Jumatatu, 31 Januari 2022

Haki huinua Taifa !


Mithali 14:34 “Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa maandiko yanatupa siri ya mafanikio makubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na maisha ya kila mtu na maisha ya taifa lolote lile kwamba; Ili tuweze kuwa na ustawi tunapaswa kuwa watu wa haki, Mungu hawezi kumvumilia mtu au taifa lolote ikiwa watu wa taifa hilo wataacha na uadilifu na kumkataa Mungu, siri ya nguvu na mafanikio ya mtu watu jamii na taifa lolote iko katika kutenda uadilifu na kuyaishi mapenzi ya Mungu na wala sio nguvu za kijeshi na uchumi, siri ya mafanikio ya kweli iko kwenye uadilifu na kutenda haki, Taifa lolote likiandaa mipango na mikakati ya kiadilifu na ya kumcha Mungu na kumuheshimu na kukaa katika uadilifu kila kitu kitafanikiwa kwa mujibu wa maandiko Mithali 14:34 Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.” Tutajifunza somo hili Haki huinua taifa kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:- 

1.       Maana ya Taifa

2.       Jinsi haki inavyoinua taifa na Dhambi inavyoleta aibu

3.       Haki huinua taifa 

Maana ya Taifa

Ni muhimu kufahamu kuwa katika maandiko lugha inayotumika kumaanisha taifa inatumika katika maana pana sana unapoangalia maana ya Taifa kwa kiingereza yaani Nation maana yake katika Dictionary inasomeka hivi National means People who possess a common kinship, a social or political group and simply a people, kwa kiyunani ni Ethnos au Ethinic, ni jamii au watu wanaotokana na mtu, au kabila au dini au lugha na kadhalika, Kwa mfano watu wanaweza kuzaliwa na baba mmoja na mama mmoja au hata wakawa mapacha lakini katika jicho la kiungu hao wanaweza kuwa mataifa mawili tofauti na kabila mbili tofauti unaona!

Mwanzo 25:21-23 Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba. Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA akamwambia, Mataifa mawili yamo tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo.”      

Unaona na pia unaweza kuiona lugha ya aina hii ikitumiwa na Yesu katika Mathayo 24:6-7 “Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.”  

Kwa msingi huo sasa Taifa linaweza kuwa ni jamii ya watu wanaotokana na mtu mmoja mmoja, taifa ni watu wa karibu sana wakati ufalme na ufalme inaweza kuwa ni mipaka ya kiserikali, kwa hiyo Mungu yu aweza kumuona au kumuita mtu mmoja na mtu huyo akamfanya kuwa taifa, yaani kama wewe ni mtenda haki na unampendeza Mungu wewe ni asili ya taifa Mungu yu aweza kukufanya wewe kuwa taifa kubwa ona

Mwanzo 12:1-3 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.”

Kwa msingi huo tunapozungumzia taifa tunamzungumzia mtu mmoja mmoja, na jamii au kabila au kundi la watu wa aina filani walio karibu sana hilo ndio taifa, na ufalme ni jamii ya watu wanaopakana kiserikali, kwa hiyo kila mmoja anapaswa kuwa mtenda haki na kuishi maisha ya kumcha Mungu kwa sababu Mungu hashindwi kukufanya wewe kuwa taifa kwa sababu taifa linaanzia na mtu mmoja kama Mungu akipendezwa nawe anaweza kukufanya kuwa taifa na kama Mungu akichukizwa nawe anaweza kukufuta ona

Kutoka 32:7-14BWANA akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao, wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri. Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu. Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu? Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako. Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele. Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wakeunaweza kuona kwa msingi huo sasa swala la kutenda haki au kwa lugha nyingine nyepesi kutembea katika mapenzi ya Mungu halianzi na mtu Fulani tu linaanza na wewe na mimi

Jinsi haki inavyoinua taifa na Dhambi inavyoleta aibu

Maandiko sasa yanatuonyesha kupitia wana wa Israel na maisha yao kwamba pale watu walipotenda haki na walipotembea katika njia za Mungu, Mungu aliwafanya kuwa imara na pale watu walipoziacha njia za Mungu, na kuyaacha mapenzi yake  Mungu aliwaacha waanguke katika mikono ya adui zao na kunyanyaswa vibaya  ona kwa mfano

Waamuzi 2:11-23 Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika. Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi. Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. Kila walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana. Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara. Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo. Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua. Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi. Basi hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akasema, Kwa kuwa taifa hili wamelihalifu agano langu nililowaamuru baba zao, wala hawakuisikiliza sauti yangu; mimi nami tokea sasa sitalifukuza taifa mojawapo la hayo aliyoyaacha Yoshua alipokufa; ili kwa njia ya hayo nipate kuwajaribu Israeli, kwamba wataishika njia ya Bwana kwenda katika njia hiyo, au sivyo. Basi Bwana akawaacha mataifa yale, wala hakuwafukuza kwa upesi, wala hakuwatia katika mikono ya Yoshua.”

Unaweza kuona kwamba pale watu wa Mungu walipoziacha njia za Mungu na kuishi kwa dhuluma na  wakajifanyia kila wanachokiona kuwa chema katika macho yao  Mungu aliwadhibu vikali sana na kuwaacha katika mikono ya adui zao ili washughulikiwe na wakati mwingine aliruhusu wachukuliwe mateka na kwenda utumwani  na sio hivyo tu akliwaacha wadhalilike na kufedheheka nah ii ndio aibu kubwa iliyokuwa inawapata pale wanapoacha njia za Mungu ambayo ndio haki ya Mungu.

2Wafalme 17:6-12 “Katika mwaka wa kenda wa Hoshea, huyo mfalme wa Ashuru akautwaa Samaria, akawahamisha Israeli mpaka Ashuru, akawaweka katika Hala na Habori, karibu na mto wa Gozani, na katika miji ya Wamedi. Yalitukia hayo kwa sababu wana wa Israeli walikuwa wametenda dhambi juu ya Bwana, Mungu wao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri watoke chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri, wakawaacha miungu mingine. Wakaziendea sheria za mataifa, ambao Bwana aliwafukuza mbele ya wana wa Israeli, na sheria za wafalme wa Israeli walizozifanya. Tena, wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo yasiyokuwa mema juu ya Bwana, Mungu wao, wakajijengea mahali pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hata katika miji yenye boma. Wakajisimamishia nguzo na maashera juu ya kila mlima mrefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; wakafukiza uvumba huko katika kila mahali pa juu, kama mataifa walivyofanya, ambao Bwana aliwafukuza mbele yao; wakaunda mambo mabaya, ili wamkasirishe Bwana; wakatumikia sanamu, ambazo Bwana aliwakataza, akasema, Msitende jambo hili.”

Pale Israel walipotubu na kucha dhambi zao na kutembea katika mapenzi ya Mungu Mungu aliwasaidia aliwapa Mwokozi, alileta ukombozi na kuwapa amani na kuondoa masumbufu yote

 Waamuzi 3:9-11 “Kisha wana wa Israeli walipomlingana Bwana, Bwana akawainulia wana wa Israeli mwokozi, aliyewaokoa, yaani, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu. Roho ya Bwana ikamjilia juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli; akatoka kwenenda vitani, naye Bwana akamtia huyo Kushan-rishathaimu, mfalme wa Mesopotamia, mkononi mwake; na mkono wake ukamshinda Kushan-rishathaimu. Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka arobaini. Kisha Othnieli, mwana wa Kenazi, akafa.” Unaweza kuona hii ndio kanuni ya Mungu, Mungu hawezi kukuinua na kukutumia katika hali ya uovu, hatunabudi kutubu, kujinyenyekesha mbele za Mungu na kumlingana Mungu yaani kutembea katika njia zake tukifanya hivyo hatutaingia katika aibu na fedhea ya aina yoyote ile na Mungu atakuwa pamoja nasi na tutakuwa na uhakika wa ulinzi wa kudumu wala Bwana hatatuuza tuumizwe na adui zetu

Haki huinua taifa

Mithali 14:15-34 “Mjinga huamini kila neno; Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu; Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa. Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa. Wabaya huinama mbele ya wema, Na wasio haki malangoni mwao wenye haki. Maskini huchukiwa hata na jirani yake; Bali tajiri ana rafiki wengi. Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri. Je! Hawakosi wawazao mabaya? Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema. Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu. Taji ya wenye hekima ni mali zao; Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu; Bali atoaye uongo hudanganya. Kumcha Bwana ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio. Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake; Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao. Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu. Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake; Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake. Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu; Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika. Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”

Suleimani katika kitabu cha Mithali anaonyesha wazi namna mtu mwenye haki anavyoweza kufanikiwa na namna watu waovu wanavyoweza kujikuta katika mashaka kinachosisitizwa katika maandiko hapa ni kwamba wale wanaomkataa Mungu na kuacha kutenda haki na kuendelea na uovu wanafanya ujinga ambao utawaharibia maisha na wale wanaomkubali Mungu na njia zake wanajipatia hekima na maarifa  na kujitengenezea ulinzi wa uhakika , kwa msingi huo neno la Mungu linapozungumza kuhusu taifa linatuzungumzia wewe na mimi na baadaye jamii yetu na jamii ya dunia kwa ujumla lakini kanuni hii inaanza kufanya kazi kwa mtu mmoja mmoja

Mithali 3:5 -8 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako. Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana, ukajiepushe na uovu. Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako.” Ukiyajua hayo Heri wewe ukiyatenda!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Hakuna maoni: