Jumanne, 27 Juni 2023

Jinsi ya kufanya agano la chumvi




Wakati wa kufanya agano la chumvi.

  1. Mizimu, mapepo, shetani na wachawi na waganga au makuhani wa kichawi huwaathiri watu katika maisha yao na kusababisha msongo wa mawazo, kwa kutumia nguvu za giza, kwa kutumia nguvu hizo za giza na za kichawi wanawasababishia watu kupoteza mwelekeom kuwa na bumbuwazi, kuteseka, kuelemewa, kuwa na uzito na kupata changamoto za kifedha na kiuchumi na changamoto nyinginezo nyingi.

 

Uchawi ni silaha ya giza inayotumiwa na wachawi kwa kusudi la kuharibu maisha ya watu wanaofanikiwa na kufanikiwa  katika mazingira mbalimbali, silaha hiyo ya giza ni silaha ya kiroho lakini matokoe yake hutokea katika hali halisi.kuteseka kwa watu waliorogwa au kuchawiwa kunategemeana na nguvu iliyotumika katika kunuiziwa nguvu za mashambulizi

Pepo watatafasiri uchawi na manuizo na kuyawasilisha kwa watu waliolengwa na kuwashambulia na matokeo yanaweza kutokea katika ulimwengu wa miili yao, mambo magumu na matukio ya ajabu huanza kutiokea katika maisha yao na njia pakee ya kuimarisha na kuleta ukombozi ni agano la chumvi

 

Ukombozi kupitia gano la chumvi ni rahisi sana kwa muonekano lakini una nguvu kubwa za ajabu sana, ukombozi huu una nguvu ya kuondoa kabisa maedhara ya nguvu zisizoonekana za kichawi na kuukausha au kuuondoa kabisa na kuondoa hali ya kushindwa kwa sababu zozote zile, kwa kufanya hivyo haimaanishi oia mkuwa tutaacha kabisa kuschughulikia nguvu za giza kwa namna za kawaida, lakini tutaendelea ili kuhakikisha kuwa tunaendelea kukua kiroho.

 

  1. Unafanya gano la Chumvi wakati gani?

 

Tunafanya agano la chumvi wakati tunapohisi kuwa kuna matukio ya vita za kiroho zilizohusisha nguvu za giza, ni kweli kwamba mtu aliyeokoka hawezi kushambuliwa na nguvu za giza kwa sababu imeandikwa hakuna ugaga wala uchawi juu ya Yakobo Hesabu 23:23  “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!

 

Lakini kumbuka tuna mashambulizi kutoka kwa mamadui, tuko vitani, majeshi ya pepo yanatumwa kwetu kwa mauizo na sadaka za iana mbalimbali na kwa maelekezo ya aina mbalimbali kwa hiyi kuna kiwango cha mashambulizi ambayo tunakutana nayo wakati mwingine kwa asilimia 30 au 60 au 90 kwa hiyo wote kwa kiwango Fulani tunashambuliwa na nguvu za giza kulingana na kiwango za kuzaa kwetu matunda kumbuka mfano wa zile mbegu zilizoangukia kwenye udongo mzuri Marko 4:8 “Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.” Kama ukuaji wetu wa kiroho unaweza kuzaa matunda kwa asilimia hizo zilizotajwa ni dhahiri na mashambulizia yanaweza kuwepo kutokana na kiwango kwa hiyo niia nyepesi ya kuondoa kiwango hicho cha mashambulizi ya nguvu za giza ni kwa kutumia ganano la chumvi  na ukifanya mara kwa mara unaziondoa kabisa katika mwili wako  tunaweza kujitibu kwa agano la chumvi mara unapohisi au kusikia changamoto hizi:-

 

-          Uchovu wa kimwili na kiroho

-          Kupoteza hamasa

-          Kupoteza uwezo wa kufikiri

-          Kuelemewa na mawazo

-          Hasira za kupita kawaida

-          Mgandamizo wa mawazo stresses

-          Aina yoyote ya ugonjwa na wakati wowote unapokuwa unahisi kuwa kuna uvamizi na hali isiyo ya kawaida katika mwili wako, uchumi wako, kazi yako, huduma yako na roho yako.

-          Lakini pia udhaifu wowowte wa kimwili, kiroho na kihisia ujue kuna mashambulizi ya mizimu, mapepo, wachawi na kadhalika basi unahitaji tiba ya agano la chumvi.

 

  1. Mambo unayohitaji kwaajili ya kutekeleza agano la chumvi

 

-          Utahitaji ndoo au beiseni

-          Utalijaza maji safi kwa asilimia 50% yaani nusu

-          Utahitaji chumvi yam awe kwa kiwango chochote kana huna ya mawe unaweza kutumia ya mezani lakini ya mezani uwezo wake utapungua kwa asilimia 30% ukilinganisha na ile ya mawe

-          Taulo la kujikaushia

-          Na sehemu ya kukanyajia

-           

  1. Jinsi ya kufanya ibada ya agano la chumvi.

 

1.       Weka maji kwenye ndoo yajae kwa asilimia 50% yaani nusu yake kwa kiwango tu cha kufunika enka za miguu

2.       Weka vijiko vidogo viwili vya chumvi ya mawe

3.       Omba kwa kumaanisha na kwa imani kwamba Mungu akuondolee nguvu zote za giza, pia omba maalumu kwaajili ya kuziharibu kabisa na kuzibomboa nguvu zote za mizimu, pepo, waganga na wachawi na kila manuizo yaliyofanywa kinyume nawe na kukuletea athari, omba maombi ni muhimu sana na yana uwezo mkubwa sana yanapofanyika sambaba na ibada hii ya ukombozi.

