Jumatano, 10 Julai 2019

Ee Bwana unijie Hima!


Zaburi 141:1-2Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo. Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.”

Muhamiaji aliyeingia Nchini Ufaransa na kugeuka Mwokozi wa haraka Mamouddou Gassama .

Utangulizi:
Tarehe 28 May 2018 Dunia ilipata habari za mshangao na mara moja jina la raia wa Mali ajulikanaye kama Mamoudou Gassama lilipata umaarufu mkubwa, Mara baada ya kijana huyo kufanya tukio la kishujaa la kumuokoa mtoto mdogo aliyekuwa ananing’inia Katika ghorofa na aliyekua anaonekana anakaribia kuachia na kupoteza maisha

Tukio hili la haraka la kuokoa maisha ya mtoto, ghafla liliweza kubadilisha jina la kijana huyuwa Mali, aliyekuwa ni mzamiaji tu katika nchi ya Ufaransa, kijana huyu alijulikana kama shujaa na watu wengi walimuita “SPIDERMAN” Gassama kutokana na ushujaa wake alialikwa na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ikulu na kupata naye chai kisha kumpongeza kwa tendo lake la ushujaa, alifutiwa halia ya kuwa mzamiaji na kupangiwa kupewa kazi na mafunzo kupitia kikosi cha uokoaji  na zimamoto cha ufaransa BRAVO alisema rais Macron akimsifia Gassama kwa kazi njema, lakini pia alimzawadia medali ya Ujasiri na kujitoa, Gassama alipanda kwa haraka baraza kwa baraza mpaga ghorofa ya tano alikokuiwako mtoto huyo wa mika minne na kufanikiwa kuyaokowa maisha yake.

Gassama anasema walikuwa wakiangalia mpira na ghafla alisikia sauti ya watu wakipiga kelele za mayowe ya kukata tamaa na alipotoka na kuona ni mtoto anasema alimuhurumia na kwa kuwa anapenda watoto hakujiuliza maswali alijikuta anapanda na kuokoa maisha ya mtoto huyo kwa haraka.

Ee Bwana nimekuita unijie hima!

Ni muhimu kufahamu kuwa katika maisha yetu yako majaribu na changamoto za aina mbalimbali na kwa kawaida changamoto na majaribu huwa hayapigi hodi wakati yanapokuja , unaweza ghafla tu ukajikuta umevunjika moyo na umekata tamaa, ama unaweza kuwa kwenye wakati wa furaha kubwa , au ukajikuta umejeruhiwa na kushindwa bila maandalizi, wala hodi, wala kibali, majanga yanakuja tu yanakukabili kama kimbunga na wakati wote majaribu yanakuja kwa kusudi la kukupeleka chini na kukukatisha tamaa

Majaribu yanaweza kukuweka au kukuacha ukiwa unabembea kama mtoto yule na huu ndio wakati ambapo uatamtaka mwokozi ajitokeze kwa haraka aje akusaidie na hiki ndicho kilichomkuta mwandishi wa Zaburi 141: 1Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo. Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioniMwandishi alikuwa anahitaji msaada wa haraka Biblia ya kiingereza ya NIV inasomeka hivi “O lord, I call to you; come quickly to me , hear my voice when I call to you”wataalamu wa maandiko wanasema Zaburi hii ni ya Daudi na ni wazi kuwa ilisemwa wakati wa tukio linalotajwa katika 1Samuel 24:1-22 hususani kwa kitendo cha Sauli aliyekuwa akimtafuta Daudi kwa hasira na kutaka kumuua, wakati huu Sauli aliingia katika pango ambalo kwa bahati Nzuri Daudi alikuwa amejificha na watu wake, Daudi angeliweza kumdhuru Sauli kwa kumkata na panga huko ENGEDI lakini Daudi aliweza kujizuia asiyadhuru maisha yake, aliweza kukata upindo nwa vazi lake, na akiwa kimyaaa baadaye Sauli alitoka katika Pango lile na Daudi alitoka katika pango lile nankisha akakaa ng’ambo na kumueleza kuwa angeweza kumuua lakini aliheshimu kuwa yeye ni mpakwa mafuta japokuwa yeye alitoka kutafuta kumuua na timu yake yote lakini yeye Daudi hakumuua

Ni Katika wakati ule wa hatari sana Daudi aliomba maombi haya wakati Adui yake akiwa karibu kabisa kumuangamiza na endapo tu angeshindwa hata kuzuia kinywa chake Sauli angegundua kuwa daudi nyuko karibu na angemuangamiza

Lilikuwa ni jaribu zito na la ghafla katika maisha ya Daudi Lakini Mungu alimetetea, tunajua kuwa wakati wa Mungu ni mzuri zaidi, na kuwa hatuwezi kumlazimisha Mungu kujibu maombi yetu, Lakini iwe ni kwa haraka au taratibu ni lazima tumuonyeshe Mungu kuwa hatuna kingine tunachikitegemea isipokuwa yeye tu

Kwa vile bado tungalimo duniani, jambo lolote laweza kutokea je wakati huo unakimbilia nini? Ni jambo gani unaweza kulitumaini kwa haraka, ni jina gani unaweza kuliita kwa haraka unapokuwa umevamiwa na changamoto, lazima tujikite katika kuonyesha kuwa tunahitaji rehema za Mungu, kila wakati katika maisha yetu, tuendelee kuliiitia jina la Mungu

Pale jijini Paris watu wengi walikuwa wamemuona mtoto yule aliyekuwa anabembea, na wote walianza kulia na kupiga kelele, mtoto alikuwa hatarini alikuwa kwenye uhitaji wa msaada wa haraka wakati huu Mungu alimtumia mkimbizi, muhamiaji, mzamiaji kutoka mali, mweusi kumuokoa mtoto huyu, Hakuwa ndugu yake wala wa jamaa yake alimuonea huruma akafanya haraka

Uko wakati katika maisha yetu tunamuhitaji Mungu kwa haraka aafnye hima atusaidie, hatujui atatumia njia gani, lakini tukimtegemea yeye yeye ni msaada ulio karibu, Yeye si Mungu aliyembali

Zaburi 46:1-3
Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.”

Namsihi sana Mungu awe Msaada ulio karibu katika maisha yako wakati yanapokujia maswala mazito ya ghafla

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima.

Endapo umebarikiwa na mafundisho haya tafadhali moyo wangu ungependa kujua sms kwa namba 0718990796 pia kwa whatsApp Ubarikiwe sana

Hakuna maoni: