Ijumaa, 30 Desemba 2022

Ikawa mwisho wa Mwaka!


2Nyakati 24:23 - 25Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.” 



Utangulizi:

Yosia alikuwa mfalme wa Yuda aliyetawala kati ya mwaka wa 640-609 Kabla ya Kristo, jijini Yerusalem, Ni mtawala aliyeingia madarakani akiwa kijana mdogo sana, Yeye ni mwana wa Amon Mwana wa Manase ambao kimsingi walikuwa wafalme waovu mno katika wafalme waliowahi kutawala Israel ya Kusini, Lakini hata hivyo Yosia alikuwa mfalme mwema sana na aliyemcha Mungu! Yeye alitawala akiwa na miaka 8 baada ya kuuawa kwa baba yake. Mfalme huyu alikuwa mcha Mungu na alitenda yaliyo haki mbele za Mungu!

2Wafalme 22:1-2 “Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi. Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.”

Wakati wa utawala wake alifanya kazi kubwa sana ikiwa ni pamoja na kuchangisha fedha za ujenzi na ukarabati wa Hekalu nyumba ya Mungu ambayo ilikuwa na nyufa kutokana na kutokujaliwa na watu wakati wa utawala wa babu yake na baba yake, Kuhani Hilikia aligundua vilevile kitabu cha torati ambapo alipomsomea mfalme alirarua mavazi yake na kutubu, kisha kuwaita watu wote wapate kuitubu na kumgeukia Mungu, walifanya agano kuwa watamtumikia Mungu kwa mioyo yao yote kwa ujumla kulikuwa na uamshi mkubwa sana wakati huo

2Wafalme 23:1-25 “Kisha, mfalme akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu. Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana. Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile. Kisha, mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni, akayachukua majivu yake mpaka Betheli. Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. Naye akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni, akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu. Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera. Akawatoa makuhani wote katika miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba, tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa mtu langoni pa mji. Walakini hao makuhani wa mahali pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate isiyo na chachu katikati ya ndugu zao. Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki. Akawaondoa farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani; akayapiga moto magari ya jua. Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni. Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi. Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu. Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli, madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera. Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo. Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria. Na nyumba zote pia za mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli. Akawaua na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu, akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu. Naye mfalme akawaamuru watu wote, akasema, Mfanyieni Bwana, Mungu wenu, pasaka, kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano. Hakika yake haikufanyika pasaka kama hiyo, tangu zamani za waamuzi waliowaamua Israeli, wala katika zamani za wafalme wa Israeli, wala za wafalme wa Yuda. Bali katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia ilifanyika pasaka hii kwa Bwana ndani ya Yerusalemu. Tena wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana. Kabla ya huyo hapakuwa na mfalme mfano wake, aliyemwelekea Bwana kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na sheria zote za Musa; wala baada yake hakuinuka mmoja mfano wake yeye.”

Unaona ni wakati wa Yosia kwa kweli kulikuwa na uamsho mkubwa sana kila kitu cha kipagani kiliharibiwa na kila aina ya miungu iliyoabudiwa iliharibiwa, alifukuza na kuharibu wenye pepo wa utambuzi, makhanithi na wachawi, anasifika kuwa alikuwa mfalme mwema ambaye kbla yaka na baada yake hakuwahi kutokea!

Sababu kubwa ya mafanikio ya Yosia

Uwezo mkubwa na uadilifu mkubwa alioupata Yosia ulitokana na malezi mazuri na thabiti kutoka kwa kuhani mkuu maarufu sana aliyeitwa Yehoiada kuhani huyu alikuwa mwaminifu na aliweza kutumika kwa miobgo kadhaa chini ya wafalme wa Yuda, Kuhani huyu alioa dada wa Mfalme Ahazia, mwaka mmoja kabla mfalme Ahazia hajauawa, Athalia mama wa mfalme alishikwa na tamaa ya madaraka na kuamua kuua watoto wote wa kifalme na kila mtu aliyeonekana na ushawishi wa kiutawala, baada ya adhima yake hiyo kufanikiwa alijitangaza kuwa mtawala ona

2Wafalme 11;1-3 “Na Athalia, mama yake Ahazia, alipoona ya kuwa mwanawe amekufa, akainuka, akawaharibu wazao wote wa kifalme. Ila Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu, umbu lake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia, akamwiba miongoni mwa hao wana wa mfalme waliouawa, yeye na mlezi wake, na kuwatia katika chumba cha kulala; wakamficha usoni pa Athalia, basi kwa hiyo hakuuawa. Alikuwako pamoja naye, amefichwa nyumbani mwa Bwana, miaka sita. Naye Athalia akaitawala nchi.” 

Yehosheba na Mumewe Yehoiada walimficha kijana pekee aliyeponyoka katika sakata hilo ambaye ni Yosia na walimlea vizuri na ilipotimia miaka sita yaani ya kufichwa kwake hii ikiwa na maana alifichwa akiwa na miaka miwili sasa Yehoiada alifanya mpango wa kumtyawaza Yosiah kuwa Mfalme wa Yuda  ona

2Wafalme 11:4-17. “Hata mwaka wa saba Yehoyada akatuma, na kuwaleta wakuu wa mamia, wa Wakari, na wa walinzi, akawaleta kwake ndani ya nyumba ya Bwana; akapatana nao, akawaapisha nyumbani mwa Bwana, akawaonyesha huyo mwana wa mfalme. Akawaamuru, akasema, Hili ndilo neno mtakalolifanya; theluthi yenu, mtakaoingia siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya mfalme; na theluthi mtakuwapo mlangoni pa Suri; na theluthi langoni nyuma ya walinzi; hivyo mtayalinda malinzi ya nyumba, kuzuia watu wasiingie. Na sehemu mbili zenu, yaani, wote watokao siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya Bwana kumzunguka mfalme. Mtamzunguka mfalme pande zote, kila mtu mwenye silaha zake mkononi; naye awaye yote aingiaye ndani ya safu auawe; mkafuatane na mfalme, akitoka na akiingia. Nao wakuu wa mamia wakafanya sawasawa na yote aliyowaamuru Yehoyada kuhani; wakawatwaa kila mtu watu wake, hao watakaoingia sabato, nao watakaotoka sabato, wakaja kwa Yehoyada kuhani. Naye yule kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao zilizokuwa za mfalme Daudi, zilizokuwamo nyumbani mwa Bwana. Walinzi wakasimama, kila mtu na silaha zake mkononi, kutoka pembe ya kuume ya nyumba mpaka pembe ya kushoto ya nyumba, kando ya madhabahu na nyumba, wakimzunguka mfalme pande zote.Ndipo akamleta nje mwana wa mfalme, akamvika taji, na kumpa ushuhuda; wakamfanya mfalme, wakamtia mafuta; wakapiga makofi, wakasema, mfalme na aishi. Na Athalia alipoisikia sauti ya walinzi na ya watu, aliingia kwa watu nyumbani kwa Bwana; akatazama, na tazama, mfalme amesimama karibu na nguzo kama ilivyokuwa desturi, nao wakuu na wapiga baragumu karibu na mfalme; na watu wote wa nchi wakafurahi, wakapiga baragumu. Ndipo Athalia akararua mavazi yake, akalia, Fitina! Fitina! Naye Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, majemadari wa jeshi, akawaambia, Mtoeni kati ya safu; naye ye yote amfuataye mwueni kwa upanga. Kwani kuhani akasema, Asiuawe nyumbani mwa Bwana. Basi wakampisha njia; akaenda kwa njia ya kuingia kwa farasi nyumbani mwa mfalme; akauawa huko. Kisha, Yehoyada akafanya mapatano kati ya Bwana na mfalme na watu, ili wawe watu wa Bwana; tena kati ya mfalme na watu.” 

Unaona chini ya uangalizi wa Yehoiada, Mfalme Yosia aliweza kutawala vema na kwa mapenzi ya Mungu, kumbuka kuwa ni yeye na mkewe ndio waliomsaidia na kumuongoza na kuuondoa utawala wa malikia na kumrudisha mfalme katika kiti cha Enzi cha baba zake kama ilivyokuwa kwa mapenzi ya Mungu kwa Daudi, kupitia kuhani mkuu huyu inchi ikawa na amani na watu wakamcha Mungu mno, Yosiah katika wakati wote wa kuhani mkuu aliweza kufanya vizuri, Mfalme alikuwa na ushawishi mkubwa, aliwaongoza watu kumrudia Bwana kila mtu aliitii sharia ya Mungu, jambo hili lilimfurahisha Mungu sana na klilikuwa Baraka kubwa sana kwa kila mtu, maandiko yalikuwa yamepuuzwa kabisa lakini alipokuwa mfalme Heshima ya kimaandiko ilirejea, watu wote wenye kutoa dhabihu mbaya za watoto na kila aina ya uovu iliharibiwa kabisa kwa ujumla alikuwa mfalme ambaye aliushawishi moyo wa Mungu na Mungu alimsikiliza ona

2Wafalme 22:19 “kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana.”

Ikawa mwisho wa Mwaka!

Pamoja na uzuri aliokuwa nao Mfalme huyu ambaye aliifanya kazi nzuri wakati wote wa uongozi wa kuhani mkuu Yehoiada ambaye aliishi miaka 130 kuhani huyu mkuu aliheshimika na watu wote kutokana na ushauri wake mzuri kwa Mfalme na watu wake alikuwa amejaa hekima ya kiungu hata hivyo jambo la kusikitisha ni kuwa baada ya kifo chake Yosia alibadilika moyo na kuanza kuwa na washauri wabaya ambao walirudisha tena ibada ya baali na maashera ona

2Nyakati 24:17-20 “Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao. Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao. Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza.”

Mungu alipeleka manabii mbalimbali kwaajili ya kuwaonya hata hivyo hawakukubali, wala hawakuwasikiliza, Hata hivyo Kuhani mkuu Marehemu Yehoiada alikuwa na kijana aliyeitwa Zekaria ambaye Roho Mtakatifu alikuja juu yake ili aweze kuwaonya, Nabii Zekaria bin Yehoiada aliwaonya kuwa kama wanamuacha Bwana ni dhahiri kuwa Bwana naye atawaacha hata hivyo hawakutaka kusikia maonyo na badala yake walipanga mpango wa kumuua ona Na mfalme Yoashi alimuua zekaria akasahau wema wote ambao mama yake na baba yake walimfanyia hili lilikuwa jambo la kusikitisha sana ona

2Nyakati 24:20-22 “Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi. Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana. Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi.”

Wakati Zeakaria anauawa alikumbuka wazi mema yote ambayo baba yake alimfanyia mfalme Yosia ni ukweli usiopingika kuwa Yosia alikuwa mtu asiye na shukurani hakulipa mema na badala yake alilipa mabaya Zekaria alimuomba Bwana wakati anauawa akasema  BWANA AYAANGALIE HAYA AKAYATAKIE KISASI, ni ukweli usiopingika kuwa Mungu wetu hujilipia kisasi wakati watu wanapokutendea yasiyopaswa wewe uwe na uvumilivu tu kwa dhambi hii aliyoifanya Yosia ukweli haikuchukua muda tangu wakati ule iluipofika mwisho wa Mwaka Bwana akajilipizia kisasi ndio maana tunasoma IKAWA MWISHO WA MWAKA ona

2Nyakati 24:23-25. “Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.”  

Hitimisho

Inawezekana wako watu umewawaidia lakini wamekugeuka, inawezekana umedhulumiwa, na watu hawataki kukulipa inawezekana umetukana, inawezekana umeonewa, leo nataka nikupe habari njema ya kuwa yuko Mungu anayelipa kisasi, kama maandiko yasemavyo ni haki mbele za Mungu kuwaluipa kisasi wale wanaowaonea ninyi

2Wathesalonike 1:6 – 9 “Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake;”

Mungu anao wakati wake wa kujilipizia kisasi dhidi ya wale wote wanaokuonea na kukutesa, kila unapopitia uonevu unayo haki ya kumwambia Mungu liangalie na hili ukalitakie kisasi na Mungu mwenyewe atausbiri wakati wake na wakati mwingine itakuwa mwisho wa Mwaka, ikawa nmwisho wa Mwaka, ikawa mwisho wa Mwaka, ikawa mwishio wa Mwaka Mungu alijilipizia kisasi dhidi ya Yosia aliyemuua Zekaria ili hali baba yake alimtendea mema hakuna sababu ya kuogopa kila aina ya uonevu katika maisha yako italipwa mwisho wa mwaka, umeonewa wewe kumbuka ikawa mwisho wa mwaka, umekopwa hujalipwa wewe kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka, umekataliwa, mumeo au mkeo ameibiwa, ikawa mwiho wa Mwaka, umedhulumiwa paka kumbuka ikawa mwisho wa Mwaka  IKAWA MWISHO WA MWAKA   

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima!

Maoni 2 :

Bila jina alisema ...

Habari Mtazamaji wangu mheshimiwa, naandika makala hii kuueleza ulimwengu jinsi Dr.diamond alivyomrudisha mpenzi wangu wa zamani kwangu, hii ndio sababu ya mimi kuchukua jukumu la kumshukuru mwigizaji huyu mkubwa anayeitwa Dr diamond kwa sababu kupitia wimbo wake. nisaidie maisha yangu yalizidi kujawa na mapenzi na nafurahi kusema kuwa Ex Boyfriend wangu ambaye tumeachana na mimi kwa kipindi cha miaka 3 alirudi kwangu akiniomba nikubaliwe, Hili lilikuwa tukio la kushtua kwani kabla sijawasiliana na Dr. diamonf ndiye niliyemsihi Ex Boyfriend wangu arudi kwangu lakini kwa msaada wa Dr.diamond sasa uhusiano wangu umerejeshwa. Unaweza pia kuwa na uhusiano bora ikiwa tu utamtumia barua pepe: ( drdiamondTemple@gmail.com ) WhatsApp +2349130958968

Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima alisema ...

Ukurasa huu umewekwa wakfu kwaajili ya Kuwaelekeza watu kwa Mungu ambaye ndiye msaada wetu mkuu, Maandiko yanasema Mungu kwetu sisi Ni kimbilio na Ngu vu msaada uonekanao tele wakati wa Mateso, hivyo kama yuko mwanadamu anatumia ukurasa huu, kujitangaza kuwa anaweza kuwasaidia wanadamu basi Mwanadamu huyo anamkufuru Mungu na ukurasa huu hautawajibika kwa mtu anayetegemea ushirikina badala ya kumtegemea Mungu, Maandiko yanasema amelaaniwa Mtu yule amtegemeaye mwanadamu na kumfanya kuwa kinga yake