Jumanne, 14 Machi 2017

Hazina katika vyombo vya Udongo.


Mstari wa Msingi: 2 Wakoritho 4:7Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu wala sio kutoka Kwetu


Utangulizi:-

Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kujitambua na kujifahamu kuwa tumeumbwa kwa njia ya jabu sana, na hivyo ni vema katika maisha yetu tukampa Mungu utukufu siku zote na kumshukuru yeye anayetuwezesha na kuyashikilia maisha yetu, Maandiko yanatufananisha sisi kwa Mungu kama viumbe dhaifu sana yaani tumeumbwa kwa udongo, sisis ni kama chombo cha udongo katika mikono ya Mungu na Mungu baba yetu ndiye mfinyanzi kwa maana hiyo imetupasa kuishi na kuendena kwa unyenyekevu mkubwa, vipawa na akili na karama Mungu alizowekeza ndani ya Mwanadamu ni hazina sio ya kujivunia bali ni kwaajili ya utukufu wa Mungu.



Vyombo vya Dongo:

2 Wakoritho 4:7Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu wala sio kutoka Kwetu” tunaweza kuutafasiri mstari huu katika lugha nyepesi ya mkuu wa wajenzi hivi “Lakini kuna vitu vya thamani kubwa sana vimewekwa katika vyombo vya dhaifu vya udongo, ili utukufu na sifa kuu iwe ya Mungu wala sio kutoka kwetu”

Kwa nini Paulo mtume anazungumza maneno mazito namna hii na je yana maana gani kwetu? Ni muhimukwanza tukawa na ufahamu wa kutosha kuhusu vyombo vya dongo, Vyombo vya udongo anavyozungumza Paulo Mtume ni vyombo vilivyotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi na kuumbwa na mfinyanzi kwa ustadi kulingana na makusudi na matakwa ya mfinyanzi husika, Mara baada ya kufinywangwa vyombo hivyo vilichomwa kwa moto ili kuweza kuvifanya imara, baada ya hatua hiyo vingeweza kupakwa rangi na kuchorwa maua ya aina mbalimbali ya kupendeza na kuwa na muonekano mzuri sana

Nyakati za Biblia zamani sana vyombo vya udongo vilitumika kwa kusudi pia la kuhifadhi au kuficha hazina au vitu vyenye thamani sana, mfano halisi ni kuwa watu wa kale waliwahi kuhifadhi katika vyungu magombo ya chuo cha nabii isaya na vitabu vingine vya ngozi vilivyotumika zamani, Mfano halisi ni katika bonde la Qumran yaliwahi kuokotwa magombo ya ngozi yaliyokuwamo katika vyombo vya dongo vya kale, vijana wa kiislamu waliokuwa wakichunga Kondoo walikuwa wakirusha mawe huenda ni katika lengo la kutafuta kondoo, walisikia mlio Fulani wa chungu katika pango, walipofika kumbe ni chungu au mitungi iliyoundwa kwa dongo na ndani yake kulikuwa na ngozi zilizokuwa na maandishi, wao wakiwa hawajui maandishi hayo walitaka kuzitumia ngozi hizo kutengenezewa viatu, Mafundi waligundua kuwa yalikuwa ni maandiko matakatifu waliyapeleka kwa Kanisa na yakahifadhiwa chuo cha nabii Isaya kwa mfano kilipatikana kamili kama ilivyo Biblia katika magombo hayo.

Kutokana na mtazamo huo Paulo mtume anatukumbusha katika 2 Wakoritho 4:7 kuwa wanadamu tunafanana sana na vyombo hivyo vya udongo, karama, akili na vipawa alivyotupa Mungu ni hazina tu iliyohifadhiwa katika vyombo dhaifu sana vya dongo, vyombo ambavyo ni dhaifu na vinaweza kuvunjika wakati wowote na kwa njia rahisi “very delicate” ukweli huu haupingiki kwa sababu biblia iko wazi kuwa wewe na mimi tuliumbwa kwa Udongo Mwanzo 2:7 Biblia inasema “. BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Unaona? Mpendwa wewe na mimi ni mavumbi yaani ni udongo tu! Mungu analijua vema sana umbo letu na kukumbuka kuwa sisi ni mavumbi Zaburi 103:14 Biblia inasema Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.” Je unajua kuwa Mungu anakumbuka kuwa sisi tu mavumbi? Ndio ni muhimu kukumbuka lakini pamoja na kuwa Mungu ametuumba kwa udongo ameweka vitu vya thamani kubwa ndani yetu ambavyo hata Malaika hawana!

Kutokana na jinsi Mungu alivyotuumba kwa thamani kubwa kiasi hicho ingawa ni dhaifu sana lakini ameweka vitu vya thamani na ujuzi wa hali ya juu na karama na vipawa ndani yetu, Hata hivyo Mungu anatuonya katika neno lake kuendelea kumuheshimu yeye na kujihadhari na majivuno ya aina yoyote na kuenda mbele zake kwa unyenyekevu mkubwa na kumrudishia yeye utukufu, heshima na adhama kwa sababu yeye ni mfinyanzi na sisi ni kama vyombo hivyo dhaifu mikononi mwake Isaya 45:9Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono?” Unaona ni maonyo makali kutoka kwa Mungu kupitia Nabii Isaya hatuwezi kuwa Jeuri kwa Mungu mimi na wewe ni kama Kigae Biblia inasema ole wetu kama tutashindana na Muumba! Isaya 64:8 “Lakini sasa, Ee Bwana, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.” Hatuwezi kushindana na Mungu Baba yetu inatupasa kuwa wanyenyekevu mno kwani sisi ni udongo na Mungu baba yetu ni mfinyanzi tu sisi ni dhaifu Mungu na atusaidie tusijivune kwa jambo lolote.

 "Paulo Mtume alikuwa dhaifu katika mwili lakini alijaa Neema na Kweli alikuwa kama Malaika"

Hazina katika vyombo vya udongo!

Paulo mtume anapozungumzia Hazina katika vyombo vya udongo alikuwa na maana pana zaidi ingawa msingi wake mkubwa ni jinsi Mungu alivyowekeza siri zake katika mioyo yetu, siri ya injili, Paulo anazungumzia nguvu na uwezo wa Mungu, vipawa na karama ambazo zimewekezwa ndani ya mtu kiasi ambacho mtu akisikia habari zako anaweza kudhani kuwa wewe ni jitu kubwa sana
Paulo alikuwa na ujuzi wa nguvu za Mungu na udhaifu wa mwili wa binadamu ambao ni kama udongo Mungu alimtumia Paulo mtume kwa miujiza ya viwango vya kupita kawaida Biblia inatoa majumuisho tu ya huduma ya Paulo na jinsi Mungu alivyomtumia kwa kusema 

·         Matendo 19:11Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida;”
·         Licha ya Mungu kumtumia Paulo kwa mijuiza mikubwa ya kupita kawaida lakini ni wazi kuwa Mtume Paulo ndiye mtume aliyefanya kazi kuliko mitume wote kama maandiko yanenavy 1Wakoritho 15:10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.
·         Licha ya Paulo kutumiwa na Mungu na kufanya kazi kuliko mitume wote yeye alipewa mafunuo makubwa sana kuliko mtume yala mtumishi yeyote Paulo alipelekwa mpaka Mbingu ya tatu akaonyeshwa mambo mazito na meneno mazito ambayo mengine ni magumu kuyaeleza angalia 2Wakoritho 12:2-4 “Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.  Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua); ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene”.
·         Paulo Mtume alikuwa Mwombaji, alikuwa akinena kwa lugha kuliko mtu yeyote, alikuwa na karama zote alikuwa na uwezo wa kuimba mpaka malango ya gereza yanafunguka, aliombea watu wa kila aina na kuponya wenye magonjwa, Paulo alikuwa Msomi ni Daktari wa Sheria aliyebobea na kadhalika 

Lakini pamoja na vipawa alivyokuwa navyo hakusahau kuwa yeye ni mavumbi alitambua kuwa Mungu ameweka hazina katika vyombo vya udongo tu na Historia ya kanisa inaeleza kuwa Paulo mtume ndiye aliyepatwa na majaribu mengi zaidi na mateso mengi zaidi kwaajili ya Kristo na injili, inasemakana kuwa Paulo mtume hakuwa jitu kubwa alikuwa ni mwembamba sana mwenye matege na nyele zake zilikuwa zimejinyonganyonga kama mmanga, aidha alikuwa na udhaifu katika mwili wake alikuwa anaumwa na pia alikuwa na macho dhaifu sana 2Wakoritho 12:7-9 Biblia inasema hivi “.Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”. 

Unaweza kuona! Paulom mtume alikuwa na mwili dhaifu na pia macho dhaifu aliomba kuondolewa tatizo hilo lakini Mungu alimwambia ni neema yangu tu inakutosha ili asiwe na Majivuno, Wagalatia 4:13-15 Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili; na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu.  Ku wapi, basi, kule kujiita heri? Maana nawashuhudu kwamba, kama ingaliwezekana, mngaling'oa macho yenu, mkanipa mimi”.  Paulo mtume alikuwa na udhaifu katika mwili wake pamoja na kuombea wengi Mungu aliyaachia kwaajili ya utukufu wake ni kwaajili ya haya Paulo anaona kuwa Mungu ameweka hazina katika vyombo vya udongo.

Ndugu msomaji wangu hatuna cha kujivunia? Tunapaswa kuwa wanyenyekevu, tunapaswa kumpa Mungu utukufu, lakini hata kama ni wadhaifu hatuna hiki ama kile hiyo haipunguzi thamani ya kuumbwa kwako mfinyanzi ameliweka kusudi lake ndani yako usikate tamaa lakini kumbuka kuwa sisi ni binadamu ni daifu na Mungu ni mwenye nguvu ni mfinyanzi na tuishi mbali na majivuno ya aina yoyote tuwapo ulimwenguni

Mungu alimtuma Musa licha ya kuwa na kigugumizi, alimtumia Elisha licha ya kuwa na Upara, alimtumia Daudi licha ya kuwa na umri mdogo na kudharaulika hata kwa baba yake, acha kujidharau kwa sababu zozote zile 

Kumbuka kuwa asili ya nguvu zetu, uzuri wetu, ujuzi wetu, heshima yetu na mali zetu zimetokana na Mungu muumba wetu. Ukiyajua nhayo heri wewe ukiyatenda

Na mkuu wa wjenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote

Ijumaa, 10 Machi 2017

Kwa nini Naipenda Israel kwanini Naipenda Yerusalem!



Zaburi 137:5,6Eee Yerusalem nikikusahau wewe Mkono wangu wa kuume na usahau, Ulimi wangu na uganadamane na Kaakaa la kinywa changu nisipokukumbuka, Nisipoikuza Yerusalemu zaidi ya furaha yangu iliyo kuu

 Pichani Jiji la yerusalem Maarfuru kama old Jerusalem ikionekana katika utukufu wake
 
UMUHIMU WA KUIPENDA ISRAEL. (JERUSALEM)

Mji wa Yerusalem ambao ni mji mkuu wa Israel ni mji muhimu sana katika maswala ya kisiasa kiimani na kiusalama mjii huu ni picha ya mji halisi ulioko peponi au mbinguni ambao ni makao makuu ya serikali ya Mungu Mbinguni, 

Mungu ana mji ulioko Juu mbinguni na mji huu unaitwa Yerusalem Wagalatia 4:25- 26Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalem wa sasa kwa kuwa anatumika pamoja na watoto, Bali Yerusalem wa juu ni mwungwana naye ndiye mama yetu sisi” 

Katika maandiko hayo Paulo mtume anaonyesha kuwa kuna Yerusalem ya Duniani naya mbinguni miji yote hii ni makao makuu ya serikali ya Mungu aliye hai, Yerusalem iliyoko Israel ni makao makuu ya Mungu Duniani na Yerusalem ulioko mbinguni ni makao makuu ya serikali ya Mungu.

Mji huu ni wa muhimu sana wengi waliotambua siri ya umuhimu wa mji huu wanaupenda na watakatifu waliotutangulia waliomba wasiisahau Yerusalem Zaburi 137:5,6Eee Yerusalem nikikusahau wewe Mkono wangu wa kuume na usahau, Ulimi wangu na uganadamane na Kaakaa la kinywa changu nisipokukumbuka, Nisipoikuza Yerusalemu zaidi ya furaha yangu iliyo kuu

 unaweza kuona Yerusalemu ni zaidi ya furaha ya watakatifu

Kama ilivyo kwa almasi katika kiti cha sofa ndivyo ulivyo mji wa Yerusalem mji huu ukokatikati ya vilele vya Safu ya milima ya Yudea (Uyahudi) na kwa ujumla ni katikati ya Dunia kijiografia, maisha na hatima ya wanadamu wote duniani iko au imefungamanishwa na mji huu wa kipekee, Tangu wakati wa Ibrahim nabii Israel imekuwa ni makao makuu ya ukombozi wa Mwanadamu, wakati huu dunia inapoelekea ukingoni Israel inaanza kuwa ngome tena ya kufunua makusudi ya Utawala wa Mungu duniani na ngoma ya kuchezwa mbele ya wanadamu na malaika.

Wakristo na hata wasio wakristo wanapaswa kuwa na uelewa wa kutosha Kuhusu Israel na Jerusalem na uhusiano wetu kiimani Biblia inaonyesha upekee wa hali ya juu kuhusu Israel na Yerusalem na kukosa ufahamu huu kunaweza kutunyima Baraka za kipekee zilizofichwa kuhusu inchi hii na mji huu

Nchi yangu na Mji wangu!

Zaburi ya 21:1 “Biblia inasema Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. “ unaweza kuona Biblia inatufundisha kuwa nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana na Dunia yote na watu wote, hivyo kuna uweli kuwa kila inchi ni ya Mungu na kila taifa ni la Mungu na watu wote ni wa Mungu katika ujumla wake, lakini katika upekee wake Israel na mji wake mkuu Yerusalem ni Mji mtakatifu wa Mungu na ushahidi wa kimaandiko upo kuthibitisha kuwa kuna utofauti kwa nchi hii na mji huu

1.    Unaitwa mji Mtakatifu “Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; Jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, MJI MTAKATIFU; Kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako Asiyetahiriwa, wala aliye najisi.” Biblia inasema katika Isaya 52:1
 
2.    Yesu mwenyewe aliupenda mji huu licha ya kuutolea Machozi katika mafundisho yake aliuita mji wa Mfalme mkuu angalia Mathayo 5:35Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;    34. lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;35. wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa YERUSALEMU, KWA MAANA NDIO MJI WA MFALME MKUU” Yesu anatambua kuwa mji huu ndio makao yake makuu, mfalme mkuu ni yeye, mji huu ni wake unawezaje kusema kuwa unampenda Yesu kisha unachukia mji wake na serikali yake na makao yake makuu?

3.    Kiti cha enzi cha Mungu Yeremia 3:17 Wakati ule watauita Yerusalemu kiti cha enzi cha Bwana; na mataifa yote watakusanyika huko Yerusalemu, kwa ajili ya jina la Bwana; wala hawatakwenda tena kwa ukaidi wa moyo wao mbaya.”

4.    Mungu aliahidi kuliweka Jina lake pale Yerusalem milele soma 2Nyakati 33:4 Biblia inasema ”Akajenga madhabahu katika nyumba ya Bwana, napo ndipo alipopanena Bwana, Katika Yerusalemu litakuwako jina langu milele

5.    Maandiko yako wazi kuwa Mungu anajivunia Yerusalem angalia Zaburi 87:1-3 Biblia inasema “Msingi wake upo Juu ya milima mitakatifu. Bwana ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo. Umetajwa kwa mambo matukufu, Ee Mji wa Mungu.”

6.    Yerusalem ni sababu ya Furaha Isaya 65:19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.”

7.    Isaya alisema kwaajili ya Yerusalem yaani sayuni sitanyamaza Isaya 62:31. Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo. 2. Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana. 3. Nawe utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa Bwana, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.” Unaweza kuona jinsi mji huu uliyounganishwa na shughuli za kinabii na kiimani wote waliokuwa wakimpenda Mungu kwa dhati waliipenda Yerusalem kwa dhati vilevile

8.    Unabii unaonyesha kuwa siku za mwisho watu wengi sana wataitembelea Israel yaani wataitembelea Yerusalem makundi kwa makundi Isaya 2:3 “1. Hili ni neno aliloliona Isaya mwana wa Amozi katika habari za Yuda na Yerusalemu. 2. Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi.  3. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu. 4. Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe. 5. Enyi wa nyumba ya Israeli, njoni, twende katika nuru ya Bwana”.Unaona unabii wa Isaya watu wote wataiendea Yerusalem huko ndiko itokako amani ya watu wote huko ndio asili nya Neno la Mungu, huku ndio asili ya mafundissho yote Yerusalem Yerusalem!

Mungu hajamaliza na Yerusalem ya Asili

Ni muhimu kwa kila mkristo kuwa na uelewa huu kuwa Mungu hajamaliza kazi yake na mji huu Yerusalem wa Duniani, nasema hivi kwa sababu mtu anaweza kujenga Hoja za kimaandiko kuwa isis kama Ibrahimu tunautazamia mji wenye misingi ambao mwenye kuujenga na kuubuni ni Mungu, akiwa na maana ya Yerusalem ya Mbinguni  sawa na Waebrania 11:10 ambapo Biblia inasema “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 9. Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 10. Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.” 

Maandiko yanaonyesha kuwa Ibrahim kwa Imani alikuwa akiutazamia Mji wa Mbinguni kwa vyovyote vile Yerusalem wa Mbinguni, Pia tunaweza kuona msisitizo wa Paulo Mtume kwa Wafilipi 3:20Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;” na tunaambiwa kuwa Yerusalem wa Mbinguni ndio mama wa yote Waebrania 12:22 na kuwa kila aliyeamini ameungamanishwa na Sayuni ya Mbinguni au Yerusalem ya Mbinguni  Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,”

Na Kama haitoshi Yesu mwenyewe alionyesha kuwa ndani ya agano jipya watu wangefurahia uwepo wa Mungu katika roho na kweli ikiwa na maana ya ibada halisi haitategemea Hekalu Yerusalem wala mlima Fulani kwa vile Mungu anataka kuabudiwa katika roho na kweli angalia Yohana 4:21-24 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu. Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”. 

Kama utaviangalia kwa makini vifungu vyote vya maandiko hapo juu unaweza kudhani kuwa Mungu hana kazi tena na mji wa Yerusalem wa sasa na Taifa la Israel, unaweza kufikiri kuwa makusudi yake yamekwisha 

Lakini turudi tena katika Mathayo 5: 35 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34. lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;35. wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa YERUSALEMU, KWA MAANA NDIO MJI WA MFALME MKUU” Yesu anaonyesha kuwa tusiape kwa Yerusalem kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu hii ina maana gani kwa nini asiseme kwa vile ulikuwa mji wa mfalme mkuu? Kwanini Mungu Hajamaliza kazi yeke na mji huu wa Yerusalem wa asili

Yesu alisema Yerusalem utakanyagwa na mataifa kwa kitambo Luka 21:24 “…..Na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia” 

“Kama Maandiko yametoa nafasi ya kukanyaga Israel na Yerusalem naamini ni vema wakristo tukaitumia nafasi hiyo ya kwenda Israel na kutembelea nchi hiyo ya kipekee kwani utakuja wakati itakuwa ngumu sana kuitembelea Israel hata kama utakuwa na uwezo huo” huu ni mtazamo wa kinabii wa mkuu wa wajenzi hapa.

Maneno hayo ya kinabii yanamaanisha kuwa mataifa wataukanyaga kwa muda na hatimeye mjii huu utarejeshwa katika utukufu wake , Yesu Kristo atakaporudi katika utukufu wake atasimamisha serikali yake kutoka mji huu na kutawala akiwa MFALMA WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA Kutoka Israel Yerusalem angalia

 Zekaria 14:4, 9Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini. , Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja” 

Kwa hiyo iko wazi kuwa mjii huu bado uko na uhusiano mkubwa na maswala ya kiimani ni wazi kuwa kuna Baraka za kimungu kama tunautakia mafanikio, na hata ingawa kunaweza kusiwe na Uhusiano wa kiibada na Israel au Yerusalem lakini huwezi kukataa kuwa kuna ahadi za mafanikio kwa wanaoiombea Israel na wamnaoutakia mema Yerusalem

Utakieni Yerusalem Amani!

Zaburi ya 122 :6-9 inasema hivi:- “Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;. Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.  Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema

Biblia inaamuru “Utakieni Yerusalem Amani” na inaunganisha Baraka kubwa na wale waipendao Yerusalem wafanikiwe wakupendao, Mema yataambatana na kila Mkristo na mtu aiye mkristo anayeitakia Mema Israel na Yerusalem

Mungu anataka tufurahi pamoja na Israel Isaya 65:18 , 19 a na 66:10-13 Biblia inasema haya

“18. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. 19. Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. 10. Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; 11. mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. 12. Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. 13. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu.”

Yesu aliipenda Yerusalem kiasi cha kuulilia mji huu, Nehemia aliugua na kufunga na kuomba kwaajili ya Yerusale, Yesu anaitamani Yerusalem mpango wake ni kuukumbatia ni kuukusanya kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake! Mathayo 23:37Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka! “ Yerusalem walikataa mapenzi ya Mungu kwa kumkataa masihi na kumsulubisha nje ya mji huu, lakini Mungu anawatamani sana Israel na ni mapenzi ya Mungu waokolewe na mjii huu kwa vyovyote vila ndio utakuja kuwa makao makuu ya Masihi Yesu.

Siri ya tai ya rangi ya blue katika shati Jeupe!
 

Kwa nini Viongozi katika Israel na Marekani huvaa tai ya rangi ya Blue? Ngoja nikuambie siri ya tai ya rangi ya blue na Nyekundu kwa Marekani, Bendera ya marekani ina rangi nyeupe, Nyekundu na blue, Chama cha republican huwakilihwa na rangi nyekundu na chama cha democratic huwakilishwa na rangi ya blue hii ni alama kubwa sana kwa taifa lao, wanapovaa tai viongozi wao huvaa kuonyesha uzalendo wa taifa lao katika maswala ya kitaifa

Pia kwa vile wamarekani wana uhusiano mkubwa sana na Israel pia kuvaa tai ya blue kwao humaanisha wazi kuipenda na kuiunga mkono Taifa la kiyahudi, Wayahudi bendera yao ni yeupe na ina mistari ya blue na nyota ya Mfalme Daud iliwa na rangi ya blue hivyo viongozi wa kitaifa kwao huvaa tai ya blue
Uganda bendera yao ina rangi nyekundu,mkenya pia na nyeusi na njano, Rais Museven hupenda kuvaa tai ya Manjano kwa vile ni rangi ya taifa lao katika bendera yao
Ukiona kiongozi wa kitaifa katika taifa ambalo halijamwaga Damu amevaa tai nyekundu maana yake huvaa tu bila kuzingatia amevaa kwa maana gani

Tai ya blue ikivaliwa na mtu anayejua maandiko humaanisha wazi kuwa anaipenda Israel, scafu na kadhalika kwa msingi huo kama unaipenda Israel katika kuonyesha mapenzi yako kwa taifa hilo vaa tai ya blue kuna siri kubwa katika jambo hilo kwaajili ya kuonyesha unaiunga mkono Israel
Kwa bahati njema kwa watanzania tai ya blue pia itakuwa ni sehemu ya Bedera yetu katika zile rangi nne mamarufu kwa hiyo tai ya blue itamaanisha uzalendo kwa taifa lako lakini kiroho Israel, hii ni siahara nyingine ya kuipenda sayuni.

Ujumbe na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.