Ijumaa, 25 Desemba 2020

Kupimwa kwa kazi ya kila mtu !

1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto” 

 

 


 


 

Utangulizi:

 

 

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu tulionao Mungu alimleta kila mtu Duniani kwa kusudi la kutimiza wajibu Fulani katika maisha yake,  kwa sababu hiyo  siku ya hukumu kila mmoja atatoa hesabu ya kazi au kusudi alilolifanya hakutakuwa na kisingizio kuwa hili linanipata kwa sababu ya Fulani, wote tutatioa hesabu mbele za Mungu na kila mtu atabeba mzigo wake kulingana na kazi au namna alivyotimiza  wajibu na kusudi lake duniani ona.;- 

 

Wagalatia 6:4-5 “Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. 

 

Tutajifunza so mo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

 

·         Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

·         Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

·         Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

 

Kwa msingi huo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anajua ni kwa nini yuko Duniani na amekuja kufanya nini duniani, kisha pambana kwa kila namna uwezavyo kuhakikisha kuwa unafikia lengo na kusudi kubwa la Mungu jkukuleta duniani, Katika maandiko Daudi anatajwa kama mtu aliyeweza kutimiza kusudi au shauri lote la Mungu, hakuondoka duniania akiwa amebakiza kazi fulani alihakikisha kuwa anaitimiza yote yaliyomo katika moyo wa Mungu na hata alitaka kuzidisha!

 

Matendo 13:36 “Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu.

 

Shauri l Mungu maana yake ni Kusudi lote la Mungu, kila mmoja anao wajibu wa kutimiza kusudi lote la Mungu, kuhakikisha kuwa unamaliza vema unahitimisha kazi yako vema, unatenda vema kusudi la Mungu, kama ni kuhubiri ni lazima tuhakikishe kuwa tunahubiri kusudi lote la Mungu, kama ni kuchunga tunachunga kwa kusudi lote la Mungu kama ni kufundisha tunafundisha kama Mungu anavyokusudia, kama ni kusoma tunasoma kama Mungu alivyokusudia, kama ni kuhubiri injili unahubiri kama Mungu alivyokusudia na kama ni kuongoza unaongoza kama Mungu alivyokusudia, Paulo Mtume alipohubiri injili aliweka wazi kuwa aliwahubiria watu kile ambacho Mungu alikusudia na hivyo  alihubiri kusudi lote la Mungu!

 

 Matendo 20:25-27 “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena. Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote. Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.”

 

Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

 

Wako watu mbalimbali katika maandiko ambao wanatajwa kuwa walitimiza makusudi ya Mungu kwa uaminifu na walitioa hesabu na kujifanyia tathimini;-

 

1.       Yesu mwenyewe alijifanyia tathimini na kutoa Ripoti kuwa amemaliza kusudi lote la Mungu, ukiacha kuwa siku ya kusulubiwa kwake alisema IMEKWISHA yaani alitimiza makusudi yote ya Mungu lakini vilevile alitoa hesabu ya kile ambacho baba alikuwa amemuagiza kukitimiza na kwa uhakikika kabisa alikuwa ameyatimiza hivyo kama asemavyo mwenyewe katika  injili ona ;-Yohana 17:1-13 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.  Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika. Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako. Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako; na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.  Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.”

 

2.       Paulo Mtume alihakikisha kuwa ametimiza kusudi lote la Mungu na kwa ujasiri kabisa alimuekleza Timotheo kuwa anasubiri taji yaani thawabu kubwa kwa sababu alikamilisha kile alichokusudiwa na Mungu kwa uaminifu mkubwa kwa mapambano na kwa mwendo mrefu na aliukamilisha  ona 2Timotheo 4;6-8 “Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;  baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”

 

3.       Musa alikuwa mwaminifu katika kazi yote nya Mungu, maana yake alikamilisha jukumu lake duniani, Musa alilitumikia kusudi la Mungu mpaka akasahau kifo, ilibidi Mungu amkubushe kwamba apande kwake mlimani akafe kwa sababu alikuwa mwaminifu mpaka sekunde ya mwisho Waebrania 3:5 “Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;

 

4.       Yoshua alikuwa kiongozi mkubwa jemadari na shujaa alitimiza makusudi ya Mungu hadi  mwisho na kuhakikisha kuwa anaonyesha msimamo wake hata kwa wana wa Israek kuwa yeye na nyumba yake wameamua kwa dhati kuwa watamtumikia Mungu aliye hai ona Yoshua 24:14-18 “Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana. Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine;  kwa maana Bwana, Mungu wetu, yeye ndiye aliyetupandisha sisi na baba zetu kutoka nchi ya Misri; kutoka nyumba ya utumwa; naye ndiye aliyezifanya ishara zile kubwa mbele ya macho yetu, na kutulinda katika njia ile yote tuliyoiendea, na kati ya watu wa mataifa yote tuliopita katikati yao. Bwana ndiye aliyewafukuza watu wa mataifa yote watoke mbele yetu, naam, Waamori waliokaa katika nchi hii; basi, kwa sababu hiyo sisi nasi tutamtumikia Bwana, maana yeye ndiye Mungu wetu.”               

 

5.       Nabii Samuel aliishi maisha ya haki, hakudhuklumu mtu na mbele ya watu wote alijipambanua kuwa hakuwa na tatizo na Mtu he was a man of integrity   alihitmisha akiwa na ujasiri kuwa hakuwahi kumuonea mtu wala kumdhulumu mtu na kuwa alihitimisha akiwa na mikono safi je wewe unahitimisha vipi katika utumishi wako, je watu watakumbuka namna ulivyowaliza? Na kuwaonea na kuwatendea mabaya? Samuel alimaliza vema ona  katika 1Samuel 12:3-5 “Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote. Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi

 

6.       Henoko alikuwa mwaminifu alitembea na Mungu, mwandishi wa kitabu cha mwanzo anamfanyia tathimini Henoko na kumuonyesha kuwa mtu wa tofauti, yeye licha ya kuzaa kama wengine licha ya kuishi maisha marefu alitembea na Mungu kiasi Mungu aliamua kumfanya kuwa malaika

 

Mwanzo 5:8-14 “ Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa. Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani. Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa. Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli. Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa. Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa. Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.  Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.”

 

Hao walikuwa ni baadhi ya watu muhimu katika biblia ambao walijifanyia tathimini katika maisha yao na kutimiza makusudi ya Mungu vema, kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake vema, tukikumbuka na kuelewa ya kuwa tutatoa hesabu mbele za Mungu, katia Nyanja yoyote ambayo Mungu amekuita unapaswa kuhakikisha kuwa unafanya vema, Florence Nightingale mwanzilishi wa uuguzi duniani alisimama vema katika kusudi lake mpaka leo anakumbukwa kwa kazi yake katika siku ya wauguzi duniani,  ni vema kila mmoja akafanya vema, mainjinia wasipunje, viwango vya barabara za lami hata kwa chepe moja la kokoto, Mizani za wafanya biashara ziwe za haki, madaktari na wafanye kwa uadilifu, Walimu wafundishe kwa bidii na wanafunzi wasome kwa bidii ni wakati wa kila mmoja kutimiza wajibu wake vema ili mbele za Mungu anwanadamu tuonekane kuwa na haki na kuepuka hukumu wakati kazi zetu zitakapopimwa!

 

Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Mungu ataipima kazi ya kila mmoja wetu kama lisemavyo neon la msingi, kila mmoja anapaswa kujifanyia tathimini kama anafanya kwa ubora kile ambacho Mungu amekusudia ndani yake, katika hukumu za Mungu ziko hukumu za aina nne Mungu aatakazowahukumu wanadamu

 

1.       Present judgment – hukumu iliyoko sasa kama mtu hajampokea Yesu hajamuamini huyo kwa sasa tunapozungumza ujumbe huu amekwisha kuhukumiwa angalia Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.  Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.” Ili kuepuka hukumu hii basi mwanadamu anapaswa kumuamini Yesu

 

2.       Hukumu ya adhabu Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hukumu hii ni hukumu ya aibu hukumu ya adhabu kwa kiyunani inaitwa KRI MA Mungu atafunua siri zote za uovu za wale wasiomuamini Mungu na wale waliotenda vibaya ona Muhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.” Mungu atafupisha maisha au hata kazi za mtu asiyetenda vema hakikisha kuwa unatenda vema

 

3.       Hukumu isiyo ya adhabu Warumi 8:1 “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hii ni hukumu ya watakatifu, pamoja na neema ya kuingia mbinguni Mungu atamlipa kila mmoja sawa na kazi njema aliyoitenda kazi hizo zitajaribiwa kwa moto  kama ni ya majani, miti na nyasi itateketea na haitaleta heshima kwetu, lakini pamoja na kumuamini Yesu tunapaswa kutenda vema hukumu hii kwa kiyunani inaitwa KRINO ni hukumu isiyo ya adhabu kwa wale walio katika Kristo lakini kazi ya kila mmoja itapimwa, Yesu ataketi katika kiti cha Enzi kiitwacho Bema na kutoa thawabu kwa kazi zetu1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto  

 

4.       Mungu anajua, un predictable judgment hii ni hukumu isiyotabirika   Warumi 14:4 ” Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.“Yeye ni Bwana ana maamuzi yake kama unavyokwenda kwa hakimu anaweza kuamua lolote kama apendavyo mwenyewe hakuna mtu anayejua rehema za Mungu, haiyamkini bwana anaweza kutyangaza rehema kwa mtu, yeyote au hata kwa watu wote kwani utamwambia nini yeye si ndio Mungu? Ndio anaweza kuamua lolote utamfanya nini aliamua utamuuliza nini, Tufanye kazi zetu kwa bidii kwani maandiko yamesema iko thawabu kubwa sana waongoze wengi katika kutenda haki nawe utafaidika!

 

Daniel 12;3  Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Hakuna maoni: