Jumatatu, 24 Mei 2021

Mtu wa kumwangali


Zaburi 37:37 “Umwangalie sana mtu mkamilifu, Umtazame mtu mnyofu, Maana mwisho wake mtu huyo ni amani.

 

Utangulizi:

 

Moja ya njia ya kujihakikishia kuwa tunasonga mbele katika safari ya imani, ni pamoja na kuhakikisha kuwa tunasahau yaliyo nyuma na kuyachuchumilia yaliyo mbele, Hii ilikuwa njia mojawapo ya mafanikio kwa Mtume Paulo ona

 

Wafilipi 3:12-13 “Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;”

 

ukimuuliza mtu ni nani anaweza kuwa mtu wako wa mfano au shujaa wako, kila mmoja anaweza kuwa na watu kadhaa ambao anavutiwa nao na anawaiga kiimani, Binafsi katika maswala ya imani navutiwa sana na Bishop Zachary Kakobe kwa kuwa ndiye aliyekuwa Mchungaji wangu wa kwanza mara baada ya kuokoka niliokokea katika kanisa lake nilipoikuwa nasima Makongo Secondary Jijini Dar, Lakini pia navutiwa sana na mafundisho ya Muhubiri Mwalimu kutoka Ghana anayeitwa Mensa Otabil napenda anavyofundisha neno la Mungu, naweza kuwa na watu wa mifano katika siasa, uongozi, watumishi na kadhalika Katika Biblia ukimuacha Yesu Kristo navutiwa sana na Paulo Mtume katika agano jipya na Daudi katika agano la kale, watu tunaowafanya kuwa mfano wetu wa kuigwa, huwa tunawaiga imani zao na kuwafuata kama vile wanavyomfuata Yesu Kristo, kuwakumbuka wale waliotuongoza, waliotuambie neon la Mungu ni agizo la kibiblia ona

 

Waebrania 13:7 “Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.”    

 

Hata hivyo maandiko yanatuasa pia kuwafuata wao na kuwaiga wao kama vile wanavyomfuata Kristo kwa sababu wao ni wanadamu

 

1Wakoritho 11:1Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.” Wanadamu wote katika maandiko ambao tunaweza kuvutiwa nao na wakawa mifano kwetu walikuwa na mambo mengi na sifa nyingi njema lakini vilevile walikuwa na madhaifu ya aina mbalimbali ya kibinadamu kwa mfano:-

 

1.       Adamu na Eva – Ndio wazazi wetu wa kwanza, hawakuzaliwa waliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, walikuwa na ushirika wa karibu na Mungu wakizungumza naye usokwa uso, Mungu alikuwa muumba kwao na baba kwao, aliwadekeza na kuwamilikisha kila walichokitaka. Walipewa mamlaka mna utawqala dhidi ya kila kitu Duniani, wanyama waliwaogopa, hata hivyo walimkaidi Mungu na kumuasi kwa kula matunda waliokatazwa na Mungu,  wakawa sababu ya kuleta kifo na mauti duniani, leo hii wote tunapata tatizo la kifo kwa sababu yao ona:-

 

Mwanzo 3:11-13 “Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala. BWANA Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.

 

2.       Nuhu aliyetajwa kuwa mtu wa haki mkamilifu katika vizazi vyake na kwamba alikwenda au kutembea pamoja na Mungu na katika ulimwengu uliokuwa umeoza kwa uovu yeye pekee na familia yake walipata neema Machoni pa Bwana ona

 

Mwanzo 6:8-9Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA.Hivi ndivyo vizazi vya Nuhu. Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.Pamoja na ukamilifu wake wote baadaye maandiko yanatutaarifu kuwa ndiye mgunduzi wa kwanza wa Pombe na ndiye mtu wa kwanza kujihushisha na ulevi na sio hivyo tu alikunywa divai akalewa  na kusababisha aibu kubwa

 

Mwanzo 9:20-22 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.”

 

3.       Ibrahimu anayetajwa kuwa baba wa imani na rafiki wa Mungu, Baada ya miaka mingi sana ya ukimya tangu Mungu alipozungumza na Nuhu, hakuwa amezungumza na mwanadamu awaye yote kwa Karne nyingi sana mpaka alipozungumza na Abrahamu na kufanya maaganio naye Ibrahimu anaitwa mtu wa kwanza kuwa na uhusiano na Mungu aliye hai baada ya karne nyingi, Ni baba wa imani kwelikweli Imani ya kiyahudi na Kikristo na Uislamu zinaitwa Abrahamic Religions yaani ni imani ambazo mizizi yake imeanzia kwa Ibrahimu Warumi 4;16 “Kwa hiyo ilitoka katika imani, iwe kwa njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazao wote; si kwa wale wa torati tu, ila na kwa wale wa imani ya Ibrahimu; aliye baba yetu sisi sote; Mungu alikuwa na urafiki wa Karibu na Ibrahimu kwatika ushirika wa ajabu sana kiasi cha kumuita rafiki yake ona Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;” Lakini hata hivyo maandiko yanatutaarifu kuwa yeye alisema uongo zaidi ya mara moja, kwa sababu ya woga na kutokumuamini Mungu kwaajili ya ulinzi wake,

 

Mwanzo 12:18-19 “Ndipo Farao akamwita Abramu, akasema, N'nini hili ulilonitendea? Mbona hukuniambia ya kuwa huyo ni mkeo? Mbona ulisema, Huyo ni umbu langu, hata nikamtwaa kuwa mke wangu? Basi sasa, huyo mke wako umchukue, uende zako.”

 

Mwanzo 20:1-5 “Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari. Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara. Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu. Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee BWANA, Je! Utaua hata taifa lenye haki? Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi. 


Isaka na Yakobo wanaotajwa na Mungu pale anaposema mimi ni Mungu wa Ibrahimu Isaka na Yakobo 


Kutoka 3:15-16 “Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, BWANA, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, BWANA, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea, akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri; wote tunafahamu kuwa Isaka alisema uongo vilevile Mwanzo 26:6-7 “Isaka akakaa katika Gerari. Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso.Yakobo ndiye aliyekuwa muongo zaidi na mwenye hila zaidi akijifanya kuwa ni Esau na wanawe pia walimdanganya kuhusiana na habari za Yusufu kuwa aliuawa na mnyama ilhali walimuuza kwa hiyo hawa wote walikuwa ni wanadamu na walikuwa na udhaifu wao!

               

4.       Musa anayetajwa kuwa mpole au mnyenyekevu kuliko watu woote wakaao juu ya uso wa nchi Ona katika Hesabu 12;3 “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.” Biblia inatuambia kuwa Musa ndiye aliyekuwa mtu mpole, myenyekevu kuliko watu wiote wakliokuwa juu ya uso wanchiyeye naye kuna wakati alikasirika sana na kunena Maneno yasiyotegemewa na hata hatimaye kushindwa kumstahi Mungu pale Meriba jambo lililomkosesha kuingia katika nchi ya Kanaani, Hesabu 20:10 “Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?             

 

 Kumbukumbu 3;23-26 “Nikamnyenyekea Bwana wakati huo, nikamwambia, Ee Bwana Mungu, umeanza kumwonyesha mtumishi wako ukubwa wako, na mkono wako wa nguvu; kwani kuna mungu gani mbinguni au duniani awezaye kufanya mfano wa kazi zako, na mfano wa matendo yako yenye nguvu? Nami nakuomba nivuke, nikaione hiyo nchi nzuri iliyoko ng'ambo ya Jordani, mlima ule mzuri, na Lebanoni. Lakini Bwana alikuwa amenikasirikia kwa ajili yenu, asinisikize; Bwana akaniambia, Na ikutoshe, usinene nami zaidi jambo hili.”      

5.       Daudi mtu anayetajwa na Mungu kuwa ni mtu aliyeupendeza moyo wake, Matendo 13;21-22 “Hatimaye wakaomba kupewa mfalme; Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila ya Benyamini, kwa muda wa miaka arobaini. Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.” Wote tunafahamu ushujaa wa Daudi, mtu aiyependa uonevu, mtu mwenye kumcha Mungu, kiongozi mkuu sana wa ibada lakini maandiko nayo yanasema yeye naye alifanya dhambi ya zinaa na mke wa Uria, alimpa na mimba, alimuua na mumewe kisha akajioza yeye mke huyu wa uria ona 2Samuel 11;2-5 “Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti? Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake. Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito., 


    2Samuel 14-27Hata ikawa asubuhi, Daudi akamwandikia Yoabu waraka, akaupeleka kwa mkono wa Uria. Akaandika katika waraka huo, kusema, Mwekeni Uria mbele ya watu penye vita vikali, kisha ondokeni, mmwache, ili apigwe akafe. Ikawa, Yoabu alipokuwa akiuhusuru mji, akamweka Uria mahali alipojua ya kuwa pana mashujaa.Watu wa mji wakatoka, wakapigana na Yoabu; na baadhi ya watu, watumishi wa Daudi, wakaanguka; Uria Mhiti naye akafa. Ndipo Yoabu akapeleka na kumwarifu Daudi habari zote za vita; akamwagiza yule mjumbe, akisema, Ukiisha kumpa mfalme habari zote za vita, itakuwa, hasira ya mfalme ikiwaka, akakuambia, Kwani mliukaribia mji namna ile ili kuupiga? Je! Hamkujua ya kuwa watapiga mishale toka ukutani? Ni nani aliyempiga Ahimeleki, mwana wa Yeru-beshethi? Je! Si mwanamke aliyemtupia jiwe la kusagia la juu kutoka ukutani? Hata akafa huko Thebesi? Kwani kuukaribia ukuta namna ile? Ndipo utakaposema, Mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa naye. Basi yule mjumbe akaenda, akafika na kumwonyesha Daudi yote aliyomtuma Yoabu. Yule mjumbe akamwambia Daudi, Watu hao walitushinda, wakatutokea nje hata uwandani, tukashindana nao hata mahali pa kuingilia langoni. Wapiga mishale wakatupiga sisi, watumishi wako, toka juu ya ukuta; na baadhi ya watumishi wa mfalme wamekufa, na Uria, Mhiti, mtumishi wako, amekufa naye. Basi Daudi akamwambia yule mjumbe, Basi, mwambie Yoabu maneno haya, Jambo hili lisiwe baya machoni pako, maana upanga hula huyu kama unavyomla huyu; zidi kutia nguvu vita vyako juu ya mji ukauangushe; nawe mtie moyo. Na yule mke wa Uria alipopata habari ya kuwa Uria mumewe amekufa, akamwombolezea mumewe. Hata maombolezo hayo yalipokwisha, Daudi akatuma mtu, akamtwaa, akamtia nyumbani mwake; naye akawa mkewe, akamzalia mwana. Lakini jambo lile alilolitenda Daudi likamchukiza Bwana.”  

6.       Suleimani alikuwa mwenye Hekima kuliko watu wote, aliwaonya watu wajiepushe na maswala mbalimbali ya uovu katika kitabu cha mithali, lakini pia aliwataka watu wamkumbuke Mungu tangu siku za ujana wao, Mungu alizungumza na Suleimani wazi wazi, na kumtaka aombe lolote, alikuwa mtoaji kwa rekodi ambazo hazijawahi kuvunjwa 1Falme 4;29-34 “Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani. Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri. Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka. Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano. Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki. Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake.” lakini aliangukia katika tamaa ya wanawake iliyokuwa ya kutisha sana akaoa wanawake wengi sana na wanawake zake wakamgeuza moyo akaabudu miungu ona 1Wafalme 11;1-4Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo. Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake              

7.       Mtume Petro alikuwa mtu wa kwanza kudai kuwa yuko tayari kwenda na Bwana Yesu gerezani na aliapa luwa hatamkana Yesu kamwe! Mathayo 26:31-33 “Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe.” Petro aliahidi mbele za Yesu kuwa yeye atakuwa tayari hata kwenda naye gerezani lakini wakati wa majaribu Petro alimkana Yesu mara tatu ona Mathayo 26:69-75 “Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya. Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo. Naye alipotoka nje hata ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti. Akakana tena kwa kiapo, Simjui mtu huyu.Punde kidogo, wale waliohudhuria wakamwendea, wakamwambia Petro, Hakika wewe nawe u mmoja wao; kwa sababu hata usemi wako wakutambulisha. Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara akawika jogoo.Petro akalikumbuka lile neno la Yesu alilolisema, Kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Akatoka nje, akalia kwa majonzi.

 

Nini cha kujifunza?

 

Sisi wote ni wanadamu tu, manabii na mitume nao ni wanadamu, wachungaji walimu , wazee mashemasi na washirika wote ni wanadamu tu, katika namna fulanifulani za uanadamu wetu tunajikwaa Yakobo ambaye alikuwa mtume na askofu mkuu wa kanisa lililokuwako Yerusalem Ndugu yake Yesu wa kunyonya aliyeitwa James the Just alikuwa muombaji na mtu wa haki alisema katika Yakobo 3:2 “Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. Sisi sote kama binadamu tunajikwaa katika mambo mengi hakuna mwanadamu aliyemkamilifu, Mungu hututumia kwa sababu ya mambo mazuri ya upande wa jambo zuri analotaka kulitimiza kwetulakini kama Mungu angelikuwa anaangalia ukamilifu wetu hakuna amabaye angeweza kusimama mbele zake sio Musa wewe wala mimi, tunapoona madhaifu kadhaa wa kadhaa kwa viongozi wa kidini, tunapaswa kukumbuka kuwa wao sio kielelezo chetu, wao ni binadamu tu, udhaifu wao hauondoi ukweli kuwa wokovu upo, Mungu anaokoa, na kielelezo chetu ntulichopewa kukifuata ni Yesu Kristo pekee, wao walitolewa ili kutumia vipawa walivyopewa na Mungu kutuelekeza kwa Kristo Waefeso 4:11-13 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye CHEO CHA KIMO CHA UTIMILIFU WA KRISTO;” Yesu Kristo ndiye Mwanzilishi wa imani yetu, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunamfuata yeye katika mwenendo wetu wote Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.” Maandiko yanatutaka tumtazame yeye kwa sababu yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote bila kufanya dhambi ona Waebrania 4:15 “Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.” Imani yetu haisimami kwa mtu inasimama katika Kristo Yesu, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaacha kuwaangalia wanadamu na kumtazama mtu mkamilifu ambaye mwisho wake utatupa amani, Ni Yesu pekeee aliye mkamilifum, ni Yesu pekee aliye kielelezo chetu, tutawafuata wengine na kujifunza kutoka kwao kama vile wanavyomfuata Yesu lakini wakikengeuka haiwi sababu ya sisi kulaumu, au kuacha wokovu au kurudi nyuma kwa sababu Yesu hajawahi kurudi nyuma, acha kuwatazama wanadamu mtazame Yesu, mtazame Yesu Kristo wa Nazareth aliye hai acha kuwashutumu wanadamu, acha kuwaangalia wao, wao ni watu tu tunaye kuhani mkuu aliyejaribiwa katika mambo yote bila kufanya dhambi, Baba mtakatifu he is not our hero he is not our rolemode, askofu mkuu, wa jimbo waangalizia, mapadri na mashemasi na kdahalika wao sio kielelelzo chetu Yesu Kristo pekeee ndio kielelezo chetu kikuuu, yeye ndiye aliyetuita tumfuate 1Petro 1:15-16 “bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.” Never compromise becase someone somewhere sheor he has compromise he/she is not our example our real example is Jesus Christ the son of the living God!

 

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!.

Hakuna maoni: