Alhamisi, 29 Julai 2021

Mapepo yasalimu amri ya Mpiga Kinubi !

1Samuel 16:23 “Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha.”



Utangulizi:

Moja ya maswala ya msingi sana katika mafundisho ya Biblia ni pamoja na swala la kusifu na kuabudu, wote tunafahamu jinsi ibada ya kusifu ilivyo na nguvu kubwa sana, na mara kwa mara maandiko yameonyesha Muitikio wa Mungu kufanya mambo makubwa sana pale anaposifiwa kwa njia ya nyimbo na vyombo mbalimbali kama kinanda, gitaa, ngoma na kwa lugha ya zamani kinubi. Na ndio maana utaweza kuona kuwa kusifu kwa njia ya vyombio na uimbaji stadi ni moja ya amri za kimaandiko na ushauri unaotolewa na mfale Daudi ona

Zaburi 33:1-4 “Mpigieni Bwana vigelegele, enyi wenye haki, Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo. Mshukuruni Bwana kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa. Mwimbieni wimbo mpya, Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe. Kwa kuwa neno la Bwana lina adili, Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.

Ziko sababu kadhaa kwanini Maandiko yanashauri hivyo  na daudi ni mojawapo ya watu waliokuwa waanzilishi na watu wenye moyo mkubwa wa ujuzi wa nguvu iliyioko katika sifa, katika maandiko kwa ujumla tunaona wazi nguvu iliyoko katika kusifu na kuabudu, lakini sio hivyo tu kuna faida kubwa na nyingi mno katika kumuimbia Mungu kunakoambatana na vifaa vya muziki

1.       Kusifu kunatupa njia ya kumfikia Mungu  Zaburi 100:1-5 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.” Kusifu katika ibada ndio ufunguo wa kuingia katika uwepo wa Mungu, jambo moja la kusikitisha sana ni kuwa katika makanisa mengi watu hufikiri kuwa ibada ya sifa ni ufunguzi tu wa ibada na kuwa sio sehemu muhimu ya ibada kwa hivyo utaweza kuona kuwa Watumishi wengi wa Mungu na wakati mwingine hata wageni wao hawajitokezi wakati wa sifa katika ibada na hujitiokeza baadaye sana wanapokaribia kupanda madhabahuni kwaajili ya kuhubiri  hili ni tatizo kubwa mno, Kusifu na kuabudu si sehemu ya kumfungulia mchungaji ibada au kulainisha mioyo ya watu ili neno la Mungu liingie vizuri ni sehemu kamili nay a muhimu sana ya ibada.

 

2.       Kusifu kunasambaratisha Kazi za adui Biblia  inataja neno kusifu kwa mara ya kwanza mara baada ya kuzaliwa kwa Yuda katika Mwanzo 29:35 “Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu BWANA; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa.” Jina Yuda maana yake Sifa au Kusifu haiajalishi utalikuta wapi jina hilo vyovyote iwavyo linamaanisha sifa, Maandiko yanamtaja Yesu kama Simba wa kabiola la Yuda ambaye ameshinda ona

 

Ufunuo 5:5 “Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba.” Mara nyingi tunatembea tukiwa na hofu, dhidi ya shetani, mawazo yako, jirani zako na tunahofu ya kuwa nini kitatokea kwetu, Adui yetu mkuu ni Shetani yeye anatajwa katika maandiko kama simba aungurumaye ona katika

 

1Petro 5: 8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.”          

 

Hata pamoja na kutajwa hivyo katika maandiko ni muhimu kwetu kufahamu kuwa shetani pamoja na majeshi yake yote hayawezi kustahimili kwa simba wa Kabila la Yuda, wakati wana wa Israel wanataka kuichukua nchi ya kanaani na kupambana na adui zao walimuuliza Bwana ni nani atatutangulia Mungu aliwajibu Yuda atawatangulia mbele yenu, kinabii Mungu aklikuwa anaonyesha Sifa zikitangulia hakuna adui atakayeweza kusimama

 

Waamuzi 1:1-2 “ Ikawa baada ya kufa kwake Yoshua, wana wa Israeli wakamwuliza Bwana, wakisema, Ni nani atakayekwea kwanza kwa ajili yetu juu ya Wakanaani, ili kupigana nao? Bwana akasema, Yuda atakwea; tazama, nimeitia hiyo nchi mkononi mwake.”   

 

Hii inatufundisha wazi tunapokuwa na vita ya kimwili au kiroho sifa itatangulia na itatuletea ushindi ona

 

2Nyakati 20:14-24 “Ndipo Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu, akajiliwa na roho ya Bwana, katikati ya kusanyiko; akasema, Sikieni, Yuda wote, nanyi mkaao Yerusalemu, na wewe mfalme Yehoshafati; Bwana awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani vita si yenu bali ni ya Mungu.  Kesho shukeni juu yao; tazameni, wanakwea kwa kupandia Sisi; nanyi mtawapata penye mwisho wa bonde, mbele ya jangwa la Yerueli.  Hamtahitaji kupigana vita, jipangeni, simameni, mkauone wokovu wa Bwana ulio pamoja nanyi, enyi Yuda na Yerusalemu; msiogope, wala msifadhaike; kesho tokeni juu yao; kwa kuwa Bwana yu pamoja nanyi. Yehoshafati akainama kichwa, kifulifuli; wakaanguka mbele za Bwana Yuda wote na wakaao Yerusalemu, wakimsujudia Bwana. Na Walawi, wa wana wa Wakohathi na wa wana wa Wakorahi, wakasimama ili wamsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana. Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwaminini Bwana, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa. Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia Bwana, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu, wakitoka mbele ya jeshi, na kusema, Mshukuruni Bwana; kwa maana fadhili zake ni za milele. Nao walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa. Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe. Hata Yuda walipofika mnara wa kulindia wa jangwani, wakalitazama hilo jeshi; nao, angalia, walikuwa maiti walioanguka nchi, wala hapana aliyeokoka.”

 

Kumbe kuna vita nyingi sana ambazo wala hatukutakiwa kuzipigana kutanguliza sifa mbele ya jeshi kunatosha, sifa ni silaha kubwa sana katika ulimwengu wa roho inafanya kazi ni zaidi ya upanga wa adui tunapaswa tu kumuamini simba wa kabila la yuda na kujua ya kuwa atatupa ushindi, kwa hivyo iko siri kubwa sana katika kumsifu Mungu, adui atakimbia na kurudi nyuma na kusambaratika endapo tu tutatambua umuhimu wa kumsifu Mungu kwa nguvu zetu zote, akili zetu zote na ujuzi ufundi na ustadi wetu wote.

 

3.       Kusifu kunafungua milango ya vifungo – Matendo 16:24-26 “Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale. Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.Tunaona nguvu kubwa ya sifa kwamba sifa zinauwezo hata wa kufungua makomeo ya gereza kama ilivyokuwa hapa kwa Paulo na Sila hii maana yake hata magereza nyingi na vifungo vingi ambavyo tumefungwa na ibilisi, wachawi, wagananga na watu wenye jicho baya vinaachia ikiwa tu tutamsifu Mungu, ni wazi kuwa Paulo aliijua siri hii na Daudi aliijua siri hii na ndio maana maisha yao yote waliyaelekeza katika kumsifu Mungu siku zote

 

Mapepo yasalimu amri ya mpiga kinubi

Tumetambua kuwa kuna siri kubwa sana katika kumsifu Mungu, maandiko katika agano jipya yameamuru tuimbe zaburi pamoja na tenzi za rohoni kwa kadiri ya neema ya Mungu mioyoni mwetu ona Waefeso 5:19 “mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;” na Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.” Maandiko yanataka tuimbe kwa moyo, kuna siri ya ajabu katika kumsifu Mungu kwa kuimba kunakoambatana na vyombo, Daudi ni mtu wa Muhimu na wa msingi aliyekuwa na ujuzi huo, mapema sana katika ujana wake na utoto wake alikwishakugundua siri inayokaa katika kusifu, Alikuwa na uwezo mkubwa wa kupiga kinubi mpaka mtu aliyekuwa na mapepo, pepo waliondoka na kumuacha hivyo mapepo yalisalimu amri ya mpiga kinubi 1Samuel 16:23 “Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha.”

Hii inatufundisha kuwa ingawa Mungu alimpeleka Daudi katika kumtumikia Sauli lakini kijana huyu alikaa ikulu na kujifunza maswala kadhaa ya uongozi, huku akiendelea kupiga kinubi ambacho kiliondoa msongo wa mawazo kwa Sauli na kusababisha uponyaji hii ni dhahiri pia kwetu kwamba kumbe tukimsifu Mungu na kuwa na ufahamu kuwa kuna kitu cha ziada katika kumsifu Mungu, uweza wa Mungu tatatngulia, utafungua milango kwaajili yetu, utamfukuza mbali adui, uatasababisha adui asambaratike lakini mapepo yatakimbia roho mbaya zitaondoka, Daudi alikuwa mpiga kinubi hodari mno na anakumbukwa kwa uandiahi na utunzi wa zaburi nyingi sana na hata leo ukienda Israel utaweza kuona kuwa amejengeea sanamu yake ambayo inaoneysha wazi akiwa nameshikilia kinubi, mapepo yasalimu amri ya mpiga kinubi, sisi nasi ni muhimu kwetu kuwa na ujuzi na ufahamu huu na khakikisha kuwa tunamsifu Mungu na kumpoigia vigelegele na kumuinua na kusababisha ushindi mkubwa na nguvu za giza kutoweka hii itatokea na inaendelea kutokea kwa kila mtu anayetambua umuhimu wa kusifu katika jina la Yesu amen.

 

Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Hakuna maoni: