1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata
ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye
hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na MLANGO
WA KUTOKEA, ili mweze kustahimili.”
Utangulizi:
Ni muhimu kuwa na ufahamu kuwa
katika maisha ya wanadamu wote sio waliookoka peke yao wote kupitia katika
majaribu mbalimbali ni jambo la kawaida na lisiloepukika, Maandiko
yanatufundisha kuwa hakuna jaribu jipya kila majaribu au jaribu unalolipitia
wewe duniani wako watu wamelipitia pia na wakati mwingine jaribu kubwa au
analipitia kwa njia ngumu kuliko unayoipitia wewe, na kwa sababu hiyo hatupaswi
kabisa kushangaa na kuona kuwa ni kitu kigeni au cha ajabu kitupatacho.
1Petro 4:12-13 “Wapenzi, msione kuwa ni
ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana
kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya
Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.”
Mitume walikuwa wanamaanisha
Msiba/Majaribu au mambo ya kuhuzunisha na ya kuumiza yanayowapata watu wa Mungu
ni ya kawaida kwa wanadamu wote ni mambo yanayowapata wanadamu wote wana wa
Mungu na wanadamu wakawaida wasiomuamini Mungu, kwa vile tu tuko Duniani basi
majaribu haya Mitihani hii/na Magumu yaani (test and trials or temptations) ni
jambo la kawaida sio geni na sio ajabu na halikupati au halijawahi kukupata
wewe peke yako, watu wengi sana wanapitia hayo kwa hiyo sio kitu kigeni, na
habari njema zaidi ambayo Roho Mtakatifu
anaizungumza leo ni kuwa kwa kila jaribu Mungu atafanya na mlango wa kutokea,
au atafanya njia mbadala ya kutokea!
Leo leo basi kwa uweza wa Roho
Mtakatifu tutachukua muda basi kujifunza na kutafakari kwa undani kuhusiana na
kifungu hiki muhimu cha maandiko kwa kukiangalia kwa kina na mapana na marefu
ili tuweze kupata kile Mungu anataka kusema nasi kwa kuzingatia vipengele
vitatu vifuatavyo:-
·
Jaribu
kawaida ya wanadamu;
·
Mungu
atafanya mlango wa kutokea:
·
Mlango wa
kutokea
Jaribu kawaida ya wanadamu:
1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata
ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye
hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na
mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”
Ni muhimu kwanza kufahamu kuwa
Paulo mtume hapa anazungumzia kwamba majaribu/na mitihani ni kawaida ya
wanadamu, Paulo hapa anawaelezea watu waliookoka wa Korintho kwamba majaribu ni
kawaida ya wanadamu; maana yake majaribu ni ya kawaida kwa watu wote, na sio
wailiookoka peke yao Katika Biblia ya kiyunani neno kawaida ya wanadamu
linasomeka kama “Anthrōpinos” ambalo kwa kiingereza
linasomeka kama “human common to man”
kwamba majaribu huwapata wanadamu wote, aina binadamu wote, watoto wa Adamu
wote, kila mtu, kila mwanadamu common to
man, common to mankind, common to men after the manner of men kwa lugha
nyingine It emphasize that no
temptation/trials is unique to an individual in its nature inakaziwa hapo kuwa hakuna jaribu au mtihani ambao unaweza kuwa wa kipekee kwa mtu fulani
tu kwa asili na kwa sababu hii mitume wengi na manabii waliandika kuwa
kamwe mwanadamu awaye yote hapaswi kuona kuwa ni ajabu, au ni kitu kigeni
kimpatacho kwa hiyo tunapopitia changamoto mbalimbali zinazozalisha huzuni/msiba
duniani hupaswi kudhani kuwa ni wewe tu unayepitia hayo, na hii inatusaidia
tusilie na kumlaumu Mungu Baba kwa nini
mimi tu “WHY ME ALONE!” kwa hiyo
maana yake swala la kujaribiwa, kuudhiwa, kupitia magumu, kuibiwa, kuonelewa,
kudhulumiwa, kuachika, kutapeliwa, kufilisika, kukosa, kufukuzwa kazi,
kushindwa kisiasa na kadhalika na mitihani mbalimbali mambo ya kuumiza
hayakupati wewe pekee huwapata “WOTE”
kwa sababu hiyo hauko peke yako na usione ajabu kwa hiyo tuwapo duniani/ulimwenguni
dhiki ni kawaida, “KAWAIDA”
Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa
na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi
nimeushinda ulimwengu.”
Yohana 16:1-4 “Maneno hayo nimewaambia,
msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila
mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu
hawakumjua Baba wala mimi. Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile
itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo,
kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi.”
1Petro 4:12-13 “Wapenzi, msione kuwa ni
ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana
kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya
Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.”
Kwa hiyo kwa mujibu wa neno la
Mungu majaribu, vishawishi na dhiki na mateso na adha ni jambo la kawaida
tuwapo Duniani, kila mwanadamu anapitia changamoto za aina mbalimbali kwa
nyakati mbalimbali, unaweza ukapitia jambo zito na ukapiga kelele kumbe wako
waliopita na wamekaa kimya hii ni hali ya kawaida na hatupaswi kuona ajabu wala
hatupaswi kuona kuwa ni kitu kigeni. Jaribu haliwapata ninyi ISIPOKUWA LILILO KAWAIDA kwa hiyo
mpenzi unayoyapitia ni ya KAWAIDA.
Mungu atafanya mlango wa kutokea:
1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata
ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye
hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na
mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”
Katika namna ya kipekee sana Neno
la Mungu linatutaarifu kuwa pamoja na kuweko kwa majaribu na mitihani ya aina
mbalimbali Paulo anasema Mungu ni mwaminifu ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita
mwezavyo yaani maana yake Mungu hataliacha jaribu likuumize au likuzamishe na
au lilete uharibifu badala yake ataleta msaada maana yake ATAFANYA NA MLANGO WA KUTOKEA hapo liko jambo la kujifunza tena
kuhusu tabia na mwenendo wa Mungu kwa watu wake Mungu atafanya mlango wa
kutokea hii maana yake ni nini?
Katika Biblia ya kiyunani neno
mlango wa kutokea linasomeka “Ekbasis” au “Exodos” ambalo kwa kiingereza ni
“a way to escape” au “exit”, “way out”, “departure” au “release” kwa Kiswahili ni mlango wa kutokea, au
njia ya kutoka au njia ya kutoka kwa uhuru, au kutolewa, Kimsingi anachokizungumzia
Paulo mtume hapo ni Njia au mlango ambao mtu huweza kuutumia kuondoka wakati wa
mazingira ya hatari au mazingira yenye shinikizo, Kwa hiyo Mungu katika Hekima
yake kama walivyo wajenzi wa majengo mbalimbali duniani na vyombo mbalimbali vya
moto huwa wanaweka mlango maalumu wa dharula linapokuwa limetokea tatizo ili
watu waweze kuokoka na kuepuka madhara wakati wa matatizo, Mlango huo au njia
hiyo huitwa mlango wa dharula, Milango hii huwa na alama maalumu za kuonyesha
mahali pa kukimbilia na kutokea endapo kutatokea jambo la dharula na imeokoa
wengi.
Mlango wa dharula kwa kawaida
huweko katika majengo yote na vyombo vyote muhimu na ni mlango au njia
inayotumika kwa makusudi ya usalama, Mlango wa kutokea EXIT hujengwa maalumu kwaajili ya matukio hatarishi kama moto au
ajali na hivyo hutoa njia iliyo wazi
kwaajili ya kuwasaidia wahusika na kupunguza hatari na vifo kwa watu wa jengo au
chombo husika badala ya kutumia mlango mmoja au mlango uliozoeleka jambo ambalo
linaweza kusababisha maumivu makubwa sana, Mlango wa dharula wa kutokea
hubuniwa na wajenzi kwa kusudi la kupunguza taharuki na kuwapa watu wepesi wa
kuepuka madhara, ni mlango unaokufanya utoroke kwa haraka bila kuchanganyikiwa
wala kubanana na watu, ni mlango unaosaidia watu kupata njia ya dhalula wakati
wa mahitaji, ni mlango unaokueepusha na kifo, ni mlango wa wokovu, ni mlango wa
kuzuia taharuki, ni mlango unaotoa urahisi na msaada wa haraka wakati wanadamu
wanapokuwa wamechanganyikiwa kwa sababu ya vita, ni mlango wa kutorokea wakati
umezingirwa na adui pande zote, ni mlango wa kukimbilia wakati wa tetemeko,
ajali ya moto na changamoto nyinginezo, ni mlango ambao mafundi huutengeneza
maalumu ukiwa na uhakika wa kutoa usalama kwa watumiaji wa majengo, magari,
treni, ndege na uvamizi wa ikulu au majengo makubwa ya watu muhimu, na majengo
ya serikalini, mlango huo huwekewa alama za mtu anayekimbia na maneno makubwa EXIT kunyesha eneo la kutokea kukiwa na
dharula, wakaguzi wa majengo na wathibiti ubora wakikuta hakuna alama hizo au
aina ya ujenzi unaotoa mlango wa kutokea wanaweza kugoma kutoa kibali cha
usalama wa jengo au chombo husika, sasa basi ikiwa wajenzi hawa wa kawaida
wanaweza kukumbuka kuweka mlango wa dharula katika majengo yao ya kawaida Paulo
anatuambia kuwa Mungu naye katika hekima yake akiwa ni Mjenzi Mkuu Mwenye
hekima na akili ya hali ya juu anajua kuwa bila kutuwekea njia ya dharula na
njia ya kutokea wakati wa changamoto tunaweza tukaelemewa na changamoto hizo na
zikatutoa katika mapenzi yake kwa hiyo ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa kwa kila
jaribu Mungu atafanya na mlango wa kutokea! Escaping way or door Haleluya!
Isaya 43:19-21 “Tazama, nitatenda neno
jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na
mito ya maji nyikani. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni;
kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu,
wateule wangu; watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.”
Mlango wa kutokea ni uweza wa
Mungu wa kukufanya ushinde kikwazo chochote na kuleta suluhu wakati mazingira
yanayokuzunguka yanaonyesha kuwa haiwezekani, Mungu wetu ni mwenye uwezo wa
kufanya njia hata jangwani yaani mahali ambapo haiwezekani kufanya njia, Neno
la Mungu linaposema atafanya njia jangwani kama unalifahamu jangwa vizuri huwa
linakuwa na michanga na upepo mkali na kwa sababu hiyo sio rahisi kuona njia
jangwani kwa hiyo Mungu wetu hufanya njia pasipo na njia, wakati mtu anapohitaji
msaada wa karibu na ikaonekana kuwa ni ngumu msaada huo kupatikana yeye kwa
uwezo wake analeta msaada huo na kwa sababu hiyo kwa kila jaribu Mungu hufanya
njia, Mungu kamwe hawezi kufungwa na mipaka ya kibinadamu na ya kimazingira na
ana uwezo mkubwa wa kuingilia kati kimuujiza na kukuwezesha kushinda mwamini
yeye tu atafungua mlango huo kama alivyowafanyia wengine, kwa kila jaribu lako
unalolipitia Mungu atafanya mlango wa
kutokea:-
-
Alifanya
mlango wa kutokea kwaajili ya Ishamel na Hajiri walipokuwa wanakabiliwa na njaa
na kiu alisababisha kisima cha maji kikatokea na Ishmael na Hajiri wakawa na
uhai na maisha yao yakaendelea wakati ambapo Hajiri alikuwa akikitazamia kifo
cha mtoto naye ye mwenyewe, Mungu alimtuma malaika wake na wakamfunulia jambo
la kufanya!
Mwanzo 21:15-21 “Yale
maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. Akaenda
akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema,
Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia. Mungu
akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni,
akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana
huko aliko. Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa
nitamfanya kuwa taifa kubwa. Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha
maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. Mungu akawa pamoja na
huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde. Akakaa
katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.”
-
Alifanya
mlango kwaajili ya wana wa Israel kwa kuifanya bahari ya Shamu kugawanyika
kisha Israel wote wakapita kwa uweza mkubwa, ingawa walikuwa wako katika
kufungwa utumwani na kuzingirwa na maadui na kuwa katika wakati Mgumu
walipoogopa na kulia kwa kukosa matumaini yeye alifungua mlango ambao haujawahi
kutarajiwa duniani!
Kutoka 14:8-18 “Na
BWANA akaufanya moyo wake Farao mfalme wa Misri kuwa mgumu, naye akawafuata
wana wa Israeli; kwa sababu wana wa Israeli walitoka kwa ujeuri. Wamisri
wakafuata nyuma yao, farasi zote na magari yote ya Farao, na askari zake wenye
kupanda farasi, na jeshi lake, nao wakawapata hali wamepanga pale karibu na
bahari, karibu na Pi-hahirothi, kukabili Baal-sefoni. Hata Farao alipokaribia,
wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao;
wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia BWANA. Wakamwambia Musa, Je! Kwa
sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona
umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri? Neno hili silo tulilokuambia
huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia
Wamisri kuliko kufa jangwani. Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu,
mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo
hamtawaona tena milele. BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. BWANA
akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee
mbele. Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya;
nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu. Nami, tazama,
nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao wataingia na kuwafuatia, nami
nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote, kwa magari yake na kwa
wapanda farasi wake. Na Wamisri watajua ya kuwa Mimi ndimi BWANA,
nitakapokwisha kujipatia utukufu kwa Farao, na magari yake, na farasi zake.”
-
Alifanya
mlango wa kutokea kwa Samsoni ambaye alipokuwa anazimia kwaajili ya kiu na
hakuwa na msaada Mungu akatokeza maji kutoka katika mwamba na roho yake
ikaburudika, mtu ambaye alikuwa afe kwa kiu lakini alipomuomba Mungu alipewa
ufumbuzi, Mungu aipasua mwamba na kumpa Samsoni maji a kunywa na roho yake
ikaburudika
Waamuzi 15:18-20 “Kisha
akaona kiu sana, akamwita Bwana akasema, Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa
mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu
wasiotahiriwa. Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi,
pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa
hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi
leo.Naye akawa mwamuzi wa Israeli: katika siku za Wafilisti muda wa miaka
ishirini.”
-
Alifungua
Mlango kwaajili ya Petro aliyekuwa gerezani na akitarajiwa kuuawa na Herode
kama tu alivyouawa mtume mwenzake siku zilizopita, Kanisa waliomba kwaajili
yake Jaribu lilionekana kama halina suluhu lakini Mungu ni mwaminifu alifanya
mlango wa kutokea
Matendo 12:1-11 “Panapo
majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya
watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. Na akiona ya
kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa
siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia
mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya
Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo
kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka
kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili,
amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara
malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga
Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka
mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha
akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua
ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na
walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia
mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara
malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya
kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika
kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.”
Kwa msingi huo bila kujali ni
hali gani unaipitia, ni changamoto gani uliyo nayo, ni mtihani gani unatokea
katika maisha yako, Kumbuka na kuelewa kuwa Mungu ni zaidi ya wajenzi na
waundaji wa vitu mbalimbali; kama wanadamu wa kawaida tu wanaweza kukumbuka
kuweka mlango wa ufumbuzi wa mambo basi kumbuka Mungu ni zaidi yao kwa hiyo kwa
kila jaribu ameweka au ataweka na mlango wa kutokea, Bwana atakutoa katika
majaribu yako, atakuokoa na changamoto zinazokukabili, atakuokoa na umasikini,
atatokeza njia katika huzuni zako, atakutoa katika upweke wako, atafungua
mlango wa ajira kwako, atatokeza mlango wa ndoa, ataokeza mlango wa uzazi Bwana
ataweka mlango wa kutoka katika madeni, ataweka mlango wa kutoka katika maumivu
yako kila jambo linalokusibu Bwana ana njia na ana mlango kwaajili ya hilo
hatupaswi kuzitumainia akili zetu wenyewe bali tunapaswa kumtumainia Mungu
kwani yeye atanyoosha mapito yetu yote maana yake atatutengenezea njia, kila
linapokukuta jambo gumu usisite kuliitia jina la Mungu kwa msaada!
Mithali 3:5-6 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako
wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye,
Naye atayanyosha mapito yako.”
Zaburi 34:17-19 “Walilia, naye Bwana
akasikia, Akawaponya na taabu zao zote. Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na
waliopondeka roho huwaokoa. Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana
humponya nayo yote.”
Mlango wa kutokea
Kimsingi Yesu Kristo anahusika
moja kwa moja kama mlango wa kutokea, tunaweza kusema kuwa yeye ndiye MLANGO WA KUTOKEA kunapotokea
changamoto za aina yeyote yeye ni mlango, yeye ni njia na yeye ndiye wa
kutazamwa katika maisha yetu linapotokea jambo lolote lililo gumu, Mungu
amemtoa Yesu Kristo kwetu kuwa mlango, kuwa njia na kuwa wa kutazamwa kama
mlango wa kutokea, kila mtu na kila mwanadamu anapokabiliwa na lolote lile na
changamoto yoyote ile tunaye Yesu Kristo ambaye ndiye mlango wa kutokea.
Yohana 10:7-9 “Basi Yesu aliwaambia tena,
Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. Wote walionitangulia ni
wevi na wanyang'anyi; lakini kondoo hawakuwasikia. Mimi ndimi mlango; mtu
akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”
Yohana 14: 6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi
njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”
Yohana 3:14-16 “Na kama vile Musa
alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi
kuinuliwa; ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye. Kwa maana
jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu
amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
Mungu mwenye upendo mkubwa sana
kwa wanadamu hajatuacha tu hivi hivi ili eti tuelemewe na majaribu ya aina
mbalimbali mpaka tushindwe yeye ni mwaminifu kwetu na huliangalia neno lake
apate kulitimiza, hangeweza na hataweza kutuacha bila ya msaada kwa sababu hiyo
unapopita majaribuni kumbuka Mungu ameweka Mlango wa kutokea ni wajibu wetu
sisi kuutumia mlango huo pale tunapochanganyikiwa na kujikuta wenyewe, kama
tusio na msaada, au wenye kusongwa na mawazo na kufikiri kuwa tutafanyaje,
kumbuka kuliitia jina la Bwana kwani kila atakayeliitia jina la Bwana
ataokolewa, Yesu ndiye Mlango wa kutokea, umebanwa kokote kule, una changamoto
yoyote ile, unakabiliwa na mambo magumu yoyote yale changamka na kukumbuka kuwa
uko Mlango wa kutokea kwaajili ya wokovu wako Mlango huo ni Yesu Kristo Mwana
wa Mungu aliye hai!
1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata
ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye
hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na
mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”
Na Rev. Innocent Samuel Kamote.
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!