Jumatano, 13 Novemba 2019

Mtu wa Kwenu akipungukiwa na Hekima!


Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.”


Utangulizi:
Neno la Mungu linasisitiza sana umuhimu na ubora wa kuwa na Hekima, Kitabu cha Mithali na Muhubiri vimekazia tena na tena vikitoa ushauri, na kuelezea umuhimu wa Hekima na vikisisitiza kuwa ni muhimukwetu kuhakikisha kuwa tunamiliki hekima kwa gharama yoyote ile

Mithali 4:7 “Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.”

Wenye hekima wanahitajika kila Mahali, Nyakati za kanisa la kwanza walijua wazi kuwa wakiwepo watu wenye hekima, uko uwezo wa kutatua changamoto za aina mbalimbali zinazolikabili kanisa na dunia kwa ujumla, Wenye hekima walihitajika katika kanisa kwaajili ya kutatua changamoto za aina mbalimbali

1Wakoritho 6:5 “Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake?
Matendo 6:1-3 “Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;
Mfalme Sulemani pamoja na utajiri na fahari kubwa sana aliyo nayo alikuwa na ufahamu kuwa Hekima ni ya thamani kuliko rubi nay a kuwa hakuna jambo linaweza kulinganishwa na Hekima

Mithali 8:11 “Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.”
Kwa nini Maandiko yanatuisistiza sana juu ya kuhitaji Hekima

1.      Itatusaidia kujua mema na mabaya katika mtazamo wa Mungu na hivyo itatupa furaha na amani Mithali 3:13-16 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi. Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye. Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.

2.      Itatusaidia kutatua matatizo yenye utata na kuyapatia ufumbuzi au kuamua vema 1Wafalme 3:16-28 “Ndipo wanawake wawili, makahaba, walimwendea mfalme, wakasimama mbele yake. Na mwanamke mmoja akasema, Ee bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunakaa katika nyumba moja; nami nalizaa nilipokuwa pamoja naye nyumbani. Kisha, siku ya tatu baada ya kuzaa kwangu, ikawa mwanamke huyu naye akazaa; na sisi tulikuwa pamoja; hapakuwa na mtu mwingine pamoja nasi nyumbani, isipokuwa sisi wawili tu. Na mtoto wa mwanamke huyu akafa usiku, maana alimlalia. Akaondoka kati ya usiku, akamwondoa mtoto wangu ubavuni pangu, mimi mjakazi wako nilipokuwa usingizini, akamweka kifuani pake, na mtoto wake mwenyewe, aliyekuwa amekufa, akamweka kifuani pangu. Nilipoondoka asubuhi nimnyonyeshe mtoto wangu, kumbe? Amekufa. Hata asubuhi nilipomtazama sana, kumbe! Siye mtoto wangu niliyemzaa. Ndipo yule mwanamke wa pili akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wangu ndiye aliye hai, na mtoto wako ndiye aliyekufa. Na mwenzake akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wako ndiye aliyekufa, na mtoto wangu ndiye aliye hai. Ndivyo walivyosema mbele ya mfalme. Ndipo mfalme akasema, Huyu anasema, Mtoto wangu yu hai, na mtoto wako amekufa. Na huyu anasema, Sivyo hivyo; bali mtoto aliyekufa ni wako, na mtoto aliye hai ni wangu. Mfalme akasema, Nileteeni upanga. Wakaleta upanga mbele ya mfalme. Mfalme akasema, Mkate mtoto aliye hai vipande viwili, kampe huyu nusu, na huyu nusu. Ndipo mwanamke yule, ambaye mtoto aliye hai ni wake, akamwambia mfalme kwa maana moyoni mwake alimwonea mtoto wake huruma, akasema, Ee bwana wangu, mpe huyu mtoto aliye hai, wala usimwue kamwe. Lakini yule mwingine akasema, Asiwe wangu wala wako; na akatwe. Ndipo mfalme akajibu, akasema, Mpe huyu wa kwanza mtoto aliye hai, maana yeye ndiye mama yake. Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.

3.      Itatusaidia kujibu mafumbo na maswali Magumu 1Wafalme 10:1-3 “Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la Bwana, alikuja ili amjaribu kwa maswali ya fumbo. Akaingia Yerusalemu na wafuasi wengi sana, na ngamia wachukuao manukato, na dhahabu nyingi sana, na vito vya thamani; alipomfikilia Sulemani, akazungumza naye mambo yote aliyokuwa nayo moyoni. Naye Sulemani akamfumbulia maswali yake yote; wala hakukuwa na neno alilofichiwa mfalme asimwambie.


Napenda tafasiri ya biblia ya kiingereza ya Amplified Bible mahali hapa inasema “SHE  CAME TO TEST HIM WITH HARD QUESTIONS” yaani alikuja kumjaribu kwa maswali Magumu, Lakini Sulemani aliyatatu yote mpaka yaliyofichika nyuma yake.

Wakati huu tunapopitia mitihani, pamoja na majaribu ya aina mbalimbali hapa duniani, ni wazi kuwa tunahitaji Hekima,Yakobo aliyesema tuombe Hekima alikuwa ni moja ya watu muhimu waliotatua matatizo mangi katika nyakati za kanisa la Kwanza,Hekima kubwa ya Mungu ikionekana kukaa juu yake, kwa msingi huo ni kama anatupa majibu yaliyo wazi kuwa ni namna gani tunaweza kuipata Hekima, Yeye anasema ni lazima tuombe, kwamba tukiomba, Mungu hana kizuizi, hawezi kuzuilia hilo, hawezi kukunyima atakupatia, Hekima hii sio ile ya Darasani hii ni Hekima inayoshuka kutoka Mbinguni. Hekima hii itakufaa,katika maeneo mengi ya maisha kuleta suluhu wakati wa mahitaji. Uongezewe neema.

Na Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.
Rev. Innocent Kamote
0718990796

Jumanne, 12 Novemba 2019

Hata Malaika wapo!



Zaburi 34:7Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.


Hatuko peke yetu! Watu wengi sana huwa wanasahau hili, wanapopita katika changamoto za iana mbalimbali huwa wanadhani kuwa MUngu amewaacha, nasio tu kudhani kuwa Mungu amewaacha lakini hawana ufahamu kuwa watu wa Mungu wanalindwa na Majeshi ya malaika tunasahau kuwa Hata malaika wapo! Ndio Malaika wapo

Biblia inasema Hawa malaika ni roho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu Waebrania 1: 13-14; “Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”

Unaona Biblia inasema kuwa malaika ni viumbe wa kiroho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu, Malaika wapo, wakati unalia na kushangaa wana wanakushangaa kwanini unalia, kwanini huwatumii je unajua waoa hutuhudumia je unajua wao hututazama kwa macho mengine  wao hututia moyo pale tunapojihisi kuwa sisi ni Duni wao hutuona kuwa sisi mashujaa, Ndugu wewe ni zaidi ya Rais unalindwa na malaika pande zote usimtie Mungu aibu, wala usimfanye Mungu kuwa Bodigadi wako, How comes ulindwe na Mfalme wa wafalme ili hali majeshi yake yapo. Wapo wapo kukupa msaada unaoutaka kumbuka wanakuita wewe shujaa ona Waamuzi 6:12 “Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa.Hakukuwa na mtu muoga duniani kama Gideon Lakini malaika alimuita Ee Shujaa, Ndio ni shujaa kwa sababu haendi peke yake Malaika kibao wapo wanaenda pamoja naye iweje asiwe shujaa, angalia mtu anayelindwa na mabaunsa pande zote anawezaje kutembea kama mtu mnyonge? Ni Shujaa ndio ni shujaa kwa nini kwa sababu anazungukwa na ulinzi wa kutosha na kupewa msaada wa kila ainna autakao.
Malaika hawana Nguvu zote kama Mungu, lakini wana nguvu kuliko binadamu, katika rekodi za juu za kibiblia, Maandiko yanasema Malaika mmoja anauwezo wa kupiga watu 185,000, ndio nasema ndio malaika mmoja tu anauwezo huo soma Isaya 37:36Basi malaika wa Bwana alitoka, akaua watu mia na themanini na tano elfu katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.          
Sasa wewe unaogopa nini? Unaogopa wachawi? Unaogopa changamoto gani Biblia inasema malaika wa Bwana hufanya kituo (Hufanya Patrol) akiwalinda wale wanaomcha Mungu, na hawa unaona mmoja tu anauwezo wa kupiga watu 185,000, Ndio maana Daudi aliimba Bwana ni ngome yangu, Jeshi lijapojipanga kupigana nani moyo wangu hautaogopa!, Malaika wapo dada, malaika wapo, kaka, malaika wapo baba, malaika wapo ndugu yangu, waache wao watumie Majini, waache watumie uchawi waache watumie kila silaha wanayoweza sisi, tunatumia Malaika tunawaamuru Malaika waingilie kati katika kila hali inayotuzunguka na watatupigania

Malaika wanauwezo wa kukutoa katika kifungo cha aina yoyote, Matendo 12:5-11Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.

    
Petro alipokuwa Gerezani katikati  ya ulinzi mkali, kila mtu akitarajia kuwa atauawa Malaika alikuja na kumtoa gerezani, jamani malaika wapo, wakristo mailka wapo Hakuna sababu ya kuogopa chochote ni lazima na muhimu kumuamini Mungu, kuamini uweza wake kujua uuumbaji wake aliumba viumbe vinavyoonekana na visivyoonekana, Malaika hawaonekani lakini maandiko yanasema wapo, Mimi naamini wapo najua wanawajibika katika kile alichowaagiza Mungu najua wanafanya kituo, sihitaji ulinzi wa mabausa, wala Bodigadi wao wapo kwaajili yangu, wapo pia kwaajili yako huna sababu ya kuogopa mchana wala usiku kwa sababu wao wapo!
Hata malaika wapo!

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote
0718990796.

Usiudharau Msalaba!


Waebrania 12:2-3 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.”


Utangulizi:
Usiudharau Msalaba wa Yesu! Angalia iko nguvu ya ajabu na uwezo wa ajabu katika Msalaba, Msalaba unaweza kukupa ushindi dhidi ya changamoto zozote unazozipitia katika maisha, Ushindi mkubwa katika maisha yetu utapatikana kwa kitafakari kazi kubwa iliyofanya na Yesu Kristo pale Msalabani, wokovu kamili umekuja kwetu kupitia Msalaba na ndio maana ni muhimu sana kuutafakari , na kukumbuka kazi aliyoifanya Yesu Pale Msalabani

Paulo Mtume anaonyesha kuwa msalaba una nguvu, na kwa watu wanaopotea unaokana kuwa ni upuuzi lakini kwetu sisi tunaookolewa ni Nguvu ya Mungu angalia katika  1Wakoritho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.Ulimwengu unafahamu kuwa katika Historia Mfalme mmoja wa kipagani wa Rumi aliyejulikana kama CONSTANTINE akiwa pamoja na askari wake vitani tarehe 27/10/312 Baada ya Kristo, akiwa katika kambini Jeshini na wanajeshi wake aliona alama ya Msalaba upande wa juu wa jua na maandishi yaliyoansikwa kwa lugha ya Kiyunani, Lakini yanasomeka au yamepata umaatrufu zaidi katika Lugha ya KilatiniIN HOC SIGNO VINCES” Kwa kiinregreza “IN THIS SIGN YOU WILL CONQUERYaani kwa ishara hii Utashinda. Unaona kwa mujibu wa mwana historia maarufu wa karne ya tatu Askofu Eusebius wa Kaisaria anaeleza kuwa Contantine alikuwa akisonga mbele na jeshi lake  bila kutaja ni mahali ganina alipoangalia juu ya jua aliona msalaba unaong’ara  juuyake  yaliandikwa maneno hayo, inasemekana kuwa Contantine hakuwa ameelewa maana ya maono yale lakini usiku alipokuwa amelala aliona katika ndoto Yesu akimfafanulia kwamba anaopaswa kuitumia alama ya msalaba dhidi ya adui zake  na kuwa atapata ushindi, Tangu wakati huo wakristo wengi wa maeneo ya kilatini huutumia msalaba kama alama ya ushindi, wachezaji wa mpira wa miguu wanapoingia viwanjani hugusa uwanja na kuonyesha alama ya msalaba, alama ya msalaba ilipata umaarufu mkubwa kutokana na ushindi alioupata Contsntine ambaye baada ya ushindi wake aliifanya Roman kuwa himaya ya Kikristo.
Msalaba si jambo la kupuuzi ni ushindi wa maisha yetu, nilipokuwa nikitafakari kwamba ni jambo gani naweza kuzungumza na waomaji wangu na wasikilizaji wangu, Roho Mtakatifu aliniambia waaembie wasiudharau Msalaba, hii haina maana ya kuwa watu waubusu na kuuheshimu msalaba wenye sanamu ya Yesu hapana, maana yake ni lazima wakubali na kumtafakari Yesu mwenyewe aliyekubali kufa msalabani kwaajili yao/yetu.

Unapofungua Biblia yako katika injili ya Luka 23:35-43 tunapata habari za watu wawili wanaowakilisha jambo mmoja  watu wanaodharau kazi ya msalaba na wa pili watu wanaouheshimu msalaba watu hawa walikuwa karibu kabisa na Yesu aliyekuwa anasulubiwa hali kadhalika na wao walikuwa wakisulubiwa siku ile hebu tusome kwanza tuone
Luka 23:35-43 “Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake. Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki,  huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe. Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI. Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”
Unaweza kuona watu walimdharau Yesu pale msalabani, wakatoa maneno ya kejeli na kumfanyia mzaha walisema aliokoa wengine na ajiokoe mwenyewe hapa msalabani hususani kama yeye ndio masihi, aidha mhalifu mmoja aliyekuwa anasulubiwa pamoja na Yesu naye bila aibu alimtukana Yesu na kusema je wewe sio Kristo jiokoe nafsi yako na sisi, huyu aliupuuzia Msalaba na kujikuta yuko jehanamu milele na milele
Lakini yule muhalifu mwingine alikuwa na dalili kadhaa zilizomletea wokovu:-
a.       Alikuwa na Hofu ya Mungu Luka 23:40 alimuuliza mwenzake Je wewe humuogopi Mungu
b.      Alitambua kuwa yeye ni mwenye dhambi Luka 23:41 alimweleza mwenzake kuwa sisi tunasulubiwa kwa sababu ya maovu yetu na uhalifu wetu, hivyo tunapata kilicho halali yetu ni malipo ya maovu yetu  Lakini sivyo ilivyo kwa Yesu yeye yuko pale akiwa hata hatia
c.       Alimuamini Yesu kuwa anaweza kumuokoa Luka 23:42 alimwambia Yesu unikumbuke utakapokuja katika ufalme wako, Yeye aliamini kuwa Yesu huyu aliyetundikwa Msalabani ni mfalme na atatawala ilikuwa ni imani ya ajabu alikuwa na utambuzi kuwa msalaba sio mwisho wa maisha ya Yesu
d.      Mwisho Luka 23:42 alijiombea aweze kuokolewa alimwambia Yesu unikumbuke utakapokuja katika ufalme wako, jamaa alijitambua kuwa amefanya maovu mengi na kuwa hasathili chochote alijiombea rehema kwa Yesu palepale msalabani, huyu alikuwa ni kama mtu anayejua kuitumia nafasi aliyoipata katika dakika ya mwisho, ni kama timu iliyokuwa imekwisha kufungwa kisha ikasawazisha goli katika dakika ya nyongeza, Yesu alimjibu Lao utakuwa pamoja nani peponi
Unapopitia changamoto za iana yoyote, mitihani ya aina yoyote, mateso ya aina yoyote, majonzi ya aina yoyote, dhuluma ya aina yoyote machozi ya aina yoyote,kuonewa kwa namna yoyote, unyama wa aina yoyote, uonevu wa aina yoyote, majaribu ya aina yoyote, kucheleweshwa kwa aina yoyote, ni lazima ukumbuke na kuuangalia msalaba hapo ndipo palipo siri ya ushindi wako, ushindi wangu uko Msalabani, siogopi chochote Nauangalia msalaba kwa alama hii nitashinda kama alivyoshinda Mfalme Constantine, wewe nawe ni mshindi ni mshindi kupitia kazi iliyofanya na Yesu pale msalabani, mwangalie Yesu, katika mapito yako mwangalie Yesu , katika mateso yako mwangalie Yesu, katika ugumu wa maisha unaoupitia mwangalie Yesu, katika kesi yako na majonzi na mateso na njaa, na uchgu na kupungukiwa na aibu nadharau nakukataliwa na kutokufaanamakosa wewe mwangalie Yesu tu, na kwa kuiangalia kazi aliyoifanya pale msalabani wewe ni mshindi, Kumbuka Msalaba! Usiudharau!

Na Mkuu wa wajenzi mwenye hekima
Rev. Innocent Kamote.
 
0718990796.

Jumatatu, 11 Novemba 2019

Hata Malaika wapo!


Zaburi 34:7Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.

Hatuko peke yetu! Watu wengi sana huwa wanasahau hili, wanapopita katika changamoto za iana mbalimbali huwa wanadhani kuwa Mungu amewaacha, nasio tu kudhani kuwa Mungu amewaacha lakini hawana ufahamu kuwa watu wa Mungu wanalindwa na Majeshi ya malaika tunasahau kuwa Hata malaika wapo! Ndio Malaika wapo

Biblia inasema Hawa malaika ni roho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu Waebrania 1: 13-14; “Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”
Unaona Biblia inasema kuwa malaika ni viumbe wa kiroho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu, Malaika wapo, wakati unalia na kushangaa wana wanakushangaa kwanini unalia, kwanini huwatumii je unajua waoa hutuhudumia je unajua wao hututazama kwa macho mengine  wao hututia moyo pale tunapojihisi kuwa sisi ni Duni wao hutuona kuwa sisi mashujaa, Ndugu wewe ni zaidi ya Rais unalindwa na malaika pande zote usimtie Mungu aibu, wala usimfanye Mungu kuwa Bodigadi wako, How comes ulindwe na Mfalme wa wafalme ili hali majeshi yake yapo. Wapo wapo kukupa msaada unaoutaka kumbuka wanakuita wewe shujaa ona Waamuzi 6:12 “Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa.Hakukuwa na mtu muoga duniani kama Gideon Lakini malaika alimuita Ee Shujaa, Ndio ni shujaa kwa sababu haendi peke yake Malaika kibao wapo wanaenda pamoja naye iweje asiwe shujaa, angalia mtu anayelindwa na mabaunsa pande zote anawezaje kutembea kama mtu mnyonge? Ni Shujaa ndio ni shujaa kwa nini kwa sababu anazungukwa na ulinzi wa kutosha na kupewa msaada wa kila ainna autakao.

Malaika hawana Nguvu zote kama Mungu, lakini wana nguvu kuliko binadamu, katika rekodi za juu za kibiblia, Maandiko yanasema Malaika mmoja anauwezo wa kupiga watu 185,000, ndio nasema ndio malaika mmoja tu anauwezo huo soma Isaya 37:36Basi malaika wa Bwana alitoka, akaua watu mia na themanini na tano elfu katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.         

Sasa wewe unaogopa nini? Unaogopa wachawi? Unaogopa changamoto gani Biblia inasema malaika wa Bwana hufanya kituo (Hufanya Patrol) akiwalinda wale wanaomcha Mungu, na hawa unaona mmoja tu anauwezo wa kupiga watu 185,000, Ndio maana Daudi aliimba Bwana ni ngome yangu, Jeshi lijapojipanga kupigana nani moyo wangu hautaogopa!, Malaika wapo dada, malaika wapo, kaka, malaika wapo baba, malaika wapo ndugu yangu, waache wao watumie Majini, waache watumie uchawi waache watumie kila silaha wanayoweza sisi, tunatumia Malaika tunawaamuru Malaika waingilie kati katika kila hali inayotuzunguka na watatupigania

Malaika wanauwezo wa kukutoa katika kifungo cha aina yoyote, Matendo 12:5-11Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.  

  
Petro alipokuwa Gerezani katikati  ya ulinzi mkali, kila mtu akitarajia kuwa atauawa Malaika alikuja na kumtoa gerezani, jamani malaika wapo, wakristo mailka wapo Hakuna sababu ya kuogopa chochote ni lazima na muhimu kumuamini Mungu, kuamini uweza wake kujua uuumbaji wake aliumba viumbe vinavyoonekana na visivyoonekana, Malaika hawaonekani lakini maandiko yanasema wapo, Mimi naamini wapo najua wanawajibika katika kile alichowaagiza Mungu najua wanafanya kituo, sihitaji ulinzi wa mabausa, wala Bodigadi wao wapo kwaajili yangu, wapo pia kwaajili yako huna sababu ya kuogopa mchana wala usiku kwa sababu wao wapo! Mungu amenituma nikujulishe tu kuwa viumbe hawa wapo, wapo wametumwa na Mungu kwa Makusudi ya kutuhudumia kwanini uteseke watumie usiogope hatuko peke yetu Malaika nao wapo
Hata malaika wapo!

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!
Rev. Innocent Kamote
0718990796.