Alhamisi, 21 Julai 2022

Waachie watu wangu waende!


Kutoka 3:7-10 “BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”



Utangulizi:

Tuwapo Duniani tunapitia changamoto za aina mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mikandamizo ya aina mbalimbali kutoka kwa Shetani ambaye ndiye adui mkubwa wa maisha ya wanadamu, Mungu hafurahii uonevu au udhalimu wa aina yoyote ule unaowapata wanadamu, Wana wa Israel kwa Muda mrefu sana walikuwa wakionewa na wamisri na wakikandamizwa ili waendelee kuwa watumwa katika nchi ya Misri, hawakuweza kutoka, na adui hakutaka kuwaachia kwa haraka mpaka Mungu alipoamua kuingilia kati.

Mungu alimtuma Musa kwa mfalme wa Misri yaani Farao ili amuamuru mfalme huyu awaachie wana wa Israel waende zao kwa kusudi alilolikusudia Mungu mwenyewe yaani wakamtumikie Mungu na kutimiza kusudi lake, Ujumbe mkubwa aliopewa Musa ulikuwa ni kumwambia Farao Mungu wa ewaebrania ameamuru uwaachie watu wake waende, WAACHE WATU WANGU WAENDE hii ilikuwa ni Amri na sio ombi ujumbe huu umerudiwa tena na tena kwa farao waachie watu wangu waende ona katika maandiko yafuatayo:-

Kutoka 5:1  Hata baadaye, Musa na Haruni wakaenda wakamwambia Farao, wakasema, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, WAPE WATU WANGU RUHUSA WAENDE, ili kunifanyia sikukuu jangwani.”

Unaona sifurahiswi kwa namna fulani na lugha inayotumika katika Kiswahili kwa sababu yenyewe iko katika mfumo wa kiungwana nani kama  ombi WAPE WATU WANGU RUHUSA WAENDE kimsingi Mungu hakuwa anaomba ruhusa Mungu alikuwa anaamuru ni amri kwa Farao WAACHIE WATU WANGU WAENDE, Lugha ya kiingereza katika maeneo yote yanayozungumzia WAPE WATU WANGU RUHUSA WAENDE  inatumia AMRI lugha inayotumika kiingereza ni neno LET MY PEOPLE GO sawa na kuamuru Waachie watu wangu waende ni aina hii ya lugha ndio inayojirudia rudia kila mahali kwenye kitabu cha kutoka  na maeneo mengine na unaweza kuona ;-

Kutoka 8:1 “BWANA akamwambia Musa, Ingia kwa Farao, ukamwambie, BWANA asema hivi, Wape watu wangu ruhusa, ili wapate kunitumikia.”

Kutoka 8:20 “BWANA akamwambia Musa, Inuka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao; angalia! Atoka aende majini; kamwambie, BWANA asema, Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie mimi.”

Kutoka 9:1 “Ndipo BWANA akamwambia Musa, Ingia wewe kwa Farao, umwambie, BWANA, Mungu wa Waebrania, yuasema, Wape ruhusa watu wangu ili waende wanitumikie.”

Kutoka 9:16-17 “lakini, nilikusimamisha wewe kwa sababu hii hii, ili nikuonyeshe uweza wangu, tena kwamba jina langu litangazwe katika dunia yote. Nawe, je! Hata sasa wajitukuza juu ya watu wangu, usiwape ruhusa waende zao”?          

Unaona ni kwanini Mungu amerudia mara kwa mara kwa msisitizo waache watu wangu waende? Mungu hafurahii udhalimu, ukandamizaji na mateso ambayo kwaasili watu wake wanayapitia Mungu aliamua kuingilia katika hali ya wana wa Israel kwa kuwa walikuwa wanaonewa na wamisri na wamisri ndio walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko Israel, Mungu hakubaliani na uonevu wa aina yoyote ile:-

Uonevu ni nini hasa!

1.       Ni kukandamizwa na kuwekwa chini ya mamlaka ya mtu mwingine mwenye nguvu zaidi yako bila matakwa yako mwenyewe

2.       Ni kuonewa au kuteswa na nguvu Fulani iliyojuu zaidi ya uwezo wako wa kawaida, bila uhuru kamili

3.       Uonevu hauko katika eneo moja tu, unaweza kuweko katika mwili, katika akili, katika nafsi, katika ndoa, katika fedha katika Elimu,Biashara, haki na kadhalika  na pia uko uonevu wa kiroho au tunaweza kusema kuwa asili yauonevu wa aina yoyote unaouona ni kutokea rohoni au katika ulimwengu wa kiroho;

Hatuna budi kugundua na kubaini ni maeneo gani ya uonevu shetani anatuonelea ili tuweze kuliitia jina la Mungu atuokoe, kumbuka Israel waliteseka mpaka pale walipolia na kutafuta msaada wa Mungu ndipo Mungu aliposhuka ili awaokoe ona Zaburi 118:5 “Katika shida yangu nalimwita BWANA; BWANA akanijibu akaniweka panapo nafasi.” Unaona kila shida unayoipitia kama mwanadamu hakikisha ya kuwa unamuita Bwana yaani Mungu naye atakuweka panapo nafasi yaani atakujibu na kutatua tatizo ulilonalo usinyamaze ukafikiri ya kuwa Mungu amekusahau, HAPANA Mungu anakutaka uwajibike na kufanya sehemu yako kwa kukataa hali unayoipitia.

Zaburi 42:9 “Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

Mwandishi wa zaburi aliamua kuomba Mungu Mwamba wake aliona kama amesahaulika adui alikuwa akimuonea na hakuwa na furaha alikumbuka kumwambia Mungu, ni lazima tumlilie Mungu atutoe katika hali zozote za mikandamizo tunazozipitia duniani kumbuka kuwa ni ahadi ya Mungu kutuweka huru kutoka kwa wale wanaotuonea, Mungu ameahidi kwamba utakuwa mbali na kunewa ona  

Isaya 54:14. “Utathibitika katika haki; utakuwa mbali na kuonewa, kwa maana hutaogopa; na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia.”

Wakati wowote uonevu sio jambo zuri, maandiko yanasema uonevu humfanya mtu awe kama kichaa, Moja ya sababu ya kuja kwa Yesu Kristo duniani kama Mwokozi ni pamoja na kufanya kazi ya kuwafungua walioonewa ona Matendo 10:38 “habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.” Adui yetu mkuu adui wa wanadamu wote na anayetuonea ni shetani yeye hutuonea katika mazingira mbalimbali na wakati mwingine anawatumia watu kuleta uonevu, shetani na mapepo na maajenti wake wanaweza kumuonea mwanadamu katika maeneo zaidi ya kumi na tano:-

·         Unaweza kuonewa Mwili

·         Unaweza kuonewa kwa asili

·         Unaweza kuonewa kiakili

·         Unaweza kuonewa Kiroho

·         Unaweza kuonewa katika Ndoa yako

·         Unaweza kuonewa kiuchumi

·         Unaweza kuonewa Kazini

·         Unaweza kuonewa katika ndoto

·         Unaweza  kuonewa kwa maneno

·         Unaweza kuonewa kihisia/Kisaikolojia/kijinsia.

·         Unaweza kuonewa kichawi

·         Unaweza kuonewa kwa ukoo mzima mnateswa ukoo wenu wote au familia yenu yote

·         Unaweza kuonewa kwa nguvu na uonevu wa kukandamizwa

·         Unaweza kuonewa katika haki zako makahamani

·         Unaweza kuonewa bila sababu

·         Unaweza kuonewa kwa sababu

·         Unaweza kuonewa kihuduma

Maandiko yanaonyesha kuwa kila aina ya uonevu hutoka kwa shetani Yohana 10:10Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.” Ni kwa sababu ya kuonewa kwa namna mbalimbali Mungu alimpaka Yesu Mafuta ili aweze kuwakomboa wanadamu, na Mungu vilevile huwapaka watumishi wake mafuta ili kuzivunja nira za uonevu ona Luka 4:18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.” Unaona Lugha inayotumika hapo kusetwa maana yake ni kuonewa huduma ya kimasihi ilitolewa na Mungu kwa wanadamu kwa kusudi la kuwaweka watu huru kutoka katika uonevu wa kila namna, kama Musa ambaye alikuwa na ujumbe waache watu wangu waende, Yesu ana ujumbe ulio bora zaidi katika ufalme wa ibilisi kumuamuru kwa jina lake kukuacha uwe huru kutoka katika aina yako ya mgandamizo uliyo nayo!

Tunawezaje basi kutoka katika migandamizo ya shetani.

1.       Kubali zawadi ya wokovu:

Ni ukweli ulio wazi kuwa wokovu ni msamaha wa dhambi, nani ukweli ulio wazi kuwa Mungu anatuhurumia na mgandamizo mkubwa na wa kwanza alionao mwanadamu ni kuwa katika maisha ya dhambi, dhambi yenyewe ikukutawala inakugeuza kuwa mtumwa inakukandamiza, wanadamu wengi wanakandamizwa na dhambi hivyo ni watumwa wa dhambi hawawezi kuimudu na hawawezi kuishinda ona Yohana 8:34 “Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.” Matatizo mengi ya wanadamu yamesababishwa na dhambi, mtu anayedumu katika dhambi naye ni mtumwa wa dhambi, dhambi ni mlango mkubwa wa mashambulizi mengi ya adui katika maisha yetu na uharibifu wa kila namna,  wakati mwingine utaweza kuona mtu aliposamehewa dhambi hapo hapo alipata na uponyaji wa mwili na akili na roho ona Zaburi 103:3 “Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,” unaona Mungu anaposamehe dhambi katika kifurushi kimoja hikihiki cha msamaha anatoa na uponyaji kwa hivyo kimaandiko ni dhahiri kwamba dhambi ikiondoka kwetu ni rahisi sana kuwa huru katika maeneo mengine Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.” Unaona yako mateso mengine ambayo yana uhusiano wa moja kwa moja na dhambi japo sio yote hivyo Mungu anapotusamehe dhambi basi moja kwa moja anatuweka huru vile vile na kutupa uzima wa maeneo mengine, unapokuwa kwenye dhambi unapoteza haki zako nyingi ikiwa ni pamoja na ulinzi wa Mungu na hivyo adui anakuwa na mamlaka ya kukuonea lakini wokovu unapokuja kwetu tunapewa haki yetu

 

Warumi 6:16-20 “Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki. Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki. Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa. Kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki.”

 

Uko uhusiano mkubwa sana wa mafanikio yetu ya kiroho yaani wokovu na afya yetu Yakobo 5:13-15 “Mtu wa kwenu amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi. Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.”


3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako kama vile roho yako ifanikiwavyo

 

Unaona kwa hiyo kuipokea zawadi ya wokovu ni kwa Muhimu na msingi wa kufunguliwa kwetu kutoka katika migandamizo ya namna mbalimbali wokovu una uhusiano mkubwa na kusamehewa dhambi Luka 1:77 “Uwajulishe watu wake wokovu, Katika kusamehewa dhambi zao.”  Na Mafanikio yetu katika mambo yote asili yake ni mafanikio ya roho zetu, Ni kwaajili ya ukombozi wa Mwanadamu Mungu alimtuma Yesu duniani ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele kwa hivyo tunapata uzima huu na uzima wa milele, Yesu alitolewa pale msalabani na kuteswa na kuuawa ili sisi tuweze kupona katika maeneo yote kama asemavyo nabii Isaya mahali Fulani hivi:-

 

Isaya 53:3-5 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

 

Kumbe ni ukweli ulio wazi kuwa tukimwamini Bwana Yesu kazi yake aliyoifanya pale msalabani na kuikubali kama zawadi tutaokolewa, Na ndani ya wokovu tutapata raha nyingi sana nafsini mwetu wokovu huwa na ukombozi mkubwa na wa aina nyingi. Yesu alikuwa ameahidi tujitie nira yake ili tusilemewe na mizigo yaani utumwa wa namna mbalimbali Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”    

 

2.       Uwe na ufahamu wa neno la Mungu.

 

Ufunuo 12:10-11 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.”

 

Neno la ushuhuda maana yake ni neno la Mungu, neno la Mungu lina nguvu na mamlaka kubwa sana kuliko tunavyodhani lenyewe linafananishwa na nyundo ivunjayo mawe vipande vipande ona Yeremia 23:28-29 “Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana. Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?

 

Unaona iwapo unataka ushindi katika maisha yako huna budi kujaa neno, Neno linafananishwa na moto au nyundo ivunjayo mawe vipande vipande, hivyo tukiujaza ufahamu wetu kwa neno la Mungu kila aina ya utumwa itavunjika haijalishi ni utumwa  wa zamani kiasi gani, au ni wenye nguvu kiasi gani wala haijalishi ni nani ametuweka kwenye utumwa huo, au utumwa huo unatokea wapi?, kinga kubwa na ya kipekee na silaha ya kumshambulia adui na kupata ushindi ni neno la Mungu.

 

Waebrania 4:12-13 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo. Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”       

 

Kamwe tusilidharau neno la Mungu wala kulichukulia kama kitu cha kawaida neno la uzima linga nguvu ya kubadili kila kitu katika maisha yetu neno la Mungu linapotamkwa huwa haliendi bure ni lazima litatimiza mapenzi ya Mungu ona

 

Isaya 55:9-11 “Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu. Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.”

 

Neno la Mungu ni roho tena ni uzima Yohana 6:63 “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.”               

 

Muda usingeweza kutosha kupitia maeneo kadhaa wa kadhaa yanayotufundisha kuhusu neno la Mungu ni ukweli ulio wazi kuwa Yesu alipopandishwa katika mlima wa majaribu alikutana na shetani na kwa kutumia neno la Mungu aliweza kupata ushindi mkubwa hakuweza kujitia chini ya ushawishi na majaribu ya yule Muovu, tunaweza kushinda hali zozote zile endapo tutakuwa na tabia ya kutafuta neno la Mungu linazungumza nini kutokana na hali yetu na ile hali tunayokumbana nayo na tukajiweka huru!

 

3.       Omba kwaajili ya ukombozi.

 

Mwanadamu anapokuwa anakandamizwa na ibilisi katika maeneo mbalimbali, kumbuka kuwa huwezi kujitoa mwenyewe katika maeneo hayo, ni lazima umuombe Mungu aje akupe msaada wa ukombozi, akukomboe kutoka katika hali unayoipitia, Neno ukombozi limetajwa mara 147 katika maandiko, Yesu ni mwokozi maana yake vilevile ni Mkombozi,  watu waliokuwa wanatazamia kuzaliwa kwa Masihi vilevile wanaitwa watu waliokuwa wakiutazamia ukombozi

 

Luka 2:36-38 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake.”

 

Yesu kwa kuwa ni Mkombozi ni vema tunapopita taabuni ni muhimu kuliitia jina lake kwaajili ya ukombozi, kwanini kwa sababu maandiko yanaonyesha ya kuwa ndani yake yeye tunao ukombozi, Waefeso 1:6-7 “Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.” Kwa hiyo tunakubaliana kuwa kuna ukombozi na huu hufanywa na Yesu Kristo kwa neema yake, Yeye alijitoa mwenyewe ili atukomboe sisi

 

Tito 2:13-14 “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.”

 

1Wakorintho 1:30-31 “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi; kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.”

 

Yesu kama mkombozi wetu yu aweza kutukomboa nafsi zetu miili yatu na roho zetu, Mungu alimkomboa Daudi katika shida zake zote na hakusahau jambo hili katika maisha yake yote, kumbe tunaweza kupitia shida na mateso ya aina mbalimbali lakini Mungu anaweza kutukomboa na shida zote ona 1Wafalme 1:30 “Naye mfalme akaapa, akasema, Bwana aishivyo, aliyenikomboa roho yangu katika shida zoteKristo Yesu anaweza kutukomboa na shida zetu zote maana yake kila eneo ambalo kwalo adui anakusudia kutukandamiza au anatukandamiza tayari tunaye mkombozi,  tunaweza kukombolewa, familia zetu, maisha yetu, ndoa zetu, uchumi wetu,  na hata kama tunadhani kuwa tuna laana ya aina yoyote laana hizo zinaweza kukombolewa kupitia Jina la Yesu, Lakini vilevile kwa imani katika kazi yake aliyoifanya pale Msalabani

 

Wagalatia 3:13-14 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.”

 

Ni wajibu wetu kama waamini kuutarajia ukombozi Zaburi 130:7-8 “Ee Israeli, umtarajie Bwana; Maana kwa Bwana kuna fadhili, Na kwake kuna ukombozi mwingi.Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.”  Mungu ameahidi kuwa tumtarajie yeye, kumtarajia maana yake kumsubiria, kumgojea katika njia ya Maombi, na kumtazamia, tunapaswa kuiamini ahadi hii ya Mungu na kumuomba ukombozi katika maeneo mbalimbali tunayokandamizwa, Yeye ana uwezo wa kutukomboa katika taabu zote, tunapomlilia yeye hutuponya na taabu zetu zote na kutukomboa  Zaburi 107:1-6. “Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. Na waseme hivi waliokombolewa na Bwana, Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi. Akawakusanya kutoka nchi zote, Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini. Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa. Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.”

 

Tukimlilia Mungu na kumuomba yeye atatuma ukombozi katika maisha yetu Zaburi 111:9 “Amewapelekea watu wake ukombozi, Ameamuru agano lake liwe la milele, Jina lake ni takatifu la kuogopwa.”

 

Hatuna budi kumuomba Mungu na kumlilia ili atukomboe na kutuachia kila mmoja asiwe chini ya uonevu na kukandamizwa na ibilisi, Mungu na amuweke huru kila mmoja na familia yake na ndugu zake na jamaa zake, Mungu atupe kuwa mbali na uonevu, Mungu na atuthibitishe katika haki!, hatuna budi kumuomba Mungu atukomboe na roho zote chafu za uharibifu, kiburi, migawanyiko, woga, uzushi, mikandamizo, rushwa, uchafu, ufisadi, tamaa, mashaka, kutokusamehe, upotoshaji, uvivu, uchawi, utapeli, uasi, hasira, ulevi, Mauti, maluweluwe, uchungu, zinaa na uasherati, ulafi, choyo, ubinafsi,  na mambo yanayofanana na hayo!.

 

4.       Tumia silaha ya kusifu:

 

Moja ya silaha Muhimu ya ukombozi wetu kutoka kwa Mungu kwa mujibu wa maandiko ni pamoja na kumsifu Mungu, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuanza maombi kwa Msingi wa kumsifia Mungu kumuheshimu na kumtukuza yaani kumsifu Luka 11:1-2 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake. Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.] Kusifu ni mlango au ufunguo wa kuingilia katika nyua yaani katika ukumbi wa Mungu kwaajili ya kupokea huduma na majibu ya mahitaji yetu Zaburi 100:1-5 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.” Kwa hiyo tunapoenda mbele za Mungu kwa ibada ya aina yoyote ile ikiwa ni pamoja na maombi ni muhimu kuanza na kusifu kwa sababu sifa kwa Mungu inafungua mambo mengi na kumfanya Bwana atujali, na kutusikiliza, Zaburi 29:1-2 “Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu; Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” Kwa nini maandiko yaaagiza kuanza ibada au maombi kwa kumsifu Mungu? Ziko sababu kadhaa wa kadhaaa:-

 

1.       Kusifu kunaandaa mioyo yetu kumwangalia Mungu huku tukiwa tunatambua sifa zake, tunapoaishwa kupelekwa kwenye uwepo wake na kutusaidia kuelewa ukuu wake pale tunapomuendea  lakini sio hivyo tu sifa zina tabia ya kuufanya uwepo wa Mungu kushuka na kutuhudumia 2Nyakati 5:13 “tena Walawi waimbaji, wote pia, yaani Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na wana wao, na ndugu zao, hali wamevaa kitani safi, wenye matoazi na vinanda na vinubi, wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na pamoja nao makuhani mia na ishirini wakipiga panda;) hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru Bwana nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya Bwana,hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya lile wingu; kwa kuwa nyumba ya Mungu imejaa utukufu wa Bwana.” Kumbuka ya kuwa Mungu anakaa katikati ya sifa Zaburi 22:3 -5 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli.Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike.”

2.       Kusifu kunaharibu vifungo vya adui Kila kitu ambacho kinakandamiza maisha ya mwanadamu na kututishia katika uonevu wa aina yoyote ile kimwili na hata kiroho vinaweza kutiishwa na kuharibiwa kupitia Maombi Matendo 16:23-26 “Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana. Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale. Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.”

3.       Kusifu na kuabudu kunamfanya adui achanganyikiwe na kupoteana, Hakuna silaha ya ajabu kama kumsifu Mungu na kumuabudu, silaha hii ni ya kipekee inapotumika katika tishio la kivita au uonevu Bila kujali kuwa jeshi lililojipanga ni kubwa kwa kiwango gani kumsifu Mungu kutatuletea ushindi wa kushangaza sana angalia 2Nyakati 20:1-4 “Ikawa baadaye, wana wa Moabu, na wana wa Amoni, na pamoja nao baadhi ya Wameuni, wakaja juu ya Yehoshafati vitani.Wakaja watu waliomwambia Yehoshafati, wakisema, Wanakuja jamii kubwa juu yako watokao Shamu toka ng'ambo ya bahari; na tazama, wako katika Hasason-tamari (ndio En-gedi).Yehoshafati akaogopa, akauelekeza uso wake amtafute Bwana; akatangaza mbiu ya watu kufunga katika Yuda yote.Yuda wakakusanyika pamoja ili wamtafute Bwana; hata kutoka miji yote ya Yuda wakaja kumtafuta Bwana.” Wakati majeshi ya wana wa Moabu na wana wa Amoni na Wameuni walipokuwa wameungana kinyume na mfalme Yeshoshafati, unaweza kuona pamoja na silaha yote ya kufunga na kumuomba Mungu safari hii maelekezo ya Mungu namna ya kupigana na kupata ushindi ilikuwa ni kupanga waimbaji ili wamsifu Mungu ona 2Nyakati 20:14-26 “Ndipo Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu, akajiliwa na roho ya Bwana, katikati ya kusanyiko; akasema, Sikieni, Yuda wote, nanyi mkaao Yerusalemu, na wewe mfalme Yehoshafati; Bwana awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani vita si yenu bali ni ya Mungu. Kesho shukeni juu yao; tazameni, wanakwea kwa kupandia Sisi; nanyi mtawapata penye mwisho wa bonde, mbele ya jangwa la Yerueli. Hamtahitaji kupigana vita, jipangeni, simameni, mkauone wokovu wa Bwana ulio pamoja nanyi, enyi Yuda na Yerusalemu; msiogope, wala msifadhaike; kesho tokeni juu yao; kwa kuwa Bwana yu pamoja nanyi. Yehoshafati akainama kichwa, kifulifuli; wakaanguka mbele za Bwana Yuda wote na wakaao Yerusalemu, wakimsujudia Bwana. Na Walawi, wa wana wa Wakohathi na wa wana wa Wakorahi, wakasimama ili wamsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana. Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwaminini Bwana, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa. Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia Bwana, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu, wakitoka mbele ya jeshi, na kusema, Mshukuruni Bwana; kwa maana fadhili zake ni za milele. Nao walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa. Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe. Hata Yuda walipofika mnara wa kulindia wa jangwani, wakalitazama hilo jeshi; nao, angalia, walikuwa maiti walioanguka nchi, wala hapana aliyeokoka. Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana.Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia Bwana; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.”

Unaona kumbe hatupaswi kuwa na hofu iko njia nyepesi sana na silaha nzito ya kutukomboa nayo ni kumsifu Mungu, hii ni silaha kuu ya kiroho hatupaswi kwa namna yoyote kudhani au kufikiri kuwa wakati wa kumsifu Mungu ni wakati wa mzaha hapana ni wakati ambapo Mungu yuko kazini hivyo hatuna budi kumaanisha linapokuja swala la kumsifu Mungu Zaburi 8:2 “Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.”  Watu wanapomsifu Mungu hata kama ni watoto kunakuwa na misingi ya nguvu na kukomesha adui na kujilipizia kisasi wote wanaoshindana nasi watatupwa nje kama tutagundua siri iliyoko katika sifa, kusifu kunatoa nguvu na kibali cha kuwafanyika hukumu dhidi ya adui zetu na wafalme wao Zaburi 149:5-9 “Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao. Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao. Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya kabila za watu. Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma. Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.”               

 

Unaona kwa msingi huo hatuna budi wakati wote kukumbuka ya kuwa kumsifu Mungu ni silaha yenye nguvu kubwa na ya ajabu sana inayoweza kusukuma nyuma majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho na mwili pia, kumsifu Mungu na kumtukuza hutufanya na kuyanoa mawazo yetu ili yaweze kumuelekea Mungu na kutambua ukuu wake na uweza wake kila siku kama ikiwezekana tuwe na Muda wa kumtukuza Mungu na kumsifu Biblia imeeleza hata vitandani mwetu, unapopita katika wakati Mgumu acha kuogopa mwamini Mungu na hakikisha kuwa unamuelekea yeye na wakati mwingine jaribu tu kumsifu na utaweza kuona Mungu atakuweka huru! Hakuna Jeshi la aina yoyote litakaloweza kushindana nawe kama wewe ni mtu uliyejaa sifa kwa Mungu, Kumsifu Mungu namna hii ndio siri ya ushindi wa Daudi katika maisha yake yote yeye alikuwa mtu aliyejaa zaburi za sifa na hivyo hakuwahi kushindwa vita ya aina yoyote!

 

Zaburi 27:1-6 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini. Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake. Mradi atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema yake, Na kuniinua juu ya mwamba. Na sasa kichwa changu kitainuka Juu ya adui zangu wanaonizunguka. Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake; Nitaimba, naam, nitamhimidi Bwana.”

 

5.       Omba upako wa Roho Mtakatifu.

 

Roho Mtakatifu ni moja ya mwanachama muhimu katika utatu wa Mungu anajihusisha sana na maeneo mengi ya ukombozi wetu, yeye ni chanzo cha ushuhuda na ufunuo, anatuongoza katika maamuzi ya kiulinzi kimwili na kiroho ili tusiiingie hatarini,  yeye ni mfariji pia na hivyo anauwezo wa kutusaidia na kutupa tumaini, Katika nyakati za agano la kale popote pale ambapo palitokea uonevu na ukahitajika msaada wa kiungu basi Roho wa Mungu alikuja kwa nguvu juu ya mmoja wapo ya waamuzi au mfalme na mfalme huyo akawaweka watu huru,  uhuru huu ulitokana na upako wa Roho Mtakatifu, tunaambiwa kuwa Upako unavunja nira  ona Isaya 10:27Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.” Maandiko yanaonyesha kuwa Upako yaani mafuta ya Roho Mtakatifu huwa yanafanya kazi ya kuondoa uonevu, Ni kazi ya Roho Mtakatifu kuwatia mafuta watumishi wake ili wafanye kazi ya kuwatoa watu kutoka katika uonevu wa namna mbalimbali ona Luka 4:18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.” Unaona mafuta yaliyokuwa juu ya Yesu kutokana na Roho Mtakatifu yalifanya kazi mbalimbali ya kuwafungua watu walioonewa na kukandamizwa na shetani, sio hivyo tu lakini na kuwaponya na kuwaweka huru, tunaweza kusoma pia katika Matendo 10:38 “habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.”

 

Nyakati za agano la kale hususani kipindi cha waamuzi na wafalme Mungu Roho Mtakatifu aliwawezesha wakati wote kufanya matendo ya ukombozi baada ya yeye kuja juu ya watumishi wake na kuwatia nguvu iliyowawezesha kuwasaidia ndugu zao wasikandamizwe au waliokuwa wanakandamizwa na maadui na kuwakimbiza adui zao ona maeneo mblimbali:-

 

Waamuzi 3:9-11 “Kisha wana wa Israeli walipomlingana Bwana, Bwana akawainulia wana wa Israeli mwokozi, aliyewaokoa, yaani, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu. Roho ya Bwana ikamjilia juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli; akatoka kwenenda vitani, naye Bwana akamtia huyo Kushan-rishathaimu, mfalme wa Mesopotamia, mkononi mwake; na mkono wake ukamshinda Kushan-rishathaimu. Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka arobaini. Kisha Othnieli, mwana wa Kenazi, akafa.”

 

Waamuzi 13:24-25 “Basi yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni, mtoto huyu akakua, Bwana akambarikia. Roho ya Bwana ikaanza kumtaharakisha katika Mahane-dani, katikati ya Sora na Eshtaoli.”

 

Waamuzi 14:19 “Roho ya Bwana ikamjilia juu yake kwa nguvu, naye akatelemkia Ashkeloni, akapiga watu waume thelathini katika watu hao, na kuzitwaa nyara zao, na kuwapa hao waliokitambua kitendawili mavao hayo. Hasira zake zikamwaka, naye akakwea kwenda nyumbani kwa baba yake.”     

 

Waamuzi 11:28-29. “Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea. Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni.”

 

Unaona popote pale waaamuzi walipowasaidia watu ili kuwaletea ukombozi utaweza kuona Roho Mtakatifu alikuja juu yao kwanza, Ni Roho huyu huyu Mtakatifu aliyeyainua maisha ya waamuzi ili kuwatetea watu wake dhidi ya migandamizo ya aina mbalimbali anaweza kwa uhalisia kutuwezesha na sisi kuondoka katika migandamizo ya aina mbalimbali, ni mfariji, ni kiongozi kwa awaye yote anayemtegemea atakuonyesha yakupasayo kufanya na kukupa mbinu unazozihitaji,  kila mtu anahitaji, kuwa na maono, hekima, ujasiri na kukabiliana na changamoto za aina mbalimbali unapotaka kulitumikia shauri la Bwana au kutimiza kusudi lake duniani, utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutimiza hilo kama utamruhusu Roho Mtakatifu akutie nguvu, unapojaribu kuongoza bila Roho Mtakatifu utaanguka lakini ili uweze kufanikiwa tunamuhitaji Roho wa Mungu. Matendo 11:22-24 “Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia. Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo. Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.”

 

6.       Mkemee shetani na majeshi yake yote.

 

Katika maombi yetu ni muhimu kukumbuka kuwa na maombi ya kufanya vita dhidi ya ibilisi, kumshughulikia shetani na majeshi yake na maajenti wake wote ni wajibu pekee tuliopewa na Mungu sio ombi ni amri ona, Mfumo wa kishetani uko katika protokali za kijeshi, hivyo Ndivyo Mungu alivyowaumba, Mungu anaitwa Bwana wa Majeshi, Yeye ndio Amiri Jeshi mkuu ana serikali na ana dola Mbinguni, Malaika waliumbwa kama vyombo vya Dola, hii ikiwa ni pamoja na Malaika walioasi baadaye yaani majeshi ya Pepo wabaya katika ulimwengu war oho, kwa msingi huo wao husikiliza amri na mari haitolewi kama ombi inatolewa kwa mamlaka kwa kuamuru kupitia mairi Jeshi mkuu wa Majeshi ya Bwana yaani Kristo ona Waefeso 6:10-13 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.”

 

Kwa msingi huo unaweza kugundua kuwa shetani na serikali zake wako katika mfumo wa kijeshi na ndio maana Yesu aliamuru tumshughulikie alitupa amri sio ombi la kumshughulikia shetani angalia mfumo wa lugha inayotumika  katika     

 

Luka 10:17-19 “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.”

 

Maandiko wakati wote yanaonyesha lugha ya kupinga na kukemea linapokuja swala la maombi yetu dhidi ya kushughulikia kazi za shetani, wakati wote maombi ya kimapambano dhidi ya ibilisi ni kukemea ni kupigana vita ona maagizo ya kimaandiko:-

 

2Wakoritho 10:3-5 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia

 

1Petro 5: 8-9 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.”

 

Yakobo 4:7-8 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. 

 

Zekaria 3:2 “Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?

 

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.”

 

Kwa kuwa shetani anataka kuwakandamiza watu wetu, sisi wenyewe,familia zetu na hata taifa letu linapokuja swala la kumtaka aachie huwa ni amri kali, achiaa, toka, nakuamuru, bwana na akukemee na kadhalika hakuna lugha laini wakati wa kumkemea shetani, ni kumuamuru aachie haraka na taaachialia

 

7.       Vunja madhabahu za uovu

 

Ni muhimu kufahamu kuwa mawasiliano yote ya kiroho kati ya Mungu na wanadamu au miungu na wanadamu hufanyika kupitia madhabahu, kwa msingi huo Mungu aliwaagiza wana wa Israel watakapoingia katika inchi ya kanaani moja ya jambo muhimu wanalopaswa kulifanya ni kuzivunja madhabahu zao agizo hili la kuharibu madhabau za uovu limerudiwa tena na tena katika maandiko ona Kutoka 34:12-13 “Ujihadhari nafsi yako, usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi ile unayoiendea, lisiwe mtego katikati yako. Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yaoUnaona unaweza kuona tena Kumbukumbu la torati 7:1-7 “Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang'oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe; wakati Bwana, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao;binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake.Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi. Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga. Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako; Bwana Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.”

Kwa nini Mungu aliamuru Madhabau za mataifa yasiyomcha Mungu yaharibiwe? Hii ni kwa sababu madhabahu ndio ni eneo la kutolea sadaka kwa miungu au kwa shetani ndio eneo la mwasiliano kati ya miungu na wanadamu, kwa hiyo madhabahu ndizo zinaziotumika kufanya mawasiliano ya kipepo na kufanya uchawi, kutengeneza hirizi, kupokea maelekezo ya kipepo, kufanya uaguzi, kufanya utambuzi kwa ramli  na mawasiliano yote kati ya miungu na wanadamu hufanyika kupitia madhabahu, ni madhabahu ndio zinazotumika kuwafunga watu na kuwaweka katika mahusiano ya kipepo na kusababisha mikandamizo, watu wanapotaka kukutana na ulimwengu wa kiroho basi pale wanapokutania kwa ibada ndio maagano ya kipepo yanapofanyika au mahusiano na mapepo ndipo yanapofanyika na ndipo maisha ya watu wengi yanapoharibiwa

 

2Wafalme 3:26-27 “Naye mfalme wa Moabu alipoona ya kwamba ameshindwa vitani, alitwaa pamoja naye watu mia saba wenye kufuta panga ili wapenye hata kwa mfalme wa Edomu; wala hawakudiriki. Ndipo akamtwaa mwanawe wa kwanza, yeye ambaye angetawala mahali pake, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta. Kukawa hasira kuu juu ya Israeli; basi wakatoka kwake, wakarudi kwenda nchi yao wenyewe.”               

 

Balaamu alipokodiwa kuja kuwalaani Israel utaweza kuona jambo la kwanza kulifanya ni kutengeneza madhabahu unaweza kuona Hesabu 23:1-5 “Balaamu akamwambia Balaki, Nijengee hapa madhabahu saba, ukaniandalie hapa ng'ombe waume saba, na kondoo waume saba.Balaki akafanya kama Balaamu alivyonena. Balaki na Balaamu wakatoa sadaka, ng'ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu. Balaamu akamwambia Balaki, Simama karibu na sadaka yako, nami nitakwenda, labda Bwana atakuja kuonana nami; na lo lote atakalonionyesha nitakuambia. Akaenda hata mahali peupe juu ya kilima. Mungu akakutana na Balaamu; naye Balaamu akamwambia, Nimetengeneza madhabahu saba, nami nimetoa sadaka ng'ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu. Bwana akatia neno katika kinywa chake Balaamu, akasema, Umrudie Balaki; ukaseme maneno haya.”

 

Kabla ya Mungu kumtumia Gideoni kama Mwamuzi wa Israel kwa uwezo wake Gideoni alipoisikia msauti ya Mungu aliye hai aliamua kuivinja kwanza Madhabahu ya baba yake ona Waamuzi 6:24-32 “Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri. Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo; ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata. Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama Bwana alivyomwambia; lakini ikawa kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku. Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng'ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa. Wakaambiana, Ni nani aliyetenda jambo hili? Hata walipotafuta habari na kuuliza, wakasema, Gideoni, mwana wa Yoashi, ndiye aliyetenda jambo hili. Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi Mlete mwanao, afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa sababu ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo. Yoashi akawaambia watu wote waliokuwa wakishindana naye, Je! Mtamtetea Baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakayemtetea na auawe hivi asubuhi; kama yeye ni Mungu, na ajitetee nafsi yake, kwa sababu mtu mmoja ameibomoa madhabahu yake. Basi akamwita Yerubaali siku hiyo, akisema, Baali na atete naye kwa ajili ya nafsi yake, kwa sababu ameibomoa madhabahu yake.”        

 

Unaona kwa sababu hiyo ni lazima tunapotaka ukombozi kutoka katika maeneo mbalimbali ya maisha yetu hatuna budi kuharibu kila njia za mawasiliano ya kishetani kwani hizo ndio madhabahu zenyewe, haribu, hirizi, pembe au vyungu, vimbo au vifaa vyote vya kiroho ambavyo umepewa na waganga au ambavyo vimezindikwa nyumbani kwenu, kumbuka kuwa Madhabahu ndio njia ya mawasiliano, na ikiwa madhabahu hiyo sio ya kiungu, basi itapingana na sheria za kiungu, za Mungu aliye hai, madhabahu ya miungu migeni itazuia neema ya Mungu wetu kwetu, itaweka mipaka ya utendaji wa kiungu kwetu, itafungua milango ya roho chafu, itasababisha matatizo yasiyoweza kupata ufumbuzi, itachelewesha sana upatikananaji wa Baraka zako, itasababisha matatizo yasiyoisha, inaweza kushababisha talaka, umasikini, kurudi nyuma, utasa, vifo, aibu  na mambo ya ajabu ajabu, madhabahu zina uwezo wa kusababisha laana au Baraka, Madhabahu ni ukumbusho kwa wale walioziinua, ili uweze kupata upenyo katika maisha yako ni lazima uziharibu madhabahu zisizo rasmi na makuhani wake, Madhabahu hugeuka na kuwa njia (Malango) ya kuvutia viumbe wa kiroho kufanya utembeleo aidha awe Mungu au miungu yaani mapepo

 

Mathayo 16:18 . “Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.”

 

Mwanzo 28:11-19 “Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake. Na tazama, BWANA amesimama juu yake, akasema, Mimi ni BWANA, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako. Na uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi, na mashariki, na kaskazini, na kusini; na katika wewe, na katika uzao wako, jamaa zote za dunia watabarikiwa. Na tazama, mimi nipo pamoja nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia. Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli BWANA yupo mahali hapa, wala mimi sikujua. Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.”

 

Unaona kwa msingi huo hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaharibu kila aina ya madhabahu ambayo iko kinyume na Mungu wetu ili kuzuia sisi kuwa chini ya utumwa wa miungu mingine kama haya yakifanyika vema basi Ibilisi atatii na kukuacha uende, waachie watu wangu waende, Wakati wote unapotaka Mungu awe pamoja nawe na kukukomboa unapotaka mpenyo katika maisha yako na unapotaka Mungu atembee nawe ni lazima kuhakikisha kuwa njia zote za mawasiliano na miungu migeni zinahabiwa na kutupwa mbali ili Mungu atembee katikati yako na familia yako haribu miungu migeni iondoe katika nyumba yako ichome moto ifukie baki na Mungu akiye hai na uwepo wa Mungu utakuwa pamoja nawe na hakuna wa kukuonea utaogopwa kila utakakopita

 

Waefeso 19:19 “Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu.”  

 

Mwanzo 35:1-5 “Mungu akamwambia Yakobo, Ondoka, panda uende Betheli, ukakae huko; ukamfanyie Mungu madhabahu huko; yeye aliyekutokea ulipomkimbia Esau, ndugu yako. Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu, mjisafishe mkabadili nguo zenu.Tuondoke, tupande kwenda Betheli, nami nitamfanyia Mungu madhabahu huko; yeye aliyenisikia siku ya shida yangu, akawa pamoja nami katika njia yote niliyoiendea. Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu. Wakashika njia, hofu ya Mungu ikaishika miji iliyowazunguka, wala hawakuwafuata wana wa Yakobo.”

 

Imani yangu ni kuwa somo hili ukilifanyia kazi na kuweka yote niliyokufundisha kivitendo utashangaa kwa miujiza ya ajabu na mpenyo wa ajabu utakaoambatana na maisha yako kuanzia leo namuomba Mungu kwamba uongezewe neema unapoadhimisha siri za ukombozi wako kupitia somo hili katika jina la Yesu Kristo  wa Nazareth Mwana wa Mungu aliye hai amen.

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatatu, 18 Julai 2022

Mwana wa Muungwana na mwana wa mjakazi


Wagalatia 4:28-31 “Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi. Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa. Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana. Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.”


Utangulizi:

Ni muhimu kuelewa kuwa Paulo Mtume alikuwa anakamilisha Mafundisho yake kwa Kanisa lililokuwako Galatia ambao walikuwa wamekumbana na kadhia ya  Mateso pamoja na Mafundisho mabaya ya Jamii ya wayahudi waliokuwa waanaamini katika sheria ya Musa na hata baada ya Injili kuhubiriwa wao waliwataka wakristo waendelee kuwa chini ya sheria ya Musa badala ya kuutumia uhuru wao waliokuwa nao katika kristo, Katika kuhitimisha mafundisho yake anaonyesha kuwa kuna wana wa Muungwana na wana wa Mjakazi.  Na anajaribu kuonyesha tofauti zao watoto hao kwamba Mwana wa Mjakazi alizaliwa kwa mapenzi ya Mwili na yule wa  Muungwana alizaliwa kwa kusubiri Ahadi ya Mungu, sawa tu na tukio la kuzaliwa kwa Ishmael na baadaye Isaka, Ishmael Alizaliwa kwa mapenzi ya mwili wakati Isaka alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ona

 Mwanzo 16:1-4 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.”     Kwa hiyo tunaweza kuona mtoto wa Kwanza wa Abraham anazaliwa kutokana na jitihada za kibinadamu yaani kwa mapenzi ya mwili na kwa mwanamke aliyekuwa mtumwa (Kijakazi)  Na mtoto wa pili alizaliwa kwa uvumilivu na subira kwa kusubiri ahadi ya Mungu na kupitia mwanamke aliyekuwa mtawala (Huru) Mwanzo 21:1-4 “BWANA akamjia Sara kama alivyonena, na BWANA akamfanyia kama alivyosema. Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia. Ibrahimu akamtahiri Isaka mwanawe, alipokuwa mwenye siku nane, kama Mungu alivyomwamuru.

Hawa wote ni watoto wa Ibrahimu, mmoja alizaliwa kutokana na mawazo na mipango ya kibinadamu na mwingine alizaliwa kwa kusubiria ahadi ya Mungu, Paulo anajaribu kuunganisha swala hili na hali halisi waliyokuwa wanaipitia Makanisa ya Galatia, taabu kubwa waliyokuwa wanaipitia ni Mateso pamoja na Mafundisho potofu ya wayahudi yanayowataka waishike sheria ya Musa huku wakiwa wamemuamini Yesu Kristo ambaye tayari alikuwa amekwisha kuwaokoa na laana ya torati, Kitendo cha aalimu hawa wa kiyahudii kulisumbua kanisa alikifananisha na Ishamael kumdhihaki Isaka, Ishmael akiwa ni mtoto wa mjakazi na Isaka akiwa ni mtoto wa Muungwana, dhihaka hii haikuweza kuvumilika kiasi ambacho Sara alitoa wazo la mjakazi na mtoto wake kufukuzwa kabisa kwani wangemuharibu kabisa Isaka kutokana na ushawishi wao wa kifisadi

Mwanzo 21:8-12 “Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya. Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka. Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka. Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe. Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.”

Unaweza kuwa na swali moyoni ambalo hata mimi nilikuwa nalo, kwamba ni aina gani ya dhihaka ilikuwa inafanyika tena siku ya sherehe hata kumuuzi Sara na kuamuru kuwa mtoto huyo afukuzwe pamoja na mama yake?  Kwa mujibu wa Marabi wa kiyahudi ni kuwa kijana huyu alikuwa na miaka kama 14 hivi na tayari alikuwa ameshaonyesha kutokuishi sawa na njia ya baba yake, na kwamba kulikuweko na dalili nyingi za kukiuka sheria za Mungu ambazo hata Abrahamu alikuwa anazishika, Sara alikuwa amebaini hilo kwa uwazi kuliko Abrahamu, Sara aliona kuwa kuna hatari mtoto wa ahadi akasawishika kufuata njia za kaka yake ambaye kwa siri wayahudi wanaeleza kuwa alikuwa akionekana anaabudu miungu ya mama yake na kushindana na kijana mdogo wa Ibrahimu. Neno dhihaka kwa waebrania linasomeka kama TSACHAQ  kufanya dhihaka katika mambo muhimu na ya msingi, neno hili pia huumika kumaanisha watu wasiomcha Mungu au wenye kupuuzia njia za Mungu. Unaweza kuliona katika zaburi na maandiko mengine ya kiyahudi;-

Zaburi 1:1-2 “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.”

Wakati Abraham na watu wake wanafanya karamu ya kumshukuru Mungu Ishamel yeye alikuwa anadhihaki kwa msingi huo kama tungekuwepo kwenye tafrija ile tungebaini kuwa watu wako makini katika kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyomfanyia Sara na Abraham na kundi la Hajiri  na mwanaye wanapuuzia na kucheka au kuona kinachofanyika ni upuuzi tu na hawajali kile Mungu alichokifanya wala hawaoni kuwa ni jambo kubwa.  Sara aliona hilo na kubaini kuwa kijana huyu na mama yake hawana budi kutimuliwa kwani hawangeweza kuishi pamoja, wala kurithi pamoja na Isaka Mwanzo 21:10 “Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.”

Paulo anautumia mfano huo sasa kulifundisha kanisa kuhusu mateso yanayofanywa na wale wanaolitesa kanisa kwa Mateso na mafundisho yasiyo sahihi ambayo yanalitesa Kanisa Kama Ishamel alivyokuwa akimdhihaki Isaka waalimu wa uongo walikuwa wakilitesa kanisa kwa kufundisha kuwa watu wanaweza kukubaliwa na Mungu kwa sababu ya bidii ya mwilini, wakati kuzaliwa kwa Isaka kulitokana na Mungu kuitimiza ahadi yake na sio juhudi za kibinadamu, Jamii kubwa ya wayahudi hata pamoja na kuiamini injili waligeuka kubwa mwiba mkubwa wa mateso katika kanisa na mafundisho yasiyo sahihi  aidha wakati wote walihakikisha kuwa wanapingana na injili na kuwaudhi wahubiri wa injili ona

Matendo 13:48-51 “Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote. Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung'utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio.”

Matendo 17:5-9 “Na Wayahudi wakaona wivu, wakajitwalia watu kadha wa kadha katika watu ovyo wasio na sifa njema, nao wakakutanisha mkutano, wakafanya ghasia mjini, wakawaendea watu wa nyumba ya Yasoni, wakataka kuwapeleka mbele ya watu wa mji; na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, na Yasoni amewakaribisha; na hawa wote wanatenda mambo yaliyo kinyume cha amri za Kaisari, wakisema na kwamba yupo mfalme mwingine, aitwaye Yesu. Wakafadhaisha ule mkutano na wakubwa wa mji walipoyasikia hayo. Nao walipokwisha kumtoza dhamana Yasoni na wenziwe wakawaacha waende zao.”

Matendo 17: 13 “Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipopata habari ya kwamba neno la Mungu linahubiriwa na Paulo hata katika Beroya, wakaenda huko nako wakawachafua na kuwafadhaisha makutano.”

Unaweza kuona kuwa kanisa sio tu lilikuwa linapitia mateso ya kawaida na upinzani dhidi ya injili lakini pia lilipingwa kwa mafundisho yasiyo sahihi Na kanisa la Galatia lilikuwa ni moja ya kanisa lililoathiriwa na mafundishi hayo

Wagalatia 3:1-9 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili? Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli. Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani

Wakristo ni watoto wa Mungu kwa njia  imani na ahadi inayotenda kazi kupitia uwezo wa Roho Mtakatifu, na kwamba tunapokea wokovu kwa neema na si kwa juhudi wala kwa matendo ili awaye yote asijisifu:-

Waefeso 2:4-9 “Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.”

Katika imani ye Kikristo tunapata kila tunachokipata kwa neema na sio kwa matendo au bidii za kibinadamu hii iko katika kaisha ya kawaida na katika maisha ya wito wa kumtumikia Mungu hakuna juhudi wala matakwa ya kibinadamu bali ya Mungu

Warumi 9:14-15 “Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.”

Hata Mungu anapoita watu katika utumishi huu anawaita watu kwa neema yake na sio kwa kujipendekeza au kwa kujidhani ya kuwa ninafaa, wako watu wanaweza kujidhania kuwa wanafaa kuwa watumishi wa Mungu na wengine hawafai, au mtu akajikinai akifikiri yeye ni zaidi ya mwingine jambo la namna hii pia liko kinyume na ile dhana ya kiungu, Mungunhuchagua vile tunavyovidhania kuwa havifai, kumbuka lililotyukuka kwa mwanadamu ni chukizo kwa Mungu!

1Wakoritho 1:26-29 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.”  

Tunawezaje kujua kuwa hawa ni wana wa Muungwana na hawa ni wana wa kijakazi? Maandiko yanaeleza wazi kuwa wana wa muungwana walizaliwa kwa ahadi na wana wa kijakazi walizaliwa kwa mapenzi ya mwili na hivyo tunaweza kuwatambua kwa matendo yao, wale waliokuwa wakiliudhi kanisa na kulitesa ndio wana wa kijakazi na wale waliowapole na waungwana Paulo ana sema

Wagalatia 4:29 “Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa

Wana wa kijakzi ni wale waliozaliwa kwa mwili na wana wa muungwana ni wale waliozaliwa kwa ahadi na uweza wa Roho Mtakatifu na matunda yao unaweza unaweza kuwatambua

Wagalatia 5:19-21 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”

Wagalatia 5:22-24 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake

-          Wana wa mjakazi hawashindwi kuua  mtu, mioyo yao imejawa na chuki na uchungu ni wakatili na hawana huruma ona Mwanzo 4:1-11 “Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA. Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.     Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA. Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua. BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.”

 

-          Hawaishi kuwa na Makundi wala Mafarakano  1Wakoritho 3:1-9 “Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe.Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.

 

-          Wanaweza kupelekana hata mahakamani  wala kudhulumiana 1Wakorintho 6:1-10 “ Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake? Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini. Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali zenu? Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.”

Unapoangalia kwa kina na upana na urefu, watu wenye matendo haya ya mwilini wanaweza kuwapo hata makanisani katika siku za leo,  na wanaweza kuwa na muda mrefu sana katika wokovu au hata kufikia ngazi Fulani ya kiroho lakini maandiko yanasema mtawatambua kwa matunda yao, kuwajua wana wa muungwa na wana wa kijakazi kwa mujibu wa maandiko ni rahisi sana kila mmoja anapaswa kujihoji na kujichunguza kama ni mwana wa Muuungwana au ni mwana wa kijakazi na kama ni wa kijakazi au kuna tabia ya kijakazi hatuna budi kutubu na kubadilika , tuongeweze neema

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!