Jumapili, 14 Januari 2024

Tazama mwana kondoo wa Mungu!


Yohana 1:26-30 “Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi. Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake. Hayo yalifanyika huko Bethania ng'ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza. Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, MWANA-KONDOO WA MUNGU, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.”




 

Utangulizi:

Nyakati za agano la kale, Watu walipotaka kumuabudu Mungu, na aidha kurejesha au kuendeleza uhusiano na Mungu, kwa vile Mungu ni Mtakatifu, uovu na dhambi ulikuwa umemtenga mwanadamu mbali na uwepo wa Mungu, hivyo njia ya kumfikia Mungu ilikuwa ni lazima imwagike damu, na ndipo Mungu aweze kuridhia uhusiano unaotafutwa na mwanadamu, kupitia damu ya Mwanakondoo, ambaye alikuwa anakufa kwa niaba ya Mwanadamu au wanadamu ili aweze kuwakubali, kwa msingi huo utaweza kuona kuwa utamaduni wa kuchinja kama njia ya kuwasiliana na Mungu unazingatiwa sana pia katika makafara ya dini za kienyeji ambazo ziko maelefu kwa maelfu katika jamii ya aina binadamu. Hii ndio ilikuwa njia ya kwanza kabisa ya mwanadamu kuridhiwa na Mungu unaona?

Mwanzo 4:2-5 “Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi. Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA. Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.”

Kwa hiyo utoaji wa sadaka/kafara za wanyama na kuteketeza ndio ilikuwa njia ya zamani zaidi ya mwanadamu kuuakaribia uwepo wa Mungu na kuridhiwa, wanyama wote yaani wanyama safi wasio najisi wangeweza kutumika kwa jambo hili lakini Kondoo ndiye aliyekuwa mnyama bora zaidi aliyenona na ambaye angeweza kufaa kwa sadaka au kafara za wanadamu kwa Mungu.  Je mwana kondoo alikuwa akimaanisha nini katika lugha ya kinabii? Hilo linatupa nafasi ya kuchukua muda leo, kutafakari kwa kina na mapana na marefu, kuhusu somo hili Tazama mwana kondoo wa Mungu kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo!

·         Mwanakondoo katika unabii

·         Nguvu ya Damu ya mwanakondoo

·         Tazama mwanakondoo wa Mungu


Mwanakondoo katika unabii

Ni muhimu kufahamu kuwa katika lugha ya kinabii, kondoo alikuwa akimwakilisha Mwanadamu, yaani kimsingi, mwanadamu ndiye aliyetakiwa kufa, lakini kwa rehema za Mungu alikuwa anaridhika kwa muda pale inapopatikana damu mbadala, lakini kwa uwazi kabisa kondoo alikuwa akimaanisha mwanadamu au kusimama kwa niaba ya mwanadamu katika lugha ya kinabii unaweza kuona kwa mfano katika kifungu cha maandiko kifuatacho:-

2Samuel 12:1-6 “Ndipo Bwana akamtuma Nathani aende kwa Daudi. Naye akamwendea, akamwambia, Palikuwa na watu wawili katika mji mmoja; mmoja wao alikuwa tajiri, wa pili maskini. Yule tajiri alikuwa na kondoo na ng'ombe wengi sana; bali yule maskini hakuwa na kitu, ila mwana kondoo mmoja, mdogo, ambaye amemnunua na kumlea; naye akakua pamoja naye, na pamoja na wanawe; hula sehemu ya posho lake, na kukinywea kikombe chake, na kulala kifuani mwake, akawa kwake kama binti. Hata msafiri mmoja akamfikilia yule tajiri, naye akaacha kutwaa mmoja wa kondoo zake mwenyewe au mmoja wa ng'ombe zake mwenyewe, ili kumwandalia yule msafiri aliyemfikilia, bali alimnyang'anya yule maskini mwana-kondoo wake, akamwandalia yule mtu aliyemfikilia. Ndipo hasira ya Daudi ikawaka sana juu ya mtu yule; akamwambia Nathani, Aishivyo Bwana, mtu huyo aliyetenda jambo hili, hakika yake astahili kufa; naye atamrudishia yule mwana-kondoo mara nne, kwa sababu ametenda neno hili, na kwa sababu hakuwa na huruma.”

Unapoangalia kifungu hiki cha maandiko, utaweza kuona Lugha ya kinabii inayotumiwa na nabii Nathani katika kuikabili dhambi ya Mfalme Daudi, Daudi alikuwa amefanya dhambi ya zinaa na dhambi hii iliambatana na ujauzito, na ili kuuficha ule ujauzito wa mke wa mtu, alitumia hila mbalimbali ambazo zilishindikana kumlaghai mume wa Bathsheba yaani Uria ili akalale kwa mkewe kwa kusudi la kumchomekea lakini alikataa, na hivyo kwa hila aliwekwa mstari wa mbele katika vita ili afe, na kisha yeye akamuoa mwanamke yule akiwa na mimba yake, kitendo cha kumuua Uria ni kitendo cha kuchinja Kondoo wa mtu masikini na katika habari hii Daudi alihukumu kuwa mtu huyo anastahili kufa yaani yeye, lakini pia anapaswa kulipa yule mwana kondoo mara nne! Hii ilikuwa ina maana Daudi alitakiwa afe, lakini vilevile walitakiwa wafe watu wanne katika familia yake, sasa ingawa Daudi alisamehewa baada ya toba na kifo kiliondolewa kwake hata hivyo watoto wake wanne Walikufa sawasawa na lugha ile ya kinabii:-

1.       Mtoto wa Daudi aliyezaliwa na Bathsheba – 2Samuel 12:15-23 “Naye Nathani akaondoka kwenda nyumbani kwake. Basi Bwana akampiga yule mtoto ambaye mkewe Uria alimzalia Daudi naye akawa hawezi sana. Basi Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya mtoto; Daudi akafunga, akaingia, akalala usiku kucha chini.Nao wazee wa nyumba yake wakaondoka, wakasimama karibu naye, ili wamwinue katika nchi; lakini hakukubali, wala hakula chakula pamoja nao. Ikawa siku ya saba, yule mtoto akafa. Nao watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia ya kuwa mtoto amekufa, maana, walisema, Angalieni, yule mtoto alipokuwa angali hai, tulisema naye, asitusikilize sauti zetu; basi hatazidi kujisumbua, tukimwambia ya kuwa mtoto amekufa? Lakini alipoona ya kuwa watumishi wake wananong'onezana, Daudi alitambua ya kuwa mtoto amekufa; basi Daudi akawauliza watumishi wake, Je! Mtoto amekufa? Nao wakasema, Amekufa. Ndipo Daudi akainuka pale chini akaoga, akajipaka mafuta, akabadili mavazi yake; akaingia nyumbani mwa Bwana, akasali; kisha akaenda nyumbani kwake, na alipotaka wakamwandalia chakula, naye akala. Watumishi wake wakamwambia, Ni neno gani hili ulilolitenda? Ulifunga na kulia kwa ajili ya mtoto, alipokuwa hai; lakini mtoto alipokuwa amekufa, uliinuka ukala chakula. Akasema, Mtoto alipokuwa hai, nalifunga, nikalia; kwa maana nalisema, Ni nani ajuaye kwamba Bwana atanihurumia, mtoto apate kuishi? Lakini sasa amekufa nifungie nini? Je! Naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake lakini yeye hatanirudia mimi.”        


2.       Mtoto wa Daudi aitwaye Amnoni - 2Samuel 13:28-33 “Kisha Absalomu akawaamuru watumishi wake, akasema, Angalieni basi, moyo wake Amnoni utakapofurahiwa kwa mvinyo; nami nitakapowaambia, Mpigeni Amnoni, ndipo mwueni, msiogope; si mimi niliyewaamuru? Iweni hodari, iweni na ujasiri. Basi watumishi wa Absalomu wakamfanyia Amnoni kama alivyoamuru Absalomu. Ndipo wakaondoka wana wote wa mfalme, wakapanda kila mtu nyumbu wake, wakakimbia. Ikawa, walipokuwa njiani, habari zikamwasilia Daudi, kusema, Absalomu amewaua wana wote wa mfalme, wala hata mmoja wao hakusalia. Ndipo mfalme akainuka, akararua nguo zake, akalala chini; nao watumishi wake wote wakasimama karibu naye, wenye nguo zao zimeraruliwa. Akajibu Yonadabu, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akasema, Asidhani bwana wangu ya kwamba wamewaua vijana wote, wana wa mfalme; maana ndiye Amnoni peke yake aliyekufa; yakini haya yamekusudiwa kwa kinywa chake Absalomu tangu siku ile alipotenzwa nguvu umbu lake, Tamari.Basi sasa bwana wangu mfalme asilitie neno hili moyoni, kudhani ya kwamba wana wote wa mfalme wamekufa maana ni Amnoni peke yake aliyekufa.”

               

3.       Mtoto wa Daudi aitwaye Absalom – 2 Samuel 18:9-15 “Na kwa bahati Absalomu akakutana na watumishi wa Daudi. Naye Absalomu alikuwa amepanda nyumbu wake, na yule nyumbu akapita chini ya matawi manene ya mwaloni mkubwa, hata kichwa chake kikakwama katika mwaloni huo, akanyakuliwa juu kati ya mbingu na nchi; na yule nyumbu aliyekuwa chini yake akaenda mbele. Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, Tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni. Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi. Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu. Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga. Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni. Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.”

 

4.       Mtoto wa Daudi aitwaye Adonai – 1Wafalme 2:22-25 “Akajibu mfalme Sulemani akamwambia mamaye, Na mbona wamtakia Adonia Abishagi, Mshunami? Umtakie na ufalme pia; kwa kuwa yeye ni ndugu yangu mkubwa; naam, umtakie yeye, na Abiathari kuhani, na Yoabu mwana wa Seruya. Ndipo mfalme Sulemani akaapa kwa Bwana, akasema, Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, isipokuwa Adonia amenena neno hili juu ya uhai wake mwenyewe. Basi kwa hiyo, Bwana aishivyo, aliyenithibitisha na kunikalisha katika kiti cha enzi cha Daudi baba yangu, akanifanyia nyumba, kama alivyoahidi, hakika atauawa leo hivi Adonia. Mfalme Sulemani akatuma kwa mkono wa Benaya mwana wa Yehoyada: naye akampiga, hata akafa.”

 

Unaweza kuona ni kwanini tumechukua muda kufuatilia vifo vinne vya wana wa mfalme Daudi, ni ili kuthibitisha neno la Nabii Nathani kuwa Daudi kwa dhambi yake ya kuua mwana kondoo mmoja (URIA) alipaswa kulipa kondoo wanne, (WATOTO WAKE). Kwanini kwa sababu kulipa mara nne ilikuwa ni sehemu ya fidia ya agizo la kitorati kuwa kama umedhulumu kitu unapaswa kulipa mara nne kama malipizi 

 Kutoka 22:1 “Mtu akiiba ng'ombe au kondoo, na kumchinja, au kumwuza; atalipa ng'ombe watano badala ya ng'ombe mmoja, na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.”

Luka 19:8-10 “Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne. Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”               

Kwanini nimechukua muda kuchambua kwa undani swala la Daudi na kulipa mara nne na vifo vya watoto wake kusudi langu kubwa ni kuonyesha tu picha ya kibiblia kuhusu kondoo, Kwamba kondoo husimama badala ya mtu na mtu husimama badala ya kondoo katika lugha ya kinabii, na ni katika picha hii ya kinabii tunapata wazi picha ya Mwana kondoo aliyetolewa kwa niaba ya Isaka wakati agizo la msingi la Mungu kwa Abraham lilikuwa ni kumtoa Isaka  mwanaye wa Pekee (AHADI) kama sadaka ya kuteteketezwa kwa Bwana:-

Mwanzo 22:1-14 “Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia. Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu. Siku ya tatu Ibrahimu akainua macho yake, akapaona mahali pakali mbali. Ibrahimu akawaambia vijana wake, Kaeni ninyi hapa pamoja na punda, na mimi na kijana tutakwenda kule, tukaabudu, na kuwarudia tena. Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja. Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa? Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja. Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni. Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe. Ndipo malaika wa BWANA akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee. Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.”

Unaweza kuona tukio hili ni tukio la kinabii, Ibrahimu na Mwanae Isaka ni manabii, Mungu anaposema na Ibrahimu kwenda kumtoa mwanae wa Pekee Isaka ni swala la kinabii, mwendo wao wa siku tatu, Isaka kubeba kuni mabegani mwake, kondoo mume amenaswa pembe zake katika kichaka zote hizi ni lugha za kinabii, ni picha ya kitu halisi ambacho Mungu alikuwa amekikusudia kwa ulimwengu, Ibrahim anamwakilisha Mungu,Isaka anamwakilisha Mwana wa pekee wa Mungu, kubeba kuni kunawakilisha Kubeba Msalaba, na mwendo wa siku tatu unamaanisha siku za mateso ya Yesu kufa na kufufuliwa kwake, Kondoo yule aliyenasa pembe zake ndiye aliyetolewa kwa niaba ya Isaka kondoo huyo pembe zake zilikuwa zimenasa katika kichaka ni picha inayomwakilisha Yesu Kristo aliyekufa msalabani huku akiwa amevikwa taji ya miiba kichwani mwake, kwa msingi huo tunaona wazi kuwa lugha ya kinabii hapa inaelezea, namna kondoo huyo alivyosimama kwa niaba ya Isaka, ni ni Picha ya kinabii kuhusu Mwanadamu mkamilifu atakayekufa kwa niaba ya wanadamu kama watamuamini Mungu na kuhesabiwa haki.

Lugha nyingine ya kinabii inaonekana katika torati ya Musa Kitabu cha Kutoka 12:3-7 “Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja; na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo. Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi. Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni. Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla.”

Hili ni tukio lingine ambalo linakolezea unabii wa Ibrahimu katika kitabu cha Mwanzo, Kwa maelekezo ya Mungu kwa Musa na Haruni, kwa wana wa Israel ili kwamba waweze kuokolewa na mauti ya kuuawa kwa kila mzaliwa wa Kwanza katika nchi ya Misri, Maelekezo ya Mungu ni kuwa lazima imwagike Damu, damu ya mwana kondoo asiye na hila yaani lazima awe mkamilifu, asiwe na marakaraka, na damu yale ikawekwa juu ya miimo ya milango, hii pia ilikuwa ni picha ya kinabii ya ukombozi wa Mwanadamu kupitia mtu ambaye hana dhambi ambaye ni Yesu Kristo, swala la unabii sio khadithi tu ni picha halisi ambazo Mungu alikuja kuzitimiza baadaye kupitia Masihi Mwana wake

Nabii Isaya naye katika namna ya kushangaza sana anamuona Masihi kama kondoo akipelekwa Msalabani, machinjoni kwa unyenyekevu mkubwa kwaajili ya ukombozi wa mwanadamu, ili wanadamu wasamehewe dhambi zao

Isaya 53:2-9 “Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote. Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu. Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.”

Kwa msingi huo tunaweza kuona wazi kuwa lugha zote za kinabii zinamzungumzia kondoo huyu, na kwa ujumla sikukuu zote za kuchinja na makafara yote zilikuwa ni picha za kinabii zinazomzungumzia Yesu kristo, Yeye ndiye mwana kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu kama ilivyotabiriwa katika maandiko. Damu yake ina nguvu ya kuondoa na kufunika kabisa makosa yetu, Mungu anapoiangalia  au kuikumbuka Damu ya mwanae anaacha kutughathibikia na damu yake inatangaza rehema kwa niaba yetu na kutununua na kutulipia deni ili sisi nasi tuweze kuwa mali ya Mungu na kuufikia uwepo wa Mungu katika njia iliyo rahisi zaidi bila kuhitaji tena damu ya wanyama. Hilo linatuleta katika kutafakari kwa kina sasa kuhusu nguvu ya Damu ya Mwana kondoo.

Nguvu ya Damu ya mwanakondoo

Tunaweza kujiuliza ni kwanini Damu? Ya mwana kondoo? Wote tunakumbuka namna na jinsi Mwanadamu alivyopoteza nafasi ya kuwa na ushirika na Mungu, baada ya dhambi, Mungu alimueleza wazi mwanadamu kuwa siku atakapoivunja sharia yake yaani kula tunda alilokuwa amekatazwa kwa hakika atakufa!

Mwanzo 2:16-17 “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”               

Kwa hiyo kwa maana nyingine kila mwanadamu akiivunja sheria ya Mungu kwa kujua au kwa kutokujua anajingiza katika dhambi na anaileta mauti katika maisha yake, dhambi kwa kawaida malipo yake ni kifo tu na sio vinginevyo

Warumi 6:23a “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti;…………….Unaona kwa msingi huo ili Mungu asiweze kuiona dhambi, ilikuwa ni lazima uhai mwingine utolewe kwa niaba ya muhisika ili Mungu asiikumbuke dhambi yake unaweza kuona na uhai huo unakaa katika Damu, Damu ndio kiwakilishi kiuu cha uhai wa Mwanadamu na wanyama,

 Waebrania 9:22 “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo.”

Kwa hiyo Dhambi zinapofanyika zinadai kifo, zinadai mauti, zinadau uhai, kwa hiyo adhabu ya uhai wa kitu kingine kinapouawa kwa niaba yako Mungu huiona damu na kwa muda huo anaacha kughadibika kwa hiyo kwa rehema za Mungu na kwa upendo wake wanyama walikuwa wanakufa kwa niaba ya Mwanadamu, kwa hiyo unapofanya dhambi Mungu hukasirishwa na kwa kuwa Mungu ni mwenye wiu kwaajili yetu tamshi lake ni sheria siku utakapokula matunda ya mti huu hakika utakufa! Sasa kwa kuwa Mungu ni Mtakatifu hatuwezi kumkaribia hivihivi Mungu akaweka njia mbadala ambayo ni dhabihu ya damu ili hasira zake zisiwake kwetu na badala yake Damu ya mwanakondoo aliyeuawa kwa niaba yetu inamfanya Mungu aturehemu hivi ndio ulimwengu wa roho ulivyo na kanuni zake  Damu husimama kwa niaba ya uhai wetu na adhabu zetu Damu ni uhai  na damu ina uhai

Walawi 17:10-12 “Kisha mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli, au miongoni mwa hao wageni wakaao kati yao, atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi. Kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Hapana mtu miongoni mwenu aliye na ruhusa kula damu, wala mgeni aketiye kati yenu asile damu.”               

-          Kumwagika kwa damu ni ufuno halisi kuwa dhambi ni swala nyeti na linagharimu sana mfumo wa maisha yetu.

-          Kumwagika kwa damu ni ufunuo wa Moyo wa Mungu kwetu kuwa Mungu anahitaji kurejesha uhusiano wake na mwanadamu na hataki watu wafie dhambini.

-          Kumwagika kwa damu ulikuwa ni ufunuo unaoonyesha ya kuwa tunahitaji mbadala wa kitu kingine kuchukua mizigo kwa niaba yetu.

-          Kumwagika kwa damu ni alama ya kitu kinachoweza kufanya upatanisho kati yetu na Mungu

-          Kumwagika kwa damu ni ufunuo wa uzito wa haki ya Mungu kupatikana kwa neema

-          Kumwagka kwa Damu ni ufunuo wa namna mwanadamu anavyoweza kurejesha uhusiano wake na Mungu

Kwa njia hii Mungu alikuwa akijifunua kwa wana wa Israel namna anavyoweza kuwa na ushirika nao, lakini Mungu sio wa Israel pekee ni Mungu wa Ulimwengu mzima na mataifa yote Je sadaka hizi za mafahari ya kondoo na mbuzi zingeendelea hata lini? hizi zote zingegharimu mamilioni ya wanyama duniani leo, hizi zilikuwa ni picha ni alama ya kinabii kuonyesha nguvu ya Damu, inavyoweza kurudisha uhusiano wetu na Mungu, inavyoweza kupatanisha inavyoweza kurudisha ushirika na Mungu, inavyoweza kusababaisha kutangaziwa rehema na kusamehewa dhambi, damu za mafahari zilifanya kwa muda tu Lakini Damu ya Yesu ingetolewa mara moja kwa kazi za milele.

Tazama mwanakondoo wa Mungu

Yohana 1:26-30 “Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi. Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake. Hayo yalifanyika huko Bethania ng'ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza. Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, MWANA-KONDOO WA MUNGU, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.”

Kimsingi manabii walikuwa wakitabiri kuja kwa Mwana kondoo halisi wa Mungu, Lakini nabii Yohana Mbatizaji yeye alikuwa akiwaonyesha wazi jamii ya watu kwamba yule aliyekuwa akitazamiwa, kusubiriwa na kuhubiriwa na manabii ndiye huyu, na sasa watu wote wanapaswa kumwamini, kuamini kazi yake atakayoifanya pale msalabani kwamba, itafanya kazi zaidi ya zile zilikuwa zikifanywa na wanyama jana leo na hata milele, mwana kondoo huyo ni Yesu Kristo ambaye kama alivyotabiriwa ndivyo ilivyokuwa

Isaya 53:7-10 “Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu. Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake. Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;”

Hakuna kiongozi mwingine yeyote wala muazilishi wa dini nyingine yeyote aliyeweza kuhitimisha unabii wake katika hali kama hii, Isipokuwa Yesu Kristo, dini na taratibu nyingine zozote duniani ambazo hazina kiongozi aliyetimiza unabii hivi ni dini za uongo, kama unaweka Imani yako kwa nabii marehemu ambaye hajawahi kumwaga damu yake wala kutoa uhai wake kwaajili ya wanadamu basi fahamu kuwa huyo siye aliyetabiriwa katika maandiko, Na deni lako la dhambi linabakia vile vile, Ni Yesu pake yake anayeruhusiwa kuwa na mamlaka na kupokea Enzi na utukufu kutokana na kazi hii ya ukombozi aliyoifanya na upendo mkuu wa Mungu alioufunua kwetu

Ufunuo 5: 11-12 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu, wakisema kwa sauti kuu, ASTAHILI MWANA-KONDOO ALIYECHINJWA, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”                

1Yohana 4:9-10 “Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. .”

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”

1Petro 1:18-21 “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; BALI KWA DAMU YA THAMANI, KAMA YA MWANA-KONDOO ASIYE NA ILA, ASIYE NA WAA, YAANI, YA KRISTO.NAYE amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.”

Mungu aliona aikamilishe kazi ile ya kinabii kupitia Mwanaye, yaani kama Ibrahimu alithubutu Kumuachia mwanaye Isaka kwaajili ya Mungu, Mungu sasa katika hali halisi hakumzuia mwanaye Yesu Kristo kwaajili yetu, upendo huu ni mkubwa sana kwani unahuisha ushirika wetu na Mungu, unatupa kibali cha kuwa na ushirika na Mungu na hivyo inafungua njia ya ajabu kwetu ya kuwa hakuna lolote ambalo Mungu anaweza kutunyima 

Warumi 8: 32 “Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?              

Maana yake ni nini? Kila changamoto tunayoweza kukutana nayo duniani iwe ndogo au kubwa, iwe dhambi au mauti, iwe hatari, iwe ya kimwili, au ya kiroho, iwe ya kiuchumia au ya kisaikolojia kamwe haitaweza kuushinda upendo wake yeye kwani anasamehe dhambi kisha anashughulika na magonjwa yetu na mateso yetu na fadhaa zetu yeye amemleta Mungu karibu na sisi, amerejesha uhusiano wetu na baba hivyo ili tuwe na uhai ili tuwe na uzima ili tufanikiwe hatuna budi kuhakikisha kuwa tunamtazama yeye katika maisha yetu yote na ndio maana Yohana mbatizaji aliwanyooshea kidole kwamba yeye hana majibu ya kutosha amekuja anayestahili na hakuna njia nyingine akawaambia watu TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU, Leo nakutangazia ya kuwa chanzo cha mafanikio yako, sio sabuni, sio chumvi, sio maji ya Baraka wala mafuta ya upako, wala udongo, wala nyayo zako, wala kula keki mimi wala kukombolewa kwa adhri yako, wala kupeleka kucha zako, wala nyele zako, Leo Roho Mtakatifu amenituma kwako nikiwa na ujumbe kama wa Yohana Mbatizaji TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU, Nasema hivi kwa changamoto zozote, kwa vita ya aina yoyote, kwa majungu ya aina yoyote, kwa  fuitina za aina yoyote, kwa dhuluma ya aina yoyote, kwa mapito ya aina yoyote, kwa njaa, kwa aibu, kwa kupungukiwa kwa lolote lile leo nakuelekeza neno moja nimepewa kwaajili yako TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU, kwa changamoto zozote zile, kwa laana zozote zile, kwa usumbufu wa mizimu, kwa usumbufu wa wachawi, kwa matatizo ya nuksi laana mikosi na balaa, kwa changamoto za kurogwa, damu ya Yesu ni zaidi ya ndele, ni zaidi ya zindiko lolote lile liwe kwamsisi, au kwasemangube au milima ya rwengera au Nchedebwa, au Liwale, na kadhalika Damu yake inamaliza yote, yeye ndio suluhisho la changamoto zetu zote na jina lake linatosha sana ni jina kuu kuliko yote, lina nguvu na mamlaka yote hivyo kwa suluhu zozote za changamoto zako nasema TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU basiiii.  Rbashakarabasiote rikabashakarabasabo, yekerekishitaraka sata Yete tara sata! TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU. Naema TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU nasema TAZAMA MWANA KONDOO WA MUNGU Haleluyaaaaa Ukimtazama yeye unapomtazama yeye hakuna kuchoka wala kukata tamaa wala kuzimia moyo


Waebrania 12:2-3 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.”


Rev. Innocent Samuel Jumaa Kamote


Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

Jumatatu, 8 Januari 2024

Kwanini Yesu alijiita Mwana wa Adamu?


Mathayo 16:13-17 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.”

 

 



Utangulizi:

 

Moja ya njia pekee ya kutambua mtu au kitu kwa kina na mapana na marefu ni pamoja na kuangalia majina ambayo mtu huyo anaitwa au anajiita, katika somo la uungu, unapomzungumzia Mungu baba na mwana na Roho Mtakatifu, moja ya nafsi ambayo inasumbua sana wanazuoni wengi wa Kikristo na zaidi wasio wakristo ni kujua asili ya Kristo, na ni kutokana na kuwepo kwa utata mwingi sana kuhusu asili ya Yesu, kumekuwepo na somo katika vyuo vya Biblia linalojaribu kuchambua kwa undani ili kumjua Yesu ni nani, somo hilo kitaalamu huitwa CHRISTOLOGY  ambalo ni muunganiko wa misamiati miwili ya kiyunani CHRIST na LOGOS ikiwa na maana ya MAARIFA KUHUSU KRISTO – Knowledge about Christ, Somo hilo kimsingi linahusika na kuchambua kwa undani sana kuhusu Yesu Kristo na asili yake, kumjua Yesu na Mungu baba yetu wa Mbinguni yalikuwa ni moja ya sehemu ya muhimu ya maombi ya Yesu Kristo kwetu!.

 

Yohana 17:1-3 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;             kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”

 

Kumjua Yesu Kristo kwa kawaida sio swala Jepesi kama tunavyofikiri, huwezi kumjua Yesu bila msaada wa Mungu, maandiko au Yesu Mwenyewe na katika maandiko pia wakati mwingine ni mpaka yeye mwenyewe ahusike kukufunulia andiko husika kwa neema yake. Leo tutachukua muda kujifunza somo hili muhimu KWANINI YESU ALIJIITA MWANA WA ADAMU tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

 

·         Jinsi kuijua asili ya Yesu Kristo kulivyowasumbua wasomi

·         Jinsi ya kumjua Yesu Kristo

·         Kwanini Yesu alijiita mwana wa Adamu

 

Jinsi kuijua asili ya Yesu kulivyowasumbua wasomi

 

Moja ya swala ambalo lilisumbua sana mnamo karne ya kwanza mpaka karne ya tatu kwa wanazuoni wakubwa sana katika kanisa la Mungu, ilikuwa ni pamoja na kuijua nafsi ya Mungu mwana, utata kuhusu Yesu ni nani sio tu ulisumbua vichwa vya wasomi, lakini hata wakati wa Yesu mwenyewe kila mmoja alikuwa akisema lake kuhusu Yesu ni nani ona :-

 

Mathayo 16:13-17 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.”

 

Katika karne ya tatu swali kuhusu Masihi ni nani bado liliendelea kuwasumbua wasomi na kila mtu alikuwa na maoni yeke kuhusu asili ya Yesu kuwa ikoje na ni nani? Kama tunavyoweza kujionea maoni mbalimbali ya wanazuoni wakiumiza kichwa kumjua Yesu.

 

1.      Waebionite – (Ebionites) – Hili ni kundi la wakristo wa kiyahudi ambao walikuweko karne za mwanzoni wakiishi maisha ya kimasikini wakiwa na Imani kuwa umasikini una uhusiano na maisha matakatifu, waoa walikuwa wakiamini kuwa YESU NI MASIHI LAKINI SIO MUNGU na kuwa kuzaliwa kwake na Mariamu kunasisitiza umuhimu wa kuishika na kuitii Torati ya Musa, Hivyo Yesu ni Mwanadamu aliyetii torati yote ya Musa na kutunukiwa kuwa masihi.

 

2.      Waanostisizim – (Gnosticism) – Hili ni kundi la watu walioamini kuwa Maarifa yanaleta wokovu na dhambi ni ujinga, kundi hili liliamini kuwa YESU ALIKUWA NI ROHO NA HAJAWAHI KUUTWAA MWILI Fundisho la aina hii lilipingwa vikali na Mtume Yohana na alilionya kanisa kuwa makini na aina ya fundisho kama hilo ona

 

 1Yohana 4:1-3 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.”            

3.      Waariyan – (Arianism) – Ni kundi la Wakristo waliofuata fundisho la Mwanatheolojia aliyeitwa Arius ambaye alikuwa mwangalizi na msomi wa chuo kikuu cha Kikristo huko Alexandria nchini Misri kati ya mwaka 256-336 Baada ya Kristo, wao waliamini kuwa Yesu sio Mungu ni kiumbe cha kwanza kuumbwa na Mungu na hivyo hayuko sawa na Mungu lakini yuko chini kidogo ya Mungu na juu ya malaika, walimuita Yesu Mwanzo wa kuumba kwa Mungu sawa na

 

Ufunuo 3:14c “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, MWANZO WA KUUMBA KWA MUNGU.”

 

Pia wanatumia andiko hili kutoka injili ya Yohana Yesu akisema baba ni Mkubwa kuliko Yeye

 

Yohana 14:28 “Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, KWA MAANA BABA NI MKUU KULIKO MIMI.”

 

4.      Wanestorian – (Nestorianism) – Hili ni kundi lingine la wasomi wa Kikristo, waliokuwa na mtazamo tofauti kuhusu asili ya Yesu, wao waliona kuwa uungu na ubinadamu hauwezi kuwa na muunganiko kwa hiyo Yesu hawezi kuwa Mungu mwanadamu, au kuwa Mungu wakati huo huo na wakati huo huo mwanadamu.

 

5.      Waapolonari – (Apollinarian) – Aplonari alikuwa ni askofu kijana wa kanisa la Laodekia lililokuwako huko Syria mwaka wa 361 baada ya Kristo, yeye aliamini pamoja na watu wake kuwa Yesu alikuwa mwanadamu lakini akili yake ilikuwa akili ya kiungu, kwa hiyo asili hizi mbili hazikuweza kujitokeza kwa pamoja ni kama anataka kusema kuwa kuna wakati Yesu alikuwa mwanadamu na alisema na kundenda kibinadamu na kuna wakati alikuwa Mungu na alitenda na kusema kama Mungu.

 

6.      Waeutiko – ( Eutychians)  - Hili ni kundi la Wakristo waliofuata mafundisho ya Eutychus ambaye aliishi huko Constantinople, kati ya mwaka  380 - 456      baada ya Kristo, wao walikuwa na fundisho kuwa Yesu alikuwa na asili mpya yaani Mungu + Mwanadamu = Asili mpya, kwa hiyo Yesu sio Mungu wala sio Mwanadamu

 

7.      Waorthodox – (Orthodox) – Hili ni Kundi la wakristo wanaoamini kuwa wanafundisho sahihi neno Orthodox maana yake ni Right opinion  wao waliamini kuwa Yesu ni Mungu mwanadamu na kwa sababu hiyo Yeye ni Mwanadamu kwa asilimia 100% na ni Mungu kwa asilimia 100% fundisho hili ndilo lililosalia kuwa fundisho sahihi mpaka sasa kwa mujibu wa kanisa la Mungu  wao wanasimamia andiko la Yohana 1:1-3, 13-14

 

Yohana 1:1-3 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.”

 

Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

 

Unaweza kuona makundi hayo yalikuwa na mijadala mikali sana kuhusu Asili ya Kristo, na hii inatufundisha wazi kuwa kumjua Yesu Kristo sio kazi nyepesi kama watu wengi wanavyodhani inahitajika neema maalumu ya kiungu kuweza kumjua Yesu, na ndio maana watu wengi sana huwa wanachanganyikiwa kuhusu, nafsi na asili ya Yesu mpaka leo, Ni muhimu sana tunapoendelea kujifunza somo hili kuwa na maombi ya kutaka kumjua Yesu zaidi, kama mwandishi wa Tenzi za injili namba 92 alivyoimba kuwa anataka kumjua Yesu na azidu kumfahamu, tunahitaji neema ya Mungu kumjua bwana wetu Yesu.

 

Jinsi ya kumjua Yesu Kristo

           

Kumjua Yesu Kristo kamwe hakuwezi kuja kwa akili za kawaida za kibinadamu, wala kwa kujenga hoja za kisomi, maandiko na Yesu Kristo Mwenyewe anaonyesha wazi kuwa kumjua Yesu Kristo kunaweza kuletwa kwetu kwa msaada wa Mungu na ufunuo wa Mungu Baba mwenyewe kwetu kupitia Roho wake Mtakatifu, maandiko au Yesu Kristo mwenyewe moja kwa moja tunaweza kupata ushahidi wa jambo hili kwa kuangalia tena andiko letu la Msingi

 

Mathayo 16:16-17 “Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.”

 

Unaona? Yesu alipouliza swali watu wanasema kuwa mwana wa Adamu ni nani, kulikuwa na majibu mbali mbali kuhusu Masihi, lakini hatimaye Simioni Petro akajibu, wewe ndiwe Kristo Mwana wa Mungu aliye hai, na mara baada ya jibu hili ambalo lilikukuwa jibu sahihi Yesu alijibu kwa kumwambia HERI WEWE SIMONI BAR-YONA; KWA KUWA MWILI NA DAMU HAVIKUKUFUNULIA HILI, BALI BABA YANGU ALIYE MBINGUNI Maneno haya yana maana gani? Rahisi tu huwezi kumjua Yesu bila kufunuliwa na Mungu mwenyewe, na kule kusema mwili na damu havikukufunulia hili, Yesu alikuwa akimaanisha Akili ya kawaida ya kibinadamu na uweza katika uhai wa mwanadamu hauwezi kutambua siri hii ya kuwa Yesu Kristo ni nani, na ndio maana umeweza kuona wasomi wengi walisumbuka kutambua asili ya Kristo na hata leo, watu wa dini nyingine hususani wakiwemo waislamu wanahangaika sana na kutatizwa mno na ukweli kuhusu asili ya Yesu Kristo,  na huwa wanadhani tuna haja ya kumkuza sana au kukufuru kwa kumpa Heshima ambayo wanadhani haistahili, jambo kubwa la Msingi ni kuwa tunamjua Mungu kupitia ufunuo kutoka kwa Mungu mwenyewe! Na neema yake wakati tunapotafakari na kumruhusu yeye atufunulie maandiko!

 

Au wakati mwingine Yesu mwenyewe huwa anahusika kutufunulia yeye mwenyewe ili tuweze kumjua au kutufunulia maandiko ili tuweze kuelewa, jambo hili linadhihirika wazi kuwa hata wanafunzi wa Yesu, waliomuona mubashara alipokuwa hai, alipofufuka ilikuwa ngumu kwao kumjua na hata kujua kile ambacho kimeandikwa kumuhusu, lakini kwa msaada wake yeye mwenyewe waliweza kubaini ukweli uliokuweko na kwa hiyo kwa kupitia ufunuo wake katika maandiko unaweza kumjua kumhusu! Angalia maandiko hapa:-

 

Luka 24:13-32Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. Macho yao yakafumbwa wasimtambue. Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao. Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo; tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona. Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe. Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya kama anataka kuendelea mbele. Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao. Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa. Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao. Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?      

 

Kwa hiyo hata maandiko kumbe tunaweza tu tukayasoma lakini kama Mungu Baba, au Mwana au Roho Mtakatifu hatakufunulia jambo au utafichwa jambo huwezi kulibaini au kulijua, wanafunzi wa Yesu ni mpaka yalipofumbuliwa macho yao ndio wakaweza kuelewa na macho yao yakafunguliwa wakamtambua, lakini pia alipokuwa akiwafunulia maandiko tena akiwakemea ENYI MSHIOFAHAMU WENYE MIOYO MIZITO YA KUAMINI YOTE WALIYOYASEMA MANABII, ukifungwa ufahamu, ukawa na moyo mzito huwezi kuelewa na kuamini hata kilichoandikwa na manabii, Yesu akikufunulia maandiko utamuelewa kwa undani, na anaweza kufanya hivyo kwa wale waliokuwa pamoja naye n ahata kwa wale wasiokuwa pamoja naye yaani hata sisi leo Yesu yu aweza kutuelekeza kitu kupitia Roho wake Mtakatifu na tukaweza kuelewa yale yaliyofichika ona hii:-

 

Wagalatia 1:11-12 “Kwa maana, ndugu zangu, injili hiyo niliyowahubiri, nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu. Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo.”

 

Paulo Mtume pia katika kifungu hiki anatuhakikishia kuwa aliihubiri injili ambayo haikuwa ya namna ya kibinadamu kwa sababu aliipokea na kufundishwa na Yesu Kristo mwenyewe kwa ufunuo, kwa hiyo unaweza kukubaliana nami wazi kuwa bila kufunuliwa jambo kuhusu Kristo ni vigumu kwa akili za kawaida kuweza kutambua kitu au jambo kuhusu Yesu Kristo, Hasa kama Bwana amekusudia kulificha au kama hatuna muda wa kusoma na kutafakari na kutaka kumjua. Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuwa na ufunuo kumhusu Kristo ili tuweze kuwa na uelewa mpana kwa kina na mapana na marefu kumuhusu Yesu!, katika somo hili sio nia yangu kumuelezea Yesu Kristo labda nitafanya hivyo wakati mwingine leongo langu kuu ni kujibu swali la Msingi kwanini Yesu alijiita mwana wa Adamu hili tutalitafakari kwa kina katika kipengele kinachofuata:-

 

Kwanini Yesu alijiita mwana wa Adamu

 

Kama umeweza kunifuatilia tangu mwanzo, leo sitaki kujibu swali Yesu ni nani, lakini nataka kujibu na kuweka wazi kwanini Yesu alijiita Mwana wa Adamu, moja  ya njia ya kumjua Yesu ni pamoja na kuyajua maandiko, kwamba yanasema nini Kumuhusu yeye, kwa hiyo katika somo la ufahamu kuhusu Yesu Kristo yaani Christology waalimu wanafanya kazi kubwa sana ya kuchambua majina yoote ya Yesu Kristo yaliyotumika katika maandiko kumuelezea, na moja ya majina hayo ni MWANA WA ADAMU tena inaonekana wazi kuwa jina hili Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyelitumia zaidi kuliko wanafunzi wake wala watu wengine, kwa hiyo kuna swali kubwa sana la msingi la kujiuliza kwanini Yesu alikuwa akijiita mwana wa Adamu? Na kabla ya kuangalia swala hilo tuone sehemu kadhaa katika maandiko Yesu akijiita mwana wa Adamu na tukio hili la kujiita mwana wa Adamu limeonekama mara zaidi ya 82 katika maandiko hususani agano jipya

 

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya MWANA WA ADAMU atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”            

 

Mathayo 13:37 “Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni MWANA WA ADAMU;”

 

Marko 14:62 “Yesu akasema, Mimi ndiye, nanyi mtamwona MWANA WA ADAMU ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija na mawingu ya mbinguni.”

 

Luka 12:8-10 “Nami nawaambia, kila atakayenikiri mbele ya watu, MWANA WA ADAMU naye atamkiri yeye mbele ya malaika wa Mungu;          na mwenye kunikana mbele ya watu, huyo atakanwa mbele ya malaika wa Mungu. Na kila mtu atakayenena neno juu ya MWANA WA ADAMU atasamehewa, bali aliyemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.”

 

Yohana 1:51 “Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya MWANA WA ADAMU.”

 

Yohana 3:13-15 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, MWANA WA ADAMU. Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo MWANA WA ADAMU hana budi kuinuliwa; ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.”

 

Mathayo 8:20 “Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini MWANA WA ADAMU hana pa kulaza kichwa chake.”

Marko 10:45 “Kwa maana MWANA WA ADAMU naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.”

 

Luka 5:24 “Lakini, mpate kujua ya kwamba MWANA WA ADAMU anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (alimwambia yule mwenye kupooza). Nakuambia, Ondoka, ujitwike kitanda chako, ukaende zako nyumbani kwako.”

 

Mathayo 26:64 “Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona MWANA WA ADAMU ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

 

Hayo ni baadhi ya maandiko machache tu ambayo yanamtaja Yesu kama Mwana wa Adamu,  na baadhi ya mikazo hii aliitaja yeye mwenyewe, swali kubwa linabaki kwanini Yesu anajiita Mwana wa Adamu?  Na ni watu wachache sana ambao walimuita Yesu mwana wa Adamu baada ya kumuona akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu ona

 

Matendo 7:55-56 “Lakini yeye akijaa Roho Mtakatifu, akakaza macho yake, akitazama mbinguni, akauona utukufu wa Mungu, na Yesu akisimama upande wa mkono wa kuume wa Mungu. Akasema, Tazama! Naona mbingu zimefunguka, na MWANA WA ADAMU amesimama mkono wa kuume wa Mungu.”            

 

Kwa mujibu wa utafiti wa kimaandiko na michango ya wanazuoni wengi kuhusu tafasiri ya kwanini Yesu alijiita Mwana wa Adamu kwa mkazo na msisitizo mkubwa? Ziko sababu kadhaa ambazo wanatheolojia wanajaribu kuelezea Kama nitakavoainisha hapa

 

1.      Kusisitiza uhusiano wake na wanadamu

 

Moja ya tafasiri inayoelezwa na wanazuoni ni kwanini Yesu alijiita mwana wa Adamu inasemekana ni kusisitiza uhusiano wake na wanadamu, hii ni kwa sababu neno Mwana wa Katika Kiibrania linasomeka BEN ambalo lina maana kubwa mbili, Mtoto wa, na uhusiano na, Kwamfano watu waliookoka wao huitwa wana wa Ufalme ona

 

Mathayo 8:11-12 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni; bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”        

 

Wakati wale watakaofufuliwa na Bwana wetu Yesu Kristo wanaitwa wana wa Ufufuo

 

Luka 20: 35-36 “lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi; wala hawawezi kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile walivyo wana wa ufufuo.”

 

Hali kadhalika wale wanaopenda Amani, Yesu aliwaita wana wa Amani unaweza kuona katika

 

Luka 10:5-65. “Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu.”

 

Na mtu ambaye ameandikiwa hukumu ya Mungu, huitwa mwana wa uharibifu mfano ni Yuda ona

 

Yohana 17:12 “Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.”

 

Kwa hiyo Yesu anapotumia neno Mwana wa Adamu anammaanisha kimsingi uhusiano wake na wanadamu, au uhusuano wake na Adamu aliye baba ya wanadamu wote, kwa msingi huo katika mkazo huu Yesu ambaye ni Mungu anataka kuonyesha ushirika wake na wanadamu, anataka kutuonyesha kuwa aliacha enzi na utukufu na kukubali kuwa mwanadamu ambaye kimsingi ni dhaifu na hivyo ni jambo la unyenyekevu sana    

 

Wafilipi 2: 6-8 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.”

 

Kwa msingi huo jina hili Mwana wa Adamu linaunganisha au kuonyesha ubinadamu wote wa Bwana Yesu, akiwa anakula, anachoka, analala, anasalitiwa, anateswa, anadhihakiwa, anateswa na anauawa na hatimaye Mungu anamfufua kutoka kwa wafu, kwa hiyo moja yaw azo la kitheolojia ni kuwa Yesu ambaye ni Mungu alikuwa anafurahia kuushiriki ubinadamu na akawa anaweza mkazo Mwana wa Adamu.

 

2.      Kwaajili ya Kutimiza unabii

 

Jambo lingine linalozungumzwa na wanazuoni kwamba ni kwanini Yesu alijiita Mwana wa Adamu ilikuwa ni kujitambulisha kuwa yeye ndiye Masihi sawa na nabii mbalimbali katika maandiko ukiwemo unabii wa Daniel tunaweza kuliona hilo wazi katika

 

Daniel 7:13-14 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.”

 

Ni uwazi kuwa unabii huu wa Daniel pamoja na maeneo mengine umesema wazi kuwa masihi atakuwa ni wa namna gani, ni aliye mfano wa Mwanadamu na akapewa Mamlaka na utukufu na ufalme, hivyo ni vya milele, kwa hiyo wanatheolojia wengi wanahisia ya kuwa Yesu alupokuwa akijiita mwana wa Adamu alikuwa pia akijidhihirisha kuwa yeye ni Masihi sawa na namna na jinsi alivyotabiri nabii Daniel.

 

Kwa ujumla kupitia Yesu kuwa mwanadamu, ameweza kufanya kazi kubwa ya kuandaa njia ya ukombozi wa mwanadamu, ukiacha kuja kuwa na Enzi na mamlaka ya utawala wa kiungu duniani lakini Masihi ameweza kufanya mengi kwaajili ya wanadamu, ameweza kuufunua uungu na wema na tabia ya Mungu kupitia uanadamu wake kwa hiyo kuna faida kubwa sana ya Yesu kuwa mwanadamu mfano

 

Kusamehe dhambi wanadamu kwa sababu ameonja unanadamu anajua udhaifu wa mwanadamu – Marko 2:10 “Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),”

 

Kumtafuta mwanadamu na kumuokoa – Luka 19:9-10 “Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”

 

Kushiriki mateso kwa niaba ya wanadamu ili kuleta ukombozi – Marko 8:31  Akaanza kuwafundisha kwamba imempasa Mwana wa Adamu kupatikana na mateso mengi, na kukataliwa na wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na baada ya siku tatu kufufuka.”

 

Kumfunua Mungu kwetu – Yesu alipokuwa na mwili wa kibinadamu alisema wazai kuwa kazi ananozifanya na maneno yote aliyokuwa anawafundisha yalikuwa yanafunua matendo ya Mungu kwa wanadamu

 

Yohana 5:19-20 “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile.Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu.”

 

Kuonyesha shauku ya Mungu kushirikiana na wanadamu – Mathayo 1L22-23 “Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema, Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.”           

 

3.      Kwaajili ya Kufunua asili yake ya uungu

 

Tunaelewa wazi kuwa Yesu ni Mungu, kule kuitwa mwana wa Mungu maana yake anashiriki uungu, kwa hiyo Yesu alikuwa akijionea fahari kuushiriki uanadamu, huku yeye akiwa na asili ya uungu, Mungu anamjua mwanadamu kama kiumbe dhaifu na mara kadhaa alilitumia neno mwanadamu akimuita Ezekiel, inasemekana Mungu anamtaja Ezekiel kama mwanadamu mara 93 kwa msingi huo Mungu alikuwa akimaanisha Ezekiel ni mwanadamu lakini sivyo Ilivyo Kwa Kristo. Yesu hakuwa dhaifu Kama Ezekiel Yeye alikuja kumfunua Mungu kwetu, alikuwa Mungu aliyeishi katika ubinadamu

 

Wakolosai 2:9 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.”

 

Kwaajili ya haya aliweza kusamehe dhambi, aliweza kuonyesha ubwana dhidi ya sabato, aliweza kuonyesha kuwa amekuja kumuokoa mwanadamu, aliweza kuonyesha kuwa ana uwezo wa kufufua wafu, aliweza kuonyesha kuwa anamamlaka ya kuhukumu, na kuonyesha kuwa atarudi tena siku moja duniani, aliweza kuonyesha kuwa ana mamlaka ya kubadili sharia ya Musa kwa kuitimiza na ana mamlaka ya kumuweka huru Mwanadamu na kumkomboa kama mwana wa Mfalme wa Mbinguni

 

Mathayo 26:64 “Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

 

Kwa sababu hizi na nyinginezo nyingi wanatheolojia wanazitumia kumuelezea Yesu na kujaribu kujibu kuwa ndio sababu kubwa na za Msingi za Yesu kujiita mwana wa Adamu. Kwa hiyo katika tafiti nyingi na vitabu vingi na wajenga hija wengi wanaishia kwenye jambo hilo na sababu hizo kwanini Yesu alijiita mwana wa Adamu!

 

Hitimisho:

 

Kwa mtazamo wangu mimi ambao ndio umenisukuma kuandaa somo hili, Yesu alipokuwa akijiita Mwana wa Adamu, kuna tofauti kabisa na Mungu alivyokuwa akimuita Ezekiel nabii Mwanadamu, Yesu alikuwa akijiita Mwana wa Adamu, katika mtazamo uleule wa namna anavyojiita au alivyoitwa Mwana wa Abraham, au Mwana wa Daudi, unapoangalia maandiko katika Kitabu za Ezekiel Mungu anapomuita Ezekiel Mwanadamu kuna tofauti na neno Mwana wa Adamu linavyotumika katika Agano jipya tunaweza kuona kwa kitambo kiasi

 

Ezekiel 3:1-4 “Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli. Basi nikafunua kinywa changu, naye akanilisha lile gombo. Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali. Akaniambia, Mwanadamu, haya! Waendee wana wa Israeli ukawaambie maneno yangu.”

 

 

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya MWANA WA ADAMU atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”

 

Katika kiingereza wakati kwa Ezekiel wanatumia son of man au a son of man kwa Yesu linatumika neno The Son of Man, kwa Ezekiel ikimaanisha mwanadamu, na Kwa Yesu Kristo ikimaanisha Mwana wa Adamu, hii maana yake ni nini?  Huyu ni mwana wa Adamu wa Ahadi ambaye Adamu alikuwa ameahidiwa, kama ilivyokuwa kwa Abrahamu ambaye alikuwa ameahidiwa na Daudi ambaye naye alikuwa ameahidiwa, mwana huyu wa Ahadi aliyeahidiwa Adamu katika kitabu cha Mwanzo:-

 

Mwanzo 3:14-15 “BWANA Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.”

 

Ijapokuwa mwana huyu wa ahadi anaitwa uzao wa Mwanamke, lakini kwa uwazi kabisa alikuwa ni mtoto wa Adamu kwa hiyo Tangu wakati huu katika wazo la Adamu na wazo la Mwanamke walikuwa wanafahamu kuwa kuna moja ya mtoto wao ambaye atakuwa suluhisho la mgogoro kati yao na Shetani, Kwa hiyo alikuwa ni mtoto wa ahadi za kinabii, fahamu kuwa katika agano la kale mwanzoni kabisa hakukuwa na nabii na hivyo Mungu baba mwenyewe ndiye aliyekuwa nabii kwa Adamu na Eva na unabii wa kwanza ni Mwanzo 3:15 uzao wa mwanamke,

 

kwa hiyo Yesu alipokuwa akijiita mwana wa Adamu alikuwa akimaanisha mwana wa Ahadi wa Adamu, na Mwana wa Ahadi wa Abraham na mwana wa Ahadi wa Daudi, huyu kwa vyovyote vile angetokea katika mti wa uzao wa Adamu, mti wa uzao wa Ibrahimu na mti wa uzao wa Daudi. Kwa hiyo Yesu alipokuwa akijita Mwana wa Adamu alikuwa anamanisha mwana wa Ahadi wa Adamu ambaye Mungu alikuwa amemkusudia kwa ukombozi, hii ni moja ya sababu ya kujiita mwana wa Adamu, na ni mwana wa adamu ambaye atateseka angalia neno KUPONDA KISIGINO na kupitia maumivu haya ya kupondwa kisigino yeye atakomesha mateso kwa kumaliza uadui kati yetu na shetani angalia neno KUPONDA KICHWA.  Yesu alitumia jina Mwana wa Adamu mara nyingi sana akitaka akili za watu zifunguke na kumwangalia mtoto wa Adamu aliyeahidiwa unaona!

 

Sababu nyingine kubwa ya Msingi ya Yesu kujiita mwana wa Adamu ilikuwa ni maalumu sana akijilinganisha na Mwana wa Adamu aliyeuawa na Ndugu yake, Mwana huyu wa Adamu alikuwa mwenye haki, hakuwa na kosa lolote lakini aliuawa tu kwa sababu alipata kibali kwa Mungu, mwana huyu wa Adamu ni Habili, ambaye aliuawa na kaka yake Kaini,  kwa msingi huo mara kwa mara Yesu alipojiita mwana wa Adamu alikuwa maalumu anajidhihirisha kuwa Yeye ndiye yule Mwenye haki aliyeuawa katika mikono ya watu wabaya, Mwana huyu wa Adamu alimuuma sana Adamu, hasa damu yake ilipomwagika hii ndio picha halisi ambayo wanatheolojia wengi hawajawahi kuizungumzia, lakini Roho Mtakatifu alinifundisha kuwa Yesu anapojiita mwana wa Adamu kwa hakika alikuwa akimaanisha MTOTO WA ADAMU MWENYE HAKI ALIYEUAWA kwa mikono ya ndugu yake na wakati huo huo msisitizo ukiwa katika kuuawa kwake ambako kimsingi kunafanana na kuuawa kwa Habili,  tumeona maswala kadhaa kumuhusu Habili katika maandiko

 

Mtoto huyu wa Adamu alikuwa Mchungaji wa wanyama – Mwanzo 4:2 “Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.”      

 

Mtoto huyu wa Adamu alikubaliwa na Mungu kutokana na Sadaka yake - Mwanzo 4:4 “Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake;”

 

Mtoto huyu wa Adamu alisalitiwa na kuuawa na ndugu yake - Mwanzo 4:8-10 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua. BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.”

 

Mtoto huyu wa Adamu alikuwa mwenye haki - Mathayo 23:32-36 “Kijazeni basi kipimo cha baba zenu. Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu. Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.”

 

Mtoto huyu wa Adamu Damu yake ilidai haki - Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.”

 

Mtoto huyu wa Adamu alikuwa tumaini la ukombozi wa Wazazi wake - Mwanzo 4:25-26 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, MUNGU AMENIWEKEA UZAO MWINGINE MAHALI PA HABILI; kwa sababu Kaini alimwua. Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la BWANA.”

 

Mtoto huyu wa Adamu alifanya matendo yake kwa Imani - Waebrania 11:4 “Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena.”

 

Jambo hili Muhimu sana linalomuhusu Mwana huyu wa kipekee wa Adamu lina umuhimu mkubwa sana ukiunganisha na matukio yaliyomkuta Bwana wetu Yesu Kristo, Habili alichunga Kondoo, Yesu ndiye Mchungaji mwema, Habili alitoa sadaka iliyokubaliwa na Mungu, Na Yesu mjumbe wa Agano jipya aliyetoa damu inenayo mema kuliko ile ya Habili, Kuuawa kwake kulileta mtoto wa matumaini ambaye baada yake watu walianza kuliitia jina la bwana, ni baada ya kifo cha Yesu Kristo wanadamu wanapata nafasi ya kumfikia Mungu na kumuabudu pasipo hofu, Habili alikuwa mwenye haki, akauawa na ndugu yake, Na Yesu hakuwa na hatia akauawa na ndugu zake kwa hiyo kwa mujibu wa maelekezo niliyopewa mimi kama mkuu wa wajenzi, Mungu alinielekeza niieleze dunia leo, jambo ambalo wanazuoni na wanatheolojia huwa hawalielezei, au hawakuwa wamefunuliwa ya kuwa Yesu anapojiita mwana wa Adamu ni ukweli ulio wazi kuwa katika ubongo wake hakuna na wazo la mtu yule katika Daniel, wala wazo la Mtu yule katika Isaya, wala wazo la kutwaa mwili, wala hakuwa na wazo lingine zaidi ya wazo la mtoto wa Adamu aliyeuawa na ndugu yake akijitaja kama Yeye ambaye atauawa na Nduguze kwaajili ya ukombozi wa ulimwengu!

 

Wanatheolojia wengi wanamtumia Habil kama alama kivuli au unabii kuhusu Kristo na wanakubali kuwa kama Habili alivyouawa na ndugu yake na sababu kubwa ikiwa ni kwa sababu Habili alikuwa mwenye haki, kadhalika Kristo naye aliuawa na Ndugu zake wayahudi akiwa hana hatia, Mungu alimkabili Kaini akihoji Yuko wapi ndugu yako angalia

 

Mwanzo 4:10-11BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.”

 

Damu ya habili ililia kwaajili ya kutaka kisasi au haki, lakini Damu yake Yesu inalia kwaajili ya rehema na msamaha na wokovu, Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.”

 

Waefeso 1:6-7 “Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.”

 

Kwa msingi huo utakubaliana nami kuwa kama Yesu alivyokuwa akisisitiza ni kwa mauti ya namna gani atauawa na katika dhana hiyo hiyo Yesu alikuwa akijiita Mwana wa Adamu, ni kama Yesu alikuwa akitaka makutano waelewe kuwa YEYE NDIYE HABILI WA PILI, na kama vile kifo hakikuweza kunyamazisha uhai wa Habili, kifo vilevile kimeshindwa kunyamazisha uhai wa Yesu Kristo. Nasisistiza tena na tena Yesu alipokuwa akijiita mwana wa Adamu alikuwa akimuwaza Habili akilini mwaka na kile ambacho wakuu wa makuhani wangemfanyia na kazi ya ukombozi ambayo angeikamilisha kwamkifo chake, aidha masikitiko na maneno ya Adamu alipomzaa Sethi aliposema MUNGU AMENIWEKEA UZAO MWINGINE MAHALI PA HABILI katika mtazamo finyu mtoto huyo ni SETHI na katika mtazamo mpana mtoto huyo ni YESU KRISTO, mtoto wa tumaini la Adamu lililopotea.

 

                       

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

 

Mkuuu wa wajenzi mwenye Hekima