Ijumaa, 25 Desemba 2020

Mfalme wa Amani!


 Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“      


Utangulizi:

Leo ni sikukuu ya Christmas wakristo kote nchini wanaungana na waktristo wote duniani katika kuadhimisha siku hii maalumu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Masihi, na mwokozi wa ulimwengu, Yesu Kristo kulikotokea huko Bethelehemu Israel zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Katika siku hii muhimu ni muhimu kwetu tukajikumbusha mambo kadhaa kumuhusu Yesu Kristo.

Andiko letu la Msingi  Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“

Kimsingi yalikuwa ni maneno ya nabii Isaya aliyetabiri kuzaliwa kwa mwokozi wa ulimwengu miaka  zaidi ya 700 kabla ya kuzaliwa kwa  Yesu, Isaya anamuona masihi kama kiongozi mkubwa sana na mwenye uwezo mkubwa wa kutatua matatizo na changamoto mbalimbali walizonazo wanadamu, Nyakati za Biblia wafalme ndio ambao walikuwa wanatakiwa kutatua changamoto zozote zilizowakumba watu wao na walipaswa kuwatatulia matatizo yao na kutioa ufumbuzi ona mfano

2Wafalme 6:24-30 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho. Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake. Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.

unaweza kuona kwa hiyo kuwa mfalme halikuwa jambo rahisi, ilikuwa ni lazima uwe na uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu, hata leo viongozi wakubwa wanapotembelea maeneo mbali mbali huzomewa risala na kuelezwa changamoto kubwa mbalimbali zinazowakabili wananchi na wanatakiwa kuzitatua, hapo moja ya wafalme alishindwa kutatua changamoto na kuamua kufunga na kuomba kwa kuvaa magunia maana yake tatizo lilikuwa kubwa sana

Mungu alizungumza na manabii kuwa atakuja kiongozi mkubwa sana atakayetatua changamoto mbali mbali za watu wake sio katika Israel tu bali dunia nzima huyu ndiye masihi, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo tunapaswa kukumbuka kuwa Mungu ametupa kiongozi mwenye uwezo wa kutatua changamoto za aina mbalimbali ulimwenguni na kwa wanadamu wote na huyu si mwingine ni Yesu Kristo.

Isaya anamuelezea kiongozi huyu kuwa ni mwenye uwezo na mamlaka kubwa  na kuwa atatua changamoto nyingi zinazowakabili wanadamu na moja ya changamoto kubwa inayowakabili  wanadamu ni kukosekana kwa amani na utulivu mioyoni mwao na ndio maana Yesu anaitwa Mfalme wa Amani, kwanini mfalme wa amani

Ni muhimu kufahamu kuwa tunapozungumzia amani hii inayozingumziwa katika maandiko;-

Tunazungumziia ustawi, utulivu starehe amani na mafanikio makubwa ya mwanadamu ambayo asili yake ni Mungu, Amani hii ilikuwepo katika bustani ya Eden kabla ya anguko la mwanadamu, lakini baada ya anguko la mwanadamu amani hii ilitoweka Neno linalotumiska kuielezea amani hii katika lugha ya kiebrania ni SHALOM, neno shalom maana yake ni amani na ustawi na mafanikio ya kiunghu katika Nyanja zote, Waaarabu wanatumia neno SALAM,  kwa kiaramu linatumika neno SALEMI, ni maneno yanayofanana sana katika lugha ya kiebrania, kiarabu na Kiswahili, kwa Kiswahili tunalo neno SALAMA  ni hali ya amani, ni hali ya kuwa mbakli na masumbufu, ni hali ya kuwa na utulivu, Daudi alipigana sana vita katika maisha yake yote mpaka Mungu akamuita mtu wa Damu, Lakini mwanaye Suleimani hakukuwa na vita wakati wake, SULEMANI, SOLOMON maana yake ni utulivu na ustawi,  Yerusalem maana yake ni mji wa amani, Dar es Salaam maana yake ni bandari ya amani, jina la mji wa mzizima Dare s Salaam lilitolewa na sultan Baraghash aliyekuwa anatawala Zanzibar na pwani na alitoa jina hilo kwa mji wa mzuizima kwa sababu aliamini badari hii ni mahali salama mno na patulivu

Isaya anazungumzia kuwa masihi anazaliwa duniani kwa kusudi na malengo ya kuleta utulivu kwa wanadamu, utulivu huu ni ustawi wa mwanadamu katika Nyanja zote  na ndio maana siku Yesu alipozaliwa malaika waliimba wimbo huu  kuonyesha kuwa kiongozi mkubwa mwokozi wa ulimwengu atakayetatua matatizo na kuleta majibu na ufumbuzi wote wa mwanadamu amezaliwa na atatoa amani kwa watu wote atakaowakubali

Luka 2:8-18 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;  maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini.  Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.”

Kila mtu anayemwamini Yesu anapewa amani hii moyoni mwake ni amani ambayo hata upatwe na changamoto ya aina gani wewe unakuwa na imani kuwa nitatoka nitatoboa kwa sababu ninaye mfalme ambaye ana uwezo wa ajabu mno anayetoa amani tofauti na jinsi ulimwengu utoavyo  amani anayotupa Kristo ni amani ya pekee nay a tofauti sana ona Yesu anatuachia mani hii Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga. “              

Hatupaswi kufadhaika wala kuogopa kwa sababu Yesu ametuachia mani, na yeye ndiye mfalme wa amani, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaruhusu amani yake itawale katika mioyo yetu na kila mahali hatupaswi kufadhaika kwa jambo lolote tunapokuwa na fadhaa, udhaifu, magonjwa, changamoto na lolote lile ambalo linatuondolea amani yetu, tunaweza kumueleza Yesu Kristo mfalme wa amani yetu na akaweza kabisa kutatua na kushughulikia yala yanayotukanili na kutupa amani ya kweli, Nikutakie sikukuu njema ya Christmas

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Hakuna maoni: