Jumapili, 7 Juni 2020

Nilichokiandika Nimekiandika!



Yohana 19:20-22 “Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani. Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.  Pilato akajibu, Niliyoandika nimeyaandika.



Utangulizi:


Leo tutachukua Muda kujifunza jambo la muhimu sana kutoka kwa moja ya Mtawala maarufu sana aliyehusika katika kumuhukumu Yesu Kristo kwenda msalabani na kusulubiwa, Mtawala huyu au Liwali kwa jina lingine anajulikana kama Pontus Pilatus kiwashili Pilato, Moja ya jambo la msingi sana tutakaloweza kujifunza ni kuhusu Msimamo wake na mtazamo wake  kuhusu Yesu kristo, tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-

·         Historia fupi ya Pontius Pilato
·         Niliyoyaandika nimeyaandika


Historia fupi ya Pontius Pilato *PONTIUS PILATUS*
Ponsyo Pilato  Moja ya watawala vijana sana kupata kutokea kama anavyoelezewa na Mwanahistoira maarufu wa karne ya kwanza aliyejulikana kama FLAVIUS JOSEPHUS aliyekuwa myahudi aliyekuwa na ujuzi wa lugha Kiaramu, Kiebrania na kigiriki (Aramaic, Latin and Greek) Lugha ambazo zilitumiwa na wasomi wengi wa nyakati ya karne ya kwanza  mtu huyu Flavius Josephus aliishi kati ya mwaka  37-100 BK na alikuwa kuhani Myahudi, alitekwa na warumi na kuwa Mkalimani wa Kaisari Vespasian kwa miaka miwili, Kitabu chake kinapatikana hata kwa ku- download electronic book kama Works of Flavius Josephus  ikitabu chake hicho ni  kirefu sana na kinachukua muda mrefu kukisoma.


Yeye anamuelezea Ponsyo Plato kwa kilatini PONTIUS PILATUS aliyekuwa liwali wa Kirumi katika inchi ya israel kati ya mwaka 26-36 wakati wa Yesu Kristo, yaani miaka 10 Pilato  Anajulikana kutokana na vyanzo mbalimbali, lakini hasa kwa sababu ya  Injili kumtaja kama hakimu aliyempeleka Yesu kuuawa msalabani. Historia yake ina0onyesha alipewa utawala akiwa kijana mdogo sana kwa sababu inasemekana alizaliwa mwaka wa 12 baada ya Yesu, kwa hivyo wakati wa hukumu ya Yesu yeye alikuwa na umri wa miaka 21 hivi, ukiacha kutajwa katika injili zote nne na kuelezewa zaidi katika injili ya Yohana pia anatajwa katika


Matendo ya
Mitume 3:13 “Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe utaweza kuona pia


Matendo ya mitume 4:27 27. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee.”
Na pia anatajwa katika


Matendo 13:28 “Na ijapokuwa hawakuona sababu ya kumfisha wakamwomba Pilato auawe.”
Na Paulo mtume alimtaja tena katika kitabu cha

1Timotheo 6:13 ”Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato,”
unaweza kuona namna mtawala huyu anavyotajwa sana katika maandiko, maana yake ni kuwa alikuwa mtu maarufu ambaye wahubiri wa hyakati za kanisa la kwanza hawakuweza kumsahahu! Kwa karne nyingi Pilato amekuwa mtu asiyeweza kusahaulika pilato anatajwa pia katika ukiri wa imani, au imani ya nikea au imani ya mitume au sala ya nasadiki kama “Zamani za Pontio Pilato aliteswa


Pilato  maisha yake ya awali hayajulikani sana japo viko vyanzo vinavyoeleza kuwa alikuwa ni  Mtot aliyezaliwa nje ya Ndoa ya Mfalme wa Tiro,  ambaye alimtuma kwenda Rumi kama muhudumu na huko aliua mtu na akatumwa kupelekwa Asia ndogo kwa makusudi ya kushughulikia watu Korofi, kutokana na ukorofi wake mkubwa alipata kibali kwa Warumi alipewa zawadi ya kutawala kama gavana wa jimbo la Uyahudi (Judea)  na Mtawala Tiberio kwaajili ya kuwashughulikia Weayahudi ambao mara kwa mara waliasi.


Alikuwa mtawala Katili sana aliyeamuru kuuawa na kusulubiwa kwa wayahudi wengi sana,  adiah aliwaudhi wayahudi sana kwa kuleta desturi za kirumi na hata kukleta habari za miungu migenikwenye hekalu, wakati mwingine aliweza hata kuchukua kodi za hekaluni na kuzitumia kwa matumizi yasiyofaa alikuwa muuaji na mtu aliyeweza kuwaua wayahudi vibaya sana moja ya habari za ukatili wake zilienea wakati wa Yesu ona katika 

Luka 13:1
Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao.”

Nilichokiandika nimekiandika!

