Ijumaa, 26 Juni 2015

Craetion Theory against Evolution Theory




SOMO: BISHANO KATI YA UUMBAJI NA MABADILIKO YA VIUMBE
(Creation theory against Evolution Theory)

Kwa miaka Mingi sana sasa karibu 133 Dunia imekuwa taabuni sana na usumbufu mwingi umetokea kutokana na kuvumiliwa vya kutosha kwa mafundisho potofu ya Charles Darwin, kuhusu uumbaji, Dunia nzima imekubali mafundisho haya yaweze kufundishwa mashuleni na kuharibu imani ya vijana wetu au kuwaingizia wazo la kukataa uumbaji wa Mungu na kutokuyaamini maandiko, Imani ya Kikristo, Kislamu na Kiyahudi, kwa Pamoja hazikubaliani kabisa na mafundisho hayo yenye nia ya kumkataa Mungu, Biblia inaonya vikali juu ya wazo la kumkataa Mungu kuwa linaleta upumbavu miongoni mwa wanadamu

Warumi 1:18-23 na 28-32 Biblia inasema hivi

[“18. Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu. 19. Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia. 20. Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru; 21. kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.      
22. Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; 23. wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.

28. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.  29. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, 30. wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31. wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; 32. ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao. ] 



Biblia inaonya vikali kuwa hatupaswi kuyafuata mawazo hayo ya kipumbavu, na kuwa sio kuyafuata tu hata kuyaunga mkono yaani kukubaliana na wayatendao!

Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia maswala kadhaa yafuatayo

·         Maana ya neno wazo (Theory)
·         Wazo la Mabadiliko ya Viumbe  (Evolution Theory)
·         Wazo la Uumbaji (Creation Theory)

1.       Maana ya neno wazo (Theory)
Neno theory kwa tafasiri ya Oxford Advanced Learners Dictionary Linasomeka hivi “Theory is a formal sets of Idea that intended to Explain why something happens or Exist” kwa tafasiri isiyo rasmi tunaweza kusema hivi  “wazo ni kikundi cha Fikra zinazokusudia kuelezea kwanini jambo au kitu kimetokea au kuwepo” Hivyo ni muhimu kugahamu kuwa tunapozungumzia Mabadiliko ya viumbe Evolution theory tunazungumzia wazo, na tunapozungumzia  wazo la Uumbaji Creation Theory Tunazungumzia Kweli ya Mungu, Kwa vile wazo la uumbaji asili yake si mwanadamu ni neno la Mungu na wazo la Maendeleo ya viumbe asili yake ni mwanadamu.
2.       Wazo la mabadiliko ya viumbe (Evolution Theory)
Evolution maana yake kupitia Oxford Advanced Learners Dictionary it is the gradual development of plant or animal for over many years of adapt to changes in their environment kwa tafasiri isiyo rasmi ni Maendeleo ya kimabadiliko ya mmea au mnyama yanayotokana na kukabiliana na mazingira yake.

Mawazo haya yanasisitiza kuwa mwanadamu pia ni kiumbe aliyebadilika kwa miaka kadhaa kwa kadiri alivyokuwa akikabiliana na mazingira yake, na kuwa kuweko kwake hakutokani na kuumbwa lakini asili ya viumbe vyote ni maji na kujiendeleza kwa viumbe hivyo

Mwanzilishi wa wazo hili anajulikana kama Charles Darwin ambaye aliishi kati ya 1809 – 1882 Yeye alikuwa ni mtoto wa Mchungaji na Mkristo na alijiingiza katika maswala ya sayansi ya wanyama, alikuwa Muingereza,alizaliwa huko Shrewsbury February 12 1809 katika familia iliyokuwa na uwezo kama mtoto wa tano, alisomea maswala ya Madawa huko Edinburgh na baadaye kuachana na shughuli hizo na kujiunga na chuo kikuu cha Cambridge akijiandaa kuwa mtumishi wa Kanisa, ingawa Darwin alikuwa akijinadi kama mkristo baadaye aliukana ukristo na alikana kuwepo kwa Mungu, na lengo lake kubwa katika wazo lake hili lilikuwa ni kukanusha kuwepo kwa Mungu, Hata ingawa Darwin alikanusha madai hayo lakini wazo lake limatia moyo   na matokeo yake ni kuukanusha uumbaji wa Mungu na hili ndio kusudi kuu la kuwepo kwa wazo hili

Biblia inasema mpumbavu amesema Moyoni hakuna Mungu, wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema, Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu,Wote wamepotoka wameoza wote pamoja, Hakuna atendaye mema La hata mmoja, Zaburi 14:1-3, 53:1

 Ni muhimu kufahamu kuwa kwa namna yoyote ile tusikubali mawazo haya ya kipumbavu yakafundishwa kwa vijana wetu mashuleni, na ama kama serikali imeyapitisha yafundishwe ni muhimu dhana hii ikashughulikiwa vilivyo na wazazi, wachungaji na watu wote wenye mapenzi mema, hatukubali waka kama mkuu wa wajenzi mweye Hekima sikubali kujiunga na kundi hili la kipumbavu lenye mlengo wa kumkataa Mungu na uumbaji wake

Biblia inaonyesha ya kuwa kuelimika kwenye faida na maarifa kunaanza na kumcha Mungu Mithali 1;7 “kumcha Bwana ni chanzo cha Maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu” Hakuna udhuru kwa vile uumbaji unadhihirisha wazi kuwa Mungu yuko, na wazo la aina hii ni la kipumbavu na lenye kumvunjia Mungu heshima Warumi 1:21 kwa Sababu walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu, wala kumshukuru, bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza”

Watanzania kama tunataka Baraka katika taifa letu ni lazima tukiri na kukubali kuwa Mungu yupo, Serikali yetu inaweza isiwe na Dini kama inavyoelezwa lakini Lazima iwe na Mungu, Lazima tutambue kuwa Mungu Muumba wa Mbingu na nchi na vyote viujazavyo yuko, na nilazima tumuogope na kuwafundisha watoto wetu kumuogopa na kumtambua!

Tukirihusu ujinga huu kuendelea kufundishwa Mashuleni inaweza kuja kutushangaza kuwaona watoto wakirudi shuleni wakina na mashaka na Tourati, Zaburi, na Injili kwa ujumla wataanza kuwa na mashaka na maandiko matakatifu, ni lazima tuwakumbushe kuwa dhana hizo ni mawazo tu na sio ukweli “this teaching is only a theory (an opinion based on observation) But its not reality”  by Master Mason Rev. Innocent Kamote.

3.       Wazo la uumbaji (Creation Theory)
Watu wanaoamini katika wazo la uumbaji kwamba Mungu aliziumba mbingu na nchi, wako sahii na wanamuamini Mungu na maandiko Matakatifu, Biblia katika kitabu cha Mwanzo inatuonyesha kuwa Mungu aliumba na kuanzisha kila kitu, Mwanzo 1:1 Hapo Mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi, Mwanzo 2:1 Basi Mbingu na nchi zikamalizika na jeshi lake lote” ni wazi kuwa Mungu aliumba kila kitu katika hali kamili kabisa, hakuna kiumbe ambacho kilibadilika kutokana na mazingira, Biblia katika kitabu cha Mwanzo inaonyesha
·         Mwanzo wa Anga, Mwanga, Ulimwengu sayari dunia, jua mwezi na nyota 1-1-18
·         Mwanzo wa Maisha na uhai Mwanzo 1:19-25
·         Mwanzo wa Binadamu Mwanzo 1:26-31 na 2
·         Mwanzo wa dhambi ulimwenguni Mwanzo 3:1-7
·         Mwanzo wa mpango wa ukombozi Mwanzo 3:8-24 na hasa 15
·         Mwanzo wa maisha na familia Mwanzo 4:1-15
·         Mwanzo wa ufugaji, na kilimo Mwanzo 4:2
·         Mwanzo wa kuabudu Mwanzo 4:1-7
·         Mwanzo wa mauaji Mwanzo 4;8
·         Mwanzo wa maendeleo makubwa, ufalme na miji Mwanzo 4:16-9:29 hasa 4:17
·         Mwanzo wa Ibada ya kweli hadharani Mwanzo 4:26
·         Mwanzo wa Mataifa Mwanzo 10:1-11:32
·         Mwazno wa Lugha mbalimbali Mwanzo 11:1,6-9
·         Mwanzo wa Taifa Teule Israel Mwanzo 12-50

Biblia inathibitisha kuwa Mungu alipomuumba mwanadamu alimuumba akiwa na akili kamili kabisa na alimpa wajibu wa kuilima na kuitunza Bustani ya Aden  Mwanzo 2:19-20, 15 Biblia inaonyesha kuwa Adamu alitoa majina kwa wanyama wote na aliwekwa katika Bustani ya Aden ili ailime na kuitunza Mwanadamu aliumbwa akiwa na akili timamu na uwezo mkubwa wa kuleta maendeleo, wanadamu walipewa Lugha na Mungu hivyo si kweli kuwa lugha ni sauti za Nasibu. Mwanadamu sio Nyani wala Sokwe

Mungu alipokwisha kuumba alijisifia na kuufurahia uumbaji wake kwa kusema Mwanzo 1:31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya na tazama ni chema sana. Biblia inaonyesha kuwa uumbaji wa Mungu ni kamili na hahukuhitaji “process from primitive to Perfect” 

Wazo la Darwin linaanzia na kile ambacho Mungu amekifanya, watu waoamini katika dhana hii hawawezi kujibu swala
1.       Ulimwengu na vyote viujazavyo vimewezaje kuweko?
2.       Maisha na uhai ulijianzishaje?
3.       Makusudi ya Mwanadamu Duniani ni nini?
4.       Hatima ya mwanadamu ni nini?
Ni wazi  Kabisa kuwa hata kisayansi wazo hili haliwezi kuthibitika kwa vile sayansi inataka Uchunguzi (Utafiti) observation Majaribio (tested) na Uhalisia (Naturalistic Evidence) Mpaka sasa hakuna mwanadamu anaweza kufanya njia hizo kuu za kisayansi na kuthibitisha wazo la Darwin, kwa hiyo mtazamo wa Darwin ni mtazamo tu na wala sio Sayansi
ü  Mawazo ya Darwin hayatambui kuwa Sayansi ina mipaka na haiwezi kujitosheleza kuelezea uumbaji
ü  Inafundisha dhana na mawazo tu na inatafasiri vibaya maandiko matakatifu na taarifa zake
ü  Inakazia mawazo ya kisayansi kamma kwamba ndio ukweli halisi
Biblia
ü  Inaelezea vema na kutambua sababu na kusudi la uumbaji
ü  Inaelezea na kuchambua kwa undani kuwa Mungu ndiye muumba na kuwa waliumba viumbe kamili na kila kimoja kwa aina zake na hakuna mchakato endelevu wa kubadili viumbe hao, Nyani wataendelea kuwa nyani na binadamu wataendelea kuwa binadamu


Wagalatia 1:9 Kama tulivyotangulia kusema , na sasa nasema tena mtu awaye yote  akiwahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo mliyoipokea na alaaniwe

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.