Ijumaa, 27 Mei 2016

Mwaka wa Bwana Uliokubaliwa!


Luka 4:18-22
18. Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19. Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. 20. Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21. Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu. 22. Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?

Moja ya maswala ya msingi namambo muhimu tunayopaswa kuyafahamu ni pamoja na kufahamu maneno haya ya neema kubwa yaliyopata kutamkwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni Maneno ambayo hata wale waliyoyasikia waliyastaajabia maneno hayo ni “KUTANGAZA MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA”

Ni muhimu kwetu kufahamu ni nini maana ya Mwaka wa Bwana uliokubaliwa? Katika kiingereza maneno hayo husomeka hivi  To proclaim the Year of Lords Favour” Neno Favour katika Biblia ya Kiyunani yaani Greek linasomeka “Dektos”  ambalo maana yake ni Kukubalika au “Neema” 

Kwa kawaida Mungu aliwaamuru wana wa Israel kuadhimisha sikukuu iliyoitwa Mwaka wa Bwana wa Neema kila Baada ya miaka 49 mwaka wa 50 Uliitwa mwaka wa Neema au mwaka wa Bwana uliokubaliwa mwaka huu ulikuwa maalumu na ulikuwa na mafundisho makuu manne yafuatayo
1.      Ulikuwa ni mwaka wa kupuliza tarumbeta yaani mwaka wa kuukaribia mlima au uwepo wa Mungu 



Kutoka 19:10-13 Biblia inasema hivi;-

10. BWANA akamwambia Musa, Enenda kwa watu hawa, ukawatakase leo na kesho, wakazifue nguo zao, 11. wawe tayari kwa siku ya tatu; maana siku ya tatu BWANA atashuka katika mlima wa Sinai machoni pa watu hawa wote. 12. Nawe utawawekea mipaka watu hawa pande zote, ukisema, Jihadharini, msipande mlima huu, wala msiuguse, hata mapambizo yake; kila mtu atakayeugusa mlima huu, bila shaka atauawa. 13. Mkono wa mtu awaye yote usimguse mtu huyo, ila hakika yake atapigwa kwa mawe, au kupigwa kwa mkuki; kwamba ni mnyama au kwamba ni mwanadamu, hataishi. Hapo panda itakapotoa sauti kwa kufuliza ndipo watakapoukaribia mlima.

Ilikuwa ni vigumu na ni hukumu ya kifo kuukaribia uwepo wa Mungu, lakini ilipopigwa tarumbeta au panda ndipo watu waliporuhusiwa kuukaribia uwepo wa Bwana, hivyo mwaka wa Bwana unazungumzia kukaribishwa uweponi mwake

2.       Ulikuwa ni mwaka wa KISABATO yaani mwaka wa MAPUMZIKO Walawi 25:8-17 Biblia inasema hivi: - 

8. Nawe utajihesabia Sabato saba za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za Sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda. 9. Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote. 10. Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake.11. Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa. 12. Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani. 13. Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake. 14. Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe; 15. kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe. 16. Kama hesabu ya miaka ilivyo ni nyingi ndivyo utakavyoongeza bei yake, na kama hesabu ya miaka ilivyo ni chache ndivyo utakavyopunguza bei yake; kwani yeye akuuzia mavuno kama hesabu yake ilivyo. 17. Wala msidanganyane; lakini utamcha Mungu wako; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Mungu alikuwa anataka watu wake wastarehe wapumzike wafurahi Jubilei, kwa hiyo ulikuwa ni wakati wa Kustarehe na kuburudika na kupumzika na kurudishiwa milki ya nkila ulichopoteza

3.       Ulikuwa ni Mwaka wa Kuachia Ardhi (25-38)

25. Kwamba nduguyo amekuwa maskini, na kuuza sehemu ya milki yake, ndipo jamaa yake aliye karibu naye atakuja, naye ataikomboa ile aliyoiuza nduguye. 26. Na kama mtu hana atakayeikomboa, naye mwenyewe amepata mali na kujiona kuwa anayo ya kutosha kuikomboa; 27. ndipo na aihesabu hiyo miaka ya kuuzwa kwake, na kilichozidi kumrudishia huyo mtu aliyeinunua; naye atairejea milki yake. 28. Lakini asipoweza kujipatia mwenyewe, ndipo hiyo iliyouzwa itakaa mkononi mwake huyo aliyeinunua, hata mwaka wa yubile; na katika yubile itatoka, naye atairejea milki yake. 29. Tena kwamba mtu anauza nyumba ya kukaa, iliyo ndani ya mji wenye kuta, ndipo ana ruhusa kuikomboa katika mwaka mmoja mzima baada ya kuiuza; atakuwa na amri ya kuikomboa muda wa mwaka mzima. 30. Na kama haikukombolewa katika muda wa mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyo ndani ya mji wenye kuta itathibitishwa milele kuwa ya huyo aliyeinunua, katika vizazi vyake; nayo haitatoka katika yubile. 31.Lakini nyumba za vijiji, ambavyo havikuzingirwa na kuta, zitahesabiwa pamoja na mashamba ya nchi; nazo zina ruhusa ya kukombolewa, nazo zitatoka katika yubile. 32. Pamoja na hayo, miji ya Walawi, nyumba za miji ya milki yao, Walawi wana ruhusa ya kuzikomboa majira yo yote. 33. Tena kama mtu mmoja wa hao Walawi akikomboa, ndipo nyumba iliyouzwa, na mji wa milki yake, itatoka katika yubile; maana, hizo nyumba za miji ya Walawi ni milki yao kati ya wana wa Israeli. 34. Lakini konde la malisho ya miji yao lisiuzwe kwa kuwa ni milki yao ya daima. 35. Na ikiwa ndugu yako amekuwa maskini, na mkono wake umelegea kwako, ndipo utamsaidia, atakaa nawe kama mgeni, na msafiri. 36. Usitake riba kwake wala faida, bali mche Mungu wako, ili ndugu yako akae nawe. 37. Usimpe fedha yako upate riba, wala usimpe vyakula vyako kwa kujitakia faida. 38. Mimi ndimi BWANA, Mungu wako, niliyewatoa katika nchi ya Misri ili niwape nchi ya Kanaani, nipate kuwa Mungu wenu.”

4.       Ulikuwa ni Mwaka wa kuwaachia watumwa uhuru na kila mtu kurejea nyumbani kwao (39-55)

39. Tena kwamba nduguyo amekuwa maskini pamoja nawe, akajiuza kwako; usimtumikishe mfano wa mtumwa; 40. kwako wewe atakuwa mfano wa mtumishi aliyeajiriwa, au mfano wa msafiri; naye atatumika kwako hata mwaka wa yubile;   41. ndipo atakapotoka kwako aende zake, yeye na wanawe pamoja naye, naye atairejea jamaa yake mwenyewe, tena atairejea milki ya baba zake. 42. Kwa kuwa hao ni watumishi wangu, niliowaleta watoke nchi ya Misri; wasiuzwe mfano wa watumwa. 43. Usitawale juu yake kwa nguvu; ila umche Mungu wako. 44. Tena katika habari za watumwa wako na wajakazi wako, utakaokuwa nao; mataifa walio kando-kando yenu, katika hao mtanunua watumwa na wajakazi. 45. Tena katika wana wa wageni wakaao kati yenu mtajinunulia, na katika jamaa zao walio pamoja nanyi, waliowazaa katika nchi yenu; wao watakuwa milki yenu. 46. Nanyi mtawafanya kuwa urithi kwa watoto wenu baada yenu, wawe milki yao; siku zote mtatwaa watumwa wenu katika hao; lakini msitawale kwa nguvu juu ya ndugu zenu, hao wana wa Israeli, wenyewe kwa wenyewe. 47. Tena kama mgeni au mtu akaaye nawe akitajirika, na nduguyo amekuwa maskini karibu naye, akajiuza kwa huyo mgeni, au kwa huyo akaaye kwako, au kwa ukoo wa jamaa ya huyo mgeni; 48. baada ya kuuzwa aweza kukombolewa; mtu mmoja miongoni mwa ndugu zake ana ruhusa kumkomboa;   49. au mjomba wake, au mwana wa mjomba wake, ana ruhusa ya kumkomboa, au mtu awaye yote aliye karibu naye wa jamaa yake, ana ruhusa ya kumkomboa; au kwamba yeye mwenyewe amepata mali, ana ruhusa ya kujikomboa mwenyewe.    50. Naye atafanya hesabu na huyo aliyemnunua, tangu mwaka huo aliojiuza hata mwaka wa yubile; na ile bei ya kuuzwa kwake itakuwa kama hesabu ya hiyo miaka ilivyo; atakuwa pamoja naye kama majira ya mtumishi aliyeajiriwa yalivyo. 51. Kwamba ikali imesalia miaka mingi, kama hesabu yake ilivyo ndivyo atakavyolipa bei ya ukombozi wake, katika hiyo fedha ambayo alinunuliwa kwayo. 52. Tena kwamba imesalia miaka michache tu hata mwaka wa yubile, ndipo atafanya hesabu naye, kama hesabu ya miaka yake ilivyo, ndivyo atakavyolipa tena bei ya ukombozi wake. 53. Kama mtumishi aliyeajiriwa mwaka hata mwaka, ndivyo atakavyokuwa pamoja naye; asitawale juu yake kwa nguvu mbele ya macho yako. 54. Tena kwamba hakukombolewa kwa njia hizi mojawapo, ndipo atatoka katika mwaka wa yubile, yeye, na watoto wake pamoja naye. 55. Kwa kuwa wana wa Israeli ni watumishi; ni watumishi wangu niliowaleta watoke katika nchi ya Misri; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Kimsingi katika agano jipya pia Yesu alipoutangaza alitangaza wakati wa neema ambapo kila alichokisema Yesu, kilikuwa ni lazima kifanyike , watu wengi katika Israel walijua kuwa mwaka huo kinabii ulikuwa unahusu ujio wa Masihi na kuwa mwenye uwezo na mamlaka ya kuutangaza mwaka huo wa Neema alikuwa ni Masihi peke yake ulikuwa ni mwaka uliokuwa ukisubiriwa ilistaajabisha sana Yesu laliposoma andiko na kutoa hutuba ya maneno sita tu “LEO MAANDIKO HAYA YAMETIMIA MASIKIONI MWENU”

Ni wazi kuwa Masihi Yesu alikuwa ametangaza maneno ya neema kubwa sana  kwamba kuanzia wakati ule hata sasa tunaishi ndani ya kipindi cha neema na ni mwaka wa Bwana ni mwaka ya Jubilei Kristo alitangza wazi kuwa ni mwaka wa 

Ø  Kukomesha kila aina ya uonevu
Ø  Kuweka huru waliosetwa na kukandamizwa na shetani
Ø  Kutangaza kuwa kila mtu anaweza kuukaribia uwepo wa Mungu bila kuuawa
Ø  Amekuja kupumzisha watu wenye mizigo na wenye kuelemewa na matatizo mbalimbali
Ø  Amekuja kuweka huru wafungwa wote wa vifungo mbalimbali

Shetani anafahamu wazi kuwa Tarumbeta imekwisha kupulizwa na kuwa anapaswa kumuachia huru kila mmoja name nakutangazia msomaji wangu Bwana akuweke huru na kukutoa katika vifungo mbalimbali na kila aina ya uonevu wa Ibilisi

Huu ni mwaka wa Bwana uliokubalika, kila kifungu na kikuachie, Roho amanitia mafuta nikutangazie uhuru uwe Huru sasa katika Jina la Yesu Kristo, Ufunguliwe, kutoka katika vifungo vya nguvu za giza, uonevu wa Ibilisi, Biashara zisitawi, upandishwe cheo, waliokufunga wadhoofike na kukuachia huru, kila kifungo nakiharibu na kukivinja katika jina la yesu Kristo aliye hai Achiaaaaaaaaa haraka  Achia wasomaji wangu huna mamlaka ya kuwatesa nina waweka huru kwa kupakwa mafuta navunja nira zote Katika Jina la yesu Kristo, Pepo majini  na mashetani huna nafasi ya kumtesa msomaji wangu mwachie sasa hivi katika jina la Yesu Uko huru sema amen kwa imani 

Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: