Jumatatu, 23 Novemba 2020

Mzeituni umeao katika nyumba ya Mungu!

Zaburi 52:8 “Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu katika hekima yake alipouumba ulimwengu, aliiuumba ili uwe zawadi kubwa kwa wanadamu,  na aliweka miti na mimea kwaajili ya uhai na utatuzi wa matatizo ya kiafya kwa wanadamu, kwa msingi huo basi utaweza kuona kuwa, Miti ina uhusiano mkubwa wa uhai maisha na hata nafsi ya mwanadamu Lakini miti pia ina uhusiano wa kiroho na maisha ya mwanadamu. Mungu aliitoa miti na mimea kama zawadi kwa wanadamu kwaajili ya kunufaisha maisha yao ona Mwanzo 1:29 “Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;

Katika miti au miche ambayo ilitolewa kama zawadi kwa wanadamu moja ya mti wa ajabu sana wenye nguvu za mwilini na rohoni ni mti wa Mzeituni, mti huu ni malimbuko ya amani ya dunia ni ni mti wa kwanza kutajwa mara baada ya gharika wakati wa nabii Nuhu, ukiacha mti wa mtini ambao ulitajwa mapema sana mara baada ya anguko la mwanadamu ona Mwanzo 8:6-12 “Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya; akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi. Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi; bali yule njiwa hakuona mahali pa kutua kwa wayo wa mguu wake, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani. Akangoja na siku saba tena; kisha akamtoa yule njiwa katika safina mara ya pili, njiwa akamjia jioni, na tazama, alikuwa na jani bichi la mzeituni kinywani mwake, ambalo amelitunda, basi Nuhu akajua ya kwamba maji yamepunguka juu ya nchi. Akangoja na siku saba tena, akamtoa yule njiwa; naye asimrudie tena kamwe.

Mungu aliweka uwezo wa ajabu katika mti huu, na miongoni mwa miti inayofanya kazi ya kuleta heshima kwa Mungu na wanadamu Mzeituni ni mojawapo ni mti  wa kwanza katika miti hiyo  maarufu ya kibiblia angalia Waamuzi 9:8-12 “Siku moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti mzeituni, Tawala wewe juu yetu. Lakini huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? Kisha miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu. Lakini huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende nikayonge-yonge juu ya miti? Kisha miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu.

Sifa za mti wa Mzeituni!

Moja ya sifa ya mti wa Mzeituni ni kuwa ni mti wenye uwezo mkubwa sana wa kustahimili ukame, lakini ni mti usioweza kufa, ni mti wenye uwezo wa kufufuka, mizizi yake ina uwezo mkubwa sana wa kwenda chini na kujiunganisha na maji, kwa sababu hiyo sio rahisi kuuua mzeituni, ukitaka kuuua lazima uchomoe mizizi yake na kuitenganisha na maji huko ardhini, hapo ndipo utaweza kuua, unaweza kuifyekelea mbali lakini baada ya muda fulani unachipua tena!

Mti huu ulitumika nyakati za Agano la kale kusimika watu waliokusudiwa kuwa watumishi wa Mungu katika Nyanja mbalimbali, kama Wafalme, Makuhani na manabii, ili mtu aweze kumtumikia Mungu katika nafasi hizo alipakwa mafuta ya mzeituni kwa maelekezo ya Mungu na maisha ya mtu huyo yalibadilika sana, Makanisa makubwa ya zamani kama Anglican na Kanisa Katoliki huyatumia mafuta ya mzeituni katika ibada za kipaimara na wakati wa kusimika viongozi wa kanisa wakiwemo makuhani wa madhehebu hayo, hii ni kwa sababu wanakumbuka huduma za kikuhani za kupoaka mafuta zilizokuwa zikifanywa na makuhani au manabii nyakati za agano la kale mifano ifuatayo itakusaidia kuelewa uhusiano wa kiroho ulioko kati ya mwanadamu na upako wa mafuta ya mzeituni unaokaribisha nguvu za Mungu Roho Mtakatifu! Ona  

1Samuel 10:1-7 “Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu? Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai; nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao. Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri; na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE. Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.

1Samuel 16:1-13Bwana akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe. Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi Bwana akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea Bwana dhabihu. Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako. Samweli akafanya hayo aliyosema Bwana, akaenda Bethlehemu. Wakaja wazee wa mji kumlaki, wakitetemeka, nao wakasema, Je! Umekuja kwa amani? Naye akasema, Naam, kwa amani; nimekuja kumtolea Bwana dhabihu; jitakaseni; njoni pamoja nami kwenye dhabihu. Akawatakasa Yese na wanawe, akawaita kwenye dhabihu.  Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo. Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye akasema, Bwana hakumchagua huyu. Ndipo Yese akampitisha Shama. Naye akasema, wala Bwana hakumchagua huyu. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku. Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye. Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na ROHO YA BWANA IKAMJILIA DAUDI KWA NGUVU tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.”           

Katika Agano jipya ishara ya kupakwa mafuta inaweza kuwa mafuta halisi ya mzeituni au kuwekewa mikono na mtumishi wa Mungu aliyepakwa mafuta aliyewekwa wakfu, sio lazima yawe mafuta kama yale yaliyokaa katika pembe lakini Mchungaji aliyepakwa mafuta anaweza kukuwekea mikono na kutamka kusudi la kukuwekea mikono na ikawa sawa kabisa na kupakwa mafuta, lakini hata akikupaka mafuta halisi ya zeituni, bado uweza utakuwa uleule wa kuwekea mikono au kupakwa mafuta, Ndio maana Yesu hakuwekewa mikono lakini alipakwa mafuta na Mungu mwenyewe mara baada ya kubatizwa na Yohana Mbatizaji, mtu anapowekwa wakfu kwa kupakwa mafuta anakuwa mtu mwenye uweza wa kiungu ndani yake na kumfanya kuwa mtu wa tofauti! Ona tangazao la Yesu la kuwa mpakwa mafuta;-

Luka 4:18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.”

Mungu anaporuhusu katika kanuni zake uwekewe mikono au upakwe mafuta unakuwa na uweza wa kiwokovu ndani yako na mungu anakupoa neema inayokuwezesha kuwatetea wengina na kutimiza majukumu yako ambayo Mungu anakuwa ameyakusudia

Mzeituni umeao katika nyumba ya Mungu!

Zaburi 52:1-9

Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.

Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila

Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.

Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.  

Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.

Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka;

Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake.

 Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake.

Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu.

Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.

 

Katika msitari wetu wa Msingi Mwandishi anaonyesha ya kuwa yuko mtu wa hila, mtu mwenye kiburi mwenye uwezo wa kupoteza watu, muovu  inaonekana mtu huyu ana madhara ni hodari na mwenye nguvu, anawaandama wanadamu anapigana nao ana hila bila shaka ni wazi kabisa mtu huyu ni Ibilisi anasimama kushindana na makusudi ya Mungu ndani ya kila mmoja wetu anataka kutuahribia anataka kutuumiza anataka kuweka jeraha katika mioyo yetu, anataka tushindwe, anazuia mafanikio yetu, anapoingana na makusudi ya mungu ndani yetu na ndani ya mwandishi wa zaburi hii ambaye ni Daudi.  Mwandishi anamkumbusha  mtu huyo (Shetani) kuwa Yuko Mungu mwenye nguvu kushinda yeye, anauwezo wa Kumuharibu milele, anauwezo wa kumfutilia mbali, na ana uwezo wa kumng’oa na Daudi anatabiri kuwa wenye haki watamcheka!  Watashangaa kwanini mtu huyu wa kiburi hakumfanya Mungu kuwa nguvu yake? Kwa nini alitumainia mali zake na kujifanya hodari kumbe hana nguvu! Daudi anaeleza kuwa mtu anayemtegemea Mungu anayeutumainia  wema wa Mungu anayetambua kuwa Mungu ni mwema siku zote yaani hata wakati wa nyakati ngumu au ndani ya jambo gumu bado Mungu ni mwema tu! Hao ni sawa na Mzeituni uliopandwa katika nyumba ya Mungu,  yaani wale wanaomtegemea Mungu na kuzitumainia nguvu zake  watamea katika nyumba ya Mungu yaani katika uwepo wa Mungu watastawi watahuishwa, kwa sababu wanategemea fadhili za Mungu wanalitizamia jina lile jema yaani jina la Yesu, hawa hawatatikiswa wala hawataogopa, wakikatwa wanachipua tena! huwezi kuwazibia wameunganishwa mizizi yao na chemichemi ya uzima na chanzo cha uhai ambaye ni Mungu!,  watu walioungwa na chemichemu ya uzima wanautazamia wema wa Mungu siku zote Zaburi 52:1, hao hawawezi kutikiswa hawaogopi wana jina wanalolitumainia wanakaa katika uwepo wa Mungu wanazitumainia fadhili za Mungu milele na milele hawa ni watu wasiowezekana

Ndugu  tunalo tumaini lisiloweza kutikiswa sisi ni kama Mzeituni unaomea katika nyumba ya Mungu. Kila anayemtegemea Mungu na anayezitegemea fadhili zake hapaswi kuogopa, hatupaswi kufadhaika maana sisi kama ilivvyo kwa daudi ni mzeituni unaomea katika Nyumba ya Mungu, Mizeituni huwa haifi, mizeituni huwa inadumu milele, mizizi yake imeungwa na chemic hemi za chini sana za maji, ili tutoweke ni mpaka wachomoe mizizi inayotuunganisha na fadhili za Mungu, Usiogope!

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Jumapili, 8 Novemba 2020

Hamjui yatakayokuwako kesho!

Mstari wa Msingi: Yakobo 4:13-15 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka. Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi.”


Utangulizi:

Mojawapo ya swali muhimu sana ambalo kila mwanadamu mwenye akili timamu huwa anajiuliza ni kuhusu kesho  “future”  kwamba itakuwaje kesho, nini kinafuata baada ya haya? Nini kinakuja, nini kitatokea wiki ijayo, mwezi ujao, mwaka ujao na wakati mwingine tunaona giza, na kujiuliza je tutakuwa na furaha au tutakuwa na dhuruba? Ni nani anaishikilia kesho yetu? Je napaswa kuwa na matumaini au kuogopa?


Itakuwaje mtihani unaokuja mbele yetu? Tutapata habari gani, itakuwaje matokeo ya uchaguzi wa, nani atashinda na itakuwaje akishinda fulani? Itakuwaje kazini, itakuwaje ndoa yangu, itakuwaje marafiki zangu, itakuwaje familia yangu? Itakuwaje afya yangu? Itakuwaje nikistaafu? Itakuwaje nikiachwa?


Watu wengi sana wanaogopa sana kuhusu maisha yajayo na kwa sababu hii ingawa wanajua umuhimu wa maswali hayo lakini kutokana na hofu au woga kisaikolojia watu wengi huwa wanapotezea swali hili Muhimu ili kupata unafuu na kutuliza maumivu yake, Mungu anajua kwamba swala kuhusu kesho ni swali tata sana kwa wanadamu na hataki tuogope wala kujisumbua hususani tunapokuwa na uhusiano mwema na yeye  Yesu Kristo anawatoa hofu kabisa waaumini wake akitaka jambo hili lisiwasumbue ona


Mathayo 6:31-34 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”


Kwa kuwa Mungu anajua kuwa swala la kesho itakuwaje ni swala zito kwa wanadamu Maandiko yanawafundisha watu wa Mungu namna inavyowapasa kuenenda, watu wenye kiburi na watu wasiomjua Mungu huwa wana uhakika sana na maisha ya kesho kunakosababishwa na majivuno na kiburi.


Neno la Mungu linaonya kujisifu kuhusu kesho!


Watu wasiomjua Mungu huwa na tabia ya kujisifu na kujivuna kuhusu Kesho! Jambo ambalo neno la Mungu limeonya sana kwa njia nyingi na kwa mifano mingi wako watu ambao hujivunia kesho kana kwamba wanajua yatakayotukia kesho Biblia inaonya vikali sana kuhusu maisha yajayo au kuhusu kesho ona Mithali 27:1 “Usijisifu kwa ajili ya kesho; Kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja.Wako watu hujivunia kuhusu kesho kana kwamba wana uhakika nayo na wanamuweka pembeni Mungu katika mipango yao na makusudi yake, Neema yake na wema wake  wako watu ambao walisahau kuwa kila kitu na kila jambo liko kwenye mikono ya Mungu, Mungu ana namna yake ya kuwanyoosha watu wenye kiburi


Ø Daniel 4:28-33 “Hayo yote yakampata mfalme Nebukadreza. Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu? Hata neno lile lilipokuwa katika kinywa cha mfalme, sauti ilikuja kutoka mbinguni, ikisema, Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako.Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni; utalishwa majani kama ng'ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote. Saa iyo hiyo jambo hilo likatimizwa, likampata Nebukadreza; alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ng'ombe, na mwili wake ulilowa maji kwa umande wa mbinguni, hata nywele zake zikakua, zikawa kama manyoya ya tai, na kucha zake kama kucha za ndege.“

 

Ø Matendo 12:20-23 “Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme. Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.


Ø Luka 12: 15-21 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo. Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.”  

 

Ø Mjezi wa Meli ya TITANIC  ambayo ilikuwa meli ya kifahari sana iliyokuwa na viwanja vya mpira, kumbi za starehe na mabwawa ya kuogelea alipoulizwa kuhusu uimara wa meli hiyo alijigamba na kusema hata Mungu hawezi kuizamisha, meli hii ilizama siku ya nne tu tangu ilipoanza safari kutoka Uingereza baada ya kugonga mwamba wa barafu katika bahari ta Atlantic  mnamo asubuhi ya tarehe 15/04.1912, Meli hii ilikuwa na abiria wapatao 2240 na kati yao zaidi ya 1500 walipoteza maisha, hatujui kesho yetu, kila aina ya kile tunachokifikia duniani hatuna budi kukumbuka kuwa ni kwa neema ya Mungu tu!


Mifano hii yote katika Biblia imeandikwa ili kutuonya sisi wanadamu ya kwamba hatuna kesho, kujilimbikizia mali na kuwa na choyo hakuongezei uzima wetu duniani, kila aina ya mafanikio tuliyionayo hayatokani na uwezo wetu ni neema ya Mungu  na wema wake ona Paulo mtume ndiye mtume aliyefanya kazi kubwa kuliko mitume wote lakini wakati wote alikumbuka kuwa alifanya chini ya neema ya Mungu na sio uwezo wake ona  1Wakoritho 15:10 “Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.Tunapaswa kuhakikisha kuwa tunaitegemea neema ya Mungu na kumtukuza yeye katika kila jambo na kumtanguliza yeye, kila mmoja anapaswa kuhakikisha anajilinda na kiburi kwa vile maisha hayako katika mikono yetu! Na Hatujui yatakayokuwako Kesho!


Hamjui yatakayokuwako kesho! 


Hakuna ajuaye kesho, Kesho iko katika mikono ya Mungu, Mungu anajua yote kuhusu kesho, Mungu anajua kila kitakachotokea anajua kitakachotokea kesho, wiki ijayo, mwezi ujao na miaka ijayo kwa hiyo kesho iko katika mikono ya Mungu Isaya 46:9-10 “kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.” Mungu anautangaza mwisho tangu mwanzo, Mungu anakujua na wewe nawe anajua unayoyahitaji anajua utakuwa nani anajua atakayeolewa na wewe anajua utakayemuoa anajua utakuwa na watoto wangapi anajua mwanzo na hata mwisho wa maisha yetu, alitambua mwisho wa Yusufu na kuutangaza kwa njozi kabla,  Mungu alikuwa anajua kuwa mavazi ya Yesu yatapigiwa kura miaka 1000 kabla ya Yesu Daudi alitabiri kitakachompata Yesu ona Zaburi 22:18 “Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura.” na Mathayo 27:35 “Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]”  Mungu anaweza kutuambia hata leo akitaka kuhusu kesho yetu na hivyo kama tunamtegemea na kumuamini tunapaswa kuwa na unyenyekevu na kumtegemea yeye na kumtanguliza yeye na kumuomba yeye, Kesho yetu iko mikononi mwa Mungu hatupaswi kusahau hilo yeye amakuwepo tangu mwanzo na yuko hata milele, Yesu ni yeye yule jana leo na milele anajua kila kitu kitakachotokea  na anampango mwema kwa aajili ya kila mmoja anayemtanguliza na kumtegemea yeye Warumi 8:28-30 “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.” 


Mkumbuke Mungu katika mipango yako yote. 


Ni muhimu kufahamu kuwa maandiko yanatufundisha kwamba tunapaswa kumtanguliza Mungu mbele katika kila jambo, katiia mipango yetu maono yetu ndote zetu na kazi zetu tunapaswa kumuomba Mungu na kumtanguliza yeye na hatupaswi kuzitegemea na kujivunia akili zetu wenyewe, Watu wenye kiburi hawa na choyo wadhalimu hujisifia tama zao na hawataki kumkumbuka wala kumtanguliza Mungu kwa namna yoyote ile Zaburi 10:2-3 “Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza. Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana Bwana na kumdharau.” 


Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima !

0718990796

Jumapili, 25 Oktoba 2020

Na utakapoponyoka, Utalivunja kongwa lake !

 

Mwanzo 27:38-40 “Esau akamwambia babaye, Una mbaraka mmoja tu, babangu? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau akapaza sauti yake, akalia.  Isaka, baba yake, akajibu, akamwambia, Angalia, penye manono ya nchi patakuwa makao yako, Na penye umande wa mbingu unaotoka juu. Kwa upanga wako wewe utaishi, nawe utamtumikia nduguyo; Na itakuwa utakapoponyoka, Utalivunja kongwa lake katika shingo yako.

 


Utangulizi:

Wengi wetu tutakuwa tunafahamu habari za Yakobo na Esau kwa sababu tumezisoma mara kadhaa katika Biblia na pengine tumezijadili mara kadhaa na pia kuzihubiri, kwa ujumla watu wengi sana wanaposoma kisa hiki, humsikitikia sana Esau na hata kumuona Esau kama mtu mjinga na aliyedanganywa mara kadhaa na kukandamizwa na Ndugu yake pamoja na mama yake, na tumesahahu kuwa uko upande mwingine ambao Esau ana jambo lake na linaweza kutufundisha kitu.

Kama tunavyoielewa habari hii yenye kusisimua na kusikitisha, Tunasoma kuwa Isaka anamjibu Esau alipouliza kama kuna mbaraka wowote japo mmoja umebaki kwaajili yake, Majibu anayopewa Esau hayaonyeshi kuwa amepata Baraka kwa sababu Isaka alikusudia kumwaga Baraka zote kwa Mwanaye mkubwa na bahati mbaya amebariki Baraka hizo kwa yakobo mwanaye mdogo ambaye alikuja kwa hila baada ya mpango mkakati wa Rebeka ona

Mwanzo 27:1-10 “
Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa. Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu. Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo; ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa. Na Rebeka akasikia, Isaka aliposema na Esau mwanawe. Basi Esau akaenda nyikani awinde mawindo, ayalete. Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, akisema, Angalia, nimemsikia baba yako akisema na Esau, ndugu yako, akinena, Niletee mawindo, ukanifanyie chakula kitamu ili nile, na kukubariki mbele za BWANA kabla ya kufa kwangu. Basi, mwanangu, sikiliza sauti yangu kama nitakavyokuagiza. Enenda sasa kundini ukanitwalie wana-mbuzi wawili walio wema, nami nitawafanya chakula kitamu kwa baba yako, namna ile aipendayo. Kisha utampelekea baba yako, apate kula, ili akubariki kabla ya kufa kwake.

Unaweza kuona kwa njama za
Rebbeka na Yakobo waliweza kuchukua Baraka zote alizokusudiwa Esau, wakati wote wakimfanya Esau kuwa mjinga  na pamoja na baba yake hata kumbariki mtu mwingine 

Mwanzo 27:26-29 “
Isaka, baba yake, akamwambia, Njoo karibu sasa, ukanibusu, mwanangu. Akakaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema, Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba alilolibariki BWANA. Mungu na akupe ya umande wa mbingu, Na ya manono ya nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo. Mataifa na wakutumikie Na makabila wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, Na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakayekulaani alaaniwe, Na atakayekubariki abarikiwe.”


Kulikuwa na tatizo kubwa sana katika familia hii, wazazi walikuwa wamegawanyika mama akiwa na Yakobo na Isaka akiwa na Esau kila mmoja alikuwa na jambo lake moyoni  Isaka alikuwa amekusudia kumbariki Esau kweli kweli na nduguye anngekuwa mtumwa wake tu, na hakukuwa na vinginevyo, Isaka anagundua kuwa amemwaga mibaraka yote kwa Yakobo wakati alikuwa ahajkusudia kumuachia yakobo chochote sasa kumbe amembariki Yakobo na jambo hili lilimpa kutetenmeka san asana Isaka lakini angefanya nini alikuwa amekwisha kutamka

Mwanzo 27:32-33 “
Isaka, baba yake, akamwuliza, U nani wewe? Akasema, Mimi ni mwanao, Esau, mzaliwa wako wa kwanza. Isaka akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa.”Lilikuwa ni tukio la kusikitisha na kutisha sana katika maisha ya Isaka na Esau na Isaka alisema japo mtu huyu amekuja kwa hila atabarikiwa  sasa ni mbaraka gani umebakia Esau alihoji kwa nguvu zake zote kuwa endapo uko mbaraka umebaki tafadhali basi baba unibariki na mimi!

Na itakuwa utakapoponyoka, Utalivunja kongwa lake katika hingo yako!

Ndipo Isaka akatamka mbaraka huu Hebu tuuangalie vizuri Mwanzo 27:38-40 “Esau akamwambia babaye, Una mbaraka mmoja tu, babangu? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau akapaza sauti yake, akalia.  Isaka, baba yake, akajibu, akamwambia, Angalia, penye manono ya nchi patakuwa makao yako, Na penye umande wa mbingu unaotoka juu. Kwa upanga wako wewe utaishi, nawe utamtumikia nduguyo; Na itakuwa utakapoponyoka, Utalivunja kongwa lake katika shingo yako.

Esau alipokea mbaraka mmoja tu lakini mbaraka huu ulikuwa na masharti, ni kweli Mungu alimuandalia penye umande na unono, lakini ili aweze kuyapata lazima afanye vita lazima apambane haitakuwa rahisi, na nduguye atamtawala lakini lazima aponyoke na kulivunja kongwa yaani nira ya utumwa na kuwa huru,  

Kongwa ni nini?

Kongwa ni neno la kiswahili lenye jina lingine liitwalo Nira, kwa kiingereza Yoke, chombo hiki huvalishwa wanyama kazi shingoni kwa kusudi la kuwatumikisha na kuwafanyisha kazi kwa lazima, Katika biblia hutumika kama alama ua utumwa, au ukoloni, chombo hiki kinapovalishwa kwa mnyama mnyama huyo hutekeleza matakwa ya Bwana wake tu na kutumikishwa kwa muda na majira na nyakati kama atakavyo bwana wake hivyo mnaya hupoteza uhuru na uwezo wa kufanya mambo yake ayatakayo, Mtu yeyote anayetaka kuwa huru katika jambno lolote linalomtumikisha bila kupenda ni lazima aponyioke na kujivua Kongwa ndipo aweze kuwa Huru! Mbaraka aliopewa Esau na baba yake ulihusisha unono na umande kutoka kwa Mungu lakini ulikuwa unahusisha nguvu zake yaani ilikuwa ili Esau awe huru kutoka kwa nduguye atumie nguvu, apigane akatae kuwa mtumwa kama nchi nyingi za afrika zilivyojipatia uhuru ni chache sana zilipata uhuru bila kumwaga damu, Esau alitamkiwa kuwa mtumwa wa Israel lakini sio milele, alitakiwa kujitetea alitakiwa kupigana alitakiwa kujichomoa na kulivunja kongwa la nduguye ili aweze kuwa huru!

Maandiko haya yalitimizwa kwani wazao wa Yakobo na Esau walikuja kuutimiza unabii huu kwa dhahiri, Wazao wa Esau ambao ndio Edomu walikuja kutawaliwa wakati wa Daudi kupitia jemadari wake Yoabu ambaye aliwatenda vibaya sana na kuwakatilia mbali na kuwapoteza wanaume wote ona  

1Wafalme 11:15-16 “
Kwa maana ikawa, Daudi alipokuwako Edomu, naye Yoabu, mkuu wa jeshi, amepanda awazike waliouawa, akiisha kumpiga kila mwanamume wa Edomu, (kwa kuwa Yoabu alikaa huko miezi sita pamoja na Israeli wote, hata alipompoteza kila mwanamume wa Edomu);”  

Kutokana ana ushindi huu wa Daudi wana wa Esau walikuwa watumwa wa Israel kwa muda Fulani  na walilipa kodi na kutawaliwa, Lakini Biblia inasema baadaye  waklikataaa na kujilipia kisasi na kutangaza uhuru wao na kujitawala ona

2Wafalme 8:20-22 “
Zamani zake, Edomu wakaasi mkononi mwa Yuda, wakajifanyia mfalme. Basi akaenda Yehoramu mpaka Sairi, na magari yake yote pamoja naye. Akaondoka usiku, akawapiga Waedomi waliomzunguka yeye na maakida wa magari; na watu wakakimbilia hemani kwao. Hivyo Edomu wakaasi mkononi mwa Yuda hata leo. Na Libna wakaasi zamani zizo hizo.” 

Biblia inaonyesha kuwa Esau alikataa kuwa mtumwa wa Israel hata leo  na hivyo unabii wa Isaka ulitimizwa, Edomu ukawa ni utawala huru na wakawa watu hatari sana kwa
Yuda na wakati wa utawala wa Ahazi Edomu waliipiga Yuda vibaya sana na kuwachukua Mateka ona

2Nyakati 28:16-17 “
Wakati ule mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa mfalme wa Ashuru ili amsaidie. Kwa kuwa Waedomi walikuwa wamekuja tena, na kuwapiga Yuda, na kuwachukua wafungwa.”

Nisikilize mpendwa ziko haki zako na Baraka zako nyingine huwezi kuzipata hivihivi, huwezi kuzipata kwa maombi pekee huwezi kuzipata kwa kufunga na kuomba ziko Baraka zako zingine zinapatikana kwa kupambana kwa kukataa kuwa mtumwa kwa kuvunja kongwa la nduguyo kongwa ni  chombo anachovalishwa mnyama wa kazi shingoni ili kumtumikisha na kumfanya afanye kazi ngumu tena si kwa hiyari yake mwenyewe. ziko haki nyingine huwezi kuzipata mpaka uende mahakamani. Ziko haki nyingine huwezi kuzipata bila kutumia nguvu au kutumia upanga, waulize wapigania uhuru wengi kama unadhani uhuru luilikuwa jambo rahisi hata kidogo, wazunghu hawangetaka kuachia unono wa rasilimali za Afrika kirahisi au kwa maneno tu, waulize kina Keneth Kaunda, Kwame Nkuruma, Julius Nyerere, Haile Sellasie, Jomo Kenyatta, Abeid Karume, Samora Machel, Martin Luther King na wapoigania haki wa kweli kama ilikuwa rahisi kuwa huru na kuliacha kongwa la kitumwa na kikoloni? Kutokana na upole wetu na ukarimu wetu, Sfrika ilipoteza uhuru wake, rdhi nzuri zilichukuliwa, mashamba mazuri yakawa ya wazungu, Eaafrika waligeuzwa vibarua kwa ujira mdogo, mazao yaliyolimwa walilzazimishwa ya kibiashara, walilipishwa kodi na walipaswa kutumia mamlaka za kifedha za kikoloni Afrika walijikuta wamepotea uhuru wao, Ukombozi wa kweli na uhuru wa kweli ungekuja kwa kupigana tu na si vinginevyo:-

Yako mambo hata kama umeokoka vipi huwezi kuyapata bila mapambano ya dhati Kama hunielewi vizuri Rais wa  sasa wa Malawi anaweza kunielewa vizuri, Yeye alikuwa Askofu mkuu wa Kanisa la Assemblies of God Malawi kwa miaka 24, kisha aliingia kwenye siasa na chama cha Malawi congress Part, aligombea urais mara kadhaa na mara ya mwisho alipambana na  chama tawala cha DPP ambao walijitangaza kuwa washindi kwa hila  na Rais Peter Mutharika aliapishwa kuwa rais wa malawi haki ikiwa imepotioshwa na uchaguzi ukiwa uimegubikwa na hila na udanganyifu wa kila aina, Askofu huyu Mstaafu haki yake aliipata mahakamani, ambapo mwaka huu 2020 uchaguzi ulipoamuriwa urudiwe na mahakama alishinda kwa asilimia 59% ya kura zote zilizopigwa na kuapishwa kuwa rais wa Malawi akiwa na miaka 65 sasa  lazarous Askofu Chakwera ni rais  wa sita wa Malawi aliyeapishwa mwaka huu june 28 2020, Inawezekana alifunga na kuomba lakini haki yake ilipatikana mahakamani!

Yako mambo mengine ni lazima upambane, yako mambo mengine hayaondoki kwa kuwa mpole yako mambo mengine hayarekebishiki kirahisi, lazima upambane , lazima uvunje kongwa la utumwa, lazima ukatae ushenzi na ujinga na dharau na ukandamizwaji, hivi ndio nchi nyingi za Afrika zilivyojikomboa haikuwa rahisi, shetani hawezi kuruhusu uhuru kwa njia rahisi, hawezi kuruhusu furaha wa njia rahisi, hawezi kuachia mateka kwa njia rahisi  lazima upambane, Isaka akamwambia Esau mwanangu unono upo na umande upo Mungu amekupa lakini wewe utakula kwa upanga  wako na nduguyo amekusudiwa kukutawala lakini ukiponyoka na kulivunja kongwa lake utakuwa huru, Ponyoka kutoka katika ukandamizwaji na maumivu na mateso tangaza uhuru wako mwenyewe  shetani asikuonee tena sio lazima ufie hapo, sio lazima ufie kwenye ndoa hiyo iliyojaaa masimango ugomvi, mikwara ubabe na kutokupatikana kwa suluhu utumwa na udhalilishaji kunyimwa tendo la ndoa, kukosa maamuzi yako, wakeo na ndugu wamekuwa na sauti kuliko wewe mwenye nyumba,  sio lazima ufie kwenye kazi hiyo iliyojaa ukandamizwaji, mateso posho ndogo kuibiwa na kuonewa na kutukanwa, wakati mwingine ili uwe na mbele njema ni lazima upambane, yako mambo ni mpaka ukasirike ndio yanawezekana !, sio lazima ufie kwenye dhehebu hilo unaweza kuanza hata huduma yako, uwezo wa kujikomboa u katika mikono yako wewe mwenyewe jikomboe wewe na ndugu zako! Sio lazima umsamehe mtu aliyedhulumu shamba lako sio kila kitu kinahusu kumuachia Mungu, vingine vinahitaji mapambano pigana weka upanga wako vunja Kongwa la utumwa utakuwa huru na uko sahihi

Wakati wa Uhuru wa zimbabwe Robert Nesta Maley aliimba maneno ya Muhimu sana kwamba wakati mwingine ni sahihi kupigana kwaajili ya Maisha yako yajayo, pata muda sikiliza  maneno yake kuhusu Zimbawe hapa naweka kiasi tu nanukuu

Every man gotta right to decide his own destiny,
And in this judgement there is no partiality.
So arm in arms, with arms, we'll fight this little struggle,
'Cause that's the only way we can overcome our little trouble.

Brother, you're right, you're right,
You're right, you're right, you're so right!
We gon' fight (we gon' fight), we'll have to fight (we gon' fight),
We gonna fight (we gon' fight), fight for our rights!

Natty Dread it in-a (Zimbabwe);
Set it up in (Zimbabwe);
Mash it up-a in-a Zimbabwe (Zimbabwe);
Africans a-liberate (Zimbabwe), yeah.

Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Alhamisi, 15 Oktoba 2020

LENGO KUU LENYE FAIDA KUU!

Wakati huu tulio nao ni wakati wa mwisho 1Yohana 2;18. “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. “ Mwisho wa mambo yote umekaribia 1Petro 4;7. “Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.” bado kitambo kidogo Yeye ajaye yaani Yesu Kristo anakuja, wala hatakawia Waebrania 10;37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.” katika wakati huu wa mwisho ni muhimu kwa kila mmoja wetu kujifunza na kutafakari kwa makini somo letu la leo ‘Lengo kuu lenye faida kuu ”Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele sita vifuatavyo.:-

*      Malengo mbalimbali ya wanadamu katika maisha

*      Tatizo kubwa la malengo ya kawaida ya wanadamu

*      Lengo kuu lenye faida kuu

*      Mifano ya watu wenye Busara waliokuwa na lengo kuu lenye faida kuu maishani mwao

*      Mifano ya watu wapumbavu ambao hawakuzingatia lengo kuu lenye faida kuu

*      Yatupasayo Kufanya




Malengo mbalimbali ya wanadamu katika maisha

     Ukimuuliza mtu awaye yote maswali haya Je ni kitu gani unachotamani kuwa nacho maishani mwako? ukipata nini utakuwa na furaha isiyo na kikomo? wanadamu mbalimbali watakuwa na majibu Tofauti katika kujibu maswali haya au kwa Maneno mengine watakuwa na malengo mbalimbali. katika Biblia tunawaona watu waliokuwa na malengo mbalimbali katika maisha yao 


Luka 12;13 “Mtu mmoja katika mkutano akamwambia, Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie urithi wetu” 

tunaona juu ya mtu mmoja aliyelenga tu kupata urithi. Ina maana hata mzazi wake alipokuwa hai aliwaza moyoni kwamba siku ya kugawiwa urithi itafika lini, Lengo lake ilikuwa ni mali za baba yake mbaya sana 


Luka 12 16-19 “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.” tunaona mtu moja mkulima aliyekuwa tajiri sana yeye lengo lake lilikuwa kujenga ghala kubwa na kuweka nafaka zake na vitu vyake ili apumzike, kula kunywa na kufurahia. Maandiko yanatupa habari za mtu mwingine  aliyekuwa na cheo kikubwa sana huko Shamu huyu aliitwa Naaman yeye alikuwa jemedari wa jeshi la mfalme wa Shamu,alikuwa mtu mkubwa mwenye Kuheshimiwa wa pili kutoka kwa mfalme huyu Tofauti na waliotangulia alikuwa na lengo la kupona ukoma 


2Falme 5;1-3. Basi Naamani, jemadari wa jeshi la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake Bwana alikuwa amewapa Washami kushinda; tena alikuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma. Na Washami walikuwa wametoka vikosi, wakachukua mfungwa mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani.  Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake.” 


Wako watu vilevile hali kadhalika wanaweza kuja kwa Yesu Kristo lakini malengo yao yakiwa ni kupokea miujiza yao, kuponywa magonjwa yao ama wanaweza kumfuata Yesu kwa sababu kadhaa wa kadhaa Mwanamke Hana, pamoja na kupendwa sana na mumewe na kupata kila kitu lakini aliwaza moyoni mwake wakati wote kupata mtoto 


1Samuel 1;1-11 “Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu  naye alikuwa na wake wawili; jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina; naye huyo Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto. Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea Bwana wa majeshi dhabihu katika Shilo. Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa Bwana, walikuwako huko. Hata siku ile ilipofika Elkana alipotoa dhabihu, kumpa mkewe Penina sehemu, akawapa na watoto wake wote, waume kwa wake, sehemu zao; lakini Hana humpa sehemu mara mbili; maana alimpenda Hana, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.  Ila mwenzake humchokoza sana, hata kumsikitisha, kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo. Tena mumewe akafanya hivyo mwaka kwa mwaka, hapo yule mwanamke alipokwea kwenda nyumbani kwa Bwana, ndivyo yule alivyomchokoza; basi, kwa hiyo, yeye akalia, asile chakula. Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo wako una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi? Ndipo Hana akainuka, walipokwisha kula na kunywa huko Shilo. Naye Eli, kuhani, alikuwa akiketi kitini pake penye mwimo wa hekalu la Bwana.  Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba Bwana akalia sana.  Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa Bwana huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe.” watu wengine katika 


Yakobo 4;13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;” 


wao walikuwa na lengo kuu  la kufanikiwa kibiashara na kupata utajiri,hata hivi leo kama ilivyokuwa kwa watu hawa lengo lao kuu ni kupata mchumba, kuolewa au kuoa, kuwa na digrii tatu, kuwa na cheo cha rais n.k Mtu aliye na lengo kuu la kupona au kupata mtoto anaweza hayo tu wakati wote na kwake mengineyo hayana uzito mkubwa kwake, wengine watakuja Kanisani kama hapa lakini lengo lao ni kupona tu, kuolewa au kuwa na mtoto na wokovu au kumtumikia Mungu kwake havina uzito mkubwa kila mmoja hana budi kujiuliza lengo lake kuu alilonalo ni nini? Wengine watatamani kuwaombea maelfu ya watu na kuwaona wanapokea miujiza yao n.k.

Tatizo kubwa la malengo ya kawaida ya wanadamu

Tatizo lililopo ni kwamba hata kama malengo waliyo nayo wanadamu yanatimia bado hayawapi furaha isiyo na kikomo. Mtu akipona ugonjwa wake au mateso yake kwa miujiza mkubwa bado hatimaye atakufa tu Lazaro aliyefufuka katika 


Yohana 11;38-44 “Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake.  Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.  Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.          


hatimaye alikufa tena,na wengine wengi walioombewa na Yesu wakapata miujiza yao kama kipofu Bartimayo aliyepata kuona,hatimaye alikufa,mtu hata akipata utajiri na mali iwe ni mamilioni ya mapesa, magari mengi, nyumba na kadhalika akifa haondoki navyo anaviacha vyote Zaburi 49;16-19 “Usiogope mtu atakapopata utajiri, Na fahari ya nyumba yake itakapozidi. Maana atakapokufa hatachukua cho chote; Utukufu wake hautashuka ukimfuata. Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, Na watu watakusifu ukijitendea mema, Atakwenda kwenye kizazi cha baba zake Hawataona nuru hata milele”. katika yote haya na malengo mengineyo mengi  hakuna cha kudumu  yote haya ni ya kupita wafalme wengi waliokuwa maarufu na wengi waliokuwa maarufu hapa duniani wamepita wamekufa na imebaki historia tu. Wanasiasa wengi, wakubwa na maarufu duniani, waimbaji, wachezaji, wasanii, matajiri na wanasayansi na wenye umaarufu wa kila aina wote wamepita duniani na historia zao zimehifadhiwa hakuna cha kudumu, wahubiri maarufu waliotikisa dunia na kila mwenye mafanikio ya kila namna duniani wamepita hakuna jipya chini ya jua mambo yote ni ubatili tu kila kitu kina mwisho na hakuna cha kudumu kwa msingi huo malengo yetu duniani ni ya muda mfupi tu na sio ya kudumu wala hayana faida za kudumu!

Lengo kuu lenye faida kuu.

Lengo kuu lenye faida kuu ni kupata uzima wa milele au kuingia mbinguni mtu anapokuwa na lengo hili moyoni mwake wakati wote na kulipa uzito mkubwa kuliko malengo mengine yote mtu huyu anakuwa ameigundua siri, kukosa uzima wa milele kunaitwa kupotea katika Biblia 

Yohana 3;16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele       

Mtu Yeyote mwenye Busara atawaza kwanza juu ya uzima wa milele kuliko uzima huu wa Muda tu katika miili yetu wakati wote atawaza kama mtu mmoja aliyekwenda mbio akitafuta juu ya jambo hili wakati wa Yesu 

Marko 10;17 “Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? “ 


unaona swala kubwa sana na la msingi kuliko yote ni kuwa kuna maisha baada ya kufa, Je utakuwa wapi baada ya maisha yako duniani kuisha?  Iko jehamnamu ya moto milele na milele na uko uzima peponi milele na milele! Mtu anayekusudia kuupata uzima wa milele ndiye mtu mwenye akili kubwa kuliko wote, wako watu katika Biblia ambao licha ya Mungu kuwabariki kwa Baraka mbalimbali walikuwa na mawazo ya ufalme wa Mungu! Nahii ilikuwa ndio busara kubwa sana!

Mifano ya watu wenye Busara waliokuwa na lengo kuu lenye faida kuu maishani mwao.

Biblia inasema Ibrahamu alikuwa tajiri sana kwa mifugo,kwa Fedha na dhahabu Mwanzo 13;2, Naye Abramu alikuwa ni tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha, na kwa dhahabu.hata hivyo wakati wote lengo lake kuu lilikuwa kuingia mbinguni, aliacha kila kitu na kuwaza juu ya mbinguni  tunaelezwa katika 

Waebrania 11;8-10, kwamba “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.  Sara, Habili, Henoko na Nuhu na wengine wengi walitamani wakati wote kuingia mbinguni kuliko kupata mtoto,kupona n.k 

Waebrania 11;16  Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.” Ayubu pamoja na utajiri wake yeye pia aliwaza juu ya kuingia mbinguni ukuu na utajiri kwake havikuwa na uzito mkubwa kuliko wokovu na kumuona Yesu 

Ayubu 1;1-3, Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu. Kisha walizaliwa kwake wana saba, na binti watatu.  Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, na watu wa nyumbani wengi sana; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.          

Mtume Paulo hakuwaza tu kuifanya kazi ya Mungu au kufanya miujiza mikubwa mingi, lakini pamoja na kutumiwa sana na kupewa mafunuo makubwa Matendo 19;11-12, Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida; hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka.” 2Petro 3;15-16  Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;  vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.” 


Paulo mtuma alikuwa ni mtume aliyafanya kazi kubwa kuliko mitume wote, aliyetumiwa na Mungu kwa miujiza ya kupita kawaida na kutumiwa kuandika Nyaraka na agano jipya karibu nusu na robo alihubiri njili na kuupoindua ulimwengu wa wakati wake hata hivyo hakusahau kuwa na lengo kuu  wakati wote lengo lake lilikuwa kwenda Mbinguni kuikaa na Kristo,Jambo hili alilitamani upeo ona  Wafilipi 1;23,” Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;” hatuna budi kukumbuka kwamba tunaweza kufanya miujiza mingi lakini tukajikuta miongoni mwa watu wa kupoteza, ikiwa tutakuwa na maisha yaliyo jaa dhambi na tukajikuta kuwa sisi ni watu wa kukataliwa  


Mathayo 7;21-23 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.  Tunaweza tukawahubiri wengine na kuwafundisha lakini sisi tukashindwa kuingia mbinguni Paulo mtume alikataa kuwa mtu atakayewahudumia na kuwahubiri wengine kisha yeye kuwa mtu wa kukataliwa ona 

1Koritho 9;26-27, Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.”  Yusufu wa Armathaya, masatahiki yeye aliwaza mbinguni Marko 15;43. “akaenda Yusufu, mtu wa Arimathaya, mstahiki, mtu wa baraza ya mashauri, naye mwenyewe anautazamia ufalme wa Mungu; akafanya ujasiri, akaingia mbele ya Pilato akauomba mwili wake Yesu.”

Mifano ya watu wapumbavu ambao hawakuzingatia lengo kuu lenye faida kuu

Mtu yule mkulima tajiri aliyekuwa na lengo kuu la kujenga ghala kubwa la kuweka nafaka na vitu vyake ili apumzike ale kunywa na kufurahia badala ya kuwaza kwanza juu ya uzima wa milele anaitwa na Mungu “mpumbavu” 

Luka 12;16-21. “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.”  Mtu mwingine tajiri Yeye aliwaza tu kula kwa anasa siku zote na kuvaa kwa anasa lakini hakuwaza juu ya uzima wa milele Tofauti na masikini lazaro matokeo yake alipokufa alikwenda kwenye mateso ya milele motoni 

Luka 16;19-30.” Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu. Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

Yatupasayo kufanya .

·         Kuwa na lengo hili kuu la kuingia mbinguni na kuliweka kuwa la kwanza ya yote mengine Mathayo 6;33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”

·         Kuhakikisha tumetubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha ili tupate rehema ya kuingia Mbinguni Mithali 28;13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.”

·         Kuangalia tusianguke dhambini tena 1Koritho 10; 12 ”Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.” na kuhakikisha lolote lile jingine mbali na lengo kuu lenye faida kuu yaani kuingia mbinguni halichukui nafasi ya kwanza, tunaweza tukaitenda kazi ya Bwana lakini tukasahau utakatifu kwanza kutenda kazi huko hakutatusaidia kuiona mbingu.

Preached by Bishop Zachary Kakobe 15 October 1995 my Spiritual Father

Composed by Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Ikamote@yahoo.com