Ijumaa, 7 Agosti 2026

HUDUMA KATIKA MAKANISA YA NYUMBANI


Matendo 2:46-47 “Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe, wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.”




Utangulizi

Ni muhimu kufahamu kuwa nyakati za kanisa la kwanza licha ya kuwa walikuwa wakikutana hekaluni kuabudu lakini pia walikuwa na tabia ya kukutana na kuabudu nyumba kwa nyumba, jambo hili lilichangia kwa kiasi kikubwa washirika kuwa na uwezo wa kutambuana kushirikiana na kutiana moyo lakini pia makanisa ya nyumbani yalichochea kwa kiasi kikubwa ukuaji wa kanisa mama, Ukiacha hilo pia wahudumu wenye huduma ya kichungaji, watenda kazi, Wanafunzi na wenye hekima wanapata nafasi ya kutumia vipawa vyao, na kujifunza kivitendo, malezi ya kanisa na kutengeneza njia rahisi ya kufungua matawi ya kanisa katika sehemu zingine za mji wetu, tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa huduma ya makanisa ya nyumbani ni mpango wa Mungu wa ukuaji wa kiroho, kihuduma na kiidadi, lakini ni moyo wa kutengeneza umoja na ushirikiano wa karibu kwa huduma ya kichungaji.

Warumi 16:3-4. “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

Ukiichunguza Biblia utaweza kuona kuwa nyakati za karne ya kwanza wakati kanisa linaanza watenda kazi walikuwa na makanisa nyumbani, kwa hiyo huduma katika makanisa ya nyumbani halikuwa swala geni au lisilo la kibiblia, na huduma hizi za makanisa ya nyumbani zimeonyesha mafanikio makubwa sana katika maeneo mengi duniani ikiwemo Afrika na Asia  na sehemu nyingine duniani, lakini pia makanisa ya nyumbani yameonyesha mafanikio makubwa katika maeneo ambayo injili inapigwa marufuku, leo basi tutachukua muda kujifunza somo hili Huduma katika makanisa ya nyumbani kwa kuzingatia vipengele vikuu vitatu vifuatavyo:-

  • Maana ya makanisa ya nyumbani
  • Huduma katika makanisa ya nyumbani
  • Faida ya huduma katika makanisa ya nyumbani               

 

Maana ya makanisa ya nyumbani

Makanisa ya nyumbani au kanisa la nyumbani ni mkusanyiko mdogo wa washirika wa Kanisa la mahali pamoja au katika mji mmoja ambao wanakusanyika katika mitaa yao, katika nyumba mojawapo ya mtenda kazi au mtu aliyejitoa kutoa nyumba yake kwa ajili ya  ibada, kwa kusudi la kukusanyika pamoja kwa ibada katika siku mojawapo ya juma inayokubalika kwaajili ya kufanya ibada za pamoja, kuomba pamoja, kujifunza neno la Mungu, kuumega mkate na kushirikiana na kujuana hali kwa ukaribu na kwa pamoja, makanisa ya nyumbani yanaweza kukutana katika sebule ya mshirika mmojawapo na yakiwa na uwezo wa kuwa na wanachama kuanzia 6-10 au 10-30 kulingana  na uwezo wa sebule au mahali pa kuabudia wanakokutana washirika hao, Makanisa ya nyumbani sio mbadala wa kanisa mama hata kidogo lakini ni vikundi vidogo vidogo vinavyoundwa na watu kwa kusudi la kulifanya kanisa mama kuendelea kuwa na nguvu na kukua katika upendo na ushirika, makanisa haya yanasaidia sana kuleta umoja wa kweli Maandiko yanaonyesha kuwa kulikuwa na makanisa ya namna hii nyakati za mitume:-

Kanisa katika nyumba ya Prisila na Akila – Warumi 16:3-4 “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

1Wakorintho 16:19-20 “Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao. Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.”

Nimfa pia anatajwa kuwa alikuwa na kanisa la Nyumbani huko Kolosai – Wakolosai 4:14-15 “Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu.Wasalimuni ndugu walioko Laodikia, na Nimfa, na kanisa lililo katika nyumba yake.”

Pia rafiki wa Paulo Mtume aitwaye Philemoni – Philemoni 1:1-3. “Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi, na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako. Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu, Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo              

Huduma katika makanisa ya nyumbani

Huduma katika makanisa ya nyumbani zinaendeshwa na watendakazi, wanafunzi pamoja na wenye hekima ambao wamepitia mafunzo mbalimbali katika kanisa letu, hawa sasa wanawajibika kuyahudumia makanisa hayo katika makazi karibu na mitaani kwao wanakokaa washirika, Neno la Mungu linaonyesha kuwa huduma za kiroho, maombezi, kuongoza watu katika wokovu, na kuwajenga watu zinaweza kufanyika pia katika nyumba za watu kwa taratibu maalumu, Yesu alithamini pia shughuli za kuwahudumia watu nyumba kwa nyumba ukiacha kuwa alikuwa akihitajika na umati mkubwa wa watu.

Marko 1:29-34 “Na mara walipotoka katika sinagogi, walifika nyumbani kwa Simoni na Andrea, pamoja na Yakobo na Yohana. Naye mkwewe Simoni, mamaye mkewe, alikuwa kitandani, hawezi homa; na mara wakamwambia habari zake. Akamkaribia, akamwinua kwa kumshika mkono, homa ikamwacha, akawatumikia. Hata kulipokuwa jioni, na jua limekwisha kuchwa, walikuwa wakimletea wote waliokuwa hawawezi, na wenye pepo. Na mji wote ulikuwa umekusanyika mlangoni.Akaponya wengi waliokuwa na maradhi mbalimbali, akatoa pepo wengi, wala hakuwaacha pepo kunena, kwa sababu walimjua.”

Luka 19:5-9 “Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako. Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha. Hata watu walipoona, walinung'unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi. Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne. Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.”

Luka 10:38-42 “Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake.Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake. Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie. Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi; lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.”

Tunajifunza hapo kutoka kwa Mwalimu mkuu Yesu Kristo kwamba nyumbani ni mahali ambapo huduma zote zinaweza kufanyika bila shaka yoyote uwepo wa Mungu unakuwepo popote walipo wawili au watatu ambao wamekusanyika kwa jina lake

Mathayo 18:18-20 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

Hata hivyo ni muhimu kufahamu kuwa huduma ya makanisa ya nyumbani ni sehemu ndogo tu ya ushirika mkuu na kwa sababu hiyo kuhudhuria katika hekalu kuu hakuwezi kupoteza maana sawa tu na kuhudhuria katika masinagogi hakukuwahi kuondoa maana ya kwenda Hekaluni, wala kuacha kuhudhuria ibada za muhimu katika kanisa letu, tunajifunza pia kuwa Paulo alihudumu katika kanisa kuu na makanisa ya nyumbani huku akitembelea nyumba kwa nyumba na kuwahudumia hii ilileta mafanikio na ufanisi mkubwa nyakati za kanisa la kwanza:-

Matendo 20:17-21 “Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa.Walipofika kwake, akawaambia, Ninyi wenyewe mnajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu wakati wote, nikimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, na kwa machozi, na majaribu yaliyonipata kwa hila za Wayahudi; ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba, nikiwashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.”

Kwa hiyo tunaweza kufundisha, kuomba, kuabudu, kuuliza maswali, kutambuana na  kuhubiri injili, na watu wakaokoka, na kujenga umoja wenye nguvu huku tukifahamiana sana kuliko katika kanisa kubwa na mpango huu ni mahususi sana endapo kanisa mama linalenga kuwa kanisa kubwa lenye kusanyiko kubwa la watu maelfu kwa maelfu

Faida ya huduma katika makanisa ya nyumbani

Kanisa la nyumbani lina faida kubwa sana endapo kanisa mama lina malengo ya kuwa kanisa kubwa lenye nwaamini maelfu kwa maelfu yaani Mega Church, Kanisa linapokuwa kubwa bila kuwa na makanisa ya nyumbani kunakuwa na ugumu wa kutambuana, kuangalia changamoto wanazokutana nazo waamini wetu, kukosa msaada wa karibu anapokuwa mtaani ambako hajui kama kuna wenzake wa karibu wanaishi huko, lakini pia kama mtu ana vipawa na karama ambazo kwa hizo Mungu yu amtumia ni vigumu kutambulika na kutumika bila mfumo wa makanisa ya nyumbani kwa hiyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa kanisa letu kuwa na mfumo huu wa makanisa ya nyumbani, pamoja na faida lukuki zinazoweza kutolewa na kanisa la nyumbani hapa tunaweza kuona faida kadhaa :-

  1. Makanisa ya nyumbani husaidia kukua kiroho – Kanisa la nyumbani linaleta utulivu na nafasi ambayo kila mmoja hutambulika lakini sio hivyo tu mtu anaweza kupata nafasi ya kuuliza maswali, kueleza  changamoto anazokuta anazo na kupata mtenda kazi wa karibu na eneo lake ambaye anaweza kumsaidia katika kujifunza na kukua kiroho kwa hiyo kanisa la nyumbani ni njia bora zaidi ya kuangaliana sisi kwa sisi katika mazingira yote

 

Waebrania 10:24-25 “tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia

 

  1. Makanisa ya nyumbani yanatoa huduma ya ushirika wa kweli – hakuna mahali ambapo watu watafahamiana kwa ukaribu kama katika ushirika wa makanisa ya nyumbani, watabebeana mizigo kama makanisa ya nyumbani, watashirikiana katika shida na furaha kama kanisa la nyumbani kwa ujumla ule upendo wa kweli katika Kristo tunaweza kuonyeshana  kwa uhalisia katika makanisa ya nyumbani, wakati kanisa kubwa linainua hisia zetu ni kanisa la nyumbani ndilo linaloleta mapinduzi makubwa ya kiroho, na kiushirika.

 

Matendo 2:41-42 “Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani yanahusika kwa ukaribu na huduma ya kichungaji – kama mshirika anapitia changamoto za aina mbalimbali mchungaji kiongozi hawezi kujua bila taarifa za wale walio karibu naye ikiwa ni pamoja na kiongozi wa kanisa la nyumbani ambaye ni mtenda kazi pamoja na Mchungaji wetu, Kanisa la nyumbani ni rahisi kumtambua kila mtu, ni rahisi kutambua mtu anayepitia changamoto ni rahisi kumuombea mtu ni rahisi kujua mtu anaye lega lega katika Imani na ni sehemu ambayo hakuna mtu anasahaulika wala kupotea  na ni rahisi kufuatiliwa  na kurejezwa katika Imani

 

Wagalatia 6:1-2 “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya uinjilisti rahisi – Ni vigumu wakati mwingine kumualika mtu katika kanisa mama na akakubali hasa kama hajawahi kuingia katika makanisa ya watu wanaohubiri wokovu, lakini ni rahisi mtu kualikika katika makanisa ya nyumbani anajisikia salama maana ni sebule ya mtu na ni kwa watu anaowajua, ni rahisi kualika majirani, na wakafika hawaogopi kuliko inavyokuwa katika majengo ya makanisa makubwa na kwa njia hiyo ni rahisi kumuhubiri injili na pia kutoa mwaliko wa kuja katika kanisa kubwa huduma za kiroho zaidi.

 

Matendo 5:42 “Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.”

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya kulea viongozi – wakati mwingine kutokana na programu ambazo zinaendelea katika kanisa kubwa kuna uwezekano wa kushindwa kuwapa watu wengine madhabahu, au kupatikana kwa uhaba, lakini makanisa ya nyumbani kwa sababu ni kundi dogo linaweza kumshirikisha kila mtu na zaidi ya yote viongozi wetu waliopata nafasi ya kupitia shule mbalimbali ya  za kihuduma wanapata nafasi ya kuhudumu na kuombea watu na kuchunga kanisa dogo na kulikuza jambo ambalo linaweza kuwarahisishia uanzishaji wa makanisa wanapokuwa wameitwa katika wito maalumu, Ni katika kanisa la nyumbani viongozi hujifunza kivitendo, karama zinagunduliwa, wachungaji wajao wanabainika, walimu wazuri wanabainika, wainjilisti wazuri wanabainika na watendakazi wapya wanabainika

 

2Timotheo 2:1-2 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu. Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.”

 

  1. Makanisa ya nyumbani ni nyenzo ya kupanuka kwa kanisa – Kanisa hutawanyika kwa haraka kutokana na kuweko kwa makanisa ya nyumbani kama eneo la kanisa kubwa liko mbali sana na sehemu fulani ni kupitia makanisa ya nyumbani tunaweza kuanzisha tawi lingine bila kuhitaji gharama kubwa za kukodisha jengo, aidha makanisa ya nyumbani hayawezi kuzuiliwa na mateso au upinzani, katika nchi nyingi ambazo injili inapingwa makanisa ya nyumbani imekuwa ni njia ya siri ya kulifanya kanisa kuendelea mbele. Makanisa ya nyumbani yametumiwa na watumishi wengi wa Mungu katika huduma zao na kusababisha ukuaji na upoanukaji mkubwa wa kanisa mama hivyo makanisa haya ni nyenzo ya ukuaji wa Kanisa kubwa kiroho, kiidadi, kijiografia na kadhalika  

 

Matendo 6:5-7 “Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia; ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao. Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.”

 

Matendo 8:1-4 “Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu. Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani. Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.”

 

-          Kanisa la The Church of Pentecost huko Ghana – ni moja ya kanisa kubwa sana miongoni mwa madhehebu ya kipentekoste wana mfumo wa makanisa ya nyumbani “cell system” zaidi ya maelfu  na kutokana na watendakazi kuyasimamia makanisa hayo kwa uaminifu kanisa limeweza kuwa na washirika karibu milioni tatu na likatumia makanisa ya nyumbani kuzalisha makanisa 99 katika nchi nyingine na sehemu mbalimbali za Afrika magharibi

 

-          Kanisa la The works and Mission Baptiost Church – Ni moja ya makanisa makubwa sana nchini Ivory Coast kanisa hili linaongozwa na Askofu Dion Robert kanisa lake lina mfumi wa makanisa ya nyumbani  ambayo yamesababisha mfumuko mkubwa wa ukuaji wa kanisa  kanisa lina cell Groups makanisa ya nyumbani 18,000,. 14,000 ya watu wazima na 4,000 ya watoto kupitia mfumo huo kanisa la Bishop Dion sasa lina washirika 150,000 katika ibada moja wakutanano kuabudu

 

-          Christian Rivival Church – Ni kanisa kubwa na linalokua kwa kasi lililoko Afrika ya kusinikanisa hili mlina mfumo wa makanisa ya nyumbani yanayounganisha watu  na majirani, kanisa hili lina maelfu ya makanisa ya nyumbani na linaongezeka kwa kasi

 

-          Lighthouse Chapel International – Ni kanisa kubwa linaoongezeka kwa kazi lina wanafunzi wanaohusika kusimamia makanisa ya nyumbani likitumia mfumo ule ule uliokuwa unatumiwa na mitume nyakati za kanisa la kwanza

 

-          Living Faith Church Woldwide (Winners Chapel, Nigeria) – ni Kanisa lenye watu 50,000 wanaoabudu mahali pamoja pale kwenye makao makuu yao wao wanatumia mfumo wa makanisa ya nyumbani yanayosimamiwa na watenda kazi, kanisa hili kwa sasa lina waamini zaidi ya milioni sita duniani

 

-          Deeper life Bible church Nigeria  - lina waamini wapoatao 65,000 wanaoabudu katika ibada moja, lakini siri mojawapo ya mafanikio yao ni mfumo wa makanisa ya nyumbani yenye viongozi mahiri na walimaanisha

 

-          Full Gospel Bible Fellowship -  Ni moja ya Kanisa la kipekee la kipentekoste lililoanzishwa nchini Tanzania na Askofu Mkuu Zakaria Kakobe, ukiacha makanisa haya kuenea nchi nzima kanisa kuu lililoko Sam Nunjoma pale Mwenge Dar es Salaam linaundwa na makanisa ya nyumbani zaidi ya 600 yaliyoenea kila mahali katika mji wa Dar es Salaam, viongozi wa makanisa ya nyumbani wana mafundisho maalumu ambayo huyatoa kwa pamoja kila mahali katika mtaa husika na viongzi hao wenye utii wa hali ya juu hutoa taarifa ya kazi wanayoifanya kwa viongozi wao na kwa mchungaji kiongozi, Makanisa hayo ya meunda umoja imara na kulifanya kanisa kuu kuwa imara, aidha zinapofungishwa ndoa kwa wingi makanisa hayo hujishughulisha au kuhusika kwa kiwango Fulani katika usimamizi wa wanandoa hao kuanzia safari zao za uchumba  na kadhalika, makanisa haya pia huusika na matukio ya misiba mazishi na mengineyo

 

Kama tunataka makanisa yetu yakue na kuwa na washirika wengi sana basi ni nashauri tujiandae na mfumo huu maalumu utakaosaidia kufikisha huduma kwa ufasaha katika jamii, na kulifanya kanisa kuwa nyenzo rahisi na inayoweza kuwafikia watu kwa njia nyepesi, tusikusanye sadaka yoyote katika makanisa ya nyumbani, hii itasaidia kuwaondolea kongwa washirika lakini pia itakuokoa na majaribu ya kifedha kama kiongozi wa makanisa ya nyumbani kutokuwa na muda wa kutoa hesabu ya mapato na matumizi, makanisa ya nyumbani yaanzishwe kwa kusudi la kufikisha huduma karibu na watu na sio kwaajili ya kukusanya mapato, washirika wote wa makanisa ya nyumbani watatoa sadaka zao katika kanisa kuu lililoko katika mji husika, makanisa ya nyumbani msisitizo wake ni wa kifamilia kuifanya familia ya Kikristo kuishi pamoja na kushirikiana na kubebeana mizigo, makanisa ya nyumbani pia ni makanisa ya Mungu, kusudi kuu ni kuabudu na kujifunza neno la Mungu  na kutiana moyo, Ni muhimu makanisa haya yakaendeshwa kwa kanuni za kimaandiko na yakatambua viongozi wao na kuwaheshimu, Makanisa ya nyumbani ni kielelezo na nuru katika mitaa yetu kuendelea kumuhubiri Kristo kivitendo na kuuishi kwa upendo kama Mungu alivyotuamuru  

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima 

Jumapili, 2 Agosti 2026

Wito wa kumtumikia Mungu katika huduma!


Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu anatoa wito kwa watu wake wote kuhakikisha ya kuwa wanamtumikia, Neno wito linamaanisha kualikwa na Mungu ili tuweze kutekeleza ajenda zake au kusudi lake ambalo amelikusudia yeye mwenyewe sawasawa na maagizo yaliyomo katika neno lake, Mungu huchagua watu wake wale anaowataka mwenyewe na kuwaalika wawe na ushirika naye na kisha awatume katika kazi yake ili kutekeleza mapenzi yake, kusudi lake na kazi yake hapa duniani na kwa sababu hiyo kuitikia wito wa kumtumikia Mungu ni utii usio na mashart

Marko 3:13-15 “Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri ya kutoa pepo.”

Kwa hiyo tangu nyakati za agano la kale Mungu amekuwa na tabia ya kuwaita na kuwachagua watu aliowataka mwenyewe kwaajili ya kutekeleza majukumu na makusudi yake yeye mwenyewe duniani, Kwa msingi huo kila mtu aliyeokoka anapaswa kuwa makini kumtumikia Mungu na kusikiliza sauti ya Mungu ili kutambua mapenzi ya Mungu katika maisha yake na kuwajibika mara moja katika kazi hii yenye Baraka na heshima kubwa, kwa bahati mbaya watu wengi sana hawapendi kumtumikia Mungu katika huduma mbalimbali Kanisani kwa kisingizio kuwa hawajaitwa, au kwa kutokuwa na ufahamu wanawajibika vipi, kwa hiyo leo tutachukua Muda kujifunza na kutafakari kwa pamoja somo hili muhimu kuhusu wito wa kumtumikia Mungu katika huduma kwa kuzingatia vipengele vikuu vitatu vifuatavyo:-


·         Maana ya neno wito katika maandiko.

·         Aina kuu tatu za wito katika huduma.

·         Jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma.


Maana ya neno wito katika maandiko.

Ni muhimu kufahamu kuwa neno wito katika maandiko lina tajwa kwa lugha ya Kiebrania kwa neno “qara” na linatajwa kwa kiyunani kama neno “Kaleō” au “klēsis” ikimaanisha kuitwa, kutengwa, kuchaguliwa au kuteuliwa na Mungu kwa kusudi la kutimiza majukumu maalumu katika ajenda za Mungu, Kwa sababu hiyo wito sio mpango wala wazo la kibinadamu au shauku binafsi bali ni mpango kamili wa Mungu juu ya maisha ya mtu katika kusudi lake au kwa kazi maalumu, kwa hiyo wito katika huduma ni mualiko wa kumtumikia Mungu au kufanya kazi pamoja na Mungu katika kutimiza kusudi lake au ajenda zake mwenyewe hapa duniani kwa wakati maalumu.

Luka 5:27-29 “Baada ya hayo akatoka, akaona mtoza ushuru, jina lake Lawi, ameketi forodhani, akamwambia, Nifuate. Akaacha vyote, akaondoka, akamfuata. Na Lawi akamfanyia karamu kubwa nyumbani mwake; palikuwa na mkutano mkuu wa watoza ushuru na watu wengineo waliokuwa wameketi chakulani pamoja nao.”

Msingi mkuu wa Mungu anapomuita mtu kwanza anataka ushirika wa karibu na mtu huyo kisha ndipo amtume, kwa hiyo mtu aliyeitwa na aliyeitikia wito wa kumtumikia Mungu katika huduma anapaswa kuwa mtu mwenye ushirika wa karibu na Mungu, ushirika huu ni wa muhimu hata kabla ya kazi yenyewe

Yohana 21:15-17 “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.”

Marko 3:13-15 “Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri ya kutoa pepo.”

Kabla Mungu hajamuita mtu anataka ushirika na wewe anataka upendo wako na anataka uwe pamoja naye kisha ndipo akutume kuhubiri na kutoa pepo au kufanya huduma nyinginezo kwa niaba yake            

Aina kuu tatu za wito katika huduma.

Maandiko matakatifu yanaonyesha kuwa Mungu aliwaita watu kwa namna mbalimbali na kwaajili ya shughuli mbalimbali, kwa hiyo tunapozungumzia swala la wito tunazungumzia mada pana sana katika nyanja zote za kisiasa, kijamii na kiimani, na kisayansi, ukichunguza kwa kina utaweza kuona kuwa kote huko Mungu hufanya kazi ya kuwaita watu kwaajili ya makusudi mbalimbali, kwa hiyo wito hauko katika kuta za kanisa pekee unavuka mipaka na kwenda mbali zaidi ya vile tunavyofikiri, hata hivyo katika somo hili nataka kuzungumzia wito ambao unaishia ndani ya mipaka ya Kanisa pekee aina hizi za wito naweza kugawa katika makundi makuu muhimu matatu yafuatayo:-

·         Wito wa jumla katika wokovu

·         Wito wa jumla katika huduma

·         Wito maalumu katika huduma

Wito wa jumla katika wokovu – Wito huu wa ujumla katika wokovu ni wito unaotolewa na Mungu Roho Mtakatifu kwa jamii ya watu wote duniani ili wamuamini Bwana wetu Yesu Kristo kama mwokozi wao na kupokea uzima wa milele, huu ni wito unaotolewa kwa watu wote wamgeukie Mungu wamrudie yeye wamche yeye na kuwa na ushirika na yeye kwa hiyo watu wote duniani wanaalikwa kila iitwapo leo kupokea wito huu wa wokovu kwa imani.

Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.”

Mathayo 11:28-30 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Warumi 8:28-30 “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.”

Wito katika wokovu ni mwaliko wa jumla kwa jamii ya watu wote duniani wa kila kabila, na kila taifa na kila tamaduni na lugha na imani, wote wanapewa mwaliko wa kumpokea Yesu Kama Bwana na mwokozi wa maisha yao baada ya kuisikia injili na kuiamini na wote wanaopokea mwito huu kwa hiyari yao bila kulazimishwa wanafanyika kuwa watoto wa Mungu

Yohana 1:12-13 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”

Wito huu pamoja na mambo mengine pia unajumuisha kuishi maisha matakatifu na kuwa na ushirika na Mungu kumfanania Yesu Kristo na kuwa na tabia au mwenendo mwema kama yeye aliyetuita alivyo kwa hiyo kila aliyeokoka anawajibu wa kuukulia wokovu, kukomaa na kuwa kama Yesu Kristo mwenyewe alivyokua, wito huu ni wa toba, ni wito wa utakatifu, ni wito wa kupumzishwa na kusamehewa dhambi na kurudishwa katika familia ya Mungu na kuwa na uhusiano naye na kumuabudu

1Petro 1:14-16 “Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu; bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”

Wito wa jumla katika huduma.

Wakati msingi wa wito wa kwanza ni kutengeneza mahusiano yetu na Mungu, mojawapo ya majukumu yetu vile vile ni kumtumikia Mungu, kila mtu aliyeokoka ameitwa kumtumikia Mungu kwa hivyo wote tuliookolewa pia tuna wajibu wa kumtumikia Mungu katika majukumu mbalimbali katika mwili wa Kristo, wito huu ni wito wa jumla kwa watu waliookoka unaowekwa na Roho Mtakatifu ndani yetu na kutubebesha majukumu ya jumla katika kuonyesha upendo kwa wengine, kumtii Mungu, kumuabudu na kuwashirikisha wengine imani yetu, wito huu unamuhusu kila mtu katika kanisa na sio viongozi au wachungaji peke yao wito huu unaonekana tangu nyakati za agano la kale.

Kumbukumbu 10:12-13 “Na sasa, Israeli, Bwana, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche Bwana, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote; kuzishika amri za Bwana na sheria zake, ninazokuamuru leo, upate uheri?

Zaburi 100:1-3 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.”

Warumi 12:6-11 “Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha. Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema. Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu; kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”

Mathayo 28:18-20 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.”

Unaona maandiko yana maagizo mengi ambapo kila mtu aliyeokolewa amepewa wajibu na anaagizwa kutumika, kila mtu aliyeokoka anaagizwa kuihubiri injili, anaagizwa kuomba anaagizwa kutoa anaagizwa kuwatumikia wengine anaagizwa kufungua na kupanda makanisa anaagizwa kufanya huduma zote, pamoja na mambo mengine tofauti ni kuwa watu hawa waliookolewa walioitwa katika wito wa ujumla watafanya kazi zao za kawaida huku wakifanya kazi za huduma kwa mujibu wa ratiba za maisha yao, na ratiba za kikanisa za kutumika kila iitwapo leo, aina hii ya wito ni wito wa ujumla katika wokovu ambapo waamini wanaagizwa kutumia vipawa vyao kumtumikia Mungu kwa  kadiri ya neema, wito huu unajumuisha kumuwakilisha Mungu popote tulipo pia iwe ni nyumbani au kazini au shuleni wewe ni wakili wa Yesu Kristo na unatumika pale ulipo kama chumvi na kama nuru.

Wito maalumu katika huduma

Wito huu au aina hii ya wito hutolewa kwa uwezo wa Roho Myakatifu kwa waamini kumuwezesha mtu huyo kusikia sauti ya Mungu kwa njia mbalimbali na kuamua kucha kila kitu hata kazi kwa kusudi la kumtumikia Mungu moja kwa moja katika kazi yake akiwa na huduma ya aidha mtume, au nabii, au mwinjilisti au mchungaji na au mwalimu aina hii pia ya huduma huwa inaambatana na huduma za kimaongozi katika kanisa na wakati mwingine karama mbalimbali za Roho Mtakatifu kuwawezesha watu hao kuuhudumia mwili wa Kristo kwa kuujenga na kuukamilisha

Waefeso 4:11-13 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”

Jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma.

Linapokuja swala la wito maalumu katika huduma watu wengi sana huwa wanajiuliza nitajuaje kama nina wito, tunapojifunza kipengele hiki kinachozungumzia jinsi Mungu anavyoita watu katika huduma tutapata ufahamu namna na jinsi Mungu anavyosema nasi kuhususiana na wito wetu kujifunza kuhusu swala hili kutatusaidia kutembea kwa uhakika katika huduma tukiwa na uhakika kuwa hatukubahatisha katika swala zima la kumtumikia Mungu katika kazi hii maalumu, Neno la Mungu linaainisha njia mbalimbali ambazo Mungu alizitumia kuwaita watu wake katika wito maalumu

1.       Mungu anaweza kumuita mtu kwa sauti yake moja kwa moja  - wakati mwingine Mungu huwaita watumishi wake moja kwa moja kwa sauti yake katika mifumo anayoijua yeye mwenyewe  watumishi wa Mungu kama Musa, Samuel na Paulo waliitwa moja kwa moja katika huduma kwa kuisikia sauti ya Bwana  wazi wazi moja ona

 

Kutoka 3:1-10 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. Malaika wa BWANA akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. BWANA alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”

 

1Samuel 3:1-10 “Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri. Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu; basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa. Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena. Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto. Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.”

 

Matendo 9:1-6 “Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu. Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”

 

2.       Mungu anaweza kuita watumishi wake kupitia maono – Maandiko yanaonyesha kuwa kwa njia ya maono pia Mungu anaweza kumuita mtu katika kazi yake maalumu na ikawa na ufanisi mkubwa, Nabii Isaya alipokea wito wake kupitia Maono na Mungu alimtumia kwa kiwango kikubwa sana  

 

Isaya 6:1-10. “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa. Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi. Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione. Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.

 

3.       Mungu anaweza kuita watumishi wake kupitia ndoto – Mungu hutumia ndoto pia kufunua kusudu lake, mpango wake na agenda zake wito maalumu wa Yusufu ulifunuliwa kupitia ndoto mapema sana katika maisha yake tangu akiwa mdogo kuwa Mungu angemtumia, kupitia hili tunaweza kujifunza hapa na kutambua ya kuwa Mungu ameita baadhi ya watu wake kumtumikia kwa kutumia njia anazoona kuwa inafaa ikiwa ni pamoja na ndoto, Mungu anatumia njia ambayo muhusika ataelewa kwa urahisi au njia hiyo inaeleweka kwa mtu huyo.

 

Mwanzo 37:5-11 “Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia; akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota. Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu. Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake. Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia. Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi? Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.”

 

4.       Mungu huweza kuita watumishi wake kupitia mtumishi wake au nabii – Wako watu kadhaa katika maandiko ambao waliitwa katika kazi maalumu kupitia manabii, Nabii alifunuliwa na kumtia mafuta yule aliyekusudiwa katika wito fulani, kwa mfano ufalme wa Sauli, au ufalme wa Daudi,  au  nabii Elisha hawa waliitwa kupitia nabii au mtumishi wa Mungu aliyekuwako wakati huo, wao kupitia ujuzi na sauti ya Roho Mtakatifu wanaweza kumjua na kumbaini mtu ambaye Mungu amemuita katika huduma  na akafaa kwaajili ya utumishi huo uliokusudiwa!

 

1Samuel 9:15-20 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema, Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia. Hata Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia habari zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu. Ndipo Sauli akamkaribia Samweli langoni, akasema, Tafadhali, uniambie, nyumba ya mwonaji iko wapi? Samweli akamjibu Sauli, akasema, Mimi ndimi mwonaji; tangulia mbele yangu ukwee mpaka mahali pa juu, kwa maana mtakula pamoja nami leo; kisha, asubuhi nitakuacha uende zako, nami nitakuambia yote uliyo nayo moyoni mwako. Na wale punda zako waliopotea siku hizi tatu, usijiudhi kwa ajili yao; maana wameonekana. Na yote yaliyotamanika katika Israeli amewekewa nani? Si wewe, na nyumba yote ya baba yako?

 

1Samuel 16:13 “Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.”  

 

1Wafalme 19:19-21 “Basi, akaondoka huko, akamkuta Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akilima, mwenye jozi za ng'ombe kumi na mbili mbele yake, na yeye mwenyewe alikuwa pamoja na lile la kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akatupa vazi lake juu yake. Naye akawaacha ng'ombe, akamfuata Eliya mbio, akasema, Nipe ruhusa, nakuomba, nimbusu baba yangu na mama yangu, kisha mimi nitakufuata. Akamwambia, Enenda, urudi; ni nini niliyokutendea? Akarudi akiacha kumfuata, akatwaa lile jozi la ng'ombe, akawachinja, akatokosa nyama zao kwa ile miti ya ng'ombe, akawapa watu, wakala. Kisha akainuka, akamfuata Eliya, akamhudumia.”

 

5.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake kupitia malaika – Wakati mwingine Mungu humtuma malaika wake kuweza kuwasilisha ujumbe wa jukumu lake kwa mtumishi wake anayekusudiwa, Katika maandikio iko mifano mingi lakini tutaangalia mifano michache ya watu kadhaa kama Gideoni na Mariam mama yake Yesu ambao walipewa kazi maalumu kwa ujumbe wa malaika

 

Waamuzi 6:11-14 “Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani. Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma? 

 

Luka 1:26-33 “Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.”

 

6.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake kupitia Roho wake Mtakatifu – Ikumbukwe kuwa njia zote hizo Roho Mtakatifu ambaye ndiye Bwana wa mavuno anazitumia katika kuhakikisha kuwa wanapatikana watenda kazi katika mashamba yake lakini hutokea wakati mwingine mwenyewe akazungumza moja kwa moja kwa njia ya unabii na kumuita au kumtaka mtu katika huduma maalumu

 

Matendo 13:1-3 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.”

 

7.       Mungu huweza kuwaita watumishi wake Kupitia Yesu Kristo mwenyewe – Wanafunzi wale kumi na wawili walikuwa ni chaguo la Yesu Kristo mwenyewe na aliwaita kama alivyopenda yeye mwenyewe hata sasa Yesu Kristo bado anaita watu wake kama apendavyo kwa njia mbalimbali na wakati mwingine yeye mwenyewe. Hata hivyo ni muhimu kuelewa kuwa katika njia hizo zote hakuna iliyobora zaidi kuliko nyingine kwa sababu zote ni njia ambazo yeye mwenyewe anazitumia kuwapata watu wa kumtumikia katika huduma maalumu, kwa hoyo mtumishi aliyetokewa na Yesu mwenyewe na kuitwa katika wito haimaanishi kuwa anaubora kushinda aliyeitwa kwa njia nyingine, kwani kimaandiko hizo zote ni nnia anazozitumia Mungu kufahamisha watu wake namna anavyowahitaji katika huduma.

 

Mathayo 4:18-19 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi. Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.”

 

Mathayo 9:9. “Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata.”                                    

Kwa hiyo tunajifunza kuwa ni Mungu mwenyewe ndiye anayeita watu wake katika huduma, na kwa sababu hiyo hakuna mtu ajitwaliaye heshima hii, wakati Mungu anapomuita mtu kwaajili ya huduma mtu huyo huwekewa kitu cha ziada na neema ya juu zaidi ili aweze kuwahudumia wengine, Hata hivyo bado hatuwezi kuwaachia hao peke yao walioitwa katika wito maalumu wa huduma kwa sababu kazi ya Mungu ni pana na hivyo wale wote ambao hawatakuwa wameitwa katika wito maalumu wanabaki katika wito wa ujumla wa kumtumikia Mungu na wakifanya kwa uaminifu na utii kazi ya Mungu itasonga mbele na kuwa Baraka kubwa kwa jamii, Unaweza kujua wito wako kupitia neno la Mungu, kupitia maombi, kupitia shuhuda za huduma za watu unao wahudumia, kuthibitishwa na viongozi, na amani ya moyo, wito ni zawadi, wito ni heshima, wito ni kuaminiwa, wito ni wajibu na kwa sababu hiyo kama Mungu amekuweka katika ajenda zake basi wewe ni wa muhimu sana itikia sauti ya Mungu leo ukamtumikie.

Yohana 12:26 “Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.”

Waebrania 3:14-15 “Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho; hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha.”                    

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumapili, 26 Julai 2026

UMUHIMU WA SHULE YA HUDUMA.


 

Waefeso 4:11-12 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa kusudi kubwa la shule ya huduma ndani ya kanisa ni kwaajili ya kukumbushana wajibu wetu wa kulijenga kanisa la Mungu, Mungu alitoa wengine kuwa Mitume, wengine kuwa Manabii, wengine kuwa Wainjilisti, wengine kuwa Wachungaji na Walimu kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, na kuhakikisha kazi ya huduma inatendeka na mwili wa Kristo unajengwa kwa hiyo kila mtenda kazi ni mjenzi katika nyumba ya Mungu Kanisa la Mungu linafananishwa na shamba, linafananishwa na jengo na sisi ndio wafanyakazi pamoja na Mungu kwa hiyo kila mtenda kazi ni mjenzi katika nyumba ya Mungu na tunapaswa kuifanya kazi yetu vema na kwa usahihi kwa sababu Mungu ataipima kazi ya kila mtu kwa hiyo kila mjenzi anapaswa kuwa makini namna anavyojenga katika jengo la Mungu.

1Wakorintho 3:6-15 “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu. Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.”

Katika nyumba ya Mungu kuna maeneo mbalimbali ambayo yanatutaka sisi kama watenda kazi kuwa makini, kuwa macho na kuyasimamia endapo tunataka kanisa letu likue kiroho na liwe kubwa lenye maelfu ya watu, ikumbukwe kuwa kadiri kanisa linavyokuwa kubwa linahitaji wahudumu wengi zaidi watakaotoa macho na kuhudumia maeneo mbalimbali na kumbuka kila tunapohudumu tunahudumia pamoja na Mungu kwa hiyo Baraka za Mungu huwa kubwa kwa kila mtenda kazi anayeifanya kazi yake kwa uaminifu, watenda kazi wengi wanapotupia macho maeneo mbalimbali ya kihuduma tunawapa watumishi wa Mungu nafasi kubwa ya kuomba na kulihudumia neno badala ya kushughulika na maswala ambayo yangeliweza kuangaliwa na watu wengine, aidha kanisa linapokua linatakiwa kuwa na wahudumu wengi zaidi ili kuzuia manung’unuiko miongoni mwa jumuiya ya  washirika katika kanisa la Mungu.

Matendo 6:1-4 “Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.”

Kwa msingi huo basi tutachukua muda kujifunza somo hili UMUHIMU WA SHULE YA HUDUMA kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo;-


  • Sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu
  • Jinsi tunavyoweza kujenga pamoja na Mungu
  • Vema mtumwa mwema na mwaminifu

 

Sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu.

Paulo mtume anaelezea wazi kuwa sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu, anasema hayo kwa kusudi la kuweka mkazo kuwa kazi ya Mungu haiwezi kwenda mbele bila wanadamu, Mungu alimuumba mwanadamu kwa kusudi la kuwa na ushirika na yeye na kwa sababu hiyo sisi tunabeba kusudi lote la Mungu hapa duniani, jukumu hili kamwe Mungu hajawahi kuwapa malaika lakini ametupa sisi, kwa hiyo ni jukumu la kila mtu aliyeokolewa kulijemga kanisa la Mungu na kuifanya kazi ya Mungu kazi hii iliyo njema.

1Wakorintho 3:9 “Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.”

2Wakorintho 6:1-2 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure. (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Mungu amempa mwanadamu jukumu zima la kuihubiri injili na kuieneza na kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi, hii ni heshima kubwa sana kwani tunapoifanya kazi hiii Mungu huwa hakuachi anakuwa pamoja nawe kwa sababu kazi hii sio yetu ni ya kwake kwa hiyo wewe kama mtoto wake unashirikiana naye katika kuikamilisha hakuna mahali popote ambapo Mungu alimuagiza mtu kazi kisha akamuacha, wakati wote mtu anapoifanya kazi ya Mungu neno la Mungu linaonyesha kuwa Bwana akawa pamoja naye

Marko 16:19-20. “Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]

Paulo anatumia mfano wa shughuli za kilimo kama kupanda na kumwagilia na hata maswala ya ujenzi kuonyesha kuwa katika mwili wa Kristo kila mmoja wetu ana majukumu mbalimbali, kutokana na vipawa mbalimbali na karama mbalimbali  lakini wote sisi tunaifanya kazi moja, kwa hiyo katika shule hii ya watenda kazi tunaainisha maeneo mbalimbali ya kiutendaji , hata kama wote tunajifunza hizi ili kumtumikia Mungu kwa pamoja baadae utaweza kuona kuwa tutamtumikia Mungu sehemu mbalimbali na kufanya huduma mbalimbali lakini katika mwili huu huu mmoja.

1Wakorintho 12:12-27 “Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi. Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo? Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa? Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.”

Kwa hiyo tutafanya kazi katika maeneo tofauti tofauti wakati mwingine kwa kupangiwa au wakati mwingine kutokana na kile kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yako lakini sisi sote tu watenda kazi na tufahamu kuwa tunaifanya kazi moja, asitokee mtenda kazi akafikiri kuwa hajaheshimiwa kwa kupangiwa eneo fulani, kokote tutakakoenda kumbuka Bwana yuko pamoja nawe na anajua kuwa unaujenga mwili wa Kristo, aidha tunafanya huduma hizi kwa neema ya Mungu kwa hiyo neema zinatofautiana kinachotakiwa kwetu ni uaminifu, usitake kuwa na huduma kama ya fulani kwa sababu kila mmoja ana neema tofauti na hivyo tutatumia neema hizo kwa kufaidiana

Waefeso 4:7-8 “Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.”

1Petro 10-11 “kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.”

Warumi 12:3-5 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani. Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.”               

Kwa hiyo utaweza kuona Mungu ametuita kutenda kazi pamoja naye kwa neema na vipawa na karama tofauti tofauti, tutumie kila alichotupa Mungu kumtumikia bila kuumiza mwili wa Kristo kwa migawanyiko na manung’uniko mbalimbali kwani wote tutaifanya kazi hii kwa kufikia lengo moja kuufikia ulimwengu na kuwaleta watu kwa Yesu na kulijenga kanisa lake ili baada ya utumishi wetu duniani tukakae naye kule mbinguni

Jinsi tunavyoweza kujenga pamoja na Mungu

Katika kanisa la Mungu kuna namna mbalimbali za utumishi ambazo kwazo tunaweza kuzitumia katika kumtumikia Mungu, Ni muhimu kwetu kufahamu kuwa tukiifanya kazi hii ya Mungu kwa hiyari, kwa moyo na kwa uaminifu Mungu mwenyewe atakupa thawabu na kukupongeza na kukufuta machozi kwa kazi hii ambayo ina upinzani kutoka kwa adui shetani lakini simama kwa uaminifu kwaajili ya Bwana kama alivyofanya mtume Paulo ambaye alivumilia

Mathayo 25:21-23. “Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.”

Washirika wanapohudumiwa vema na kufikiwa katika mazingira yote hasa katika makanisa makubwa wanaona kuwa wanajaliwa hata kama hawamuoni mchungaji kiongozi kutokana na majukumu yake umoja wa kanisa utaimarika, kanisa letu litakuwa kwa kasi kwa ukuaji wa aina zote nazungumzia ukuaji wa kiroho, ukomavu na wa kiidadi na kuwa kanisa la maelfu, umoja utaimarika hata pamoja na ukubwa wa kanisa, na wingi wetu utageuka utajiri na afya ya kila mmoja wetu na miujiza haitakoma umati utavuta umati na Mungu atataka kujidhihirisha kwenye kusanyiko la watu wengi, sasa haya ndio maeneo na mazingira tunayoweza kumtumikia Mungu wetu:-

  1. Kuwahudumiwa waamini wapya – Mojawapo ya eneo Muhimu sana ambalo watenda kazi wote, wanafunzi wote na wenye hekima wote tunapaswa kulipa uzito mkubwa sana sana ili tupate kanisa lililobora ni kuwahudumia waamini wapya, au kuwahudumia watoto wachanga kiroho, kuwafuatilia, kuwalisha kwa neno la Mungu na kufanya malezi, Kama tunampenda sana Yesu upendo wetu utaonekana kwa jinsi tunavyowalisha kondoo zake

 

Yohana 21:15-17 “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.”

 

Agizo hili ni pana kwani linahusu ulishaji mzima wa kondoo, watumishi wa Mungu walioitwa katika wito maalumu wataifanya kazi ya kuwalisha kondoo katika ibada, tulizojipangia na katika semina zitakazojitokeza na kadhalika, lakini watenda kazi, wanafunzi na wenye hekima (Wiseman) wao watapaswa kuhakikisha kuwa wanawahudumia na kuwalisha watoto wachanga kiroho kwa kuwafundisha masomo ya mwanzo ya wokovu, ukiwaimarisha waamini wapya katika wokovu, kwa kuwaombea, kwa kuwafundisha kuisoma Biblia, na kuwaelekeza kuhusu maisha  tamaduni na Misingi  ya imani ya kanisa letu

 

  1. Kuwahudumia waamini wote ibadani    - Eneo lingine la huduma zetu kama watendakazi, wanafunzi na wenye hekima ni kuwahudumia watu wote wanaohudhuria ibada katika kanisa letu, watu waliopitia shule hii ya huduma watawahudumia watu kwa kuwapokea vizuri na kwa heshima, kuwapokelea vitu vyao, watoto na kuwaongoza mahali sahihi pa kuketi, sio hivyo tu kama ni mgeni utafanya kila jitihada kutambua anaitwa nani namba zake za simu na atakuwa pamoja nasi kwa muda gani, kama ni wadhaifu tutawatia nguvu, na tutaanza kuwapandisha imani kuwa umefanya uamuzi wa busara kuja kuabudu katika kanisa letu hili zuri, hakikisha kuwa kila mtu ana mazingira salama ya kuabudu, atajua vyoo viko wapi, wasaidie kujua mambo muhimu wanayopaswa kuyajua, tutakuwa tayari kuhudumu pamoja na Muhubiri katika ibada kuu na maombezi na kusawaidia watu wanaoanguka kwa mapepo au nguvu za Mungu na wale wanaofunguliwa na kuhakikisha kuwa tunawahifadhi kwa nguo maalumu safi na kuwafunika, Pia kuwapeleka mahali salama na sahihi zaidi na katika ibada nyingine maalumu kama ubatizo, meza ya Bwana, kubariki watoto, na kadhalika

 

Yohana 10:14 “Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi

 

1Wathesalonike 5:14 “Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.”

 

Waefeso 4:1-3 “Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.”

 

  1. Kusaidia huduma ya kichungaji – Watendakazi wote, wanafunzi na wenye hekima wanapaswa pia kufanya kazi ya kutoa msaada wa huduma ya kichungaji, ikumbukwe kuwa Mchungaji hawezi kufanya kila kitu peke yake, na akilazimika kufanya yote muda wa kukaa katika neno la Mungu na maombi utafilisiwa na kuathiri huduma za kiroho za jumla  na ndio maana mitume waliona vema kuwa na mashemasi kwaajili ya majukumu

 

Matendo 6:1-7 “Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno. Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia; ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao. Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.”

 

Warumi 16:3-4. “Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.”

 

Kutoka 18:17-22 “Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako. Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao; nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.”

 

Wasaidizi wa huduma ya kichungaji watafanya majukumu ambayo yangewezwa kufanywa na mchungaji katika kanisa, majukumu hayo ni pamoja na kuwatembelea washirika, kuwasaidia katika maombi, kufanya ufuatiliaji, na kufanya uashauri wa kichungaji, huduma hizi zote zinafanyika chini ya utumishi wa mchungaji kiongozi katika kanisa

 

  1. Kuwahudumia wale wanaotokwa na pepo – watenda kazi, wanafunzi na wenye hekima ni wajibu wao kuhakikisha kuwa mambo yote katika nyumba ya Bwana yanafanyika kwa kufuata utaratibu, Mungu ni Mungu wa utaratibu na anataka mambo yote yafanyike kwa utaratibu, kwa msingi huo, moja ya huduma wanayotakiwa kuifanya ni kuwahudumia wenye kuteswa na mapepo hasa katika ibada za maombezi, wanaousumbuliwa na pepo kama ni wakati ibada inaendelea ni lazima wahamishiwe kwenye vyumba maalumu vya maombezi, lakini kama machungaji yuko katika kuwashughulikia na wanaangushwa au kusumbua miongoni mwa watu watolewe na kupelekwa mbele au sehemu maalumu wanakoweza kuwa na nafasi ya kuhudumiwa na kufunguliwa kanisa linapokuwa tayari na watendakazi wanapokuwa tayari kuhudumu pamoja na Mchungaji na kuhudumu pamoja na Roho wa Mungu kwa utaratibu maalumu, Mungu Roho Mtakatifu atafanya miujiza mikubwa zaidi, kama pepo watasumbua wakati neno la Mungu linaendelea, wenye pepo wapelekwe sehemu nyingine ili neno la Mungu lihubiriwe kwanza, na wasipoteze usikivu!

 

1Wakorintho 14:39-40 “Kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha. Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”

 

Waefeso 6:11-12 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”

 

Mapepo yanaweza kuwaathiri watu lakini kumbuka kuwa watu sio pepo, kwa hiyo utu wa aliyeathiriwa uthaminiwe na atunzwe kwa heshima zote, tusiwakasirikie wala tusiwe na msisimko ni lazima tuwe wapole na waungwana tuwahifadhi tuwasaidie kufunguka, tuwapeleke sehemu maalumu zilizoainishwa, tuwafute vizuri na tuchukue taarifa zao kwaajili ya ufuatiliaji na kwaajili ya kutunza muujiza na ushuhuda wa baadae

 

Mwondoe mwemye pepo katikati ya umati wa watu, kama ikiwezekana, tumia mamlaka kwa ustaarabu kuyakemea na sio kelele, usitumie nguvu kumbuka pepo wanatoka kwa jina la Yesu na kwa nguvu za Roho Mtakatifu wewe na mimi sio tunaotoa pepo, Pepo wanatolewa na Roho, sisi wajibu wetu ni kuwapa imani na kuwasaidia wao kupokea muujiza wao, msikemee watu wengi pepo mmoja mamlaka moja inatosha.

 

Mathayo 12:28-29 “Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.”         

 

2Timotheo 2:24 “Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;”

 

  1. Kuwahudumia watu wanaoangushwa chini – uwe na uwezo wa kutambua ni aina gani ya sababu imempeleka mtu chini, sio kila anayeanguka chini ni kwa sababu ya pepo, wengine wanaweza kuigiza tu, na wengine wanaweza kuwa wamehemewa na hisia kali, na wengine ni kwa sababu ya nguvu za Mungu anaangushwa chini lakini anaweza asiwe na pepo, kwa hiyo usikimbilie kukemea pepo, kwa sababu wengine huangushwa tu na nguvu za Mungu na anaweza kujisikia vibaya kudhaniwa kuwa ana pepo.

 

Luka 5:16-17 “Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba.Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.”

 

Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”

 

Wahudumu, watendakazi, wanafunzi na wenye hekima kumbuka ya kuwa lolote linaweza kutokea wakati wa maombezi, na wakati wa ibada jiandae kusimama nyuma kwa huduma, kwa wale wanaohudumiwa,  jiepushe kusukuma watu, tunza heshima ya watu hususani wanawake, wafunike wanapokuwa wamekaa vibaya, hakikisha kunakuwa na utulivu na amani tengeneza mazingira ya Amani, wasaidie kwa upole, omba kimya kimya, na usiwakasirikie wala kuwaudhi wao ni kama wagonjwa wetu na sisi ndio wahudumu wao, jua ya kuwa Mungu ndiye anayewahudumia pamoja nawe kwa sababu hiyo tuwahudumie kwa huruma na upendo

 

  1. Kuwahudumia wageni ambao ni mara yao ya kwanza – Wakristo wanahimizwa kuwa wakarimu, unapowapokea watu vizuri kwa tabasamu la upendo na kuwapa muongozo mzuri, bila papara na kwa kuwaonyesha upendo wao watajua kuwa kweli hapa ni kanisani, kanisani ni mahali ambapo watu wanapaswa kupokelewa kwa upendo kuliko mahali kokote kule, kanisani ni zaidi ya dukani, hotelini, gengeni  na kadhalika waonyeshe watu uungwana mkubwa, msalimie vizuri, mpe ratiba na muelekeo wa ibada,  usimuache akajitenga, zungumza kwa lugha za kawaida, waonyeshe shukurani waonyeshe kuwafuatailia baada ya ibada, wageni wangependa kuagana na mtu yule yule aliyempokea mwanzoni hasa kama ulimpokea vizuri, kwa hiyo yule utakayempokea mwanzoni ni mteja wako mpaka mwisho usimpoteze

 

Waebrania 13:1-2 “Upendano wa ndugu na udumu. Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.”

 

Yohana 13:34-35 “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”

 

1Wakorintho 9:19-23 “Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi. Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria. Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu. Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.”          

 

  1. Kuwahudumia viongozi wa serikali – Viongozi wa serikali na viongozi wakubwa wa kitaifa wanaweza kuwa wakristo wenzetu katika kanisa la Mungu lakini pia wanaweza kuwa rafiki zetu na wanaweza kutembelea kanisa letu kwa taarifa au ghafla watendakazi katika kanisa tunapaswa kuwahudumia kwa heshima na ustaarabu pia, heshimu nafasi waliyo nayo lakini usiwaabudu, usilichuje neno la Mungu kwaajili yao, weka heshima sawa na maelekezo ya injili, Mungu hana upendeleo, lakini anayestahili heshima heshima, viongozi wahudumiwe vizuri na kukaribishwa na kama iko sehemu maalumu ya wageni maalumu wanaweza kuelekezwa hapo, kama ni kiongozi mwenye itifaki (Protocol) kadhaa wasikilize viongozi wa itifaki walioambatana naye na shirikiana nao katika utaratibu mzuri, mawasiliano mazuri na kadhalika, kauli za kisiasa kanisani haziruhusiwi, unabii unaohusu wanasiasa, haufai, isipokuwa kama Mungu amesema hivyo, na hakuna sababu za kulazimisha maombi ya kitaifa kama hakukuwa na programu hiyo msibadili gea angani, jiamini, tunza heshima jiepushe na mizaha inayoweza kutafasiriwa vibaya maneno yako yajae neema.

 

Warumi 13:7-8 “Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima. Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.”

 

1Petro 2:17 “Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme

 

Wakolosai 4:5-6. “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.”  

 

  1. Kuwahudumia watumishi wa Mungu – Watenda kazi, wahudumu, wanafunzi pamoja na wenye hekima katika kanisa wanawajibu pia wa kumuhudumia mchungaji, wakati wote huduma inapoendelea pamoja na shughuli nyingine tutakuwa katika maombi ya kimya kimya tukiendelea kuhudumu pamoja na mtumishi wa Mungu, wafunikwe kwa kuwaombea, uwe na karama ya kupambanua roho na kung’amua kwa haraka watu wanaotaka kuwashambulia watumishi wa Mungu, angalia kama amechoka, angalia kama amekata tamaa, angalia kama anapingwa, angalia kama anahitaji kitambaa cha jasho, maji ya kunywa ama kama analetewa kitu kibaya, wekeni utaratibu wa ulinzi na usalama kwaajili ya kanisa zima na kwaajili ya mtumishi wa Mungu, dhibiti watu kumfikia kwa haraka bila utaratibu, au wale wanaotaka kumshambulia, wekeni timu ya itifaki ya namna ya kumfikia mtumishi wa Mungu, kataza wanaomsengenya, wasahihishe wasiomuelewa, mlinde bila kupigana, muheshimu bila kumuabudu, heshimu mipaka, wajibika kwake, lindeni kile Mungu ameweka ndani yake,  Mke wake na familia yake na kadhalika, tunapowahudumia watumishi wa Mungu tunamuhudumia Mungu pia.

 

Yohana 12:20-21. “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu. Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu. Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.”

 

Zaburi 105:14-15”Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.”

 

1Timotheo 5:17 “Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha

                 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima