Jumanne, 11 Juni 2019

Bwana atamwuza Sisera katika mkono wa mwanamke!


Waamuzi 4:1-9Hata alipokufa Ehudi, wana wa Israeli wakafanya yaliyo maovu tena mbele za macho ya Bwana. Bwana akawauza na kuwatia katika mkono wa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori; na Sisera, aliyekaa katika Haroshethi wa Mataifa, alikuwa amiri wa jeshi lake. Wana wa Israeli wakamlilia Bwana; kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma mia kenda; naye akawaonea wana wa Israeli kwa nguvu muda wa miaka ishirini. Basi Debora, nabii mke, mkewe Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule. Naye alikaa chini ya mtende wa Debora, kati ya Rama na Betheli, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu; wana wa Israeli wakakwea kwake, awaamue. Huyo akatuma mtu akamwita Baraka wa Abinoamu toka Kedesh-Naftali, akamwambia, Je! Bwana, Mungu wa Israeli, hakutoa amri, akisema, Enenda, ukawavute kwako, huko katika mlima wa Tabori, watu elfu kumi wa wana wa Naftali, na wa wana wa Zabuloni? Nami nitakuvutia Sisera, amiri wa jeshi lake Yabini, hata mto wa Kishoni, pamoja na magari yake, na wingi wa watu wake; nami nitamtia mkononi mwako. Baraka akamwambia, Kama utakwenda pamoja nami ndipo nitakwenda; bali kama huendi pamoja nami, mimi siendi. Basi akasema, Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini safari utakayoiendea haitakupatia heshima wewe; maana Bwana atamwuza Sisera katika mkono wa mwanamke. Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi.



Utangulizi:-

Ni muhimu kufahamu kuwa katika kanuni za Mungu, Mungu hufanya kazi kwa njia tofauti na njia za wanadamu, na kwa mawazo tofauti na mawazo ya wanadamu, na hata kwa uzoefu tofauti na uzoefu wa wanadamu, Biblia inaonyesha hekima hii ya Mungu na namna yake katika utendaji nwake wa kazi ona:-

1Wakoritho 1:26-29Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu

Katika kitabu cha waamuzi Yaeli ni mojawapo ya mfano wa watu dhaifu ambao MUngu aliweza kuwatumia kuleta ushindi mkubwa kwa wana wa Israel waliokuwa wakionewa na wakanaani chini ya Mfalme Yabin kwa zaidi ya miaka 20, wanawake kumbuka katika jamii ya kiyahudi walikuwa hawapewi umuhimu mkubwa sana waoa hata kuhesabiwa walikuwa hawahesabiki, lakini tunaona Mungu akiwatumia baadhi yao kwa utukufu wake.

Yaeli alikuwa moja ya wanawake ambao Biblia haijawahi kuzungumza habari zao kwa undani, tunajua tu kuwa alikuwa miongoni mwa ma bedui walioishi jangwani na aliyeolewa katika Familia ya Heber mkenizi au mkeni. Mwanamke huyu ndiye aliyetumiwa kukamilisha ushindi wakati wa waamuzi Debora na Baraka.

Israel katika Shida na dhiki.

Ushindi dhidi ya wakanaani ulikuja wakati wana wa Israel wamechoswa na mateso yaliyokuwa yakiwakabili kutoka kwa mfalme wa kanaani Yabin mfalme huyu alikuwa anatawala kanaani na Biblia inasema kuwa alikuwa na Mkuu wa majeshi (Amiri wa majeshi) aliyejulikana kama Sisera, hawa walikuwa na jeshi kali sana Biblia inaeleza kuwa alikuwa na Magari ya chuma mia tisa,  na aliweza kuwaonea sana Israel tena biblia inasema aliwaonea kwa nguvu muda wa miaka 20, halki hii ilikuwa ngumu, Mungu alikuwa kama amewauza yaani ameruhusu wateseke kutokana na kumsahau yeye ingawa yeye hangeliweza kulisahahu Agano lake, hali hii ilipelekea wana wa Israel kulia na kuuugua kwa sababu ya msiba ule wa mateso.

Israel walipolia kwaajili ya mateso yale Maandiko yanaeleza kuwa alikuwepo nabii mke jina lake Deborah aliyekuwa akiwaamua Israel, yeye alijaa Roho na kuambiwa na Bwana amuite mtu anaitwa Baraka ambaye Mungu alimchagua aweze kuyakabili majeshi ya Yabin na kamanda wake Sisera, aliyekuwa Hodari na katili sana na aliyewatesa sana wana wa Israel

Hata hivyo katika namna ya kushangaza Baraka alisisitiza kuwa hawezi kwenda bila Deborah kumbuka Debora alikuwa mwanamke Waamuzi 4:6-9Huyo akatuma mtu akamwita Baraka wa Abinoamu toka Kedesh-Naftali, akamwambia, Je! Bwana, Mungu wa Israeli, hakutoa amri, akisema, Enenda, ukawavute kwako, huko katika mlima wa Tabori, watu elfu kumi wa wana wa Naftali, na wa wana wa Zabuloni? Nami nitakuvutia Sisera, amiri wa jeshi lake Yabini, hata mto wa Kishoni, pamoja na magari yake, na wingi wa watu wake; nami nitamtia mkononi mwako. Baraka akamwambia, Kama utakwenda pamoja nami ndipo nitakwenda; bali kama huendi pamoja nami, mimi siendi. Basi akasema, Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini safari utakayoiendea haitakupatia heshima wewe; maana Bwana atamwuza Sisera katika mkono wa mwanamke. Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi”.


Bwana atamwuza Sisera katika mkono wa mwanamke!

Debora alikubali ombi la Baraka lakini alimueleza wazi kuwa kutokana na ktaka kwenda vitani na mwanamke ili halinyeye ni mwanaume basi Sisera atauawa na mwanmke  na mwanamke huyo ndiye Yael, Majeshi ya Baraka yalijipanga huku Debora nabii akiwa pamoja naye na bwana alianza kuyafadhaisha majeshi ya Sisera na kuanza kuwapiga vibaya jambo lililopelekea Sisera kukimbia ili kuayasalimisha maisha yake, alikimbilia kwa Yael ambaye nyumba yake iliuwa na mani nay eye hivyo alifikiri kuwa atasalimika alifunikwa na nguo nzito ili kujipumzisha na alipoomba maji ya kunywa alipewa maziwa, maziwa huwa yana tabia ya kuleta usingizi mzito sana na yael alipoona Sisera amelala alichukua mambo na nyundo na kuipigilia kichwani mpaka ardhini na kumuua.

Waamuzi 4:21-24Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akashika nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akamtia kile kigingi katika kipaji chake, nacho kikapenya, hata kuingia mchangani; kwa maana usingizi mzito ulikuwa umemshika; basi akazimia, akafa.  Na tazama, Baraka alipokuwa akimfuatia Sisera; Yaeli akatoka ili kumlaki, akamwambia, Njoo, nami nitakuonyesha yule mtu unayemtafuta. Basi akamwendea, na tazama, Sisera amelala humo, amekufa, na hicho kigingi kilikuwa kipajini mwake.  Basi hivyo Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani mbele ya wana wa Israeli siku hiyo. Mkono wa wana wa Israeli ukazidi kupata nguvu juu ya Yabini, mfalme wa Kanaani, hata walipokuwa wamemwangamiza Yabini, mfalme wa Kanaani.”

Njia za Mungu sio njia zetu, ni muhimu kufahamu kuwa Nabii katika Biblia anasimama kwa niaba ya watu wa Mungu na Mwanamke anasimama kwa niaba ya kanisa, Kanisa likiomba ni lazima ifahamike kuwa kuna nguvu kubwa sana ya ajabu iliyofichika katika kanisa lake kila mtu anaweza kujipatia ushindi mkubwa kupitia Yesu Kristo, yeye hataweza kulisahahu agano lake alilolifanya nasi pale msalabani atatupa ushindi kwa dhahiri,

·         Ushindi wako hautakuja katika njia ya kawaida unayoidhani Mungu anakwenda kufanya jambo jipya litakalokushangaza

·         Mungu atatumia ulicho nacho katika mkono wako kukupa ushindi nalitumia nyundo na mambo tu kumaliza tatizo kubwa lililodumu kwa miaka 20

·         Haijalishi kuwa tatizo lako lilikuwa baya au ni baya kiasi gani na limekugharimu miaka mingapi leo kwa neno la kinabii kama la Debora ninatamka muujiza na uponyaji kwaajili yako katika jina la Yesu

·         Haijalishi adui yako ana nguvu kiasi gani Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa lakini alikimbia mbele ya upanga wa Baraka nataka nikuambie na nkukutamkia kinabii leo kuwa kwa jina la Yesu Kristo aliye hai tatizo lako lazima likimbie mbele yako bila kujali kuwa lina nguvu kiasi gani
·         Haijalishi kuwa hujajibiwa mamombi kwa muda gani lakini leo natabiri kwako katika jina la Yesu Kristo Israel waliteseka kwa miaka 20 lakini ka neno la Nabii Debora na na upanga wa Baraka siku moja tu ilileta ushindi mkubwa katika maisha ya Israel na kuwafanya salama leo ninatangaza usalama wako natangaza kwa neno la kinabii na uweza wa jina la Yesu kuwa utajibiwa maombi yako

·         Mungu anakwenda kuzigeuza fadhaa zako kuwa furaha, adui zako kuwa watumwa wako, watesi wako kuwa wakimbizi, waoneziwako kuwa waonewa, waliokutisha kuwa waoga, natangaza mapinduzi ya kijeshi dhidi ya nguvu za giza, dhidi ya majeshi yanpopi wabaya katika ulimwengu wa Roho kwa jina laYesu Kristo na kwa njia ya imani natanmka ushindi dhidi ya msomaji wangu namsikilizaji wangu awekwe huru na amani idumu kwake


·         Hajalishi kuwa kesi yako imesumbua kwa miaka mingapi, wanaokudai hawajarudisha madeni, waliokudhulumu na kukuonea Nasimamisha mwamuzi leo, tunaye muamuzi leo,. Muamuzi wetu leo sio Baraka wala sio Debora wala sio Yael Yuko muamuzi  mwenye haki aliyetupa ushindi kwa njia ya Msalaba huyu ni mwanaume anaitwa Yesu, na akuweke huru leo na akutetee na akutegemeze na akukomboe na akupe furaha na akufungue na akukumbuke na akutazame na akusikie na akufariji na akuinue dhidi ya udhalimu wa kila aina katika masiha yako!

·         Yail hakutumia nguvu hakuwa na uzoefu wa vita hakwenda hata vitani hajui hata kupigana lakini ndiye aliyeu Shujaa aliyesumbua Israel kwa miaka 20, Ndugu zangu neema ya Mungu ikiwa juu yako hakuna kitakachoweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako!

Ramakarashat! Rimasakarutarama! sakatarino, trembeshederengendebe! rimosakarapati yetereseka yatoroseka yakarakata yatoromoskomoli, yenderebisakuramato rimamama sakarenderebe katabash karabakat yerekerebeshe masokolipatei birikuromoto sakarambat.

Nakuombea neema ya Mungu kila amwaminieye hatatahayarika  atakupa kushinda, na kukutetea na kukufungua uwe mtu wa kipekee mtu wa tofauti mtu wa kushangaza na kwa njia laini bwana ana atende na kukutetea dhidi ya uonevu wa kila namna katika jina la Yesu amen. Adui yako na auzwe kwenye mkono wa mwanamke tu. Na aaaibike kwa namna ya ajabu katika Jina la Yesu, amen. Mungu bhatafanya kwa sababu ya ujuzi wetu, uzoefu wetu, elimu yetu bali atafanya kwa sababu ya neema siri ya ushindi wa kanisa ni neema sio mazoezi, sio nguvu, sio uwezo ni neema yake neema yake na iwe juu yako kama ilivyokuwa kwa Yael

Rev. Innocent Kamote.
Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.