Jumatatu, 15 Mei 2017

Je Hapana Zeri Katika Gileadi? (Zeri ya Gilead)

Mstari wa Msingi: Yeremia 8: 22 “Je Hapana Zeri katika Gilead? Huko Hakuna tabibu? Mbona basi haijarejea afya ya Binti ya watu wangu?

 Mmea aina ya zeri kama unavyoonekana katika Picha

Ni muhimu kufahamu kwamba hapa duniani hakuna jambo lolote Gumu lisilo na majibu, kila jambo na kila tatizo lina majibu yake na ufumbuzi wake, Magonjwa hali kadhalika yanaweza kutibiwa kwa tiba za aina mbali mbali, Mungu aliwapa wanadamu mimea ambayo ndani yake aliweka nguvu za uponyaji kwaajili ya matibabu ya aina mbali mbali.

Nyakati za Biblia watu walitumia pia madawa yatokanayo na mimea kutibu magonjwa na mateso ya aina mbalimbali, kulikuwa na miti mingi sana iliyotumika kama tiba, kabla ya kuanza kutumia zaidi kemikali ambazo nyingi zina uharibifu mkubwa katika mwili wa wanadamu na hivyo kuchangia udhaifu mkubwa wa aina binadamu walioko leo juu ya uso wa nchi. Moja ya miti maarufu sana iliyotumika kwa tiba katika Israel na mashariki ya kati ulikuwa ni mmea ujulikanao kama Zeri ambao ulikuwa unapatikana kanaani na katika mji wa Gilead.

Zeri ni nini hasa?

Zeri kwa kiingereza (BALM) ulikuwa ni mmea ambao ulikuwa maarufu sana nyakati za Biblia mmea huu ulipatikana katika nchi ya milimamilima iliyokuwa nga’mbo ya Jordan iliyojulikana kama milima ya Gilead, mmea huu uliuzwa kwa bei kubwa sana na wafanya biashara wa zamani waliokuwa matajiri walitajirika kwa kuuza zeri, 

Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na ZERI na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri.” 

Unaweza kuona aidha katika nyakati za Biblia kama mtu anakupenda sana na kukuheshimu sana moja ya zawadi ya ngazi ya juu kabisa ambayo mtu anageweza kukupatia ilikuwa ni pamoja na ZERI angalia
Mwanzo 43:11 “Israeli, baba yao, akawaambia, Kama ndivyo, fanyeni hivi; twaeni tunu za nchi katika vyombo vyenu, mkamchukulie mtu huyo zawadi, ZERI kidogo, na asali kidogo, ubani, na manemane, na jozi, na lozi”.

Kwa nini Zeri ilikuwa bidhaa ya thamani na zawadi kubwa sana, Zeri ilikuwa na sifa ya kuponya majeraha yote ya mwili “recovering” na vidonda mbalimbali pia vikiwemo vidonda vya kuumwa na nyoka, aidha watu pia waliitumia zeri katika kuhifadhia mwili wa mwanadamu aliyekufa usioze, Hivyo kama dawa nyingine zote zingeshindwa kutibu jeraha la mtu ndipo sasa ili kuokoa maisha yake ilipaswa kuitafuta Zeri kwa vile hii ilijulikana kama dawa isiyoshindwa hata hivyo dawa hii ilikuwa ghali sana ingekugharimu kuuza vyote ulivyo navyo ili kutibiwa na wataalamu wa Gilead upate kupona. Dawa hii likuwa haishindwi kutibu jambo kama mtu anetibiwa na dawa zote na ikashindikana watu walimshauri aende Gilead kwa wataalamu kataumie Zer.

Yeremia 46:11Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.” 

Ni wazi kuwa kama mtu angetumia dawa bila mafanikio dawa ya mwisho ingekuwa Zeri ni zeri tu ndiyo ambayo ingeweza kutibu maumivu aliyoyapata mtu".

Yeremia 51:8Babeli umeanguka na kuangamia ghafula; mpigieni yowe; twaeni zeri kwa maumivu yake; ili labda apate kuponywa

Katika namna ya kushangaza sana hata hivyo yalikuweko magonjwa ambayo yalikuwa ahayasikii dawa yaani magonjwa sugu, ilipotokea kuwa mgonjwa haonyeshi badiliko, kila mara alionekana yuko vilevile hapati kugangwa lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kusikia Zeri imeshindwa au wataalamu wa Gilead wameshindwa, katika mstari wa Msingi Yeremia alikuwa anazungumzia tatizo la kiroho na tabia ya wana wa Israel ambao walishindwa kutubu na kubadilika kiasi cha kufikia ngazi ya kuhukumiwa na Mungu, Nabii alikuwa akiomboleza na kujiuliza kuwa dawa isiyoshindwa imekosekana? Matabibu wa Gilead hawako, Yeremia alikuwa anamaanisha kuweko kwa toba na manabii, Israel walishindwa kuwasikiliza manabii na pia walikosa moyo wa toba nJe hapana zeri katika Gilead? Na Matabibu maana naona afya ya watu wangu haijarejea?

Kimsingi zeri ya Gilead ilikuwa ghali sana na hata hivyo haikuweza kuponya majeraha mengine yaliyowasibu watu.

Marko 5:25-28Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya, aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona

Zeri ulikuwa ni mti halisi lakini vilevile ulikuwa ni picha ya Yesu Kristo, katika muujiza huu alioufanya Yesu ni dhahiri biblia inatuonyesha zeri kutoka mbinguni, inatuonyesha mwanaume mwenye uwezo wa kumfanya mtu akawa recovered akapona akawa kamili, unaweza kuhangaika huko na kule kwaajili ya mahitaji yako, kwaajili ya afya yako ya kimwili na kiroho, kwaajili ya majeraha ya moyo wako, kwaajili ya majeraha ya adui zako, kwaajili ya majeraha ya ndoa na kazini na shuleni na hata kanisani, unaweza kuangaika huku na kule kwaajili ya mahitaji yako ya aina mbalimbali lakini lao ninakutangazia kuwa iko dawa isiyoshindwa Dawa hii ni Yesu Kristo peke yake yeye anaweza yote kwake hakuna linaloshindikana ni dawa ya waliokata tamaa, dawa ya waliojeruhiwa na kudharaulika, ni dawa ya maisha yetu, feature yetu haiku mikononi mwa wanadamu, iko mikononi mwa Yesu tu, huyu ndio wa kumkimbilia, huyu ndio wa kumpapatikia, huyu ndio wa kumtazama kwa kila unalokaboliana nalo katika maisha katika masomo, katika ndoa, kazini nk. Mwangalie Yesu na utafanikiwa yeye ni zaidi ya zeri ya Gilead ni Zawadi ya upendo wa hali ya juu kutoka kwa Mungu baba 

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa Pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.

Na. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima

Maoni 5 :

Jeff alisema ...

Hongera sana na shukrani sana kwa naelezo mazuri kuhusu zeri. Ni jani ninalolifahamu ila sikujua kuwa ndio zeri. Asante sana. Geoffrey

Jeff alisema ...

Hongera sana na shukrani sana kwa naelezo mazuri kuhusu zeri. Ni jani ninalolifahamu ila sikujua kuwa ndio zeri. Asante sana. Jeff

Unknown alisema ...

Dah! Mwenyezi mungu akubaliki sana kwa kutoa dondoo za kibiblia nzuri

Bila jina alisema ...

Nahitaji mbegu za zeri.Namba ya simu 0658777269

Bila jina alisema ...

Ameen