Jumanne, 22 Machi 2016

Ujumbe: Neema ya Mungu Haitendi Haki !


ONYO! “Kama hauna akili ujumbe huu haukufai, Usisome ujumbe huu kama hauna akili hutaelewa”acha!


1Wakoritho 1:26-31 Biblia inasema hivi:-
“26. Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; 27. bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; 28. tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; 29. mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. 30. Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi; 31. kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.”

Ndugu zangu unapoyatafakari maisha kwa undani sana na hasa maisha ya kiroho unaweza kuchanganyikiwa na ukagundua kuwa kitu au jambo linaitwa neema ya Mungu ni gumu kupokelewa kuliko unavyofikiri, ni rahisi kutafakari mambo juujuu na ukasema ni kwa neema ya Mungu lakini neema sio jambo jepesi kama unavyofikiri, leo sitaki kabisa kufafanua nini maana ya neema kwa vile nafikiri tutazunguka tu lakini natka kukazia kuwa Neema ya Mungu haitendi Haki! Najua kuwa hii ndio lugha nyepesi itakayokusaidia leo kuelewa ninapotaka kuizungumzia neema ya Mungu.
Neema ya Mungu haitendi haki swala hili kwa asili sio sahihii lakini ndio litakalotusaidia leo kuelewa maana ya neema ya Mungu tukinena kiwazimu, kichwa hiki kinatusaidia kujua kuwa wewe na mimi sio Mungu na Mungu sio mimi na wewe, wakale walisema “ Mungu sio Athumani” hebu tufafanue kwa kina zaidi

Tunapoisoma biblia neno la Mungu mara nyingi tunasoma katika mtazamo wetu our own perspective, Hata ingawa tunafahamu kuwa hili ni neno la Mungu na kuwa njia zake sio njia zetu wala mawazo yake sio mawazo yetu, angalia tunapokosea akili zetu hutuambia kuwa tunahitaji kuadhibiwa kwa sababu ya makosa yetu ndio nah ii ndio Haki kabisa, tunajisikia kuwa tumemkosea Mungu na ni lazima tuadhibiwe ndio hiyo ndio haki, sio hivyo tu wanaotuzunguka wanaweza kuona kwamba tumemkosema Mungu na ni vema tukiadhibiwa na ni haki kabisa si tumekosea si amekosea ni haki akaadhibiwa ni haki tukasimamia aadhibiwe ni haki akione cha mtemakuni ni haki akome afundishwe asirudie tena ajutie kosa lake aipate fresh, ashughulikiwe  na ndio usahii wa mambo kwa mawazo yetu ya kibinadamu, Lakini shida au Tatizo la Mungu haangalii mambo kama tunavyoangalia sisi, sisis tunataka haki, tunatadhamia thawabu kwa mtu aliyetenda vizuri na mabaya kwa aliyefanya vibaya Mungu ni tofauti, haangalii kama tunavyoangalia sisi mtazamo wake sio sawa na wa kibinadamu “your perception is not always Gods reality” Mtazamo wako sio ukweli kuhusu Mungu wakati wote. Mungu aliweka mipango kabla sisi hatujazaliwa alijua kipi kitakuwa sahii na kipi hakitakuwa sahii katika maisha alijua wapi utakaa vema na wapi utakosea alijua kabla hajakuumba, na wakati wote huo mpango wake ni kutufanikisha, kuanguka kwetu sio jambo la kushangaza kwa Mungu sio habari hata its not a news yeye anaendelea na mpango wake wa kutufanikisha tu yuko busy kutufanikisha, sio lazima afungwe  na haki, anaangalia mpango wake yuko kwenye kutii mapenzi yake na makusudi aliyotuumba kwayo

Angalia kifungu cha maandiko tulichokisoma pale juu, ni mfano ulio wazi kuhusu neema, kama Paulo angesema Mungu anachagua watu maalumu, wenye akili, wenye cheo, wenye uwezo, waliowakamilifu, watenda mema anawatafuta watu wa aina hii duniani awabariki na kuwatumia kwa utukufu wake, hii ingekuwa ni sawa na inakubalika katika akili ya kawaida Logical na lingekuwa ni jambo jema na wote tungejitahidi sana kuwa wazuri kiasi ambacho Mungu angeshawishika kutuchagua, kama Mungu angekuwa anaagalia watu wa aina hiyo wachapa kazi, wenye bidiii, wasio na maswalimaswali hata katika maswala ya uadilifu, waungwana  kwa akili zetu za kawaida tusingeweza kulaumu chochote maana ni haki tu.

Paulo Mtume alichaguliwa na Mungu na kutumiwa kuandika karibu nusu na zaidi ya agano jipya, kamakuchaguliwa kwake kulitokana na kushinda mashindano ya mitume walio bora tusingelikuwa na maswali maana ni haki, amewashinda mitume wengine, lakini la kushangaza ni kuwa Mtume huyu hakuwa hata katika orodha ya mitume wale 12, wakati Yesu anapaa ndo kwanza huyu alikuwa upande wa pili akiwapiga vita wakristo na kuwatesa vibaya na kusimamia  mauaji yao, aliomba hata kibali cha kuwatesa na kuwaburuza wakristo kila waliko, cha kushangaza sasa Yesu anamchagua huyu na kumtumia kwa kiwango kikubwa kuliko mitume wote, hii inachanganya akili zetu za kawaida hii sio haki, huyu hafai, muuaji mtesi wa kanisa alitakiwa afe, hii ndio ilikuwa haki yake lakini anachaguliwa kuwa mtume hii sio haki kabisa hii ndio NEEMA YA MUNGU!

Sasa tunajifunza nini hapa?
1.       Neema ya Mungu haitendi haki. Unapofundishwa kwa kutishiwa kuwa kila upandacho utavuna au kuna kuvuna kile ulichopanda inakubalika akilini kuwa ni sawa logically unakubali na kuelewa kuwa utakachopanda utavuna, ni rahisi kuelewa kuwa apandacho mtu ndicho atakachovuna hii ni sawa hii ni haki, ni haki mtu mbaya kupatwa na mabaya na mtu mwema kupata mema ni sawa tunavuna kila tunachokistahili, lakini kama tunastahili mema kwa kutenda mema na mabaya kwa kutenda ubaya sasa hapo ni malipo na sio neema tena. Mungu hatendi haki hata kidogo Mungu hufanya mambo kwa sababu anatupenda, anakupenda na ananipenda

2.       Usijaribu kupigana na neema ya Mungu kwa akili za kibinadamu, wakati mwingine ni vigumu kuelewa kwa nini Mungu anafanya kitu Fulani kwako au kwangu, ni muhimu tu kukubali kuwa ni upendo wa Mungu na kupokea kila jambo kwa upendo, upendo wake ndio unaomshukuma afanye kitu katika maisha yetu, Mungu anaposema kuwa anataka kukubariki na kukutumia sana na akili yako inapopambana na kusema mbona sistahili unapigana na neema, Mungu anapombariki mwingine huku unafahamu kabisa udhaifu wake ukaanza kushangaa nankushutumu unapigana na neema ni lazima tukubali kuelemewa na Neema ya Mungu acha kupigana na neema acha




3.       Luka 15: 11- 32 Biblia inasema hivi “11. Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;   12. yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.        13. Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati. 14. Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. 15. Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. 16. Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. 17. Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18. Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19. sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.                 20.Akaondoka,akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21. Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22. Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23. mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24. kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia. 25. Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.  26. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?  27. Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. 28. Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi. 29. Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu; 30. lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona. 31. Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako. 32. Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.” Yesu alitoa ujumbe huu hapo juu kwa sababu ya watu waliokuwa wkipigana na NEEMA YA MUNGU utawezaje kujua kuwa Yesu aliwaonya watu hao ili wasiingilie Kazi anazozifanya Mungu kwa kutumia akili zao logic angalia mistari hii ya awali katika Luka 15:1-2 Biblia inasema hivi  1. Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. 2. Mafarisayo na waandishi wakanung'unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula naoAngalia maneno ya aya hizi kwa umakini na Mungu akusaidie Yesu alikuwa anajiwa na watu ambao kwa akili za kawaida walikuwa wabaya, waliitwa wenye dhambi, wahalifu kwa hiyo wale watakatifu wenye haki walinung’unika kwa nini mwokozi anatenda jambo kama hili, kwa akili za kawaida ilikuwa ni haki, Yesu ni Mungu na Mungu ni mwenye haki, rafiki zake ni wenye haki, anapaswa kuwahudumia na kuwajali na kukaa nao na kuwatendea mema., Mfano wa Yesu alioutoa kufuatia manung’uniko hayo unaonyesha tena Neema ya Mungu haitendi haki, kwa vipi?

Mwana mpotevu alikuwa tayari amepewa sehemu ya urithi wake na mali yake, alitaka kuishi mbali na baba alitaka kuwa huru, amelelewa vizuri hakuna alichokikosa kwa baba yake sasa anataka kuchukua kilicho chake akaishi maisha ya uhuru, Baba yake alimruhusu, alimuachia alimpa alichokiomba na kukidai, aliondoka na kila kilichochake, alivitumia kwa anasa na maisha ya ukahaba, Hakuna alichobakiza nyumbani. Alichezea mali yake na uhuru wake, alifanya anayoyataka , mwisho yakamkuta mabaya aliishiwa na kupigika sana, hakuna alichobakiza alipoteza uhuru wake akawa kibarua akawal mlisha nguruwe, kwa mtazamo wa kawaida mtoto huyu kibinadamu ungemfanya nini? Alistahili malipo yake angeachwa akione cha mtema kuni angetaharizwa kipi kinakurudisha nyumbani umesahau nini? Umebakiza nini hii ndio haki aliyopaswa kufanyiwa kibinadamu alitakiwa kufukuzwa, angeachwa aonje joto ya jiwe akione cha mtema kuni!
Kutokana na taabu aliyokutana nayo aliamua kurudi kwa baba, Jambo la kushangaza ni kile baba alimfanyia

 “Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21. Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22. Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23. mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24. kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.” 

 Hiki ndicho alichokifanya baba yake alimuonea huruma maana yake Rehema za baba yake na neema ya baba yake ilimsukuma kumtendea mwanawe sherehe kubwa na kumfanya mfalme Prince na watu wote wa nyumbani kwa babaye walifurahi, Baba alijua kuwa mwanaye sasa anaweza kutofautisha maisha ya uhuru na usalama aliokuwa ameupata kwa baba yake, ni mwanaye ulitegemea atamfanya nini? Mwenyewe alielewa wazi kuwa anapaswa kuwa mtumwa tu, baba akamfanya Prince kijana wa kifalme, tunapokosea sisi na wanaotuzunguka tunategemea kuwa Mungu hawezi kutukubali tena wala kutufanyia mema haya ni mawazo mabaya kwa Mungu wetu ni kuushushia hadhi upendo wake kumbuka kuwa mfano huu na fundisho hili halitii moyo hata kidogo kuishi maisha ya dhambi lakini pia halikubaliani hata kidogo na fikra za majivuno na kiburi cha kujifikiri kuwa wewe unastahili kwa vile ni mwema kuliko Fulani, kipimo cha wema anacho Mungu na kwa rehema zake na neema yake ana haki ya kumuona mmoja kuwa sawa na wewe au kumuona mmoja kuwa bora kuliko wewe hata kama kwa vipimo vyako wajiona kuwa uko sahii, hakuna kiburi kikubwa na kibaya duniani kama kujiona unastahili nje ya neema ya Mungu, kama utakuwa na mawazo hayo utaiona Neema ya Mungu kuwa Haikutendei haki.
Hukumu na aibu ilimkuta ndugu mkubwa badala ya furaha kwake ilikuwa huzuni majuto na mkususa na kukasirika na ilikuwa siku yake ya kuhubiriwa kwamba kwanini afurahii Baba kumpata mwanaye, kwa nini hafurahii baba kumfanyia hserehe mwanaye ni wazi kuwa kwa akili za kawaida kaka mkubwa alijiona ni mwenye haki na mwenye kustahili, lakini lisahau kuwa amejikweza kwa matedno yake ya haki, aka kiburi Mungu huwapinga wenye kiburi bali huwapa wanyenyekevu neema. Haya ndio yaliyomkuta 

“Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.  26. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?  27. Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. 28. Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi. 29. Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu; 30. lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona. 31. Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako. 32. Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.”

Kama kazi ya baba huyu ingekuwa ni kuhukumu na kutokuhurumia kuacha kuutumia ukarimu wake basi angekuwa ametenda haki, kama baba angemfanyi sherehe mwana wake mkubwa na kumpongeza kwa kuwa mtoto mwaminifu angekuwa ametenda haki na wote tungekuwa na ujuzi na watu wote wangeelewa kuwa Baba ni mtenda haki amemlipa kila mmoja sawa na kutenda kwake sasa tatizo ni Moja Mungu ni wa rehema na neema hapa anaonyesha Upendo, rehema na neema na ndipo linapokuja swala lililowazi linaloacha vinywa vyetu wazi kuwa Neema ya Mungu Haitendi haki kwa nini haitendi haki ili ibaki kuwa Neema, Bila shaka nikisema ni kwa neema sasa kila mmoja atakuwa anaelewa maana ya neema.

Unataka haki unataka Neema? Mimi nachagua Neema ya Mungu.

Sala ya kuomba neema:-

Baba ninakushukuru sana nakushukuru kwa Neema yako, kadiri ninavyojifunza kuhusu neema nagundua mambo ya kushangaza sana, Unajua vema kuliko ninavyojua, na ninavyojijua, unajua mara ngapi nimekosa na mara ngapi nimekulazimisha uingie name hukumuni uniadhibu, na wakati mwingine nimejiadhibu na hata kuadhibiwa na wengine kwa makosa yangu, lakini nashukuru kwa Upendo wako na kwa msamaha wako, umeniita hata hivyo, unanitumia hata hivyo pamoja na kunijua nilivyo, sio kwa sababu ya akili nyingi sana, sio kwa sababu ya kutoka katika familia ya wenye hekima, wenye vyeo, watawala, si kwasababu nimestahili, bali ni kwa neema yako, Kwa neema yako tunawashangaza wengi, kwa neema yako nitakuabudu na kukusifu siku zote za maisha yangu, kwa neema yako Maadui zangu wataisoma namba, kwa neema yako wanaoniwazia mabaya watatahayari, kwa neema yako umewatetemesha na kuwaziba vinywa watesi,kwa neema yako umenipa mema ya umande wan chi, kwa neema yako mdogo atakuwa elfu, kwa neema yako, Kaka zangu na Ndugu zangu wataniinamia, hawataponyoka kamwe katika kongwa langu,kwa neema yako umenibariki, kwa neema yako umeniinua, kwa neema yako kila kinywa kitakachoinuka kinyuma name kitahukumiwa, kwa neema yako utabatilisha kila shauri lisiolo haki dhidi yangu, kwa neema yako, kwa neema yako kila dua mbaya itageuzwa kuwa Baraka kubwa sana kwangu, kwa neema yako utanyamazisha woote walioona hududa dhidi yangu, kwa neema yako kila silaha itakayofanyika juu yangu haitafanikiwa, nipe kuhubiri, kwa neema, nipe kuimba kwa neema, nitumia kwa neema, weka moyoni mwangu jumbe mbalimbali kwa neema, Neema neema neema

Wimbo kuhusu Neema
Wimbo: Mungu amenihurumia

1. Mungu ametuhurumia, tendo hili kubwa sana,
sikustahili jambo hili, nimelipata bure tu!
sasa najua hayo yote, sasa najua hayo yote,
nasifu rehema zake, nasifu rehema zake

2. Nalistahili kupotea, lakini nahurumiwa,
Mungu amenipatanisha na yeye kwa Yesu Kristo,
sababu hii namtumikia, sababu hii namtumikia,
nasifu huruma yake.

3. Mungu mwenye huruma nyingi, usininyime huruma,
naitafuta siku zote nikiulizwa na watu,
hivi vyote vyatoka wapi? hivi vyote vyatoka wapi?
Nasema ni huruma tu!
Ubarikiwe!

Mungu na wakimbizi:


Ni muhimu kufahamu kuwa kuwahudumia wakimbizi ni mpango wa Mungu!, Leo tutachukua Muda wa kutosha kwa kina na upana na urefu kuangalia huduma muhimu kwaajili ya wakimbizi Duniani, Mwaka 2004 pekee karibia watu milioni tatu na nusu walikuwa ni wakimbizi barani Afrika pekee, ambao walikimbia na kuishi nje ya nchi zao, na wengine zaidi ya milioni kumi walikuwa ni wakimbizi ndani ya nchi zao, wengi walikuwa hawakimbii tumatukio ya majanga ya kiasili nlakini walikuwa wanakimbia matatizo ya kisiasa, ugomvi wa kimadaraka, matatizo ya kidini, ukabila na maswala mengineyo je neno la Mungu linasema nini kuhusu wakimbizi, kanisa limewahi kutafakari nini kuhusu wakimbizi? Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:- 

 Kundi kubwa la wakimbizi wakiondoka Syria, wakimbizi nao ni watu


·         Neno la Mungu na wakimbizi
·         Mungu anawajali wakimbizi
·         Wakimbizi na mafundisho ya agano jipya

Neno la Mungu na wakimbizi:

Biblia inatambua kuweko kwa watu ambao wamewahi kukimbia huko na huko mbali na Nchi zao, kaini alikuwa mtu wa kwanza kufahamu madhara ya ukimbizi Mwanzo 4:12,”Utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake, utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao Duniani” Neno utakuwa mtoro ni sawa na utakuwa mkimbizi. Yakobo na Familia yake waliishimaisha ya ukimbizi kutokana na majanga ya njaa nchini kwao Mwanzo 47:3-4, “Farao akawauliza hao nduguze Kazi yenu ni nini? Wakamwambia Farao, Tumekuja kukaa ugenini katika nchi hii, kwa sababu wanyama wa watumwa wako hawana malisho, maana njaa ni nzito sana katika nchi ya kanaani, Basi twakusihi uturuhusu sisi watumwa wako tukae katika nchi ya gosheni” Yesu pia alikuwa mkimbizi huko Misri kwaajili ya kuokoa Maisha yake yaliyokuwa yakitafuta na mfalme Herode Mathayo 2:13-14. “Na hao walipokwisha kwenda zao tazama malaika wa Bwana alimtokea yusufu katika ndoto, akasema  Ondoka umchukue mtoto na mama yake , ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie kwa maana Herode anataka amwangamize, Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku akaenda zake Misri” ziko sababu mbalimbali na mazingira ya aina mbalimbali yanayoweza kusababisha kila mmoja wetu kuwa mkimbizi kwa namna moja ama nyingine.

Mungu anawajali wakimbizi

Biblia iko wazi kuwa Mungu anawajali wakimbizi, alionyesha kujalia sana maisha ya Kaini hata pamoja na kuwa ukimbizi wake ulisababishwa na makosa yake mwenyewe Mwanzo 4:15. Mungu alimwambia Musa katika Torati kuandaa miji ya makimbilio kwaajili ya wakimbizi watakaokimbilia kutokana na sababu mbalimbali ama ambao watu wangelikuwa wanatafuta kuwaua, Kutoka  21:12-14, Hesabu 35:9-34, Kumbukumbu 4:41-43, 19:3-13, Nyakati 6:42-55. Mungu aliagiza pia kuwa wageni walioambatana na Israel pia wanahitaji kuheshimiwa kimsingi tunapaswa kuwajali aina zote za wakimbizi waliokimbia nchi zao kwa sababu zozote zile ziwe za kisiasa, vita uchumi njaa  na ugumu mwingine wote wanapaswa kuheshimiwa kuhifadhiwa kutunzwa vizuri, kupendwa na kuhifadhiwa,kwa heshima na usawa sawa na raia wengine tukiwahesabu kuwa ni ndugu na jamaa zetu Walawi 25, Isaya 16:1-4, Ezekiel 47:21-23 Lawi 19:33-34.

Wakimbizi na mafundisho ya agano jipya

Agano jipya linasisitiza sana kuwahudumia wageni kuwapenda na kuwajali wenye mateso na masikini Mathayo 25:31-40, tofauti ya ndugu na wakimbizi iliondolewa kabisa katika agano jipya Yohana 13:34 kutokana na umoja wa waamini Yohana 17:20-23 na kutokana na udugu na wote kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo.
Hivyo ni muhimu kwa kanisa kujihusisha na kuwahudumia wakimbizi punde linapotokea swala la wakimbizi na kukutana na mahitaji yao ya muhimu haraka , kama usalama, upendo, chakula mavazi, malazi, maji safi,madawa, Kumbuka kuwa Yesu atakuja kubagua Kondoo na mbuzi kwa misingi ya namna tunavyowajudumia wengine au wenye uhitaji Mathayo 25:31-46, bila huduma hizi ni vigumu kwa wakimbizi kuikubali injili, wanyarwanda wana usemi usemao “Inda irimo ubusa ntigira amatwi” yaani tumbo tupu halina masikio, Ni muhimu kanisa likakumbuka hilo likakumbuka kuwahubiri injili lakini pia kusikiliza injili kutoka kwao ikiwa wanauwezo wa kuhudumu ili kuwalea na kukuza huduma zao punde warudipo au kuwa wamisionari katika taifa letu, hivi ndivyo nyakati za kanisa la kwanza walivyofanya pia Matendo 8;1-4, 18:1-2, Hali hii itainua heshima yao na kuwatia moyo, kanisa pia linapaswa kufanya kitu cha ziada sio tu kuwaletea maji katika birika bali kuwaelekeza namna wanavyoweza kuchimba visima wenyewe ili kujipatia maji, kanisa linapaswa pia kujihusisha katika swala zima la kuangalia chanzo cha ukimbizi na kukishughulikia hii ina maana kuwa kanisa linapaswa kujishughulisha na swala la kufanya upatanisho na kutafuta majibu ya matatizo ili kuyatatua na watu waweze kurejea katika nchi zao kwa amani badala ya kuiacha kazi hiiikafanywa na serikali zaidi, Kanisa ni lazima lisimamie demokrasia, Haki, upatanisho na mswala ya uongozi kwa ujumla, unaweza kufikiri kuwa kazi hii ni ya kiserikali zaidi nay a kijamii zaidi kuliko ya kiroho, lakini nataka nikuambie kuwa ni ya Kiroho zaidi na inapaswa kanisa kuwa sambamba na mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na huduma kwa wakimbizi

Ni muhimu kuwahudumia vema wakimbizi wao pia ni binadamu, kuna historia za kutisha kuwa sehemu nyingine wakimbizi wanabakwa, wanakataliwa, wanawekewa uzio, au wanafanyiwa hila wafe,n.k. hivi karibuni katika nchi ya Syria kutokana na vita kumekuwa na wakimbizi wengi wanaokimbilia ulaya na wengine wanapitia Libiya lakini wengi wamefanyiwa hila wakikimbia kuokoa maisha yao wengine wameuawa na mataifa mengine yameingia hofu ya kuwapokea Mungu isaidie Dunia kuwa mahali panapofaa kukaa ni wajibu wetu kupiga vita kila kinachosababisha watu kukimbia nchi zao na kujaribu kutatua migogoro iliyoko Duniani ili kila Nchi ipate Ustawi unaokusudiwa na Mungu.

Yeye aliye na sikio na alisikie neno hili ambalo Roho aliambia kanisa.

Jumamosi, 19 Machi 2016

Mafundisho Kuhusu Ubatizo:-



Ni muhimu kufahamu kuwa Mafundisho kuhusu Ubatizo katika nyakati hizi tulizonazo yamechakachuliwa sana,  na hivyo kuliweka kanisa katika wakati mgumu wa kuamua watu wabatizwe vipi kutokana na kila mtu kubatiza katika namna anayoiona kuwa iko sahii na kujenga hoja za kibinadamu hata kuliko kuliangalia Neno la Mungu linasema nini kuhusu Ubatizo, Mungu na ampe neema kila mmoja wetu na moyo uliopondeka ili wote kwa pamoja tuache tofauti zetu na kuliangalia neno la Mungu linasema nini kuhusu Ubatizo, tuchukulie kana kwamba tumeokota Biblia na sisi wote hatujui Neno la Mungu na tunaisoma hiyo Biblia na tunagundua kuwa tunaweza kumuamini Mungu na tukabatizwa je unafikiri tungebatizwa vipi?  Hii ndio aina ya ubatizo ninayotaka kuizungumzia sawa na Neno la Mungu linavyojieleza na sio sawa na tamaduni za watu na historia za kipagani.

 watu wengi sana hubatizwa pale alipobatiziwa Yesu mto Jordan (Jordan river) huko Israel.

Kwa msingi huo leo tutachukua Muda pamoja na mkuu wa wajenzi mwenye hekima kuchambua kwa kina somo kuhusu ubatizo kwa upana na urefu, ili tuweze kufahamu kwa undani kuhusu ubatizo na kuondoa utata ulioko miongoni mwa jamii ya Kikristo.

Yesu aliamuru kwamba wote watakaomuamini na kubatizwa wataokoka, Biblia inasema katika Mathayo 28:18-20 “18. Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 19. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;    20. na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.” Unaweza pia kuona katika Marko 16:15-16 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe, aaminiye na kubatizwa ataokoka asiyeamini atahukumiwa

Ni muhimu kwetu basi tukachukua muda kuchambua agizo hili la Yesu la kubatiza na kuangalia kwa undani kile tuilichoagizwa ili kukifanyia kazi kama Mungu alivyoagiza. Tutajifunza somo hili Mafundisho kuhusu Ubatizo kwa kuzingatia Vipengele vitano vifuatavyo:-


  • ·         Maana ya Neno Ubatizo
  • ·         Maana na Historia ya Ubatizo
  • ·         Kanuni na jinsi ya kubatiza
  • ·         Sifa ya mtu anayestahili kubatizwa
  • ·         Namna ya kubatiza.


Maana ya Neno Ubatizo:-

Kwa kuwa tunazungumzia ubatizo ni vema kwanza tukaelewa asili ya neno Ubatizo neno Ubatizo tulilo nalo kwa Kiswahili katika kiingereza wanatumia neno “Baptize” au “Baptisms” ambalo kwa asili limetokana na Neno la kiyunani yaani KIGIRIKI  BaptizoBatizo,  ambalo maana yake ni Kuzamisha au kudumbukiza, “to dip or sink” or “immerse” pia ubatizo unaweza kufananishwa na kuchovya kama mtu anavyoweza kudumbukiza tonge la ugali katika mchuzi, nyakati za Biblia pia lilitumika kumaanisha kuchovya na kufyonza kabisa asili ya kitu kwa mfano nguo ya kitani ilipowekwa katika rangi ili kuibadili iwe na rangi ingine ilidumbukizwa katika rangi na nguo hiyo ilitoka ikiwa imebadilika kutoka weupe wake wa asili kuingia katika rangi iliyodumbukizwa kwayo tendo hilo pia liliitwa Ubatizo unaweza kuona, hii ndio maana halisi ya ubatizo hata kwa mujibu wa “Strong concordance” na “NAS Exhaustive Concordance”  na vyanzo vingine vya Lugha za kiyunani.

Maana na Historia ya Ubatizo:

Kama tulivyoweza kuona maana ya Ubatizo hapo juu ni wazi kuwa hii ndio maana halisi ya ubatizo na maana hii imathibitishwa na hata kukubaliwa kuwa ndio maana halisi ya ubatizo kwa mujibu wa wataalamu na wasomi wa Lugha ya kigiriki yaani kiyunani, na wanahistoria waliobobea katika maswala ya kanisa, ingawa ni muhimu pia kufahamu kuwa wayahudi walioishi nyakati za Kanisa la kwanza walibatiza pia kwenye maji mengi au kwa kuzamisha kwa kusudi la kuwabadilisha wale waliokuwa mataifa wa kawaida walioamini katika dini ya kiyahudi ambao waliitwa “Proselyte’s” ubatizo wao ulikuwa na maana ya kuwa wameacha miungu yao na kumuamini Mungu wa wayahudi, kitamaduni inaelezwa kuwa mwongofu alisimama katika maji na kisha kuzamisha kichwa chake katika maji huku sheria au Torati ya Musa ikisomwa, na tendo hilo pia lilimuhesabu kuwa ametakaswa na  na ameanza kuishi maisha mapya  kama mtu wa watu wa agano la Mungu.

Katika tamaduni za kiyunani pia kulikuwako na biashara zilizoshamiri za uuzaji wa nguo za rangi ya zambarau soma Matendo 16:11-14 nguo hizi zilikuwa mfano wa batiki zilizamishwa katika sufuria za maji yenye rangi na hivyo nguo hizo zlifyonza maji na rangi kabisa na kusababisha rangi kupenya katika nguo na nguo ilitoka ikiwa na rangi iliyokusudiwa kitendo hiki pia kiliitwa UBATIZO.

Ni wazi kutokana na maana na historia na tamaduni, swala la kunyunyizia maji au kumwagia maji binadamu kwa madai kuwa unabatiza haliko katika historia nzima ya kubatiza, lakini liko katika tamaduni za kitorati za kutakasa kitu au vitu, pia kibiblia swala hilo halimaanishi ubatizo, Kibiblia kuhani alitakasa vitu au vyombo vilivyotumika kwa kazi maalumu hekaluni, lakini linapokuja swala zima la Ubatizo kubatiza kwa kunyunyizia hakuna mashiko ya kihistoria wala ya kimaandiko, kuna uwezekano tu kuwa aina hii ya ubatizo ilifanywa kwa wagonjwa mahututi ama ambao walikuwa hawawezi kuelekea eneo la Ubatizo na pia ama kwa kuheshimu watu wenye nyadhifa kubwa kama wafalme, au pia kwa sa babu ya kubatiza wakristo waliokimbilia mafichoni wakati wa mateso, hata hivyo kwa sababu zozote zile kama zilizoainishwa hapo juu, haziwezi kuhalalisha ubatizo huo kuwa wa kibiblia ama wa kihistoria, na kwa vyovyote vile ubatizo huo sio agizo la kibiblia na uko uwezekano kuwa uliingizwa kwa mitazamo ya kipagani au kwa kuweko na mwingiliano wa kipagani.
Iko wazi kuwa ubatizo wa kimaandiko kabisa ambao hata wapagani yaani watu wasio na dini wakiokota biblia leo wakajifunza neno na kubatizana basi ni wazi ubatizo halisi utahitaji maji mengi na ya kuzamisha, ambayo ndio maana halisi ya kibiblia kwa mujibu wa Maandiko Warumi 6:1-4.
Ubatizo unafanana na tendo la kuzika mwanadamu Warumi 6:1-4
Ubatizo ni picha ya wokovu
Ubatizo ni kivuli cha kufanana na Bwana Yesu kiroho
Ubatizo ni alama ya kuoshwa ni alama ya kile ambacho kimekwisha kufanyika ndani ya moyo Matendo 22:16
Ubatizo ni ushuhuda Wagalatia 3:27
Umuhimu wa ubatizo, kanisa halipaswi kupuuzia swala zima kuhusu ubatizo, hata ingawa ubatizo wenyewe hauokoi, wala hauna nguvu ya kuokoa, watu hawabatizwi ili waokoke, lakini wanabatizwa kwa sababu wameokoka, kwa hiyo ubatizo sio tiketi ya wokovu lakini ni tendo muhimu katika kumkiri Yesu hadharani na ni muhimu katika kuonyesha utii, kama vile Rais anapoteuliwa anathibitika kuwa Rais kamili pale anapoapishwa, tunapokuwa tumemuamini Yesu kuwa ni bwana na mwokozi wetu, kokote pale tunamkiri Yesu kuwa ni bwana na Mwokozi hadharani kwa kukubali kubatizwa.

Kanuni na Jinsi ya kubatiza

Ni muhimu kufahamu kuwa kanini kuu ya kubatiza ni kile kilichoagizwa na Bwana Yesu tu Mathayo 28:19 Kubatiza kwa jina lka Baba na la mwana na la Roho Mtakatifu. Haya ndio Maneno yanayopaswa kutamkiwa mtu anayebatizwa sawa na Yesu alivyoagiza, mtu anapomwamini Yesu anakiri hadaharani kwa njia ya ubatizo na mbatizaji atatamka maneno haya Kwa kuwa Fulani…….bin Fulani…..umemwamini Bwana Yesu Kristo kuwa alikufa msalabani kwaajili ya ondoleo la dhambi na kuwa amekuwa bwana na mwokozi wa maisha yako kwa mamlaka niliyopewa na Mungu mimi nakubatiza kwa jina la baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu amen!, Maneno wakabatizwa kwa jina lake Yesu Kristo yaliyotumiwa na petro katika Matendo 2:28, hayawakilishi kanuni ya kubatizia, bali yanazungumzia Mamlaka ya ubatizo mara baada ya mtu kumuamini Yesu Kristo, kwa Mfano “Didache” yaani maandiko ya nyakati za zamani wakati wa mitume yaliyoandikwa mika 100 baada ya Kristo (100 AD) yanataja Ubatizo ulioagizwa na Yesu kama Ubatizo wake Yesu Kristo lakini katika ufafanuzi wake jinsi walivyobatiza walitumia kanuni ya kubatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakataifu, Hivyo kanuni iliyotumika kubatiza ilizingatia utatu wa Mungu. Paulo anapozungumzia ubatizo wa wana wa Israel katika bahari ya shamu anataja Ubatizo wake Musa hii haimaanishi Paulo alikuwa anataja juu ya Kanuni bali mamlaka ya Musa kwa vile kila mmoja baada ya kuvuka bahari ya shamu alikubali wazi kuwa Musa ni mjumbe wa Mungu wa Mbinguni kwaajili yao, “1Koritho 10:2” ni katika mtazamo huohuo unapozungumzia ubatizo wa Yesu Kristo unazungumzia sio kubatizwa kwa jina lake Yesu tu, bali kubatizwa kwa Mamlaka au agizo lake Yesu Kristo baada ya kumkubali na kumuamini kama kiongozi wetu mkuu wa wokovu wetu, kubatizwa kwa jina lake Yetu kungemaanisha vilevile kama alivyoagiza, kubatizwa kwa Jina la Baba , Mwana na Roho Mtakatifu, hivyo si sahii katika kanuni ya ubatizo kutaja jina la Yehova tu au jina la Yesu tu, kanuni ya ubatizo inabaki kubatizwa kwa jina la Baba, mwana na Roho, Mtakatifu.
Uatatu wa Mungu ulikuwa ni jambo muhimu sana kutajwa katika nyakati za mitume kwaajili ya kuwakilisha upatikanaji wa neema na ushirika na upendo 2Wakoritho 13:14. Aidha tendo la ubatizo nyakati za Biblia na kama ilivyo maana halisi kibiblia ilikuwa ni lazima lihusishe maji mengi  Yohana 3:22-23”
Ubatizo kwa kuwa ulifanyika katika maji mengi ulihusisha kupandana kushuka kutoka majini, wakati wote Biblia ilipotaja swala la ubatizo au mtu kubatizwa lugha za kushuka na kupanda kutoka kwenye maji zilitawala kama unavyoweza kuona katika mazingira yafuatayo:-

-          Marko 1:9-11
-          Mathayo 3:16
-          Matendo 8: 36-39
-          Matendo 16:13-15
-          Matendo 16:30-34

Sifa ya mtu anayestahili kubatizwa:

Watu wenye sifa ya kubatizwa ni wale ambao kwa moyo wa dhati wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha na wanaishi maisha ya utakatifu sawa na injili ya Bwana Yesu Kristo, ni watu waliomwamini Yesu na wameisikia injili na kuiamini, hao wana sifa ya kubatizwa, Nyakati za kanisa la Kwanza swala la ubatizo liliambatana na maswala makuu matatu yafuatayo;-
1.       Kumwamini Yesu kwa moyo wako wote kuwa ndiye Mwana wa Mungu Matendo 8:36-39
2.       Kuliitia jina la Bwana yaani kuomba Matendo 22:16
3.       Kujiweka wakfu kutoka matendo maovu na kuishi kwaajli ya Mungu 1Petro 3:20-21
Kwa msingi huo mtu mwenye sifa ya kubatizwa anapaswa kuwa na sifa za kuweza kuisikia injili, kusikiliza mahubiri, na kisha kuyaamini na ndipo inapowezekana mtu huyo kubatizwa Marko 16:15-16Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe, aaminiye na kubatizwa ataokoka asiyeamini atahukumiwa” Mtu aliye na sifa za kubatizwa ni lazima awe na uwezo wa kusikia injili na kuipambanua na kuikubali yaani kuiamini na kutubu dhambi zake yeye mwenyewe, ni lazima ahubiriwe, ni lazima aamini ni lazima akiri ni lazima aliitie jina la Bwana, ni lazima asikie kutoka kwa muhubiri Warumi 10:10-17 “10. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. 11. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. 12. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; 13. kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. 14. Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? 15. Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema! 16. Lakini si wote walioitii ile habari njema. Kwa maana Isaya asema, Bwana, ni nani aliyeziamini habari zetu? 17. Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.Utaweza kuona sifa za namna hiyo zikijirudia kwa mkazo katika maandiko unaweza kusoma Matendo 8:36-39, Matendo.2:38-41, Matendo 16:14-15, Matendo 16:29-34. Kwa Msingi huo basi watu wenye sifa ya kubatizwa ni wale wenye uwezo wa kupambanua injili moyoni wenye uwezo wa kujua mema na mabaya. Kwa kuwa watoto wadogo hawana dhambi na hawana ujuzi au wezo wa kupambanua jema au baya na hawana uwezo wa kuamua kuamini au kutokuamini ni wazi tu kuwa ubatizo wa maji mengi hauwahusu  kwa ufupi watoto hawabatizwi, hii haimaanishi kuwa tunawazuia kuja kwa Kristo au kuingia katika ufalme wa Mungu hapana Yesu alisema watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao, kwa msingi huo wanayo tiketi ya kuingia katika ufalme wa Mungu Mathayo 19:13-14 watoto wadogo huwekwa wakfu kwa Mungu katika ibada lakini hawabatizwi wao hubarikiwa tu.Luka 18:15-16.

Namna ya kubatiza.

Yeye anayebatiza na wanaobatizwa watafika nga’mbo ya maji yenye uhai yaani yaliyo safi na yanayotembea na kama ni kisima kiwe kina uwezo wa kuruhusu maji kuingia mapya na yaliyotumika kutoka, wataimba kama sehemu ya ibada na baada ya nyimbo maandiko kadhaa au mojawapo yanayohusiana na ubatizo yatasomwa na kisha Maji yatabarikiwa na eneo la kubatizia litawekwa wakfu, mbatizazi ataingia katika maji mengi na kuhakikisha kuwa anasimama vema mahali ambapo ataweza kuwazamisha wanaobatizwa, wabatizwaji wanaweza kuwa na mavazi maalumu ya kubatiziwa au kuwa na nguo za kubadilisha mara baada ya kubatizwa, aidha ni vema wakaweko wahudumu wenye nguo maalumu ambao watawahifadhi wanaobatizwa mara baada ya kupanda kutoka majini kuwazinga kwa nguo hizo na kuwasindikiza mahali pa kubadilisha nguo kavu, mbatizaji atakapokwisha kuyatakasa maji kwa kuyaweka wakfu, wanaobatizwa watajipanga mstari na kuanza kubatizwa kwa zamu ni vema wahudumu wakawa karibu kabisa na anayebatiza kwaajili ya kutoa msaada wa huduma zinazojitokeza wakati wa ubatizaji kama woga wa maji, kujazwa Roho Mtakatifu wakati wa kubatizwa na kuondoka kwa Pepo wabaya wakati wa kubatizwa haya ni matendo ya kawaida ambayo hujitokeza wakati watu wanabatizwa.
Wanaobatizwa waelekezwe namna ya kujihami wasinywe maji au maji kuwaingia puani, waelekezwe namna ya kuwa wepesi na kutokusababisha kuangukia majini tendo la ubatizaji lifanyike kwa utaratibu bila papara.

Mbatizaji atauliza majina kamili ya anayebatizwa nakama kuna jina jipya analotaka kulituimia kubatizwa kama alitokea katika uislamu na imani nyinginezo
Mbatizaji atamuuliza anayebatizwa kama amemkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi na kama anaamini kazi aliyoifanya Yesu Msalamabani ikiwa ndivyo mbatizaji atatamka yafuatayo
Kwa kuwa …………………..Umemkubali Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako na kuiamini kazi aliyoifanya Msalabani kwaajili yetu

Mimi kwa mamlaka niliyopewa nakubatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu na kisha atamzamisha kwenye maji, mfano wa mtu anayezikwa ardhini na kisha atamtoa katika maji, wakati huu kila sehemu ya mwili wa anayebatizwa itapaswa kuzama kabisa katika maji mfano wa marehemu anavyolazwa, baada ya kitendo hicho utamuinua kwa haraka na kusimama katika hali ya kawaida na kisha utamuombea neema kwa maisha yake na kumbariki katika sehemu ya maisha yake ya wokovu  na kumuacha aende zake.