Jumatatu, 30 Machi 2015

UJUMBE: Kushuka Kwa Mungu!


Mstari wa Msingi Kutoka 3: 7- 11
Biblia inasema hivi katika Mistari hiyo hapo “BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; 8. NAMI NIMESHUKA ILI NIWAOKOE NA MIKONO YA WAMISRI, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.              10. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. 11. MUSA AKAMWAMBIA MUNGU, MIMI NI NANI, HATA NIENDE KWA FARAO, NIKAWATOE WANA WA ISRAELI WATOKE MISRI?”

Wengi wetu tunaposikia kitabu cha kutoka na kujifunza unapoambiwa uelezee maana ya kitabu hiki kutoka ni rahisi kujibu kuwa kutoka ni jina la mojawapo ya kitabu kilichoandikwa na Musa kati ya vitabu vyake vitano viitwavyo Pentateuch kitabu hiki kiliitwa kwa Kilatini Exodus kutokana na tafasiri ya kiyunani ya neon “Exodos”au English Exodus na maana yake ni Kutoka, “Going Out” “Exit”au “departure” Hii ni tafasiri rahisi sana na haitoi maana kamili ya kazi ya Mungu aliyoifanya Kule Misri inapunja utendaji wake na kuufedhehi!

Hiwezekani  Mungu ASHUKE tu kwa jambo rahisi kiasi hicho! Haiwezekani! Popote unaposikia au kuona Biblia inasema kuwa Mungu ALISHUKA ni lazima uelewe kuwa kulikuwa na uzito mkubwa sana wa jambo au tukio  na Mungu anaposhuka ujue analokwenda kulifanya ni la kihistoria na ni la kupita kawaida!

Kwa halali kabisa kitabu hiki kinafunua mambo kadhaa muhimu sana kuhusu Mungu
1.       Kinamfunua Mungu kama “Yehova” IAM who IAM Yeye alijulikana kama Mungu muumba katika kitabu cha Mwanzo sasa ni Mungu Mwokozi he is going to perform great Redemption
2.       Kinafunua tabia ya uungu ya kupinga uonevu, kwa taifa moja lenye nguvu kuwanyonya wanyonge kwa ufupi Mungu ndiye aliyekuwa wa kwanza kupinga na kukomesha utumwa
3.       Kinafunua juu ya uongozi wa kweli wa Mungu kwa wanadamu kwa kuwapa sheria
4.       Na kinaelekeza namna Mungu navyoweza kufikiwa na wanadamu kwa njia ya Ibada
Iwapo ningepewa nafasi ya kutoa jina kwa kitabu hiki mimi ningekiita “Redemption” simply!
Baada ya kutoa utangulizi huo sasa - Ni muhimu kuwa na Ufahamu kuwa Misri lilikuwa ni taifa la namna gani ili uweze kupata picha kwanini Mungu alishuka kuwaokoa wana wa Israel yeye mwenyewe?
·         Misri lilikuwa ndio taifa la kwanza lenye jamii yenye maendeleo makubwa sana “Civilization”
·         Kihistoria jamii ya wamisri ilikusanyika kwa wingi kutokana na kukua kwa jangwa la sahara kati ya mwaka wa 7000 mpaka wa 5000 (K.K.)kabla ya Kristo
·         Jamii ya watu waliokusanyika waliweza kuwa na maendeleo makubwa sana kutokana na matumizi ya maji ya mto Nile kwa kilimo na umwagiliaji
·         Bonde la mto nile lilikuwa na rutuba ya kutosha kutokana na kutiririka kwa mbolea toka Ethiopia na maeneo mengine yenye asili ya mto nile
·         Kutoakana na kuwepo kwa rutuba hii kuliwafanya watu wengi kufanya makazi ya kudumu pale Misri na kukawa na maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo
·         Misri ilianza kuwa taifa kamili kutokana na kuweko kwa jamii mbalimbali na falme ndogondogo zilizoungana na baadaye kuwa na mataifa makubwa mawili yaani Upper Egypt na Lower Egypt au Delta Nile maendeleo haya yalitokea karne nne kabla ya Kristo, mwaka wa 3200 baadaye falme hizi mbili ziliungana na kuwa ufalme mmoja chini ya watawala waliojulikana kama farao
·         Kutokana na ugunduzi wa chuma uliokuweko miaka mingi wamisri waliweza kuendeleza teknolojia ya vifaa mbalimbali kwa kilimo huku wakiwa na kiu ya ujuzi na maarifa na sanaa na taaluma mbalimbali, Misri ilipata neema ya kuwa na watu wengi, Uongozi imara na kukua kwa maarifa, wamisriwalikuwa na maarifa makubwa ambayo mengina yanatumika na ulimwengu huu wa leo tulio nao:-
*      Kulikuwa na ujuzi wa kuandika katika magombo ya karatasi ziitwazo “papyrus”
*      Walikuwa ndio watu wa kwanza kugundua na kutumia kalenda yenye siku 365
*      Walikuwa na ujuzi wa maswala ya nyota na unajimu
*      Uwezo mkubwa wa uhandisi na ujenzi kwa kutumia Mawe na ujuzi wa kutumia shaba na dhahabu, walikuwa na ujuzi wa Mathematics na Geometric
*      Wamisri walikuwa hodari katika maswala ya upasuaji na utabibu na hata kutunza maiti isiozekwa muda mrefu
*      Tawala za kisiasa zenye nguvu za kifarao ambazo zimedumu kwa zaidi ya miaka 3000 inasemakena ya kuwa Misri ndio taifa lililojiunda katika mfumo wa taifa na maendeleo kwa muda mrefu zaidi kuliko yote duniani
*      Kutokana na utaalamu huo waliweza kuwa na Jeshi kali lenye silaha na ujuzi wa kutumia farasi na wanyama wengineo
*      Utawala wa farao inaaminika kuwa ulidumu kwa miaka 3200 KK mpaka 352KK, kabla ya Kristo.
*      Hata hivyo kiroho Misri waliabudu miungu mingi sana miungu mikuu ilikuwa karibu kumi na Pharao mwenyewe na ukoo wake alihezabika kama uzao uliotoka kwa mungu hivyo farao alikuwa mungu
Ni katika mazingira haya ni wazi kuwa uwezo wa Misri ulikuwa mkubwa sana, na wenye fahari kubwa sana hakuna utawala ungeweza kuingo’oa Misri ni katika mazingira kama hayo Musa alikuwa na uelewa kamili kuwa jambo ambalo Munguanamtaka akalifanye lilikuwa gumu na lisilowezekana kamwe,Kumbuka maneno ya Musa “MUSA AKAMWAMBIA MUNGU, MIMI NI NANI, HATA NIENDE KWA FARAO, NIKAWATOE WANA WA ISRAELI WATOKE MISRI”  lakini wakati huo huo wana wa Israel wanafanyika kuwa watumwa katika misri na wanalia na kutaka ukombozi katika mazingira yasiyowezekana! Hili lilikuwa jambo gumu sana   Biblia inasema hivi katika Kutoka 2:23-25,
“Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa. 24. Mungu akasikia kuugua kwao, Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya na Ibrahimu na Isaka na Yakobo. 25. Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu akawaangalia”.
Ni muhimu kufahamu mazingira na Lugha ya kibiblia ni vema ikaeleweka wazi kuwatoa Israel Misri halikuwa jambo jepesi, haikuwa hadithi ya kupendeza watu tu ulikuwa ni utendaji wa Mungu ulio mkubwa sana ulikuwa ni mkono wa Mungu uliohodari!
Biblia ina maneno kadhaa kuhusu kutolewa kwa wana Israel Misri ziko lugha kama
Kutoka 13:3 “ …Kwa kuwa bwana aliwatoa Mahali hapa(Misri) kwa nguvu za mkono wake…” Unaona!
Kutoka 7: 4-5…Nitaweka mkono wangu juu ya Misri na kuyatoa majeshi yangu…watoke Misri kwa hukumu zilizo kuu na wamisri watajua kuwa ndimi Bwana! Unaweza Kuona!
Mungu hangeweza kutafuta utukufu kwa kitu cha Hovyo hovyo,Misri ilikuwa na uwezo mkubwa na Mungu alitaka kuonyesha uweza wake ulio mkuu ili yamkini hata wamisri wajua ya kuwa Mungu ndiye Bwana!
Ni kwa sababu hii Mungu aliamua kuacha kiti chake cha Enzi mbinguni na KUSHUKA! Ili aje kuwaokoa wana wa Israel Msomaji wangu mpendwa wote tunafahamu uweza wa Mungu ni mkuu na kuwa Mungu yuko mahali pote kwa wakati mmoja hata hivyo tunaambiwa kuwa makazi yake makuu ni mbinguninlakini katika mazingira Fulani HUSHUKA apate kuleta msaada kwa wanadamu,
Inawezekana unapitia wakati mgumu, unaugua, na unalia unaliona tatizo lako katika ndoa yako, kazini, shuleni na kadhalika, kuwa ni kubwa  nataka nikuhakikishie kuwa Mungu amesikia kilio chako na hawezi kuvumilia tena na ili dunia ijue ya kuwa Yeye ni Bwana atanyoosha mkono wake ulio hodari kukuokoa ataacha makao yake kuja kushughulikia Upweke ulio nao, utumwa ulionao, atashughulika na wewe na kukuponya na kukuokoa na kukupa kila unachomlilia
Hatakama adui amejenga ngome, ameendelea kitaalamu kama Misri ana miaka Miingi na ujuzi mkubwa Mungu kwa neema yake atashughulika na kila kinachokusumbua nawe utaimba Bwana ni Nuru yangu na wokovu wangu Nimuogope nani? Kama alivyowaokoa Israel atakuokoa wewe nawe!
Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: