Jumatatu, 1 Februari 2016

Africa Katika Mpango wa Mungu

Afrika Imelaaniwa?

Ni swali la miaka kadhaa ambalo wengi tumejuliza kuhusu bara letu la Afrika kutokana na hali duni iliyonayo bara letu la Afrika ni kama kwamba ndio bara lililo nyuma zaidi ya mabara mengine umasikini uliokithiri vita vya wenyewe kwa wenyewe na matatizo kadhaa ya magonjwa na maradhi, je Mungu ana makusudi mema na Afrika? Naam Mungu hana upendeleo Mungu ana mpango na makusudi mema na Bara la Afrika vumbua siri hii na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima Rev. Innocent Kamote, katika kijitabu hiki Afrika katika Mpango wa Mungu.


SOMO: AFRIKA KATIKA MPANGO WA MUNGU
     Umasikini ni moja ya matatizo makubwa sana Afrika, Afrika ni moja ya Bara ambalo bado liko nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na Mabara mengine, hata ingawa umasikini uko dunia nzima lakini kuna umasikini mkubwa uliokithiri katika nchi za Afrika, miji mingi ya Afrika imejawa na watu masikini ambao mwanakosa huduma muhimu sana, miundo mbinu hafifu, mitaa isiyopangiliwa, watoto wa mitaani, ukosefu wa maji safi ya kunywa naya kutosha, huduma duni za afya, tatizo la wakimbizi,watu wasio na mavazi, ombaomba na maswala kadhaa yenye kuvunja moyo. Ni nini tatizo la Afrika? Je Mungu anaijali Afrika? Je Mungu ameiacha Afrika? Mbingu zina mpango gani na Afrika? Tutachukua Muda kutafakari somo hili Muhimu Afrika katika Mpango wa Mungu kwa kuzingatia vipengele kadhaa vitano vifuatavyo:-

·         Dhana potofu kuhusu sababu za Umasikini wa Afrika
·         Mpango wa Mungu kwa Bara la Afrika
·         Kuhani mkuu kwa mfano wa Yethro.
·         Tatizo la Afrika na ufumbuzi wa matatizo yake kibiblia
·         Mungu ataitumia Afrika wakati wa zamu yake.

Dhana potofu kuhusu sababu za Umasikini wa Afrika
Kama tulivyoona katika utangulizi kuwa Afrika inakabiliwa na hali ya umasikini wa kupita kawaida mtafiti mmoja nchini Kenya alifanya utafiti kati ya 1988 -1990 na kubaini kuwa moja kati ya kila watu watatu barani afrika hawashibi, yaani wanakabiliwa na njaa kwa msingi huo zaidi ya watu milioni 168 wa afrika hwashibi, licha ya kuwa na uhaba wa chakula cha kutosha, makazi yasiyoridhisha na ukwasi umasikini unatawala Afrika kwanini kwanini? Wataalamu wa maswala ya kiroho wanafikiri yafuatayo

1.       Afrika imelaaniwa
Hii ni moja ya dhana potofu sana ambayo imewatawala Waafrika kwa Karne nyingi hatujui ni nani mwanzilishi wa msemo huu au dhana hii lakini imejengeka kwa miaka mingi na watu wanafikiri ndivyo ilivyo kimaandiko pia Je Mungu aliruhusu Afrika ilaaniwe? Maandiko yanayotumika kuhalalisha dhana hii potofu ni Mwanzo 9: 25 – 27 Maandiko haya yanasema Hivi
“Akasema na alaaniwe Kanaani, Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake, Akasema Na atukuzwe Bwana Mungu wa Shemu na kanaani awe mtumwa wake, Mungu akamnafsishe Yafeth na akae katika Hema za Shemu na Kanaani awe mtumwa wake”
Dhana hii kuwa Afrika imelaaniwa, kihistoria iliweza kutumiwa vibaya, kwa mfano Huko Afrika ya kusini, watu weupe waliitumia dhana hii kuwakandamiza watu weusi, wakidai kuwa kibiblia wao ni watumwa wa watumwa, kwa vile Mungu amewalaani tagu awali,
Ni muhimu kufahamu kuwa Ahadi za Mungu “Zinategemea” yaani ni “conditional” Laana iliyotamkwa hapo inaweza kumpata mtu yeyote mwenye tabia kama ya Hamu na mwanae Kanaani, wao kimsingi walikuwa na tabia ya kutokuheshimu wazazi na hivyo walipoteza heri,maswala ya ngono na picha za ngono na simulizi zake kwao kilikuwa ni kitu cha kawaida na walifikia ngazi ya kufikiri kuwa kila mtu angekubaliana na mawazo yao yaliyofikia ngazi za kuacha kuheshimu wazazi wao
Ni Tabia ya Hamu ndiyo iliyopelekea mwanae Kanaani kupoteza haki ya mzaliwa wa kwanza na kutamkwa kama mtu atakayekuwa mtumwa, Ni dhahiri kuwa kama Kanaani na kupitia Hamu Baba yake wangeshikamana na utii na heshima kwa Mzazi wake Nuhu, wao ndio wangekuwa Kinara na taa ya dunia na Mungu asingeliwapokonya Ile nchi Nzuri ijulikanayo kama Israel leo.
Laana ya Nuhu ilikuwa inategemea, na utii au kutokutii kwa Kanaani, na pale walipojiingiza katika utendaji wa dhambi na kuacha sheria na mapenzi walipoteza haki ya mzaliwa wa Kwanza jambo hili si geni kimaandiko kwa vile Hata Reuben Mzaliwa wa kwanza wa Yakobo kwa kushindwa kumuheshimu baba yake na kufanya kosa kubwa zaidi ya lile la kanaani alipoteza haki ya mzaliwa wa Kwanza Mwanzo Mwanzo 49: 3-4 Ni wazi kuwa Biblia inaonyesha kuwa Reuben alikuwa mzaliwa wa kwanza wa Yakobo yaani Israel na hivyo alikuwa na haki ya Mzaliwa wa Kwanza na nafasi ya kwanza ya heshima na ukuu na uongozi na nguvu lakini badala yake nafasi yake ilichukuliwa kutokana na kulala na mke wa Baba yake Mwanzo 35:22, Kumbukumbu 27:20 hii ni wazi kuwa kushindwa kitabia kunakodhihiriswhwa na matendo mabaya ya dhambi na kukosa Heshima kunaweza kumuondoa mtu katika nafasi aliyokusudiwa na Mungu
     Makosa ya Reuben yalikuwa ni makubwa zaidi kuliko ya Hamu kuuona Uchi wa Baba yake, kimsingi wote walipoteza haki ya kuwa viongozi hiki ndicho kilichotokea kwa kanaani  na hivyo wana wa shemu walikuja na kuichukua nchi yao na wakanaani wengi waliuawa na kutawanyika maeneo mengine.
     Hivyo dhana hii ya kitheolojia kuwa AFRICA Imelaaniwa ni dhana Potofu kibiblia na haikubaliki katika mazingira na mpango wa Mungu Mungu si wa taifa Fulani tu Mungu ni wa mataifa yote Matendo 10: 34 - 35 “…Hakika natambua ya kuwa Mungu hana Upendeleo Bali Katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na Yeye” 

2.       Afrika iliwatumikisha wana wa Israel
Ziko baadhi ya dhana kuwa huenda umasikini wa Afrika umechangiwa na historia ya kuwatumikisha wana wa Israel kwa miaka zaidi ya 400 huko Misri mpaka Musa nabii alipowakomboa kutoka nchi ile ya Utumwa, na kwa sababu ya kuwatumikisha watu wa Mungu huenda ikawa sababu ya umasikini tulio nao leo kwa vile Mungu alimwambia Ibrahimu “nitawabariki wakubarikio naye akulaaniye nitamlaani” Mwanzo 12:2-3.

Ni muhimu kufahamu kuwa Israel kuja Misri ulikuwa ni mpango wa Mungu, Mungu alimjulisha Abraham Mapema mpango huu Mwanzo 15 : 13 – 16, Mungu alimuahidi Ibrahimu kuwa uzao wake utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake na kuwa huko watatumikishwa lakini watatoka na mali nyingi na taifa lile litahukumiwa
Ni dhahiri kuwa Israel kuelekea Misri ulikuwa ni mpango wa Mungu na Kutoka huko Mungu aliwabariki sana walitoka na Mali nyingi, walishuhudia Mungu akilihukumu taifa lile na walipata Mafunuo na mafunzo kuhusu Mungu kutoka Misri na taratibu ustaarabu na sheria za kuongoza Taifa.
·         Israel walipata nafasi ya kuwa taifa kwa kushuka Afrika
·         Walijifunza kuhusu Mungu wa kweli kutoka afrika
·         Walijifunza sheria na taratibu za kimaongozi na vita kutoka Afrika
Misri ilihukumiwa na hakukuwa na laana yoyote kuihusu Afrika kwa sababu ya utumwa ule.
·         Ujerumani wakati wa Hitler waliwafanyia Wayahudi ukatili na mauaji ya Halaiki yet Ujerumani ni moja ya mataifa makubwa lililoendelea kiuchumi duniani natambua kuwa wajerumani waliomba radhi kwa hilo na wanalipa fidia lakini bado wana hali Nzuri, Kama afrika ingekuwa inaadhibiwa kwa kuwatesa wayahudi Ujerumani na ulaya ingeadhibiwa kwa kuwatesa wayahudi na kwa kumuua Yesu

3.       Afrika iko gizani kwa sababu ya Upagani/na Uchawi uliokithiri na ibada za mizimu
Wako wanaofikiri kuwa Afrika iko gizani na inafunikwa na wimbi la Umasikini kwa sababu ya kuabudu mizimu, miungu uchawi na upagani uliokithiri dhana hii pia haina ukweli wowote wa kusababisha Mungu asiibariki Afrika
·         Historia inaonyesha kuwa nchi nyingi za Ulaya kabla ya Ukristo ziliabudu miungu na kulikuwa na Upagani mzito na mkubwa, athari za kuabudu sanamu zilizokuwa ulaya bado zinaonekana ndani ya Kanisa Katoliki na Anglikana, Hata hivyo nchi hizo zimepiga hatua
·         Japan ni moja ya nchi zilizoendelea sana lakini ilikuwa ni nchi iliyogubikwa na kuabudu miungu kwa hali ya juu, nchi ya Japan ina dini inaitwa Shinto na wanaabudu Mungu Jua Bendera ya taifa hilo ina picha ya jua jekundu katikati hata wafalme wa Japan huabudiwa kama Mungu lakini Japan imeendelea sana
·         India ni nchi iliyokuwa masikini sana lakini sasa inakua kwa kasi kuondoka katika umasikini, India kunaongoza kwa upagani kuliko Afrika, kuna miungu inayoabudiwa zaidi ya  milioni 280 Lakini sasa wanauzwezo hata wa kutengeneza Mabom ya atomic, wanazalisha injini za treni, wana viwanda vya magari ni wataalamu wa maswala ya tiba na madawa, wanapiga hatua kwa kasi sana lakini kuna upagani wa hali ya juu, dini ya Uhindu, Budha na sikhiism ziko kule India Lakini wameendelea sasa
·         Korea Kaskazini inapiga hatua ingawa sio kama Korea ya kusini ambao wao wameendelea zaidi, Korea  Kaskazini Rais wao KIM IL SUNG ni Mungu anaabudiwa, Afrika haijawahi kufikia dhambi ya kuabudu Mtu, MAO TSE TUNG huko China aliheshimika kama Mungu, Ukomonist uliitawala china na hakuna uhuru wa kuabudu Lakini leo china ina nguvu kubwa duniani ni moja ya taifa ambalo limeendelea na uchumi wake unakua kwa kasi sana, ni tishio kwa mataifa makubwa lakini ni taifa la kipagani dini zao ni pamoja na dini ya Taoism.
Ni lazima tujiulize what’s wrong with Africa? Kuna tatizo gani Afrika? Je Mungu ameilaani Afrika? Je nini sababu ya Afrika kuwa Nyuma je Mungu anaipa kipaumbele Afrika? Je Mungu ameisahau Afrika?  Mungu hana mpango na Afrika? Hilo sasa linatuleta kutafakari kipengele kifuatacho Mpango wa Mungu kwa bara la Afrika

Mpango wa Mungu kwa Bara la Afrika

1.       Maana ya jina Afrika
    Ni muhimu kuwa na ufahamu kuwa kabla hatujazungumza mpango wa Mungu kwa Afrika tuwe na ujuzi kuhusu jina Afrika na maana yake, Asili ya jina Afrika wengi wetu tunaweza tukawa hatuifahamu lakini neno hili Afrika kwasili linatokana na neno la kilatini afrika  Africa ambalo maana yake ni JUA na neno la KiyunaniAphrike” ambalo maana yake isiyo ya Baridi, Jina hili lilitumiwa mwanzoni na Warumi wakilitumia kuwaita watu wa Libya, Tunisia na Algeria Hivyo Neno Afrika maana yake ni inchi ya Mwanga wa Jua, Hata hivyo wazungu waliokuja mwanzoni kutembelea Afrika waliliita bara la Giza the “Dark Continent” pengine kwa sababu ya kutolijua vema bara hili.
     Nyakati za Agano la Kale Afrika ilijulikana sana kwa uwakilishi wa Mataifa mawili makubwa EGYPT na ETHIOPIA  Neno Ethiopia linatokana na maneno mawili ya Kiyunani  Ethio Pian  e’thi o pia  maana yake burnt Faces / au dark faced  yaani  watu wenye ngozi nyeusi au uso mweusi, nchi hii ilijulikana kama nchi ya NubiNubian Kingdom”na iko kusini mwa Misri na kaskazini mwa Sudani ni maarufu na ilijulikana kama ardhi ya malikia wa sheba, kwa ujumla Misri, Ethiopia au Kushi na Kirene zinapotajwa katika biblia hutajwa kwaniaba ya Afrika, huwakilisha Afrika, kwa Upande wa Jina Egypt waebrania waliita Misri, Mizraim na Misr kwa kiarabu  na hii ndio asili ya jina Misri kwa Kiswahili, Nchi hii iliwakilisha na maeneo makuu mawili ambayo zamani yalijulikana kama Upper Egypt na Lower Egypt kitu kikubwa ikiwa ni ardhi kuu za aina mbili ardhi nyekundu yaani jangwani na ardhi nyeusi yaani  ardhi yenye rutuba nyingi na udongo mweusi, hivyo Egypt au Mizraim maana yake ni Nchi ye Udongo mweusi wenye rutuba.Ama aina mbiliza Udongo Mizraim alikuwa moja ya wana wa Hamu mwana wa Nuhu Mwanzo 10:6-13 1Nyakati1:8,11. 

2.       Afrika katika mpango wa Mungu
1.       Mungu anao mpango na Afrika kama alivyo na mpango na mataifa yote duniani Matendo 10:34-35
2.       Mungu ameweka majira na nyakati kwa kila taifa ingawa wote twatoka katika chanzo kimoja Matendo 17:26-28 sisi sote tu wazao wake. Zamu ya Afrika inakuja!
3.       Mungu alimuahidi Ibrahimu kuwa Mpango wake ni kubariki mataifa yote ya dunia kupitia yeye Mwanzo 12:2-3
4.       Mungu atawaita watu ambao si watu wake Warumi 9:25-26
5.       Viashiria vya kinabii kuhusu mpango wa Mungu kwa Afrika
·         Mfalme wa Kwanza kuongoza Dunia Nimrod alikuwa mwafrika Mwanzo 10:6-12
·         Kutakuwa na Madhabahu ya Bwana Afrika (Misri) Isaya 19: 19- 25, Ashuru (Asia) na Israel watakuwa Baraka kwa Dunia
·         Ujio wa Malkia wa kushi Mathayo 12: 42, 1Falme 10:1, 2Nyakati 9:1 ni Ishara ya Kanisa la Afrika litakavyomjia Kristo na Litakavyobarikiwa, Malikia huyu alikuja na vito vya thamani sana kwaajili ya mfalme Suleman na Mfalme alimrudishia mara dufu, Mungu ataibariki Afrika kwa namna ya kushangaza Afrika itamzalia Matunda Mungu.
·         Africa ndio waliomsaidia Yesu wakati akiwa na wakati Mgumu yaani wakati wa Mateso Mathayo 27: 32 na Marko 15:21, maandiko yanaonyesha kama mkirene alishurutishwa kuubeba msalaba wa Yesu, lakini taarifa za kitamaduni zinaeleza kuwa mtu huyu alimuonea Yesu Huruma  hasa aliposhuhudia akianguka na msalaba huo na alimsaidia msalaba wake hii ni ishara ya Afrika kushiriki mateso ya Kristo, na Kristo hakukataa kusaidiwa Msalaba na Simeon Mkirene, Kirene ni mji mkubwa uliokuwa kaskazini mwa Afrika wengi huusisha na nchi ya Libya, ni wazi kuwa katika jamii ambazo zimewahi kuteseka na kushuhudia dhiki na uonevu ni Afrika na Israel Uko wakati Mungu atayafutamachozi ya Afrikana kulketa faraja kubwa duniani
·         Kati ya Manabii na walimu wa Neno la Mungu waliokuweko Antiokia wawili wanatajwa kutoka Afrika Simeon aitwaye Niger (Niger ni Afrika Niger au Nigeria pia hunaanisha mtu mweusi) Lukio Mkirene Libya (Afrika) Matendo 13:1-3, Hawa alihubiri nyakati za kanisa la kwanza, walituma wamisionary na kuwategemeza.
·         Mungu alitoa kipaumbele zaidi kwa Towashi wa Kushi (Ethiopia) Matendo 8: 26-39 na kinabii ina maana pana zaidi nitakayoizungumzia baadaye Ethiopia ni kinara cha Afrika na makao makuu ya Afrika yako pale Addis Ababa Ethiopia
·         Afrika itapeleka habari njema kwa mfalme wakati wa hali ngumu sana 2 Samuel 18: 19-33 Unabii unaonyesha kuwa tutabeba habari njema wakati ulimwengu ukiwa na hali ngumu na uvunjifu mkubwa na mmomonyoko mkubwa wa maadili na uadilifu.

3.       Kuhani mkuu kwa mfano wa Yethro
Unapoisoma biblia utaweza kuona Biblia ikizungumzia kuwepo kwa kuhani mkuu kwa Mfano wa Melkizedeki Waebrania 5: 5-6
Ni wazi kuwa Maandiko hayo ya ukuhani yanamuhusu Kristo, kwa vile katika sheria ya Musa Ukuhani ulifuata Order/mstari wa/ ya kabila ya lawi, hivyo ni walawi peke yao katika jamii ya Israel walipaswa kutoa kuhani na sio nje ya hapo, na hivyo Yesu Kristo kama Kuhani mkuu hakuwa wa kabila ya lawi Yeye ni kuhani watofauti kwa Mfano wa Melkizedeki.

Hata hivyo Biblia inatupa taarifa za kuweko kwa Kuhani mkuu mwingine ambaye naye alikuwepo kabla ya sheria ya Musa huyu ni Yethro, Yethro alikuwa ni kuhani wa Mungu aliyemuabudu Mungu wa kweli Yehova na alikuwa mkwe wa Musa na ana mchango mkubwa sana kwa Israel kumjua Mungu Hakuna kitu kinazungumzwa kuhusu kuhani huyu muhimu na wengi hawajua anawakilisha nini
Habari njema ni kuwa kuhani huyu mkuu ni wa muhimu sana kwa hivyo lazima tufuatilie chimbuko lake kisha tutapata picha ya kinabii na mpango wa Mungu dhidi ya Afrika. Biblia inasema nini kuhusu Yethro
·         Huyo Yethro ni nani
·         Jina Yethro maana yake ni wingi au ubora (Abundantly or Excellence )
·         Alikuwa Kuhani mkuu wa Midian lakini jambo la muhimu ni wapi wamidian wametokea na kuhani  ni nani na ana asili ipi “Biblia inayo majibu”
·         Wamidian ni watoto wa Ibrahim ambao alizaa na Ketura baada ya kifo cha Sara Mwanzo 25:1-6, 1Nyakati1:32-33 Yethro alikuwa kuhani wa wamidian maana yake ni wana wa Ibrahimu kwa Ketura hivyo wamidian walikuwa na ujuzi kuhusu Mungu wa kweli
·         Uthibitisho unaotutambulisha hili unapatikana katika sifa ya Mungu kumchagua Ibrahimu Mwanzo 18: 17-18 Mungu alimchagua Ibrahimu kwa vile alijua kuwa Ibrahimu atawafundisha wototo wake njia ya Mungu hivyo wamidian waliishika nja ya Mungu waliyojifunza kutoka kwa baba yao, walimuabudu Mungu na walikuwa na ujuzi naye
·         Sasa tunamuona Yethro kama kuhani wa Midian lakini mtu huyu alikuwa ni mtu wa namna gani
1.       Alimpa Musa usalama na kumtunza alipokuwa mkimbizi na kumuoza mke yaani binti yake aliyeitwa Sipora, kuhani huyu alionyesha wema kwa Musa alipokuwa ukimbizini
2.       Alikuwa na ujuzi kuhusu Mungu wa Kweli YEHOVA  na ndiye aliyemtambulisha Musa kuhusu Mungu Yehova kwa vile kabla ya hapo Musa na waebrania wote walimjua Mungu kama Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo na kwa vile walikuwa utumwani hawakuwa na nafasi ya kumjua Mungu kwa Muda mrefu, ndio maana watu hawa walitaabika na kuabudu miungu mara kadhaa,Kutoka 18:1-11.
3.       Alikuwa na ujuzi kuhusu Mgawanyo wa Uongozi Kutoka 18:13-23
4.       Ndiye kuhani aliyeweza kutoa dhabihu kabla ya ukuhani wa Musa na Haruni Yeye alikuwa na Nguvu ya kusongeza sadaka za kuteketezwa Kutoka 18: 12
5.       Yethro alijulikana kwa majina makuu mawili katika Biblia maarufu zaidi ni Yethro na linguine ni Reuel Kutoka 2:18 na Heabu 10:29
6.       Familia ya Yethro ilikuwa na ujuzi mkubwa kuhusu Yehova na walifahamu umuhimu wa kushika agano la Tohara ambalo hata Musa alilipuuzia Kutoka 4: 24-26, angalia kuwa mke wa Musa aliweza kumuokoa mumewe kwa kumtahiri mtoto wao Musa alikuwa hajatilia maanani mkewe Sipora alikumbuka na kuokoa maisha ya Musa
7.       Swali bado linabaki palepale Huyu Yethro mtu muhimu namna hii ni nani Hesabu 12 : 1-2 Mistari hii inaweka wazi kuwa kumbe mke wa Musa alikuwa mkushi Yaani Mwafrika, kwa msingi huo Yethro ambaye alikuwa kuhani mkuu wa Midian alikuwa mkushi Mwafrika, Huu ni unabii ulio wazi kuwa Afrika ina ujuzi wake wa asili kuihusu Mungu Yehova na namna ya kuabudu, Miriam na Haruni walimnena mke wa Musa kwa sababu gani, ilikuwa wao kabla ya kuja mke wa Musa walikuwa ni washauri wakuu, sasa amekuja mkewe Musa na anaujuzi kutoka kwao kuhusu Mungu Yehova sasa Musa anamsikiliza mkewe zaidi na Miriam na haruni wanaona wivu sasa wanataka kutumia weusi wake kumkandamiza na Mungu anaingilia kati na kuwaadhibu, kisa hiki ndicho kimeruhusiwa na Roho Mtakatifu kutufunulia juu ya Yethro Afrika ni kuhami mkuu kwa mfano wa Yethro, “Africa is a high priest of the most High God in the order of Jethro
8.       Afrika ni jicho la Israel, katika maandiko ya Biblia inaonekana wazi kuwa Musa alihitaji ujuzi wa njia ya kuelekea kanaani nchi iliyojaa maziwa na asali na walitambua kuwa Mungu amekusudia kuwabariki huko lakini laihitaji uongozi na ujuzi wa kupita jangwani nani angesaidia Hesabu 10: 29 – 34 Musa sasa anawaingiza Afrika katika safari ya kanaani na kuahidi kuwa mema ambayo Bwana anayaandaaa kwa ajili ya Israel nao pia watainjoy uzao wa Yethro ulikwenda na Israel hata Kanaani Waamuzi 4:11.
9.       Africa itanyoosha mkono wake kwa Mungu Zaburi 68:31,Isaya 45:14,Sefania 3: 10. Isaya 66: 18-21, Moja ya waanzilishi wa umoja wa Afrika “OAU” alikuwa ni Rais wa Ghana Kwame Nkuruma  Rais Kwame alikuwa ni mtu aliyesoma theology hivyo alikuwa Mchungaji na Mwalimu, Kwame alitabiri kule Addis Ababa kupitia Zaburi 68:31 Kuwa Afrika itainua mkono wake kwa Mungu
10.   Afrika ni kimbilio la viongozi na manabii
-          Abraham alifika afrika Misri kwaajili ya kujikimu kwa chakula Mwanzo 12:10
-          Familia ya Yakobo Israel walishuka Misri kwaajili ya chakula na kupewa sehemu nzuri ya nchi yenye rutuba sana ifaayo kwa mifugo 
 
Tatizo la Afrika na ufumbuzi wa matatizo yake kibiblia
Kwa jicho la kinabii tunaweza kuziona sifa za Afrika na Matatizo ya Afrika kwa kumtazama Towashi wa Kushi, na pia tukatambua mapenzi ya Mungu kwa Afrika Matendo 8: 26-40
·         Swali kubwa la kujiuliza ni kwanini Mungu anatoa kipaumbele kikubwa kwa Towashi wa kushi, wakati mwinjilisti Philipo alikuwa amehubiri samaria na kazi kubwa ilikuwa imefanyika kiasi ambacho kanisa la Yerusalem Lilimtuma Petro na Yohana kumsaidia Filipo?
i.                    Mungu alitoa kipaumbele kwa Bara la afrika kufikiwa na injili kupitia towashi huyu
ii.                  Malaika wa Bwana alihusika  kumuelekeza Filipo kuhusu Towashi wa Kushi kama ilivyokuwa kwa Cornelio wa kirumi kupitia Petro 26
iii.                Roho mtakatifu aliongea na Filipo kumuelekeza kumsogelea Towashi wa kushi 29 je kwanini towashi huyu anapewa kipaumbele hivi.
a.       Mtu huyu alikuwa anapenda kuabudu, alikwenda Israel kuabudu 27
b.      Alikuwa ni mtu mkubwa sana ni mtunza hazina za Malkia wa Kushi Kandake
c.       Alikuwa na kiu ya kumtafuta Mungu na kulisoma neon lake
d.      Alikuwa na utayari wa kufundishika, alijifunza kutoka kwa Myahudi huyu Filipo
e.      Alikuwa na ujuzi wa Lugha Kiibrania na kiyunani zilizomuwezesha kujisomea Gombo la nabii Isaya
f.        Gombo la nabii Isaya lilikuwa na mvuto kwa vile alitabiri maswala mengi kuhusu Kushi yaani Afrika Isaya 19: 19- 25
g.       Lakini pia walikuwa wakimtazamia masihi na walivutiwa na habari zake katika kitabu cha nabii isaya towashi huyu wa Kushi alikuwa akisoma Isaya 53 na swali lake lilikuwa katika Mstari wa 7-8 na kupitia mistari hii Filipo alimuhubiri injili na aliamini na kudai abatizwe na alifurahi na kurejea kwao Histiria ya kanisa inaonyesha kuwa kanisa liliingia Afrika mapema kupitia towashi huyu
Picha ya kinabii kuhusu Towashi huyu
1.       Alikuwa Towashi – maana yake hana uwezo wa kuzalisha
2.       Alikuwa anasoma lakini haelewi
Kibiblia haya ndio matatizo makuu ya Bara la Afrika, Ni bara lenye hazina kubwa sana malighafi na utajiri uliotukuka, lakini kibiblia inaonekana suluhu yake itapatikana kwa
1.       Uongozi: bora
2.       Elimu: ya kutosha lazima afrika ijikwamue kielimu, Afrika inahitaji uongozi wa kuelewa, wanasoma lakini wanahitaji Filipo kuwawezesha kuelewa vema
3.       Uzalishaji: Afrika inahitaji kujiimarisha katika swala zima la uzalishaji mali Picha ya towashi wa Ethiopia (Kushi) ni alama ya kinabii kuihusu Afrika, Ina uwezo wote lakini haizalishi malighafi zake yenyewe, wajanja wanaigeuza Afrika kuwa soko la bidhaa na wakazi wa kichuuzi, viongozi watakaoitwa na Mungu kuiongoza afrika ni lazima wawe na mtazamo wa kujitegemea, dhana ya kujitegemea haiwezi kuweko kama kila kitu kinafanyika katika mataifa mengine na sisi tukabakimkama wanunuzi tu! ni lazima tuzalishe kila kitu wenyewe, na kuwapa mitaji wawekezaji kutoka Afrika ni lazima tuwe na Nguvu ya maaumuzi ya wakati wetu ujao (Robert Nesta Maley Bob Maley) Aliimba "Every Human being has the right to decide for his Destination " alipokuwa akishangilia uhuru wa Zimbabwe, Uhuru wa kweli wa AFRICA  Ni lazima uendane na uchapaji kazi na maamuzi ya dhadi ya kujikwamua sisi wenyewe ili tuwe na uwezo wa kuamua kesho yetu itakuwaje Mungu anatusubiri tufikie hatua hiyo ndipo aiinue Afrika, ni wakati wa Mungu nkuitumia Afrika na ni wakati wetu umefika kutoa misada kwa mataifa mengine

·         Mungu ataitumia Afrika wakati wa zamu yake.
Kuna mambo yanabadilika duniani, miaka michache iliyopita Amerika na Canada na ulaya ndizo nchi zilizokuwa na utajiri mkubwa sana duniani, lakini katika miaka kumi iliyopita mambo yamebadilika, China na India nzi zilizokuwa masikini sana na baadhi ya nchi za asia zimepanda juu sana kiuchumi, na kuanza kuwa tishio kuliko Marekani na mataifa mengine ya Ulaya, Mexico, Brasil, china  na india zinapanda kiuchumi sana duniani
     Miaka 20 ijayo hali ya Afrika itabadilika na kuwa tofauti, mexico iliyokuwa nchi ya daraja la tatu na Brazili na India na China zimekuwa kiuchumi na baada ya miaka kadhaa itakuwa zamu ya Afrika, ni kweli kuwa kwa sasa hali ya afrika imekuwa na matatizo mengi, vita vya wenyewe kwa wenyewe, shida na matatizo lukuki na tunafikiri kuwa hatuwezi kuinuka
    Ni muhimu kufahamu kuwa kila taifa ambalo limeendelea kwa sasa limepitia matatizo mengi ambayo Afrika inapitia China iliathiriwa na Ukomonisti kwa miaka wakaonekana kama wanachelewa, India ilikuwa inaongoza kwa kuua viongozi wake kila wakati, na Brazil ilikuwa duni lakini ndani ya kipindi kifupi kumekuwa na mabadiliko makubwa, sana uchumi wa mataifa mengi ya Magharibi sasa unaporomoka sana, Ugiriki hali ni mbaya uturuki inashindwakulipa hata wafanya kazi, uchumi wa ulaya unaporomoka na uchumi wamarekani hali kadhalika hali ni mbaya
    Afrika itakuja juu wakati wa zamu yake na Mungu ataitumia Afrika
Ndimi Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote
 



Simba aliye wa kabila la Yuda!


Ufunuo 5:1-5 Biblia inasema hivi  “1. Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba. 2. Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, N'nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? 3. Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. 4. Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. 5. Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba”


Mungu ni wa ajabu sana nilipokuwa najisomea Biblia na kufika katika Mstari wa tano nikayaona maneno hayo Simba aliye wa Kabila la Yuda!  Maneno hayo yalinishangaza sana ni wazi kuwa Simba anayetajwa hapo ni Yesu Kristo hilo halina mjadala,  ni wazi kuwa Yesu ni Masihi na masihi alikuja kupitia ukoo wa Yuda hilo pia halina mjadala, Daudi pia alitokea ukoo huu wa kabila la Yuda hilo halikuwa na mjadala, Jambo kubwa lililovuta hisia kwangu ni kutajwa kwa Yuda mwenyewe hapa ndipo penye mjadala


Yuda wanaotajwa katika biblia wanaweza kuwa wengi, lakini walio maarufu ni watatu 1. Ni Yuda Iskariote umaarufu wake umekuja kutokana na tendo lake la kumsaliti Bwana Yesu, 2 Yuda ndugu yake Yakobo hawa ndi ndugu wa kunyonya wa Yesu Kristo na waandishi wa nyaraka za Yakobo na ule waraka wa Yuda, hawa wako katika agano jipya, Yuda anayetajwa akiunganishwa na Masihi ni Yuda wa agano la Kale huyu ni mtu wa namna gani?

Yuda alikuwa miongoni mwa watoto wa kiume wa Israel au Yakobo, alipata umaarufu sana kuliko ndugu zake, Kabla kidogo ya kuondoka ulimwenguni Yakobo ambaye ndiye Israel alitoa unabii kuhusu maswala ya maisha ya wanae ya baadaye, alimtabiria mema sana Yuda Mwanzo 49:8-12 moja ya maswala hayo muhimu ni kuja kwa Masihi kupitia kabila la Yuda

Yakobo alikuwa na wana 12 lakini swali la kujiuliza kwa nini Yuda awe maarufuna wa muhimu labda zaidi kuliko wengine? Kwa nini ni kama amebarikiwa zaidi, kwa nini aunganishwe na ubaba wa kuja kwa Masihi kwa nini Yesu aitwe SIMBA ALIYE WA KABILA LA YUDA? Ni lazima kuna maswala ya kujifunza kumhusu Yuda 

Ni wazi kuwa tunaelewa kuwa Mungu alinmtumia Yuda kutimiza mpango wake, Mungu katika hekima yake iliyo ya ajabu kuliko ya wanadamu, huwatumia wanadamu kwa makusudi yake na kwa neema yake na rehema, “1Koritho 1:26-29” si lazima uwe maalumu sana au utoke katika ukoo muhimu sana au uwe na tabia maalumu sana ndipo Mungu akutumie Hapana ! unapomchunguza Yuda utagundua ni kwa neema na rehema na wala si kwa matendo tunastahili Baraka za Mungu

Matatizo ya Yuda
Mwanzo 37:26 Yuda alihusika kwa kiwango kikubwa pia katika miakakati na mipango ya kumuuza Yusufu ndugu yake, ilikuwa ni kama ana huruma na ujanja wa kumuokoa Yusufu asiuawe, lakini Bado anawajibika kwa mkiwango kikubwa katika uovu wa kumuuza ndugu yake wa Damu awe mtumwa.

Mwanzo 37:31-35 Yuda na ndugu zake, wakiwa wamejikausha walishiriki wazi katika kusema uongo kwa baba yao kuhusu Yusufu, kumbuka wote walikubaliana waseme ameliwa na mnyama mkali,kumbuka zilikuwa ni habari za msiba wa kuumiza kwa Israel Baba yao, Yuda alishiriki utayari wa kumuaminisha Israel kuwa mwanae amekufa na kunyamaza na uongo huo kwa miaka zaidi ya 13, huku mzee akilalamika kupoteza mwana mpendwa, Kama amri ya kuwaheshimu wazazi ili upate heri na miaka mingi duniani Yuda alikuwa amaeharibu tayari

Mwanzo 38:1 Yuda huyuhuyu ulipofika wakati wa kuoa, Yeye aliamua kuoa mwanamke mkanaani , hii ilikuwa kinyume na tamaduni za Israel na Isaka na hata Ibrahimu, wote wliona umuhimu wa kuoa kwao lakini yeye hakuona umuhimu huo kwake mwanamke ni mwanamke tu alioa mkanaani
Mwanzo 38:7-10 Yuda kupitia mwanamke huyu mkanaani alipata watoto, wa kiume, lakini wawili kati yao mungu aliwaua mapema kwa sababu walikuwa waovu mbele za Bwana bila shaka unakumbuka Eri  na Onani, Unadhani nani anawajibika na uovu wa watoto hao? Utasema ni mwanamke mkanaani sawa lakini nani aliyemuoa? Na wanapouawa wanao unaowategemea nani anapitia uchungu?

Mwanzo 38:12-16 Yuda alikuwa ni mtu aliyeshindwa kuutawala mwili, aliongozwa na tamaa ya mwili, alifiwa na mkewe sawa , lakini anakwenda njiani anaona mwanamke kahaba anaingia kwake akifikiri ni kahaba, hakuwa na muda wala hata umakini wa kuangalia mwanamke huyo ni nani alitimiza tamaa yake na kuondoka zake

Mwanzo 38:24-30 Yuda alukuwa na moyo wa Kuhukumu, angalia kuwa analipogundua mkwewe Tamari ana mimba, hata pamoja na kuwa ndiye aliyemwekea mtego kwa kujifanya kahaba kwa sababu hakumpa haki zake, Yuda anawajibika kwa matendo yake ya hukumu akiamuru apigwe kwa mawe huku akiwa amesahau kuwa na Yeye ni mzinifu tu, ashukuriwe Mungu kuwa Tamari alimtaja mtu aliyempa mimba na kuonyesha ushahidi, na kupitia uhusiano huu wa kijinga na wa aibu kunazaliwa Mapacha  na mmoja anaingia katika mstari wa kutuletea Masihi Mathayo 1:3

Unamwangaliaje Yuda? Je ni kama asiyefaa kabisa kutumiwa na Mungu? Angelikuweko leo katika makanisa yanayojiita ya kiroho angetengwa na kufungwa kwa siku kadhaa, au anagefukuzwa kanisani na maadiko yangetumika kuwa hizi ni nyakati za agano jipya ni tofauti na zamani za ujinga? Na ingesahaulika kuwa mwanadamu ni yuleyule kihistoria, Ukweli kwa Mungu unabaki palepale Mungu alikuwa ana mpango naye, Mungu alikuwa anashughulika naye amfanye kuwa Baraka kwa wengine Mwanzo 49:8-12 

Yuda alikuwa kama pande la Mti usiofaa na Mungu alikuwa na Mpango wa kuuchonga ufae kwa kazi zake, Kama ni mwanafunzi mzuri wa Biblia utagundua kwa haraka kuwa wako wengi waliotumiwa na Mungu kwa namna na viwango vya kipekee, lakini maisha yao yakiwa yamepitia katika mpango mbaya wa kusikitisha na kuumiza

Rahabu aliyekuwa kahaba wa kutupwa katika mji wa Yeriko alimjua Mungu na akawa miongoni mwa hao waliomleta masihi (Joshua 2:1 Mathayo 1:5)
Ruth aliyekuwa mpagani na kutokea kabila la madui wa Israel alimjua Mungu na kuingia katika mstari wa waliomzaa Yesu

Daudi wa ukoo huo huo wa Yuda aliyezini na kuua kupitia Bathsheba anamzaa Sulemani ambao wote wanaingia katika Mababa waliomleta Yesu Kristo
Mathayo aliyekuwa Mtoza ushuru, aliyeajiriwa na serikali ya kirumi, watoza ushuru walijulikana kama wezi, waongo, na wadhalimu, wasaliti, Mungu alumuokoa na kumtumia kwa utukuifu wake ikiwamo kuandika injili Mathayo 10;3 akawa miongoni mwa Mitume
Paulo mtume akishuhudia yeye mwenyewe kwamba alikuwa mwenye dhambi, mtukanaji na muongo Itimotheo 1:12-15 na Matendo 26:9-11

Je ninani nanastahili kuwa Muhudumu wa Agano jipya? Paulo mtume anasema Mungu ndiye atustahilihishaye 2Wakoritho 3:5

Ndugu zangu Mabadiliko ni Mchakato, tunapompokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi katika maisha yetu uhalisia wa maisha hugawanyika katika maeneo makuu matatu, kuna mabadiliko ambayo utayapokea mara moja Instant na mengine utaanza kukamilishwa taratibu na hatimaye utakamilika katika kifo, Instant Sanctification, Progressive sanctification and Perfect Sanctification !

Mwanzo 43: 1-9 Maisha ya Yuda baada ya miaka yalikuwa yamebadilika kabisa, Yuda aliyekuwa na Ubinafsi,Uasherati, Umimi choyo na kuhukumu sasa ameacha kabisa kujifikiri mwenyewe

Anafikiri kuhusu Familia yake yote anajua kuwa wanahitaji chakula ili waishi, anafikiri kuhusu Familia yao na maisha yao ya baadaye watakuwaje

Anafikiri kuhusu Ndugu yake Simeon ambaye amefungwa na Yusufu anafikiri namna atakavyomrudisha nyumbani lakini sasa ni lazima waende na Benjamin

Yuda amabye alikuwa hafikiri sawasawa sasa  amekuwa na ushawishi yuko tayari kuyatoa maisha yake kwa  Usalama wa Simeon, Benjamin, Baba yake na Familia nzima, yuko tayari kubeba lawama za wote milele kama hatathibitisha uaminifu kwa baba yake Yuda sasa Amekuwa amekomaa
Mungu hutumia majaribu na mapito kadhaa katika maisha kutubadilisha kitabia Yakobo 1:12, 1Petro 6-7
Mungu wakati wote ana mpango wa kukamilisha ndoto zetu na makusudi yake katika maisha yetu yuko tayari kugharimika kwa namna yoyote katika kuhakikisha kuwa kusudi lake ndani yetu linatimia uisnihukumu, nisikuhukumu, tusihukumiane kabla ya wakati Mungu ni Mfinyanzi na sisi tu Udongo maadamu tuko mikononi mwake atatugeuza kokote apendako Yeremia 18:1-6

Yuda yuko tayari kuwa Mtumwa kwa aajili ya Ndugu yake na Baba yake mzazi ndugu Yakobo wasiumizwe Mwanzo 44:33, Yuda alikuwa mwenye moyo wa toba sasa na mwenye kuamini katika hukumu za Mungu na kisasi cha Bwana Mwanzo 44;16

Mungu atatutumia kwa kiwango cha juu na kutufanya Baraka tutakapofikia katika badiliko kuu ambalo yeye amelikusudia Wagalatia 4:1-5 tusikubali kubaki kama watoto wadogo tuliodumaa Mungu anatutaka tukue na kubadilika 1Petro 2;2 2Petro 3;18 Waebrania 5:11-61 Biblia inatutaka tukue

Ukiyajua hayo heri wewe ukiyatenda

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.
Rev. Innocent Kamote.

SINA KITU SASA LAKINI NINA CHA KUKUMBUKA!


Ndugu wawili walipanga kuwa na safari, na siku moja jiono waliamua kujipumzisha katika moja ya misitu mikubwa, walipokuwa wakiangalia huko na huko humo waliona jiwe lililokuwa na maandishi yafuatayo;-




"Ulimwengu wa Mafanikio uko na wale wanaothubutu"

Yeyote atakayeliona jiwe hili” walilisoma “ na aingie moja kwa moja msituni wakati wa jua kupunga yaani jioni, Ndani ya msitu mto utatokea ogelea mto huo mpaka ufike upande wa pili, hapo utaona gari zuri na ufunguo wake endesha gari hilo mpaka kwenye kilele cha mlima bila kuangalia nyuma, utakapofika mlimani utaona nyumba na ndani ya nyumba niyo Utapata furaha kuu” walipomaliza kusoma habari hii katika jiwe Kaka mdogo akasema Kaka tafadhali twende….. tunaweza kuogelea na kuuvuka mto huu na kuchukua gari na kupata nyumba na huko mlimani tutaipata furaha kuu!

Sitakwenda sitaingia msituni na kuogelea sita vuka huko alisema Kaka mkubwa na kisha akamsahauri nduguye, “fikiria labda yaliyoandikwa humu ni fumbo, au labda tunaweza kuwa hatujasoma sawasawa, au tumesoma na hatukuelewa, na hata kama yaliyoandikwa hapa ni kweli jaribu kuwaza kama tutavuka na tusiuone mto au kama tunaweza kuuona na tukashindwa kuogelea  au kama tutaogelea na kuvuka nay ale yaliyoahidiwa upande wa pili yakawa hayako na badala ya kupata furaha kuu, tukajikuta tunaangamia, tutawezake kuupanda mlima bila kupumzika wala kugeuka nyuma inawezekana ile furaha kuu tunayoitazamia ikawa ni msiba mkuu sana kwetu

“Kwa maoni  yangu” alisema kaka mdogo “Hauko sahii” Yaliyoandikwa katika jiwe hili hayangelikuweko hapa pasipo sababu, Na ni wazi kwamba Hakuna madhara yanayoweza kutupata endapo tutajaribu kama tutajaribu, aidha kwa upande mwingine kama hatutalifanyia kazi hili kuna mtu mwingine atasoma na kulifanyia kazi yaani haya yaliyoandikwa kwenye jiwe na atapata furaha kuu, sisi tutapoteza na mimi sitaki tupoteze nafasi hii”

Kaka mmkubwa alijibuna kusema kuna mithali isemayo “ Mtaka cha uvunguni shurti ainame” yaani katika kutafuta furaha kuu tutapata majaribu na maumivu, na pia mithali nyingine inasema “Ndege aliye mkononi ni bora kuliko wawili walioko Porini” Kaka mdogo akajibu na kusema nimesikia Basi yeye anayeogopa asiingie msituni, Basi kaka mdogo akaingia msituni na kuanza safari na mkubwa akabaki nyuma, ndugu mdogo aliingia msituni usiku na akauona mto uliokuwa umeelezwa, akaogelea na kuvuka nga’mbo na akaiona gari na ufunguo wake na kuingia na kuiendesha  akapanda mlimani bila kuangalia nyuma alienda kwa muda mrefyu na hatimaye aliiona nyumba, kaka mkubwa alirudi nyumbani.

Aliingika katika nyumba ile na kuikuta iko vizuri sana imeandaliwa vema na alipoingia mara kundi kubwa sana la watu wakaja kumpokea kwa ujasiri, wakamkaribisha katika mji wao wakampaka mafuta na kumtawadha kuwa Mfalme wao akaishi kwa furaha kuu akitawala kwa miaka mitano, mwaka wa sita aliinuka mtawala mwingine wa mji mwingine mwenye nguvu na wakafanya vita na ufalme wake na katika vita ile mfalme huyu alishindwa na kila kitu kilitawaliwa na Yule mfalme mwenye nguvu, kwa kuwa hakuuawa aliamua kurudi kwa kaka yake

Kaka yake alikuwa akiishi kijijini na hakukuwana mabadiliko yoyote katika maisha yake hakuwa tajiri wala masikini aliishi kawaida tu, Kaka mkubwa alifurahi kumuona ndugu yake wakakumbatiana kwa furaha hasa kwa kuonana katika maongezi yao Kaka mkubwa alimwambie ndugu yake unaona nilikuambia nilikuwa sahii mimi nimeishi kwa raha mustarehe japo maisha yangu yalidumaa niko vilevile, wewe umerudi duni ingawa ulikuwa mfalme na umekutana na taabu kubwa sana na vita  kaka mdogo alijibu, “Sijutii niliyokutana nayo nimevuka mto na nimepanda mlima, nimekuwa mfalme na nimetawala inawezekana nimerudi nikiwa sina kitu sasa lakini nina cha kukumbuka na kuelezea watu wewe huna cha kuelezea wala cha kukumbuka” – wise man Leo Tolstoy interpreted by wise Master mason Rev. Innocent Kamote.

"Ulimwengu wa Mafanikio uko na wale wanaothubutu"