Ijumaa, 5 Machi 2021

Kumbuka aliyokufanya Amaleki !


Kumbukumbu 25:17-19 Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri; jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu. Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha Bwana, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.”


Utangulizi:

Moja ya matukio mabaya sana ambayo Israel walitakiwa kuyakumbuka Daima ni pamoja na ukatili mkubwa waliofanyiwa na wana wa amaleki (Amaleki). Musa analikumbuka sana tukio hili baya na la kinyama na anawaandikia Israel na kumkumbusha Joshua kutokulisahau tukio hili baya na la kinyama  lililopata kufanywa na Wamaleki!. Wana wa Israel walikuwa wamefanyiwa mambo ya kikatili sana katika nchi ya Misri, waliteswa na kutumikishwa katika utumwa mkubwa na mzito kwa muda wa zaidi ya miaka 400, waliugua na kulia na kibinadamu haingekuwa rahisi mtu awaye yote kuwaondoa katika utumwa huo mzito isipokuwa tu pale ambapo Mungu alikuja kuingilia kati unawezakuona.


Kutoka 3;7-10 BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.


Huu ndio ulikuwa mpango wa Mungu na mapenzi kamili ya Mungu, kwamba awakomboe wana wa Israel na kuwafikisha katika nchi ya mkanaani nchi iliyojawa maziwa na asali, aweze kuwafariji na kuwafundisha mapenzi yake ili kwamba kupitia wao jamaa zote za dunia zipate kubarikiwa kupitia mwana wake mpendwa Yesu Kristo ambaye kinabii angetokea Israel na kuwa ishara ya kuaminiwa duniani kote, kwa hiyo Taifa hili lilikuwa limebeba mpango na mapenzi kamili ya Mungu, Mungu aliwapitisha katika jangwa hili zito na la kutisha apate kuwafundisha imani na kumtegemea yeye ili wawe watu wake Lakini wakiwa njiani pamoja na vikwazo vingi walivyokuwa wamekutana navyo walitokewa kabila hili la jangwani waliojulikana kama Amaleki watu hawa walifanya vita na Israel, Kitabu cha kutoka kimetuficha sababu ya vita hii kinaeleza tu walivyotokea na kupigana na Israel na Yoshua akatumwa kuwapiga kwa msaada wa maombi ya Musa unawezakuona katika

Aliyoyafanya Amaleki:-

Kutoka 17:8-14 Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na Waamaleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima. Ikawa, Musa alipouinua mkono wake, Israeli walishinda; na alipoushusha mkono wake, Amaleki walishinda. Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa. Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga. BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena

Mungu anakasirishwa sana na tendo la Amaleki kushindana na Israel na akaagiza kuwa Musa ni lazima alihubiri jambo hili kwa Yoshua na  wana wa Israel walikumbuke tukio hili milele, aliambiwa aliweke tukio hili katika kitabu cha kumbukumbu ukumbusho kuwa kizazi cha Amaleki kitashughulikiwa siku zote mpaka kifutike kabisa duniani, sababu kubwa ni kuwa kilikuwa kizazi cha watu katili sana hawakuwa na huruma hawakuwaonea huruma watu waliotoka katika mateso kwa muda mrefu sana waliotakiwa kuhurumiwa waliostahili kuhurumiwa  na waliokuwa wanahitaji msaada, watu waliokuwa wanahitaji msaada na huruma na huduma na kutiwa moyo na msaada wa kibinadamu ambao Mungu alikuwa amefungua mlango kuwatoa katika mateso amaleki walikosa utu kabisa hawakuwahurumia watu ambao walistahili kibinadamu kuhurumiwa, hawakuwahurumia wanyonge, hawakuwahurumia watu waliokuwa wamechoka na kuzimia wala hawakumuhofu Mungu na kwa tukio hili Musa analiweka vizuri katika kitabu cha kumbukumbu la Torati kwamba Amaleki kwamba Israel walikuwa wamewaacha nyuma watu wanyonge wagonjwa na wenye uhitaji wa namna mbalimbali ili labda huenda wapate huduma za kitabibu, maji na huduma nyinginezo lakini Amaleki aliwapiga bila kujali ilihali wakijua kuwa ni watu wanaohitaji huduma na msaada wa kibinadamu ona.

Kumbukumbu 25:18. jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu

 Tukio hili halikuwa tukio lenye kuheshimu ubinadamu, watu wanapokuwa vitani sharia za kivita zinakataza kushambulia maeneo ya kiraia, lakini mbaya zaidi kushambulia hospitali au sehemu zinazotoa huduma za kijamii, wanawake watoto na raia, lakini sio hivyo tu wakati wa vita taifa lile linalopigana linapaswa kuhakikisha kuwa wanajali utu na ndio maana utaweza kuona baadhi ya mataifa wanapokuwa na vita na wananchi wakapata shida ya njaa huwa wanatoa msaada wa chakula na madawa, Katika ulimwengu huu ulio haribika ni dhambi kubwa sana kumuongezea mtu tatizo ilihali yeye mwenyewe ana tatizo au anatoka katika matataizo, kwaajili ya shida zetu, wamekuwepo watu katika jamii ambao matendo yao ni kama waamaleki, badala ya kuwasaidia watu wanyonge wenyewe wamekuwa kikwazo kikubwa sana  kwa watu hao wanyonge, mtu ni mgonjwa anahitaji msaada ana matatizo wanaweza kuwako hata wahubiri au watoa huduma kama hospitalini ambao watadai fedha kutokana na huduma wanayoitoa, mtu anaweza kuwa mlemavu lakini watu wakamuhuzunisha na kumjeruhi roho yake kwa kumuongezea masimango, mtu anaweza kuwa mjamzito akakutana na huduma na maneno ya kukatisha tamaa huko leba wanakojifungulia, mtu anaweza kuwa yatima watu wakawatumia yatima hao kwa manufaa yao, mtu anaweza kuwa mlemavu, kipofu au mwenye ualbino na watu wakawatumia hao kwa manufaa yao wenyewe, mtu anaweza kuwa mjane  anahitaji msaada lakini ujane wake ukatumika kwa manufaa ya wengine, ukatili wa kijinsia, uonevu kwa wanyonge kutokujali, kukosa utu na lugha mbovu sehemu za huduma ni maswala ambayo yanaweza kufanywa na watu ambao wanaweka kwazo kama walivyo Amaleki ambao kwa makusudi kabisa walishindana na kusudi la Mungu la kuwapeleka watu katika nchi ya mkanaani lakini pia kwa kuwaonea wanyinge, jambo hili linahifadhiwa katika kumbukumbu za Mungu na ndipo Mungu hujitakia kisasi, na kuwa na vita na jamii ya watu hao milele, dhuluma na uonevu unawekwa katika kumbukumbu za Mungu na ni lazima vilipiwe ni kwaajili ya haya miaka mingi baadaye Mungu alimtaka mfalme Sauli kuwafutilia mbali Amaleki kwa sababu ya uovu wao lakini hata hivyo Mfalme Sauli alimuudhi sana Mungu kwa sababu alishindwa kuyatii maneno ya Musa mtumishi wake na agizo la Mungu na mapenzi yake ya kutaka kujilipizia kisasi dhidi ya Amaleki

Muhukumu wa ulimwengu lazima atende haki;-

1Samuel 15:1-19 Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda. Ndipo Sauli akawaita watu, akawahesabu huko Telemu, askari waliopanda farasi mia mbili elfu, na watu wa Yuda kumi elfu.  Sauli akaufikilia mji wa Amaleki, akauvizia bondeni. Sauli akawaambia Wakeni, Haya! Enendeni zenu, mkashuke ili kujitenga na Waamaleki, nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao; maana mliwatendea wana wa Israeli mema, walipopanda kutoka Misri. Basi hao Wakeni wakaondoka, wakajitenga na Waamaleki. Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri. Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema, Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha. Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho, akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali. Samweli akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana. Samweli akasema, Maana yake nini, basi, hiki kilio cha kondoo masikioni mwangu, na huu mlio wa ng'ombe ninaousikia? Sauli akasema, Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki; maana watu waliwaacha hai kondoo na ng'ombe walio wazuri, ili wawatoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, nao waliosalia tumewaangamiza kabisa. Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Ngoja, nami nitakuambia neno aliloniambia Bwana usiku huu. Naye akamwambia, Haya, sema. Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha kabila za Israeli? Naye Bwana akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli. Kisha Bwana akakutuma safarini, akasema, Enenda ukawaangamize kabisa wale Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hata watakapoangamia. Mbona, basi, hukuitii sauti ya Bwana, bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana?

Onyo kwa watu wenye dhukluma:-

Kuwatumiwa wanyonge kwa manufaa yakio mwenyewe ni dhambi kubwa sana, Mungu anachukizwa na udhalimu wa kila namna maandiko yanasema wala wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu, Kitendo cha waameleki kuwazuia Israel wasiende kulitimiza kusudl la Mungu kilikuwa ni kitendo cha kutokujali mpangio wa Mungu, laziki tendo la kuwaonea watu wanyonge na kuwatendea uahlifu liliwekwa katika kumbukumbu za Mungu, lakini tendo la kuwahurumia amaleki na kutiokuangamiza au kumlipizia Bwana kisasi sawasawa na neno lake kulikofanywa na Sauli kulimuudhi sana Mungu, Maana yake ni kuwa Mungu hatakubali mtu awaye yote aliye mnyonge na mnyenyekevu aonewe kupita kawaida, ni lazima ataliweka jambo hilo katika kumbukumbu na kujitakia kisasi milele,

Warumi 12:19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.”

Mungu alitunza uovu wa wana wa Amekeli na alikusudia kujilipizia kisasi, na ole wake mtu yule ambaye atawaacha waameleki, Dhambi yao ilikuwa kubwa , walikuwa waonevu, walikuwa wenye dhuluma, walikuwa wasiojali utu, waliwaonea wanyinge, walishindana na kusudi la Mungu, kuna mambo unaweza kuyafanya kuna ukatili unaweza kuufanya lakini sio kwa watu wanyonge ambao maisha yao yalikuwa ya taabu na Mungu aliwasaidia dhidi ya wamisri,  watu waliohitaji huruma kufarijiwa kuinuliwa na kutiwa moyo, Mungu asingeliweza kupuuzia hata kidogo, Lazima atawangalia wanyonge

Isaya 66:2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.”

Mungu ni lazima atatenda haki Mwanzo 18:25b ………. "Hasha: Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?

Mungu atakulipa endapo unaonewa kwa haki na kudhukumiwa hebu mlilie Mungu lalama mbele zake omba na kuliitia jina lake na kisha utaona ukuu wa Mungu katika maisha yako, wale wanaoowatumia wanyionge kwa manufaa yao tubu na achana na unevu wa kila namna Mungu asije akakuhukumu!

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima

Hakuna maoni: