Jumapili, 3 Mei 2026

Ndoa na iheshimiwe na watu wote!


Waebrania 13:4. “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”




Utangulizi:

Leo tutachukua muda kujifunza kwa kina na mapana na marefu undani wa mafundisho ya Biblia kuhusiana na swala la kuheshimu ndoa, tukio ambalo nyakati za leo, limekuwa likichukuliwa si kwa uzito ule ambao Mungu mwenyewe anautoa katika ndoa, Ndoa za siku hizi zimepoteza heshima kuanzia kwa wanandoa wenyewe na mpaka katika jamii inayozizunguka ndoa kutokana na maarifa katika eneo hili kuwa finyu, Agizo la kuheshimiwa kwa ndoa ni agizo zito linalopewa kipaumbele na Mungu, Neno Iheshimiwe katika lugha ya kiyunani yaani Kigiriki(Koine Greek) linasomeka kama neno “timios” likimaanisha kuwa ndoa ni ya thamani sana, ndoa ni ya heshima kubwa sana, ndoa haipaswi kutiwa unajisi, ndoa inatakiwa kuchukuliwa kwa uzito na kwa utukufu wa Mungu, ndoa haipaswi kuchukuliwa kwa wepesi, kwa hiyo hii ina naana ya kuwa Ndoa sio swala la kuchukuliwa kawaida, bali ni swala la kiadilifu na ni takatifu kwa sababu ndoa ilianzishwa na Mungu mwenyewe kama yanenavyo maandiko:-

Mwanzo 2:18-24 “BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. BWANA Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye. BWANA Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, na ule ubavu alioutwaa katika Adamu BWANA Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

Kwa msingi huo swala la kuiheshimu ndoa ni agizo la Mungu kwa watu wote waliomo katika ndoa wenyewe na wale ambao bado hawajaingia katika ndoa, na wanajamii wote wanapaswa kuiheshimu, kuithamini na kuepuka kwa namna yoyote ile kuiharibu na kuipotosha ndoa, Kimsingi Mungu anaonya jamii iache kuichezea ndoa, kuidharau na hata kuiharibu, kwa sababu zozote zile yakiwemo majungu, uchochezi na ushawishi mbaya na usiofaa, au kuitia unajisi. Tutajifunza somo hili Ndoa na iheshimiwe na watu wote kwa kuzingatia vipengele vikuu muhimu vitatu vifatavyo:-


·         Maana ya kuheshimiwa kwa ndoa.

·         Kwa nini kuna ulazima na umuhimu wa kuheshimu ndoa.

·         Ndoa na iheshimiwe na watu wote.


Maana ya kuheshimiwa kwa ndoa.

Ili tuweze kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu agizo la kibiblia kuhusiana na andiko Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi ni muhimu kwetu tukaangalia andiko hili kwanza kutoka katika lugha yake ya asili ya Kiyunani yaani Kigiriki kisha tulifanyie uchambuzi yakinifu, ili tupate maana na msisitizo ulio wazi kutoka kwenye maandiko hayo. Andiko hili linaweza kuwa na tafasiri hii katika lugha ya Kiswahili, Kiyunani na Kiingereza maandiko yanasomeka kama ifuatavyo:-

Kiswahili: Waebrania 13:4. “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”

Kiyunani: (Timios ho gamos en pasin, kai hē koitē amiantos; pornous gar kai monoecious krinei ho Theos)

Kiingereza: (Hebrews 13:4 Marriage should be honoured by all and the marriage bed kept pure, for God will judge the adulterer and all the sexually immoral) NIV.

Neno ho gamous – Neno hilo maana yake ni Ndoa ni Muungano halali unaojumuisha mwanamke na mwanaume unaokubalika na kubarikiwa na Mungu, kwa hiyo Biblia haitambui ndoa za jinsia zinazofanana, kwa hiyo kuheshimu ndoa ni pamoja na kuheshimu jinsia husika, na kuunganisha wana ndoa wenye jinsia zinafananazo au waliobadili jinsia katika maisha yao baada ya kuzaliwa ni kufuru! na ni kuivunjia ndoa heshima yake katika ngazi ya juu sana

Neno hē koitē – Neno hili ambalo maana yake limetajwa kama kitanda cha ndoa au marriage bed Kiyunani linamaanisha tendo la ndoa, yaani tendo halali ambalo limehalalishwa kwa wana ndoa, kwa hiyo usafi unaotajwa hapo sio wa kitanda na Godoro, bali Mwandishi anazungumzia uadilifu wa tendo la ndoa katika agano halali la ndoa, kwa hiyo kuingilia ndoa ya mtu na kuitia unajisi ni kosa kubwa linalomuuzunisha Mungu, na sio hivyo tu kutoka nje ya ndoa nalo ni kosa kubwa kwa Mungu

Mwanzo 39:7-9 “Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami. Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu. Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?

Ayubu 31:9-12 “Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu; Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake. Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu, Nao ungeyang'oa maongeo yangu yote.”  

Neno amiantos – maana yake isiyo na doa, isiyotiwa unajisi, isiyochafuliwa, au isiyosababisha madhara kwa tafasiri ya moja kwa moja ni safi yaani isiyochafuliwa kwa dhambi kwa msingi huo tafasiri ya moja kwa moja ya mstari huu wa msingi maana yake ni kwamba ndoa haipaswi kuwa iliyochafuliwa amiantos kwa kiingereza  “undefiled”, “pure” or “unpolluted” au “harmless”. Isitiwe unajisi wala wewe usijitie unajisi kwa kuingia katika ndoa ya mtu, yaani unaichafua na wewe unachafuka

Walawi 19:20 “Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake. Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye.”

Neno monoeciousmaana yake ni tendo la ndoa linalofanyika nje ya agano la ndoa uzinzi, au kuchanganya mbegu za uzazi baina ya wanandoa, kuingizia mtoto asiye halali, katika ndoa ya mtu mwingine, au kuchanganya viungo vya uzazi vya aina mbili katika kiungo kimoja, kuchangia mke, Katika mimea tendo hili linaitwa “hermaphrodite”,ambalo linatafasiriwa hivi kwa kiingereza Hermaphrodite which means male and female reproductive organs in the same individual msichangine mke au mume,

Neno Porneia – Lina maana tendo la ndoa linalofanyika kabla ya agano la ndoa au kwa kuhusisha tamaa au kumtumia mwenzi wako vibaya uchafu au uasherati.  

“Kwa hiyo Muungano halali wa ndoa uheshimiwe na watu wote na tendo la ndoa kati ya wanandoa lisiwe linalotiwa unajisi kwa sababu wazinzi na waasharati Mungu atawahukumia adhabu”

Kwa msingi huo Mstari huu wa msingi na unaojitegemea unahimiza wana ndoa kujitunza kwa uaminifu katika ndoa, wao wenyewe wakiwa mstari wa mbele kuheshimu makubaliano yote ya ndoa yaani lile agano na kuepuka kwa sababu zozote zile za kuleteana uchafu wa kingono, picha chafu za ngono, tamaa mbaya na udanganyifu, huku wanandoa wakionywa kutokuutumia mwili wa mwenzi wako vibaya au kumtumia vibaya, kuishi kwa kuheshimiana, kutokuzaliana watoto haramu, kusikilizana, kujaliana, kupendana na kuwa na nia moja kiroho, kuepuka kufanya au kusababisha tendo la ndoa lifanyike nje ya mapenzi na makusudi ya Mungu au nje ya agano, huku wana jamii wakiagizwa kuheshimu sana ndoa takatifu, na kutokuiingilia ndoa ya mtu mwingine au kuwa sababu ya ndoa takatifu kuvunjika, kuichukulia ndoa kwa heshima kubwa na kutokuvunja viwango vya uadilifu katika ndoa, kutokuingilia na kuharibu, kuingilia na kuvuruga, kuwachafua wana ndoa na kuwaletea fitina ama sababu zozote zile zitakazopelekea kuachana kwao, hiyana wivu, uchonganishi majungu na maneno ya kuwakatisha tamaa au kuwashauri vibaya.

Kwa nini kuna ulazima na umuhimu wa kuheshimu ndoa.

Ndoa ni lazima iheshimiwe kwa sababu imeanzishwa na Mungu mwenyewe kama agano la kudumu ambalo linatupa picha ya uhusiano wa Kristo na Kanisa, Ndoa ndio msingi wa Familia jamii na taifa lolote lile, Kamwe hakuwezi kuwa na jamii duniani bila kuweko kwa ndoa, Katika ndoa ndiko Mungu anakotarajia watoto wakue katika Imani nidhamu na ustaarabu, huwezi kuwa na jamii bora kama hakuna ndoa zilizo bora, kama jamii haiheshimu ndoa tutajipatia jamii zilizo hovyo sana duniani.

Katika nyakati hizi za sasa kwa mujibu wa tafiti za karibuni imebainika kuwa heshima kwa ndoa imeshuka kwa kiwango kikubwa kwa asilimia sitini na nne 64% kwa tafiti za kati ya mwaka 1970 mpaka 2024 watu wengi sana katika nyakati za leo hawajiheshimu wala hawaheshimu ndoa, kuanzia kwa wananandoa wenyewe na kwa jamii nzima, bila kujali umri, heshima au cheo, hofu kuhusu mke wa mtu au mume wa mtu katika jamii imeshuka na jambo hili liko mpaka katika makanisa ya Mungu, wanandoa wa siku hizi wanagombania kwenye mitandao ya kijamii, wazee wa zamani wakati mwingine waliweza kuhitilafiana na hata kuachana na jamii isijue siku hizi kuachana ni matangazo, ni fahari na imefikia hatua hata sasa zimekuwepo sherehe za kuadhimisha talaka, mlipendana wenyewe huko sirini mkaona wenyewe huko mitandaoni mnaenda kuanikana na kupata maoni ya watu wapuuzi wa dunia hii ili iweje? 

Ni kwa nini Jamii inapaswa kuheshimu ndoa kama agizo la kibiblia linavyosema hapa ziko sababu kadhaa

1.       Ndoa ni mpango wa Mungu -  Wazo la ndoa kamwe sio la kibinadamu, Ni Mungu ndiye aliyeanzisha ndoa na Ndoa inaonekana mwanzo kabisa wa uumbaji wa Mungu,  katika agano la kale huu ulikuwa ni mpango halali na kamili wa Mungu katika kuanzisha jamii yenye uadilifu kuelekea kwake kwa hiyo halikuwa wazo la Mwanadamu

Mathayo 19:4-6 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.”

Kwa maelezo hayo ya Bwana wetu Yesu Kristo na hitimisho lake Alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe maana yake Mungu anapowakutanisha watu na wakafanikiwa kuoana hawana sababu wala hakuna sababu zinazokubalika kwa wao kuachana mpaka Mungu mwenyewe atakapoamua kumchukua mmoja nyumbani, maana yake ni kuwa Ndoa imeanzishwa na Mungu na inatoka kwa Mungu  na hakuna mwanadamu aliye na kibali cha kuimaliza au kuiachanisha, hili linatakiwa kufahamika hivyo kwa wanandoa wenyewe na wana jamii, unapoingilia mke wa mtu au mume wa mtu maana yake wewe utakuwa na adhabu kubwa sana kwa Mungu na laana kwa sababu unataka kuwa sababu ya watu kutengana, au unaweza kusababisha watu kuachana,kufarakana, Yesu anatufundisha hapa kuwa hata talaka sio mpango wa Mungu iwe watu hao waliooana wameokoka au hawajaokoka Mungu anatambua muungano huo na ameufanya.

2.       Ndoa ni eneo la kukua kiroho na kiadilifu – Mungu ameikusudia ndoa kutokuwa swala la uhusiano pekee bali eneo la ukuaji wa kiroho na maadil na uvumilivui, Ndoa ni njia ya kukua na kumfikia Mungu kwa hiyo mojawapo ya sehemu ya ukuaji wa kiroho na kimaadili ni pamoja na kujenga uhusiano wa karibu kati ya wanandoa na hivyo kusababisha ukaribu na Mungu, ndoa zenye msingi imara wa kiroho na uadilifu zinatengeneza jamii yenye uadilifu na uhusiano mzuri na Mungu, Adam na Hawa walipokosea katika maswala ya kiroho na uadilifu uzao wote wa mwanamke ulipata changamoto zinazoathiri jamii mpaka leo.

Mwanzo 3:1-6 “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani? Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.”

3.       Ndoa imewekwa kwa kusudi la kuzuia zinaa – Mojawapo ya sababu za kibiblia ya kuwapo kwa ndoa ni kwaajili ya kuzuia zinaa, na Paulo mtume analizungungumzia hili kwa uwazi kwamba ndoa imewekwa kwaajili ya kuzuia uzinzi na uchafu kwa sababu hiyo sababu zozote zile zinazopelekea uchafu ufanyike na zinaa ifanyike Mungu atahukumu, na ndio maana wana ndoa wanapaswa kuhakikisha amani inakuwepo, na shetani hapati nafasi ya kuharibu ndoa, katika namna ya kushanganza sana nyakati za leo hata pamoja na maandiko kuonya wanandoa wamekuwa wakikomoana kwa kunyimana na kutokuridhishana na kupelekea shetani kupata nafasi ya kuharibu ndoa hii ni namna nyingine pia ya kutokuheshimu ndoa.

 

1Wakoritho 7:2-5 “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.”

 

4.        Ndoa ndio eneo la kwanza la mahusiano na upendo -   Mungu alikusudia ndoa iwe eneo la kwanza la mahusiano na upendo, Mwanadamu ni kiumbe cha kijamii, moja ya changamoto iliyoonekana kabla ya anguko la mwanadamu ilikuwa sio vema mtu huyu awe peke yake kwa hiyo Mungu alitaka awepo mtu mwenye kumfaa Adamu na kutoa huduma ya ushirika na kuanzisha jamii, Uhusiano huu wa ndoa unaruhusu wanandoa kukua katika uhusiano na upendo na imani kwa pamoja kuingilia ndoa ya watu ni kuharibu mpango huu wa upendo wa Mungu na ustawi wa ndoa hizo na kuleta vurugu katika jamii, ndoa iheshimiwe, kuingilia mahusiano ya wengine ni wizi, unaingia kuiba upendo usiokuwa wako, jenga wako acha kuharibu wa wengine, heshimu wako wacha kuharibu wa watu wengine  

Mwanzo 2:18. “BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Waefeso 5:22-33 “Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.”

5.       Ndoa ni agano takatifu – Ndoa sio tu ushirika wa kawaida wa kijamii ni agano, Ni agano takatifu linaloapwa au linalomuhusisha Mungu, likiwa limekusudiwa kuwa agano la kudumu na lisilovunjika, kuharibu ndoa kwa sababu zozote zile ikiwepo swala la zinaa na uasherati au talaka, linamleta Mungu katika kuingilia na kuhukumu kwa sababu ya kupuuziwa kwa agano lake, Agano ambalo Mungu ni shahidi

Malaki 2:13-16 “Tena mnatenda haya nayo; mnaifunikiza madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kulia na kwa kuugua, hata asiiangalie tena hiyo dhabihu, wala kuitakabali mikononi mwenu na kuiridhia. Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.”                      

6.       Kwa sababu Mungu atahukumu wasioheshimu ndoa – Neno la Mungu katika msingi wa andiko tunalojifunza katika somo hili limetoa onyo kali kwa kosa lolote lile litakalohusika katika kuharibu ndoa, Mungu anaona na atahukumu kama alivyosema kwa hiyo hata kama jamii itapotoka na ikapuuzia mpango huu wa Mungu, Mungu mwenyewe atahukumu vikali Katika amri zake za uadilifu ziko amri mbili ambazo zimewekwa na Mungu kwa kusudi la kuilinda ndoa ndani ya zile amri kumi za uadilifu. Kutoka 20:14. “Usizini.”

Kutoka 20:17 “Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.”

Waebrania 13:4. “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”

Jamii inapaswa kukumbuka kuwa ndoa ni muungano wa Mke na Mume uliowekwa na Mungu, Ndoa ni mali ya wenye ndoa, watu wanapaswa kuiheshimu na kuiogopa ndoa, miaka ya zamani jamii ilikuwa inaogopa sana kusikia mke wa mtu au mume wa mtu anatoka nje ya ndoa yake, miaka ya siku hizi watu wanajionea fahari kutoka nje ya ndoa, upofu wa kijamii umeingia na hawaoni tena uzito wa dhambi ya zinaa, agano la ndoa halijaliwi, hakuna heshima, kwa ndoa nyakati za leo na labda kanisa pia limeacha wajibu wake wa kufundisha na kuonya, Bwana atupe neema kutubu na kukaa katika mstari ulionyooka ambao umekusudiwa na Mungu kwaajili ya ndoa, vijana kwa wazee katika jamii wafundishwe na kuelekezwa kuwa jambo hili litaumiza wengi na kuondoa Baraka za Mungu katika maisha yao endapo watachukulia ndoa kama jambo jepesi na la kawaida na kuzivunjia ndoa heshima.

Ndoa na iheshimiwe na watu wote.

Waebrania 13:4. “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”

Maandiko yanapoagiza swala zima la kuiheshimu ndoa, yanaagiza kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote, neno watu wote katika Biblia ya kiyunani linasomeka kama neno “Pántōn”  ikimaanisha kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote bila kumtenga yeyoye, hii maana yake wanaopaswa kuiheshimu ndoa ni wana jamii wote ambao kimsingi tunaweza kuwaelezea katika makundi kama sita hivi, yaani wanandoa wenyewe, wasio na ndoa, wazazi wa wana ndoa, Jamii kwa ujumla yaani majirani marafiki na watu wote katika jamii wakiwemo viongozi wa mila na desturi, Kanisa na viongozi wa kiroho, na mifumo yote ya Serikali na utawala wa nchi, makundi hayo yote yanajumuishwa katika agizo la kuiheshimu ndoa kila kundi kwa jinsi yake na kwa namna yake kama neno la Mungu linavyoagiza.

1.       Wanandoa wenyewe – Katika agizo la kuiheshimu ndoa kundi la kwanza kabisa linalopaswa kuiheshimu Ndoa ni wana ndoa wenyewe, ni lazima kila mwanadamu mwanamke na mwanamume wanaoingia kwenye ndoa wawe na ufahamu wa kutosha na akili ya kutosha na ujuzi wa kutosha na hekima ya kutosha kuelewa kuhusu ndoa, ndoa ni nini na kwa nini wameacha wazazi wao na kuanza jumuia mpya ndani yake kuna wajibu gani na ni namna gani wanapaswa kuiheshimu sana ndoa, Kabla hujataka watu wengine waiheshimu ndoa yako kwanza wewe mwenyewe uliyeko kwenye ndoa ni lazima uwe unaiheshimu na kujiheshimu, ziko kanuni zinazoiongoza ndoa na kama wana ndoa wenyewe watakuwa wapumbavu na kutokuziheshimu na kujiheshimu ndoa hiyo itashambuliwa na shetani na kuwa na wavamizi

a.       Lazima wanandoa watoshelezane – Moja ya jambo kubwa na la muhimu linalowaunganisha wana ndoa ni tendo lenyewe la ndoa, tendo hili likifanyika kwa ubora na kwa utoshelevu linaleta amani na utulivu na kuleta utoshelevu, tafiti ziko wazi kuwa changamoto zote au nyingi zinazopelekea kuwako kwa migogoro ya ndoa zimebainisha kuwa ni tendo la Ndoa lenyewe kutokufanyika kwa utoshelevu au wanandoa kutokutoshelezana, wana ndoa wengi hawatoshelezani katika tendo la ndoa, na wengi hawana muda hata wa kufanya maandalizi na wala hawafurahii jambo hili linapelekea mmomonyoko wa uadilifu na kushuka kwa heshima ya ndoa, wanawake kwa wanaume wanapaswa kuhakikisha kuwa wanatoshelezana.  

Wimbo uliobora 5:15-19 “Unywe maji ya birika lako mwenyewe, Na maji yenye kububujika katika kisima chako. Je! Chemchemi zako zitawanyike mbali, Na mito ya maji katika njia kuu? Yawe yako mwenyewe peke yako, Wala si ya wageni pamoja nawe. Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako. Ni ayala apendaye na paa apendezaye; Maziwa yake yakutoshe sikuzote; Na kwa upendo wake ushangilie daima.”

b.      Wananandoa hawapaswi kunyimana – Ndoa inapoteza heshima yake sio tu kwa sababu ya kutokutoshelezana lakini pia kwa sababu ya kunyimana, na changamoto hii katika tafiti za ndoa hujitokeza hasa kwa wanawake na baadae wanaume hujibu mapigo kwa kunyimana ni jambo la kusikitisha na kufedhehesha kuwa hata wanawake waliookoka na kupata mafundisho mara kwa mara bado pia huwa wanampa ibilisi nafasi na kuharibu ndoa zao kwa sababu ya tabia endelevu za kunyimana na kutopeana haki ya ndoa bila sababu za msingi, mioyo ya wanaume wengi sana imeumizwa na matukio ya aina hii ambayo kimsingi ni hujuma iliyo wazi kwa ndoa nadhani ni mwanamke mpumbavu tu ndiye anayeweza kumnyima mumewe kinyume na maandiko na kwa kufanya hivyo huyo anakuwa ndio wa kwanza kulivunja agano. Aidha ni marufuku kwa wanandoa kuuziana tendo la ndoa yaani kulitumia tendo hilo kamammadai kuwa usiponifanyia hiki hutapata hii, jambo hili la kuifanyia ndoa biashara ni kosa kama kosa la kunyimana

1Wakorintho 7:3-5 “Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.”

c.       Wanandoa wenyewe hawapaswi kutendeana mambo ya hiyana – Maandiko yanawaonya wana ndoa kuokutendeana  mambo ya hiyana, kimsingi mambo ya hiyana ni maswala yote ambayo Mungu anachukizwa nayo kwani yanatikisa na kuharibu misingi ya ndoa, na kuharibu uhusiano, kimsingi kama wana ndoa wanaheshimu Ndoa basi hawapaswi kutendeana mambo hayo ambayo nabii Malaki anayatilia mkazo katika agizo la kiungu.

Malaki 2:13-16 “Tena mnatenda haya nayo; mnaifunikiza madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kulia na kwa kuugua, hata asiiangalie tena hiyo dhabihu, wala kuitakabali mikononi mwenu na kuiridhia. Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.”

Mambo ya hiyana ambayo tunaweza kuyabainisha ambayo wana ndoa wasioheshimiana huyafanya au huweza kuyafanya na yakazuia maombi yao na ibada zao ni pamoja na kukoseana adabu au heshima, wanandoa wanapaswa kuheshimiana, na kutengeneza mazingira ya kujenga upendo na ushirikiano, lakini wakiwa wanafarakana na kugombana kukoseana heshima jambo hilo linavunja uadilifu wa ndoa na heshima ya ndoa na kuiharibu, sio hivyo tu kila mwanandoa anapaswa kutimiza wajibu wake na majukumu yake, kujali watoto, kujenga familia yenye afya, kujenga Imani thabiti na utii heshima na upendo, wanandoa wanapaswa kuwa mbali kabisa na usaliti, na kuvunja uaminifu, kuwa na mahusiano na wanawake au wanaume wengine kinyume na uadilifu wa ndoa, kupeana talaka, aidha kwa mwanamke kuidai talaka au kwa mwanaume kutoa talaka, Katika nyakati za leo wanawake katika nchi zilizoendelea wameitumia ndoa sio kwa upendo bali kama mtaji ya kwamba akiolewa na mwanaume tajiri ataachana naye baadae ili apate malipo ya kugawana nusu ya mali ya mwanaume ya utajiri wake Mungu alikusudia ndoa ziwe za kudumu na Mungu anachukia kuachana, pia kufunika nguo kwa udhalimu maana yake ni kunyimana tendo la ndoa, au kufanya zinaa na kadhalika haya yote yote pamoja na migogoro, na kukomoana Malaki anayaita mambo ya hiyana kila mmoja katika ndoa ana wajibu wa kuhakikisha kuwa ndoa inaheshimika na inadumu kama Mungu anavyotaka, wote tuna wajibu wa kuzuia mambo yanayoleta migogoro na uharibifu katika ndoa.

d.      Wanandoa wanapaswa kuhakikisha kuwa malazi yanakuwa safi - Neno hē koitē – Neno hili ambalo maana yake limetajwa kama kitanda cha ndoa au marriage bed Kiyunani linamaanisha tendo la ndoa, linapaswa kuwa safi, Usafi unaotajwa hapo ni kutokutiwa unajisi kwa kitanda cha ndoa kwa wana ndoa wenyewe lakini pia inazungumzia usafi wa kawaida na usafi wa tendo lenyewe hii ikiwa na maana ya kuwa lazima tendo la ndoa lifanyike kwa ufasaha, wanandoa wajifunze namna ya kufurahishana kwa kulifanya tendo hili kwa uhodari hii ikiwa ni pamoja na kutumia mitindo tofauti tofauti, “styles” za tendo la ndoa maadamu tu hazihitilafiani na mapenzi ya Mungu, wanandoa wanapaswa kuhakikisha kuwa wanabadilisha mitindo ya kushirikiana tendo hilo, ili kuondoa uchovu na mazoea ya aina moja ya mitindo, wakati mwingine ikibidi hata eneo, wako watu wengine ambao hufikiri kuwa mitindo hii ni dhambi, Lakini Mungu alimuumba mwanadamu na kumpa tendo hili kwa kusudi la kuongezeka na pia kwa kusudi la kufurahia na kuondoa migandamizo ya mawazo ya safari na uchovu wa dunia na kuleta usingizi mzuri Isaka na Rebeka walikuwa na ndoa yenye furaha kwa sababu walikuwa na mitindo tofauti, walikuwa marafiki walikuwa wakicheza pamoja na kutekenyana na kuchezeana michezo ambayo watu walipoona walijua kuwa huyu alikuwa mke na mume  

Mwanzo 26:6-9 “Isaka akakaa katika Gerari. Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso. Ikawa alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia dirishani, akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe.Abimeleki akamwita Isaka, akasema, Yakini huyu ni mkeo, mbona ulisema, Ni ndugu yangu huyu? Isaka akamwambia, Kwa sababu nalisema, Nisife kwa ajili yake.”

2.       Wasio na Ndoa – Agizo la kuheshimu ndoa pia linawahusu pia wasiokuwa na ndoa hawa nao wameamriwa katika andiko hili la msingi kuithamini na kutokuhusika kuichezea ndoa, Neno la Mungu linawataka wasiooa na wasiolewa kutokutamani mke wa mtu au mume wa mtu, lakini sio hiyo tu wanapaswa kuepuka ngono kabla ya ndoa kwa hiyo hawapaswi kufanya uasherati, tendo la ndoa linapaswa kufanyika ndani ya ndoa halali tu, kulifanya tendo hili kabla ya wakati wake ni dhambi na kunapelekea kutokuwa na heshima katika ndoa, zaidi hawapaswi kuivamia ndoa ya mtu mwingine na hawapaswi kuitumia miili yao kuharibu ndoa, wasiooa au kuolewa wanapaswa kujiepusha na kuufanya uchafu wa aina yoyote ile unaoharibu ndoa hata kama wewe hauko kwenye ndoa waogope wenye ndoa kama tatizo ili usije ukaadhibiwa na Mungu.

Kutoka 20:17 “Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.”

Wathesalonike 4:3-4 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;”

3.       Wazazi wa wenye ndoa – Mojawapo ya watu wanaoonywa pia na kuagizwa kuiheshimu ndoa ni pamoja na wazazi, wazazi wengi wasio na ufahamu wameharibu sana ndoa za watoto wao kwa sababu ya tabia ya kuingilia uongozi wa wanandoa na kwa sababu hiyo kuchochea migogoro, au wakati mwingine kwa kushindwa kuwasaidia wana ndoa na kutokuwaambia ukweli au kuamua changamoto zao kwa upendeleo, wanandoa wanapoambiwa kuwa mtu atamuacha baba yake na mama yake maana yake, maana yake wao wanapaswa kuanza serikali yao na hivyo wazazi wanapaswa kuwa walezi na washauri wa mbali na sio wenye kuingilia maamuzi  ya wanandoa na kuendelea kuwafanya wachanga siku zote, wazazi wanaosababisha migongano kwa wana ndoa wanavunja moja kwa moja agizo la ndoa na iheshimiwe na watu wote.

Mwanzo 2:23-24 “Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

4.       Jamii kwa ujumla, marafiki, majirani, viongozi wa mila na desturi – Maandiko yapoagiza kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote inawataka wana jamii wote kuheshimu ndoa wakiwemo marafiki, majirani, viongozi wa mila na desturi, wote wanapaswa kuiheshimu ndoa, Viongozi wa kimila ni lazima wasimamie haki na kuondoa mila zote potofu zinazoeneza uzinzi na uasherati kupitia tamaduni za aina mbalimbali, wana jamii wanapaswa kuiheshimu ndoa kwa kutokueneza udaku, habari mbaya na fitina au taariza zinazoweza kuihatarisha ndoa, jamii inapaswa kujiepusha na ushauri mbaya kwa wana ndoa, wanajamii waache maneno maneno na kuwaacha wenye ndoa waishi kwa amani, mtu yeyote anayesambaza habari za kuharibu ndoa ya mtu anafanya dhambi na haiweki ndoa katika vipimo vya Mungu, ziko mila ambazo kundi rika la aina fulani lina uwezo wa kutembea na wake wa wenzake wa rika hilo mila hizo zikomeshwe na hazifai kwani ni kinyume na uadilifu wa ndoa uliowekwa na Mungu, mila zinaweza kuwa bora kama tu hazivunji kanuni na utaratibu uliowekwa na Mungu

Mithali 6:16-19 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.”

Mithali 12:22-23 “Midomo ya uongo ni chukizo kwa Bwana; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake. Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu

5.       Kanisa na viongozi wa kirohoKanisa na viongozi wa kiroho wanapaswa kukazia na kutokuwa lele mama katika kufundisha uadilifu na uaminifu na utakatifu katika ndoa ni lazima kanisa lisimame katika zamu yake na kuhakikisha ya kuwa maagizo ya Mungu yanafanyiwa kazi katika jamii, na kuwasaidia wana ndoa bila kuziingilia na kuziharibu viongozi wa kanisa ni lazima watumie mamlaka yao vizuri na sio kuharibu ndoa za watu kwani ni makosa kiroho.

Mathayo 19:4-6 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.”

6.       Serikali na watawala watunga sheria za nchi – Serikali inawajibika kuziheshimu ndoa kwa kuweka taratibu nzuri na kutunga sheria zenye kuilinda jamii na kuilinda ndoa, kwa kuzuia vitendo vya kimapenzi vyenye kusababisha uhalifu ndani yake mfano uzinzi, ubakaji, ulawiti na matendo ya nguvu au uingiliaji wa kingono wa watoto wadogo na kuzuia matendo ya ukahaba mitaani, serikali lazima ilinde Ndoa kwa sheria, mamlaka inapaswa kuisimamia mema kwa mujibu wa neno la Mungu

Warumi 13:1-4 “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake; kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.”

Hitimisho:

Neno la Mungu linatoa wito wa kuiheshimu ndoa, wito huu nunaihusua jamii nzima kila mtu anapaswa kutambua kuwa ndoa ni Muungano unaotokana na Mungu  na sio wa kibinadamu, kila mtu anapaswa kuishi kwa uaminifu, usafi, na kuepuka dhambi zinazolichafua agano la ndoa, kuhakikisha kuwa unakuwa mfano wa heshima na upendo wa Kristo na kuhakikisa ya kuwa hugusi mali za watu ili kuepusha laana na kifo katika maisha yako, kila mtu anayegusa ndoa za mtu mwingine anajiweka katika hatari ya hukumu ya Mungu na kifo

Mwanzo 20:1-9 “Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari. Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara. Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu. Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee BWANA, Je! Utaua hata taifa lenye haki? Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi. Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse. Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao. Abimeleki akaamka asubuhi na mapema, akawaita watumwa wake wote, akawaambia maneno hayo yote masikioni mwao, nao watu hao wakaogopa sana. Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.”

Wanandoa wanapaswa kujiepusha kwa namna yoyote ile kujitangaza katika mitandao ya kijamii kama wanaachana, kufanya hivyo kunafungua mlango wa mmomonyoko wa uadilifu, kufungua mlango wa maoni maovu kutoka kwa watu wenye nia mbaya, Kumpa ibilisi nafsi na kupanua wigo wa mashambulizi zaidi, ni jambo la kusikitisha sana kuwa watu waliokuwa wanaishi chumba kimoja na wakati mwingine wana watoto unasikia mitandaoni kuwa wameachana wana simu za mkononi lakini wanajibizania mitandaoni, upumbavu  na ushamba wa namna hii unaweza kufanywa na mabaradhuli tu au watu wasiomjua Mungu, kwa ndoa ya kikristo  na hata isiyo ya kikristo ni muhimu kuweka akiba ya maneno kwani wanandoa wanaweza kurudiana baada ya kuhitilafiana sasa ikiwa mliweka ugomvi wenu na mafarakano yenu mtandaoni ikitokea mnarudiana mtatangaza? Mtataka tena maoni ya jamii nzima yaje kwenye stutus zenu hasa kama ninyi ni wakristo basi tuwe na adabu!

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.              

Jumapili, 26 Aprili 2026

Walinisukuma sana ili nianguke!

 


Zaburi 118:10-14. “Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia. Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.”




Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa katika maisha yetu wakati mwingine tunaweza kujikuta tumezungukwa na shinikizo la vitisho kutoka kila upande wa maisha yetu, unaweza kuzingirwa na mazingira hatarishi ya vita kutoka kila pembe ya maisha yako, unaweza kuzingirwa na shinikizo la upweke, shinikizo la kukosa afya, shinikizo la afya ya akili, shinikizo la kifedha na kiuchumi, shinikizo la hofu ya changamoto za kazini, shinikizo la matukio ya kutisha na kuumiza moyo, shinikizo la mabadiliko katika maisha, malezi, ndoa, na kadhalika hizi zote zinaweza kuwa hali zinazokusukuma ili ukate tamaa na kuvunjika moyo, na kuzungukwa na hofu za kifo, lakini Neno la Mungu leo linatukumbusha kuwa Bwana atakusaidia, yeye ni nguvu na wokovu, atakuwa msaada mkubwa kwetu tutakapoliitia jina lake atatusikia na atatuitikia kwa wingi wa neema na rehema zake.

Zaburi 116:1-5 “Haleluya. Nampenda Bwana kwa kuwa anaisikiliza Sauti yangu na dua zangu. Kwa maana amenitegea sikio lake, Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote. Kamba za mauti zilinizunguka, Shida za kuzimu zilinipata. Naliona taabu na huzuni; Nikaliitia jina la Bwana. Ee Bwana, nakuomba sana, Uniokoe nafsi yangu. Bwana ni mwenye neema na haki, Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema.”

Mungu atakuwa msaada wako wewe na mimi tunapokuwa katika mashinikizo ya maisha haya, iwe shinikizo la kimwili au la kiroho Mungu atakusaidia nawe utaufurahia uweza wa Bwana katika kututetea na kutupigania katika hali yoyote ile unayoipitia usilie wala usikate tamaa utasaidiwa naye

·         Maana ya kusukumwa sana.

·         Walinisukuma sana ili nianguke.

·         Nguvu za Mungu wakati wa kusukumwa.


Maana ya kusukumwa sana.

Zaburi 118:12-13 “Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.”

Kimsingi kifungu hiki cha maandiko kinaonyesha kuwa Mwandishi alikuwa amezingirwa na majeshi ya mataifa mbalimbali na kumuwekea shinikizo kubwa kutoka kila upande ili waweze kumshinda lakini aliwakatilia mbali kwa jina la Bwana na kuwashinda, Kimsingi maadui walimsonga sana ili ikiwezekana ashindwe na kumalizwa lakini Bwana alimsaidia.

Kwa asili maneno Ulinisukuma sana ili nianguke; lakini Bwana akanisaidia yanapaswa kusomeka hivi Walinisukuma sana ili nianguke Lakini Bwana akanisaidia, hii ni kwa sababu maadui waliokuwa wakimsonga walikuwa ni wengi na sio mmoja na ukweli huo unaweza kuthibitishwa na matoleo mengine ya Biblia kwa mfano Biblia za kiingereza zifuatazo zinaonyesha kuwa neno hili lilipaswa kuwa katika wingi “Walinisukuma” na sio katika umoja “Ulinisukuma” angalia kwa makini English

Christian Standard Bible inasema hiviThey pushed me hard to make me fail but the Lord helped me

Contemporary English Version inasema hiviTheir attacks were so fierce that I nearly fell, but the Lord helped me

New International Version inasema hiviI was pushed back and about to fall, but the Lord helped me

God’s word translation inasema hivi They pushed hard to make me fall, but the Lord helped me

Unapoangalia asili ya kifungu kizima utaweza kugundua kuwa mwandishi alikuwa akizungumzia kwa wingi, wingi wa maadui, wingi wa mataifa, wingi wa mashinikizo ya changamoto  na majaribu ya kufutiliwa mbali na maadui na kwa msaada wa Mungu aliwakatilia mbali maadui zake kumbuka walikuwa wengi kama nyuki lakini aliwateketeza kama moto wa miiba, sasa hebu tuangalie maana ya kusukumwa, Neno kusukumwa katika lugha ya Kiebrania linasomeka kama “dâchâh dâchach” linalosomeka kwa sauti “daw-khaw” ambalo kwa kiingereza linasomeka kama “outcast”  ambapo maelezo yake ni someone who is rejected or cast out, as from home or society or some way excluded, looked down upon or ignored kwa tafasiri ya Kiswahili ni mtu aliyekataliwa na jamii, aliyefukuzwa nje ya nyumbani au katika jamii, mtu aliyeonekana kuwa hana maana wa kudharaulika, asiyefaa kwa lolote asiye na mchango wowote, kwa hiyo mwandishi alikuwa ni mtu aliyekataliwa, aliyefukuzwa na anayewindwa na maadui kila upande auawe huku akiwa katika mashinikizo mbalimbali yanayomkabili kila upande kiroho na kimwili kiakili na kisaikolojia kwa ujumla alikuwa kama anazidiwa kiasi cha kukaribia kuzimia au kushindwa, maadui hawakutaka awe na utulivu kila wakati walimchokoza na kumsumbua na walitaka kuhakikisha anatokomea huko huko shimoni, hata hivyo mwandishi aliwashinda adui zake wote na hatimaye alirudi katika jamii na kuwa mtu mkubwa sana, Jambo ambalo liliwashangaza watu wote, Mateso haya yalimpata Daudi kimsingi

Zaburi 118:22-23 “Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.” 

Walinisukuma sana ili nianguke.

Kimsingi zaburi hii iliandikwa na Daudi kutokana na maisha aliyoyapitia, lakini kwa vile mtu huyu alikuwa nabii alikuwa pia anazungumza kwa niaba ya Israel, Yesu Kristo pamoja na wewe na mimi, Israel ni Taifa ambalo linaonelewa na kuchukiwa na jamii ya kimataifa sana, ni taifa ambalo adui zake wanatamani walifute lisiwepo, linazingirwa na watu wanaolichukia kutoka kila upande, hata sasa tunapozungumza Israel iko katika vita na baadhi ya nchi za kiarabu na vikundi vya kigaidi wote wakipeleka shinikizo ili ikiwezekana waweze kuwafuta, Israel inachukiwa na Hamas (Harakat al-Muqawama al-Islamiya au Islamic Resistance Movement) hiki ni chama cha siasa nan a Jeshi la waislamu wa Sunni walioko Palestina Eneo la Ukanda wa Gaza, Lengo lao likiwa ni kufutilia mbali wayahudi kokote duniani, Inachukiwa na Hezbollah (Hezb Jeshi au chama Allah- Mungu) Chama cha Mungu au Jeshi la Mungu hawa walioko Lebanon wakisaidiwa na Iran neno Hezbollah maana yake chama cha Allah lengo lao kuu ni kuiangamiza Israel hili ni kundi la kigaidi la Washiha, Israel inachukiwa na Iran ambao wanaiona Israel kama kansa ambayo inatakiwa kufutwa, wanapambana na mamlaka ya Palestina huko ukanda wa Magharibi, inashambuliwa na kundi la wa Houthis hawa wanaitwa Ansar Allah ni tawi la Madhehebu ya Shiha (Shiite) ambao wako Yemen wanaoungwa mkono na Iran, kila mahali kuna shinikizo na yote yanalenga kuwamaliza watu wa Mungu, Daudi kama nabii anaiona Israel kuwa watasaidiwa na Mungu na pamoja na mashinikizo yanayowakabili kama yeye alivyozingirwa na maadui Mungu ataandaa meza machoni pa watesi wetu.

Zaburi 23:4-5. “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.”

Aidha unabii huu pia unamhusu Yesu Kristo, ambaye naye alikataliwa na jamii na kukatiliwa mbali na watu wake na kuteswa vibaya walimsukumia mbali hata katika shimo la mauti lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, Yesu huyu atakuja tena na kuwa mtawala wa ulimwengu wakati wa utukufu pale Israel litakapokuwa taifa kubwa litakaloitawala Dunia mfalme wake atakuwa ni Yesu

Isaya 53:3-5 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Unabii huu pia unakuhusu wewe na mimi, Shetani anatuchukia bure anafanya mashambulizi kupitia watu na mapepo anatushinikiza kila sehemu na kila mahali kwaajili ya kumpenda Mungu tumekuwa na maadui kila mahali, kwaajili ya kumtumikia Mungu tunachukiwa lakini tunakumbushwa na zaburi hii ya kuwa Mungu hatatuacha hivi hivi hatimaye atakuja kutusaidia nasi tutatawala pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo katika ufalme wake!

Mwandishi anatumia lugha picha kuonyesha bidii na juhudi za maadui dhidi yetu wanasukuma sana wanajitahidi wana hasira, lakini hata hivyo kwa msaada wa Mungu maadui walishughulikiwa mmoja baada ya mwingine kwa kukatiliwa mbali kwa jina la Bwana tunaweza kuwa na maadui wa kimwili, maadui wa kiroho na maadui wa maisha yaani masumbufu ya maisha haya na yanaweza kutuletea shinikizo za namna mbalimbali lakini kwa mujibu wa mwandishi ni kuwa Bwana atatusaidia.

Tunaweza kusukumwa na watu kupitia chuki zao, wivu, kejeli au vitendo vya kutukatisha tamaa, mambo haya yanaweza kufanywa na wenzetu, majirani na hata wanafamilia wanaweza kutusukuma kwa maneno au kwa vitendo, Yusufu alitupwa shimoni alitendwa vibaya lakini Mungu alimsaidia.

Mwanzo 49:22-25 “Yusufu ni mti mchanga wenye kuzaa, Mti mchanga wenye kuzaa karibu na chemchemi, Matawi yake yametanda ukutani. Wapiga mishale walimtenda machungu, Wakamtupia, wakamwudhi, Lakini upinde wake ukakaa imara, Mikono yake ikapata nguvu, Kwa mikono ya Mwenye Enzi wa Yakobo; Kwa jina la mchungaji, yeye jiwe la Israeli, Naam, kwa Mungu wa baba yako atakayekusaidia; Kwa mibaraka ya mbinguni juu. Mibaraka ya vilindi vilivyo chini, Mibaraka ya maziwa, na ya mimba.”

Tunaweza kusukumwa wakati mwingine na hali mbaya ya maisha, ugumu wa maisha kutokumudu hali ngumu ya maisha umasikini, magonjwa makali, kushindwa au hasara za kifedha, zote zionaweza kutumika kama misukumo inayokugandamiza ili uanguke, unaweza kusukumwa na upinzani wa nguvu za giza, nguvu za mashetani kusukumwa na hofu, woga na mashaka au majaribio ya kuachana na imani, mifumo ya dunia  ya uchumi na siasa yote yanaweza kukufanya ukawa katika shinikizo ambalo linalenga kukuangusha vyote hivi vinalenga kukusukuma ili uanguke lakini Mungu ndiye msaada wetu, Mungu wetu yuko pamoja nasi, Mungu wetu atatusaidia hatakuacha uaibike!

Zaburi 124:1-8 “Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa, Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia. Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu. Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu; Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo. Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao. Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka. Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.”

Nguvu za Mungu wakati wa kusukumwa.

Neno la Mungu linaonyesha wazi kuwa wakati watu, maisha na shatani anapoifanya kazi ya kutusukuma ili tushindwe kumbe Mungu ananyoosha mkono wake kutusaidia hiki ndicho anachokishuhudia mwandishi wa zaburi, na kutukumbusha kuwa msaada wetu uko kwa Mungu yeye ndiye anayetusaidia hataacha tuanguke, wala hataacha tuzimie hasinzii wala halali atafanya kitu tu

Zaburi 118:10-14. “Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia. Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.”

Isaya 41:10-13 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.”

Yeremia 1:18-19 “Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii. Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.”

Haijalishi kuwa maisha yako yanazingirwa na mashinikizo ya namna gani lakini kila mahali Mungu yuko na atakusaidia, watu wanaweza kuinuka kinyume nawe, hali inaweza kuinuka kinyume nawe, mazingira yanaweza kuwa kinyume nawe, wakuu wa dini wanaweza kuwa kinyume nawe, lakini Mungu atakuwa msaada mkubwa kwako yeye atakufanya wewe kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma na ukuta wa shaba maana yake Mungu anakuhakikishia kuwa huwezi kuvamiwa pamoja na mashinikizo ya upinzani na vitisho vya kila aina wewe katika yeye ni Mshindi na zaidi ya kushinda, haijalishi nani wanakusukuma ili uangamie, nani anakuusukuma ili uanguke kwa jina la Bwana watakatiliwa mbali katika jina la Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.

Jumapili, 19 Aprili 2026

Kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika!


Zaburi 40:11-13 “Nawe, Bwana, usinizuilie rehema zako, Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima. Kwa maana mabaya yasiyohesabika Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, Na moyo wangu umeniacha. Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima.”




Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kwamba kuna nyakati katika maisha yetu ambapo mtu unaweza kujikuta katikati ya matatizo mengi kwa wakati mmoja, Kibiblia hali hiyo sio ngeni na kama unakutana na hali kama hiyo wewe sio wa kwanza, Mwandishi wa zaburi hii anaelezea naye hali halisi ya mambo yaliyomkuta, akiwa katika mashinikizo ya changamoto zaidi ya moja anazungukwa na mabaya yasiyohesabika na kutusaidia sisi kuelewa njia ya kufuata na kufanya wakati tunapozungukwa na mabaya yasiyohesabika, usifikiri wakati wowote kuwa labda una laana au una nuksi au Mungu anapatiliza makosa na dhambi zako hapana, ziko nyakati tu katika maisha ya mwanadamu inaweza kutokea ukapita katika hali kama hiyo na hayo ni mambo ya kawaida na wala hupaswi kukata tamaa

2Wakorintho 4:8-10 “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi; siku zote twachukua katika mwili kuuawa kwake Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu.”

Unaona mtume Paulo anaeleza pamoja na kuwa mtu wa Mungu lakini walikuwa wakizungukwa na mabaya yasiyohesabika yeye anaeleza kwa lugha nyingine kuwa twadhikika pande zote, twaona shaka, twaudhiwa, twatupwa lakini hawakati tamaa, hawasongwi, hawazidiwi, hawaangamizwi wala Mungu hawaachi, kuwa mtu wa Mungu au kuwa katika agano na Mungu haimaanishi kuwa na maisha mepesi, iangalie Israel katika ulimwengu wa kimwili ina picha halisi katika ulimwengu wa kiroho sawa na yale unayoyapitia, wanashambuliwa na Hezibollah, (Washiha wenye siasa kali) wanashambuliwa na Hamas (Wasuni wenye siasa kali), wanashambuliwa na Houthis (Wa Ansar wenye siasa kali) wanashambuliwa na Palestinian Islamic Jihad hawa wote wanafanya mauaji, wanateka watu, wanalipua mabomu, wanarusha maroketi na makundi haya yote ya kigaidi yanafadhiliwa na taifa Fulani lenye uchumi mzuri,  jambo linalowafanya wasiishi kwa amani ni ukweli ulio wazi bila mkono wa Mungu Israel isingeliweza kusimama, halikadhalika watu wa Mungu kila upande unashambuliwa na adui yetu shetani na hili ni swala la kawaida katika maisha ya watu wa Mungu hupaswi kuogopa, kwa sababu halitadumu, Leo basi tutachukua muda  kujifunza somo hili  Kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika! Kwa kuzingatia vipengele muhimu vitatu vifuatavyo:-

·         Kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika.

·         Mambo ya kufanya unapozungukwa na mabaya yasiyohesabika.

·         Msaada wa Mungu wakati unazungukwa na mabaya yasiyohesabika.

Kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika

Neno  mabaya yasiyohesabika katika lugha ya asili ya Kiebrania yanasomeka “Ra’ot ein mispar” katika muunganiko huo wa maneno au misamiati miwili ya Kiebrania tunapata neno “Ra’ot” ambalo maana yake kwa kiingereza “trouble” au “evils” kwa Kiswahili ni mabaya, maovu, shinikizo, changamoto au matatizo na neno “Ein Mispar”  ambalo maana yake “countless”, au “without number” yasiyohesabika, yasiyo na idadi, kwa hiyo neno “Ra’ot ein mispar” linapounganishwa pamoja kwa kiingereza unapata neno “countless troubles” au “evil without numbers  maana yake ya kina ni kuwa mtu anayepitia matatizo mengi mfululizo au matatizo mengi kwa wakati mmoja, au changamoto zisizoweza kuhesabika au kujulikana zinaisha lini, mtu anayepitia mashinikizo kutoka pande zote hali hii inapompata mwanadamu kimsingi unaweza kukata tamaa na unazidiwa nguvu  unajiuliza kimsingi unawezaje kutoka katika hali hiyo kama ni magonjwa unajihisi mauti inakuzunguka kila upande mtu unaweza kupitia changamoto nyingi mpaka ukajiuliza kichwani nimekanyaga wapi, wakati Ayubu, Yeremia na Yona  wanapitia hali kama hii ya kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika  wao kwa nyakati tofauti tofauti walisema:-

Ayubu 19:8-10 “Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu. Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu. Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling'oa kama mti.”

Maombolezo 3:1-7 “Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake. Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru. Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu. Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu. Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito.”

Yona 2:3-5 “Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu. Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako; Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu. Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu; Vilindi vilinizunguka; Mwani ulikizinga kichwa changu;”

Wenzetu hawa kwa nyakati tofauti tofauti kama ilivyokuwa kwa Daudi mwandishi wa zaburi tunayoitafakari walipitia katika nyakati za kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika, kwa hiyo kuzungukwa na mabaya sio jambo geni kwa watakatifu na watu wa Mungu ni hali ya kimaandiko na tunajifunza hivyo kutoka katika maandiko kila mtu wa Mungu anaweza kupitia. Mpendwa je wewe unazungukwa na mabaya yasiyohesabika pande zote?  Watu wa Mungu katika maandiko walipitia, je unapopita katika hali kama hiyo unafanyaje? Wenzetu walifanyaje? Yako mambo ya kufanya  

Mambo ya kufanya unapozungukwa na mabaya yasiyohesabika

Zaburi 40:11-13 “Nawe, Bwana, usinizuilie rehema zako, Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima. Kwa maana mabaya yasiyohesabika Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, Na moyo wangu umeniacha. Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima.”

Tunajifunza kutoka katika andiko la Msingi wakati wenzetu walipozungukwa na mabaya yasiyohesabika hawakulaumu mtu wala hawakutafuta mchawi wala sababu au kufikiri kuwa wamerogwa na badala yake WALIOMBA usinizuilie rehema maana yake waliomba rehema, fadhili zako zinihifadhi daima walitafuta fadhili za Bwana, walimueleza Mungu wazi wazi kuwa changamoto hizi zimewazidi, walieleza moyo umekufa ganzi, na waliomba msaada wa Mungu, kilio cha mtu anayezungukwa na mabaya humfanya Mungu aingilie kati sawasawa na ahadi zake katika neno lake

Zaburi 50:15 “Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.” Kwa hiyo neno la Mungu linaonyesha kuwa kila aliyezungukwa  na mabaya yasiyohesabika aliliitia jina la Bwana katika taabu yake na Bwana akasikia na kuwaokoa, sisi nasi tukiliitia jina la Bwana Mungu atasikia na kujibu

Pamoja na maombi na kulia na kumimina mioyo yao mbele za Mungu watakatifu waliotutangulia WALIMTUMAINI Bwana, hapo tunajifunza kuwa walitambua kuwa hakuna mwingine anayeweza kuwasaidia isipokuwa Mungu, hii ni kwa sababu ni kawaida kibinadamu kufikiria mtu wa kukusaidia unapopita katika changamoto fulani fulani lakini lakini wanadamu wanaweza kutumiwa kukuletea shinikizo kubwa zaidi wakati wa changamoto zako hivyo omba kisha weka tumaini lako kwa Bwana

Mithali 3:3-6 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako. Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu. Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.”

Zaburi 56:1-4 “Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita. Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi. Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe; Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?

Msaada wa Mungu wakati unazungukwa na mabaya yasiyohesabika

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu huwa pamoja na wale wanaopitia au kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika, na hatakuacha uangamie Paulo anaeleza kuwa twazikika pande zote lakini hatuangamii kwa nini Paulo anasema kuwa hatutaangamia hata tupitapo katika changamoto nzito?

2Wakorintho 4:8-10 “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi; siku zote twachukua katika mwili kuuawa kwake Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu.”

1.       Bwana huwa Karibu ili kuokoa na kuponya - Zaburi 34:19 “Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa. Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote.”

2.       Bwana atakuwa pamoja nawe na atakupa watu - Isaya 43:2-4 “Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza. Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.”

3.        Bwana atafanya mlango wa kutokea - 1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”

4.       Bwana atakusaidia Isaya 41:10-13 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.”

5.       Bwana atakupa hatima iliyo njema – Yakobo 5:10-11 “Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu. Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

Hitimisho

Ndugu zangu kaka zangu na dada zangu kuzungukwa na mabaya yasiyohesabika sio mwisho wako ni hatua ya Mungu kukupeleka katika kiwango kingine ni daraja tu ni mlango wa miujiza mikubwa Bwana hatakuacha uzidiwe ataleta msaada wake haraka, hauna sababu ya kulia au kulalamika au kukata tamaa najua wakati unapozungukwa na mabaya yasiyohesabika ni wakati ambapo kila kitu kinakatisha tamaa ni wakati ambapo unaweza kupoteza tumaini lakini neno la Mungu limetutia moyo ya kuwa Mungu hatatuacha atatuokoa na kutuponya, atakuwa pamoja nawe na atatoa watu wakusaidie, atafanya mlango wa kutokea, atakuwa pamoja nawe hakuna kitu kitakachoweza kusimama mbele yako, yeye atakusaidia na kukupa mwisho ulio mwema jambo kubwa la msingi ni kusimama na kuuona wokovu wa Bwana, Kama Mungu anavyowasaidia Israel na kuwalinda na kuwatetea pamoja na kuzingirwa na wabaya wasiohesabika kila upande lakini Mungu haogopi atakuandalia meza katikati ya watesi wako

Kutoka 14:13-14 “Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.”

Wimbo: “Roho wa Bwana twakualika utawale, Karibu Roho, fanya mapenzi ya Bwana”

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima