Jumatatu, 25 Februari 2019

Tukalia tulipoikumbuka Sayuni!

Zaburi 137: 1-4 “Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni. Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu. Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni. Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?

 
Utangulizi: 
  
Kila mwanadamu katika maisha yake ana historia ambayo imejaa milima na mabonde katika mapito mbalimbali ya maisha, Ukimuuliza mtu swali akuelezee au akuandikie siku ambayo hatakuja kuisahau katika maisha yake kwamba siku ambayo ilimpa furaha kubwa sana (Golden Age) au siku ambayo aliwahi kuuzunika sana (Ashes Age) utaweza kugundua kwamba wengi wataandika siku zao ambazo hawatazisahahu katika maisha yao kutokana na huzuni na mapito mazito waliyoyapitia.
Wengine wataeleza siku yao wasioweza kuisahahu kama siku ya harusi yake, au siku ya msiba wa mtu wake aliye karibu, au siku timu yake ilipofungwa, au siku timu yake ilipopata ushindi, au siku alipopata kazi, au siku alipofukuzwa kazi, kila mmoja anaweza kuelezea siku yake ya huzuni za wakati wake wa furaha hii ni hali ya kawaida katika maisha ya mwanadamu, na ndio maana waswahili wanasema maisha ya mwanadamu yana milima na mambonde. Halii hii pia inaweza kugusa hata taifa fulani au bara fulani na kadhalika. 

Zaburi hii ya 137:1-9 imegawanyika katika sehemu kuu tatu. 

·         Mstari wa 1-4 inaelezea hali halisi ya huzuni waliyokuwa nayo wayahudi huko utumwani, walilia na walivitundika vinubi vyao juu ya miti kwa sababu wasingeliweza kuimba wimbo wa kumuabudu Mungu ugenini 

·         Mstari 5-6 inaelezea jinsi walivyojipa moyo na kujiapiza juwa haitakuja itokee waisahau Sayuni yaani Yerusalem yaani uwepo wa Mungu, na ni afadhali kusahahu mkono wa kulia au kuwa bubu kuliko kuisahai Sayuni 

·         Mstari 7-9 jamaa anaomba kwamba Mungu ashughulike na Babeli pamoja na Edomu ambao walishangilia kuangamia kwa Wayahudi na kuboibmolewa kwa Yerusalem    

Katika kifungu za Zaburi hii leo tunaweza kupata picha ya wana wa Israel waliorejea kutoka utumwani, ambao walishuhudia uzuri wa Taifa lao lilipokuwa chini ya uongozi wa Mungu na baadaye lilipoadhibiwa na kuruhusiwa kwenda utumwani 

Zaburi 137:1-4Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni. Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu. Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni. Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?

Mwandishi wa zaburi hii japokuwa wengine wanadhani ni Yeremia lakini mimi bila shaka naamini atakuwa Ezra au mojawapo ya watu waliorejea kutoka uhamishoni  kwa sababu anajaribu kuelezea hali halisi waliyoipitia walipokuwa nje ya Israel yaani utumwani huko Babeli, na historia haionyeshi kuwa yeremia alikwenda uhamishoni Babeli kama ilivyo kwa Ezekiel na Daniel, kwani inasemekana huenda yeye Yeremia alikwenda Misri.  Ingawa nchi ya Babeli yaani Iraq na Iran ya leo zilikuwa na mito mkubwa na mizuri na yenye matawi mengi sana yaliyochangia taifa hilo kuwa na uwezo mkubwa wa kujitosheleza kwa chakula na umwagiliaji na ujenzi ulioruhusu maji kupita katikati ya majiji yao mito kama Mto Kebari, Mto Frati na mto Tigris na ustaarabu mkubwa na wa hali ya juu, Babeli ulikuwa mji wa kifahari sana ndio ulikuwa mji wenye bustani zinazoelea angani na kuingizwa katika moja ya maajabu saba ya kale ya dunia (The Seven wonders of the ancient world ) ukiacha pyramid la Chiops lililoko Gezer nchini Misri hata leo, Bustani na uzuri wa jiji la Babeli lilikuwa linashika nafsi ya pili kwa ajabu zake duniani, Mfalme Nebuchadnezar aliwahi kujisifia kuhusu ujenzi wa mji huu na akaadhibiwa na Mungu kwa kiburi chake akidhani kuwa alifanya kwa nguvu zake na utukufu wake  

