano la kale  alikuwa mbali na nyumba ya Bwana alikuwa katika sehemu ya chanzo cha mto Jordani mahali unapoishia mlima Hermoni kaskazini mwa nchi ya Israel na kuanzia kilele cha Mizari,  akiwa huko safarini mbali na nyumba ya Mungu anahisi upweke na anaona kama Mungu amemuacha, nasfi yake inaumia, mambo hayaendi na ni kama maombi yanaonekana kutokujibiwa na anakata tamaa nafsi yake inainama kwa sababu ana kiu na hisia ya kuwa mbali na Mungu  kuna namna anakosa muunganiko na Mungu wake

Zaburi 42:8-11 “Mchana Bwana ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, Naam, maombi kwa Mungu aliye uhai wangu. Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea? Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, Pindi wanaponiambia mchana kutwa,Yuko wapi Mungu wako? Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.”

Mazingira magumu ya maisha – Mwandishi akiwa mbali na nyumba ya Mungu iliyokuwako Yerusalem anazungukwa na changamoto za maisha na mazingira magumu, anaomba kwa kulia machozi, lakini ni kama hajibiwi, huku akishutumiwa na kuhojiwa yuko wapi Mungu wake, anaonewa, anatukanwa maumivu yanaingia mpaka kwenye mifupa yake, nafsi yake inajikuta inainama, Tunapozungukwa na shida za kifamilia, ugumu wa maisha, magonjwa na kukosa mahitaji muhimu na kila aina ya fadhaa haya yote yanaweza kuisababisha nafsi ya mwanadamu kuinama.

Zaburi 42:3-5 “Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako. Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu. Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.”

Shinikizo kutoka kwa watu – tunaishi katika dunia ambayo wakati mwingine watu wanaweza kukuchukia bila sababu, wanasema maneno mabaya dhidi yako au wanakuzushia, au unakuwa wimbo kwenye vinywa vyao, unakataliwa, unadharauliwa, unasemwa na kusengenywa kila mahali, maneno ya watu yanakuvunja moyo unasikia jinsi wanavyokushutumu na kukusimanga na kukusema vibaya inasababisha shinikizo la maisha na kumvunja vunja mtu wa ndani na nasfi inainama

Zaburi 42:10-11 “Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako? Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.”

Kukumbuka nyakati nzuri zilizopita – Kuna nyakati ambapo tunakumbuka nyakati nzuri tulizokuwa nazo, nyakati za furaha na vicheko, nyakati za amani na furaha ya moyo, nyakati  huru, Mwandishi ni kama anakumbuka nyakati hizo, alikuwa anaenda Hekaluni tena akiwa kiongozi wa ibada ulikuwa ni wakati wa furaha lakini sasa wakati huo anaukosa, unaweza kukumbuka nyakati ambazo ulikuwa uko vizuri, ukilinganisha na hali ya sasa, mambo yako yalikuwa mazuri, ujana wako ulikuwa bomba na ni kama nyakati hizo zimepita haraka unakosa yale uliyokuwa ukiyatamani  na nafsi yako inainama

Zaburi 42:4-5 “Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu. Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.”

Hali ya uchovu wa kiroho – Ziko nyakati ambapo kimsingi mambo yanapokuwa hayaendi uko mpweke unachoka sana unachoka kuomba, unachoka kusubiri na unaweza kuchoka hata kupigana vita nafsi inashuka na unamuhitaji Mungu, nafsi inakosa nguvu na ni mpaka Bwana akutegemeze na kukuinua kutoka hapo ulipoinama ndipo unapoweza kupenya  mwandishi alikuwa anapitia hali  hii.

Zaburi 145:13-14 “Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote. Bwana huwategemeza wote waangukao, Huwainua wote walioinama chini.”

Nafsi yangu kwa nini kuinama?

Mwandishi wa zaburi hii hakubaliani na hali anayoipitia na badala yake anaihoji nafsi yake kwanini kuinama? Kwanini upate shida, kwanini uteseke? Kwanini ufadhaike, yeye anaamini ya kuwa atamsifu Mungu aliye afya ya uso wake, yaani uso wake hautakuja kukunjamana kamwe, yeye ataendelea kufurahia uzuri wa Bwana kwani anaziona njia za huzuni kuwa ni swala la Muda tu  na anajua ya kuwa, Mungu huwa hakai kimya wakati nafsi zetu zinapoinama, yeye kama baba anayejali huwahurumia wamchao na kuwaokoa, Neno la Mungu linaonyesha wazi kuwa Mungu hutoa faraja ya kipekee pale watu wake wanapochoka na kuelemewa kwa hivyo badala ya kufikiri kuwa uko peke yako Neno la Mungu linaonyesha kuwa yeye atajitokeza na kutoa msaada hivyo lazima uikumbushe nafsi yako wajibu wake kwa Bwana na neno la Mungu linasema nini kukuhusu au kuihusu ili usiiname unapoikumbusha nafsi yako kuendelea kumtegema Bwana haitokuja itokee ukazimia kupitiliza:-

1.       Anaalika wote waliochoka wanaolemewa wamjie na kuwa atawapa pumziko na raha nafsini mwao. - Mathayo 11:28-30 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

 

2.       Mungu huwapa nguvu wale waliochoka wale wanaomtumaini kama ilivyokuwa kwa mwandishi wa Zaburi hii - Isaya 40:29-31 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”

 

3.       Tunaweza kumuomba Mungu atutie nguvu pale nafsi zetu zinapochoka na kuelemewa - Zaburi 119:25-28 “Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako. Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako. Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako. Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, Unitie nguvu sawasawa na neno lako.”

 

4.       Iambie nafsi yako imsubiri Bwana kwa kimya maana yeye hatakuangusha - Zaburi 62:1-6 “Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya, Wokovu wangu hutoka kwake. Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana. Hata lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama kitalu kilicho tayari kuanguka,Hufanya shauri kumwangusha tu katika cheo chake; Huufurahia uongo. Kwa kinywa chao hubariki; Kwa moyo wao hulaani. Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa kimya. Tumaini langu hutoka kwake. Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana.”

 

5.       Iamuru nasfi yako kumuhimidi Bwana na kutokusahau fadhili zake - Zaburi 103:1-5 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Naam, vyote vilivyo ndani yangu Vilihimidi jina lake takatifu. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote. Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote, Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;”

Ikumbushe nafsi yako kuwa haitakiwi kubaki chini hata kama kuna changamoto za aina gani zinakukabili, Mungu yuko kwa hiyo kama nafsi yako inaweza kuinama yuko Mungu mwenye uwezo wa kuiinua, kama nafsi yako inaweza kulia yuko Mungu anayeweza kuifanya ikaimba sifa, kama nafsi yako inaweza kukata tamaa yuko Mungu mwamba wa wokovu wako anaweza kuleta tumanini, kama nafsi yako inaweza kusumbuka na kuelemewa yuko Mungu anayeweza kuleta furaha na kuipa raha nafsi yako, Neno la Mungu linakutaka umtumainie Bwana na kumsifu hata wakati wa changamoto kali za maisha inuka acha kuketi chini tunaye Mungu aliye karibu wala hajakuacha yeye ni kimbilio na nguvu na msaada uonekanao tele wakati wa mateso hivyo hupaswi kuogopa lolote, hata nchi itetemeke, hata milima itikisike, hata moyo wa bahari uumuke yuko Mungu ambaye ukimtegemea na kumtumaini Moyo wako hauwezi kufadhaika kamwe yeye hatakuangusha  kamwe hatakuacha wala hatakupungukia, usikate tamaa, usione kuwa mazingira ni magumu, Mungu yuko kila mahali sio Yerusalem peke yake uwepo wa Mungu uko hata mapangoni, hata ukimbizini atakushika, utainuka.

“Mungu yuko hapa, Yesu Kristo  naye yuko hapa, Roho wake Mungu  yuko hapa na malaika wako hapa,x2 kwa nini mimi niteseke  na hali wewe uko hapa, usiniache uniguse mana Mungu yuko hapa, kwanini mimi nipate tabu, nidharauliwe na kutupwa hovyo usiniache uniguse, maana Mungu yuko hapa” 

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima