Jumatano, 29 Agosti 2018

Habari za Mapito ya Zamani!


Yeremia 6:16Bwana asema hivi, Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katika njia hiyo.”



Kama Jamii yoyote itapoteza Historia, maana yake imepoteza Muelekeo” Rev Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye hekima

Utangulizi. 

Ni muhimu kufahamu kuwa Maisha yetu hayawezi kuwa na furaha ya kweli kama mara kwa mara hatutajifunza kutokana na Historia, Historia ni mwalimu mkubwa sana wa kutusaidia kujua tunatoka wapi na tuko wapi na tunakwenda wapi, “Kama jamii yoyote itapoteza Historia, maana yake itapoteza muelekeo” Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima, Kwa msingi huo kuna umuhimu wa kujifunza kutokana na Historia, semi kadhaa za Kihistoria zinatusaidia kujua umuhimu wake
·         Historia sio mzigo katika kumbukumbu zetu bali ni Mwangaza wa Nafsi zetu lord Acton- History is not a burden on the memory but an illumination of the soul – Lord Action.
·         Mtu asiyejali Historia ni sawa na Kiziwi ni sawa na kipofu – Aldof Hittler  The man who has no sense of history, is like a man who has no ears or eyes. Adolf Hitler
·         Baada ya kufanya makosa au kuteseka, na kupoteza muelekeo Mtu mwenye akili huangalia nyayo zake – Napoleon - After making a mistake or suffering a misfortune, the man of genius always gets back on his feet. Napoleon
·         Tunasoma kutokakatika Historia kile ambacho Hatujakisoma katika Historia – Desmond Tutu - We learn from history that we don’t learn from history! Desmond Tutu
·         Raia wenzangu, Hatuwezi kuiepuka Historia Abrahamu Lincoln - Fellow citizens, we cannot escape history. Abraham Lincoln

Kama tunavyoweza kuona hapo juu, umuhimu wa Historia ni wazi kuwa neno la Mungu pia limeandikwa kwa makusudi ya kutukumbusha na kutufundisha kutokana na Historia Biblia inasema hivi :-  

1Wakoritho 10:1-11Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; wote wakala chakula kile kile cha roho; wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu. Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.” Kumbe kila mmoja anaweza kujifunza kitu kutokana na Historia.

Katika kifungu cha maandiko Yeremia 6:16 Mungu anatoa wito kwa wana wa Israel, yaani wayahudi kuuliza kwa habari za mapito ya zamani, yaani katika wakati huu kulikuwa na ukengeufu mkubwa na mmomonyoko mkubwa wa uadilifum watu walikuwa wakifuata njia zao wenyewe na hivyo walipoteza raha na amani ya kweli, Taifa, Kanisa, Jamii na kila mmoja anapaswa kuangalia njia zake na kujifunza kutokana na Historian a kuangalia njia za Zamani na kujikagua kama tuko sahihi au lah nini kimepoteza furaha tuliyokuwa nayo, ka sababu gani tupo hapo tulipo? Kwa nini hilo au lile linatokea? Nabii Yeremia alitumwa na Mungu kuwakubusha wayahudi kuifuata njia ile ili waweze kufanikiwa  

Yeremia 7:22-23Maana sikusema na baba zenu, wala sikuwaamuru kwa habari za sadaka za kuteketezwa na dhabihu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri; lakini naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru mpate kufanikiwa.”       

Unaweza kuona iko njia ya mafanikio ambayo Mungu aliwaonyesha Israel Tangu zamani lakini wao walikuwa wamekaidi kuifuata na hivyo maisha yao yalijaa taabu na kukosa raha na amani,  Hakuna namna yoyote ambayo tunaweza kuwa na amani ya kweli endapo tutakuwa nje ya njia ya kweli au kama tumeiacha njia ya Mungu, Kama Mungu anatupenda kwa dhati anachokifanya ni kuwatuma watumishi wake manabii wake kutukumbusha kurudi katika njia, Mungu anataka watu wake wajifunze kutokana na Historia Israel walipofanya vema na kuzishika nzjia za Mungu Mungu aliwarudia na kuwa pamoja nao, lakini walipofanya mabaya Mungu aliwaacha na walipata tabu sana
Sisemi kwamba kila taabu inasababishwa na kuacha njia ya Mungu hapana lakini kuna raha kupitia taabu huku ukiwa na Mungu, na kuna utungu mkubwa kupitia taabu huku ukiwa umemuacha Mungu, Katika nyakati hizi tulizo nazo pia Mungu ametupa njia ya kuifuata 

Yohana 14:6Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” 

Linapotokea jambo Gumu la kuumiza na kukatisha tamaa ni muhimu kuangalia Habari ya mapito ya zamani, baba zetu na watakatifu waliotutangulia walifanya nini? Wao walimtegemea Mungu hawakuzitegemea akili zao wenyewe, walimuweka Mungu mbele, walimfamya Mungu kuwa kinga yao, walimfanya yeye kuwa mtetezi wao, walimfanya kuwa ngao yao, walimfanya kuwa tumaini lao, walimgeukia yeye na kwa sababu hiyo walipata raha nafsini mwao, Historia inaonyesha kuwa Yesu hajawahi kumuangusha mtu aliyemtegemea  

Mathayo 11:28-29Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

Yesu amewahakikishia raha wale wote wanaoshikamana naye, Hakuna namna unaweza kujikwamua katika jambo lolote bila ya Yesu, Taifa jamii na kanisa kama tunataka kufanikiwa basi tunapaswa kuangalia njia zetu kama tumekengeuka tukajifunze habari za mapito ya zamani na kuangalia kwamba tunaenenda sawasawa au hapana? Tumfanye Yesu kuwa tegemeo letu, ngao yetu, kimbilio letu, mwamba wetu, tumaini letu na tukimtegemea yeye na kutii maelekezo yake tutapata raha nafisni mwetu, 
Tenzi namba 16 Kumtegemea Mwokozi kwangu tamu kabisa…………..

Na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Hakuna maoni: