Jumatatu, 24 Aprili 2023

Raha Nafsini mwenu !


Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”




Utangulizi:

Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”

Mojawapo ya maneno muhimu sana aliyowahi kuyazungumza Yesu Kristo ni Pamoja na maneno haya tuliyoyasoma katika kifungu hiki cha maandiko, Mstari huu una maana pana sana na unaweza kutufunza maswala mengi sana, Kwa mwanafunzi wa maandiko anayepita hapa haraka haraka anaweza kupoteza maana muhimu sana inayopatikana katika mistari hii, Leo tutachukua Muda hata hivyo kuangalia kwa undani sana Ahadi ya kumfuata Yesu ambayo matokeo yake ni Kuapata raha nasfini, Kila mwanadamu duniani  anahitaji raha, Mapumziko, au kustarehe na kuondoa msongo wa mawazo, kusoma kwetu, kazi zetu maisha yetu, na lolote lile tunalolifanya hata kumuabudu Mungu kwetu kilele chake ni kuwa na Raha, Duniani na kuwa na raha mbinguni, kwa hiyo kila mmoja anahitaji raha, tutajifunza somo hili kwa kuzingatia maswala kadhaa yafuatayo:-

·         Maana ya neno raha:-

·         Aina tano za raha katika maandiko:-

·         Nanyi mtapata raha nafsini mwenu

Maana ya neno raha:-

Neno raha linalotumika hapa na Bwana wetu Yesu Kristo, linatokana na neno la Kiyunani  “ANAPAUO” ambalo kwa kiingereza ni repose  au rest ambalo tafasiri ya kiingereza ni Freedom from activity, or freedom from daily struggle, Ni hali ya kuwa mbali au kuwekwa huru kutoka katika mahangaiko ya maisha ya kila siku, au usumbufu au msongo au kitu chenye maumivu, au mzigo wenye kuelemea kwa mujibu wa Biblia unafuu huu hauwezi kutolewa na mwanadamu bali unaweza kutolewa na Mungu mwenyewe ona ;-

Kutoka 33:12-14 “Musa akamwambia BWANA, Angalia, wewe waniambia, Wachukue watu hawa; nawe hukunijulisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Walakini umesema, Nakujua jina lako, nawe umepata neema mbele zangu. Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako. Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”

Ushahdi wa kimaandiko unaonyesha kuwa raha hii ni ya kinabii na pia ilikuwa inatarajiwa na watu wengi wa Mungu asili ya hii raha haitokani na mwanadamu bali inatolewa na Mungu mwenyewe  raha hii pia inaitwa utulivu, au starehe  au usalama au amani ya Mungu raha hii inaitwa “Margoa” katika lugha ya Kiebrania

 Yeremia  6:16 “Bwana asema hivi, Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katika njia hiyo.”

Mungu amekusudia kumpa raha kila mmoja kama atakaa katika kanuni zake, na raha hii ilitabiriwa katika maandiko kwa muda mrefu, Bwana ampe neema kila mmoja wetu aweze kuifurahia raha hii katika jina la Yesu Kristo Ameen!

Aina tano za raha Katika maandiko!

Kwa mujibu wa maandiko kuna aina tano za Raha zinazotajwa katika maandiko n azote ni unabii wa raha halisi tutakayoipata mbinguni, rah azote ni za Muda na zina changamoto mbalimbali ukilinganisha na raha ya milele hata hivyo katika raha hizi raha nafsini ni ya muhimu kwaajili ya kustahimili majaribu ya aina mbalimbali tunayoyapitia tukiwa hapa duniani nitazielezea kwa ufupi lakini ndani zaidi nitaizungumzia raha nafsini mwenu!

1.       Raha ya Sabato -  Mungu alikusudia kuwa watu wake wawe na siku sita za kufanya kazi wakipambana na shughuli za kila siku za maisha na siku ya saba walitakiwa kuwa na utulivu ili Mungu aweze kuwahudumia, na kuziganga na kuziponya nafsi zao, lakini waalimu wengi wa kiyahudi walikaza sana sheria ya  Musa na sharia ya sabato na kupata jumla ya sheria 613 zilizopatikana na kuifanya sharia ya Mungu kuwa ngumu mzigo na kongwa la kuwasumbua watu, siku ya sabato yenyewe ilikuwa ngumu, Wayahudi hawakutakiwa kufanya  jambo lolote siku hiyo hata kuponywa kwa wagonjwa siku ya sabato kwao ilikuwa ni tatizo, kuokoa uhai na kuhudumia roho, mwili na nafsi  ya mwanadamu kwa huruma  lilikuwa ni tatizo ona

 

Luka 6:1-10 “Ikawa siku ya sabato moja alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao. Basi baadhi ya Mafarisayo wakawaambia, Mbona mnafanya lisilo halali siku ya sabato? Yesu akawajibu akawaambia, Hamkulisoma hata hilo alilolifanya Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wale aliokuwa nao? Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaitwaa mikate ile ya Wonyesho, akaila akawapa na hao wenziwe, ambayo si halali kuila ila kwa makuhani peke yao. Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato. Ikawa siku ya sabato nyingine aliingia katika sinagogi akafundisha; na mlikuwamo mtu ambaye mkono wake wa kuume umepooza. Na waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone kwamba ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumshitakia. Lakini yeye akayatambua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Ondoka, simama katikati; akaondoka akasimama. Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya; kuponya roho au kuangamiza? Akawakazia macho wote pande zote, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.”

 

Kwa hiyo raha ya sababto haikuwa na manufaa mpaka Yesu Kristo mwenyewe ambaye ndiye Bwana wa sabato alipokuja na kuleta pumziko la kweli, kila raha iliingiliwa na changamoto za kumnyima mwanadamu raha kamili iliyokusudiwa na Mungu.

 

2.       Raha ya Kanaani – Mungu alipowaokoa wana wa Israel kutoka katika nchi ya utumwa kule Misri alikuwa na kusudi kubwa la kuwapa raha, raha hii iliitwa raha ya kanaani, nchi iliyosifiwa kuwa ina wingi wa maziwa na asali,  raha hii aliyepewa jukumu la kuhakikisha anawaingiza katika raha hii ni Yoshua ona :-

 

Yoshua 21:43-44 “Basi Bwana aliwapa Israeli nchi hiyo yote, ambayo aliapa kwamba atawapa baba zao; nao wakaimiliki, na kukaa mumo. Kisha Bwana akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.”

 

Hata hivyo raha hii kwa mujibu wa historia ya kimaandiko inaonyesha kuwa bado wana wa Israel hawakuwa na raha kamili katika ardhi ya kanaani, badala yake walisumbuliwa mara kwa mara na wenyeji wa inchi ile na hivyo hawakuweza kuwa na amani maandiko yanaonyesha ile haikuwa raha kamili iko raha, ayahudi walisumbuliwa mara kwa mara na adui zai, wenyeji wa kanaani, Mungu wakati mwingine aliinua waamuzi ili kuwasaidia katika taabu yao kwa hiyo Raha ya kanaani  inayokusudiwa na Mungu kwa wana wa Israel iliingia dosari na mushikeli na kuwafanya wasiwe na amani ona  kwa hiyo maandiko yalitabiri kuwako kwa raha nyingine ya watu wa Mungu nje ya raha ya kanaani:-

 

Waebrania 4:8-9 “Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye. Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.”             

 

Raha ya kanaani pia ilikuwa ya Muda na Mungu kupitia manabii na watumishi wake alitabiri kuja kwa raha nyingine, Israel hawakupata raha kamilifu katika nchi ya kanaani hata leo!

 

3.       Raha ya ndoa -  ni Neno lililotumiwa na Naomi katika kitabu cha Ruthu kuonyesha kuwa Ndani ya ndoa watu waliooana wakiishi kwa kanuni zilzokudsudiwa na Mungu ndani ya ndoa kuna raha zake, tunafahamu kuwa raha zote hizo ambazo Mungu amekusudia kuwapa wanadamu zina vita lakini hata hivyo ndani ya ndoa kuna raha, kuna raha ya ajabu sana na Naomi  alitamani Ruthu aolewe ili apate raha hii ni raha ya ndoa  Ruthu 3:1 “Kisha Naomi akamwambia mkwewe, Je! Mwanangu, si vizuri nikutafutie raha, ili upate mema?”

 

raha hii inatamaniwa na kila mwanadamu mwenye akili timani, wanawake wote kuanzia umri wa miaka 18 na kuendelea ndoto hii hujengeka kwao ukiacha kuwa na mafanikio mengine wanataka raha, Lakini kama ilivyo kwa raha nyingine shetani anaipiga vita sana Raha ya ndoa na kutaka kuiharibu, ndoa nyingi zinavunjika na makusudia yaliyokusudiwa na Mungu yanaondoka, leo hii watu waovu wantaka kuziharibu ndoa kabisa hata kuleta ndoa zisizo katika mpango wa Mungu ili kuharibu taasisis hii muhimu iliyokusudiwa na Mungu, wana ndoa wakiomba pamoja kunakuwa na nguvu kubwa sana katika maombi na wakizozazna maombi yao yanaharibiwa!

 

4.       Raha ya wokovu – Hii ni raha inayopatikana kwa kumwamini Yesu na kumfanya Yesu kuwa Bwana na Mwokozi, katika mstari wetu wa Msingi Yesu anapotoa Mwaliko wa kwenda kwake kwa wote wanaolemewa na Mizigo na kujivika nira yake hii ilikuwa ni wito wa  wa kumuamini yeye na kupokea wokovu, Raha hii, pia huwapa wanadamu tiketi ya kuingia Mbinguni kwa hiyo tunaweza kuiita raha ya wokovu kama raha ya kuingia mbinguni  na ni raha ya milele

 

Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”

 

Yesu anatoa mwaliko wa starehe na pumziko kwa watu wote wanaomuamini na kwa hakika atawaleta katika wokovu na ukombozi wa mwili nafsi na roho na hatimaye atawaingiza mbinguni kwenye raha ya milele

 

Raha hii ya wokovu na ambayo itatufikisha mbinguni ni raha ya milele na ni raha ambayo itawafutilia mbali maadui wote wa wanadamu ikiwemo kifo na pia Mungu atakomesha uonevu wote na kufuta machozi ya taabu zote za  wanadamu walizokutana nazo duniani ona

Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”

 

Unaweza kupata raha hii sasa kwa kumkubali Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako na kwa kuamini kazi yake yote aliyoifanya pale Msalabani, kwani kwa kupigwa kwake sisi tumepona! Unapomuamini Yesu anaitwaa mizigo yako, anakusamehe dhambi zako unapata raha ya msamaha wa dhambi, Daudi akasema Heri mtu yule ambaye Bwana hamuhesabii dhambi, raha ya namna hii inapatikana kwa kukubali neema ya Yesu na kama umeikubali kamwe usikubali kabisa kumuacha Yesu!

 

5.       Raha nasfi – Raha hii pia kwa bahati nzuri ni raha ambayo Yesu ameitaja pia katika mstari ule ule wa msingi ona Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”

 

Raha hii ni raha inayopatikana pia ndani ya nafsi ya Mwanadamu, kama tutaweka tegemeo letu kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, katika mstari wa Msingi kuna starehe, pumziko linalopatikana kwa kukubali mwaliko wa kumfuata Yesu,  na ambayo pia inatufikisha katika raha ya milele, lakini Yesu anaitaja raha Nasfini mwenu, raha hii inakuja kwa kumfuata Yesu, kujitia nira na kujifunza kutoka kwake raha hii ni raha ya namna gani hilo sasa linatuleta katika kutafakari kiini cha somo letu leo katika kipengele cha mwisho!

Nanyi mpatata raha nafsini mwenu!

Hakuna jambo la msingi duniani kama kuwa na Raha nasfini mwako, hii ni raha ambayo haiwezi kuondolewa na mtu, ni raha anayotupa Kristo mwenyewe na raha hii haijali mazingira wala hali ya hewa ni raha inayopatikana kwa kumtegemea Mungu, kwa kumfanya Mungu kuwa ndio msaada wako na raha hii hata Mungu akuache upite katika shida au mateso haiondolewi na mazingira ya aina yoyote, wanadamu wa kawaida na shetani hawezi kuiondoa raha hii inakaa ndani inakaa nafsini, haiondoki kwa sababu eti ndoa imevunjika, haiondoki eti kwa sababu umeondoka kazini, haiondolewi kwa sababu, eti hauna fedha, haondolewi eti kwa sababu unateswa, hii ni raha ambayo haitikisiki kwa lolote, kwamba umeolewa hujaolewa una raha, kwamba u tajiri au umasikini una raha, kwamba una majaribu au huna una raha ni raha ambayo hata ukipita katika mateso unaweza kujawa na tabasamu na kufurahi,

-          Ni raha  ambayo haisababishi upungukiwe na kitu zaidi ya kukukamilisha ona Yakobo 1:2-4  kwamba Mungu anaporuhusu changamoto za aina yoyote ile wewe wala hauauzuniki unajua ya kuwa unanolewa na Mungu kwaajili ya utumishi uliokusudiwa na Mungu, unakamilishwa na hutapungukiwa na kitu

 

Yakobo 1:2-4 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.”

 

-          Ni raha ambayo hata kama maadui wanakusumbua na kutaka kukutesa au kukudhaklilisha bado hawawezi kufanikiwa kwa sababu wewe unafurahia kuteseka kama Yesu au kwaajili ya Yesu Matendo 5:41-42 “Nao wakatoka katika ile baraza, wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya Jina hilo. Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.” Wakati mwingine hata kama unauawa bado adui zako wakikukazia  macho watauona uso wako uko kama uso wa malaika watu walifikiri wanaweza hata kumuua Stefano na wakadhani kuwa watamfadhaisha lakini walipomkazima macho kutokana na raha ya nasfi uzo wake ukawa kama uzo wa malaika ona

 

Matendo 6:8-15. “Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu. Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano; lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.  Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu. Wakawataharakisha watu na wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza.  Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati; maana tumemsikia akisema kwamba Yesu huyo Mnazareti atapaharibu mahali hapa, na kuzibadili desturi tulizopewa na Musa. Watu wote walioketi katika ile baraza wakamkazia macho yao, wakamwona uso wake kuwa kama uso wa malaika.”

 

-          Raha ya nasfi inatokana na upendo wa Mungu kwetu, upendo aliouonyesha kupitia kumtoa Bwana wetu Yesu Kristo hivyo ukiwa na raha ya nafsi hakuna mazingira,  hakuna mwenye mamlaka, wale malaika wala lolote linaloweza kukutenga na upendo wa Kristo Yesu ataendelea kuwa ni bwana katika mazingira yoyote yale his love never fails at all

 

 Warumi 8: 33-39 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

 

Yesu alikuwa anatambua umuhimu wa raha ya nafsi hii ukiwa nayo, hakuna kitu kitakusumbua duniani, utatoboa katika mazingira ya aina yoyote, na utatoboa katika maneno yoyote na mipango yoyote mibaya, kila mtu anayekusudia kukuondolea raha ya nasfi hatafanikiwa utadunda kila mahali ukiwa na raha moyoni, raha hii inapatikana kwa kumfanya Yesu kuwa tegemeo lako na sio wanadamu!                Tumfuate Yesu tufuate njia yake nasi tutapata raha nsfini mwetu!

 

Nyimbo za injili Namba 73: Ushirika mkuu, Furaha yangu!.

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumanne, 11 Aprili 2023

Baba Mikononi mwako Naiweka Roho yangu!


Luka 23:44-46 “Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda, jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati. Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.”

Utangulizi:

Tunaendelea kujifunza kuhusu maneno ya Yesu aliyoyasema pale msalabani, ambayo yana maana pana sana kama utapata nafasi ya kujifundisha moja baada ya jingine, Leo nataka kuzungumzia kuhusu maneno ya mwisho miongoni mwa maneno saba aliyoyazungumza Yesu pale msalabani ambalo ni BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU!, Maneno haya ni sehemu ya maombi aliyokuwa akiyaomba Bwana Yesu Pale msalabani kwa kutumia Zaburi, yeye alipaza sauti kubwa sana na kuyasema maneno haya na kisha akakata roho, watu wengi sana huyaogopa maneno haya wakidhani ya kuwa ukiyasema basi utakuwa unajitakia kifo, au unaweza ukayasema inapofika saa yako ya mwisho, lakini maneno haya yana maana tofauti kabisa na namna ambavyo wengi wetu tumefikiri kwa siku nyingi, hata hivyo kabla ya kuyafanyia uchambuzi na upembuzi yakinifu ni vema kwanza tukajikumbusha tena maneno mengine katika maneno yote saba aliyoyasema Bwana Yesu Pale msalabani, maneno hayo ni pamoja na :-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Baba mikononi mwako naiweka roho yangu

Kama tulivyoona ya kwamba maneno haya BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU Yalizungumzwa na Bwana Yesu kama maneno ya mwisho pale msalabani na kisha Yesu akakata roho na matukio mengi ya kushangaza yakajitokeza wakati mwana wa Mungu akikata roho, Maandiko haya ya msingi yanatuambia hivi tuone tena:-

 Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu

kimsingi maneno haya yana asili ya Lugha ya kiibrania na yanatoka moja kwa moja katika Zaburi ya 31:5 thelathini na moja, mstari wa tano, Na hivyo kimsingi Mwandishi au waandishi wa agano jipya waliruka maneno muhimu kutoka katika zaburi hii ambayo yana maana pana sana nay a muhimu  linapokuja swala la kufufuka kwa Yesu na sikukuu ya Pasaka, labda waandishi walikuwa na dhana kama yetu ya kufikiri kuwa Yesu alikuwa amevuta pumzi yake ya mwisho ya uhai na kuamua kufa kwa kukabidhi roho yake kwa baba yake, basi. Lakini maneno haya yanasomeka namna hii katika Zaburi yenyewe ya asili ambayo Yesu alikuwa akiinukuu kama maombi pale msalabani  ona -

Zaburi ya 31:5 “Mikononi mwako naiweka roho yangu; Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli.”

Aidha ili ieleweke vema pia zaburi hii katika kiingereza inasiomeka namna hii hasa kwa tafasiri ya Biblia ya kiingereza ya ESV yaani “English Standard Version” yanasomeka hivi Psalm 31:5 “Into your hand I commit my spirit; you have redeemed me, O LORD, Faithful God”, Kwa msingi huo pale msalabani Yesu alikuwa anasali kwa kunukuu Zaburi ya 31:5 akiwa katika hali ya mateso makali mno wakati akiwa katika hali yake ya mwilini duniani akiteseka maneno aliyoyasema Yesu kwa tafasiri ya ESV yalitakiwa kusomeka hivi MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU,UMENIKOMBOA EE BWANA, MUNGU MWAMINIFU, Kwa hiyo utakubaliana nami kuwa kuna maneno ya msingi yalirukwa au yalipoteza maana wakati wa kufanya tafasiri katika lugha mbalimbali, nataka sasa nikuchukue taratibu ili iweze kujua kwa uwazi maneno haya na maana yake namna yalivyo na nguvu kuliko tunavyoweza kufikiri utanielewa tu, kwanza tuangalia neno NAIWEKA kwa undani kisha tuunganishe na maneno yaliyorukwa katika Luka 23:46 na kuyaona kwa uhalisia wake katika Zaburi 31:5

Usemi huo unakubaliana wazi kabisa na Lugha za kiibrania na kiyunani ambapo neno NAIWEKA ROHO YANGU kwa kiingereza “I COMMIT” katika lugha ya Kiibrania linatumika neno “AFKID” na kiyunani neno “DIAPRATO”, Neno la kiibrania AFKID kwa kiingereza linasomeka kama “I DEPOSIT” ambalo Kiswahili chake ni kuweka amana au kuacha kitu cha thamani kubwa mfano fedha kwa mtu au taasisi unayoiamini kwa kusudi la kuja kuchukua kitu hicho baadaye, mfano ni kama vile tunavyoweka fedha zetu bank na kisha tunakuwa na haki au uhakika wa kuzichukua wakati wowote unaona!, na neno la kiyunani “DIAPRATO” kwa kiingereza “ENTRUST” ambalo maana yake kukabidhi jukumu Fulani muhimu kwa mtu unayemuamini kuwa atalifanya, atalinda na kukuwakuilisha salama, Hatakuangusha. Kama Neema ya Mungu itakuwa imefunuliwa kwako sasa utakuwa umefahamu kuwa  Yesu aliposema BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU, kama alinukuu Zaburi 31:5 Basi Yesu alikuwa akisema maneno haya “BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA AMANA ROHO YANGU, UMENIKOMBOA EE BWANA, MUNGU MWAMINIFU.

Hii maana yake ni nini maana yake Yesu alipaza Sauti yake kwa imani pasipo shaka akatamka kwa uhakika kuwa anaiweka Roho yake amana kwa Mungu mwaminifu na ambaye anaweza kumrejeshea na sio anaweza kukaa nayo jumla jumla, Yesu aliamini katika uweza wa baba yake ya kuwa anauweza wa kuirejesha Roho yake tena na sio hivyo tu yeye mwenyewe anauwezo wa kuichukua atakapokua anaitaka kama wewe unavyoweza kuchukua fedha zako kutoka katika bank wakati unapotaka, Hii maana yeke ni kuwa Yesu kristo aliutoa uhai wake yeye mwenyewe  na hakuna mtu anayeweza kumuondolea uhai, lakini licha ya kuutoa mwenyewe yeye pia anauwezo wa kuutwaa tena uhai wake au roho yake, Aidha tunajifunza kuwa maneno yale yalikuwa na maana ya kuiweka roho yake kwa muda tu, na kisha ataichukua tena, kwa hiyo kukata roho kwa Yesu kulikuwa ni kwa muda na kuwa angafufuka tena !

Yohana 10:17-18 “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.”

Kwa msingi huo Yesu alimaanisha kuwa hakuna anayeweza kuuondoa uhai wake hapa inajumuisha kila kitu mbinguni na duniani hakuna anayeweza kuiondoa uhai wake, kifo cha Msalabani ilikuwa ni hiyari yake mwenyewe kwaajili ya kuwakomboa wanadamu na ndio maana anapendwa na baba  kwa sababu hakuna aliyemshurutisha, Yesu anayo mamlaka ya kuyatoa maisha yake na anayo mamlaka ya kuyachukua tena, hivyo ni kwa hiyari yake mwenyewe kwa kawaida yeye humuheshimu baba yake, na hafanyi neno Bila kuagizwa na baba hasa alipokuwa Duniani neno linasema:-

Yohana 5;19  Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile.”

Yesu anazungumza hii katika hali ya ubinadamu wake hali ya kumtegemea baba yake akiwa duniani, hali ya kujinyenyekeza, lakini neno lake baba mikononi mwako naiweka roho yangu linatufungulia akili kujua uweza na mamlaka kubwa aliyonayo Yesu Kristo, lakini linatuthibitishia kuwa alikuwa na uhakika wa kufufuka!

Yesu hakufa kama afavyo mchuuzi, ulikuwa ni mpango wake kamili wa kumuokoa mwanadamu, mpango ambao baba wa mbinguni alifurahishwa nao, kwa mamlaka hii, tunaweza kukabidhi chochote kwake, na anauwezo wa kuturejeshea, kama kuna vitu tulipokonywa au kuumizwa au kuibiwa au kudhulumiwa vyovyote iwavyo tunaye Yesu mwenye uwezo wa kuturejeshea maradufu yeye anauwezo wa kufisha na kuuhisha, anajeruhi na anaponya, nani yeye mwenye uwezo wa kuokoa hivyo kama kuna kitu kimepotea katika maisha yetu iwe amani, furaha na kadhalika Huyu Yesu anauwezo mkubwa ana mamlaka kubwa yeye ni Mungu na anajitambulisha kuwa hakuuawa isipokuwa ilikuwa kwa hiyari yake ni sadaka aliyojitoa yeye anauwezo wa kuutoa uhai wake na kuuchukua tena na anaweza kufanya hivyo na lolote kwa yeyote akimtumainia yeye, Maandiko yanasema!  

Kumbukumbu 32:39 “Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi; Naua Mimi, nahuisha Mimi, Nimejeruhi, tena naponya; Wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu,”

Hakuna jambo la Msingi kama kukabidhi maisha yetu, mali zetu, ndoa zetu, kazi zetu, watoto wetu, waume zetu, wake zetu, mashamba yetu, magari yetu, afya zetu, na lolote lila katika mikono salama ya baba wa mbinguni ambaye tunajua anaweza kulinda kile tunachiomkabidhi, hakikisha kuwa katika maisha yako unamkabidhi Mungu mwaminifu maisha yako kwa sababu yeye anauwezo wa kutunza, kulinda na kukurejeshea kila kinachopotea ni kwa Mungu pekee ndipo tunapokuwa na uhakika wa kurejezewa kila kilichopotea endapo kweli katika maisha yetu tulimkabidhi yeye, watu wengi wamekabidhi maisha yao na mali zao kwa watu mabaradhuli na wakapoteza Yesu anatukumbusha kuwa ukijikabidhi kwa Mungu mwaminifu hakuna cha kupoteza ! ni muhimu wakati huu wa msimu wa Pasaka kukabidhi maisha yetu kwa Mungu mwaminifu yeye atayarejesha tena yatakapopotea kwa sababu yoyote ile, tukiamini kazi aliyoifanye Yesu Msalabani hakika yeye naye atatufufua siku ya mwisho

Yohana 6:53-54 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.”

Na Rev Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima!



Imekwisha !


Yohana 19:28-30Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu. Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani.  Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, IMEKWISHA. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.




Utangulizi:

Mojawapo kati ya usemi wenye maana sana kati ya semi saba za Yesu alizozisema akiwa msalabani na ambazo zinatajwa katika sehemu mbalimbali za injili, moja ya usemi huo wa muhimu ni usemi wa sita wenye Neno IMEKWISHA  ambalo leo katika siku ya pasaka tutachukua muda kulijadili kwa undani na kupata maana iliyokusudiwa, maneno mengine kati ya maneno saba aliyoyasema Yesu msalabani ni pamoja na:-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Maana ya neno IMEKWISHA

Ni muhimu kufahamu kuwa Neno IMEKWISHA ambalo katika kiingereza kiingereza linasomeka “IT IS FINISHED  katika Biblia ya kiyunani yaani Kigiriki linasomeka kama “TETELESTAI  Neno hili ndio neno la Mwisho kabisa katika maneno aliyoyatamka Yesu pale msalabani kabla ya kutamka neno “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu” na kufariki dunia pale msalabani, Neno hili Imekwisha TETELESTAI limetokana na neno TELEO la kiyunani ambalo maana yake ni Kukamilisha kazi, kumaliza kazi, kutimiza kazi, to complete or to accomplish, neno hili lina umuhimu mkubwa kwa sababu linazungumzia kumaliza kazi kwa furaha, au kwa mafanikio, utamu wa neno hili ni kama vile mtu anapokuwa amemaliza mtihani wa mwisho katika kozi ya mwisho, au mtihani wa mwisho kabisa wa kumaliza shule au chuo au kama vile mtu aliyekamilisha malipo ya mwisho ya ununuzi wa nyumba au gari, au kukamilisha kwa usahihi kile ulichowaza au kufikiri kuwa utakifanya na ukakifanya kwa usahihi kabisa, Kama vile Mungu alivyosema tazama kila kitu kimekuwa chema, well done, kazi imefanyika kwa ufasaha.

Lakini ni muhimu kufahamu kuwa neno hili IMEKWISHA liko katika wakati uliopita kwa namna linavyoonekana hapa  lakini katika kiyunani ni sentensi kamili Perfect tense na kwa sababu hiyo neno hili linapata umuhimu mkubwa kwa sababu lina maanisha imekwisha katika wakati uliopita, uliopo na ujao kwa msingi huo neno hili linaendelea kufanya kazi kila siku na kila wakati, Neno hili pia lilimaanisha kuwa kama kulikuwa na deni, basi deni hilo limelipwa milele, wale wamuaminio Yesu hawana wanachodaiwa, kama ilikuwa ni kesi imefutwa na hati za mashitaka zimeharibiwa kabisa Wakolosai 2:14-15 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo”.Neno hili ni kama kupewa ruhusa kutoka hospitalini baada ya kuugua kwa muda na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kila mtu akijua umekwisha kisha ukainuka tena ukiwa mzima wa afya. Ni neno muhimu sana katika kazi ya ukombozi wa mwanadamu na wokovu wetu.

Umuhimu wa neno IMEKWISHA.

Yesu alipolia kwa sauti kuu IMEKWISHA alimaanisha katika wakati uliopita, sasa na itaendelea kuwa imekwisha hata baadaye. Kumbuka kuwa hakusema nimekwisha hii ingemaanisha kuwa ameshindwa na kifo, lakini alilia akisema IMEKWISHA! maana yake nimeikamilisha kwa ufasaha kazi niliyokuja kuifanya. Kwa msingi huo neno imekwisha lina maana ya hakuna kilichosazwa katika kazi ya ukombozi aliyokuja kuifanya na hivyo alikuwa akizungumza ukweli kuwa kila kitu kimekamilishwa sasa ni mambo gani Yesu aliyakamilisha yako mengi mno lakini baadhi ni pamoja na:-

1.       Alikamilisha kazi yote aliyokuwa ametumwa na baba yake kuja kuifanya duniani Yohana 17:4 “Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.

2.       Alikamilisha kazi ya kuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea Luka 19:10 “Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”

3.       Alikamilisha kazi ya kutukomboa sisi na adui zetu Luka 1:68-74 “Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa. Ametusimamishia pembe ya wokovu Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake. Kama alivyosema tangu mwanzo Kwa kinywa cha manabii wake watakatifu; Tuokolewe na adui zetu Na mikononi mwao wote wanaotuchukia; Ili kuwatendea rehema baba zetu, Na kulikumbuka agano lake takatifu; Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu, Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu,

4.       Alikamilisha unabii katika torati na manabii uliozungumza kumuhusu yeye kwa unabii, ishara, alama na vivuli kuhusu ujio wake na kazi zake kutoka kitabu cha Mwanzo mpaka kitabu cha Malaki ambako kuna nabii zaidi ya 300 kuhusu Masihi Mwanzo 3:15 na Isaya 53

Kwa msingi huo hatupaswi tena kuteseka, kuwa watumwa, kukandamizwa, kuonewa, kuugua na kuteswa na magonjwa, kuwa watumwa wa dhambi na shetani, hatupaswi kumuogopa awaye yote, Nguvu za giza, na wachawi na washirikina na waganga, na mapepo na majini na mashetani na shetani hazina uwezo juu yetu kwa imani katika kazi aliyoifanya Bwana Yesu pale msalabani, laana ya torati, na sheria, hatuna deni, hatuna deni la jana wala la leo wala la kesho kazi imekamilika yakikutokea majanga angalia msalaba kumbuka kazi iliyofanyika msalabani, kumbuka kuwa mwanaume huyu amemaliza amakamilisha kazi ya ukombozi huna hatia hata kidogo hakuna wa kukuhukumu, wewe hata kama ulikuwa na historia mbaya sana yeye anawweza kuifuta na kuiandika upya endapo utamwamini Bwan Yesu, Neno imekwisha ni neno lenye nguvu kama vile siku unapotangazwa uhuru wa taifa lililotawaliwa na wakoloni, tunapoadhimisha siku ya kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo yaani katika siku hii ya pasaka ni lazima tujikumbushe kuwa Yesu amekamilisha kazi ya kutuweka huru na kuvitangazia vifungo vinavyotuzunguka kwa kuvitangazia kuwa imekwisha, Mateso yamekwisha, kazi za shetani zimekwisha, majini na mapepo kazi zao zimekwisha kila aina ya vifungo na utumwa wa ibilisi ni lazima zisikie na kukumbuka kuwa imekwisha

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Naona Kiu - Nina kiu!

 

Yohana 19:28-30 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, NAONA KIU. Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani. Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.”


Utangulizi

Hivi karibuni Wakristo wote duniani tunaingia katika moja ya Majuma muhimu sana katika kukumbuka mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye aliteseka na kufa kwaajili yatu pale msalabani, Katika wakati huu moja ya maswala ya msingi ambayo huwa tunayakumbuka kwa Pamoja ni pamoja na maneno ya Yesu Kristo pale Msalabani wakati alipokuwa anateseka, kwa ujumla katika injili zote nne unapokusanya maneno yote aliyoyatamka Yesu kabla kidogo ya kukata roho ni Pamoja na maneno haya saba ya mwisho ambayo wakristo huyachukulia kwa uzito mkubwa, Moja ya maneno ambayo tutayatafakari kwa pamoja leo ni pamoja na neno Naona kiu, au Nina kiu,ambalo ni neno la tano katika manenio hayo muhimu, Pamoja na neno hili, lakini maneno yote saba aliyozungumza Kristo ni Pamoja na :-

1.       Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

2.       Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

3.       Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

4.       Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

5.       Naona kiu au Nina kiu Yohana 19:28

6.       Imekwisha Yohana 19:30

7.       Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Tutajifunza somo hili Naona kiu au Nina kiu kwa kuzingatia maswala mawili ya msingi yafuatayo:-

·         Maana ya neno KIU

·         Naona kiu

Maana ya neno Kiu.

Neno kiu kwa kiingereza THIRST ni hali ya  kuhisi au kutaka kunywa kitu Fulani na hasa maji, ni Hali yenye msukumo wenye nguvu wa kutaka kutimiza kitu au jambo Fulani, hali hii wakati mwingine kama ni katika mwili wa mwanadamu inatokana na umuhimu wa mwili kuhitaji maji, kutokana na umuhimu wake na pia kutokana na joto au ukavu Fulani unaojitokeza katika mwili, Neno hilo Kiu katika biblia ya kiyunani linasomeka kama “DIPSAO” kimatamshi  “DIP – SAH – O” Ambalo maana yake kiu halisi au kiu ya jambo Fulani  (to thirst for LITERALLY or FIGURATIVELY) Kwa hiyo Yesu alipozungumza kuhusu kiu kimsingi inaweza kuwa ilikuwa kiu halisi ya kutaka kunywa maji au kiu ya kutaka kuyatimiza mapenzi ya Mungu, nani wazi kuwa kiu aliyokuwa nayo Yesu haikuweza kutimizwa na dunia kwani badala ya kumpa maji wao walimpa divai, na sifongo jambo lililopeleka Yesu kutokunywa, kwa kuwa hiyo haikuwa kiu yake sahihi, Leo tunapotafakari kiu aliyokuwa nayo Yesu Msalabani ni Muhimu kula mmoja wetu kujihoji ana kiu  ya namna gani na je kiu yake inaweza kutimizwa na dunia au inaweza kutimizwa na Mungu? Kiu ya Yesu ilitimizwa na Mungu na haikuweza kutimizwa na wanadamu! Marko 15:23 “Wakampa mvinyo iliyotiwa manemane, asiipokee.” Kile alichokitamani Kristo katika shauku na kiu yake hakikuwa kile ambacho dunia imempa, Mungu atupe neema ya kuweza kutimiza kiu sahihi tuwapo ulimwenguni katika jina la Yesu!

Naona kiu!

Yohana 19:28 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.”   

Moja ya namna ya kuadhimisha Pasaka ni pamoja na kukumbuka Mateso na siku ya mateso ya Bwana wetu Yesu ambayo yametuletea ukombozi, katika siku ile ya mateso Kristo alizungumza maneno Saba muhimu sana katika maisha ya kila Mwanadamu, Katika maneno hayo saba Neno Noana kiu ndio neno la Msingi sana na kiini kikubwa sana cha Mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo na katika uhitaji wa Mwanadamu wakati tunapopitia mateso kutoka kwa wanadamu wenzetu huku tukiwa na lengo la kudumisha uhusiano wetu na Mungu!, Hapo ndipo Kiu ya kila jambo tulilonalo inapokutana na shida na changamoto mbalimbali,  maneno yote sana yana umuhimu wake na kila moja lina ujumbe wake ingawa leo tutalipa uzito neno la Tano NAONA KIU ;-  bila kupuuzia jumbe katika maneno mengine:-

1.       NENO LA MSAMAHA – Tunapopitia katika wakati Mgumu hasa unaosababishwa na wanadamu wenzetu hatuna budi kufahamu kuwa wakati huo wao wanaona kuwa wako sahihi katika lile wanalokufanyia nan i wewe ndio unaonekana kuwa mkosaji, wakati hio wao huwa dhaifu sana na wewe unayepelekwa matesoni ndio unapaswa kuonyesha ukomavu hivyo kwaajili ya mafanikio Yako samahe – Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo

2.       NENO LA UHAKIKA – Wakati tunapopitia mateso tunapaswa kukumbua ya kuwa wako watu wanaoona umuhimu wetu, na bado wanatutegemea wana wanapaswa kuhakikishiwa kuwa wanakuwa na wakati mzuri hata pamoja na kuteseka kwetu au kuteseka pamoja nao, wahakikishie ya kuwa Mateso ni njia ya kutupeleka katika hali iliyo bora zaidi – Leo hii utakuwa pamoja nani peponi

3.       NENO LA HESHIMA – Wako wale wanaodhalilika unapodhalilika, wako wanaoteseka unapoteseka wako wanaokutegemea ni muhimu kwetu kufahamu kuwa Yesu alikuwa anategemewaa na Ndugu zake na wazazi wake, wakati akiwa katika mateso alitaka kuhakikisha kuwa wazazi wake wanakuwa salama na hivyo alikabidhi Majukumu ya usimamizi wa familia kwa mwanafunzi aliyeaminika kuwa anaweza kumsaidia – Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako

4.       HALI YA UPWEKE – Kila mwanadamu anahitaji kuwa na watu wa kumtia moyo, upweke ni moja ya changamoto kubwa sana kwa mwanadamu hasa anapokuwa mtu mzima lakini zaidi sana tunapopitia katika mateso, wanadamu kwa kawaida hudhani ya kuwa Mungu amemuacha  hsusani anapopita katika magumu au anapokuwa amelemewa na dhambi, - Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha

5.       NAONA KIU – kiu inawakilisha kiini kikuu cha mateso, kila mwanadamu anateseka kwa sababu ya kiu, kila mwanadamu ana kiu anayotaka kuiona inatimizwa katika maisha yake, Kwa bahati mbaya wakati mwingine kiu zetu huharibiwa na watu wenye nia mbaya ambao wanataka kuona kiu yetu ikitimizwa kwa mlango mwingine, Yesu Kristo katikati ya mateso na katika kilelel cha mateso alijisikia kiu bila shaka ilikuwa ni kiu nzuri kiu ya maji safi lakini tunaambiwa watesi walimpa siki badala ya maji, jambo lililopelekea yeye kukataa kunywa Mathayo 27:33-34 “Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa, wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.” Dunia haita kubali utimize kiu yako, na wakati mwingine utapewa  kitu mbadala kinyume na kiu yako, na kama kiu yako imetoka katika kwa Mungu ni dhahiri kuwa dunia haitakubali uitimize kiu hiyo na badala yake watataka unywe kitu kingine Kiu ya Kristo ilikuwa ni kuwakomboa wanadamu na kuona kuwa watu wote wanaishi kwa amani huku yeye akiwa ni mfalme wa amani, lakini badala yake Dunia ilimfanyia mambo mengine, katika wakati huu tulio nao ni lazima tuwe wakali ili kwamba kiu yetu sisitimizwe kwa njia nyingine, Mapenzi ya Mungu yasikataliwe, Baraka za Mungu zisigeuzwe kuwa laana,

-          Wengi walikuwa na kiu ya kuolewa na kuoa ili wawe na amani katika ndoa zao lakini dunia imewapa machungu badala ya amani

-          Mungu alikusudia tuishi kwa furaha na amani lakini leo hii dunia imewapa vilio na mateso kiu yao ya kuwa na furaha duniani imeharibiwa badala ya maji wamepewa sifongo

-          Wengi wamelima na kupanda wakitarajia mvua itanyesha wapate mazao, lakini dunia imewanyima mvua na imawapa ukame na hali ya uchumi imakuwa sio

-          Mungu alikusudia dunia iwe kama paradiso ka ma watu wangeitunza lakini watu wameharibu mazingira  na hatimaye leo dunia inashuhudia mabadiliko mabaya ya hali ya hewa na ukiharibika kwa anga linalozuia miali mikali ya jua kutufikia moja kwa moja Ozone layer, kuongezeka kwa hewa ya ukaa na hali joto ma mabadiliko makubwa

-          Dunia ilitarajiwa iwe ni sehemu ya ustaarabu, uadilifu na yenye kutunza utamaduni lakini leo tunashuhudia uharibifu mkubwa wa ustaarabu na mmomonyoko mkubwa wa uadilifu, kuharibika kwa tamaduni zenye manufaa na badala yake dunia leo inataka kuwe na ndoa za jinsi moja na kuzalishwa kw agenda ya tatu isiyo ya kiume wala ya kike, Haya pamoja na mambo mengine ni uharibifu wa kiu ya Yesu Kristo unaofanywa na wanadamu

-          Mungu alikuwa na kiu ya kuona haki ikitendeka na dunia ikifanikiwa kila mahali, maana haki huinua taifa lakini dhambi ni aibu ya taifa zima, leo hii wote tunashuhudia haki ikipindishwa kwa rushwa na upendeleo na hukumu zikipotoshwa huo nao ni uharibifu wa kiu ya Mungu

-          Wewe una kiu gani na dunia imekupa maji ya namna gani? Hatuna bhudi kujiweka katika neema ya Mungu na kumuomba Mungu atufanikishe ili kiu yetu na kiu yake isiharibiwe katika maisha yetu tuwapo duniani

6.       KILIO CHA USHINDI – Imekwisha, Yesu alitimiza majukumu yake yote duniani kwa ushindi mkubwa TETELESTAI  Neno hili Imekwisha TETELESTAI limetokana na neno TELEO la kiyunani ambalo maana yake ni Kukamilisha kazi, kumaliza kazi, kutimiza kazi, to complete or to accomplish, kila mmoja wetu analo jukumu la kutimiza awapo duniani

7.       KILIO CHA UTII – baba mikononi mwako naiweka roho yangu, Yesu alitii mambo yote ambayo Mungu alikuwa amemuagiza ayatende, usikubali kuondoka duniani bila kutimiza ndoto ambazo Mungu amekukabdihi uzitimilize

Hitimisho!

Kwa hiyo unapoangalia maneno haya saba ya Bwana wetu Yesu Krist utagundua kuwa yote yana umuhimu mkubwa sana lakini neno la tano lina umuhimu mkubwa sana katika swala zima la matarajio ya mwanadamu na kile ambacho dunia inatupa kwa msingi huo basi usalama wetu na kutimia kwa kiu yetu vinaweza kupatikana kwa Mungu mwenyewe

-          Mathayo 5:6 “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa” Kama kiu yetu itakuwa ni ya haki na bila shaka hii ni kiu yenye kutaka kuyatimiza mapenzi ya Mungu basi kiu hiyo itatimizwa

-          Yohana 7: 37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.”  Yesu anatoa mwaliko wa kila mtu mwenye kiu aje kwake anywe unaona ni dhahiri kama kiu aliyoisema Yesu ingekuwa kiu HALISI literal Maandiko yasingeweza kuzungumza katika hali kama hii haba ni uhitaji wote wa kimwili na Kiroho Dunia haiwezi kututimizia kiu halisi tuliyo nayo Lakini Yesu anaweza na ametyuahidi kuwa atatimiza hivyo kiu yetu atatupa maji halisi tunywe

Ni maombi yangu kwako katikka pasaka hii kuwa Mungu akutane na kiu yako hamu yako na shauku yako inaweza kutimizwa na Yesu aliyegharimika kufa kwaajili yako pale Msalabani

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima!


Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

 

Mathayo 27:46 - 49. “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya. Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha. Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”


Utangulizi:

Leo tutachukua Muda kujifunza kwa undani mojawapo ya maneno Muhimu katika maneno yaliyosemwa na Yesu Kristo wakati wa Mateso yake pale msalabani MUNGU WANGU MUNGU WANGU MBONA UMENIACHA, tunataka kujifunza maana ya maneno haya kwa kina na kuangalia uhalisia wa ubinadamu hususani wakati wanadamu wanapopitia mateso, Pamoja na menono haya muhimu, tutakayoangalia leo maneno mengine kwa mfululizo katika maneno saba aliyozungumza Kristo pale msalabani kwa mujibu wa injili zote nne ni pamoja na :-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Maana ya Maneno Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha?

Mathayo 27:46 “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”

Ni muhimu kufahamu kuwa Mwandishi wa kitabu cha Mathayo anajaribu tu kufupisha kile ambacho Yesu Kristo alikisema na pia anajaribu kutafasiri lugha kiaramu ambayo Yesu aliitumia wakati anazungumza maneno hayo. Maneno hayo Eloi, Eloi, Lamasabakthan, katika lugha ya asili yanasomeka kama Eli, Eli, Lama Sabachthan ni sehemu ya maneno kamili ambayo Yesu aliyazungumza ka lugha ya kiaramu, maneno hayo yanatafasirika hivi Eli, (Adonai) Eli (Adonai) Lama (Why?) kwanini ?, mbona? Sabachthani (You have left, Abandoned) me) Umeniacha.  Kimsingi ni kuwa katika kini cha mateso yake Yesu Kristo alikuwa anatimiza na kumuomba Mungu sawa na Zaburi ya 22:1-22 ambapo katika Zaburi hii Daudi ambaye alipendwa sana na Mungu alikuwa akimuomba Mungu kutokana na Mapito aliyokuwa akiyapitia ambayo kimsingi pia yalikuwa ni mapito ya kinabii yaliyohusiana na Yesu Kristo Mwenyewe Mwana wa Daudi, Kumbuka kuwa Yesu alikuja kutimiza maandiko ambayo torati na manabii na maandiko yote yaliweka bayana kuwa Masihi hana budi kuteseka 

Luka 23:13- 27 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. Macho yao yakafumbwa wasimtambue. Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao. Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo; tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona. Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.”

Unaona kimsingi Yesu alikuwa ameandikiwa kila atakalokuja kulitenda na kulinena katika Torati, Manabii na Zaburi au maandiko hivyo Neno Mungu wangu Mungu wangu ilikuwa ni nukuu ya Zaburi ya 22 ambayo ina mukhtasari wa Mateso ya Bwana Yesu yaliyotabiriwa na Daudi katika zaburi hiyo hebu tuyaangalie tuweze kuona 

Zaburi 22:1-20 “Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha. Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli. Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa. Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike. Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.  Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi. Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga; Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma. Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu. Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho. Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura. Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.”

Kimsingi maombi ya Daudi na Maombi ya Yesu Kristo yanafanana na hatujawahi kuona wakati wowote Mungu akimuacha Daudi au akimuacha Yesu Kristo lakini kwanini walilia maneno hayo na kuomba dua hizo wakati wa mateso yao ilihali wote tunajua kuwa maandiko yanamsifia Daudi kama mtu aliyeupendeza Moyo wa Mungu ona

Matendo 13:22 “Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.”

Aidha katika namna kama hiyo Mungu katika neno lake vilevile anajivunia Kristo Yesu mwanae kama mtu aliyeupendeza moyo wake ona

Mathayo 3:16-17 “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake; na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.”

Inawezekanaje Mungu kuwaacha awapendao? Mungu anatujali sana katika kiwango ambacho hata mama anaweza kumsahau mtoto wake lakini sio Mungu wetu ona

Isaya 49:15-16 15. “Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe. Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima. Kimsingi kila mwanadamu anapokuwa na mafanikio watu”               

Mungu wetu anatujali mmno lakini katika hali ya kawaida kila mwanadmu anapopitia mateso na changamoto za aina mbalimbali kwa kawaida wanadamu wana tabia ya kuwa mbali nawe wanatabia ya kukuacha ubaki peke yako na wakati huu Mungu hukaa kimya ili mateso yale yaweze kuleta somo linalokusudiwa kwako hivuo kibinadamu zinakuweko fikra ya kuwa huenda Mungu amekuacha, Ayubu alipokuwa na mafanikio makubwa sana tunaambiwa watu wengi sana walimwendea na nyumba yake ilijaa watu wa kila aina maandiko yanasema na watu wa nyumbani wengi sana ona

Ayubu 1:3 “Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, NA WATU WA NYUMBANI WENGI SANA; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.”

Tunaambiwa kuwa wakati wa mateso yake Ayubu watu wote waliokuwa nyumbani mwake walimkimbia mpaka pale Ayubu alipobarikiwa tena ndio tunaelezwa kuwa watu wote wakamwendea ona

Ayubu 42:10-12 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza. Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja. Basi hivyo Bwana akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu, na punda wake elfu.”

Ni swala la kawaida kwamba wakati wa mateso watu wanakukimbia na mara kadhaa inadhaniwa kuwa Mungu amekuacha nani kilio cha kawaida Pale mtu anapopita katika magumu kufikiri mkuwa ni Mungu ndiye aliyemtendea hayo, Ndio maana Daudi alilia katika Zaburi ya 22 japo ilikuwa pia ni unabii kw Mwanaye Yesu Masihi ambaye naye alilia akijua ya kuwa anaitimiza Zaburi ya 22 yote alitioandikiwa humo yalitokea siku ya mateso yake maneno mabaya , kugawanywa kwa nguo zake kwa kuzipigia kura, kugomelewa mikono yake na miguu yake msalabani, kudharauliwa na kuwekwa katika mikono ya watu wabaya wapate kumdhihaki, na kumdhalilisha, Kifo cha Msalabani hakikuwa kifo cha kawaida kilikuwa ni kifo cha maumivu ya kila aina kisaikolojia na nafsi na mwili Yesu ni kama alikuwa amabaki pake yake msalabani, saa ya kujaribiwa huwa ni kama tunabaki peke yetu, kundi kubwa la watu waliofaidika na huduma yake hakuna hata mmoja aliyeweza kusogea na kufanya utetezi wakati Masihi alipokuwa anateseka Msalabani na ndio maana akaisema zaburi ya 22 ambayo hutambulika zaidi kwa Mstari wake wa kwanza Mungu wangu Mungu wangu mbiona umeniacha!

Msalabani Yesu hakuwa ametundikwa kwa sababu nya dhambi yake ilikuwa ni kwaajili ya dhambi zetu mimi na wewe, nani mimi na wewe ndio ambao tulipaswa kuyabeba maumivu yale, lakini Mwokozi alibeba kwa niaba yetu na kilio kilikuwa kwa ajili yetu na ubinadamu wetu, alilia kuonyesha kuwa wanadamu wakati wote tunahitaji msaada wa Mungu na kuwa peke yetu hatuwezi, adui yetu yu aweza kufanya jambo lolote la kutuumiza sana kama tutabaki bila msaada wa Mungu, Mtu mmoja aliimba wimbo unasema nafikiria ukiniacha roho yangu itakuwaje Bwana ? itakuwa ni mawindo ya adui kwa wepesi sana… wakati wote tunapokuwa na maisha yetu bila ya Mungu tunajiweka katima hatari ya kushambuliwa na kuumizwa na ibilisi, magonjwa matesi na dhiki za dunia hii, lakini ashukuriwe Mungu kuwa pale msalabani Yesu Kristo alikuwa anateseka kwaajili yatu na kwaajili ya ukombozi wetu ili kuukaribisha uwepo wa Mungu katika maisha yetu

Isaya 53:4-5 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!