Ijumaa, 8 Desemba 2017

Kwa taya la Punda!


Waamuzi 15:16Samsoni akasema, Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, Kwa taya ya punda nimepiga watu elfu.”


Then Samson said, "With a donkey's jawbone I have made donkeys of them. With a donkey's jawbone I have killed a thousand men

Ni Muhimu kufahamu kuwa ushindi wetu katika mazingira ya aina yoyote ile na katika vita vya kiroho unatoka kwa Mungu, Mungu alikwisha kutuahidi mapema sana katika torati kuwa atatupa ushindi, bila kujali ni aina gani ya silaha inayotumiwa na adui, yeye anatia moyo kuwa tusiogope wala mioyo yenu isizimie, Mungu asiyeonekana kwa macho ya kibinadamu yuko nyuma ya watu wake kuwapa nguvu isiyoweza kuonekana na kusababisha ushindi. 

Kumbukumbu  20:1-4Utokapo kwenda vitani kupigana na adui zako, na kuona farasi, na magari, na watu wengi kuliko wewe, usiwaogope; kwa kuwa Bwana Mungu wako, yu pamoja nawe, aliyekukweza kutoka nchi ya Misri. Na iwe, msongeapo mapiganoni, kuhani na akaribie na kusema na watu, awaambie, Sikizeni, enyi Israeli, hivi leo mwasongea mapiganoni juu ya adui zenu mioyo yenu na isizime; msiche, wala msiteteme, wala msiingiwe na hofu kwa ajili ya wao; kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi.”

Mungu aliahidi kuwa atatupa Ushindi, na kuwa ndani yetu ameweka uwezo wa kupiga watu elfu uwezo huu unatoka kwake na sio wa mtu binafsi au kwa akili ya mtu binafsi Kumbukumbu 32:30Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama Bwana asingaliwatoa?”

Ni wazi tu kuwa Samson alielewa ahadi za Mungu na aliamua kutunga shairi na kutengeneza Fumbo kubwa sana la siri ya nguvu zake kwamba ameweza kupiga watu elfu KWA TAYA LA PUNDA, lakini ukweli ulio wazi ni kuwa Samsoni alijiliwa na ROHO WA MUNGU na ndiye aliyempa ushindi huu na nguvu ya kupiga watu 1000

Tunajifunza wazi kuwa siri ya ushindi wetu inatokana na NGUVU ZA ROHO MTAKATIFU ambaye hapa Samson anamtaja kama taya la Punda, sio kweli kwamba Samson aliwaangamiza maadui kwa Taya la punda bali nyuma ya taya la punda ilikuweko nguvu isiyoonekana iliyomuwezesha Samson kupata ushindi

Waamuzi 15:14-20. Alipofika Lehi, Wafilisti wakapiga kelele walipokutana naye; ndipo roho ya Bwana ikamjia kwa nguvu, na zile kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitani iliyoteketezwa kwa moto, na vile vifungo vyake vikaanguka mikononi mwake. Naye akaona mfupa mbichi wa taya ya punda, akautwaa, akapiga watu elfu kwa mfupa huo;  Samsoni akasema, Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, Kwa taya ya punda nimepiga watu elfu. Ikawa, alipokuwa amekwisha kunena akautupa ule mfupa wa taya mkononi mwake; na mahali pale pakaitwa Ramath-lehi.Kisha akaona kiu sana, akamwita Bwana akasema, Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu wasiotahiriwa. Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo.Naye akawa mwamuzi wa Israeli: katika siku za Wafilisti muda wa miaka ishirini.”

Ushindi wa Samsoni haukuwa katika mikono yake wala katika taya la punda bali ulitokana na nguvu za Roho wa Mungu yaani Roho Mtakatifu,

Samson aliweza kusababisha uharibifu mkubwa miongoni mwa maadui za Mungu Wafilisti, kwa kutumia Taya la Punda huu ulikuwa ni muujiza mkubwa wenye maana ya kuwa Mungu hutumia mambo manyonge na mapumbavu na yaliyodharaulika  ya dunia kudhihirisha Nguvu zake, kwa sababu hiyo ushindi huu ni dhahiri kuwa haukutokana na aina ya silaha, wala mikono ya Samson Lakini alikuwa ni Roho Mtakatifu aliyetumia Mkono pamoja na taya la punda kuleta ushindi, tunayaweza yote katika yeye atutiaye Nguvu Wafilipi 4:13Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Mungu anapokusudia kutupa ushindi dhidi ya adui zetu ni lazima kuitunza ile nguvu ya asili inayotupa ushindi nguvu hii ni Roho Mtakatifu.

Aidha ni muhimu kukumbuka kuwa  Pale “Ramoth lehi” Kulikuwa na hekalu la miungu ya kifilisti ambamo ndani yake kulikuwa na alama ya taya la punda alama hii ilikuwa inawakilisha nguvu za siri za miungu ya wafilisti ambao waliamini kuwa Mungu huyu aliwapa ushindi dhidi nya adui zao, ni wazi kabisa na inawezekana kabisa kuwa watu wale 1000 waliopigwa na Samsoni huenda walikuwa ni makuhani wa miungu hiyo pale “Ramoth lehi” Jina “Ramoth lehi” ni muungano wa Maneno mawili ya Kiebrania na wafilisti Ramoth kwa Wafilisti ilimaanisha DRAGON au Joka na LEHI maana yake Palipotupwa mfupa wa Punda Taya la punda,  Nguvu ya joka iliyokuwa linaabudiwa na wafilisti katika eneo hili tendo la Samsoni kuwapiga kwa kutumia taya la punda ilikuwa ni ishara ya wao kupigwa na nguvu ya siri, na kwa sababu hawakuwa wametambua nguvu ya Samsoni bila shaka wakati hu ndipo walipoanza uchunguzi wa kutaka kujua siri ya Nguvu ya Samsoni ni nini?



Pichani Samsoni akiwa amepiga watu wengi 1000 pale Ramoth lehi, 

Samson alikuwa ametumiwa na Roho Mtakatifu kwani nguvu za Mungu zilikuja juu yake kwa nguvu lakini maadui hawakutambua, ndugu msomaji wangu ni muhimu ukafahamu kuwa iko nguvu ya siri itakayosambaratisha kila anayekupinga na kukusaidia wakati nwa mahitaji yako nguvu hii ni Roho Mtakatifu, Bwana atawasambaratisha wote wanaoshindana nawe kupitia nguvu za Roho Mtakatifu, nguvu hii ya Mungu isiyoonekana kwa macho iliweza kuwapa ujasiri watakatifu wote waliotutangulia na ndio itakayohusika na inayohusika kuwashughulikia adui zako hata Leo, Kule Marekani watu fulani hutumia alama ya vidole viwili, kwa kulaza vidole viwili vya katikati na kusimamisha viwili, wakimaanisha nguvu ya siri nguvu hii inayowapa ushindi inaweza kuwa ya Joka (Satanic Sign) au kwa Wakristo wanaomjua Mungu inaweza kuwakilisha Heshima kwa Roho Mtakatifu aliyewapa ushindi dhidi ya adui zao (Honor Sign)  kwa hiyo taya la punda kwa wafilisti ilikuwa nguvu ya siri ya Joka na kwa wayahudi taya la Punda ilitumika kama alama ya Nguvu za siri za Roho wa Bwana.

Na. Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi wa mwenye Hekima

Hakuna maoni: