Jumatano, 12 Agosti 2026

HUDUMA KATIKA VITUO VYA KUZALISHA NGUVU (POWER HOUSE)


Matendo 4:31-33 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.”




Utangulizi:

Neno la Mungu linatuonyesha ya kuwa nyakati za kanisa la kwanza Mitume walikuwa na kundi la watu waliokuwa wanawaombea, wao walikuwa kama askari wa mstari wa mbele katika kuihubiri injili na walipopata mashambulizi walitoa taarifa kwa kanisa na Kanisa liliwaombea kulingana na mashambulizi waliyoyasikia au kuyapata ona kwa mfano katika mistari hii ya Biblia utangundua kuwa kazi ya Mungu na watumishi wa Mungu wanapaswa kuombewa

Matendo 4:18-33 “Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka; maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya kuponya ulipita miaka arobaini. Hata walipofunguliwa, wakaenda kwa watu wao, wakawapasha habari ya mambo yote waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee. Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili? Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika.Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.”                

 

Matendo 12:1-5 “Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.”

Maombi ndio asili ya nguvu ya maswala yote ya kiroho katika kanisa la Mungu, na kwa sababu hiyo kila kanisa linalotaka kuwa na mafanikio katika kazi ya kuhubiri injili linapaswa kuwa na kiwanda cha kuzalisha maombi, kiwanda hiki ni nyumba ya kuzalisha nguvu yaani Power house, Katika dunia ya maendeleo ya viwanda na uchumi mwenye nguvu ni yule mwenye kuzalisha umeme wa uhakika, kwa hiyo kanisa ni lazima tuwe na viwanda vya kutosha kuzalisha umeme au nguvu na viwanda hivyo au kiwanda hicho ni katika dunia ya kawaida vinaitwa Power House, Power house ni kituo cha kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme na kusambaza katika maeneo mengine na kusababishwa mwanga, uhai, na harakati nyinginezo sasa kanisa linapaswa kuwa na Power House. Kwa msingi huo tunajifunza somo hili sasa Huduma katika vituo vya kuzalisha Nguvu (Power House) Kwa kuzingatia vipengele vitatu

·         Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu (Power House)

·         Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu (Power house)

·         Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power House)

Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu (Power House)

Kama tulivyojifunza katika utangulizi kuwa neno Power House au nyumba ya kuzalisha nguvu ni kituo kinachohusika na uzalishaji wa umeme unaoingizwa katika gridi ya taifa kwaajili ya kuleta Nuru, nguvu na kusababisha michakato ya maendeleo endelevu kuchukua nafsi yake katika inchi, katika msingi kama huo, kanisa likiwa na vituo vya maombi ni sawa na taifa kuwa na vituio vya kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme, Kituo cha maombi huzalisha nguvu za Mungu kutoka mbinguni na kusababisha mwenendo na utendaji mzima wa kanisa kufanya kazi kwa mpenyo na kwa njia rahisi, kanisa ni matokeo ya chumba cha maombi

Matendo 1:12-14. “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato. Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.”

Unaweza kuona kuwa kanisa lilizaliwa kama matokeo ya Maombi, wakati watu hawa wakiomba katika chumba cha juu, hapo ndipo mahali ambapo Nguvu za Mungu ziliachiliwa na watu wakajazwa Roho Mtakatifu na kazi ya Mungu ikaanza kuenea duniani tangu wakati ule hata leo,

Matendo 2:1-4 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.”            

Wakati wote tumeona kuwa Mungu alianzisha jambo wakati ambapo alikuwepo mtu anaomba, Petro alipokuwa anaomba na Kornelio naye alipokuwa katika kuomba Mungu aliweka mfumo wa kuwakutanisha watu hawa na watu wa Kornelio wakajazwa Roho Mtakatifu, kazi ya Mungu ikazidi kuenea haya yote yalisababishwa na mtu Fulani kujichimbia katika chumba cha maombi na kutoa muda wake au hata kuacha kula na kuruhusu utendaji wa Mungu Roho Mtakatifu katika kazi yake ambaye kimsingi ndiye Bwana wa Mavuno!

Matendo 10:1-6 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro. Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda.”

Matendo 10:9-13 “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana; akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia, akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi; ambayo ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao, na ndege wa angani. Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule.”

Matendo 10:44-48 “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu, Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi? Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.”

Watu wa Mungu wanapojichimbia mahali Fulani kuomba kwa bidii, Mungu husababisha matukio makubwa sana ya kushangaza, hufumua nguvu za utendaji na nguvu za Roho wake Mtakatifu na kusababisha uamsho mkubwa au kuleta muelekeo au kufungua mlango wa injili au kusababisha usikivu wa kiungu na kutoa melekezo na kusababisha mfumuko mkubwa sana wa kazi ya Mungu duniani, lakini haya yote husababishwa na watu wanaoomba yaani watu wanapojifungia katika chumba cha maombi na kuomba kwa bidii

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

Kwa hiyo pamoja na kanisa kuwa na mfumo wa huduma ya makanisa ya nyumbani ambayo kimsingi yanaweza kuwa yanakutana labda siku ya jumamosi (kulingana na makubaliano ya kanisa) na itakuwa vema basi siku kama alhamisi ikawa ni siku ya maombi kwaajili ya huduma zote za kanisa (Power House) huku jumatono ikiwa ni siku ya mafundisho na ijumaa ikiwa siku ya maombi na maombezi na jumapili ikiwa ni siku ya Bwana vyovyote kwa kadiri ya neema ya kila kanisa lakini nilisisitizalo mimi ni uwepo wa Nyumba za kuzalisha nguvu (Power Houses) na viongozi. Kanisa lolote lile linalotaka maendeleo bila ya kuwa na Power House haliwezi kuwa na mwanga, wala haliwei kuwa na uhai, wala hakutakuwa na harakati, na mpango kazi na mkakati wa kanisa itageuka kuwa mipango ya kawaida tu ya kibinadamu, kama unamtaka Bwana na nguvu zake basi anapatikana katika nyumba za maombi.(Power Houses)

Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu (Power house)

Mpaka hapo umeanza kupata picha kwamba ni muhimu kwa kanisa kuwa na vituo vya maombi, hata kama maombi hayo hufanyika ndani ya saa moja tu kati ya saa kumi na moja jioni hata saa kumi na mbili jioni, Lakini tunatambua sasa uhai wa kanisa lolote lile ni maombi, uamsho wa aina yoyote hauwezi kuendelea pasipo maombi, nguvu za Mungu na utendaji wa Mungu hauwezi kuendelea kuwepo katika kanisa bila ya maombi, hamna kitu kwa sababu hamwombi, lolote tunalilitaka lifanyike katika kanisa lazima kuwe na watu wanaooomba, maombi, maombi maombi.

·         Power House hufungua mbingu – Neno la Mungu linaonyesha kuwa Mungu huwa anafunga mbingu, habari ya kuzifunga mbingu ilikuwa inajulikana tangu zamani za kale nyakati za Biblia kuwa Mungu anaweza kuzifanya mbingu kuwa ngumu, anaweza kuzifunga wakati mwingine kama matokeo ya watu kutokutii lakini kupitia maombi inaonekana wazi kuwa Mungu anaweza kuzifungua mbingu:-

 

1Wafalme 8:35-39 “Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa; basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao. Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote; maombi yo yote au dua yo yote ikifanywa na mtu awaye yote, au na watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo wake, na kuikunjua mikono yake kuielekea nyumba hii; basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote);”

 

Kumbukumbu 28:23-25 “Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma. Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie. Bwana atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.”

 

2Nyakati 7:13-15 “Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”

 

Neno la Mungu linaonyesha kuna wakati Mungu huzifunga mbingu, na hii maana yake sio kwaajili ya mvua tu lakini Mungu anaweza hata kuzifunga mbingu za mtu mmoja mmoja na hata mbingu za kanisa Fulani na kama tunataka kuona mkono wa Mungu ukitusaidia basi “Power houses” zinaweza kuwa sababu ya kufunguliwa kwa milango hii ambayo imefungwa, kwa nguvu za Maombi Mungu huzifungulia mbingu

 

Luka 3:21-22 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”

 

·         Power House ni Chanzo cha nguvu za utumishi – Tumetumwa kama kondoo katikati ya mbwa mwitu hatari, ni kauli inayoonyesha kuwa watu wa Mungu wana maadui wasioonekna na wanaoonekana, kwa sababu hiyo kila aliyetumwa na Mungu alipewa nguvu kwaajili ya kukabiliana na upinzani tunaita Power encounter, shetani ni mpinzani wa injili, wachawi na kadhalika hatuwezi kwenda bila nguvu za Mungu na tunazihitaji nguvu za Mungu wakati wote na ni wapi tunaweza kupata/au kuzalisha nguvu kwaajili ya utumishi huu ni katika nyumba  za mombi “Power houses” ni chumba cha maombi ndicho kinachoweza kutupa nguvu na ujasiri wa kukabiliana na aina yoyote ile ya upinzani wa kiinjili na maendeleo endelevu ua utumishi tuliopewa

 

Luka 4:1-2 “Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.”

 

Matendo 1:8 “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”

 

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”

 

Mafundisho yetu ili yaweze kubadilisha maisha ya watu ni lazima yaombewe na kinyume cha hapo yatakuwa nadharia tu, huduma yetu ili iendelee kuleta matokeo chanya inapaswa kujaziwa na maombi, huduma ikifanyika bila ya maombi ya kutosha mwili tu ndio utakaokuwa umefanya kazi yake tunahitaji nyumba ya uzalishaji wa nguvu za Mungu katika maisha yetu ya kiroho ili mambo yaende!

 

·         Power House ni ulinzi wa Kanisa -  Ni muhimu kufahamu kuwa maombi pia hufanya kazi ya kuweka ulinzi wa rohoni, hutulinda na yule muovu, hutuepucha na majaribu, huzuia mashambulizi ya adui, hufunika wahudumu, watendakazi, wachungaji na familia zao na mali zao kwa hiyo tunayahitaji maombi kama tunavyohitaji maji ya kunywa , Lazima watu waombe na kusimama katika zamu yao kama walinzi wa rohoni

 

Matendo 12:5-7 “Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi.”

 

Mathayo 6:13 “ Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

 

Mathayo 26:40-41 “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”

 

Habakuki 2:1-3 “Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.”       

 

·         Power House huvunja minyororo – Maombi ni silaha ya kiroho inayovunja vunja nira yaani vifungo na minyororo ya aina mbalimbali, maombi huwatoa watu utumwani na kuwaweka huru walikandamizwa, yanaondoa mizigo mizito na kuwapa watu uhuru na raha ya kiungu, yanavunja laana ya kizazi na kizazi, kurejesha uhuru wa kiroho, upako huo wa kuvunja nira unapatikana kwa njia ya maombi, maombi yanaweza kufungua mpaka magereza za kawaida  na kuvunja hata nira za chuma

 

Isaya 10:27 “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.”

 

Isaya 58:6 “.Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

 

Matendo 16:25-31 “Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa. Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”             

 

·         Power House ni nguvu ya kupokea maelekezo na muelekeo – hatuwezi kwenda wenyewe, hatuwezi kwenda peke yetu, tunamuhitaji Mungu atupe muelekeo na maelekezo katika kazi yake ni katika wakati wa kuomba mbele zake na utulivu ndipo ambapo Mungu hutupa muelekeo na maelekezo, kwa hiyo kanisa ni muhimu kwetu kuwa na vituo vya kuzalisha nguvu yaani Power House ili tusiongozwe na mawazo yetu bali tuongozwe na Roho Mtakatifu ili tuweze kuifanya kazi yake kwa usahihi, kanisa lisilo na power house huongozwa na mawazo ya wanadamu na kanisa lenye power House huongozwa na Roho Mtakatifu

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

Matendo 16:6-10 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemkia Troa. Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.”                

Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power House)

Watenda kazi wetu, wahudumu, wanafunzi na wenye hekima wote wanapaswa kusimamia kwa uaminifu vituo vya maombi ya kuzalisha nguvu kokote viliko, ni afadhali kitu kingine kisimame lakini sio maombi Kanisa hatuna budi kuhakikisha kuwa maombi yetu yanakuwa endelevu, na tuone kusimama kwa maombi kama kusimama kwa moyo katika mwili wa mwanadamu ndio maana maombi yanapaswa kuendelea “Ombeni bila kukoma”, watu wote waombaji wanapaswa kuwa watu wa toba, wenye kujitia nidhamu kwaajili ya kuomba, wanaopenda kusihi maisha matakatifu, wenye tabia ya unyenyekevu na wanaojua kukaa kimya mbele za Mungu, aidha waombaji hawapaswi kuwa na midomo michafu kwa sababu midomo hiyo hiyo ndio inayotumika kuomba hivyo haifai kutumika kwenye mambo mengine hasa yasiyofaa katika mapenzi ya Mungu.

Yakobo 3:10-12 “Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.”

Watendakazi wetu walioandaliwa katika shule za uongozi na huduma ndio watakaohusika na kituo cha kuongoza maombi ya Power house maombi haya yataongozwa kila wakati katika siku na muda utakaokuwa umepangwa na kanisa

1.       Toba litakuwa jambo  la kwanza na la muhimu katika maombi

2.       Kurekebisha Mahusiano kutakuwa ni jambo muhimu katika hatua za maombi

3.       Kufunga itakuwa ni sehemu mojawapo ya muhimu katika maombi yetu

4.       Shukurani itakuwa ni sehemu muhimu ya maombi

5.       Toba za kila mtu binafsi, kwa niaba ya kanisa na kwaniaba ya taifa itahusika

6.  Tutaomba uwepo wa Mungu, Nguvu zake, huduma na kuombea wachungaji watumishi wote na watendakazi, Mungu awalinde awatumie na kuwapa afya njema

7.       Tutakemea na kuvunja nguvu za giza, kukemea mapepo na kutangaza ushindi

8.    Tutaombea kanisa, miji yetu na taifa, tutamuomba Mungu aponye wanaoteseka na kufanya ishara na miujiza akichochea karama za Roho, aokoe na kuponya na kurahisisha kazi yake kotekote

9.       Tutamsikiliza Mungu na kukaa kimya kusubiri maelekezo yake   

Power house ni tofauti na kikundi maalumu cha maombi, hii ni kiungo au kiwanda cha kuzalisha waombaji katika kanisa hivyo inapaswa kulishirikisha kanisa zima katika mfumo kama ule wa makanisa ya nyumbani,  Neno la Mungu linapaswa kuwa muongozo wa maombi haya, “Power house” sio mashindano ya kuomba, wala sio sehemu ya kujitukuza na kuonyesha uhodari wa kuomba, wala sio sababu ya kutokutii uongozi wa kanisa, ni kituo cha nidhamu kinachoomba kwaajili ya maswala mbalimbali ya kazi ya Mungu, hakipaswi kuwa chanzo cha machafuko, ni sehemu ya upendo kwa Mungu na kwa kazi yake, ni ushirika wa maombi ya washirika wote na wageni wanaopenda kujiunga kuomba nasi, Bwana ampe neema kila mtenda kazi kulijua hili na kulifanyia kazi katika jina la Yesu Ameen

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumapili, 9 Agosti 2026

JINSI YA KUANZISHA KANISA LA NYUMBANI


Mathayo 18:18-20 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”




Utangulizi:

Tumejifunza huduma ya makanisa ya nyumbani na tumeona faida zake kwamba Mungu anaheshimu makusanyiko yetu yanayojenga umoja upendo na ushirikiano, Lakini sasa hatuna budi kwenda ndani zaidi na kujifunza kivitendo sasa namna ya kustawisha Kanisa la nyumbani, sasa tunaweza je kuanza Kanisa la nyumbani

1.       Ni lazima kumuomba Mungu – Kila kitu katika ulimwengu wa roho kinaweza kupata ufunguzi endapo kitaanza na maombi, Nyakati za kanisa la kwanza Paulo mtume na wengineo watenda kazi pamoja naye waliweza kuifanya kazi kubwa ya Mungu ambayo kimsingi ilianzia katika maombi, kila kitu cha kiroho ni matokeo ya maombi kwa hivyo tunapotaka kuanzisha kanisa la nyumbani ni lazima tumuombe Mungu na Mungu atatoa muongozo na kutupa neema na mpenyo wa jinsi ya kunzisha makanisa hayo.

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

Mathayo 9:36-38 “Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”

 

2.        Kufanya utafiti wa mitaa na kubainisha vigezo – ili tuweze kuufikia mji kimkakati na kihuduma hatuna budi kufanya utafiti, wa kina kuhusu mitaa ambayo tunalenga kufungua kanisa la nyumbani na kubainisha vigezo vitakavyotusaidia kuweka makanisa ya nyumbani, katika maandiko tunaona kwamba Israel walipotaka kuirithi nchi ya kanaani walituma wapelelezi kuangalia nchi, kwa hiyo ni muhimu kufanya survey (ulinganifu na utafiti) wa kujua wapi tunaweka nini na nani anaweza kufika eneo Fulani na kanisa linaweza kuwa wapi, kwa mfano kama eneo husika ni wanajeshi, au askari ni nani anaweza kutuwakilisha katika eneo hilo, ama kuna chuo kikuu ni nani anaweza kutuwakilisha katika eneo hilo au ni uzunguni, uswahilini na kadhalika ni muhimu kujua ni watu gani tunawafikia ili tuweze kukidhi vigezo vyao, kwa mfano kama eneo ni la wasomi wa vyuo vikuu na likawako kanisa la nyumbani huko, mtendakazi atakayepelekwa kusimamia atakuwa ni yule anayeendana na vigezo vya eneo husika, Kanisa lazima tufanye mambo kwa kutumia busara na akili, tujue idadi ya watu  hasa washirika wetu na ile jamii ya wale tunaotaka kuwafikia ni wa aina gani !

 

Hesabu 13:17-20 “Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani, mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;”

 

Yoshua 2:1-2 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko. Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.

 

Yoshua 7:2-3 “Kisha Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko mpaka mji wa Ai, ulio karibu na Bethaveni, upande wa mashariki wa Betheli, akawaambia, akisema, Pandeni juu mkaipeleleze nchi, basi wakapanda juu wakaupeleleza Ai. Wakarejea kwa Yoshua wakamwambia, Wasiende watu wote, ila waende watu kama elfu mbili, tatu, wakaupige Ai; usiwataabishe watu wote kwa kuwaendesha huko; maana watu hao ni wachache tu.”

                       

3.       Tutambue nyumba na mwenyeji wetu – Kanisa la nyumbani linaitwa la nyumbani kwa sababu linafanyia ibada zake katika sebule za watu, kila mtu anaustaarabu wake na anaipenda sebule yake, kwa hiyo kukaribisha watu katika sebule yako ili kufanyike ibada ni kujitoa katika hali ya juu sana sio swala jepesi, lakini jambo hili Mungu analiheshimu na kusababisha Baraka, utoaji wa nyumba au mahali kwaajili ya kuabudia linapaswa kuwa jambo la hiyari na sio la kulazimishwa, mtu anayejitoa nyumba yake sio lazima iwe nzuri au kamili bali anaitoa kwaajili ya Bwana mtu huyu Mungu atamheshimu sana na kumbariki mno, Mungu aliibariki nyumba ya Oded-Edom kwa sababu alikubali Sanduku la Agano la Bwana Mungu wa Israel likae nyumbani mwake, Mtu anayekubali nyumba yake iwe sehemu ya kufanyia ibada hana tofauti na Obedi- Edom

 

Luka 10:5-7 “Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.”

 

2Samuel 6:10-12. “Basi Daudi hakutaka kulileta sanduku la Bwana kwake mjini mwa Daudi; ila Daudi akalihamisha nyumbani kwa Obed-edomu, Mgiti. Sanduku la Bwana akalitia katika nyumba ya Obed-edomu, Mgiti, muda wa miezi mitatu; naye Bwana akambarikia Obed-edomu, na nyumba yake yote. Kisha mfalme Daudi akaambiwa ya kwamba, Bwana ameibarikia nyumba ya Obed-edomu, na vitu vyote alivyo navyo kwa ajili ya sanduku la Mungu. Daudi akaenda, akalileta sanduku la Mungu, toka nyumba ya Obed-edomu mpaka mji wa Daudi, kwa shangwe.”

 

4.       Weka viongozi waliopitia shule ya huduma – Baada ya kuwa tumepata haya yote tunaweka viongozi wetu ambao wamejifunza kutoka kwetu wana mafundisho yetu yaliyo sahihi, walio waaminifu kwetu, wanaotii uongozi, wanaojua kuhudumia watu wenye Imani yetu, viongozi hao ni viongozi watumisi na sio wachungaji wenye mamlaka kamili ya kichungaji

 

Matendo 14:21-23 “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.”

 

Mfumo wa ibada katika makanisa ya nyumbani haupaswi kuzidi saa moja

  1. Utafungua kwa maombi.
  2. Itafanyika ibada ya kusifu na kuabudu kwa ufupi.
  3. litahubiriwa neno la Mungu la kibiblia na sio maoni ya mtu (sawa na mafundishio katika kanisa letu) tunakuwa na mafundisho maalumu na tutayagawa kwa walimu wa makanisa ya nyumbani na watafundisha kwa kadiri watakavyokuwa wanapangiwa na kiongozi husika.
  4. Ushirika, maswali, maombi na maombezi, na taarifa za ufuatiliaji.
  5. Kufunga kwa maombi.  

 

Hakuna kanisa la nyumbani linalotakiwa kujiendesha kinyume na utaratibu uliowekwa na kanisa mama ambalo ndilo lenye mamlaka ya mwisho.

Kama kanisa la nyumbani litakapokuwa kubwa taarifa itatolewa na litalazimika kugawanywa na kuwa na kiongozi mwingine aliyepitia shule ya huduma

Kiongozi wa kanisa la nyumbani jihadhari na mafundisho potofu. Jilinde na uasi au kulikata kundi, jihadhari kuligeuza kanisa kuwa klabu ya maswala ya kijamii na michango ya upatu kila kitu kifanyike kwakufuata utaratibu usafi na ushuhuda mwema wa Kirsto

Kanisa la nyumbani sio mfumo au wazo jipya ni mpango wa Mungu wa kibiblia tangu zamani za mitume na kwa kufanya hivi waliupindua ulimwengu

Kama ilivyo kwa watenda kazi kiongozi wa kanisa la nyumbani atawajibika kutoa taarifa katika mfumo utakaowekwa na kanisa kuu.

1Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”

Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Ijumaa, 7 Agosti 2026

HUDUMA KATIKA MAKANISA YA NYUMBANI


Matendo 2:46-47 “Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe, wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.”




Utangulizi

Ni muhimu kufahamu kuwa nyakati za kanisa la kwanza licha ya kuwa walikuwa wakikutana hekaluni kuabudu lakini pia walikuwa na tabia ya kukutana na kuabudu nyumba kwa nyumba, jambo hili lilichangia kwa kiasi kikubwa washirika kuwa na uwezo wa kutambuana kushirikiana na kutiana moyo lakini pia makanisa ya nyumbani yalichochea kwa kiasi kikubwa ukuaji wa kanisa mama, Ukiacha hilo pia wahudumu wenye huduma ya kichungaji, watenda kazi, Wanafunzi na wenye hekima wanapata nafasi ya kutumia vipawa vyao, na kujifunza kivitendo, malezi ya kanisa na kutengeneza njia rahisi ya kufungua matawi ya kanisa katika sehemu zingine za mji wetu, tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa huduma ya makanisa ya nyumbani ni mpango wa Mungu wa ukuaji wa kiroho, kihuduma na kiidadi, lakini ni moyo wa kutengeneza umoja na ushirikiano wa karibu kwa huduma ya kichungaji.

Warumi 16:3-4. “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

Ukiichunguza Biblia utaweza kuona kuwa nyakati za karne ya kwanza wakati kanisa linaanza watenda kazi walikuwa na makanisa nyumbani, kwa hiyo huduma katika makanisa ya nyumbani halikuwa swala geni au lisilo la kibiblia, na huduma hizi za makanisa ya nyumbani zimeonyesha mafanikio makubwa sana katika maeneo mengi duniani ikiwemo Afrika na Asia  na sehemu nyingine duniani, lakini pia makanisa ya nyumbani yameonyesha mafanikio makubwa katika maeneo ambayo injili inapigwa marufuku, leo basi tutachukua muda kujifunza somo hili Huduma katika makanisa ya nyumbani kwa kuzingatia vipengele vikuu vitatu vifuatavyo:-

  • Maana ya makanisa ya nyumbani
  • Huduma katika makanisa ya nyumbani
  • Faida ya huduma katika makanisa ya nyumbani               

 

Maana ya makanisa ya nyumbani

Makanisa ya nyumbani au kanisa la nyumbani ni mkusanyiko mdogo wa washirika wa Kanisa la mahali pamoja au katika mji mmoja ambao wanakusanyika katika mitaa yao, katika nyumba mojawapo ya mtenda kazi au mtu aliyejitoa kutoa nyumba yake kwa ajili ya  ibada, kwa kusudi la kukusanyika pamoja kwa ibada katika siku mojawapo ya juma inayokubalika kwaajili ya kufanya ibada za pamoja, kuomba pamoja, kujifunza neno la Mungu, kuumega mkate na kushirikiana na kujuana hali kwa ukaribu na kwa pamoja, makanisa ya nyumbani yanaweza kukutana katika sebule ya mshirika mmojawapo na yakiwa na uwezo wa kuwa na wanachama kuanzia 6-10 au 10-30 kulingana  na uwezo wa sebule au mahali pa kuabudia wanakokutana washirika hao, Makanisa ya nyumbani sio mbadala wa kanisa mama hata kidogo lakini ni vikundi vidogo vidogo vinavyoundwa na watu kwa kusudi la kulifanya kanisa mama kuendelea kuwa na nguvu na kukua katika upendo na ushirika, makanisa haya yanasaidia sana kuleta umoja wa kweli Maandiko yanaonyesha kuwa kulikuwa na makanisa ya namna hii nyakati za mitume:-

Kanisa katika nyumba ya Prisila na Akila – Warumi 16:3-4 “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

1Wakorintho 16:19-20 “Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao. Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.”

Nimfa pia anatajwa kuwa alikuwa na kanisa la Nyumbani huko Kolosai – Wakolosai 4:14-15 “Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu.Wasalimuni ndugu walioko Laodikia, na Nimfa, na kanisa lililo katika nyumba yake.”

Pia rafiki wa Paulo Mtume aitwaye Philemoni – Philemoni 1:1-3. “Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi, na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako. Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu, Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo              

Huduma katika makanisa ya nyumbani

Huduma katika makanisa ya nyumbani zinaendeshwa na watendakazi, wanafunzi pamoja na wenye hekima ambao wamepitia mafunzo mbalimbali katika kanisa letu, hawa sasa wanawajibika kuyahudumia makanisa hayo katika makazi karibu na mitaani kwao wanakokaa washirika, Neno la Mungu linaonyesha kuwa huduma za kiroho, maombezi, kuongoza watu katika wokovu, na kuwajenga watu zinaweza kufanyika pia katika nyumba za watu kwa taratibu maalumu, Yesu alithamini pia shughuli za kuwahudumia watu nyumba kwa nyumba ukiacha kuwa alikuwa akihitajika na umati mkubwa wa watu.

Marko 1:29-34 “Na mara walipotoka katika sinagogi, walifika nyumbani kwa Simoni na Andrea, pamoja na Yakobo na Yohana. Naye mkwewe Simoni, mamaye mkewe, alikuwa kitandani, hawezi homa; na mara wakamwambia habari zake. Akamkaribia, akamwinua kwa kumshika mkono, homa ikamwacha, akawatumikia. Hata kulipokuwa jioni, na jua limekwisha kuchwa, walikuwa wakimletea wote waliokuwa hawawezi, na wenye pepo. Na mji wote ulikuwa umekusanyika mlangoni.Akaponya wengi waliokuwa na maradhi mbalimbali, akatoa pepo wengi, wala hakuwaacha pepo kunena, kwa sababu walimjua.”

Luka 19:5-9 “Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako. Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha. Hata watu walipoona, walinung'unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi. Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne. Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.”

Luka 10:38-42 “Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake.Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake. Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie. Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi; lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.”

Tunajifunza hapo kutoka kwa Mwalimu mkuu Yesu Kristo kwamba nyumbani ni mahali ambapo huduma zote zinaweza kufanyika bila shaka yoyote uwepo wa Mungu unakuwepo popote walipo wawili au watatu ambao wamekusanyika kwa jina lake

Mathayo 18:18-20 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

Hata hivyo ni muhimu kufahamu kuwa huduma ya makanisa ya nyumbani ni sehemu ndogo tu ya ushirika mkuu na kwa sababu hiyo kuhudhuria katika hekalu kuu hakuwezi kupoteza maana sawa tu na kuhudhuria katika masinagogi hakukuwahi kuondoa maana ya kwenda Hekaluni, wala kuacha kuhudhuria ibada za muhimu katika kanisa letu, tunajifunza pia kuwa Paulo alihudumu katika kanisa kuu na makanisa ya nyumbani huku akitembelea nyumba kwa nyumba na kuwahudumia hii ilileta mafanikio na ufanisi mkubwa nyakati za kanisa la kwanza:-

Matendo 20:17-21 “Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa.Walipofika kwake, akawaambia, Ninyi wenyewe mnajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu wakati wote, nikimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, na kwa machozi, na majaribu yaliyonipata kwa hila za Wayahudi; ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba, nikiwashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.”

Kwa hiyo tunaweza kufundisha, kuomba, kuabudu, kuuliza maswali, kutambuana na  kuhubiri injili, na watu wakaokoka, na kujenga umoja wenye nguvu huku tukifahamiana sana kuliko katika kanisa kubwa na mpango huu ni mahususi sana endapo kanisa mama linalenga kuwa kanisa kubwa lenye kusanyiko kubwa la watu maelfu kwa maelfu

Faida ya huduma katika makanisa ya nyumbani

Kanisa la nyumbani lina faida kubwa sana endapo kanisa mama lina malengo ya kuwa kanisa kubwa lenye nwaamini maelfu kwa maelfu yaani Mega Church, Kanisa linapokuwa kubwa bila kuwa na makanisa ya nyumbani kunakuwa na ugumu wa kutambuana, kuangalia changamoto wanazokutana nazo waamini wetu, kukosa msaada wa karibu anapokuwa mtaani ambako hajui kama kuna wenzake wa karibu wanaishi huko, lakini pia kama mtu ana vipawa na karama ambazo kwa hizo Mungu yu amtumia ni vigumu kutambulika na kutumika bila mfumo wa makanisa ya nyumbani kwa hiyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa kanisa letu kuwa na mfumo huu wa makanisa ya nyumbani, pamoja na faida lukuki zinazoweza kutolewa na kanisa la nyumbani hapa tunaweza kuona faida kadhaa :-

  1. Makanisa ya nyumbani husaidia kukua kiroho – Kanisa la nyumbani linaleta utulivu na nafasi ambayo kila mmoja hutambulika lakini sio hivyo tu mtu anaweza kupata nafasi ya kuuliza maswali, kueleza  changamoto anazokuta anazo na kupata mtenda kazi wa karibu na eneo lake ambaye anaweza kumsaidia katika kujifunza na kukua kiroho kwa hiyo kanisa la nyumbani ni njia bora zaidi ya kuangaliana sisi kwa sisi katika mazingira yote

 

Waebrania 10:24-25 “tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia

 

  1. Makanisa ya nyumbani yanatoa huduma ya ushirika wa kweli – hakuna mahali ambapo watu watafahamiana kwa ukaribu kama katika ushirika wa makanisa ya nyumbani, watabebeana mizigo kama makanisa ya nyumbani, watashirikiana katika shida na furaha kama kanisa la nyumbani kwa ujumla ule upendo wa kweli katika Kristo tunaweza kuonyeshana  kwa uhalisia katika makanisa ya nyumbani, wakati kanisa kubwa linainua hisia zetu ni kanisa la nyumbani ndilo linaloleta mapinduzi makubwa ya kiroho, na kiushirika.

 

Matendo 2:41-42 “Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani yanahusika kwa ukaribu na huduma ya kichungaji – kama mshirika anapitia changamoto za aina mbalimbali mchungaji kiongozi hawezi kujua bila taarifa za wale walio karibu naye ikiwa ni pamoja na kiongozi wa kanisa la nyumbani ambaye ni mtenda kazi pamoja na Mchungaji wetu, Kanisa la nyumbani ni rahisi kumtambua kila mtu, ni rahisi kutambua mtu anayepitia changamoto ni rahisi kumuombea mtu ni rahisi kujua mtu anaye lega lega katika Imani na ni sehemu ambayo hakuna mtu anasahaulika wala kupotea  na ni rahisi kufuatiliwa  na kurejezwa katika Imani

 

Wagalatia 6:1-2 “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya uinjilisti rahisi – Ni vigumu wakati mwingine kumualika mtu katika kanisa mama na akakubali hasa kama hajawahi kuingia katika makanisa ya watu wanaohubiri wokovu, lakini ni rahisi mtu kualikika katika makanisa ya nyumbani anajisikia salama maana ni sebule ya mtu na ni kwa watu anaowajua, ni rahisi kualika majirani, na wakafika hawaogopi kuliko inavyokuwa katika majengo ya makanisa makubwa na kwa njia hiyo ni rahisi kumuhubiri injili na pia kutoa mwaliko wa kuja katika kanisa kubwa huduma za kiroho zaidi.

 

Matendo 5:42 “Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.”

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya kulea viongozi – wakati mwingine kutokana na programu ambazo zinaendelea katika kanisa kubwa kuna uwezekano wa kushindwa kuwapa watu wengine madhabahu, au kupatikana kwa uhaba, lakini makanisa ya nyumbani kwa sababu ni kundi dogo linaweza kumshirikisha kila mtu na zaidi ya yote viongozi wetu waliopata nafasi ya kupitia shule mbalimbali ya  za kihuduma wanapata nafasi ya kuhudumu na kuombea watu na kuchunga kanisa dogo na kulikuza jambo ambalo linaweza kuwarahisishia uanzishaji wa makanisa wanapokuwa wameitwa katika wito maalumu, Ni katika kanisa la nyumbani viongozi hujifunza kivitendo, karama zinagunduliwa, wachungaji wajao wanabainika, walimu wazuri wanabainika, wainjilisti wazuri wanabainika na watendakazi wapya wanabainika

 

2Timotheo 2:1-2 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu. Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya kupanuka kwa kanisa – Kanisa hutawanyika kwa haraka kutokana na kuweko kwa makanisa ya nyumbani kama eneo la kanisa kubwa liko mbali sana na sehemu fulani ni kupitia makanisa ya nyumbani tunaweza kuanzisha tawi lingine bila kuhitaji gharama kubwa za kukodisha jengo, aidha makanisa ya nyumbani hayawezi kuzuiliwa na mateso au upinzani, katika nchi nyingi ambazo injili inapingwa makanisa ya nyumbani imekuwa ni njia ya siri ya kulifanya kanisa kuendelea mbele. Makanisa ya nyumbani yametumiwa na watumishi wengi wa Mungu katika huduma zao na kusababisha ukuaji na upoanukaji mkubwa wa kanisa mama hivyo makanisa haya ni nyenzo ya ukuaji wa Kanisa kubwa kiroho, kiidadi, kijiografia na kadhalika  

 

Matendo 6:5-7 “Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia; ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao. Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.”

 

Matendo 8:1-4 “Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu. Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani. Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.”

 

-          Kanisa la The Church of Pentecost huko Ghana – ni moja ya kanisa kubwa sana miongoni mwa madhehebu ya kipentekoste wana mfumo wa makanisa ya nyumbani “cell system” zaidi ya maelfu  na kutokana na watendakazi kuyasimamia makanisa hayo kwa uaminifu kanisa limeweza kuwa na washirika karibu milioni tatu na likatumia makanisa ya nyumbani kuzalisha makanisa 99 katika nchi nyingine na sehemu mbalimbali za Afrika magharibi

 

-          Kanisa la The works and Mission Baptiost Church – Ni moja ya makanisa makubwa sana nchini Ivory Coast kanisa hili linaongozwa na Askofu Dion Robert kanisa lake lina mfumi wa makanisa ya nyumbani  ambayo yamesababisha mfumuko mkubwa wa ukuaji wa kanisa  kanisa lina cell Groups makanisa ya nyumbani 18,000,. 14,000 ya watu wazima na 4,000 ya watoto kupitia mfumo huo kanisa la Bishop Dion sasa lina washirika 150,000 katika ibada moja wakutanano kuabudu

 

-          Christian Rivival Church – Ni kanisa kubwa na linalokua kwa kasi lililoko Afrika ya kusinikanisa hili mlina mfumo wa makanisa ya nyumbani yanayounganisha watu  na majirani, kanisa hili lina maelfu ya makanisa ya nyumbani na linaongezeka kwa kasi

 

-          Lighthouse Chapel International – Ni kanisa kubwa linaoongezeka kwa kazi lina wanafunzi wanaohusika kusimamia makanisa ya nyumbani likitumia mfumo ule ule uliokuwa unatumiwa na mitume nyakati za kanisa la kwanza

 

-          Living Faith Church Woldwide (Winners Chapel, Nigeria) – ni Kanisa lenye watu 50,000 wanaoabudu mahali pamoja pale kwenye makao makuu yao wao wanatumia mfumo wa makanisa ya nyumbani yanayosimamiwa na watenda kazi, kanisa hili kwa sasa lina waamini zaidi ya milioni sita duniani

 

-          Deeper life Bible church Nigeria  - lina waamini wapoatao 65,000 wanaoabudu katika ibada moja, lakini siri mojawapo ya mafanikio yao ni mfumo wa makanisa ya nyumbani yenye viongozi mahiri na walimaanisha

 

-          Full Gospel Bible Fellowship -  Ni moja ya Kanisa la kipekee la kipentekoste lililoanzishwa nchini Tanzania na Askofu Mkuu Zakaria Kakobe, ukiacha makanisa haya kuenea nchi nzima kanisa kuu lililoko Sam Nunjoma pale Mwenge Dar es Salaam linaundwa na makanisa ya nyumbani zaidi ya 600 yaliyoenea kila mahali katika mji wa Dar es Salaam, viongozi wa makanisa ya nyumbani wana mafundisho maalumu ambayo huyatoa kwa pamoja kila mahali katika mtaa husika na viongzi hao wenye utii wa hali ya juu hutoa taarifa ya kazi wanayoifanya kwa viongozi wao na kwa mchungaji kiongozi, Makanisa hayo ya meunda umoja imara na kulifanya kanisa kuu kuwa imara, aidha zinapofungishwa ndoa kwa wingi makanisa hayo hujishughulisha au kuhusika kwa kiwango Fulani katika usimamizi wa wanandoa hao kuanzia safari zao za uchumba  na kadhalika, makanisa haya pia huusika na matukio ya misiba mazishi na mengineyo

 

Kama tunataka makanisa yetu yakue na kuwa na washirika wengi sana basi ni nashauri tujiandae na mfumo huu maalumu utakaosaidia kufikisha huduma kwa ufasaha katika jamii, na kulifanya kanisa kuwa nyenzo rahisi na inayoweza kuwafikia watu kwa njia nyepesi, tusikusanye sadaka yoyote katika makanisa ya nyumbani, hii itasaidia kuwaondolea kongwa washirika lakini pia itakuokoa na majaribu ya kifedha kama kiongozi wa makanisa ya nyumbani kutokuwa na muda wa kutoa hesabu ya mapato na matumizi, makanisa ya nyumbani yaanzishwe kwa kusudi la kufikisha huduma karibu na watu na sio kwaajili ya kukusanya mapato, washirika wote wa makanisa ya nyumbani watatoa sadaka zao katika kanisa kuu lililoko katika mji husika, makanisa ya nyumbani msisitizo wake ni wa kifamilia kuifanya familia ya Kikristo kuishi pamoja na kushirikiana na kubebeana mizigo, makanisa ya nyumbani pia ni makanisa ya Mungu, kusudi kuu ni kuabudu na kujifunza neno la Mungu  na kutiana moyo, Ni muhimu makanisa haya yakaendeshwa kwa kanuni za kimaandiko na yakatambua viongozi wao na kuwaheshimu, Makanisa ya nyumbani ni kielelezo na nuru katika mitaa yetu kuendelea kumuhubiri Kristo kivitendo na kuuishi kwa upendo kama Mungu alivyotuamuru  

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima 

Jumapili, 2 Agosti 2026

Wito wa kumtumikia Mungu katika huduma!


Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu anatoa wito kwa watu wake wote kuhakikisha ya kuwa wanamtumikia, Neno wito linamaanisha kualikwa na Mungu ili tuweze kutekeleza ajenda zake au kusudi lake ambalo amelikusudia yeye mwenyewe sawasawa na maagizo yaliyomo katika neno lake, Mungu huchagua watu wake wale anaowataka mwenyewe na kuwaalika wawe na ushirika naye na kisha awatume katika kazi yake ili kutekeleza mapenzi yake, kusudi lake na kazi yake hapa duniani na kwa sababu hiyo kuitikia wito wa kumtumikia Mungu ni utii usio na mashart

Marko 3:13-15 “Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri ya kutoa pepo.”

Kwa hiyo tangu nyakati za agano la kale Mungu amekuwa na tabia ya kuwaita na kuwachagua watu aliowataka mwenyewe kwaajili ya kutekeleza majukumu na makusudi yake yeye mwenyewe duniani, Kwa msingi huo kila mtu aliyeokoka anapaswa kuwa makini kumtumikia Mungu na kusikiliza sauti ya Mungu ili kutambua mapenzi ya Mungu katika maisha yake na kuwajibika mara moja katika kazi hii yenye Baraka na heshima kubwa, kwa bahati mbaya watu wengi sana hawapendi kumtumikia Mungu katika huduma mbalimbali Kanisani kwa kisingizio kuwa hawajaitwa, au kwa kutokuwa na ufahamu wanawajibika vipi, kwa hiyo leo tutachukua Muda kujifunza na kutafakari kwa pamoja somo hili muhimu kuhusu wito wa kumtumikia Mungu katika huduma kwa kuzingatia vipengele vikuu vitatu vifuatavyo:-


·         Maana ya neno wito katika maandiko.

·         Aina kuu tatu za wito katika huduma.

·         Jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma.


Maana ya neno wito katika maandiko.

Ni muhimu kufahamu kuwa neno wito katika maandiko lina tajwa kwa lugha ya Kiebrania kwa neno “qara” na linatajwa kwa kiyunani kama neno “Kaleō” au “klēsis” ikimaanisha kuitwa, kutengwa, kuchaguliwa au kuteuliwa na Mungu kwa kusudi la kutimiza majukumu maalumu katika ajenda za Mungu, Kwa sababu hiyo wito sio mpango wala wazo la kibinadamu au shauku binafsi bali ni mpango kamili wa Mungu juu ya maisha ya mtu katika kusudi lake au kwa kazi maalumu, kwa hiyo wito katika huduma ni mualiko wa kumtumikia Mungu au kufanya kazi pamoja na Mungu katika kutimiza kusudi lake au ajenda zake mwenyewe hapa duniani kwa wakati maalumu.

Luka 5:27-29 “Baada ya hayo akatoka, akaona mtoza ushuru, jina lake Lawi, ameketi forodhani, akamwambia, Nifuate. Akaacha vyote, akaondoka, akamfuata. Na Lawi akamfanyia karamu kubwa nyumbani mwake; palikuwa na mkutano mkuu wa watoza ushuru na watu wengineo waliokuwa wameketi chakulani pamoja nao.”

Msingi mkuu wa Mungu anapomuita mtu kwanza anataka ushirika wa karibu na mtu huyo kisha ndipo amtume, kwa hiyo mtu aliyeitwa na aliyeitikia wito wa kumtumikia Mungu katika huduma anapaswa kuwa mtu mwenye ushirika wa karibu na Mungu, ushirika huu ni wa muhimu hata kabla ya kazi yenyewe

Yohana 21:15-17 “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.”

Marko 3:13-15 “Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri ya kutoa pepo.”

Kabla Mungu hajamuita mtu anataka ushirika na wewe anataka upendo wako na anataka uwe pamoja naye kisha ndipo akutume kuhubiri na kutoa pepo au kufanya huduma nyinginezo kwa niaba yake            

Aina kuu tatu za wito katika huduma.

Maandiko matakatifu yanaonyesha kuwa Mungu aliwaita watu kwa namna mbalimbali na kwaajili ya shughuli mbalimbali, kwa hiyo tunapozungumzia swala la wito tunazungumzia mada pana sana katika nyanja zote za kisiasa, kijamii na kiimani, na kisayansi, ukichunguza kwa kina utaweza kuona kuwa kote huko Mungu hufanya kazi ya kuwaita watu kwaajili ya makusudi mbalimbali, kwa hiyo wito hauko katika kuta za kanisa pekee unavuka mipaka na kwenda mbali zaidi ya vile tunavyofikiri, hata hivyo katika somo hili nataka kuzungumzia wito ambao unaishia ndani ya mipaka ya Kanisa pekee aina hizi za wito naweza kugawa katika makundi makuu muhimu matatu yafuatayo:-

·         Wito wa jumla katika wokovu

·         Wito wa jumla katika huduma

·         Wito maalumu katika huduma

Wito wa jumla katika wokovu – Wito huu wa ujumla katika wokovu ni wito unaotolewa na Mungu Roho Mtakatifu kwa jamii ya watu wote duniani ili wamuamini Bwana wetu Yesu Kristo kama mwokozi wao na kupokea uzima wa milele, huu ni wito unaotolewa kwa watu wote wamgeukie Mungu wamrudie yeye wamche yeye na kuwa na ushirika na yeye kwa hiyo watu wote duniani wanaalikwa kila iitwapo leo kupokea wito huu wa wokovu kwa imani.

Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.”

Mathayo 11:28-30 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Warumi 8:28-30 “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.”

Wito katika wokovu ni mwaliko wa jumla kwa jamii ya watu wote duniani wa kila kabila, na kila taifa na kila tamaduni na lugha na imani, wote wanapewa mwaliko wa kumpokea Yesu Kama Bwana na mwokozi wa maisha yao baada ya kuisikia injili na kuiamini na wote wanaopokea mwito huu kwa hiyari yao bila kulazimishwa wanafanyika kuwa watoto wa Mungu

Yohana 1:12-13 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”

Wito huu pamoja na mambo mengine pia unajumuisha kuishi maisha matakatifu na kuwa na ushirika na Mungu kumfanania Yesu Kristo na kuwa na tabia au mwenendo mwema kama yeye aliyetuita alivyo kwa hiyo kila aliyeokoka anawajibu wa kuukulia wokovu, kukomaa na kuwa kama Yesu Kristo mwenyewe alivyokua, wito huu ni wa toba, ni wito wa utakatifu, ni wito wa kupumzishwa na kusamehewa dhambi na kurudishwa katika familia ya Mungu na kuwa na uhusiano naye na kumuabudu

1Petro 1:14-16 “Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu; bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”

Wito wa jumla katika huduma.

Wakati msingi wa wito wa kwanza ni kutengeneza mahusiano yetu na Mungu, mojawapo ya majukumu yetu vile vile ni kumtumikia Mungu, kila mtu aliyeokoka ameitwa kumtumikia Mungu kwa hivyo wote tuliookolewa pia tuna wajibu wa kumtumikia Mungu katika majukumu mbalimbali katika mwili wa Kristo, wito huu ni wito wa jumla kwa watu waliookoka unaowekwa na Roho Mtakatifu ndani yetu na kutubebesha majukumu ya jumla katika kuonyesha upendo kwa wengine, kumtii Mungu, kumuabudu na kuwashirikisha wengine imani yetu, wito huu unamuhusu kila mtu katika kanisa na sio viongozi au wachungaji peke yao wito huu unaonekana tangu nyakati za agano la kale.

Kumbukumbu 10:12-13 “Na sasa, Israeli, Bwana, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche Bwana, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote; kuzishika amri za Bwana na sheria zake, ninazokuamuru leo, upate uheri?

Zaburi 100:1-3 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.”

Warumi 12:6-11 “Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha. Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema. Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu; kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”

Mathayo 28:18-20 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.”

Unaona maandiko yana maagizo mengi ambapo kila mtu aliyeokolewa amepewa wajibu na anaagizwa kutumika, kila mtu aliyeokoka anaagizwa kuihubiri injili, anaagizwa kuomba anaagizwa kutoa anaagizwa kuwatumikia wengine anaagizwa kufungua na kupanda makanisa anaagizwa kufanya huduma zote, pamoja na mambo mengine tofauti ni kuwa watu hawa waliookolewa walioitwa katika wito wa ujumla watafanya kazi zao za kawaida huku wakifanya kazi za huduma kwa mujibu wa ratiba za maisha yao, na ratiba za kikanisa za kutumika kila iitwapo leo, aina hii ya wito ni wito wa ujumla katika wokovu ambapo waamini wanaagizwa kutumia vipawa vyao kumtumikia Mungu kwa  kadiri ya neema, wito huu unajumuisha kumuwakilisha Mungu popote tulipo pia iwe ni nyumbani au kazini au shuleni wewe ni wakili wa Yesu Kristo na unatumika pale ulipo kama chumvi na kama nuru.

Wito maalumu katika huduma

Wito huu au aina hii ya wito hutolewa kwa uwezo wa Roho Myakatifu kwa waamini kumuwezesha mtu huyo kusikia sauti ya Mungu kwa njia mbalimbali na kuamua kucha kila kitu hata kazi kwa kusudi la kumtumikia Mungu moja kwa moja katika kazi yake akiwa na huduma ya aidha mtume, au nabii, au mwinjilisti au mchungaji na au mwalimu aina hii pia ya huduma huwa inaambatana na huduma za kimaongozi katika kanisa na wakati mwingine karama mbalimbali za Roho Mtakatifu kuwawezesha watu hao kuuhudumia mwili wa Kristo kwa kuujenga na kuukamilisha

Waefeso 4:11-13 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”

Jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma.

Linapokuja swala la wito maalumu katika huduma watu wengi sana huwa wanajiuliza nitajuaje kama nina wito, tunapojifunza kipengele hiki kinachozungumzia jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma tutapata ufahamu namna na jinsi Mungu anavyosema nasi kuhususiana na wito wetu kujifunza kuhusu swala hili kutatusaidia kutembea kwa uhakika katika huduma tukiwa na uhakika kuwa hatukubahatisha katika swala zima la kumtumikia Mungu katika kazi hii maalumu, Neno la Mungu linaainisha njia mbalimbali ambazo Mungu alizitumia kuwaita watu wake katika wito maalumu

1.       Mungu anaweza kumuita mtu kwa sauti yake moja kwa moja  - wakati mwingine Mungu huwaita watumishi wake moja kwa moja kwa sauti yake katika mifumo anayoijua yeye mwenyewe  watumishi wa Mungu kama Musa, Samuel na Paulo waliitwa moja kwa moja katika huduma kwa kuisikia sauti ya Bwana  wazi wazi moja ona

 

Kutoka 3:1-10 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. Malaika wa BWANA akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. BWANA alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”

 

1Samuel 3:1-10 “Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri. Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu; basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa. Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena. Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto. Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.”

 

Matendo 9:1-6 “Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu. Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”

 

2.       Mungu anaweza kuita watumishi wake kupitia maono – Maandiko yanaonyesha kuwa kwa njia ya maono pia Mungu anaweza kumuita mtu katika kazi yake maalumu na ikawa na ufanisi mkubwa, Nabii Isaya alipokea wito wake kupitia Maono na Mungu alimtumia kwa kiwango kikubwa sana  

 

Isaya 6:1-10. “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa. Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi. Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione. Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.

 

3.       Mungu anaweza kuita watumishi wake kupitia ndoto – Mungu hutumia ndoto pia kufunua kusudu lake, mpango wake na agenda zake wito maalumu wa Yusufu ulifunuliwa kupitia ndoto mapema sana katika maisha yake tangu akiwa mdogo kuwa Mungu angemtumia, kupitia hili tunaweza kujifunza hapa na kutambua ya kuwa Mungu ameita baadhi ya watu wake kumtumikia kwa kutumia njia anazoona kuwa inafaa ikiwa ni pamoja na ndoto, Mungu anatumia njia ambayo muhusika ataelewa kwa urahisi au njia hiyo inaeleweka kwa mtu huyo.

 

Mwanzo 37:5-11 “Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia; akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota. Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu. Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake. Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia. Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi? Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.”

 

4.       Mungu huweza kuita watumishi wake kupitia mtumishi wake au nabii – Wako watu kadhaa katika maandiko ambao waliitwa katika kazi maalumu kupitia manabii, Nabii alifunuliwa na kumtia mafuta yule aliyekusudiwa katika wito fulani, kwa mfano ufalme wa Sauli, au ufalme wa Daudi,  au  nabii Elisha hawa waliitwa kupitia nabii au mtumishi wa Mungu aliyekuwako wakati huo, wao kupitia ujuzi na sauti ya Roho Mtakatifu wanaweza kumjua na kumbaini mtu ambaye Mungu amemuita katika huduma  na akafaa kwaajili ya utumishi huo uliokusudiwa!

 

1Samuel 9:15-20 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema, Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia. Hata Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia habari zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu. Ndipo Sauli akamkaribia Samweli langoni, akasema, Tafadhali, uniambie, nyumba ya mwonaji iko wapi? Samweli akamjibu Sauli, akasema, Mimi ndimi mwonaji; tangulia mbele yangu ukwee mpaka mahali pa juu, kwa maana mtakula pamoja nami leo; kisha, asubuhi nitakuacha uende zako, nami nitakuambia yote uliyo nayo moyoni mwako. Na wale punda zako waliopotea siku hizi tatu, usijiudhi kwa ajili yao; maana wameonekana. Na yote yaliyotamanika katika Israeli amewekewa nani? Si wewe, na nyumba yote ya baba yako?

 

1Samuel 16:13 “Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.”  

 

1Wafalme 19:19-21 “Basi, akaondoka huko, akamkuta Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akilima, mwenye jozi za ng'ombe kumi na mbili mbele yake, na yeye mwenyewe alikuwa pamoja na lile la kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akatupa vazi lake juu yake. Naye akawaacha ng'ombe, akamfuata Eliya mbio, akasema, Nipe ruhusa, nakuomba, nimbusu baba yangu na mama yangu, kisha mimi nitakufuata. Akamwambia, Enenda, urudi; ni nini niliyokutendea? Akarudi akiacha kumfuata, akatwaa lile jozi la ng'ombe, akawachinja, akatokosa nyama zao kwa ile miti ya ng'ombe, akawapa watu, wakala. Kisha akainuka, akamfuata Eliya, akamhudumia.”

 

5.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake kupitia malaika – Wakati mwingine Mungu humtuma malaika wake kuweza kuwasilisha ujumbe wa jukumu lake kwa mtumishi wake anayekusudiwa, Katika maandikio iko mifano mingi lakini tutaangalia mifano michache ya watu kadhaa kama Gideoni na Mariam mama yake Yesu ambao walipewa kazi maalumu kwa ujumbe wa malaika

 

Waamuzi 6:11-14 “Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani. Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma? 

 

Luka 1:26-33 “Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.”

 

6.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake kupitia Roho wake Mtakatifu – Ikumbukwe kuwa njia zote hizo Roho Mtakatifu ambaye ndiye Bwana wa mavuno anazitumia katika kuhakikisha kuwa wanapatikana watenda kazi katika mashamba yake lakini hutokea wakati mwingine mwenyewe akazungumza moja kwa moja kwa njia ya unabii na kumuita au kumtaka mtu katika huduma maalumu

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

7.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake Kupitia Yesu Kristo mwenyewe – Wanafunzi wale kumi na wawili walikuwa ni chaguo la Yesu Kristo mwenyewe na aliwaita kama alivyopenda yeye mwenyewe hata sasa Yesu Kristo bado anaita watu wake kama apendavyo kwa njia mbalimbali na wakati mwingine yeye mwenyewe. Hata hivyo ni muhimu kuelewa kuwa katika njia hizo zote hakuna iliyobora zaidi kuliko nyingine kwa sababu zote ni njia ambazo yeye mwenyewe anazitumia kuwapata watu wa kumtumikia katika huduma maalumu, kwa hoyo mtumishi aliyetokewa na Yesu mwenyewe na kuitwa katika wito haimaanishi kuwa anaubora kushinda aliyeitwa kwa njia nyingine, kwani kimaandiko hizo zote ni nnia anazozitumia Mungu kufahamisha watu wake namna anavyowahitaji katika huduma.

 

Mathayo 4:18-19 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi. Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.”

 

Mathayo 9:9. “Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata.”                                    

Kwa hiyo tunajifunza kuwa ni Mungu mwenyewe ndiye anayeita watu wake katika huduma, na kwa sababu hiyo hakuna mtu ajitwaliaye heshima hii, wakati Mungu anapomuita mtu kwaajili ya huduma mtu huyo huwekewa kitu cha ziada na neema ya juu zaidi ili aweze kuwahudumia wengine, Hata hivyo bado hatuwezi kuwaachia hao peke yao walioitwa katika wito maalumu wa huduma kwa sababu kazi ya Mungu ni pana na hivyo wale wote ambao hawatakuwa wameitwa katika wito maalumu wanabaki katika wito wa ujumla wa kumtumikia Mungu na wakifanya kwa uaminifu na utii kazi ya Mungu itasonga mbele na kuwa Baraka kubwa kwa jamii, Unaweza kujua wito wako kupitia neno la Mungu, kupitia maombi, kupitia shuhuda za huduma za watu unao wahudumia, kuthibitishwa na viongozi, na amani ya moyo, wito ni zawadi, wito ni heshima, wito ni kuaminiwa, wito ni wajibu na kwa sababu hiyo kama Mungu amekuweka katika ajenda zake basi wewe ni wa muhimu sana itikia sauti ya Mungu leo ukamtumikie.

Yohana 12:26 “Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.”

Waebrania 3:14-15 “Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho; hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha.”                    

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima