Jumapili, 27 Desemba 2020

Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari!

Mwanzo 31:24 “Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.     


Utangulizi:

Je umewahi kupitia mambo magumu katika maisha yako mpaka unaamua kukimbia? Umewahi kupitia mitihani mizito mpaka unaamua kufanya maamuzi magumu?  Maisha ya Yakobo yaani Israel duniani hayakuwa mepesi kama tunavyoweza kufikiri, alipitia mambo magumu mno, alipitia maisha ya taabu na dhiki kuliko Ibrahimu na Isaka baba zake ona

Mwanzo 47:7-9 “Yusufu akamleta Yakobo babaye ndani akamweka mbele ya Farao Yakobo akambariki Farao.  Farao akamwuliza Yakobo, Je! Siku za miaka ya maisha yako ni ngapi? Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, tena za taabu, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.”

Moja ya maeneo ambayo huenda Israel aliyakumbuka katika taabu alizozipitia ni pamoja na maisha yake  ya ujombani, alikokuwa akimtumikia Laban Mjomba wake, Hatimaye Yakobo na wake zake na wanae waliamua kuondoka kwa mjomba kwa kutoroka bila hata kuaga kwa kuhofia kuwa huenda Labani atamuonea tena Yakobo kama alivyomuonea siku zote za maisha yake, Hata hivyo Labani aligundua kutoroka kwa Yakobo na kuwa msafara wake ulikuwa ukielekea Gilead akamuwahi na kumkuta baada ya wiki nzima

Mwanzo 31:21-23 “Basi akakimbia yeye na yote aliyokuwa nayo; akaondoka akauvuka mto, akaelekeza uso wake kwenda mlima wa Gileadi. Hata siku ya tatu Labani akaambiwa ya kwamba Yakobo amekimbia, akatwaa ndugu zake pamoja naye, akamfuata mwendo wa siku saba. Akampata katika mlima wa Gileadi.”

Hatuwezi kujua kuwa Labani alikusudia kumfanya nini Yakobo? Hatujui nini kilikuwa katika akili zake lakini bila shaka alikuwa amenogowa na utumishi wa Yakobo, alitamani kuendelea kumfanya yakobo kuwa mtumwa wake siku zote, hakufikiri wala kutamani kuona kuwa siku moja Yakobo anakuwa huru, anamuabudu Mungu wa baba zake kwa uhuru, ana kuwa na kabila zake mwenyewe, anajitawala na kutimiza hivyo kusudi la Mungu, labani alikuwa ni muabudu miungu, hakuweza kujua kusudi la Mungu ndani ya Yakobo. Lakini alikuwa na hisia zilizowazi kuwa mtu huyu anaye Mungu aliye hai, anajua na kufahamu kuwa Yakobo alitajirika kwa jasho lake huku Mungu wa baba zake akiwa ameweka mkono wake kumbariki mtu huyu aliyeonewa na kupangiwa maisha tangu siku ya kwanza, Labani asingeweza kukubali hata kidogo kumuachia Yakobo kama farao alivyokataa kuwaachia wana wa Israel Kule misri baadaye, Yako mambo ambayo ulimwengu hauwezi kukubali kutuachia wala shetani hakubali kukuachia kwa sababu uweza wa Mungu uko juu yako na adui zako wanafaidika na uwepo wako, Africa wazungu hawawezi kukubali kukuachia ujitawale hawawezi kukuacha uchakate kila ulicho nacho kwa sababu wanafaidika na utumwa wako, wakati mwingine ili tuweze kuwa huru katika eneo Fulani ni mpaka Mungu aingilie kati, na Mungu huingilia kati pale anapoona tu mechoshwa na hali hiyo, hata hivyo Labani hangekubali na hivyo Mungu wa Israel aliingilia kati na kumuonya katika ndoto kwamba Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari!

Kwa Lugha nyingine usiiingilie kati kusudi la Mungu lililoko ndani yakem usimzuie, Yakobo ni lazima aishi kanaani, ni lazima aende katika nchi ya ahahdi ndani yake kuna kusudi Yeye anajua na Mungu anajua kwa hiyo umemtafuta umemuona lakini lazima umuache aende zake usmwambie la heri wala la shari katika uamuzi wake huu unasikia labani? Labani alikuwa amefikisha Hatua ambayo angeingia kwenye ugimzi na Mungu, alikuwa akimuonea Yakobo mara kadhaa na inawezekana kabisa pia alitaka kumdhuru wakati ulikuwa umefika sasa Yakobo lazima awe huru, na Labani achague kurejea katika nchi yake ama akutane na mkono wa Mungu! Ona

Mwanzo 31:6-16 “Nanyi mmejua ya kwamba kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu. Na baba yenu amenidanganya, akabadili mshahara wangu mara kumi; lakini Mungu hakumwacha kunidhuru. Aliposema, Walio na madoadoa watakuwa mshahara wako, wanyama wote wakazaa madoadoa. Aliposema, Walio na milia watakuwa mshahara wako, ndipo wanyama wote wakazaa wenye milia.  Hivi Mungu akamnyang'anya mali yake baba yenu, na kunipa mimi. Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka. Na malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, Yakobo! Nikasema, Mimi hapa. Akasema, Inua, basi, macho yako, ukaone; mabeberu wote wanaopanda wanyama wana milia, na madoadoa, na marakaraka; maana nimeona yote aliyokutendea Labani. Mimi ni Mungu wa Betheli, huko ulikotia mafuta nguzo, na kuniwekea nadhiri. Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile uliyozaliwa. Raheli na Lea wakajibu, wakamwambia, Je! Imetubakia sehemu au urithi katika nyumba ya baba yetu? Hakutufanya kama wageni, maana ametuuza, naye amekula fedha zetu kabisa? Maana mali yote ambayo Mungu amemnyang'anya baba yetu, mali hiyo ndiyo yetu na ya wana wetu. Basi yo yote Mungu aliyokuambia, uyafanye.

Unaona unaposoma kifungu hicho unaweza kuona  na kupata picha ya kuwa maisha ya Yakobo, hayakuwa rahisi, kulikuwa na kila aina ya ukatili   na uonevu kutoka ujombani,  Labani alijaribu kwa kila namna kumfanya yakobo awe mtumwa wake wa kudumu, mtumwa wa maisha yake yote, Mungu alikuwa ni shahidi wa kile Labani alikuwa anamfanyia Yakobo, ni jambo la kushangaza kwamba mjomba wako mwenyewe kaka wa mama yako anakuwa kikwazo cha kusudi la Mungu maishani mwako sasa ilikuwa lazima Yakobo aende Nyumbani, aende alikozaliwa arudi Betheli kwenye nyumba ya Mungu, anede kwenye kusudi la Mungu, aende kwa baba yake aende akamuabudu Mungu wa baba yake katika nchi ya ahadi, Mungu mwenyewe alisema aende na kuwa atakuwa pamoja naye

Mwanzo 31:2-3 “Yakobo akaona uso wa Labani, ya kuwa hakumtazama vema kama jana na juzi. BWANA akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe.”

Inaonekana kulikuwa na hali ngumu katika nyumba ya labani na ni wazi kuwa Israel alikuwa mvumilivu mno, ziko hali zinaweza kukuta mpaka majirani wakaona jinsi unavyoteseka na kuvumilia, ziko hali zinaweza kukukuta mpaka Mungu mwenyewe anakuambia sasa toka na kuwa nitakuwa pamoja nawe

Ni Mungu pia aliyemshauri Yakobo kurejea na ni Mungu aliyemuahidi atakuwa pamoja naye, yakobo alitoroka kama mahusiano yalikuwa mema haiwezekani kutoroka kwa mjomba lakini kutoroka huku kimya kimya kunaashiria kuwa hakli haikuwa nzuri ujombani, Labani anagundua bila shaka anamfuatilia Yakobo akiwa na hasira kali, akiwa amekusudia kumdhuru na kumfanyia jambo baya sana Lakini Mungu wa wote wenye mwili alimkemea Labani alimuonya katika ndoto alimtokea na kumueleza waziwazi Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari! Ndio  kuna watu ni wakorofi, hatuwawezi kwa akili zetu na unyonge wetu, ndio wenye nguvu, ndio waliotuajiri ndio wajomba zetu lakini Mungu akiwa upande wako hatakuacha uonewe, atamkemea kila mtu anayesimama kinyume na kusudi la Mungu ndani yako kumbuka

Zaburi 105:14-15 “Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao.  Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.

Haijalishi audi zako wana uwezo kiasi gani, wana nguvu kiasi gani, wana uzoefu kiasi gani wana mali kwa kiasi gani vyovyote iwavyo Bwana atawakemea Mungu alimkemea Labani  kwaajili ya Yakobo, Mungu atamkemea kila mmoja anayesimama kinyume nawe kwa kuwa wewe umtumishi wake, Labani ni lazima akumbuke kuwa hawezi kushindana na kusudi la Mungu lililo ndani yako Lazima akumbuke jinsi Mungu alivyomuonya na kusema naye, ana nguvu ana uwezo anaweza kukudhuru lakini Bwana amesema naye ajihadhari asiseme le heri wala la shari nini kingemtokea unajua unaelewa hakuna mtu anaweza kushindana na kusudi la Mungu hata kidogo Labani angeshughulikiwa lakini afadhali alikumbuka maonyo ya Mungu ona

Mwanzo 31:25-29. “Labani akamfikia Yakobo, na Yakobo alikuwa amepiga hema zake katika mlima, na Labani na ndugu zake wakapiga hema zao katika mlima wa Gileadi.Labani akamwambia Yakobo, Umefanya nini? Umenihadaa, ukawachukua binti zangu kama mateka waliotwaliwa kwa upanga. Mbona umekimbia kwa siri ukanihadaa, wala hukuniambia, nipate kuagana nawe uende zako kwa furaha, na nyimbo, na ngoma, na kinubi?Wala hukuniacha niwabusu wanangu, na binti zangu; basi umetenda upumbavu. Ninao uwezo mkononi mwangu wa kukufanyia madhara; lakini Mungu wa baba yako usiku huu ameniambia, akisema, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.

Nakuombea neema kwa Mungu, wewe unayeteseka kwa sababu mbali mbali, natamka maneno ya kinabii juu yako dhidi ya adui zako dhidi ya wanaokuonea dhidi ya wenye kutunga hila juu yako, kwamba wakuache wajihadhai wasinenen neno la Kheri wala la shari juu yako!  Wewe una Mungu aliye hai, wewe hauabudu vinyago, wewe una kusudi la Mungu ndani yako nasema wakuache nasema wakuache nasema wasikusimange nasema wasikusengenye nasema kwa lugha ya kinabii nawakemea wenye kukusudia mdhara juu yako wasinene wasipange la kheri wala la shari wakumbuke neno hili kwani Mungu yule yule wa Israel Mungu yuleyule wa Yakobo na baba yetu Isaka na Ibrahimu huyu huyo ndiye mtetezi wetu, huyo huyo ndiye atakayefanya njia , huyo huyo ndiye  jemedari wetu, huyo huyo hataacha mtu atuoneee hata kama ni wenye uwezo na mamlaka atawakemea

Baraka za Mungu yule nimuabuduye na ziwe na kila aneysoma waraka huu, Bwana kubariki na kuwa upande wako, wasinene la Kheri wala la shari dhidi yako katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth amen

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Familia takatifu !

Andiko la Msingi: Luka 2:41-49 “41. Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42. Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu; 43. na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari. 44. Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao; 45. na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46. Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47. Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48. Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.49. Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa mara baada ya sikukuu ya krismas Kanisa huwa linasheherekea siku ya familia takatifu, Tayari Yesu Kristo amezaliwa na tayari imekuwa familia kamili, Yenye baba, Mama na mtoto, hii sasa ni familia ya watu wanaomcha Mungu, Familia ndio asili ya kila kitu, hakuwezi kuwa na taifa pasipo familia, hakuwezi kuwa na kabila pasipo familia, hatuwezi kuwa na viongozi wazuri wasiotoka katika familia, hatuwezi kuwa na watetea haki, waamuzi, wanamapinduzi,  manabii, na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine hawajatokana na familia, hivyo familia ndio taasisi ya kwanza kabisa kabla ya kuweko kwa taasisi nyingine, Kwa msingi huo basi ili tuweze kuwa na kila jambo zuri, lazima jambo hilo lianzie katika familia, Leo tutachukua muda kujifunza namna familia ya Yesu, ambayo ilimjumuisha Mariamu, mama yake na Yusufu Baba yake mlezi na kijana mtoto Yesu. Hii ilikuwa ni familia ambayo imeleta Baraka kubwa sana duniani na hivyo kuna mambo ya kujifunza

1.       Hakuna familia isiyokuwa na Changamoto.

Ni muhimu kufahamu kuwa kila familia inapitia changamoto zake, Familia ya Yesu ilipitia changamoto za aina mbalimbali, Lakini kutokana na kumtanguliza Mungu, Mungu aliwatoa katika changamoto hizo:-

 

a.       Walipitia katika umasikini uliokithiri ;-

 

Kabla ya Yesu kuzaliwa ni wazi kabisa kuwa Yusufu na Mariamu hawakuwa na uchumi mzuri, walikuwa na ukata, usafiri waliotumia ulikuwa usafiri wa punda,  sadaka walizokuwa wakitoa Hekaluni ilikuwa ni njiwa wawili ambayo ni sadaka ya chini mno iliyotolewa na watu waliokuwa masikini, Hata hivyo umasikini huu haukuwa sababu ya manung’uniko kwao, wala sababu ya kuiba, au kutapeli, au kukopa na kutokurudisha, au kuomba omba, waliweza kuvumilia na kuendelea kumtegemea Mungu huku wakifanya kazi kwa bidii, Maisha yao yalibadilika baadaye baada ya sadaka ya Mamajusi waliotoa dhahabu, uvumba na manemane hivyo ndio viliweza kuibadili hali ya familia hii iliyomtegemea Mungu, Wakristo lazima tujifunze kuwa wavumilivu na kuusubiri wakati wa Mungu wa kutufanikisha bila kupitia short cut kwani Mungu ana majira na nyakati za kutubariki, Familia hii ilivumilia magumu na changamoto walizozipitia mpaka Mamajusi walipotoa zawadi zilizowatajirisha sana ona

Mathayo 2:10-12 “10. Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno. 11. Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane. 12. Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.”


Tunaimba kwamba mjini mwaka mfalme Daudi palikuwa zizi nyoge... Yesu alizaliwa katika hali ya unyonge lakini maisha ya uvumilivu na subira ilibadilisha maisha ya familia yake na wakawa sasa wana uwezo wa kwenda Misri na kuishi huko kwa muda wakijikimu maisha yao, Lazima kila familia iwe na uvumilivu, usijilinganisha na watu wengine mtegemee Mungu, na Mungu atawabariki

 

b.      Walimsikiliza Mungu (Walitii mapenzi ya Mungu):-

 

 

Familia takatifu lazima iwe na uwezo wa kumsikiliza Mungu, Kumsikiliza Mungu ni kulisikiliza neno lake, kusikiliza watumishi wake na kuhudhuria ibada, Familia hii iliweza kudumu kwa sababu ilikuwa familia ya wazazi ambao wote walikuwa na uwezo wa kumsikiliza Mungu, kuliko kusikiliza maneno ya watu wa mtaani, Yusufu alipoona Mariamu ana Mimba biblia inasema aliamua kumuacha kwa siri! Unaona lakini mapema sana Malaika wa Bwana alimuonya Yusufu asimuache mariamu mkewe, ona katika

Mathayo 1:19-21 “19. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri. 20. Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

Unaona Kama Yusufu angekuwa ni mwenye kusikiliza maneno ya watu wa mitaani ndoa yake ingevunjika mapema na familia hii isingekuwa Baraka kwa dunia, Familia takatifu ni lazima iwe familia inayosikiliza maneno ya Mungu na kufuata uongozi wa Mungu, ni kwa kujua unyenyekevu na usikivu wa Yusufu, Mungu alisema na Yusufu tena kupitia malaika wake ili kukimbilia Misri na kuyalinda au kuyatunza maisha ya Yesu asiuawe na Herode ona 

Mathayo 2:13-14 “13. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize. 14. Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

Unaona ni maisha ya usikivu wa Yusufu ulioweza kumfanya Mariamu na mtoto Yesu kuwa salama kule misri na kuepuka kifo kutoka kwa Herode, Leo hii familia nyingi zinaharibika na watoto wanaenea mitaani wakipoteza muelekeo, au hata wakikosa kusoma kwa sababu ya wazazi waliokosa usikivu kwa Mungu na kwa wazazi, vijana wengi wanaishi vile wanavyojisikia na kujibu kile wanachojisikia na hata wazazi wamekosa kuwa mfano bora kwa kuigwa na watoto wao kwa sababu ya kutikumcha Mungu, Yusufu, na Mariam na Yesu walikuwa ni familia ya mfano katika kumcha Mungu.

 

c.       Walimuabudu Mungu;’-

 

Mstari wa msingi tuliousoma unasema “Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka,” Unajua maana yake nini hawakukosa ibada kuu katika hekalu lililokuwako Yerusalem, wazee wake maana yake wazazi wake kila mwaka walikwenda Hekaluni kusali na hawakuenda wenyewe walikwenda na vijana wao akiwemo Yesu, wao wenyewe walimuabudu Mungu lakini waliwafundisha watoto wao kumuabudu Mungu na kumpenda jambo hili lilijenga uhusiano mkubwa wa Yesu na Mungu baba wa Mbinguni, kiasi ambacho licha ya Yesu kuwaheshimu wazazi wake alimuona Mungu baba wa Mbinguni kuwa baba yake

Luka 2:48-49 “48. Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. 49. Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?

tuwafunze watoto wetu wajue kuwa japo sisi ni wazazi wao lakini wanaye baba wa Mbinguni wamsikilize, wamtiii wampende wamuabudu familia takatifu lazima wajijenge tabia ya kuabudu. Kuimba, kuomba, kusoma neno la Mungu na kuhudhuria makusanyiko ya ibada na kujifunza na kudumisha uhusiano na Mungu ni jukumu la kila familia kuhimizana na kutiana moyo, kumuheshimu Mungu.

 

d.      Walipeleka watoto shule

 

Katika desturi za kiyahudi kijana aliyefikisha miaka 12 alikuwa tayari amefunzwa kuijua Torati na kufanya kazi za kujitegemea, wengine walijivunza uvuvi, wengine ukulima, wengine ujenzi na wengine kushoma mahema kama Paulo mtume, Yesu alikuwa na ujuzi wa torati na alikuwa amejifunza ujenzi “Carpenter” hii iliwajengea watoto uwezo wa kujiamini na kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha Hivyo Yesu alijengewa kupenda kujifunza na alikuwa msikivu kwa walimu wake na alikuwa mdadisi aliuliza maswali ona

“Luka 2:45-47 45. na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46. Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47. Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.”

Familia takatifu na iliyo njema inapaswa kuhakikisha kuwa watoto wao wanapata Elimu nzuri, na wanakuwa na uwezo wa kujitegemea wanaweza kufanya kazi mbalimbali, na wanakuwa na ujuzi wa maadili na sheria za ukoo na familia zao, leo hii tunaona kuna mmomonyoko mkubwa wa uadilifu lakini ni kwa sababu tatizo kubwa limeanzia katika ngazi ya familia, wazazi wanapaswa kuwa kitu kimoja na kuhakikisha kuwa wote kwa pamoja wanawajengea watoto uwezo wa kijitegemea ili watoto hao wasigeuke kuwa mzigo kwetu endapo hatutawaandaa vema Yesu alijengewa uwezo mkubwa sana na hatimaye akawa Mwalimu mwema alikuwa na wanafunzi 12 maalumu na wanafunzi wengine wengi, aliuitwa RABBI yaani Mwalimu, uwezo wake mkubwa wa kufundisha ulitokana na uwezo wake mkubwa wa kujifunza, kawaulize walimu hakuna Mwalimu mzuri ambaye sio mwanafunzi mzuri, Lazima tuwajengee uwezo wa kielimu watoto wetu

 

e.      Waliwalea watoto wao katika uadilifu

 

Tunasoma hivi katika Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Swali jepesi la kujiuliza je watoto wetu leo na familia zetu leo zinampendeza Mungu na wanadamu? Tunaambiwa Yesu alizidi kukua akiwa na hekima lakini vilevile akimpendeza Mungu na wanadamu, Je tunampendeza Mungu na wanadamu, hii haiwezi kutokea kama hatutakuwa chuo cha maadili kwa vijana wetu, ni muhimu kuwafunza watoto wetu, na kuwalea katika uadilifu, tikifanya hivi tutakuwa na watoto wenye muelekeo thabiti katika taifa letu, leo hii tujnashuhudia mmomonyoko mkubwa waa maadili lakini sababu kubwa ni kuanzia ngazi ya familia kutokujali uadilifu na mwenendo mwema kwa watoto wetu.

 

f.        Walijali Ndugu jamaa na kule walikozaliwa/kulelewa

 

“Human being is a social being” Mungu hakutuuumba tuishi kama kisiwa, aluiposema si vema mtu huyu awe peke yake alimaanisha wanadamu tunahitajiana wakati mwingine ili uweze kujengeka unapaswa kuwa na muda wa kusikiliza wengine na hapo ndipo tunapoweza kujengwa na kukua au kutiana moyo, Mariam alipopata ujauzito wa ajabu malaika alimueleza kuwa jamaa yako  Elizabeth pia ana mimba ya mtoto wa kiume, kusudi kubwa ilikuwa ili Mariamu aweze kutiwa moyo kustahimili kile kilichomtokea hivyo Mariamu alimtembela Elizabeth ona

Luka 1:36-44 “36. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; 37. kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. 38. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake. 39. Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, 40. akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti. 41. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu; 42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. 43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi? 44. Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.


Unaoma Mariamu anamtembelea Elizabeth anajifunza mambo mablimbali kutoka kwa mwanamke mzee mwenye uzoefu wa kutembea na Mungu, na hivyo anajifunza mambo mbalimbali Mariamu kutoka kwa watu wa rika linguine je leo hii wanawake watu wazima huwafunza wanawake vijana ? je watu hutembeleana nyakati  za leo? Je watu hutembelea kule walikozaliwa au kulelelwa familia zenye upendo hutembeleana Yesu pia alitembelea Nazareth kule alikolelewa na kuwafundisha mambo makubwa ya Mungu ona

Luka 4:16-21 “16. Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.17. Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa, 18. Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19. Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. 20. Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21. Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.


Yesu alienda Nazareth kule alikolelewa, Ni muhimu kukumbuka na nyumbani, watu wengi sana wanapofanikiwa hawakumbuki nyumbani, watu wengi wa Tanga waliosoma zamani walitawanyika huko na huko na kusaidia watu wengine na kuwaelimisha lakini waliisahau Tanga,  wabunge wengi  hukumbuka nyumbani wajkati wa kupiga kura, Yesu pamoja na umaarufu wake wote na alikuwa Mungu hakuweza kusahau kule alikolelewa, tunawashangaa wachaga tu wanapoenda nyumbani msimu wa sikukuu, hebu na sisi tujifunze na kukumbuka kuenda kule tulikolelelwa na kukulia na kuwa Baraka kwao pia

Tuwe tayari kujitoa kwa wengine

Kusudi kubwa la Yesu kuzaliwa ni ili awaokoe watu wake na dhambi zao Yusufu alielezwa hili mapema ona

Mathayo 1:20-21 “20. Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.”


Yusufu alielezwa mapema kuwa Yesu ni mwokozi, familia ina wajibu wa kulea vijana na kukuza viongozi ambao watakuwa faida si kwaajili yao tu bali kwaajili ya ulimwengu mzima Mariamu pia alijulishwa kuwa mtoto wake sio wake pekee bali amewekwa kwaajili ya wenginona

Luka 2:34-35 “34. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. 35. Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

  
Ilikuwa wazi kuwa Mungu aliwaamini Mariamu na Yusufu kuwa walezi wa kiongozi mkubwa ambaye atakuwa Baraka kubwa kwa ulimwengu ni mwokozi wa ulimwengu, kama familia hatuna budi kuwatunza wanafamilia wote na kuwasaidia kutimiza ndoto zao ili makusudi yote ya Mungu yapate kutimizwa ndani mwao, nani ajuaye kuwa mtoto uliyembeba ni Raisi ajaye, ni Mwalimu ajayem, ni daktari ajaye, Mungu ana makusudi na kila aliyezaliwa na hakunanayezaliwa kwa bahati mbaya hivyo tuendelee kuwa na ustawi katima familia zetu ili Mungu ajiinulie watumishi wake kutioka katika familia zetu watakaokuwa Baraka kwa wengine

Yohana 13:17 “Mkiyajua hayo heri ninyi mkiyatenda!”

Bwana Mungu awabariki na kuwafadhili tunapoadhimisha siku ya familia takatifu katika jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu amina

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!

0718990796

Ijumaa, 25 Desemba 2020

Mfalme wa Amani!


 Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“      


Utangulizi:

Leo ni sikukuu ya Christmas wakristo kote nchini wanaungana na waktristo wote duniani katika kuadhimisha siku hii maalumu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Masihi, na mwokozi wa ulimwengu, Yesu Kristo kulikotokea huko Bethelehemu Israel zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Katika siku hii muhimu ni muhimu kwetu tukajikumbusha mambo kadhaa kumuhusu Yesu Kristo.

Andiko letu la Msingi  Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“

Kimsingi yalikuwa ni maneno ya nabii Isaya aliyetabiri kuzaliwa kwa mwokozi wa ulimwengu miaka  zaidi ya 700 kabla ya kuzaliwa kwa  Yesu, Isaya anamuona masihi kama kiongozi mkubwa sana na mwenye uwezo mkubwa wa kutatua matatizo na changamoto mbalimbali walizonazo wanadamu, Nyakati za Biblia wafalme ndio ambao walikuwa wanatakiwa kutatua changamoto zozote zilizowakumba watu wao na walipaswa kuwatatulia matatizo yao na kutioa ufumbuzi ona mfano

2Wafalme 6:24-30 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho. Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake. Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.

unaweza kuona kwa hiyo kuwa mfalme halikuwa jambo rahisi, ilikuwa ni lazima uwe na uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu, hata leo viongozi wakubwa wanapotembelea maeneo mbali mbali huzomewa risala na kuelezwa changamoto kubwa mbalimbali zinazowakabili wananchi na wanatakiwa kuzitatua, hapo moja ya wafalme alishindwa kutatua changamoto na kuamua kufunga na kuomba kwa kuvaa magunia maana yake tatizo lilikuwa kubwa sana

Mungu alizungumza na manabii kuwa atakuja kiongozi mkubwa sana atakayetatua changamoto mbali mbali za watu wake sio katika Israel tu bali dunia nzima huyu ndiye masihi, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo tunapaswa kukumbuka kuwa Mungu ametupa kiongozi mwenye uwezo wa kutatua changamoto za aina mbalimbali ulimwenguni na kwa wanadamu wote na huyu si mwingine ni Yesu Kristo.

Isaya anamuelezea kiongozi huyu kuwa ni mwenye uwezo na mamlaka kubwa  na kuwa atatua changamoto nyingi zinazowakabili wanadamu na moja ya changamoto kubwa inayowakabili  wanadamu ni kukosekana kwa amani na utulivu mioyoni mwao na ndio maana Yesu anaitwa Mfalme wa Amani, kwanini mfalme wa amani

Ni muhimu kufahamu kuwa tunapozungumzia amani hii inayozingumziwa katika maandiko;-

Tunazungumziia ustawi, utulivu starehe amani na mafanikio makubwa ya mwanadamu ambayo asili yake ni Mungu, Amani hii ilikuwepo katika bustani ya Eden kabla ya anguko la mwanadamu, lakini baada ya anguko la mwanadamu amani hii ilitoweka Neno linalotumiska kuielezea amani hii katika lugha ya kiebrania ni SHALOM, neno shalom maana yake ni amani na ustawi na mafanikio ya kiunghu katika Nyanja zote, Waaarabu wanatumia neno SALAM,  kwa kiaramu linatumika neno SALEMI, ni maneno yanayofanana sana katika lugha ya kiebrania, kiarabu na Kiswahili, kwa Kiswahili tunalo neno SALAMA  ni hali ya amani, ni hali ya kuwa mbakli na masumbufu, ni hali ya kuwa na utulivu, Daudi alipigana sana vita katika maisha yake yote mpaka Mungu akamuita mtu wa Damu, Lakini mwanaye Suleimani hakukuwa na vita wakati wake, SULEMANI, SOLOMON maana yake ni utulivu na ustawi,  Yerusalem maana yake ni mji wa amani, Dar es Salaam maana yake ni bandari ya amani, jina la mji wa mzizima Dare s Salaam lilitolewa na sultan Baraghash aliyekuwa anatawala Zanzibar na pwani na alitoa jina hilo kwa mji wa mzuizima kwa sababu aliamini badari hii ni mahali salama mno na patulivu

Isaya anazungumzia kuwa masihi anazaliwa duniani kwa kusudi na malengo ya kuleta utulivu kwa wanadamu, utulivu huu ni ustawi wa mwanadamu katika Nyanja zote  na ndio maana siku Yesu alipozaliwa malaika waliimba wimbo huu  kuonyesha kuwa kiongozi mkubwa mwokozi wa ulimwengu atakayetatua matatizo na kuleta majibu na ufumbuzi wote wa mwanadamu amezaliwa na atatoa amani kwa watu wote atakaowakubali

Luka 2:8-18 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;  maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini.  Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.”

Kila mtu anayemwamini Yesu anapewa amani hii moyoni mwake ni amani ambayo hata upatwe na changamoto ya aina gani wewe unakuwa na imani kuwa nitatoka nitatoboa kwa sababu ninaye mfalme ambaye ana uwezo wa ajabu mno anayetoa amani tofauti na jinsi ulimwengu utoavyo  amani anayotupa Kristo ni amani ya pekee nay a tofauti sana ona Yesu anatuachia mani hii Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga. “              

Hatupaswi kufadhaika wala kuogopa kwa sababu Yesu ametuachia mani, na yeye ndiye mfalme wa amani, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaruhusu amani yake itawale katika mioyo yetu na kila mahali hatupaswi kufadhaika kwa jambo lolote tunapokuwa na fadhaa, udhaifu, magonjwa, changamoto na lolote lile ambalo linatuondolea amani yetu, tunaweza kumueleza Yesu Kristo mfalme wa amani yetu na akaweza kabisa kutatua na kushughulikia yala yanayotukanili na kutupa amani ya kweli, Nikutakie sikukuu njema ya Christmas

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Kupimwa kwa kazi ya kila mtu !

1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto” 

 

 


 


 

Utangulizi:

 

 

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu tulionao Mungu alimleta kila mtu Duniani kwa kusudi la kutimiza wajibu Fulani katika maisha yake,  kwa sababu hiyo  siku ya hukumu kila mmoja atatoa hesabu ya kazi au kusudi alilolifanya hakutakuwa na kisingizio kuwa hili linanipata kwa sababu ya Fulani, wote tutatioa hesabu mbele za Mungu na kila mtu atabeba mzigo wake kulingana na kazi au namna alivyotimiza  wajibu na kusudi lake duniani ona.;- 

 

Wagalatia 6:4-5 “Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. 

 

Tutajifunza so mo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

 

·         Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

·         Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

·         Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

 

Kwa msingi huo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anajua ni kwa nini yuko Duniani na amekuja kufanya nini duniani, kisha pambana kwa kila namna uwezavyo kuhakikisha kuwa unafikia lengo na kusudi kubwa la Mungu jkukuleta duniani, Katika maandiko Daudi anatajwa kama mtu aliyeweza kutimiza kusudi au shauri lote la Mungu, hakuondoka duniania akiwa amebakiza kazi fulani alihakikisha kuwa anaitimiza yote yaliyomo katika moyo wa Mungu na hata alitaka kuzidisha!

 

Matendo 13:36 “Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu.

 

Shauri l Mungu maana yake ni Kusudi lote la Mungu, kila mmoja anao wajibu wa kutimiza kusudi lote la Mungu, kuhakikisha kuwa unamaliza vema unahitimisha kazi yako vema, unatenda vema kusudi la Mungu, kama ni kuhubiri ni lazima tuhakikishe kuwa tunahubiri kusudi lote la Mungu, kama ni kuchunga tunachunga kwa kusudi lote la Mungu kama ni kufundisha tunafundisha kama Mungu anavyokusudia, kama ni kusoma tunasoma kama Mungu alivyokusudia, kama ni kuhubiri injili unahubiri kama Mungu alivyokusudia na kama ni kuongoza unaongoza kama Mungu alivyokusudia, Paulo Mtume alipohubiri injili aliweka wazi kuwa aliwahubiria watu kile ambacho Mungu alikusudia na hivyo  alihubiri kusudi lote la Mungu!

 

 Matendo 20:25-27 “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena. Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote. Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.”

 

Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

 

Wako watu mbalimbali katika maandiko ambao wanatajwa kuwa walitimiza makusudi ya Mungu kwa uaminifu na walitioa hesabu na kujifanyia tathimini;-

 

1.       Yesu mwenyewe alijifanyia tathimini na kutoa Ripoti kuwa amemaliza kusudi lote la Mungu, ukiacha kuwa siku ya kusulubiwa kwake alisema IMEKWISHA yaani alitimiza makusudi yote ya Mungu lakini vilevile alitoa hesabu ya kile ambacho baba alikuwa amemuagiza kukitimiza na kwa uhakikika kabisa alikuwa ameyatimiza hivyo kama asemavyo mwenyewe katika  injili ona ;-Yohana 17:1-13 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.  Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika. Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako. Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako; na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.  Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.”

 

2.       Paulo Mtume alihakikisha kuwa ametimiza kusudi lote la Mungu na kwa ujasiri kabisa alimuekleza Timotheo kuwa anasubiri taji yaani thawabu kubwa kwa sababu alikamilisha kile alichokusudiwa na Mungu kwa uaminifu mkubwa kwa mapambano na kwa mwendo mrefu na aliukamilisha  ona 2Timotheo 4;6-8 “Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;  baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”

 

3.       Musa alikuwa mwaminifu katika kazi yote nya Mungu, maana yake alikamilisha jukumu lake duniani, Musa alilitumikia kusudi la Mungu mpaka akasahau kifo, ilibidi Mungu amkubushe kwamba apande kwake mlimani akafe kwa sababu alikuwa mwaminifu mpaka sekunde ya mwisho Waebrania 3:5 “Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;

 

4.       Yoshua alikuwa kiongozi mkubwa jemadari na shujaa alitimiza makusudi ya Mungu hadi  mwisho na kuhakikisha kuwa anaonyesha msimamo wake hata kwa wana wa Israek kuwa yeye na nyumba yake wameamua kwa dhati kuwa watamtumikia Mungu aliye hai ona Yoshua 24:14-18 “Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana. Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine;  kwa maana Bwana, Mungu wetu, yeye ndiye aliyetupandisha sisi na baba zetu kutoka nchi ya Misri; kutoka nyumba ya utumwa; naye ndiye aliyezifanya ishara zile kubwa mbele ya macho yetu, na kutulinda katika njia ile yote tuliyoiendea, na kati ya watu wa mataifa yote tuliopita katikati yao. Bwana ndiye aliyewafukuza watu wa mataifa yote watoke mbele yetu, naam, Waamori waliokaa katika nchi hii; basi, kwa sababu hiyo sisi nasi tutamtumikia Bwana, maana yeye ndiye Mungu wetu.”               

 

5.       Nabii Samuel aliishi maisha ya haki, hakudhuklumu mtu na mbele ya watu wote alijipambanua kuwa hakuwa na tatizo na Mtu he was a man of integrity   alihitmisha akiwa na ujasiri kuwa hakuwahi kumuonea mtu wala kumdhulumu mtu na kuwa alihitimisha akiwa na mikono safi je wewe unahitimisha vipi katika utumishi wako, je watu watakumbuka namna ulivyowaliza? Na kuwaonea na kuwatendea mabaya? Samuel alimaliza vema ona  katika 1Samuel 12:3-5 “Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote. Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi

 

6.       Henoko alikuwa mwaminifu alitembea na Mungu, mwandishi wa kitabu cha mwanzo anamfanyia tathimini Henoko na kumuonyesha kuwa mtu wa tofauti, yeye licha ya kuzaa kama wengine licha ya kuishi maisha marefu alitembea na Mungu kiasi Mungu aliamua kumfanya kuwa malaika

 

Mwanzo 5:8-14 “ Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa. Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani. Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa. Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli. Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa. Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa. Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.  Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.”

 

Hao walikuwa ni baadhi ya watu muhimu katika biblia ambao walijifanyia tathimini katika maisha yao na kutimiza makusudi ya Mungu vema, kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake vema, tukikumbuka na kuelewa ya kuwa tutatoa hesabu mbele za Mungu, katia Nyanja yoyote ambayo Mungu amekuita unapaswa kuhakikisha kuwa unafanya vema, Florence Nightingale mwanzilishi wa uuguzi duniani alisimama vema katika kusudi lake mpaka leo anakumbukwa kwa kazi yake katika siku ya wauguzi duniani,  ni vema kila mmoja akafanya vema, mainjinia wasipunje, viwango vya barabara za lami hata kwa chepe moja la kokoto, Mizani za wafanya biashara ziwe za haki, madaktari na wafanye kwa uadilifu, Walimu wafundishe kwa bidii na wanafunzi wasome kwa bidii ni wakati wa kila mmoja kutimiza wajibu wake vema ili mbele za Mungu anwanadamu tuonekane kuwa na haki na kuepuka hukumu wakati kazi zetu zitakapopimwa!

 

Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Mungu ataipima kazi ya kila mmoja wetu kama lisemavyo neon la msingi, kila mmoja anapaswa kujifanyia tathimini kama anafanya kwa ubora kile ambacho Mungu amekusudia ndani yake, katika hukumu za Mungu ziko hukumu za aina nne Mungu aatakazowahukumu wanadamu

 

1.       Present judgment – hukumu iliyoko sasa kama mtu hajampokea Yesu hajamuamini huyo kwa sasa tunapozungumza ujumbe huu amekwisha kuhukumiwa angalia Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.  Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.” Ili kuepuka hukumu hii basi mwanadamu anapaswa kumuamini Yesu

 

2.       Hukumu ya adhabu Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hukumu hii ni hukumu ya aibu hukumu ya adhabu kwa kiyunani inaitwa KRI MA Mungu atafunua siri zote za uovu za wale wasiomuamini Mungu na wale waliotenda vibaya ona Muhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.” Mungu atafupisha maisha au hata kazi za mtu asiyetenda vema hakikisha kuwa unatenda vema

 

3.       Hukumu isiyo ya adhabu Warumi 8:1 “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hii ni hukumu ya watakatifu, pamoja na neema ya kuingia mbinguni Mungu atamlipa kila mmoja sawa na kazi njema aliyoitenda kazi hizo zitajaribiwa kwa moto  kama ni ya majani, miti na nyasi itateketea na haitaleta heshima kwetu, lakini pamoja na kumuamini Yesu tunapaswa kutenda vema hukumu hii kwa kiyunani inaitwa KRINO ni hukumu isiyo ya adhabu kwa wale walio katika Kristo lakini kazi ya kila mmoja itapimwa, Yesu ataketi katika kiti cha Enzi kiitwacho Bema na kutoa thawabu kwa kazi zetu1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto  

 

4.       Mungu anajua, un predictable judgment hii ni hukumu isiyotabirika   Warumi 14:4 ” Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.“Yeye ni Bwana ana maamuzi yake kama unavyokwenda kwa hakimu anaweza kuamua lolote kama apendavyo mwenyewe hakuna mtu anayejua rehema za Mungu, haiyamkini bwana anaweza kutyangaza rehema kwa mtu, yeyote au hata kwa watu wote kwani utamwambia nini yeye si ndio Mungu? Ndio anaweza kuamua lolote utamfanya nini aliamua utamuuliza nini, Tufanye kazi zetu kwa bidii kwani maandiko yamesema iko thawabu kubwa sana waongoze wengi katika kutenda haki nawe utafaidika!

 

Daniel 12;3  Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Upendo mwingi!

Yoahan 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”



Utangulizi:

Moja ya maagizo ya mwisho kabisa ya Yesu Kristo kwa wanafunzi wake kabla ya kuteswa, kufa na kufufuka ilikuwa ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wake wanakuwa na upendo, wote tunafahamu kuhusu kupenda, lakini Yesu hakutaka tu tuwe tunapenda lakini alitaka wawe na upendo mwingi sana, unaweza kujiuliza upendo mwingi ni upendo wa namna gani? Biblia nyingine za Kiswahili zinatumia neno upendo mkuu, biblia ya kiingereza inatumia neno “The Great love” ambalo ka Kiswahili ni Upendo mwingi au upendo mkuu! Kwanini Yesu anazungumzia upendo mwingi kwani kuna upendo kidogo au mchache ndio kuna upendo kamili “Perfect Love au “sacrificial love” na upendo mwingine wenye upungufu!

Katika Lugha ya kiyunani neno upendo linaelezewa vizuri, sana kwa kuzingatia maeneo manne

1.       Phileo – Huu ni upendo au uhusiano wa kirafiki, unampenda mtu kwa sababu ni rafiki yako mahusiano yenu ni ya kirafiki, upendo huu una mipaka, kwa sababu unaweza kufa unaweza kuharibika ndio maana unaweza kuona watu wanafarakana na wanaweza hata kusalitiana na urafiki ukageuka kuwa uadui mkubwa

2.       Storge – Huu ni Upendo au uhusiano wa kindugu, unampenda mtu kwa sababu ni ndugu yako, mna uhusiano wa damu, uhusiano wa kubaiolojia ni babam ni mama, ni mama mdogo ni baba mdogo, ni binamu, ni shangazi, ni babu, ni bibi na kadhalika upendo huu pia una mipaka na unaweza kuharibika na ndugu wakageuka kuwa maadui wakubwa sana

3.       Eros – Huu ni upendo au uhusiano wa kimapenzi, ni upendo wa asili ya kibinadamu ambao mvutio wake unatokana na mapenzi, so unaweza kumpenda mtu kwa sababu ana usio mzuri, hana malolo, Yakobo alimpenda Raheli kuliko Leah kwa sababu Lea alikuwa na macho dhaifu alikuwa na malolo, unaweza kumpenda mtu kwa sababu ana makalio makubwa, mazito, hips za kutikisa dunia, ana chuchu zilizosimama, saa sita ni mkwaju wa nguvu umbo namba nane, potable au ana mzigo mzito wa kitikisa dunia na kadhalika huu ni upedno wenye hisia za kimapenzi

4.       Agape – Upendo huu sasa ndio unaoitwa upendo mwingi, ni upendo wenye kujitoa sacrificial love , upendo huu ni mgumu kuwa nao, ni watu wachahce sana wanaweza kuwa na upendo kama huu, Yesu aliuita upendo huu kuwa ni upendo mkuu, ni upendo mwingi, unahusisha kupenda mpaka kuyatia maisha yako kwaajili yaw engine Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele upendo huu mtu akiwa nao ndio tunasema amekomaa kiroho, ni upendo ambao una sifa za kipekee 1Wakoritho 15:1-13Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.”

 

Ukomavu wetu wa juu sana Kiroho utajulikana pale tunapokuwa tayari kuyatoa maisha yetu kwaajili ya wengine 

 

Yuda - Mwanzo 44:1-34,·  Alikuwa mwenye upendo mwingi sana alikuwa tayari kufa kwaajili ya kuitunza familia yake na baba yake na kwaajili ya ndugu zake

Daudi - 2Samuel 18:31-33·   alikuwa na upendo mwingi kiasi ambacho alilia kwaajili ya Absalom mwanaye japokuwa yeye alikuwa amekusudia kumuua baba yake

 

Yesu Kristo Yohana 15:13:- “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake· kwa ajili ya rafiki zake”.

 

1. Daktari mmoja wa Uingereza aitwaye Will Pooley alikuwa ni moja ya madaktari waliokuwa mstari wa mbele Nchini “Sierra Leone” huko walikuwa na wenzake wengi wakipambana na wagonjwa wa EBOLA na virusi vyake katika harakati hizo Madaktari wengi sana na Manesi wengi sana wakiwemo wa Afrika Magharibi waliambukizwa virusi vya ebola wakati walipokuwa wakiwauguza wagonjwa na wengi wao walikufa Ugonjwa utokanao na kirusi cha Ebola ni ugonjwa hatari wenye uwezo wa kusababisha kifo kwa asilimia 90. Shirika la afya duniani, WHO katikatovuti yake inasema kwa mara ya kwanza ulibainika mwaka 1976 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan. Chanzo cha kirusi hiki hadi sasa hakijulikani lakini popo aina ya (Pteropodidae) wanaonekana kuwa wabebaji wa kirusi hicho, kwa mujibu wa ushahidi uliopo sasa. Maambukizi hupatikana kwa kila aina ya majimaji yanayotoka katika mwili wa binadamu ni ugonjwa hatari na unaoua kwa haraka na hauna tiba Will Pooley alipoupata ugonjwa huu alirejeshwa katika ndege maalumu na kuanza kutibiwa chini ya uangalizi maalumu huko uingereza Jambo la kushangaza ni kuwa baada ya kupona kwa bahati tu Will Pooley alitangaza nia yake ya kurudi tena Sierra Leone kusaidiana na wenzake kupambana na ugonjwa huo. Mtu huyu aliwashangaza wengi sana na kuwaogopedha wengi sana akiwa amepona kwa asilimia 100%alisema atarudi Africa kusaidia zaidi maana alizaliwa kwaajili ya hayo, jambo hili lilimfanya aandikwe kama shujaa na mwanadamu mwenye uwezo wa kujitoa kwa kiwango cha juu.

 

2. Maximilian Kolbe alikuwa ni Padre aliyetokea Poland aliuawa kama mfungwa tarehe 14 August 14,1941, Jeshi la wa NAZI waligundua kuwa baadhi ya wafungwa wamejaribu kutoroka na hivyo waliamua kuwaua wafungwa kadhaa, walijaribu kuwaua kwa njia mbalimbali, na hivyo walichagua wafungwa 10 ili wauawe na kifo chao kiliamuriwa kuwa kifo cha njaa, wafungwa waliamuriwa kujitoa mmoja mmoja yeye mwenyewe na mfungwa wa kwanza kuchaguliwa alijulikana kama Franciszek Gajowinczek mfungwa huyu alipochaguliwa alilia kwa huzuni kubwa akimtaja mkewe, watoto wake na familia yake na kusikitika kuwa hatowaona tena kutokana na swala hili Maximillian alisimama na kusogea mbele na kuomba afe yeye kwa niaba ya Franciszek ombi lake lilikubaliwa, wafungwa waliwekwa kizuizini kwa muda wa siku kadhaa bila kula wengine walikunywa mikojo yao ili waweze kuishi, Maximillian alikaa kwa wiki mbili bila kufa huku wengine wote wakiwa wamekufa, walimchoma sindano ya kufa hakufa na hivyo waliamua kukata kichwa Pope John Paul II alimtangaza kuwa Mtakatifu kutokana na moyo wake

 

3. Mifano hii inatusaidia kujua kile ambacho Bwana wetu Yesu amekifanya Pale alipojibu kuwa kwaajili ya haya Nalizaliwa alikuwa akimkumbusha Pilato kuwa yeye amekuja kuwafia wanadamu, amekuja kuwaonyesha upendo wa Mungu jinsi ulivyo Isaya 53:1-5 “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani. Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” Huu ni upendo mkubwa sana Yesu alikufa kwaajili yetu, Hatuna budi kuhakikisha kuwa tunasimama upande wake siku zote za maisha yetu, tusihesabu damu yake ya thamani kuwa kitu cha hovyo tudumu katika wokovu na kuwa wavumilivu kwaajili ya Mungu wetu.”

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima