Ijumaa, 30 Desemba 2022

Ikawa mwisho wa Mwaka!


2Nyakati 24:23 - 25Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.” 



Utangulizi:

Yosia alikuwa mfalme wa Yuda aliyetawala kati ya mwaka wa 640-609 Kabla ya Kristo, jijini Yerusalem, Ni mtawala aliyeingia madarakani akiwa kijana mdogo sana, Yeye ni mwana wa Amon Mwana wa Manase ambao kimsingi walikuwa wafalme waovu mno katika wafalme waliowahi kutawala Israel ya Kusini, Lakini hata hivyo Yosia alikuwa mfalme mwema sana na aliyemcha Mungu! Yeye alitawala akiwa na miaka 8 baada ya kuuawa kwa baba yake. Mfalme huyu alikuwa mcha Mungu na alitenda yaliyo haki mbele za Mungu!

2Wafalme 22:1-2 “Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi. Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.”

Wakati wa utawala wake alifanya kazi kubwa sana ikiwa ni pamoja na kuchangisha fedha za ujenzi na ukarabati wa Hekalu nyumba ya Mungu ambayo ilikuwa na nyufa kutokana na kutokujaliwa na watu wakati wa utawala wa babu yake na baba yake, Kuhani Hilikia aligundua vilevile kitabu cha torati ambapo alipomsomea mfalme alirarua mavazi yake na kutubu, kisha kuwaita watu wote wapate kuitubu na kumgeukia Mungu, walifanya agano kuwa watamtumikia Mungu kwa mioyo yao yote kwa ujumla kulikuwa na uamshi mkubwa sana wakati huo

2Wafalme 23:1-25 “Kisha, mfalme akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu. Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana. Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile. Kisha, mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni, akayachukua majivu yake mpaka Betheli. Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. Naye akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni, akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu. Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera. Akawatoa makuhani wote katika miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba, tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa mtu langoni pa mji. Walakini hao makuhani wa mahali pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate isiyo na chachu katikati ya ndugu zao. Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki. Akawaondoa farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani; akayapiga moto magari ya jua. Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni. Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi. Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu. Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli, madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera. Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo. Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria. Na nyumba zote pia za mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli. Akawaua na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu, akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu. Naye mfalme akawaamuru watu wote, akasema, Mfanyieni Bwana, Mungu wenu, pasaka, kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano. Hakika yake haikufanyika pasaka kama hiyo, tangu zamani za waamuzi waliowaamua Israeli, wala katika zamani za wafalme wa Israeli, wala za wafalme wa Yuda. Bali katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia ilifanyika pasaka hii kwa Bwana ndani ya Yerusalemu. Tena wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana. Kabla ya huyo hapakuwa na mfalme mfano wake, aliyemwelekea Bwana kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na sheria zote za Musa; wala baada yake hakuinuka mmoja mfano wake yeye.”

Unaona ni wakati wa Yosia kwa kweli kulikuwa na uamsho mkubwa sana kila kitu cha kipagani kiliharibiwa na kila aina ya miungu iliyoabudiwa iliharibiwa, alifukuza na kuharibu wenye pepo wa utambuzi, makhanithi na wachawi, anasifika kuwa alikuwa mfalme mwema ambaye kbla yaka na baada yake hakuwahi kutokea!

Sababu kubwa ya mafanikio ya Yosia

Uwezo mkubwa na uadilifu mkubwa alioupata Yosia ulitokana na malezi mazuri na thabiti kutoka kwa kuhani mkuu maarufu sana aliyeitwa Yehoiada kuhani huyu alikuwa mwaminifu na aliweza kutumika kwa miobgo kadhaa chini ya wafalme wa Yuda, Kuhani huyu alioa dada wa Mfalme Ahazia, mwaka mmoja kabla mfalme Ahazia hajauawa, Athalia mama wa mfalme alishikwa na tamaa ya madaraka na kuamua kuua watoto wote wa kifalme na kila mtu aliyeonekana na ushawishi wa kiutawala, baada ya adhima yake hiyo kufanikiwa alijitangaza kuwa mtawala ona

2Wafalme 11;1-3 “Na Athalia, mama yake Ahazia, alipoona ya kuwa mwanawe amekufa, akainuka, akawaharibu wazao wote wa kifalme. Ila Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu, umbu lake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia, akamwiba miongoni mwa hao wana wa mfalme waliouawa, yeye na mlezi wake, na kuwatia katika chumba cha kulala; wakamficha usoni pa Athalia, basi kwa hiyo hakuuawa. Alikuwako pamoja naye, amefichwa nyumbani mwa Bwana, miaka sita. Naye Athalia akaitawala nchi.” 

Yehosheba na Mumewe Yehoiada walimficha kijana pekee aliyeponyoka katika sakata hilo ambaye ni Yosia na walimlea vizuri na ilipotimia miaka sita yaani ya kufichwa kwake hii ikiwa na maana alifichwa akiwa na miaka miwili sasa Yehoiada alifanya mpango wa kumtyawaza Yosiah kuwa Mfalme wa Yuda  ona

2Wafalme 11:4-17. “Hata mwaka wa saba Yehoyada akatuma, na kuwaleta wakuu wa mamia, wa Wakari, na wa walinzi, akawaleta kwake ndani ya nyumba ya Bwana; akapatana nao, akawaapisha nyumbani mwa Bwana, akawaonyesha huyo mwana wa mfalme. Akawaamuru, akasema, Hili ndilo neno mtakalolifanya; theluthi yenu, mtakaoingia siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya mfalme; na theluthi mtakuwapo mlangoni pa Suri; na theluthi langoni nyuma ya walinzi; hivyo mtayalinda malinzi ya nyumba, kuzuia watu wasiingie. Na sehemu mbili zenu, yaani, wote watokao siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya Bwana kumzunguka mfalme. Mtamzunguka mfalme pande zote, kila mtu mwenye silaha zake mkononi; naye awaye yote aingiaye ndani ya safu auawe; mkafuatane na mfalme, akitoka na akiingia. Nao wakuu wa mamia wakafanya sawasawa na yote aliyowaamuru Yehoyada kuhani; wakawatwaa kila mtu watu wake, hao watakaoingia sabato, nao watakaotoka sabato, wakaja kwa Yehoyada kuhani. Naye yule kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao zilizokuwa za mfalme Daudi, zilizokuwamo nyumbani mwa Bwana. Walinzi wakasimama, kila mtu na silaha zake mkononi, kutoka pembe ya kuume ya nyumba mpaka pembe ya kushoto ya nyumba, kando ya madhabahu na nyumba, wakimzunguka mfalme pande zote.Ndipo akamleta nje mwana wa mfalme, akamvika taji, na kumpa ushuhuda; wakamfanya mfalme, wakamtia mafuta; wakapiga makofi, wakasema, mfalme na aishi. Na Athalia alipoisikia sauti ya walinzi na ya watu, aliingia kwa watu nyumbani kwa Bwana; akatazama, na tazama, mfalme amesimama karibu na nguzo kama ilivyokuwa desturi, nao wakuu na wapiga baragumu karibu na mfalme; na watu wote wa nchi wakafurahi, wakapiga baragumu. Ndipo Athalia akararua mavazi yake, akalia, Fitina! Fitina! Naye Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, majemadari wa jeshi, akawaambia, Mtoeni kati ya safu; naye ye yote amfuataye mwueni kwa upanga. Kwani kuhani akasema, Asiuawe nyumbani mwa Bwana. Basi wakampisha njia; akaenda kwa njia ya kuingia kwa farasi nyumbani mwa mfalme; akauawa huko. Kisha, Yehoyada akafanya mapatano kati ya Bwana na mfalme na watu, ili wawe watu wa Bwana; tena kati ya mfalme na watu.” 

Unaona chini ya uangalizi wa Yehoiada, Mfalme Yosia aliweza kutawala vema na kwa mapenzi ya Mungu, kumbuka kuwa ni yeye na mkewe ndio waliomsaidia na kumuongoza na kuuondoa utawala wa malikia na kumrudisha mfalme katika kiti cha Enzi cha baba zake kama ilivyokuwa kwa mapenzi ya Mungu kwa Daudi, kupitia kuhani mkuu huyu inchi ikawa na amani na watu wakamcha Mungu mno, Yosiah katika wakati wote wa kuhani mkuu aliweza kufanya vizuri, Mfalme alikuwa na ushawishi mkubwa, aliwaongoza watu kumrudia Bwana kila mtu aliitii sharia ya Mungu, jambo hili lilimfurahisha Mungu sana na klilikuwa Baraka kubwa sana kwa kila mtu, maandiko yalikuwa yamepuuzwa kabisa lakini alipokuwa mfalme Heshima ya kimaandiko ilirejea, watu wote wenye kutoa dhabihu mbaya za watoto na kila aina ya uovu iliharibiwa kabisa kwa ujumla alikuwa mfalme ambaye aliushawishi moyo wa Mungu na Mungu alimsikiliza ona

2Wafalme 22:19 “kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana.”

Ikawa mwisho wa Mwaka!

Pamoja na uzuri aliokuwa nao Mfalme huyu ambaye aliifanya kazi nzuri wakati wote wa uongozi wa kuhani mkuu Yehoiada ambaye aliishi miaka 130 kuhani huyu mkuu aliheshimika na watu wote kutokana na ushauri wake mzuri kwa Mfalme na watu wake alikuwa amejaa hekima ya kiungu hata hivyo jambo la kusikitisha ni kuwa baada ya kifo chake Yosia alibadilika moyo na kuanza kuwa na washauri wabaya ambao walirudisha tena ibada ya baali na maashera ona

2Nyakati 24:17-20 “Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao. Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao. Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza.”

Mungu alipeleka manabii mbalimbali kwaajili ya kuwaonya hata hivyo hawakukubali, wala hawakuwasikiliza, Hata hivyo Kuhani mkuu Marehemu Yehoiada alikuwa na kijana aliyeitwa Zekaria ambaye Roho Mtakatifu alikuja juu yake ili aweze kuwaonya, Nabii Zekaria bin Yehoiada aliwaonya kuwa kama wanamuacha Bwana ni dhahiri kuwa Bwana naye atawaacha hata hivyo hawakutaka kusikia maonyo na badala yake walipanga mpango wa kumuua ona Na mfalme Yoashi alimuua zekaria akasahau wema wote ambao mama yake na baba yake walimfanyia hili lilikuwa jambo la kusikitisha sana ona

2Nyakati 24:20-22 “Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi. Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana. Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi.”

Wakati Zeakaria anauawa alikumbuka wazi mema yote ambayo baba yake alimfanyia mfalme Yosia ni ukweli usiopingika kuwa Yosia alikuwa mtu asiye na shukurani hakulipa mema na badala yake alilipa mabaya Zekaria alimuomba Bwana wakati anauawa akasema  BWANA AYAANGALIE HAYA AKAYATAKIE KISASI, ni ukweli usiopingika kuwa Mungu wetu hujilipia kisasi wakati watu wanapokutendea yasiyopaswa wewe uwe na uvumilivu tu kwa dhambi hii aliyoifanya Yosia ukweli haikuchukua muda tangu wakati ule iluipofika mwisho wa Mwaka Bwana akajilipizia kisasi ndio maana tunasoma IKAWA MWISHO WA MWAKA ona

2Nyakati 24:23-25. “Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.”  

Hitimisho

Inawezekana wako watu umewawaidia lakini wamekugeuka, inawezekana umedhulumiwa, na watu hawataki kukulipa inawezekana umetukana, inawezekana umeonewa, leo nataka nikupe habari njema ya kuwa yuko Mungu anayelipa kisasi, kama maandiko yasemavyo ni haki mbele za Mungu kuwaluipa kisasi wale wanaowaonea ninyi

2Wathesalonike 1:6 – 9 “Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake;”

Mungu anao wakati wake wa kujilipizia kisasi dhidi ya wale wote wanaokuonea na kukutesa, kila unapopitia uonevu unayo haki ya kumwambia Mungu liangalie na hili ukalitakie kisasi na Mungu mwenyewe atausbiri wakati wake na wakati mwingine itakuwa mwisho wa Mwaka, ikawa nmwisho wa Mwaka, ikawa mwisho wa Mwaka, ikawa mwishio wa Mwaka Mungu alijilipizia kisasi dhidi ya Yosia aliyemuua Zekaria ili hali baba yake alimtendea mema hakuna sababu ya kuogopa kila aina ya uonevu katika maisha yako italipwa mwisho wa mwaka, umeonewa wewe kumbuka ikawa mwisho wa mwaka, umekopwa hujalipwa wewe kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka, umekataliwa, mumeo au mkeo ameibiwa, ikawa mwiho wa Mwaka, umedhulumiwa paka kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka  IKAWA MWISHO WA MWAKA   

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima!

Jumapili, 25 Desemba 2022

Kuokolewa katika mikono ya Herode!

 


Mathayo 2:12-16 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize. Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu. Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.”



Utangulizi.

Moja ya  wafalme aliyekuwa katili sana na mroho, mwenye tamaa na mbinafsi na muongo alikuwa ni mfalme Herode mkuu, kwa ujumla alikuwa ni mfalme mwenye kutisha sana, ni katili na muuaji aidha ni mwenye dhuluma, Huyu alikuwa tofauti sana na mfalme wetu Yesu Kristo, ambaye alikuja kwaajili ya ukombozi wa wanadamu, wakati Herode alikuwa na mpango wa kuangamiza na kuua, Mfalme Yesu alikuja na mpango wa wokovu, Herode alikuwa na mpango wa mateso, Yesu alikuja akileta matumaini na upendo, Herode alikuwa ni mkatili mwenye chuki na mwenye mpango wa kuangamiza, Kristo alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea tena alikuja ili watu wawe na uzima tena wawe nao tele, Katika wakati huu wa kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo hatuna budi vilevile katika wakati huu kujikumbusha Mambo ya msingi na ya muhimu yanayoyakabili maisha yetu na kisha kupata hekima ya kiungu namna ya kuokolewa katika mikon ya adui zetu.

Yesu alizaliwa wakati ambapo mfalme muovu na adui wa maisha yake alikuwa anatawala na mfalme huyu aliposikia habari kuwa Yesu Kristo amezaliwa ni ukweli ulio wazi kuwa badala ya kufurahi alifadhaika sana ona

Mathayo 2:1-3 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.”

Mfalme Herode aliita baraza la wazee wa kiyahudi na wakuu wa makuhani na kufanya uchunguzi wa kina, na sio hivyo tu aliwahoji mamajusi na kutaka kujua kuwa ni kwa muda gani na wakati gani sahihi mtoto huyo atakuwa amezaliwa kufuatia mwenendo ya nyota waliyoiona nani wapi, na zaidi ya yote alitaka aletewe habari kamili kuhusu huyo mtoto kwa kusudi la kutaka kumuangamiza ona

Mathayo 2:4-8 “Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi? Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii, Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli. Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota. Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.”

Ni muhimu kufahamu kuwa roho ya Herode inatenda kazi hata leo, katika ulimwengu wa kisiasa, makazini, duniani na hata makanisani, katika nyakati hizi za mwisho hatuna budi kuhakikisha kuwa wakati wote tunaendenda kwa hekima sana kwani hali halisi ya kiroho ya watu wengi imebadilika sana, wauaji wakubwa kabisa, wenye chuki, waharibifu, wabambikiaji, wasingiziaji, wenye siasa chafu, wachawi na watu wenye wivu wenye uchungu nyakati za leo hawako nje ya kanisa bali sasa wako ndani ya kanisa na hata madhabahuni, tunazungukwa na mbwa mwitu wakali huku wewe na mimi tukiwa kama kondoo tu, Bila kuweka tumaini letu kwa Mungu ni rahisi sana kujeruhiwa, kuumizwa na kutendewa kila aina ya ubaya na hata kuuawa kwa njia za ajabu au kuwekewa sumu, na watu ambao wala hatukuwahi kudhani kuwa wanaweza kuwa wasaliti na wenye kupingana na mpango wa Mungu katika maisha yetu, hali inatisha sana kwa sasa, watu wanatuma mpaka watu watushambulie, wako watumishi wa Mungu ambao sasa wamekuwa wachawi hata wokovu sijui waliuacha lini, wako washirikina pia hali inatisha hata hivyo Mungu aliye hai yuko macho na bila shaka atakuokoa na kila mpango mbaya wa ibilisi na maajenti wake katika maisha yako na yangu!

Herode alikuwa ni mtu wa namna gani?

Herode ambaye pia alijulikana kama Herode mkuu alikuwa ni mtawala wa Israel iliyokuwa chini ya utawala wa Warumi, Kimsingi yeye alizaliwa mwaka wa 72 kabla ya Kristo na kwa asili alitokea maeneo ya Idumeya yaani Eneo la Edomu wana wa Esau, Yeye na ukoo wake waliwekwa kuwa watawala vibaraka kwa niaba ya utawala wa warumi, Mwanzoni yeye alitawala Galilaya na uyahudi kabla ya utawala wa watoto wake watatu ambao waligawana majimbo baada ya kifo chake na Herode Akleo akatawala Idumeya, Uyahudi na Samaria na Herode Antipas alitawala Galilaya na Philip alitawaka huko Jordan, Kwa mujibu wa mwanahistoria maarufu wa kiyahudi wa  karne ya Kwanza Josephus, Herode mkuu alikuwa ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa sana ambaye ili kuongeza ushawishi wake alimuoa binti wa kuhani mkuu wa kiyahudi Kayafa na pia wakati wa utawala wake alilikarabati Hekalu la pili la Yerusalem na  kuliongezea eneo mlima wa Hekalu kwa upande wa kaskazini, Jambo lililopelekea yeye kukubalika na Wayahudi wengi.  Hata hivyo pamoja na umaarufu wake mkubwa hivyo ni jambo la kushangaza ya kuwa alipozaliwa Yesu Kristo Mfalme huyu alifadhaika na kugadhibika na ili aweze kujihakikishia usalama wake alihakikisha kuwa anawaua watoto wote wapatao miaka miwili kule Bethelehemu ili yamkini aweze kumuua Yesu Kristo ona

Mathayo 2:16 “Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.”

Unaweza kuona Herode alikuwa ni mtu mwenye ghadhabu, mbinafsi na aliyekuwa hataki upinzani, alitamani kuwa yeye katika madaraka wakati wote, alitamani kuwa yeye abaki kuwa maarufu wakati wote, alikuwa mtu katili aliweza kuua watoto wote ili kujihakikishia usalama wake ni jambo la kusikitisha kuwa hii roho ya Herode ni roho inayotenda kazi katika nyakati zetu na katika kanisa la leo, Mara ngapi tumesikia viongozi wakubwa na maarufu wakiwaua wengine kisiasa na kuwachafua wengine kwa skendo za kutengeneza ili yamkini waweze kubakia wao tu madarakani, au wao tu waonekane kuwa ni safi na wenguine waonekane kuwa hawafai, au kuharibu umaarufu wa wengine  na wao tu waweze kuwa maarufu, hujawaona watu wenye kila kitu na wenye nguvu zote lakini wakifukuzana na watu masikini wasio na kitu wala nguvu yoyote wakitaka kuwazima ili yamkini wabakie wao tu hii ni roho chafu na mikono mibaya ya Herode, roho ya Herode ni roho ya watu wenye uchungu, hasira na tama mbaya wakiwa wamejawa na ubinafsi wa kila aina ni roho ya watu ambao hawawezi kufurahi nyota za wengine kung’aa lakini pamoja na hayo Bwana ana ujumbe muhimu leo Usiogope Bwana amenituma nikupe ujumbe huu kama nabii wake na kama malaika wake leo nakuletea habari njema ya kuwa wakati Herode anataka kusababisha misiba katika jamii, Mungu atakunusuru wewe na atakulinda na kukupa mlango wa kutokea mpaka atakapokufa Herode, Bwana atakuficha katika mikono yake nawe utakuwa salama hutaogopa madamu Mungu anakukubali, leo ziko habari njema kwaajili yako ona Yesu amezaliwa kwaajili yako na yeye ni mwokozi sio wa mtu mmoja tu wa ulimwengu mzima na hivyo amani inapaswa kutawala duniani kwa kila mtu ambaye Bwana ana mridhia najua wewe na mimi Bwana anaturidhia   

Luka 2:8-17 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.”

Kwaajili ya hayo ni imani yangu nani mpango wa Mungu ya kuwa pamoja na changamoto unazozipitia katika huduma, kazini ndoa na maeneo mengine Mungu hatimaye atatuokoa na mipango mikakakati ya heriode katika maisha yetu

Kuokolewa katika mikono ya Herode !

Mathayo 2:12-15 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.  Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.”

Kila mtu mwenye mapenzi mema Mungu ana mpango mkakati ulio mwema na maisha yako na kwa jinsi Mungu alivyomwema anatuwazima mem, Mungu hana mpango wa kusababisha maombolezo katika maisha yetu wala hana malipizi anayotulipiza kwaajili ya maovu yetu, Mungu ni mwema mno yeye anatuwazia mema hana kisasi juu yetu yeye sio mwanadamu ana mpango mwema na mahususi kuliko mpango alionao Herode wako na wangu ona ;-

Yeremia 29:11-13 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza. Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote..”       

Vile adui zako na zangu wanavyotuwazia sivyo Mungu anavyotuwazia nataka kuanzia Christmas hii uweze kuelewa kuwa hakuna adui anayeweza kusimama mbele yako na kupingana au kushindana na mapenzi ya Mungu yaliyowekwa ndani yako, kila baya linalokusudiwa na adui dhidi yako Mungu ataligeuza kuwa Baraka, kila adui anayekutafuta akuangamize ataangamiza wengine na wewe utajikuta umefichwa; msomaji wangu nataka nikuhakikishie yakuwa ujumbe huu ni halisi katika maisha yako hakuna wa kukupata, hakuna atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako sio kwa Herode huyu tu lakini kwa kila mkono wa Herode yeyote atakayeinuka juu yako Mungu atakuokoa na mikono yake, wakati wa Petro alikuweko herode mwingine aliyaangamiza maisha ya Yakobo mtume na akataka kumuangamiza na Petro, lakini Mungu akawa mwaminifu akamfungua Petro kutoka katika mikono ya Herode Mungu huyu huyu atakufungua na wewe   atakuweka huru na Herode wako atatokwa na roho Hakuna herode aliyewafuatilia watu wa Mungu na kuwatesa na kuwaua ambaye  alibaki salama, Herode aliyetaka kumuua Yesu alikufa Yesu akiwa amefichwa Misri na herode aliyemuua Yakobo alipotaka kumuua Petro Mungu aklituma malaika wake ona

Matendo 12:1-23 “Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi. Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba. Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.  Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango. Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake. Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu. Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine. Hata kulipopambauka askari wakaingiwa na fadhaa nyingi, amekuwaje Petro. Na Herode alipomtafuta, asimwone, aliwauliza-uliza wale walinzi, akaamuru wauawe. Kisha akatelemkia kutoka Uyahudi kwenda Kaisaria, akakaa huko. Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme. Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.”

Hitimisho.

Ujumbe wangu wa Chrismas hii ni unabii, ni ujumbe ambao sio tu wa sikukuu hii lakini ni ujumbe wa maisha ya siku zote wote wanaoonewa na watu wenye nyadhifa zilizokubwa kupita wao wasiogope ni ujumbe wa matumaini na kukutia moyo ya kuwa Mungu yuko na anaifuatilia mipango ya Herode na ata shughulika naye ni ujumbe wa maonyo pia kama una roho ye herode lazima utubu na kubadilika Mungu hawezi kufurahia udhalimu, kusudi lake ni pana mno na yuko tayari kulilinda kusudi lake kwa gharama yeyote wewe sio wa Muhimu kuliko wanaochipukia uwe na roho ya malezi walee wengine na kuwainua na kuwaunga mkono usijidhanie ya kuwa uko mwenyewe au kuwa wewe ndiwe maalumu sana kwa Mungu, kujenga hekalu hakutakusaidia, kuoa mtoto wa kuhani mkuu hakutakusaidia, kuwa na wapelelezi hakutakusaidia, kuwa na jeshi hakukusaidiaa kitu Mungu wetu ni mwenye Nguvu na hekima yake ni kubwa kuliko hekima ya kibinadamu, hii ni Chrismas ya wokovu nani ya habari njema kwa wote wanaoonewa na maonyo  makali kwa waonevu! Kamwe asitokee mtu akashindana na kusudi la Mungu lililoko ndani yako kwani atapotea kama walivyopotea wakina herode na kusudi la Mungu ndilo litakalosimama.

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Ijumaa, 18 Novemba 2022

Fikirini Maua ya Mashamba!


Mathayo 6:28-32 “Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo. Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.


Utangulizi:

Katika moja ya hutuba yake nzuri na ya muhimu maarufu iama hutuba ya Mlimani, Yesu Kristo anatumia mfano wa Ndege wa angani na Maua ya kondeni, kutengeneza hoja za kifikra akilini (logic of comparison) kuonyesha namna Mungu anavyowathamini wanadamu kuliko ndege wa angani na maua ya kondeni na kama Mungu anaweza kujali sana vitu hivyo vidogo mno katika uumbaji wake basi kwa hakika anawajali sana wanadamu ambao ni kilele cha uumbaji wake, na ambao ameutawaza juu ya kazi zake zote

Zaburi 8:4-8 “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima; Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. Kondoo, na ng'ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni; Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini.

Katika nyakati za leo wasomaji wengi wa neno wanaweza wasielewe au isiingie akilini kwanini Yesu alitumia mfano huu na je watu wa nyakati zake waliweza kumuelewa?

Kwanini maua ya mashamba?

Kal Vahomer ni kanuni ya siri ambayo Yesu aliitumia, Neno la kiibrania KAL VAHOMER ni neno linalohusiana na kanuni ya kiualimu iitwayo kutoka wazo dogo kwenda wazo kubwa au kutoka wazo rahisi kwenda wazo gumu From minor to the Major au from simple to Complex hii ilikuwa ni moja ya kanuni iliyotumiwa na walimu wengi wa nyakati ya karne ya kwanza, kulikuwa na kanuni kama saba walizotumia marabi wa kiyahudi kutafasiri maandiko au mafundisho na KAL VAHOMER ilikuwa ni mojawapo kutoka jambo dogo kulinganisha na jambo Kubwa, kama Mungu anajali maua je si zaidi au je hatazidi, mtondo huu pia Yesu aliutumia katika sehemu nyingine za mafundisho yake au maneno yake mfano

Luka 23:31  Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

unaona kwa msingi huo ujengaji wa hoja alioutumia Yesu hapo unafanana na ule ujengaji wa hoja alioufanya katika mfano wa maua ya kondeni, ikiwa wanautendea mti mbichi hivi, itakuwaje kwa mti mkavu?, yaani kama mwenye haki anatendewa mambo kama haya itakuwaje kwa mtu asiye haki? kwa hiyo hapa yesu tena alitumia kanuni ya ufundishaji iliyoitwa KAL VAHOMER ambayo ilikuwa imeenea wakati huo na ilikuwa ya Muhimu sana Kwa hiyo ilikuwa ni rahisi kwa jamii ya nyakati za karne ya kwanza kuweza kuelewa jambo hili.

Fikirini Maua ya Mashamba!

Kimsingi Yesu Kristo alikuwa anazungumza na kundi la watu wa chini sana waliokuwa masikini na hata kufikia ngazi ya kukosa mahitaji yao ya kila siku kama chakula na mavazi ambayo kimsingi ni mahitaji ya msingi sana ya mwanadamu, Kristo anataka kuwaondoa watu hawa katika mawazo ya kufikiri kuhusu chakula na mavazi na kutaka kuwatia moyo waache kuhofu kuhusu hayo na badakla yake wamtegemee Mungu, kuhofu au kuogopa ni ibada, kama mtu atakuwa anawaza ale nini au avae nini mawazo yake yataelekea katika kuitumikia fedha ili apate mahitaji yake, Yesu anataka tuwe na imani tuisjisumbue, anataka kutujengea uwezo wa kuamini  kwamba Mungu anatujali sana kama maua hayafanyo kazi yoyote na Mungu huyavika na kuyafanya yapendeze sana hata kuliko fahari ya Sulemani, ikiwa Mungu huyavika maua kwa fahari kubwa ingawa kimsingi hayana maisha marefu ukilinganisha na mwanadamu lakini maua hayaogopi na kama Mungu anaweza kuyafanyia hivyo maua hashindi kutufanyia sisi wanadamu mahitaji yetu Maandiko yanatufundisha ya kuwa Mungu anajishughulisha sana na mambo yetu

1Petro 5:6-7 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. 

Kimsingi umasikini hauko katika chakula mavazi tu Yesu alizungumzia hayo kutokana na hadhiranya watu wa wakati ule ambao wengi walikuwa masikini, inawezekana katika jamii ya leo tukawa chakula na nguo kwetu sio jambo la kuhofia lakini watu wanahofia kodi za nyumba, wanahofia ada za shule za watoto, wanahofia mikopo ya chuo, wanahofia marejesho ya vikoba, weanahofia magonjwa na changamoto mbalimbali, wanahofia kupanda kwa bei za bidhaa kama mafuta na vyakula, wanahofia mmomonyoko mkubwa wa maadili, ziko fedhea na mizigo ya aina nyingi sana ambayo inaumiza watu katika maisha haya haya yote tunapoyaleta kwa Mungu wetu ambaye anatujali sisi kuliko anavyojali maua na ndege wa angani uwezekano wa Mungu kukutana na mahitaji yetu na kutuondolea hofu ni mkubwa kuliko hofu yenyewe

Mathayo 11:28-30 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Yesu anataka tuiweke mbali hofu ya aina yoyote katika maisha anataka kutupa Pumziko yeye mwenyewe ameonyesha ya kuwa kuhofia hakuwezi kutuongezea kitu hakuwezi hata kuongeza lisaa limoja la uhai wetu Luka 12:25 “Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja? unaiona kwa msingi huo maandiko yanatuonyesha ya kuwa tunapoogopa tunapokutana na hofu watakatifu waliotutangulia hata katika hali ngumu na duni na stresses za maisha wao bado  waliweka tumaini lao kwa Mungu

Zaburi 118:5-7 “Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.”

Kwa msingi huo hatupaswi kuhofia jambo lingione lolote na badala yake tuaxchie kila kitu katika mahitaji yetu kijulikana na Mungu, Mungu anawalisha ndege wa anagali na kuyavisha maua mavazi ya rangi mbalimbali za kupendeza na hayafanyi kazi yoyote wala hayana maisha marefu lakini kama Mungu anaweza kuyajali kiasi kile ni wazi na upana ya kuwa Mungu anatujali sisi kuliko tunavyoweza kufikiri, kwa msingi huo kila amwaminiye Mungu hapaswi kuishi kwa hofu na wasiwasi tumwamini Mungu kwa mahitaji yetu yote ya kiwmili na kiroho naye atashughulika maua hayafanyi kazi lakini afadhali sisis tunafanya kazi na Mungu katika mapenzi yake tukimtegemea na kumuomba atatujibu sawasawa na kuhitaji kwetu kwa mapenzi yake

Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!     

Jumatano, 16 Novemba 2022

Jinsi ya kuwa Adui wa Roho Mtakatifu!


Isaya 63:9-10Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale. Lakini wakaasi, wakamhuzunisha Roho yake Mtakatifu; kwa hiyo akawageukia, akawa adui, akapigana nao.”


Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu wetu ni mwingi wa rehema huruma na neema, Sifa za Mungu wetu kamwe haziwezi kulinganishwa na mwingine awaye yote, Musa alipotaka kumjua Mungu Mungu alijifunua kwake kwa sifa nzuri zenye kuwavutia sana wanadamu zinazoashiria kuwa Mungu ni mwema mno ona

Kutoka 34:6-7 “BWANA akapita mbele yake, akatangaza, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.”  

Unaona tunamwabudu na kumtumikia Mungu mwenye huruma nyingi, mwenye fadhili, na si mwepesi wa Hasira mwingi wa rehema na kweli nani mwenye kuonea watu huruma hii ni sifa kubwa sana ya Mungu aliye baba na muumba kwetu sifa hii na tabia hii ya uungu iko kwa Mungu etu ambaye amejifunua kwetu kama Baba, mwana na Roho Mtakatifu, yeye ni mwingi wa huruma kama maandiko yanenavyo 

Zaburi 145:7-9 “Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako. Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.”

Hata hivyo pamoja na wingi huu wa rehema na neema na huruma za Mungu wetu, ni ukweli ulio wazi kwamba maandiko yanatuonya sana sana sana kutokumkosea ROHO MTAKATIFU Onyo hili limerudiwa tena na tena kama tahadhari kubwa sana katika maandiko ya kwamba katika maisha yetu kama mtunataka kufurahia neema ya Mungu na uwepo wake basi katika ufunuo wa Mungu wetu hasa kuhusiana na ROHO MTAKATIFU tunaonywa sana kutokumfanyia dhambi au kasirani ROHO MTAKATIFU hii maana yake ni nini maana yake mtu anaweza kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu na akajikuta yuko matatani.  Katika nafsi hizi tatu kwa mujibu wa mafundisho ya Yesu mwenyewe tunaweza kumkosea Mungu baba na Mwana pia na mlango wa neema ukapatikana lakini tahadhari kubwa inatolewa kuhusu kumkosea ROHO MTAKATIFU.

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”

Unaona maneno hayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye anatuonya sana namna ya kujihadhari ili tusiweze kuwa na uadui na Roho Mtakatifu kwani tunaweza kujikuta katika wakati Mgumu  hii maana yake ni nini maana yake tunaweza kujikuta tunamtenda dhambi Mungu Roho Mtakatifu na akageuka na kuwa adui yetu na kupigana nasi!          

Namna ya kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu.

Taasisi nyingi leo zinazomtaja Mungu, na zilizokuwa na nguvu sana duniani zilianza kupoteza umaarufu wake mara baada ya kuanza kupingana na kazi za Roho Mtakatifu na kufanikiwa kutengeneza uadui naye, ni jambo la kusikitisha kwamba katika nchi nyingi za ulaya na ikiwemo Uingereza makanisa mengi sana yaliyokuwa taasisi kubwa yamebakiwa na majengo ambayo mengine yamenunuliwa na kuwa misikiti au kuwa maduka au majumba ya makumbusho na pia kuwa makasino lakini ukichunguza kwa kina chanzo kikubwa cha kufikia hatua hiyo ni kupoteza uamsho na kufikia ngazi ya kufanikiwa kuwa na uadui na Roho Mtakatifu! Uwepo wa Roho Mtakatifu una nafasi kubwa sana katika maisha yetu na mafanikio yetu ya kimwili na kiroho hata hivyo hatuna budi kuzingatia tahadhari zilizotolewa na Mungu kwa neno lake kuhusu Mungu Roho Mtakatifu ni namna gani tunaweza kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu

1.       Angalieni msimtie Kasirani -  kumtia kasirani maana yake ni kumuudhi kwa sababu ya manunguniko na malalamiko na kutokuamini, wakati tunapokuwa tumeokolewa hatuna budi kufahamu kuwa ni kazi ya roho Mtakatifu kutuongoza na kutusaidia yeye ni msaada ulio karibu sana anafanya kazi katika kiwango kile kile ambacho angekifanya Kristo akiwa katikati yetu yeye huitwa msaidizi Yohana 14:16 – 18 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.”

 

Unaona Mpango wake Mungu ni kuwa pamoja nasi, Pamoja na kuwa Yesu alipaa Mbinguni lakini hakutuacha yatima ametuletea Msaidizi yaani Roho Wake mtakatifu ili akae nasi ni rafiki wa karibu na ni kiongozi wetu hivyo hatupaswi kumtia kasirani ona

 

Kutoka 23:20-22Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea. Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake. Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.”

 

Ni muhimu kufahamu kuwa malaika anayetajwa hapa na Bwana kwamba atawaongoza wana wa Israel na kuwa wajihadhari wasimtie Kasirani ni ROHO MTAKATIFU Yeye katika agano la kale anaitwa malaika wa uso wake kama unavyoweza kuona katika andiko la Msingi

 

Isaya 63:9-10Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale. Lakini wakaasi, wakamhuzunisha Roho yake Mtakatifu; kwa hiyo akawageukia, akawa adui, akapigana nao.”

 

Unaweza kuona maonyo ya kibiblia kwamba tunaweza kumkosea ROHO MTAKATIFU kwa kumtia kasirani na hatimaye akageuka na kuwa adui na kupigana nasi, haya yalifanywa na wana wa Israel walipookolewa kutoka Misri lakini njiani mara kwa mara walimkosea Mungu Roho Mtakatifu kwa kufanya maovu ambayo yaliwafanya waangamizwe jangwani  ona

  
1Wakoritho 10:1-11Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; wote wakala chakula kile kile cha roho; wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu. Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani

 

Unaona? Wana wa Israel kwa rehema na huruma za Mungu waliokolewa kutoka utumwani Misri kwa nia nzuri ya upendo wa Mungu ili kusudi awapeleke katika nchi ya mkanaani akawape raha na maziwa na asali na kila walichokitamani, hata hivyo katika namna ya kushangaza sana utaweza kuona walimuhuzunisha Mungu na kumtia kasirani Roho wa Mungu na hatimaye wakaangamizwa jangwani.

 

Ni kwa sababu ya somo hili Paulo mtume anasema mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano ili kutuonya sisi tuliofikiwa na miisho ya zamani hizi yaani zamani hizi ni zama hizi ambapo ROHO MTAKATIFU Yuko kazini hapa duniani akifanya kazi pamoja nasi, kwa msingi huo basi kanisa au taasisi yoyote inayomtaja Mungu kama haitajali kutunza uwepo wa ROHO MTAKATIFU kwa heshima kubwa ni ukweli ulio wazi kuwa tutakuwa na uadui naye!

 

2.       Wala Msimuhuzunishe - Namna nyingine ambayo tunaweza kujenga uadui na Roho Mtakatifu ni Pamoja na kumuhuzunisha ona Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.”  Kumuhuzunisha ROHO MTAKATIFU huambatana na kumkasirisha  neno la kiyunani linalotumika kuhusiana na kumuhuzunisha ROHO MTAKATIFU Katika kiyunani ni LYPEITE Kwa kiingereza ni Cause Grief Ambalo maana yake ni kumsababishia MAJONZI hili ni wimbi zito la masikitiko na kukasirishwa kunakotokana na kupingwa kunakosababishwa na ugumu wa mioyo ya watu kwa makusudi jambo la namna hii lilimtokea Masihi pale watu walipiokuwa wanataka asiponye mtu kwa sababu ni siku ya sabato Marko 3:4-5 “Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza. Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.”        Katika taasisi mbalimbali na madhehebu mbalimbali ya Kikristo wakati mwingine wamekuweko watu ambao kwa makusudi kabisa wanapinga na kazi za Roho Mtakatifu katika taasisi au maisha ya mtu, wako watu wanaweza kupinga maombi, wanaweza kupinga uponyaji au hata ustawi wa tabia njema iliyoko ndani ya Mtu ambayo imetokana na kazi za ROHO MTAKATIFU shughuli kama hizo zinamuhuzunisha sana Mungu Pale katika Marko 5:6 ukisoma utaona viongozi wa dini sio tu walichukizwa na Yesu kuponya siku ya sabato lakini vilevile walikuwa na makusudi ya kumuangamiza! Wako watu pia wanaopinga na mahubiri, au muhubiri au kazi zinazofanywa na wahubiri wa Injili,  nimefanya kazi ya kichungaji miaka 12, na kufundisha vyo vya Biblia miaka 12 na pia kuongoza taasisi ya kielimu kwa shule ya seminari miaka 10 na mara kadhaa nimeona watu wakishindana na ROHO MTAKATIFU wazi wazi na wakati mwingine nilidhani wananichukia mimi jambo ambalo nimeshalizoea lakini kumbe niligundua baadaye kuwa kazi ile ambayo Roho wa Mungu ameiweka ndani yangu ilikuwa inapingwa vikali, sio hivyo tu mahali popote ambako watu wanaishi kwa MANENO MAOVU, UCHUNGU, GHADHABU, HASIRA KELELE NA MATUKANO NA UBAYA WA KILA NAMNA  Hayo nayo hayo nayo ni sababu kubwa ya kusababisha MAJONZI kwa ROHO MTAKATIFU hili ndio tukio lililopelekea Paulo Mtume kuwataka Kanisa la Efeso wawe mbali na maswala ya aina hiyo kwani ndiyo yanayopelekea kuhuzunika kwa Majonzi kwa ROHO MTAKATIFU jambo ambalo litapelekea aliache kanisa, aondoke au asifanye kazi tena na hapo uadui nay eye huwa unaweza kufikia kikomo. Waefeso 4:29-31 “Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;”

 

3.       Msimzimishe Roho1Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho;” Ni muhimu kukumbuka kuwa  katika kumueleze ROHO MTAKATIFU  moja ya alama zinazotumika keelezea utendaji wa Roho Mtakatifu ni pamoja na MOTO, wote tunaweza kuwa na ufahamu juu ya umuhimu wa Moto katika maisha ya Mwanadamu, tunajua kuwa maendeleo makubwa ya mwanadamu yalichangiwa pia na ugunduzi wa Moto, Roho wa Krito vilevile hufanya kazi kama Moto katika maisha ya waaminio

 

Isaya 4:3-4 “Tena itakuwa ya kwamba yeye aliyebaki katika Sayuni, na yeye aliyeachwa ndani ya Yerusalemu, ataitwa mtakatifu; yaani, kila mmoja aliyeandikwa miongoni mwa hao walio hai ndani ya Yerusalemu; hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza.”

 

Unaona maandiko yanatufundisha wazi kuwa utendaji wa Roho Mtakatifu ni kama mfano wa Moto hufanya kazi ya kuichoma mioyo yetu na kuteketeza yasiyofaa ndani yetu ili tuweze kuwa watakatifu, upendo wa Mungu huwaka ndani yetu, upendo wa kuhubiri, kuabudukumtumikia Mungu kwa uaminifu, kufanya maombi, kuwasaidia wengine moto huo wa kihuduma ndani yetu huwashwa na ROHO MTAKATIFU tangu anapokuja ndani yetu ona Matendo 2:3-4 “Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.” 

 

Unaona hii ni Ishara ya Roho wa Mungu kuwasha moto wa uamsho ndani yetu ili tumpende Mungu na wenzetu, kwa msingi huo hatupasw kamwe kuuzima moto huo, Neno linalotumika katika maneno ya kiyunani kuhusu KUZIMA  ni neno SBENNUMI – “sben-noo-mee” kwa kiingereza to extinguish  ambalo maana yake ni tendo endelevu la kuzima moto, msimzimishe ROHO kanisa ua taasisi au mtu binafsi anaweza kuendelea kuuzimisha moto wa Roho Mtakatifu kwa kukosa furaha, kuacha kuomba, kuacha kushukuru, kupinga unabii, kupinga mapenzi ya Mungu, kupinga mambo mema na kutokujitenga na uovu au ubaya wa kila namna haya ndio mojawapo ya maswala yanayochangia kumzimisha ROHO WA BWANA ona 1Wathesalonike 5:14-22 “Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote. Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. Furahini siku zote; ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. Msimzimishe Roho; msitweze unabii; jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; jitengeni na ubaya wa kila namna.”        Unaona kwa mujibu wa maelezo na maonyo ya Mtume Paulo matukio yote hayo yakifanyika kwa waamini na taasisi za kidini tunamfanya Roho wa Mungu auzunike na kwa sababu hiyo tunatengeneza uadui na Mungu nay eye atatutapika na matokeo yake taasisi au watu binafsi wanapoa ona

 

Ufunuo 3:13-22 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa

 

Unaona kwa msingi huo kama watu watauzima moto wa Roho kwaajili ya sababu mbalimbali tulizojifunza hapo juu ni ahadi ya ROHO MTAKATIFU mwenyewe ya kuwa watatutapika, yeye hapenzi watu vuguvugu, yeye anatutaka tutubu na kama hatutafanya hivyo hakuna kingine tunachoweza kuzawadiwa bali tutapoteza Rehema na neema yake na kujikuta tumeunda uadui na Roho Mtakatifu. Nisikilize Mungu habadiliki, tabia ya Mungu ni ileile sisi wanadamu hubadilika Kabla ya gharika ya wakati wa Nuhu iliyofutilia mbali wanadamu wengi na kumuacha Nuhu na familia yake wanadamu walitenda maovu, walijaa uovu waliacha kumsikiliza ROHO MTAKATIFU kwa kufanya uovu na kuwaza kufanya mabaya kila wakati hivyo walimuhuzunisha na walimzimisha pia na walishindana  naye nadhani ni pale alipokuwa akiwashauri kuwa wema na wao wakapuuzia  Mwanzo 6:3-6BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini. Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu, wakazaa nao wana; hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo” unaona madhara watu waliposhinda ana Roho ya Mungu, miaka ya kuishi mwanadamu ilipunguzwa, Mungu aklijuta kumuumba mwanadamu, rehema zake na huruma zake zikafikia mpaka akahuzunika akawafuta wanadamu, watu wanaopinga ana mapenzi ya Mungu, taasisi zinazopigana na kusudi la Mungu, na watu wenye tabia endelevu ya kushinda ana kazi ya Mungu kupitia roho Mtakatifu watapunguziwa maisha, watafutwa kwa sababu wameamua kuwa adui wa Mungu

 

4.       Msimpinge Roho Mtakatifu – Matendo 7:51-52 “Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo. Ni yupi katika manabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? Nao waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake, mkamwua;”            Namna nyingine ya kuwa adui wa Roho Mtakatifu ni kumpinga ni neno gumu na lenye kusikitisha sana kadiri nilipokuwa naendelea kujifunza somo hili nilikuwa nawaza maoyoni hivi somo hili ni sehemu ya INJILI kweli au kuwatisha watu? Lakini Roho Mtakatifu akanikumbusha maeno ya BWANA YESU na haya ya STEFANO kwa habari ya ROHO MTAKATIFU maonyo ya kucheza naye hayana utani wala mchezo kabisa, hakuna mzaha linapokuja swala la kucheza na Roho Mtakatifu lugha ya kimaandiko ni kali na ngumu na haina mzaha! Kumpinga Roho Mtakatifu ni dhambi nyingine ambayo wanadamu wanaweza kumtendea Mungu aidha walioamini au hata wasioamini maadamu tu utaingia kwenye anga zake na kumpinga madhara yake yatakuhusu, Kumpinga Roho Mtakatifu katika lugha ya kiyunani linatumika neno ANTIPIPTO ambalo kiingereza chake ni resist au oppose kwa kuwa Roho Mtakatifu hawezi kuonekana kwa macho ya kibinadamu

 

Yohana 14:16-17 “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.”          

 

Sasa unawezaje kumpinga yeye usiyemuona kwa macho, ukweli ni wazi kuwa kumpinga ROHO MTAKATIFU Huambatana na kuwapinga watumishi wake, wale wanaobeba ujumbe wake NI YUPI KATIKA MANABII AMBAYE BABA ZENU HAWAKUMWUUDHI Wayahudi walipinga ana Musa, walipinga ana manabii, walimpinga yesu Kristo waliwapimga mitume na hata kuwaua walipinga maneno yale na ujumbe ule ambao waliubeba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, Roho wa Mungu leo anaweza kugeuka adui na akapigana nasi kama tu tunazuia kazi mzake na kupinga ujumbe wake huku tukiwadharau na kuwapiga na kuwapinga watumishi wake na kushindana na kazi yake hiki ndicho ambacho mafarisayo na Masadukayo walikifanya na wayahudi wengi wenye wivu walishindana sana na wajumbe wa injili hata wakitaka wasihubiri wala kumtaja Yesu ona

 

Matendo 4:1-10 “Hata walipokuwa wakisema na watu wale, makuhani na akida wa hekalu na Masadukayo wakawatokea, wakifadhaika sana kwa sababu wanawafundisha watu na kuhubiri katika Yesu ufufuo wa wafu.Wakawakamata, wakawaweka gerezani hata asubuhi; kwa kuwa imekwisha kuwa jioni. Lakini wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya watu waume ikawa kama elfu tano.Hata asubuhi wakubwa na wazee na waandishi wakakusanyika Yerusalemu, na Anasi Kuhani Mkuu, na Kayafa pia, na Yohana na Iskanda, na wote wale waliokuwa jamaa zake Kuhani Mkuu.Walipowaweka katikati wakawauliza, Kwa nguvu gani na kwa jina la nani ninyi mmefanya haya? Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu.”     

 

Matendo 5:14-39 “walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake; hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao. Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa. Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu, wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza; lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu. Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete. Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari, wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.  Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo. Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu. Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe. Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti. Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio.Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua. Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo, akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa. Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu. Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika. Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.”

 

Wakati wote unaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume ambacho kimsingi ndio tunasoma kwa kina na mapana na marefu utendaji wa Roho wa Mungu ndio utaweza kuona jinsi watu kadha wa kadhaa walivyoweza kupinga ana kazi ya Mungu na wajumbe wa ile kazi na hiki ndicho anachokikemea STEFANO na kuwaonya wayahudi kwamba waache kumpinga ROHO MTAKATIFU   ikiwa ni pamoja na kushupaza shingo zao. Kumpinga Roho Mtakatifu na kazi zake au watumishi wake leo limekuwa moja wapo ya Dhambi inayopelekea Mungu kuwaacha watu wake Roho Mtakatifu leo anapingwa sana na waliokoka na wasiookoka yako mashirika leo na wako watu leo wamefilisika kiroho na wanafanya kila jitihana waweze kuinuka tena lakini inashindikana sababu kubwa ni kupinga ana Roho wa Mungu, watu wanapinga uamsho, wanapinga ujazo wa Roho, wanapinga miujiza, wanapinga wajumbe wa Mungu, wanahakikisha kuwa mnakuwa na usumbufu na mnakosa utulivu ili mradi tu kuharibu hali ya kiroho na injili. Ukitaka kuwa adui wa ROHO MTAKATIFU hakikisha kuwa unapinga anaye, yeye aliye na sikio na alisikie neno hili.

 

5.       Usimwambie uongo Roho Mtakatifu - Matendo 5:3-5 “Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.”  Kumwambia uongo ROHO MTAKATIFU  ni mojawapo ya dhambi mbaya ambayo nyakati za kanisa la kwanza ilisababisha watu kufa mara moja, lakini hata leo watu wanaweza kutengeneza uadui na ROHO WA MUNGU kwa mtindo unaofanana na Anania na Safira kimsingi watu hawa walifanya unafiki, walikuwa wakiigiza jambo ambalo sio sahihi mbele za Mungu kwanza tuichambue asili ya dhambi yao

 

Kulikuwa na mpango wa watu kuishi kwa umoja na kwa pamoja na kwaajili ya kanisa watu wengi walikuwa wakiuza mali zao na kukabidhi kwa mitume kwa kusudi la kuwasaidia wengine moja ya watu waliofanya hayo na kupata umaarufu na sifa kubwa katika kanisa ni Barnabas ona

 

Matendo 4:34-37 “Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa,wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji. Na Yusufu, aliyeitwa na mitume Barnaba, (maana yake, Mwana wa faraja), Mlawi, asili yake ni mtu wa Kipro, alikuwa na shamba akaliuza, akaileta fedha, akaiweka miguuni pa mitume.”

 

Nadhani ni kutokana na watu kadhaa kusifiwa na mitume kwa moyo wao wa utoaji tayari Anania na Safira nao walipata msukumo wa kufanya hivyo lakini nadhani wakiwa na nia ya kujipatia sifa tu, kutoa mali zako na kuziuza kwaajili ya utoaji wa kanisa halikuwa tatizo, na hata kuzuia sehemu ya fedha kwaajili ya familia haikuwa tatizo, kama Petro Mtume alivyohoji

 

Matendo 5:4 “Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.”               

 

Swala kubwa lilikuwa kumdanganya ROHO MTAKATIFU na kumjaribu, Shetani alikuwa ameshamjaza Anania na mkewe nia ovu nia yao ilikuwa ni kutaka sifa, kutoka katika jamii ya kanisa, wao waliwaambia mitume kuwa wametoa vyote kumbe kuna ambacho walijifichia, walikuwa wakijaribu kuwadanganya watu hasa wa jamii ya kanisa kumbe kiuhalisia walikuwa wakimdanganya ROHO MTAKATIFU ona

 

Matendo 5:3-5 “Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.”

 

Mungu alikusudia kanisa lake liwe kama mfano wake yeye aliyetuumba ni agizo la kibiblia kwamba tuuvue kabisa utu wa kale na kuacha kabisa kuambiana uongo angalia Wakolosai 3:9-10 “Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.”

 

Leo hii sio ajabu watu kuambiana uongo, kumekuwa na watu waogo na wadanganyaji kuliko nyakati za kanisa la Kwanza, kumekuwa na wimbi kubwa la watu wanafiki na wanaotaka sifa na kujijengea jina katika jamii kupitia umaarufu feki, vyovyote iwavyo kusema uongo ni ishara iliyo wazi kuwa Ibulisi ambaye ni baba wa uongo anatawala ona

 

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.”

 

Kwa misingi hii unaweza kuona ya kuwa kama unadanganya watu na kutaka sifa na kudanganya watumishi wa Mungu ni wazi kuwa unatengeneza uadui na ROHO MTAKATIFU jambo ambalo litakugharimu.

 

6.       Kumfanyia Jeuri Roho wa Neema – Waebrania 10:26-29 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?Nyakati za agano la kale mtu aliyeivunja sharia ya Musa aliuawa pasipo huruma

 

Hesabu 15:30-35 “Lakini mtu afanyaye neno lo lote kwa kusudi, kama ni mzalia, kama ni mgeni, huyo amtukana Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake. Kwa sababu amelidharau neno la Bwana, na kuyavunja maagizo yake; mtu huyo atakatiliwa mbali, uovu wake utakuwa juu yake. Kisha wakati huo wana wa Israeli walipokuwako jangwani, wakamwona mtu mmoja akikusanya kuni siku ya Sabato. Hao waliomwona akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni, na kwa mkutano wote. Nao wakamweka kifungoni, maana, lilikuwa halijasemwa atakalotendwa. Bwana akamwambia Musa, Mtu huyo lazima atauawa; mkutano wote watampiga kwa mawe huko nje ya marago.”

 

Agano jipya ni agano lililobora zaidi ya lile la agano la kale kama mtu angeliweza kuuawa kwaajili ya kuvunja sharia katika agano la kale ni zaidi sana mtu anapoivunja sharia ya kifalme katika agano jipya kama asemavyo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, Mwandishi anatoa maonyo makali sana kuhusiana na ukengeufu, kurudi nyuma na kumkana Yesu Kristo jambo ambalo ni kinyume na utendaji mzima wa Roho Mtakatifu ambaye hufanya kazi ya kuwapa watu neema ili watubu na kumuamini Yesu kwa msingi huo mtu anapoifanya shingo yake kuwa ngumu na kutukana maswala kadhaa ya wokovu na kuukana anajiweka kwenye uadui na Roho wa Kristo nani sawa kabisa na kumfanyia Jeuri ROHO WA NEEMA kwa msingi huo kufanya dhambi kusudi, kunaleta hukumu yenye kutisha kwa sababu kufanya hivyo ni kumfanyia jeuri yeye.

 

7.       Kumkufuru Roho Mtakatifu. – Kilele cha juu zaidi katika dhambi zinazoweza kumfanya mtu kuwa na uadui na Roho Mtakatifu ni kumkufuru, neno Kukufuru katika lugha ya Kiyunani linatumika neno Blasphemia – sawa na neno Blasyphemy katika kiingereza ambalo maana yake ni kusema maneno mabaya au kuzungumza vibaya kuhusu Mungu, jambo hili limezungumzwa na Bwana wetu Yesu Kristo Mwenyewe

 

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”

 

Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ndio dhambi pekee ambayo haina msamaha kwa mujibu wa maelekezo ya Yesu kristo, na ndio maana utaweza kuona kumekuweko na maonyo ya kutosha kuhusu kuacha kutenda dhambi kinyume na mapenzi ya ROHO MTAKATIFU,  ukimkufuru Roho umefanya dhambi ya milele, kukufuru ni hali ya kuzungumza mabaya, au kutukana na kuudhi maswala yote Matakatifu yanayohusiana na Mungu Yesu alitoa maonyio ya namna hii katika mazingira ambayo mafarisayo walikuwa wanapinga kazi zote za Mungu alizokuwa akizifanya hata kufikia ngazi ya kutukana na kusema ya kuwa kazi hizo za kiungu zinafanywa na shetani kupoitia Yesu ona

Mathayo 12:22-32 “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.  Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi? Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo. Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama. Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje? Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu. Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake. Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya. Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.

 

Matendo na maneno yote anayosemewa na kutendewa Roho Mtakatifu kilele chake kinakamilika katika kumkufuru na hivyo kila wakati inapotokea anahuzunishwa, anazimishwa, anaongopewa, anapingwa, anafanyiwa jeuri, anafanyiwa kasirani kielele chake ni kuondoka, kuacha, kutokujishughulisha na ninyi tena na kutokusababisha moyo wa toba utokee na hatimaye kusababisha kuhesabika kana kwamba umekufuruau umemkufuru, Ndio maana leo tunaweza kuiona watu wengi, makanisa mengi na taasisi nyingi zimechwa na ROHO WA BWANA  kwa sababu hawakuzingatia maswala kadhaa yanayimuhuzunisha Mungu ROHO MTAKATIFU  na kumfikisha katika hatua ya kuondoka na kwenda mbali nasi.

Hitimisho:

Kuondoka kwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu sio tu kunatutengenezea uadui naye lakini inshara ya kuondoka kwa utukufu wa Mungu, mar azote maandiko yameeleza kuwa wanadamu wamepungukiwa na utukufu wa Mungu mara baada ya kutenda dhambi Warumi 3:23  kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Utukufu wa Mungu unakuwepo kwetu kwa ukamilifu wakati ambapo Roho wa Mungu akiwa hai ndani yetu, akiwa anatenda kazi akiwa anatuongoza, ikiwa tunamsikiliza, lakini tunaelezwa kuwa tunapomuasi anageuka anakuwa adui anapigigana nasi, kwa kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu ieleweke wazi kuwa nafsi hii katika utatu wa Mungu inapokasirishwa na kufikia hatua ya kupigana nasi ujue hakuna mwamuzi tena

 

1Samuel 2:22-25. “Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania. Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote. Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa Bwana. Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa Bwana, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu Bwana amekusudia kuwaua.”  

 

Inapofikia ngazi Mungu mwenye rehema na neema nyingi mwingi wa huruma na asiye mwepesi wa Hasira anafikia ngazi ya kumuua mtu ujue jambo hilo limekuwa machukizo makubwa kwa Mungu wetu, unapokuwa na uadui na Mungu kinachofuata ni kifo na wakati huo huo Mungu anaweza kuamua kukuacha na kuondoa utukufu wake hakuna jambo baya duniani kama kupungukiwa na utukufu wa Mungu. Israel walipokuwa wamemtenda dhambi ukweli ni kuwa utukufu wa Mungu ulikuwa ukiondoa hatua kwa hatua na hatimaye ukaenda katika inchi ya mbali ona katika kitabu cha Ezekiel uwepo wa Mungu ulikuwa ukiondoka taratibu kutoka katika patakatifu hata kwenye kizingiti, kutoka kizingitini hata ukutani, kutoka ukutani hata mlimani na kutoka mlimani hata ukaldayo katika nchi ya utumwa

Ezekiel 10: 4. “Utukufu wa BWANA ukapaa kutoka kwa kerubi yule, ukasimama juu ya kizingiti cha nyumba; nayo nyumba ikajazwa na lile wingu, na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa BWANA.,”

Ezekiel 10:18-19. “Kisha huo utukufu wa BWANA ukatoka pale juu ya kizingiti cha nyumba, ukasimama juu ya makerubi.Nao makerubi wakainua mabawa yao, wakapaa juu kutoka katika dunia machoni pangu, hapo walipotoka nje, nayo magurudumu yakawa kando yao; wakasimama mahali pa kuingilia pa mlango wa upande wa mashariki wa nyumba ya BWANA; na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.”                

Ezekiel 11:23-25. “Utukufu wa BWANA ukapaa juu toka katikati ya mji, ukasimama juu ya mlima wa upande wa mashariki wa mji. Na roho hiyo ikaniinua, ikanichukua katika maono, kwa nguvu za roho ya Mungu, hata Ukaldayo, kwa watu wale wa uhamisho. Basi maono niliyoyaona yakaniacha. Ndipo nikawaambia watu wa uhamisho habari ya mambo yote aliyonionyesha BWANA.” 

Kadiri watu wa Mungu wanapofanya machukizo ya aina mbalimbali, Mungu huupunguza utukufu wake na kuondoka kidogo kidogo utukufu wa Mungu ni sihara ya uwepo wa Mungu ni uwepo wa Roho wake Mtakatifu, Israel walipotenda ya kuchukiza uwepo huo uliondoka na kwenda utumwani Babeli na ndipo sa unapoweza kuona watu waliokuwa utumwani walikuwa na nguvu na uwezo mkubwa sana wa Kiroho na Mungu alitukuzwa lakini Israel panyewe pakabaki ukiwa, Mtu wa Mungu wewe ndio hekalu la Mungu je utukufu wa Mungu umeondoka na kufikia ngazi gani kama utukufu umekuacha na kwenda Babeli huna budi kulia na kutubu, Leo hii mtakapoisikia sauti yake msiifanye mioyo yenu kuwa Migumu. Chunga sana hakuna jambo baya duniani kama kutengwa mbali na uso wa Mungu hakuna jambo linatisha duniani kama kumuasi Roho Mtakatifu na kumuacha akawa adui yetu na kupoigana nasi Bwana ampe neema kila mmoja wetu asiwe adui wa ROHO MTAKATIFU KATIKA JINA LA YESU AMEN.

Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.