Jumanne, 12 Mei 2020

Mtego wa shughuli Nyingi!

1Petro 4:15 “Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.  

Utangulizi:
 Ni muhimu kufahamu kwamba ili mtu wa Mungu aweze kuwa imara kiroho anahitaji muda mwingi wa kukaa katika uwepo wa Mungu, kuomba, kujisomea neno na kutafakari na kuimba na kujizatiti kiroho kuliko tunavyoweza kufikiri, maandalizi yetu ya kiroho binafsi ni muhimu kwa ushindi dhidi ya ibilisi kuliko hata huduma, Mojawapo ya mbinu kubwa sana anayoitumia ibilisi ili kuwamaliza watu wengi kiroho na hatimaye ili aweze kuwaangusha ni kuwaingiza katika MTEGO WA SHUGHULI NYINGI kwa msingi huo ni muhimu kwetu kuijua mbinu hii ili shetani asipate kutushinda kwa kutokuzijua mbinu zake angalia  2Wakoritho 2:11 “Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake Biblia ya kiingereza inatumia maneno “Let Satan should get advantege of us – yaani asije akapata faida, akapata kitu kwetu, akafaidika, kwa mbinu “Fikra” zenye hila zenye kuumiza zenye ujanja cunning strategies mbinu anazitumia adui ili aweze kutushinda, Biblia inatutahadharisha kuwa wajuzi na wajanja katika mbinu za ibilisi ili asitunase, moja ya mbinu hii ni mtego wa shughuli nyingi!
Shetani anajua nguvu zako na uweza wako ulio nao, anajua wazi kuwa asili ya nguvu zako iko katika chanzo cha ngubu za Roho Mtakatifu unachokitegemea, ambacho kimeungwa katika kujityoa kwako binafsi kwa Mungu self devotional kwa msingi huo hataki na wala hatakubali upate nafasi ya kurudi magotini na katika kulisoma neno la Mungu na badala yake atakupa kitu mbadala ili akutumie kwenye hilo na baada ya muda flani aje na mbinu zilezile za kukuangusha ukiwa mtupu kabisa, mtego huu na mbinu hii anayoitumia shetani ni Mtego wa shughuli Nyingi.
Ni muhimu kufahamu kuwa unaweza kuwa unampenda Mungu sana na unapenda sana uwe na Muda wa kuomba na kububujika katika uwepo wa Mungu, unapenda upate nafasi ya kufunga na kuomba na kutafakari neno na kuhudhuria ibada na kufanya mambo yote yatakayokuweka karibu na Mungu na kuna uwezekano kabisa umekomaa kiroho na umefikia ngazi ambayo hakuna jaribu jipya litakuja kwako usilibaini, Shetani akiisha kufahamu hilo hatakuwa na Majaribu ambayo anajua kuwa utashituka kwa haraka bali atakuja na Mtego wa shughuli nyingi, kwa mtego huu atakutumia kwa muda mrefu uwe unashughulika na mambi mengi sana ambayo yanaweza kuwa kama ya kiroho hivi lakini baada ya Muda utagundua kuwa umepungukiwa sana na uwepo wa Mungu na katika wakati huu anaweza kukusambaratisha atakavyo akihakikisha kuwa hauna na wala haupati nguu ya kuinuka tena!  
Binafsi Kuna jambo nimekuwa nikimuomba Mungu sana, kuhusu maisha yangu katika siku za karibuni ili kwamba Mungu aweze kuingilia kati na kunisaidia, nampenda sana Mungu, napenda sana neno lake na napenda sana kuomba na pia kuandaa jumbe za neno la Mungu kwa kusudi la kuwasaidia watu wake, napenda kukaa uweponi mwake,  hiyo ni kazi yangu, ni wajibu wangu ndio kazi niliyoitiwa, nimeitwa kuujenga mwili wa Kristo na hili nalifanya kwa uaminifu, Lakini nahisi kuna kitu kimepungua kwangu, nahisi kiu ya kumuhitaji Mungu, nafanya kazi yake lakini nahisi nimemmisi Mungu, sio yeye tu nimemisi pia baadhi ya watu, ndugu zangu jamaa zangu na hata marafiki zangu nahisi kama kuna jambo ninapoteza sio kiroho bali na hata kimwili, kwa sababu hata ratiba ya kula haiko sawasawa nimekuwa na shughuli nyingi mno mno nikiwa natafakari hilo siku moja nikaelewa kuwa ni mtego wa Ibilisi!
Fikiaria kama unaweza kuwa na shughuli nyingi, kiasi cha kutokuwa na Muda na marafiki, jamaa, familia, mkeo, wanao, na hata muda wa kula au ahata kufanya mazoezi na unarejea nyumbani ukiwa umechoka mno, hata kula kwenyewe unaona uvivu! Kumbuka shughuli ulizokuwqa ukizifanya sio dhambi hata kidogo ni shughuli zilizoko katikati yako na huduma yako, kwa hiyo ni kama za huduma yako, wale watu waliofikia ngazi ya kuwa viongozi, Maasskofu, waangalizi, mitume na manabii watakubaliana nami katika hili kuwa kadiri unavyokuwa na majukumu haya makubwa na shughuli zionaongezeaka mno ni shughuli za kati kati katika ya uwepo wa Mungu na uwepo wa dunia hapa ndipo shetani anapokuweka kwa kusudi la kukuingiza katika mtego huu ninaouzungumzia shetani anaogopa sana akuachie mtu kama wewe ukae katika uwepo wa Mungu anajua utampa shida sana angalia mistari ifuatayo:-

Luka 4:1-2 “Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa

Luka 4:14-15 “Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando. Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.”

Katika maandiko hayo hapo juu Yesu alikaa katika uwepo wa Mungu kwa muda wa kutosha alikuwa anafunga na kuomba alishinda majaribu yote makubwa ya ibilisi, na sasa anaingia katika jamii akiwa na NGUVU ZA ROHO nguvu hizi ndio zinazomfanya Yesu anakuwa maarufu kil a mahali habari zake zinaenea kila sehemu na watu wote wanamsifu na kumtukuza, Kukaa katika kuutafuta uwepo wa Mungu ni jambo la muhimu na lenye kumuogopesha sana shetani kuliko jambo lolote lile shetania anajua ni vigumu kumshinda mtu anayekaa katika uwepo wa Mungu lakini ni rahisi sana kumpata mtu kwa kumfanya ashighulike na mambo ya wengine kuliko kushughulika na yeye binafsi

Jambo hili hunitokea na mimi bila kupenda unakuwa busy unakuwa na shughuli nyingi tu zenye kuchosha  nikitafakari wakati mwingine naingia shaka kama yanafanana na kile Mungu ameniitia au nimeingia katika metgo wa ibilisi? Siku moja nikiwa nimechoka majira ya saa tatu usiku nikiwa nimevaa suti niliyoivaa tangu asubuhi, na nikiwa sijachukua mazoezi wala kuoga nikiwa nawasubiri watu fulani ambao nilikuwa na kikao nao tangu asubuhi mpaka saa sita nikaenda kunywa chai ya mchana, kisha wao wakenda mjini na kuniahidi watarejea na hivyo nikawa nawasubiri warejee mpaka ilipofika saa tatu usiku waliniahidi wanakuja nikaendelea kusubiri sikubadilisha nguo sikutaka kuondoa nguo nzito mwilini mwangu nawasubiri watu wa Mungu niwahudumie, nilipompigia simu mmoja akaniambia ndio yuko mezani anakula ameshindwa kurudi kha mimi nilikuwa sijaweza kufanya jambo lolote namshubiri yeye, nilimweleza mke wangu naye akaniambia omba ili kwamba roho ya Masumbufu ikuachie unakuwa busy sana lakini ni ubize ambao ni kama unakutesa wewe, ratiba za kula hazikai vizuri, ratiba za mazoezi huzifuati sawasawa, kukaa na familia na hata muda wako wa kuandaa neno la Mungu kaa sawa alinieleza mke wangu!

Nikaomba na kumuuliza Mungu mbona maswala yasiyo ya muhimu lakini yanayoonekana kama ni ya muhimu sana yananiandama maisha yangu  naona nashughulika nayo kuliko yale niyapendayo kuyatenda? Ndipo Roho Mtakatifu akaniambia “UMEINGIA KATIKA MTEGO WA SHUGHULI NYINGI”

Nilifikiri ninamtumikia Mungu na ninafanya kazi zake sasa nimeingiaje kwenye mtego washughuli nyingi? Nilikuwa najiuliza mbona kazi zimeongezeka sana nyingine njema ni za kazini, na taasisi yetu ni ya kimungu tunamtumikia Mungu sasa nimeingiaje kwenye mtego wa shughuli nyingi? Ni Mungu ndiye aliyeniita nilidhani kuwa wakati huu nimekuwa na shughuli nyingi kwa sababu nimekuwa mtu mzima kwa hiyo majukumu yananipeleka nisikokutaka nilijipa moyo kwa neno la Mungu Yesu alimwambia Petro ulipokuwa kijana ulikwenda kokote ulikotaka wewe utakapokuwa mtu mzima mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikotaka, Yesu alikuwa anaongelea juu ya mauti ya Petro katika Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.” Tafasiri ya Maneno haya ya Yesu ipo katika mstari wa 19 Yesu alitabiri namna Patro atakavyokufa akimtukuza Yesu, Mimi niliutumia mstari wa 18 pekee kukubali tu ukweli kuwa ukiwa kijana unakuwa na uhuru mkubwa wa kujifanyia lolote ulipendalo nafasi inakuwa nyingi mno na  unaweza kwenda kokote utakako ukiisha kuwa mtu mzima na mwenye majukumu shughuli zinakufunga kiasi ambacho huwezi kufanya utakalo, bali majukumu yanakulazimisha uyafanye nilitumia maandiko haya kujipa moyo kuwa huenda ndio mambo yalivyo lakini Roho Mtakatifu alisisitiza tu “UMEINGIA KATIKA MTEGO WA SHUGHULI NYINGI” UMEINGIA KATIKA MTEGO WA SHUGHULI NYINGI?

Sasa niliamua kuwa mpole na kumsikiliza Roho Mtakatifu, lakini pia safari hii nilimsikiliza mke wangu, ni nadra sana kwangu kusikiliza mwanamke narudia tena ni nadra sana kwangu kumsikiliza mwanamke hii niachie mwenyewe labda yatokana na athari zangu za kimaandiko na kimaisha huwa simsikilizi mwanamke  aaa huwa namsikiliza sana lakini kwa vile niko  na shughuli nyingi (busy) na huwa anazungumza habari nyingine za kwenye mitandao ya kujamii huwa nahesabu kama mtu anayeweza kunipotezea Muda lakini safari hii alichoniambia “omba ili kwamba roho ya Masumbufu ikuachie u nakuwa busy sana lakini ni ubize ambao ni kama unakutesa wewe,” akili ilinijia kuwa nachoka sana na kufadhaika sana kwa shughuli nizifanyazo kila siku nikihangaikia watu na taasisi  nimekuwa  na shughuli nyingi kweli kweli busy mno hakuna wakati wakupumzika,  shughuli zenyewe ukizitafakari sio dhambi ila ziko katikati ya shughuli za kimungu ni shughuli za kanisa kabisa lakini hazikupi nafasi ya kuukaribia uwepo wa Mungu hizi ndio zinaitwa Mtego wa shughuli nyingi, Mtego huu ndio Ibilisi anautumia kulikamata kanisa la leo, chunguza kwa undani makanisani kila idara ina shughuli, kanisa lina shughuli wachungaji wanashughuli, kuna shughuli za VIJANA, Kuna shughuli za WAMAMA, kuna shughuli za WABABA, kuna shughuli za UJENZI, kuna shughuli za UINJILISTI, kuna shughuli za Vikao vywa WACHUNGAJI, Kuna shughuli za WAANGALIZI, kuna shughuli za MAASKOFU kuna shughuli za UMOJA WA MAKANISA, kuna shughuli, Kuna mipango kadhaa ya maswala kadhaa, kuna shughuli nyingi mno, siku moja nilifika kwenye kituo Fulani cha Polisi kwenye shughuli nikamuona rafiki yangu mmoja ASKOFU wa kanisa Fulani aliwa pale POLISI mimi nilikwenda kutoa taarifa ya mhasibu wetu alikuwa amechukua fedha nyingi za taasisi yetu zilizotakiwa kwenda TRA na tulipokuwa tunambana azirudishe akawa hato maelezo yaliyonyooka kwa hiyo nilimpeleka POLISI na ilinipasa kufika hapo kuandikisha maelezo sikuwa na nania ya kumfunga lakini nilitaka pesa zirudi tu zilikuwa milioni 16, sikuwahi kufikiri kuwa nitafika Polisi hata siku moja, Nilishangaa kumuona Askofu yuko pale, Nilimuuliza Mchungaji Vipi mbona uko hapa akaniambia kuna Mchungaji wangu yuko Ndani amefungwa nimekuja kumletea chakula tulikaa sana pale kituoni wakati huu somo hili lilikuwa ndio linafunuliwa kwangu upesi nikajisemea Moyoni ni “ULE MTEGO WA SHUGHULI NYINGI” ulimwengu umekuwa wa shughuli nyingi, ninasimamia shule ya Seminary mahali ambapo injili inahubiriwa wanafunzi wetu ni wa kiume tu baadhi ya wanafunzi watatu walijihusisha na dhambi ya USHOGA tukawafukuza, wazazi wao wakapingana nasi vikali, wakitaka vijana wao warudishwe shuleni, Afisa Elimu wilaya na Mkoa pia walisimama na wazazi ili kuwatetea warejee shuleni, Msimamo wetu ni kuwa hatuwezi kuwarudhisha shuleni wanafunzi waliokiuka maswala ya uadilifu kwa kiwango kama hiki, ilikuwa shughuli kubwa sana, vikaoa kadhaa vilikaliwa, vikao vya Kamati ya nidhamu, vikao vya walimu, vikao vya bodi ya shule, vikaoa na wazazi vikao na maafisa Elimu, vikaoa na watu wa usalama wa taifa  ilichukua miezi mitatu kuumaliza mgogoro huo wa kuvutana sisi HAWARUDI maafisa Elimu wanasema WATARUDI lilikuwa jambo la kushangaza viongozi wakubwa wanaotakiwa kusimamia uadilifu katika maswala ya Elimu wakitetea ujinga na uchafu, tena wakisema haifai Mchungaji kuwa mkuu wa shule? Nilikuwa naumia moyoni nilitamani Mungu afanye kitu flani na Mungu alifanya lakini mapambano hayo dhidi ya uovu yalichukua miezi mitatu kumalizika na kumbuka maafisa Elimu wote walikuwa wakristo na wazazi wa watoto walioshiriki uovu ule walikuwa wakristo kwa nini shetani alikuwa akitusumbua hivi dunia imeharibika ibilisi alikuwa anataka tuwe na shughuli nyingi tujiumize na kujichosha kwa jambo rahisi la walioshiriki vitendo viovu kinyume na sheria za shule na imani yetu na neno la Mungu walitakiwa kuondoka mara moja lakini tulitumia miezi mitatu kuvutana shetani alitaka kuleta usumbufu na kutuingiza katika mtego wa shughuli nyingi. Sasa basi ni muhimu kujihoji basi mtego wa shughuli nyingi ni nini?
Maana ya Mtego wa shughuli Nyingi.
Nilijiuliza kwanza huu mtego wa shughuli nyingi ni upi? Katika moja ya mafunzo ya awali sana ya wokovu tulijifunza kuhusu kuwa na shughuli nyingi kunavyozuia ukuaji wa mtu kiroho hasa kupitia mfano wa Mpanzi ambapo zile mbegu zilizoangukia katika miiba humaanisha watu wanaolipokea neno la Mungu, lakini kwa sababu ya kusongwa na shughuli za ulimwengu wanashindwa kukua vizuri na hatimaye kushindwa kuzaa matunda! tujikumbushe maana za mfano ule


Mathayo 13:18-23 “Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.  Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha; lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa. Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai. Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.”


Nilitafakari sana kifungu hiki cha maandiko kwamba je inawezekana kwamba nimegeuka kuwa kundi la wale waliopandwa kwenye miiba? Ambao shughuli za dunia na udanganyifu wa mali hulisonga neno lisikue?au lisizae, sitaki kujihesabia haki sitafuti vitu vya dunia nimeridhika Mungu amenipa kila kitu ambacho mwanadamu wa kawaida anatakiwa kuwa nacho sitaki mambo makubwa kwa hiyo udanganyifu wa mali hauwezi kunisumbua lakini naweza kukiri kuwa shughuli za dunia zimenifunga, shughuli za dunia ni nyingi na sio lazima ziwe dhambi, lakini ni kazi za kawaida lakini hili silo lile ambalo Roho Mtakatifu alimaanisha.


Kwa hiyo nilitafakari kifungu kingine Katika wimbo uliobora 1:6 “Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.“


Kifungu hiki pia sio tatizo kubwa sana huyu ni mtu ameajiriwa na au amefanywa mtumwa maisha yake yamemlazimisha kuwa mtumishi wa wengine kiasi ambacho ameshindwa kutimiza wajibu wa kuangalia mambo muhimu yanayiomuhusu yaani shamba lake mwenyewe la mizabibu, huu sio mtego wqa shughuli nyingi  ni mazingira flani tu ya kuajiriwa na kutokufanya maswala yako mwenyewe, hili halikuwa lile ambalo Roho Mtakatifu alikuwa analikemea kwangu “UMEINGIA KATIKA MTEGO WA SHUGHULI NYINGI”
Kwa hiyo nilitafakari kifungu kingine tena kuhusu siku ile Yesu alipomtembela Martha na Mariamu ona 


Luka 10:38- 42 ”Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake. Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake. Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie. Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi; lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.”


Hichi alichokisema Yesu kwa Martha kilikuwa ni cha Muhimu sana angeweza kuketi kama Mariam na kumsikiliza Yesu ambaye anauwezo hata wa kushusha chakula kutoka mbinguni, Yeye alikuwa akisumbuka kwaajilya kumpikia Yesu hakikuwa tatizo kama Martha  angepika na kuleta chakula  kwa Yesu angekula yeye ni mwanadamu kwa wakati ule angekula lakini tatizo la Martha alinung’unika na kushitaki kuhusu Mariamu Hivyo Yesu alitaka kuonyesha ubora wa Mariamu kwa upande mwingine kumsikiliza Yesu na kukaa minguuni pake ni shughuli muhimu sana, Kuliko alichokuwa anakifanya Martha,  Martha alikuwa  na shughuli nyingi (busy) lakini hili halikuwa tatizo isipokuwa kama tu amenung’unika lakini shughuli yake ilikuwa ni sahihi kimila na kitamaduni kushughulika kwaajili ya Yesu  aliyekuwa mgeni wao haikuwa tatizo kama tutakuwa na shughuli nyingi bila kuwanu;gunikia wengine sio tatizo, mimi ninashughulika kwaajili ya Yesu na sitaki kumlaumu Mtu lakini hili sio lile ambalo Roho Mtakatifi analikemea kwetu Mungu anatuonya na kutukemea kuhusu hili  “UMEINGIA KATIKA MTEGO WA SHUGHULI NYINGI”


Andiko la msingi hasa linasema hivi 1Petro 4:15 “Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au KAMA MTU AJISHUGHULISHAYE NA MAMBO YA WATU WENGINE.


Nitalinukuu andiko hili pia kwa lugha ya kiingereza uweze kuliona vizuri kile kinachomaanishwa hapa 1Peter 4:15 “If you suffer, It should not be as a murderer or thief or any other kind of criminal or EVEN AS A MEDDLER” Neno Meddler – maana yake mwenye kujishughulisha na mambo ya watu katika njia isiyo sahihi, au yenye kuingiliana na shughuli muhimu za kazi, au kujishughulisha ma maswala yasiyopaswa au yasiyotakiwa toleo lingine la kiingereza linatumia neno “Busybody” mtu anayeteseka kwa kujishughulisha na mambo ya wengine yanayoonekana kama mambo yake  au ya Mungu lakini sio ya Mungu KJV inasema hivi  1Peter 4:15But let none of you suffer as a murderer, or as a thief, or as an evildoer, or as a busybody in other men's matters.”



 

Mtu aliyeingia katika mtego wa shughuli nyingi ni mtu anayejishughulisha na maisha ya wengine lakini mtego huu ni mtego wa dhambi isiyokusudiwa, hili ni tatizo kubwa sana unajishughulisha na mambo ambayo sio kazi ya wito wako Mungu aliokuitia na hili pekee ni tatizo tosha na mbaya zaidi mtu mwenye kujishughulisha na mambo ya wengine ana muda mchache au hana muda kabisa wa kushughulikia mambo yake, hawafanyi dhambi lakini wakati wote hufukiri kuhusu wengine hawana muda wa kutubu husaidia wengine kutubu, hawana muda wa kusoma neno husaidia wengine kuelewa neno, hawana Muda kuomba huhamasisha watu kuomba, hawana muda hata wa kula huhudumia watu walioshiba huku yeye akiwa na njaa, hutatua matatizo ya wengine huku yake hakuna anayeyajali kwa ujumla wanapoteza lengo na hawana muda hata wa kujitathimini, wanaweza kunyoosha kidole kwa wengine huku vitatu vikiwarejea wenyewe ikiwa ni ishara ya Mungu Baba Mwana na Roho Mtakatifu wakitusihi kujiangalia wenyewe zaidi kujitathimini na kujilinda na kujihami



 

Huu ni mtego wa Ibilisi anatufanya tupeleke mawazo yetu kwenye kitu vitu ambavyo havitaweza kubadilika ili kwamba tusiweke mawazo yetu katika mabadiliko yetu wenyewe, ni kwaajili ya haya Shetani anataka tuangalie mambo ya wengine ambao ni vigumu kuwabadilisha ili kwamba tusijiangalie wenyewe ambao tunauwezo wa kubadilika kwa haraka kumbuka mtu aliyebadilika yeye mwenyewe ndio mwenye uwezo mkubwa zaidi wa kuwabadilisha wengine, shetani haogopi mtu anayeshughulikia mambo ya wengine bali anaogopeshwa zaidi na mtu anayetumia muda mwingi kwa mabadiliko yake mwenyewe



 

Kwa hiyo utaweza kuona kuwa na shughuli nyingi sio sifa bali ni wazi kuwa ni mtego wa Ibilisi, kukaa kwetu katika uwepo wa Mungu na kubadilika kwetu ndio kwa muhimu zaidi na kunakoweza kubadilisha wengine kuliko shughuli zetu za kushughulika katika kubadilisha mambo!

 



Shetani amefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kulipa kanisa kuwa na shughuli, makanisa mengi  leo yana mipango na shughuli na watumishi wengi wa Mungu leo wanashughulikia mipango na shughuli, vijana wako kwenye mipango na shughuli, wamama wako kwenye mipango na shughuli, wababa wako kwenye mipango na shughuli, waangalizi wa makanisa wako kwenye mipango na shughuli, maaskofu na viongozi wako kwenye mipango na shughuli, Muda mwingi unaotumika ni wa vikao vya mipango na shughuli wajkati mwingine vikao vya mipango na shughuli ndio huwa vinakuwa virefu kuliko hata ibada yenyewe leo washirika wanakwenda katika ibada lakini wakiwa wamejaa mawazo ya mipango na shughuli, penginepo watatakiwa kutoa taarifa ya mipango na shughuli sasa haya nyanapozidi kuliko yale tutakayoyatolea Hesabu atakapokuja mwana wa Adamu ndio yanaitwa mtego wa Ibilisi na mtego huu una madhara yake angalia kisa kifuatacho:-



 

Baba Mtakatifu Gregory the great (Pichani hapo Juu) wakati wa mwisho wa huduma yake ya kichungaji alikuwa akitafakari kuhusu swala zima na kujishughulisha na mambo ya wengine yeye alitumia mfano wa stori ya Dina katika Biblia hakutumia neno Mtego wa shughuli nyingi bali alifananaisha na kile kinachomtokea mtu aliyenaswa na mtego wa shughuli nyingi, alisema kwanza shetani hutoa mawazo yenye ushawishi kwa mtu ili kumuhakikishia ulinzi na usalama wa uongo kwa kusudi la kumbomoa mtu huyo polepole na mfano huu ni sawa na yake yaliyomtokea Dina.
Mwanzo 34:1-3Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, akatoka kuwaona binti za nchi. Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri. Moyo wake ukaambatana na Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana, akasema na huyu msichana kwa maneno mazuri.” 


Dina alitoka kwenda kuwaona mabinti wa nchi, kila mara mtu anapoacha kuifikiri nafsi yake na kuanza kujishughulisha na wengine Shekemu mtawala wa dunia ataiwinda nafsi hiyo na kuibikiri au kuitia unajisi, shetani nwakati wote huitia unajisi nafsi ya mtu inayojishughulisha na mambo ya nje wakati mwingine bila yeye kujua na shetani atazungumza na wewe kwa maneno mazuri, kwa sababu shetani anatufikiri sisi kuwa watu wenye kufaa kwake  shetani wakati wote atatupa tumaini la uongo lakini hatima yake ni kututia unajisi tu, habari ya Dina ni sawa na mtu anayeingizwa taabuni na shetani, Shetani ataendelea kuzungumza vizuri na mtu anayejishughulisha na mambo ya wengine ili aweze kumnasa katika mtego wake (Binti Bikira wakati wote huwakilisha Kanisa, Binti za nchi huwakilisha wana wa dunia hii na Mfalme wao huwakilisha Mungu wa dunia hii yaani Shetani)


Inawezekana tukawa hatufanyi dhambi, lakini tukanaswa katika mtego wa shughuli nyingi, tukionana  na kukutana na watu wa dunia hii wenye dhambi na wakatutia unajisi kwaajili ya kushughulika nao, tunapaswa kulinda nafsi zetu zisiondoke katika ushirika na Mungu, shetani anataka tuwe na shughuli nyingi (busy) na shughuli za dunia tushughulike na wenye dhambi na kujisahau taratibu, anataka atunase duniani taratibu tutapungua katika kusimamia neno la Mungu, tutapungua katika kuomba, tutapungua katika kuhudumu, kuhudhuria ibada, kutenda mema kuona wagonjwa, kuhudumia yatima, kujenga ushirika, kujenga umoja, kukuza familia kuimarisha ndoa, kukuza ndugu kuonyesha kuwajali baba na mama na washirika weengine, tutakuwa na shughuli nyingi kiasi cha kushindwa kusimamia watoto wetu na malezi yao na masomo yao, tutakuwa na shughuli mno mpaka tunachoka na kushindwa kuona umuhimu wa wa kuwa karibu na Mungu, Kumbuka Dunia haibadilishwi na watu wanaobadilisha wengine bali inaweza kubadilishwa na watu waliobadilika wao wenyewe kwanza, “unapojaribu kubadilisha wengine utayeyuka mwenyewe kama sabuni” tunaposhughulika na wengine tunaweza kuingia vilevile katika mtego wa kujilinganisha nao na kuona aaa mimi sio mbaya sana ukilinganisha na hawa na shetani anaweza kutunasa kijanja sana na kuzungumza lugha nzuri na sisi bila sisi kuelewa kuwa tumeingia katika mtego wa shughuli nyingi,


Mtu aliyechoka kwa shughuli nyingi anapoteza uwezo wa kuona mambo ya Msingi ya kiroho, Kutokana na kuchoshwa kwa shughuli nyingi tunapoteza kujitambua kuwa sisi ni nani kwa Mungu, tunaweza kujikuta tunapuuzima mambo ya msingi kwa sababu tu shughuli nyingi zimetuzinga, mtu mwenye utulivu wa nafsi anaweza kuina kwa jicho lingine na kuyapima mambo kwa uzito unaiostahiki kuliko mtu aliyechoka, Shetani anajua nguvu zako na uwezo wako wa kiroho anajua kuwa unatambua mbinu zake zote kwa kiwango kikubwa anajua uzoefu wako hivyo hawezi kukupata tena vilabuni, hawezi kukupata tena kwa zinaa, hawezi kukupata tena kwa majaribu na mateso lakini anajua akikuacha ufanye shughuli nyingi sana utachoka na kwa urahisi sana atakubembeleza wakati umechoka na kukuchukulia kitu chako cha thamani kile ambacho Mungu amekupa ni wakati gani Esau aliuza urithi wake wa Mzaliwa wa Kwanza ni wakati amechoka na uwezo wa kufikiri umepungua 

Mwanzo 25:29-34 “Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana. Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu.Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza. Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi? Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza. Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.”


Jinsi ya kujitoa katika Mtego wa shughuli nyingi!.


Ni lazima tuchukizwe na hali ya kudhalilishwa na kubakwa na na kunajisiwa na ibilisi na kukataa kumuacha azungumze nasi lugha nzuri ya kutupendezesha, Lazima uamke na kujipima na siku za mwanzoni mwa wokovu wako tulipokuwa tunaomba sana na kusoma neno la Mungu sana mambo yalirahisishwa na wala hatukuwa na shughuli nyingi, sasa angalia tuna shughuli nyingi lakini je tunaomba kama zamani je haujihisi kupungukiwa na kitu? Sasa basi tufanye nini lazima tukubali kujipima sawa na neno la Mungu!


Ni lazima tujishughulishe sana katika kuomba ili Mungu atuepushe na mtego wa shughuli nyingi na kuhakikisha kuwa hatukubali kuwa washirika wa shughuli  nyingi na kumpa Ibilisi nafasi, jambo moja la msingi la kukumbuka ni kuwa mtu mwenye shughuli nyingi ni mawindo rahisi sana ya ibilisi, kwa kuwa tunaangalia sana mambo ya wengine kiasi cha kusahau kuangalia mambo yako mwenyewe, ni rahisi kunajisiwa na kuingia katika taabu kwa sababu ya kushughulika na mambo ya wengine, unaweza tu kusahaulishwa na ule mpango wa ibilisi wa kukulinganisha kuwa hata hivyo mimi sio mbaya sana ukilinganisha na wengine, unaweza tu kujifikiri kuwa wewe ni bora sana ukijilinganisha na wengine kumbuka kuwa kiwango cha ubora wetu si watu wengine bali ni Yesu Kristo yeye ndio kielelezo chetu na kiwango cha ubora wetu na ni kupitia neema na rehema tunaweza kufikia kiwango chake tatizo kubwa la watu walioingia katika mtego wa shughuli nyingi ni kuwa wanajishughulisha sana na mambo ya wengine na wanasahau kujihukumu wenyewe kwa msingi huo basi ni muhimu kwanza


1.       1Wakoritho 11:31 “Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa.”  Kila mtu aliyeokoka anapaswa kujipima mwenyewe na kujiangalia mara kwa mara kwamba yuko katika kiwango gani cha kumpenda Mungu na kuacha shughuli nyingi na kujitoa zaidia katika dua na sala na maombi na kulia sana machozi


2.       Tunapaswa kujilinda na kujihami na sifa tunapofanya kazi ya Mungu wakati mwingine watu watatusifu na wenye mahitaji yao wengi watatujia tutajikuta tunawahudumia sana wao na kusahau kuwa nguvu za kuwahudumia hazitokani na nafsi zetu tuuige mfano wa Yesu ambaye mara kadhaa alijitenga na umati wa watu waliokuja kwa nia njema ili awahudumie lakini yeye alikumbuka kwenda kuomba angalia Luka 5:15-16Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao. Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba.” Leo hii wako watu wanafanya huduma na kushinda wakishughulika na watu kuanzia asubuhi mpaka jioni wanasahahu kuwa ni mtego wa shughuli nyingi Yesu alikumbuka mara kwa mara kujiepusha na kwenda kuomba


3.       Kila unapojiandaaa na jukumu kubwa ni muhimu kutanguliza maombi, Dr David Yong Cho wa kanisa la Full Gospel of Yoido kule Korea kusini huomba masaa matatu asubuhi kabla ya kuingia katika shughuli za kila siku, Martin Luther aliomba masaa matatu asubuhi kabla ya kuingia katika shughuli za kila siku Yesu mwana wa Mungu kwa maandalizi ya huduma yake alifunga na kuomba kwa siku 40 Luka 4:1-2, 14-15 “Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.” “Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando. Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.” 


4.       Ni muhimunpia kuwaamini wengine na kugawa majukumu si vema kila kitu ukakifanya wewe, kwa mamlaka uliyonayo unaweza kuwapa majukumu wengine na kuwaelekeza wakafanya kama ambavyo wewe ungefanya  Yesu aliwatuma wale 12 na wakafanya kazi nzuri wakamletea ripoti na akawaagiza wapumzike ona Marko 6:30-32 “Na mitume wakakusanyika mbele ya Yesu; wakampa habari za mambo yote waliyoyafanya, na mambo yote waliyoyafundisha. Akawaambia, Njoni ninyi peke yenu kwa faragha, mahali pasipokuwa na watu, mkapumzike kidogo. Kwa sababu walikuwako watu wengi, wakija, wakienda, hata haikuwapo nafasi ya kula.Wakaenda zao faragha mashuani, mahali pasipokuwa na watu.” Unaona Yesu alitambua kuwa watu wanaofanya hduma wabahitaji muda wa kuwa faragha na kupumzika 


5.       Kunapokuwa na mambo ya kuhuzunisha au habari ngumu pia huna budi kuhakikisha kuwa unajitenga na shughuli nyingi upate nguvu mpya Mathayo 14:1-13 “Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake, Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake. Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye. Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye. Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii. Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode. Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba. Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji. Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe; akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani. Kichwa chake kikaletwa katika kombe, akapewa yule kijana; akakichukua kwa mamaye. Wanafunzi wake wakaenda, wakamchukua yule maiti, wakamzika; kisha wakaenda wakampasha Yesu habari. Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.”


6.       Hatuwezi kufanya maamuzi muhimu huku tukiwa katika shughuli nyingi ni muhimu kukumbuka kuwa kila maamuzi muhimu yanahitaji maombi ili kwamba Mungu aweze kuingilia kati, viongozi nwengi sana wamefanya maamuzi mengi mabaya bila kufikiri wala kuwaza kwa sababu wako kwenye mtego wa shughuli nyingi kisha linawajia jambo linalohitaji maamuzi na wanaamua bila kuwa katika uwepo wa Mungu  Yesu alipotaka kuamua hata kuchagua viongozi aliomba usiku kucha Luka 6:12-13 “Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume;” 


7.       Tunapokuwa na Msongo wa mawazo inatupasa kuomba kwa masaa ya kutosha na hasa tunapotambua kuwa kuna mambio magumu mbeleni yanatukabili Luka 22:39-44 “Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye. Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni. Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]” 


8.       Kumbuka wakati wote Maombi ndiyo yanayotuweka karibu na Mungu, kusoma neno la ke na kulitafakari na kumtii yeye hutupa nguzu za rohoni kwa hiyo ni muhimu sana kwetu kuhakikisha kuwa tunaufurahia uwepo wa Mungu zaidi ya kukubali kuwa na shughuli nyingi Luka 5:16 “Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba."  

         
Kama tutakuwa na shughuli nyingi na Mungu, Mungu ataweka wepesi katika yale tunayoyashughulikia kwa hiyo tusikubali kuingia katika mtego wa shughuli Nyingi

Mchungaji: Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima         

Jumamosi, 25 Aprili 2020

Dhambi ya Ushoga!


Warumi 1:26-29 “Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;  wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.  Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kwamba tunaishi katika Nyakati wa Mwisho sana; Maandiko Matakatifu yanatuonya kwamba katika nyakati hizi za mwisho tunapaswa kuwa na akili na kukesha katika sala, yaani kudumu katika kuomba na tunaonywa kuwa nyakati hizi ni nyakati za hatari, Moja ya matukio Mabaya ambayo yataongezeka katika nyakati hizi za mwisho ni pamoja na kuongezeka kwa uovu na mmomonyoko mkubwa wa kimaadili, zikiwemo dhambi za ushoga au mapenzi ya jinsia moja, Dhambi hizi zilikuweko tokea awali lakini katika nyakati za leo zimeongezeka na kuenea kwa kasi zaidi kuliko kawaida kutokana na kukua kwa teknolojia na kupanuka kwa utandawazi.

 2Timotheo 3:1-4Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;
Katiika nyakati hizi za hatari duniani Moja ya dhambi inayoashiria kuharibika kwa kiwango kikubwa cha mwanadamu ni pamoja na kuongezeka kwa dhambi ya ushoga  na kwa bahati mbaya Dunia imelikalia kimya suala hili, Mataifa viranja wanalifanyia kampeni za makusudi ili swala la mapenzi ya jinsia moja liweze kuenea na kukubalika kwa ulimwengu ili yamkini, lionekane kuwa ni swala la kawaida na wanaolifanya waweze kujisikia kutokuhukumiwa na dhamira zao kwa vile kilio cha wengi ni harusi;  Lakini watumishi wa kweli ya Mungu hawawezi na wala hawataweza kulinyamazia swala hili kwani Bwana ametupaka mafuta tuwaambie watu Njia za bwana zilizonyooka!

Swala la Mapenzi ya jinsia moja liko kinyume na maandiko na utamaduni wa kibinadamu, lakini limeenea limeingia katika kila dini na madhehebu, limekaliwa kimya na baadhi ya watu wameanza kulipitisha kisheria na hata kukubaliana na kuozesha watu wa jinsia moja: Lazima tuseme wazi kuwa hapa Dunia imepotoka mno,Dunia imelewa Dunia imewayawaya kama mlevi, Dunia imepinduka kama machel, Dunia imeoza, hapa hatuwezi kupakalia kimya, wala ahtuwezi kuwapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa ni lazima tujikumbushe msimamo wa Kibiblia kuhusu swala hili. Hii ni dhambi na ni hatari kwa afya na maisha ya mwanadamu, Kiroho, Kimwili, kiakili na kisaikolojia.

Wengine wanadai kuwa wamezaliwa wakiwa namna hii, wanaamini kuwa ni tatizo la kimaumbile, au mvurugiko wa homoni katika miili yao na kuwa swala hili ndio limepelekea wao kuwa na uhitaji wa mapenzi ya jinsi moja, swali kubwa la kujiuliza je kuna ukweli kuwa watu huzaliwa Shoga? Wengi sasa wanadai kuwa wamezaliwa hivyo na ndio maumbile yao na wako tayari kudai haki ya kutambuliwa kama watu wengine katika jamii, Lakini je Neno la Mungu linasema nini juu ya swala hili? Neno la Mungu liko wazi kuwa swala hili ni dhambi na linatokana na tamaa na kutaka kufanya majaribio kunakotokana na mgandamizo wa kufikiriwa kuwa swala hili ni zuri kutoka katika jamii, marafiki, ndugu na kadhalika lakini swala hili sio mpango wa Mungu na ni wazi bila kupaka mafuta kuwa liko kinyume na mapenzi ya Mungu na hakuna utetezi wa kisayansi wala kisaikolojia Neno la Mungu linatutaka tujiepushe na jambo hili tuliangalie neno:-

Msimamo wa Neno Kuhusu Mapenzi ya jinsia moja.

Neno la Mungu ndio mamlaka ya mwisho, na ya juu zaidi ya mwanadamu, Neno la Mungu ndio taa ya miguu yetu, neno la Mungu ndio Muongozo wetu, Neno la Mungu lina maelekezo yote yatupasayo wanadamu namna na jinsi ya kuenenda na ni  Katika neno lake Mungu hufunua mapenzi yake, katika neno lake Mungu hutupa maelekezo sahihi,  na namna ya kuishi na kuenenda Biblia inasema hivi:- tunapozungumzia dhambi ya ushoga au mapenzi ya jinsia moja ni muhimu kwanza tukawa na ufahamu kuhusu misamiati inayotumiwa na dunia kulizungumzia swala hili

·         Homosexuality - the quality or characteristic of being sexually attracted solely to people of one's own sex, Hali yoyote ya kujisikia au kuvutiwa kimapenzi na mtu wa jinsia kama yako au mtu jinsia moja (Ushoga)
·         Bisexuality is -  romantic attraction, sexual attraction, or sexual behavior toward both males and females, or to more than one sex or gender. Hali yoyote ya kujisikia  kuvutiwa kimapenzi na mtu wa jinsia yoyote ya kiume au ya kike (hawani watu wanaochanganya kotekote)

·         Heterosexual - sexually attracted to people of the opposite sex, Hali ya kuvutiwa au kujisikia kufanya mapenzi na mtu wa jinsia tofauti na yako hii ndio ngono ya kawaida.

·         Asexual - (‘ace’ for short) is someone who does not experience, or experiences very little, sexual attraction Hali ya kutokujisikia wala kuvutiwa kufanya ngono  kabisa au kutokuvutiwa kabisa na maswala ya ngono

Katika aina hizo za matumizi ya kingono tutaangalia zaidi aina hizo kubwa mbili za ngono ambazo ziko kinyume na mapenzi ya Mungu na ndizo ambazo tunatumia neno ushoga kuzitaja japo lugha ya kibiblia inakazia mapenzi ya jinsia moja, yaani mwanamke kwa mwanamke au mwanaume kwa mwanaume hii ndio dhambi ambayo Maandiko yanaikemea na kuikataza kwa kiwango kikubwa sana! Tuliangalie sasa neno la Mungu katika swala hili!

Walawi 18:22, 24-25Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote; na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa”.

Unaweza kuona kuwa mojawapo ya sababu ya kufutiliwa mbali kwa mataifa yaliyoimiliki kanaani ni kwasababu ya dhambi za aina hii, Mungu anawaonya Israel kuwa inchi itawatapika watu watendao mambo mfano wa hayo, taifa linalotenda mambo ya jinsi hii au kuruhusu mambo ya jinsi hii linajiweka katika wakati mbaya na mgumu  wa hukumu ya Mungu, Mungu hulifuta au kumfuta mtu awaye yote anayetenda machukizo ya kiwango hiki cha kushiriki mapenzi ya jinsia moja. Mapenzi ya jinsia moja ushoga huitia nchi unajisi na kuiharibu! Ardhi au nchi ikilaaniwa inawatapika watu wake yaani inawakataa inawaua kwa sababu iliumbwa kwaajili ya utukufu wa Mungu, wakati wowote dunia inapo hukumiwa ni lazima tuelewe insababishwa na aina hii ya uovu pamoja na maovu mengine.

Mwanzo 19 inatupa habari za miji ya Sodoma na Gomora namna Mungu alivyoweza kutuma malaika wakaihukumu miji hii kwa moto kutokana na kukithiri kwa aina hii ya dhambi, Watu wa miji ya Sodoma na Gomora waliharibika kiasi cha kutokutamani tena kulala na mwanamke na walitamani sana kufikia ngazi ya kutamani wanaume wapya na wageni waliotembelea nchi yao! Akili zao zilikuwa zinawaza ni mwaume gani hajabikiriwa bado wambikiri, bikira za wanawake kwao hazikuwa tena na maana, wanawake kwao hawakuwa na maana wao walikuwa wanatamani mwanaume mpya wamfundishe mambo ya kisodoma, Mungu alipothibitisha kuwa uovu umefikia kiwango hiki alikusudia kuwaangamiza wote kwa moto na salfa kutoka mbinguni kwa kutumia malaika zake ona:-

Mwanzo 19:1-13Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi. Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha. Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala. Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote. Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua. Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake. Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi. Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu. Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango. Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango. Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango. Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za BWANA; naye BWANA ametupeleka tupaharibu.”

Ni jambo la kusikitisha kuwa Mungu aliwatuma wageni Malaika kule katika Mji wa Sodoma na Gomora, Lutu kama mtu mwenye haki alikuwa mwenyeji wa wageni hao, watu wa mji yaani wenyeji walikuwa wamejawa na tamaa kubwa ya ngono za jinsia moja waliwataka wageni hao ili wafanye nao mapenzi ya jinsia moja lilikuwa ni jambo lenye kushangaza, kwani hata Lutu alipokataa kutoa ushirikiano wa kuwatoa wageni wake walimuahidi kumfanyia yeye kitu mbaya kuliko hao wageni wake, Hali ilikuwa mbaya Malaika waliingilia kati na kumuokoa Lutu  na walieleza kuwa Mungu amewatuma waweze kupaharibu mahali hapo kutokana na uovu wake.

Ni jambo lenye kushangaza sana kwamba ulimwengu wa leo umefikia kiwango cha aina hii cha uharibifu ambao hata wanyama hawajawahi kufikia, Ndoa za jinsia moja ni kielelezo cha juu zaidi cha uharibifu wa Mwanadamu, Ushoga ni uharibifu wa juu zaidi wa uadilifu wa mwanadamu, Leo hii watu wa mataifa yenye nguvu ndio wanaoshawishi dunia ifikie huko kwa madai ya kivuli cha haki za binadamu na haki za mashoga, tunaweza kuheshimu mambo mengine kuhusu haki za binadamu, lakini hatuwezi kukubali kutoa kipaumbele kwa jambo lolote lile ambalo liko kinyume na na Neno la Mungu, swala la Mapenzi ya Jinsia moja Mungu amelikataza na analichukulia kwa uzito mkubwa mno, na pia analishughulikia kwa uzito pale inapobidi, na ameiweka dhambii hii kuwa ni kilele cha uharibifu wa juu zaidi wa mwanadamu.

Warumi 1:26-32Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;  wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;  ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.”

Mungu hangeweza kuweka katazo la aina hii kama angekuwa anakubaliana kuwa kuna watu amewaumba au wamezaliwa na mfumo wa aina hii, kuna uwezekano wa kisayansi wa mtu kuzaliwa akiwa na homoni nyingi za kike au za kiume lakini uko uwezekano wa kutumia dawa zenye kuleta, uwiano wa homoni na kumfanya mtu awe sawasawa,  sio hivyo tu mwanadamu wa asili yoyote ile na wa jinsia yoyote ile anapaswa kuishi kwa kiasi na hivyo ni lazima itambulike wazi kuwa swala la Ushoga ni dhambi kama ilivyo dhambi ya ukahaba kwa vile ni matumizi mabaya ya makusudi ya tendo la Ndoa ambalo Mungu alikusudia lifanyike katika utaratibu uliokusudiwa

Neno la Mungu katika torati lilikataza tabia ya umalaya na tabia ya ushoga, Mungu hakutaka iwe hivyo kwa wayahudi (Israel ) na kwa taifa lolote lile. Aidha kila mzazi na wana jamii wanapaswa kuwafundisha vijana mapema kuwa na ufahamu sahihi kuhusu NGONO “sex orientation” na kuwahimiza kujitambua mapema kuwa wao ni wajinsia gani na wanatakiwa kuishi vipi na kuwa na tabia zipi, Wazee wetu zamani walikuwa na tabia za kukuza sana uanaume na kuupona uanawake kwa sababu za misingi za kujaribu kuwatofautisha au kuwasaidia kujitambua kuwa wao ni nani:- maandiko yanakataza kuweko kwa mashoga au Makhanisi miongoni mwa watu wa Mungu!


Kumbukumbu la Torati 23:17Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.”


Mungu anataka kulilinda tendo la Ndoa lifanyike katika usafi na utaratibu, hawezi Mungu kuachia swala la ngono lifanyike hovyohovyo na ndio maana utaweza kuona kuna makatazo makali sana kuhusu swala hili, shetani anajua namna anavyoweza kuwaangamiza wanadamu kiafya na kiroho na kisaikolojia na ndio maana nyakati za leo Maelfu kwa maelfu ya watu wanavutwa kwa wingi kuingia katika ngono hizi zilizo kinyume na maumbule ya asili,  na zisizo salama  shetani ana wajumbe wake ambao wanaitetea ili iaonekana ni ya kawaida huku watu wote hasa watu wa Mungu wakiwa wamenyamaza kimya, wakati biblia inakataza sio tu kutenda bali hata kukubaliana na wanaotenda hayo ni machukizo kwa Bwana Mungu wetu na jambo hili ni lazima lieleweke wazi hivyo.


Paulo mtume anapowataja watu ambao hawataingia katika ufalme wa Mungu kwa uzito kabisa hajaacha kuwataja watu wanaoshiriki ngono ya jinsia moja au wanaowafanyia wenzao aina hii ya ngono, sio hivyo tu bali onyo limetolewa pia kwa wale wanaowafanyia wake zao kinyume na maumbile, angalia jinsi neno la Mungu lilivyo wazi kuhusu swala hili!


1Wakoritho 6:9-10Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.”


Kumbe basi maandiko katika agano la kale na agano jipya yamerejea kwa wingi kwa kina na kwa upana na urefu katazo la Neno la Mungu kuhusu aina hii ya uovu!


Mapenzi ya jinsia moja ni dhambi

Ni muhimu kufahamu kuwa mapenzi ya jinsia moja kwa mujibu wa maandiko ni dhambi, Mungu yuko kinyume kabisa na mapenzi ya jinsia moja kwa sbabau ni kinyume na mapenzi yake na mpango wake wa uumbaji, Mapenzi ya jinsia moja yanaharibu kabisa Mfumo wa mwanadamu kimwili, kiroho na kiuadilifu lakini pia unaharibu kabisa mpango mzima wa Mungu kuhusu tendo la ndoa ambalo Mungu amelikusudia lifanyika katika utakatifu na utaratibu uliowekwa na Mungu chini ya baraka ya kuizaliana na kuongezeka, Kwa mujibu wa maandiko dhambi ya Ushoga inachukua nafasi ya juu kabisa ya dhambi ambazo ni machukizo kwa Mungu Biblia inakemea kwa ukali zaidi swala hili katika maandiko kadhaa yafuatayo:-


1.       Mambo ya walawi 18:22-24Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko. Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote;
               
2.       Mambo ya walawi 20:13Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.” 
               

3.       Warumi 1:22-32 “Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo. Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao. Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.  Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;  ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.


4.       1Timotheo 1:9-11akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji, na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima; kama vile ilivyonenwa katika Habari Njema ya utukufu wa Mungu ahimidiwaye, niliyowekewa amana.

5.        1Wakoritho 6:9-10Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.  

6.       Wagalatia 5:19-21Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,  ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.’’

               
7.       1Wafalme 14:21-24Naye Rehoboamu mwana wa Sulemani akatawala katika Yuda. Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. Na jina la mamaye aliitwa Naama, Mwamoni. Basi Yuda wakafanya maovu machoni pa Bwana; wakamtia wivu, kwa makosa yao waliyoyakosa, kuliko yote waliyoyafanya baba zao. Maana hao pia wakajijengea mahali pa juu, na nguzo, na maashera, juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi. Na mahanithi walikuwako katika nchi, wakafanya sawasawa na machukizo yote ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli.

8.       Kumbukumbu 22:5Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako.”


9.       Kumbukumbu 23:1 “Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.  Mstari huu katika biblia ya kiingereza NIV unasomeka hivi “ No one who has been emasculated m  by crushing or cutting may enter the assembly of the LORD. Neno EMASCULATED  maana yake katika iingereza linasomeka hivi - Emasculation of a human male is the removal of both the penis and the testicles, the external male sex organs. Depending on the context, this may be seen as consensual body modification, or non-consensual genital mutilation  ni tendo la kuondoa sehemu za kiume za nje  ni mtindo wa kuasi au wa kubadilisha maumbile Transgender na kumfanya mtu aliyekuwa na maumbile ya kiume kuwa ya kike wengine huwaita “SHEMALES” au “LADYBOYS  katika nyakqati hizi za uwepo wa dhambi hii sasa dunia imefikia hatua ya kuwa na majike dume shemales  au ladyboys waliongeza jinsia ya tatu ukiacha mbili alizoziumba Mungu.

10.   Yuda 1:7 “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.” Unaona maandiko yote hayo hapo juu ni makatazo kuhusu dhambi hii ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja, ukaka poa au u dada poa katika maandiko haukubaliki

Kwa nini Biblia iko kinyume na ushoga?

Biblia inaonyesha kuwa ushoga ni dhambi ya kiwango cha juu zaidi kuliko kuabudu miungu, ulevi na anasa, kutokumcha Mungu na kadhalika Biblia inaonyesha wazi kuwa Walawiti na wafiraji hawataurithi ufalme wa Mungu, Dhambi ni dhambi lakini inapofikia wanadamu wakaanza kufanya dhambi hii ambayo maandiko huiita machukizo Maana yake ni kwamba mwanadamu ameharibika kwa kiwango cha ngazi ya juu mno, inapofikia ngazi yoyote maandiko yakakuonyesha kuwa watu wameharibika lazima neno la Mungu litagusia kuwepo kwa dhambi ya ulawiti na ufiraji unapoona hili limetajwa mahali maana yake ni kuwa mwandishi anataka kukuonyesha kiwango cha juu zaidi cha uharibifu, kwa nini neno la Mungu linatuonye dhidi ya kushiriki mapenzi haya ya jinsia moja?;-

1.       Ufiraji na ulawiti au usagaji na ushoga unaashiria kiwango cha juu zaidi cha uharibifu wa mwanadamu.
Nyakati za kitabu cha waamuzi zinaitwa nyakati za giza katika israel kwa sababu Israel wakikuwa hawana wafaklme wala viongozi wenye nguvu ya kuwaongoza kama ilivyokuwa Musa na Yoshua hivyo watu walijifanyia mambo yoyote waliyoyaona kuwa mema machoni pao katika mlango wa 19 wa kitabu hiki mwandishi anaonyesha kuwa Pamoja na Mungu kuwainulia waamuzi wana wa israel lakini uovu katika israel ulikuwa umefikiwa kiwango cha juu sana cha uharibifu na stori hii inaonyesha wakati wote wanadamu wanapofikia kiwango cha juu cha uharibifu utaweza kuina dhambi za kiwango cha juu na uharibifu mkubwa wa uvunjifu wa maadili ukijitokeza ona mfano huo katika mstari wa 16-30
Waamuzi 19:16-30 “Kisha, tazama, akatokea mtu mume mzee, atoka kazini kwake shambani, wakati wa jioni; mtu huyo alikuwa ni wa ile nchi ya vilima vilima ya Efraimu, naye alikuwa anakaa katika Gibea hali ya ugeni lakini wenyeji wa mahali hapo walikuwa Wabenyamini. Naye alipovua macho yake, akamwona huyo mtu msafiri katika njia kuu ya mji; huyo mzee akamwuliza, Waenda wapi wewe? Nawe watoka wapi? Akamwambia, Sisi twapita hapa kutoka Bethlehemu-yuda, twaenda huko upande wa mbali wa nchi ya vilima vilima ya Efraimu; ndiko nilikotoka nami nilikwenda Bethlehemu-yuda; nami sasa naiendea nyumba ya Bwana wala hapana mtu anikaribishaye nyumbani mwake. Walakini nyasi tunazo, na chakula cha hawa punda zetu; mkate pia tunao na divai kwa mimi na huyu kijakazi wako, na kwa huyu kijana aliye pamoja nasi watumishi wako; hapana uhitaji wa kitu cho chote. Kisha huyo mzee alisema, Na iwe amani kwako; lakini na haya yaliyokupungukia na yawe juu yangu mimi lakini usilale njiani.  Basi akamtia ndani ya nyumba yake, akawapa punda chakula; nao wakaosha miguu, wakala na kunywa. Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu mabaradhuli wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua. Naye mtu mwenye nyumba akawatokea hapo nje, na kuwaambia, La, sivyo, ndugu zangu nawasihi msifanye uovu jinsi hii; kwa kuwa mtu huyu ameingia ndani ya nyumba yangu, msifanye upumbavu huu. Tazama, binti yangu yupo hapa, ni mwanamwali, na suria wake huyo mtu; nitawaleta hapa nje sasa nanyi watwezeni, na kuwatenda hayo myaonayo kuwa ni mema; lakini mtu huyu msimtende jambo la upumbavu namna hii. Lakini hao watu hawakukubali kumsikia; basi mtu huyo akamshika suria wake, na kumleta nje kwao; nao wakamjua, na kumtenda uovu usiku kucha hata asubuhi kisha kulipoanza kupambauka wakamwacha aende zake. Ndipo huyo mwanamke akaja alfajiri, akaanguka chini mlangoni pa nyumba ya mtu yule alimokuwamo bwana wake, hata kulipokucha. Bwana wake akaondoka asubuhi, akaifungua milango ya nyumba, akatoka nje ili aende zake, na tazama, huyo mwanamke suria yake alikuwa ameanguka pale mlangoni pa nyumba, na mikono yake ilikuwa i pale kizingitini. Akamwambia, Haya ondoka, twende zetu; lakini hakuna aliyemjibu; ndipo akamwinua akamweka juu ya punda; mtu huyo akaondoka, akaenda mahali pake mwenyewe. Naye alipokwisha kuingia nyumbani mwake, akatwaa kisu, kisha akamshika huyo suria yake, akampasua kiungo kwa kiungo, vipande kumi na viwili akampeleka katika mipaka yote ya Israeli. Basi ikawa, wote walioliona jambo hilo wakasema, Jambo kama hili halijatendeka wala kuonekana tangu siku hiyo wana wa Israeli walipokwea kutoka katika nchi ya Misri hata leo; haya, lifikirini, fanyeni shauri, mkanene.”      
          

2.       Ushoga uko kinyume na tendo la ndoa


Tendo la ndoa lilianzishwa na Mungu kwa makusudi ya ustawi wa jamii duniani ili wanadamu wazaliane na kuongezeka Mathayo 19:4-6 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.” Yeye aliyewaumba mwanzo aliwaumba mtu mume na mtu mke unaona hii ni wazi kuwa tendo la ndoa lilikusudiwa na Mungu kuwa tendo la kipekee litakalohushisha wanandoa na sio vinginevyo Biblia inakataza hata zinaa na uasherati, matendo haya yakifanyika hivyo na bila ya utaratibu yanaweza kusababisha watu walee watoto wasio wao kwa asili, ndio maana Mungu aliweka utaratibu tamaa inayokusudiwa kibiblia ni tamaa ya mtu kuwa na mkewe na mumewe na wameamuriwa kupeana bila amri ona 1Wakoritho 7:2-5 “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.  Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.  Kimsingi unaweza kuona mkazo wa kibiblia kuhusu ndoa na umuhimu wake na jinsia imewekwa wazi kuwa tendo linalopaswa kufanyika kwa mume na mke au mke na mume na sio vinginevyo, Jambo hili hata kwa asili utaweza kuona viumbe vyote vinakubaliana na agizo hili la kimungu 


3.       Ushoga uko kinyume na baraka za Ndoa. 


Mwanzo 1:27-28 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.Mungu alipomuumba mtu mke na mtu mume aliwabariki akitaka wakazaliane na kuongezeka watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja yaani wanawake kwa wanawake na wanaume kwa wanaume hawawezi kutimiza kusudi hili la kimungu na hivyo wanafanya machukizo makubwa hawawezi kuiongeza dunia na kwa matendo yao wanafanya machukizo na swala ambalo liko kinyume na mapenzi ya Mungu tendo la ushoga kwa uwazi linaashiria mwisho wa dunia kwa sababu wiote wanaotenda haya watakufa bila kuacha uzao duniani.


4.       Mashoga hawawezi kuwa na ndoa halali. 


Mungu aliikusudia Ndoa kuwa jambo lenye kuheshimika sana Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.” Ndoa inayoweza kuheshimiwa kwa mujibu wa maandiko ni ndoa ya mke na mume ni ndoa ya watu wa jinsia zisizofanana, wakati biblia ikiagiza kuheshimika kwa ndoa ya aina hii ni muhimu kukumbuka kuwa Biblia haijawahi kutaka mwaname kulala na mwanaume mwenzake kama kulala na mwanamke swala hili ni machukizo na haliwezi kuwa la kuheshimika Mambo ya walawi 18:22-24Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko. Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote;” 


5.       Ndoa ya mashoga haiwezi kumwakilisha Kristo. 


Ndoa zimekusudiwa kuwa kielelezo cha uhusiano ulioko kati ya Kristo na Kanisa ona katika Waefeso 5:23-25 “Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;Katika kielelezo hiki ndoa na uhusiano wake inafananishwa na uhusiano ulioko kati ya Yesu na kanisa , ni wazi kuwa tabia za ushiga na ndoa ya jinsia moja ni uasi na kufuru kubwa kinyume na kielelezo hiki, ushoga unamkana Mungu, ushoga naharibu na kuvunjilia mbali kweli ya Mungu na haiwezi kupakwa mafuta kwa jinsi yoyote ile. 


6.       Ushoga unaashiriki kiwango cha juu kabisa cha matatizo ya akili. 


Utafiti wa kisayansi umebaini kuwa katika viwango vya juu kabisa vya matatizo ya kisaikolojia yaani matatizo ya akili ambayo ni pamoja na msongo wa mawazo, matumizi ya madawa ya kulevya, kujiua na usagaji na ushoga  ni mojawapo ya alama za kiwango cha juu zaidi cha matatizo ya akili aidha kukubaliana na maswala ya ushoga duniani kuwa ni jambo la kawaida pia ni ishara ya kuhari9bika kwa akili za mwanadamu ushoga ni haribiko la juu zaidi ambalo ni gumu kulirekebisha na hivyo dawa yake ni kuharibu kabisa au kuwaacha watu hao waangamie katika hasira za Mungu Biblia inakubaliana na na tafiti hizi za kisayansi  Warumi 1:22-32Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo. Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina. Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.” Unaona Biblia haielezi tu wale wanaoshiriki uchafu bali hata wanaokubaliana na uchafu huo nao ni wenye matatizo makubwqa sana Mungu anachukizwa na jambo hili kwa kuwa linaharibu kabisa akili ya mwanadamu na kumfanya asiwe na akili, unakuta mwanaume kwa sababu ya kuathiriwa na tabia za kishoga anavaa Heleni, analegeza suruali, anavaa chupi za kike anajichubua, anapaka wanja, anapaka lipstiki, anakunywa soda za kike kama mirinda au fanta, anajisikia kama ana mimba, kama anaweza kuzaa akama anataka kunyonyesha, ana joto anahisikia kuingiliwa marafiki zake ni wanawake, analegeza vidole, kila wanachokifanya wanakifanya kama wanawake hili ni haribiko la akili na saikolojia mlinalotokana na mtu kuharibika na kuvurugwa! 


7.       Ushoga ni kubadili matumizi ya asili 


Kwa asili Mungu aliuumba unyeo “Anus” kwaajili ya kutolea kinyesi na sio kwaajili ya kuingiliwa, njia ya haja kubwa rectum ni tofauti kubwa kimaumbile na uke vigina na hazifanani vigina umeandaliwa tayari kwa kuingiliwa na uume lakini sio ilivyo kwa upande wa pili, uke una maji maji maalumu yanayoangaa kuingiliwa na uume lakini sivyo ilivyo kwa utumbo mkubwa , uke una misuli maalumu ya asili unayoweza kustahimili lakini sivyo milivyo kwa unyeo, uke unauwezo wa kustahimili msuguano wowote lakini sivyo ilivyo kwa unyeo, Unyeo umeumbwa na misuli midogomidogo na maalumu kwaajili ya utoaji wa kinyesi nje na sio kupokea kitu kutoka nje na kama kutafanyiwa tendo hilo baada ya muda Fulani misuli yake italegea na kushindwa kustahimili kuuzia kinyesi, aidha uwezekano mkubwa wa kusababisha michubuko utakuwepo na kuruhusu magonjwa mabaya ya kuambukiza ikiwemo UTI kwa sababu hili sio tukio la asili na biblia inalitamka hivyo Warumi 1:26-27Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.” 


8.       Ushoga unaharibu nafsi. 


Nasfi ya mwanadamu ina nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kiroho, vita vyote vya kiroho hufanyika katika nafsi nasfi ikishindwa anguko la kiroho hutokea na nafsi ikishinda ushindi mkubwa wa kiroho hutokea  na ndio maana maandiko yanatutaka tulinde moyo wetu yaani nasfi zetu kwani huko ndiko ziliko chemichemi za uzima  Mithali 4:23. “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.”  Ni muhimu kufahamu kuwa neno Moyo au mwili katika Biblia ya Kiibrania hutajwa kwa kutumia neno “NEPHESH” neno hili maana yake ni  “NAFSI, AU AKILI AU NIA” Maandiko yanajua umuhimu wa nia au nafsi au akili akilia au nafsi au nia ikishikwa na kitu kingine au ikitekwa inakubali kuwa mateka kule ilikotekwa Neno la Mungu linatuagiza tuijaze akili yetu neno la Kristo ona  Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.” Kwa nini maandiko yanatutaka neno la Kristo likae kwa wingi ndni yetu maana yake tuijaze mioyo yetu au nafsi zetu na akili zetu kwa neno la Mungu, Ni neno la Mungu na utii kwa neno la Mungu linaloweza kutugeuza nia zetu na kutufanya kwa upya Warumi 12:2 “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” Unaweza kuona jinsi neno na Mungu linavyotoa kipaumbele katika kujaa neno lake na kuzielekeza nasfi zetu kumtukuza na kumuhimidi Bwana Mungu wetu! Daudi alijiambia nafsi yake na kuiimbisha zaburi ili imhimidi bwana ona Zaburi 103:1-5 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Naam, vyote vilivyo ndani yangu Vilihimidi jina lake takatifu. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote. Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;” kwa hiyo nasfi ni moja ya sehemu muhimu sana, akili na nia ni moja ya sehemu muhimu sana kwa mustakabali wa maisha yetu, sasa basi Mapenzi nayo yana tabia ya kushika nafsi na kuiharibu, zinaa ina tabia ya kushiika nasfi na kuiharibu uasherati nao una tabia ya kushika nasfina kuiharibu lakini kwa bahati mbaya dhambi ya ushoga, ulawiti na ufiraji zina uwezo wa kiwango ca juu cha uharibifu na kuweza kuishika nafsi na kuiharibu na ndio maana Mungu katika hekima yake anajua kuwa watu wakifikia kiwango hicho cha tabia chafu ni vigumu sana kuacha mwenendo wa aina hiyo kwani unakamata sana nafsi na kuiteka kabisa kwa hiyo watu wa aina hiyo wanastahili hukumu Warumi 1:26-27 “Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, WAKAPATA NAFSINI MWAO malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.” 


9.       Ushoga unaharibu mwili. 


Watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja wanajitahidi sana duniani kulifanya tendo hili lionekane kama tendo la kawaida na lisilo na madhara yoyote, lakini ukweli unabaki wazi kuwa swala hili lina madhara makubwa sana katika mwili wa mwanadamu, Mungu aliuumba mwili wa mwanadamu kwa heshima kubwa sana  kwa matumizi ya utukufu wa Mungu, Mwili umeumbwa kwaajili ya Mungu na sio kwaajili ya zinaa


1Wakoritho 6:12-13 “Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote. Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili.” Watu wa Mungu na dunia nzima inapaswa kuelewa kuwa tukiitoa miili yetu kwaajili ya zinaa ni dhambi maana Mungu aliuumba mwili kwa utukufu wake na hivyo ni mbaya zaidi tukiinajisi miili yatu kwa kufanya ngono ya jinsia moja , ushoga na usagani una madahara makubwa sana katika maisha ya mwanadamu na unaharibu kwa kiwango kikubwa mfumo wa utendaji wa mwili na maumbile Mungu atatuadhibu kwa kuharibu miili yetu 1Wakoritho 6:18-20 18. “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.” Ni jambo la kusikitisha kuwa kwa dhambi ya ushoga ni vigumu kumtukuza Mungu, kama wanadamu wataruhusu tamaa ya ushoga kuchukua nafasi na kuitawala dunia ni lazima ieleweke wazi kuwa tutaharibu kabisa jamii ya aina buinadamu duniani
Ushoga hasa ulawiti na ufiraji ni moja ya sababu kuwa sana ya magonjwa ya zinaa au ngono magonjwa ya zinaa au ngono ni pamoja na :- 

·         Kisonono (Gonorrhea) ni mojawapo ya magonjwa najisi ya ngono,Mtu anapokuwana kisonono nyakati za biblia alitengwa kusudi asiwaambikize wengine lakini ni ugonjwa ambao mtu aliweza kupona (Walawi 15;1-15) 

·         Clamidia Huu dalili zake haziko wazi lakini zina usaha mweupe unao natanata uumeni au ukeni. 

·         Chankroid sijapata jina zuri la Kiswahili lakini ugonjwa huu wa zinaa mtu huwa na vidonda sehemu za siri na maumivu makali hususani wakati wa kujisaidia,kuvimba tezi sehemu za siri na wakati mwingine kupasuka na kutoa usaha  na kuwa na utando mweupe mdomoni. 

·         Ukimwi/HIV – Ukosefu wa kinga ya mwili ni moja ya magonjwa ya zinaa lakini kwa njia iliyowazi mtu anaweza kuambukizwa kirahisi zaidi kama ataingia kwenye mapenzi ya jinsia moja hususani ya wanaume kwa wanaume, na tabia za ushoga

·         Kubadilika kwa maumbile – kutokana na tendo la kumwagiwa shahawa kwenye utumbo mkubwa shahawa hizo hufanyiwa digestion yaani husagwa tena kama chakula na kurejeswa mwilini japo nyingine zinaweza kumwagika kitendo hiki hupelekea, Mabadiliko ya mwili wa mwanaume kuwa kama mwanamke, aidha kutokana na kuwepo kwa chemikali ya Lactic acid ambayo katika mbegu za kiume ina milgram 2.11 kati ya mils 3 za mbegu za kiume acid hii ina nbakteria wanaotumika kuchachusha kitu kwa hiyo bakteria hao huchahusha na kujijenga katika eneo la utumbo mkubwa na hivyo kusababisha miwasho itakayopelekea mfirwaji kujisikia kuingiliwa tena na tena , aidha kutokana na michubuo ya uume kuingia sehemu ya haja kubwa kunasababisha kutokea kwa uvimbe mdogo mdogo wenye usumbufu, muwasho usiokuwa wa kawaida, kulegea kwa njia ya haja kubwa, kuharibika kwa uwezo wa utumbo mkubwa kuzuia choo, kuharibika kwa mfumo wa nguvu za kiume ambazo kwa kwaida zinategemea sana uimara wa mishipa ya nyuma, kulegea kwa maumbile na maumbile kuanza kuwa ya kike, na mabadiliko ya sauti ambayo huanza kuwa nyembamba na mabadiliko ya homoni na maumbile ya kisaikolojia na kumfanya mtu aliyeingiliwa kuanza kuwa kama mwanamke, kujificha kisaikolojia na kuanza kutunisha misuli ili kujazia ili mtu aonekane kuwa ni mwanaume kweli, kushituka kihisia kunakotokana na kujikausha ili watu wasijue kuwa unaingiliwa hivyo ubongo huwa unakandamiza hisia kwa kusudi la kujikausha ili usijulikane kuwa unafanya jambo hilo na hivyo ikitokea ukijambishwa unaathirika kiakili! Na kushituka sana kwa kufikiri kuwa aliyekujambisha amejua kuwa wewe ni shoga. Kwa ujumla  ya kishoga ni mabaya  Matukio haya yote husababishwa na hali hii ya kumkataa Mungu na kukataa kutawaliwa na Mungu na hivyo kuutia mwili uchafu yaani unajisi Mungu atahukumu mageuzi ya aina hii yanayofanywa na wanadamu dhidi ya uumbaji wake Yuda 1:5-8 “Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini. Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu. Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu. 
            
·         Kwa kawaida kitaalamu Mbegu za kiume shahawa kwa mujibu wa lugha ya kitaalamu zinaitwa Spermatozoa kwa kifupi Sparm zinabeba viluwiluwi vinavyotarajiwa kuwa binadamu kati ya milioni 200- milioni 500 kwatika ujazo mmoja wa shahawa zenye ujazo wa milgram 5 na ndani yake kuna Lactic acid, vulume ya mils 2;11, magnesium 0.374. Potassium 3.71 na Protein 0.171

10.   Mashoga hawana sifa ya kumtumikia Mungu.

Nyakati za Biblia kulikuwa na sifa maalumu za watu waliotakiwa kumtumikia Mungu, katika sifa hizo za kimwili na kiroho Mungu hakuwahi kuruhusu Mashoga wawe watumishi wake na sio tu kumtumikia yeye bali hata kusogelea mkutano wa watu wa Mungu  ona Kumbukumbu 23:1 “Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.  Mtu ambaye amehasiwa asiye na uume au ambaye uume umelegea au hasimamishai hakupaswa kuingia katiia mikutano wa watu wa Mungu na sio hivyo tu hakupaswa kumtumikia Mungu ona Mambo ya Walawi 21:17-21 “Nena na Haruni, umwambie, Mtu awaye yote wa kizazi chako wewe katika vizazi vyao, aliye na kilema, asikaribie kusongeza chakula cha Mungu wake. Kwa kuwa mtu awaye yote aliye na kilema hatakaribia; mtu kipofu, au kiwete, au mtu aliye na pua iliyoharibika, au aliye na kitu kilichozidi vimpasavyo mwili, au mtu aliyevunjika mguu, au aliyevunjika mkono, au aliye na kijongo, au aliye kibeti, au aliye na kilema cha jichoni, au aliye na upele, au mwenye buba, au aliyevunjika mapumbu; mtu awaye yote wa kizazi cha Haruni kuhani aliye na kilema asikaribie kuzisongeza sadaka za BWANA kwa njia ya moto; ana kilema huyo asikaribie kusongeza chakula cha Mungu wake.” Mungu hakukubali walemavu wamtumikie Mungu, lakini zaidi pia alikazia kuwa hata mtu aliyevunjika mapumbu yaani mwauame khanithi ambaye anaingiliwa kama mwanamke huyu hapaswi kabisa kumtumikia Mungu, Katika agano jipya utaweza kuona sifa za mtu anayetakiwa kumtumikia Mungu zinatajwa kwamba ni lazima awe mwanaume au mume wa mke mmoja 1Timotheo 3:2 “Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, MUME WA MKE MMOJA, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;Unaona mkazo huo Mume wa mke mmoja unamaana ni lazima awe mwanaume rijali, mwanaume mwenye kujihusisha na ushoga hawezi kuwa mwenye kufaa katika kumtumikia Mungu.


Sababu zinazopelekea kuweko kwa mapenzi ya jinsia moja duniani


Ushoga ni hali ya kuvutiwa kimapenzi kwa mtu watu wa jinsia inayofanana, ni mtindo wa maisha ya kimapenzi wa kati ya watu wa jinsia moja yaani mwanaume kwa mwanaume au mwanamke kwa mwanamke, hii ni hali inayowatokea watu kihisia, na kimvuto na kitamaa kwa watu wa jinsia moja inaweza pia kuelezewa kama mtazamo wa mtu wa kimapenzi au tabia ya mtu au watu fulani katika jamii ambao wanavutiwa kushirikiana kimapenzi na watu wa jinsia kama yao, Biblia imepiga marufuku aina hii ya tamaa au mvuto au hisia au hata kujihusisha na mapenzi ya jinsi hii, lakini hakuna anayeeleza kuwa ni sababu gani zinapelekea jambo hili kujitokeza au kuwepo, hata wanasayansi wanapata taabu sana na bado hawajagundua sababu za moja kwa moja zenye uhakika zinazopelekea kuwepo kwa aina hii ya mapenzi miongoni mwa jamii ya aina buinadamu.

Wataalamu wa utafiti wa swala la kwanini watu wanajihusisha na mapenzi ya jinsi moja wanasema kuna dhana kubwa mbili zinazotolewa na watafiti wa swala hili

1.       Kuna wanaosema kuwa swala hili watu huzaliwa nalo

2.       Kuna wanaodai kuwa swala hili ni tatizo la kisaikolojia na kimazingira

Kuhusu swala la kuzaliwa na hali hii  wataalamu wa uchunguzi wa mfumo wa ubongo wakishirikiana na Simon Leyay, mtaalamu wa mapacha J Michael Bailey na Richard c Pillard na mtaalamu wa geneology dean H Hamer wamesema katika utafiti waoa kuwa hakuna mtu anazaliwa shoga, hivyo dhana pekee inayobaki kuwa inaweza kuwa sababu ya ushoga ni swala la kisaikolojia na kimazingira, kwa msingi huo neno la Mungu lisingeweza kuwa kali kwa jambo ambalo liko nje ya uwezo wa kibinadamu au ka ma wanadamu wangekuwa wanazaliwa na ushoga kwa msingi huo uko uwezekano wa mtu kuchagua kuwa awe ni mtu wa namna gani. Sababu za kimazingira zinazoweza kupelekea mtu kuwa shoga ni kama ifuatavyo:-

Hapa ziko sababu ambazo zinaweza kukubalika kisaikolojia kusaidia kujua kwa nini watu hujihusisha na mapenzi ya jinsi moja:-

a.       Sababu za Msongo wa mawazo depression mawazo yanayosababisha mtu kuwa jna huzuni na kuanza kuona hana uthamani kwa jamii yake rafiki zake na watu wa jinsia yake,
b.      Urithi wa vichocheo vingi homons kutoka kwa mama na malezi ya kudekezwa, hii huchangiwa kuanzia mimba hasa mzazi anapotarajia mtoto wa kike zaidi
c.       Kunyanyaswa “bulled” kwa Maneno au vitendo tangu utoto wako
d.      Msukumo wa kukataa au kutaka kubadilisha jinsia yako
e.      Kujilinganisha na wengine kimaumbile
f.        Kuogopa kukataliwa na kutengwa au kuwa npeke yako
g.       Kukusa msaaada wa kujielewa
h.      Kulelewa katika sheria kali sana zinazokukataza kuchangaana na sex tofauti
i.         Vifungo vya muda mrefu
j.        Kuangalia picha na mikanda ya ngono
k.       Kuwa na makundi mabaya na marafiki wabaya
l.         Kukosa mafundisho sahihi ya neno la Mungu tyangu utoto
m.    Mashambulizi ya ibilisi kwa watu wenye akili na vipawa ili akuharibu mapema
Jinsi ya kuishinda dhambi ya ushoga!
1.       Amini kuwa Mungu anasamehe
Kwa kawaida kwa vile dhambi ya ushoga ni ya ngazi ya juu sana na maandiko pamoja na jamii wanaipinga sana wengi wanadhani kuwa dhambi hii ni sawa na kumkufuru Roho Mtakatifu na hivyo haisameheki, Biblia inaonyesha nwazi kuwa Mungu anauwezo wa kusamehe dhambi hii na kuwabadilisha wale wanaomjia kwa imani ona 1Wakoritho 6:9-11 Biblia inasema hiviAu hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu”.  Kama watu walioshiriki mapenzi ya jinsia moja yaani usagaji na ushoga wakimuamini Yesu na kutubu na kuacha njia zao mbaya kwa imani wanweza kabisa kubadilishwa mstari wa 11 katika kifungu hicho ni wa muhimu wakati huu kwa sababu unaeleza hivi “Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu”. Kwamba kule Koritho Mungu aliokoa watu wa aina zote wakiwemo watu waliofanya ulawiti na ufiraji, kwa msingi huo hatuwezi kuizuia neema ya Mungu inayookoa watu wote, lakini hata hivyo tunaweza kuona ugumu mkubwa sana na madhara makubwa sana yanayotokana na mtu kujiingiza katika dhambi hii labda tukinena kiwazimu afadhali dhambi nyingine, Lakini hata hivyo hatuwezi kumuwekea Mungu mipaka kwani mwaliko wa Mungu kwa msamaha unaonyesha kuwa anasamehe dhambi ya kiwango chpchote kile ona Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.” Andiko hili lamaanisha kuwa Mungu yuko tayari kusamehe dhambi bila kujalia dhambi hiyo ilikuwa mbaya kiasi gani mara mtu anapotubu na kukiri mbele za Mungu, Mungu husamehe hii ndio tabia yake yeye ni mwaminifu katika kusamehe 1Yohana 1;9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.Unaweza kuona ni wazi kuwa neno la Mungu linafungua mlango kwa kila mtu kama tukiziungama dhambi zetu bwana ni mwenye rehema anasamehe  na kuosha kabisa na kukufanya upya hasa kama utaendelea kuitegemea neema yake na kukaa kwa imani kila kitu kitakuwa kipya 2Wakoritho 5:17-21 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.” Ndani ya Kristo ya kale yanapita na kila kitu kinakuwa kipya Mungu anauwezo wa kusamehe na uwezo wa kubadilisha na anauwezo wa kuweka dhambi zako mbali nawe kabisa Zaburi 103:10-13 “Hakututenda sawasawa na hatia zetu, Wala hakutulipa kwa kadiri ya maovu yetu. Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao.  Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.
2.       Kubali kugeuzwa nia yako!
Warumi 12:1-2 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” Mapambano makubwa na vita kubwa ya mwanadamu hupiganwa katika nia yaani katika akili kwa msingi huo ni muhimu kumuomba Mungu aihuishe nia yako na kuifanya upya roho iliyotulia ndani yako ili kwamba usimtende Mungu dhambi Zaburi 51:9-10 “Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote. Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yanguKila mtu aliyeokolewa alikuwa na dhambi zake ambazo alipokuwa duniani zilikuwa zinamtesa au kumtawala na kumtumikisha ni muhimu kufahamu kuwa tunapokuwa tumeokolewa dhambi zileziole tulizokuwa tukiziednea zamani ndio zitakuwa mtego mkubwa wa adui kuzitumia kututega tena ili turejee dhambini kwa hiyo nia zetu zinapogeuzwa na sisi kukubali kugeuzwa nia zetu tunaifungia dhambi mlango wa kutupata tena na ndio maana ni muhimu sana kumuomba Mungu  atufanyie upya nia zetu na zaidi sana atulinde na tujilinde na ile dhambi ituzingayo kwa haraka yaani ile dhambi tuliifanya sana kabla ya kukutana na Yesu hiyo katika maandiko huitwa dhambi ituzingayo kwa haraka Waebrania 12:1-3”Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu  Mtu aliyetoka katika ushoga dhambi imzingayo kwa upesi ni ya ushoga na anapaswa kujilinda nao.

3.       Jiingize katika kuomba sana .

Maombi ni silaha yenye nguvu kubwa sana hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaomba na kujisomea neno la Mungu, na kumuabudu Mungu jambo hili litatutengenezea mfumo mpya wa tabia na hofu ya Mungu ndani yetu jambo hili litabadilisha kabisa maisha yetu, Katika kumuomba Mungu lazima tumuombe Mungu atuchunguze mioyo yetu ili kuondoa njia zenye kuleta majuto Zaburi 139:23-24 “Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.” Mungu anauwezo wa kubadili mitazamo ya mioyo yetu na kuondoa kabisa mambo yanayotuudhi na hatimaye atatupa amani na nguvu ya kutusaidia kushinda kila aina ya tamaa mbaya Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.Tegemea nuwezo wa Mungu na nguvu zake, usijitumainie mwenyewe  wewe huwezi  kujibadili tabia kwa nguvu zako jiachilie katika neema ya Mungu madamu tu moyoni unachukizwa na jambo hilo kutoka moyoni 2Wakoritho 4:7 . “Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.”

4.       Hakikisha unaujaza moyo wako kwa mawazo yenye kujenga .

Achana na marafiki wabaya wahubiri wa ushoga wana maneno mazuri sana yenye kuvutia kuelezea jambo hili kana kwamba ni jambo jema sana  watakuingizia kwenye akili yako kuwa nhili swala ni jema wakati ni swala baya katika njia za Mungu1Wakoritho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema” Biblia ya kiingereza inaita “bad company” hakikisha kuwa unaepuka kila aina ya mazungumzo au unavunja urafiki na watu wabaya wanaozungumzia maswala ya ushoga, badala yake ijaze akili yako kwa neno la Mungu Zaburi 119:9-11 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.  Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambihakikisha kuwa unajisomea neno la Mungu na kulitii yaani kufuata masharti yake, na wakati wote kutafakari na kujadili au kutafakari mambo yaliyo mema Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.” Ni neno la Mungu pekee lenye nguvu ya kubadilisha maisha yetu kwa sababu lenyewe lina uwezo wa kutambua mawazo ya mioyo yetu na kututengeneza Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” 1Wakoritho 6:9-11 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.”     Waefeso 5:3 “Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;

5.       Jilinde moyo wako na picha chafu.(pornography)

Hakikisha kuwa unajilinda na kitu chochote kinachohusika na kuinua hisia za mwili wako, iwe ni picha magazeti na stori za mapenzi au vipindi katika televisheni, vitabu na majarida na vijiwe vya stori zinazochochea ngono, Wakolosai 3:5-6 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.

6.       Pigana vita kali kwaajili ya mabadiliko yako !

Kama unapambana na tamaa ya mapenzi ya jinsia moja ni lazima ufahamu kuwa vita uliyonayo sio nyepesi, lazaima upambane “ Nimemuomba sana Mungu anisaidie, nimesoma maandiko, nimefunga lakini sielewi  nitashindaje” alisema kijana mmoja anayepamba na ushoga, vita dhidi ya dhambi inayotuzinga kwa harapa au upesi sio nyepesi, ni vema kutokujiingiza kabisa na kama umejiingiza ni lazima upambane, huwezi kupigana vitanhii kwa nguvu zako mwenyewe hakuna tiba rahisi, kila mtu anayetaka kumpendeza Mungu lazima apambanae na nlolote lile linalokushusha kutoka kwenye kiwango ambacho Mungu amekikusudia, Mungu anajua mapambano tuliyonayo 1Yohana 3:19-20 “Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.” Unapomtii Mungu unafungua mlango wa kupokea baraka na kuna thawabu kubwa za kumtii yeye Zaburi 19:8-11 “Maagizo ya Bwana ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya Bwana ni safi, Huyatia macho nuru. Kicho cha Bwana ni kitakatifu, Kinadumu milele. Hukumu za Bwana ni kweli, Zina haki kabisa. Ni za kutamanika kuliko dhahabu, Kuliko wingi wa dhahabu safi. Nazo ni tamu kuliko asali, Kuliko sega la asali. Tena mtumishi wako huonywa kwazo, Katika kuzishika kuna thawabu nyingi.Ni muhimu kumtegemea Mungu na kupambana na tamaa mbaya katika mioyo yetu tusichoke  Wagalatia 6:9 “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” Kadiri tutakavyoendelea kupambana na tamaa hii mbaya hatimaye tutajikuta tuko katika uhusiano ulioimara sana na Mungu

7.       Hakikisha unautiisha mwili kwa kufanya mazoezi.


ITimotheo 4:8Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.”  Maandiko yanatukumbusha nkuwa tunapaswa kufanya mazoezi japo kwa kiasi, na kuishi maisha matakatifu, kila kitu Duniania ambacho tunajiandaa kukifanya kinahitaji mazoezi, na wakristo pia wanapaswa kufanya mazoezi kufanya mazoezi sio dhambi, mazoezi yana umuhimu mkubwa katika mkaisha yetu ya kimwili na kiroho, lakini pia katika kuzitiisha tamaa za mwili. Kwa nini Biblia inatutaka tufanya mazoezi kwa kiasi?  Kwa sababu mazoezi yana tambia ya kuwa ikama ibada ya sanamu, ukitapenda sana yanakuwa kama ibada kwa hiyo tunapaswa kuwa na kiasi, pia Wakrito hawapaswi kufanya mazoezi kwa kusudi la kubadili maumbile yao yaani Bodybuilding na pia kwa kusudi la kuongeza uzito weightlifting, wakristo wanapaswa kufanya mazoezi kwa kusudi la kujiweka imara na kuiondoa katika miganamizo ya mawazo na kuruhusu akili zetu kufanya kazi zizuri, kujenga kuiamini na kujiweka sawa, kwa hiyo tufanye mazoezi lakini tusiyageuze mazoezi kuwa kama ibada, Tunaweza kumuheshimu Mungu kwa kuituza miili yetu 1Wakoritho 6:19-20Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;  maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.” Angalia pia 1Wakoritho 10:31 “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.


Na Mchungaji Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!
0718990796.