Jumatatu, 15 Mei 2017

Je Hapana Zeri Katika Gileadi? (Zeri ya Gilead)

Mstari wa Msingi: Yeremia 8: 22 “Je Hapana Zeri katika Gilead? Huko Hakuna tabibu? Mbona basi haijarejea afya ya Binti ya watu wangu?

 Mmea aina ya zeri kama unavyoonekana katika Picha

Ni muhimu kufahamu kwamba hapa duniani hakuna jambo lolote Gumu lisilo na majibu, kila jambo na kila tatizo lina majibu yake na ufumbuzi wake, Magonjwa hali kadhalika yanaweza kutibiwa kwa tiba za aina mbali mbali, Mungu aliwapa wanadamu mimea ambayo ndani yake aliweka nguvu za uponyaji kwaajili ya matibabu ya aina mbali mbali.

Nyakati za Biblia watu walitumia pia madawa yatokanayo na mimea kutibu magonjwa na mateso ya aina mbalimbali, kulikuwa na miti mingi sana iliyotumika kama tiba, kabla ya kuanza kutumia zaidi kemikali ambazo nyingi zina uharibifu mkubwa katika mwili wa wanadamu na hivyo kuchangia udhaifu mkubwa wa aina binadamu walioko leo juu ya uso wa nchi. Moja ya miti maarufu sana iliyotumika kwa tiba katika Israel na mashariki ya kati ulikuwa ni mmea ujulikanao kama Zeri ambao ulikuwa unapatikana kanaani na katika mji wa Gilead.

Zeri ni nini hasa?

Zeri kwa kiingereza (BALM) ulikuwa ni mmea ambao ulikuwa maarufu sana nyakati za Biblia mmea huu ulipatikana katika nchi ya milimamilima iliyokuwa nga’mbo ya Jordan iliyojulikana kama milima ya Gilead, mmea huu uliuzwa kwa bei kubwa sana na wafanya biashara wa zamani waliokuwa matajiri walitajirika kwa kuuza zeri, 

Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na ZERI na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri.” 

Unaweza kuona aidha katika nyakati za Biblia kama mtu anakupenda sana na kukuheshimu sana moja ya zawadi ya ngazi ya juu kabisa ambayo mtu anageweza kukupatia ilikuwa ni pamoja na ZERI angalia
Mwanzo 43:11 “Israeli, baba yao, akawaambia, Kama ndivyo, fanyeni hivi; twaeni tunu za nchi katika vyombo vyenu, mkamchukulie mtu huyo zawadi, ZERI kidogo, na asali kidogo, ubani, na manemane, na jozi, na lozi”.

Kwa nini Zeri ilikuwa bidhaa ya thamani na zawadi kubwa sana, Zeri ilikuwa na sifa ya kuponya majeraha yote ya mwili “recovering” na vidonda mbalimbali pia vikiwemo vidonda vya kuumwa na nyoka, aidha watu pia waliitumia zeri katika kuhifadhia mwili wa mwanadamu aliyekufa usioze, Hivyo kama dawa nyingine zote zingeshindwa kutibu jeraha la mtu ndipo sasa ili kuokoa maisha yake ilipaswa kuitafuta Zeri kwa vile hii ilijulikana kama dawa isiyoshindwa hata hivyo dawa hii ilikuwa ghali sana ingekugharimu kuuza vyote ulivyo navyo ili kutibiwa na wataalamu wa Gilead upate kupona. Dawa hii likuwa haishindwi kutibu jambo kama mtu anetibiwa na dawa zote na ikashindikana watu walimshauri aende Gilead kwa wataalamu kataumie Zer.

Yeremia 46:11Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.” 

Ni wazi kuwa kama mtu angetumia dawa bila mafanikio dawa ya mwisho ingekuwa Zeri ni zeri tu ndiyo ambayo ingeweza kutibu maumivu aliyoyapata mtu".

Yeremia 51:8Babeli umeanguka na kuangamia ghafula; mpigieni yowe; twaeni zeri kwa maumivu yake; ili labda apate kuponywa

Katika namna ya kushangaza sana hata hivyo yalikuweko magonjwa ambayo yalikuwa ahayasikii dawa yaani magonjwa sugu, ilipotokea kuwa mgonjwa haonyeshi badiliko, kila mara alionekana yuko vilevile hapati kugangwa lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kusikia Zeri imeshindwa au wataalamu wa Gilead wameshindwa, katika mstari wa Msingi Yeremia alikuwa anazungumzia tatizo la kiroho na tabia ya wana wa Israel ambao walishindwa kutubu na kubadilika kiasi cha kufikia ngazi ya kuhukumiwa na Mungu, Nabii alikuwa akiomboleza na kujiuliza kuwa dawa isiyoshindwa imekosekana? Matabibu wa Gilead hawako, Yeremia alikuwa anamaanisha kuweko kwa toba na manabii, Israel walishindwa kuwasikiliza manabii na pia walikosa moyo wa toba nJe hapana zeri katika Gilead? Na Matabibu maana naona afya ya watu wangu haijarejea?

Kimsingi zeri ya Gilead ilikuwa ghali sana na hata hivyo haikuweza kuponya majeraha mengine yaliyowasibu watu.

Marko 5:25-28Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya, aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona

Zeri ulikuwa ni mti halisi lakini vilevile ulikuwa ni picha ya Yesu Kristo, katika muujiza huu alioufanya Yesu ni dhahiri biblia inatuonyesha zeri kutoka mbinguni, inatuonyesha mwanaume mwenye uwezo wa kumfanya mtu akawa recovered akapona akawa kamili, unaweza kuhangaika huko na kule kwaajili ya mahitaji yako, kwaajili ya afya yako ya kimwili na kiroho, kwaajili ya majeraha ya moyo wako, kwaajili ya majeraha ya adui zako, kwaajili ya majeraha ya ndoa na kazini na shuleni na hata kanisani, unaweza kuangaika huku na kule kwaajili ya mahitaji yako ya aina mbalimbali lakini lao ninakutangazia kuwa iko dawa isiyoshindwa Dawa hii ni Yesu Kristo peke yake yeye anaweza yote kwake hakuna linaloshindikana ni dawa ya waliokata tamaa, dawa ya waliojeruhiwa na kudharaulika, ni dawa ya maisha yetu, feature yetu haiku mikononi mwa wanadamu, iko mikononi mwa Yesu tu, huyu ndio wa kumkimbilia, huyu ndio wa kumpapatikia, huyu ndio wa kumtazama kwa kila unalokaboliana nalo katika maisha katika masomo, katika ndoa, kazini nk. Mwangalie Yesu na utafanikiwa yeye ni zaidi ya zeri ya Gilead ni Zawadi ya upendo wa hali ya juu kutoka kwa Mungu baba 

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa Pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.

Na. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima

Ijumaa, 5 Mei 2017

Kama Mlivyonena Ndivyo nitakavyowafanyia!


Katika maandiko haya,(HESABU 13:25-33; 14:1-12,26-32),

Hesabu 14:26-32 “Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,  Je! Nichukuane na mkutano mwovu huu uninung'unikiao hata lini? Nimesikia manung'uniko ya wana wa Israeli, waninung'unikiayo.  Waambieni, Kama niishivyo, asema Bwana, hakika yangu kama ninyi mlivyonena masikioni mwangu, ndivyo nitakavyowafanyia ninyi;”

Hesabu 13:25-33 “Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini. . Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.  Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake.  Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko.  Amaleki anakaa katika nchi ya Negebu; na Mhiti, na Myebusi, na Mwamori wanakaa katika milima, na Mkanaani anakaa karibu na bahari; na kando ya ukingo wa Yordani.  Kalebu akawatuliza watu mbele ya Musa, akasema, Na tupande mara, tukaitamalaki; maana twaweza kushinda bila shaka. Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.    Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.  Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.”

Hesabu 14:1-12 “1. Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri? Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli.  Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.  Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope. Lakini mkutano wote wakaamuru wapigwe kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika hema ya kukutania, mbele ya wana wa Israeli wote. Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao.  Nitawapiga kwa tauni, na kuwaondolea urithi wao, nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, kisha yenye nguvu kuliko wao.  


Utangulizi:
Ni muhimu kufahamu kuwa ulimi wa Mwanadamu una nguvu ya kusababisha madhara makubwa na pia kuleta uponyaji mkubwa, kwa kuwa wanadamu wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, Mungu aliuumba ulimwengu kwa Neno tu alitamka na ikawa, wakati wote utendaji wetu na matukio yetu katika maisha yanatokana nay ale tunayoyazungumza Mithali 18:20-21Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”Kama hivi ndivyo ni jambo la msingi sana kujichunga ni kitu gani tunakizungumza na kukitamka kwa vile tunaweza kuumba jambo hilo.

Kumbuka hata wokovu wetu unapatikana kwa kumuamini Yesu moyoni na kwa kumkiri kwa kinywa na ni kwa kinywa tu tunaweza kuliitia jina la Bwana na kupata msaada Warumi 10:9-13  Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.  Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.  Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.

Kwa msingi huo kama tunataka kuwa mbali na mauti na kama tunataka kuleta uzima katika maisha yetu ni lazima tuwe na semi zilizo na manufaa katika maisha yetu na hata ya wengine

Jambo la kujifunza:
Wana wa Israeli wanatumia ulimi kuzungumza maneno kama haya "AHERI TUNGALIKUFA KATIKA JANGWA HILI" na maneno kama "HATUWEZI".Mungu akasema atawafanyia hivyo walivyosema na kweli walikufa katika jangwa hilo.

Kalebu Mwana wa Yefune na Yoshua Mwana wa Nuni walisema maneno ya ushindi kama haya "TWAWEZA KUSHINDA BILA SHAKA na BWANA YU PAMOJA NASI".

Tunajifunza juu ya makundi mawili.Kundi la kwanza ambao ndio wengi wanazungumza maneno HASI NA YA KUSHINDWA na kweli walishindwa.

Kundi la pili ambao ni wachache sana wanazungumza maneno ya CHANYA YA KUSHINDA na kweli walishinda na kuingia nchi ya ahadi.

Watu wa Mungu ikiwa Mungu anatufanyia jambo sawa na ukiri wetu, ikiwa uzima na mauti uko katika uwezo wa ulimi wetu, ikiwa kwa ulimi tunaweza kukiri na hata kupata wokovu ni muhimu kwetu ,KWA KILA JAMBO TUZUNGUMZE MANENO CHANYA  YA KUSHINDA sawasawa na Neno la Mungu,NA BWANA mwenye kutushindia atakuwa pamoja nasi kufanikisha yote kiroho na kimwili.

MANENO TUNAYOSEMA NDIYO BWANA ANAYOTUFANYIA YAWE MEMA AU MABAYA!Maana anasema CHAGUENI HIVI LEO!(YOSHUA 24:14-15;WAFILIPI 2:13;WARUMI 8:31-32,37-39;WAFILIPI 4:13).Mungu aweke mlinzi vinywani mwetu ili sikuzote tuzungumze maneno ya kuumba ushindi katika Jina la Yesu Kristo.(ZABURI 141:1-3)

Ni imani yangu kuwa Tangu sasa utatumia kinywa chako vema na kujizungumzia ushindi, acha kujizungumzia kukata tamaa, jizungumzie mambo mema wazungumzie wengine mema  Na mungu atatubariki sawasawa na ukiri wetu.

Sources. Rev.George Swenya Full Gospel Bible Fellowship Church Tanga.

Ukarabati: Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima