Jumanne, 29 Machi 2022

Mbweha wadogo waiharibuo mizabibu


Wimbo uliobora 2:15 “Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.”


Utangulizi:

Kitabu cha wimbo uliobora ni mojawapo ya kitabu katika vitabu vijulikanavyo kama vitabu vya mashairi, vitabu vingine ni pamoja na Ayubu, Zaburi, Mithali, Muhubiri na kitabu hiki cha wimbo ulio bora, Katika vitabu hivi kuna mafunzo mengi sana ya hekima kuhusu maisha, na kwa kuwa ni vitabu vya mashairi wakati mwingine unaweza kukutana na lugha au misemo yenye kushangaza lakini yenye mafunzo muhimu sana kwa jamii!, kitabu cha wimbo ulio bora hata hivyo mashairi yake ni mashairi ya kimapenzi na ni mtu na mpenzi wake waliokuwa wakiimbiana na kujibizana, katikati ya mahaba yao wakaambiana maneno haya Wimbo Ulio Bora 2:15 “Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.” Kimsingi lugha hii ni lugha ya kimashairi na inatufunza mamswala ya msingi katika Nyanja nyingi za maisha katika maeneo mbalimbali, Wafasiri wengi wa maandiko na wanatheolojia wanakiri kuwa mahusiano haya ya kimapenzi yalikuwa ni kati ya kijana wa kifalme Suleimani na mwanamke Mshulami, hata hivyo kitheolojia wimbo huu unahusu vilevile mahusiano yaliyoko kati ya Yesu na Kanisa lake. Tunajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo:- 

1.       Mbweha wadogo waiharibuo mizabibu!

2.       Maana ya mbweha wadogo waiharibuo Mizabibu


Mbweha wadogo waiharibuo mizabibu!

Nyakati za Biblia katika Isarael hasa kutokana na geographia ya nchi ya Kanaani au Israel Mbweha walijulikana kama wanyama wadogo waharibifu, hususani kwa sababu wao walijihusisha na kilimo ikiwemo kilimo cha mizabibu, Na wanyama hawa walikuwa miongoni mwa wanyama waharibifu kwa mizabibu hususani pale inapoanza kutoa maua au kuchanua !, inawezekana kuwa wako wanyama wengi wakubwa zaidi na waharibifu, kama ilivyo Afirka tembo wanaweza kuingia kwenye mashamba ya watu na wakafanya uharibifu mkubwa kwa dakika chache, Mashariki ya kati mashamba ya mizabizu yalikuwa yakizungushiwa wigo wa mawe ili kuyalinda na wanyama waharibifu na hivyo yalikuwa salama, ona

Marko 12:1-2 “Akaanza kusema nao kwa mifano; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akazungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. Hata kwa wakati wake akatuma mtumwa kwa wale wakulima, ili apokee kwa wakulima katika matunda ya mizabibu”.  

Lakini huenda hata hivyo Mbeha ndio walikuwa adui wakubwa wa mizabibu na labda zaidi sana wakati yakichanua maua. Lakini hata hivyo watu wengi waliwadharau mbweha kama wanayama wasi hatarishi sana, ukilinganisha na wengine, Kimsingi unapoiangali Biblia inaweza kumaanisha kuwa Mbweha alitumika pia au kuhesabiika miongoni mwa wanyama wanaoweza kutumika kwa uharibifu  na hivyo pamoja na kujilinda dhidi ya wanyama wengine wakubwa na waharibifu wakulima wa mizabibu hawakupaswa kabisa kuwadharau mbweha kwani nao wanachangia uharibifu hata kama watacheza cheza kwenye mashamba ya zabibu na kuangusha maua ambayo ndio asili ya kupata matunda, Ki biblia Mbweha ni mnyama aliyetumika kuonyesha hali ya uharibifu mfano Samsoni aliwatumia Mbweha kuchoma mashamba ya ngano ya wafililisti

Waamuzi 15:3-5 “Samsoni akasema, Safari hii nitakuwa sina hatia katika habari za hawa Wafilisti, hapo nitakapowadhuru. Samsoni akaenda akakamata mbweha mia tatu; kisha akatwaa vienge vya moto akawafunga mbweha mkia kwa mkia, akatia kienge kati ya kila mikia miwili. Alipokwisha kuviwasha moto vile vienge, akawaachia mbweha kati ya ngano ya Wafilisti, akayateketeza matita, na ngano, hata na mashamba ya mizeituni.”

Pia mbweha walitumika kama ishara ya dharau kubwa sana, kama kitu kilikuwa cha uongo, au chenye viwango vya chini sana au mtu mwoga kupita kawaida au chenya kuzuia mapenzi ya Mungu kilichodharaulika mno kama manabii wa uongo, au ujenzi ulio chini ya kiwango, au mtu mwoga kuliko kawaida manabii na watu wa nyakati za biblia walilitumia neno mbweha kwa kitu kilicho dharaulika mfano ona

Nehemia 4:1-5 “Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba tulikuwa tukiujenga ukuta, akaghadhibika, akaingiwa na uchungu sana, akawadhihaki Wayahudi. Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto? Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema, Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe. Sikia, Ee Mungu wetu; maana tunadharauliwa; ukawarudishie mashutumu yao juu ya vichwa vyao, ukawatoe watekwe katika nchi ya uhamisho; wala usiusitiri uovu wao, wala isifutwe dhambi yao, mbele zako; kwa maana wamekukasirisha mbele ya hao wanaojenga.”

Ezekiel 13:1-4 “Kisha neno la BWANA likanijia, kusema, Mwanadamu, tabiri juu ya manabii wa Israeli wanaotabiri, uwaambie wanaotabiri kwa mioyo yao wenyewe, Lisikieni neno la BWANA; Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao manabii wajinga, wanaoifuata roho yao wenyewe, wala hawakuona neno lo lote!Ee Israeli, manabii wako wamekuwa kama mbweha, mahali palipo ukiwa.”

Luka 13:31-33 “Saa ile ile Mafarisayo kadha wa kadha walimwendea, wakamwambia, Toka hapa, uende mahali pengine, kwa sababu Herode anataka kukuua. Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika. Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.”              

Kwa hiyo suleimani na mpenzi wake walipokuwa wakiimbiana wimbo wa mapenzi na kuona kuwa penzi lao limechanua waliimbina na kupeana tahadhari kuwa watajilinda na maadui wakubwa wa mapenzi yao lakini fvilevile wasidharau maadui wadogo ambao nao wanaweza kuathiri pezni lao lisiweze kuzaa marunda, Maadui wakubwa wa mapenzi walifanannishwa na wanyama wakubwa huko Misri maadui wakubwa wa mapenzi walifananishwa na mamba, na Israel maadui wadogowadogo wa mapenzi walifananishwa na mbwea, kwa hiyo katika wimbo wao wa kimapenzi Suleimani hakutaka hata vitu vidogovidogo vinavyodhauliwa na watu,  wengi kwao visiharibu mapenzi yao kwa gharama yoyote wala viziwe tishio la mapenzi yao,  ili mahusiano yaweze kuwa imara kuna vitu vidogo vidogo vingi ambavyo havipaswi kupuuziwa, kwani vikipuuzwa navyo vinaweza kufifisha upendo, na vinaweza kuwa hatari sana hivyo wapendanao lazima wahakikishe kuwa wanajilinda dhidi ya maadui wakubwa na wale wadogowadogo ili kutunza mahusiano mema katika upendo wao,  Upendo haulindwi na kumnunulia mtu nguo pekee, au kumnunulia chakula, au kumtunza, au kumzalisha, au kumpa fedha ya saloon, au kumuachia fedha mezani, au kufanya kazi kwa bidii ili uitunze familia yako, au kushughulika sana katika tendo la ndoa au kumpa mumeo au mkeo kila siku, kuna vitu vidogovidogo sana ambavyo vinaweza kumfanya mwenzi wako ajisikie yuko peponi, leo hii watu wanagombana sana, hawasameheani, kila mmoja na simu yake, hakuna kupokeana, hakuna mazungumzo na vitu vingi ambavyo ni vya muhimu katika kujenga uhusiano hata hivyo kumbuka sitaki kuzungumzia mapenzi katika somo langu hili mimi nazungumzia maswala ya rohoni

Maana ya mbweha wadogo waiharibuo Mizabibu

Ni muhimu kufahamu kama tulivyosema awali kuwa Mbweha sio wanyama wakubwa sana wanaoweza kusababisha uharibifu mkubwa kama tembo au dubu na kadhalika, mbweha wana urefu wa inchi kama 20 na uzito kama wa kilo nane hivi, lakini tatizo lao kubwa ni kuwa wana uwezo wa kuharibu maua lakini pia kutafuna na kusababisha mzabibu kukauka na ukakosa matunda na ndio maana nyakati za Biblia licha ya kuwadharau mbweha lakini pia walikuwa na kampeni ya kuwakamata na kuwaua kabisa kutokana na uwezo wao mkubwa wa kusababisha uharibifu

Wimbo Ulio Bora 2:15 “Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.”

Jambo kubwa analolizungumza Suleimani hapa ni kuwa mapenzi yake na Mshulami ndio yanaanza kuchanua hivyo anatoa tahadhari kwa maswala ambayo kimsingi ynaweza kuleta uharibifu mkubwa katika mahusiano  yawe ya kimapenzi yawe na watu au na Mungu, watu wengi sana wanaompokea Yesu wanaweza kuwashinda maadui wakubwa wanaoonekana kwa nje wanaweza kuwa sio waizi, wanaweza kuwa sio wazinzi, wanaweza kuwa sio walevi, wanaweza kuwa hawaviti sigara, wanaweza kuwa sio wasengenyaji, wala sio wafitini, wala sio wachonganishi, wanaweza kuwa sio wenye tamaa ya fedha lakini kuna vitu ambavyo watu wengi wanavidharau, Maswala ambayo yanaharibu maisha yetu, na kuharibu ndoa zetu, yanayoharibu ushuhuda wetu, au yanayotutia gizani, yanayoharbu mahisiano wakati mwingine sio yale yanayoonekana kwa macho wakati mwingine ni yale yaliyoko mioyoni mwetu

1.       Ubinafsi -  wanadamu wengi sana wanasumbuliwa na ubinafsi, wanataka kujitukuza wenyewe, wanataka wao wenyewe ndio wabaki juu, wajitumikie wenyewe wajifurahishe wenyewe na wawe juu yaw engine tu  Biblia inaonyesha kuwa ni watu wachache sana ambao huangalia mambo ya wengine lakini wengi sana huangalia maslahi yao

 

2Timotheo 3:2-4 “Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;”

 

Kujipenda mwenyewe ni moja ya dhambi ambayo inaweza kuonekana kuwa ni ndogo lakini inaweza kusababisha madhara makubwa sana katika ndoa, familia na hata taifa au kanisa ni rahisi kufikiri kuwa ubinafsi sio tatizo lakini ni tatizo kubwa sana ambalo kwa hili wengi watakosa nafasi ya kuingia mbinguni hii ni ile hali ya mimi kwanza, mtu anaweza kuwa sio mzinzi, wala mlevi wala mwizo lakini akawa ni mbinafsi kuliko kawaida mchoyo anataka afanikiwe yeye tu

 

Luka 18:18-25 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele? Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu. Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako. Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu. Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate. Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi. Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu! Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”

 

Tatizo kubwa la huyu tajiri ilikuwa iko dhambi ya choyo na umimi na ubinafsi ambayo yeye aliiona kama sio tatizo kubwa kwa sababu ameshika mari zote lakini kumbe alikuwa na mbweha anayeharibu mzabibu wake ambayo ni choyo na umimi na ubinafsi mkubwa kujikana nafsi sio jambo jepesi

 

Mathayo 16:24-26 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

 

Ubinafsi umeharibu maisha ya watu wengi duniani umeharibu mahusiano ya watu, umeharibu ndoa, umeharibu na kusababisha vita, mafarakano na migawanyiko mikubwa katika jamii, imeleta misiba mikubwa na hata vifo kwa sababu ya ubinafsi tu japo linaonekana ni jambo dogo

 

2.       Uchungu:

Watu wengi sana wanadhani ni haki wao kuwa na uchungu na hawaoni kuwa kuwa na uchungu ni dhambi inaonekana ndogo lakini ina madhara makubwa, kwa sababu ya uchungu na hofu mtu anajikuta akakosoa tu kila kitu au anakosoa mtu, linaweza lisiwe tatizo kubwa lakini biblia imaonya kwamba ni shina ambalo likiwemo ndani ya mtu linaweza kuleta madhara makubwa kwa jamii

 

Waebrania 12:14-15 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.”

               

3.       Kutokusamehe:

 

Kusamehe ni swala la kutangaza msamaha kwa mtu mwingine, bila kujali amakukosea nini katika maandiko kibiblia msamaha wa Mungu unahusiana na dhambi zetu lakini ili tusamehewe na Mungu sharti lake ni kuwa lazima tuwasamehe wengine  kutokuwasamehe wengine kunakuweka katika magereza ngumu ya kukufanya nawe usisamehewe na Mungu

 

Mathayo 18:21-35 “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini. Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi. Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni. Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho. Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni. Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi; nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe? Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote. Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.

 

Sio rahisi kusamehe lakini inahitajika neema ya Mungu, kuachia makosa ya aina mbalimbali ambayo tumetendewa na wenzetu watu wengi sana wanafikiri kuwa wa haki ya kutokusamehe wakidhani kuwa kununa kwao na kukasirika kwao ni halali kwa Mungu, lakini ni ukweli ulio wazi kuwa mtu asiposamehe anaharibu kabisa maombi mfano katika sala ya Bwana

 

Mathayo 6: 12. “Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.” Watu wengi kwaajili ya kutokusamehe wamepoteza kwa Mungu na wanadamu.

 

4.       Hasira

Hasira ni mojawapo ya udhaifu ambao watu wengi wanafikiri ni sifa kuwa nazo kumbe ni moja ya tabia mbaya sana, Mtu anayeweza kujizuia asikasirike ni mtu mwenye nguvu sana kuliko anayekasirika hovyo maandiko yanatuagiza kuwa tusiache jua likachwa kabla hatujaondoa hasira vifuani mwetu  andiko hili halitii moyo kuwa na hasira lakini linatia moyo kuhakikisha kuwa tunafanya mapatano na wale tuliowakosea kwa sababu ya hasira zetu kabla jua halijachwa  na kama tutashindwa kufanya hayo mapema tunampa shetani nafasi ya kupanda mbegu ya uchungu ambayo itakuwa na kuathiri wenguine

 

Waefeso 4:26-27 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.

 

Maandiko yanataka tuweke mbali na kuzifisha kabisa dhambi mbalimbali kubwa na nyinginezo tunazozidharau ikiwepo hasira na ghadhabu

 

Wakolosai 3:5-8 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu. Katika hayo ninyi nanyi mlitembea zamani, mlipoishi katika hayo. Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu

 

Ni hasira iliyomfanya Musa na Haruni kukataliwa na Mungu kuingia katika inchi ya mkanaani 


Hesabu 20:12 “Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa.”Hasira za Musa zikamfanya azungumze na kutenda mambo yasiyopasa ona 


Zaburi 106:32-33. “Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao, Kwa sababu waliiasi roho yake, Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.”Kutokana na kujaa ghadhabu Nabii Musa alimkosea Mungu na kupata hasara kwa kuzungumza na kutenda yasiyofaa watu wengi sana wamepata hasara kwa sababu ya hasira zilizowapelekea kutenda na kunena yasiyofaa hao ni mbweha wadogo wanaoharibu mizabibu

 

5.       Wivu.

 

Ni hali ya kutokujisikia vizuri kwa sababu ya mafanikio ya mtu mwingine, ubora wake, mafanikio yake na kibali chake au bahati yake wako watu wanaumia sana wanapoona wengine wamefanikiwa, wameolewa wao hawajaolewa, wamefanikiwa wao bado, wamefaulu wao wamefeli, wanakibali wao hawana, wanakubaliwa na Mungu wao hawana kitu na wanajisikia vibaya kiasi cha kukasirika kukosoa na hata kubeza ana wakati mwingine hata kuua kwa sababu ya wivu wenye uchungu ona

 

Mwanzo 4:3-5 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA. Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.”

 

Hali kama hii ilimtokea pia kaka mkubwa katika Mfano ule wa mwana mpotevu pale alipoona ndugu yake aliyepotea na akarudi japo alichukua mali za baba yake kama sehemu ya urithi unaomuangukia akaenda kuzitapanya na makahaba aliporejea baba yake alimpokea kwa furaha lakini kaka mkubwa aliposikia alisusa na kulaumu maamuzi ya baba yake

 

Luka 15:11-32 “Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati. Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia. Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi. Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;  lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona. Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako. Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.”

 

Wako watu wana wivu wa ajabu sana kwa sababu wanachukizwa na neema ya Mungu iliyojuu yako hata wanaposikia umekosea wanatamani kama Mungu angekuua au kukutupilia mbali jehanamu ya moto, hawataki kabisa kuona Mungu amekurehemu na anaendelea kukubariki hii ni tabia mbaya sana na hawa ni mbweha waharibuo mzabimu, Bwana ampe neema kila mmoja kuwa mbali na wivu wenye uchungu katika jina la Yesu.

 

6.       Unafiki.

 

Watu wengi sana ni wanafiki, unafiki ni tabia ya kuigiza pretending Mungu hapandezwi na unafiki, kujipendekeza na kutaka sifa ili hali moyo wako uko mbali naye au na mapenzi yake 


Mathayo 15:7-9 “ Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.” 


Unafiki ni dhambi inayooenakana kuwa ni ya kawaida sana kwa watu wengi wanaodai kuwa wanamcha Mungu, bila kujua kuwa Mungu anachukizwa na jambo hili na Mungu alimuadhibu vikali Anania na mkewe kwa sababu ya dhambi ya unafiki 


Matendo ya mitume 5:1-10 “Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe, aliuza mali,akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume. Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya. Vijana wakaondoka, wakamtia katika sanda, wakamchukua nje, wakamzika. Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia, naye hana habari ya hayo yaliyotokea. Petro akamjibu, Niambie, Mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? Akasema, Ndiyo, kwa thamani hiyo. Petro akamwambia, Imekuwaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu yao waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe.Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.”

 

Kwa hiyo utaweza kuona dhambi zile tunazazidharau na kuzifikiri kuwa ni ndogo zina athari kubwa sana katika kuharibu uhusiano wetu na Mungu na hivyo nazo Mungu anataka tuzishughulikie

 

7.       Choyo:

 

Maandiko yanatahadharisha sana kuhusu choyo, watu wengi sana ni wachoyo, na watu wengi sana wanapenda kujimilikisha vitu vingi wakifikiri kuwa kwa kuwa na vitu watakuwa na uzima Yesu aktika mafundisho yake alionya kuhusu choyo anasema katika Luka 12:15 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.” Wako watu wana masanduku na nguo zimejaa kwenye begi zao masanduku mengine yamejaa mpaka zipu zimeachia au wanashundilia kwa miguu wakati wa kuyafunga lakini hawagawi Yesu akikolezea mungu mafundisho yake alionya kuwa sisi ni wapitaji tu katika ulimwengu huu na hivyio kujilimbikizia au mpango wa kujilimbikizia hautatufikisha kokote 


Luka 12:16-20 “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.  Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?                


choyo ni moja ya mbweha wadogo na waharibifu, kuna choyo za aina nyingi, moja ya choyo maarufu sana katika mapenzi na inayokera na kuharibu mahusiano ni pamoja na kunyimana tendo la ndoa aina hii ya choyo imeharibu mapenzi sana na watu wengi wameachana kwa sababu wako wanaotumia fursa ya tendo la ndoa kuwekea mgomo na kuesa nafsi za wengine aina hii ya choyo imekemewa vikali katika maandiko 


1Wakoritho 7:1-5 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.”  Neno la  Mungu linatahadharisha pia kuhusiana na jambo hili na ain azote za choyo Bwana na ampe neema kila mmoja wetu kujilinda na choyo za aina mbalimbali ili tuwe na mahusiano imara kwa Mungu na wanadamu        

Athari za kutokukamata mbweha wadogo:-

-          Kunatokea kumzimisha Roho Mtakatifu Wathesalonike 5:19Msimzimishe Roho;”

-          Tunashindwa kuzaa matunda ya Roho Wagalatia 5:19-23 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

-          Tunapoteza furaha Zaburi 51:11-12Usinitenge na uso wako, Wala roho yako mtakatifu usiniondolee. Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.”

-          tunapoteza amani Wafilipi 4:7 “Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”

-          inaharibu uhusiano na Mungu 1Yohana 1:3 “hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.”


-          Tunapoteza ujasiri katika maombi Warumi 8:26Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.”

-          tunakuwa waoga 1Yohana 2:28Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika kuja kwake.”

Dhambi hizo tunazofikiri kuwa sio tatizo katika maisha yetu zinatuletea athari na kuharibu hali yetu ya kiroho na wakati mwingine kuturudisha nyuma na kuharibu uhusiano wetu na Yesu, hatuna budi kuhakikisha tunashughulikia maswala ya ndani tunayofafikiri kuwa ni madogo madogo na kumbe yanaharibu sana uhusiano wetu na Mungu, ukiyajua hayo heri wewe ukiyatenda.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Rev. Innocent Samuel Kamote


Na sisi je tufanye nini?


Luka 3:2-14wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani. Akafika nchi yote iliyo karibu na Yordani, akihubiri ubatizo wa toba liletalo ondoleo la dhambi, kama ilivyoandikwa katika chuo cha maneno ya nabii Isaya; Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake. Kila bonde litajazwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patalainishwa; Na wote wenye mwili watauona wokovu wa Mungu. Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto. Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?  Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo. Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi?  Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa. Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.”

Utangulizi:

Moja ya manabii wa ajabu sana ambao unaweza kujifunza habari zao na ukashangaa ni pamoja na na Nabii Yohana mbatizaji, Huduma yake ya kinabii ilikuwa imejawa na kuwaandaa watu watubu, kwaajili ya kumpokea Masihi, Ni wazi kuwa Masihi kwa namna anavyoelezewa na maandiko ni kiongozi wa ngazi ya juu mno na ambaye sio wa kawaida na hivyo Mungu aliona kuwa hawezi kupokelewa kienyeji bila mioyo ya watu kuandaliwa ili iweze kustahimili ujio wa Masihi, kwa hiyo Mungu katika mpango wake alikusudia kumtuma Yohana Mbatizaji nabii, Hili linadhihirishwa wazi na nabii Isaya miaka 700 kabla ya ujio wa Yesu, alitabiri juu ya ujio wa Yohana mbatizaji na huduma yake ambayo ilikuwa na umuhimu mkubwa sana katika kuandaa mazingira ya kumpokea Yesu Duniani ona:-  

Isaya 40:3-5 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu. Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa; Na utukufu wa Bwana utafunuliwa, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.”

Unaweza kuona umuhimu wa nabii huyu ulikuwa mkubwa mno, kwani alitumwa kuwaandaa watu watubu kabla ya huduma ya masihi kwa kuwa masihi mwenyewe ndio wokovu wa Bwana utakaofunuliwa kwa watu kwa jinsi ya Mwili, Masihi mwenyewe ni utukufu wa Mungu, na kwa sababu watu wangemuona kwa macho yao ya mwili ilikuwa ni muhimu kuandaa mioyo yao ili macho yao yauone wokovu wa Bwana na utukufu utakaofunuliwa kwa watu wote ona:-

Luka 2:25-32 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema; Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako, Uliouweka tayari machoni pa watu wote;Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.”

Kuja kwa Masihi kuliambatana na mahubiri mazito yaliyokuwa yakiwataka watu wawe na toba ya kweli iliyoambatana na kuzaa matunda na kubatizwa ili kudhihirisha kuwa kweli watu wamebadilika na wako tayari kumpokea Masihi, ilikuwa ni lazima jamii iwe na usafi wa moyo na kuwa mioyo yao ilikuwa lazima iwe tayari kwaajili ya Mungu na kwaajili ya wanadamu, Ili Yesu akute na atembelee jamii ilikuwa ni lazima njia isafishwe, palipo na kilima pasawazishwe na kila mahali ambako hakuko sawa sawa ilikuwa ni lazima pawe sawa, kila kikwazo ilikuwa ni lazima kiondolewe ili watu waweze kuishuhudia neema ya Mungu maishani mwao, ilikuwa ni lazima watu wawe mbali na uchungu, waondoe chuki dhidi ya Mungu, na maudhi na kero zote walizokuwa wakiwafanyia wanadamu wenzao, Yohana aliwaonya juu ya hukumu ya Mungu itakayokuja endapo kizazi kile hakitatubu, Hata hivyo ujumbe wa Yohana mbatizaji ulikuwa na mtindo wenye kufurahisha sana kwa sababu watu walimwendea wakitubu kwa kupitia kazi zao (professional), Mtindo wake wa kimaonyo na kimahubiri unaonyesha wazi kuwa ni watu ndio walimuendea wenyewe wakitubu, na kuuliza maswali, lakini sio hivyo watu walienda kimakundi kutokana na uhalisia wa kazi zao na kila mmoja akitaka kujua kuwa afanyaje ili asimkwaze Mungu na jamii na ndio maana swali kubwa la ujumbe huu ni *Na sisi je tufanye nini?*

1.       Kwa Jamii (Makutano) – Yohana mbatizaji alishangaaa kuona jamii kubwa ya watu wakikimbia kwenda kutubu na hivyo aliiambia jamii waziwazi, Kwamba waondoe uchungu mioyoni mwao Luka 3:7 “Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?Kitendo cha kuwaita makutano kizazi cha nyoka kilimaanisha kuwa watu wengi walikuwa upande wa shetani ambaye ndiye nyoka, lakini sio hivyo tu jamii ilikuwa na uchungu na malalamiko ya kila aina, na sio hivyo tu ilikuwa ni jamii iliyojaa hila na dhuluma na vilio vya kila aina, manung’uniko na hali ya kujiona kuwa hawakufanyiwa sawa, watu ambao wakati wote hawana jema Yohana aliwaonya watu wa namna hii Kuwa kamwe hawatafurahia uwepo wa Masihi, Na ujio wa Masihi hautakuwa na maslahi wa jamii yenye uchungu, jamii yoyote yenye uchungu hata uwafanyie nini hawatakuja kuridhika hata siku moja, hawatakuja kutoa shukurani, wakati wote watalalamika, uwepo wa Mungu na Baraka za Mungu na Hazifanyi kazi kwa jamii ambayo imejaa uchungu, Na ndio maana Yoaha nanakiita kizazi cha nyoka!Uchungu wakati wote katika maisha unapunguza sana neema ya Mungu, Maandiko yanatuonya kutokuwa na uchungu!

 

Waebrania 12:15 “mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.”

 

Yohana alikuwa anaiona hukumu ya Mungu na kuwa mafanikio hayawezi kuja kwa jamii ambayo wakati wote inalalamika tu au kwa jamii ambayo haitendeani mema au kwa jamii iliyojaa dhuluma, wizi, ubabaishaji, na hila za kila aina au jamii ambayo hairushusu hofu ya Mungu kutawala! Kama jamii ina uchungu wa aina yoyote hicho ni kizazi cha nyoka!

 

Waefeso 4:31-32 “Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”

 

Kizazi cha nyoka ni jamii iliyojawa na uchungu na uchungu ni sumu, ghadabu, hasira ni lazima iondoke katika jamii, uovu na ubaya wa kila namna ni lazima uondoke katika jamii ambayo inamtaka Masihi awe kiongozi wao, apite katikati yao aweze kuwa Baraka na kuleta uponyaji, ni lazima iwe jamii inayojaliana na kufadhiliana jamii ambayo imeacha umimi ubinafsi na uchoyo, Maandiko yanaitaka jamii kuondoa uchungu kwa kujilinda na choyo na kufadhiliana ona

 

Luka 12:15 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”

 

Si vema Yesu akaja katika jamii na kuikuta ina sumu, ina uchungu, na hasira, ina ubaya ina uovu, ina hali ya kutokusameheana au  isiyosamehe, jamii inayosingiziana, Yesu anaitaka jamii iwe na fadhili na ndio maana Yohana mbatizaji aliiiambia jamii kama una cha ziada gawia wasio nacho !

 

Luka 3:10-11 “Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi? Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo

 

Jamii isiyo na umimi itajifunza kutoa na kufadhiliana na itaachana na ubinafsi na kuangaliana wao kwa wao, leo hii jamii haiko hivyo kila mtu ana uchungu na kila mtu yuko kwenye kujikusanyia, kila mtu anangalia mambo yake na tumekuwa na jamii isiyo na shukurani na bingwa wa kulalamika na kujenga hoja za malalamishi ndio anaonekana shujaa katika jamii! Kama jamii ikiwa katika hali hiyo kweli hicho ni kizazi cha nyoka na hakina budi kubadilika na kutoka katika hali ya kuwa wana wa ibilisi na kuwa wana wa Mungu!

 

2.       Mafarisayo na Masadukayo (Madhehebu mbalimbali) – Wakati wa Yohana mbatizaji na Yesu pia kulikuwa na watu wa Madhehebu ya aina mbalimbali, madhehebu makubwa ya watu waliokuwepo nyakati hizo walikuwa ni pamoja na Mafarisayo na masadukayo, hawa walikuwa madhehbu maarufu sana nao waliposikia huduma ya Yohana mbatizaji walimwendea na wakatubu kwa wingi lakini Yohana hakuwaacha bila maonyo watu wa Madhehebu aliwaonya kuwa ni lazima waache kiburi cha kidini na kidhehebu, lakini lazima waache kujihesabia haki, Mafarisayo na Masadukayo walijifikiri kuwa wao ni madhehebu bora kwa sababu Ibrahimu ni baba yao Mbatizaji aliwaonya kwa manenio haya ona:-

 

Mathayo 3:7-10 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba; wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”

 

Mafarisayo na masadukayo yalikuwa ni madhehebu makubwa nyakati za Yohana na Masihi, Mafarisayo katika theolojia yao walikuwa wakiamini katika ufufuo wa wafu, waliamini katika malaika na maono na walikubaliana na vitabu vya Musa na manabii, lakini Masadukayo wao hawakuamini katika ufufuo, wala hawakuamini katika malaika na maono na waliamini vitabu vitano vya Musa tu na hawakujali vitabu vya manabii, kila mmoja alikuwa akijiona bora kutokana na madhehebu yake aliyokuwa nayo,Lakini zaidi sana walidhani ya kuwa Mungu anawahesabia haki kwa vile wao ni wana wa Ibrahimu, hata leo katika jamii zetu watu wanadhani kuwa kuwa na madhehebu ndio kuuchinja, wananadi sana madhehebu yao kuliko kumnadi Yesu, Yohana Mbatizaji aliwakazia akawaambia sikiliza Mungu anataka matunda yatokanayo na toba, Mungu anataka watu waliotubu na kugeuka na kuacha dhambi, ishu sio kuwa mtoto wa Ibrahimu kwa sababu Mungu anaweza kumuinulia Ibrahimu watoto hata kutoka katika mawe, Hivyo Dhehebu lako sio ishu wala sio dili, dili ni Yesu, Dili ni Masihi, dili ni toba ya kweli na mabadiliko, Mungu anataka matunda mazuri, hakuna matunda mazuri mti huo utakatwa na kutupwa motoni:-

 

Wagalatia 5:19-24 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.”

 

Wakati Yohana akikazia kuwa shoka limekwisha kuwekwa tayari na ni moto tu unahusu watu wasio na toba Paulo anaongezea kuwa watu wenye matunda yasiyofaa hawatauona ufalme wa Mungu, Kama una dini nzuri watu wanataka kuona matendo yako na sio vinginevyo, kama una dhehebu zuri watu wanataka kuona mabadiliko dini au dhehebu lako halitusaidiii katika jamii Mungu anataka matunda kinyume cha hapo ni hukumu tu. Wayahudi na waislamu na wakristo wanatokana na Imani ya Ibrahimu na wote wanakiri kuwa Ibrahimu nabii ni baba yao wa imani, Ni muhimu kufahamu kuwa dini na madhehebu hayatatusaidia kama hakuna matunda ya kweli na toba ya kweli

 

Yakobo 1:26-27 “Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.”

 

Kwa msingi huo Yohana aliionya jamii kuacha kujivunia dini zao na Madhehbu yao, wako watu ambao wako tayari kufa kwaajili ya dini zao wanazing’ang’ania kama chapati na hawana mpango na Yesu, na sio hivyo tu wanakiri ya kuwa wana dini lakini matunda hayaonekani, kama watu wana dini ya kweli chuki inatoka wapi, majungu yanatoka wapi, kiburi na dharau kinatoka wapi, fitina na majungu na kujipendekeza kunatokea wapi?  Mbona watu hawajilindi na mawaa, mbona hawajilindi na dunia, mtu anakiri kuwa na dhehebu safi lakini amejaaa viwango vya kidunia. Ni lazima watu watubu na kuzaa matunda.Vinginevyo hukumu itamhusu kila mmoja bila kujali ana dhehebu au dini nzuri kiasi gani!

 

3.       Watoza ushuru - Luka 3:12-13 “Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi? Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa.”

 

Kundi hili nalo wakati wa Yohana mbatizaji lilijitokeza kutubu, hawa walikuwa ni watoza ushuru, kundi hili liliagizwa kuacha dhuluma na kutoza zaidi ya kiwango kilichowekwa, kundi hili lilikuwa ni kundi la watu wenye tamaa ya fedha na waliojilimbikizia mali ka njia ya dhuluma, Dhambi yao kubwa ilikuwa ni kuzidisha na kutoza zaidi ya jinsi ilivyoamuriwa  ni watu waliokuwa wamejaa dhuluma sana, waliwadhulumu wananchi lakini pia hawakufikisha mapato serikalini, jamii ya watoza ushuru walihesabika kuwa hawana uzalendo na wala wakati mwingine sio waaminifu na hawafikishi kile kiwango cha fedha wanachokusanya au wakati mwingine walitoza juu ya kiwango kwa faida zao wenyewe! Hwa pia waliongezea manung’uniko katika jamii na kwa wayahudi watu hawa waliwekwa katika kundi la watu wenye dhambi sana, Kundi hili pia lilitakiwa kuacha uovu wake na kujiandaa kumpokea Yesu

 

 Luka 19:2-10 “Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri. Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo. Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile. Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako. Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha. Hata watu walipoona, walinung'unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi. Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”

 

Watoza ushuru walikuwa wamejitajirisha kupitia mali za dhuluma, na kuzidisha kiwango cha fedha kilichowekwa, hawa Yohana mbatizaji aliwajibu walipo uliza na sisi je tufanye nini aliwaambia wasitoze zaidi ya kiwango kilichowekwa, sehemu nyingi sana leo hii kumekuweko na watu ambao wanatoza zaidi ya kiwango kilichowekwa, unadhani kwanini serikali inapiga marufuku swala la twisheni kwa walimu? Kwa sababu tayari ada zipo zimewekwa, lakini kwanini walimu wanafanya twisheni, kwa nini wanachukua fedha ili wakufundishe pembeni pembeni, ada unayolipa haiwatoshi? Kuna namna nyingi sana watu wanatoza zaidi ya kiwango kilichowekwa,  wako pia wafanya biashara ambao wanatoza zaidi ya kiwango kinachokusudiwa na ukitaka kuwaweza we sema tu unadai risiti, watakuambia kuna bei ya kuandika kwenye risiti na bei ya bila risiti, Kristo hawezi kukubaliana na jamii ya watu yenye dhuluma ili aweze kuweka makazi anahitaji watu watubu kama alivyofanya Zakayo, aliamua kutubu na kurudhisha kwa jamii kile alichokusanya, wako watu wanakusanya na hawarudishi kwa jamii, lakini vilevile hawafikishi serikalini kama kila aina ya ushuru ungekuwa unafika inakotakiwa serikali ingekuwa imepiga hatua kubwa sana ya maendeleo, watu wangeweza kunufaika na mataifa yao na nchi zao na huduma za kijamii bila kuhitaji kukopa katika mataifa au mabenki, hakungekuwa na sababu ya kuinamia mataifa mengine, kuhitaji msaada, watoza ushuru hali kadhalika walifanya kazi za kubambikizia watu kodi nzito, kutishia kufunga biashara ugomvi na wafanya biashara dhuluma na mambo mengine ya kusikitisha lakini hata hivyo wakitubu Yesu atawapokea.

 

4.       Askari – Luka 3:14 “Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu

 

Maandiko hayaonyeshi kuwa kazi ya uaskari kuwa ni kazi mbaya au isiyofaa kwani ni wazi Askari waliomjia Yohana mbatizaji hapa ilikuwa ndio mahali pa kuwaambia waache kabisa kazi hiyo kama ingekuwa haifai, katika ulimwengu huu ulioharibika askari ni wa Muhimu na wanahitajika kwa sababu kuna watu ni waizi, na bila kuweko askari wakati mwingine ni ngumu kuitunza amani inayokusudiwa, Lazima askari wawepo ili kukomesha umwagikaji mkubwa wa damu na kuzuia uhalifu, kulinda taifa raia na mali zao na kuhakikisha usalama unakuwepo kila eneo, hivyo nabii hakusema waache kazi hii lakini aliwaonya wasidhulumu mtu na wala wasishitaki mtu kwa uongo kubambikizia watu kesi na kuwa watosheke na mishahara yao,Jaribu hili ndilo lililokuwa likiwakabili askari na hasa jeshi la polisi ambao walikuwa wakilinda usalama wa raia na mali zao katika mswala haya matatu kuna mambo ya ksingi ya kujifunza kwetu kwa kila kitu walichojibiwa askari kupitia Yohana mbatizaji.Sisi ni aksari tufanye nini:-

 

1.       Msimdhulumu mtu.

 

Dhuluma kwa kiingereza maana yake ni “unrighteousness” au KAKIA kwa kiyunani yaani ni hali ya kutokutenda haki, kutenda kwa ubaya, kutenda kwa kuumiza, kutenda bila kujali, watu wengi sana hawatendi haki hususani askari na hata watu wasio askari, lakini hata hivyo neno la Mungu linamtaka kila mtu atende haki kutokutenda haki kunaondoa neema ya Mungu

 

Tito 2:11-12 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;”

 

Kutokutenda haki sio mpango wa Mungu, Mungu alimwita Abrahamu ili awafundishe watu wake kutenda haki, na hii ndio sababu kubwa kwa nini Mungu alimchagua Ibrahimu, Mungu mwenyewe anaeleza:-

 

Mwanzo 18:17-19 “BWANA akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo, akiwa Ibrahimu atakuwa taifa kuu, hodari, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa? Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya BWANA, wafanye haki na hukumu, ili kwamba BWANA naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake.”

 

Mungu hukasirishwa sana wanadamu wanapoacha kutenda haki na kufadha udhalimu

 

Warumi 2:18 “Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu, atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake; wale ambao kwa saburi katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutokuharibika, watapewa uzima wa milele;     na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu;”

 

Na ndio maana sasa katika mahubiri ya Yohana Mbatizaji aliwataka askari kuhakikisha kuwa hawadhulumu mtu na hii ilikuwa ni agizo la kwanza kwao haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya taifa zima !

 

2.       Wala msimshitaki mtu kwa uongo:

 

Kushitaki watu kwa uongo ni moja ya dhambi kubwa sana zinazofanywa na askari Katika Biblia mara kadhaa tumewahi kushuhudia watu wakiuawa na kuhukumiwa kwa kusingiziwa makosa yasiyokuwa yao, siku hizi unaweza kupewa kesi nzito kama Uhaini, unaweza kubambikiziwa ugaidi, au utakatishaji wa fedha au uhujumu uchumi na kadhalika kesi ambazo zinaweza kukunyima dhamana na ukajikuta unasota rumande Moja ya amri katika amri za Mungu ni pamoja na kutokushuhudia uongo

 

Kutoka 20:16 “Usimshuhudie jirani yako uongo”. Ni wazi kuwa kwa mujibu wa sheria za Musa kushuhudia uongo lilikuwa ni moja ya makosa mazito na kama mtu anagebainika kutaka kumsingizia mtu uongo adhabu yake ilipaswa kuwa sawa na kile alichokuwa akimshitaki mwenzi wake, waamuzi walitakiwa kuchunguza ka makini sana kama mtu anatoa ushuhuda wa uongo kisha yeye anayeshuhudia uongo alipaswa alipaswa kuhukumiwa katika kosa lileliole analolishuhudia ili mwenzake ahukumiwe

 

Kumbukumbu la torati 19:18-19 “nao waamuzi na watafute kwa bidii; na tazama, yule shahidi akiwa shahidi wa uongo, naye ametoa ushahidi wa uongo juu ya nduguye;ndipo mtamfanyia kama alivyodhani kumfanyia nduguye; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako          

 

Agizo la torati liliwataka waamuzi vilevile kutokumhurumia mtu aliyewashitaki wengine kwa uongo yaani aliyetoa ushahidi wa uongo alitakiwa asihurumiwe

Kumbukumbu la torati 19:21  Wala jicho lako lisiwe na huruma; uzima kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.”

 

Awaye yote ambaye angemshitaki mtu kwa uongo au kutoa ushahidi wa uongo kama alikuwa ana lengo la kumuumiza mwenzake waamuzi wangebaini wangetakiwa kutokumhurumia mtu huyo na angehukumiwa sawa na kosa alilokuwa akilitolea ushaidi wa uongo bila huruma, kwa hiyo unaweza kuona kwa nini Yohana mbatizaji alikuwa mkali kwenye swala hili ni wazi kabisa ilikuwa ni kosa kubwa na zito mbele ya macho ya Mungu kushuhudia uongo dhidi ya mtu mwingine.

 

Ukiacha maamuzi yanayoweza kutolewa na waamuzi au serikali, Mungu pia huingilia kati pale askari na watu wengine wowote wanapoacha kutenda haki na kujaribu kumshitaki mtu kwa uongo, Kitabu cha Esta ni mfano uliowazi wa mtu aliyeitwa Haman ambaye alikuwa mshauri wa Mfalme Ahasuero alimshauri vibaya kwa makusudi ya kuwaangamiza wayahudi, hususani kwa sababu ya chuki yake dhidi ya Mordekai, hii ikitokana na wivu mkubwa aliokuwa nao dhidi yake unaweza kuona

 

Esta 5:9-14 “Basi Hamani alitoka siku ile kwa furaha na ukunjufu wa moyo; lakini Hamani alipomwona Mordekai mlangoni pa mfalme, ya kwamba hasimami wala kutetemeka mbele yake, alijaa ghadhabu juu ya Mordekai. Walakini Hamani akajizuia, akaenda zake nyumbani kwake; akatuma kuwaita rafiki zake na Zereshi mkewe. Naye Hamani akawasimulia habari za fahari ya mali zake, na wingi wa watoto wake, nayo mambo yote pia ambayo mfalme amemfanikisha katika hayo, na jinsi alivyompandisha juu ya maakida na watumishi wa mfalme. Zaidi ya hayo Hamani akasema, Naye malkia Esta hakumkaribisha mtu ye yote pamoja na mfalme katika karamu aliyoiandaa, ila mimi peke yangu; hata na kesho pia nimealikwa naye pamoja na mfalme. Bali haya yote yanifaa nini, pindi nimwonapo yule Mordekai, Myahudi, ameketi mlangoni pa mfalme? Basi Zereshi mkewe akamwambia, na rafiki zake wote, Na ufanyizwe mti wa mikono hamsini urefu wake, na kesho asubuhi useme na mfalme ili Mordekai atundikwe juu yake; ndipo utakapoingia kwa kicheko pamoja na mfalme karamuni. Basi neno likampendeza Hamani, akaufanyiza ule mti.” Unaweza kuona pia.

 

Esta 6:4 “Mfalme akasema, Yupo nani behewani? Ikawa Hamani alikuwa ameingia katika ua wa nje wa nyumba ya mfalme, aseme na mfalme, ili kumtundika Mordekai juu ya mti ule aliomwekea tayari.”

 

Esta 7:9-10 “Ndipo aliposema Harbona, msimamizi-wa-nyumba mmojawapo wa wale waliohudhuria mbele ya mfalme, Tazama, basi, mti wa mikono hamsini urefu wake, Hamani aliomwekea tayari Mordekai, ambaye alinena vema kwa ajili ya mfalme, upo umesimamishwa nyumbani kwa Hamani. Mfalme akasema, Mtundikeni juu yake.Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.”

 

Maandiko yanaonya kuwa wote wanaoshitaki wengine kwa uongo wako chini ya hukumu ya Mungu na hukumu ileile wanayoikusudia kwa wenzao itawapata wenyewe, wale waliomshitaki Daniel ili atupwe kwenye tundu la simba walitafunwa wao, maandiko yanasema kila aliyechimba shimo aliingia mwenyewe pia, Mungu hafuirahii udhalimu hata kidogo

 

Zaburi 5:4-6 “Maana huwi Mungu apendezwaye na ubaya; Mtu mwovu hatakaa kwako; Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako; Unawachukia wote watendao ubatili. Utawaharibu wasemao uongo; Bwana humzira mwuaji na mwenye hila

 

Jambo la kushangaza ni kuwa wakati mwingine unaweza kuona kuwa hata makanisani na sehemu zenye watu wanaodhaniwa kuwa watu wa Mungu watu husingiziana, hubambikiziana kesi za uongo na kusababisha madhara makubwa wakati mwingine unaweza kuumizwa na watu wanaoshuhudia uongo lakini Mungu anajua na atakufariji kwa namna yake, Yesu alitambua kuwa wako watu wanashitakiwa kwa kubambikiziwa kwa uongo kwa kutokusimama katika haki au kuisimamia kweli

 

Mathayo 5:11-12 “Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu”.

 

Haijalishi watu watatuzushia nini kwa uongo tumtegemee Mungu, Mungu atatulipia tu unaweza kuzushiwa uongo na kubambikiziwa kesi mbaya sana na ukaumia na kupata hasara lakini Mungu atakuja kufanya kitu

 

Zaburi 119:69-72 “Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako. Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Mimi nimeifurahia sheria yako. Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, Nipate kujifunza amri zako. Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.”

 

Ni jambo la kusikitisha sana kuona jamii ikiwa imejaa watu ambao wanaweza kutunga jambo zito na gumu dhidi ya watu wengine na kuwaharibia maisha, wahubiri wa haki ya Mungu kama ilivyo kwa Yohana mbatizaji, asingeweza kuvumilia dhuluma katika jamii wala asingetaka Yesu Kristo aikute dhuluma lakini kutokana na jamii iliyokuwa imejaa uovu hata Yesu mwenyewe alishitakiwa kwa uongo na mafarisayo na Yesu Kristo aliposhutumiwa uongo alinyamaza kimya wala hakujibu neno

 

Isaya 53:7-8 “Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.” 

 

Unajua kwanini Yesu hakufunua kinywa chake kujitetea dhidi ya washitaki wake, maandiko yalionyesha katika Torati kuwa ni jukumu la Waamuzi kuamua na kuchunguza kwa makini kama mtu analeta ushahidi wa uongo na ni jambo la kusikitisha kuwa Pilato pia alishindwa kufanya maamuzi ya hali na kuachilia Yesu auawe huku ushahidi ukiwa wazi kuwa ni ushahidi wa uongo

 

Mathayo 27:22-26 “Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe. Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe. Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe. Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu. Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe.”             

 

Kama unadhani kubambikizia mtu kesi na kumshitaki mtu kwa uongo ni jambo jepesi ni lazima ujiohoji na uhoji kuwa ukiacha kusudi la Mungu la mwokozi kufa pale msalabani kesi ya kubambikiziwa Yesu ilimwachaje Mariamu mama yake? Na je ndugu zake Yesu na wanafunzi wake hii maana yake wale wote waliomshitaki Yesu kwa uongo nao vilevile kwa sharia ya Musa walitakiwa kusulubiwa lakini Yesu alitangaza sharia mpya ya msamaha ndio maana akawaombea baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo ni kwaajili ya haya mahubiri ya Yihana mbatizaji na makatazo yake yalikuwa ni ya muhimu sana kwa wanadamu na jamii sio tu ya wakati ule bali hata naya wakati wa sasa.

 

3.       Kutokutosheka na Mishahara –

 

Yohana aidha aliwajibu na kuwataka askari vilevile kutosheka na mishahara yao, ni wazi kuwa kutokuridhika ni tatizo kubwa sana la mwanadamu tangu anguko la mwanadamu lilipotokea hakuna kitu kinatosha wanadamu wamekuwa na tamaa na miongoni mwao wakiwa askari kwa sababu wao kama walinda usalama katika jamii wana nafasi ya kuona fursa mbalimbali na hivyo ni rahisi kwao kama ilivyo vilevile kwa watu wengine kuingia katika mlango wa tamaa hususani katika fedha na kuwa na roho ya kutokutosheka

 

1Timotheo 6:7-10  Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo. Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”

 

Hali ya kutokuridhika na kuwa na tamaa kwa vyombo ambavyo vinatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa haki au kwa mwanadamu awaye yote ni tatizo la siku nyingi katika jamii mbalimbali hali hii huharibu uhusiano wetu na Mungu na wanadamu na kuharibu hali ya kiroho, Mungu angehukumu vilevile hali hii kwani hata zamani katika Israel ilikuwa ni njia ya matajiri kujipatia utajiri kwa njia zilizoharamu maswala haya yalikemewa na manabii kama Amosi, Mika na Yeremia Mfano katika kitabu cha Amos watu waliweza kuuza utu wa watu kwa sababu ya jozi za viatu tu 

 

Amosi 2:6b “Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu;”

 

Kwa msingi huo Yohana katika mahubiri yake alikuwa akiitaka jamii hususani askari kuwa na shukrani kuridhika kwani moja ya matunda ya ukomavu wa ubinadamu ni pamoja na kuridhika Lakini Mungu anawataka watu wake kuitenda haki ili Baraka za Mungu ziweze kumiminika katika maisha yetu

 

Mika 6:8 “Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Lazima jamii ikubaliane na maandiko kuwa unapaswa ufike wakati turidhike na maandiko yanatufundisha kuwa kuridhika kuna faida kubwa sana

 
1Timotheo 6:6-19 “Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo. Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi. Bali wewe, mtu wa Mungu, uyakimbie mambo hayo; ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole. Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi. Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo; ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana; ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha. Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo; huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli

 

Kwa mtindo huu utakubaliana nami kuwa Nabii Yohana mbatizaji alikuwa Mtu aliyeibhubiri haki ya Mungu kwa konyooka bila kujali cheo cha mtu yeye aliwaonya watu wote masikini kwa matajiri, wafalme na hata watumwa akiwataka wote kuandaa njia ya masihi na kuwa tayari kwa mioyo iliyotubu mbele za Mungu.kila mmoja  hana budi kujiuliza nay eye je anafanya nini katika nafasui yake! Na afanye ulio wajibu wake

 

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima