Matendo 4:31-33 “Hata walipokwisha kumwomba
Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu,
wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na
moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote
alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. Na
mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema
nyingi ikawa juu yao wote.”
Utangulizi:
Neno la Mungu linatuonyesha ya
kuwa nyakati za kanisa la kwanza Mitume walikuwa na kundi la watu waliokuwa wanawaombea,
wao walikuwa kama askari wa mstari wa mbele katika kuihubiri injili na
walipopata mashambulizi walitoa taarifa kwa kanisa na Kanisa liliwaombea
kulingana na mashambulizi waliyoyasikia au kuyapata ona kwa mfano katika
mistari hii ya Biblia utangundua kuwa kazi ya Mungu na watumishi wa Mungu
wanapaswa kuombewa
Matendo 4:18-33 “Wakawaita, wakawaamuru
wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu. Petro na Yohana wakawajibu
wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu,
hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona
na kuyasikia. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya
kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu
kwa hayo yaliyotendeka; maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya
kuponya ulipita miaka arobaini. Hata walipofunguliwa, wakaenda kwa watu wao,
wakawapasha habari ya mambo yote waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee.
Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola,
wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote
vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi,
mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili?
Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na
juu ya Kristo wake. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa
na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu
Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako
yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao;
ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako
kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu.
Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote
wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu
walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya
kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu
vyote shirika.Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu
nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.”
Matendo 12:1-5 “Panapo majira yale yale Herode
mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua
Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi
akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha
kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne
wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi
Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili
yake.”
Maombi ndio asili ya nguvu ya
maswala yote ya kiroho katika kanisa la Mungu, na kwa sababu hiyo kila kanisa
linalotaka kuwa na mafanikio katika kazi ya kuhubiri injili linapaswa kuwa na
kiwanda cha kuzalisha maombi, kiwanda hiki ni nyumba ya kuzalisha nguvu yaani Power house, Katika dunia ya maendeleo
ya viwanda na uchumi mwenye nguvu ni yule mwenye kuzalisha umeme wa uhakika, kwa
hiyo kanisa ni lazima tuwe na viwanda vya kutosha kuzalisha umeme au nguvu na
viwanda hivyo au kiwanda hicho ni katika dunia ya kawaida vinaitwa Power House,
Power house ni kituo cha kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme na kusambaza
katika maeneo mengine na kusababishwa mwanga, uhai, na harakati nyinginezo sasa
kanisa linapaswa kuwa na Power House. Kwa msingi huo tunajifunza somo hili sasa
Huduma katika vituo vya kuzalisha Nguvu (Power
House) Kwa kuzingatia vipengele vitatu
·
Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu
(Power House)
·
Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu
(Power house)
·
Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power
House)
Maana ya kiroho ya Nyumba za kuzalisha nguvu (Power House)
Kama tulivyojifunza katika
utangulizi kuwa neno Power House au nyumba ya kuzalisha nguvu ni kituo
kinachohusika na uzalishaji wa umeme unaoingizwa katika gridi ya taifa kwaajili
ya kuleta Nuru, nguvu na kusababisha michakato ya maendeleo endelevu kuchukua
nafsi yake katika inchi, katika msingi kama huo, kanisa likiwa na vituo vya
maombi ni sawa na taifa kuwa na vituio vya kuzalisha nguvu ya nishati ya umeme,
Kituo cha maombi huzalisha nguvu za Mungu kutoka mbinguni na kusababisha
mwenendo na utendaji mzima wa kanisa kufanya kazi kwa mpenyo na kwa njia
rahisi, kanisa ni matokeo ya chumba cha maombi
Matendo 1:12-14. “Kisha wakarudi kwenda
Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu,
wapata mwendo wa sabato. Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa
wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo
na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.Hawa wote
walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu
mama yake Yesu, na ndugu zake.”
Unaweza kuona kuwa kanisa
lilizaliwa kama matokeo ya Maombi, wakati watu hawa wakiomba katika chumba cha
juu, hapo ndipo mahali ambapo Nguvu za Mungu ziliachiliwa na watu wakajazwa
Roho Mtakatifu na kazi ya Mungu ikaanza kuenea duniani tangu wakati ule hata
leo,
Matendo 2:1-4 “Hata ilipotimia siku ya
Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi
kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa
wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia
kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha
nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.”
Wakati wote tumeona kuwa Mungu
alianzisha jambo wakati ambapo alikuwepo mtu anaomba, Petro alipokuwa anaomba
na Kornelio naye alipokuwa katika kuomba Mungu aliweka mfumo wa kuwakutanisha
watu hawa na watu wa Kornelio wakajazwa Roho Mtakatifu, kazi ya Mungu ikazidi
kuenea haya yote yalisababishwa na mtu Fulani kujichimbia katika chumba cha
maombi na kutoa muda wake au hata kuacha kula na kuruhusu utendaji wa Mungu
Roho Mtakatifu katika kazi yake ambaye kimsingi ndiye Bwana wa Mavuno!
Matendo 10:1-6 “Palikuwa na mtu Kaisaria,
jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa
Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na
kumwomba Mungu daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana,
malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa
akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na
kuwa ukumbusho mbele za Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni,
aitwaye Petro. Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa
ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda.”
Matendo 10:9-13 “Hata siku ya pili,
walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda
kuomba, yapata saa sita ya mchana; akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini
walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia, akaona mbingu zimefunuka, na chombo
kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi; ambayo
ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao,
na ndege wa angani. Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule.”
Matendo 10:44-48 “Petro alipokuwa akisema
maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. Na wale
waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro,
kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa maana
waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu, Ni
nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile
vile kama sisi? Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi
azidi kukaa siku kadha wa kadha.”
Watu wa Mungu wanapojichimbia
mahali Fulani kuomba kwa bidii, Mungu husababisha matukio makubwa sana ya
kushangaza, hufumua nguvu za utendaji na nguvu za Roho wake Mtakatifu na
kusababisha uamsho mkubwa au kuleta muelekeo au kufungua mlango wa injili au
kusababisha usikivu wa kiungu na kutoa melekezo na kusababisha mfumuko mkubwa
sana wa kazi ya Mungu duniani, lakini haya yote husababishwa na watu wanaoomba
yaani watu wanapojifungia katika chumba cha maombi na kuomba kwa bidii
Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika
kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni
aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa
mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na
kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile
niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao,
wakawaacha waende zao.”
Kwa hiyo pamoja na kanisa kuwa na
mfumo wa huduma ya makanisa ya nyumbani ambayo kimsingi yanaweza kuwa
yanakutana labda siku ya jumamosi (kulingana na makubaliano ya kanisa) na
itakuwa vema basi siku kama alhamisi ikawa ni siku ya maombi kwaajili ya huduma
zote za kanisa (Power House) huku jumatono ikiwa ni siku ya mafundisho na
ijumaa ikiwa siku ya maombi na maombezi na jumapili ikiwa ni siku ya Bwana
vyovyote kwa kadiri ya neema ya kila kanisa lakini nilisisitizalo mimi ni uwepo
wa Nyumba za kuzalisha nguvu (Power Houses) na viongozi. Kanisa lolote lile
linalotaka maendeleo bila ya kuwa na Power House haliwezi kuwa na mwanga, wala
haliwei kuwa na uhai, wala hakutakuwa na harakati, na mpango kazi na mkakati wa
kanisa itageuka kuwa mipango ya kawaida tu ya kibinadamu, kama unamtaka Bwana
na nguvu zake basi anapatikana katika nyumba za maombi.(Power Houses)
Umuhimu wa kuwa na Nyumba za kuzalisha nguvu (Power house)
Mpaka hapo umeanza kupata picha
kwamba ni muhimu kwa kanisa kuwa na vituo vya maombi, hata kama maombi hayo
hufanyika ndani ya saa moja tu kati ya saa kumi na moja jioni hata saa kumi na
mbili jioni, Lakini tunatambua sasa uhai wa kanisa lolote lile ni maombi,
uamsho wa aina yoyote hauwezi kuendelea pasipo maombi, nguvu za Mungu na
utendaji wa Mungu hauwezi kuendelea kuwepo katika kanisa bila ya maombi, hamna
kitu kwa sababu hamwombi, lolote tunalilitaka lifanyike katika kanisa lazima
kuwe na watu wanaooomba, maombi, maombi maombi.
·
Power
House hufungua mbingu – Neno la Mungu linaonyesha kuwa Mungu huwa anafunga
mbingu, habari ya kuzifunga mbingu ilikuwa inajulikana tangu zamani za kale
nyakati za Biblia kuwa Mungu anaweza kuzifanya mbingu kuwa ngumu, anaweza
kuzifunga wakati mwingine kama matokeo ya watu kutokutii lakini kupitia maombi
inaonekana wazi kuwa Mungu anaweza kuzifungua mbingu:-
1Wafalme 8:35-39 “Ikiwa
mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba
wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati
ule utakapowatesa; basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa
wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo
kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao.
Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au
panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo
wote, au uele wo wote; maombi yo yote au dua yo yote ikifanywa na mtu awaye
yote, au na watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo
wake, na kuikunjua mikono yake kuielekea nyumba hii; basi, usikie huko
mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia
zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya
wanadamu wote);”
Kumbukumbu 28:23-25 “Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba,
na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma. Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe
vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie. Bwana
atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini
utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote
za duniani.”
2Nyakati 7:13-15 “Nikizifunga
mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu
tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na
kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka
mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu
yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”
Neno la Mungu
linaonyesha kuna wakati Mungu huzifunga mbingu, na hii maana yake sio kwaajili
ya mvua tu lakini Mungu anaweza hata kuzifunga mbingu za mtu mmoja mmoja na hata
mbingu za kanisa Fulani na kama tunataka kuona mkono wa Mungu ukitusaidia basi “Power houses” zinaweza kuwa sababu ya
kufunguliwa kwa milango hii ambayo imefungwa, kwa nguvu za Maombi Mungu
huzifungulia mbingu
Luka 3:21-22 “Ikawa,
watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu
zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua;
sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”
·
Power
House ni Chanzo cha nguvu za utumishi – Tumetumwa kama kondoo katikati ya
mbwa mwitu hatari, ni kauli inayoonyesha kuwa watu wa Mungu wana maadui
wasioonekna na wanaoonekana, kwa sababu hiyo kila aliyetumwa na Mungu alipewa
nguvu kwaajili ya kukabiliana na upinzani tunaita Power encounter, shetani ni
mpinzani wa injili, wachawi na kadhalika hatuwezi kwenda bila nguvu za Mungu na
tunazihitaji nguvu za Mungu wakati wote na ni wapi tunaweza kupata/au kuzalisha
nguvu kwaajili ya utumishi huu ni katika nyumba
za mombi “Power houses” ni
chumba cha maombi ndicho kinachoweza kutupa nguvu na ujasiri wa kukabiliana na
aina yoyote ile ya upinzani wa kiinjili na maendeleo endelevu ua utumishi
tuliopewa
Luka 4:1-2 “Na
Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho
muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa
hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.”
Matendo 1:8 “Lakini
mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa
mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata
mwisho wa nchi.”
Matendo 4:31 “Hata walipokwisha
kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho
Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”
Mafundisho yetu
ili yaweze kubadilisha maisha ya watu ni lazima yaombewe na kinyume cha hapo
yatakuwa nadharia tu, huduma yetu ili iendelee kuleta matokeo chanya inapaswa
kujaziwa na maombi, huduma ikifanyika bila ya maombi ya kutosha mwili tu ndio
utakaokuwa umefanya kazi yake tunahitaji nyumba ya uzalishaji wa nguvu za Mungu
katika maisha yetu ya kiroho ili mambo yaende!
·
Power
House ni ulinzi wa Kanisa - Ni
muhimu kufahamu kuwa maombi pia hufanya kazi ya kuweka ulinzi wa rohoni,
hutulinda na yule muovu, hutuepucha na majaribu, huzuia mashambulizi ya adui,
hufunika wahudumu, watendakazi, wachungaji na familia zao na mali zao kwa hiyo
tunayahitaji maombi kama tunavyohitaji maji ya kunywa , Lazima watu waombe na
kusimama katika zamu yao kama walinzi wa rohoni
Matendo 12:5-7 “Basi
Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili
yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala
katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango
wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika
mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi.
Minyororo yake ikamwanguka mikononi.”
Mathayo 6:13 “ Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe
na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele.
Amina.] ”
Mathayo 26:40-41 “Akawajia
wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha
pamoja nami hata saa moja? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i
radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Habakuki 2:1-3 “Mimi
nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione
atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. Bwana
akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye
apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa,
inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia,
ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.”
·
Power
House huvunja minyororo – Maombi ni silaha ya kiroho inayovunja vunja nira
yaani vifungo na minyororo ya aina mbalimbali, maombi huwatoa watu utumwani na
kuwaweka huru walikandamizwa, yanaondoa mizigo mizito na kuwapa watu uhuru na
raha ya kiungu, yanavunja laana ya kizazi na kizazi, kurejesha uhuru wa kiroho,
upako huo wa kuvunja nira unapatikana kwa njia ya maombi, maombi yanaweza
kufungua mpaka magereza za kawaida na
kuvunja hata nira za chuma
Isaya 10:27 “Tena
itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake
shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.”
Isaya 58:6 “.Je!
Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza
kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira? “
Matendo 16:25-31 “Lakini
panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia
nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa
tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango
ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa. Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye
alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua,
akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu,
akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe,
akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha
akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia,
Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”
·
Power
House ni nguvu ya kupokea maelekezo na muelekeo – hatuwezi kwenda wenyewe,
hatuwezi kwenda peke yetu, tunamuhitaji Mungu atupe muelekeo na maelekezo
katika kazi yake ni katika wakati wa kuomba mbele zake na utulivu ndipo ambapo
Mungu hutupa muelekeo na maelekezo, kwa hiyo kanisa ni muhimu kwetu kuwa na
vituo vya kuzalisha nguvu yaani Power House ili tusiongozwe na mawazo yetu bali
tuongozwe na Roho Mtakatifu ili tuweze kuifanya kazi yake kwa usahihi, kanisa
lisilo na power house huongozwa na mawazo ya wanadamu na kanisa lenye power
House huongozwa na Roho Mtakatifu
Matendo 13:1-3 “Na
huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni
Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa
ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.Basi hawa walipokuwa wakimfanyia
Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa
kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao
juu yao, wakawaacha waende zao.”
Matendo 16:6-10 “Wakapita
katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri
lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia,
lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemkia Troa. Paulo
akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na
kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.Basi alipokwisha kuyaona yale maono,
mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu
ametuita tuwahubiri Habari Njema.”
Huduma katika vituo vya kuzalisha nguvu (Power House)
Watenda kazi wetu, wahudumu,
wanafunzi na wenye hekima wote wanapaswa kusimamia kwa uaminifu vituo vya
maombi ya kuzalisha nguvu kokote viliko, ni afadhali kitu kingine kisimame
lakini sio maombi Kanisa hatuna budi kuhakikisha kuwa maombi yetu yanakuwa
endelevu, na tuone kusimama kwa maombi kama kusimama kwa moyo katika mwili wa
mwanadamu ndio maana maombi yanapaswa kuendelea “Ombeni bila kukoma”, watu wote
waombaji wanapaswa kuwa watu wa toba, wenye kujitia nidhamu kwaajili ya kuomba,
wanaopenda kusihi maisha matakatifu, wenye tabia ya unyenyekevu na wanaojua
kukaa kimya mbele za Mungu, aidha waombaji hawapaswi kuwa na midomo michafu kwa
sababu midomo hiyo hiyo ndio inayotumika kuomba hivyo haifai kutumika kwenye
mambo mengine hasa yasiyofaa katika mapenzi ya Mungu.
Yakobo 3:10-12 “Katika kinywa kile kile
hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je!
Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Ndugu zangu,
Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi
haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.”
Watendakazi wetu walioandaliwa
katika shule za uongozi na huduma ndio watakaohusika na kituo cha kuongoza
maombi ya Power house maombi haya yataongozwa kila wakati katika siku na muda
utakaokuwa umepangwa na kanisa
1. Toba
litakuwa jambo la kwanza na la muhimu
katika maombi
2. Kurekebisha
Mahusiano kutakuwa ni jambo muhimu katika hatua za maombi
3. Kufunga
itakuwa ni sehemu mojawapo ya muhimu katika maombi yetu
4. Shukurani
itakuwa ni sehemu muhimu ya maombi
5. Toba
za kila mtu binafsi, kwa niaba ya kanisa na kwaniaba ya taifa itahusika
6. Tutaomba
uwepo wa Mungu, Nguvu zake, huduma na kuombea wachungaji watumishi wote na
watendakazi, Mungu awalinde awatumie na kuwapa afya njema
7. Tutakemea
na kuvunja nguvu za giza, kukemea mapepo na kutangaza ushindi
8. Tutaombea
kanisa, miji yetu na taifa, tutamuomba Mungu aponye wanaoteseka na kufanya
ishara na miujiza akichochea karama za Roho, aokoe na kuponya na kurahisisha
kazi yake kotekote
9. Tutamsikiliza
Mungu na kukaa kimya kusubiri maelekezo yake
Power house ni tofauti na kikundi
maalumu cha maombi, hii ni kiungo au kiwanda cha kuzalisha waombaji katika
kanisa hivyo inapaswa kulishirikisha kanisa zima katika mfumo kama ule wa
makanisa ya nyumbani, Neno la Mungu
linapaswa kuwa muongozo wa maombi haya, “Power
house” sio mashindano ya kuomba, wala sio sehemu ya kujitukuza na kuonyesha
uhodari wa kuomba, wala sio sababu ya kutokutii uongozi wa kanisa, ni kituo cha
nidhamu kinachoomba kwaajili ya maswala mbalimbali ya kazi ya Mungu, hakipaswi
kuwa chanzo cha machafuko, ni sehemu ya upendo kwa Mungu na kwa kazi yake, ni
ushirika wa maombi ya washirika wote na wageni wanaopenda kujiunga kuomba nasi,
Bwana ampe neema kila mtenda kazi kulijua hili na kulifanyia kazi katika jina
la Yesu Ameen
Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.



.jpg)