4.       Hakikisha umekaa sawa sawa na miguu yako hususani enka ziwe zimezama katika maji, miguu yako isigusane bali iwe mbalimbali kati ya sentimita 2-3 hii inasaidia kuodoa uchawi wote uliorogwa kwa nguvu za giza, kama miguu yako itagusana itakuwa kikwazo kwa ibada hii, 

5.       Hakikisha miguu inakaa kati ya dakika 10-15 na usizidishe zaidi ya dakika 15, ukizidisha nguvu za giza zinazotoka kwa njia ya miguu zinaweza kuingia mwilini mwako

6.       Wakati miguu yako inapokuwa katika maji yenye chumvi anza kuomba au kunuiza kwa jina la Yesu  Mungu au kuimba maombi

7.       Wote wenye pumzi wote waishio duniani wote wampendao  (Wamchao) Mungu na waseme fadhili zake ni za milele

8.       Wote wanaoeneza habari zake watangazao habari njema duniani kote na waseme fadhili zake ni za milele.

 

Kwa ufupi utaimba zaburi 118:1-14         

1. Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

3. Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

4. Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

5. Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.

6. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

7. Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.

8. Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.

 

9. Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.

10. Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

11. Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

12. Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

13. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.

14. Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.

 

Hitimisho:

Baada ya kumaliza maombi haya ya ukombozi kulinga nan a mahitaji yako unaweza kuanza kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake anaokupa na namna anavyokuzunguka

Utayamwaga maji yake chooni na kisha utasafisha ndoo na maji safi. Utakausha miguu yako vema kwa taulo na kisha utajipaka mafuta ya mzeituni na kuomba Mungu akupeleke kwenye kiwango kingine cha maswala mbalimbali uyatakayo. Ibada inaweza kufanyika pia kwa makusudi mbalimbali ambayo mengine hayajaainishwa katika somo hili mfano kuweka wakfu, kiongozi, kujilinda na cheo chako na kadhalika

Mwisho wa ibada hii.

Matokeo:

  1. Athari zote za nguvu za Giza na mashambulizi ya wachwi, waganga na mapepo na shetani zinaondoka
  2. Maji ya agano la chumvi yana nguvu kubwa sana yenyewe tu kunyonya nguvu zote za giza
  3. Nguvu za giza na magonjwa yote yanayoambatana na nguvu hizo yanaondoka na wakati mwingine maji yanaweza kuwa na rangi nyeusi kama ishara ya kuondoka kwa nguvu hizo, au yanaweza kuwa na uvuguvugu au yakawa na harufu mbaya hii ni shara ya vitu vibaya kuondoka mwilini mwako

 

KUMBUKA:  Somo hili lina uhusiano na huduma za kinabii, sio vizuri kufundisha au kulifanyia kazi kanisani ikiwa huamini katika huduma za kinabii

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

 

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima


Agano la Chumvi!


2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?” 



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Chumvi ni moja ya madini muhimu sana duniani, na kuwa chumvi ina matumizi mengi na makubwa zaidi ya kunogesha ladha ya chakula, Chumvi imekuwa ikitumika katika jamii na tamaduni mbalimbali duniani kwa matumizi mengi tofauti tofauti, Neno Mshahara kwa kiingereza ni “SALARY” inasemekana neno hili chimbuko lake ni neno “Salt – Money” likimaanisha fedha inayostahili hela ya chumvi kwa askari wa kirumi, yaani malipo ya mshahara yalikuwa ni kwaajili ya kununulia chumvi, Kutokana na umuhimu wa chumvi katika nyakati hizo!

Chumvi ilitumika nyakati za zamani kumaanisha urafiki wa kudumu, au kutimiza ahadi miongoni mwa watu na kwa wayunani (Greeks) waliihesabu chumvi kuwa ina asili ya uungu, Katika tamaduni za kiarabu hata sasa endapo watu wawili walipatana jambo walijiapiza na kulamba chumvi wakimaanisha ni patano la kulindana milele, ni ishara ya uaminifu wa kudumu na hata kama ikitokea kuwa wamekuwa maadui au walikuwa maadui walipaswa kuheshimu kulindana huko endapo walifanya patano au agano la chumvi.

Nyakati za agano la kale walipofanya agano la patano katika ya mtu na mtu mapatano hayo yaliweza kuthibitishwa na kulamba chumvi mbele ya mashahidi na tendo hili lingemaanisha kuwa ni patano la kudumu, Ahadi ya kudumu milele, ahadi isiyoweza kuvunjika na kama mtu ataivunja aharibikiwe vibaya na kupata madhara makubwa sana.

Kwa msingi huo unapoona katika maandiko 2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?Mfalme Abiya Hapa alikuwa akizungumza na Israel na Yeroboamu kuwaonya wasipigane naye na kuwajulisha kuwa Mungu yuko Pamoja na ufalme wa agano na Daudi kwa sababu lilikuwa ni agano la chumvi, Abiya aliwathibitishia Israel kuwa watapigwa Na kamwe hawataweza kushindana na ufalme wa ukoo wa Daudi kwa vile ana agano la chumvi na Mungu, akimaanisha agano thabiti, lisiloweza kubatilika la ahadi ya Mungu aliyoiweka kwa Daudi na uzao wake milele na kwamba hakuna mtu anaweza kuiharibu.

Nyakati za agano la kale maandiko yaliamuru kila aina ya sadaka za mbegu na nafaka ziambatanishwe na chumvi ili kufanya “agano la chumvi” kila aina ya sadaka ya nafaka iliambatanishwa na chumvi angalia

Mambo ya walawi 2:13 “Tena, kila toleo la sadaka yako ya unga utalitia chumvi; wala usiiache sadaka yako ya unga kupungukiwa na chumvi ya agano la Mungu wako; utatoa chumvi pamoja na matoleo yako yote.”  

Aidha Mungu alipowachagua wana wa walawi kuwa makuhani wake kwa vile hawakuwa na urithi Mungu aliwapatia chakula kupitia sadaka zilizoletwa na watu wake na jambo hili Mungu aliliita “Agano la Chumvi”

Hesabu 18:19 “Sadaka zote za kuinuliwa za vitu vitakatifu, wana wa Israeli wavisongezavyo kwa Bwana, nimekupa wewe na wanao na binti zako pamoja nawe, ni haki yenu ya milele; ni agano la chumvi la milele mbele za Bwana kwa ajili yako, na kizazi chako pamoja nawe.

Hapa Mungu alikuwa anamaanisha kuwa patano hilo au agizo hilo ni la kudumu na halitaweza kubatilishwa ni agano la chumvi! Vilevile ukuhani wake na kabila ya lawi ni wa milele. Kwa msingi huo utaweza kuona kuwa wzo kuhusu chumvi lilipewa umuhimu mkubwa sana katika maandiko, Leo chumvi inapatikana kwa urahisi katika tamaduni nyingi ikiwa na umuhimu uleule japo inaweza isihitajike sana katika uhifadhi kutokana na teknolojia ya kuwepo kwa mafriji majumbani, lakini nyakati za Biblia chumvi ilikuwa na umuhimu mkubwa sana kwaajili ya kutunzia vitu visiharibike kama tu ilivyokwa mafriji leo, na ndio maana utaweza kuona katika mifano ya Yesu aliwataja wanafunzi wake au kanisa kuwa ni chumvi ya ulimwengu akimaanisha vilevile kuwa usalama wa ulimwengu unategemea sana uwepo wa kanisa ili kuutunza usiharibiwe na uovu

Mathayo 5:13 “Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.” Kwa msingi huo neno la Mungu linapozungumzia kuhusu agano la chumvi linazungumzia katika uelewa kuwa ni uaminifu wa Mungu katika kutunza ahadi zake kwa mwanadamu bila kuvunjia, ni tabia ya Mungu kuendelea kuwa mwema hata katika mazingira ya udhaifu wa kibinadamu yeye anabaki kuwa mwaminifu.

Chumvi inahusishwa na umilele

Chumvi imekuwa ikijulikana tangu zamani kuwa inauwezo wa kutunza vitu visiharibike, ina uwezo wa kulinda, na inawezekana Mungu aliamuru matumizi ya chumvi katika kutunza nyama ili isiharibike idumu lakini iwe na ladha na hivyo chumvi ilikuwa kitu cha thamani kwa makuhani ambao waliishi kwa kuitegemea sadaka za kila siku.

Wazo la agano la Chumvi linabeba uthamani mkubwa kutokana na uwezo wake wa kutunza kitu kwa muda mrefu na wa kudumu bila kuharibika, Nyakati za Biblia na mpaka wakati wa Kristo Chumvi ilikuwa ni bidhaa ya thamani kubwa sana, Na kwa msingi huo ndio maana utaweza kuona Yesu akiwaambia wanafunzi wake kuwa ninyi ni “Chumvi ya ulimwengu” akimaanisha kuwa watu waliomuamini Yeye wanathamani kubwa sana Duniani kwaajili ya kuitunza na kuishawishi dunia kuishi katika haki sawa na injili yake aidha Yesu alitaka kuonyesha kuwa wanafunzi wake wanapaswa kuwa watu watakaodumu na ambao ni vigumu kuharibiwa! 

Mathayo 5:13 “Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.”

Yesu hatarajii awaye yote ambaye amemuamini aharibike na kufikia hatua ya kushindwa kabisa kuwa ladha kwa ulimwengu, Chumvi yenyewe ni ngumu sana kuharibika lakini vilevile hufanya vitu vingine visiharibike, chumvi inadumu, chumvi inazuia uharibifu, chumvi inaleta ladha, chumvi ni tiba inaleta uponyaji, chumvi inadumisha, ingawa tuna namna nyingine nyingi leo za kuzuia vitu visiharibike lakini bado chumvi imekuwa ni njia bora na ya kale zaidi ya kuhifadhi vitu visiharibike. Kwa msingi huo unapozungumza chimvi unazungumzia kudumu milele na kutokuharibiwa!

Chumvi pia katika mafundisho ya Yesu Kristo ilihusika kumaanisha agano la amani na watu wote, kwamba tuwe na moyo wa chumvi ndani yetu kwa kuwa na amani sisi kwa sisi, kuwa na uhusiano usioharibika, Kristo anatarajia kuwa wanafunzi wake watakuwa watu wenye amani ya kudumu na isiyoweza kuharibika kwa namna yoyote, kwa msingi huo kwa Mungu anashangaza sana pale wanafunzi wake wanapoharibu mahusiano, wanapokuwa na bifu la kudumu, wanaposhindwa kusameheana wanaposhindwa kupatana na wanaposhindwa kuwa na amani wao kwa wao na hata ndoa ya kikristo kuvunjika pia ni sawa na chumvi kuharibika ni jambo baya ambalo kimsingi ni jambo lisilotarajiwa litokee!

Marko 9: 50 “Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi” 

Hivyo chumvi ni agano la Amani chumzvi haitarajiwi kuharibika hcumvi haitarajiwinkutikufaa tena chumvi haitarajiwi kuruhusu uharibifu.

AGANO LA CHUMVI.

Neno agano la chumvi limejitokeza mara tatu katika maandiko, huenda inamaanisha kuhusu utatu, kwa maana nyingine linamuhusisha Mungu, Ukiacha andiko la Msingi sehemu nyingine ni

Hesabu 18:19 “Sadaka zote za kuinuliwa za vitu vitakatifu, wana wa Israeli wavisongezavyo kwa Bwana, nimekupa wewe na wanao na binti zako pamoja nawe, ni haki yenu ya milele; ni AGANO LA CHUMVI LA MILELE mbele za Bwana kwa ajili yako, na kizazi chako pamoja nawe.

Na utaweza kuona tena katika Walawi 2:13 “Tena, kila toleo la sadaka yako ya unga utalitia chumvi; wala usiiache sadaka yako ya unga kupungukiwa na chumvi ya agano la Mungu wako; utatoa chumvi pamoja na matoleo yako yote.”

Mungu alifanya maagano kadhaa na watu wake mbalimbali akitumia alama mbalimbali muhimu za kupita kawaida.

·         Agano la Mungu na Nuhu lilihusisha upinde wa Mvua.

 

Mwanzo 9:15-17 “nami nitalikumbuka agano langu, lililoko kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili, wala maji hayatakuwa gharika tena kuwaharibu wote wenye mwili. Basi huo upinde utakuwa winguni; nami nitauangalia nipate kulikumbuka agano la milele lililoko kati ya Mungu na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili kilichoko katika nchi. Mungu akamwambia Nuhu, Hii ndiyo ishara ya agano nililoliweka kati yangu na wote wenye mwili walioko katika nchi”.

               

·         Agano la Mungu na Ibrahimu lilihusisha Nyota na tohara ya govi

 

Mwanzo 15:5, 18 “Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”, Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

 

Matendo 7:8 “Akampa agano la tohara; basi Ibrahimu akamzaa Isaka, akamtahiri siku ya nane. Isaka akamzaa Yakobo. Yakobo akawazaa wale kumi na wawili, wazee wetu.”

 

·         Agano la Mungu na wana wa Israel kupitia Musa lilihusisha  amri kumi katika Mawe.

 

Kutoka 34:28 “Naye alikuwa huko pamoja na BWANA siku arobaini na masiku yake; hakula chakula, wala hakunywa maji. Naye akaandika katika hizo mbao, hayo maneno ya maagano, hizo amri kumi.”

 

·         Agano la Mungu na Mfalme Daudi lilihusisha Chumvi.

 

2Nyakati 13:5 je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?

 

Makusudi makubwa ya somo hili ni kuzungumzia agano hili la chumvi na matumizi ya chumvi katika maeneo mbalimbali ya kiibada kama tunavyoweza kuona katika siku za karibuni kukiwa na matumizi makubwa sana ya chumvi maarufu kama chumvi ya upako!

Matumizi ya Chumvi.

Kwaajili ya kuleta ladha – Chumvi inatumika katika kuleta ladha na utamu katika chakula au kinywaji au kitu kingine kwa kuchanganya na chumvi na kuleta ladha

Kwaajili ya Kutunza – Chumvi inatumika kuhifadhi na kutunza nyama na samaki na kadhalika visioze

Kwaajili ya tiba – Chumvi hutumika kukausha, kuandaa kwaajili ya kutunza kitu kisiharibike, kwa kusafishia na kutakasa.

Kwaajili ya uwiano – ukiizidisha hainogi, ukiipunguza hainogi ni mpaka iwekwe kwa kiwango chenye kuwiana

Umuhimu wa chumvi katika maisha ya Ukristo.

Mathayo 5:13aNinyi ni chumvi ya ulimwengu” hii ina maana gani, Biblia inatufundisha sisi tuliomuamini Kristo kwamba tunapaswa kuwa chumvi ya ulimwengu, tupo hapa duniani kwa wakati kuhakikisha kuwa tunautunza ulimwengu uliooza kwa dhambi  na kuuponya kutoka katika chuki dhidi ya Mungu na mambo ya Mungu.

Sifa halisi za Chumvi na maana zake za kiroho.

Huwezi kuila Chumvi peke yake!

Jaribu kuchukua kijiko kimoja cha chumvi kisha dumbukiza mdomoni kwako, hutaweza kuimeza, Chumvi haiko kwaajili ya kuliwa yenyewe ni lazima uiweke katika kitu kingine ili uweze kuitumia pamoja na kitu hicho, Ni lazima uitumie chumvi kwa kiwango sahihi yaani kinachotosha kulingana na kitu unachokula na hapo ndipo unapoweza kukifurahia, ukiweka kidogo hutaweza kufurahia na ukizidisha utapoteza ladha lazima itumiwe vizuri kwa uwiano sahihi. Biblia inasema katika

Wakolosai 4:6Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.

Maneno yetu kukolea munyu yaani chumvi maana yake kujawa na kiasi, kuzungumza kwa upendo, Kufanya mambo yote tukiongozwa na upendo Maisha ya Ukristo yasipojawa na upendo yanakuwa hayana maana hata kama tumeajaliwa kila kitu 1Wakoritho 13:1Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.”

Kama watu tuliookolewa kwa damu ya Yesu tunapaswa kuwa na ushuhuda, kwa hivyo maneno yetu ni mojawapo ya maneneo ambayo watu wasiookolewa hutafuta kutushambulia, wanasema kuwa tunapowazungumzia kuhusu neno la Mungu, tunawahukumu, Hatupaswi wakati wote tu kuhukumu mambo, kwani wakati tunapoonekana kuihukumu dhambi, ni lazima tuonyeshe kuwa tunawapenda na kwa sababu hiyo tutaweza kufanikiwa kuwaleta kwa Yesu kwa upendo na uvumilivu wala tusijinyeshe kuwa sisi ni wema zaidi kuliko wanadamu wa kawaida au kwa sababu ya wiokovu wetu kuwa labada sisi hatuwezi kukosea, kimsingi duniani tunajifunza sana kwa kukosea kwa hiyo wote tunakosea kama asemavyo Yakobo ndugu yake bwana ona

Yakobo 3:1-2 “Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi. Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.”

Aidha hatuna budi kuvumiliana sisi kwa sisi, kutokana na uwezo wa chumvi kustahimili muda mrefu duniani bila kupoteza ladha chumvi inatufundisha uwezo wa kuvumilia na kuchukuliana

2Timothy 4:2lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.”

Ni muhimu kushughulika na wengine kwa busara biblia inatoa muongozo kwa mfano namna na jinsi ya kushughulika na kiongozi katika kanisa 1Timotheo 5:1-3Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote. Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli” unaweza kuona kuwa kuwa chumvi kunatupasa kuhakikisha kuwa tunawaheshimu wengine, tunakemea kwa uvumilivu, hatuwakemei wazee, tunawaheshimu wajane na kuzungumza na wengine kama dada na kaka zetu

Aidha wanawake pia wanapaswa kuwa makini na namna wanavyozungumza na waume zao 1Petro 3:1-2Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.Hakuna jambo linatia maudhi kama kumsikia mwanamke akizungumza kama baharia. Biblia inapozungumia maneno kukolea munyu au chimvi ina maanisha pia namna bora ya uzungumzaji wa wanawake katika kutii kwao waume zao kimsingi Mungu hapendezwi na kelele na mafarakano katika ndoa ambayo yanaweza yakasababishwa na wanawake, ni matarajio ya kibiblia kuwa wanawake walioolewa watakuwa chumvi katika ndoa zao

Biblia pia inatuonya juu ya matumizi bora ya Meneno kwa maana kuwa sio vema kwetu kuapa, kulaani au kukufuru Yakobo 5:12 “Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, wala kwa mbingu wala kwa nchi; wala kwa kiapo kinginecho chote; bali ndiyo yenu na iwe ndiyo, na siyo yenu iwe siyo, msije mkaangukia hukumu.” Kumbe Mungu anachukizwa sana kumsikia Mkristo akitumia maneno yasiyojaa munyu.

Maneno yetu pia hayapaswi kuleta aibu na kuharibu ushuhuda wa Bwana wetu Yesu  Tito 2:7-8 “katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.” Chumvi ni fundisho kwetu sisi wahubiri wa injili katika kuhakikisha kuwa maisha yanakuwa kielelezo ambapo tutaweza kusababisha watu washindwe kutuhukumu na kupata sababu za kupinga hawa wale ambao wako kinyume na injili.

Chumvi inaweka ladha

Wote tunafahamu kuwa ni vigumu sana kufurahia chakula cha aina yoyote hususani mboga kama chumvi ikikosekana kwa hiyo ili mboga ziwe tamu ni lazima chumvi iwekwe katika uwiano husika ona Ayubu 6:6a “Je! Kitu kisicho na ladha yumkini kulika pasipo chumvi?ni rahisi watu kukubali ujumbe wetu wa injili ya wokovu kama ujumbe huo utatolewa katika roho sahihi, watu wamuelewe mwokozi na mpango na makusudi ya Mungu kabla ya kushawishika kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao! Mahubiri yetu, maneno yetu na matendo yetu na mafundisho yetu yajawe na ladha ya hekima yenye kuwavutia watu kwa kuwaonjesha ile ladha ya wokovu na utamu tulio nao katika Kristo        

Chumvi hutumika kuyeyusha barafu.

Katika nchi ambazo wakati wa baridi kunakuwa na umende ujulikanao kama snow na barafu ambazo wakati mwingine hujikusanya hata kufikia futi sita na kadhalika mara nyingi wamekuwa wakitumia chumvi pia katika kuyeyusha barafu ili iwe rahisi kwa watu kupita na kuendelea na shughuli zao, kwa hivyo tunajifunza pia kuwa chumvi ina ngubu ya kutekebisha hali joto na kuhakikisha kuwa mambo yanakuwa sawa Neno la Mungu lina uwezo wa kuweka sawa mioyo ya watu kuliko kitu kingine chochote

Zaburi 147:16-18 “Ndiye atoaye theluji kama sufu, Huimwaga barafu yake kama majivu, Hutupa mvua ya mawe kama makombo, Mbele ya baridi yake ni nani awezaye kusimama? Hulituma neno lake na kuviyeyusha, Huuvumisha upepo wake, maji yakatiririka.”

Matumizi mazuri ya maneno yetu tunayoyatumia katika kuwajibu watu na kuzungumza nao yanatusaidia katika kuyeyusha mioyo ya watu kwa neno la Mungu ambalo lina nguvu ya kushughulika na watu wa kila aina na wenye mioyo migumu na wanaojihami tunapowahubiri Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.”

Chumvi hutumika kama tiba.

Chumvi pia hutumika kama sehemu ya matibabu, watu wanaitumia chumvi kuiweka kwenye eneo la kidonda kilichotokana na kujikata, Wamisri pia waliitumia chumvi kama tiba na pia kwenye utunzaji wa maiti ili isharibike kazi kubwa ya chumvi katika tiba hufanya kazi ya kukausha majimaji yote na kuleta ukavu, Neno la Mungu linauwezo wa kukausha dhambi katika maisha ya watu, Roho Mtakatifu anaweza kuondoa mambo yasiyofaa katika maisha yetu  na kumfanya mtu kuwa kiumbe kipya

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.”

Endapo kuna eneo katika maisha yako linakupa changamoto na unapambana kubadilika ushindi wako unathibitishwa kupatiana kwa neno la Mungu, kila kitu uvutaji wa sigara, masengenyo, wivu, uchungu, kiburi,  na kadhalika Mungu yuko tayari kutoa msaada  na amini ya kuwa atakusaidia.

Maisha ya Mwanadamu ni chumvi.

Unapojaribu kuonja kila aina ya majimaji yanayotoka kwenye mwili wa mwanadamu yana ladha ya chumvi chumvi, chumvi inatufundisha kuwa Mungu Roho Mtakatifu anapokuwa ndani ya mtu humwezesha mtu huyo kuwa na ladha nzuri katika maeneo yake yote kila ulifanyalo katika maisha linatukuwa na ubora wenye kuleta radha kwaajili ya utukufu wa Mungu Luka 6:45 “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.”

Maneno yako yatakuwa yanampa Mungu utukufu, japo wako wanaoweza kuchukizwa na jambo hili na kwao itakuwa ni kama chumvi inawekwa kwenye majeraha yao lakini neno la Mungu ndio lilivyo

Chumvi inatufundisha kuishi maisha ya kiasi.

Wote tunajua pale chumvi inapozidi na tunajua vilevile chumvi inapopungua, wakristo wameitwa kuishi maisha ya kiasi ili kila kit duniani kiwe kitamu ona

Tito 2:11-12 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;”            

Maisha ya kiasi yana umuhimu mkubwa katika maeneo mengi, hata ya kiafya chumvi ikizidishwa sana inaweza hata kusababisha magonjwa kama shinikizo la juu la damu na kadhalika , kama maisha yetu hayana kiasi ni ngumu pia kwetu kuihubiri injili, Maisha ya kiasi ya na umuhimu mkubwa katika afya ya kimwili na kiroho, chumvi inatukumbusha kuishi maisha ya kiasi.

Agano la Chumvi.

2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?

Agano ni patano linalofanywa baina ya watu wawili, huku kila upande ukiahidi kuwa mwaminifu kwa mwingine, agano ni tofauti na mapatano, ni tofauti na kiapo, ni tofauti na nadhiri, kwa vile agano huwa linamuhushisha Mungu mwenyewe, Hata upande wa kibinadamu unapokuwa sio mwaminifu upande unaobaki wa Mungu unapaswa kuwa mwaminifu katika kulitimiza agano au patano, hata pale Daudi alipokesea pamoja na watoto wake wote ambao walishindwa kukaa katika njia yake  kiasi kwamba ilikuwa Mungu awaangamize lakini kwaajili ya agano lake na Daudi ilimpasa Mungu kuwa mwaminifu katika upande wake ili ahadi ile isianguke,

 1Wafalme 9:3-5 “Bwana akamwambia, Nimeyasikia maombi yako na dua zako, ulizotoa mbele zangu. Nimeitakasa nyumba hii uliyoijenga ili niweke jina langu humo milele; tena macho yangu na moyo wangu utakuwapo hapo siku zote; na wewe, ukienda mbele zangu kama alivyokwenda Daudi, baba yako, kwa ukamilifu wa moyo, na kwa adili, kufanya hayo yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, ndipo nitakapokifanya imara kiti cha ufalme wako juu ya Israeli milele; kama nilivyomwahidia Daudi, baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kukaa katika kiti cha enzi cha Israeli.”             

Unaona Mungu alikuwa amemuahidi Daudi akimwambia ya kuwa “HUTAKOSA MTU WA KUKAA KATIKA KITI CHA ENZI CHA ISRAEL MILELE” Agano hili ndio linaitwa agano la chumvi, namna agano hili lilivyofanyika Nabii Nathan au Gadi mmojawapo aliyetumwa kuleta ujumbe huu ndiye aliyemfanyia Daudi na watoto wake wote agano la chumvi.

 

Jinsi ya kufanya agano la chumvi

Wakati wa kufanya agano la chumvi.

  1. Mizimu, mapepo, shetani na wachawi na waganga au makuhani wa kichawi huwaathiri watu katika maisha yao na kusababisha msongo wa mawazo, kwa kutumia nguvu za giza, kwa kutumia nguvu hizo za giza na za kichawi wanawasababishia watu kupoteza mwelekeom kuwa na bumbuwazi, kuteseka, kuelemewa, kuwa na uzito na kupata changamoto za kifedha na kiuchumi na changamoto nyinginezo nyingi.

 

Uchawi ni silaha ya giza inayotumiwa na wachawi kwa kusudi la kuharibu maisha ya watu wanaofanikiwa na kufanikiwa  katika mazingira mbalimbali, silaha hiyo ya giza ni silaha ya kiroho lakini matokoe yake hutokea katika hali halisi.kuteseka kwa watu waliorogwa au kuchawiwa kunategemeana na nguvu iliyotumika katika kunuiziwa nguvu za mashambulizi

Pepo watatafasiri uchawi na manuizo na kuyawasilisha kwa watu waliolengwa na kuwashambulia na matokeo yanaweza kutokea katika ulimwengu wa miili yao, mambo magumu na matukio ya ajabu huanza kutiokea katika maisha yao na njia pakee ya kuimarisha na kuleta ukombozi ni agano la chumvi

 

Ukombozi kupitia gano la chumvi ni rahisi sana kwa muonekano lakini una nguvu kubwa za ajabu sana, ukombozi huu una nguvu ya kuondoa kabisa maedhara ya nguvu zisizoonekana za kichawi na kuukausha au kuuondoa kabisa na kuondoa hali ya kushindwa kwa sababu zozote zile, kwa kufanya hivyo haimaanishi oia mkuwa tutaacha kabisa kuschughulikia nguvu za giza kwa namna za kawaida, lakini tutaendelea ili kuhakikisha kuwa tunaendelea kukua kiroho.

 

  1. Unafanya gano la Chumvi wakati gani?

 

Tunafanya agano la chumvi wakati tunapohisi kuwa kuna matukio ya vita za kiroho zilizohusisha nguvu za giza, ni kweli kwamba mtu aliyeokoka hawezi kushambuliwa na nguvu za giza kwa sababu imeandikwa hakuna ugaga wala uchawi juu ya Yakobo Hesabu 23:23  Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!

 

Lakini kumbuka tuna mashambulizi kutoka kwa mamadui, tuko vitani, majeshi ya pepo yanatumwa kwetu kwa mauizo na sadaka za iana mbalimbali na kwa maelekezo ya aina mbalimbali kwa hiyi kuna kiwango cha mashambulizi ambayo tunakutana nayo wakati mwingine kwa asilimia 30 au 60 au 90 kwa hiyo wote kwa kiwango Fulani tunashambuliwa na nguvu za giza kulingana na kiwango za kuzaa kwetu matunda kumbuka mfano wa zile mbegu zilizoangukia kwenye udongo mzuri Marko 4:8 “Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.” Kama ukuaji wetu wa kiroho unaweza kuzaa matunda kwa asilimia hizo zilizotajwa ni dhahiri na mashambulizia yanaweza kuwepo kutokana na kiwango kwa hiyo niia nyepesi ya kuondoa kiwango hicho cha mashambulizi ya nguvu za giza ni kwa kutumia ganano la chumvi  na ukifanya mara kwa mara unaziondoa kabisa katika mwili wako  tunaweza kujitibu kwa agano la chumvi mara unapohisi au kusikia changamoto hizi:-

 

-          Uchovu wa kimwili na kiroho

-          Kupoteza hamasa

-          Kupoteza uwezo wa kufikiri

-          Kuelemewa na mawazo

-          Hasira za kupita kawaida

-          Mgandamizo wa mawazo stresses

-          Aina yoyote ya ugonjwa na wakati wowote unapokuwa unahisi kuwa kuna uvamizi na hali isiyo ya kawaida katika mwili wako, uchumi wako, kazi yako, huduma yako na roho yako.

-          Lakini pia udhaifu wowowte wa kimwili, kiroho na kihisia ujue kuna mashambulizi ya mizimu, mapepo, wachawi na kadhalika basi unahitaji tiba ya agano la chumvi.

 

  1. Mambo unayohitaji kwaajili ya kutekeleza agano la chumvi

 

-          Utahitaji ndoo au beiseni

-          Utalijaza maji safi kwa asilimia 50% yaani nusu

-          Utahitaji chumvi yam awe kwa kiwango chochote kana huna ya mawe unaweza kutumia ya mezani lakini ya mezani uwezo wake utapungua kwa asilimia 30% ukilinganisha na ile ya mawe

-          Taulo la kujikaushia

-          Na sehemu ya kukanyajia

-           

  1. Jinsi ya kufanya ibada ya agano la chumvi.

 

1.       Weka maji kwenye ndoo yajae kwa asilimia 50% yaani nusu yake kwa kiwango tu cha kufunika enka za miguu

2.       Weka vijiko vidogo viwili vya chumvi ya mawe

3.       Omba kwa kumaanisha na kwa imani kwamba Mungu akuondolee nguvu zote za giza, pia omba maalumu kwaajili ya kuziharibu kabisa na kuzibomboa nguvu zote za mizimu, pepo, waganga na wachawi na kila manuizo yaliyofanywa kinyume nawe na kukuletea athari, omba maombi ni muhimu sana na yana uwezo mkubwa sana yanapofanyika sambaba na ibada hii ya ukombozi.

4.       Hakikisha umekaa sawa sawa na miguu yako hususani enka ziwe zimezama katika maji, miguu yako isigusane bali iwe mbalimbali kati ya sentimita 2-3 hii inasaidia kuodoa uchawi wote uliorogwa kwa nguvu za giza, kama miguu yako itagusana itakuwa kikwazo kwa ibada hii, 

5.       Hakikisha miguu inakaa kati ya dakika 10-15 na usizidishe zaidi ya dakika 15, ukizidisha nguvu za giza zinazotoka kwa njia ya miguu zinaweza kuingia mwilini mwako

6.       Wakati miguu yako inapokuwa katika maji yenye chumvi anza kuomba au kunuiza kwa jina la Yesu  Mungu au kuimba maombi

7.       Wote wenye pumzi wote waishio duniani wote wampendao  (Wamchao) Mungu na waseme fadhili zake ni za milele

8.       Wote wanaoeneza habari zake watangazao habari njema duniani kote na waseme fadhili zake ni za milele.

 

Kwa ufupi utaimba zaburi 118:1-14         

1. Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

3. Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

4. Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

5. Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.

6. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

7. Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.

8. Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.

 

9. Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.

10. Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

11. Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

12. Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

13. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.

14. Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.

 

Hitimisho:

Baada ya kumaliza maombi haya ya ukombozi kulinga nan a mahitaji yako unaweza kuanza kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake anaokupa na namna anavyokuzunguka

Utayamwaga maji yake chooni na kisha utasafisha ndoo na maji safi. Utakausha miguu yako vema kwa taulo na kisha utajipaka mafuta ya mzeituni na kuomba Mungu akupeleke kwenye kiwango kingine cha maswala mbalimbali uyatakayo. Ibada inaweza kufanyika pia kwa makusudi mbalimbali ambayo mengine hayajaainishwa katika somo hili mfano kuweka wakfu, kiongozi, kujilinda na cheo chako na kadhalika

Mwisho wa ibada hii.

Matokeo:

  1. Athari zote za nguvu za Giza na mashambulizi ya wachwi, waganga na mapepo na shetani zinaondoka
  2. Maji ya agano la chumvi yana nguvu kubwa sana yenyewe tu kunyonya nguvu zote za giza
  3. Nguvu za giza na magonjwa yote yanayoambatana na nguvu hizo yanaondoka na wakati mwingine maji yanaweza kuwa na rangi nyeusi kama ishara ya kuondoka kwa nguvu hizo, au yanaweza kuwa na uvuguvugu au yakawa na harufu mbaya hii ni shara ya vitu vibaya kuondoka mwilini mwako

KUMBUKA. Mafundisho haya ya katika shule za kinabii na kama imani yako inakinzana usitilie maanani wala usifundishe kanisani kwako!

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima