Alhamisi, 26 Januari 2017

Mfano wa tai ayashukiaye Mawindo!


Andiko: Ayubu 9: 25 -26 Biblia inasema “ Basi siku zangu zina mbio kuliko Tarishi; Zakimbia wala hazioni mema, Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiayemawindo.”



Leo tutachukua muda kutafakari kwa kina somo kuhusu Mfano wa tai ayashukiaye Mawindo, Ni muhimu kuwa na ufahamu kuwa Mungu aliviumba viumbe vingi duniani kwa makusudi mbali mbali lakini mojawapo ya kusudi kuu ni kutufunza mambo mbalimbali ya msingi, Tai ni moja ya Ndege au kiumbe ambaye biblia imezungumza sifa zake kwa kina na mapana na marefu na tunaweza kujifunza mambo kadhaa ya muhimu kutoka kwa kiumbe hiki.
Kuna usemi wa wahenga kuwa ndege wa aina moja huruka pamoja, Usemi huu kwa Tai ni tofauti tai wanaruka pekeyo na wanafurahia kuruka juu sana, sifa zake zinawekwa katika Biblia kwa vile ni ndege mwenye sifa za kipakee ni ndege asiyeshindwa na ukubwa wa mawindo yake.
Kwa nini Biblia inampa Tai sifa za hali ya juu sana ni muhimu kwetu kujifunza sifa zake na kuzilinganisha na maisha yetu.

1.       Tai ni wenye uwezo mkubwa wa kuona mbali.



Ayubu 39:27-29 Biblia inasema hivi “ Je! Tai hupaa juu kwa amri yako, Na kufanya kioto chake mahali pa juu?  Hukaa jabalini, ndiko kwenye malazi yake, Juu ya genge la jabali, na ngomeni. Toka huko yeye huchungulia mawindo; Macho yake huyaangalia toka mbali.”

Tai kama utamfanyia uchunguzi na kumchungulia kwa mbali ni ndege makini sana Biblia inamsifia kuwa “macho yake huyaangalia mawindo toka mbali” ndi ndege hodari katika kuwinda macho yake amebarikiwa uwezo wa kuona mbali sana na anaona kwa uwazi kabisa inasemekana anauwezo wa kumuona mwenzake akiwa Maili 50 kwa uwazi kabisa! Jambo hili linatufundisha nini? Naamini unaweza kupata picha Fulani

Mamia ya watu hodari wamewahi kuishi duniania na kupita wakiwemo watu maarufu sana duniani na viongozi wakubwa

Ili dunia iweze kuwa na Mafanikio makubwa sana inahitaji watu na viongozi wenye uwezo wa kuona mbali sana, Abraham Lincoln rais wa 16 wa Marekani aliongoza katika wakati mgumu sana wenye matatizo mengi na inchi ikiwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, lakini ndiye aliyefanikiwa kuweka misingi ya umoja na kukomesha utumwa na kuifanya Marekani iwe kama ilivyo leo,

Ili dunia iweze kuwa na mafanikio ni lazima iwe na watu wenye uwezo wa kuona mbali, wanaoangalia faida za mbeleni za kwao na za kizazi kinachokuja badala yao
·         Watu wasio na maono ya mbali wanaweza kutugawa kupitia dini na ukabila
·         Watu waioona mbali hawajali kutunza Mazingira
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kuharibu mahusiano
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kuua wanyama kama tembo kwa faida yao
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kufanya Ufisadi kwa kuifilisi nchi
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kujisomea kwa bidii
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kujiwekea akiba
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kuhusu maisha yao baada ya kufa duniani
Awaye yote aliye kama tai atakuwa na ujuzi wa kuona mbali na kuzingatia faida za siku zijazo kuliko kuangalia leo. Unayaona mwindo yako kwa mbali. Ni lazima tuwe na maono makubwa yaliyopimwa kwa kina na yatakayoleta faida kubwa na matokeo makubwa katika jamii.

2.       Tai ni ndege wasioogopa Mawindo.


Tai ni ndege asiyeogopa hata kidogo, wakati wote anapambana kuhakikisha anashinda, atapambana kuhakikisha anapata mawindo yake au anatawala,unapoangalia sinema za maisha ya tai utaweza kuona  hawaogopi mawindo haijalishi mawindo yao ni makubwa kiasi gani hata kama ni mbuzi ambaye anaonekana kuwa mkubwa kuliko uwezo wake tai ni lazima atabeba, wana ujuzi mkubwa wa kuwinda na ni mahodari, tai haogopi
Ni muhimu kufahamu kuwa kama unataka kufanikiwa katika maisha haya usiogope kufanya jambo gumu, usiogope kukabiliana na watu wakubwa au waliokuzidi umri, hakikisha kuwa unakipigania kile unachokipenda,
·         Usiogope kupigania unachokipenda
·         Usiogope kusimama katika kweli hata kama itakuletea madhara
·         Usiogope ukubwa wa tatizo unalopambana nalo pigania mpaka kieleweke
·         Usiogope ugumu wa masomo unayosoma
·         Usiogope au kuonea aibu aina ya kazi unayoifanya
·         Lengo lako kuu ni kuhakikisha unafanikiwa
·         Usiogope mateso utakayoyapata kwaajili ya imani au kile unachokipigania
·         Usiogope kuanzisha huduma au kufungua kanisa, usiogope kuwa mmisionary, usiogope kugombea urais kama Mungu anataka ufanye jambo kwa faida yako lifanye
·         Uisogope kufanya lolote ili kufafikia malengo yako, Tai hawaogopi mawindo yao hata kama anachokiwinda ni kikubwa kuliko umbile lake.

3.       Tai ni Hodari hawaogopi Dhuruba.


Ukitaka kujua uhodari wa Tai utaweza kuuona wakati wa dhoruba, wakati huu ndege wengine wote hukimbia na kujificha kwa kuogopa dhoruba , kwa tai mambo ni tofauti anafunua mbawa zake na kuzitanua na kupaa kwenda juu zaidi, taia wanatabia ya kutumia dhoruba kwa faida, wakati ndege wa kawaida wakiogopa, ni muhimu kufahamu kuwa watu wanaolinganishwa na tai hawakimbii changamoto zozote bali huzitumia changamoto kusimama na kuongeza viwango, Mungu anataka watu wasiokimbia changamoto bali wenye uwezo wa kukabiliana nazo huku wakisimama katika kusudi au kuelekea juu zaidi

4.       Tai wanaruka juu sana.



Ndege huyu ndiye anayejulikana kama mfalme wa ana inasemekana tai wanauwezo wa kuruka juu kiasi cha fiti 10,000, katika kiwango hicho hutaweza kumuona ndege mwingine na ukimuona ni lazima atakuwa tai, Tai haruki wala kutafutiza chakula pamoja na njiwa, alisema Dr, Myles Munroe Marehemu, alisema wakati njiwa wakiwa ardhini wanacgakuachakua siku nzima na kulalamika, Taia hawanung’uniki, hawapigi kelele, wanapaa juu sana wakisubiri mawindo wakisubiri nafasi waweze kuitumia, watu wakuu duniani ni wale wanaotatua matatizo na sio wanaolalamika, wanatumia nafasi na changamoto yoyote kama tai dhoruba inapotokea.

5.       Tai hawali kibudu
Ni muhimu kufahamu kuwa sifa nyingine ya tai ni pamoja na kutokula kibudu tai hawali wasichokiua wenyewe, siku zote wanakula nyama ya mawindo yao wenyewe, wanakula nyma safi na mpya hivi ndivyo watu wakuu katika dunia wanavyopaswa kuwa
Watu wakubwa duniani hukaa na watu wenye mawazo mapana na wenye kufikiri na wenye uwezo wa kuamua, watu hodari wasiokata tamaa, hawa ndio watu wanaoweza kulete mabadiliko makubwa Duniani, watu wenye uwezo wa kuleta badiliko unapowasikiliza au kukaa nao karibu, watu wenye ushawishi
Kamwe usipoteze muda na watu wanaopoteza muda
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kusengenya
Kamwe usipoteze muda na watu wasio na imani
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kuzungumzia wengine
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kupiga majungu na fitina
Kamwe usipoteze muda na watu ambao kuanguka kwa wengine ndio furaha yao
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kuhukumu
Kamwe usipoteze muda na watu wenye mitazamo hasi wenye kujihusisha na rushwa na uovu hivyo ni vibudu, tafuta vya kwako mwenyewe mawindo yako mwenyewe.



Tai anayekula Mizoga!
Ni muhimu kufahamu kuwa tai tunayemzungumzia hapa  mwenye sifa tulizozitaja anaitwa Eagle huyu hali mizoga na taia anayetajwa katika Mathayo 24:28 huyu ndiye taia anayekula mizoga huyu anaitwa VULTURE
§  Mathayo 24:28Kwa kuwa popote ulipo mzoga ndipo watakapokusanyika tai”
§   Matthew 24: 28 "Whenever there is carcass, there the VULTURE will gather” NIV.
§  Matthew 24: 28 "For wheresoever' the carcase  is there will eagles be gathered together KJV
Tai anayekula Mizoga haitwi “Eagle” anaitwa  “Vulture”
Huyu ni aina nyingine ya tai ambaye hupatikana mashariki ya kati nyikanani na katika mbuga za wanyama Afrika tai huyu ndiye anayekula mizoga kiingereza sahii anaitwa VULTURE huyu ndiye ambaye Yesu anazungumza katika injili ya Mathayo  

Tai aina ya Vulture ndiye anayekula Mizoga na sio Tai aina ya Eagle

6.       Tai wanauwezo wa kujitia nguvu mpya
Zaburi 103:4-5 “ Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,  Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;”


Isaya 40:31 “Bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”
 
Moja ya tabia ya tai ya kushangaza sana ni uwezo wake wa kujitia nguvu kwa upya ukiacha kuwa wanauwezo wa kuona mbali lakini wana maisha marefu inasemekana Tai anapofikisha miaka 30 anakuwa anachakaa na manyoya yake yanakuwa yamezeeka hivyo kuathiri uwezo wake wa kiutendaji, inapofikia hivyo tai hakati tamaa ya kuishi badala yake hutafuta kilele kikubwa cha mlima na kutulia kwa miezi mitano anagonga mdomo wake katika mawe ya miamba na kungoa ngozi ya juu, hujinyonyoa manyoa nyake yote wakati huu ajajigomoa na kuanza kuwa na manyoya mapya mdomo mpya na magamba mapya jambo hili humfanya tai awe na uwezo wa kurejexza uhai wake kwa miaka mingine 30-40, Ndo maana biblia inasema ujana wako utarejezwa kama tai
 Watu wenye akili ni watu wanaoweza kujitafakari na kuangalia yote waliyoyafanya katika maisha yao liwe jema au baya linapokuwa baya unaachana nalo  wanatafuta nini lililo jema na lipi wanaweza kuliendeleza na jipya gani wanaweza kuenda nalo, na kujifunza jambo jipya la kufanya siku hadi siku.
Kamwe sukubali kudumaaa
Usikubali kubaki vilevile siku zote

7.       Tai wanatoa mafunzo kwa vifaranga vyao


Amini usiamini tai wanaotoa mafunzo kwa vijana wao, tai wanafikiriwa kuwa ni ndege katili sana wakati wa kutoa mafunzo na kama hujui makusudi yao unaweza kukubaliana kuwa ni ndege wakatili, jambo moja la kushangaza kuhusu tai ni uwezo wake wa kutoa mafunzo kwa vifaranga vyake, utafiti unaonyesha kuwa hakuna aina ya ndege mwenye mvuto na mpole kama tai kwa watoto wake kushinda tai
Mama wa tai anapogundua kuwa wakati umefika kwa vifaranga vyake kujifunza kuruka, anawabeba vifaranga wake mgongoni na kupanua mbawa zake anaruka juu sana kisha anajiondoa kutoka kifaranga chake na kukiachia kiangukekinapoanguka kinajifunza kuruka akiona kinaogopa na kinataka kuanguka anakidaka na kukirejeza katika kiota chake, atafanya hivyo mpaka kimejifunza kuruka.

Watu wakubwa sana duniani sio mabosi, wakati wote wanawafanya wengine kukua katika jamii na wanawapa changamoto lakini wanawasaidia kukua na kujiamini na kuendelea kuwapa maelekezo wengine mpaka wameweza kufanya vilevile kama wao wafanyavyo.

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima
0718990796

Jumapili, 22 Januari 2017

Siri ya Kufanya mambo ya Kushangaza!



Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu amemkusudia kila mwanadamu kuwa na uwezo wa kufanya mambo ya kushangaza, Mwanadamu hakuumbwa kama kiumbe kingine cha kawaida, wanadamu sio viumbe wa mchezo mchezo, wanadamu sio tu viumbe vya kijamii lakini inaonekana kuwa mwanadamu ni kiumbe kilichobarikiwa uwezo mkubwa sana wa kubuni mambo na kutengeneza vitu na vingine vikadumu kwa muda mrefu sana, Mwanadamu ni kiumbe wa kushangaza, Nyani wanaweza kushangaza namna wanavyoruka toka tawi moja hata lingine lakini hakuna jipya wanaloweza kulifanya, sivyo ilivyo kwa wanadamu ni kiumbe wa ajabu Mungu amaemuumba kwa ajabu mno mno.

Matendo 6:8 Biblia inasema “Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.”

Biblia inatuambia kuwa Stefano alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu, maana yake Mungu anaweza kumtumika kila mtu kwa karama yake kufanya mambo makubwa ya kutisha na kushangaza

·         Maana ya neno Kushangaza
·         Mifano ya watu waliofanya mambo makubwa ya kushangaza
·         Siri ya kufanya mambo ya kushangaza

Maana ya neno Kushangaza.

Neno Maajabu tunalolizoma katika Matendo 6:8 limatokana na neno la Kiyunani “TERAS” Kiebrania “PALA” ambalo kiingereza husomeka kama “WONDERS”, “MARVELLOUS”, au “ TREMENDUS” Kwa hiyo kufanya maajabu maana yake ni kufanya mambo ya kushangaza, kila mmoja anaweza kuushangaza ulimwengu kwa kadiri ya neema na uwezo aliopewa na Mungu.

Mifano ya watu waliofanya mambo makubwa ya kushangaza
Dunia imakuwa na historia ya watu wengi waliofanya mabo makubwa ya kushangaza na wengine wanakumbukwa hata leo, kutokana na mambo makubwa waliyoyafanya
Muda hauwezi kutosha kuelezea Jinsi wamisri walivyojenga Pyramid  zaidi ya miaka 2500 kabla ya Kristo ni majengo ya ajabu sana hawakuwa na cranes wala winch lakini katika ujuzi mkubwa wa kihesabati waliweza

1.       Huko ufaransa katika jiji la Paris uko mnara mkubwa sana unaojulikana kama Iron Lady wenyewe wanauita “La Dame de Fer” yaani mwanamke wa chuma mnara huu unavutia maelfu ya watu kila mwaka kwenda kuuangalia mnara huo wa chuma mzuri na wa kuvutia lakini jambo la kushangaza mnara huu pia ujulikanao kama “Eiffel Tower” umejengwa mwaka 1889 na ulibuniwa na Enjinia “Gustave Eiffel  inaweza kukushangaza mnara wa siku nyingi hivyo unamvuto mkubwa mpaka leo duniani



2.       Empire states Mimi niliwahi kufika mahali hapa katika jiji la New York Jengo hili lilikuwa ndio jingo refu zaidi katika jiji la New York na lilikuja kupitwa baadaye na Trade towers zilizojengwa mnamo miaka ya 1931-1975, kwa miaka zaidi ya 40 kabla ya 1931 Jengo hili limekuwa ni la aina yake.



3.       Stature of Liberty ni Sanamu iliyoshikilia Mwenge iko katika lango la bandari ya jiji la New York ni moja ya sanamu yenye mvuto mkubwa sana hata leo lakini ilizinduliwa tarehe 28 October 1886 na mbunifu wake aliitwa Fredrick Berthold  




4.       Ikulu ya marekani WHITE HOUSE ni ikulu yenye mvuto mkubwa sana ilianza kukaliwa na maraisi wote walioko Marekani tangu rais Adam ni nzuri naya kifahari watu wengi hutembelea hapo mimi pia nilipata nafasi ya kupiga picha hapo, pamoja na mvuto mkubwa wa nyumba hiii ya kifahari na yenye kupendeza huwezi kuamini kuwa ilijengwa kati ya mwaka 1792 – 1800.


    Tukiwa White House  kutoka kushoto Athur Chikoka, Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye hekima, William Boniventure Kifutumo Nyadili, Yohana Martin Komba, Imani Peter Mngazija, Onstard Mashauri, Hubert Gumbo na baraka kolombo tulipotembelea Marekani mwezi Juni 2014 

5.       Kwa nini mifano hii yote? Ni kuonyesha kuwa wanadamu wanauwezo mkubwa sana wa kufanya maajabu wa kufanya mabo ya kutisha na kushangaza, tunaweza kufanya katika, masomo yetu, katika kuimba, katika kucheza soka katika kufundisha katika kupika na kila eneo Mungu analotupa tunaweza kulifanyia kazi kwa bidii na juhudi na kwa maarifa makubwa na tukaonekana watu wa tofauti

Mungu ndi ye mfanya maajabu makubwa zaidi duniani na Mbinguni kwa uwezo wake neema yake na roho wake anaweza kabisa kutusaidia kufanya mamnbo makubwa ya kupita kawaida ya kutisha na kushangaza
Siri ya kufanya mabo ya kushangaza
1.       Jiunganisha na Mungu kwa wokovu
2.       Jaa Roho Mtakatifu
3.       Omba neema na uweza Matendo 5:12, 6:8, 19:11
4.       Muombe Mungu Ishara na maajabu vifanyike Matendo 4:43
5.       Mwambie Mungu akujalie Matendo 14 :3
6.       Uwe na Bidii katika kila unalolifanya 

Ukiyajua hayo Heri wewe ukiyatenda.
Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima.

Jumapili, 8 Januari 2017

Bwana Mungu wako Atakutangulia.


Mstari wa msingi: Kumbukumbu la Torati 31: 8


" Naye Bwana yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia, wala kukuacha usiogope wala usifadhaike"

Huu ni Mwaka mpya 2017 kwa kawaida wako watu wanaopenda mabadiliko lakini wako pia wanaoogopa Mabadiliko

Miaka inabadilika
Siku zinabadilika
Watu wababadilika

Kadiri miaka inavyokwenda mambo pia hubadilika
Musa alitembea na wana wa Israel kwa miaka 40 katika Jangwa, watu walikuwa wamemzoea lakini Mungu alimwambia Musa kuwa hutavuka MTO huu wa Jordan na alimuandaa Joshua kuwaongoza Israel

Wakati huu Israel na makuhani pia walikuwa na Hofu kuwa itakuwaje sasa
Kila wakati tunapokabiliana na Mazingira mapya, majira mapya, msimu mpya wa masomo, kazi mpya, miradi mipya, uongozi mpya, nk na hata Mwaka mpya huwa tubajiuliza itakuwaje?
Musa aliyajua Mashaka ya Israel, Mungu anayajua Mashaka yako katika Mwaka huu mpya anakutia Moyo

Atakutangulia, jangwa hili ni pana ni zito wakanaani wako mbele yetu ni lazima tuwakabili lakini kibinadamu hatuwezi wenyewe kabisa
Musa anatia Moyo

1. BWANA MUNGU WAKO ATAKUTANGULIA

2.ATAKUWAPAMOJA NAWE

3.HATAKUPUNGUKIA

4.HATAKUACHA

HIVYO HATUPASWI KUOGOPA WALA KUFADHAIKA MAANA MUNGU ATATUFANIKISHA

Mungu anapokutangulia hufanya miujiza mikubwa atakufungulia hazina zilizofichwa na utajiri na kusawazisha mapito yako, lakini vilevile atakupigania

Isaya 45:2-3.

 "2. Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma;    3. nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni Bwana, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli."

Mungu na akutangulie Mwaka huu
Na. Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatatu, 12 Desemba 2016

“Gimpel the fool” Gimpel mpumbafu au fala!



Naitwa Gimpel  mjinga au fala, Ingawa sifikiri kabisa mwenyewe kuwa ni fala au mjinga, kama watu wanavyonifikiri, Lakini ndivyo wazushi wanavyoniita, walinipa majina tangu nikiwa shuleni, nilipewa majina kama saba hivi waliniita Jinga, Punda, Bichwa maji, Levi, Mshamba, Wakuja, na Fala, na jina la mwisho ndio likawa maarufu zaidi, nilikuwa najiuliza kwa nini naitwa fala? Eti kwa sababu nadanganyika kirahisi, siku moja waliniambia Gimpel unajua kuwa mke wa Rabbbi amejifungua? Niliondoka shuleni mara moja ili kwenda kumuangalia, lakini kumbe ulikuwa ni uongo! Nilijiuliza nilipaswa kuangalia nini je tumbo lake kwamba halikuwa kubwa? au nilipaswa kuangalia nini ningejuaje kama ana mimba? Je ulikuwa ni ujinga nilioufanya? Aaah sijui lakini kundi lote la watu walinicheka, waligonga mikono yao na kurukaruka na kunizomea mpaka saa ya maombi ya usiku, haikunidhoofisha kwa sababu sikuwa mjinga lakini nafikiri walikuwa wamenipatia siku hiyo, mimi namcha sana Mungu, nikasema litapiata tu.

Nilipokuwa nikitoka shuleni kurejea nyumbani nilisikia mbwa wakibweka, kwa vile nilikuwa siogopi mbwa sikujali, lakini nilifikiri moyoni je kama mbwa hao ni kichaa na wataning’ata itakuwaje najua madhara ya kung’atwa na mbwa mwenye kichaa, hivyo niliamua kutimua mbio kama niliyenunua gari, lakini jambo la ajabu nilishangaa watu waliokuwa sokoni na madukani waliangua kicheko kikubwa sana, kumbe mtu mmoja aliiigiza mlio kama wa mbwa je ningewezaje kujua kuwa ni mtu? Lakini nilionekana kuwa mjinga pia.

Watu wengi walipogundua kuwa mimi ni mtu ambaye ninaweza kudanganyika kirahisi basi kila mmoja alijaribu anachoweza kukifanya ili mradi kunidanganya, wengine waliniambia Kaisari anakuja kwenu, wengine mwezi umeanguka huko Turbeen, tumegundua sanduku la thamani nyuma ya bafuni kwenu, na mengineyo mengi ili mradi tu walijua kuwa naweza kumuamini kila mmoja, na ndivyo ilivyo nilimuamini kila mtu na niliamini hakuna lisilowezekana kama ilivyoandikwa katika hekima za mababa, si hivyo tu niliamini katika wingi wa watu mfano kama kijiji kizima wangeniambia jambo ningeamini mpaka pale waliponiambia kuwa tunakutania, niliwaamini na nilijua ni jambo jema kuwaamini watu kuliko kuwa na mashaka nao.

Mimi nilikuwa yatima na bibi yangu aliyenilea alikuwa amezeeka sana na mwenye kukaribia kufa, hivyo nilipewa kazi ya kusaidia kuuza mikate kwa mtu mmoja aliyekuwa na baker ya mikate, nilipokuwa zamu pale karibu kila msichana aliyekuja kuoka mikate aliweza kunidanganya kama sio mara moja na zaidi, wengine wakiniambia kuna thawabu kubwa mbinguni kama ukiwa muungwana, wengine waliniambia mke wa kuhani amejifungua dume la ngombe tangu mwezi july, Ngo’mbe ameruka juu ya dari na kutaga yai, ili mradi tu wanidanganye, kijana mmoja aliyekuwa mwanafunzi wa Yashiva alikuja na kuniambia Gimpel ulipokuwa umesimama pale Masihi alikuja na kufufua watu wote makaburini na baba yako na mama yako wamesimama makaburini wakikuita, 

Kusema ukweli nilifahamu wazi kuwa jambo kama hilo haliwezi kutokea, lakini nilipoambiwa niliingia shaka kuwa labda huenda kuna kitu na nikashindwa kukishuhudia kwa macho yangu mwenyewe, lakini wakati wote nilidanganywa dahaa niliamua kuwa sitaamini jambo lolote na niliweka Nadhiri kutokuamini mtu, lakini hata hivyo walinichanganya sana nisingeweza kujua mwisho wa jambo kubwa mpaka lililo dogo nimelielewa kwanza.

Niliamua kwenda kwa Rabbi mmoja ili kupata ushauri, aliniambia “ni afadhali kuwa mjinga siku zote kuliko kuwa mwovu kwa saa moja” “wewe sio mjinga” alisema “wao ndio wajinga” kwa sababu yeye anayemsababishia ndugu yake makwazo na aibu Jehanamu inamuhusu, Kama haitoshi Binti wa rabbi alinichukua mpaka ndani, tukiwa tunaondoka katika sebule ya Rabbi binti yake aliniambia umeshawahi kubusu ukuta? Nikamwambia hapana kwanini hasa? Akaniambia ni sheria na unapaswa kuitimiza kila unapotembelea hapa, daah hilo halikuwa na madhara ati lakini aliangua kicheko naona alikuwa amenipata tena

Nilitamani sasa kuhamia mji mwingine, lakini kila mtu alikuwa akijishughulisha kunitafuta mimi, walinitafuta walinivuta koti langu mpaka wakararibia kulichana walinisemesha mpaka masikio yangu yalikuwa kama yanataka kulowa mate, alikuwa kama mwenye kulea mtoto hivi lakini niliambiwa kuwa huyu hakuwa mtoto wake ni mtoto wa ndugu yake na yeye ni bikira na bado ni msafi hajanajisika, niliwaambia mnapoteza muda wenu siwezi kumuoa mwanamke huyo, hata hivyo waliniambia unajiaibisha mwenyewe na kuwa watanipeleka kwa Rabi na kunishitaki kuwa ninataka kumchafulia jina lake, niliwatazama na kujua kuwa nnaweza kuwakimbia kwa vile wamenifanya kama mtani wao, waliniambia inaweza kuwa heshima kubwa kwa Mwalimu wako Rabbi kama tu utamuoa mwanamke huyu aliyelelewa na Rabbi itakujengea heshima, lilikuwa jambo zuri kidogo kwangu kwa vile nilijihoji kuwa huwezi kuvuka maisha haya pasi na kupitia hatua hii ya kuoa 

Nilimfuata katika nyumba yake ya udongo iliyokuwa imejengwa eneo kubwa la mchangani na kuingia ndani, kundi kubwa la watu walinifuata wakiimba nyimbo walikuwa kama nyuki wanaotaka kuingia mzingani, nilipofika karibu walisimama na kuniacha niingine mwenyewe, niliingia na kupenya katika kuta nyembaba za nyumba hiyo huku nguo nyingi zikiwa zimeanikwa, huku nyuma walikaa kimya na waliogopa kumsemesha chochote Elka maana ndio jina lake, wanamjua kuwa hapendi kuzungumza lakini akizunhgumza ana maneno makali sana, niliingia ndani na kumkuta akiwa anaosha miguu yake akiwa hajavaa viatu, alikuwa amevaa nguo ya kitani ambayo ilikuwa imefunuka upande mmoja, nywele zake zilikuwa nimebanwa vizuri kwa nyuma na chache zikiwa zinaning’inia usoni, alikuwa ameumbika vizuri, nilivuta pumzi na kukaribia kuzimia, alikuwa ananijua vema bila shaka, aliniangalia na kuniambia angalia nnani anayekuja kisha? alifuta kiti na kuniamuru nikae

Tuliongea swala zima la kuoana lakini nilimwambia sikatai lolote lakini ninaomba uniambie ukweli kabisa  wewe kweli ni bikira? Na je huyu mtoto kweli ni wa ndugu yako? Usinidanganye tafadhali kwa sababu mimi ni Yatima

Mimi pia ni yatima alijibu, kila atakayejaribu kukudanganya na yeye mwishoni na apinde pua yake, ni imani yangu kuwa watu hawawezi kutuchukulia kwa faida zao, mimi nataka ulipe mahari ya Elfu Hamsini tu sina makuu, na ngoja nikusanye michango mwenyewe unajua kwa nini alizungumza kwa uwazi kuwa ni mwanamke ndiye anayelipa mahari na sio wewe, kwa hiyo usianze kupiga bajeti kuwa nitafanyaje wewe kubali tu tuoane, kisha aliniambia waweza kurejea ulikotoka

Niliwaza du leo huenda nitaachana na kazi ya kuoka mikate, na mji wetu haukuwa mji wa watu masikini,waliandaa kila kitu na kuendelea na maandalizi ya harusi, haikuwa jambo gumu kwa harusi kuandaliwa wakati ule maandalizi yalifana na siku ya harusi iliwadia kumbuka harusi yetu ilikuwa ya kiyahudi kwa vile wote tulikuwa wayahudi, siku ya harusi ilipofika tulijiandaa kama kawaida, Harusi ilifanyika katika geti la uwanja wa makaburi, watu walifurahi kuimba na kunywa kweli kweli, wakati agano la ndoa lilipokuwa likifanyika nilisikia Rabbi mkuu aliuliza Bibi harusi ni mjane au mwanamke aliyeachwa, mwanamke aliyekuwa akimsaidia bi harusi alijibu kwa niaba yake ni yote mjane na aliyeachika, dah ulikuwa wakati wa giza nene kwangu, lakini sikuwa na jinsi wakati hu je ningetimua mbio wakati wa shughuli za harusi? Hali ilikuwa ngumu kwangu.

Watu waliiimba huku wakiwa wamevaa mavazi meupe na baada ya mahubiri wengine walirusha Maputo meupe juu wakimsifu Mungu na kwaajili ya kuwakumbuka marehemu, wengine walifurahi na kucheza mpaka karibu na mimi na wengine walinikumbatia kwaajili ya kunipongeza, zawadi zilitolewa nyingi sana lakini katika moja ya vitu vilinishangaza vijana wawili walikuwa wamebeba kijikitanda kidogo cha mtoto, niliuliza je tunahitaji hii kitu? Ni ya nini hii? Waliniambia usijali wala usiumize ubongo wako kitanda kitakuwa mikononi mwako, nilijiuliza sana maswali mmh hii nini tena naenda kupata utani mwingine, lakini nilijipa moyo kuwa mji mzima hawawezi kuwa vichaa kiasi hiki na haiwezekani mji mzima waamua kunifanya mjinga.

Jioni nilikwenda kugonga katika chumba cha mke wangu lakini hakuniruhusu kuingia kwake nilisema nini hiki sasa kwani tuliozwa ili kuja kutazamana? Aliniambia hapana lakini niko katika siku zangu! Nilimwambia lakini jana ulichukuliwa kwenda kuogeshwa ina maana hawakuliona hili? Alinijibu jana sio leo, na leo sio jana unaweza kuipiga leo kama unaiweza mmh kwa kifupi ilibidi nisubiri

Baada ya miezi minne alishikwa na uchungu wa kujifungua  mtoto, kha wanakijiji walikuwa kimya tu wala hawakunicheka sielewi aina hii ya unafiki, uchungu ulikuwa umemshika  na alikuwa amejiegemeza katika ukuta na kujaribu kutembea aliita Gimpel nakufa tafhadhali nisaidie alilia nisamehe, wanawake walikuja na kuingia chumbani mwake na wengine walianza kuchota maji na kutafuta beiseni la maji ahaa ningefanya nini nilikwenda kwenye sinagogi na kuanza kuomba nikirudia Zaburi kadhaa

Mji mzima walisikia jambo lile na habari zilitapakaa, nilisimama kwenye kona nikumuomba Mungu na kuimba zaburi hilo ndio nililoweza kulifanya katika wakati ule mgumu wa kufikiri mke niliyeoa anajifungua ndani ya miezi minne

Watu waliosikia walisikitika na kusema maombi maombi maombi, maombi hayawezi kumfanya mwanamke akawa mjamzito, mmoja alisema maneno mazito kwangu yaani wewe ni sawasawa na Ngo’mbe, kuna jambo zaidi ya hilo kwa Mungu!

Mke wangu alijifungua mtoto wa kiume, siku ya ijumaa tuliingia kwenye sinagozi na kiongozi wa sinagogi wakati wa matangazo alisema kuna sherehe kubwa sana kwa tajiri Gimpel kwani kwake kumezaliwa mtoto wa kiume, watu wote katika sinagogi waliangua kicheko, nilijisikia vibaya sana , lakini sikuwa na la kufanya maswala yote ya ibada ya mtoto na swala la kumtahiri yalikuwa yananihusu mimi

Mji mzima walihudhuria sherehe na shughuli nzima ya tohara ya mtoto, watu walikuja na vinywaji na zawadi na wengi walinipongeza na nilitakiwa kutoa jina nilimpa jina la marehemu baba yangu mzazi roho yake na istarehe kwa amani masikini, dah Baada ya sherehe watu wote waliondoka na nilibaki peke yangu na mke wangu alichungulia kwenye pazia na kuniita Gimpel

Mbona uko kimya meli yako imezama?
Nitasema nini? Umenifanyia jambo jema sana mara ya pili hii kama mama yangu angelikuwa hai na kulisikia hili angefariki mara ya pili nilimjibu
We chizi nini? Unawezaje kusema ujinga kiasi hicho alijibu kwa ukali sana Nilimwambia nani anapaswa kuwa Bwana hapa?
Unanini wewe eeh unawaza nini kwani? aliuliza tena kwa ukali Nilimwambia wazi kwamba je hii ndio njia sahii ya kumfanyia Yatima? Umefanya unyama wa hali ya juu nilimwambia
Aliniambia ondoa ujinga huu kichwani mwako mtoto ni wako!, anawezaje kuwa wangu nilihoji, amezaliwa wiki kama kumi na nne tu tangu tumeoana?

Aliniambia kuwa amini mtoto huyu ni wako akanieleza kuwa huyu mtoto alizaliwa akiwa hajatimiza siku zake, akaniambia nilikuwa na bibi yangu ambaye pia aliwahi kuzaa mtoto ambaye alikuwa hajatimiza umri wake kwa hiyo maji hufuata mkondo hata huyu hajatimiza umri wake kabisa na kisha alianza kuapa kwa mwenyezi Mungu kuwa hajaniambia uongo hata kidogo, sikuweza kumuamini nilimuita Rabbi na tukazungumza siku ya pili na aliniambia ni jambo la kawaida lilimtokea hata Adamu na Eva walienda kitandani wawili na wakajikuta wamekuwa wane, je hakuna mwanamke duniani ambaye sio uzao wa Eva? Walinihoji kiasi cha kuninyamazisha nilinyamaza lakini nani ajuaye mambo yanavyokuwa? na nilikuwa namuheshimu Rabbi na sikufikiri kama anaweza kunidanganya pia hivyo nilikuwa mpole


Taratibu nilianza kusahau machungu yangu, nilimlea mtoto kama wangu nilicheza naye alinizoea akitiwa zongo niliweza kumpeleka haraka wa watoa zongo na kalikuwa kananipokea na nilifanya kazi kwa bidii sana ili kumtunza mtoto huyu kama unavyoelewa ni gharama sana swala la malezi, nilifanya kazi kama ngo’mbe au punda na nataka nikwambie sijawahi kumchukia Elka kutokana na uovu ule, maisha yaliendelea ni kilea mwanangu na mke wangu kila siku jioni niliwaletea zawadi ya mkate, pia niliwaletea zawadi mbalimbali na mapocho pocho wakati mwingine niliiba ili niwaletee zawadi zenye kufaa naamini nitasamehewa kwa wizi huo lakini hii ilitokana na upendo wangu kwa familia yangu na kuonyesha kuwajali.

Nilikuwa nalazimika kulala mbali na nyumbani kutokana na kazi zangu na siku za ijumaa nilirudi hata hivyo mke wangu alikuwa akitoa udhuru wa namna mbalimbali katika kunipatia unyumba akitoa sababu mara kichwa kinauma, mara kiungulia na mara hivi au vile, kama mnavyojua wanawake walivyo, nilijisikia uchungu moyoni kwaajili ya hilo, zaidi ya hilo alikuwa na kaka yake mdogo ambaye alikuwa amekuwa na ni kijana katili sana aliposikia nikimkoromea aliwasha taa na kunimulika alinionya kuwa anaweza kunipiga vibaya na kwakuwa alikuwa na nguvu kunizidi nilinyamaza, walinitishia kunipa talaka pia hali ilikuwa ngumu, Nilihisi kuna mwanaume mwengine anayekula chakula changu na kuondoka lakini nitafanyaje mimi ni wale watu wanaoachia kila kitu mikononi mwa Mungu nilisema kama yuko mtu ananiibia Mungu atamlipa!

Siku moja usiku mashine yetu ya kuokea mikate ilipata shida na hivyo nilitakiwa kurudi nyumbani usiku nilifurahi kwani nilisema leo nitalala na mimi usingizi japo kidogo na mke wangu, lakini nilipofika karibu na nyumbani nilisikia kama watu wanaokoroma zaidi ya mmoja sikufurahi alikuwa mke wangu na mwingine alikuwa anakoroma kama Ngo’mbe alikuwa ni jamaa amelala na mke wangu nilipotaka kulala ilileta shida kubwa sana na makelele yalizidi kuwa makubwa kiasi ambacho niliona itakuwa aibu mji mzima na pia nitamwamsha mtoto hivyo nilirejea Kazini na kuchukua safleti za magunia nikatandika na kulala, hata hivyo sikupata usingizi nilikuwa nikijiuliza usiku kucha kuwa uonevuu huu uitaisha lini ni lini mimi nitaendelea kuwa mjinga, je hata ujinga na wajinga kama mimi hivi hakuna mwisho wao nilijiwazia Gimpel hataendelea kuwa mjinga nafikiri kuna mwisho wa kila kitu.



Asubuhi nilikwenda kwa Rabbi kwaajili ya maswala haya kesi hii ilikuwa na mvuto mkubwa sana na hivyo ilivutia watu wengi Elka aliposikia alikuja akiwa na mtoto, na alikanusha kila kitu na kusema huenda uko nje ya akili zako umerukwa na akili,Rabi alimkemea na kusema anajua maswala ya ndoto, maono na kupamabanua mambo, alimkemea huku akigonga meza, lakini alisimamia msimamo wake kuwa hakufanya jambo hilo ni uzushi tu alisema Elka.

Wauza nyama na wafanya biashara ya farasi wote walisimama upande wake na kumtetea, mwanamke mmoja alijitokeza na kuniambia tumeshakufahamu tabia zako, mara mtoto alianza kujikojolea na hivyo Elka alitakiwa kuondoka haraka kwa sababu katika sinagogi kuna sanduku la agano na haipaswi kitendo kile kutendeka katika sinagogi. Hivyo Elka alitolewa,

Nilimwambia Rabii nifenye nini sasa?
Lazima umpe talaka mara moja alinijibu Rabbi
Nikamuuliza je akikataa?
Aliniambia lazima utoe talaka hilo ndio la msingi na si vinginevyo
Nikamwambia sawa Rabbi ngoja nifikiri
Hakuna cha kufikiri ndugu yangu vinginevyo utabaki naye katika paa moja na tabia ileile
Je nikitaka kumuona mtoto niliuliza?
Achana naye huyo kahaba mwache aendelee na huyo mjinga wake
Alikazia hakikisha unalifanyia kazi hilo na si vinginevyo maadamu mimi ni hai sitaki kusikia tena
Wakati huo ulikuwa mchana na nilijiambia kuwa nitahakikisha ninalifanyia kazi.

Usiku nilipokuwa nimejituliza kwenye magunia nililifikiri jambo hilo kwa uchungu sana, nilimtafakari yeye na mtoto pia, Hasira zangu zilipanda sana lakini pia nilitafakari kuwa mimi sio mtu wa kukasirika kiasi kile, niliwaza na kutafakari kuwa wakati mwingine wanadamu hawawezi kuishi bila kukosea na kwa vile amekataa kabisa kwa kiapo huenda labda mimi niliona maluweluwe tu yaani unaweza kuona kama mtu halisi kumbe hakukuwa na mtu na kama ndivyo nitakuwa simtendei haki Elka na nilipotafakari hilo nilianza kububujikwa na Machozi, kisha asubuhi nilikwenda kwa Rabbi na kumwambia kuwa huenda nilikosea, Rabi aliniambia kama ni hivyo sina la kuamua katika kesi yako na unachopaswa kukifanya labda uendelee kumtunza mkeo lakini usilale naye tena na unapotuma matumizi tumia mtu na usionane naye tena.

Miezi tisa ilipita kabla marabi wote hawajafikia muafaka na mwisho walikubaliana na maoni yangu na waliandika barua sikufahamu kama lingechukua muda mrefu hivyo, hata hivyo baada ya miezi hii tisa Mke wangu alijifungua mtoto mwingine na sasa alikuwa mtoto wa kike, siku ya sabato nilimpeleka mtoto kwaajili ya Baraka za kikuhani na nilikaribishwa karibu na Torati na na kuombwa nitoe jina na nilimpa mtoto jina la mama mkwe wangu,watu walionifahamu walinitia moyo kuendelea na maswala yangu kwani walihisi labda nitaelemewa na huzuni wakinicheka, nilijiapiza kuwa sasa nitaamini kila neno atakaloniambia mke wangu kwani nisipomuamini yeye leo kesho nitashindwa kumuamini hata Mungu

Niliendelea kuitunza familia yangu na kuwasaidia chakula na kila kitu kilichowafaa, pia niliendelea kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa jirani yangu na aliyekuwa anajifunza kazi, siku moja kijana huyu aliniembelea nyumbani na kuniambia Gimpel una mke mzuri kijana na watoto wawili wazuri sana ambao kwa kweli hustahili lakini kile watu wanachokisema kuhusu mkeo, kha watu wana midomo mirefu nafikiri unachopaswa kufanya ni kuwapuuza kama kama ulivyopuuzia msimu wa baridi uliopita.

Siku moja Rabbi alinitumia ujumbe na kuniuliza una uhakika kuwa uliwaza vibaya kuhusu mkeo? Nilimwambia ndio nina uhakika, aliniambia kwa nini sasa ulikuja ukishuhudia kuona mwenyewe kwa macho? Nika mwambia yalikuwa ji maruweruwe tu, aliniambia sasa unaweza kwenda nyumbani na kuendelea na maisha maana marabi wamekuruhusu nilibusu mkono wa rabi na kuondoka.

Nilitamani kwenda nyumbani mara moja sio jambo dogo kuishi mbali na familia, lakini nilijitia moyo kwenda kazini na kisha nitakwenda nyumbani jioni, jua lilipokuchwa nilifanya maandalizi na kubeba zawadi kibao na mikate na nikaanza kuelekea nyumbani, kulikuwa na mbaramwezi ya kutosha siku ile kulikuwa na kabaridi na barafu zilikuwa zinaanguka, niliona nyota kwa mbali na nilikuwa nikitembea kichwani kawimbo kalinijia na nilitamani kutembea huku ninaimba lakini nilihofia kuwaamsha watu waliokuwa wamelala, lakini nilikuwa nauwaza maana ni wimbo unaofukuza mashetani, niliendelea na safari, nilipokaribia nyumbani moyo wangu ulianza kudunda kwa kasi kama moyo wa mtu mhalifu, niliingiwa na hofu ya ghafla moyo wangu ukidunda kwa kasi sana, nilifika na kuona mwangaza ndani kutokana na Nuru ya mbaramwezi niliweza kuona mtoto mpya aliyezaliwa kakiwa kamelazwa aidha pia nilimuona mke wangu Elka akiwa amelala na nilipokaribia kabisa nilimuona my amelala karibu na mke wangu Elka na nilipoangalia vizuri unaweza kuhisi alikuwa nani? Alikuwa ni yule kijana niliyekuwa ninamsaidia, Ghafla ingawa mbaramwezi inawaka niliona giza kali,nilitetemeka na meno yalianza kugongana, mikate na zawadi zilizokuwa mkononi zilianguka ghafla na mke wangu alishituka usingizini huku akuliza nanii? Kwa sauti Gimpel? Imekuwaje umerudi na uko hapa? Mi nilijua umekatazwa? Sasa fanya jambo moja tafadhali nenda kaangalie kama mbuzi na kondoo hapo zizini wako salama maana mmoja alikuwa anaumwa, nilikwenda nilikuwa nimesahau kama tuna mbuzi na nilipozikia kuwa anaumwa nilimuonea huruma, nilipofungua mlango wa zizi, mbuzi yule alisimama na inaonekana alikuwa salama na wengine wote,baada ya hilo nilirejea ndani na kuuliza yuko wapi yule mjinga mke wangu aliniuliza mjinga gani? Nilimwambia yule kijana akaniambia hizo ndoto zako inaonekana una mapepo mjinga mkubwa we nitapiga kelele utokezako sasa hivi tokaa nilipotaka kuleta fujo Yule ndugun yake aliamka na kuja kutaka kunishambulia alinipiga vibaya kwa nyuma na nikafikiri amevunja shingo yangu nilitulia na kujiuliza kuna kitu hakiko sawa kwangu, mara yule nduguye aliniambia usije ukafanya kasfha nyingine hapa na hiyo mikate yako hakuna atakayekula hapa, Nilitulia 

 Sawa inatosha sasa Elka alisema na aliniamuru kulala kimya mpaka asubuhi bila kufanya lolote, asubuhi nilimuona yule kijana na nilitaka kumuonya lakini alinikemea kwa sauti kubwa kama mbwa na kuniambia nisikilize inakupasa uende kwa mganga au mtu yeyote mwenye uwezo wa kutibu akutibu kwa sababu nafikiri kuna misumari kicwani mwako haiku sawasawa duh, jamani kufupisha hii habari niliishi na mke wangu katika hali hizo kwa miaka 20, alizaa watoto sita wakiume wawili na wakike wane kwa mtindo huohuo mimi nikiamini tu kuwa ni wa kwangu, marabi waliniambia endelea kutenda mema kwani wenye haki huishi kwa imani

Ghafla mke wangu alianza kuugua kuanzia kwenye maziwa na kushuka chini kadiri siku zilivyoenda hali ilizidi kuwa mbaya, na ilionekana wazi kuwa hawezi kuishi, nilijaribu kuwaita madaktari na waganga kumtibu na kila siku walikuja kumwangalia na kumtibu nilimuuguza na kuacha kwenda kazini wakati huu nilikuwa na Bakeri yangu ya mikate na nilikuwa mtu tajiri lakini nilikuwa sijamwambia, pamoja na juhudi za kitabibu hakuna nafuu yoyote mke wangu aliipata hali ilizidi kuwa mbaya kabla hajafa aliniita kitandani na kuniambia Nisamehe sana Gimpel 

Nilimwambia unaomba msamaha kwa lipi?
Umekuwa mke mwaminifu na mwema sana
Ole wangu Gimpel alijibu mimi sio mwema Gimpel nimekudanganya kwa miaka hii yote sasa nataka kupatana na Muumba na leo nataka nikuweke wazi kuwa watoto hawa wote sio wa kwako, yaani kama kichwani mwangu ningekuwa ana akili ya mbao ingekuwa vizuri
Nilidakia ni wa nani sasa?
Sijui Gimpel tafadhali  nimetembea na wanaume wengi sana na sifahamu lakini nina uhakika sio wa kwako huna hata mmoja hapa, wakati ninashangaa aligeuka na kukata roho uso wake ukiwa na tabasamu ni kama alikufa akiwa ananiambia nimemdanganya Gimpel maisha yangu yote.

Siku moja baada ya kipindi cha maombolezo kuisha raho chafu ilinijia ikiwa na sura yake ikaniambia Gimpel mbonma unalala? ulimwengu mzima umekudanganya na ukaamua kuulipa kwa kuudanganya, nilimuuliza mimi nimeudanganyaje ulimwengu? Unawezaje kubeba mkojo katika kapu usiku na mchana na kutokuachie uende chooni? Kivipi?

Mimi nilikuwa nakudanganya kuwa hawa ni watoto wako na nilikuwa nalala na wanaume wengine lakini nawe ulikuwa unaudanganya ulimwengu kuwa hawa ni watoto wako na mimi ni mkeo
Nilimwambia je hujui kuwa kuna hukumu ya mwisho? 

Aliniambia hakuna hukumu ya mwisho ulimwengu umekudanganya, umetoa fedha nyingi ukaaminishwa kuwa umenunua paka tumboni mwako wakati hakuna paka hicho ndio kilichokukuta nikamwambia vipi kuhusu Mungu? 

Akaniambia hakuna Mungu pia ninachokuambia ni cha kusadikika tu.  Nilitamani kumpiga kwa nguvu lakini nilikuwa nimejaa hofu na nilitaka kupiga kelele kuelezea kilichotokea, mara yule kijana alikuja niliyekuwa nikimsaidia na baadaye alilala na mke wangu nilimkamata na kumtupia katika tanuru la moto la mikate kwa hasira nilimuua na kumzika pamoja na tanuru alisikika akisema leo umejilipizia kisasi, baada ya tukio hilo niliinamisha kichwa na  nilijikaza nikalala usingizi mara tena Elka akanijia katika ndoto akiwa na sanda akaniambia umefanya nini Gimpel 

Nilimwambia ni kwa sababu ya makosa yako kisha, nikaanza kulia akaniambia we we ni mjinga wewe ni mjinga kwa sababu mimi nilikuwa muongo kwenye kila kitu cha uongo na nilijidanganya hata nafsi yangu na sasa ninalipwa yote ukweli sikuwa nimemdanganya yeyote nilikuwa najidanganya mwenyewe najuta najuta sana, nilimuangalia uso wake na alikuwa mweusi sana,  kwa kuwa alikuwa motoni lakini aliniambia huna nafasi tena peponi uliyokuwa umewekewa kwa muda mrefu imefutwa,niliamka na nikakaa nikagundua kuwa kumbe kila kitu kilikuwa kimekaa sawa anayedanganya anajidanganya khah 

Niliharibu kila kitu kwenye bakeri ya mikate nilikwenda nyumbani na kuchukua mali sehemu Fulani niliwagaia watoto wote niliwaambia nimemuona mama yenu usiku wa leo ameungua vibaya motoni niliwaambia kila mmoja asahau kabisa kuwa yuko mtu anaitwa Gimpel na wao hawakujibu neno lolote walibaki kushangaa

Niliwabussu na kuwatakia maisha mema na nilivaa mabuti yangu na kuanza kuondoka kila aliyeniona mjini alinishangaa na kuniuliza unaenda wapi niliwajibu naenda ulimwenguni na nilihama mji ule kabisa walioniuliza niliwaambia nimedanganywa miaka yote ya ujana wangu lakini kwa kuishi kwangu sana nimegundua kuwa watu hawa hawakuwa waongo kwani ndio mtindo wa maisha usipodanganywa leo utadanganywa kesho na kama sio mwaka huu basi mwaka ujao na kila mtu anaweza kudanganya hata bila kukusudia

Nilihamia mji mwingine na huko nilikuwa nikipokelewa na watu kadhaa wa kadha nilikula chakula katika meza kadhaa isipokuwa usiku nikilala mji nioondoka ulikuwa unanijia na Elka pia nilijiuliza ulimwengu huu ni ulimwengu wa namna gani, Nilikuwa nikiishi maisha ya kuwasimulia vijana hadithi mbalimbali katika maisha yangu na nilizisimulia kiasi ambacho nilikuwa nasahau na kuzirudia zingine na watoto waliokuwa wakinifuata babu tusimulie khadithi niliwasimulia na wengine waliniiambia haa babu hii tayari.



Stori hii imeandikwa na Isaack Bashevis, Mwimbaji na mtunzi wa kiyahudi
Akionyesha maisha ya zamani huko ulaya miaka ya 1800 hivi wakati jamii ya kiyahudi ilipokuwa inaishi ulaya na inakuonyesha jinsi Gimpel alivyoweza kuozwa binti wa Kikuhani na rabi, lakini akidanganywa kuwa ni bikira na jinsi alivyoendelea kudanganywa maisha yake yote watu wakiitumia nafasi yake ya kumcha Mungu kama njia ya kumhadaa bila kujali kuwa alikuwa yatima pia ulimwengu ni ulimwengu wa udanganyifu, na ni ulimwengu ambao hauwezi kukuhurumia kwa sababu zozote zile, unaweza kuwa muongo wakati unajaribu kuwa mkweli, wanadamu ni waongo, makuhani pia ni waongo, hakuna uadilifu, mashetani nao ni waongo ni nani wa kuaminiwa? Unamuamini sana mkeo, Mumeo? Mchungaji wako? Chagua wa kumuamini mkweli ni mmoja tu Mungu pekee.

Imetafasiriwa na Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima