Jumapili, 28 Januari 2024

Talitha Kumi !

 


Marko 5:38-42 “Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu.  Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu. Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. Akamshika mkono kijana, akamwambia, TALITHA, KUMI; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu.”



Utangulizi:

Leo tutachukua muda kujifunza kwa kina na mapana na marefu kuhusu Vazi maalumu la kiyahudi liitwalo TALLIT, Vazi hili huvaliwa na wanaume wa kiyahudi na baadhi ya Wakristo walio na ufaamu wa kutosha kuhusiana na vazi hilo, Vazi hilo maalumu mfano wa (mtandio) lilitengenezwa kwa Pamba au Sufu nyeupe, Ni vazi lenye umbo la Mstatili na huvaliwa mapegani na kiasi kidogo sehemu za kifuani kwa kujitanda, kwa kawaida ni vazi Jeupe lenye mistari ya blue nyeusi (Dakr Blue) au Nyeusi inayotoka upande mmoja waa chini na juu kutoka mwanzo mpaka mwisho,  Vazi hili ni moja ya Nyenzo muhimu sana ya kiroho iliyotumiwa tangu zamani na wayahudi na baadhi ya manabii n ahata Yesu mwenyewe, Vazi hili linaaminika kuwa na nguvu za Kiroho na huvaliwa kwaajili ya kufanyia maombi pamoja na kupata ulinzi wa Mungu, Asili ya vazi hili ni kutokana na maagizo ya Mungu katika Torati kitabu cha

Hesabu 15:37-40 “Kisha Bwana akasema na Musa, na kumwambia, Nena na wana wa Israeli, na kuwaagiza ya kwamba wajifanyie vishada katika ncha za nguo zao, katika vizazi vyao, tena ya kwamba watie katika kila kishada cha kila ncha nyuzi za rangi ya samawi; nacho kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote ya Bwana, na kuyafanya; tena kwamba msiende kutanga-tanga kuandama mioyo yenu wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo kwanza; ili mpate kukumbuka na kuyafanya maagizo yangu yote, na kuwa watakatifu kwa Mungu wenu.”

Wayahudi wenye asili ya ASHKENAZ wanaliita vazi hilo TALLIS Ni vazi ambalo linachochea moyo wa utii na maombi na linalotaka uwe na uhusiano wako binafsi na Mungu, kama watu watajifunza na kufahamu umuhimu wa vazi hili na wakalitumia vema wanaweza kuchochea uhusiano wao na Mungu kwa njia ya maombi na utii kwa Mungu hivyo kuzaliwa watu wenye nguvu za kiroho za kupita kawaida. Tutajifunza somo hili THALITHA KUMI Kwa kuzingatia vipengele vinne vifuatavyo:-

·         Ufahamu kuhusu Asili ya TALLIT

·         Mambo  ya kujifunza katika vazi la TALLIT

·         Nguvu ya kiroho kwa matumizi sahihi ya TALLIT

·         Thalitha Kumi ( TALITHA CUMI)

Ufahamu kuhusu Asili ya TALLIT

Tallit ni Vazi au Mtandio maalumu unaotumika wakati wa kuomba ni moja ya alama Muhimu sana ya kiroho na Nyenzo ya kiroho ambayo Wakristo wengi hawafahamu umuhimu wake, watumishi wengi wa Mungu hawajawahi kupewa ufahamu wa kutosha kuhusu vazi hilo, Lakini kujifunza juu ya vazi hilo na umuhimu wake na matumizi sahihi ya vazi hilo na kusha kuyatendea kazi, kunaweza kutuletea uamsho mkubwa sana katika maisha ya maombi kwa waktristo bila ya kutumia nguvu, kuwa na ufahamu kuhusu umuhimu wa vazi hili sidhani kama inawahusu Wayahudi peke yao kwani ni fundisho la kibiblia kuanzia na agano la kale mpaka agano jipya, hivyo kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu Tallit kutatuleta katika kiwango kingine kizuri cha kujenga uhusiano wetu na Mungu na kuleta matokeo yanayokusudiwa katika maisha yetu na ya wengine!

Tallit ni Vazi au mtandio maalumu vazi la ibada linalotumiwa na wayahudi na Baadhi ya Wakristo kwa kusudi la kuiungamanisha na Mungu hususani wakati wa Maombi ya Alfajiri, au siku za sabato kwa wayahudi na siku takatifu, Tallit pia huvaliwa wakati wowote mtu anapokua anahitaji kumuomba Mungu hususani anapokuwa bali na Sinagogi ua hekalu.

Nguo hii mara nyingi hutengenezwa kwa kitani nyeupe na huwa na umbo la mstatili na huvaliwa kama mtandio wa mabegani lakini pia huwekwa kichwani wakati wa maombi, Nguo hiyo Nyeupe huwa na michirizi au mishari ya Rangi ya bluu Nyeusi katika upande wa chini na wa juu inayotoka mwanzo wa nguo mpaka mwisho wa Nguo, Aidha vazi hili maalumu huwa na Nyuzi nyuzi zinazofungwa mbili mbili zinazoning’inia katika pindo la vazi hilo, Nyuzi nyuzi hizo zinazoning’inia mwishoni mwa ncha za vazi hilo huitwa TZITZI kwa kiyahudi

Jina hilo Tallit kwaasili linatokana na neno la KIARAM TALLIT ikiwa na maana ya TO COVER   kujifunika au kujitanda na kwaasili ilitokana na agizo la Mungu katika Toarati kama tulivyoona katika

Hesabu 15:37-40 Kisha Bwana akasema na Musa, na kumwambia, Nena na wana wa Israeli, na kuwaagiza ya kwamba wajifanyie vishada katika ncha za nguo zao, katika vizazi vyao, tena ya kwamba watie katika kila kishada cha kila ncha nyuzi za rangi ya samawi; nacho kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote ya Bwana, na kuyafanya; tena kwamba msiende kutanga-tanga kuandama mioyo yenu wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo kwanza; ili mpate kukumbuka na kuyafanya maagizo yangu yote, na kuwa watakatifu kwa Mungu wenu.”

Vazi hili kwa mujibu wa masimulizi ya kiyahudi linawekwa ahadi za Mungu ndani yake pamoja na amri kumi za Mungu, maandiko hayo huwekwa kwa ufundi sana katika vazi hilo moja na kufikisha ahadi za Mungu 613 Awali katika maelekezo ya Mungu Nyuzi nyuzi zilitakiwa kuwa nne tu yaani katika kila ncha ta TALLIT nyuzi moja Kumbukumbu 22:12 “Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.”  Hata hivyo baadaye marabi walizifanya nyuzi nyuzi hizo kuwa nyingi kwaajili ya kuwakilisha ahadi za Mungu na maagizo yote ya USI na Yale mtu anayopaswa kutenda. Kuusi kubwa la nyuzi nyuzi hizo ni kujikumbusha amri zote na maagizo yote ya Mungu nyuzi nyuzi hizo huitwa TZITZI

Kuvaa vazi hili hakukuwa kwaajili ya mapambo bali kuolikuwa kunaashiria kuwa mtu huyo hana utani na maswala yote kuhusu Mungu, lilikuwa ni vali linalomkumbusha mtu kujitoa kwa Mungu na kwamba anawajibika kuishika sharia yote ya Musa, Mafarisayo waliyavaa sana mavazi hayo lakini hata hivyo wakiwa na nia ya kujionyesha kwa watu kuwa ni wenye haki, walisahau kabisa kuwa Mungu huangalia moyo na haangalii kama wanadamu waangaliavyo na kwa sababu ya tabia yao mbaya Yesu aliwachana na wala hakuwaacha salama

1Samuel 16:7 “Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.”

Mathayo 23:25-28 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang'anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi. Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote. Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi.”

Unaona vazi hilo ni agizo la utii kwa Mungu na hivyo halipaswi kuvaliwa kinafiki na kwa klusudi la kujionyesha ua kukubalika ni vazi ambalo ukilivaa kama unamuomba Mungu unaomba kwelikweli na kama unazishika mari zake unazitii hasa kwa hiyo halipaswi kuvaliwa ili mradi, bali linapaswa kuvaliwa na watu waliomaanisjha kwelikweli kutka moyoni na wale waliomaanisha wakilivaa uweza na nguvu za Mungu huambatana nao sio hivyo tu watu wakigusa TZI TZI wanapokea uponyaji na nguvu za kiungu kwa mujibu wa mahitaji yao kama tutakavyoona katika somo hili

TALLIT ni mojawapo ya vazi la thamani kubwa sana duniani na huuzwa kwa bei karibu mara nne ya bei ya suti kali nchini Israel vazi hili huuzwa kati ya fedha ya kitanzania laki nne mpaka laki tano hivi, Vazi hili kwa wastani linaweza kuwa na urefu wa inchi 72 katika kona zeke kuu nne kuliandikwa SHEMA, sikie ee Israel Bwana Mungu wako ni Bwana mmoja, mistari yake ilitakiwa kuchorwa kwa wino wa samaki aina ya Ngisi  

Mambo ya kujifunza katika vazi la TALLIT

Bila shaka unaanza kupata picha sasa kwamba vazi hili sio la kawaida kwani kuanzia matengenezo yake mpaka matumizi yake ni maelekezo ya neo la Mungu, hata hivyo ukiacha kuwa vazi hili hutumika kwa maombi ya ahadi za Mungu, bado pia mvaaji anapaswa kujifunza mambo kadhaa ambayo yanapaswa kuonekana katika maisha yake kupitia matumizi ya vazi hili, vazi hili lina mafunzo muhimu makubwa ya kujifunza kama ifuatavyo:-

1.       Utawala wa Mungu katika maisha Yetu

 

Asili ya vazi hili ni maandiko na Mungu aliagiza vzazi hili kwa jamii ya wayahudi na dunia nzima ili watu watambue kuwa Mungu ndiye anayetawala maisha yetu, unapojifunika vazi hili maana yake unatambua ukuu wa Mungu kuwa Mungu yuko juu yako hata pamoja na kila unachikionea fahari Duniani, sawa tu na mtu anavyovaa kibandiko au Barakashia,  na zile nyuzi nyuzi zinatufundisha ya kuwa Mungu nanataka wakati wote tukumbuke sharia zake na kuzitii, kwa hiyo vazi hili lnadai utii kwa Mungu, haitoshi tu kutambua kuwa Mungu yuko juu ya yote kisha ukawa unaenda kama utakavyo

 

1Yohana 2:3-6 “Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake. Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake.Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.”

 

Mtu anayevaa vazi hilo ni lazima awe anamjua Mungu, anatambua ukuu wake na kuwa yeye anawajibika kwake na kuwa yuko juu ya yote kwa hiyo anayevaa Tallit ni lazima aenende kama yeye alivyoendenda!

 

2.       Mungu ni Mtakatifu Sana

Mtu anapojifunika na vazi hilo humaanisha kuwa hastahili kumwangalia Mungu, wala hustahili kumuona yeye kwa macho ya nyama kwa sababu Mungu ni mtakatifu sana hakuna mtu anaweza kumuona Mungu akaishi

Kutoka 33:19-20 “Akasema, Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza jina la BWANA mbele yako; nami nitamfadhili yeye nitakayemfadhili; nitamrehemu yeye nitakayemrehemu. Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.”  

Tallit ni vazi Jeupe na michirizi yake ya blue huwakilsha mbingu ambayo ni makao makuu ya Mungu, na Mungu wetu ni Mtakatifu sana kwa hiyo mtu awaye yote anayeivaa TALLIT au kikofia kama baraghashia anapaswa kuishi maisha matakatifu, kwa sababu kuvaa vazi hilo kuna maanisha kuwa wewe umejitoa muhanga kuishi kama vile apendavyo Mungu

1Petro 1:15-16 “bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.” Kwa msingi huo uvaaji wa Tallit ni tangazo kuwa Mungu ni Mtakatifu na kwamba nasi tunapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wetu wote                

3.       Utii kwa Mungu ni Muhimu sana

 

Nyuzi nyuzi katika vazi lile inakumbusha juu ya sharia za Mungu na kuwa sharia hizo zinadai utii kutoka kwetu ili Mungu aweze kututimizia ahadi zake, kwa hiyo kuvaa vazi hilo halafu ukawa hauna utii kwa Mungu ni kuvaa ufarisayo tu, Makusudi makubwa ya vazi hili ukiacha kuomba na kustawisha uhusiano wetu na Mungu vazi hili linatukumbusha wajibu wa kumtii Mungu, Mungunanapendezwa na utii kwake, wote tunafahamu Mungu alimkataa Sauli kwa sababu ya kukosa utii, maandiko yanaagiza tumtii Mungu

 

1Samuel 15:22-23 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.”

 

Watu waliomuamini Yesu kama bwana na mwokozi wa maisha yao huitwa watoto wa kutii, maana yake Mungu anategemea tutaishi maisha ya utii kwake hivyo mtu anapotamani kuwa na vazi hili maalumu na akafanikiwa kuwa nalo halitakuwa na faida kwako kama hutaishi maisha ya utii

 

1Petro 1:14 “Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;”

Tunapomtii Mungu, katika mkaisha yetu na kutambua jinsi kutii kulivyo Muhimu, itatusaidia katika maisha yetu kuwa na nguvu dhidi ya shetani na kazi zake

 

Yakobo 4:7-10 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu. Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.”

 

4.       Kuwa mbali na kiburi

 

Vazi la Tallit linapovaliwa huvunika kichwa na mabega yetu, wakati huo tunatambua kuwa Mungu ndiye mtawala wa kila kitu, na tunakubali kuwa yuko juu ya yote tukiwemo sisi na kuinyesha kuwa tunamtii yeye, hata hivyo kuvaa vazi hili pia kuna maanisha unyenyekevu kama mtu anataka Baraka za Mungu ni muhimu sana mtu huyo akawa mnyenyekevu, Hakuna dhambi ambay Mungu huihukumu kwa haraka sana kama kiburi, huwezi kusema kuwa umejitoa sana kwa kumaanisha kwa Mungu kisha alama za kiburi zinaonekana kwako, unyenyekevu kwa Mungu kwanza na unyenyekevu kwa wanadamu, pale wakati wote tunapojihesabu kuwa sisis sio kitu kwa Mungu na sio bora ukilinganisha na wanadamu wengine, Vazi hili ni ishara ya kujinyenyekeza kwa Mungu, na hivyo unapokwenda mbele zake na vazi hili maana yake umejinyenyekeza kwake

 

Isaya 66:2 “Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.”    

 

1Petro 5:6-7 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.”

 

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.”

Unaona ni wazi kabisa kuwa kijapo kiburi ndipo ijapo aibu, Mungu huwapinga wenye kiburi bali huwapa neema wanyenyekevu, kwa hiyo vazi hili linawakilisha kuwa tumenyenyekea kwa Mungu, unapohitaji maombi kwake anakusikia kutokana na mwenendo wako wa unyenyekevu

 

5.       Ulinzi wa Mungu

 

Vazi hili vilevile ni ishara ya kuwa unazingirwa na uwepo wa Mungu, kwa kuwa Tallit vilevile inawakilisha Hema ya kukutania ni vazi ambalo unapolileta kichwani humaanisha kuwa umeingia katika patakatifu na uko tayari kusema na Mungu kama vile unavyokuwa umeingia hekaluni, Tallit ni Hekalu binafsi, na TZITZI ni Pazia la hekalu lililopasuka unapojifunika maana yake umeingia katika uwepo wa Mungu na hivyo uwepo huo unakufunika ni ishara ya kuzingirwa na ulinzi wa Mungu pande zote

 

1Petro 1:3-5 “Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu. Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.”

 

6.       Kuishi kwa Neno la Mungu

                               

Tallit ni vazi ambalo linawakilisha neno la Mungu, ahadi za Mungu na amri zake, Vazi hili linawakilisha neno la Mungu linamkumbusha mvaaji kuwa anapaswa kusoma neno la Mungu hii inakusaidia kutokusahau wema wa Mungu, linakukumbusha kutiokuwa mawindo kwa haraka katika mitego ya adui,  kwa hiyo kuvaa vazi hili kunakutaka sio tu kuwa na ujuzi wa neno la Mungu bali kuishi kwa neno  na ndio maana Vazi hili linahesimiwa sana na wayahudi kwa sababu lilikuwa ni vazi linalosaidia kuwaleta watu karibu na Mungu  katika maisha yao ya kila siku.

 

Luka 4:3-12 “Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate. Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu. Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde; na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.  Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.”

 

7.       Kuwa mbali na Unafiki

 

Mtu anayevaa Tallit hapaswi kuishi maisha ya kinafiki, ukivaa Tallit katika jamii ya kiyahudi, watu watakuja kwako na kukusogelea kwa kusudi la kulishika vazi hilo kwa Imani ili Mungu aweze kukutana nao, TALLIT ni nyumba binafsi ya Mungu, ni Nyumba ya sala ni hema yako binafsi ya kukutania, hivyo watu wenye ujuzi kuhusu vazi hilo na hawana uwezo wa kulinunua au viwango vya kutosha kulivaa watakimbilia kwako kwa uponyaji kwani vazi hilo ni Ishara ya Masihi ni Ishara ya kuwa wewe ni mtu wa Mungu, ni Ishara ya kuwa una Mungu wa Israel 

 

Zakaria 8:22-23 “Naam, watu wa kabila nyingi na mataifa hodari watakuja Yerusalemu kumtafuta Bwana wa majeshi, na kuomba fadhili za Bwana. Bwana wa majeshi asema hivi, Siku hizo watu kumi, wa lugha zote za mataifa, WATAUSHIKA UPINDO WA NGUO YAKE YEYE ALIYE MYAHUDI; naam, wataushika wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.”

 

Unaona ukivaa TALLIT kwa watu wanaojua maandiko, watu waliovunjika moyo, watu wenye shida watakluzingira wakihitaji huduma kutoka kwako, Ndio maana kuvaa vazi hilo kwa nia ya kujionyesha huku ukiwa hauna nguvu za Mungu halisi kunakemewa vikali na Yesu Mwenyewe, kwani Mafarisayo waliyatanua mavazi yao na kuziongezea urefu TZITZI

 

Mathayo 23:2-5 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa; basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi. Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;”

 

Angalia Mstari wa 5b kwa makini Mstari huu katika kiingereza unasomeka hivi, …. “They make their Phylacteries wide and the tassels on their garments lon;” neno hilo TASSELS katika kiingereza Ndio TZITZI yaani hirizi au matamvua, ni nyuzi nyuzi zinazoning’inia mwishoni mwa pindo la vazi hilo liitwalo TALLIT Kwa hiyo mafarisayo waliyafanya manyuzi nyuzi ya TALLIT zao kuwa marefuuuu ili iwe rahisi watu kuyashika lakini hayakuwa na majibu ya kutosha kwa watu kukutana na mahitaji yao, Kristo alikuja kuonyesha kuwa kwake hakuna miujiza ya kuigiza au fake kwa hiyo watu waliposhika upindo wa vazi lake walipata msaada, kama utakusudia kuvaa vazi hili achilia mbali maisha na tabia za kuigiza uwe halisi, ulifanyie kazi zinazolingana sio kwaajili ya kuonekana bali kwaajili ya kuwakutanisha watu na Mungu wa Israel, Mtakeni bwana na nguvu zake, Ni lazima ukiwa unaivaa TALLIT basi tuje tushike upindo wa vazi lako na kukutana na Mungu, Ni Tallit ndio vazi la miujiza, Shetani leo amedanganya watu siri iliyoko katika vazi hili na wahubiri wanatumia makoti yao eti kuachilia upako na kuangusha watu, sikatai kuwa koti lako linaweza kuwa na nguvu za Mungu Lakini usisahau Mungu hajaagiza koti aliagiza TALLIT nachelea kuwa kutumia koti inaweza kuwa sawa tu na Walawi walioacha kulibeba sanduku mabegani mwao wakatumia Mkokoteni wa kukokotwa na ng’ombe., jambo lililopelekea Uza kuawa, ni vazi hili ndilo linatakiwa kufanya kazi hiyo na sio suti yako ya polista

 

Kuna mambo mengi ya kujifunza kuhusiana na vazi hilo lakini muda usingeliweza kutosha kuchambua moja baada ya jingine hata hivyo hayo ni ya msingi niliyokuainishi kwaajili ya kumfanya mvaaji kuwa na uwepo wa Mungu katika maisha yake n ahata kuweza kuleta athari kwa wengine, hata hivyo vazi hilo likivaliwa kwa kanuni hizo kuna mambo mengi sana ya kushangaza ambayo yanaweza kufanyika kupitia vazi hilo.

Nguvu ya kiroho kwa matumizi sahihi ya TALLIT

Nguvu za Uponyaji:

Vazi hili liitwalo TALLIT likiwa limevaliwa na mtu sahihi na akazingatia mafundisho sahihi niliyoeleza hapo juu, uwepo wa nguvu za Mungu hutenda kazi kupitia mtu huyo na vazi hilo, Vazi hili linalovaliwa sana na wayahudi, nikukumbushe tu pia lilivaliwa sana na baadhi ya manabii na pia lilivaliwa na Bwana wetu Yesu Kristo, baadhi ya manabii na wafalme na Hata Yesu mwenyewe ambaye aliishika Sheria yote ni wazi kuwa alikuwa na vazi hili na kutokana na maisha yeke ya utii kwa Mungu vazi hili kupitia pindo za vazi yaani TZI TZI kulikuwa na miujiza kadhaa iliyofanyika kupitia vazi hili, moja ya stori ya kusisimua kuhusu nguvu za kiroho pale mtu alipotumia TALLIT Ni pale wakati Mwanamke aliyekuwa na kansa alipoamua kulishika vazi hilo lililokuwa mabegani mwa Yesu! Ona

Marko 5:25-36 “Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,  na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya, aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona. Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule. Mara Yesu, hali akifahamu nafsini mwake kwamba nguvu zimemtoka, akageuka kati ya mkutano, akasema, Ni nani aliyenigusa mavazi yangu? Wanafunzi wake wakamwambia, Je! Wawaona makutano wanavyokusonga-songa, nawe wasema, Ni nani aliyenigusa? Akatazama pande zote ili amwone yule aliyelitenda neno hilo. Na yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka, akijua lililompata, akaja akamwangukia, akamweleza kweli yote. Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, enenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena. Hata alipokuwa katika kunena, wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema, Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu? Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu.”

Katika injili ya Marko hapo tunaona mwanamke huyu akiyashika mavazi ya Yesu kama unavyoweza kuona hata hivyo ni ukweli usiopingika kuwa Mwanamke huyu hakushika mavazi yote ya Yesu yeye alishipa PINDO la vazi la Yesu PINDO hapa ndio TZITZI yaani zile nyuzi nyuzi zilizokuwa zikining’inia  katika hilo vazi, wayahudi waliamini kuzishika hizo ni Kumshika Mungu mwenyewe au neno lake au YESHUA yaani masihi, kwa kuwa mwanamke huyu alikuwa amesikia kuwa Yesu ni Masihi na alisikia kazi nyingi alizozifanya Yesu yeye alikuwa na Imani kuwa akiigusa TALLIT inayotumiwa na mtu huyu maarufu yeye angepona Luka  anaelezea kwa kina kuwa alichoshika mwanamke huyu ni Upindo wa vazi lake yaani alishika TZITZI na kanisa ile iliyomsumbua kwa miaka 12 ilikata mara moja

Luka 8:43-46 “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote, alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma. Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga. Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.”

Mwanamke huyu alipokea uponyaji kwa sababu alifahamu Nguvu ya kiroho ya vazi lile alilokuwa analitumia Yesu, kwa nini kwa sababu Yesu hakuvaa ili mradi tu, alivaa akiwa anaitiis heria ya Mungu, kwa hiyo unaposikia uponyaji kwa kupitia upindo wa vazi haimaanishi upindo wa vazi la suti au dela hapana ni vazi maalumu la matumizi ya ibada kwa wayahudi na wakristo wanaoelewa, kwa msingi huo kama Yesu alivaa vazi hili hakuna sababu kwa wakristo kuacha kulitumia vazi hili kwani linahamasisha mambo yote ya muhimu yanayoweza kuleta uamsho mkubwa na kurejesha uhusiano mkubwa na Mungu.

Nguvu za miujiza na upako maradufu

Vazi la Tallit pia kwa mujibu wa tamaduni za kiyahudi lilikuwa linaweza kurithiwa, hasa kama lilikuwa linatmiwa na mtu mwema, na kulirithi vazi hilo kulimaanisha kurithi upako na miujiza ya mtu huyo, tunafahamu kuwa vazi hili pia lilitumiwa na nabii Eliya ambaye baadaye alipotwaliwa alimuachia vazi hilo Elisha na akalitumia kufanya miujiza mbalimbali angalia maandiko

2Wafalme2:5-10. “Basi wana wa manabii, waliokuwako Yeriko, wakamkaribia Elisha, wakamwambia, Je! Unajua ya kuwa Bwana atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako? Akajibu, Naam, najua, nyamazeni. Eliya akamwambia, Tafadhali kaa hapa; maana Bwana amenituma niende mpaka Yordani. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Wakaendelea mbele wote wawili. Basi watu hamsini wa wale wana wa manabii wakaenda wakasimama, kuwakabili kwa mbali; na hao wawili wakasimama karibu na Yordani. Eliya akalitwaa vazi lake la juu, akalikunja, akayapiga maji, yakagawanyika huku na huku, na hao wawili wakavuka pakavu. Hata ikawa, walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, Omba kwangu lo lote utakalo nikutendee, kabla sijaondolewa kwako. Elisha akasema, Nakuomba, sehemu maradufu ya roho yako na iwe juu yangu. Akasema, Umeomba neno gumu; lakini, ukiniona nitakapoondolewa kwako, utalipata; la hukuniona, hulipati.”

Bila shaka kuna kitu unajifunza kuhusiana na vazi hilo, ukweli ni kuwa Eliya aliponyakuwaliwa na Mungu kwenda mbinguni vazi hili lilimuangukia Elisha na akalitmia tena kwa matumizi kama yale kuuvuka mto Jordani, lakini sio hivyo tu upako zaidi kama ule wa Eliya na mamlaka yake ikawa juu ya Elisha

2Wafalme 2:11-15 “Ikawa, walipokuwa wakiendelea mbele na kuongea, tazama! Kukatokea gari la moto, na farasi wa moto, likawatenga wale wawili; naye Eliya akapanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli. Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili. Kisha akaliokota lile vazi la Eliya lililomwangukia, akarudi, akasimama katika ukingo wa Yordani. Akalitwaa lile vazi la Eliya lililomwangukia, akayapiga maji, akasema, Yuko wapi Bwana, Mungu wa Eliya? Naye alipoyapiga maji, yakagawanyika huku na huku, Elisha akavuka. Na hao wana wa manabii, waliokuwako Yeriko wakimkabili, walipomwona, walisema, Roho ya Eliya inakaa juu ya Elisha. Wakaja kuonana naye, wakainama kifudifudi mbele yake.”

Unaweza kuona mamlaka ya kiungu iliyokuwa juu ya Eliya ilimkalia Elisha kupitia vazi hilo, vazi hili likitumiwa na mtu kwa ufasaha lina uponyaji, lina ufufuo, lina upako na faida nyingi za kiroho.

Nguvu ya kuondoa mamlaka

Kwa mujibu wa masimulizi ya kiyahudi wanasema mtu anapofariki dunia mwili wake au jeneza lake hufunikwa na vazi hili la TALLIT na zile nyuzi nyuzi yaani TZITZI hukatwa kumaanisha kuwa ndio mwisho wake wa kushika sharia yaani amefariki dunia au amekataliwa, kwa hiyo katila lugha ya kinabii ukiishika vazi hili na TZITZI zake zikakatika humaanisha mwisho wa mamlaka yako, Tulio hili lilitokea wakati Nabii Samuel akiwa amevaa Vazi hili na alipokuwa akimkemea Sauli kwa kukosa utii wakati anageuka kuondoka sauli aliushika upindo wa vazi hili na likamchanikia hii ilimaanisha mwisho wake umefika

1Samuel 15:25-28 “Basi sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja nami, nipate kumwabudu Bwana. Samweli akasema, Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la Bwana, Bwana naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa Israeli. Naye Samweli alipogeuka, aende zake, SAULI AKAUSHIKA UPINDO WA VAZI LAKE, nalo likararuka. Basi Samweli akamwambia, Leo Bwana amekurarulia ufalme wa Israeli, naye amempa jirani yako, aliye mwema kuliko wewe.”

Unaweza kuona kumbe vazi lile pia linanguvu ya kinabii, linaishara ya uwepo wa Mungu kuondoka juu ya mtu kama mtu huyo hatakuwa mtii, Sauli alijitabiria vibaya kwa kushika TZITZI nyuzi nyuzi hizi na lile vazi lilararuka kumbe mamlaka yakemimefikia ukingoni

Nguvu ya kupokonywa mamlaka

Kama mtu akikukatia vazi hili huashiria pia amechukua mamlaka yako katika ulimwengu war oho na amekufikisha mwisho, katika mapigano baridi  yaliyokuwepo kati ya Sauli na Daudi ukweli ilikuwa Sauli alikuwa akimtafuta Daudi ili aweze kumuua, na huenda katika kabi ya Daudi kulikuwa na unabii kuwa iko siku Bwana atamtia adui yako mikononi mwako, na siku hiyo ilifika na watumishi wa Daudi walimkumbusha Daudi kuhusu ujumbe huo, hata hivyo katika namna ya kushangaza sana Daudi aliukata tu Upindo wa Vazi la sauli badala ya kumuua, kukatiwa hizo ilikuwa ni Ishara ya kifo katika ulimwengu wa Roho jambo ambalo kwakweli lilimuuma sana Daudi na kumfadhaisha sana Sauli kwani alijua wazi kabisa kinabii anakufa

1Samuel 24:1-12. “Ikawa, Sauli aliporudi baada ya kuwafuatia Wafilisti, aliambiwa ya kwamba, Daudi yuko katika nyika ya Engedi. Ndipo Sauli akatwaa watu elfu waliochaguliwa katika Israeli wote, akaenda kumtafuta Daudi na watu wake juu ya majabali ya mbuzi-mwitu. Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, na huko kulikuwa na pango; Sauli akaingia ndani ili kuifunika miguu. Na Daudi na watu wake walikuwa wakikaa mle pangoni ndani sana. Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia Bwana, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, AKAUKATA UPINDO WA VAZI LAKE SAULI KWA SIRI. Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli. Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA,neon hili,kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake. Daudi naye akainuka baadaye, akatoka pangoni, akamwita Sauli, akisema, Bwana wangu, mfalme. Na Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama uso wake hata nchi, akamsujudia. Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru? Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA Tena, baba yangu, tazama, tafadhali, tazama upindo wa vazi lako mkononi mwangu; maana ikiwa nimeukata upindo wa vazi lako, nisikuue, ujue, na kuona ya kuwa hakuna uovu wala kosa mkononi mwangu, wala sikukukosa neno; ingawa wewe unaniwinda roho yangu ili kuikamata.Bwana atuamue, mimi na wewe, na Bwana anilipizie kisasi changu kwako; lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.”

Nguvu ya kugawanywa kwa ufalme

Tunaona pia vazi hilo hilo likiwa katika mabega ya Ahiya nabii ambaye alilikata kata kumaanisha kugawanyika kwa ufalme katika Israel maana yake ni kuwa vazi hilo linapochana chanwa kinabii huashiria kuraruliwa kwa mamlaka au ufalme

1Wafalme 11:29-35 “Ikawa zamani zile Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya, Mshiloni, alikutana naye njiani; naye Ahiya amevaa vazi jipya, na hao wawili walikuwa peke yao mashambani. Ahiya akalishika lile vazi jipya alilokuwa amelivaa, akalirarua vipande kumi na viwili. Akamwambia Yeroboamu, Twaa wewe vipande kumi, maana Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nitaurarua ufalme, na kuuondoa katika mkono wa Sulemani, nami nitakupa wewe kabila kumi, (lakini yeye atakuwa na kabila moja kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalemu mji ule niliouchagua katika miji yote ya kabila za Israeli);kwa sababu wameniacha mimi wakaabudu Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu wa Wamoabi, na Milkomu, mungu wa wana wa Amoni wala hawakuenda katika njia zangu, kutenda mema machoni pangu, kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, kama Daudi baba yake. Walakini sitauondoa ufalme wote katika mkono wake; lakini nitamfanya awe mkuu siku zote za maisha yake, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi niliyemchagua kwa maana alizishika amri zangu na sheria zangu, lakini nitauondoa ufalme katika mkono wa mwanawe, nami nitakupa wewe kabila kumi.”

Kwa hiyo unakubaliana nami kuwa vazi hili lina nguvu za kiroho na miujiza mbalimbali kama tulivyojifunza katika neno la Mungu, nadhani kama manabii wengi na walimu wa neno la Mungu wataweka mkazo mkubwa kwenye matumizi ya TALLIT na kuwaelekeza watu namna na jinsi ya kutumia unaweza kuondosha kabisa matumizi ya sabuni za upako na nyenzo nyingine za kiroho zisizo za kimaandiko,  badala ya kukanyaga mafuta watu wangekuwa wanatumia TALLIT wangekua kiroho, wangevuta uhusiano wao na Mungu na baraka nyingi zingeweza kuambatana na maisha ya wakkristo na kusababisha ukaribu na Mungu, hakuna nyenzo ya kiroho inaweza kumleta mtu karibu na Mungu kama TALLIT hii hata rozari haiingii yeye aliye na sikio na alisikie neno hili.

Sasa swali kubwa sana ni kwanini kichwa cha somo hili ni neno THALITHA KUMI? je kuna uhusiano wowowte kati ya TALLITH na TALITHA KUMI ?  jibu ni ndio na uko uhusiano mkubwa sana wa matamshi ya Bwana Yesu alipokuwa akimfufua Binti Yairo na fundisho zima la TALLIT hilo linatupa nafasi ya kujifunza kwa kina katika kipengele kinachofuata

Thalitha Kumi (TALITHA CUMI)

Marko 5: 38-42 “Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu.  Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu. Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. Akamshika mkono kijana, akamwambia, TALITHA, KUMI; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu.”

Neno Thalitha Cumi neno TALLIT yote ni maneno ya KIARAMU na ni maneno yenye mzizi mmoja, Kutokana na Matumizi ya TALLIT kwaajili ya Maombi, kama mtu aliomba Mungu ampe mtoto ndani ya TALLIT yake na Mungu akampa mtoto wa kike mtoto huyu angeitwa THALITHA, kwa hiyo katika Lugha ya Kiaramu Binti mdogo wa kike mwenye umri ambao haujafikia kuolewa aliitwa THALITHA, kwa hiyo THALITHA linaweza kuwa ni jina kamili la mtoto wa kike, au Jina la Jumla la mtoto wa kike au Msichana,  kwa Msingi huo linapounganishwa na neno CUM – KOOM , Yaani RISE au AMKA, unapata sentensi MSICHANA AMKA  au Kijana Amka. Hivyo Yesu alipotamka maneno THALITHA CUM aidha alikuwa amesema MSICHANA AMKA au alitaja jina la Msichana moja kwa moja ambaye aliitwa THALITHA.  Kama Jina la msichana huyu aliitwa THALITHA basi ni wazi kwa kuwa Petro alikuwepo miongoni mwa wanafunzi watatu walioshuhudia tukio hili basin aye wakati ameitwa kumsaidia Dorcas ambaye naye aliitwa THABITHA  ambalo nalo lilikuwa jina la KIARAMU lakini sasa ni kwa Mwanamke mtu mzima  THABITHA kwa KIARAM maana yake ni GRACIOUS au Neema  unaweza kuona katika

Matendo 9:36-42 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani. Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu. Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao. Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi. Akampa mkono, akamwinua; hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai.  Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana.”

Unaona Kwa msingi huo THALITHA lilikuwa jina la Kiaramu la Mtoto wa kike linalotokana na imani ya mtu aliyeomba kupitia TATLIT, au kuonyesha furaha kwa kupata Binti mdogo.  Huo ni moja ya uwezekano huo

Kwa msingi huo maneno haya TALLIT na THALITHA yana uhusiano wa Karibu na ni Marko pekee katika injili ndiye aliyeyatumia maneno haya.  Yesu aliyatumia maneno haya wakati anamfufua mtoto wa Yairo na ilikuwa siku ileile na muda uleule ambapo kulikuwa na tukio la kuponywa kwa mwanamke yule aliyekuwa ameugusa upindo wa vazi la Yesu yaani TZITZI, mwanammke huyu aliteseka kwa miaka 12 na binti aliyefufuliwa alikuwa na umri wa miaka 12. siku ile kulikuwa na nini hasa? Kwa nini siku hii miujiza mingi mikubwa ilifanyika kupitia vazi hili la Yesu?  

Kimsingi ni siku ambayo Yesu alikuwa akifanya miujiza kwa kutumia TALLIT na bila shaka kwa maelekezo ya ROHO MTAKATIFU  na kimsingi huyu BINTI ndiye  aliyekuwa mlengwa kwani Yesu alikuwa akielekea kwenda kumuombea na mwanamke mwenye kutokwa Damu aliingilia kati tu na kuhudumiwa, kisha taarifa zilikuja kuwa kijana huyu msichana alikuwa amefariki, lakini Yesu alikwenda na kumuinua.

Kama umefuatilia somo hili vizuri kuhusu TALLIT utagundua kuwa Vazi lile lina nguvu sana na hapa tunaona likihusika katika maombezi ya kumfufua binti aliyewakuwa amekufa tayari, katika muujiza huu watu wengi wamezingatia tafasiri ya Marko kwamba Yesu alisema msichana amka THALITHA KUMI ni kweli, lakini kuna maswala makuu mawili hapa ambayo yamejificha ni hivi:-

Kumbuka kuwa mtu akifa katika Israel mwili wake ufunikwa na TALLIT na TZITZI (Nyuzi nyuzi) hukatwa kumaanisha mwisho wa kuzishika mari za Mungu na Sheria, kwa hiyo katika mazingira ya muujiza huu ni aidha mwili wa msichana ulikuwa umefunikwa kwa TALLIT na Yesu hakuita tu, wala hakushika mkono, Yesu aliifunua TALLIT na kusema maneno TALLITHA CUMI,  TALLIT INUKA na kijana akainuka huu ndio uwezekano mmojawapo wa namna na jinsi muujiza huu ulivyofanyika

Namna nyingine ambayo inawezakuwa ilifanyika hapa ni aidha Yesu aliitumia TALLIT yake mwenyewe ile ambayo iliguswa na mwanamke aliyekuwa anatokwa damu,  na kuifunika ile maiti na kisha kuifunua huku akisema TALITHA CUMI akimaanisha TALLIT INUKA na mara msichana yule akainuka huu ni uwezekano mwingine

Kwa hiyo katika muujiza huu mkubwa sana tunaona tena Nguvu ya TALLIT ikitumiwa sio tu kuponya mtu mwenye Kansa bali pia kiunua mtu aliyekufa hii ni kwa sababu neno TALLIT na TALITHA ni neno moja, Kwa hiyo Yesu alitumia kifaa au nyenzo hii ya kiroho katika kufanya muujiza mikubwa siku ile, Wakristo tunaweza kutumia TALLIT japo Bei ni ghali lakini ni Dhahiri ni vazi linaloweza kusaidia kuleta uamsho mkubwa katika kanisa la Mungu, vazi hili ni la thamani kubwa sana na Yesu alilitumia na siku ile alipokuwa anasulubiwa ilionekana sio vema kulipasua na badala yake walilipigia kura ili liweze kuchukuliwa na askari mmoja kwanini kwa sababu walijua nguvu iliyokuwa ikitenda kazi kwa Yesu na waliiheshimu TALLIT aliyokuwa anaivaa kwa hiyo vazi lililopigiwa kura lilikuwa ni TALLIT

Mathayo 27:35 “Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]

Kwa msingi huo basi katika shule za kinabii, wale wenye kupenda kutumia vifaa vya kiroho, hakuna kifaa cha kiroho cha muhimu na ambacho tunaona Yesu anakitumia kama TALLIT, Hatumuoni Yesu akitumia chumvi wala Mafuta, wala sabuni, wala maji ya upako, Lakini vazi hili Yesu alilitumia kwa maelekezo ya Roho wa Mungu, Vazi hili ni la kinidhamu na ni chuo cha mafunzo, vazi hilo ni la msingi na la muhimu na sidhani kama itakuwa ni vibaya likitumiwa na wakristo kama urithi wa moja ya mambo ya msingi kutoka katika dini ya kiyhaudi, TALLIT ni tofauti na NAIVERA Kanzu maalumu ambayo huvaliwa na makuhani.  Kumbuka hilo.

Hitimisho - Tuombe

Baba Katika jina la Yesu Leo nasema Katika jina la Yesu Inuka ewe uliyekufa, inuka ewe uliyelala, na ninakutangazia  kama biashara yako imekufa Utainuka,  Ndoa yako ina viashiria vya uchungu amka, Yesu alisema mtoto amka naamsha kila kitu kilichokufa katika maisha yako, nakausha kila chemichemi ya uharibifu inayobubujika kwa miaka mingi katika maisha yako Kwa jina la Yesu Kristo Thalitha KUM, inuka katika masomo, inuka katika uchumi, inuka katika huduma, inuka katika hekima, inuka katika haki, katika jina la Yesu Kristo, Bwana uliyenifunulia Somo hili leo wafungue na kuwainua wasomaji wangu  waliojifunza somo hili kwa kina na mapana na marefu na kukuibaliana na mafundisho haya uliyomfunulia mtumwa wako katika jina la Yesu THALITHA kum katika kile eneo la maisha yako, katika ufahamu wako, katika kazi yako, katika uzao wako na sehemu zote za maisha yako nilizozitaja na nisizo zitaja Amen

 

Na Rev. Innocent Mkombozi, Samuel Hamza, bin jumaa, bin Athumani Sekivunga Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumapili, 21 Januari 2024

Unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani ?


Luka 20:1-8 “Ikawa siku moja, alipokuwa akiwafundisha watu hekaluni, na kuihubiri habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wazee walimtokea ghafula; wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii? Akajibu akawaambia, Nami nitawauliza ninyi neno moja; niambieni, Ubatizo wa Yohana, je! Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu? Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema ulitoka mbinguni, atasema, Basi, mbona hamkumwamini? Na tukisema ulitoka kwa wanadamu, watu wote watatupiga kwa mawe, kwa kuwa wamemkubali Yohana kuwa ni nabii.  Wakajibu, kwamba, Hatujui ulikotoka. Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”




Utangulizi:

Yesu alikuwa akiifanya kazi kubwa ya kuhubiri, kufundisha neno na kufanya kazi mbalimbali ikiwemo uponyaji, pamoja na makemeo na makaripio ya aina mbali mbali pale ilipobidi, siku moja akiwa anafundisha, na kuihubiri habari njema, wakuu wa makuhani, waandishi na wazee walimtokea na kuhoji mamlaka yake, kwamba anafanya kazi hii kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyempa mamlaka hii? Kwa ujumla kundi hili la watu walikuwa ni wajumbe wanaowakilisha baraza la utawala na mahakama ya juu ya maamuzi ya kiyahudi linalojulikana kitaalamu kama “SANHEDRIN” swali lao kwa Yesu lilikuja hasa baada ya tukio la Yesu kutengeneza kikoto cha mkambaa na kupindua meza za watu waliokuwa wakifanya biashara Hekaluni, huku akikemea na kuonyesha namna Hekalu linavyopaswa kuheshimiwa na sio swala la kufanyiwa biashara!

Luka 19:45-48 “Akaingia hekaluni, akaanza kuwatoa wale waliokuwa wakifanya biashara, akiwaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. Naye akawa akifundisha kila siku hekaluni. Lakini wakuu wa makuhani, na waandishi, na wakuu wa watu walikuwa wakitafuta njia ya kumwangamiza; wasione la kutenda, kwa kuwa watu wote walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.”

Jamii kubwa ya watu waliokuwa wakihusika na biashara hizi walikuwa ni jamii ya wazee, waandishi na makuhani, hawa ndio waliokuwa washika dau la kisiasa, na ndio mara nyingi sana walikuwa wakikutana na makemeo ya Yesu kwa uwazi na ndilo kundi la watu waliokuwa wakimtafuta ili waweze kumwangamiza, kimsingi hawakuwa wasikivu kwa injili wala mafundisho ya Yesu lakini walikuwa wakimtaka Yesu na kutafuta namna wanavyoweza kumkwamisha ili wamuue au kumshitaki, kwa sababu Yesu alikuwa maarufu kuliko wao na jamii kubwa ya watu walikuwa wakiandamana naye na kumsikiliza! Baraza hili la “SANHEDRIN” kimsingi ndilo lilokuwa na haki au lililojipa haki ya kuidhinisha jambo lolote lile ikiwa ni pamoja na kutoa kibali kwa marabi, majaji na waalimu kufundisha au hata kibali cha kushughulika na watu wanaominiwa kuwa wako kinyume na mafundisho sahihi ya kiyahudi!

Matendo 9:1-2 “Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.”

Ni katika Mtazamo kama huu ndipo walipojivika ujasiri wa kumkabili Yesu na kumuhoji kuwa anayafanya haya kwa mamlaka gani?  Leo nataka tuchukue Muda kujifunza mambo ya msingi muhimu katika somo hili UNATENDA MAMBO HAYA KWA MAMLAKA GANI kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

1.       Ufahamu kuhusu Baraza la wazee wa kiyahudi (Sanhedrin)

2.       Unatenda mambo haya kwa mamlaka Gani?

3.       Ufahamu kuhusu Mamlaka ya Yesu Kristo!

Ufahamu kuhusu Baraza la wazee wa kiyahudi (Sanhedrin)

Baraza la wazee wa kiyahudi liliundwa na kusanyiko la wazee au wataalamu wa sheria wa aina mbalimbali wapatao 71, ambapo Kuhani mkuu ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa baraza hilo, akisaidiwa na wazee sabini, Baraza hili lilikuwa na mamlaka ya kimahakama katika jamii ya kiyahudi, na hivyo ilikuwa ni kama mahakama ya juu zaidi ya kiyahudi, iliyokubaliwa na serikali ya kikoloni ya Warumi kwaajili ya kushughulika na maswala ya Kidini, kiraia, kisiasa, kijamii na kudhibiti uhalifu unaoweza kufanywa na watu wa jamii ya kiyahudi, pia walikuwa na mamlaka ya kutoa kibali kwa marabi waliokubalika na baraza kuwa na wanafunzi na kufundisha, walikuwa pia na kibali cha kuruhusu au kumtangaza mtu kuwa hakimu, yaani mwamuzi, Rabi na Mzee, kwa hiyo katika wakati wa Yesu rabi ndio walikuwa na kofia zote tatu na hivyo waliweza kufanya kazi zote, za kufundisha, kutoa hukumu na maagizo ya kiutawala, hawa walipatikana kwa idhini ya baraza hilo,  kwa hiyo hata walimu wa kidini walipaswa kuwa na kibali cha Baraza hilo la wazee,  kwa hiyo swali lao la hadharani kwa Yesu Kristo lilikuwa lina makusudi ya wazi ya kumdhalilisha Yesu Kristo, wakiwa na maana ya kwamba anayoyafanya anayafanya kwa idhini ya nani na kwa sababu hiyo watu wangesikia na kujua kuwa Yesu ni Mwalimu (Rabbi) ambaye hajaidhinishwa na mahakama hiyo!

Neno hilo SANHEDRIN Ni neno la kiyunani SUNEDRION au SANHEDRIM neno hili limetokana na muunganiko wa maneno mawili SUN na HEDRA ikiwa na maana ya TOGETHER na SEAT yaani Kukusanyika pamoja, Kwa hiyo ni baraza la wazee wenye hekima walioalikwa chini ya kuhani mkuu kumsaidia kufanya kazi za kitawala katika jamii hiyo

Kwaasili kundi hili kwa mujibu wa maandiko ya kiyahudi yaitwayo MISHNA liliundwa kama matokeo ya wazee waliokuwa pamoja na nabii Musa nyakati za agano la kale, ambao Mungu aliwaita kwa kusudi la kumsaidia Musa katika maamuzi mbalimbali na usaidizi wa kulibeba taifa la Israel wazee hao walikuwa muhimu sana angalia:- 

Hesabu 11:16-17 “Kisha Bwana akamwambia Musa, Nikusanyie watu sabini, miongoni mwa wazee wa israeli, ambao wewe wawajua kuwa ndio wazee wa watu hawa, na maakida juu yao; ukawalete hata hema ya kukutania, wasimame huko pamoja nawe. Nami nitashuka niseme nawe huko, nami nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao; nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja nawe, ili usiuchukue wewe peke yako.”

Wazee hao waliwekwa kwa maelekezo ya Mungu kwa nabii Musa kwaajili ya maswala ya kiserikali katika Israel japo kwa Muda na hakuna agizo la kuendeleza mfumo huo lililotolewa na Mungu, Kwa hiyo hakuna historia ya kutosha kuhusu uanzishwaji huu wa SANHEDRIN lakini inajulikana tu kuwa walipata Baraka za warumi kushughulika na maswala  wayahudi isipokuwa idhini ya kuua Muhaini wa kisisasa ilishughulikiwa na mahakama ya Kirumi, tunaliona katika maandiko wakiwa katika utendaji tangu wakati wa Yesu hata wakati wa Nyakati za kanisa la Kwanza.

Mathayo 26:57-59 “Nao waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokuwa wamekutanika waandishi na wazee. Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho. Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;”

Marko 15:1 “Mara kulipokuwa asubuhi wakuu wa makuhani walifanya shauri pamoja na wazee na waandishi na baraza nzima, wakamfunga Yesu, wakamchukua, wakamleta mbele ya Pilato.”

Matendo 5:21 “Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.”

Ni baraza hili ndilo lililohusika kumshitaki Yesu na kutoa ushawishi wa kuuawa kwake na ni baraza hili pia lililohusika kwa kiasi kikubwa katika upinzani dhidi ya Kanisa nyakati za karne ya kwanza, na ni wengi jamii hii iliyokuwa wanamiliki biashara zilizokuwa zikiendeshwa pale Hekaluni na ambazo Bwana Yesu alizikemea na kupindua meza.   

Unatenda mambo haya kwa mamlaka Gani?

Kama nilivyogusia awali kwamba swali hili lilikuwa na makusudi ya kumdhalilisha Yesu Kristo, Baraza la wazee SANHEDRIN ndio waliokuwa na mamlaka ya kuruhusu watu wafundishe neno baada ya wao kuidhinisha jambo hili liliwapa upofu na uziwi na kiburi kwa kujidhani kuwa wao ndio mamlaka ya mwisho na kuwa rabi anayekubalika na wao na aliyepita katika viwango vyao ndiye sahihi na anayepaswa kusikilizwa na watu!

Lilikuwa ni swali la kumuhukumu Yesu Kristo Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii? Swali hili halikuulizwa ili kupata taarifa bali liliulizwa kuwa hii mamlaka ya kufundisha wewe umeitoa wapi kusudi kubwa lilikuwa ni kumvunjia Yesu heshima ili watu wajue kuwa anafanya kazi hiyo bila kibali chao, aidha Kama Yesu angejibu kuwa anafanya hayo Kama Mwana wa Mungu kwa kuwa Yeye ni masihi basi wangepata nafasi ya kumuhukumu kwani angekuwa kama amekufuru na kimsingi Yesu hakutaka hata pepo wamdhihirishe yeye kuwa ni nani! Hakutaka kujifunua kama Masihi

Baraza hili hili pia lilimfanyia hujuma hiyo hiyo hivyo hivyo Yohana Mbatizaji, kwani ni baraza hili ndilo lililotuma wajumbe kwenda kumuuliza swali YOHANA MBATIZAJI kuwa yeye ni Kristo au ni nani? Lakini hawakuhusika katika kumuamini hii ni kwa sababu hakuonekana kupitia pia katika mikono yao na pia walimpuuzia hawakumuamini!

Yohana 1:19-22 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani? Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo. Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La. Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?

Ni watu wa kawaida ndio ambao walimuamini Yohana Mbatizaji na kutambua kuwa ni nabii, na ndio maana Yesu aliwauliza swali kwa swali lao, kuwa Ubatizo wa Yohana mbatizaji ulitoka wapi na waliogopa kujibu kwa sababu hawakuamuamini, na watu walimuamini, kukaa kimya kwao na kutokujibu swali la Yesu kuwa hawajui mamlaka ya Yohana mbatizaji ilitoka wapi, ilikuwa ni kuonyesha ujinga wao kuwa kama hawajui mamlaka ya Yohana mbatizaji imetoka wapi ni wazi kuwa Hawawezi kujua mamlaka ya Yesu Kristo ambayo ni pana zaidi  na ni wazi kuwa baraza hilo hawana mamlaka ya kumzuia au kumpangia nabii cha kufanya. Nabii ni msemaji kwa niaba ya Mungu, ni mdomo wa Mungu, kama mtu hajui mamlaka ya nabii inatokea wapi ni vigumu kujua mamlaka ya Mwana wa Mungu.

Hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kuhoji mamlaka ya Yesu, wala kwa muhubiri wa injili, kundi la makuhani na wazee wa Sanhedrin walikuwa na ujinga katika vichwa vyao na ufahamu wao hawakuwa hata wamefunuliwa maandiko kuijua mamlaka ya Kristo ambayo ilitabiriwa pia katika maandiko Nabii Isaya anaeleza kuhusu mtoto mwanaume mwenye uweza wa kifalme mabegani mwake yaani mwenye nguvu za kiserikali huyu Ndiye Yesu ona

Isaya 9:6-9 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.”

Yakobo alitabiri kuwa huyu ana fimbo ya Enzi yaani mamlaka na utawala na mataifa watamtii Mwanzo 49:10 “Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.”

Kama Sanhedrin wangelijua maandiko yanasema nini kumuhusu Kristo, ukweli ni kuwa wasingelithubutu hata kidogo kuhoji ni kwa mamlaka gani anayatenda hayo anayoyatenda wao walikuwa  wakitafakari ubatili na kumfanyia ghasia wakiwa wamesahau kuwa yeye ndiye mfalme wa wafalme na bwana wa mabwana na kuwa wafalme wote wa dunia wanapaswa kwenda kwa kicho mbele zake

Zaburi 2:1-12 “Mbona mataifa wanafanya ghasia, Na makabila wanatafakari ubatili? Wafalme wa dunia wanajipanga, Na wakuu wanafanya shauri pamoja, Juu ya Bwana, Na juu ya masihi wake.Na tuvipasue vifungo vyao, Na kuzitupia mbali nasi kamba zao. Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka. Ndipo atakaposema nao kwa hasira yake, Na kuwafadhaisha kwa ghadhabu yake. Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, Na miisho ya dunia kuwa milki yako.Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi. Na sasa, enyi wafalme, fanyeni akili, Enyi waamuzi wa dunia, mwadibiwe. Mtumikieni Bwana kwa kicho, Shangilieni kwa kutetemeka. Shikeni yaliyo bora asije akafanya hasira, Nanyi mkapotea njiani,Kwa kuwa hasira yake itawaka upesi,Heri wote wanaomkimbilia.”

Ni Dhahiri kama wangetambua mamlaka iliyoelezewa kuhusu masihi na aliyokuwa nayo Yohana mbatizaji na kama wangemuamini na kumsikiliza ilikuwa ni rahisi kwao kuwa wanyenyekevu na kuwa na hofu na Yesu Kristo kwa sababu hakuwa wa kawaida hata kidogo

Mathayo 3:11-12 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”

Yohana alikuwa amekwisha kueleza wazi kuwa yeye hastahili hata kuwa mtumwa wa Yesu Kristo wala hata kulegeza gidamu ya viatu vyake, mwenyewe alisema ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, na zaidi ya yote ndiye atakayehukumu wanadamu na kuwatupa motoni wale wasiomuamini, Yalikuwa ni maneno ya kutisha sana ambayo Yohana alizungumza kuhusu Yesu, kuhoji kuwa Yesu anafanya hayo kwa mamlaka gani ni upofu na uwendawazimu wa hali ya juu sana, Kama wangemuamini na kumsikiliza Yohana alivyokuwa akizungumza kuhusu Yesu basi walipaswa kujificha  na kukoma kabisa kuhoji jambo lolote alilokuwa akilifanya bwana Yesu wala wasingelithubutu hata kumsogelea. Yohana anasemaje tena kuhusu Yesu? Angalia andiko hili:-

Yohana 3:26-31 “Wakamwendea Yohana, wakamwambia, Rabi, yeye aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani, yeye uliyemshuhudia, tazama, huyo anabatiza na watu wote wanamwendea. Yohana akajibu, akasema, Hawezi mtu kupokea neno lo lote isipokuwa amepewa kutoka mbinguni. Ninyi wenyewe mwanishuhudia ya kwamba nalisema, Mimi siye Kristo, bali nimetumwa mbele yake. Aliye naye bibi arusi ndiye bwana arusi; lakini rafiki yake bwana arusi, yeye anayesimama na kumsikia, aifurahia sana sauti yake bwana arusi. Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi kuzidi, bali mimi kupungua. Yeye ajaye kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote.”

Ni wazi kuwa Yesu ni kama alikuwa anawaambia kwamba mngemuelewa vizuri Yohana mbatizaji, isingekuwa ngumu kumuelewa yeye, lakini tatizo la baraza walimkataa Yohana mbatizaji na ndio maana ilikuwa ngumu kwao kumuelewa Yesu, Yohana anasema AJAYE KUTOKA JUU HUYO YU JUU YA YOTE  Yohana aliwaeleza kuwa yeye sio Kristo lakini ametumwa mbele yake ni wazi kuwa watu wenye akili nyingi wangeweza kumpa kipaumbele nabii aliyefuata baada ya Yohana kwa vile huyo ndiye masihi na ambaye Yohana alikuwa ametumwa mbele yake, huyu ana mamlaka kubwa ana mamlaka nzito sana yuko juu ya yote, na manabii walinena habari zake unawezaje kuhoji mamlaka yake?     Yohana anasema sistahili hata kulegeza gidamu (Kamba) za viatu vyake!                                            

Ufahamu kuhusu Mamlaka ya Yesu Kristo!

Neno mamlaka katika maandiko ni moja ya neno maarufu sana na wakati mwingine linatafasiriwa kama Nguvu na Uweza, Neno Mamlaka, kwa Kiebrania ni Mamlakah na katika kiyunani ni EXOUSIA neno hili limetumika zaidi ya mara 102 katika agano jipya pekee, Mamlaka ni itifaki ya Kiungu,  na linapotumika humaanisha UFALME, NGUVU, UTAWALA,  na AMRI au mamlaka  kwa kiingereza KINGDOM, DOMINION, REIGN AND SOVEREIGNTY or AUTHORITY RIGHT, PRIVILEGE and ABILITY Hii ni Tabia ya uungu, Yesu Kristo Ana mamlaka pana sana na hatuwezi kuizungumzia katika somo moja kama hivi, unapozungumzia habari za Yesu unazungumzia serikali ya kiungu, haitaji kibali cha mwanadamu kufanya jambo, anaweza kumshirikisha mwanadamu au kumjulisha kwa upendo wake lakini huwezi kuingilia mamlaka yake huwezi kuhoji utawala wake, huwezi kuzuia matakwa yake anauwezo wa kufanya lolote! Na zaidi ya yote maandiko yanaonyesha kuwa Yesu amewekwa juu ya hayo yote ona

Wakolosai 1:15-20 “naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae; na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.”   

Unaona ikiwa Yesu na Mamlaka hii inayoelezewa katika maandiko basi hakuna jambo la kipuuzi na la kijinga na kukosa nidhamu duniani kama kupuuzia mamlaka aliyo nayo Kristo, kwa hiyo nadhani baraza hili ambalo lilikuwa linasheheni watu wenye akili na taaluma mbalimbali na uwezo wa kuhukumu mambo inasikitisha kuona kuwa wanakosa akili na hekima ya kutambua mamlaka ya Yesu Kristo na ulikuwa ni mshahara mzuri sana kwa Yesu kutokuwafafanunulia anafanya yale kwa mamlaka gani na badala yake aliwarudisha darasa la kwenda kwanza kujifunza ilikotoka mamlaka ya Yohana mbatizaji

Ni mpaka macho yako yatiwe Nuru tena kwa maombi ndipo uweze kujua mamlaka inayotenda kazi katika Kristo ni mamlaka ya juu sana

Waefeso 1;18-23 “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.”

Hebu niambie kuna mamlaka gani ambayo inaweza kuzidi mamlaka ya Yesu Kristo? Na ndio maana hata tunapotumia jina lake kuamuru lolote linatokea kwa idhini yake yaani kwa mamlaka yake, Jina lake maana yake ni mamlaka yake, licha ya kuwa na mamlaka yote Yesu amejidhihirisha kuwa na mamlaka katika maeneo kadhaa kama yanavyonena maandiko:-

Yesu Kristo ana mamlaka Yote Mbinguni na Duniani hii ni mamlaka kubwa sana ni mamlaka ya kiungu - Mathayo 28:18-20 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.”

Yesu Kristo ana mamlaka juu ya watu wote - Yohana 17:2-3 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.  Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”

Yesu Kristo ana mamlaka ya kusamehe dhambi - Mathayo 9:2-6 “Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.”

Yesu Kristo ana mamlaka juu ya Pepo - Marko 1:23-27 “Na mara palikuwapo ndani ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu; akapaza sauti, akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza? Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu. Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, umtoke. Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka. Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii! ”   

Yesu Kristo ana mamlaka dhidi ya Kifo - Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”    

Yesu Kristo ana mamlaka dhidi ya Magonjwa yote - Mathayo 8:2-3 “Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika.”        

Yesu ana mamlaka juu ya malaika - Mathayo 13:41-43 “Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie.”

Yesu Kristo ana mamlaka dhidi ya sheria ya Musa - Yohana 1:16-17. “Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema. Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.”

Yesu ametupa mamlaka ya kufunga au kufungua lolote – Mathayo 18:18-20 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

Yesu ametupa mamlaka dhidi ya Shetani na wajumbe wake – Luka 10:17-19. “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.”

Unapoitambua mamlaka ya Kristo unapata ujasiri mkubwa, na swali  hilo hilo wakituliiza sisi wakati tunapoifanya kazi ya Yesu aliyotutuma unaweza kujua kuwa ni madhara gani yanaweza kumkuta mtu anayeshindana na mamlaka hii ona Luka 10:16Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.” Unaona katika protokali za kibiblia tunapoifanya kazi ya Mungu alafu mtu akahoji unayatenda mambo haya kwa mamlaka gani mtu huyo anamtafuta pweza aliko na yatakayomkuta atashindwa kusimulia hata wajukuu wake kwa nini? Kwa sababu tunafanya kazi chini ya mamlaka kubwa sana sana sana !

Hitimisho!

Kuna mambo mengi sana ya kuzungumzia kuhusu mamlaka ya Yesu, lakini Muda hauwezi kutosha Mamlaka ya Bwana wetu Yesu Kristo ndio mamalaka ya juu zaidi kuliko zote duniani na mbinguni na haipaswi kuhojiwa na mtu awaye yote, Kimsingi Yesu alikuwa mnyenyekevu mno hata kuweza kuwasikiliza wajumbe wa kundi la makuhani na wazee waliohoji mamlaka yake, Eti unayatenda mambo hayo kwa mamlaka gani?  Watu wote tuliopewa agizo la kuihubiri injili tuna mamlaka kubwa na kibali cha kwenda kila mahali kuihubiri njili na kila kitu kimetiishwa chini yetu hakuna kitakachoweza kusimama mbele yetu siku zote za maisha yetu, kwa unyenyekevu inatupasa kutii sheria za kila nchi na taifa zilizowekwa zisizokingana na Mamlaka ya kiungu, kwaajili ya unyenyekevu, lakini mamlaka inayotenda kazi ni kubwa na iko juu yetu. Ni baraza hili ambalo Petro na Yohana aliwahoji yupi wa kumtii Mungu au wanadamu, wako watu wenye mamlaka za duniani ambao hutumia mamlaka zao vibaya wakitaka kudhibiti watumishi wa Mungu,  lakini hatuna budi kufahamu ya kuwa Mungu ametupa mamlaka iliyokubwa sana kupitia Yesu Kristo ni mamlaka ile ileiliyotenda kazi ndani ya Kristo ndiyo inayotenda kazi ndani yetu! Hatupaswi kuogopa

Matendo 4:17-19 “Lakini neno hili lisije likaenea katika watu, na tuwatishe wasiseme tena na mtu awaye yote kwa jina hili. Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;”

Matendo 5:26-29 “Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe.Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.”

Mathayo 28:18-20 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.”

Kwa msingi huo tunapokwenda kuifanya kazi ya Mungu huku tukiwa tumefuata taratibu zote basi sasa asitokee mtu kututishia na kutaka kuizuia kazi ya Mungu, na wote wanaojihusisha na ushirikina na uchawi na kutaka kushindana na mamlaka ya kiungu tuliyopewa nawaamuru katika jina la Yesu waharibikiwe katika kila mpango wao wa maisha mpaka waokoke katika jina la Yesu, kwa mamlaka niliyopewa kila mahali ambako kuna kizuizi kwaajili ya injili nakiamuru kizuizi hicho kusambaratishwa na kuharibika hata kisiwepo tena katika jina la Yesu Kristo aliye hai, tumia mamlaka hii katika kila jambo lililo kinyume na ustawi wa maisha yako katika mapenzi ya Mungu Kumbuka kuwa ni mamlaka ile ile iliyomtuma Yesu ndiyo tuliyopewa, unaweza kuitumia mamlka hii kukemea lolote lililo kinyume naustawi wako na ustawi wa Ufalme wa Mungu, Yesu ana mamlaka kubwa sana, Hata lile hekalu alisema Imeandikwa NYUMBA YANGU hekalu lile pia lilikuwa ni nyumba yake hata wewe ni mali yake ni aibu kubwa kuhojo mamlaka ya Kristo kwani YU JUU YA YOTE. Asante kwa kufuatilia masomo haya Uongezewe neema !

 

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!