Jumapili, 7 Aprili 2024

Mpaka mlima wa Mizeituni!


Luka 22:39-44 “Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye. Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni. Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]



Utangulizi:

Katika msimu huu wa Pasaka bado tunaendelea kujifunza maswala kadhaa muhimu na madogo madogo, ambayo wakati mwingine kwa sababu ya kutazama mfumo mzima wa mateso ya Bwana tunaweza kujikuta ni kama tunayapuuzia, lakini yana umuhimu Mkubwa, leo nataka kuzungumzia kile ambacho kimejitokeza katika Mlima wa Mizeituni sehemu iitwayo Gethsemane na kuhusiana na tukio zima la Yesu Kristo kuwa na huzuni na kuingia katika maombi lakini zaidi sana hari yake kuwa kama matone ya damu.  Mahali hapa muhimu panaitwa Mlima wa Mizeituni, lakini vilevile sehemu muhimu ya mlima huu wa mizeituni pia panajulikana kama Bustani iitwayo Gethsemane.  

Mathayo 26:36-39 “Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe. Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka. Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami. Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.”

Mahali hapo ndio mahali ambapo kimsingi tunaweza kusema ushindi halisi wa Msalaba ulikoanzia, akiwa hapo kumbuka kuwa msaliti ndio alikuwa amekwenda kuwaleta maadui wa kumkamata Yesu, Hapa ndio mahali ambapo, Pia angekamatwa, hapa ndio mahali ambapo angeweza kukata tamaa, hapa ndio mahali ambapo alihitaji msaada wa Mungu, Malaika na wanadamu, Ndipo mahali ambapo angehitaji maombi kutoka kwa wenzake wa karibu ambao kimsingi walilala, hapa ndipo mahali ambapo wale walioahidi kwenda naye gerezani na hata kuwa tayari kufa naye walimkimbia, Hapa ndio mahali ambapo alizidiwa na msongo wa mawazo, hapa ndipo mahali ambapo shetani alisema naye kuhusu msalaba kama anaweza kuukabili au kukinywea kikombe cha mateso, hapa ndio mahali ambapo mipango ya adui iliyokuwa mibaya ilikuwa inaenda kufanikiwa, Ndipo mahali ambapo alitiwa nguvu na kukubaliana kuukabili Msalaba, Kimsingi ni kama Yesu alikuwa hapa katika chumba cha wangonjwa mahututi, mgonjwa ambaye anapambania uhai wake aishi ama afe na kisha mgonjwa anakubali kifo kwa Amani, kwa hiyo mlima wa mizeituni, Bustani ya Gethsemane ni eneo la maamuzi magumu. Ni eneo ambalo wakati na Muda muafaka wa ukombozi wa mwanadamu unaenda kuanza, ni eneo la mapito ya moyoni. Na ya kihisia, na ya hofu na ya kutisha zaidi kuliko hata msalaba wenyewe. Kila mwanadamu katika maisha yake huwa anapitia katika bustani hii, kwa namna moja ama nyingine, ni mahali ambapo tunapaswa kuruhusu Mapenzi ya Mungu yatimizwe! Tunajifunza somo hili, Mpaka mlima wa Mizeituni kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-

 

·         Mlima wa Mizeituni, Bustani iitwayo Gethsemane

·         Mpaka mlima wa Mizeituni

 

Mlima wa Mizeituni, Bustani iitwayo Gethsemane

Ni Muhimu kufahamu kuwa Neno la Mungu, limekuja kwetu kwa uweza wa Roho Mtakatifu, na Ni Roho huyu wa Mungu aliyewaongoza waandishi kuweka rekodi hizi kwa kusudi la kutufundisha maswala mbali mbali. Katika injili zote tunaona wakiwa wameelezea kuhusiana na Mahali hapa alipokamatwa Yesu, Pakiwa panajulikana kama mlima wa Mizeituni, au bustani ya Gethsemane lakini pia panaitwa Mahali pale, Kama ilivyo umuhimu wa Golgotha au Kalvari, Mlima wa Mizeituni na hasa hapo Gethsemane pana umuhimu mkubwa sana katika safari ya ukombozi wa mwanadamu.

Mathayo 26:30 “Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.”

Luka 22:39 “Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye.”

Marko 14:26 “Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda mlima wa Mizeituni.”

Kwa hiyo tunaona Injili zote zikitaja habari za Mlima wa Mizeituni, Ni mlima maarufu na wa zamani sana una ukubwa wa kama kilomita mbili hivi, mlima huu uko upande wa Mashariki mwa mji wa Yerusalem, Mlima huu una urefu wa mita 78 au futi 250 ni mrefu kuliko mlima wa hekalu, na hivyo ni eneo zuri ambalo unaweza kukaa na kuliangalia hekalu vizuri, Yesu alipenda kuutumia mlima huu kwa maombi, kwa hiyo palikuwa ni mahali ambapo alipendelea kupatembelea mara kwa mara akiwa Yerusalem na alitumia mlima huo kufanya maombi, mlima unaitwa mlima wa mizeituni kwa sababu unafunikwa na miti hiyo ya mizeituni na kulifanya eneo hilo kupendeza kwa ukijani wa Miti hiyo, Mahali hapa Ndipo mahali ambapo Yesu alipatumia kupaa mbinguni angalia

Matendo 1:9-12 “Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni. Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.”

Na ni katika mlima huu huu Yesu atakaporudi atashukia hapo akitokea mbinguni na kufanya vita na Mpinga Kristo, na kusimamisha utawala wake, kwa hiyo Mlima huu ni mlima wa kihistoria katika ukombozi wa mwanadamu na utawala wa Mungu yaani ufalme wa Mungu.  

Zekaria 14:3-4 “Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita. Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.”

Kwa hiyo mlima wa mizeituni ni mahali, muhimu sana katika unabii na historia nzima ya ukombozi wa mwanadamu na kusimama kwa serikali ya kiungu yaani ufalme wa Mbinguni, kwa msingi huo Yesu hakwenda tu katika mlima wa mizeituni kwa bahati mbaya, katika eneo hili la Mlima wa Mizeituni juu ilikuweko sehemu ambayo ilikuwa na bustani nzuri na sehemu hiyo iliitwa Gethsemane, kwa hiyo utaweza kuona tena waandishi wa Injili wakiitaja sehemu hiyo angalia tena katika neno la Mungu hususani baadi ya vitavu vya injili.

Mathayo 26:36 “Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.”

Marko 14:32 “Kisha wakaja mpaka bustani iitwayo Gethsemane; akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa muda niombapo.”      

Kwa hiyo katika mlima huo wa mizeituni vilevile kulikuwako bustani ambayo iliitwa Gethsemane na Luka anapaita mahali pale hii ni kwa sababu mahali hapo palikuwa ni maarufu sana hata leo

Luka 22:40 “Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni.”

Kwa Msingi huo ni muhimu kufahamu kuwa eneo hili muhimu katika historia ya ukombozi wa mwanadamu, linaitwa Mlima wa Mizeituni, lakini Pia Bustani ya Gethsemane, lakini Luka anapaita mahali pale, na kuonyesha kuwa Yesu alikuwa na desturi ya kwenda katika eneo hilo mara kadhaa, eneo hili kwa maelezo ya kale na katika injili ya Yohana palikuwa ng’ambo ya kijito Kedroni, ambapo ndipo bustani hii ilipokuwepo na Yesu alipachagua kama mahali pa maombi unaweza kuona

Yohana 18:1 “Alipokwisha kusema hayo, Yesu alitoka pamoja na wanafunzi wake kwenda ng'ambo ya kijito Kedroni, palipokuwapo bustani; akaingia yeye na wanafunzi wake.”

Eneo hili linaloitwa GETHSEMANE ambalo ni jina lenye asili ya Kiaram ambalo maana yake Sehemu ya kukamulia mafuta, (oil Press) kwa hiyo uko uwezekano ya kuwa katika bustani ile ya Mizeituni, kulikuweko na mashine za kukamulia mafuta ya zeituni,  na ndio sababu pakaitwa pia GETHSEMANE, lakini vile vile kwanini Luka anapaita MAHALI PALE, mahali hapo palikuwa na historia maarufu ya watu hasa Mfalme mkuu Daudi kwenda kuabudu, lakini sio hivyo tu Ni eneo ambalo Daudi aliposalitiwa na Mwanae Absalom alikimbia na kuvuka mto huu yeye na watu wake na wakapanda mlima huu wa mizeituni wakiwa wanalia sana, wakiwa hawana viatu na wakiwa wamejifunika nguo zao vichwani  mahali hapa kimsingi palikuwa na sehemu ambapo Mungu alikuwa akiabudiwa, Lakini Mfalme Daudi na watu wake walipanda mahali hapa wakiwa wamekata tamaa, wakiwa wanalia machozi, wakiwa hawajui mbele yao itakuwaje. Unaweza kuona katika andiko hili:-

2Samuel 15:30-32 “Daudi akapanda akishika njia ya kuupandia mlima wa Mizeituni, akilia alipokuwa akipanda; naye alikuwa amejifunika kichwa chake, akaenda hana viatu; na watu wote waliokuwa pamoja naye wakajifunika vichwa vyao, kila mmoja wao, wakapanda juu, wakilia walipopanda Mtu mmoja akamwambia Daudi ya kwamba, Ahithofeli yu katika hao waliopatana na Absalomu; Daudi akasema, Ee Bwana, nakusihi, uligeuze shauri la Ahithofeli liwe ubatili. Ikawa, Daudi alipofika juu, hapo Mungu alipoabudiwa, tazama, Hushai, Mwarki, akaja kumlaki na joho Lake Limeraruliwa, tena ana udongo kichwani mwake.               

Kwa hiyo unaweza kuona Gethsemane katika mlima wa mizeituni. Zaituni zilikamuliwa na zikatoa mafuta, lakini vilevile ulikuwa ni mlima wa kutoa machozi, Daudi na watu wake walipanda mlima huu huku wanalia, na Yesu alipanda mlima huu akiwa Analia, Daudi alipanda mlima huu akiwa amekata tamaa na kupoteza matumaini akiwa amesalitiwa na Mwanae Absalom na Yesu anapanda mlima huu akiwa amekata tamaa na anapoteza tumaini kuukabili Msalaba akiwa amesalitiwa na mmoja ya Mwanafunzi wake Muhimu, huku roho yake ikiwa ina huzuni mno

Mpaka mlima wa Mizeituni

Luka 22:39-44 “Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye. Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni. Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu. Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]

Tunaona katika andiko letu la msingi kuwa Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka mlima wa mizeituni, Mahali hapa Yesu alikuwa ameelemewa na Huzuni, Huzuni kubwa kwa sababu anakabiliwa na kifo na sio kifo cha kawaida ni kifo cha msalaba, hakuna mauti mbaya kama mauti ya msalaba, katika historia za hukumu ya kifo, kila taifa lilikuwa lina namna yake ya kuua

Waingereza mtu alipohukumiwa kifo walitumia kitanzi, wakati warumi walitumia shoka lililotundikwa, na wayahudi walitumia kupiga mawe mpaka kifo, warumi walikuwa na hukumu nyingine ya kifo kwa raia asiyekuwa Mrumi ambayo ilikuwa ni kumtundika msalabani, kifo hiki kilikuwa ni kibaya zaidi kwa sababu ni mauti ya polepole, ilikuwa pia ni mauti ya aibu, kwa sababu watu walisulubiwa wakiwa tupu na kudhalilishwa, wayahudi waliamini kuwa Mungu hawezi kuruhusu mtu mwema kufa msalabani, mtu aliyehukumiwa kifo cha msalabani alihesabika kuwa amelaaniwa,

Wagalatia 3:13-14 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.”

Kwa hiyo katika mawazo ya Kristo kama Mwana wa Mariam yaani kibinadamu mauti hii ilikuwa ni ya kuiepuka, angetamani sana kikombe hiki kimuepuka aliomba kwa hisia kali sana na hapa alikuwa amejawa na msongo wa mawazo, na ni katika eneo hilo hilo ambapo zaituni zilikuwa zinakamuliwa Yesu alikamuliwa na msongo wa mawazo, kiasi cha kutoka jasho (Hari) la damu, tukio hili kisayansi linaitwa Agony – ambalo maana yake ni Msongo mkubwa wa mawazo unaoathiri hali halisi ya mwili kiasi cha mishipa ya damu kuzidiwa na kupanuka kwa vinyeleo na kuruhusu jasho na damu kutoka, tukio hili liliweza kuelezewa na Luka pekee kwa vile yeye alikuwa tabibu, Kwa hiyo Yesu alikuwa ameleemewa na huzuni kubwa kwa sababu aina ya mateso ilikuwa mbaya kubebeka, na malaika walikuja kumtia nguvu kuwa anapaswa kubeba, kwa hiyo tunapata picha hii Yesu alipokuwa Gethsemane

-          Ni mahali ambapo mtu anaelemewa na huzuni kubwa na msongo mkubwa wa mawazo

-          Ni mahali ambapo mtu anakuwa amesalitiwa na kuachwa peke yake

-          Ni mahali ambapo unajaribu kuomba msaada watu hata wakuombee na wanalala

-          Ni mahali ambapo mtu unakata tamaa na kupoteza matumaini

-          Ni mahali ambapo unaweza kuchanganyikiwa kwa sababu mipango ya adui ndiyo inayokwenda kufanikiwa

-          Ni mahali ambapo ni kama Mungu anasikia maombi ya adui zako na mipango yao na ya kwako haisikiwi

-          Ni mahali ambapo hakuna faraja kutoka upande wowote

-          Ni mahali ambapo shetani angependa ubaki hapo ili akulize akukamue

-          Ni mahali ambapo manabii walipanda wakiwa wanalia, machozi wamekata tamaa

-          Ni mahali ambapo Imani yako inakamuliwa ili ikiwezekana iishe na urudie hapo

-          Ni mahali ambapo pamejaa mashaka na marafiki wamekuacha peke yako

-          Ni mahali ambapo ni kama uko chumba cha wagonjwa mahututi na unaota ndoto za kugombea uhai au kifo

-          Ni mahali ambapo huwezi kuamua mambo, na mambo yako yanaamuliwa na adui zako

-          Ni mahali ambapo unachokiona mbele yako ni kifo tu maombi hayajibiwi

-          Ni mahali ambapo ni kama maamuzi yamepita na huwezi hata kukata rufaa tena

-          Ni mahali ambapo utatiwa mikononi mwa adui na rafiki zako wote watakukimbia

-          Ni mahali ambapo unakutana na vita ya kiakili, kihisia na kiroho, na ni mahali pa maamuzi magumu!

Mungu katika hekima yake huruhusu nyakati Fulani na sisi katika maisha yetu tupite tupande mpaka mlima wa Mizeituni, tuende mpaka Gethsemane tukakamuliwe huko, tukalizwe huko, akili zetu zizungumze na shetani, huku Mungu akiwa kimyaa, Katika hali ya kawaida wakati wa mapito na mateso huwa hauonekani kuwa ni wakati mzuri, unakuwa ni wakati wa kukamuliwa, unakuwa ni wakati wa taarifa mbaya, unakuwa ni wakati wa kuamua kufanya mapenzi ya Mungu au kuyaacha taarifa njema ni kuwa Yesu hakukata tamaa, Yesu hakuvunjika moyo na malaika wa Bwana walikuja kumtia nguvu na akawa yuko tayari kuyakabili mateso ya Msalaba, Daudi alilia katika mlima huu, lakini alifanikiwa kujipanga na kukabiliana na Absalom na Mungu alimpa ushindi, Mungu alijibu maombi ya Yesu kwa kumtia nguvu aukabili Msalaba lakini alijua ya kuwa siku ya tatu atamfufua na kumpeleka katika maisha yasiyozuilika  Ushindi wa maisha yetu na furaha ya kweli hupatikana, pia kwa kupitia njia ya mateso,  tumepewa sio kumwamini tu bali na kuteswa kwaajili yake

Wafilipi 1:28-29 “wala hamwaogopi adui zenu, katika neno lo lote; kwao hao ni ishara mathubuti ya kupotea, bali kwenu ninyi ni ishara ya wokovu, huo utokao kwa Mungu. Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;”                

Mungu atatuacha tupite katika wakati Mgumu, ambao utatuletea ushindi mkubwa sana na hivyo hatupaswi kuogopa tunapopita Gethsemane wakati ambapo umeachwa peke yako na hakuna wa kukushika mkono usiogope Yesu Kristo anaijua njia hiyo na ni yeye aliyesema Twendeni mpaka mlima wa mizeituni mlima huu sio wa mateso pekee bali ni mlima wa ushindi, ni mlima wa mahali ambapo sio Yesu atakamatwa tu, na kugongwa kisigino, lakini ni mahali ambapo Yesu atakanyaga tena na mlima huu utapasuka na watachinjiliwa mbali adui zake ni mlima ambapo ufalme wa Mungu utastawi, kumbuka muda wa kupita hapa sio mrefu ni mfupi sana

1Petro 5:8-11 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu. Uweza una yeye hata milele na milele. Amina.”

Baada ya mateso ya kihisia pale Gethsemane Yesu alitiwa nguvu kuukabili Msalaba, alikwenda msalabani na alipitia dhihaka na mateso akiwa ana utulivu mkubwa sana akijua faida ya mateso yale na kufufuka kwake

-          Alikuwa na nguvu ya kuwaombea maadui zake

-          Alikuwa na nguvu ya kuruhusu majambazi waende peponi

-          Alikuwa na nguvu ya kutangaza kuwa kazi ya ukombozi umekamilika

-          Alikuwa na nguvu ya kukabidhi roho yake kwa Amani akijua ya kuwa Baba yake atamfufua

-          Alikuwa na nguvu ya kuruhusu pazia la hekalu kupasuka na watu kuifikia neema ya Mungu

-          Alikuwa na nguvu ya kufufua watu waliokufa zamani na miili yao kuonekana kwa muda

-          Alikuwa na nguvu dhidi ya Mauti akitupa waamini wote tumaini kubwa lenye Baraka

-          Alikuwa na nguvu ya kusamehe dhambi

-          Alikuwa na nguvu ya kututhibitishia na kutuhakikishia wokovu

-          Alikuwa na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii zote duniani

-          Alikuwa na nguvu ya kutioa faraja na tumaini kiasi cha kumuwezesha kila mtu kuwa tayari kufa kama yeye

-          Alikuwa na nguvu na mamlaka yote mbinguni na duniani

-          Alikuwa anamejithibitishia kuwa atarudi tena na kukanyaga mlima wa mizeituni

-          Alikuwa na nguvu ya kuwafanya adui zake na wote waliokuwa wakimtesa walikiri hakika alikuwa mwema

Ushindi wote huo hapo juu ni kwa sababu Pale Gethsemane Yesu alikubali Mapenzi ya Mungu, kwamba hata tunapopitia katika njia zilizo ngumu sana hatuachi kuomba tunaomba na baba akiwa kimya tunakubali mapenzi yake yatimizwe

Luka 22:41-43. “Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.”  

Ni pale Gethsemane ndipo Yesu alipotengeneza nguvu ya kukabiliana na hali zote zilizokuwa mbele yake kumbuka alisema ombeni kusudi msiingie majaribuni, aliweza kuyashinda majaribu yote na malaika wa Bwana walikuja kumtia nguvu

Ni pale Gethsemane ndipo Yesu alipoonja hisia na mateso yetu ya kibinadamu tunapokuwa taabuni alionyesha uanadamu wake na sisi tunapopita katika majaribu makali anaujua uanadamu wetu, Ni hapa ndipo wanafunzi wa Yesu walipofahamu umuhimu wa maombi, ni hapa ndipo alipowafundisha namna wanavyoweza kukabiliana na ushindi wanapokuwa matatani.

Mathayo 26:41 “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”

Ni pale Gethsemane ndipo Yesu alionyesha kuwa kweli yeye ni Mpakwa mafuta kwa sababu alikubali kuukabili msalaba bila vurumai yoyote aliukabili msalaba kwa upole na unyenyekevu mkubwa

Isaya 53:3-7 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote. Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.”

Ni pale Gethsemane Ndipo Yesu alipoanza harakati za ukombozi wa mwanadamu kwa kukabiliana na matukio yote kuanzia mahakamani, kusulubiwa kufa na kufufuka akiwa sadaka kamili ya upatanisho na msamaha wa dhambi zetu akitupatanisha sisi na Mungu

1Timotheo 2:5-6 “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.”

Ni Gethsemane ndipo Yesu alipoandaa ukamilisho wa eneo muhimu la huduma yake duniani akionyesha kumtii Mungu hata mauti ya msalaba, akiwa tayari kukamilisha mapenzi ya Mungu, huruma zake kubwa kwa wanadamu na wajibu wake mkubwa kama mwokozi wa ulimwengu jambo ambalo limemletea sifa kubwa sana Mbinguni

Wafilipi 2:5-11 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

Ndugu msomaji wangu, kumbuka wakati wote unapopitia mateso, ni kama uko Gethsemane, ni kama Mwalimu amekuambia upande mlima wa mizeituni, utakuwepo kwa Muda mfupi na ukimtii Mungu katika wakati huo Mungu, atakupeleka katika maisha ya Gethsemane, na kukupeleka katika maisha yasiyoweza kuzuilika, wote sasa tunaweza kuona umuhimu wa mlima wa mizeituni na eneo la Gethsemane, tunajifunza kujitia nguvu katika Bwana, kuwa na ujasiri na utayari wa kukabiliaba na mambo magumu ambayo kwa kawaida Mungu huyafupiza sana lakini hutupa matokeo mazuri sana tunapokuwa tumeyatii mapenzi yake. Mungu akutie nguvu wakati wote unapopanda mlima wa mizeituni na kupita eneo la kukamuliwa, Malaika wa bwana watakutia nguvu utakuwa na moyo wa ujasiri na utashinda na kuwa msaada mkubwa kwa ulimwengu unaokuzunguka Uongezewe neema!

 

Na. Rev. Mkombozi Innocent Samuel bin Jumaa bin Athumani Sekivunga Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima



Jumapili, 31 Machi 2024

Maisha yasiyozuilika!


Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”     




Utangulizi:

Leo ni sikukuu ya Pasaka, ambapo wakristo nchini wanaungana na wakristo wote duniani kuadhimisha kuteswa, kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo kulikotokea zaidi ya miaka 2000 iliyopita Huko Yerusalem Nchini Israel, Katika wakati huu wa Pasaka Leo ni Muhimu kujikumbusha kuwa Mungu ametupa maisha yasiyozuilika, Kristo Yesu alipofufuka ametufundisha na kutukumbusha  kuwa kuna maisha yasiyozuilika, Yesu anatufundisha kupitia kufufuka kwake kuwa yako maisha yasiyozuilika,  na kuwa uko uwezekano wa kuishi maisha yasiyozuilika, Haya ni maisha ambayo Mungu alikusudia kila mmoja ayaishi katika ulimwengu huu ambao una vikwazo vingi sana, Lakini kama mtu akiwa na Yesu ataweza kuishi maisha yasiyoweza kuziilika!  Maisha yasiyozuilika ni maisha ya kushinda vikwazo:-

1Yohana 5:11-13 “Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima. Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu.”

Unaweza kujiuliza kuwa Mchungaji anataka kuzungumzia nini? Je maisha yasiyozuilika nini Ni uzima wa milele? Ama ni kitu gani na kwa vipi maisha hayo yana uhusiano na Yesu aliyefufuka?  Tutachukua muda kujifunza kwa ufupi na kwa kina ili tuweze kuelewa maisha hayo yasiyozuilika kwa kuzingatia vipengele viwili tu vifuatavyo:- 

·         Maana ya maisha yasiyozuilika

·         Maisha yasiyozuilika

Maana ya Maisha yasiyozuilika! 

Tunapozungumzia kuhusu Maisha yasiyozuilika, tunazungumzia kuwa na maisha yasiyo na mipaka, au maisha yanayoshinda vikwazo, maisha ya uhuru na na yaliyojaa neema ya Mungu inayotusaidia kufikia ndoto zetu huku tukishinda kila aina ya kikwazo kinachowekwa na shetani au wanadamu,  Maisha yanayoweza kuwa na ushindi, bila kujali nguvu kutoka nje inasema nini, Unapoyasoma maandiko yanaonyesha wazi kuwa Mpango wa Mungu kwa mwanadamu tangu mwanzo ilikuwa ni aina hii ya maisha na Yesu aliyefufuka anatukumbusha kupitia hatua yake ya kufufuka kuwa yako maisha yasiyozuilika!, Mapena na mara kadhaa Yesu alikuwa amesema atafufuka  na alisema kuwa atafufuka siku ya tatu na mpango huu Yesu alitaka ueleweke wazi kwa wanafunzi wake na hata kwa adui zake na ndio maana alirudia tena na tena maneno yake hayo ona:-

-          Mathayo 16:21-23 “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka. Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”

 

-          Marko 8:31-32a “Akaanza kuwafundisha kwamba imempasa Mwana wa Adamu kupatikana na mateso mengi, na kukataliwa na wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na baada ya siku tatu kufufuka. Naye alikuwa akinena neno hilo waziwazi.”

 

-          Luka 9:21-22 “Akawaonya, akawakataza wasimwambie mtu neno hilo; akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa na siku ya tatu kufufuka.”

 

-          Mathayo 17:22-23 “Nao walipokuwa wakikaa Galilaya, Yesu akawaambia, Mwana wa Adamu anakwenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua, na siku ya tatu atafufuka. Wakasikitika sana.”

 

-          Marko 9:30-32 “Wakatoka huko, wakapita katikati ya Galilaya; naye hakutaka mtu kujua. Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akawaambia, Mwana wa Adamu yuaenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua; hata akiisha kuuawa, baada ya siku tatu atafufuka. Lakini hawakulifahamu neno lile, wakaogopa kumwuliza.       

 

-          Luka 9:43-45 “Wote wakashangaa, wakiuona ukuu wa Mungu. Nao walipokuwa wakiyastaajabia mambo yote aliyoyafanya, aliwaambia wanafunzi wake, Yashikeni maneno haya masikioni mwenu, kwa kuwa Mwana wa Adamu anakwenda kutiwa katika mikono ya watu. Lakini hawakulifahamu neno lile, likafichwa kwao wasilitambue; wakaogopa kumwuliza maana yake neno lile.”

Kwa hiyo huu ulikuwa ni mpango wa Mungu, Na Bwana Yesu aliusema mapema kwamba kifo hakiwezi kumzuia, hakuna kitu kinaweza kuzuia mpango wake wa kufufuka kutoka kwa wafu, huu ndio ulikuwa ujumbe mkuu wa Yesu, Lakini katika namna ya kushangaza shetani pamoja na majeshi yake yote walikuwa na mpango wao wa kuzuia ili yamkini ikiwezekana Yesu asifufuke ona 

Mathayo 27:62-66 “Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato, wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka. Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza. Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo. Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.”

Unaona njama zilipangwa na viongozi wa kidini wakishirikiana na serikali ya kirumi kuhakikisha kaburi la Yesu linalindwa salama, Kulindwa salama maana yake ni kulinda kwa uhakika, kuhakikisha kuwa hakuna linalobatilika, lindeni kwa kukakisha kuwa haibiwi, lindeni kwa kuhakikisha kuwa hafufuki!  Kwa hiyo wayahudi walitaka kuhakikisha Yesu anabaki kaburini na hatoki tena na hachomoki kabisa kutoka katiia mpango wake huo, walimuwekea ulinzi waliweka mipaka, waliweka kizuizi, walitaka kuakikisha kuwa hakubadiliki neno, Hata hivyo hawakujua kuwa Yesu aliishi maisha yasiyozuilika na hakuna kitu ambacho kingeweza kumzuia asitoke kaburini, hata kifo hakiwezi kumzuia na kumfanya abaki kaburini, Kristo alikuwa na maisha yasiyozuilika, na kifo kisingeliweza kumzuia hakuna cha kumzuia Yesu katika mpango wake.

Maisha yasiyozuilika    

Mathayo 28:1-7 “Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi. Na tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la nchi; kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaja akalivingirisha lile jiwe akalikalia. Na sura yake ilikuwa kama umeme, na mavazi yake meupe kama theluji. Na kwa kumwogopa, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu. Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa. Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia.” 

Yesu alisema atafufuka, na wapinzani wake walitaka kuhakikisha kuwa Yesu hafufuki, waliweka walinzi katika kaburi lake, waliweka muhuri kuhakikisha kuwa hakuna neno linalobatilika lakini Yesu/Mungu akisema neno lake hakuna mtu anaweza kusimama kinyume na makusudi na mpango wa Mungu, Yesu alikuwa akituonyesha wazi kuwa tunaweza kuishi maisha yasiyozuilika, kila anaemwamini Yesu na kuiamini kazi aliyoifanya pale msalabani, atakuwa na maisha yasiyozuilika, sio kifo tu lakini kila kitu kinachojaribu kusimama kinyume na kile unachokusudia kukifanya, au biashara zako, au ndoa yako, au mafanikio yako, au kazi yako, au vyovyote vile, unapaswa kukumbuka kuwa Yesu anatuonyesha njia kuwa hakuna anayeweza kukuwekea mipaka katika maisha yako, Kristo aliyefufuka ni mfano mzuri wa maisha yasiozuilika, tangu mwanzo Mungu alikusudia kuwa watu wake wawe mashahidi wa kazi zake na wakati wote kazi zake na mpango wake hakuna anayeweza kuzuia 

Isaya 43:12-13 “Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, nami ni Mungu. Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia?

Kufufuka kwa Yesu Kristo ndio ulikuwa ushindi mkubwa sana dhidi ya shetani maajenti wake na kazi zake zote, na ilikuwa ndio kilele cha utekelezaji wa kazi ya ukombozi wa Mwanadamu, kwa hiyo shetani alikuwa anataka kuzuia na kuiwekea mipaka kazi iliyofanywa na Bwana, wakati wote unapokaribia katika mafanikio yako, au inapokaribia kuwa Mungu anataka kubadilisa kabisa mpango wa maisha yako na kukuinua, Kuzimu inataharuki na itahakikisha inapambana na kuzuia  mpango wa Mungu katika maisha yako, wakati huo shetani anasahau kuwa Yesu amekupa maisha yasiyozuilika, Kila mtu aliyeokolewa yuko upande wa Mungu yuko na Bwana na Mungu ametupa maisha yasiyizuilika, Kama hakuna kitu cha kututenga na Upendo wa Mungu ni wazi vilevile kuwa hakuna kitu kitaweza kutuzuia katika jambo lolote lile zingatia kuwa Yesu aliyefufuka anaza mamlaka za mauti na kuzimu na zaidi ya yote yeye ndiye huo ufufuo na uzima sasa jaribu kuwaza na kifikiri nini kinaweza kuzuia maisha yako ? angalia maandiko:- 

Warumi 8:31-39 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye? Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

Unaona maandiko yanaonyesha ukimuamini Yesu unapewa maisha yasiyozuilika na hakuna cha kutuzuia, hakuna wa kutushitaki, maana wako watu watatafuta mambo ya kukushitaki, walimshitaki Yesu mbona! tena kwa ushahidi wa uongo, watatafuta kukudhihaki, watakufanyia kila kitu kibaya ili yamkini ikiwezekana ukate tamaa, wanaweza kutuhukumu, wanaweza kutupangia aina ya adhabu, wanaweza kutupangia aina ya hukumu, wanaweza kukadiria aina ya maisha yetu, wanaweza kujifanya wana hatima ya maisha yetu kwa vyovyote vile  lakini kumbuka kuwa hawajafa kwaajili yetu,  Yesu ndiye aliyekufa na zaidi ya hayo amefufuka katika wafu, na yuko mkono wa kuume anatuombea, maombi ya Yesu kwaajili yako na yangu hayawezi kukataliwa, yuko mkono wa kuume wa baba kwa sababu hiyo kumbe kufufuka kwake kuna umuhimu mkubwa sana kwa sababu kunatupa maisha yasiyozuilika, kila anayepambana na kusudi la Mungu ndani yako anapaswa kuchukua tahadhari kubwa kwa sababu huenda anataka vita na Mungu, na akipigana na Mungu atajikuta yuko kwenye madhara makubwa kwa sababu tumepewa maisha yasiyozuilika, Wayahudi sio tu walitaka kuzia Yesu asifufuke lakini pia walitaka kuizua kazi yake mtu mmoja mwenye hekima akawaonya wayahudi kuwa waache kupambana na kazi za Yesu, kama walimsindwa Yeye waachie kazi yake ona   

Matendo 5:33-39 “Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua. Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo, akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa. Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu.Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika.Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.”    
          

Pasaka hii ni onyo dhidi ya watu wote wanaokusudia na waliokusudia kushindana na mapenzi ya Mungu, kwa kanisa, kwa watumishi wake, na kwa maisha yako kwamba wajihadhari waache kushughulika na watu wenye maisha yasiyozuilika, mtu aliyeokolewa na kumuamini Bwaa Yesu kuwa bwana na mwokozi wa maisha yake hakuna cha kumzuia hata ukimuua, anapita tu kutoka mautini na kuingia uzimani, 

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.”

Hakuna raha kama kuishi maisha yasiyozuilika maana kuna faida nyingi sana, na hatuwezi kuzimaliza zote lakini lakini zote hizi tunapewa kwa sababu Mungu alitaka tuwe na maisha yasiyozuilika  

-          Watashindana nawe na hawatakushinda – Yeremia 1:18-19 “Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii. Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.”

 

-          Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa – Isaya 54:17 “Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.”

 

-          Hakuna uchawi wala uganga utakuweza – Hesabu 23:23 “Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati. Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!

               

-          Adui atakuja kwa njia moja atatawanyika kwa njia saba - Kumbukumbu 28:7 “Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.”                 

Ndugu yangu unapoadhimisha sikukuu ya pasaka leo, Nakuombea kwa Mungu, na ni maombi yangu kuwa kila mmoja wetu aweze kuishi maisha yasiyozuilika, Yesu Kristo aliyefufuka ana mamlaka ya kuzimu na mauti, hivyo kila amuaminiye maana yake hakuna mtu anakuweza, sio mauti sio kuzimu, wala lolote linaweza kuyafanya maisha yako yakawa na kizuizi, Alipomwambia Yohana asiogope anakuambia na wewe na mimi tusiogope

Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”     

Pasaka hii Mungu akuondolee vikwazo vya kila aina katika maisha yako na vile utakavyokutana navyo Mungu akupe kuvishinda, Mimi nilikutana na vikwazo vingi na vizuizi vyingi sana katika maisha yangu, huduma na utumishi, lakini hakuna hata kimoja kiliweza kuyazuia maisha yasiyozuilika Bwana anaweza hata kuandaa meza Machoni pa watesi wako na kukupaka mafuta mpaka kikombe chako kikafurika, Ubarikiwe na usihi maisha yasiyozuilika, kukiwa na maji tembea juu ya maji, wakitaka kukukamata pita katikati yao wende zako, wakikutupa katika makanwa ya simba hutatafunwa, wakikutupa katika tanuru la moto hutatekeketa, bahari ikiwa kikwazo bwana atafanya njia, kila iana ya dhiki na mateso na majaribu utayapitia lakini, utatoboa, wakikuzika na kulilinda kaburi ili usifufuke tetemeko na malaika wa bwana atawafanya aduinzako wawe kama wafu nawe utatoka. Kwa nini kwa sababu Yesu ametukirimia Maisha yasiyozuilika, na kwa jina lake kila kikwazo kinachisimama mbele yako kitabomolewa na kusawazishwa katika jina la Yesu. Nakutakia msimu mzuri wa sikukuu ya Pasaka Mungu akutunze!

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Ijumaa, 29 Machi 2024

Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi!


Marko 14:27-31 “Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Naye akazidi sana kusema, Ijaponipasa kufa nawe, hata hivyo sitakukana kamwe. Na wote wakasema vile vile.”   

          



Utangulizi:

Tunakaribia kabisa katika juma muhimu la Pasaka, na jumbe mbalimbali zitakuwa zinahubiriwa katika majira haya na msimu huu kuelekea katika wakati wa Pasaka, mimi nami nimetia mkono wangu nipate kuzungumza lile ambalo Mungu anataka kusema na watu wake katika majira haya ya Pasaka, Katika majira haya ya pasaka nataka tujikumbushe kwamba uko umuhimu wa kujishusha, tunapokumbuka na kuadhimisha pasaka tunakumbuka tu sio ukombozi wa Mwanadamu pekee bali na umuhimu wa kuchukua nafasi ya chini kwa kujinyenyekeza na kuacha kabisa kujiona Bora kuliko wengine

Wafilipi 2:3-8 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.”

Unaona tunajifunza kwamba Pasaka ni unyenyekevu, Kitendo cha Yesu Kristo kuubeba Msalaba na kukibali mateso ili hali alikuwa Mungu, katika msimu huu wa Pasaka kinatukumbusha kuwa wakati wote tunapaswa kuufuata mfano wake, na kuacha kujitutumua au kujiweka katika nafasi ambayo sisi wenywewe tunadhani kuwa ni wa muhimu kuliko wengine, kila mmoja amuhesabu mwenzake kuwa ni bora kuliko nafsi yake! Tutajifunza somo hili Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi! Kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-


·         Maana ya neno Kunguwazwa

·         Hata wajapokunguwazwa wote lakini sio mimi

·         Mambo muhimu ya kujifunza


Maana ya neno Kungunguwazwa

Marko 14:27-31 “Yesu akawaambia, MTAKUNGUWAZWA ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Naye akazidi sana kusema, Ijaponipasa kufa nawe, hata hivyo sitakukana kamwe. Na wote wakasema vile vile.”

Ni muhimu kufahamu kuwa lugha ya Kiswahili inayotumika mahali hapo kama Kunguwazwa ni lugha ya Kiswahili cha kizamani, Neno Mtakungwaza katika Biblia ya kiingereza ya KJV mstari wa 27 unasomeka hivi And Jesus saith unto them All Ye shall be OFFENDED because of me this night” kwa hiyo neno kukunguwazwa katika kiingereza ni Offended ambalo kwa kiyunani ni SKANDALIZO Ambalo maana yake ni kuingia mtegoni, au kukwazwa au kukoseshwa, au kuchukizwa kama linavyotumiwa na waandishi wengine

Mathayo 26:31-35 “Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote MTACHUKIZWA kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Petro akamwambia, Ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe. Na wanafunzi wote wakasema vivyo hivyo.”

Kukunguwazwa huku au kuchukizwa kuna uhusiano wa kumkana au kumkimbia Yesu, usiku wa kukamatwa kwa Yesu, ulikuwa ni usiku wa kujaribiwa kwa wanafunzi wake, na shetani alikuwa ameruhusiwa ili awapepete kama ngano, kwaaajili ya kuonyesha kuwa bado walikuwa hawako imara kumtetea au hata kuwa pamoja na Yesu wakati ule

Luka 22:31-34 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano; lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako. Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni. Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui.”

Yesu Kristo alikuwa amejua kuwa usiku ule atakaokamatwa, utakuwa ni usiku wa majaribu makubwa kwa wanafunzi wake, aliwataka waombe kule bustanini ili wasiingie majaribuni, ulikuwa ni usiku wa kutosha, Imani ya kila mwanafunzi na uaminifu wa kila mwanafunzi ungepimwa wakati wa kukamatwa kwa Yesu, wote wangekimbia maana yake wangemkana Yesu kivitendo na kutokukubali kufa naye, Japo walimuahidi, Lakini katika namna ya kushangaza Petro ndiye ambaye aliharibu zaidi siku ile kuliko wanafunzi wote nan die aliyeombewa na Bwana, na alielezwa wazi kuwa yeye angamkana Yesu mara tatu, kwa sababu alijiamini mno kuliko wengine akidhani kuwa wengine ni wadhaifu kuliko yeye   

 Hata wajapokunguwazwa wote lakini sio mimi

Wakati Yesu akiahidi kuwa usiku ule kila mmoja atakungwazwa kwaajili yake kama tusomavyo katika andiko la Msingi Marko 14:27-31 “Yesu akawaambia, MTAKUNGUWAZWA ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Naye akazidi sana kusema, Ijaponipasa kufa nawe, hata hivyo sitakukana kamwe. Na wote wakasema vile vile.”

Petro yeye alijiamini kupita kawaida, na kutaka kumthibitishia Yesu kuwa yeye hatakunguwazwa, na akamhakikishia Yesu kuwa yuko tayari kufa naye n ahata kwenda gerezani pamoja naye Petro alimwambia Bwana Hata wajapokunguwazwa wote lakini sio mimi, Petro alikuwa na uhakika kuwa hawezi kukomsea Yesu hata siku Moja, wengine wanaweza kumkosea Yesu lakini sio mtu kama yeye, Petro alikuwa na ujasiri mkubwa sana, wote tunajua jnsi Petro alivyikuwa mwanafunzi muhimu katika wanafunzi wa Yesu, yeye anatajwa kuwa ni nguzo za kanisa 

-          Wagalatia 2:9 “tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;”

 

Nyakati za Kanisa la Kwanza Petro au Kefa alijulikana kuwa ni Nguzo, katika madarasa ya uanafunzi ya Yesu Kristo, Petro Yakobo na Yohana, walikuwa dara sa la juu zaidi kuliko wanafunzi wenguine wote, walishuhudia mambo makubwa sana, na walijua siri ambazo wanafunzi wengine hawakujua

 

-          Mathayo 17:3-9 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani; akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang'aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru. Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye. Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye. Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana. Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope. Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake. Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.”

 

Unaona Petro alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wachache waliokwenda pamoja na Yesu katika mlima mrefu faraghani na kuona maono mazito na walielezwa wasimwambie mtu awaye yote kwa hiyo unaweza kuona uimara wa Petro, unaweza kujua kuwa alimjua Yesu kwa viwango vikubwa na vya juu zaidi alikuwa shahidi wa Yesu Kristo mwenye ujuzi mkubwa na wa juu zaidi hata wa kuelezea Yesu ni nani, Yeye mwenyewe alikiri kuwa ni miongoni mwa watu waliouona utukufu wake

 

-          1Petro 1:16-18 “Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.”  

 

Petro alikuwa miongoni mwa wanafunzi wa yesu waliowahi kuisikia sauti ya Mungu baba ikisema huyu ndiye Mwanangu mpendwa ninayependezwa naye, na kama haitoshi miongoni mwa wanafunzi wa Yesu aliyeweza kujibu swala la Yesu kwa ufasaha zaidi ya wanafunzi wengine na kusifiwa kuwa alikuwa amefunuliwa na baba wa Mbinguni Petro alikuwa ni wa kwanza

 

-          Mathayo 16:13-17 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.”

 

Petro alikuwa ni Mwanafunzi wa kipekee, alimjua Yesu Vizuri na alikuwa tayari kumfuata alifuzu mitihani yote ya Bwana Yesu, alijaribu mambo mengi kuliko wengine ja unajua ya kuwa ni yeye ndiye mwanafunzi pekee aliyejaribu kutembea juu ya maji?

 

-          Mathayo 14:25-30 “Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.”

 

Petro alikuwa miongoni mwa wanafunzi wa Yesu ambao, walipata mafunzi mazui nay a kina nay a ndani zaidi hususani wakati Yesu anafufua wafu

 

-          Marko 5:37-43 “Wala hakumruhusu mtu afuatane naye, ila Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye Yakobo. Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu. Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu. Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu. Akawaonya sana, mtu asijue habari ile; akaamuru apewe chakula

 

Hata muda mchache kidogo kabla ya kukamatwa kwa Yesu, Petro, Yakobo na Yohana walichukuliwa hatua moja zaidi na Bwana kwaajili ya kuwataka waombe kwa kukesha pamoja naye

 

Marko 14:33-35 “Akamtwaa Petro na Yakobo na Yohana pamoja naye, akaanza kufadhaika sana na kuhangaika. Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe. Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke.”     

 

Unaweza kuona maswala kadhaa kuhusu Petro kwamba alikuwa ni mtu wa namna gani, na alikuwa na nafasi ya namna gani katika moyo wa Yesu, na sasa bwana anaposema wote watakunguzwazwa usiku ule kwaajili yake unaweza kupata picha ya mtu anayezungumzwa kwa kujiamini kuwa HATA WAJAPOKUNGUWAZWA WOTE LAKINI SIO MIMI, yaani Petro alikuwa ana uhakika ambao haukuwa na shaka ndani yake kuwa yeye anaweza kuwa tayari kwenda na Yesu gerezani, yeye anaweza kumtetea Yesu, yuko tayari hata kufa naye, na hata kama wanafunzi wengine wote watamkimbia Yesu na kumkana jambo kama hilo sio rahisi kwake Petro alizungumza kwa kujiamini sana, huku akiwa na ujasiri uliopitiliza, akijiona yeye ana kitu cha ziada na wengine ni wadhaifu, alijitumaini nafsi yake na akili zake, Watu wanaojifikiria kuwa wao ni wajanja na wenye akili na ujuzi kuliko wengine mara nyingi ndio ambao wakati mwingine hawafai kwa lolote  high self-esteem was also linked to a higher frequency of violent and aggressive behaviours , Watu wanaojiamini kupita kawaida wakati mwingine ndio hujiweka katika nafasi kubwa ya kukosea na kuharibu kabisa,  na wakati mwingine inaongoza katika uharibifu muwa wa mahusiano ya kila aina, kujiamini sio kitu kibaya kwani wakati mwingine kinaongoza katika aina Fulani ya mafanikio, lakini katika mazingira mengine kujiamini kupita kawaida kunatuletea udanganyifu wa moyo, unaweza kujikuta unajikweza kupita kawaida, au unaahidi kitu ambacho hauna uwezo nacho au uwezo wa kukitekeleza,  na Yesu alikuwa anamuelewa Petro alipojipambanua kuwa HATA WAJAPOKUNGUWAZWA WOTE LAKINI SIO MIMI Yesu alikuwa anamuona kuwa usiku ule hata kabla ya kuwika jogoo jamaa atamkana Yesu mara tatu

Luka 22:33-34.” Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni. Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui.”

Mambo muhimu ya kujifunza

Ni makossa makubwa sana kufikiri au kuamini kuwa njia yako ya kufikiri na kutenda iko juu sana kuliko wengine, au kufikiri kuwa wewe ndiye uko sahihi wakati wote, watu wengi wamefunga mlango wa kupokea mawazo yaw engine na kunufaika na ushauri wa watu wengine  kwa sababu wamefikiri kuwa wao ni bora kuliko wengine na wamedhani wengine ni dhaifu, kufikiri hivyo ni kuona maluwe luwe tu kama Petro maluluwe luwe haya yanaweza kukufikirisha kuwa wewe huwezi kukosea na hutakuja kukosea huku ni kujiamini kuliko pitiliza, Petro alikuwa akimthibitishia Yesu kuwa yeye atakuwa pamoja naye kwa gharama yoyote ile, hakuwa amejua kuwa Yesu ni Mungu na kuwa Mungu anamuona,

Wako watu wa namna kama ya Petro ambao wanajiamini kupita kawaida, wanafikiri kuwa wanamjua yesu kwa ukaribu kuliko yeyote, wanamjua Mungu kuliko wengine, wana mafundisho sahihi kuliko wengine , wana dhehebu zuri kuliko wengine, wana uzoefu na Mungu kuliko wengine, wana ni hadari, ni waombaji, ni watoaji, wako mstari wa mbele katika utumishi, wanaomba sana, wanafunza sana, wamefanikiwa sana na pengine hawana dhambi au hawawezi hata kuanguka, wao wamenyooka kuliko wengine, wao wana nidhamu kuliko wengine, wao waaakili kuliko wengine, Mtazamo wa aina hii hauwezi kukubalika na Yesu,  maandiko yanaonya wazi wazi kila ajidhaniae ya kuwa amesimama na aangalie asianguke

-          1Wakorintho 10:11-12 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.”

 

Onyo linatolewa kwa kila Mkrito na mafunzo yanaelekezwa kwetu kwamba wakati wote tusijifikiri kuwa sisi ni bora kuliko wengine, Waandishi wa habari nchini Marekani waliwahi kumuuliza Billy Gharamu kwamba ana maoni gani kuhusu anguko la Muhubiri mwenzake aitwaye Jimmy Swaggat Grahamu alijibu kama swaggart ameanguka mimi naweza kuanguka zaidi yake, Usifikiri wale wanao anguka kuwa hawampendi Mungu kama wewe, Mungu hapadezwi kabisa na kiburi, kiburi na majivuno na kujihesabia haki paee ni anguko tosha  ndio maana maandiko yanatuonya kuwahesabu wengine kuwa ni bora kuliko sisi

 

-          Wafilipi 2:3 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.”

 

Maandiko yanataka wakati wote tujicheki wenyewe kwanza kabla ya kuacha kuwacheki wengine

 

-          Luka 6:41-42 “Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii? Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako.”

 

Mungu atasimama hukumuni na kila mtu anayejifikiri kuwa ana haki inayotokana na juhudi zake, kiufupi maandiko yanaonyesha kukataliwa n ahata kukemewa kwa watu wanaojifikiri kuwa wana ubora Fulani kuliko wengine

 

-          Luka 18:9-14 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”

 

-          Isaya 65:5 “watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.”

 

Wako watu duniani ambao kwa vipimo vyao vya kibinadamu hufikiri kuwa wana haki kuliko wengine kwa sababu ya juhudi zao,  na hivyo wanashindwa kuona asili yao ya dhambi,  na kutokustahili kwao, hawajui kwamba bila msaada wa Mungu hatuwezi lolote, na kuwa wakati wote tunahitaji rehema za Mungu, neema na msaada wake, kwa sababu ya matendo yao ya nje na wema wa kinafiki wa kujionyesha na kukandamiza wengine wakiwashutumu kuwa ni wenye dhambi na wao ni watakatifu, ni dhaifu na waio ni wenye nguvu, hawana msimamo na wao ndio wanaostahili, ni dhana ya aina hii ndio ilitompoza Petro akidhani ya kuwa yeye ni mwenye nguvu na sio dhaifu kama wanafunzi wengine hili ndio tatizo kuwa la watu wengi wa Mungu, kudhani kuwa wao ndio wao.

 

Nabii Eliya aliwahi kujiamini na kujifikiri kua katika Israel Nzima watu wote wameabudu sanamu na kusujudia mabaali alifikiri amebaki yeye peke yake na kwa kiburi chake alijieleza mbele za Mungu kuwa amesalia yeye peke yake, ona  

 

1Wafalme 19:9-10. “Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya? Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.”

 

Warumi 11:2-4 “Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu, Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu. Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.”

 

Mungu alitaka kushughulika na kiburi cha Eliya aliwashitaki watu wa Mungu kana kwamba wote wameasi na wote hakuna aliyesalia ila yeye peke yake, watu wa Mungu hawashitakiwi, Mungu alimjibu kuwa anao wengine elfu saba wala hawajapiga goti lao kwa baaali, unapokuwa na kiburi unajiona uko katika ulimwengu wa pake yako, unauona umashuhuri wako wewe mwenyewe lakini Mungu anaiona mioyo, tuache kujiamini kupitiliza, na badala yake wakati wote tuombe Mungu atupe unyenyekevu, ujumbe mkubwa katika pasaka hii ni kutembea kwa unyenyekevu, Petro alijiamini aliona kuwa yeye hawezi kukosea Lakini Yesu alimwambia hata kabla ya kuwika jogoo utanikana mara tatu!     

Ni Petro tena yule yule aliyehitaji kufundishwa tena kuhusu kuwahubiri mataifa, kitendo chake cha kuwa myahudi alifikiri hana kibali cha kuwahubiri mataifa, akijiamini tena kupita kawaida kwamba Wayahudi ni safi na mataifa ni najisi, na katika moyo wake aliwaita mataifa najisi Ni Mungu tena alimkemea Petro kuwa kilichotakaswa na Mungu usikiite wewe najisi

 

Matendo 11:8-9. “Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu. Sauti ikanijibu mara ya pili kutoka mbinguni, Alivyovitakasa Mungu, usivinene wewe najisi.”

 

Wakati wote lazima tukumbuke kuwa chochote ambacho Mungu ametujaalia ni kwa neema yake na sio vinginevyo, juhudi zetu na jitihada binafsi hazina kitu cha ziada cha kutusaidia, tutembee kwa unyenyekevu mbele za Mungu na kuacha kiburi na majivuno na kila tunapozungumza tuweke akiba ya maneno kumbuka Mungu huwapinga wajikwezao bali huwapa wanyenyekevu neema alisema Petro

 

1Petro 5:5Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”   

 

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.”

 

“Hata wajapokunguwaa wote lakini sio Mimi alisema petro kwa kujiamini kumbe atamkana Yesu mara tatu tena kwa kuapia”

 

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima