Ijumaa, 30 Desemba 2022

Ikawa mwisho wa Mwaka!


2Nyakati 24:23 - 25Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.” 



Utangulizi:

Yosia alikuwa mfalme wa Yuda aliyetawala kati ya mwaka wa 640-609 Kabla ya Kristo, jijini Yerusalem, Ni mtawala aliyeingia madarakani akiwa kijana mdogo sana, Yeye ni mwana wa Amon Mwana wa Manase ambao kimsingi walikuwa wafalme waovu mno katika wafalme waliowahi kutawala Israel ya Kusini, Lakini hata hivyo Yosia alikuwa mfalme mwema sana na aliyemcha Mungu! Yeye alitawala akiwa na miaka 8 baada ya kuuawa kwa baba yake. Mfalme huyu alikuwa mcha Mungu na alitenda yaliyo haki mbele za Mungu!

2Wafalme 22:1-2 “Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi. Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.”

Wakati wa utawala wake alifanya kazi kubwa sana ikiwa ni pamoja na kuchangisha fedha za ujenzi na ukarabati wa Hekalu nyumba ya Mungu ambayo ilikuwa na nyufa kutokana na kutokujaliwa na watu wakati wa utawala wa babu yake na baba yake, Kuhani Hilikia aligundua vilevile kitabu cha torati ambapo alipomsomea mfalme alirarua mavazi yake na kutubu, kisha kuwaita watu wote wapate kuitubu na kumgeukia Mungu, walifanya agano kuwa watamtumikia Mungu kwa mioyo yao yote kwa ujumla kulikuwa na uamshi mkubwa sana wakati huo

2Wafalme 23:1-25 “Kisha, mfalme akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu. Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana. Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile. Kisha, mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni, akayachukua majivu yake mpaka Betheli. Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. Naye akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni, akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu. Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera. Akawatoa makuhani wote katika miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba, tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa mtu langoni pa mji. Walakini hao makuhani wa mahali pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate isiyo na chachu katikati ya ndugu zao. Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki. Akawaondoa farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani; akayapiga moto magari ya jua. Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni. Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi. Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu. Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli, madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera. Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo. Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria. Na nyumba zote pia za mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli. Akawaua na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu, akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu. Naye mfalme akawaamuru watu wote, akasema, Mfanyieni Bwana, Mungu wenu, pasaka, kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano. Hakika yake haikufanyika pasaka kama hiyo, tangu zamani za waamuzi waliowaamua Israeli, wala katika zamani za wafalme wa Israeli, wala za wafalme wa Yuda. Bali katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia ilifanyika pasaka hii kwa Bwana ndani ya Yerusalemu. Tena wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana. Kabla ya huyo hapakuwa na mfalme mfano wake, aliyemwelekea Bwana kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na sheria zote za Musa; wala baada yake hakuinuka mmoja mfano wake yeye.”

Unaona ni wakati wa Yosia kwa kweli kulikuwa na uamsho mkubwa sana kila kitu cha kipagani kiliharibiwa na kila aina ya miungu iliyoabudiwa iliharibiwa, alifukuza na kuharibu wenye pepo wa utambuzi, makhanithi na wachawi, anasifika kuwa alikuwa mfalme mwema ambaye kbla yaka na baada yake hakuwahi kutokea!

Sababu kubwa ya mafanikio ya Yosia

Uwezo mkubwa na uadilifu mkubwa alioupata Yosia ulitokana na malezi mazuri na thabiti kutoka kwa kuhani mkuu maarufu sana aliyeitwa Yehoiada kuhani huyu alikuwa mwaminifu na aliweza kutumika kwa miobgo kadhaa chini ya wafalme wa Yuda, Kuhani huyu alioa dada wa Mfalme Ahazia, mwaka mmoja kabla mfalme Ahazia hajauawa, Athalia mama wa mfalme alishikwa na tamaa ya madaraka na kuamua kuua watoto wote wa kifalme na kila mtu aliyeonekana na ushawishi wa kiutawala, baada ya adhima yake hiyo kufanikiwa alijitangaza kuwa mtawala ona

2Wafalme 11;1-3 “Na Athalia, mama yake Ahazia, alipoona ya kuwa mwanawe amekufa, akainuka, akawaharibu wazao wote wa kifalme. Ila Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu, umbu lake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia, akamwiba miongoni mwa hao wana wa mfalme waliouawa, yeye na mlezi wake, na kuwatia katika chumba cha kulala; wakamficha usoni pa Athalia, basi kwa hiyo hakuuawa. Alikuwako pamoja naye, amefichwa nyumbani mwa Bwana, miaka sita. Naye Athalia akaitawala nchi.” 

Yehosheba na Mumewe Yehoiada walimficha kijana pekee aliyeponyoka katika sakata hilo ambaye ni Yosia na walimlea vizuri na ilipotimia miaka sita yaani ya kufichwa kwake hii ikiwa na maana alifichwa akiwa na miaka miwili sasa Yehoiada alifanya mpango wa kumtyawaza Yosiah kuwa Mfalme wa Yuda  ona

2Wafalme 11:4-17. “Hata mwaka wa saba Yehoyada akatuma, na kuwaleta wakuu wa mamia, wa Wakari, na wa walinzi, akawaleta kwake ndani ya nyumba ya Bwana; akapatana nao, akawaapisha nyumbani mwa Bwana, akawaonyesha huyo mwana wa mfalme. Akawaamuru, akasema, Hili ndilo neno mtakalolifanya; theluthi yenu, mtakaoingia siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya mfalme; na theluthi mtakuwapo mlangoni pa Suri; na theluthi langoni nyuma ya walinzi; hivyo mtayalinda malinzi ya nyumba, kuzuia watu wasiingie. Na sehemu mbili zenu, yaani, wote watokao siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya Bwana kumzunguka mfalme. Mtamzunguka mfalme pande zote, kila mtu mwenye silaha zake mkononi; naye awaye yote aingiaye ndani ya safu auawe; mkafuatane na mfalme, akitoka na akiingia. Nao wakuu wa mamia wakafanya sawasawa na yote aliyowaamuru Yehoyada kuhani; wakawatwaa kila mtu watu wake, hao watakaoingia sabato, nao watakaotoka sabato, wakaja kwa Yehoyada kuhani. Naye yule kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao zilizokuwa za mfalme Daudi, zilizokuwamo nyumbani mwa Bwana. Walinzi wakasimama, kila mtu na silaha zake mkononi, kutoka pembe ya kuume ya nyumba mpaka pembe ya kushoto ya nyumba, kando ya madhabahu na nyumba, wakimzunguka mfalme pande zote.Ndipo akamleta nje mwana wa mfalme, akamvika taji, na kumpa ushuhuda; wakamfanya mfalme, wakamtia mafuta; wakapiga makofi, wakasema, mfalme na aishi. Na Athalia alipoisikia sauti ya walinzi na ya watu, aliingia kwa watu nyumbani kwa Bwana; akatazama, na tazama, mfalme amesimama karibu na nguzo kama ilivyokuwa desturi, nao wakuu na wapiga baragumu karibu na mfalme; na watu wote wa nchi wakafurahi, wakapiga baragumu. Ndipo Athalia akararua mavazi yake, akalia, Fitina! Fitina! Naye Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, majemadari wa jeshi, akawaambia, Mtoeni kati ya safu; naye ye yote amfuataye mwueni kwa upanga. Kwani kuhani akasema, Asiuawe nyumbani mwa Bwana. Basi wakampisha njia; akaenda kwa njia ya kuingia kwa farasi nyumbani mwa mfalme; akauawa huko. Kisha, Yehoyada akafanya mapatano kati ya Bwana na mfalme na watu, ili wawe watu wa Bwana; tena kati ya mfalme na watu.” 

Unaona chini ya uangalizi wa Yehoiada, Mfalme Yosia aliweza kutawala vema na kwa mapenzi ya Mungu, kumbuka kuwa ni yeye na mkewe ndio waliomsaidia na kumuongoza na kuuondoa utawala wa malikia na kumrudisha mfalme katika kiti cha Enzi cha baba zake kama ilivyokuwa kwa mapenzi ya Mungu kwa Daudi, kupitia kuhani mkuu huyu inchi ikawa na amani na watu wakamcha Mungu mno, Yosiah katika wakati wote wa kuhani mkuu aliweza kufanya vizuri, Mfalme alikuwa na ushawishi mkubwa, aliwaongoza watu kumrudia Bwana kila mtu aliitii sharia ya Mungu, jambo hili lilimfurahisha Mungu sana na klilikuwa Baraka kubwa sana kwa kila mtu, maandiko yalikuwa yamepuuzwa kabisa lakini alipokuwa mfalme Heshima ya kimaandiko ilirejea, watu wote wenye kutoa dhabihu mbaya za watoto na kila aina ya uovu iliharibiwa kabisa kwa ujumla alikuwa mfalme ambaye aliushawishi moyo wa Mungu na Mungu alimsikiliza ona

2Wafalme 22:19 “kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana.”

Ikawa mwisho wa Mwaka!

Pamoja na uzuri aliokuwa nao Mfalme huyu ambaye aliifanya kazi nzuri wakati wote wa uongozi wa kuhani mkuu Yehoiada ambaye aliishi miaka 130 kuhani huyu mkuu aliheshimika na watu wote kutokana na ushauri wake mzuri kwa Mfalme na watu wake alikuwa amejaa hekima ya kiungu hata hivyo jambo la kusikitisha ni kuwa baada ya kifo chake Yosia alibadilika moyo na kuanza kuwa na washauri wabaya ambao walirudisha tena ibada ya baali na maashera ona

2Nyakati 24:17-20 “Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao. Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao. Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza.”

Mungu alipeleka manabii mbalimbali kwaajili ya kuwaonya hata hivyo hawakukubali, wala hawakuwasikiliza, Hata hivyo Kuhani mkuu Marehemu Yehoiada alikuwa na kijana aliyeitwa Zekaria ambaye Roho Mtakatifu alikuja juu yake ili aweze kuwaonya, Nabii Zekaria bin Yehoiada aliwaonya kuwa kama wanamuacha Bwana ni dhahiri kuwa Bwana naye atawaacha hata hivyo hawakutaka kusikia maonyo na badala yake walipanga mpango wa kumuua ona Na mfalme Yoashi alimuua zekaria akasahau wema wote ambao mama yake na baba yake walimfanyia hili lilikuwa jambo la kusikitisha sana ona

2Nyakati 24:20-22 “Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi. Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana. Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi.”

Wakati Zeakaria anauawa alikumbuka wazi mema yote ambayo baba yake alimfanyia mfalme Yosia ni ukweli usiopingika kuwa Yosia alikuwa mtu asiye na shukurani hakulipa mema na badala yake alilipa mabaya Zekaria alimuomba Bwana wakati anauawa akasema  BWANA AYAANGALIE HAYA AKAYATAKIE KISASI, ni ukweli usiopingika kuwa Mungu wetu hujilipia kisasi wakati watu wanapokutendea yasiyopaswa wewe uwe na uvumilivu tu kwa dhambi hii aliyoifanya Yosia ukweli haikuchukua muda tangu wakati ule iluipofika mwisho wa Mwaka Bwana akajilipizia kisasi ndio maana tunasoma IKAWA MWISHO WA MWAKA ona

2Nyakati 24:23-25. “Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.”  

Hitimisho

Inawezekana wako watu umewawaidia lakini wamekugeuka, inawezekana umedhulumiwa, na watu hawataki kukulipa inawezekana umetukana, inawezekana umeonewa, leo nataka nikupe habari njema ya kuwa yuko Mungu anayelipa kisasi, kama maandiko yasemavyo ni haki mbele za Mungu kuwaluipa kisasi wale wanaowaonea ninyi

2Wathesalonike 1:6 – 9 “Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake;”

Mungu anao wakati wake wa kujilipizia kisasi dhidi ya wale wote wanaokuonea na kukutesa, kila unapopitia uonevu unayo haki ya kumwambia Mungu liangalie na hili ukalitakie kisasi na Mungu mwenyewe atausbiri wakati wake na wakati mwingine itakuwa mwisho wa Mwaka, ikawa nmwisho wa Mwaka, ikawa mwisho wa Mwaka, ikawa mwishio wa Mwaka Mungu alijilipizia kisasi dhidi ya Yosia aliyemuua Zekaria ili hali baba yake alimtendea mema hakuna sababu ya kuogopa kila aina ya uonevu katika maisha yako italipwa mwisho wa mwaka, umeonewa wewe kumbuka ikawa mwisho wa mwaka, umekopwa hujalipwa wewe kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka, umekataliwa, mumeo au mkeo ameibiwa, ikawa mwiho wa Mwaka, umedhulumiwa paka kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka  IKAWA MWISHO WA MWAKA   

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima!

Jumapili, 25 Desemba 2022

Kuokolewa katika mikono ya Herode!

 


Mathayo 2:12-16 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize. Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu. Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.”



Utangulizi.

Moja ya  wafalme aliyekuwa katili sana na mroho, mwenye tamaa na mbinafsi na muongo alikuwa ni mfalme Herode mkuu, kwa ujumla alikuwa ni mfalme mwenye kutisha sana, ni katili na muuaji aidha ni mwenye dhuluma, Huyu alikuwa tofauti sana na mfalme wetu Yesu Kristo, ambaye alikuja kwaajili ya ukombozi wa wanadamu, wakati Herode alikuwa na mpango wa kuangamiza na kuua, Mfalme Yesu alikuja na mpango wa wokovu, Herode alikuwa na mpango wa mateso, Yesu alikuja akileta matumaini na upendo, Herode alikuwa ni mkatili mwenye chuki na mwenye mpango wa kuangamiza, Kristo alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea tena alikuja ili watu wawe na uzima tena wawe nao tele, Katika wakati huu wa kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo hatuna budi vilevile katika wakati huu kujikumbusha Mambo ya msingi na ya muhimu yanayoyakabili maisha yetu na kisha kupata hekima ya kiungu namna ya kuokolewa katika mikon ya adui zetu.

Yesu alizaliwa wakati ambapo mfalme muovu na adui wa maisha yake alikuwa anatawala na mfalme huyu aliposikia habari kuwa Yesu Kristo amezaliwa ni ukweli ulio wazi kuwa badala ya kufurahi alifadhaika sana ona

Mathayo 2:1-3 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.”

Mfalme Herode aliita baraza la wazee wa kiyahudi na wakuu wa makuhani na kufanya uchunguzi wa kina, na sio hivyo tu aliwahoji mamajusi na kutaka kujua kuwa ni kwa muda gani na wakati gani sahihi mtoto huyo atakuwa amezaliwa kufuatia mwenendo ya nyota waliyoiona nani wapi, na zaidi ya yote alitaka aletewe habari kamili kuhusu huyo mtoto kwa kusudi la kutaka kumuangamiza ona

Mathayo 2:4-8 “Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi? Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii, Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli. Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota. Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.”

Ni muhimu kufahamu kuwa roho ya Herode inatenda kazi hata leo, katika ulimwengu wa kisiasa, makazini, duniani na hata makanisani, katika nyakati hizi za mwisho hatuna budi kuhakikisha kuwa wakati wote tunaendenda kwa hekima sana kwani hali halisi ya kiroho ya watu wengi imebadilika sana, wauaji wakubwa kabisa, wenye chuki, waharibifu, wabambikiaji, wasingiziaji, wenye siasa chafu, wachawi na watu wenye wivu wenye uchungu nyakati za leo hawako nje ya kanisa bali sasa wako ndani ya kanisa na hata madhabahuni, tunazungukwa na mbwa mwitu wakali huku wewe na mimi tukiwa kama kondoo tu, Bila kuweka tumaini letu kwa Mungu ni rahisi sana kujeruhiwa, kuumizwa na kutendewa kila aina ya ubaya na hata kuuawa kwa njia za ajabu au kuwekewa sumu, na watu ambao wala hatukuwahi kudhani kuwa wanaweza kuwa wasaliti na wenye kupingana na mpango wa Mungu katika maisha yetu, hali inatisha sana kwa sasa, watu wanatuma mpaka watu watushambulie, wako watumishi wa Mungu ambao sasa wamekuwa wachawi hata wokovu sijui waliuacha lini, wako washirikina pia hali inatisha hata hivyo Mungu aliye hai yuko macho na bila shaka atakuokoa na kila mpango mbaya wa ibilisi na maajenti wake katika maisha yako na yangu!

Herode alikuwa ni mtu wa namna gani?

Herode ambaye pia alijulikana kama Herode mkuu alikuwa ni mtawala wa Israel iliyokuwa chini ya utawala wa Warumi, Kimsingi yeye alizaliwa mwaka wa 72 kabla ya Kristo na kwa asili alitokea maeneo ya Idumeya yaani Eneo la Edomu wana wa Esau, Yeye na ukoo wake waliwekwa kuwa watawala vibaraka kwa niaba ya utawala wa warumi, Mwanzoni yeye alitawala Galilaya na uyahudi kabla ya utawala wa watoto wake watatu ambao waligawana majimbo baada ya kifo chake na Herode Akleo akatawala Idumeya, Uyahudi na Samaria na Herode Antipas alitawala Galilaya na Philip alitawaka huko Jordan, Kwa mujibu wa mwanahistoria maarufu wa kiyahudi wa  karne ya Kwanza Josephus, Herode mkuu alikuwa ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa sana ambaye ili kuongeza ushawishi wake alimuoa binti wa kuhani mkuu wa kiyahudi Kayafa na pia wakati wa utawala wake alilikarabati Hekalu la pili la Yerusalem na  kuliongezea eneo mlima wa Hekalu kwa upande wa kaskazini, Jambo lililopelekea yeye kukubalika na Wayahudi wengi.  Hata hivyo pamoja na umaarufu wake mkubwa hivyo ni jambo la kushangaza ya kuwa alipozaliwa Yesu Kristo Mfalme huyu alifadhaika na kugadhibika na ili aweze kujihakikishia usalama wake alihakikisha kuwa anawaua watoto wote wapatao miaka miwili kule Bethelehemu ili yamkini aweze kumuua Yesu Kristo ona

Mathayo 2:16 “Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.”

Unaweza kuona Herode alikuwa ni mtu mwenye ghadhabu, mbinafsi na aliyekuwa hataki upinzani, alitamani kuwa yeye katika madaraka wakati wote, alitamani kuwa yeye abaki kuwa maarufu wakati wote, alikuwa mtu katili aliweza kuua watoto wote ili kujihakikishia usalama wake ni jambo la kusikitisha kuwa hii roho ya Herode ni roho inayotenda kazi katika nyakati zetu na katika kanisa la leo, Mara ngapi tumesikia viongozi wakubwa na maarufu wakiwaua wengine kisiasa na kuwachafua wengine kwa skendo za kutengeneza ili yamkini waweze kubakia wao tu madarakani, au wao tu waonekane kuwa ni safi na wenguine waonekane kuwa hawafai, au kuharibu umaarufu wa wengine  na wao tu waweze kuwa maarufu, hujawaona watu wenye kila kitu na wenye nguvu zote lakini wakifukuzana na watu masikini wasio na kitu wala nguvu yoyote wakitaka kuwazima ili yamkini wabakie wao tu hii ni roho chafu na mikono mibaya ya Herode, roho ya Herode ni roho ya watu wenye uchungu, hasira na tama mbaya wakiwa wamejawa na ubinafsi wa kila aina ni roho ya watu ambao hawawezi kufurahi nyota za wengine kung’aa lakini pamoja na hayo Bwana ana ujumbe muhimu leo Usiogope Bwana amenituma nikupe ujumbe huu kama nabii wake na kama malaika wake leo nakuletea habari njema ya kuwa wakati Herode anataka kusababisha misiba katika jamii, Mungu atakunusuru wewe na atakulinda na kukupa mlango wa kutokea mpaka atakapokufa Herode, Bwana atakuficha katika mikono yake nawe utakuwa salama hutaogopa madamu Mungu anakukubali, leo ziko habari njema kwaajili yako ona Yesu amezaliwa kwaajili yako na yeye ni mwokozi sio wa mtu mmoja tu wa ulimwengu mzima na hivyo amani inapaswa kutawala duniani kwa kila mtu ambaye Bwana ana mridhia najua wewe na mimi Bwana anaturidhia   

Luka 2:8-17 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.”

Kwaajili ya hayo ni imani yangu nani mpango wa Mungu ya kuwa pamoja na changamoto unazozipitia katika huduma, kazini ndoa na maeneo mengine Mungu hatimaye atatuokoa na mipango mikakakati ya heriode katika maisha yetu

Kuokolewa katika mikono ya Herode !

Mathayo 2:12-15 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.  Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.”

Kila mtu mwenye mapenzi mema Mungu ana mpango mkakati ulio mwema na maisha yako na kwa jinsi Mungu alivyomwema anatuwazima mem, Mungu hana mpango wa kusababisha maombolezo katika maisha yetu wala hana malipizi anayotulipiza kwaajili ya maovu yetu, Mungu ni mwema mno yeye anatuwazia mema hana kisasi juu yetu yeye sio mwanadamu ana mpango mwema na mahususi kuliko mpango alionao Herode wako na wangu ona ;-

Yeremia 29:11-13 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza. Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote..”       

Vile adui zako na zangu wanavyotuwazia sivyo Mungu anavyotuwazia nataka kuanzia Christmas hii uweze kuelewa kuwa hakuna adui anayeweza kusimama mbele yako na kupingana au kushindana na mapenzi ya Mungu yaliyowekwa ndani yako, kila baya linalokusudiwa na adui dhidi yako Mungu ataligeuza kuwa Baraka, kila adui anayekutafuta akuangamize ataangamiza wengine na wewe utajikuta umefichwa; msomaji wangu nataka nikuhakikishie yakuwa ujumbe huu ni halisi katika maisha yako hakuna wa kukupata, hakuna atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako sio kwa Herode huyu tu lakini kwa kila mkono wa Herode yeyote atakayeinuka juu yako Mungu atakuokoa na mikono yake, wakati wa Petro alikuweko herode mwingine aliyaangamiza maisha ya Yakobo mtume na akataka kumuangamiza na Petro, lakini Mungu akawa mwaminifu akamfungua Petro kutoka katika mikono ya Herode Mungu huyu huyu atakufungua na wewe   atakuweka huru na Herode wako atatokwa na roho Hakuna herode aliyewafuatilia watu wa Mungu na kuwatesa na kuwaua ambaye  alibaki salama, Herode aliyetaka kumuua Yesu alikufa Yesu akiwa amefichwa Misri na herode aliyemuua Yakobo alipotaka kumuua Petro Mungu aklituma malaika wake ona

Matendo 12:1-23 “Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi. Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba. Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.  Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango. Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake. Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu. Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine. Hata kulipopambauka askari wakaingiwa na fadhaa nyingi, amekuwaje Petro. Na Herode alipomtafuta, asimwone, aliwauliza-uliza wale walinzi, akaamuru wauawe. Kisha akatelemkia kutoka Uyahudi kwenda Kaisaria, akakaa huko. Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme. Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.”

Hitimisho.

Ujumbe wangu wa Chrismas hii ni unabii, ni ujumbe ambao sio tu wa sikukuu hii lakini ni ujumbe wa maisha ya siku zote wote wanaoonewa na watu wenye nyadhifa zilizokubwa kupita wao wasiogope ni ujumbe wa matumaini na kukutia moyo ya kuwa Mungu yuko na anaifuatilia mipango ya Herode na ata shughulika naye ni ujumbe wa maonyo pia kama una roho ye herode lazima utubu na kubadilika Mungu hawezi kufurahia udhalimu, kusudi lake ni pana mno na yuko tayari kulilinda kusudi lake kwa gharama yeyote wewe sio wa Muhimu kuliko wanaochipukia uwe na roho ya malezi walee wengine na kuwainua na kuwaunga mkono usijidhanie ya kuwa uko mwenyewe au kuwa wewe ndiwe maalumu sana kwa Mungu, kujenga hekalu hakutakusaidia, kuoa mtoto wa kuhani mkuu hakutakusaidia, kuwa na wapelelezi hakutakusaidia, kuwa na jeshi hakukusaidiaa kitu Mungu wetu ni mwenye Nguvu na hekima yake ni kubwa kuliko hekima ya kibinadamu, hii ni Chrismas ya wokovu nani ya habari njema kwa wote wanaoonewa na maonyo  makali kwa waonevu! Kamwe asitokee mtu akashindana na kusudi la Mungu lililoko ndani yako kwani atapotea kama walivyopotea wakina herode na kusudi la Mungu ndilo litakalosimama.

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!