Daniel 4:29-33 “Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu? Hata neno lile lilipokuwa katika kinywa cha mfalme, sauti ilikuja kutoka mbinguni, ikisema, Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako. Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni; utalishwa majani kama ng'ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote. Saa iyo hiyo jambo hilo likatimizwa, likampata Nebukadreza; alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ng'ombe, na mwili wake ulilowa maji kwa umande wa mbinguni, hata nywele zake zikakua, zikawa kama manyoya ya tai, na kucha zake kama kucha za ndege.” 

Unaweza kuona Babeli kulikuwa ni kuzuri sana kuliko hata Sayuni, lakini wana wa Israel walilia walipoikumbuka Sayuni kwanini? Unaweza kuwa na ndoa ya kifahari sana lakini huo sio uthibitisho wa furaha ya kweli, unaweza kuwa na kila kitu lakini kama Mungu hamo haiwezi hiyo kitu kukupa furaha ya kweli unaweza kuwa katika nchi iliyoendela sana lakini hili sio suluhisho la furaha ya kweli ya mwanadamu, unaweza kuwa na mume mzuri na mke mzuri lakini bila uwepo wa Mungu ni sawa na shamba la miwa karibu na shule ya msingi, wako watu wengi wanalia japokuwa wanaishi katika mageti, na nyumba nzuri, na magari mazuri si dhambi kuwa navyo lakini the best ni kuwa na uwepo wa Mungu, Mungu ndiye furaha yetu ya kweli, Elimu na ujuzi na maendeleo hayatupi guarantee ya uhakika wa furaha yetu.

Kwa nini walilia walipoikumbuka sayuni?

Wayahudi waliketi na kutafakari, kwamba wao ingawa walikuwa katika nchi nzuri sana yenye mito mingi, Machozi yaliwatoka kwa sababu sasa walikuwa wametengwa mbali na uwepo wa Mungu, walipotafakari juu ya Nyumba ya Mungu iliyokuwako Sayuni yaani Yerusalem, walipokumbuka makaburi ya baba zao, walipokumbuka sikukuu zao namna na jinsi walivyokuwa wakipanda kwenda kumuabudu Mungu wa baba zai Ibrahim na Isaka na Yakobo, Jinsi walivyokuwa na fahari kuu wakati wa utawala wa Daudi na Solomon, walikumbuka walivyokuwa wakikwea kwenda kuabudu na makuhani wakiwaongoza, walivyokuwa wakitoa sadaka za kuteketeza na kumuabudu Mungu wa kweli kwa furaha na uhuru wao waliokuwa nao, jinsi walivyotumia vinubi na vinanda kumsifu na kumuheshimu Mungu huu ulikuwa ni wakati ambao ni kama golden age kwao, ulikuwa ni wakati wa furaha

Sasa Israel wako utumwani hawana uhuru wao wenyewe, hawawezi kuabudu kama walivyozoea, wanapangiwa kila kitu, waliowachukua mateka wanawasanifu wanasema wawaimbie kama walivyokuwa wakiimba huko sayuni, wakati wao wakiwa na huzuni waliowateka kama mateka wanataka waimbiwe wanataka wafurahie, wao kwao ilikuwa ni swala gumu, uzuri wa Babeli haukuwa na maana kwao, walikumbuka misiba mikubwa, walikumbuka walivyoamuriwa wawaue ndugu zao kwa upanga, wamepoteza mali zao, hawana mashamba yao, hawana nyumba zao,  hawana serikali yao, hawana wafalme wao matumaini waliyokuwa nayo yametokweka, walikumbuka mateso waliyoyapata, walikumbuka walivyochomwa moto, walikumbuka manabii waliokuwa nao, walikumbuka jinsi Mungu alivyowadekeza na kuwapa kila walichokihitaji, sasa ni kama mbingu zimefungwa, ni kama wameondolewa kwenye uwepo wa Bwana, hakuna tena hekalu kubwa kama lile la Sulemani,Unawezaje kuimba wimbo wa Bwana katika nchi ya Ugenini

Waliikumbuka Sayuni waliikumbuka Yerusalem, waliweka nadhiri na kujiapisha kuwa hawatakuja waisahau Yerusalem na kama ikitokea ni sawa na kusahahu mkono wa kulia au mdomo ugande kwa kushikana na ulimi kuliko kuisahau Israel, lakini pia walikumbuka jinsi wakati wanaondoka watu wa Edomu walikuwa wakishangilia kuharibiwa kwa mji huo Bomoeni bomoeni bomoeni walisema na pia waliomba kisasi dhidi ya Babeli kwamba isiachewe salama 

Zaburi 137:5-9 “Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau. Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu. Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini! Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi. Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.” 

Hivi ndivyo inavyotokea katika maisha yetu na maisha ya kanisa la Mungu, hakuna jambo ba ya sana kama kutengwa mbali na uwepo wa Mungu, hatuwezi kufurahia fahari za dunia na dhambi, hatuwezi kuabudu kwa uhuru ikiwa tumechukuliwa mateka, aidha inatia uchungu sana wakati unapopitia mambo magumu kisha wakawepo kando watu wa kufurahia unayoyapitia au kuunga mkono kile unachokipitia, Maandiko yanaonyesha kuwa mwandishi aliomba Mungu akutane na watesi na mashabiki wao pia awalipize kisasi, hatuwezi kuwa na furaha kamili kama maadui zetu wanaisshi na wanashangilia kuangamia kwetu, ni lazima Mungu afanye kitu ili yamkini hata kama wanaishi waweze kuona na kujua kuwa Mungu hawatupilii mbali watu wake, ni lazima wasikie na wajue, Mungu awapatilize,  Natangaza habari njema kwako ya kuwa uko wakati wako wa golden age unakuja ikiwa utakubali Yesu Kristo akutawale, jitegemeze kwake yeye atakutetea anatayafuta machozi yako yote nawe utapata raha nafsini mwako, jitie katika utawala wake nawe utaonja ya kuwa Yesu hatakuacha yeye ni mwema katika maisha yako, hatakusahau kamwe. Kumbuka kurudi katika uwepo wa Mungu, usikubali kutengwa mbali na uwepo wake, uwepo wa Mungu ndio furaha ya kweli, ndio ushindi wa maisha yetu, kila kitu kitakuwa na maana kwetu iwapo tutajikinga katika uwepo wake Zaburi 27:1-4, wale wote wanaotazamia kuwangamia kwetu lazima wajue na wasikie kuwa Mungu wetu yu hai nay a kuwa anafanya kazi kubwa ya kutukomboa pale tunapojitegemeza kwake.

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!.

Jumanne, 5 Februari 2019

“Ukialikwa na mtu Harusini ! ”

Mstari wa Msingi: Luka 14:7-11
 
Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema, Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe, akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya (AIBU) kushika mahali pa nyuma. Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.  Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”



Utangulizi:

Maandiko matakatifu yanatufundisha namna bora ya kuishi katika ulimwengu huu, na kupata mafanikio, moja ya njia iliyo bora zaidi ya kuishi maisha ya furaha na amani ni pamoja na kuishi maisha ya unyenyekevu, pamoja na kuwaheshimu watu wengine au watu wote, Maandiko yanasema katika.

 Wafilipi 2:3Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

Yesu Kristo katika kufundisha kwake alipenda sana kutumia mifano ya aina mbalimbali kwaajili ya kufundisha watu kuhusu ufalme wa Mungu, na ili watu waweze kuelewa alitumia story pamoja na matukio mbalimbali halisi yaliyotokea kuwafundisha watu maisha na ufahamu kuhusu utendaji wa Mungu na tabia zake ili waweze kuishi kwa amani, Ingawa Yesu alitumia mifano lakini mifano hii ilibeba maana kubwa sana na za kweli kuhusu maisha.

Katika kifungu cha Maandiko tunayosoma leo, Katika Luka 14, Yesu alikuwa amealikwa katika chakula cha jioni na moja ya maafisa wakubwa sana wa Mafarisayo, Watu wengine wengi sana walikuwepo au walialikwa pia, kulikuwa na watu muhimu wengi sana wastahiki na pia watu wengine wengi waliokuwa na nyadhifa mbalimbali  na wale ambao bila shaka walijifikiri kuwa ni wa muhimu sana, walipokuwa wakiingia Yesu alikuwa akifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea, wengi walikwenda kukaa moja kwa moja kwenye viti maalumu vya Meza kuu, hatujui nini kilitokea lakini Yesu alipata somo la kuwafundisha wanafunzi wake,  kwa kile kilichotokea kwani tunaweza kukiona japokuwa mwandishi hakukigusia wazi inawezekana wengi walikwenda kukaa mahali ambapo huenda hapakuwa pameandaliwa kwa ajili yao  na hivyo haikuwa sahihi kwao kukaa, na inawezekana baadaye walihamisha na kupelekwa katika viti vya kawaida na hawakujisikia vizuri, (Zamani hakukuwa na utaratibu wa kuweka majina mezani, Lakini aliyepanga viti na meza yaani mwenyeji ndiye aliyekuwa na jibu moyoni kuwa nani anastahili kukaa wapi). Yesu anatumia tukio hili kutufundisha jinsi njia ya unyenyekevu ilivyo ya muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku na zaidi sana katika ufalme wa Mungu.

Kuna nukuu nyingi sana duniani zinazotufundisha kuhusu umuhimu wa unyenyekevu na hapa nimechagua chache:-

Mtakatifu Augustino alisema “it was Pride that Changed the Angels to be devils and its humility that makes man as Angels” yaani “Ni kiburi kilichowafanya malaika kuwa pepo na ni unyenyekevu unaowafanya wanadamu kuwa kama malaika

Thomas Merton alisema “Pride makes us artificial and humility makes us really” kwamba “kiburi hutufanya kuwa fake na unyenyekevu hutufanya kuwa halisi

Rev. Innocent Kamote “Many ways may let people down, but have never ever seen humility letting someone down njia nyingi zinaweza kuwaangusha watu chini lakini sijawahi ona unyenyekevu ukiwaangusha mtu chini

Unaweza kuona Yesu anataka tuelewe kanuni za ufalme wa Mungu na kanuni za maisha haya, ni wazi kuwa mgeni hajui kuwa anapaswa kukaa katika kiti gani, ni lazima asubiri kukaribisha mwenyeji ndiye anayejua, Katika ufalme wa Mungu mwenyeji wetu ni Yesu, ni uhusiano wetu na mwenyeji wetu ndio utakaoamua kuwa ni kiti gani tutakalia, wako wengine wanajifikiri kuwa ni bora, kutokana na Dini zao, au madhehebu yao, au elimu zao, au kabila zao, au familia wanayotokea, au mkoa, au kutokana na huduma aliyo nayo, au kwa sababu anatumiwa sana na Mungu kufanya miujiza mikubwa, mtu anaweza akapiga hesabu zake kichwani mwake akajidhani kuwa yeye ni  wa muhimu kuliko wengine, Ni mwenyeji wetu Yesu ndiye ana mamlaka ya kuhamisha watu viti, anaweza kukuambia ndugu kakae mbele au anaweza kukuambia ndugu kakaye nyuma!

Mwanafunzi anapokwenda shuleni, anakuwa amekuja kujifunza, amekuja kukaa chjini ya walimu amekuja kufuata maelekezo, amekuja kufuata program zote za shule,  na hivyo wanafunzi wa aina hii hukubali kukaa chini ya walimu kwa unyenyekevu na kukubali kufundishika, wanakaa chini wanajifunza na kutafuta majibu ya maswala husika huku wakitii kila wanachoagizwa, Mwanafunzi yeyote ambaye anajidhani kuwa yuko smatter kuliko mwalimu wake, huwa na kiburi hawawezi kukubali kufuata maelekezo ya walimu wao wala program za shule na hatimaye matokeo yataeleza baadaye who is more smatter?

Yesu Kristo alikuwa ni mwana wa Mungu, lakini aliishi maisha ya unyenyekevu, alikuwa mtii alikubali kuelekezwa na alihukumiwa na alikubali kutii mpango wa Mungu na kumtii hata katika mauti ya msalaba ambayo ni mauti ya aibu sana kutokana na uwezo wake mkubwa wa unyenyekevu Mungu amemuadhimisha mno.


Wafilipi 2:4-11 “Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba

Ili Mungu atuinue na kutuheshimu katika kanuni za ufalme wa Mungu njia ya kuwa wa muhimu sana ni kujishusha sana, njia ya kupanda juu sana ni kuwa mnyenyekevu sana ukikumbuka kuwa kuwa mnyenyekevu hakumaanishi kuwa wewe ni mjinga bali ni hekima ya Mungu ya hali ya juu ni njia ambayo Yesu aliichagua katika maisha na akatuachia kielelezo tuifuate kwani ina mafanikio makubwa sana.

Zaburi 138: 6 “Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

Mithali 18:12 “Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.”

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.

Aidha Yesu alikuwa anataka tujifunze kuwaheshimu wengine na kutambua uweza wa wengine, mwaka 18th April 1980 ilikuwa nisiku ya Zimbabwe kupata uhuru wake kutoka kwa Muingereza, katika siku hiyo walialikwa wageni maarufu kabisa duniani akiwemo Rais maarufu wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mambo mengine, Zimbabwe ilimualika Mwanamziki maarufu wa muziki wa Regge duniani 

Robert Nesta "Bob" Marley (6 Februari 1945 - 11 Mei 1981) yaye alikuwa mwimbaji na mwanamuziki muhimu kutoka nchini Jamaika. Alivuma hasa kunako miaka ya 1970 na 1980.  Ambaye ameweza kuifanya staili ya muziki wa reggae kuwa maarufu sana duniani. Muziki wake mwingi ulikuwa unazungumzia dini ya Rastafari ambayo yeye alikuwa anaifuata. Kuna baadhi ya nyimbo zake zinahusu masuala ya dini na zingine siasa.

Katika wakati wa kusalimiana Mwalimu Julius Nyerere alipopeana mkono na mwanamuzik Bob Marley hakuwa amependezwa naye kwani alionekana kuwa mtu rafu asiyekata nyele zake na kama mvuta bangi hivi, lakini katika wakati Mwanamuziki huyo alipotumbuiza ndipo mwalimu Nyerere alipokwenda kumkumbatia na kumkubali mwanamziki huyo kutokana na nyimbo zake nzuri zenye kuhamasisha fikra za kiukombozi wimbo mojawapo muhimu ulikuwa ni pamoja na wimbo kuhusu Zimbabwe ambao ulikuwa na maneno yenye hamasa ya hali ya juu, yaliyodhihirisha kuwa Bob alikuwa msanii mahiri mwana mapinduzi aliyeipenda afrika kwa dhati kutoka Moyoni.

Every man gotta right to decide his own destiny
And in this judgment there is no partiality
So arm in arms, with arms
We'll fight this little struggle
'Cause that's the only way
We can overcome our little trouble

No more internal power struggle
We come together to overcome the little trouble
Soon we'll find out who is the real revolutionary
'Cause I don't want my people to be contrary

To divide and rule could only tear us apart
In everyman chest, there beats a heart
So soon we'll find out who is the real revolutionary
And I don't want my people to be tricked by mercenaries

Maneno haya na uwezo mkubwa alioonyesha mwanamuziki huyo ulimfanya Mwalimu Julius Nyerere amualike Bob Marley kuitembelea Tanzania lakini kabla ya kuitembelea Tanzania Bob alifariki kwa ugunjwa wa Kansa ambapo May 11 1981 alifariki Dunia, Bob alipowasili Zimbabwe alitumia ndege ya Boeing 777 na vyombo vyake vya music vilikuwa na uzito wa tani 21. 

Kila mwanadamu Dunainai ana kitu cha ziada ndani yake na kwa sababuhiyo tunapaswa kuwaheshimu wenzetu na kutambua kuwa wana umuhimu mkubwa duniani kulinga ana nafasi zao

Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.