Jumanne, 5 Februari 2019

“Ukialikwa na mtu Harusini ! ”

Mstari wa Msingi: Luka 14:7-11
 
Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema, Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe, akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya (AIBU) kushika mahali pa nyuma. Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.  Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”



Utangulizi:

Maandiko matakatifu yanatufundisha namna bora ya kuishi katika ulimwengu huu, na kupata mafanikio, moja ya njia iliyo bora zaidi ya kuishi maisha ya furaha na amani ni pamoja na kuishi maisha ya unyenyekevu, pamoja na kuwaheshimu watu wengine au watu wote, Maandiko yanasema katika.

 Wafilipi 2:3Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

Yesu Kristo katika kufundisha kwake alipenda sana kutumia mifano ya aina mbalimbali kwaajili ya kufundisha watu kuhusu ufalme wa Mungu, na ili watu waweze kuelewa alitumia story pamoja na matukio mbalimbali halisi yaliyotokea kuwafundisha watu maisha na ufahamu kuhusu utendaji wa Mungu na tabia zake ili waweze kuishi kwa amani, Ingawa Yesu alitumia mifano lakini mifano hii ilibeba maana kubwa sana na za kweli kuhusu maisha.

Katika kifungu cha Maandiko tunayosoma leo, Katika Luka 14, Yesu alikuwa amealikwa katika chakula cha jioni na moja ya maafisa wakubwa sana wa Mafarisayo, Watu wengine wengi sana walikuwepo au walialikwa pia, kulikuwa na watu muhimu wengi sana wastahiki na pia watu wengine wengi waliokuwa na nyadhifa mbalimbali  na wale ambao bila shaka walijifikiri kuwa ni wa muhimu sana, walipokuwa wakiingia Yesu alikuwa akifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea, wengi walikwenda kukaa moja kwa moja kwenye viti maalumu vya Meza kuu, hatujui nini kilitokea lakini Yesu alipata somo la kuwafundisha wanafunzi wake,  kwa kile kilichotokea kwani tunaweza kukiona japokuwa mwandishi hakukigusia wazi inawezekana wengi walikwenda kukaa mahali ambapo huenda hapakuwa pameandaliwa kwa ajili yao  na hivyo haikuwa sahihi kwao kukaa, na inawezekana baadaye walihamisha na kupelekwa katika viti vya kawaida na hawakujisikia vizuri, (Zamani hakukuwa na utaratibu wa kuweka majina mezani, Lakini aliyepanga viti na meza yaani mwenyeji ndiye aliyekuwa na jibu moyoni kuwa nani anastahili kukaa wapi). Yesu anatumia tukio hili kutufundisha jinsi njia ya unyenyekevu ilivyo ya muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku na zaidi sana katika ufalme wa Mungu.

Kuna nukuu nyingi sana duniani zinazotufundisha kuhusu umuhimu wa unyenyekevu na hapa nimechagua chache:-

Mtakatifu Augustino alisema “it was Pride that Changed the Angels to be devils and its humility that makes man as Angels” yaani “Ni kiburi kilichowafanya malaika kuwa pepo na ni unyenyekevu unaowafanya wanadamu kuwa kama malaika

Thomas Merton alisema “Pride makes us artificial and humility makes us really” kwamba “kiburi hutufanya kuwa fake na unyenyekevu hutufanya kuwa halisi

Rev. Innocent Kamote “Many ways may let people down, but have never ever seen humility letting someone down njia nyingi zinaweza kuwaangusha watu chini lakini sijawahi ona unyenyekevu ukiwaangusha mtu chini

Unaweza kuona Yesu anataka tuelewe kanuni za ufalme wa Mungu na kanuni za maisha haya, ni wazi kuwa mgeni hajui kuwa anapaswa kukaa katika kiti gani, ni lazima asubiri kukaribisha mwenyeji ndiye anayejua, Katika ufalme wa Mungu mwenyeji wetu ni Yesu, ni uhusiano wetu na mwenyeji wetu ndio utakaoamua kuwa ni kiti gani tutakalia, wako wengine wanajifikiri kuwa ni bora, kutokana na Dini zao, au madhehebu yao, au elimu zao, au kabila zao, au familia wanayotokea, au mkoa, au kutokana na huduma aliyo nayo, au kwa sababu anatumiwa sana na Mungu kufanya miujiza mikubwa, mtu anaweza akapiga hesabu zake kichwani mwake akajidhani kuwa yeye ni  wa muhimu kuliko wengine, Ni mwenyeji wetu Yesu ndiye ana mamlaka ya kuhamisha watu viti, anaweza kukuambia ndugu kakae mbele au anaweza kukuambia ndugu kakaye nyuma!

Mwanafunzi anapokwenda shuleni, anakuwa amekuja kujifunza, amekuja kukaa chjini ya walimu amekuja kufuata maelekezo, amekuja kufuata program zote za shule,  na hivyo wanafunzi wa aina hii hukubali kukaa chini ya walimu kwa unyenyekevu na kukubali kufundishika, wanakaa chini wanajifunza na kutafuta majibu ya maswala husika huku wakitii kila wanachoagizwa, Mwanafunzi yeyote ambaye anajidhani kuwa yuko smatter kuliko mwalimu wake, huwa na kiburi hawawezi kukubali kufuata maelekezo ya walimu wao wala program za shule na hatimaye matokeo yataeleza baadaye who is more smatter?

Yesu Kristo alikuwa ni mwana wa Mungu, lakini aliishi maisha ya unyenyekevu, alikuwa mtii alikubali kuelekezwa na alihukumiwa na alikubali kutii mpango wa Mungu na kumtii hata katika mauti ya msalaba ambayo ni mauti ya aibu sana kutokana na uwezo wake mkubwa wa unyenyekevu Mungu amemuadhimisha mno.


Wafilipi 2:4-11 “Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba

Ili Mungu atuinue na kutuheshimu katika kanuni za ufalme wa Mungu njia ya kuwa wa muhimu sana ni kujishusha sana, njia ya kupanda juu sana ni kuwa mnyenyekevu sana ukikumbuka kuwa kuwa mnyenyekevu hakumaanishi kuwa wewe ni mjinga bali ni hekima ya Mungu ya hali ya juu ni njia ambayo Yesu aliichagua katika maisha na akatuachia kielelezo tuifuate kwani ina mafanikio makubwa sana.

Zaburi 138: 6 “Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

Mithali 18:12 “Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.”

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.

Aidha Yesu alikuwa anataka tujifunze kuwaheshimu wengine na kutambua uweza wa wengine, mwaka 18th April 1980 ilikuwa nisiku ya Zimbabwe kupata uhuru wake kutoka kwa Muingereza, katika siku hiyo walialikwa wageni maarufu kabisa duniani akiwemo Rais maarufu wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mambo mengine, Zimbabwe ilimualika Mwanamziki maarufu wa muziki wa Regge duniani 

Robert Nesta "Bob" Marley (6 Februari 1945 - 11 Mei 1981) yaye alikuwa mwimbaji na mwanamuziki muhimu kutoka nchini Jamaika. Alivuma hasa kunako miaka ya 1970 na 1980.  Ambaye ameweza kuifanya staili ya muziki wa reggae kuwa maarufu sana duniani. Muziki wake mwingi ulikuwa unazungumzia dini ya Rastafari ambayo yeye alikuwa anaifuata. Kuna baadhi ya nyimbo zake zinahusu masuala ya dini na zingine siasa.

Katika wakati wa kusalimiana Mwalimu Julius Nyerere alipopeana mkono na mwanamuzik Bob Marley hakuwa amependezwa naye kwani alionekana kuwa mtu rafu asiyekata nyele zake na kama mvuta bangi hivi, lakini katika wakati Mwanamuziki huyo alipotumbuiza ndipo mwalimu Nyerere alipokwenda kumkumbatia na kumkubali mwanamziki huyo kutokana na nyimbo zake nzuri zenye kuhamasisha fikra za kiukombozi wimbo mojawapo muhimu ulikuwa ni pamoja na wimbo kuhusu Zimbabwe ambao ulikuwa na maneno yenye hamasa ya hali ya juu, yaliyodhihirisha kuwa Bob alikuwa msanii mahiri mwana mapinduzi aliyeipenda afrika kwa dhati kutoka Moyoni.

Every man gotta right to decide his own destiny
And in this judgment there is no partiality
So arm in arms, with arms
We'll fight this little struggle
'Cause that's the only way
We can overcome our little trouble

No more internal power struggle
We come together to overcome the little trouble
Soon we'll find out who is the real revolutionary
'Cause I don't want my people to be contrary

To divide and rule could only tear us apart
In everyman chest, there beats a heart
So soon we'll find out who is the real revolutionary
And I don't want my people to be tricked by mercenaries

Maneno haya na uwezo mkubwa alioonyesha mwanamuziki huyo ulimfanya Mwalimu Julius Nyerere amualike Bob Marley kuitembelea Tanzania lakini kabla ya kuitembelea Tanzania Bob alifariki kwa ugunjwa wa Kansa ambapo May 11 1981 alifariki Dunia, Bob alipowasili Zimbabwe alitumia ndege ya Boeing 777 na vyombo vyake vya music vilikuwa na uzito wa tani 21. 

Kila mwanadamu Dunainai ana kitu cha ziada ndani yake na kwa sababuhiyo tunapaswa kuwaheshimu wenzetu na kutambua kuwa wana umuhimu mkubwa duniani kulinga ana nafasi zao

Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.

Hakuna maoni: