Jumapili, 9 Mei 2021

Wewe u mwana wa mwanamke mwingine!

Waamuzi 11:1-2 “Basi huyo Yeftha, Mgileadi, alikuwa mtu shujaa sana, naye alikuwa ni mwana wa mwanamke kahaba; Gileadi akamzaa Yeftha. Mkewe huyo Gileadi akamzalia wana; na hao wana wa mkewe hapo walipokuwa wamekua wakubwa wakamtoa Yeftha, na kumwambia, Wewe hutarithi katika nyumba ya babaetu; kwa sababu wewe u mwana wa mwanamke mwingine.”



Utangulizi:


Wewe u mwana wa mwanamke mwingine! Yalikuwa ni maneno ya kukatisha tamaa yaliyotolewa kwa kijana shujaa aliyejulikana kama Yeftha, Mwandishi wa kitabu cha Waebrania katika agano Jipya anamtaja kama mojawapo wa mashujaa wa imani ona Waebrania 11:32-34Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.”

Yeftha ni moja ya waamuzi wakubwa miongoni mwa waamuzi wanaotajwa katika Biblia, waamuzi walikuwa ni viongozi wa mpito waliotumiwa na Mungu, kuwasaidia Israel walipokuwa hawana mfalme tangu kufa kwa Yoshua mpaka kupakwa mafuta kwa mfalme wa Kwanza aliyeitwa Sauli, Jina Yeftha maana yake ni ni Bwana atafanya njia, au Bwana atafungua.

Yeftha alikataliwa na ndugu zake, baada ya kifo cha baba yake kwa sababu eti alizaliwa na mwanamke Kahaba, sababu hii inawezekana kabisa ilitokana na sifa zake kuwa alikuwa mtu mwema tene mwenye ujuzi kuhusu Mungu na hodari sana, alikuwa ni shujaa, kuzaliwa kwake na mwanamke kahaba haikuwa sababu yay eye kukata tama katika maisha yake, alijiendeleza kitabia na kuwa mtoto mwema sana kuliko wenzake kwa wivu walimkataa kwa maneno mabaya ya ubaguzi kuwa yeye ni mwana wa mwanamke mwingine hii haikuwa sababu ya kumzuia Yeftha ambae aliamua kwenda kuishi katika mji mwingine ulioitwa Tobu, watu wote hohehahe walimkusanyikia na kuishi Pamoja naye,  Israel walipoonewa na wana wa Ammoni na kuteswa vibaya walimkumbuka Yeftha na wakatuma wazee kumuomba Yeftha aje kuwa shujaa wao, naye kwa neema ya Mungu akijazwa Roho Mtakatifu, na kuonyesha ujuzi wake katika Torati na historia ya wana wa Israel alikubali kuja na kuwatetea na kuwaokoa dhidi ya wana wa Amoni ona


Waamuzi 11:4-11 “Ikawa baadaye, wana wa Amoni wakapigana na Israeli. Ikatukia, hapo wana wa Amoni walipopigana na Israeli, wazee wa Gileadi wakaenda kumtwaa huyo Yeftha katika ile nchi ya Tobu; wakamwambia Yeftha, Njoo wewe uwe kichwa chetu, ili tupate kupigana na wana wa Amoni. Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, Je! Ninyi hamkunichukia mimi na kunifukuza nitoke katika nyumba ya baba yangu? Basi kwani kunijilia hivi sasa wakati mlio katika taabu?  Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Kwa ajili ya hayo sasa tumegeuka kukuelekea wewe tena, ili uende pamoja nasi na kupigana na wana wa Amoni, nawe utakuwa kichwa chetu juu ya wenyeji wote wa Gileadi. Basi Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi Kwamba mwanirejeza kwetu tena ili kupigana na wana wa Amoni, naye Bwana akiwatoa mbele yangu, je! Mimi nitakuwa kichwa chenu? Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Yeye Bwana atakuwa shahidi kati yetu; hakika yetu tutafanya sawasawa na neno lako. Ndipo Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na hao watu wakamfanya awe kichwa, tena mkuu, juu yao; naye Yeftha akanena maneno yake yote mbele ya Bwana huko Mispa.”


Licha ya kufanywa kiongozi na mwamuzi wa Israel ni wazi kuwa Yefhta aliijua sharia alitenda haki na hata vita yake na namna alivyokuwa anajenga hoja alijenga kwa haki, akiitumia torati, Yeftha hakuwa na makosa ni baba yaka ndiye aliyezaa na mwanamke kahaba, lakini kigezo hiki cha kilitumiwa na ndugu zake kumkataa na kumbagua, huenda jambo hili pia liliingiliwa na wazee kwa kuwa katika Israel maamuzi yasingelifanyika bila wazee kuingilia kati wote wakiwa wametiwa upofu na wivu tu, uwezo wa Yeftha katika kulijua neno la Mungu unaonekana wazi kwa hoja anazozijenga dhidi ya mfalme wa wana wa Amoni kabla hajampa mkon’goto ona

Waamuzi 11:11-28 “Ndipo Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na hao watu wakamfanya awe kichwa, tena mkuu, juu yao; naye Yeftha akanena maneno yake yote mbele ya Bwana huko Mispa. Basi Yeftha akatuma wajumbe waende kwa mfalme wa wana wa Amoni akasema, Je! Wewe una nini nami, hata umenijilia kupigana juu ya nchi yangu? Mfalme wa wana wa Amoni akawajibu hao wajumbe wa Yeftha Kwa sababu Israeli waliitwaa nchi yangu, hapo walipokwea kutoka katika nchi ya Misri, tokea Arnoni mpaka Yaboki, na hata Yordani; basi sasa rudisha hizo nchi tena pasipo matata. Yeftha akatuma wajumbe mara ya pili waende kwa huyo mfalme wa wana wa Amoni; akamwambia, Yeftha akuambia hivi; Israeli hakuitwaa nchi ya Moabu, wala nchi ya wana wa Amoni; lakini hapo walipokwea kutoka Misri, na Israeli walienenda katika bara hata kuifikilia Bahari ya Shamu, na kufikilia Kadeshi; ndipo Israeli wakatuma wajumbe waende kwa mfalme wa Edomu, wakisema, Nakuomba sana unipe ruhusa nipite katika nchi yako; lakini mfalme wa Edomu hakusikia. Ni vivyo wakampelekea wajumbe mfalme wa Moabu; wala yeye hakukubali; basi Israeli wakakaa katika Kadeshi. Kisha akaenda nyikani na kuizunguka hiyo nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu, nao wakapita upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga marago upande wa pili wa Arnoni; wala hawakuingia ndani ya mpaka wa Moabu, kwa maana Arnoni ilikuwa ni mpaka wa Moabu. Kisha Israeli wakatuma wajumbe waende kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni: Israeli wakamwambia, Twakuomba utupe ruhusa tupite katika nchi yako, mpaka mahali pangu. Lakini huyo Sihoni hakuwaamini Israeli ili wapite ndani ya mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, nao wakapanga kambi katika Yahasa, wakapigana na Israeli. Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawapiga; basi Israeli wakaimiliki hiyo nchi ya Waamori, wenye kukaa nchi hiyo. Nao wakaumiliki mpaka wote wa Waamori, tokea Arnoni hata Yaboki, tokea hiyo bara hata Yordani. Basi sasa yeye Bwana, Mungu wa Israeli, amewapokonya Waamori watoke mbele ya watu wake Israeli, na wewe wataka kuwatamalaki? Je! Wewe hutakitamalaki hicho ambacho huyo Kemoshi mungu wako akupa kukitamalaki? Kadhalika, awaye yote ambaye Bwana, Mungu wetu, amemfukuza atoke mbele yetu hao ndio tutakaowatamalaki. Na wewe sasa, je! U mwema kuliko Balaki mwana wa Sipori, huyo mfalme wa Moabu, kwa lo lote? Je! Yeye alishindana na Israeli, au kupigana nao? Wakati Israeli waliokuwa wakikaa Heshboni na miji yake, na katika Aroeri na miji yake, na katika miji hiyo yote iliyo huko kando ya Arnoni, muda wa miaka mia tatu; mbona ninyi hamkuipata tena katika majira hayo? Basi mimi sikukufanyia wewe dhambi, lakini wewe unanitenda uovu kwa kupigana nami; yeye Bwana, yeye Mwamuzi, na awe mwamuzi hivi leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni. Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea.”



inaonyesha wazi jinsi alivyokuwa mtu wa haki na mwenye ujuzi wa neno la Mungu, Mungu alimjaza kwa Roho wake na kusikiliza dua yake na maombi yake akamuwezesha kuwaokowa wana wa Israel kwa kuwapiga wana wa amoni ona 


Waamuzi 11:29-33 “Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni. Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli, ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa. Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake. Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli.”


Ni dhahiri kuwa Yeftha alikuwa amekubalika na Mungu, sio lazima wakati wote tukubalike kwa wanadamu, lakini Mungu akikukubali na kuweka mkono wake lazima mlango uliofungwa na wanadamu utafunguliwa tu , lazima bwana atafanya njia, Kujitoa kwa Yeftha kwa Mungu na uaminifu wake kwa Mungu hakujawahi kufikiwa na myahudi wala mkristo awaye yote yeye ni mtuwa pekee aliyeweka nadhiri ngumu sana na kuitimiza, japokuwa kuna mgogoro mubwa wa kimjadala kuhusu Nadhiri yake, lakini ni ukweli usiopingika kuwa mwana huyu wa kahaba, mtoto wa mwanamke mwingine alikuwa vizuri kwa Mungu wake kuliko wana wengine, Ni kitu gani tunaweza kujifunza kutoka kwake ni kuwa hatupaswi kukata tama katika maisha,  kila kikwazo katika maisha yetu tunaweza kukitumia kuwa nafasi ya kipekee kutupeleka katika hatua nyingine:- Hatupaswi kukatishwa tamaa na jambo lolote!


Mwanzilishi wa Kampuni ya kutengeneza injini za aina mbalimbali ikiwemo magari, pikipiki, jenereta na mashine za pump za kumwagilia na kuoshea magari Chini Japan aliyejulikana kama SOICHIRO HONDA alizaliwa mwaka 17 November 1906  na alifariki mwaka 5 August 1991 akiwa na miaka 84 Kampuni yake iliitwa Honda Motor Company ltd. Aliondoka nyumbani akiwa na miaka 15 tu na akaanza kuwa fundi wa kutengeneza magari na kuuza vifaa nya magari vilivyotumika, alikuwa nimmtu mchapakazi sana na alipenda sana magari, na kutamani kuwa fundi wa kuyatengeneza, lakini hata hivyo alikataliwa kwa sababu na mambo yalikuwa magumu kwa sababu hakuwa na Elimu yeyote, wenzake walimpa kazi ya kuwapikia chakula na kusafisha duka la spea za magari. Aliamua kujiendeleza mwenyewe ili kuendeleza kipawa chake alijiunga na timu ya mbio za magari, lakini wakati Fulani alianguka na kupata ajali ambayo ilimjeruhi mwili wake na hakuweza kuendelea tena,  na akaachana na swala la mbio za magari, Baada ya kupona Soichiro alianza kutengeneza Piston rings kwa uwezo wake, alizipeleka kwa kampuni ya TOYOTA ili awauzie, lakini walimfukuzilia mbali kwa aibu, walikataa kabia uvumbuzi wake wakisema ni wa hali ya chini, kukataliwa kwake hakukumfanya ake chini aliendelea kukazana na kuamua kuanzisha kiwanda chake hatimaye aliweza, leo hii ndio mtu mwenye pikipiki imara sana kuliko aina nyingine ya pikipiki duniani.

Mungu hamtupi mja wake, Hijalishi umetiokea katika ukoo gani, au jamii gani au una historia mbaya kiasi gani, wala haijalishi watu wanasema nini juu yako, jambo kubwa la kuuliangalia ni Mungu anasema nini juu yako, tunaweza kupitia katika hali ya kukataliwa, Lakini hilo lisitutishe tumpe Mungu nafasi ya kutuonyesha nini kiko mbele yetu, Na kwa neema na uweza wa Roho Mtakatifu Bwana atakufanya uwe kimbilio la Ndugu zako na jamaa zako wote walipokupuuzia  na kukudharau watakuja wakuinamie kumbuka jiwe walilolikataa waashi hilo limekuwa jiwe kuu la msingi Yeftha aliambiwa wewe u mwana wa mwanmke mwingine, ni kama wanamwambia wewe sio ndugu yetu halisi, lakini baadaye walikwenda kumuhitaji na kuhitaji msaada wake!


Na Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.



Hakuna maoni: