Jumanne, 24 Desemba 2019

Fimbo ya kukomesha Manung’uniko!.



Hesabu 17:1-11Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,Nena na wana wa Israeli, kisha upokee kwao fimbo, fimbo moja kwa ajili ya nyumba ya kila baba, katika wakuu wao wote, kama nyumba za baba zao zilivyo, fimbo kumi na mbili; kisha andika jina la kila mtu katika fimbo yake. Na katika fimbo ya Lawi utaliandika jina la Haruni; maana, itakuwa fimbo moja kwa kila kichwa cha nyumba za baba zao. Nawe utaziweka katika hema ya kukutania mbele ya huo ushahidi, hapo nikutanapo pamoja nanyi.  Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung'uniko ya wana wa Israeli, wanung'unikiayo juu yenu. Basi Musa akawaambia wana wa Israeli, ndipo wakuu wao wote wakampa fimbo, fimbo moja kwa kila mkuu, kama nyumba za baba zao zilivyokuwa, fimbo kumi na mbili; na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao.  Kisha Musa akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana katika hema ya kukutania.  Ilikuwa siku ya pili yake, Musa akaingia ndani ya hema ya ushahidi; na tazama, ile fimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa malozi mabivu. Kisha Musa akazileta nje hizo fimbo zote kutoka hapo mbele za Bwana na kuziweka mbele ya wana wa Israeli wote; nao wakaangalia, na kila mtu akaitwaa fimbo yake. Kisha Bwana akamwambia Musa, Irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili itunzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung'uniko yao waliyoninung'unikia, ili wasife.  Basi Musa akafanya vivyo; kama Bwana alivyomwagiza, ndivyo alivyofanya.” 
          

Utangulizi:

Ni muhimu kila mmoja wetu kuwa na ufahamu wa kutosha kwamba linapokuja swala la Uongozi, tujue kuwa uongozi unatoka kwa Mungu, na kwa sababu hiyo hatuna budi kufahamu kuwa tunapaswa kuiheshimu mamlaka ambayo Mungu ameiruhusu itawale kwa wakati huo, Biblia inasema katika

Warumi 13:1-2Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.”

Kumbe basi ni wazi kuwa Mungu anahusika kwa kiwango chote katika kuruhusu aina flani ya mamlaka itawale, hii ni kila mahali na katika kanisa lake bado ni Mungu ndiye anayechagua yeye mwenyewe na kuwaweka watumishi wake ili waliongoze kanisa hakuna mtu anayejiita mwenyewe japo wako walimu wa uongo, manabii wa uongo, wachungaji wa uongo, wainjilisti wa uongo, manabii wa uongo na mitume wa uongo maandiko yanaonyesha kuwa wapo, lakini wale halisi tunaambiwa kuwa Mungu aawachagua yeye mwenyewe ona katika

Waefeso 4:11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;” Biblia ya kiingereza ya The Amplified Bible inasomeka katika maneno hayo hivi nanukuu “He Himself Appointed and gave men to us” yaani Yesu mwenyewe, Ndiye anayechagua nani aongoze watu wake bila kujali ni njia gani anaitumia! Swala la kuchagua viongozi hufanywa na Mungu kwa matakwa yake na sio yetu ni muhimu kukumbuka hili ona

Marko 3:13-14Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,” unaona anaita anaowataka mwenyewe kwa makusudi, kusudi la kwanza wawe pamoja naye yaani wakae katika uwepo wake, wawe na uwepo wa Mungu na pili awatume wawe wajumbe wake wawe wawakilishi wake, watimize makusudi yake wahubiri injili. Jambo hili si kwa sababu ya juhudi za kibinadamu wala si kwa sifa za kibinadamu bali kama Mungu atakavyo  Mungu huchagua viongozi kwa rehema zake tu na sio uwezo wa kibinadamu ona

Warumi 9:15-16Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

Kwa msingi huu basi ni muhimu kufahamu kuwa tunaponung’unika juu ya kiongozi fulani na au kusimama kinyume naye kumpinga au kumuasi na kuanza kumpiga vita ni wazi kabisa kuwa unapambana na Mungu, na hili ndio tatizo kubwa la wanadamu, Mungu anapochagua mtu wa kuongoza na kutimiza kusudi lake sio lazima mtu huyo awe anafiti katika akili zako, wakatimwingine unaweza kuona kwa nje kuwa ni mtu dhaifu sana na ni kama hatoshi, lakini ndani yake mapenzi ya Mungu yatatimizwa!.

Kunung’unikiwa kwa Mamlaka ya Musa na Haruni.

Katika Mstari wa msingi hapo juu tunagundua kuwa Mamlaka ya Musa na Haruni ilinung’unikiwa na baadhi ya watu, Kama wewe ni kiongozi kumbuka kuwa wewe sio wa kwanza kunumg’unikiwa wala kutukanwa au kuasiwa au kupingwa hadharani au kusengenywa au kusemwa vibaya, Musa na haruni walikuwa viongozi waaminifu, waliojitoa na kuwapenda watu wao, waliohatarisha maisha yao kwa kumkabili Farao wakiwa hawana Jeshi na kudai uhuru wa waisrael, wakiwa na lengo la dhati kutoka moyoni kuwapeleka katika nchi ya mkanaani nchi iliyojawa maziwa na asali lakini mamlaka yao ilinung’unikiwa, baadhi ya waisrael wa kabila ya lawi walianza maneno maneno kwamba Musa na haruni wanajipa madaraka makubwa mno wanajitukuza sana angalia katika

Hesabu 16:1-4Basi Kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, akatwaa watu, pamoja na Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi, waliokuwa wana wa Reubeni; nao, pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa; nao wakakusanyika kinyume cha Musa na Haruni, na kuwaambia, Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, Bwana naye yu kati yao; n'nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa Bwana? Musa aliposikia maneno haya, akapomoka kifudifudi;

Hesabu 16:8-11Musa akamwambia Kora, Sikizeni basi, enyi Wana wa Lawi; Je! Mwaona kuwa ni jambo dogo kwenu, kuwa Mungu wa Israeli amewatenga ninyi na mkutano wa Israeli, ili apate kuwakaribisha kwake; ili mfanye utumishi wa maskani ya Bwana, na kusimama mbele ya mkutano ili kuwatumikia; tena ya kuwa amekuleta uwe karibu, na ndugu zako wote wana wa Lawi pamoja nawe? Nanyi, je! Mwataka na ukuhani pia? Kwa sababu hii wewe na mkutano wako wote mmekusanyika kinyume cha Bwana; na Haruni, je! Yeye ni nani hata mkamnung'unikia?

Unaona vifungu hivyo? Watu wakuu wenye cheo, watu wazito wenye mamlaka kubwa maarufu na wanaojulikana wanalalamika wananung’unika kinyume na Musa na haruni na maarufu zaidi wanatajwa kuwa Korah, Dathan na Abiramu wanazungumza maneno ya kutisha mno wanasema hivi “Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, Bwana naye yu kati yao; n'nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa Bwana?” Ni maneno ya ajabu sana kutoka kwa watu ambao huwezi kufikiri kuwa wanaweza kusema maneno kama hayo, Musa na haruni waliposikia walijua madhara ya uasi walianguka kwa Mungu kifudifudi na kuanza kuwaombea wao walikuwa wanajua wazi kuwa mtu akinza kushinda na mamlaka zilizoko anapamba na Mungu, walipata madhara makubwa sana kwa sababu ya ujeuri wao na maneno yao mabaya waliyoyasema biblia inatuelezea kuwa walifutiliwa mbali kwa mtindo wa kipekee kwani walimezwa na ardhi ona

Hesabu 16:28-33Musa akasema, Kwa jambo hili mtajua ya kwamba Bwana amenituma, ili nifanye kazi hizi zote; kwa kuwa mimi sikuzifanya kwa akili zangu mwenyewe.  Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi Bwana hakunituma mimi. Lakini Bwana akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao washukia shimoni wali hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau Bwana Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka;  nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote. Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni.”

Hawa walikufa namna hiyo kwa sababu walimuasi Mungu na waliwaasi viongozi, huwezi kuja kuwa kiongozi mzuri kama unamtukana kiongozi aliyepo, watu hawatakuja wakuheshimu kama unashindwa kuwaheshimu wengine au viongozi walioko, ndio maana Daudi aliendelea kuwa mpole kwa Sauli kwa sababu alikuwa ni mpakwa mafuta kwa wakati ule licha ya kuwa na madhaifu ya kibinadamu, kumbuka kuwa aushikaye upanga ataangamia kwa upanga, ni kanuni ileile mbovu unayoitumia kumsakama kiongozi aliyeko madarakani ndio hiyo hiyo itakuangamiza utakapokuja kutawala, kama una ndoto au Mungu amekuotesha kuwa utakuja kuwa kiongozi kumbuka hilo, viongozi waliokuwa na sifa kama Korah Dathan na Abiramu, walipomuasi Musa na Haruni walipoteza kabisa sifa zao na leo tunawasoma kama mfano wa watu wasiofaa, haiwezekani usema unamcha Mungu na wakati huo huo ukawa Humuogopi Mungu, je wadhani tutakuja kukulinda na kukupigia saluti zetu ilihali tunajua wazi kuwa hukuwaheshimu waliotangulia?  Mungu aliwafutilia mbali waasi, walikuwa wamejifunza kuwa “Usimtukane Mungu wala usimlaani mkuu wa watu wako” soma Kutoka 22:28 Lakini hawakujali walifutiliwa mbali

Hata hivyo kama haitoshi baada ya hawa kuuawa na Mungu mwenyewe siku ya pili tu badaya ya watu kumuogopa Mungu, vuiongozi wengine wakuu wa kabila za Israel, walinungu’unika tena angalia Hesabu 16:41Lakini siku ya pili yake mkutano wote wa wana wa Israeli wakamnung'unikia Musa, na Haruni, wakasema, Ninyi mmewaua watu wa Bwana.

Ukweli ninkuwa Mungu alikuwa amekusudia kuwafutilia mbali mkutano wote walioanzisha manung’uniko Lakini Musa na haruni tena wakijua madhara yatokana nayo na roho ya kuasi walipomoka kifudifudi na kuwaombea watu kwa Mungu kwamba hasira zake zisiwaangamize, Ndipo Mungu alipoamua kutuma pigo kali lililoua waisrael wapatao 14,700 unaweza kuona katika

Hesabu 16:45-50Ondokeni kati ya mkutano, ili niwaangamize mara moja. Wao wakapomoka kifudifudi. Musa akamwambia Haruni, Haya, shika chetezo chako, ukatie moto ndani yake, moto wa madhabahuni, kisha utie na uvumba juu ya moto, ukakichukue haraka, wende nacho katika huo mkutano, ukawafanyie upatanisho; kwa kuwa ghadhabu zimetoka kwa Bwana; hiyo tauni imeanza. Basi Haruni akakishika chetezo kama Musa alivyonena, akapiga mbio akaenda katikati ya mkutano; na tazama, tauni ilikuwa imeanza kati ya watu; akatia uvumba juu ya moto na kufanya upatanisho kwa ajili ya hao watu. Akasimama kati ya hao waliokufa na hao waliokuwa wakali hai; tauni ikazuiwa. Basi waliokufa kwa tauni walikuwa kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya hao waliokufa katika jambo la Kora. Haruni akamrudia Musa pale mlangoni pa hema ya kukutania; hiyo tauni ikazuiwa.”

Unaona hapa maandiko yanaeleza kuwa walioangamizwa kwa uasi hapa walikuwa wengi kuliko wale wa kwanza, Tabia ya wanadamu kunung’ung’unikia viongozi haikuanza leo, hata nyakati za biblia tunaona wanungunikaji wakiongezeaka kila wakati na Mungu aliona njia ya kuwaangamiza itasababisha wafutike wengi hivyo Mungu alianzisha mpango mahususi wa kukomesha manung’uniko hayo milele.

Umuhimu wa fimbo ya Haruni!

Fimbo ya Haruni inawakilisha jambo muhimu sana katika mpango wa Mungu, hususani katika swala zima la kuwaongoza wana wa Israel kutoka utumwani Misri kuelekea Kanaani katika nchi ya ahadi, Kwa mujibu watamaduni za Israel na kwa mujibu wa kanuni za kinabii, fimbo huwakilisha Mamlaka na utawala, Wachungaji walitumia fimbo kuongoza na kurekebisha maisha ya Kondoo Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.Mungu alipomuita Musa alikuwa Mchungaji wa kundi la mkwewe na alitaka akawaongoze Waisrael kutoka Misri, aliitumia fimbo ya Musa kuonyesha uwezo wake na nguvu zake kwa kufanya miujiza akiitumia fimbo ya Musa ona katika


Kutoka 4:1-5 “Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea. BWANA akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, Ni fimbo. Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.BWANA akamwambia Musa, Nyosha mkono wako, kamshike mkia; (akaunyosha mkono wake akamshika, naye akageuka kuwa fimbo mkononi mwake;) ili kwamba wapate kusadiki ya kwamba BWANA, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amekutokea."

Hesabu 20:11 “Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.  

    
Mungu aidha alimchagua kaka wa Musa Haruni ambaye naye alitumiwa kufanya miujiza kwa fimbo yake ona
Kutoka 7:19 “BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Shika fimbo yako, kaunyoshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya mito yao, juu ya vijito vyao, na juu ya maziwa ya maji yao, na juu ya visima vyao vyote vya maji, ili yageuke kuwa damu, nako kutakuwa na damu katika nchi yote ya Misri, katika vyombo vya mti, na katika vyombo vya jiwe

Kutoka 8:5 BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha mkono wako na fimbo yako juu ya mito, juu ya vijito, na juu ya maziwa ya maji, ukawalete vyura waje juu ya nchi yote ya Misri.

Kutoka 8:16BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri.

Ni fimbo ya haruni ambayo iligeuka nyoka mbele za Farao, na hata wachawi wa farao walipogeuza fimbo zao kuwa nyoka ni fimbo ya Haruni iliyogeuka kuwa nyoka iliyomeza fimbo za wachawi wote

Kutoka 7:8-10
BWANA akanena na Musa na Haruni, akawaambia, Farao atakaponena nanyi, na kuwaambia, Jifanyieni miujiza; ndipo utakapomwambia Haruni, Shika fimbo yako, uibwage chini mbele ya Farao, ili iwe nyoka. Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, wakafanya vivyo kama BWANA alivyowaambia; Haruni akaibwaga fimbo yake chini mbele ya Farao, mbele ya watumishi wake, ikawa nyoka.” Fimbo ya Haruni iliyogeuza maji yote ya Misri na mto nile kuwa damu

Kutoka 7:19-21BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Shika fimbo yako, kaunyoshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya mito yao, juu ya vijito vyao, na juu ya maziwa ya maji yao, na juu ya visima vyao vyote vya maji, ili yageuke kuwa damu, nako kutakuwa na damu katika nchi yote ya Misri, katika vyombo vya mti, na katika vyombo vya jiwe. Musa na Haruni wakafanya hivyo, kama BWANA alivyowaambia; naye akaiinua ile fimbo, na kuyapiga maji yaliyokuwa mtoni, mbele ya Farao, mbele ya watumishi wake; na hayo maji yote yaliyokuwa katika mto yakageuzwa kuwa damu. Hao samaki waliokuwa mtoni nao wakafa; na ule mto ukatoa uvundo, Wamisri wasipate kunywa maji ya mtoni; na ile damu ilikuwa katika nchi yote na Misri.”                  

Na miujizi mingine Mingi ilifanyika kupitia Fimbo hii ya haruni, Baada ya Musa na Haruni kuwaongoza wana wa Israel nje ya utumwa Jangwani Mungu alimchagua Haruni nwanae kuwa makuhani

Kutoka 28:1Nawe umlete Haruni ndugu yako karibu nami, na wanawe pamoja naye, miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani. Haruni, na Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari, wana wa Haruni.” na Hesabu 18:1Bwana akamwambia Haruni, Wewe na wanao na nyumba ya baba zako pamoja nawe mtachukua uovu wa patakatifu; wewe na wanao pamoja nawe mtauchukua ukuhani wenu.”  na Walawi wote waliosalia walikuwa wahudumu katika nyumba ya Mungu kwaajili ya kusimamia utoaji wa sadaka za kuteketeza na usimamizi wa ibada kwa taifa zima.  Hivyo ni wazi kuwa Mungu alimtumia Haruni na Musa na ni wazi kuwa walitumika kwa kiwango kikubwa katika ukombozi wa wana wa Israel wakitumiwa na Mungu na ni wazi kuwa Mungu alikuwa amemchagua aweze kuwa kuhani mkuu, Hata hivyo watu hawakuacha kumnung’unikia.

Fimbo ya kukomesha manung’uniko

Kwa vile mara kwa mara watu walikuwa wakinung’unikia na kusahau wapi walikotoka na walikotolewa Mungu alinza kuingilia kati ili aweze kukomesha manug’ung’uniko Mungu alimuamuru Musa kuwaita viongozi wote wa Kabila za Israel na kuwataka wote walete fimbo zao na kuwa fimbo zao ziandikwe majina na fimbo ya Haruni iandikwe jina lake ikiwakilisha kabila la walawi, na Mungu alimwambia Musa kuwa aziweke hizo fimbo katika hema ya kukutania na kuwa fimbo itakayochipuka itaashiria kuwa mtu huyo ndie ambaye Mungu amemchagua  na jambo hili litakuwa mwisho wa Manunguniko

Hesabu 17:5
Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung'uniko ya wana wa Israeli, wanung'unikiayo juu yenu.”

Waliacha fimbo zao mbele za Bwana na asubuhi kumbe Fimbo ya haruni iliyokuwa ikiwakilisha kabila la walawi ilikuwa imechipuka imetoamajani, na imeota maua na ilizaa tunda liitwalo lozi (almond) Ilidhihirisha wazi kuwa Mwenye nguvu, mwenye kuteua viongozi, mwenye kuweza kufanya kilichokufa kuwa hai, mwenye uwezxo wote  na mwenye kutia uzima alikuwa amemchagua Haruni, adiha Fimbo hiyo Musa aliiagiza iwekwe katika Sanduku la agano ili uwe ukumbusho wa milelena hii ingekomesha manunguniko ambayo yangeweza kusababisha vifo kila wakati

Waebrania 9:4yenye chetezo cha dhahabu, na sanduku la agano lililofunikwa kwa dhahabu pande zote, mlimokuwa na kopo la dhahabu lenye ile mana, na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, na vile vibao vya agano;”

Fimbo ya haruni iliyochipuka ilibaki kuwa ushahidi dhidi ya uchaguzi wa Mungu wa maongozi, Kuchipuka kwa fimbo hii pia kulikuwa na maana kuwa Mungu hatakuwa na Muda  wa kushughulika na waasi tena na mtumishi wake atakuwepo pale uwepo wa Mungu ulipo, Mungu hatawavumilia watu wanaoutesa mwili wa Kristo na kuugawanya, Mungu hatawavumilia watu wanaowashambulia viongozi aliowaweka mwenyewe madarakani, Mungu atasimama upande wa viongozi wake siku zote za maisha yake, atahakikisha kuwa wanastawi hata wakipigwa vita, wanazaa matunda, na kutoa maua yaani wataendelea kuwa watu wa kukumbukwa kutokana na yale watakayoyafanya kwa uweza wa Mungu milele na milele, unaweza kujutahidi kuwachafua watu wa Mungu na kuwashutumu na kuwasengenya, na kuwanena vibaya lakini Mungu si mjinga atasimama na watu wake atawastawisha kumbukumbu zao zitawekwa na hawataondoka kamwe katika moyo wa wala wanaowaongoza na moyo wa Mungu, Uongozi unaotoka kwa Mungu kamwe hauwezi kundolewa kwa fitina za wanadamu, Mungu anataka chaguo lake liheshimike na katika kanisa lazima ieleweke wazi kuwa wote wenye kuleta mafarakano na kutaka kutugawa wanapaswa kukemewa vikali

Yakobo 5:9Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.”

Mungu yuko tayari kuhukumu na kuwashughulikia watu wenye kunung’unika, Mungu anataka tushirikiaqna na kuchukuliana na kuhakikisha kuwa tunaleta maendeleo kwa pamoja hatupaswi kulalamika na kufikiri kuwa labda wewe unafaa zaidi kuliko mwingine sisi sote ni viongozi lakini kamwe hatuwezi kuongoza kwa wakati mmoja Mungu katika mpango wake anataka mmoja aongoze hivyo mmoja wetu anaposimikwa kuongoza sisi wengine tukae kimya na kumsaidia kufanikisha mambo kwa faida ya wote badala ya kutafuta kuwafutilia mbali huku tukisahau mchango wao katika jamii,  Mungu anapolkuwa amekuweka mahali, au amekupa cheo fulani kumbuka kuwa sio watu wote watafurahia lakini kumbuka Mungu amekuweka katika sabduku lake la agano ili akukumbuke daima amekuweka katika uwepo wake ni malaka yako ndiyo itakayostawi, ni wewe ndiwe utakaewaokoa watu wako, ni wewe ndiye ambaye Mungu ataitumia fimbo yako kukutana na kiu ya watu wako, kuwakimbiza adui zaokuwaweka huru watu wako, kuondoa ujinga wao, kuondoa umasikini wao, kuwapa raha ya kanaani wanayoitizamia kuwapatanisha na Mungu hivyo hupaswi kuogopa kelele za watu kustawi kwako na kuzaa kwako matunda kutanyamazisha kelele za adui zako, kuwa chaguo la Mungu hakumaanishi kuwa tutakosa wapinzani kumbuka hata shetani ni mpinzani wa Mungu, hatupaswi kuogopa kamwe, haruni na Musa waliosnga mbele walikuwa na ujasiri waliwaonea huruma hata wapinzani wao kwa sababu walijua kuwa wanaowapinga wanapingana na Mungu mwenyewe, Ndugu yangu kama wachawi wanakupinga, maadui wanakupinga watru wanakuasi watu wanakuteta wanakusengenya wewe endela kutekeleza agizo la mungu endelea kupiga kazi, kazi zako zitatangaza kuwa wewe ni mtu wa namna gani, Yesu pia watu hawakumuamini lakini alitoa wito kwa wapinzani wake na adui zake waangalie yale aliyoyafanya kuwa yanatokana na uweza wa uungu ndani yake Musa na Haruni unaweza kuwapima katika mzani wako na ukawaona hawafai Lakini kazi walizozifanya kupitia Mamlaka waliyopewa na Mungu zinatangaza wazi kuwa wao ninani, na hayo ndio matundana ustawi wa watumishi wa Mungu unawapiga vita waoa wanaizdi kustawi na kuchanja mbuga piga kazi zaidi kadiri adui zako wanavyojipanga kwa majungu wewe endelea mbele na fimbo yako itakomesha manung’uniko

 Yohana 10:37-38 Kama sizitendi kazi za Baba yangu, msiniamini; lakini nikizitenda, ijapokuwa hamniamini mimi, ziaminini zile kazi; mpate kujua na kufahamu ya kuwa Baba yu ndani yangu, nami ni ndani ya Baba.

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

0718990796

Siku ya Bwana !

Ufunuo 1:10 “Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, Kama sauti ya baragumu,



 
Utangulizi:
Leo nataka kuchukua muda wa kutosha pamoja na wewe msikilizaji na msomaji wangu kuzungumzia moja ya jambo muhimu la kibiblia litupasalo sisi kujifunza na hili lina uhusiano mkubwa na SIKU YA BWANA (JUMAPILI), Katika fungu la maandiko ya msingi utaweza kuona jambo la kushangaza kuwa Mtume Yohana japo alikuwa utumwani uhamishoni katika kisiwa kiitwacho Patmo kwaajili ya Mateso, Bado aliweza kuwa katika Roho siku ya Bwana! (JUMAPILI) Hili ni jamnbo la kushangaza sana na ni muhimu tukalipa kipaumbele kwani kuna kitu cha kujifunza:

Mtume Yohana alikuwa mzee wa siku nyingi sana na alikuwa amepelekwa uhamishoni mbali na ndugu jamaa na marafiki mbali na makanisa na mbali na wale wote waliokuwa naye katika imani, alitupwa katika kisiwa kikame chenye mawe katika inchi ya Ugiriki visiwani, ili asiweze kuendelea kuihubiri injili na wala kumuelezea Yesu Kristo kwa watu wengine, kwa ufupi alikuwa mfungwa kwaajili ya injili. Lakini pamoja na kutengwa mbali na jamaa zake na watu wake anaandika kuwa alikuwa katika “ROHO SIKU YA BWANA!” (Jumapili) hii maana yake nini? Alikuwa katika roho siku ya JUMAPILI! kama katika mazingira magumu namna hiii mtume Yohana alikuwa anakumbuka bila kalenda akiwa mbali akiwa porini akiwa kisiwani akiwa matesoni kuwa leo ni siku ya Bwana yaani ni jumapili, maana yake ni kuwa hatuna udhuru au sababu za kutosha kuacha kuipa umuhimu siku hii siku ya jumapili ambayo hujulikana katika maandiko kama siku ya Bwana.

Maana ya siku ya Bwana!

Ni muhimu kufahamu kuwa Neno siku ya Bwana linapotamkwa katika Kiswahili au linapoandikwa katika Kiswahili, linatunyima aina fulani ya upana wa kulizungumzia kwa raha inayokusudiwa hii ni kwa sababu katika kiigereza kuna maneno makuu mawili ambayo yanatumika kuelezea siku ya Bwana  mfano angalia “THE DAY OF THE LORD”  na angalia pia neno “THE LORDS’ DAY” Misamiati hii miwili yote kwa lugha ya  Kiswahili huitwa “SIKU YA BWANA” kwa misngi huo sasa  Ni muhimu kufahamu kuwa neno siku ya Bwana kinabii linaweza kuwa na maana pana sana tofauti na ile ninayotaka kuizungumzia leo, Neno siku ya Bwana kinabii  (THE DAY OF THE LORD) linamaanisha siku za mwisho, ama majira ya neema na majira ya hukumu kuanzia ujio wa Yesu Kristo mara ya Kwanza kwa wokovu mpaka ujio wake mara ya pili kwa hukumu, kipindi hiki kinabii kinaitwa vilevile siku ya Bwana.”THE DAY OF THE LORD” Kwa mfano

1.       Siku Mungu alipotangaza hukumu kwa watu wake Wayahudi au Israel kuwaonya au kuruhusu wavamiwe na maadui zao kinabii hii pia iliitwa siku ya Bwana Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.” Unaona hapa siku ya Mungu kuhukumu watu wake kwa sababu kadhaa inaitwa siku ya Bwana yaani siku ya Hasira siku ya kuadhibu watu wake unaweza pia kuona katika Amos 5:18-20 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.  Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma. Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga.”

2.       Siku ya Bwana kinabii vilevile ilimaanisha siku za mwisho yaani tangu ujio wa Yesu Kristo mara ya kwanza, alipozaliwa, umwagiko au ujio wa Roho Mtakatifu, unyakuo wa kanisa,  kuja kwa Yesu mara ya pili, kuja kuhukumu ulimwengu, na kuja kutawala  na mbingu mpya na nchi mpya au kipindi cha neema hiki pia manabii walikiita siku ya Bwana Yoel 2:31 “Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo.” Pia nunaweza kuona katika Matendo 2:14-20 “Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu. Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli, Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri. Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.”

3.       Siku ya bwana kinabii pia humaanisha wakati wa kunyakuliwa kwa kanisa  na  kurudi kwa Yesu mara ya pili  na pia wakati wa hukumu ya watakatifu na mengineyo unaweza kuona katika 1Wathesalonike 5:2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.” 2Wakoritho 1:14 “14. vile vile kama mlivyotukiri kwa sehemu, ya kwamba sisi tu sababu ya kujisifu kwenu, kama ninyi mlivyo kwetu sisi, katika siku ile ya Bwana wetu Yesu.”

Unaweza kuona kwa hiyo siku ya Bwana (The Day of The Lord) ni siku ya Bwana kinabii ina maana kdaa kama zilivyoainishwa hapo juu na siku ya Bwana (The Lords’ Day) inayotajwa pekee katika ufunuo 1:10 ni siku tofauti, ni siku ya jumapili ni siku ambayo katika somo hili ndio tutakayoizungumzia zaidi kwa kusudi la kuonyesha kwanini tunaabudu jumapili.

Siku ya Bwana tofauti na siku ya sabato!      

                       
               
Wengine hufikiri kuwa siku ya Bwana inaweza kuwa siku ya Sabato kwa sababu ni siku iliyotengwa na Mungu mwenyewe ili wanadamu wapate kumkumbuka na kumuabudu na kupumzika, siku hii inadhaniwa kuwa ni ile sabato ambayo Mungu aliwaamuru wana wa Israel waiadhimishe kwaajili kukumbuka ukombozi wao kutoka utumwani kule Misri!

Kumbukumbu la Torati 5: 14-15 “ lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng'ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako ye yote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile vile kama wewe. Nawe utakumbuka ya kuwa wewe ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, na ya kuwa Bwana, Mungu wako, alikutoa huko kwa mkono wenye nguvu, na mkono ulionyoshwa; kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wako, alikuamuru uishike sabato.” 

Kwa kawaida sabato hii ya wayahudi huanzia ijumaa jioni na kuishia jumamosi jioni, siku hii ilikuwa ni siku ambayo Mungu aliamuru Israel wasifanye kazi yoyote, wao wala watoto wao wa kiume, wala binti zao,wala watumwa wao, wala wanyama wao, siku hii pia ilikuwa ni siku ya kuadhimisha kazi ya uumbaji wa Mungu na kuikumbuka kama siku ambayo Bwana mwenyewe anatajwa katika maandiko kuwa alipumzika au alistarehe! Na aliiitakasa siku hiyo:-

Mwanzo 2:2-3 “Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.” Ona pia

Kutoka 20:8-11 “Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.”  Na pia

Kutoka 23:12 “Siku sita utafanya kazi yako, na siku ya saba utapumzika; ili kwamba ng'ombe wako na punda wako wapate kupumzika, kisha mwana wa mjakazi wako na mgeni wapate kuburudika.”

Sabato ilikuwa ni ishara kwa wana wa Israel yaani wayahudi kwamba Mungu amewafanya kuwa taifa tofauti na mataifa mengine ili waweze kumcha Bwana Mungu wao. Lakini ni muhimu kufahamu kuwa hakuna mahali popote katika maandiko Sabato imewahi kutajwa kama siku ya Bwana hata kidogo, Sabato iliendelea kutajwa kama sabato katika Biblia agano la kale na agano jipya na sio siku ya Bwana  siku ya Bwana ni siku tofauti    

        
Mathayo 12:5 “Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia? “ angalia pia;-

Yohana 7:23 “Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato?”

Aidha kwa mujibu wa Mafundisho ya Mitume inaonekana wazi kabisa kuwa sabato ilikuwa ni kivuli, yaani “typology” kuhusu pumziko halisi la rohoni ambalo ni Yesu Kristo. Sabato ni alama ya kinabii kuhusu Pumziko halisi ambalo Mungu atalileta kwa watu wake, Neno Sabato kwa ufupi maara yake ni Raha, katika biblia ya kiingereza hutumika neno “Rest” au kustarehe raha zimatajwa katika biblia Mara sita mara tano ikiwa ni raha ya kinabii inayotabiriwa kuwa watapewa wanadamu baada ya taabu zao za hapa duniani jumla ya raha zote zinazotajwa katika maandiko ni pamoja na raha

1.       Raha au starehe ya Mungu mwenyewe Mwanzo 2:1-3 “Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.      Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.”
Sabato hii ya Bwana ni sabato ya kinabii, katika kitabu cha Mwanzo Mungu mwenyewe alikuwa nabii kabla ya kutuma manabii, ana ametabiri maswala kadhaa yajayo, Mungu alitabiri kuhusu starehe ijayo kupitia sabato hii, hii ni sabato yake, juu ya kazi zake haitajwi tena popote au labda Musa aliiweka kwaajili ya mkazo wa sabato ya kiyahudi ili Israel waweze kujifunza kutoka kwa Mungu, lakini ni wazi kuwa Mungu hapumziki Yesu alisema baba yangu anatenda kazi hata sasa  Yohana 5:16-17 “Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.  Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi.” Wayahudi walikuwa na fikra potofu kuhusu siku ya sabato, walifikiri Mungu anaopumzika Yesu alikuwa na ujuzi tofauti kuhusu pumziko hili la Mungu, Mungu hakustarehe hii ilikuwa ni alama ya kinabii ya kuja kuwaokoa watu wake na kuwapa sterehe ya kweli baada ya maisha na kazi ngumu za duniani 

  
2.       Raha au Starehe ya Sabato Kutoka 20:8-11” Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.” Mungu aliiweka sabato hii katika amri zake kwa kusudi la watu wa Mungu kuwa na nafasi ya Mungu katika mioyo yao, kwa nini ilikaziwa sana ilikuwa ni kivuli cha starehe halisi pumziko halisi ambalo ni Yesu Kristo.   

   
3.       Raha au starehe ya Ndoa Ruthu 3:1” Kisha Naomi akamwambia mkwewe, Je! Mwanangu, si vizuri nikutafutie raha, ili upate mema?” hii ni aina ya sterehe, au Pumziko ambalo kila mwanamke hutamani kuwa nalo katika maisha yake ndoa


4.       Raha au starehe ya kanaani iliyotolewa na Yoshua Waebrania 4:8 “Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye.Mungu aliwaahidi Israel waliokuwa wakipata shida Jangwani, aliwaahidi starehe aliwaahidi pumziko katika nchi ya kanaani pumziko ambalo Yoshua alikuwa amekabidhiwa kuwapa hii ni sabato ya kanaani, hata hivyo hawakuweza kustarehe, walipambana na maadui baada ya kufa kwake Joshua, raha ya kanaani ilikuwa ni ubnabii tu war aha kamili itakayoletwa na Yesu Kristo.

5.       Raha au Starehe ya wokovu ni raha ya nasfi inayotokana na kumpokea Yesu Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. nJitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”      Mtu akimuamini Bwana Yesu anapata starehe sabato, pumziko la nasfi hata sasa pamoja na taabu zote na changamoto za dunia liko pumizko katika mioyo ya watu waliomuamini Bwan wetu Yesu

6.       Raha au starehe ya watu wa Mungu wakati Mungu atakaposimamisha utawala wake hii ndiyo iliyokuwa imetabiriwa katika maandiko Waebrania 4:9 “Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.Hii ndio sabato iliyo tabiriwa kwa watu wa Mungu itawapata watu wote waliomuamini Yesu Kristo huu utakuwa ni wakati ambapo masikani ya Mungu itakuwa pamoja na wanadamu milele.

Wakolosai 2:16-17 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”. Paulo anayazungumza haya akiwa na ufahamu kamili kuwa sabato ni KIVULI yaani TYPOLOGY  au unabii wa pumziko la mwanadamu, Raha hii iliyoahidiwa ndiyo ambayo watu wa Mungu wanapaswa kuhakikisha kuwa wanaingia hii ni raha ya Mbinguni. Ona:-

Waebrania 4:1-11 “Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu: Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote; na hapa napo, Hawataingia rahani mwangu. Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao, aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo,kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye. Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi

Ni wazi kuwa sabato haijawahi kuitwa siku ya Bwana katika maandiko bali iliitwa sabato hivyohivyo na hii ilikuwa muhimu kwa wayahudi na sio mataifa mengine,  Wayahudi waliomuamini Masihi nyakati za kanisa la kwanza waliendelea kuitambua sabato kama siku takatifu kwa sababu ilikuwa mila na desturi yao, aidha ilikuwa ni siku ya makusanyiko na yangeliweza kufaa kwaajili ya kuihubiri injili na hata mataifa walioamini nyakati zile kwaajili ya ndugu zao wayahudi,kaka na dada zao waliendelea kuiheshimu Sabato kama njia ya kumuheshimu Mungu, kwa hiyo kumuabudu Mungu siku ya sabato sio tatizo, Mungu haangalia usahihi wa siku ya kuabudu bali huangalia usahihi wa msukumo wa Moyo kama mioyo yetu inasukumwa kuiheshimu na kuishika sabato kama sehemu ya kuishika sheria basi hapo moyo wako hauko sahihi mbele za Mungu  na tayari umetengwa na Kristo! Ona maandiko yanasema:-

Wagalatia 5:4 “Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.

Kama dhamiri zetu ziko safi mbele za Mungu tuko huru kuabudu siku yoyote ile iwe jumamosi au jumapili au hata nyinginezo Mungu anapendezwa na dhamiri au mikao yetu ya moyo na sio siku, au kujitia chini ya Sheria, Mungu hapendezwi na watu wanaomuabudu yeye kwa midomo tu huku mioyo yao ikiwa mbali naye, awaye yote ambaye anakuja katika ibada kwa sababu tu ni lazima aje siku hiyo au kwa sababu ya sheria za kibinadamu moyo wake hauna nafasi katika Mungu bali uko mbali naye.

Isaya 29:13 “Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;

Mathayo 15:7-9 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.    

          
Mungu hafurahishwi na watu wanaoshika sheria, maagizo na matakwa lakini anataka moyo unaowakwa kwa upendo kwake kama mtu anampenda Mungu na kwa moyo wake wote akaamua kuabudu siku yoyote iwe jumamosi, au jumapili, au jumatatu au jumanne au jumatano, au alhamisi au ijumaa Mungu ataukubali moyo wa Mtu huyo biLa kujaLi anaabudu lini!

Waebrania 12:28-29 “Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho; maana Mungu wetu ni moto ulao”.

Zaburi 51:15-17 “Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, Na kinywa changu kitazinena sifa zako. Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.                Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.”   

Unaona Mungu hataudharau moyo wa mtu mnyenyekevu, mwenye kumcha yeye moyo uliovunjika na uliojawa na shukurani kama moyo huo utamuendea siku yoyote ile kwa unyenyekevu bila kujali siku hiyo ni siku ya namna gani moyo wa aina hii Mungu atautazama
Isaya 66:2 “Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu

Neno siku ya Bwana katika Biblia ya kiyunani linasomeka kama neno (mia) limetumika mara nyingi zaidi katika injili kumaanisha siku aliyofufuka Yesu, siku hiii ndio ambayo wakristo wa nyakati za kanisa la kwanza waliiheshimu na kuitumia kwa ibada zaidi na ikijulikana kama siku ya Bwana, Msingi mkuu wa somo hili ni kuangalia sababu za kimaandiko na za kihistoria kwanini wakristo wameichagua siku ya Bwana yaani jumapili kuwa siku rasmi ya ibada na kwanini tunaabudu jumapili, huku hoja ya msingi ikibakia kuwa kwa Mungu siku zote ni sawa na Mungu humkubali awaye yote anayemuabudu kwa dhati bila kuacha kuzingatia kuwa siku hii Kristo alijifunua na anajifunua katika siku hii muhimu ambapo mauti ilimezwa kwa ushindi wa Kristo dhidi ya kifo katika siku ya kwanza ya juma!

Nalikuwa katika roho siku ya Bwana!

Baada ya kufahamu hasa maana ya siku ya Bwana na mapenzi ya Mungu kuhusu kuabudiwa kwake ni muhimu kufahamu kuwa  siku ya Bwana inayotajwa katika Ufunuo 1:10 ni siku ya Jumapili hili ni swala lililo wazi kimaandiko, siku hii ni siku ambayo wakristo wa nyakati za kanisa la kwanza waliadhimisha kila wiki kama siku muhimu aliyofufuka Yesu Kristo na ilijulikana kama siku ya kwanza ya juma, ni wazi kuwa  neno hili siku ya Bwana katika agano jipya linatajwa hapa tu, Lakini ni ukweli usiopingika kuwa Yohana alikuwa akiwandikia watu wakristo ambao walikuwa wanajua wazi kuwa akitaja siku ya Bwana namaanisha jumapili yaani siku ya kwanza ya juma, jambo ambalo wakristo wa nyakati za kanisa la kwanza walikuwa wakilijua wazi kwamba siku walizokuwa wakikutana kuabudu ilikuwa siku ya kwanza ya juma ambayo ni jumapili na sababu kubwa ni kuwa ilikuwa ndio siku ambayo Bwana Yesu alifufuka kutoka kwa wafu, siku hii iliitwa au kujulikana kama siku ya kwanza ya juma, ilikuwa ni siku ya namna gani kwa  mujibu wa maandiko na historia ya kanisa:-

1.       Ilikuwa ni siku ambayo Yesu alifufuka kutoka kwa wafu Mathayo 28:1-7 “Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi. Na tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la nchi; kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaja akalivingirisha lile jiwe akalikalia. Na sura yake ilikuwa kama umeme, na mavazi yake meupe kama theluji. Na kwa kumwogopa, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu. Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa. Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia.

Marko 16:1-6Hata sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka. Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza; wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi? Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno. Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu. Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulibiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka

Luka 24:1 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari. Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi, Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu. Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta; nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, hao waliwaambia, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya,

2.        Baada ya kufufuka kwake iko wazi katika maandiko kuwa Yesu alikuwa na tabia ya kuwatokea wanafunzi wake katika siku hii ona:-

Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.”

Yohana 20:19 “  Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu.”

Yohana 20:26 “Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu.”
3.       Kuja maalumu na umwagiko wa Roho Mtakatifu ulifanyika jumapili siku ya kwanza ya juma  hii ni wazi kutokana na desturi kuwa Pentecost iliadhimishwa  siku ya 50  baada ya kukamilika kwa sabato saba sawa na agizo la

Walawi 23:15-16 “Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba; hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea BWANA sadaka ya unga mpya.”

Neno Pentecost maana yake “50” Hamsa au hamsini siku hii ilihesabiwa siku 50 tangu baada ya pasaka yaani zikiisha kupita sabato saba siku ya pili yake waliadhimisha siku ya Pentecoste ni katika siku hii wanafunzi walipokuwa wamejifungiwa wakiwa wanaomba Roho Mtakatifu alikuja maalumu duniani na kuwajaza wote na kanisa lilianza rasmi katika siku hii ambayo kismingi nayo ilikuwa siki baada ya sabato yaani siku ya kwanza ya juma angalia katika

Matendo 2:1-4  Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.                 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.”

4.       Nyakati za kanisa la kwanza watu walikutana kila siku kuabudu nyumba kwa nyumba angalia Matendo 2:46 -47 “Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,  wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.

Hata hivyo kutokana na kuongezeka kwa majukumu mbalimbali katika maisha ya kila siku na kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi walifikia muafaka kuwa ni vema ikatengwa siku maalumu kama siku ya kuabudu na ikatengwa siku ya bwana kama siku ya kuadhimisha siku ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, aidha pia ilikuwa ni maalumu kwa kuonyesha kuwa wakristo wako mbali au huru kutoka katika sheria za Musa na siku iliyofikiriwa ilikuwa ni siku ya bwana yaani jumapili, Kwa hiyo mitume akiwepo na Paulo waliiadhimisha siku hii na kuitumia kamasiku ambayo waamini wa Kikristo wangekutana na kumuabudu Mungu kwa pamoja

Matendo ya mitume 20:7 “Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.”

1Wakoritho 16:2 “Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;

5.       Kitabu cha Ufunuo wa Yohana kilifunuliwa kuanzia siku ya Bwana yaani jumapili Ufunuo 1:10-19  Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, Kama sauti ya baragumu, ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia. Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu;  na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini. Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto; na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi. Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo.

Unaweza kuona ni katika siku hii ya Bwana yaani Jumapili Yohana akiwa anamuabudu Mungu akiwa amezama rohoni akikumbuka wazi kuwa ndio siku ya ushindi na ndio siku ambayo wakristo hukutana kuabudu yeye alikuwa katika roho akiungana nao kumuadhimisha Yesu na ndio unaona sasa Yesu akimtokea katika siku hii na kumuagiza aandike kitabu cha ufunuo ni wazi kabisa kuwa kibiblia siku hii sio ya kupuuzwa na uko umuhimu mkubwa wa kuabudu katika siku hii sawa na fundisho la mitume na kama yanenavyo maandiko

6.       Ushahidi wa Mababa wa kanisa
-          Ignatius aliandika hivi “hatupaswi kuihika sabato tena. Lakini tunapaswa kuishi sawa na siku ya Bwana ambayo nuru ya kweli iliangaza”
-          Justin mfia dini alisema alipokuwa akiutetea Ukristo “Jumapili ni siku ambayo sisi tu akusanyika kwa sababu ni siku ambayo Mungu alileta mabadiliko makubwa kwa kuondoa giza ulimwenguni na ndio siku ambayo Yesu Kristo mwokozi wetu alifufuka kutoka kwa wafu
-          Mafundisho ya mitume yaliyokusanywa Mwaka 105 AD ynasema hivi, “Mitume kwaajili ya hayo waliichagua siku ya Bwana siku ya kwanza ya juma kwaajili ya ibada na kwaajili ya kusoma maandiko na kushiriki Meza ya Bwana kwa sababu ni siku ya kwanza ya Juma ndipo Yesu alifufuka” 


-          Eusebous mwana historia aliyeheshimika sana nyakati za kanisa hata wakati wa mfalme Contantine  aliandika hivi “Tangu mwanzo wakristo walikusanyika siku ya kwanza ya juma kwa makusudi ya kuabudu kusoma maandiko, kuhubiri na kushiriki meza ya Bwana , kwa sababu Yesu alipata ushindi dhidi ya kifo siku hii na amakuwa wa kwanza katika cheo na hivyo anapaswa kuheshimiwa kuliko sabato ya kiyahudi”
               
7.       Yesu Kristo ndiye Bwana wa Sabato 

Ni muhimu kufahamu maana ya maneno haya Yesu ndiye Bwana wa Sabato, Meneno haya yamerejewa mara kadhaa katika injili za

Mathayo 12:8 “Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato”. na Marko 2:28 “Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.” Na Luka 6:5 “Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.”

Yalikuwa ni maneno ya Yesu mwenyewe kuwa Yeye ndiye bwana wa Sabato Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema haya? Alikuwa akimaanisha Yeye ndiye mwenye mamlaka dhidi ya sheria zote na taratibu zote ikiwemo sheria ya Sabato, Yesu alisema kwa maneno mengine yeye ni mkuu kuliko sabato, yeye ni mkuu kuliko sheria , yeye ndiye mfanya sheria , Mafarisayo walikuwa wameikazia sheria na kutunga shetria zipatazo 39 za kuikazia zaidi siku ya sabato na kuisimamia kana kwamba wao ndio wafanya sheria Yesu alikuwa akiwaambia wazi kuwa yeye ndio  Muumba na ndio kwa asili mwanzilishi wa sabato hakuna mtu mwenye mamlaka ya kumuamrisha aitumiaje ilihali yeye ndiye mtawala wa kanuni hiyo 

Yohana 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.” Ona pia

Waebrania 1:10 “Na tena, Wewe,Bwana,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako;”

 Yeye ni zaidi ya Mafarisayo na ndiye mwenye mamlaka ya kuwakosoa mila na desturi zao wanazofikiri kuhusu Matumizi ya sabato yeye ndiye mwenye mamlaka kamili ya kutafasiri matumizi sahihi ya sabato Yeye kama mtawala dhidi ya sheria zote ikiwemo sabato ana mamlaka ya kuitumia kama apendavyo yuko juu ya sheria hii, Yeye ndiye sabato yenyewe hakna mwanadamu anaweza kupata pumziko la kweli pasipo Yesu, yeye alikuja na kufa na kufufuka ili atukomboe nalaana yote ya torati ikiwemo mateso ya kuishika sabato, Wokovu tulio nao katika Kristo umeifanya sheria ya agano la kale ikiwemo sabato isiwe na maana tena  kimsingi sabato  ilifanyika yaani iliwekwa au ilikuwepo kwaajili ya mwanadamu na sio mwanadamu kwaajili ya sabato    

Marko 2:27 “Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.”

maana yake sabato ilikuwa ni unabii kwaajili ya kuwapa wanadamu pumziko baada ya kufanya kazi kwa mikono yao wenyewe kwa siku sita, tafasiri sahihi ni kuwa hakuna mtu anaweza kujiokoa kwa kazi zake mwenyewe wokovu wa kweli na pumziko la kweli ljnatoka kwa Mungu, sasa tunaweza kustarehe katika neema yake badala ya kuhangaika kutafuta kibali cha Mungu kwa nguvu zetu wenyewe Yesu amkuja kuifanya kazi hiyo

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”

Sasa hapa Yuko mfalme na hapa iko katiba, hapa ziko mali na hapa yuko mtoa mali, hapa uko uhai na hapa yuko mtoa uhai, hapa iko sabato na yuko bwana wa sabato, wewe utachagua nini? Aliyeweka sheria au sheria yenyewe, wale wanaoadhimisha ibada siku ya jumapili wamemchagua Yesu mwenyewe na wale wanaoadhimisha sabato wamechagua sheria ya Musa 

Sabato, muandamo wa mwezi na kadhalika zilikuwa ni alama kivuli alama za kinabii zinazomuhusu Yesu Kristo na hivyo wakristo hawapaswi kuhukumiwa na mtu awaye yote kuhusu maswala hayo ambayo kwa sasa hayana maana, huku tukitilia maanani kuwa hatupaswi vilevile kuwahukumu wanaozing’ang’ania kama wana dhamiri safi na hakuna anayepaswa kumshambulia mwenzake muhimu ni Yesu Kristo

Wakolosai 2:16-17 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.

Ikumbukwe pia wazi kuwa jumapili siku ya Bwana wala sio mbadala wa sabato, yaani kwa maneno mengine jumapili sio sabato ya wakristo, ni siku ya kumuabudu Yesu, pamoja na kuwa tunaweza kujichagulia siku yoyote kwa mapumziko na kumuabudu Yesu aliyekufa na kufufuka kwaajili yetu na sio kwa misingi ya Torati ya Musa,

Warumi 6:14-15 “Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema. Ni nini basi? Tufanye dhambi kwa sababu hatuwi chini ya sheria bali chini ya neema? Hasha!

Watu waliookolewa wako huru kumuabudu Mungu siku yoyote na hakuna siku yenye maana kuliko nyingine awaye yote anayekuja na hoja ya kufikiri au kubishana kuhusu siku ni mpumbavu na hayajui maandiko, hakuna sababu ya kumuhukumu mtu awaye yote anayeabudu siku fulani kama anaabudu kwa moyo, cha msingi ni nani  anayeabudiwa na sio siku gani anaabudiwa, Mtu aliyekomaa kiroho hawezi kupata shida ya ipi ni siku ya kuabudu Paulo mtume alishafunga mjadala kuhusu siku ya kuabudu, lakini ni vema ikaeleweka wazi kuwa sabato ilisisitizwa kama alama kivuli cha starehe au raha ijayo ambayo ina uhususiano na raha ya wokovu na raha ya milele pumziko la kweli la wanadamu lililoandaliwa na Mungu.

Warumi 14:4-5 “Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha. Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.”

Hitimisho:

Siku ya Bwana ni muhimu kwa sababu ndio siku ambayo Yesu alifufuka, ndio siku ambayo sabato halisi alitukomboa na kutuweka huru, ndio siku ambayo Yesu alikuwa akiwayokea wanafunzi wake, ndio siku ambayo tamaduni za kanisa la kwanza walikuwa wakikkutana kusoma neno, kuomba, kuumega mkate na kushirikiana na ndio siku ambayo mtume yohan a alikuwa katika roho, na ni siku ambayo inajitofautisha na wale waliomkataa Yesu wakiwemo baadhi ya wayahudi, ni siku ya kipekee inayoonyesha kuwa tuko huru mbali na sheria ya Musa na kongwa zima la sheria za kiyahudi ambazo haziwezi kuokoa ni siku ya neema ya Mungu! Mwenye masikio ya kusikia na asikie!

Na Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye hekima!
0718990796