Ijumaa, 8 Desemba 2017

Mwamba wa roho uliowafuata “spiritual rock that accompanied them”


1Wakoritho 10:4wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo




Katika kifungu hiki cha maneno Paulo mtume anajaribu kuitimia historia ya Israel na safari yao ya jangwani kwa kusudi la maonyo kwa Kanisa la korintho na kwa wakristo wote leo, Hata hivyo ndani yake kuna maswala yamsingi ya kujifunza na moja wapo ya tukio Muhimu linalotajwa hapa ni Israel kuunywea Mwamba wa Roho uliokuwa ukiwafuata, hili ni moja ya tukio muhimu sana na ambalo lina kitu cha kujifunza.

Kwa mujibu wa tamaduni za kiyahudi katika kitabu chao cha komentari ya kiyahudi kiitwacho “Haggada  Marabi wengi walikuwa wanaamini kuwa Waisrael Jangwani walikuwa na Mwamba uliokuwa ukiwafuata na kuwapa maji, inaaminika kuwa mwamba huu ulikuwa unaweza kuuimbia kwamba utoe maji nao uliweza kutoa maji  

Hesabu 21: 16-18Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho Bwana alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji. Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu; Bubujika Ee kisima; kiimbieni; Kisima walichokichimba wakuu, Ambacho wakuu wa watu wakakifukua, Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.”
 
Hata hivyo Marabi wengine wanaamini kuwa kulikuwa na kijito kilichokuwa kikitiririsha kuwafuata waisrael na  kutoka mlima Sinai kuhakikisha kuwa unawapatia maji 

Kumbukumbu 9:21Kisha nikaitwaa ile dhambi yenu, huyo ndama mliyemfanya, nikamteketeza kwa moto, nikamponda, nikamsaga tikitiki, hata akawa laini kama vumbi; nikalitupa vumbi lake katika kijito kilichoshuka kutoka mlimani

Na wengine wanaamini kuwa kulikuwa na jiwe maalumu lililokuwa likidongoroka lenyewe kuwafuta na kuwapatia maji tangu Musa alipoupiga mwamba, vyovyote iwavyo Paulo mtume aliitumia mifano hii ya kiimani ya wayahudi kuonyesha jinsi ambavyo Mungu alikuwa akiwajali watu wake, kwamba Yesu alikuweko Jangwani katika ulimwengu wa roho kuhakikisha kuwa anawahudumia watu wake anatoisheleza mahitaji yao, anahakikisha kuwa hawapungukiwi na kitu, kwamba anatimiza kiu yao, na kwamba anatimiza mahitaji yao ya kila siku, kama jinsi ambavyo Mungu aliwalisha watu wake kwa mana vilevile aliwalihakikisha kuwa wanakuwa na maji ya kunywa ya kutosha wao na mifugo yao, Ni Mungu yuleyule anayeweza kuwapatia watu mahitaji yao wakiwa jangwani ndiye ambaye anatoa neema wakati wa mahitaji yetu

Kristo ambaye ni Mwamba wa kiroho kwetu yuko kuhakikisha kuwa anatimiza mahitaji yetu leo, atakutana na kiu ya kila mmoja wetu, kama tunahitaji kufaulu, kupona, kutimiziwa mahitaji yetu yeye yupo kutuhudumia na kutoa neema jangwani, anajua jangwa hili zito unalolipitia anajua kuwa utakutana na kiu za aina mbalimbali, anajua kuwa aunahitaji kushibishwana kuburudisha kutokana na uchovu wa safari, nisikilize Japokuwa Mungu ameruhusu upite katika jangwa hilo yeye hatakuacha yuko pamoja nawe na nakuhakikishia kuwa atakuwa wingu wakati wa Mchana, yaani atakuwekea uvuli wakati wa hari wakati wa joto atakufunika jua lisikuumize, aidha atakuwa Nuru kwako wakati wa usikum hutaita katika giza yeye atakuwa pamoja nawe, atakulisha kwa mana jangwani lazkini atahakikisha wewe na nyimba ya baba yako na mlango wa baba zako anawaburudhisha kwa maji ,kutoka katika mwamba huu na ni mwamba wa ajabu kwani unakufuata katika safari yako ili kukuburudisha.

Tunapojikumbusha maneno haya ya kihistoria na maonyo tunataka kuangalia neema ya Mungu kwa wanadamu na upendo wake kwetu kuwa Mungu alijishughulisha sana na Israel na anajishughulisha sana na mahitaji yetu pia.

Ujumbe. Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: