Jumatatu, 29 Aprili 2019

Wamisri wakatuonea, wakatutesa, !


Kumbukumbu la torati 26:6-9 “Wamisri wakatuonea, wakatutesa, wakatutumikisha utumwa mzito.  Tukamlilia Bwana, Mungu wa baba zetu; Bwana akasikia sauti yetu, akaona na taabu yetu, na kazi yetu, na kuonewa kwetu.  Bwana akatutoa kutoka Misri kwa mkono wa nguvu, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa utisho mwingi, na kwa ishara, na kwa maajabu; naye ametuingiza mahali hapa, na kutupa nchi hii, nchi ijaayo maziwa na asali.”

 Sinagogi la Kiyahudi huko San Diego, lililoshambuliwa kwa Risasi 28/04/2019

Utangulizi:
Jana tarehe 28 April 2019  sawa na mwezi Nisan 23 5779 kwa kalenda ya kiyahudi, nilipata habari ya kuuawa kwa Myahudi mmoja kutokana na shambulio la risasi lililofanyika huko San Diego katika mojawapo ya sinagogi la kiyahudi, na wengine watatu kujeruhiwa vibaya, nilikuwa bado sijasahau tukio la kuuawa kwa wakristo wakati wa Pasaka Nchini Sri-lanka nikafikiri na kuwaza kwamba bado dunia ya leo iliyoendelea kuna watu bado wanafikiri wanaweza kuwepo duniani peke yao bila kuchanganyika na watu wanaotofautiana nao kimawazo kifikira kiitikadi na kiimani? Dunia inapaswa kutafakari kwa kina kuhusu ukomavu na uwezo wa kuchukuliana katika jamii na kupendana bila kujali tofauti zetu,
Biblia inasema katika 1Yohana 4:8Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.” Hii ni wazi kuwa bado dunia haijamjua Mungu, na kuwa jamii inapaswa kukumbuka na kuhimiza na kufundisha kuhusu upendo, ni muhimu kufanya kilalinalowezekana kuing’oa chuki miongoni mwa wakazi wa dunia, na kukumbuka kuwa Yesu hakuwa mjinga alipokuwa akifundisha Upendo, alikuwa anajua wazi kuwa dunia itakuja kufikia na kuwa na matukio haya tunayoyashuhudia leo katika jamii iliyoendelea.
Katika kifungu cha maandiko ya msingi, Musa alikuwa anawakumbusha wana wa Israel sheria za Mungu na hususani kwa kizazi kipya ambao wengi waoa walizaliwa Jangwani au na wale waliotoka Misri wakiwa vijana na waliokuwa wadogo, Musa alikuwa akizungmzia kumtolea Mungu sadaka za shukurani watakazomtolea Mungu watakapokuwa katika nchi ya amani nchi iliyojaa maziwa na asali nchi ya Israel aliwalekeza kwamba watakapotoa wamkumbushe Mungu kuwa walionewa huko Misri, lakini walipomlilia Mungu akawaokoa na kuwaleta katika inchi hii iliyojaa maziwa na asali
Katika kifungu hiki Kumbukumbu la Torati 26:6 ““Wamisri wakatuonea, wakatutesa, wakatutumikisha utumwa mzito. .”
Biblia ya kiingereza  NIV inasomeka hivi Deuteronomy 26:6But the Egyptians mistreated us and made us suffer, subjecting us to harsh labor.”
Biblia ya Kiyahudi iitwayo (The Israel Bible) inasomeka hivi Deuteronomy 26:6The Egyptians DEALT HARSHLY WITH US and oppressed us; they imposed heavy labor upon us.”
Musa aliwakumbusha Jambo hili la msingi walikumbuke watakapokuwa wakiabudu, kwa sadaka ya shukurani, wamkumbushe Mungu kuwa walitendwa vibaya na wamisri neno kuonewa, kuteswa na kutendwa vibaya katika lugha ya Kiebrania linatumika neno “VAYAREIU”  likimaanisha kuwa lakini rafiki zetu walitugeuka,walitutenda mabaya, wakatuonea, wakatutesa, wakatudhulumu kisha wakatugeuza  kuwa watumwa kwa utumwa mbaya na mzito” Hii ilimaanisha kuwa Israel hawakushuka Misri wakiwa watumwa walikuwa rafiki wa wamisri, walikuwa wapendwa, walikuwa jamaa na ndugu wa waisrael, lakini hatimaye ukafika wakati wakawageuka, wakavunja urafiki, wakaanza kuwabagua na kutengeneza sheria za kuwabana, na kuwaonea na kuwatesa na kuwakandamiza na hatimaye kuwafanya watumwa wao, Ndipo ulipofika wakati wayahudi wakamlilia Mungu awatoe katika utumwa ule mzito na Mungu akawaokoa akawapeleka katika nchi ya ahadi, ambako huko npekee ndipo mahali ambapo Wayahudi watakuwa salama na wakamfurahia Mungu.
Leo hii sio Misri tu ambao wamewakaribisha Wayahudi kisha wakawaonea baadaye, ziko nchi nyingi tu ambazo zimewapokea wayahudi wakiwa kama marafiki, kama ilivyotokea Ujerumani na Uganda, lakini baadaye katika namna isiyoweza kueleweka watu hao waliwageuka nakuwaona wayahudi kama adui na watu wasiofaa, ili mtahudi aweze kuwa salama ni lazima popote pale walipo warudi katika nchi yao ya asili nchi yao ya ahadi ili wamuabudu Mungu pasipo hofu na watoe sadaka ya shukurani na mateso yao yote yatageuka kuwa historia
Wako watu wengi sana leo wanateseka lakini chanzo cha mateso yao hakikuwa chuki na majuto na dhuluma ambazo wanaziona sasa, inawezekana wewe ni House girl ulichukuliwa kama dada wa kazi kwa nia nzuri, ukaenda mjini kama rafiki na ndugu, na ukapokelewa vema huko ulikokwenda mama na baba wa nyuma uliyofikia walikataa kuitwa anko walisema utuite mama au baba, lakini baada ya siku kadhaa hali ilibadilika umeanza kuitwa hili, limbwa, paka , nyau. Fala na kadhalika.

Inawezekana ulioa au kuolewa kwa nia nzuri kabisa, wakati unachumbiwa ulikuwa ni rafiki, hukuwa mtumwa mliitana majina mazuri, sweetie, asali wangu, maua, dear, dally na kadhalika lakini hapa unaposoma ujumbe huu mambo yamegeuka wewe sasa ni jibwa, fala, lione, liangalie, sijui nililioa la nini, mlango wa nane, balaa nuksi, mwiba na kadhalika.
Inawezekana wakati uaajiliwa ulikaribishwa kwa furaha, bosi aliwataka wenyeji wakupe saada mkubwa utakaouhitaji, ulidekezwa, ulifanywa kama moja ya wamiliki wa kampuni, ulikuwa ni wakati wa furaha umepata kazi mpya, lakini baada ya sikukadhaa, Mambo yamebadilika, unaonekana kama mzigo, unateseka, unapelekeshwa unaonekana hifai tena.
Kila mahali walikokwenda Wayahudi walikaribishwa walipokelewa kwa ukarimu lakini leo watu wanawalipua, wanawapiga risasi, kama majambazi au watu wasiofaa, huko san diego wayahudi wameuawa katika sabato ya kwanza ya Pasaka walipokuwa katika ibada na mama mmoja mwenye miaka 60 alifariki na wengine watatu kujeruhiwa vibaya, mmoja akiwa kiongozi wa kidini Rabbi na mkuu wa sinagogi husika kinawafanya wengine wawe na chuki dhidi ya wengine, kwa nini wakristo wameuawa Srilanka na kwa nini waqyahudi wameshambuliwa nani atawasemea
Hujawahi kuona unakaribishwa mahali vizuri, unapeewa na ofisi, unasifiwa kila mahali unahesabika kama mtu mwema kisha baada ya muda wewe ndio unaonekana kama mwiba wa kila mmoja pale ulipo?
Hali hii ndio inayowatokea Israel Duniani kote, ndio inayoatokea Wakristo, watu wanaona kuwa ni haki kuvaa mabomu na kuwalipua
Iko siri moja kubwa na ya kipekee, ni kukaa katika ahadi za Mungu tu, Ili Israel iweze kuwa salama hawana budi kuungana na kukaa Israel pekee ili wajilinde wakae katika nchi ya ahadi waliyoahidiwa baba zao Ibrahimu Isaka na Yakobo ndio wanaweza kujithibitishia usalama wao.
Wako watu wengi leoa hawako salama kwa sababu walifanya urafiki na shetani, walipokelewa na shetani , ibilisi kwa furaha sana wakiwa kama marafiki, Lakini kumbuka kuwa shetani hana urafiki na mtu awaye yote lazima atakugeuka tu atakutesa atakugeuza kuwa mtumwa na atakudhulumu, shetani anataka ufanye mambo kwa faida yake na maslahi yake hakuna mafanikio ya kweli kwa shetani, ili uwe salama huna budi kurudi kwa Yesu kristo na kujificha kwake, yeye ndio nchi halisi ya ahadi na kwake kuna usalama, Kwa ibilisi haijalishi kuwa wewe ni mwenye haki au la kwake nifuraha kubwa ukiangamia yeye na watu wake hawatajali haki yako, wakati umefika wa wewe kukaa katika uwepo wa Mungu kwa usalama wako, ili amani ipatikane katika ndoa yako hakikisheni mnamkaribisha Mungu na kujifunza upendo kama yeye alivyoagiza.
Isaya 5:1 Mwenye haki hupotea, wala hakuna atiaye hayo moyoni; na watu watauwa huondolewa, wala hakuna afikiriye ya kuwa mwenye haki ameondolewa asipatikane na mabaya
Hakuna wanaojali kile kinachowapata wayahudi leo. Lakini Palestina ikiguswa tu dunia itapiga kelele hata kama wakati mwingine wao ndio wachokozi na ndio wanaoanzisha kurusha maroketi, Israel ikijibu kama sehemu na wajibu wa kujihami na kujilinda, Israel ikijilipizia kisasi kwa adui zake dunia inapiga kelele je wadhani Wayahudi sio watu, nani atawapigia kelele na kuielimsha jamii duniani kuwa nao wanastahili kutetewa na kuangaliwa kwa maslahi yao duniani, Mimi sisemi kwa sababu nina asili ya Kiebrania tu hapana bali nataka haki itetendeke duniani ifikie hatua tujifunze pendo lake Yesu na kuielimisha katika jamii yetu, kila mmoja anapaswa kujua kuwa kama tunampenda Mungu tutathamini uhai wa watu wake kuliko imani zetu, Dunia pia inapaswa kuelewa kuwa ili Israel iweze kuwa salama  nilazima waelekee katika nchi ya ahadi na kukaa katika taifa lao wenyewe, ili sisi nasi tuweze kuwa salama turudi katika uwepo wa Mungu. Tutafanikiwa. Israel walimlilia Mungu, akawasikia akaziona taabu zao na kuonewa kwao aakawaokoa kwa mkono wa nguvu ulionyooshwa na wakajiliwa na kipindi cha neema  I stand with Israel.”
Rev. Innocent Kamote.
Mkuu wa wajenzi mwenye hekima

Hakuna maoni: