Jumamosi, 30 Oktoba 2021

Chuma hunoa chuma!

Mithali 27:17 “Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake


Utangulizi:

Chuma hunoa chuma ni moja ya andiko maarufu na lenye hekima sana katika utumishi tulioitiwa hapa duniani, biblia ya Kiswahili inatumia neno chuma hunoa chuma ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake lakini katika kiingereza andiko hilo linasomeka “As Iron sharpens Iron, so one person sharpens another”, kwa hiyo tungeweza kusema hivi kwa lugha ya Kiswahili changu kama chuma kinavyonoa chuma ndivyo ilivyo kwa kila mtu na jirani yake.

Usemi huu unatusaidia kujitambua kuwa tunategemeana na hakuna mtu anaweza kutoboa peke yake, yaani ili kwamba wewe uweze kuwa mtu mwema zaidi, unaweza kuwa mzuri zaidi kwa kuwafanya wengine kuwa wazuri zaidi.  Au unaweza kuwa mzuri zaidi kwa kujifunza kutoka kwa wengine, sisi peke yetu hatutoshi, lakini tuko hivi tulivyo kwa sababu tulijifunza kutoka kwa wengine, tulikubali kuongozwa, na tulipokea hekima na maonyo kutoka kwa wengine, Biblia inasema enenda pamoja na wenye hekima nawe utakuwa na hiyo hekima! Ona

Mithali 13:20Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.”

Chuma kunoa chuma katika hali ya kawaida maana yake kuna manufaa ya ajabu sana inapotokea vyuma vikasuguana kwa pamoja, inatengeneza makali ambayo yana uwezo mkubwa sana wa kukata kitu kwa urahisi, chuma kinaweza kubaki na makali yake ya kawaida, na kikapoteza ufanisi au kubaki hali ileile kwa utendaji uleule au kuwa butu, lakini kinaponolewa  au kugongwa na chuma kingine kinakuwa tofauti kabisa, kwa msingi huo kwa kadiri chuma hicho kinavyozidi kunolewa au kugongwa au kufuliwa ndio kinavyozidi kuwa na makali zaidi, chuma hunoa chuma humaanisha au inamaanisha ni kumchonga mtu kitabia, mwenendo, maisha, kitaaluma, kihekima, uzoefu na kadhalika, kwa msingi huo kunakuwa na faida pande zote mbili na matokeo yake ni kuwa pande zote mbili huwa kali na hatimaye wote hufanya vizuri katika kazi zao, kama ni kukatua au kukata vitu vipande vipande.  Au kufanikisha wajibu ule uliokusudiwa na mwenye chuma. Mwanadamu hakuumbwa awe peke yake tunasema kwa kiingereza “human being is a social being” kwa hiyo tunahitajiana katika mazingira mbalimbali ili tuweze kufika

Mwanzo 2:18 “BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Wataalamu wa Elimu ya jamii katika ukristo Christian sociology wanakubaliana kuwa andiko hilo licha ya kuwa kwaasili lilimuhusu Adam na Eva, lakini kwa upana linahusu ile hali ya mty kuwa peke yake haikuwa njema katika uumbaji wa Mungu, na kuwa Mungu aliona kuwa mtu anahitaji watu, wenzake wengine, na ndio maana aliwabariki ili waongezeke na kuitawala Dunia so its absolutely that human being is a social being

Na ndio maana nyakati za kanisa la kwanza walionywa kutokuacha kukusanyika ili watu waendelee kuonyana kwa kadiri siku ile ilivyokuwa inakaribia, tunaweza kusali peke yetum, tunaweza kumuabudu Munghu tukiwa wenyewe lakini kwanini tunahitaji kwenda ibadani kwanini tunahitaji kujumuika na wenzetu katika ibada kwa sababu tunahitajiana pia hata kama tumeokolewa

 Waebrania 10:24-25 “tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.”

Kwa msingi huo basi jni wazi kuwa usemi huu chuma hunoa chuma unamaana pana sana kwetu na kwa jamii nzima na kuna mambo mengi mno ya kujifunza tunayoweza kuyapata kutokana na usemi huu kama ifuatavyo:-

1.       Chuma hunoa chuma ni usemi unaotufundisha kuwa na umoja

 

Tumeona kuwa usemi unasema chuma hunoa chuma ina maana ya pia mtu wa aina Fulani anaweza kumsaidia au kusaidiwa au kusaidiana na mwingine kuwa wa aina Fulani kwa hiyo kanuni hii ya biblia inatufundisha nguvu ya umoja katika kanuni za kiroho umoja una nguvu sana, biblia inaeleza wazi kuwa umoja ni wa thamani sana popote pale unapotaka mafanikio kama ni ya kitaasisi au serikali au taifa lazima kwanza watu wawe na umoja hilo ni la msingi sana.

 

Muhubiri 4:9-10 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

 

Maandiko yanaonyesha kuwa ni afadhali au ni heri kuwa wawili kwa sababu kuna kuinuliwa kuliko mtu akiwa peke yake, lakini kazi yao pia huwa kubwa kuliko kazi ya mtu mmoja sio hivyo tu, watu wapoomba wakiwa wawili au watatu Mungu hufanya au hujibu maombi yao kwa urahisi zaidi kwa msingi huo umoja au kuwa zaidi ya mmoja kuna uwepesi unaoweza kupatikana kwa kusaidiana na kwa kutegemeana na kwa kuwekana sawa na kuna faida kubwa sana za kimwili, kiroho, kiuchumi, kisaikolojia, kisiasa, na kijamaa na kadhalika

 

Mathayo 18:19-20 “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

 

Maombi ya watu wawili waliopatana yana nguvu kubwa sana na Mungu huyajibu lakini sio hivyo tu Mungu anakuwepo katikati ya watu wanapokusanyika kwa jina lake, maandiko yanasema watu wanapokaa kwa umoja Mungu huachilia upako wake kwa namna ya kushangaza kutoka kwa kluhani mkuu Yesu Kristo

 

Zaburi 133:1-3 “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja. Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. Maana ndiko Bwana alikoamuru baraka, Naam, uzima hata milele.” 

 

Kwa hiyo katika ulimwengu war oho Mungu anafahamu sana umuhimu wa umoja, kama kuna jambo mojawapo muhimu ambalo Yesu aliliombea kanisa na wanafunzi wake ni kuwa na umoja ona

 

Yohana 17:20-22 “Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.”

 

Hakuna taasisi yoyote ile inayoweza kusimama kama tasisi hiyo haina umoja, shetani anajua kuwa ili aweze kuwaharibia watu atamwaga roho ya mafarakano ili kuwe na makundi nah ii ndio dalili mbaya sana ya kuanguka kwa taasisi au taifa au hata ndoa.ni pale umoja unapokuwa umeondoka. Lazima tuwe na nia moja, tupendane inapotokea kila mtu anaangalia maslahi yake, moyo wa ubinafsi na kujiona bora kuliko wengine hapo ndipo mambo huanza kuharibika

 

Wafilipi 2:1-4 “Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine

 

kwa msingi huo kanuni ya chuma kunoa chuma ina maanisha kuwa na umoja kushikamana kwa nyenzo zinazofanana ili kujenga na kufanikisha kazi ya Mungu au ujenzi wa jamii au taifa kwa mshikamano unaokubaliana na kuelekezana, kwa msingi huo kujitenga na jamii au kutiokukubali kuchangamana na wenzako kunaweza kuwa na mchango mbaya sana katika makuzi na ufanisi wa mtu mmoja mmoja.

 

2.       Chuma hunoa chuma ni usemi unaotufundisha pia kutoambatana na watu wenye tabia mbaya.

 

Chuma hunoa chuma ni msemo pia unaotufundisha kuambatana na watu wenye tabia njema

1Wakoritho 15:33  Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.” Ni vema kuuangalia mstari huu kwa kiingereza unasema hivi 1Corinthians 15:33 “Do not be misled, Bad Company corrupts good characterusemi huu umetokana na usemi wa kiyunani unaotafasirika hivi  “DO NOT BE FOOLED, DECEIVED, MISLED, BAD FRIEND, COMPANY WILL RUIN GOOD HABITS, OR CHARACTER, OR MORALS, Imenukuliwa kutoka katika mashairi ya zamani sana ya kigiriki kati ya mwaka 342-291 KK., Yaani kama chuma hunoa chuma basi chuma hicho vilevile kikiwa kiovu kitakufanya uwe muovu zaidi, kwa msingi huo maandiko yanatufundisha kujihadhari na watu waovu, au kuacha kuwa na mahusianio na watu wabaya, huwezi kuwa na tabia njema kama u nashikamana na watu wenye tabia mbaya mafundishio ya yesu Kristo ya na ukatili mikubw zaidi wakati masihi alipokuwa akitahadharisha mambo ya kukosesha

 

Mathayo 18:7-9 “Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; lakini ole wake mtu yule aliletaye jambo la kukosesha! Basi mkono wako au mguu wako ukikukosesha, ukate ukautupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima hali umepungukiwa na mkono au mguu, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. Na jicho lako likikukosesha, ling'oe, ukalitupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum ya moto.”

 

Yesu alitumia maneno haya kumaanisha kuvunja uhusiano na mtu anayesababisha wewe ukosee, anazungumzia kuacha kuambatana na watu waovu wanaokuharibia ambao badala ya kukunoa uwe mzuri wanakunoa uwe mbaya, badala ya kukuongoza katika mkema wanakuongoza kufanya uovu, utaharibikiwa lugha ya Paulo mtume inanyoosha pia moja kwa moja katika tahadhari ya swala hili ona

 

2Wakoritho 6:14-18 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,”

 

maandiko yako wazi na yanatutaka tuwe makini na wale tunaoambatana nao, wana ushawishi wa ina gani je ni chuma cha aina gani usije ukanolewa kuwa muovu zaidi hivyo ni muhimu ukawa makini na kuchagua mtu wa kuambatana naye asiwe mvuta bangi, asiyetumia madawa ya kulevya, walevi, wazinzi, makahaba, majambazi, wezi, waongo, matepeli, watu wa misheni town, wenye tama, wasengenyaji, watukanajim  wasagaji, mashoga, wavuta sigara, waasi maandiko yanatuasa kuachana na makutano wa aina hii hawa tukiambatana nao watatunoa na tutakuwa waovu zaidi, Musa anasema mtu akikushawishi katika uovu muue

 

Kumbukumbu la Torati 13:6-10 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako; katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia; usimkubalie wala usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche;mwue kweli; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika kumwua, na baadaye mikono ya watu wote. Nawe mtupie mawe hata afe; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.”

 

Maandiko yanatuonya kuacha kuandamana na mkutano katika kutenda maovu, kwa sababu hiyo hata kama utaona kuwa kuna kundi au watu wanakusudia kufanya jambo baya ni muhimu wewe ukajihadhari kama lengo la umoja wao ni kwenda kufanya maovu, pima wewe mwenyewe lolote lile iwe ni maandamanio, migomo uasi au lolote ambalo unaona liko kinyume na Mapenzi ya Mungu au neno lake wewe usiambatane nao hata kama wako wengi

 

Kutoka 23:2 “Usiandamane na mkutano kutenda uovu; wala usitie ushahidi wako katika neno lo lote kwa kugeukia kando na kuandamana na mkutano ili kupotoa hukumu;”  

 

Neno la Mungu liko makini sana kuhusu kuambukizwa kutenda uovu, na lina msimamo mkalisana kuhusu kujiunga na jamii isiyotaka kutenda mema, kwa msingi huo kama ni chuma hunoa chuma basi kama chuma hicho ni cha uovu waovu hunoa waovu wenzao na hivyo utakua uemambatana na wapumbavu na wala sio wenye hekima na biblia inaonyesha matokeo kuwa utaumia.     

 

3.       Chuma hunoa chuma ni usemi unatufundisha kuwa na tabia ya kutiana moyo.

 

Chuma hunoa chuma maana yake pia kuna watu wanaoweza kututia moyo, tunachohitaji sisi ni kutiwa moyo, kuna watu wakitiwa moyo tu wanafanya vizuri chuma hunoa chuma humaanisha ni kupata mtu anayeweza kujua hali yako na ni nini unachohitaji kukifanya kisha akakutia moyo kufanya vizuri, Mungu mwenyewe amefanya kazi ya kututia moyo kwa neno lake akitutaka tusigope kabisa anajua kuwa wako watu wakitiwa moyo hufanya vizuri. imani yao hupanda na Mungu ametuhakikishia ushindi mkubwa usiokuwa wa kawaida watu wanapotiwa moyo ona mifano ya kutiana moyo katika maandiko:-

 

Isaya 41:6-13 “Wakasaidiana, kila mtu na mwenzake, kila mtu akamwambia ndugu yake; Uwe na moyo mkuu. Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo akamhimiza yule apigaye fuawe, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, Ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike. Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;  wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.”

 

Wakati mwingine sio tu kungoja kutiwa moyo lakini unaweza kujitia moyo mwenyewe kama chuma kwelikweli kwa kuuthibitishia ulimwengu kuwa wewe sio dhaifu na wewe ni hodari jikabidhi kwa Mungu na Bwana Mungu yeye hatajali hata kama uko peke yako atakusaidia yeye ni sehemu yetu ya kujitia moyo hivyo wakati unapokuwa katika halia inayokuhusu wewe pekee hakikisha kuwa unajitia moyo mwenyewe .

 

Yoeli 3:9-10 “Tangazeni haya kati ya mataifa; takaseni vita; waamsheni mashujaa; watu wa vita na wakaribie; na wapande juu. Yafueni majembe yenu yawe panga, na miundu yenu iwe mikuki; aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari.”

 

Watu wawapo duniani wanahitaji kutiwa moyo, ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa tunawatia moyo wengine, lakini wako watu ambao kazi yao ni kuvunja moyo, lakini usikubali kwa namna yoyote ile kuvunjika moyo Maandiko yanatutaka pia tujitie moyo, ukijitia moyo mwenyewe unakuwa chuma na baadaye utawasaidia watu wanaovunjika moyo!

 

Nehemia alipokuwa anaujenga ukuta wa Yerusalem alikutana na changamoto za wapinzani ambao walikuwa ni wakatishaji tamaa na walikuwa wanatoa maneno ya kejeli kuhusiana na ukuta wa jiji la Yerusalem alilokuwa analijenga Nehemia kama msimamizi, ni ukweli usiopingika kuwa kama Nehemia hangekuwa shupavu yeye angekata tama na hivyo watu wengine neo wangekata tama! Ona

 

 Nehemia 4:1-3 “Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba tulikuwa tukiujenga ukuta, akaghadhibika, akaingiwa na uchungu sana, akawadhihaki Wayahudi. Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto? Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema, Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe.”

 

Nehemia alitishiwa na hata kutumiwa manabii wa uongo, lakini hata hivyo hakukata tama na matokeo yake kazi ilisonga mbele kupitia yeye na wale aliokuwa akiwaongoza ona matisho aliyokutana nayo na namna alivyoweza kustahimili:-

 

Nehemia 6:11-13 “Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia. Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri. Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie.”   

 

Chuma kuona chuma kunamaanisha kusaidiana kuinuana kutiana moyo ambako mwisho wa yote kutakuwa na faida kwa watu wote, sio mtu mmoja kila mmoja anahitaji kutiwa moyo au kujitoa moyo ili hatimaye aweze kuwa Baraka kwa wengine, kwa eneo lake ili mambo yaweze kuwa mema.

 

4.       Chuma hunoa chuma ni usemi unatufundisha kuwa tayari kubadilika:-

 

Chuma kunoa chuma maana yake vilevile ni kukubali kubadilika, vile vyuma vinaposuguana kunatokea mabadiliko chanya, lakini wakati mwingine chuma kunoa chuma humaanisha unaweza kuchoma moto chuma kimojawapo kikaiva katika moto kisha ukatumia nyundo kugonga kile chuma kingine mpaka kikanyooka, chuma kinachogongwa kinabadilika na kuwa katika umbile lililokusudiwa na mhunzi, kwa hiyo unapogongwa badilika usipobadilika utagongwa zaidi au utaondolewa,  Mungu anaweza kutuinulia marafiki wazuri ambao wanaweza kutusaidia kukua na kukomaa wao wanaweza kuwa wakweli kwetu na wanaweza kutuambia ukweli, kutushauri au kutukemea na kutujenga, na kutukosoa, kosoa zao zinaweza kuwa za kutusaidia hivyo kuna umuhimu kwetu kukubali kubadilika  na kufuata mashauri yao ama kufuata ushauri wa neno la Mungu, ni Baraka kuwa na watu wanaotunyoosha japo tunaweza tusijisikie vizuri kwa wakati Fulani, kibinadamu iko wazi kuwa wanadamu wachache sana wanaopenda kuambiwa ukweli, na wanaokubali kukemewa  lakini lazima tukubali kukemewa kuna watu hawakubali maonyo, hawataki kukemewa hawataki kuambiwa ukweli, tabia ya aina hii ni sawa na chuma kukataa kunolewa na anguko linaweza kutokea kwa watu wasiokubali maonyo.

 

Mithali 29:1 “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.”

 

Neno la Mungu linatutahadharia kwamba ni muhimu kukubali maonyo wako watu hawataki kuonywa wakiguswa tu wanavimba wanageuka wanakuwa jeuri wanajibu wanajitetea wanajigamba wanajiona kuwa hawastahili kuguswa maandiko yanasema hao wamekuwa wana haramu kama sisi ni wana wa halali basin i muhimu kwetu tukawa watu tunaokubali maonyo

 

Waebrania 12:5-11 “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali.Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake. Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani. Maandiko aidha yanawataka viongozi wa kiroho kukaripia na kuonya na kukemea

 

2Timotheo 4:2-4 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho. Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.”

 

 Watu waliyakubali maonyo baadaye walikuja kuwa viongozi wazuri sana Petro ndiye mwanafunzi nwa Yesu aliyekemewa mara nyingi sana, lakini alikuwa na uelewa mkubwa sana kuwa kwa Yesu kuna maneno ya uzima wa milele,

 

Mathayo 16:21-23 “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka. Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”     

 

Petro pamoja na makemeo makali sana hakumwacha Yesu aliendelea kushikamana naye Yohana 6:66-68 “Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena. Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.

 

Petro alikuwa na uelewa kuwa kukemewa kule kungekuja kumleta katika nafasi ya kuwa kiongozi na kufanya vizuri, Nyakati za kanisa la kwanza watu waliokuja kuwa viongzi wazuri ni wale ambao waliwahi kukemewa hadharani mbele ya wote na wakiwa wanajua umuhimu wa maonyo waliyapokea na kubadilika na kuja kuwa viongozi wazuri sana akiwemo Tizo aliyekuja kuwa askofu wa makanisa, Mungu aklimuinua sana na kuja kuwa kiongozi mkubwa sana na Paulo mtume alijivunia baadaye kwa sababu alikubali maonyo

 

 2Wakoritho 8:16-23Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo wa Tito. Maana aliyapokea kweli yale maonyo; tena, huku akizidi kuwa na bidii, alisafiri kwenda kwenu kwa hiari yake mwenyewe. Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote. Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu. Tukijiepusha na neno hili, mtu asije akatulaumu kwa habari ya karama hii tunayoitumikia; tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu.Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu.  Basi mtu akitaka habari za Tito, yeye ni mshirika wangu, na mtenda kazi pamoja nami kwa ajili yenu; tena akitaka habari za ndugu zetu, wao ni mitume wa makanisa, na utukufu wa Kristo.” Baadaye sifa zake zilienea makanisani kote alikuwa ni mtu mwema mtendakazi pamoja na Paulo mtume  na mtume wa makanisa unapokuwa kanisani, shuleni kazini na kila mahali ili uweze kuwa mzuri na kufiti kwa kazi basin i vema ukakubali kunolewa.

 

5.       Chuma huona chuma ni usemi unaotukumbusha kujifunza kutoka kwa wengine

 

Wakati mwingine Mungu hutumia watu, kujifunza kutoka kwa mtu mwingine hii ni kanuni pia ya chuma kunoa chuma training

 

2Timotheo 2:2 “Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.”

 

Paulo mtume hapa anaonyesha kuwa Timotheo alijifunza vitu kutoka kwake  na anataka Timotheo ayatumie yale aliyiojifunza kutoka kwake awakabidhi watu waamini fu watakaofaa kuwafundisha na wengine, kujifunza kutoka kwa wengine ni njia sahihi ya kujinoa, chuma kinapokinoa chuma kingine husaidia kukifanya chuma kilichonolewa kutumika kama jinsi chuma kile kilivyokusudiwa na aliyekinoa, Maandiko yanaionyesha wazi kuwa wale waliojifunza kutoka kwa Yesu Kristo walitambulika kwa namna walivyokuwa na ujasiri mkubwa sawasawa na ule aliokuwa nao Yesu Kristo,  hii ilisababishwa na yule aliyewanoa namna alivyo ona

 

Matendo 4:13 “Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.”

 

Viongozi wa dini walishangazwa sana na uwezo mkubwa wa Petro na Yohana, ujasiri, uwezo wa kujieleza na kujiamini na miujiza waliyoifanya walitaka kujua kuwa watu hawa ni watu wa namna gani wamesomea wapi, wengi wa viongozi wa dini ya kiyahudi walikuwa walimu waliwafunza watu lakini walishangaa neno watu wasio na Elimu na Maarifa lina maana ya (watu wasiokuwa na ujuzi wa Torati maamuma, hawakupitia darasa lolote la viongozi wa kidini wanaotambulika lakini wasio na maarifa unlearned and ignorant kwa kiyunani (Idiotai)  watu walioibuka tu, wasiojulikana wanatokea wapi) walikuja kubaini kuwa watu hawa ni ni wazi kuwa mafunzo yao waliyapata kwa Yesu, Yesu alipochagua wanafunzi wake hakwenda kwenye madarasa ya watu maalumu alichukua watu wa kawaida tu wasio na Elimu na kuwanoa wakawa vile anavyotaka

 

Mathayo 4:18-22 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi. Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita. Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata.”

 

Hawa walikuwa watu walionolewa na Yesu mwenyewe, walikuwa mashujaa, walikuwa majasiri, walikuwa na uwezo wa kunena, walikuwa na uwezo wa kujenga hoja za kimaandiko na kuthibitisha wazi kuwa Yesu ni Bwana, jambo lililopelekea wajiulize hawa wametokea wapi ni ukweli ulio wazi kuwa wao walikuwa wamejifunza kila kitu kutoka kwa Yesu Kristo,

 

Wakati Paulo mtume yeye alikuwa mtu aliyejifunza kutoka katika shule za viongozi wa kiyahudi waliokuwa maarufu sana wakati huo,

 

Matendo 22:3-5 “Mimi ni mtu wa Kiyahudi, nalizaliwa Tarso, mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu, miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu wa jitihadi kwa Mungu kama ninyi nyote mlivyo leo hivi; nikawaudhi watu wa Njia hii hata kuwaua, nikawafunga, nikiwatia gerezani, wanaume na wanawake. Kama Kuhani Mkuu naye anishuhudiavyo, na wazee wa baraza wote pia, ambao nalipokea barua kwao kuwapelekea ndugu wale, nikaenda Dameski, ili niwalete wale waliokuwa huko hata Yerusalemu, hali wamefungwa, ili waadhibiwe.”

 

Sasa unaweza kuona kuwa Paulo mtume tofauti na Petro na Yohana yeye alikuwa amepitia shule za kiyahudi na aliweza kujitambulisha hivyo na hawa wazee walikuwa wanamjua na Gamaliel alikuwa ni Rabbi aliyeheshimika sana ona

 

Matendo 5:34-35 “Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo, akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa.”

 

Unaona Gamaliel anatajwa kama Mwalimu wa Torati aliyeheshimika sana alikuwa rabbi wanahistoria wa nyakati za kanisa la kwanza wanaeleza kuwa rabbi huyu alifundisha kati ya mwaka wa 22-55 Baada ya Kristo, na hivyo kuna uwezekano mkubwa alimfundisha Paulo aliyekuwa na umri wa miaka kama 16 hivi, gamaliel alikuwa ni farisayo aliyebobea kutika katika shule ya Rabbi Hillel, wa kizazi kabla kidogo ya Yesu kristo, wakati huo kulikuwa na marabbi maarufu sana Rabi Hillel na rabbi Shammai, hawa walihusika kwa kiwango kikubwa kuwanoa wayahudi wengi katika maswala ya sharia na mitazamo mikubwa miwili yay a Reberal  na conservative, kwa msingi huo kila mmoja alinolewa kwa namna Fulani kutoka kwa mwingine, Muda usingeliweza kutosha kuonyesha kuwaona wengi waliopata mafunzo kutoka vyanzo mbalimbali 

 

Musa alipata Elimu ya kimisri ona Matendo 7:22-25 “Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa hodari wa maneno na matendo. Umri wake ulipopata kama miaka arobaini akaazimu moyoni mwake kwenda kuwatazama ndugu zake Waisraeli.Akamwona mmoja akidhulumiwa, akamtetea, akamlipia kisasi yule aliyekuwa akionewa, akampiga huyo Mmisri. Alidhani kwamba ndugu zake watafahamu ya kuwa Mungu anawapa wokovu kwa mkono wake, lakini hawakufahamu.” Ni Elimu hii aliyoipata na elimu ya dini aliyoipata kule Midian kwa Yethro mkwewe vilimuwezesha kuwa mwanzilishi na kiongozi mkubwa na wa kwanza au baba wa Taifa la Israel na kulijengea ustaarabu mwingi sana, tukubali kumbe basi kujifunza kutoka kwa wengine na hasa wale wakali kweli kweli ili watunoe na tuwafuate Waebrania 13:7 “Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.”

 

Kwa hiyo hapa usemi unatukumbusha wazi kwamba ili tuweze kuwa wazuri sana kuna manufaa ya kujifunza kutoka kwa wengine na kuwasaidia wengine kuwa wazuri zaidi, kumbuka hakuna mtu nanaweza kuwa mtu peke yake                 na hivi tulivyo ni matokeo ya kujifunza kutoka kwa wengine!

 

6.       Chuma hunoa chuma ni usemi unaotukumbusha umuhimu wa neno la Mungu

 

Kwa karne nyingi sana imethibitika wazi kuwa neno la Mungu limekuwa na nguvu kubwa sana ya kubadilisha maisha ya mwanadamu kuliko namna nyingine zozote, kama mtu anataka kunolewa vema kunyooshwa na kuwa mwema awe tayari kunyenyekea kwa neno la Mungu Biblia inalisifia neno la Mungu kama upanga ukatao kuwili ona

 

Waebrania 4:12-13 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo. Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.

 

Lenyewe lina uwezo wa kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo, na limekuwa na sifa za kubadilisha maisha ya watu  wa makabila mbalimbali na kuwapa utamaduni wa kibiblia lenyewe kama nyndo vilevile linauwezo wa kuvunja vunja na kulainisha

 

Yeremia 23:28-29 “Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana. Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?

 

Neno la Mungu lina nguvu ya kuumba Mwanzo 1:1-31 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.  Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji. Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo. Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili. Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo. Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo. Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu. Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka; tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo. Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi na kuutawala mchana na usiku na kutenga nuru na giza; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne. Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu. Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano. Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo. Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.”

 

Neno la Mungu lina nguvu ya kuhekimisha 2Timotheo 3:14-17 “Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.  Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”

 

Neno la Mungu lina nguvu ya kuleta mabadiliko Isaya 55:10-11 “Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.”             

 

Neno la Mungu lina uwezo wa kutusaidia kuzishinda dhambi Zaburi 119:9-11 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako. Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.”

 

Mtu awaye yote anayetaka kunolewa katika maisha yake basi na ajifunze kunyenyekea na kukaa katika neno la Mungu, Mungu analiheshimu sana neno lake lakini sio hivyo tu anawaangalia watu waliopondeka watetemekao wasikiapo neno lake Isaya 66:2 “Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.”

 

Muda usingeliweza kutosha kuona namna na jinsi neno la Mungu linavyofanya kazi katika mazingira mbali mbali lakini lenyewe ni chuma ni nyundo ivunjayo mawe vipande vipande lina uwezo wa kuzalisha nguvu za aina yoyote ile tuitakayo, lina uwezo wa kutunoa na kutufanya upa na kututakasa na kutuweka sawa!

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima



Hakuna maoni: