Jumatatu, 27 Februari 2017

Mkono wa Bwana!


Mstari wa Msingi: Isaya 53:1Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”


Kware kama wanavyoonekana Pichani ni ndege watamu sana na wenye afya ya ajabu 

Utangulizi:

Neno mkono linapotumika katika maandiko humaanisha utendaji au uweza, Na tunapoona neno Mkono wa Mungu moja kwa moja humaanisha uweza na utendaji wa Mungu, yako mambo kadhaa katika maisha yetu hayawezi kufanikiwa kama mkono wa Mungu hautakuwa juu yako ama kuwa pamoja nawe, Katika maandiko tunamuona Naomi akilia akiamini kuwa alipatwa na mikasa mbalimbali mibaya kwa sababu Bwana ameondoa mkono wake juu yake 

(Ruthu 1:11-13) “Naye Naomi akasema, Enyi wanangu, mrejee; kwani kufuatana na mimi? Je! Mimi ninao watoto wa kiume tena tumboni mwangu, hata wawe waume zenu? Enyi wanangu, mrejee; nendeni zenu; kwa kuwa mimi ni mzee, siwezi kupata mume tena. Kama ningesema, Natumaini; kama ningepata mume hata usiku huu, na kuzaa watoto wa kiume;  je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa Bwana umetoka juu yangu”.  
     
kwa msingi huo Nyakati za Biblia watu wengi waliofanikiwa walifahamu kuwa mkono wa Bwana uko pamoja nao, Hakuwezi kuwa na mafanikio ya aina yoyote kama Mkono wa Bwana ukitupungukia, lakini uko ushindi mkubwa sana kama Mungu akiunyoosha mkono wake kutenda jambo.

Uweza wa mkono wa Bwana

·         Mkono wa Mungu ukinyoosha kila kilicho kigumu kinashughulikiwa Kutoka 3:19-20 Biblia inasema hivi “19. Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu. Nami nitaunyosha mkono wangu, na kuipiga Misri kwa ajabu zangu zote, nitakazofanya kati yake, kisha baadaye atawapa ruhusa kwenda.” 

·         Mkono wa Bwana ukinyooshwa hakuna jambo gumu la kumshinda Hesabu 11:4-15, 18-23, 31-32. “4. Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N'nani atakayetupa nyama tule? 5. Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu; 6. lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu. 7. Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtama na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola. 8. Watu wakazunguka-zunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa nyunguni, na kuandaa mikate; na tamu yake ilikuwa kama tamu ya mafuta mapya. 9. Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao. 10. Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika. 11. Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? 12. Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? 13. Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwani wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula. 14. Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15. Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.”

“18. Kisha uwaambie watu hawa, Jitakaseni nafsi zenu kabla ya kesho, nanyi mtakula nyama; kwa maana mmelia masikioni mwa Bwana, mkisema, Ni nani atakayetupa nyama, tule? Maana huko Misri tulikuwa na uheri. Basi kwa sababu hiyo Bwana atawapa nyama, nanyi mtakula. 19. Hamtakula siku moja, wala siku mbili, wala siku tano, wala siku kumi, wala siku ishirini; 20. lakini mtakula muda wa mwezi mzima, hata hapo nyama hiyo itakapotoka katika mianzi ya pua zenu, nanyi mtaikinai, kwa sababu mmemkataa Bwana aliye kati yenu, na kulia mbele zake, mkisema, Tulitoka Misri kwa maana gani? 21. Musa akasema, Watu hawa ambao mimi ni kati yao, ni watu sita mia elfu waendao kwa miguu; nawe umesema, Nitawapa nyama, ili wale muda wa mwezi mzima. 22. Je! Makundi ya kondoo na ng'ombe yatachinjwa kwa ajili yao, ili kuwatosha? Au samaki wote wa baharini watakusanywa pamoja kwa ajili yao, ili kuwatosha? 23. Bwana akamwambia Musa, Je! Mkono wa Bwana umepungua urefu wake? Sasa utaona kwamba neno langu litatimizwa kwako, au sivyo.”

“31. Kisha upepo ukavuma kutoka kwa Bwana, nao ukaleta kware kutoka pande za baharini, nao ukawaacha wakaanguka karibu na kambi, kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, na kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, kuizunguka, nao wakafikilia kiasi cha dhiraa mbili juu ya uso wa nchi. 32. Watu wakaondoka mchana huo wote, na usiku huo wote, na siku ya pili yote, kuwakusanya hao kware; yeye aliyepata ya upungufu kuliko wenziwe alipata kiasi cha homeri kumi; nao wakawaanika wote kando-kando ya kambi kuizunguka pande zote.”            

Dhiraa mbili  (2 Cubic )ni sawa na Futi Tatu kwenda juu au mita moja, na mwendo wa siku nzima ni sawa na KM.

Siri ya Mkono wa Bwana

·         Isaya anauliza Ni nani aliyesadiki Habari tuliyoileta na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Kisha isaya anaeleza habari za Yesu Kristo na mateso yake ambayo yameleta ukombozi mkuu kwa wanadamu

·         Ni wazi kuwa Biblia inapozungumzia juu ya mkono wa Bwana inaeleza siri iliyo wazi kuwa Yesu ndio mkono wa Bwana ni wazi kuwa ukiiamini injili, Habari njema na kuiamini kazi iliyofanyika msalabani kwamba ni kwaajili yetu, na kuwa Yesu ametunukiwa jina kuu kuliko yote nay a kuwa tukiliitia jina lake tunaokolewa

·         Hakuna jambo litakalokuwa Gumu kwetu, hakuna jambo linaloshindikana Mkono wa Bwana utafunuliwa kwako tu, mweke Yesu mbele, kubali kazi zake usimkatae Yesu utauona uwezo wake, Musa alilia alikata tamaa wanataka Nyama, nitoe wapi nyama Kama nimepata fadhili machoni pako inatosha Heri nife, inawezekana umefikia pointi ngumu sana katika maisha yako, kwamba sasa Mungu uko wapi, kwanini haya yanatokea, heri uniuwe kabala ya aibu hii, yatosha baba lakini nakuthibitishia leo kuwa Mkoo wa Bwana haujapunguka urefu wake

·         Yeye alisema niite nami nitakuitika na kukuonyesha Mambo makubwa na Magumu usiyoyajua

Kizuizi kwa Mkono wa Bwana
·         Isaya 59:1-2 1. “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2. lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”. 

 Biblia inaonyesha wazi kuwa ni dhambi tu ndio inaweza kumfanya Mungu aionyeshe mkono wake na ni maovu tu ndio yanayoweze kumfanya asisikie sasa dawa ya hili ni rahisi, lazima tukubali kutubu na Yesu anatusubiri na tukiungama yeye ni mwaminifu na atatusamehe kabisa 1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.”

Na Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Alhamisi, 23 Februari 2017

WALIO PAMOJA NASI NI WENGI KULIKO WALE WALIO PAMOJA NAO.



ANDIKO LA MSINGI: 2WAFALME 6:15-16 “.Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?  Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”

Utangulizi:

Ni muhimu kwa kila Mkristo kuwa na ufahamu kwamba ulimwengu wa kiroho ni halisi, na kuwa kama tulivyojifunza, kwamba kuna vita vya kiroho katika ulimwengu wa roho, kwamba ziko pande mbili zinazoshindana, upande wa Mungu na Shetani na kuwa wakati mwingine vita hii hujitokeza katika hali halisi ya mwilini.

Ili ushindi wetu uweze kuwa Dhahiri,ni muhimu kuwa na uelewa wa kutosha namna na jinsi ambavyo ulimwengu war oho unavyotenda kazi, ujuzi huu wakati wote utakufanya utembee katika ushindi na kuwa mbali na hofu ya jambo lolote linalohsindana nawe.
Nabii Elisha alikuwa moja ya manabii muhimu sana katika Israel, hii ilitokana na uwezo wake mkubwa sana katika kuuona ulimwengu war oho na kujua kila kinachoendelea upande wa maadui wa Israel, kutokana na umuhimu wake siku alipougua na kukaribia kufa, mfalme alilia san asana na kusema “ Baba yangu baba yangu Gagari la Israel na Mpanda farasi wake” 2 Wafalme 13:14 Biblia inesema

Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!

Kilio hiki kilikuwa kina maanisha mtu huyu anayekufa alikuwa ni wa muhimu kwa Israel kuliko jeshi zima, Elisha alikuwa ametumiwa na Mungu sio tu kama Nabii lakini pia kama Mlinzi na mtetezi wa Izrael na Mfalme pia, Mfalme alijua kuwa kufa kwa Elisha ni sawa na kutoweka kwa Jeshi la Ulinzi la Israel kwa sababu kadhaa wa kadhaa.

·         Elisha alikuwa ni zaidi ya Idara ya Usalama wa taifa kwa Marekani, tunaweza kusema alikuwa ni zaidi ya FBI au CIA, alikuwa na uwezo wa kuona maadui na mipango yao zaidi ya rada kali sana katika Israel inayoitwa “GREEN PINE” Rada hii ina uwezo wa kuhisi hatari kwa zaidi ya KM 400, Elisha alikuwa ni zaidi ya Green Pine”


Pichani ni Rada aina ya Green Pine ambayo imegunduliwa na kuundwa na Jeshi la Israel pekee

·         Ulinzi wa Elisha ulikuwa ni zaidi ya “IRON DOME” hii ni silaha nzito yenye uwezo wa kuhisi mashambilizi ya adui na kufyatua makombora ya kudhoofisha makombora ya adui kabla hayajaleta madhara

 Pichani ni silaha aina ya Irone Dome ni silaha iliyogunduliwa Israel ina uwezo mkubwa sana wa kulinda na kuharibu mashambulizi dhidi ya silaha za adui na vituo vyao

·         Elisha alikuwa ni zaidi ya “DELILAH CRUISE MISSILE” yenye uwezo wa kupiga km 250 ikiwa na uzito wa kg 187 au “PROTECTOR USV RAFAEL” ambazo ni boti zenye uwezo wa kufanya kazi ya boti 9-11 za kijeshi na inauwzo wa kutumiwa na watu sita na kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja, umuhimu wa silaha hizo zote nzito zinazotumiwa na Jeshi la Israel kwa wakati wa sasa zilikuwa sawa na Elisha mmoja tu umuhimu wake kwa ufahamu kuhusu silaha hizo Google Top 10 Most Powerful weapons of Israel pia unaweza kupitia Defencyclopedia.com)

Pichani ni Israel Rafael Protector USV ni chombo chenye uwezo mkubwa sana na chenye kufanya kazi nyingi katika Jeshi la Israel

 Kwa nini Elisha alikuwa wa Muhimu kiasi hicho?

2Wafalme 6:8-14 Biblia inasema “Basi, mfalme wa Shamu alikuwa akifanya vita na Israeli. Akafanya mashauri na watumishi wake, akasema, Kituo changu kitakuwapo mahali fulani. Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli, kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami. Mfalme wa Israeli akapeleka watu mpaka mahali pale alipoambiwa na yule mtu wa Mungu, na kuhadharishwa; akajiokoa nafsi yake, si mara moja, wala si mara mbili. Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili; akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionyesha, ni mtu yupi miongoni mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli?, Mmojawapo wa watumishi wake akasema, La, bwana wangu, mfalme; lakini Elisha, yule nabii aliye katika Israeli, humwambia mfalme wa Israeli maneno uyanenayo katika chumba chako cha kulala.  Akasema, Enendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu kwenda kumchukua. Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani. Kwa hiyo akapeleka huko farasi, na magari, na jeshi kubwa; wakafika usiku, wakauzingira mji ule pande zote.”

Unaposona kifungu hicho utaweza kuona umuhimu wa Elisha kwa Israel uwezo wake wa kuona mambo katika ulimwengu war oho ulimpa ujasiri mkubwa kiasi cha kuliteka Jeshi zima la madui wa Shamu, Kijana wake Elisha alikuwa haoini katika ulimwengu wa Kiroho na hiyo aliogopa sana lakini Elisha alimtia moyo asiogope

Kuna watu wengi sana wanaogopa tena wanaogopa nguvu za giza, au wanapoona mapambano ya vita za aina mbalimbali kwa jinsi ya mwili wanaogopa sana woga wao ni kama wa mtumishi wa Elisha shida yao ni kutokuujua ulimwengu wa Kiroho ulivyo

-          Mtu anaweza kuogopa Hirizi tu
-          Mtu anweza kuogopa kuwa ametumiwa njiwa
-          Mtu anwexza kuogopa milio ya Bundi tu wakati wa usiku
-          Mtu anaweza kuogopa akisikia vitu vinatembea juu ya dali au bati
-          Mtu anaweza kuogopa kusikia milio ya Mapaka
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu tu ameota ndoto mbaya
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu tu ya nguvu za giza au wachawi na wapiga madogoli
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu ya vitisho vya aina mbalimbali duniani

Ukijujua ulimwengu wa Roho kwamba tunazungukwa na majeshi ya Malaika hutaweza kuogopa Elisha alikuwa anajua kuwa analindwa na nguvu za kupita kawaida, Malaika wenye farasi za moto walikuwa wamemzingira pande zote, ikiwa Elisha wa agano la kale alikuwa analindwa kiasi hiki sisi nasi tunalindwa na nguvu za Mungu, Zaburi 3:5-6, 27:3 Waebrania 1:14 Roho watumikao kuwahudumia wale watakaourithi wokovu wapo kutuhudumia na kutulinda hivyo hatupaswi kuogopa

 2Wafalme 6; 16-17 “Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao. Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.”
 Pichani ni silaha ya Mashambulizi iliyogunduliwa Israel iitwayo "Delilah Cruise Missile"

Mungu akikufungua macho ukaona namna unavyolindwa na majeshi ya Malaika hutaweza kuogopa Daudi akasema Jeshi lijapojipanga kupigana name Moyo wangu hautaogopa”

Jumatatu, 13 Februari 2017

Mshitaki wa Ndugu zetu!



Andiko la Msingi: Ufunuo 12:10Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini MSHITAKI wa ndugu zetu, yeye AWASHITAKIYE mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.”


Marko 15:3Nao wakuu wa Makuhani walikuwa WAKIMSHITAKI mambo mengi



Ni muhimu kufahamu kuwa shetani ndiye adui mkuu wa kila mwanadamu na kwa watu wa Mungu, Naye hufanya kazi kwa mbinu mbalimbali katika kuwashambulia wanadamu na watu wa Mungu moja ya mbinu kuu anayoitumia katika kufanya mashambulizi kwetu ni kutushitaki, au kutushutumu au kutulaumu, Leo tutachukua muda kutafakari kwa kina moja ya mbinu hii anayoitumia shetani kutushambulia ili asipate kutushinda kwa kukosa kuzijua Fikra zake au mbinu zake katika Jina la Yesu. 2Wakoritho 2:11Shetani asije akapata kutushinda kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.” Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

·         Maana ya neno Mshitaki.
·         Makusudi makuu ya mshitaki wetu.
·         Jinsi ya kumshinda Mshitaki wetu.

Maana ya neno Mshitaki.
Neno mshitaki kwa asili linatokana na neno la Kiyunani “Kategoros” au “Kategor” ambalo kwa kiingereza ni “An accuiser” which means one who blames another, or charges another with crime ambalo maana yake ni “Yeye mwenye kutafuta na kuinua lawama kwa Mwingine” au yeye mwenye kushitaki mwingine kwa uhalifu, Unaweza kuona ni katika namna ya kushangaza sana shetani mwenyewe au kupitia maajenti wake huitumia mbinu hii katika kuhakikisha anabomoa kazi ya injili, au sifa za mtu, au kanisa, ili lisiweze kukubalika kwa wasioamini au kuwafanya walioamini kupungukiwa na imani. Neno hili limetajwa mara kadhaa katika biblia likionyesha kusudi la Ibilisi au maajenti wake wakilifanya kwa kusudi la kuharibu mpango wa Mungu!. Mfano:-

Yohana 8:10 Biblia inasema hivi “Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia Mwanamke, wako wapi wale WASHITAKI wako? Je Hakuna aliyekuhukumu kuwa na Hatia? Akamwambia  Hakuna Bwana Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako wala usitende dhambi tena” 

Katika kifungu hicho hapo juu mwanamke huyu alikamatwa katika kosa la zinaa na kwa mujibu wa Torati wazinzi walipaswa kupigwa mawe hata kufa, hata hivyo katika nyakati hizi serikali ya Warumi ndio ilikuwa inatawala Dunia na Israel pia, wao walikuwa wamepiga marufuku mtu yeyote kuendesha hukumu ya kifo isipokuwa serikali ya Rumi, katika kisa hicho hapo juu shetani aliitumia dhambi ya mwanamke huyu na washitaki wake ili kumtega Yesu aingie katika mtego wa kuruhusu hukumu ya kifo na hatimaye Yesu apate kushitakiwa unaona? Kisa kinaonekana kumlenga mtu mwingine lakini ndani yake kinamlenga Yesu Kristo ili ashitakiwe yeye, Mungu alimpa Hekima namna ya kuwasaidia wote akiwemo mwanamke huyo, shetani ndiye mshitaki wetu mkuu kumbuka, swala la kumtega Yesu ili aingie hatiani lilikuwa ni swala la kila siku la shetani na maajenti wake ili wapate kisa cha kumshitaki

Mathayo 12:10Na tazama yumo mtu mwenye mkono umepooza: wakamwuliza, wakisema Ni halali kuponya  watu siku ya Sabato? Wapate KUMSHITAKI.”

Marko3:2Wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato wapate KUMSHITAKI

Marko 12:13-15Wakatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno, Kumnasa kwa maneno maana yake wapate namna ya KUMSHITAKI

Marko 15:3Nao wakuu wa Makuhani walikuwa WAKIMSHITAKI mambo mengi
Muda usingeliweza kutosha kuweza kuangalia maandiko mengi zaidi yanayoonyesha neno hilo Mshitaki linavyotumiwa katika Biblia katika maeneo mengoi sana kote huko shetani akitafuta hatia dhidi ya watu wa Mungu.

Makusudi makuu ya Mshitaki wetu!
Shetani kuitwa mshitaki wetu sio jambo geni katika agano jipya tangu zamani hizi zimekuwa sifa zake kubwa na tabia yake kuu mno, shetani ameonekana katika maandiko mengi ya kale akifanya kazi ya kuwashitaki wenye haki mfano katika :-

Ayubu 1:6-11 Bilia inasema hivi “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.  
       
Ayubu 2:1-5 Biblia inasema hivi “Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za Bwana. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi? Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu. Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako. Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake

Zekaria 3:1-5Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni? Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika. Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi. Nikasema, Na wampige kilemba kizuri kichwani pake. Basi, wakampiga kilemba kizuri kichwani pake, wakamvika mavazi; naye malaika wa Bwana akasimama karibu”.
1Nyakati 21:1Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Israeli.”

Unaweza kuona kazi za shetani katika vifungu vyote vya maandiko hapo juu kwa nini shetani hutumia lawama, mashitaka, na masingizio kwa wanadamu na kwa jamii ya wenye haki ambao maandiko yanawaita Ndugu zetu yaani waamini? Kusudi kubwa ni kuharibu sifa na kuvunjilia mbali ushawishi walionao waamini katika jamii ili Mungu azomewe na kazi zake za ukombozi zionekane kuwa bure, Hii ndio imekuwa sifa ya Shetani na maajenti wake siku zake zote Kazi hii Maandiko yanaonyesha kuwa shetani huifanya Usiku na Mchana

Kwa kutumia maandiko hayo utaweza kuliona wazi kusudi la shetani kuwashitaki wateule
Ø  Anamshitaki Daudi ili Israel wapigwe wakataliwe na Mungu, Mungu awakasirikie watu wake na wapate hasara na shetani kufurahia angamizo la watu wa Mungu
Ø  Anamshitaki Zakaria ili asihesabiwe haki, aonekane hana sifa kwa Mungu aliyemchagua
Ø  Anamshitaki Ayubu kuonyesha kuwa mungu haabudiwi tupu, kwamba watu wake wanamuabudu kwa sababu Mungu amewapa Maisha mema, ili ionekanane kwamba binadamu akikosa kitu hawezi kumuweka Mungu mbele.
Ø  Kushitaki pia huja kwa kusudi la kutuletea Mateso katika jamii, akipata kitu cha kutusingizia na tukauhumiwa tutateseka sana kwaajili ya Kristo.
Ø  Anataka kuharibu mioyo yetu na kutujengea mazingira ya kuwa wenye hatia na usijione kuwa unastahili. Kisha upoteze Haki zako. Na kuleta aibu kubwa
Ø  Jumla ya yote ni ili karama tunayoitumikia iweze kulaumiwa yaani watu waone kuwa hakuna wokovu

Jinsi ya kumshinda Mshitaki wetu.

1.      Biblia inaonya kwamba tuwe na kiasi na wenye kukesha! 1Petro 5:8Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa MSHITAKI wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Njia pekee ya Kumshinda ni kuishi maisha ya kiasi, Mungu alituokoa ili tupate kuishi kwa kiasi, tusizidiwe na mambo ya ulimwengu huu kiasi ya kwamba yatatutoa katika mapenzi yake na adui akapata sababu ya kulaumu, Tito 2:11-12 Biblia inasema hivi “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;” Unaweza kuona Mungu anatutaka tuishi kwa kiasi na kwa haki adi Yetu shetani asipate la kutushitaki Mungu anapokuwa ametuokoa anatupa nguvu dhidi ya mamlaka na utawala wa shetani na shetani hawezi kufurahia kuanguka kwetu au kupatikana kwetu katika lawama ni njia yake ya kututamani ili kwamba turejee katika utawala wake, njia pekee ni kujitia nidhamu ni kuishi kwa kiasi.

2.      Biblia inatukumbusha namna nyingine ya kumshinda mshitaki wetu ni kuendelea kumwangalia Yesu Kristo ambaye kwa upendo wake mkubwa alitufia msalabani na zaidi ya yote ndiye anayetuombea, lazima tujue kuwa ni vigumu kutenganishwa na upendo huu Warumi 8:33- 39Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.     Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu, Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki, iko wazi kuwa haki tuliyonayo sio haki yetu wenyewe ni haki inayotokana na Kristo, ni muhimu kwetu kuendelea kuwa kuishi kwa imani na kuendelea kuaminikatika upendo wake nayeye mwenyewe atamkemea Shetani, kama ilivyokuwa kwa kuhani mkuu Zekaria, Shetani alipomshitaki Malaika alimtetea na kumtaka bwana amkemee, lazima tuendelee kumwangalia Yesu kama mtetezi wetu aliye hai.

3.       Damu ya Yesu ni jibu lingine la kumshinda mshitaki wetu, Yohana 12:10-11Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. Kama tukiwa na hisia za hatia tusiogope hatia sio jambo baya kusudi lake ni kutuleta katika toba, na toba hii inatupa wepesi wa kusamehewa na kuitumia damu ya Yesu kwa imani iliyomwagika msalabani tu narudi katika kuhesabiwa haki na shetani anapoteza nafasi ya kutushitaki.
4.      Yesu Kristo ni mpatanishi wetu Ni lazima tuelewe kuwa tunaye mpatanishi anayestahili yeye ndiye anayeweza kusimama mahali palipobomoka kati yetu na Mungu na kutupatanisha hatupaswi kuogopa turudi kwa mung mara tunapogundua kuwa tumemkosea na Kristo kama wakili wetu anatuombea kwa baba na kutupatanisha na Mungu kabla ibilisi hajapata la kutushitaki 1Yohana 2:1-2Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,  naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” 

        Hatupaswi kuogopa na kufikiri kuwa kila kitu kimeisha eti kwa sababu tulikosea jambo la msingi ni kurudi kwa Mungu na pia kuelewa kuwa tunaye mpatanishi na atafanyia upatanisho na Mungu.

5.      Usishitaki watu wa Mungu bali uwaombee, watu wengi wa Mungu hasa wana tabia ya kushutumu sana wanapoona makosa ya wengine badala ya kuwaombea Mungu kamwe hafurahii tabia ya aina hiyo, Mungu anaweza kukuhukumu wewe kwa vile unageuka na kusimama katika nafasi ya shetani kosa kama hili liliwahi kufanywa na Nabii Eliya Warumi 11: 2-4Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu, Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu. Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali”. Wakristo ni lazima wajifunze kuombeana na kusamehe kwa haraka kutokusamehe kwa haraka ni kumpa ibilisi nafasi Efeso 4:26-27 inasema “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.” Shetani anapataje nafasi ni kwa watu kutokusameheana nah ii inaweza kumpa yeye wakati wa kutushitaki kwa kulijua hili Paulo mtume aliagiza msamaha kwa ndugu aliyefanya dhambi na kupokea maonyo, alilisihi kanisa kumsamehe mtu huyo, kwani kama wasingelifanya hilo shetani angeweza kuwashinda angalia 2Wakoritho 2:10-11Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo, Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.” Unaweza kuona kumbe kutokusamehe kunaweza kumpa ushindi mshitaki wetu ni lazima tuwe wenye kusamehe na kutokuwashutumu na kuwalaumu wengine, na badala yake kuwaombea vinginevyo shetani atapata nafasi kwetu pia.
Itaendelea na Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!