Jumapili, 16 Agosti 2026

HUDUMA YA USHAURI WA KICHUNGAJI

 

1Petro 5:2 “Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.”




Utangulizi

Moja ya majukumu ya huduma ya kichungaji, ni pamoja na kulichunga kundi na kulisimamia, Neno kulichunga kundi na kulisimamia katika kiyunani yanatumika maneno mawili “Poimainō” na “Episkopeō  ambayo kwa kiingereza yanatafasirika kama “Feed” na “look deligently” ambayo maana yake kwa Kiswahili ni kulisha na kuchunga “look deligently” “Carefully examine”  “seek with total dedication” kufanya uangalizi makini, kuchunguza kwa makini, kutafuta kwa kujidhabihu, kwa msingi huo huduma ya kichungaji sio kuwalisha kondoo peke yake lakini pia kuwachunga yaani kuchunguza kile wanachopitia, wana ugonjwa gani wanapitia changamoto gani kisha kuzitatua kwa upendo hapo ndipo linapokuja swala la kufanya ushauri nasihi, au ushauri wa kisaikolojia ingawa kazi ya ushauri wa kichungaji ni zaidi ya ushauri wa kisaikolojia kwa sababu kuna ukaribu sana na maswala ya  nafsi na roho.Kazi ya ushauri wa kichungaji ni kazi ya kufariji kwa changamoto wanazopitia watu wa Mungu pamoja na kutafuta suluhu kwa pamoja  katika ile changamoto anayopitia mtu husika.

Ayubu 2:11-13 “Basi ikawa hao rafikize Ayubu watatu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikilia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumlilia Ayubu na kumtuliza moyo. Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.”

Ayubu alipopatwa na mabaya, Rafiki zake walitoka kwa kusudi la kusaidia kubeba pamoja naye maumivu yake na kumfariji na kujadiliana naye kwa pamoja ili yamkini waweze kufikia suluhu ya kifalsafa ya swali kubwa linaloulizwa na wanadamu wanapopitia changamoto nini sababu ya mateso na kwa nini yanipate mimi, kufanya huduma ya aina hii ni sehemu ya huduma ya kichungaji ambayo wahudumu, watendakazi, wanafunzi na wenye hekima tunapaswa kuifanya pia kwaajili ya kuwabebea mizigo kondoo wa Bwana wanaopitia changamoto mbalimbali. Huduma hii ni ya malezi, huduma hii ni ya uangalizi, huduma hii ni ya ulinzi dhidi ya kondoo, huduma hii ni ushauri, na kutia moyo

Wagalatia 6:1-2 “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.”

Tutajifunza somo hili ushauri wa kichungaji kwa kuzingatia vipengele vitatu muhimu vifuatavyo:-

 

  • Maana ya Huduma ya ushauri wa Kichungaji
  • Umuhimu wa huduma ya ushauri wa kichungaji
  • Misingi ya Ushauri wa Kichungaji

 

Maana ya Huduma ya ushauri wa Kichungaji

Ushauri wa kichungaji  ni mfumo maalumu wa huduma ya kisaikolojia unaotumia njia za kiroho na kisaikolojia kwaajili ya kumtia mtu moyo kiakili ili kumuwezesha mtu huyo kuchukuliana na mazingira ya changamoto ngumu inayomkabili na kuponya majeraha ya kihisia ambayo kwa kawaida inaathiri maendeleo ya kimwili, kiroho na kiakili, Kimsingi njia za kisaikolojia zinaweza kutumika kumponya mwanadamu kiakili na ndio maana wako wanasaikolojia wanaofanya kazi za ushauri hata hivyo huduma ya kichungaji ya ushauri ina nguvu zaidi kwa sababu haiishii katika akili pekee bali huenda mpaka katika roho na kuleta ufumbuzi wenye manufaa, kwa hiyo ushauri wa kichungaji sio tiba ya kitabibu, wala sio ushauri wa kisaikolojia, bali ni huduma inayolenga kuleta uponyaji wa ndani na kujenga mwelekeo mwema wa maisha, Na ndio maana katika sifa za Yesu Kristo yeye pia anaitwa Msahuri wa ajabu unaona!

Isaya 9:6-7 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina Lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.”

Sio hivyo tu Roho Mtakatifu katika utendaji wake kamili, moja ya shughuli anayoifanya ni pamoja na ushauri nasihi

Isaya 11:1-4 “Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda. Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana; na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake; bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.”

Huduma ya ushauri wa kichungaji huwasaidia watu kihisia, kiroho, na kimaadili na hufanyika kwa kutumia neno la mungu na hekima inayowekwa kwetu na Roho Mtakatifu kwa sababu yeye ndiye anayeyajua mambo ya roho ya mwanadamu na pia anayajua mambo ya Mungu kwa hiyo mtu anayefanya kazi ya ushauri wa kiroho anapaswa kuwa amejazwa Roho Mtakatifu kwaajili ya huduma hii na utumishi huu

1Wakorintho 2:10-14 “Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho Huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Maana Ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.”

Kupitia huduma ya ushauri wa kichungaji Bwana Yesu aliweza kumsaidia kimaadili mwanamke msamaria ambaye kimsingi alikuwa anaishi maisha ya kikahaba huku akichukuwa waume za watu, na kuishi katika usumbufu, wa kisaikolojia, alikuwa akichota maji saa za mchana muda ambao wanawake wengine walikuwa wameacha kwenda kuchota maji, alijihukumu mwenyewe kutokana  na maisha ya ukahaba, japo alikuwa na ufahamu fulani kuhusu kuabudu lakini haikuwa katika njia sahihi, Yesu alipokutana naye alimshauri mambo ya ajabu ambayo yaliweza kabisa kugeuza maisha yake na maisha ya watu wa mji mzima wa Samaria

Yohana 4:4-26 “Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita. Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe. Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula. Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.) Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai? Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake? Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka. Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii! Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye.”            

Ni kupitia huduma ya ushauri wa kichungaji Yesu aliweza kufanikiwa kubadilisha tabia na ufahamu wa kiimani kwa mwanamke Msamaria na Wasamaria wote waliokuja kumsikiliza baada ya ushuda wa kufunguliwa kwa mwanamke huyu, Yako mambo ambayo maombi na maombezi pekee hayatoshi kukamilisha uponyaji wa mtu lakini kupitia ushauri tunaweza kuwafikia watu wa Mungu na kuwasaidia wakapona kiakili kiroho na kisaikolojia, haya yanaweza kufanyika kupitia huduma ya ushauri, kusikiliza, kuuliza maswali na kuelekeza katika ukweli wa mambo!    

Umuhimu wa huduma ya ushauri wa kichungaji.

Kimsingi kila mwanadamu anahitaji ushauri, hakuna mwanadamu anajitosheleza yeye mwenyewe hata kama mwanadamu huyo yuko karibu na Mungu, kuna wakati mtu mwingine anaweza kuliona jambo kwa jinsi nyingine au katika pembe nyingine na akalitolea ufumbuzi, kwa mfano Musa alikuwa akifanya huduma ya ushauri na watu wengi walikuwa wakimuendea, na akawa akiwashauri na kuwaamua, hata hivyo pamoja na haya aliyokuwa akiyafanya kuhani mkuu wa Midian Yethro alikuja na kumshauri kitu cha kufanya ili yeye na watu anaowahudumia  waweze kuwa salama

Kutoka 18:13 -24 “Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na hao watu wakasimama kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni. Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema, Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni? Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu; wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake. Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako. Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao; nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe. Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani.Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.”

Tunajifunza hapo kwamba kila mwanadamu anahitaji ushauri, Musa alikuwa nabii mkubwa sana na mwenye kuzungumza na Mungu uso kwa uso, Lakini alishauriwa na mkwewe namna njema na bora ya kutumika, ni ukweli uliokuwa wazi kuwa Musa peke yake angeumia kuifanya kazi hiyo kwali aliifanya asubuhi mpaka jioni, sisi nasi kama watenda kazi hatuiwezi kuiacha kazi hii mikononi mwa wachungaji pekee ni lazima kundi la watu wa makumi, na mamia na maelelfu waluiofunza kama hivi katika shule ya huduma wahusike pia katika kutoa ushauri wa kichungaji kwa washirika wetu kwani sio kila jambo linaweza kuponywa kutokea madhabahuni, watu wanahitaji kusikilizwa, kuuliza maswali na kujibiwa na kufunguliwa pia kwa njia ya mazungumzo na kusaidiwa sana kiroho huduma hii ni muhimu sana kwa sababu

1.       Inawalinda kondoo wasipotee – kuna makundi makubwa ya watu makanisani yaani katika makanisa ya kiroho wanapotea kimya kimya sababu kubwa ni kukaa na changamoto na kukosa msaada na ushauri wa kichungaji unaoweza kuwatatulia shida zao na kuwarejeza ni kama vile laiti wangelipata mtu wa kuwasikiliza kwa kina!

 

Mathayo 18:12-14 “Mwaonaje? Mtu akiwa na kondoo mia, mmoja akampotea, je! Hawaachi wale tisa na tisini, akaenda milimani, na kumtafuta yule aliyepotea? Hata akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisa na tisini wasiopotea.Vivyo hivyo haipendezi mbele za Baba yenu aliye mbinguni kwamba mmoja wa wadogo hawa apotee.”

 

2.       Ushauri wa kichungaji husaidia kuleta uponyaji wa ndani – wako watu wengi ambao wana maumivu ya ndani, hawaumwi na hawana mapepo, lakini wana maumivu moyoni kwaajili ya mambo yaliyopita, maumivu ya kihisia, na kadhalika ambao wanahitaji uponyaji wa ndani ambao unaweza kuletwa kwao kwa ushauri wa kichungaji kama watumishi wa Mungu tunajihusisha sana na kondoo wa Bwana, Mchungaji biashara yake ni watu, kwa hiyo mtumishi wa Mungu wa ngazi yoyote ile na wa kundi la kiwango chochote kile huduma ya ushauri wa kichungaji inatuhusu, watu wakipata mchungaji wa namna hii watamuamini na kuona kweli unajishughulisha na mambo yao kuchunga ni pamoja na kujishughulisha na maisha ya waamini wetu  na kuwasikiliza na kuwaganga wapone

 

Matendo 20:28 “Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.”

 

Zaburi 23:1-6 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.”

 

3.       Kusaidia kondoo  kufanya maamuzi sahihi – Washirika kama ilivyo kwa kila mtu anahitaji wakati fulani kufanya maamuzi, ulimwengu wa roho una tabia ya kusubiria wakati wa maamuzi kwa sababu wakati huo nafsi ya mwanadamu inaweza kuingia katika uamuzi chanya au uamuzi hasi, kwa sababu hiyo hakuna wakati Muhimu duniani kama wakati wa kufanya maamuzi, kwa sababu hiyo wakati mwingine wanadamu hutafuta mahali sahihi wanapoweza kusaidwa kufanya maamuzi sahihi, kuna maamuzi ya kifamilia, maisha, ndoa, utumishi, kazi, utatuzi wa migogoro, uchaguzi wa mwenza, ununuzi wa vitu vya thamani na kadhalika

 

Zaburi 32:8-10 “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama. Msiwe kama farasi wala nyumbu, Walio hawana akili. Kwa matandiko ya lijamu na hatamu Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia. Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, Bali amtumainiye Bwana fadhili zitamzunguka.”

       

4.       Ushauri wa kichungaji ni ulinzi dhidi ya matukio mabaya – Kwa kutoa ushauri wa kichungaji waamini wanalindwa dhidi ya hisia, usalama, muongozo wa kiroho na kisaikolojia, kanuni na kuinua nia  vyote inakuwa ngao kwa kila mtu, na kuwalinda dhidi ya uharibifu, skendo na kadhalika kwa kuwapa maelekezo sahihi ya kimaandiko au muongozo wa Mungu, kusahihisha, kulinda na hatari, na mafundisho au Imani potofu

 

Matendo 27:21-25 “Na walipokuwa wamekaa wakati mwingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao, akasema, Wanaume, iliwapasa kunisikiliza mimi na kutokung'oa nanga huko Krete, na kupata madhara haya na hasara hii. Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu. Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.”

       

5.       Hujenga uaminifu, upendo na uwajibikaji – Huduma ya ushauri wa kichungaji inajenga uwajibikaji wa wahudumu wa injili kwa washirika wao, lakini pia unapofanikisha mambo yao unajijengea kuaminiwa, na kuunda upendo wa kweli, huduma hii inaashiria kuwa unajali watu, unapenda watu, unaheshimu watu, na unawathamini kwa hiyo washirika watafunguka zaidi kwa kanisa lao na wahudumu wa kanisa lao kwani utawatunzia pia siri zao na kuwaongoza kwa hekima bila kuathiri amani yao kwa hiyo huu ndio moyo wa huduma ya kichungaji

 

1Wakorintho 13:4-8 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.”

       

Misingi ya Ushauri wa Kichungaji

Huduma ya ushauri wa kichungaji ina miiko yake na misingi yake ya kimaadili ni huduma ya muhimu sana lakini inahitaji uangalifu mkubwa kwa sababu hiyo inahitaji sana hekima na maarifa na akili, na ndio maana makanisa mengi yameshindwa kuwa na huduma za namna hii na kuwaacha watu wahangaike kwa mataifa kutafuta ushauri, kwa wanasaikolojia, na washauri wengine, Mungu anatarajia watu wa ndani katika kanisa wawe na hekima ya kufanya maamuzi na mashauri badala ya maswala ya kikanisa kupelekwa kwa mataifa, Hata hivyo kama viongozi na watenda kazi katika kanisa watakosa hekima hii na kuzingatia misingi ya ushauri wa kichungaji watu wanaweza kusema heri kwenda kwa mataifa na sisi tutakuwa tumeshindwa kutimiza wajibu wetu ipaswavyo;-

1Wakorintho 6:1-6 “Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake? Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini.”

Mambo yafuatayo yazingatiwe basi na kila mtenda kazi, mhudumu, mwanafunzi, na wenye hekima katika kanisa

1.       Kusikiliza – anapokuja mtu mwenye majanga yake kwaajili ya kutafuta ushauri wa kichungaji ni vema sana akasikilizwa, mtu mmoja alisema ni kama Mungu ametupa masikio mawili na mdomo mmoja ili tusikilize zaidi kuliko kusema sana, kwa hiyo tujitie nidhamu kumsikiliza mtu ajielezee bila kuwa na kiherehere cha kuzungumza au kujibu kwa haraka ama kudhani kuwa tuna ufumbuzi wa haraka ni muhimu kusikiliza kwanza.

 

Yakobo 1:19 “Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;”

 

2.       Usiri – watu wanachukizwa wakati mwingine na ushauri wa kichungaji hasa katika makanisa ya kipentekoste kwa sababu  wakati mwingine unatoka tu katika chumba cha ushauri tayari habari zako watu wanazo, au unatolewa habari zako madhabahuni kwenye bomba kama mfano  wakati wa mahubiri labda linaweza kuachwa kutajwa jina lako tu hii ni swala linasikitisha sana ni lazima tuwe na moyo wenye kutunza siri au mafriji yanayogandisha, si vizuri siri za mshauriwa zikatoka nje au kufanyiwa masimulizi au mifano utoaji wa siri huharibu huduma hii, kama madaktari wanavyoficha siri tunza siri za watu, hatupendi kusikia nimekuambia tafadhali usije ukamwambia mtu, na mwingine unamsikia aliyeniambia kaniambia nisimwambie mtu lakini wakati huo huo habari zimeenea

 

Mithali 11:12-14 “Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.”

 

Mithali 25:2 “Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.”

 

3.       Zingatia mahusiano – Ni vema kujihami kwa sababu katika kutoa ushauri wa kichungaji kumejitokeza changamoto za aina nyingi na ndio maana watumishi wengine wa Mungu hawapendi kufanya huduma hii, jilinde, mlinde na anayekuja kushauriwa msikae faragha sana, epukeni ukaribu wa kimwili na kihisia usiofaa, zingatia kulinda uhusiano na jinsia tofauti kwa tahadhari kubwa ili kujiepusha na kashfa na skendo za aina mbalimbali, Paulo amabye hakuwa na mke alifanya kazi pamoja na Prisila na Akila waliokuwa mume na mke kwaajili ya kutunza ushuhuda ili neno la Mungu lisitukanwe!

 

1Wathesalonike 5:22-23. ”jitengeni na ubaya wa kila namna. Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.”

 

Waefeso 5:3-5 “Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wowote wala wa kutamani kama iwashtahilivyo watakatifu, wala aibu wala maneno ya upuuzi wala ubishi; hayo hayapendezi bali afadhali kushukuru, maana neno hili mnalijua hakika ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu

 

Matendo 18:18 “Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri.”

 

4.       Usiutumie ushauri kwa manufaa binafsi – kutokana na huduma hizi kuwa adimu na huduma ya kichungaji ya ushauri kutolewa bure watumishi wengi wa Mungu wamekuwa wakijinufaisha kifedha na kuwatoza watu fedha nyingi hasa wale wanaotaka kuwaona uso kwa uso kwaajili ya Ushauri, kamwe usitumie huduma hii kama njia ya kujinufaisha, kuchukua rushwa, na kuteka watu kingono, au kuwatawala watu, kuwaendesha na kudhibiti nafsi zao hilo jambo sio la haki, aidha ni muhimu kujilinda kwa sababu wakati mwingine yule unayempa ushauri anaweza kuwa ni majibu ya tatizo lako binafsi wewe mtoa ushauri, na mkajikuta manajaribiwa kwa kuwa majibu ya kila mmoja kwa mwenzake.

 

2Wakorintho 2:15-17 “Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo? Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo.”

                       

5.       Tambua mipaka ya kihuduma - Unapokuwa umesikiliza vya kutosha wale tunaowahudumia unaweza kugundua kuwa kuna maswala mengine huwezi kuwa na majibu nayo, hayo yanaweza kuwa yanahitaji madaktari au wana saikolojia, kwa hiyo unaweza kumuelekeza mtu aende sehemu sahihi kulingana na changamoto yake na kufanya hivyo sio kushindwa kwa sababu sisi tunashughulikia maswala ya kiroho, Yesu aliweza kumfufua Lazaro  lakini swala la kumfungua sanda haikuwa kazi yake, na Yesu aliweza kumfufua binti Yairo lakini kazi ya kumpa chakula haikuwa ya kwake, unapotoa ushauri fanya eneo lako ambalo kimsingi ni la kiroho na kisaikolojia kwa sehemu na mengine kama yako nje ya uwezo wako mpeleke kunakohusika, mfano Menopouse na Andrepouse Ukomo wa hedhi na changamoto zake na   ukomo wa uzazi kwa wanaume  yanaweza kuzungumzwa na wataalamu wa afya

 

Yohana 11:41-44 “Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.”

 

Marko 5:39-43 “Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu.Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu. Akawaonya sana, mtu asijue habari ile; akaamuru apewe chakula.”

 

6.       Uwe muadilifu – huduma ya ushauri inahitaji uwe mwadilifu, wakati mwingine kile unachikishauri inawezekana kikasababisha uwe majibu ya yule unayemshauri, mfano anakuja mwanamke mzuri tu na anakuletea kesi kuwa mumewe hamridhishi kwenye tendo la ndoa, na wewe mhudumu una changamoto nyumbani unanyimwa tendo la ndioa na mkeo au nawe huridhishi unajikuta majibu ya changamoto yako yako kwa mteja wako bila uadilifu binafsi huduma hii inaweza kukuweka pasipo, au unaweza kushauri kwa uchungu mfano anakuja mwanaume ambaye ananyimwa tendo la ndoa na wewe ni muhanga wa kunyimwa unaweza kujikuta mnaungana kuwachukia wanawake uadilifu ni nyenzo muhimu, jilinde na mjaribu, jilinde na tuhuma jilinde na kusingiziwa,

 

1Timotheo 3:2-5 “Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) 

 

Wagalatia 6:1-2 “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.”

 

Hitimisho

 

Huduma hii ni ya moyo, ni huduma ya usikivu, ni huduma ya huruma, ni huduma ya kujali, ni huduma ya uaminifu, ni ulinzi wa kondoo wa Bwana hatuna budi kumuomba Mungu atupe moyo wa huruma ili tuwahudumie watu wake. uwe na watu karibu ili kama mshauriwa atakuwa na pepo kuwe na msaada wa kihuduma wakati pepo zinakemewa na kutolewa ikiyajua hayo heri wewe ukiyatenda !

 

Yeremia 3:15 “nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu.”

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

 

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatano, 12 Agosti 2026

HUDUMA KATIKA VITUO VYA KUZALISHA NGUVU (POWER HOUSE)


Matendo 4:31-33 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.”




Utangulizi:

Neno la Mungu linatuonyesha ya kuwa nyakati za kanisa la kwanza Mitume walikuwa na kundi la watu waliokuwa wanawaombea, wao walikuwa kama askari wa mstari wa mbele katika kuihubiri injili na walipopata mashambulizi walitoa taarifa kwa kanisa na Kanisa liliwaombea kulingana na mashambulizi waliyoyasikia au kuyapata ona kwa mfano katika mistari hii ya Biblia utangundua kuwa kazi ya Mungu na watumishi wa Mungu wanapaswa kuombewa

Matendo 4:18-33 “Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka; maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya kuponya ulipita miaka arobaini. Hata walipofunguliwa, wakaenda kwa watu wao, wakawapasha habari ya mambo yote waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee. Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili? Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika.Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.”                

 

Matendo 12:1-5 “Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.”

Maombi ndio asili ya nguvu ya maswala yote ya kiroho katika kanisa la Mungu, na kwa sababu hiyo kila kanisa linalotaka kuwa na mafanikio katika kazi ya kuhubiri injili linapaswa kuwa na kiwanda cha kuzalisha maombi, kiwanda hiki ni nyumba ya kuzalisha nguvu yaani Power house, Katika dunia ya maendeleo ya viwanda na uchumi mwenye nguvu ni yule mwenye kuzalisha umeme wa uhakika, kwa hiyo kanisa ni lazima tuwe na viwanda vya kutosha kuzalisha umeme au nguvu na viwanda hivyo au kiwanda hicho ni katika dunia ya kawaida vinaitwa Power House, Power house ni kituo cha kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme na kusambaza katika maeneo mengine na kusababishwa mwanga, uhai, na harakati nyinginezo sasa kanisa linapaswa kuwa na Power House. Kwa msingi huo tunajifunza somo hili sasa Huduma katika vituo vya kuzalisha Nguvu (Power House) Kwa kuzingatia vipengele vitatu

·         Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu (Power House)

·         Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu (Power house)

·         Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power House)

Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu (Power House)

Kama tulivyojifunza katika utangulizi kuwa neno Power House au nyumba ya kuzalisha nguvu ni kituo kinachohusika na uzalishaji wa umeme unaoingizwa katika gridi ya taifa kwaajili ya kuleta Nuru, nguvu na kusababisha michakato ya maendeleo endelevu kuchukua nafsi yake katika inchi, katika msingi kama huo, kanisa likiwa na vituo vya maombi ni sawa na taifa kuwa na vituio vya kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme, Kituo cha maombi huzalisha nguvu za Mungu kutoka mbinguni na kusababisha mwenendo na utendaji mzima wa kanisa kufanya kazi kwa mpenyo na kwa njia rahisi, kanisa ni matokeo ya chumba cha maombi

Matendo 1:12-14. “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato. Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.”

Unaweza kuona kuwa kanisa lilizaliwa kama matokeo ya Maombi, wakati watu hawa wakiomba katika chumba cha juu, hapo ndipo mahali ambapo Nguvu za Mungu ziliachiliwa na watu wakajazwa Roho Mtakatifu na kazi ya Mungu ikaanza kuenea duniani tangu wakati ule hata leo,

Matendo 2:1-4 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.”            

Wakati wote tumeona kuwa Mungu alianzisha jambo wakati ambapo alikuwepo mtu anaomba, Petro alipokuwa anaomba na Kornelio naye alipokuwa katika kuomba Mungu aliweka mfumo wa kuwakutanisha watu hawa na watu wa Kornelio wakajazwa Roho Mtakatifu, kazi ya Mungu ikazidi kuenea haya yote yalisababishwa na mtu Fulani kujichimbia katika chumba cha maombi na kutoa muda wake au hata kuacha kula na kuruhusu utendaji wa Mungu Roho Mtakatifu katika kazi yake ambaye kimsingi ndiye Bwana wa Mavuno!

Matendo 10:1-6 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro. Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda.”

Matendo 10:9-13 “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana; akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia, akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi; ambayo ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao, na ndege wa angani. Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule.”

Matendo 10:44-48 “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu, Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi? Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.”

Watu wa Mungu wanapojichimbia mahali Fulani kuomba kwa bidii, Mungu husababisha matukio makubwa sana ya kushangaza, hufumua nguvu za utendaji na nguvu za Roho wake Mtakatifu na kusababisha uamsho mkubwa au kuleta muelekeo au kufungua mlango wa injili au kusababisha usikivu wa kiungu na kutoa melekezo na kusababisha mfumuko mkubwa sana wa kazi ya Mungu duniani, lakini haya yote husababishwa na watu wanaoomba yaani watu wanapojifungia katika chumba cha maombi na kuomba kwa bidii

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

Kwa hiyo pamoja na kanisa kuwa na mfumo wa huduma ya makanisa ya nyumbani ambayo kimsingi yanaweza kuwa yanakutana labda siku ya jumamosi (kulingana na makubaliano ya kanisa) na itakuwa vema basi siku kama alhamisi ikawa ni siku ya maombi kwaajili ya huduma zote za kanisa (Power House) huku jumatono ikiwa ni siku ya mafundisho na ijumaa ikiwa siku ya maombi na maombezi na jumapili ikiwa ni siku ya Bwana vyovyote kwa kadiri ya neema ya kila kanisa lakini nilisisitizalo mimi ni uwepo wa Nyumba za kuzalisha nguvu (Power Houses) na viongozi. Kanisa lolote lile linalotaka maendeleo bila ya kuwa na Power House haliwezi kuwa na mwanga, wala haliwei kuwa na uhai, wala hakutakuwa na harakati, na mpango kazi na mkakati wa kanisa itageuka kuwa mipango ya kawaida tu ya kibinadamu, kama unamtaka Bwana na nguvu zake basi anapatikana katika nyumba za maombi.(Power Houses)

Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu (Power house)

Mpaka hapo umeanza kupata picha kwamba ni muhimu kwa kanisa kuwa na vituo vya maombi, hata kama maombi hayo hufanyika ndani ya saa moja tu kati ya saa kumi na moja jioni hata saa kumi na mbili jioni, Lakini tunatambua sasa uhai wa kanisa lolote lile ni maombi, uamsho wa aina yoyote hauwezi kuendelea pasipo maombi, nguvu za Mungu na utendaji wa Mungu hauwezi kuendelea kuwepo katika kanisa bila ya maombi, hamna kitu kwa sababu hamwombi, lolote tunalilitaka lifanyike katika kanisa lazima kuwe na watu wanaooomba, maombi, maombi maombi.

·         Power House hufungua mbingu – Neno la Mungu linaonyesha kuwa Mungu huwa anafunga mbingu, habari ya kuzifunga mbingu ilikuwa inajulikana tangu zamani za kale nyakati za Biblia kuwa Mungu anaweza kuzifanya mbingu kuwa ngumu, anaweza kuzifunga wakati mwingine kama matokeo ya watu kutokutii lakini kupitia maombi inaonekana wazi kuwa Mungu anaweza kuzifungua mbingu:-

 

1Wafalme 8:35-39 “Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa; basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao. Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote; maombi yo yote au dua yo yote ikifanywa na mtu awaye yote, au na watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo wake, na kuikunjua mikono yake kuielekea nyumba hii; basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote);”

 

Kumbukumbu 28:23-25 “Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma. Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie. Bwana atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.”

 

2Nyakati 7:13-15 “Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”

 

Neno la Mungu linaonyesha kuna wakati Mungu huzifunga mbingu, na hii maana yake sio kwaajili ya mvua tu lakini Mungu anaweza hata kuzifunga mbingu za mtu mmoja mmoja na hata mbingu za kanisa Fulani na kama tunataka kuona mkono wa Mungu ukitusaidia basi “Power houses” zinaweza kuwa sababu ya kufunguliwa kwa milango hii ambayo imefungwa, kwa nguvu za Maombi Mungu huzifungulia mbingu

 

Luka 3:21-22 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”

 

·         Power House ni Chanzo cha nguvu za utumishi – Tumetumwa kama kondoo katikati ya mbwa mwitu hatari, ni kauli inayoonyesha kuwa watu wa Mungu wana maadui wasioonekna na wanaoonekana, kwa sababu hiyo kila aliyetumwa na Mungu alipewa nguvu kwaajili ya kukabiliana na upinzani tunaita Power encounter, shetani ni mpinzani wa injili, wachawi na kadhalika hatuwezi kwenda bila nguvu za Mungu na tunazihitaji nguvu za Mungu wakati wote na ni wapi tunaweza kupata/au kuzalisha nguvu kwaajili ya utumishi huu ni katika nyumba  za mombi “Power houses” ni chumba cha maombi ndicho kinachoweza kutupa nguvu na ujasiri wa kukabiliana na aina yoyote ile ya upinzani wa kiinjili na maendeleo endelevu ua utumishi tuliopewa

 

Luka 4:1-2 “Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.”

 

Matendo 1:8 “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”

 

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”

 

Mafundisho yetu ili yaweze kubadilisha maisha ya watu ni lazima yaombewe na kinyume cha hapo yatakuwa nadharia tu, huduma yetu ili iendelee kuleta matokeo chanya inapaswa kujaziwa na maombi, huduma ikifanyika bila ya maombi ya kutosha mwili tu ndio utakaokuwa umefanya kazi yake tunahitaji nyumba ya uzalishaji wa nguvu za Mungu katika maisha yetu ya kiroho ili mambo yaende!

 

·         Power House ni ulinzi wa Kanisa -  Ni muhimu kufahamu kuwa maombi pia hufanya kazi ya kuweka ulinzi wa rohoni, hutulinda na yule muovu, hutuepucha na majaribu, huzuia mashambulizi ya adui, hufunika wahudumu, watendakazi, wachungaji na familia zao na mali zao kwa hiyo tunayahitaji maombi kama tunavyohitaji maji ya kunywa , Lazima watu waombe na kusimama katika zamu yao kama walinzi wa rohoni

 

Matendo 12:5-7 “Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi.”

 

Mathayo 6:13 “ Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

 

Mathayo 26:40-41 “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”

 

Habakuki 2:1-3 “Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.”       

 

·         Power House huvunja minyororo – Maombi ni silaha ya kiroho inayovunja vunja nira yaani vifungo na minyororo ya aina mbalimbali, maombi huwatoa watu utumwani na kuwaweka huru walikandamizwa, yanaondoa mizigo mizito na kuwapa watu uhuru na raha ya kiungu, yanavunja laana ya kizazi na kizazi, kurejesha uhuru wa kiroho, upako huo wa kuvunja nira unapatikana kwa njia ya maombi, maombi yanaweza kufungua mpaka magereza za kawaida  na kuvunja hata nira za chuma

 

Isaya 10:27 “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.”

 

Isaya 58:6 “.Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

 

Matendo 16:25-31 “Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa. Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”             

 

·         Power House ni nguvu ya kupokea maelekezo na muelekeo – hatuwezi kwenda wenyewe, hatuwezi kwenda peke yetu, tunamuhitaji Mungu atupe muelekeo na maelekezo katika kazi yake ni katika wakati wa kuomba mbele zake na utulivu ndipo ambapo Mungu hutupa muelekeo na maelekezo, kwa hiyo kanisa ni muhimu kwetu kuwa na vituo vya kuzalisha nguvu yaani Power House ili tusiongozwe na mawazo yetu bali tuongozwe na Roho Mtakatifu ili tuweze kuifanya kazi yake kwa usahihi, kanisa lisilo na power house huongozwa na mawazo ya wanadamu na kanisa lenye power House huongozwa na Roho Mtakatifu

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

Matendo 16:6-10 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemkia Troa. Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.”                

Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power House)

Watenda kazi wetu, wahudumu, wanafunzi na wenye hekima wote wanapaswa kusimamia kwa uaminifu vituo vya maombi ya kuzalisha nguvu kokote viliko, ni afadhali kitu kingine kisimame lakini sio maombi Kanisa hatuna budi kuhakikisha kuwa maombi yetu yanakuwa endelevu, na tuone kusimama kwa maombi kama kusimama kwa moyo katika mwili wa mwanadamu ndio maana maombi yanapaswa kuendelea “Ombeni bila kukoma”, watu wote waombaji wanapaswa kuwa watu wa toba, wenye kujitia nidhamu kwaajili ya kuomba, wanaopenda kusihi maisha matakatifu, wenye tabia ya unyenyekevu na wanaojua kukaa kimya mbele za Mungu, aidha waombaji hawapaswi kuwa na midomo michafu kwa sababu midomo hiyo hiyo ndio inayotumika kuomba hivyo haifai kutumika kwenye mambo mengine hasa yasiyofaa katika mapenzi ya Mungu.

Yakobo 3:10-12 “Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.”

Watendakazi wetu walioandaliwa katika shule za uongozi na huduma ndio watakaohusika na kituo cha kuongoza maombi ya Power house maombi haya yataongozwa kila wakati katika siku na muda utakaokuwa umepangwa na kanisa

1.       Toba litakuwa jambo  la kwanza na la muhimu katika maombi

2.       Kurekebisha Mahusiano kutakuwa ni jambo muhimu katika hatua za maombi

3.       Kufunga itakuwa ni sehemu mojawapo ya muhimu katika maombi yetu

4.       Shukurani itakuwa ni sehemu muhimu ya maombi

5.       Toba za kila mtu binafsi, kwa niaba ya kanisa na kwaniaba ya taifa itahusika

6.  Tutaomba uwepo wa Mungu, Nguvu zake, huduma na kuombea wachungaji watumishi wote na watendakazi, Mungu awalinde awatumie na kuwapa afya njema

7.       Tutakemea na kuvunja nguvu za giza, kukemea mapepo na kutangaza ushindi

8.    Tutaombea kanisa, miji yetu na taifa, tutamuomba Mungu aponye wanaoteseka na kufanya ishara na miujiza akichochea karama za Roho, aokoe na kuponya na kurahisisha kazi yake kotekote

9.       Tutamsikiliza Mungu na kukaa kimya kusubiri maelekezo yake   

Power house ni tofauti na kikundi maalumu cha maombi, hii ni kiungo au kiwanda cha kuzalisha waombaji katika kanisa hivyo inapaswa kulishirikisha kanisa zima katika mfumo kama ule wa makanisa ya nyumbani,  Neno la Mungu linapaswa kuwa muongozo wa maombi haya, “Power house” sio mashindano ya kuomba, wala sio sehemu ya kujitukuza na kuonyesha uhodari wa kuomba, wala sio sababu ya kutokutii uongozi wa kanisa, ni kituo cha nidhamu kinachoomba kwaajili ya maswala mbalimbali ya kazi ya Mungu, hakipaswi kuwa chanzo cha machafuko, ni sehemu ya upendo kwa Mungu na kwa kazi yake, ni ushirika wa maombi ya washirika wote na wageni wanaopenda kujiunga kuomba nasi, Bwana ampe neema kila mtenda kazi kulijua hili na kulifanyia kazi katika jina la Yesu Ameen

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumapili, 9 Agosti 2026

JINSI YA KUANZISHA KANISA LA NYUMBANI


Mathayo 18:18-20 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”




Utangulizi:

Tumejifunza huduma ya makanisa ya nyumbani na tumeona faida zake kwamba Mungu anaheshimu makusanyiko yetu yanayojenga umoja upendo na ushirikiano, Lakini sasa hatuna budi kwenda ndani zaidi na kujifunza kivitendo sasa namna ya kustawisha Kanisa la nyumbani, sasa tunaweza je kuanza Kanisa la nyumbani

1.       Ni lazima kumuomba Mungu – Kila kitu katika ulimwengu wa roho kinaweza kupata ufunguzi endapo kitaanza na maombi, Nyakati za kanisa la kwanza Paulo mtume na wengineo watenda kazi pamoja naye waliweza kuifanya kazi kubwa ya Mungu ambayo kimsingi ilianzia katika maombi, kila kitu cha kiroho ni matokeo ya maombi kwa hivyo tunapotaka kuanzisha kanisa la nyumbani ni lazima tumuombe Mungu na Mungu atatoa muongozo na kutupa neema na mpenyo wa jinsi ya kunzisha makanisa hayo.

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

Mathayo 9:36-38 “Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”

 

2.        Kufanya utafiti wa mitaa na kubainisha vigezo – ili tuweze kuufikia mji kimkakati na kihuduma hatuna budi kufanya utafiti, wa kina kuhusu mitaa ambayo tunalenga kufungua kanisa la nyumbani na kubainisha vigezo vitakavyotusaidia kuweka makanisa ya nyumbani, katika maandiko tunaona kwamba Israel walipotaka kuirithi nchi ya kanaani walituma wapelelezi kuangalia nchi, kwa hiyo ni muhimu kufanya survey (ulinganifu na utafiti) wa kujua wapi tunaweka nini na nani anaweza kufika eneo Fulani na kanisa linaweza kuwa wapi, kwa mfano kama eneo husika ni wanajeshi, au askari ni nani anaweza kutuwakilisha katika eneo hilo, ama kuna chuo kikuu ni nani anaweza kutuwakilisha katika eneo hilo au ni uzunguni, uswahilini na kadhalika ni muhimu kujua ni watu gani tunawafikia ili tuweze kukidhi vigezo vyao, kwa mfano kama eneo ni la wasomi wa vyuo vikuu na likawako kanisa la nyumbani huko, mtendakazi atakayepelekwa kusimamia atakuwa ni yule anayeendana na vigezo vya eneo husika, Kanisa lazima tufanye mambo kwa kutumia busara na akili, tujue idadi ya watu  hasa washirika wetu na ile jamii ya wale tunaotaka kuwafikia ni wa aina gani !

 

Hesabu 13:17-20 “Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani, mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;”

 

Yoshua 2:1-2 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko. Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.

 

Yoshua 7:2-3 “Kisha Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko mpaka mji wa Ai, ulio karibu na Bethaveni, upande wa mashariki wa Betheli, akawaambia, akisema, Pandeni juu mkaipeleleze nchi, basi wakapanda juu wakaupeleleza Ai. Wakarejea kwa Yoshua wakamwambia, Wasiende watu wote, ila waende watu kama elfu mbili, tatu, wakaupige Ai; usiwataabishe watu wote kwa kuwaendesha huko; maana watu hao ni wachache tu.”

                       

3.       Tutambue nyumba na mwenyeji wetu – Kanisa la nyumbani linaitwa la nyumbani kwa sababu linafanyia ibada zake katika sebule za watu, kila mtu anaustaarabu wake na anaipenda sebule yake, kwa hiyo kukaribisha watu katika sebule yako ili kufanyike ibada ni kujitoa katika hali ya juu sana sio swala jepesi, lakini jambo hili Mungu analiheshimu na kusababisha Baraka, utoaji wa nyumba au mahali kwaajili ya kuabudia linapaswa kuwa jambo la hiyari na sio la kulazimishwa, mtu anayejitoa nyumba yake sio lazima iwe nzuri au kamili bali anaitoa kwaajili ya Bwana mtu huyu Mungu atamheshimu sana na kumbariki mno, Mungu aliibariki nyumba ya Oded-Edom kwa sababu alikubali Sanduku la Agano la Bwana Mungu wa Israel likae nyumbani mwake, Mtu anayekubali nyumba yake iwe sehemu ya kufanyia ibada hana tofauti na Obedi- Edom

 

Luka 10:5-7 “Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.”

 

2Samuel 6:10-12. “Basi Daudi hakutaka kulileta sanduku la Bwana kwake mjini mwa Daudi; ila Daudi akalihamisha nyumbani kwa Obed-edomu, Mgiti. Sanduku la Bwana akalitia katika nyumba ya Obed-edomu, Mgiti, muda wa miezi mitatu; naye Bwana akambarikia Obed-edomu, na nyumba yake yote. Kisha mfalme Daudi akaambiwa ya kwamba, Bwana ameibarikia nyumba ya Obed-edomu, na vitu vyote alivyo navyo kwa ajili ya sanduku la Mungu. Daudi akaenda, akalileta sanduku la Mungu, toka nyumba ya Obed-edomu mpaka mji wa Daudi, kwa shangwe.”

 

4.       Weka viongozi waliopitia shule ya huduma – Baada ya kuwa tumepata haya yote tunaweka viongozi wetu ambao wamejifunza kutoka kwetu wana mafundisho yetu yaliyo sahihi, walio waaminifu kwetu, wanaotii uongozi, wanaojua kuhudumia watu wenye Imani yetu, viongozi hao ni viongozi watumisi na sio wachungaji wenye mamlaka kamili ya kichungaji

 

Matendo 14:21-23 “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.”

 

Mfumo wa ibada katika makanisa ya nyumbani haupaswi kuzidi saa moja

  1. Utafungua kwa maombi.
  2. Itafanyika ibada ya kusifu na kuabudu kwa ufupi.
  3. litahubiriwa neno la Mungu la kibiblia na sio maoni ya mtu (sawa na mafundishio katika kanisa letu) tunakuwa na mafundisho maalumu na tutayagawa kwa walimu wa makanisa ya nyumbani na watafundisha kwa kadiri watakavyokuwa wanapangiwa na kiongozi husika.
  4. Ushirika, maswali, maombi na maombezi, na taarifa za ufuatiliaji.
  5. Kufunga kwa maombi.  

 

Hakuna kanisa la nyumbani linalotakiwa kujiendesha kinyume na utaratibu uliowekwa na kanisa mama ambalo ndilo lenye mamlaka ya mwisho.

Kama kanisa la nyumbani litakapokuwa kubwa taarifa itatolewa na litalazimika kugawanywa na kuwa na kiongozi mwingine aliyepitia shule ya huduma

Kiongozi wa kanisa la nyumbani jihadhari na mafundisho potofu. Jilinde na uasi au kulikata kundi, jihadhari kuligeuza kanisa kuwa klabu ya maswala ya kijamii na michango ya upatu kila kitu kifanyike kwakufuata utaratibu usafi na ushuhuda mwema wa Kirsto

Kanisa la nyumbani sio mfumo au wazo jipya ni mpango wa Mungu wa kibiblia tangu zamani za mitume na kwa kufanya hivi waliupindua ulimwengu

Kama ilivyo kwa watenda kazi kiongozi wa kanisa la nyumbani atawajibika kutoa taarifa katika mfumo utakaowekwa na kanisa kuu.

1Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”

Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!