Inasemekana makazi makuu ya Pilato yalikuwa ni Kaisaria hata hivyo Pilato alikuwa na desturi ya kuja Yerusalem siku za sikukuu kwaajili ya kutuliza Ghasia na kuwadhibiti wayahudi, wakati wa kukamatwa kwa Yesu, kwa vile yalikuwa ni majira ya Pasaka Pilato alikuwako Yerusalem, wakuu wa makuhani walipokwisha kumuhukumu Yesu kwa mila na desturi zao, waliona vema pia kumpeleka kwa Pilato walifahamu tabia zake na hivyo walijua kuwa kwa ukatili aliokuwa nao Hakuna myahudi anayehusishwa na vurugu angeweza kusalimika, mambo kadhaa yaliweza kujitokeza wakati wa hukumu ya Bwana Yesu

Moja ya muujiza mkubwa sana kuwahi kutokea ni kwa jamaa huyu muuaji na katili kuonekana akinawa mikono na kugoma kumpeleka Yesu Msalabani  kwa sababu alibaini wazi kuwa Yesu hakuwa na hatia yoyote na alielewa kuwa Wayahudi wanamleta kwake kwa sababu ya husuda tu hili lilikuwa jambo la kushangaza kwa vile alikuwa hacheleweshi kesi, na haponyi mtu, kusitasita katika kumuhukumu Bwana Yesu ilikuwa ni moja ya tabia mpya na ya ajabu iliyowastaabisha wayahudi kwa sababu walijua wamempeleka penyewe, Aidha Familia yake ilikuwa na taarifa za Mapema kuwa anakuja mtu mwenye haki na kuwa Pilato anapaswa kuwa na tahadhari namna atakavyoshughulika na kesi ya mtu huyo ujumbe huu alipewa na mke wake akimtahadharisha kuhusu hukumu ya siku ile Pamoja na hayo alifanya kila jitihada kumuokoa Yesu kupitia Mfungwa aliyekuwa hatari na muhaini zaidi kuliko Yesu lakini hata hivyo wakuu wa dini bado walijaa husuda yaani wivu dhidi ya Yesu Ona


Mathayo 27: 16-19 “Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba. Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo? Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda. Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.”  


Pilato pia alikuwa ni mtu pekee aliyeweza kupata nafasi ya kuzungumza na Yesu kipekee na kujua kusudi la kuwepo kwa Yesu Duninani. Yeye alimuelewa wazi Yesu kuwa amekuja kuishuhudia kweli, na kuwa yeye mwenyewe Yesu ndio kweli, aidha alitambua wazi kupitia Yesu kuwa mamlaka aliyonayo yeye imetoka juu yaani imetoka kwa Mungu na pia alipata nafasi ya kujua na kuelewa kuwa Yesu alikuwa mfalme kweli lakini ufalme wake haukuwa wa ulimwengu huu


Yohana n18:33-38a “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi? Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu? Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini? Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa. Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu. Pilato akamwambia, Kweli ni nini?


Ni wazi kabisa mpaka wakati Pilato anakuja kutoa hukumu kupitia mashinikizo ya kisiasa kutoka kwa wayahudi tayari kitu Fulani kilikuwa kimejengeka moyoni mwake kuhusu Yesu Kristo na kama isingalikuwa maandiko yatimizwe ni wazi kuwa Pilato angemuachia Yesu huru!


Hapa sasa tunaona wazi kuwa Maadui wa Yesu Kristo walikuwa wanategemea kuwa kwa kuwa wamemleta Yesu Kwa Pilato hawezi kusalimika lakini hawakuwa wamejua kuwa  Mungu aliandaa kitu katika Moyo wa Pilato na kuwa hawakujua kuwa Pilato alikuwa anaujua wivu wao na akaandaa  aibu kubwa sana na udhalilishaji ambao wangeupata kuhusu ubaya wao huo, aibu hii yalikuwa ni maneno yaliyowekwa na Pilato juu ya Msalaba wa Yesu.

Pilato aliandika meneno hayo na kuyaweka katika msalaba wa Yesu yaliyokuwa yakisomeka “YESU WA NAZARETH MFALME WA WAYAHUDI Wayahudi wengi sana waliyasoma maneno haya kwa sababu mahali aliposulubiwa Yesu palikuwa ni karibu na lango la jiji la Yerusalem na ni mahali ambako wengi walipita, Meneno haya yaliandikwa kwa lugha kubwa tatu Kiaramu, Kilatini na Kiyunani hivyo yaliweza kusomwa na watu wote hata wageni waliokuja kutoka sehemu mbalimbali duniani kwaajili ya sikukuu ya pasaka, wakuu wa makuhani hawakuyafurahia hata kidogo maneno yale kwa hiyo walimwendea Pilato na  kumwambia, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi Pilato akajibu, Niliyoandika nimeyaandika.”
Ilikuwa ni desturi kwa kila muhalifu anayehukumiwa kusulubiwa  na warumi kuwekewa mashitaka yake juu ya msalaba ili kwamba kila anayepita aweze kuona ili iwe fundisho kwake, Lakini kwa Kristo ilikuwa kitu cha kushangaza sana ! hayakuwa mashitaka bali lilikuwa Tangazo halisi kwa ufunuo halisi

Yesu hakuonekana na hatia alikuwa amehukumiwa kwa sababu ya wivu wa wayahudi tu na Pilato alifahamu, Wayahudi walikuwa wamechukizwa naye kwa sababu yeye alisema wazi kuwa ni mwana wa Mungu na pia ndiye mrithi halali wa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, Pamoja na hayo miujiza mikubwa aliyoitenda na umati mkubwa uliomfuata na kumkubali ulisababisha wayahudi kupoteza umaarufu wao wa kidini, watu walikuwa wamemkubali Yesu kuwa ndiye masihi wao, Wayahudi na Viongozi wa kidini  wao walijua kwa makosa haya ingeweza kumshawishi Pilato kutoa hukumu kali kwa kufikiri kuwa Yesu anamuasi kaisari kwa kujiita Mfalme, Lakini Pilato alielea ukweli Yesu ni mfalme wa namna gani na  kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao Viongozi wa dini, kwa hivyo hakukuwa na mashitaka zaidi ya hayo Kila ambaye angeona mashitaka hayo angeweza kueneza habari kuwa Yuko Mfungwa amesulubiwa msalabani na ni Mfalme wa wayahudi, hana makosa mengine ni mfalme wa wayahudi habari zingeweza kuenea Rumi, Uyahudi na kila mahali walikotumia lugha zile alizoandika Pilato, Bila shaka kosa hili la uandishi halikuwa kosa la kibinadamu,  wala Pilato hakuwa amekosea katika kile alichokiandika ilikuwa wazi kabisa kwamba Pilato alikuwa na ufunuo sahihi kuwa Yesu alikuwa Mfalme wa Kiroho kwa watu wote  walipomwambia ayaondoe maneno yale Pilato alijibu  kwa kiyunani Ho Gegrapha gegrapha! na kilatini Quod scrips scrips, what i have written I have written yaani Nilichokiandika nimekiandika  Pilato alimaanisha kuwa ujuzi wake kuhusu Yesu hakuna mtu wa aina yoyote anaweza kuubatilisha ule ulikuwa ni ukweli uliowazi kabisa ambao Pilato alikuwa ameubaini na ambao alitaka watu wote watambue, Kila mmoja leo anapaswa kukubali na kutambua Kuwa Yesu ni Mashihi, Yeye ndiye aliyekusudiwa kwa wayahudi na ulimwengu mzima litakuwa ni jambo la ajabu sana kwa Mtu mkatili ikama Pilato kubaini ukweli na kujua kuwa Yesu ni mfalme wa wayahudi na akaanidla kwa lugha tatu kuu za wakati uoe akitaka kila mtu na kila lugha na kila taifa wajue  YESU WA NAZARETH HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI, Viongozi wa kidini walimsihi ayaondoe maneno hayo lakini jambo lingine la kushangaza aligoma alisema *NILICHIKIANDIKA NIMEKIANDIKA* Kwa lugha nyingine Pilato alikuwa anasema amethibitisha, ana uhakika, alichikithibitisha hakiwezi kutenguliwa milele, Pilato alikuwa gavana alikuwa liwali alikuwa kiongozi mkubwa alikuwa katili alikuwa muuaji, alikuwa na mamlaka kubwa sana alihukumu Kesi ya yesu alikuwa kijana alikuwa na akili sana alikuwa katili lakini alikiri kwa maandiko tena hadharani ya kuwa Yesu ni mfalme wa Wayahudi, alikuwa anakubali wazi kuwa yesu ni Bwana aluikuwa ameifahamu kweli swali lake kubwa kwa Yesu Kweli ni nini ? Yesu ndiye njia na kweli na uzima, leo hii kila mmoja anapaswa kumkiri Yesu kwa utukufu wa Mungu baba haijalishi una cheo gani haijalishi umefanya dhambi ngapi umwamini Yesu, ukubali kuwa Yesu ni Bwana na uwe tayari kumtetea Yesu kwamba ulichokiamini umekiamini, ulichiokithibitisha umekithibitisha ulichokiandika umekiandika Yesu ni Mfalme wa wayahudi!

Kwa mujibu wa kanisa la Orthodox la Ethiopia wanamtambua Pilato kama Mtakatifu mwenye heri wakiamini kuwa alimkubali Yesu kwa kuokoka na hivyo ni mtu mwenye kuheshimika sana. Ndio maana anatajwa katika ukiri wa imani ya Mitume ! NILICHOKIANDIKA NIMEKIANDIKA!

Na Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi, mwenye Hekima.
0718990796

Hakuna maoni: